Ijumaa, 2 Machi 2018

Kuingia kwa mfalme Kinyume cha Sheria!


Andiko la msingi: Esta 4:15-16Basi Esta akawatuma ili wamjibu Mordekai, Uende ukawakusanye Wayahudi wote waliopo hapa Shushani, mkafunge kwa ajili yangu; msile wala kunywa muda wa siku tatu, usiku wala mchana, nami na wajakazi wangu tutafunga vile vile; kisha nitaingia kwa mfalme, kinyume cha sheria; nami nikiangamia, na niangamie.”



Utangulizi:

Wiki hii ni wiki ya sikukuu ya PURIM kule Israel wayahudia huandimisha sikukuu ya Purim kwa mujibu wa kalenda ya kiyahudi sikukuu hii ya Purim huazimishwa kila ifikapo February 28 na 29 ya kila mwaka  ambayo ni sawa na siku ya 13, 14  na 15 ya mwezi wa Adar na Nissan yaani sawa na katikati ya mwezi Februari na March ya kalenda ya kawaida, Wayahudi huadhimisha sikukuu hii kutokana na amri ya Mordekai pamoja na malkia Esta kuwa ni lazima siku hii ikumbukwe. Esta 9: 29-32Ndipo malkia Esta, binti Abihaili, pamoja na Mordekai Myahudi, alipoandika kwa mamlaka yote kuithibitisha barua hii ya pili ya Purimu. Akapeleka barua kwa Wayahudi wote katika majimbo yote mia na ishirini na saba ya ufalme wake Ahasuero, maneno ya amani na kweli, ili kuzithibitisha siku hizo za Purimu kwa majira yake, kama Mordekai Myahudi na malkia Esta walivyoamuru, na kama walivyojiagizia juu yao wenyewe, na juu ya wazao wao, kwa habari ya kufunga na kilio.  Amri yake Esta ikayathibitisha mambo hayo ya Purimu; ikaandikwa katika kitabu” Ni kutokana na agizo hilo ndio mpaka leo Wayahudi huadhimisha sikukuu iitwayo PURIM au PURI wakimaanisha siku waliyopigiwa KURA au Kupitishiwa MSWAADA wa kuuawa Lakini kwa neema ya Mungu wakaokolewa. Siku ya Purim ni siku ya furaha sana kwa Wayahudi, wao hushangilia na kufurahi na kuruka ruka na kucheza ngoma na kunywa divai, Lakini katika masinagogi na ibada huwa ni wakati wa kusomwa kwa kitabu cha Esta.
Tutajifunza somo hili kwa kuzingatia mambo muhimu yafuatayo:-

·         Sababu na Mpango wa kuangamizwa kwa Wayahudi.
·         Utaratibu wa Sheria na tamaduni za kiamedi na kiajemi.
·         Kuingia kwa mfalme Kinyume cha sheria.

Sababu na Mpango wa kuangamizwa kwa Wayahudi.

Ni muhimu kufahamu kuwa Kitabu cha Esta ni mojawapo ya kitabu ambacho kiliandikwa kuonyesha Msimamo wa kiimani wa wayahudi waliokuwa Uhamishoni, wakati huu wayahudi waliokuwa uhamishoni huko Babeli maisha yao na imani yao kwa Mungu wa kweli ilikuwa imani kali sana na hawakutaka kuleta mchezo na msimamo wao wa kiimani katika Mungu wa kweli wa Israel, walikuwa wamejifunza madhara makubwa ya kumuacha Mungu hata kwa sekunde moja, hivyo walishikamana na Mungu wao kwa uthabiti hata pamoja na kuwa mbali na Israel, Kisa na sababu ya kutaka kuangamizwa kwao kinaashiria wazi kuwa ulikuwa ni mpango wa Ibilisi, ili kufuta Historia ya kuwepo kwa Mungu, kisa au sababu inaanzia kwa mtu mmoja aliyeitwa Hamani ambaye alipandishwa Cheo na Mfalme kuamuru watu wote walio chini yake wamsujudie Esta 3:1-4Baada ya hayo mfalme Ahasuero alimwongezea cheo Hamani bin Hamedatha, Mwagagi, akampandisha, akamwekea kiti chake juu ya maakida wote waliokuwapo pamoja naye. Nao watumishi wote wa mfalme, walioketi mlangoni pa mfalme, wakainama na kumsujudia Hamani, maana ndivyo alivyoamuru mfalme kwa habari zake. Bali Mordekai hakuinama, wala kumsujudia. Basi watumishi wa mfalme walioketi mlangoni pa mfalme wakamwambia Mordekai, Mbona wewe waihalifu amri ya mfalme? Ikawa, waliposema naye kila siku asiwasikilize, wakamwarifu Hamani, ili kuona kama mambo yake Mordekai yatasimama; maana alikuwa amewaambia ya kuwa yeye ni Myahudi.”  Unaweza kuona maandiko yanaonyesha sababu ya kisa cha wayahudi kuchukiwa ilikuwa ni tamaa na ubinafsi wa mtu mmoja tu kutaka Heshima na kuabudiwa, wakati mwingine migogoro mikuwa ya kitaifa au taasisi inaweza kuanza kwa chuki ya mtu mmoja tu, kwa maslahi yake na tamaa zake akaingiza wengine katika mgogoro mkubwa, ni Chuki ya hamani dhidi ya Mordekai ndio iliyopelekea Hamani kutaka kuwaangamiza Wayahudi wote, Esta 3:5-15Hata Hamani alipoona ya kwamba Mordekai hainami wala kumsujudia, alighadhibika sana.  Akaona si shani kumtia mikono Mordekai peke yake; maana wamemjulisha kabila yake Mordekai; kwa hiyo Hamani alitaka kuwaangamiza Wayahudi wote waliokuwa wakikaa katika ufalme wote mzima wa Ahasuero, yaani, watu wake Mordekai. Basi mwezi wa kwanza, ndio mwezi wa Nisani, mwaka wa kumi na mbili wa mfalme Ahasuero, wakapiga Puri, yaani kura, mbele yake Hamani; siku kwa siku, na mwezi kwa mwezi, hata mwezi wa kumi na mbili, ndio mwezi wa Adari. Basi Hamani akamwambia mfalme Ahasuero, Kuna taifa moja waliotawanyika na kukaa mahali mahali katikati ya mataifa walioko katika majimbo yote ya ufalme wako. Nao sheria zao zimefarakana na sheria za kila taifa; wala hawazishiki amri za mfalme; kwa hiyo haimpasi mfalme kuchukuliana nao. Basi, mfalme akiona vema, na iandikwe kwamba waangamizwe; nami nitalipa talanta kumi elfu za fedha mikononi mwao watakaosimamia shughuli hiyo, waziweke katika hazina ya mfalme. Ndipo mfalme alipoivua pete yake mkononi, akampa Hamani bin Hamedatha, Mwagagi, adui ya Wayahudi. Kisha mfalme akamwambia Hamani, Hiyo fedha umepewa, na watu pia, fanya uonavyo vema. Basi, waandishi wa mfalme wakaitwa, siku ya kumi na tatu ya mwezi wa kwanza; na barua zikaandikwa, kama vile Hamani alivyoagiza vyote, kwa maakida wa mfalme, na maliwali waliokuwa juu ya kila jimbo, na wakuu wa kila taifa; kila jimbo kwa mwandiko wake, na kila taifa kwa lugha yake; zikaandikwa kwa jinsi la mfalme Ahasuero, na kutiwa muhuri kwa pete yake. Barua zikapelekwa kwa mikono ya matarishi mpaka majimbo yote ya mfalme kuwaangamiza Wayahudi wote, na kuwaua, na kuwafisha, vijana kwa wazee, watoto wachanga na wanawake pia, siku moja, yaani, siku ya kumi na tatu ya mwezi wa kumi na mbili ndio mwezi wa Adari; na kuyachukua mali yao kuwa nyara.  Nakili ya andiko, ya kupigwa mbiu katika kila jimbo, ilitangazwa kwa mataifa yote wawe tayari siku ile ile.Matarishi wakaondoka wakaenda haraka kwa amri ya mfalme; kukapigwa mbiu huko Shushani ngomeni. Mfalme na Hamani wakaketi ili kunywa divai; bali mji wa Shushani ukafadhaika” Mpango huu ulikuwa ni mpango mbaya sana haukuwa na tofauti na kile alichokifanya “Adolf Hittler” ambaye yeye alifanikiwa kuwaua wayahudi wengi sana Duniani, ni jambo lenye kushangaza kuwa wakati mwingne shetani anaweza kukuza na kutekeleza chuki kubwa isiyokuwa na sababu maalum kwa watu wa Mungu, wanatheolojia wanaiita chuki hii kuwa ndio chuki ya ajabu iliyomkuta Yesu Kristo aliyeuawa na watu aliowatendea Mema, Mfalme alikuwa amesahau na wala hajui kuwa Mordekai alikuwa ni afisa usalama wa ngazi ya juu kabisa aliyefanikiwa kuokoa Maisha yake alipotaka kuuawa na sasa bila kuelewa amekubaliana na hamani na kupitisha sheria mbaya zaidi isiyoweza kutanguliwa ili kuwaangamiza wayahudi bila kufikiri Esta 2:21-23Ikawa siku zile, Mordekai alipokuwa akiketi mlangoni pa mfalme, wawili katika wasimamizi wake mfalme, Bigthana na Tereshi, wangoje mlango, walighadhibika, wakataka kumpelekea mikono mfalme Ahasuero. Basi Mordekai akapata kulijua jambo hilo, naye akamjulisha Esta, malkia; naye Esta akamwambia mfalme habari hiyo kwa jina la Mordekai. Na jambo hilo lilipochunguzwa, na hakika ikapatikana, hao wote wawili wakatundikwa juu ya mti. Hayo pia yakaandikwa katika kitabu cha taarifa mbele ya mfalme.”

Pamoja na wema huu na ulioweza kuwekwa katika taarifa Mfalme hakuona kuwa Mordekai na jamii yake ya Wayahudi kama watu waliokuwa na maana na alikubali waangamizwe ni muhimu kufahamu kuwa hapa ilikuwa imebaki siku ya kupigwa kura tu kuwa ni lini wayahudi watauawa lakini mswada ulikuwa umekwisha kupitishwa na kwa mujibu wa sheria za kiamedi na kiajemi jambo hili lisingeliweza kutanguliwa kwa namna yoyote, ili tuweze kufahamu vema hebu tuangalie desturi zao zilikuwaje katika kipengele kifuatacho.

Utaratibu wa Sheria na tamaduni za kiamedi na kiajemi.

Kwa mujibu wa Historia ya kibiblia Sheria za Uamedi na uajemi katika desturi yao zilikuwa zikipitishwa au zikiamriwa hakukuwa na kurudi nyuma kwa namna yoyote na ni vigumu hata mfalme mwenyewe kuweza kuitangua sheria na desturi iliyopitishwa naye msimamo wa aina hii ulithibitika wazi na lilikuwa ni jambo la fedhea na aibu kubwa sana kwa mfalme kugeuka nyuma ilionekana kama mfalme huyu sio mwenye moyo thabiti na imara na ni mfalme kigeugeu kutengua sheria kungeweza kumfanya mfalme asiaminike na watu wagepoteza imani naye japokuwa bado mfalme alikuwa ndio mwenye mamlaka ya mwisho na mwenye uwezo hata wa kutangua lolote kwa manufaa yake na taifa lake, Jambo hili liliwafunza Israel kuwa thabiti katika kutunza uadilifu wao kwa Mungu, hata ingawa walikutwa na hatari za kuishi katika mazingira magumu na yenye maamuzi kama hayo ya kushangaza.

-          Daniel 6: 12Ndipo wakakaribia, wakasema mbele ya mfalme katika habari ya ile marufuku ya mfalme; Je! Hukuitia sahihi ile marufuku, ya kwamba kila mtu atakayeomba dua kwa Mungu awaye yote, au kwa mtu awaye yote, katika muda wa siku thelathini, ila kwako, Ee mfalme, atatupwa katika tundu la simba? Mfalme akajibu, akasema, Neno hili ni kweli, kama ilivyo sheria ya Wamedi na Waajemi isiyoweza KUBADILIKA.”

-          Esta 1:19Basi mfalme akiona vema, na itoke kwake amri ya kifalme, nayo iandikwe katika sheria za Waajemi na Wamedi ISITANGUKE, ya kwamba Vashti asifike tena mbele ya mfalme Ahasuero; na umalkia wake mfalme ampe mwingine aliye mwema kuliko yeye.”

Unaweza kuona kuwa sheria zao zilikuwa kali na za kidikteta zisizoweza kutanguaka au kubadilishwa, hata hivyo kutokana na chuki na wivu kwa wayahudi wakati mwingine sheria za aina hii zilipitishwa ili kushindana na watu wa Mungu kama Daniel, pia Shadrak, Meshak na Abdednego, pia katika kitabu cha esta yanamkuta Mordekai na jamii nzima ya kiyahudi, ambao sasa wamepitihwa kuwa wauawe katika muswada huu wa sheria za watu hawa ambazo ni ngumu mno kuiztanbgua au kzibadilisha.

Ni muhimu kufahamu kuwa katika ulimwengu wa Kiroho, hali kadhalika ni vigumu kubadilisha jambo ambalo Mungu ameliamuru lipite au lisipitishwe, na sio hivyo tu lakini hata upande wa shetani ni vigumu kwake kuwa kigeugeu, yeye anapodhamiria kuleta uharibifu kwako huwa hatanii, anapokusudia kukushuhsia hukumu huwa hana muda wa kupoteza, mtu mwenye chuki anapokuendea kwa mganga na wachawi ili kukuharibu ni vigumu kwa Mchawi kurudi nyuma na kugeuka, ikiwa shetani amekukusudia kukuharibia, kukuaibisha,anahakikisha kuwa anakubana katika kiwango ambacho huwezi kuchomoka mpaka akubamize, atakufuatilia bila kurudi nyuma bila kubadilika bila kuitangua dhamira yake, jambo hili lilitambulika vema kwa wayahudi pia kuhusu makusudio mabaya ya Waamedi na waajemi dhidi yao. Maandiko wakati wote yanatuonyesha kuwa ni Mungu pakee anayeweza kuubadili Moyo wa mfalme kama apendavyo  Mithali 21:1Moyo wa mfalme huwa katika mkono wa Bwana; Kama mifereji ya maji huugeuza po pote apendapo.”  Unaona Biblia inatuthibitishia kuwa ni Mungu peke yake ndiye anayeweza kuugeuza moyo wa mfalme kokote apendapo yaani atakapo Mungu, lakini sio hivyo tu ni kwake yeye ndiko tunakoweza kukata rufaa ya sheria za kipuuzi zilizopitsihwa kwa misingi ya uonevu wa Ibilisi ni kwanamna gani tunaweza kufanya hilo ni kwa kuingia kwa mfalme kinyume cha sheria.

Kuingia kwa Mfalme kinyume cha sheria.

Kwa vile Esta na Mordekai walikuwa wanazifahamu sheria za waamedi na waajemi pamoja na desturi zao kwamba halikuwa jambo rahisi kuweza kuwaponya wayahudi na kujikoa wao wenyewe na mauti iliyokuwa imekusudiwa kuwakumba, Esta na Mordekai walikuwa wamekwisha kuwa na ujuzi kuwa wakati wowote unapokutana na jambo gumu ni maombi na pamoja na kufunga na kuomba tu ndio ilikuwa njia pekee ya kuweza kutangua sheria za kubahatisha za wanadamu, Esta aliamini katika nguvu ya kufunga na kuomba, watu wengi na dini nyingi zinaamini katika nguvu ya kufunga na kuomba hata na mimi ninaamini kuna nguvu katika kufunga na kuomba Yesu pia aliamini katika nguvu ya kufunga na kuomba yeye mwenyewe Yesu akasema kuna na mambo mengine hayawezekani isipokuwa kwa kufunga na kuomba Mathayo 17 :21[Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga.]Yesu alikuwa akimaanisha  kuwa kuna nguvu kubwa katika maombi yenye kujitoa kwa jambo lolote lile kama maombi ni hafifu matokeo yake yanakuwa hafifu na kama maombi ni yenye bidii matokeo yake yanakuwa makubwa sana, Esta alikuwa sio anakabiliwa na sheria na Muswada uliokuwa umepitishwa tu lakini kama malikia ambaye angeweza kuingia kwa mfalme kuwaombea wayahudi rehema yeye mwenyewe alikuwa anakabiliwa na desturi isiyotanguliwa ambayo nayo ingemgharimu kifo, kulikuwa na sesturi nyingne ya kiajemi ya kuwa malikia kama hujaitwa kwa mfalme na kisha ukaingia kwa mfalme bila kibali chake ungehukumiwa kufa, isipokuwa tu kama utapata neema na kunyooshewa fimbo ya dhahabu, kupitia nguvu ya maombi haya Esta alipata kibali kwa mfalme na kunyooshewa fimbo ya dhahabu na kupata neema ya kuwaombea wayahudi na kuitangua sheria iliyokuwa imewekwa Esta 4:15-16Basi Esta akawatuma ili wamjibu Mordekai, Uende ukawakusanye Wayahudi wote waliopo hapa Shushani, mkafunge kwa ajili yangu; msile wala kunywa muda wa siku tatu, usiku wala mchana, nami na wajakazi wangu tutafunga vile vile; kisha nitaingia kwa mfalme, kinyume cha sheria; nami nikiangamia, na niangamie.” Ni baada ya tukio hili ndipo Mungu alipoleta wokovu kwa  wayahudi na Mordekai na matendo yake mema mema Mordekai yaliyokuwa yamekaliwa yalikumbukwa na msalaba aliokuwa ameandaliwa kutundikwa ulitundikwa Hamani adui yake na adui wa Wayahudi  Esta 9:1-21 . “Hata ulipofika mwezi wa kumi na mbili, ndio mwezi wa Adari, siku yake ya kumi na tatu, amri ya mfalme na mbiu yake ilipowadia kutekelezwa; ambayo siku ile adui za Wayahudi walitumaini kuwatawala, bali kumebadilika kinyume, hata Wayahudi waliwatawala wale waliowachukia; siku ile ile Wayahudi wakakusanyika mijini mwao katika majimbo yote ya mfalme Ahasuero ili kuwatia mikono wale watu waliowatakia hasara; wala asiweze mtu kuwazuia, kwa kuwa hofu yao imewaangukia watu wote. Nao maakida wa majimbo, na majumbe, na maliwali, na wale waliofanya shughuli ya mfalme, waliwasaidia Wayahudi; kwa sababu hofu ya Mordekai imewaangukia. Maana Mordekai alikuwa mkuu nyumbani mwa mfalme, na sifa yake imevuma katika majimbo yote, kwa kuwa huyo Mordekai amezidi kukuzwa. Basi Wayahudi wakawapiga adui zao wote mapigo ya upanga, na machinjo, na maangamizo, wakawatenda kama wapendavyo wale waliowachukia. Hata huko Shushani ngomeni Wayahudi wakawaua watu mia tano, na kuwaangamiza.  Wakawaua na Parshandatha, na Dalfoni, na Aspatha, na Poratha, na Adalia, na Aridatha, na Parmashta, na Arisai, na Aridai, na Waizatha, wana kumi wa Hamani bin Hamedatha, adui ya Wayahudi; walakini juu ya nyara hawakuweka mikono. Siku ile mfalme akaletewa hesabu ya hao waliouawa huko Shushani ngomeni. Mfalme akamwambia malkia Esta, Wayahudi wamewaua watu mia tano hapa Shushani ngomeni na kuwaangamiza, pamoja na wana kumi wa Hamani, je! Wamefanyaje basi katika majimbo ya mfalme yaliyosalia! Basi, una nini uombalo? Nawe utapewa; ama unayo haja gani tena? Nayo itatimizwa. Ndipo Esta aliposema, Mfalme akiona vema, Wayahudi walioko Shushani na wapewe ruhusa kufanya tena kesho sawasawa na mbiu ya leo, na hao wana kumi wa Hamani watundikwe juu ya mti ule. Mfalme akaamuru vifanyike vivyo hivyo, mbiu ikapigwa huko Shushani, wakawatundika wale wana kumi wa Hamani. Basi Wayahudi wa Shushani wakakusanyika tena siku ya kumi na nne pia ya mwezi wa Adari, wakawaua watu mia tatu huko Shushani; walakini juu ya nyara hawakuweka mikono. Nao Wayahudi wengine waliokaa katika majimbo ya mfalme walikusanyika, wakazishindania maisha zao, wakajipatia raha mbele ya adui zao, wakawaua waliowachukia, watu sabini na tano elfu; walakini juu ya nyara hawakuweka mikono. Hii ndiyo siku ya kumi na tatu ya mwezi wa Adari; na siku ya kumi na nne ya mwezi huo wakapumzika, wakaifanya kuwa siku ya karamu na furaha. Lakini Wayahudi wa Shushani walikusanyika siku ya kumi na tatu ya mwezi huo, na siku ya kumi na nne pia; na siku ya kumi na tano ya mwezi uo huo wakapumzika, wakaifanya kuwa siku ya karamu na furaha. Kwa sababu hii Wayahudi wa vijijini, wakaao katika miji isiyo na boma, huishika siku ya kumi na nne ya mwezi wa Adari, kuwa siku ya furaha na karamu, sikukuu ya kupelekeana zawadi. Basi Mordekai aliyaandika mambo hayo; naye akapeleka barua kwa Wayahudi wote waliokaa katika majimbo yote ya mfalme Ahasuero, waliokuwa karibu na waliokuwa mbali, kuwaonya wazishike siku ya kumi na nne ya mwezi wa Adari, na siku ya kumi na tano yake, mwaka kwa mwaka,” Unaona kilio cha wayahudi kilibadilika kuwa furaha adui za wayahudi waliuawa wao, msalamba walikuwa wameutundika hamani kwaahiji ya Mordekai alitundikwa yeye mwenyewe, Heshima aliyokuwa akiitafuta Hamani ilipotea na Heshima ile alipewa Mordekai Esta 5:14, 6:1-2, Mfalme hatimaye aliongeza wema wake kwa wayahudi Esta 7. Mungu na kuongezee wema ikiwa utakubali kujitia chini yake na kuutafuta uso wake kwa kufunga.

Ndugu yangu mpendwa muamini Mungu yaamini maandiko huitaji kuhangaika dhidi ya adui zako ndani yako uko uwezo, unaozidi nguvu ya wadhalimu, unaozidi nguvu ya wachonganishi unaozoidi nguvu ya ibilisi, unaozidi nguvu za wanafiki, unaozidi nguvu za waganga na wachawi, unaozidi nguvu za maadui zako iko furaha uliyoandaliwa unayo ya kuingia kwa mfalme kinyume cha sheria na kukata rufaa, pale nguvu zetu zoinapopungua, pale kanisa linap[olemewa pale ibilisi na adui anapotukalia langoni iko dawa moja tu kwa kufunga na kuomba tutaweza kumsambaratisha adui na kupata kibali kwa mfalme na kutangua sheria yoyote inayotenda kazi kinyume na maisha yako; ni kwa kufunga na kuomba ni kwa kufunga na kuomba ni kwa kufunga na kuomba tunaweza kulete furaha ya kweli katima maisha yetu asomaye na afahamu.

Na mkuu wa wajenzi mwenye Hekima.

Rev. Innocent Kamote.

Mariam mama yake Bwana Yesu!




Mstari wa Msingi: Luka 1:26-33Mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na Mungu kwenda mpaka mji wa Galilaya, jina lake Nazareti, kwa mwanamwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu, jina lake Yusufu, wa mbari ya Daudi; na jina lake bikira huyo ni Mariamu. Akaingia nyumbani kwake akasema, Salamu, uliyepewa neema, Bwana yu pamoja nawe. Naye akafadhaika sana kwa ajili ya maneno yake, akawaza moyoni, Salamu hii ni ya namna gani? Malaika akamwambia, Usiogope, Mariamu, kwa maana umepata neema kwa Mungu.  Tazama, utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; na jina lake utamwita Yesu. Huyo atakuwa mkuu, ataitwa Mwana wa Aliye juu, na Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi, baba yake. Ataimiliki nyumba ya Yakobo hata milele, na ufalme wake utakuwa hauna mwisho
 

 


Maana ya jina Mariam.

Jina Mariam au Maria limetokana na jina la Kiyunani Maria na kwa kiaram Maria, kwa kiibrania Miriam kwa kiarabu Maryam ni Jina maarufu sana katika maandiko ya Kikristo na Kiislamu, Mariam ni mwanamke anayesadikiwa kuwa alibarikiwa sana kutokana na kupata neema ya Kumzaa mwokozi wa Ulimwengu yaani Bwana Yesu Kristo (Masihi). Jina hili Mariam maana yake ni mtumishi wa Mungu!

Mariam anatajwa kama mwanamke aliyekuwa mwanamwali yaani Bikira aliyekuwa anakaribia kuolewa au aliyekuwa amechumbiwa anasifiwa kwa sifa kubwa ya kuwa mwanamke mwaminifu aliyejitunza na mnyenyekevu aliyekuwa na uelewa wa juu sana kuhusu Neno la Mungu na Mapenzi ya Mungu. Mwanamke huyu alikuwa na asili ya ukoo wa Daudi ingawa aliishi Galilaya katika mji mdogo wa Nazareth kama yanenavyo maandiko yaani Agano jipya na Quran

Mwanamke huyu shujaa anatwaja na maandiko yote agano jipya na Quran kwamba alikuwa Bikira na alikuwa amebakiza muda tu wa kufungishwa ndoa kwa Yusufu ambaye naye pia alikuwa wa ukoo wa Mfalme Daudi, Bikira wa aina hii aliitwa PARTHENOS kwa kiyuinani yaani mwana mwali, aliyekuwa tayari kwa kutimiza tu ibada ya ndoa, alionekana kuwa ana mimba ni mimba ambayo vitabu vitakatifu vinaeleza wazi kuwa haikutokana na uashetari wala mbegu za kiume za mwanamume awaye yote, bali zilitokana na muujiza wa kiungu sawasawa na jinsi alivyotabiri nabii Isaya “TAZAMA BIKIRA ATACHUKUA MIMBA NAYE ATAZAA MWANA WA KIUME NAYE WATAMUITA JINA LAKE IMANUEL YAANI MUNGU PAMOJA NASI” 

Isaya 7:14Kwa hiyo Bwana mwenyewe atawapa ishara. Tazama, bikira atachukua mimba, atazaa mtoto mwanamume, naye atamwita jina lake Imanueli.”

Tukio hili halikuweza kumuumiza Yusufu kwa vile alikuwa na uelewa mpana wa Mapenzi ya Mungu aidha malaika wa bwana mjumbe wa Mungu Gabriel alimtokea na kumpa ufafanuzi kuhusu ujauzito huo, ni kutokana na hali hii Mariam aliambatana na Yusufu mpaka Bethelehemu kwaajili ya kuhesabiwa kutokana na amri ya Kaisari Augusto kwamba wahesabiwe watu wa utawala wake kila mmoja kwao na kwa vile Yusufu na Mariamu kwa asili ni watu wa Bethelehemu huko Uyahudi walikwenda huko ili wahesabiwe na kwa bahati nzuri Masihi alizaliwa huko, ili kutimiza Unabii wa Mika katika Mika 5:2 kwamba “Bali wewe, Bethlehemu Efrata, uliye mdogo kuwa miongoni mwa elfu za Yuda; kutoka kwako wewe atanitokea mmoja atakayekuwa mtawala katika Israeli; ambaye matokeo yake yamekuwa tangu zamani za kale, tangu milele.

Mwanamke huyu maarufu anatajwa kama mara 50 hivi katika injili, Quran imempa Sura maalumu iitwayo Surat al  Maryam  na inasemekana Quran inamtaja mara nyingi zaidi kama mwanamke mtakatifu katika Quran Maryam ametajwa mara 70

Mariam alitokewa Malaika Gabriel na kuelezwa rasmi kuwa amechaguliwa na Mungu kuwa mama wa Masihi, ni mwanamke mwenye uwezo mkubwa sana wa kuvumilia kwani licha ya kuwa na mtoto mwema mno kama Yesu injili imethibitisha kuwa alikuwepo wakati mwanae anasulubiwa na kuuawa kwaajili ya dhambi za ulimwengu hili lilikuwa ni tukio chungu sana na lilihitaji kuyajua mapenzi ya Mungu hasa na kwa uwazi Mariamu huenda katika kipindi hiki alikumbuka maneno ya nabii mzee aliyeitwa simeon ambaye aliahidiwa na Mungu kuwa hatakufa mpaka atakapomuona Masihi mzee huyu alimweleza maneno mazito Mariamu kumuandaa tayari kwa machungu ya kusulubiwa kwa mwanae miaka michache ijayo. 

Luka 2:21-35Hata zilipotimia siku nane za kumtahiri, aliitwa jina lake Yesu; kama alivyoitwa na malaika kabla hajachukuliwa mimba. Kisha, zilipotimia siku za kutakasika kwao, kama ilivyo torati ya Musa walikwenda naye hata Yerusalemu, wamweke kwa Bwana, (kama ilivyoandikwa katika sheria ya Bwana, Kila mtoto mwanamume aliye kifungua mimba ya mamaye na aitwe mtakatifu kwa Bwana), wakatoe na sadaka, kama ilivyonenwa katika sheria ya Bwana, Hua wawili au makinda ya njiwa wawili. Na tazama, pale Yerusalemu palikuwa na mtu, jina lake Simeoni, naye ni mtu mwenye haki, mcha Mungu, akiitarajia faraja ya Israeli; na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake. Naye alikuwa ameonywa na Roho Mtakatifu ya kwamba hataona mauti kabla ya kumwona Kristo wa Bwana. Basi akaja hekaluni ameongozwa na Roho; na wale wazazi walipomleta mtoto Yesu ndani, ili wamfanyie kama ilivyokuwa desturi ya sheria, yeye mwenyewe alimpokea mikononi mwake, akamshukuru Mungu, akisema, Sasa, Bwana, wamruhusu mtumishi wako, Kwa amani, kama ulivyosema;  Kwa kuwa macho yangu yameuona wokovu wako, Uliouweka tayari machoni pa watu wote; Nuru ya kuwa mwangaza wa Mataifa, Na kuwa utukufu wa watu wako Israeli. Na babaye na mamaye walikuwa wakiyastaajabia hayo yaliyonenwa juu yake. Simeoni akawabariki, akamwambia Mariamu mama yake, TAZAMA, HUYU AMEWEKWA KWA KUANGUKA NA KUINUKA WENGI WALIO KATIKA ISRAELI, NA KUWA ISHARA ITAKAYONENEWA. NAWE MWENYEWE, UPANGA UTAINGIA MOYONI MWAKO, ili yafunuliwe mawazo ya mioyo mingi.”

Mariamu hata baada ya kufufuka kwa Yesu alijiunga na wanafunzi wa kanisa la kwanza pale Yerusalem na maandiko yanamtaja kuwa aliungana katika maombi na wanafunzi na alikuwa miongozi mwa watu 120 waliojazwa Roho Mtakatifu japo kwa Mariamu huenda tukio hilo lilikuwa likijirudia kwa mara nyingine kwani Raoho wa Mungu alikuwa juu yake mapema zaidi ili aweze kukabidiwa jukumu la Kumbeba Bwana Yesu.

Kwa mujibu ya masimulizi ya kihistoria hasa ya wakatoliki na makanisa ya Othodox wanaamini kuwa mwili wake ulinyakuliwa Mbinguni moja kwa moja lakini swala hili linaitwa “Assumption” yaani inasadikiwa tu lakini hakuna uthibitisho wa moja kwa moja, Masimulizi mengine yanaeleza kuwa huenda alikuweko mpaka mwaka wa 70 AD wayahudi walipotawanywa na kupoteana na kutokuweko kwa uhakika kuwa ni wapi alifia, Mtume Yohana alipewa jukumu la kumlea Mariam lakini hata hivyo hajawahi kueleza lolote kuhusu Mwisho wake aidha baadhi ya wanawe kama Yuda aliyeandika waraka na Yakobo pia  ndugu zake bwana hawajawahi kueleza lolote kuhusu mama yao.
Mariamu anaheshimika na watu wengi sana na mamilioni ya watu wanaamini kuwa ni moja ya watakatifu muhimu sana katika dini, wengine wanaamini kuwa amewahi kuwatokea kimuujiza katika karne kadhaa, makanisa ya Othodox na Catholic na Anglican na Lutheran yanaamini kuwa kwa kuwa yesu ni Mungu na alizaliwa na Mariam basi Mariamu ni mama wa Mungu, baadhi ya mashirika ya kikatoliki kama Marian wao wanaamini na kumuita kuwa ni mama wa Mungu na wanaamini kuwa hata yeye kama ilivyo kwa yesu Kristo hakuwa na dhambi na kuwa alizaliwa pasipokuwa na dhambi, siwezi kusema lolote katika hili lakini ukweli ni kuwa Quran pia imemkubali sana Maryam na kuonyesha heshima kubwa sana juu yake akitetewa kuwa hakuwa na dhambi tofauti na mama wa Muhamad ambaye hatajwi kabisa katika kitabu hichi ukicha khadithi.

Pamoja na ubora wote huu kuhusu Mariamu na utakatifu wake kwetu sisi na kwangu mimi Mariamu ni mtakatifu kama walivyo watakatifu wote katika biblia, nakubali kuwa Yesu alimuheshimu sana mama yake lakini vilevile sisi nasi tunamuheshimu sana na kama mbingu zilivyomuheshimu sana kuwa ni Mtakatifu hilo hatuna mashaka nalo, kila mtu anaweza kuwa kama Mariamu tu kama tukiyashika maneno ya Mungu Yesu alisema “MAMA NA NDUGU ZANGU NI AKINA NANI? NI WALE WANAOLISIKIA NENO LA MUNGU NA KULISHIKA”  ni imani yangu pia kuwa furaha atakayokuwa nayo Mariamu inaweza kuwa furaha ya kila mmoja anayelisikia neno la Mungu na kulishika Yesu akasema  alipoulizwa ni furaha gani aliyonayo mwanamke aliyekuzaa na kukulea alijibu AMA NI FURAHA GANI WALIYONAYO WANAOLISIKIA NENO LA MUNGU NA KULITII” 

Katika kitabu cha matendo Mariamu anaonekana akiwa muombaji sawa na waombaji wengine kama Petro na wengineo, mariamu amebarikiwa hatuna shaka na hilo, Mariamu ytuko mbinguni kama watakatifu wengine hatuna shaka na hilo, Lakini Mariamu sio njia na kweli na uzima, yeye sio njia ya kumfikia Mungu aliye hai, yeye sio njia ya kutumika kutuombea kwa baba mbinguni, yeye sio mama wa Mungu, wala sio mke wa Mungu, yeye aliendelea kuwa mke wa Yusufu na alizaa watoto sita zaidi ukiacha Yesu mwanawe wa kwanza aliyemzaa kwa muujiza soma Mathayo 13:54-56Na alipofika nchi yake, akawafundisha katika sinagogi lao, hata wakashangaa, wakasema, Huyu amepata wapi hekima hii na miujiza hii? Huyu si mwana wa seremala? Mamaye si yeye aitwaye Mariamu? Na nduguze si YAKOBO, NA YUSUFU, NA SIMONI, NA YUDA? Na MAUMBU  (Dada zake) yake wote hawapo hapa petu? Basi huyu amepata wapi haya yote?”

Kama u mwanafunzi wa Biblia utaona wazi kuwa ndugu zake Yesu wametajwa katika Biblia Yakobo. Yusufu, Simoni na Yuda yaaninkaka wane na neno maumbu maana yeke dada zake ambao inakisiwa walikuwa wawili hivyo jumla ya wana wa Mariamu ni Saba na aliozaa na Yusufu ni sita, so kama Mariamu ni mama wa Mungu basi pia ni mama wa wanadamu! Kumbuka ni Yesu pekee ndie alikuwa mwana wa miujiza na yusufu aliendelea kuzaa na kufurahia maisha yake na Mariam inasadikiwa tu kuwa Yusufu alifariki mapema zaidi.

Wakati watu wanakazania kumuomba Mariamu ni muhimu kujikumbusha kuwa Mariamu alikuwa akimuomba Yesu pamoja na wanafunzi wake aliungana nao katika maombi Matendo ya Mitume 1:12-14Kisha wakarudi kwenda Yerusalemu kutoka mlima ulioitwa wa Mizeituni, ulio karibu na Yerusalemu, wapata mwendo wa sabato.Hata walipoingia, wakapanda orofani, walipokuwa wakikaa; Petro, na Yohana, na Yakobo, na Andrea, Filipo na Tomaso, Bartholomayo na Mathayo, Yakobo wa Alfayo, na Simoni Zelote, na Yuda wa Yakobo. Hawa wote walikuwa wakidumu kwa moyo mmoja katika kusali, pamoja nao wanawake, na Mariamu mama yake Yesu, na ndugu zake.” Unaona Mariamu mama yake Yesu na ndugu zake walikuwa miongoni mwa watu waombaji waliokuwa wakimuomba Mungu kwa jina la Yesu, dhana inayojengwa na baadhi ya watu wanaotaka kupotoshja maandiko wakisema kuwa Mariamu ni muombezi wanajenga hoja kupitia muujiza wa kana ya Galilaya wakati Yesu alipohudhuria harusini na kisha watu wakatindikiwa na Divai, Mariamu alikuja kumuomba Yesu na kumpa taarifa ya kutoikuweko kwa Divai Yesu hakukubali kwa urahisi kwani mariamu alitaka Yesu atumie uwezo wake wa kimuuijiza kabla ya wakati wa Mungu, hata hivyo alimuomba kwa imani na kuwagiza wanafunzi wake kuwa atakalowaagiza walifanye dhana hii haitufundishi kumuomba mariamu aku kumfanya mariamu kuwa ni muombezi bali inatufundisha kuwa tukiwa na uhitaji wowote ni lazima tumweleze Bwana yesu kwa imani naye ataenda Yohana  2:1-9Na siku ya tatu palikuwa na arusi huko Kana, mji wa Galilaya; naye mama yake Yesu alikuwapo. Yesu naye alikuwa amealikwa arusini pamoja na wanafunzi wake. Hata divai ilipowatindikia, mamaye Yesu akamwambia, Hawana divai. Yesu akamwambia, Mama, tuna nini mimi nawe? Saa yangu haijawadia. Mamaye akawaambia watumishi, Lo lote atakalowaambia, fanyeni. Basi kulikuwako huko mabalasi sita ya mawe, nayo yamewekwa huko kwa desturi ya Wayahudi ya kutawadha, kila moja lapata kadiri ya nzio mbili tatu. Yesu akawaambia, Jalizeni mabalasi maji. Nao wakayajaliza hata juu. Akawaambia, Sasa tekeni, mkampelekee mkuu wa meza. Wakapeleka. Naye mkuu wa meza alipoyaonja yale maji yaliyopata kuwa divai, (wala asijue ilikotoka, lakini watumishi walijua, wale walioyateka yale maji),” 

Ni muhimu kufahamu kuwa Yesu Kristo ni Mkuu kuliko Mariam, neema aliyopewa Mariamu ilikuwa ni kushiriki Baraka kubwa ya kumleta masihi Duniani, Lakini Mungu hajamfanya Mariamu kuwa mwombezi kwa sababu zozote zile Makuhani waombezi wote katika uyahudi walikuwa wanaume, Mariamu hakuwa nabii kama ilivyokuwa kwa Miriam wa agano la kale aliyekuwa Dada wa Musa na Haruni,  alikuwa ni mwanamke shujaa jasiri na mwenye imani katika kutunza neno na ahadi za Mungu, Mungu hajawahi kumfanya Mariamu kuwa malkia wa Mbinguni wala hajawahi kumfanya mariamu kuwa sehemu ya ibada, Mariam atasikitika sana kama atarudi duniani na kukuta akuombwa na kuabudiwa kama Mungu kwa unyenyekevu aliokuwa nao angeshangaa kukuta kufuru hii.

Njia pekee ya kumfikia Mungu ni Yesu naye ndiye kipatanisho pekee kati ya Mungu na wanadamu, 1Yohana 2:1-2Watoto wangu wadogo, nawaandikia haya ili kwamba msitende dhambi. Na kama mtu akitenda dhambi tunaye Mwombezi kwa Baba, Yesu Kristo mwenye haki, naye ndiye kipatanisho kwa dhambi zetu; wala si kwa dhambi zetu tu, bali na kwa dhambi za ulimwengu wote.” 

Unapotumia Muda wako kumuomba Mungu kupitia Mariamu unapoteza lengo la maombi yako huku ukiwa na nia nzuri lakini sio ya kimaandiko ni vema dua zetu na maombi yetu tukamuombababa wa Mbinguni kwa njia ya mwanae Yesu Kristo pekee

Yohana 16:23-24Tena siku ile hamtaniuliza neno lo lote. Amin, amin, nawaambia, Mkimwomba Baba neno lo lote atawapa KWA JINA LANGU.  Hata sasa hamkuomba neno KWA JINA LANGU; ombeni, nanyi mtapata; furaha yenu iwe timilifu.”
 
Wengi hawana furaha hawajawahi nkufurahia uwepo wa Mungu na utendaji wa Mungu kwa sababu hawajawahi kuomba kwa jina la Yesu wamedanganywa na kudanganyika wakiomba kupitia majina mengine Yesu Mwenye yu ashauri hivi Yohana 14:13-14Nanyi mkiomba lo lote kwa jina langu, hilo nitalifanya, ili Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Mkiniomba neno lo lote kwa jina langu, nitalifanya”: ni jambo la kusikitisha sana katika Karne hii ya uwazi na ukweli yautafiti na ujuzi ya hekima na maarifa neno la mungu liko wazi kila mahali bado kuna watu wanatumia jina la Mariamu katika maombezi, ni malizie kwa kusema kuwa Roho Mtakatifu ndiye anayetuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa.

Kama hujui kuomba ruhusu Roho Mtakatifu akufundisha kuomba maana yeye ndio muombezi mkuu na sio Mariamu Warumi 8:26-27 “Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa. Na yeye aichunguzaye mioyo aijua nia ya Roho ilivyo, kwa kuwa huwaombea watakatifu kama apendavyo Mungu.” 

Ni imani yangu kuwa utaifahamu kweli nayo itakuweka Huru katika jina la Yesu Kristo aliye hai amen!

Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima       

Ijumaa, 16 Februari 2018

Je ! Mifupa hii yaweza kuishi?



Mstari wa Msingi: Ezekiel 37:1-3 “.Mkono wa Bwana ulikuwa juu yangu, naye akanichukua nje katika roho ya Bwana, akaniweka chini, katikati ya bonde; nalo limejaa mifupa; akanipitisha karibu nayo pande zote; na tazama, palikuwa na mifupa mingi katika ule uwanda! Nayo, tazama, ilikuwa mikavu sana.  Akaniambia, Mwanadamu, je! Mifupa hii yaweza kuishi? Nami nikajibu, Ee Bwana MUNGU, wajua wewe”.


Je! mifupa hii yaweza Kuishi?
Utangulizi:

Ni muhimu kufahamu kuwa Wana wa Israel walikuwa wameokolewa na Mungu kwa uweza mkubwa sana wote tunakumbuka jinsi Mungu alivyomuadhibu farao kwa mapigo mazito chini ya mkono wa Mtumishi wake Musa na Haruni, mpaka Mungu alivyojipatia taifa na kulistawisha katika nchi ya mkanaani na kuwa na ustawi mkubwa sana chini ya waamuzi na wafalme. Hata hivyo ni jambo la kusikitisha kuwa baada ya muda mfupi, walimuacha Mungu na kuabudu miungu na kumpuuzia Mungu aliyewaokoa, ukweli ni kuwa walisahau historia nzima na kugeukia njia zao, Hivyo Mungu aliruhusu waweze kwenda utumwani tena.

Mwaka kama wa 722BK na 586BK  Mungu aliruhusu Israel kuchukuliwa uhamishoni na Yuda kuchukuliwa uhamishoni Babeli chini ya utawala wa mfalme Nebuchadnezer, Jeshi la Nebuchadnezer liliizingira Yerusalem na kuharibu na kusambaratisha vibaya Hekalu lililokuwako Yerusalem na kulichoma moto kuwa majivu, na wayahudi walichukuliwa kwenda Utumwani Babeli, hiki ndio kilikuwa kifo cha Taifa hili na mwisho wa matumaini yao. Huu ulikuwa ni msiba mkubwa sana ambao haukuwa na matumaini ya kuupoza.

Daniel 1:1-4 “Katika mwaka wa tatu wa kumiliki kwake Yehoyakimu, mfalme wa Yuda, Nebukadreza mfalme wa Babeli,alikwenda Yerusalemu akauhusuru.Bwana akamtia Yehoyakimu, mfalme wa Yuda, katika mkono wake, pamoja na baadhi ya vyombo vya nyumba ya Mungu; naye akavichukua mpaka nchi ya Shinari, mpaka nyumba ya mungu wake; akaviingiza vile vyombo katika nyumba ya hazina ya mungu wake.  Mfalme akamwambia Ashpenazi, mkuu wa matowashi wake, awalete baadhi ya wana wa Israeli, wa uzao wa kifalme, na wa uzao wa kiungwana;  vijana wasio na mawaa, wazuri wa uso, wajuzi wa hekima, werevu kwa sababu ya maarifa yao, wenye kufahamu elimu, watakaoweza kusimama katika jumba la mfalme; tena alimwambia awafundishe elimu ya Wakaldayo, na lugha yao.    

Katika wakati huu watu wazuri na vijana wazuri na kila kitu kizuri kilichukuliwa utumwani Yerusalem ilibaki ukiwa huku kukiwa hakuna matumaini tena, Ezekiel nabii alikuwa ni miongozi mwa watu waliochukuliwa utumwani kwa mujibu wa historia.

Ni katika wakati huu sasa Ndipo Mungu alimwambia nabii Ezekiel katika maono aweze kuangalia bonde hili lisilo na matumaini, bonde lenye umauti usio na tumaini la kurejea tena na mifupa ilikuwa imetapakaa na ni mikavu hakukuwa na matumaini ya uhai na ndipo Mungu alipomuuliza Ezekiel swali hili Je mifupa hii mikavu yaweza kuishi?

Kwa ukweli maono haya yalikuwa yanalihusu Taifa la Israel kwa wakati huo kwa sababu walikuwa wamekata tamaa, walikuwa wamepoteza tumaini, waliona mauti na kujihisi kuwa ni kama wamekatiliwa mbali Ezekiel 37:11Kisha akaniambia, Mwanadamu, mifupa hii ni nyumba yote ya Israeli; tazama, wao husema, Mifupa yetu imekauka, matumaini yetu yametupotea; tumekatiliwa mbali kabisa.”ni kweli kuwa hakukuwa na namna na jinsi ya kujiokoa kutoka katika msiba huo, kwani watu wengi waliuawa na wengine walichukuliwa kwenda utumwani , Israel iilikuwa tayari limegeuka kuwa bonde lisilo na uhani, na ni lenye mauti sisyo na matumaini hii ilikuwa ni picha ya kukosekana kwa matumaini.

Tukio la jinsi hii lilijirudia tena Israel waliporudi tena kutoka utumwani, walipata Hekalu na Yesu alikuja lakinimnamo mwaka wa 70 hivi walitawanywa kotekote uhamishoni duniani na hakukuwa na matumaini tena na hekalu lilibomolewa lakini ilipofika 1948 Israel ilipata uhuru wake na kufanyika taifa tena Mungu ni mwaminifu kwa watu wake Historia inatushuhudia.

Hali hii sio tu kuwa ilikuwa inaihusu Israel wakati ule, lakini inawezekana ikawa inatuhusu sisi nasi katika siku hii ya leo, inawezekana uko mahali hapa unaisikia sauti hii, au unasoma makala hii, lakini ukiwa katika hali ya uzuni nzito inayokukabili, moyoni mwako ukiwa umepoteza matumaini, huoni nuru mbele matumaini yako yamepotea, una vyeti kadhaa vya madaktari, una shuhuda kadhaa za watu wenye tatizo kama lako na wote mmeambia kuwa tatizo lako haliwezekani, inawezekana ni wachawi wameharibu ukoo wenu, ni adui zako wamesema wale tumewaweza kwa hali hii hawachomoki tena, hawainuki tena uko katika giza nene, inawezekana watu wakakuona una-smile lakini Moyoni huna amani ya kweli, moyoni ni misiba, moyoni ni kukavu, hufurahii uwepo wa Bwana, unalia kilio cha ndani unajiuliza matumaini yatatokea wapi? Unajiuliza kehso itakuwaje? Unajiuliza nawezaje kukabiliana na aibu hii? Kila kitu kimesambaratika hakuna matumaini ya kusimama tena, ndoto zako zimeyeyuka? Mambo unayotaka ni kama hayaendi?

Namshukuru Mungu kwa Jibu alilolitoa Ezekiel 37:3bNami nikajibu Ee Bwana Mungu wajua wewe.” Ezekiel yuko katika Bonde lililojaa mifupa mikavu tena iliyotawanyika na kwaakili za kibinadamu hakuna uwezekano wa kuweko uzima wala ufufuo, ni vigumu kukubali hali halisi ya uzima hapa ni vigumu hata kufariji we ungejibuje swali kama hili, Lakini jibu la nabii Ezekiel linaonyesha kwa sehemu alijua kuwa Mungu anaweza kuwa anaelewa zaidi.

Ezekiel ni kama alikuwa anajua kuwa Mungu anaelewa zaidi, ni yeye pekee anayeweza kuingilia kati na kufanya kitu katika mazingira ambayo akili ya mwanadamu imefika mwisho, Ezekiel alikuwa anajua kuwa Mungu anaweza kufanya lolote analolitaka, kwa Mungu hakuna linaloshindikana, Mungu akitaka mifupa hii mikavu iiishi itaishi.

Mungu amenituma leo nikutangazie kuwa yasiyowezekana kwa wanadamu, Kwa Mungu yanawezekana kwake liko tumaini kubwa sana na hupaswi kukata tamaa, kila matumaini yanayofifia katika moyo wako na ndoto zako Bwana anaweza kukuinua tena Ee bwana Mungu wajua wewe ilikuwa ni sauti ya Ezekiel akimjibu Mungu ashukuriwe Mungu Ezekiel hakusema haiwezekani, lakini alisema Mungu anajua liko tumaini katika yeye, atakufufua tena atakupa uhai, kama alivyoipa Israel uhai, wa kisiasa na kiroho na kuliponya taifa lile na kulilinda hata liko tena leo.

Mungu atakuinua tena, Simama tena changamka usikae chini na kusikitika kuwa itakuwaje iko pumzi ya uhai leo, Bwana atakuganga kwa upya, kila kilicho na uhai na kisicho na uhai kinasikia neno la Mungu leo neno la Mungu linakuja kwako kama pumzi ya uhai nawe utajua ya kuwa Bwana ndiye Mungu Ezekiel 37:4-6Akaniambia tena, Toa unabii juu ya mifupa hii, uiambie, Enyi mifupa mikavu, lisikieni neno la Bwana. Bwana MUNGU aiambia mifupa hii maneno haya; Tazama, nitatia pumzi ndani yenu, nanyi mtaishi. Nami nitatia mishipa juu yenu, nami nitaleta nyama iwe juu yenu, na kuwafunika ngozi, na kutia pumzi ndani yenu, nanyi mtaishi; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana.” 

Nakuomea ili kwamba Bwana afufue na kurejeza matumaini yako kila yanakoonekana kufifia aku kufa katika jina la Yesu Kristo wa Nazareth aliye hai.

Ni matumaini yangu kuwa umebarikiwa na ujumbe huu ningependa kupata maoni yako kama ujumbe huu umekubariki, na ni imani yangu utakubariki, au utabariki washirika wako usisite kumshukuru Mungu japo kwa ujumbe was sms

Rev. Innocent Kamote.

Mkuu wa Wajenzi mwenye Hekima.

0718990796