Jumanne, 27 Juni 2023

Jinsi ya kufanya agano la chumvi




Wakati wa kufanya agano la chumvi.

  1. Mizimu, mapepo, shetani na wachawi na waganga au makuhani wa kichawi huwaathiri watu katika maisha yao na kusababisha msongo wa mawazo, kwa kutumia nguvu za giza, kwa kutumia nguvu hizo za giza na za kichawi wanawasababishia watu kupoteza mwelekeom kuwa na bumbuwazi, kuteseka, kuelemewa, kuwa na uzito na kupata changamoto za kifedha na kiuchumi na changamoto nyinginezo nyingi.

 

Uchawi ni silaha ya giza inayotumiwa na wachawi kwa kusudi la kuharibu maisha ya watu wanaofanikiwa na kufanikiwa  katika mazingira mbalimbali, silaha hiyo ya giza ni silaha ya kiroho lakini matokoe yake hutokea katika hali halisi.kuteseka kwa watu waliorogwa au kuchawiwa kunategemeana na nguvu iliyotumika katika kunuiziwa nguvu za mashambulizi

Pepo watatafasiri uchawi na manuizo na kuyawasilisha kwa watu waliolengwa na kuwashambulia na matokeo yanaweza kutokea katika ulimwengu wa miili yao, mambo magumu na matukio ya ajabu huanza kutiokea katika maisha yao na njia pakee ya kuimarisha na kuleta ukombozi ni agano la chumvi

 

Ukombozi kupitia gano la chumvi ni rahisi sana kwa muonekano lakini una nguvu kubwa za ajabu sana, ukombozi huu una nguvu ya kuondoa kabisa maedhara ya nguvu zisizoonekana za kichawi na kuukausha au kuuondoa kabisa na kuondoa hali ya kushindwa kwa sababu zozote zile, kwa kufanya hivyo haimaanishi oia mkuwa tutaacha kabisa kuschughulikia nguvu za giza kwa namna za kawaida, lakini tutaendelea ili kuhakikisha kuwa tunaendelea kukua kiroho.

 

  1. Unafanya gano la Chumvi wakati gani?

 

Tunafanya agano la chumvi wakati tunapohisi kuwa kuna matukio ya vita za kiroho zilizohusisha nguvu za giza, ni kweli kwamba mtu aliyeokoka hawezi kushambuliwa na nguvu za giza kwa sababu imeandikwa hakuna ugaga wala uchawi juu ya Yakobo Hesabu 23:23  “Hakika hapana uchawi juu ya Yakobo, Wala hapana uganga juu ya Israeli. Sasa habari za Yakobo na Israeli zitasemwa, Ni mambo gani aliyoyatenda Mungu!

 

Lakini kumbuka tuna mashambulizi kutoka kwa mamadui, tuko vitani, majeshi ya pepo yanatumwa kwetu kwa mauizo na sadaka za iana mbalimbali na kwa maelekezo ya aina mbalimbali kwa hiyi kuna kiwango cha mashambulizi ambayo tunakutana nayo wakati mwingine kwa asilimia 30 au 60 au 90 kwa hiyo wote kwa kiwango Fulani tunashambuliwa na nguvu za giza kulingana na kiwango za kuzaa kwetu matunda kumbuka mfano wa zile mbegu zilizoangukia kwenye udongo mzuri Marko 4:8 “Nyingine zikaanguka penye udongo ulio mzuri, zikazaa matunda, zikimea na kukua, na kuzaa, moja thelathini, moja sitini, na moja mia.” Kama ukuaji wetu wa kiroho unaweza kuzaa matunda kwa asilimia hizo zilizotajwa ni dhahiri na mashambulizia yanaweza kuwepo kutokana na kiwango kwa hiyo niia nyepesi ya kuondoa kiwango hicho cha mashambulizi ya nguvu za giza ni kwa kutumia ganano la chumvi  na ukifanya mara kwa mara unaziondoa kabisa katika mwili wako  tunaweza kujitibu kwa agano la chumvi mara unapohisi au kusikia changamoto hizi:-

 

-          Uchovu wa kimwili na kiroho

-          Kupoteza hamasa

-          Kupoteza uwezo wa kufikiri

-          Kuelemewa na mawazo

-          Hasira za kupita kawaida

-          Mgandamizo wa mawazo stresses

-          Aina yoyote ya ugonjwa na wakati wowote unapokuwa unahisi kuwa kuna uvamizi na hali isiyo ya kawaida katika mwili wako, uchumi wako, kazi yako, huduma yako na roho yako.

-          Lakini pia udhaifu wowowte wa kimwili, kiroho na kihisia ujue kuna mashambulizi ya mizimu, mapepo, wachawi na kadhalika basi unahitaji tiba ya agano la chumvi.

 

  1. Mambo unayohitaji kwaajili ya kutekeleza agano la chumvi

 

-          Utahitaji ndoo au beiseni

-          Utalijaza maji safi kwa asilimia 50% yaani nusu

-          Utahitaji chumvi yam awe kwa kiwango chochote kana huna ya mawe unaweza kutumia ya mezani lakini ya mezani uwezo wake utapungua kwa asilimia 30% ukilinganisha na ile ya mawe

-          Taulo la kujikaushia

-          Na sehemu ya kukanyajia

-           

  1. Jinsi ya kufanya ibada ya agano la chumvi.

 

1.       Weka maji kwenye ndoo yajae kwa asilimia 50% yaani nusu yake kwa kiwango tu cha kufunika enka za miguu

2.       Weka vijiko vidogo viwili vya chumvi ya mawe

3.       Omba kwa kumaanisha na kwa imani kwamba Mungu akuondolee nguvu zote za giza, pia omba maalumu kwaajili ya kuziharibu kabisa na kuzibomboa nguvu zote za mizimu, pepo, waganga na wachawi na kila manuizo yaliyofanywa kinyume nawe na kukuletea athari, omba maombi ni muhimu sana na yana uwezo mkubwa sana yanapofanyika sambaba na ibada hii ya ukombozi.

4.       Hakikisha umekaa sawa sawa na miguu yako hususani enka ziwe zimezama katika maji, miguu yako isigusane bali iwe mbalimbali kati ya sentimita 2-3 hii inasaidia kuodoa uchawi wote uliorogwa kwa nguvu za giza, kama miguu yako itagusana itakuwa kikwazo kwa ibada hii, 

5.       Hakikisha miguu inakaa kati ya dakika 10-15 na usizidishe zaidi ya dakika 15, ukizidisha nguvu za giza zinazotoka kwa njia ya miguu zinaweza kuingia mwilini mwako

6.       Wakati miguu yako inapokuwa katika maji yenye chumvi anza kuomba au kunuiza kwa jina la Yesu  Mungu au kuimba maombi

7.       Wote wenye pumzi wote waishio duniani wote wampendao  (Wamchao) Mungu na waseme fadhili zake ni za milele

8.       Wote wanaoeneza habari zake watangazao habari njema duniani kote na waseme fadhili zake ni za milele.

 

Kwa ufupi utaimba zaburi 118:1-14         

1. Haleluya. Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema, Kwa maana fadhili zake ni za milele.

2. Israeli na aseme sasa, Ya kwamba fadhili zake ni za milele.

3. Mlango wa Haruni na waseme sasa, Ya kwamba fadhili zake ni za milele.

4. Wamchao Bwana na waseme sasa, Ya kwamba fadhili zake ni za milele.

5. Katika shida yangu nalimwita Bwana; Bwana akanijibu akaniweka panapo nafasi.

6. Bwana yuko upande wangu, sitaogopa; Mwanadamu atanitenda nini?

7. Bwana yuko upande wangu, msaidizi wangu, Kwa hiyo nitawaona wanaonichukia wameshindwa.

8. Ni heri kumkimbilia Bwana Kuliko kuwatumainia wanadamu.

 

9. Ni heri kumkimbilia Bwana. Kuliko kuwatumainia wakuu.

10. Mataifa yote walinizunguka; Kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.

11. Walinizunguka, naam, walinizunguka; Kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.

12. Walinizunguka kama nyuki, Walizimika kama moto wa miibani; Kwa jina la Bwana naliwakatilia mbali.

13. Ulinisukuma sana ili nianguke; Lakini Bwana akanisaidia.

14. Bwana ni nguvu zangu na wimbo wangu, Naye amekuwa wokovu wangu.

 

Hitimisho:

Baada ya kumaliza maombi haya ya ukombozi kulinga nan a mahitaji yako unaweza kuanza kumshukuru Mungu kwa ulinzi wake anaokupa na namna anavyokuzunguka

Utayamwaga maji yake chooni na kisha utasafisha ndoo na maji safi. Utakausha miguu yako vema kwa taulo na kisha utajipaka mafuta ya mzeituni na kuomba Mungu akupeleke kwenye kiwango kingine cha maswala mbalimbali uyatakayo. Ibada inaweza kufanyika pia kwa makusudi mbalimbali ambayo mengine hayajaainishwa katika somo hili mfano kuweka wakfu, kiongozi, kujilinda na cheo chako na kadhalika

Mwisho wa ibada hii.

Matokeo:

  1. Athari zote za nguvu za Giza na mashambulizi ya wachwi, waganga na mapepo na shetani zinaondoka
  2. Maji ya agano la chumvi yana nguvu kubwa sana yenyewe tu kunyonya nguvu zote za giza
  3. Nguvu za giza na magonjwa yote yanayoambatana na nguvu hizo yanaondoka na wakati mwingine maji yanaweza kuwa na rangi nyeusi kama ishara ya kuondoka kwa nguvu hizo, au yanaweza kuwa na uvuguvugu au yakawa na harufu mbaya hii ni shara ya vitu vibaya kuondoka mwilini mwako

 

KUMBUKA:  Somo hili lina uhusiano na huduma za kinabii, sio vizuri kufundisha au kulifanyia kazi kanisani ikiwa huamini katika huduma za kinabii

 

Na Rev. Innocent Samuel Kamote

 

Mkuu wa wajenzi mwenye hekima


Hakuna maoni: