Jumatatu, 5 Machi 2018

Njia za kurahisisha Maisha yako!


Andiko la Msingi: Mathayo 6:25 -27Kwa sababu hiyo nawaambieni, Msisumbukie maisha yenu, mle nini au mnywe nini; wala miili yenu, mvae nini. Maisha je! Si zaidi ya chakula, na mwili zaidi ya mavazi? Waangalieni ndege wa angani, ya kwamba hawapandi, wala hawavuni, wala hawakusanyi ghalani; na Baba yenu wa mbinguni huwalisha hao. Ninyi je! Si bora kupita hao?  Ni yupi kwenu ambaye akijisumbua aweza kujiongeza kimo chake hata mkono mmoja?”



Na maisha ya nini kuyasumbukia!

Nyakati hizi tulizonazo ni nyakati ambazo ni ngumu sana kimaisha, watu wengi sana wanaishi maisha ya huzuni yasiyo na furaha na yaliyojawa na wingi wa migandamizo ya maisha, siku inaweza kupita na ukajikuta hakuna ulichokamilisha kila wakati unafikiri labda utapata siku nzuri ambayo unaweza kukamilisha maswala yako yote muhimu unayotaka kuyakamilisha,  lakini mambo sivyo yalivyo, watu wengi wa kizazi hiki wamekuwa busy na maisha lakini ni wachache wanaofurahia kuwa busy kwao, kwa mtindo huu utaweza kugundua kuwa Maisha yanakuwa magumu na muda unakuwa hautoshi, Hakuna wa kulaumiwa muda wako unapokuwa hautoshi, unapokuwa umekusudia kufanya mambo mengi lakini mwisho wa siku unajikuta hakuna hata moja ulilolikamilisha, unaweza hata kumlaumu Mungu unaweza kufikiri kuwa muda hautoshi kumbuka  hivyo sivyo maisha yanavyopaswa kuwa; Yesu alikusudia watu wake waishi maisha mepesi yasiyo na mizigo mizito wala hofu wala kongwa la utumwa! 

Ni muhimu kufahamu kuwa Yesu alikusudia watu waishi maisha yaliyojaa pumziko na raha nafsini mwao na ili mtu aweze kufurahia maisha hana budi kuzingatia maswala muhimu ya kibiblia na mafundisho ya Yesu juu ya kuishi kwa raha bila usumbufu wa aina yoyote Mathayo 11:28-29Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha. Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;”

Kama mungu alikusudia watu wawe na furaha wasiwe na Mizigo, wasielemewe wasisumbuke kwanini watu wengi wanasumbuka leo na kuishi maisha ya kujichosha? Yesu alihoji ni nani kwenu ambaye kwa kujisumbua aweza kuongeza kimo chake hata mkono mmoja? Mungu anatufundisha katika neno lake jnsi na namna ya kuishi kwa furaha? Yafuatayo yatatusaidia kuishi maisha rahisi na kujikuta tunafurahi bila kuelemewa na lolote

1.       Fanya jambo moja tu kwa wakati.

Mathayo 6: 24 “Hakuna mtu awezaye kutumikia mabwana wawili; kwa maana atamchukia huyu, na kumpenda huyu; ama atashikamana na huyu, na kumdharau huyu. Hamwezi kumtumikia Mungu na mali.Ingawa mstari huu unaweza kuwa na maana pana nyingi lakini moja ya maana rahisi anayotaka kuikazia Yesu Kristo ni kuwa kuna mafanikio ya kufanya jambo moja kwa wakati mmoja kuliko kutamani kufanya mambo mengi kwa wakati mmoja, watu wengi wanaojichosha katika maisha na kujikuta muda hautoshi na wanaamka wakiwa wamechoka ni wale wanaotaka kufanya mambo mengi kwa wakati mmoja, akili yetu inapokuwa katika jambo lingina na mikono yetu ikitenda kitu kingine maisha yatakuwa magumu na tunaweza kumaliza siku hakuna ulichokamilisha!

Wataalamu wa mapishi wanasema kuwa unaweza kutenganisha kiini cheupe cha yai na kiini cha manjano cha yai na ukavitumia kwa matumizi fulani ya mapishi yaliyo mazuri, lakini hata hivyo utapoteza muda na ni vigumu kuliko kama utavuruga yai lote na kulila moja kwa moja.

Mwanafunzi amabaye anakusudia kufanya au kujisomea masomo mengi kwa wakati mmoja wa maandalizi hawezi kuwa na ufanisi kama yule anayefanya moja baada ya jingine, mwanafunzi ambaye atakuwa na simu ya mkononi, yenye kila kitu huku anasoma atapoteza mwelekeo hata kama ni mzuri kiasi gani, mwanafunzi anayeshiriki Mapenzi huku anasoma, atapoteza mwelekeo, kwa kanuni ya Yesu huwezi kutumikia mabwana wawili, fanya jambo moja kwanza Mungu hataki ujisumbue Wafilipi 4:6 “Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.” Jaribu kufanya jambo moja tu kwa wakati mmoja na utaweza kuona unafanikiwa na kuyafurahia maisha, na kisha pumzika. Hutachanganyikiwa wala hutalala na stresses.

Mungu aliifurahia kazi yake ya uumbaji aliyokuwa akiifanya na kuikamilisha kwa siku ile ile, kila siku alitimiza wajibu wa uumbaji fulani na alipokamilisha alifurahi na kupumzika Mwanzo 1:3-4, Mungu akasema, Iwe nuru; ikawa nuru. Mungu akaiona nuru, ya kuwa ni njema;” Mungu akatenga nuru na giza. kila kitu alikuwa akikikamilisha na kujipongeza siku moja baada ya nyingine hivyo kwa siku sita ulimwengu uliumbwa

2.       Usiogope kuhusu kesho?.

Mathayo 6:34 “Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake.” Mungu anatutarajia tumuamini katika kiwango ambacho hatutaogopa kuhusu kesho itakuwaje, aliwafundisha wana wa Israel kutokuogopa maisha yao kwamba itakuwaje kesho kwani kila siku alikuwa amewaandalia riziki yao, hii haimaanishi kuwa tusiweke akiba, hii haimaanishi kuwa tutumie vibaya kile tulicho nacho, hapana hapa Mungu anatufundisha kwamba tusiogope kesho itakuwaje, watu wanaoogopa kesho itakuwaje wanaishi maisha ya taabu sana  nay a kujitesa na hivyo wanaweza kukosa raha, Mungu aliwafundisha Israel Jangwani kwamba mtu hataishi kwa mkate tu, bali kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu, Kutoka 16: 15-21Wana wa Israeli walipokiona, wakaambiana, Nini hiki? Maana hawakujua ni kitu gani. Musa akawaambia, Ndio mkate ambao BWANA amewapa ninyi, mle. Neno hili ndilo aliloagiza BWANA, Okoteni ninyi kitu hicho kila mtu kama ulaji wake ulivyo; kichwa pishi, kama hesabu ya watu wenu ilivyo; ndivyo mtakavyotwaa, kila mtu kwa ajili ya hao walioko hemani mwake.Wana wa Israeli wakafanya hivyo, wakaokota wengine zaidi, wengine kupungua. Nao walipoipima kwa pishi, yeye aliyekuwa ameokota kingi hakubakiwa na kitu, na yeye aliyekuwa ameokota kichache hakupungukiwa; wakaokota kila mtu kama ulaji wake ulivyokuwa. Musa akawaambia, Mtu awaye yote asikisaze hata asubuhi. Lakini hawakumsikiza Musa; wengine miongoni mwao wakakisaza hata asubuhi, nacho kikaingia mabuu na kutoa uvundo; Musa akawakasirikia sana. Basi wakaokota asubuhi baada ya asubuhi, kila mtu kama ulaji wake ulivyokuwa; na hapo jua lilipokuwa ni kali, kikayeyuka.”

Watu wengi sana wanahofu kuhusu maisha ya baadaye kuwa yatakuwaje kiasi ambacho wanaweza kusahahu kuhusu mapenzi ya Mungu, jambo hili ni hatari, kujiandaa kwa maisha ya baadaye ni kwa muhimu sana, na biblia haikatazi hilo lakini ni uzembe mkubwa kumsahahu Mungu kwaajili ya maisha haya kwa sababu yeye ndiye mwenye kuutunza uzima wetu, watu wanaoogopa kesho pia wanakuwa wachoyo Luka 12: 15-26 “1Akawaambia, Angalieni, jilindeni na choyo, maana uzima wa mtu haumo katika wingi wa vitu vyake alivyo navyo. Akawaambia mithali, akisema, Shamba la mtu mmoja tajiri lilikuwa limezaa sana; akaanza kuwaza moyoni mwake, akisema, Nifanyeje? Maana sina pa kuyaweka akiba mavuno yangu. Akasema, Nitafanya hivi; nitazivunja ghala zangu, nijenge nyingine kubwa zaidi, na humo nitaweka nafaka yangu yote na vitu vyangu.  Kisha, nitajiambia, Ee nafsi yangu, una vitu vyema vingi ulivyojiwekea akiba kwa miaka mingi; pumzika basi, ule, unywe, ufurahi. Lakini Mungu akamwambia, Mpumbavu wewe, usiku huu wa leo wanataka roho yako! Na vitu ulivyojiwekea tayari vitakuwa vya nani? Ndivyo alivyo mtu ajiwekeaye nafsi yake akiba, asijitajirishe kwa Mungu.Akawaambia wanafunzi wake, Kwa sababu hiyo nawaambia, Msisumbukie maisha yenu, mtakula nini; wala miili yenu, mtavaa nini. Kwa kuwa maisha ni zaidi ya chakula, na mwili ni zaidi ya mavazi. Watafakarini kunguru, ya kwamba hawapandi wala hawavuni; hawana ghala wala uchaga, na Mungu huwalisha. Bora ninyi mara nyingi kuliko ndege!  Na yupi kwenu ambaye akijisumbua aweza kujiongeza kimo chake hata mkono mmoja? Basi, ikiwa hamwezi hata neno lililo dogo, kwa nini kujisumbua kwa ajili ya yale mengine?” Unaona Mungu hataki tusumbukie maisha Mungu hataki tuwe na hofu kuhusu kesho yeye ndiye anayejua maisha yetu na hivyo anataka tuwe na furaha, furahia kila unachokikamilisha kwa siku ile,  na usiogope kuhusu kesho itakuwaje Mungu anajua.

3.       Rizika na ulichonacho.

Waebrania 13:5-6 “.Msiwe na tabia ya kupenda fedha; mwe radhi na vitu mlivyo navyo; kwa kuwa yeye mwenyewe amesema, Sitakupungukia kabisa, wala sitakuacha kabisa. Hata twathubutu kusema, Bwana ndiye anisaidiaye, sitaogopa; Mwanadamu atanitenda nini?”

Tamaduni za dunia ya sasa zinafikiri kuwa na furaha ni kuwa na vitu vingi au kuwa na kila kitu lakini ukweli umedhihirika kuwa wale wanaoishi maisha rahisi ndio wenye furaha kubwa duniani kuliko wengine wote, utafiti umethibitisha kuwa watu wanaoishi muda mrefu zaidi kuliko wote duniani ni Mabedui wanaishi jangwani hawa wanauwezo wa kufikisha hata miaka 200 ya maisha yao, sababu kuu ni kuwa wameridhika na maisha yao, Maisha yamebadilika sana kwa sababu watu wameharibu tamaduni zao kuanzia namna mtu anapozaliwa mpaka namna mtu anavyozikwa. leo hii hata kuzika mtu imekuwa ni gharama kubwa sana, Mungu anataka watu wafurahie maisha na hivyo ni muhimu kuridhika na kile ulicho nacho Wafilipi 4:11-13Si kwamba nasema haya kwa kuwa nina mahitaji; maana nimejifunza kuwa radhi na hali yo yote niliyo nayo. Najua kudhiliwa, tena najua kufanikiwa; katika hali yo yote, na katika mambo yo yote, nimefundishwa kushiba na kuona njaa, kuwa na vingi na kupungukiwa. Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.” Kumbuka kuwa sio dhambi kuwa na vitu lakini ni dhambi kumezwa na tamaa, ni kwa sababu ya kutokuridhika watu wengi wameingia katika mateso makubwa sana na hata kufarakana na imani, mioyo tetu inapofungamanisha na maswala ya vitu vya dunia inaweza kutuletea maumivu makubwa sana na tukafikia ngazi ya kutokuyafurahia maisha 1Timotheo 6:6-10Walakini utauwa pamoja na kuridhika ni faida kubwa. Kwa maana hatukuja na kitu duniani, tena hatuwezi kutoka na kitu; ila tukiwa na chakula na nguo tutaridhika na vitu hivyo. Lakini hao watakao kuwa na mali huanguka katika majaribu na tanzi, na tamaa nyingi zisizo na maana, zenye kudhuru, ziwatosazo wanadamu katika upotevu na uharibifu. Maana shina moja la mabaya ya kila namna ni kupenda fedha; ambayo wengine hali wakiitamani hiyo wamefarakana na Imani, na kujichoma kwa maumivu mengi.”  Kama tutajifunza kumfurahia Mungu kwa kile alichotupa tutaishi maisha ya raha na amani, hakuna sababu ya kushindana na awaye yote, kila mtu ana maisha yake na hatuwezi kufanana kwa sababu ninachikiwaza sio unachokiwaza, ninachoamini sio unachokiamini kwa hiyo kila mmoja aepuke maisha ya mashindano na ajifunze kuridhika na kile alicho nacho. Watu wakiishi hivi hakutakuwa na wizi na maisha yatakuwa mazuri.

4.       Muweke Mungu mbele.

Mathayo 6: 31-33 “Msisumbuke, basi, mkisema, Tule nini? Au Tunywe nini? Au Tuvae nini? Kwa maana hayo yote Mataifa huyatafuta; kwa sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hayo yote. Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa.” Yesu anatupa kanuni nyingine ya namna ya kuishi bila kuhangaika au kusumbuka anatoa maangizo ya aina mbili kwa wakati mmoja kumtafuta Mungu kwanza na haki yake na mengine yote tutazidishiwa;  maana yake ni nini? kama tuko duniani kwa makusudi ya Mungu na kila tunachokifanya ni kwaajili ya kutimiza kusudi hilo basi ni vema tukamtafuta Mungu kwanza, yaani “kama Mungu ni chanzo cha kila kitu ni vema tukaacha kutafuta au kuhangaika na kila kitu na tukampata  Yeye aliye chanzo” Chakula na mavazi pamoja na mahitaji yetu mengine ni jukumu la kawaida la baba mwenye upendo, Yesu anaweka wazi kuwa ni afadhali kuhangaika na kumtafuta yeye au kumsikiliza yeye inaweza kuwa muhimu zaidi kuliko kusumbuka na maswala mengineyo Luka 10:38-42 “Ikawa katika kuenenda kwao aliingia katika kijiji kimoja; mwanamke mmoja jina lake Martha akamkaribisha nyumbani kwake. Naye alikuwa na umbu lake aitwaye Mariamu, aliyeketi miguuni pake Yesu, akasikiliza maneno yake. Lakini Martha alikuwa akihangaika kwa utumishi mwingi; akamwendea, akasema, Bwana, huoni vibaya hivyo ndugu yangu alivyoniacha nitumike peke yangu? Basi mwambie anisaidie.Bwana akajibu akamwambia, Martha, Martha, unasumbuka na kufadhaika kwa ajili ya vitu vingi; lakini kinatakiwa kitu kimoja tu; na Mariamu amelichagua fungu lililo jema, ambalo hataondolewa.”
Unaona mtu anapochagua kumsikiliza Mungu amechagua fungu lililojema, ni muhimu sana kupata ujuzi kuhusu nini ni mapenzi ya Mungu na kuyafanya kwa wakati huo, na ni muhimu kuwa na ushirika na Mungu kwanza kabla ya kuanza kusumbuka na kutimiza kusudi lake, wakati mwingine tunaweza kusumbuka bila mafanikio kwaajili ya kujishughulisha kutafuta mafanikio bila kusikia neno la mfanikishaji

Kwa akili zetu wakati mwingine tunaweza kusumbuka sana kufanya mambo bila kufanikiwa lakini kwa kutii na kufuata au kuomba uongozi wa Mungu tunaweza kupata mafanikio makubwa katika jambo lilelile ambalo limeshindikana mwanzoni Luka 5:4-7 “Hata alipokwisha kunena, alimwambia Simoni, Tweka mpaka kilindini, mkashushe nyavu zenu mvue samaki. Simoni akajibu akamwambia, Bwana mkubwa, tumefanya kazi ya kuchosha usiku kucha, tusipate kitu; lakini kwa neno lako nitazishusha nyavu. Basi, walipofanya hivyo walipata samaki wengi mno, nyavu zao zikaanza kukatika; wakawapungia mikono washirika wao waliokuwa katika chombo cha pili, waje kuwasaidia; wakaja, wakavijaza vyombo vyote viwili, hata vikataka kuzama.” Unaona tunapomtanguliza Mungu na kumtii yeye kwanza kwa kuwa yeye ndio chanzo cha mambo yote hutupa maelekezo stahiki yanayoweza  kutupa mafanikio tunayoyataka    

Biblia inaonyesha kuwa kama tukimtumikia Mungu yaani kumuabudu na kumuweka yeye Mstari wa mbele atatuponya Magonjwa, ataondoa utasa, na kutimiza siku zako za kuweko duniani Kutoka 23:25-26 “Nanyi mtamtumikia BWANA, Mungu wenu, naye atakibarikia chakula chako, na maji yako; nami nitakuondolea ugonjwa kati yako. Hapatakuwa na mwenye kuharibu mimba, wala aliye tasa, katika nchi yako; na hesabu ya siku zako nitaitimiza.” Torati inaonyesha kuwa kuna Baraka nyingi sana kama watu wataitii sauti ya Mungu na kumuweka yeye mbele, Neno la Mungu moja tu kwetu linaweza kubadilisha kabisa mfumo wa maisha yetu na tukaishi maisha ya furaha.

5.       Sahahu yaliyopita.

Wafilipi 3:13 “Ndugu, sijidhanii nafsi yangu kwamba nimekwisha kushika; ila natenda neno moja tu; nikiyasahau yaliyo nyuma, nikiyachuchumilia yaliyo mbele;”
               
Moja ya kikwazo kikubwa sana katika maisha ya watu wengi kinachowakosesha wasiweze kuwa na furaha au kusumbuka ni kutokusahau Historia, ingawa Historia ni nzuri lakini wote tutakubaliana kuwa ziko historia nyingine haziwezi kutupa maisha yenye furaha, kwa msingi huo Biblia inatutaka tusahau yakiyo nyuma na kuchuchumilia yaliyo mbele, historia yetu ya maisha ya nyuma ni ya kuitupa.

Mara kadhaa wana wa Israel walijikosesha Baraka za Mungu kwa sababu walikumbuka Misri katika inchi ya utumwa na kudharau uhuru ambao Mungu alikuwa amewazawadia, Mungu alikuwa amewapa ukombozi mkuu lakini mara kwa mara walimuhuzunisha kwa kukosa shukurani Hesabu 14:1-4 “Mkutano wote wakapaza sauti zao wakalia; watu wakatoka machozi usiku ule. Kisha wana wa Israeli wote wakamnung'unikia Musa na Haruni; mkutano wote wakawaambia, Ingekuwa heri kama tungalikufa katika nchi ya Misri, au, ingekuwa heri kama tungalikufa katika jangwa hili. Mbona Bwana anatuleta mpaka nchi hii ili tuanguke kwa upanga? Wake zetu na watoto wetu watakuwa mateka; je! Si afadhali turudi Misri?  Wakaambiana, Na tumweke mtu mmoja awe akida, tukarudi Misri.” Kutokana na kuwa na hali ya manunguniko na kukosa shukurani kwa Mungu ugumu uliongezeka katika maisha yao safari ya jangwani ilikuwa ndefu na yenye misiba Mingi inakisiwa kuwakila siku waisrael 70 walikufa, ni lazima tusahahu tulikotoka na nkuendelea kumtumikia Mungu kwa nguvu na kumuabudu yeye kwa nguvu, kamwe tusiangalie nyuma kule alikotutoa Bwana Luka 17:32-33 “Mkumbukeni mkewe Lutu. Mtu ye yote atakaye kuiponya nafsi yake, ataiangamiza; na ye yote atakayeiangamiza ataiponya.” Yesu alikumbusha juu ya kujikana nafsi na kuendelea kumcha yeye na kutimiza wajibu wetu kwa Mungu bila kugeuka nyuma, Yesu alitumia mfano wa mkewe Lutu, na kuonya juu ya jkutaka kuiokoa nafsi yetu, Yesu anazungumzia juu ya kujihurumia na kutokujikana kwa Mungu, wengi kwaajili ya kujihurumia wamepoteza Baraka na uwepo wa Mungu Paulo Mtume alikuwa ni mtume aliyepata neema kubwa ya Mungu kuliko mitume wote, alipelekwa mpaka mbigu ya tatu na kupewa mafunuo makubwa sana hata hivyo hakuwahi kuridhika wala kuangalia historia yake yeye alijua kuwa furaha yake inapatikana kwa kuendelea kusahau yaliyo nyuma na kuchuchumilia yaliyo mbele, aliwataka kanisa la kolosai kuangalia Wakolosai 3:1-2 “Basi mkiwa mmefufuliwa pamoja na Kristo, yatafuteni yaliyo juu Kristo aliko, ameketi mkono wa kuume wa Mungu.   Yafikirini yaliyo juu, siyo yaliyo katika nchi.” Ni Muhimu kujifunza kuangalia mbele ondoa uchungu wote na hakikisha kuwa unasamehe wote waliokukosea uchungu una tabia ya kutufungia Baraka na uwepo wa Mungu hivyo kusahau  yaliyopita ni pamoja na kusamehe wale waliotukosea Hesabu 4:13 “Nao watayaondoa hayo majivu madhabahuni; na kutandika nguo ya rangi ya zambarau juu yake;” Kusamehe na kuondoa kila aina ya uchungu ni sawa na kazi za makuhani ambao walitakiwa kuhakikisha wanaondoa majivu katika madhabahu ili moto uendelee kuwaka.

6.       Fanya kila kitu kwa utukufu wa Mungu.

1Wakoritho 10:31 “Basi, mlapo, au mnywapo, au mtendapo neno lo lote, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu.” Moja ya mambo ambayo yanawaumiza watu wengi sana duniani ni kufanya mambo kwa mashindano au kwa kutaka kushindana au kujilinganisha, watu wengi sana wanakosa amani na kusumbuka katika maisha haya kwa sababu wanajilinganisha na wengine, hawafanyi mambo kwa nia njema nia ya Mungu kutukuzwa.

Mara zote mashindano yameleta kiburi, yameleta dharau yameleta maumivu na majuto,siku hizi kuna mashindano mpaka ya kutoa sadaka tabia ya aina hii imeumiza wengi Mungu hatahukumu kile tunachokifanya bali atahukumu kwa nini tumefanya, ni muhimu nia yetu nadhamiri zetu za kutenda lolote tunalolitenda ikawa ni kwaajili ya Mungu kutukuzwa, kamwe neno la Mungu haliitii moyo kufanya jambo kwa mashindano, Wafilipi 2:3Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake.” Unaweza kuona tabia ya kushindana ikiingia kanisani au kwa watu wa Mungu inaweza kuleta vita na magomvi hata kuomba kwetu kunaweza kugeuzwa kuwa kuomba kubaya kuomba kwa tamaa kwa sababu ya mshindano na sio kwaajili ya utukufu wa Mungu Yakobo 4:1-3 “Vita vyatoka wapi, na mapigano yaliyoko kati yenu yatoka wapi? Si humu, katika tamaa zenu zifanyazo vita katika viungo vyenu? Mwatamani, wala hamna kitu, mwaua na kuona wivu, wala hamwezi kupata. Mwafanya vita na kupigana, wala hamna kitu kwa kuwa hamwombi! Hata mwaomba, wala hampati kwa sababu mwaomba vibaya, ili mvitumie kwa tamaa zenu.” Kama kila kitu tukifanyacho hakifanyiki kwaajili ya utukufu wa  Mungu maisha yetu yatakuwa yenye uchungu mwingi, na hata kuomba kwetu kutaathiriwa tutakuwa tunaomba kwa sababu ya kutaka kitu fulani kwa tamaa na sio kwaajili ya utukufu wa Mungu kanuni kuu ya msingi hapa ni kufanya kila jambo kwaajili ya utukufu wa Mungu.

7.       Jifunze kukataa.

Mathayo 5:37 “Bali maneno yenu yawe Ndiyo, ndiyo; Siyo, siyo; kwa kuwa yazidiyo hayo yatoka kwa yule mwovu.”

Yakobo 5:12 “Lakini zaidi ya yote, ndugu zangu, msiape, wala kwa mbingu wala kwa nchi; wala kwa kiapo kinginecho chote; bali ndiyo yenu na iwe ndiyo, na siyo yenu iwe siyo, msije mkaangukia hukumu.”

Nyakati za Biblia hususani wakati wa Yesu Kristo wayahudi wengi sana walikuwa wakiogopa sana kuapa au kujifunga katika ahadi yoyote kwa kumuhusisha Mungu hii ni kwa sababu waliogopa kuwa endapo watashindwa kutimiza ahadi basi watakuwa wamejifunga kwa Mungu, hivyo hawakutaka kumuhusisha Mungu ili hata wakivunja ahadi wasiweze kuwajibika kwa Mungu wakijua kuwa hawafungwi, swala hili lilipunguza uaminifu wa watu na kuwanyima raha, tatizo la kutokuwa wakeli linawatesa sana hata wafrika wengi wanaogopa kusema Ndio au sio inayotoka Moyoni wanaweza kusema Ndio lakini kumbe moyonimwao hawako radhi na hilo, au wanaweza kusema sio kumbe kuna kitu wanakihitaji

Neno la Mungu kupitia Yesu Kristo linatutaka tuwe watu wenye maamuzi yaliyo wazi tu kuwa kama jambo ni ndio iwe ndio kivitendo maana sisi ni wa Mungu na kama jambo sio iwe sio kwa maana sisi ni watu wa Mungu hakuna sababu ya kupiga siasa, wengi wanaogopa kusema sio kwa wake za, mabosi wao kwa kuogopa kuuwaumiza mioyo lakini baadaye wanajuta kwa nini sikukataa au kwanini nilikubali Heri kama ningelikataa

Kutokusema HAPANA ni tatizo kubwa sana la kisaikolojia wana saikoloji wanaliita tatizo hilo “CANT SAY NO SYNDROM  wengi wanaoogopa kusema hapana wanafikiri kwamba labda wao sio Bora sana, hivyo wanafikiri kuwa wanaweza kuwapendeza wengine kwa kuwakubalia kila wanachokitaka, au wanafikiri kuwa wanapaswa kuwatumikia wengine na kuwa wema sana kiasi wakisema hapana watawaudhi, au anafikiri kuwa akisema hapana atakataliwa, wanafikiri kuwa watu watawapenda wakiwakubalia kila kitu, wanadhani kusema hapana ni swala la kikatiali sana, wanafikiri kuwa wataonekana kuwa wabinafsi wakisema hapana, au wanafikiri kuwa wengine hawatakiwi kuona yeye kuwa ni mkaidi, na tafasiri mbaya ya maandiko heri wenye upole maana watairithi inchi.

Biblia imatupa kweli muhimu au kanuni ya muhimu ya kuyafurahia maisha ambayo ni kusema Ndio au Hapana
Vijana wengi wa kiume wakiombwa na wasichana kuwa wapenzi inakuwa vigumu kwao kusema hapana kwa sababu ya kuwaonea huruma biblia inatutaka tuseme hapana kwa hapana kweli na ndio kwa ndio kweli na sio kutoa maelezo.
Kusema hapana sio swala rahisi, wengi wanaogoipa kusema hapana, kiroho kutokusema hapana kuna maanisha kuwa tuna roho ya woga; 2Timotheo 1:7 “Maana Mungu hakutupa roho ya woga, bali ya nguvu na ya upendo na ya moyo wa kiasi.Kutokana na woga huu hususani woga wa kuumiza wengine kwa sababu kusema hapana mara nyingi kunaumiza wengine watu wengi sana wamejikuta au tumejikuta katika matatizo ya aina mbali mbali
·         Dereva anaweza akawa anaendesha kwa kasi sana na kuhatarisha maisha lakini ukaogopa kumwambia punguza mwendo
·         Jambo linaweza likawa liko kinyume cha Sheria.lakini kwa vile wengine wanafanya ukashidwa kusema hapana
·         Jambo linaweza kuwa hukubaliani nalo, lakini kwa vile wengi wamelikubali hutaki kuonekana tofauti

Inahitajika roho ya ujasiri, bila kuumiza moyo wa mtu mwingine kusema Hapana tofauti na mtazamo wake, au wakati mwingine kusema hapana hata kama jambo hilo litamuumiza muhusika Daniel 3:13-18Basi Nebukadreza akatoa amri kwa hasira na ghadhabu, waletwe hao Shadraka, na Meshaki, na Abednego. Basi wakawaleta watu hao mbele ya mfalme. Nebukadreza akajibu, akawaambia, Enyi Shadraka, na Meshaki, na Abednego, je! Ni kwa makusudi hata hammtumikii mungu wangu wala kuisujudia sanamu ya dhahabu niliyoisimamisha? Basi sasa, kama mkiwa tayari wakati mtakapoisikia sauti ya panda, na filimbi, na kinubi, na zeze, na santuri, na zomari, na namna zote za ngoma, kuanguka na kuisujudia sanamu niliyoisimamisha, ni vema; bali msipoisujudia, mtatupwa saa iyo hiyo katika tanuru iwakayo moto; naye ni nani Mungu yule atakayewaokoa ninyi na mikono yangu? Ndipo Shadraka, na Meshaki, na Abednego, wakajibu, wakamwambia mfalme, Ee Nebukadreza, hamna haja kukujibu katika neno hili. Kama ni hivyo, Mungu wetu tunayemtumikia aweza kutuokoa na tanuru ile iwakayo moto; naye atatuokoa na mkono wako, Ee mfalme. Bali kama si hivyo, ujue, Ee mfalme, ya kuwa sisi hatukubali kuitumikia miungu yako, wala kuisujudia hiyo sanamu ya dhahabu uliyoisimamisha”.  Shadraka na Meshaki na Abednego walijifunza kusema hapana katikakweli waliweza kumkatalia mfalme katika kile walichokiamini, kuwa kwao na kwa imani yao hakiko sahihi.

1Wafalme 21: 1-4 “Ikawa baada ya hayo, Nabothi Myezreeli alikuwa na shamba la mizabibu katika Yezreeli, karibu na nyumba ya kifalme ya Ahabu mfalme wa Samaria. Ahabu akasema na Nabothi, akamwambia, Nipe shamba lako la mizabibu nilifanye shamba la mboga, maana ni karibu na nyumba yangu; nami nitakupa badala yake shamba la mizabibu lililo zuri zaidi; au ukipenda, nitakupa fedha sawasawa na thamani yake. Nabothi akamwambia Ahabu, Bwana apishe mbali nikupe wewe urithi wa baba zangu. Basi Ahabu akaenda nyumbani kwake, ana moyo mzito, tena amekasirika, kwa sababu ya neno lile aliloambiwa na Nabothi Myezreeli, akisema, Sitakupa urithi wa baba zangu. Akajilaza kitandani pake, akageuza uso wake, akakataa kula.”  Unaona Nabothi pia alikuwa mtu mwenye ujasiri wa kusema hapana katika jambo alilokuwa anaamini kuwa ni sahihi kwa utamaduni wake na kwa mujibu wa mila zao.

Unaona kutokuwa na uwezo wa kusema hapana ni tatizo linalowasumbua watu wengi duniani kwani wanaogopa kuumiza wengine, wengi tunaogopa kusema hapana kwa viongozi wetu, kwa wake zetu, kwa waume zetu, kwa wachumba zetu kwa wazazi wetu na kadhalika na kutokna na hayo wengi wameishi maisha ya kinafiki au kufanya mambo yanayoweza kumiza nafsi zao.

Matendo ya Mitume 5:27-29 “Walipowaleta, wakawaweka katika baraza. Kuhani Mkuu akawauliza, akisema, Je! Hatukuwaamuru ninyi kwa nguvu, msifundishe kwa jina hili? Nanyi, tazameni, mmeijaza Yerusalemu mafundisho yenu, na mnataka kuileta damu ya mtu yule juu yetu. Petro na mitume wakajibu, wakisema, Imetupasa kumtii Mungu kuliko wanadamu.” 

8.       Kataa kufanya jambo ambalo hutalikamilisha.

Luka 14:28-32Maana ni nani katika ninyi, kama akitaka kujenga mnara, asiyeketi kwanza na kuhesabu gharama, kwamba anavyo vya kuumalizia? Asije akashindwa kuumaliza baada ya kuupiga msingi, watu wote waonao wakaanza kumdhihaki, wakisema, Mtu huyu alianza kujenga, akawa hana nguvu za kumaliza. Au kuna mfalme gani, akitaka kwenda kupigana na mfalme mwingine, asiyeketi kwanza na kufanya shauri, kwamba yeye pamoja na watu elfu kumi ataweza kukutana na yule anayekuja juu yake na watu elfu ishirini? Na kama akiona hawezi, hutuma ujumbe kutaka sharti za amani, mtu yule akali mbali.”

Maandiko yanatufundisha kuwa ni tabia ya uungu kuanza jambo na kulikamilisha, Mungu hana kigeugeu kama ameanza kazi njema mioyoni mwetu atahakikisha kuwa anaikamilisha Wafilipi 1:6  “Nami niliaminilo ndilo hili, ya kwamba yeye aliyeanza kazi njema mioyoni mwenu ataimaliza hata siku ya Kristo Yesu;”
Yesu Kristo pia anaitwa katika maandiko mwanzilishi na mwenye kutimiza imani yetu hii inatukumbusha kuwa Mungu akianza jambo huwa haliachii njiani kwa msingi huo ni muhimu kwa kila mmoja wetu kuhakikisha kuwa hauishii njiani katika maswala ya aina mbalimbali, kuanzia maswala ya imani, miradi na lolote lile unalolianzisha ni muhimu kuhakikisha kuwa haliishiinjiani, “Mtu atakumbukwa kwa kila alichokamilisha na sio kwa kile alichojaribu”    Waebrania 12:2 “tukimtazama Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake aliustahimili msalaba na kuidharau aibu, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu.”

Mambo mengi sana hapa duniani yanahitaji subira na uvumilivu, hakuna kitu kinaweza kutokea mara moja tu vingine vinahitaji subira, watu wasio na subira hawawezi kukamilisha mambo, kukomaa kwetu pia kiroho na kitabia na mwenendo hakutokei kwa usiku mmoja tu ni mchakato, watu wengi wanaoshindwa kiroho ni wale ambao wanatarajia kitu kitokee mara moja tu na kufanikiwa kwa haraka yako mambo buna budi kuwa na subira na uvumilivu. Usianzishe jambo kwa msukumo wa kihisia tu hapana lazima ufikiri kwa kina namna utakavyokamilisha mambo uwe na busara kama mkulima ambaye analima na kisha anasubiria mavuno yake Yakobo 5:10-11 “Ndugu, watwaeni manabii walionena kwa jina la Bwana, wawe mfano wa kustahimili mabaya, na wa uvumilivu. Angalieni, twawaita heri wao waliosubiri. Mmesikia habari ya subira yake Ayubu, mmeuona mwisho wa Bwana ya kwamba Bwana ni mwingi wa rehema, mwenye huruma.”

9.       Mwachie Mungu Mizigo yako.

Ni muhimu kufahamu kuwa ingawa tunamwanini Mungu na tunamwamini Yesu, hii haimaanishi kuwa hatutapitia changamoto za namna mbalimbali, madamu tumo ulimwenguni bado tunaweza kupitia dhiki na vikwazo na changamoto mbalimbali Yohana 16:33 “Hayo nimewaambieni mpate kuwa na amani ndani yangu. Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu.” Kwa nini Yesu anatuambia kuwa duniani tunayodhiki? Yesu hataki tushangae tunapopitia majaribu ya namna mbalimbalia hata kama sisi ni watu wake, Majaribu yanatufundisha kuvumilia na kutuleta katika ukamilifu Yakobo 1:2-4 2. “Ndugu zangu, hesabuni ya kuwa ni furaha tupu, mkiangukia katika majaribu mbalimbali; mkifahamu ya kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huleta saburi. Saburi na iwe na kazi kamilifu, mpate kuwa wakamilifu na watimilifu bila kupungukiwa na neno”. Hata hivyo pamoja na faida hizo za majaribu Mungu anataka tumtike yeye fadhaa zetu zote

Zaburi 55:22 “Umtwike Bwana mzigo wako naye atakutegemeza, Hatamwacha mwenye haki aondoshwe milele.”

 1Petro 5:6-7 “Basi nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake;  huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu.”

Kwa mujibu wa maandiko hayo tunapata picha iliyo wazi  na ukweli kuhusu Mungu, kwamba yeye hatatuacha tuondoshwe, yaani ahatatuachan tuaibike, Yeye anatujalia Mungu anaonyesha wazi kuwa anauwezo wa kutusaidia kiakili, kihisia, kiroho na kimwili, yuko tayari na anauwezo kama alivyoahidi katika neno lake Mungu huruhusu au hufanya mambo yote yaani magumu na mepesi kwa kusudi la kutupatia mema sisi tumpendao Warumi 8:28 “Nasi twajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao katika kuwapatia mema, yaani, wale walioitwa kwa kusudi lake.” Kwa msingi huo ni muhimu kupeleka kwake kila jamnbo linalosumbua maisha yetu, hata wakati wa shida na tunapokuwa na mashaka hata ya kumuamini yeye , Yeye hubaki mwaminifu na anafanya kazi kwaajili yatu kwa utukufu wake, na ametuahidi kuwa hatatuacha tujaribiwe kuliko tuwezavyo na kwamba kwa kila jaribu ameweka mlango wa kutokea  kwa msingi huo hatatuangusha kama ilivyo ahadi yake 1Wakoritho 10:13 “Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili.”

10.   Wewe ni zaidi ya Mshindi.

Warumi 8:37 “Lakini katika mambo hayo yote tunashinda, na zaidi ya kushinda, kwa yeye aliyetupenda.”
Wakristo wengi sana wanaufahamu mstari huu au andiko hili na hulitaja mara kwa mara kwa tafasiri mbalimbalui, kwa mujibu wa somo hili kuwa zaidi ya mshuindi maana yake ni kuwa na ujasiri kwa jambo lolote linalokutokea katika maisha kupitia Yesu Kristo au kwaajili ya Yesu Kristo tunaweza kabisa kulikabili kwa ushindi, hatutaogopa na hatutaishi kwa kusumbuka kwa vile tunajua hata kama tutazamishwa katika hali ngumu kwa kiwango chochote kila Kristo atatusaidia na kutupa ushindi

Mungu ni mkuu kuliko Hofu zetu, kwa msingi huo maandiko yanatutaka

1.       Tuwe na furaha hata wakati wa taabu na masumbufu ya ulimwengu huu tukijua ya kuwa Mungu anaweza kuyatumia kuzalisha uvumilivu, kututunza, kuwa na tabia njema , sifa njema na matumaini Warumi 5:3-4Wala si hivyo tu, ila na mfurahi katika dhiki pia; mkijua ya kuwa dhiki, kazi yake ni kuleta saburi; na kazi ya saburi ni uthabiti wa moyo; na kazi ya uthabiti wa moyo ni tumaini;”              
2.       Kwamba tutumia masumbufu yetu kama njia ya kutukuza kiimani na ya kutupeleka katika ngazi nyingine ya kumtumaini Mungu kuliko njia zetu na akili zetu kwaajili ya utukufu wake Mithali 3:5-6 “Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote, Wala usizitegemee akili zako mwenyewe; Katika njia zako zote mkiri yeye, Naye atayanyosha mapito yako.”               
3.       Njia ya kutii na kutufanya tuwe wema kwa kila mtu, uwezo wa kusamehe na kuchukuliana Waefeso 4:31-32 “Uchungu wote na ghadhabu na hasira na kelele na matukano yaondoke kwenu, pamoja na kila namna ya ubaya; tena iweni wafadhili ninyi kwa ninyi, wenye huruma, mkasameheane kama na Mungu katika Kristo alivyowasamehe ninyi.”     
4.       Kwaajili ya kutuleta katika toba ili tushughulikie dhambi zetu na kuwa wakeli na kuishi maisha ya haki 1Yohana 1:9 “Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote.”

Maombi:
Mungu baba uliyejaa upendo na fadhili, rehema zako zina wakuchao kizazi na hata kizazi, ututie nguvu wakati wote wa masumbufu ya ulimwengu huu, uwe pamoja nasi hata tuwapo na mashaka, utupe kujificha kwako wakati wa shida namasumbufu ya ulimwengu huu, utupe kukukimbilia wewe ili tusiaibike kweli wanaokutumaini wewe ni kama mlima wa Sayuni  hawatatikisika milele, Katika jina la Yesu Kristo mwana wako ninakurudishia sifa na utukufu, Amen

Na mkuu wa Wajenzi mwenye Hekima

Rev. Innocent Kamote.

Ijumaa, 2 Machi 2018

Kuingia kwa mfalme Kinyume cha Sheria!


Andiko la msingi: Esta 4:15-16Basi Esta akawatuma ili wamjibu Mordekai, Uende ukawakusanye Wayahudi wote waliopo hapa Shushani, mkafunge kwa ajili yangu; msile wala kunywa muda wa siku tatu, usiku wala mchana, nami na wajakazi wangu tutafunga vile vile; kisha nitaingia kwa mfalme, kinyume cha sheria; nami nikiangamia, na niangamie.”



Utangulizi:

Wiki hii ni wiki ya sikukuu ya PURIM kule Israel wayahudia huandimisha sikukuu ya Purim kwa mujibu wa kalenda ya kiyahudi sikukuu hii ya Purim huazimishwa kila ifikapo February 28 na 29 ya kila mwaka  ambayo ni sawa na siku ya 13, 14  na 15 ya mwezi wa Adar na Nissan yaani sawa na katikati ya mwezi Februari na March ya kalenda ya kawaida, Wayahudi huadhimisha sikukuu hii kutokana na amri ya Mordekai pamoja na malkia Esta kuwa ni lazima siku hii ikumbukwe. Esta 9: 29-32Ndipo malkia Esta, binti Abihaili, pamoja na Mordekai Myahudi, alipoandika kwa mamlaka yote kuithibitisha barua hii ya pili ya Purimu. Akapeleka barua kwa Wayahudi wote katika majimbo yote mia na ishirini na saba ya ufalme wake Ahasuero, maneno ya amani na kweli, ili kuzithibitisha siku hizo za Purimu kwa majira yake, kama Mordekai Myahudi na malkia Esta walivyoamuru, na kama walivyojiagizia juu yao wenyewe, na juu ya wazao wao, kwa habari ya kufunga na kilio.  Amri yake Esta ikayathibitisha mambo hayo ya Purimu; ikaandikwa katika kitabu” Ni kutokana na agizo hilo ndio mpaka leo Wayahudi huadhimisha sikukuu iitwayo PURIM au PURI wakimaanisha siku waliyopigiwa KURA au Kupitishiwa MSWAADA wa kuuawa Lakini kwa neema ya Mungu wakaokolewa. Siku ya Purim ni siku ya furaha sana kwa Wayahudi, wao hushangilia na kufurahi na kuruka ruka na kucheza ngoma na kunywa divai, Lakini katika masinagogi na ibada huwa ni wakati wa kusomwa kwa kitabu cha Esta.
Tutajifunza somo hili kwa kuzingatia mambo muhimu yafuatayo:-

·         Sababu na Mpango wa kuangamizwa kwa Wayahudi.
·         Utaratibu wa Sheria na tamaduni za kiamedi na kiajemi.
·         Kuingia kwa mfalme Kinyume cha sheria.

Sababu na Mpango wa kuangamizwa kwa Wayahudi.

Ni muhimu kufahamu kuwa Kitabu cha Esta ni mojawapo ya kitabu ambacho kiliandikwa kuonyesha Msimamo wa kiimani wa wayahudi waliokuwa Uhamishoni, wakati huu wayahudi waliokuwa uhamishoni huko Babeli maisha yao na imani yao kwa Mungu wa kweli ilikuwa imani kali sana na hawakutaka kuleta mchezo na msimamo wao wa kiimani katika Mungu wa kweli wa Israel, walikuwa wamejifunza madhara makubwa ya kumuacha Mungu hata kwa sekunde moja, hivyo walishikamana na Mungu wao kwa uthabiti hata pamoja na kuwa mbali na Israel, Kisa na sababu ya kutaka kuangamizwa kwao kinaashiria wazi kuwa ulikuwa ni mpango wa Ibilisi, ili kufuta Historia ya kuwepo kwa Mungu, kisa au sababu inaanzia kwa mtu mmoja aliyeitwa Hamani ambaye alipandishwa Cheo na Mfalme kuamuru watu wote walio chini yake wamsujudie Esta 3:1-4Baada ya hayo mfalme Ahasuero alimwongezea cheo Hamani bin Hamedatha, Mwagagi, akampandisha, akamwekea kiti chake juu ya maakida wote waliokuwapo pamoja naye. Nao watumishi wote wa mfalme, walioketi mlangoni pa mfalme, wakainama na kumsujudia Hamani, maana ndivyo alivyoamuru mfalme kwa habari zake. Bali Mordekai hakuinama, wala kumsujudia. Basi watumishi wa mfalme walioketi mlangoni pa mfalme wakamwambia Mordekai, Mbona wewe waihalifu amri ya mfalme? Ikawa, waliposema naye kila siku asiwasikilize, wakamwarifu Hamani, ili kuona kama mambo yake Mordekai yatasimama; maana alikuwa amewaambia ya kuwa yeye ni Myahudi.”  Unaweza kuona maandiko yanaonyesha sababu ya kisa cha wayahudi kuchukiwa ilikuwa ni tamaa na ubinafsi wa mtu mmoja tu kutaka Heshima na kuabudiwa, wakati mwingine migogoro mikuwa ya kitaifa au taasisi inaweza kuanza kwa chuki ya mtu mmoja tu, kwa maslahi yake na tamaa zake akaingiza wengine katika mgogoro mkubwa, ni Chuki ya hamani dhidi ya Mordekai ndio iliyopelekea Hamani kutaka kuwaangamiza Wayahudi wote, Esta 3:5-15Hata Hamani alipoona ya kwamba Mordekai hainami wala kumsujudia, alighadhibika sana.  Akaona si shani kumtia mikono Mordekai peke yake; maana wamemjulisha kabila yake Mordekai; kwa hiyo Hamani alitaka kuwaangamiza Wayahudi wote waliokuwa wakikaa katika ufalme wote mzima wa Ahasuero, yaani, watu wake Mordekai. Basi mwezi wa kwanza, ndio mwezi wa Nisani, mwaka wa kumi na mbili wa mfalme Ahasuero, wakapiga Puri, yaani kura, mbele yake Hamani; siku kwa siku, na mwezi kwa mwezi, hata mwezi wa kumi na mbili, ndio mwezi wa Adari. Basi Hamani akamwambia mfalme Ahasuero, Kuna taifa moja waliotawanyika na kukaa mahali mahali katikati ya mataifa walioko katika majimbo yote ya ufalme wako. Nao sheria zao zimefarakana na sheria za kila taifa; wala hawazishiki amri za mfalme; kwa hiyo haimpasi mfalme kuchukuliana nao. Basi, mfalme akiona vema, na iandikwe kwamba waangamizwe; nami nitalipa talanta kumi elfu za fedha mikononi mwao watakaosimamia shughuli hiyo, waziweke katika hazina ya mfalme. Ndipo mfalme alipoivua pete yake mkononi, akampa Hamani bin Hamedatha, Mwagagi, adui ya Wayahudi. Kisha mfalme akamwambia Hamani, Hiyo fedha umepewa, na watu pia, fanya uonavyo vema. Basi, waandishi wa mfalme wakaitwa, siku ya kumi na tatu ya mwezi wa kwanza; na barua zikaandikwa, kama vile Hamani alivyoagiza vyote, kwa maakida wa mfalme, na maliwali waliokuwa juu ya kila jimbo, na wakuu wa kila taifa; kila jimbo kwa mwandiko wake, na kila taifa kwa lugha yake; zikaandikwa kwa jinsi la mfalme Ahasuero, na kutiwa muhuri kwa pete yake. Barua zikapelekwa kwa mikono ya matarishi mpaka majimbo yote ya mfalme kuwaangamiza Wayahudi wote, na kuwaua, na kuwafisha, vijana kwa wazee, watoto wachanga na wanawake pia, siku moja, yaani, siku ya kumi na tatu ya mwezi wa kumi na mbili ndio mwezi wa Adari; na kuyachukua mali yao kuwa nyara.  Nakili ya andiko, ya kupigwa mbiu katika kila jimbo, ilitangazwa kwa mataifa yote wawe tayari siku ile ile.Matarishi wakaondoka wakaenda haraka kwa amri ya mfalme; kukapigwa mbiu huko Shushani ngomeni. Mfalme na Hamani wakaketi ili kunywa divai; bali mji wa Shushani ukafadhaika” Mpango huu ulikuwa ni mpango mbaya sana haukuwa na tofauti na kile alichokifanya “Adolf Hittler” ambaye yeye alifanikiwa kuwaua wayahudi wengi sana Duniani, ni jambo lenye kushangaza kuwa wakati mwingne shetani anaweza kukuza na kutekeleza chuki kubwa isiyokuwa na sababu maalum kwa watu wa Mungu, wanatheolojia wanaiita chuki hii kuwa ndio chuki ya ajabu iliyomkuta Yesu Kristo aliyeuawa na watu aliowatendea Mema, Mfalme alikuwa amesahau na wala hajui kuwa Mordekai alikuwa ni afisa usalama wa ngazi ya juu kabisa aliyefanikiwa kuokoa Maisha yake alipotaka kuuawa na sasa bila kuelewa amekubaliana na hamani na kupitisha sheria mbaya zaidi isiyoweza kutanguliwa ili kuwaangamiza wayahudi bila kufikiri Esta 2:21-23Ikawa siku zile, Mordekai alipokuwa akiketi mlangoni pa mfalme, wawili katika wasimamizi wake mfalme, Bigthana na Tereshi, wangoje mlango, walighadhibika, wakataka kumpelekea mikono mfalme Ahasuero. Basi Mordekai akapata kulijua jambo hilo, naye akamjulisha Esta, malkia; naye Esta akamwambia mfalme habari hiyo kwa jina la Mordekai. Na jambo hilo lilipochunguzwa, na hakika ikapatikana, hao wote wawili wakatundikwa juu ya mti. Hayo pia yakaandikwa katika kitabu cha taarifa mbele ya mfalme.”

Pamoja na wema huu na ulioweza kuwekwa katika taarifa Mfalme hakuona kuwa Mordekai na jamii yake ya Wayahudi kama watu waliokuwa na maana na alikubali waangamizwe ni muhimu kufahamu kuwa hapa ilikuwa imebaki siku ya kupigwa kura tu kuwa ni lini wayahudi watauawa lakini mswada ulikuwa umekwisha kupitishwa na kwa mujibu wa sheria za kiamedi na kiajemi jambo hili lisingeliweza kutanguliwa kwa namna yoyote, ili tuweze kufahamu vema hebu tuangalie desturi zao zilikuwaje katika kipengele kifuatacho.

Utaratibu wa Sheria na tamaduni za kiamedi na kiajemi.

Kwa mujibu wa Historia ya kibiblia Sheria za Uamedi na uajemi katika desturi yao zilikuwa zikipitishwa au zikiamriwa hakukuwa na kurudi nyuma kwa namna yoyote na ni vigumu hata mfalme mwenyewe kuweza kuitangua sheria na desturi iliyopitishwa naye msimamo wa aina hii ulithibitika wazi na lilikuwa ni jambo la fedhea na aibu kubwa sana kwa mfalme kugeuka nyuma ilionekana kama mfalme huyu sio mwenye moyo thabiti na imara na ni mfalme kigeugeu kutengua sheria kungeweza kumfanya mfalme asiaminike na watu wagepoteza imani naye japokuwa bado mfalme alikuwa ndio mwenye mamlaka ya mwisho na mwenye uwezo hata wa kutangua lolote kwa manufaa yake na taifa lake, Jambo hili liliwafunza Israel kuwa thabiti katika kutunza uadilifu wao kwa Mungu, hata ingawa walikutwa na hatari za kuishi katika mazingira magumu na yenye maamuzi kama hayo ya kushangaza.

-          Daniel 6: 12Ndipo wakakaribia, wakasema mbele ya mfalme katika habari ya ile marufuku ya mfalme; Je! Hukuitia sahihi ile marufuku, ya kwamba kila mtu atakayeomba dua kwa Mungu awaye yote, au kwa mtu awaye yote, katika muda wa siku thelathini, ila kwako, Ee mfalme, atatupwa katika tundu la simba? Mfalme akajibu, akasema, Neno hili ni kweli, kama ilivyo sheria ya Wamedi na Waajemi isiyoweza KUBADILIKA.”

-          Esta 1:19Basi mfalme akiona vema, na itoke kwake amri ya kifalme, nayo iandikwe katika sheria za Waajemi na Wamedi ISITANGUKE, ya kwamba Vashti asifike tena mbele ya mfalme Ahasuero; na umalkia wake mfalme ampe mwingine aliye mwema kuliko yeye.”

Unaweza kuona kuwa sheria zao zilikuwa kali na za kidikteta zisizoweza kutanguaka au kubadilishwa, hata hivyo kutokana na chuki na wivu kwa wayahudi wakati mwingine sheria za aina hii zilipitishwa ili kushindana na watu wa Mungu kama Daniel, pia Shadrak, Meshak na Abdednego, pia katika kitabu cha esta yanamkuta Mordekai na jamii nzima ya kiyahudi, ambao sasa wamepitihwa kuwa wauawe katika muswada huu wa sheria za watu hawa ambazo ni ngumu mno kuiztanbgua au kzibadilisha.

Ni muhimu kufahamu kuwa katika ulimwengu wa Kiroho, hali kadhalika ni vigumu kubadilisha jambo ambalo Mungu ameliamuru lipite au lisipitishwe, na sio hivyo tu lakini hata upande wa shetani ni vigumu kwake kuwa kigeugeu, yeye anapodhamiria kuleta uharibifu kwako huwa hatanii, anapokusudia kukushuhsia hukumu huwa hana muda wa kupoteza, mtu mwenye chuki anapokuendea kwa mganga na wachawi ili kukuharibu ni vigumu kwa Mchawi kurudi nyuma na kugeuka, ikiwa shetani amekukusudia kukuharibia, kukuaibisha,anahakikisha kuwa anakubana katika kiwango ambacho huwezi kuchomoka mpaka akubamize, atakufuatilia bila kurudi nyuma bila kubadilika bila kuitangua dhamira yake, jambo hili lilitambulika vema kwa wayahudi pia kuhusu makusudio mabaya ya Waamedi na waajemi dhidi yao. Maandiko wakati wote yanatuonyesha kuwa ni Mungu pakee anayeweza kuubadili Moyo wa mfalme kama apendavyo  Mithali 21:1Moyo wa mfalme huwa katika mkono wa Bwana; Kama mifereji ya maji huugeuza po pote apendapo.”  Unaona Biblia inatuthibitishia kuwa ni Mungu peke yake ndiye anayeweza kuugeuza moyo wa mfalme kokote apendapo yaani atakapo Mungu, lakini sio hivyo tu ni kwake yeye ndiko tunakoweza kukata rufaa ya sheria za kipuuzi zilizopitsihwa kwa misingi ya uonevu wa Ibilisi ni kwanamna gani tunaweza kufanya hilo ni kwa kuingia kwa mfalme kinyume cha sheria.

Kuingia kwa Mfalme kinyume cha sheria.

Kwa vile Esta na Mordekai walikuwa wanazifahamu sheria za waamedi na waajemi pamoja na desturi zao kwamba halikuwa jambo rahisi kuweza kuwaponya wayahudi na kujikoa wao wenyewe na mauti iliyokuwa imekusudiwa kuwakumba, Esta na Mordekai walikuwa wamekwisha kuwa na ujuzi kuwa wakati wowote unapokutana na jambo gumu ni maombi na pamoja na kufunga na kuomba tu ndio ilikuwa njia pekee ya kuweza kutangua sheria za kubahatisha za wanadamu, Esta aliamini katika nguvu ya kufunga na kuomba, watu wengi na dini nyingi zinaamini katika nguvu ya kufunga na kuomba hata na mimi ninaamini kuna nguvu katika kufunga na kuomba Yesu pia aliamini katika nguvu ya kufunga na kuomba yeye mwenyewe Yesu akasema kuna na mambo mengine hayawezekani isipokuwa kwa kufunga na kuomba Mathayo 17 :21[Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga.]Yesu alikuwa akimaanisha  kuwa kuna nguvu kubwa katika maombi yenye kujitoa kwa jambo lolote lile kama maombi ni hafifu matokeo yake yanakuwa hafifu na kama maombi ni yenye bidii matokeo yake yanakuwa makubwa sana, Esta alikuwa sio anakabiliwa na sheria na Muswada uliokuwa umepitishwa tu lakini kama malikia ambaye angeweza kuingia kwa mfalme kuwaombea wayahudi rehema yeye mwenyewe alikuwa anakabiliwa na desturi isiyotanguliwa ambayo nayo ingemgharimu kifo, kulikuwa na sesturi nyingne ya kiajemi ya kuwa malikia kama hujaitwa kwa mfalme na kisha ukaingia kwa mfalme bila kibali chake ungehukumiwa kufa, isipokuwa tu kama utapata neema na kunyooshewa fimbo ya dhahabu, kupitia nguvu ya maombi haya Esta alipata kibali kwa mfalme na kunyooshewa fimbo ya dhahabu na kupata neema ya kuwaombea wayahudi na kuitangua sheria iliyokuwa imewekwa Esta 4:15-16Basi Esta akawatuma ili wamjibu Mordekai, Uende ukawakusanye Wayahudi wote waliopo hapa Shushani, mkafunge kwa ajili yangu; msile wala kunywa muda wa siku tatu, usiku wala mchana, nami na wajakazi wangu tutafunga vile vile; kisha nitaingia kwa mfalme, kinyume cha sheria; nami nikiangamia, na niangamie.” Ni baada ya tukio hili ndipo Mungu alipoleta wokovu kwa  wayahudi na Mordekai na matendo yake mema mema Mordekai yaliyokuwa yamekaliwa yalikumbukwa na msalaba aliokuwa ameandaliwa kutundikwa ulitundikwa Hamani adui yake na adui wa Wayahudi  Esta 9:1-21 . “Hata ulipofika mwezi wa kumi na mbili, ndio mwezi wa Adari, siku yake ya kumi na tatu, amri ya mfalme na mbiu yake ilipowadia kutekelezwa; ambayo siku ile adui za Wayahudi walitumaini kuwatawala, bali kumebadilika kinyume, hata Wayahudi waliwatawala wale waliowachukia; siku ile ile Wayahudi wakakusanyika mijini mwao katika majimbo yote ya mfalme Ahasuero ili kuwatia mikono wale watu waliowatakia hasara; wala asiweze mtu kuwazuia, kwa kuwa hofu yao imewaangukia watu wote. Nao maakida wa majimbo, na majumbe, na maliwali, na wale waliofanya shughuli ya mfalme, waliwasaidia Wayahudi; kwa sababu hofu ya Mordekai imewaangukia. Maana Mordekai alikuwa mkuu nyumbani mwa mfalme, na sifa yake imevuma katika majimbo yote, kwa kuwa huyo Mordekai amezidi kukuzwa. Basi Wayahudi wakawapiga adui zao wote mapigo ya upanga, na machinjo, na maangamizo, wakawatenda kama wapendavyo wale waliowachukia. Hata huko Shushani ngomeni Wayahudi wakawaua watu mia tano, na kuwaangamiza.  Wakawaua na Parshandatha, na Dalfoni, na Aspatha, na Poratha, na Adalia, na Aridatha, na Parmashta, na Arisai, na Aridai, na Waizatha, wana kumi wa Hamani bin Hamedatha, adui ya Wayahudi; walakini juu ya nyara hawakuweka mikono. Siku ile mfalme akaletewa hesabu ya hao waliouawa huko Shushani ngomeni. Mfalme akamwambia malkia Esta, Wayahudi wamewaua watu mia tano hapa Shushani ngomeni na kuwaangamiza, pamoja na wana kumi wa Hamani, je! Wamefanyaje basi katika majimbo ya mfalme yaliyosalia! Basi, una nini uombalo? Nawe utapewa; ama unayo haja gani tena? Nayo itatimizwa. Ndipo Esta aliposema, Mfalme akiona vema, Wayahudi walioko Shushani na wapewe ruhusa kufanya tena kesho sawasawa na mbiu ya leo, na hao wana kumi wa Hamani watundikwe juu ya mti ule. Mfalme akaamuru vifanyike vivyo hivyo, mbiu ikapigwa huko Shushani, wakawatundika wale wana kumi wa Hamani. Basi Wayahudi wa Shushani wakakusanyika tena siku ya kumi na nne pia ya mwezi wa Adari, wakawaua watu mia tatu huko Shushani; walakini juu ya nyara hawakuweka mikono. Nao Wayahudi wengine waliokaa katika majimbo ya mfalme walikusanyika, wakazishindania maisha zao, wakajipatia raha mbele ya adui zao, wakawaua waliowachukia, watu sabini na tano elfu; walakini juu ya nyara hawakuweka mikono. Hii ndiyo siku ya kumi na tatu ya mwezi wa Adari; na siku ya kumi na nne ya mwezi huo wakapumzika, wakaifanya kuwa siku ya karamu na furaha. Lakini Wayahudi wa Shushani walikusanyika siku ya kumi na tatu ya mwezi huo, na siku ya kumi na nne pia; na siku ya kumi na tano ya mwezi uo huo wakapumzika, wakaifanya kuwa siku ya karamu na furaha. Kwa sababu hii Wayahudi wa vijijini, wakaao katika miji isiyo na boma, huishika siku ya kumi na nne ya mwezi wa Adari, kuwa siku ya furaha na karamu, sikukuu ya kupelekeana zawadi. Basi Mordekai aliyaandika mambo hayo; naye akapeleka barua kwa Wayahudi wote waliokaa katika majimbo yote ya mfalme Ahasuero, waliokuwa karibu na waliokuwa mbali, kuwaonya wazishike siku ya kumi na nne ya mwezi wa Adari, na siku ya kumi na tano yake, mwaka kwa mwaka,” Unaona kilio cha wayahudi kilibadilika kuwa furaha adui za wayahudi waliuawa wao, msalamba walikuwa wameutundika hamani kwaahiji ya Mordekai alitundikwa yeye mwenyewe, Heshima aliyokuwa akiitafuta Hamani ilipotea na Heshima ile alipewa Mordekai Esta 5:14, 6:1-2, Mfalme hatimaye aliongeza wema wake kwa wayahudi Esta 7. Mungu na kuongezee wema ikiwa utakubali kujitia chini yake na kuutafuta uso wake kwa kufunga.

Ndugu yangu mpendwa muamini Mungu yaamini maandiko huitaji kuhangaika dhidi ya adui zako ndani yako uko uwezo, unaozidi nguvu ya wadhalimu, unaozidi nguvu ya wachonganishi unaozoidi nguvu ya ibilisi, unaozidi nguvu za wanafiki, unaozidi nguvu za waganga na wachawi, unaozidi nguvu za maadui zako iko furaha uliyoandaliwa unayo ya kuingia kwa mfalme kinyume cha sheria na kukata rufaa, pale nguvu zetu zoinapopungua, pale kanisa linap[olemewa pale ibilisi na adui anapotukalia langoni iko dawa moja tu kwa kufunga na kuomba tutaweza kumsambaratisha adui na kupata kibali kwa mfalme na kutangua sheria yoyote inayotenda kazi kinyume na maisha yako; ni kwa kufunga na kuomba ni kwa kufunga na kuomba ni kwa kufunga na kuomba tunaweza kulete furaha ya kweli katima maisha yetu asomaye na afahamu.

Na mkuu wa wajenzi mwenye Hekima.

Rev. Innocent Kamote.

Mariam mama yake Bwana Yesu!




Mstari wa Msingi: Luka 1:26-33Mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na Mungu kwenda mpaka mji wa Galilaya, jina lake Nazareti, kwa mwanamwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu, jina lake Yusufu, wa mbari ya Daudi; na jina lake bikira huyo ni Mariamu. Akaingia nyumbani kwake akasema, Salamu, uliyepewa neema, Bwana yu pamoja nawe. Naye akafadhaika sana kwa ajili ya maneno yake, akawaza moyoni, Salamu hii ni ya namna gani? Malaika akamwambia, Usiogope, Mariamu, kwa maana umepata neema kwa Mungu.  Tazama, utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; na jina lake utamwita Yesu. Huyo atakuwa mkuu, ataitwa Mwana wa Aliye juu, na Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi, baba yake. Ataimiliki nyumba ya Yakobo hata milele, na ufalme wake utakuwa hauna mwisho
 

 


Maana ya jina Mariam.

Jina Mariam au Maria limetokana na jina la Kiyunani Maria na kwa kiaram Maria, kwa kiibrania Miriam kwa kiarabu Maryam ni Jina maarufu sana katika maandiko ya Kikristo na Kiislamu, Mariam ni mwanamke anayesadikiwa kuwa alibarikiwa sana kutokana na kupata neema ya Kumzaa mwokozi wa Ulimwengu yaani Bwana Yesu Kristo (Masihi). Jina hili Mariam maana yake ni mtumishi wa Mungu!

Mariam anatajwa kama mwanamke aliyekuwa mwanamwali yaani Bikira aliyekuwa anakaribia kuolewa au aliyekuwa amechumbiwa anasifiwa kwa sifa kubwa ya kuwa mwanamke mwaminifu aliyejitunza na mnyenyekevu aliyekuwa na uelewa wa juu sana kuhusu Neno la Mungu na Mapenzi ya Mungu. Mwanamke huyu alikuwa na asili ya ukoo wa Daudi ingawa aliishi Galilaya katika mji mdogo wa Nazareth kama yanenavyo maandiko yaani Agano jipya na Quran

Mwanamke huyu shujaa anatwaja na maandiko yote agano jipya na Quran kwamba alikuwa Bikira na alikuwa amebakiza muda tu wa kufungishwa ndoa kwa Yusufu ambaye naye pia alikuwa wa ukoo wa Mfalme Daudi, Bikira wa aina hii aliitwa PARTHENOS kwa kiyuinani yaani mwana mwali, aliyekuwa tayari kwa kutimiza tu ibada ya ndoa, alionekana kuwa ana mimba ni mimba ambayo vitabu vitakatifu vinaeleza wazi kuwa haikutokana na uashetari wala mbegu za kiume za mwanamume awaye yote, bali zilitokana na muujiza wa kiungu sawasawa na jinsi alivyotabiri nabii Isaya “TAZAMA BIKIRA ATACHUKUA MIMBA NAYE ATAZAA MWANA WA KIUME NAYE WATAMUITA JINA LAKE IMANUEL YAANI MUNGU PAMOJA NASI” 

Isaya 7:14Kwa hiyo Bwana mwenyewe atawapa ishara. Tazama, bikira atachukua mimba, atazaa mtoto mwanamume, naye atamwita jina lake Imanueli.”

Tukio hili halikuweza kumuumiza Yusufu kwa vile alikuwa na uelewa mpana wa Mapenzi ya Mungu aidha malaika wa bwana mjumbe wa Mungu Gabriel alimtokea na kumpa ufafanuzi kuhusu ujauzito huo, ni kutokana na hali hii Mariam aliambatana na Yusufu mpaka Bethelehemu kwaajili ya kuhesabiwa kutokana na amri ya Kaisari Augusto kwamba wahesabiwe watu wa utawala wake kila mmoja kwao na kwa vile Yusufu na Mariamu kwa asili ni watu wa Bethelehemu huko Uyahudi walikwenda huko ili wahesabiwe na kwa bahati nzuri Masihi alizaliwa huko, ili kutimiza Unabii wa Mika katika Mika 5:2 kwamba “Bali wewe, Bethlehemu Efrata, uliye mdogo kuwa miongoni mwa elfu za Yuda; kutoka kwako wewe atanitokea mmoja atakayekuwa mtawala katika Israeli; ambaye matokeo yake yamekuwa tangu zamani za kale, tangu milele.

Mwanamke huyu maarufu anatajwa kama mara 50 hivi katika injili, Quran imempa Sura maalumu iitwayo Surat al  Maryam  na inasemekana Quran inamtaja mara nyingi zaidi kama mwanamke mtakatifu katika Quran Maryam ametajwa mara 70

Mariam alitokewa Malaika Gabriel na kuelezwa rasmi kuwa amechaguliwa na Mungu kuwa mama wa Masihi, ni mwanamke mwenye uwezo mkubwa sana wa kuvumilia kwani licha ya kuwa na mtoto mwema mno kama Yesu injili imethibitisha kuwa alikuwepo wakati mwanae anasulubiwa na kuuawa kwaajili ya dhambi za ulimwengu hili lilikuwa ni tukio chungu sana na lilihitaji kuyajua mapenzi ya Mungu hasa na kwa uwazi Mariamu huenda katika kipindi hiki alikumbuka maneno ya nabii mzee aliyeitwa simeon ambaye aliahidiwa na Mungu kuwa hatakufa mpaka atakapomuona Masihi mzee huyu alimweleza maneno mazito Mariamu kumuandaa tayari kwa machungu ya kusulubiwa kwa mwanae miaka michache ijayo. 

Luka 2:21-35Hata zilipotimia siku nane za kumtahiri, aliitwa jina lake Yesu; kama alivyoitwa na malaika kabla hajachukuliwa mimba. Kisha, zilipotimia siku za kutakasika kwao, kama ilivyo torati ya Musa walikwenda naye hata Yerusalemu, wamweke kwa Bwana, (kama ilivyoandikwa katika sheria ya Bwana, Kila mtoto mwanamume aliye kifungua mimba ya mamaye na aitwe mtakatifu kwa Bwana), wakatoe na sadaka, kama ilivyonenwa katika sheria ya Bwana, Hua wawili au makinda ya njiwa wawili. Na tazama, pale Yerusalemu palikuwa na mtu, jina lake Simeoni, naye ni mtu mwenye haki, mcha Mungu, akiitarajia faraja ya Israeli; na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake. Naye alikuwa ameonywa na Roho Mtakatifu ya kwamba hataona mauti kabla ya kumwona Kristo wa Bwana. Basi akaja hekaluni ameongozwa na Roho; na wale wazazi walipomleta mtoto Yesu ndani, ili wamfanyie kama ilivyokuwa desturi ya sheria, yeye mwenyewe alimpokea mikononi mwake, akamshukuru Mungu, akisema, Sasa, Bwana, wamruhusu mtumishi wako, Kwa amani, kama ulivyosema;  Kwa kuwa macho yangu yameuona wokovu wako, Uliouweka tayari machoni pa watu wote; Nuru ya kuwa mwangaza wa Mataifa, Na kuwa utukufu wa watu wako Israeli. Na babaye na mamaye walikuwa wakiyastaajabia hayo yaliyonenwa juu yake. Simeoni akawabariki, akamwambia Mariamu mama yake, TAZAMA, HUYU AMEWEKWA KWA KUANGUKA NA KUINUKA WENGI WALIO KATIKA ISRAELI, NA KUWA ISHARA ITAKAYONENEWA. NAWE MWENYEWE, UPANGA UTAINGIA MOYONI MWAKO, ili yafunuliwe mawazo ya mioyo mingi.”

Mariamu hata baada ya kufufuka kwa Yesu alijiunga na wanafunzi wa kanisa la kwanza pale Yerusalem na maandiko yanamtaja kuwa aliungana katika maombi na wanafunzi na alikuwa miongozi mwa watu 120 waliojazwa Roho Mtakatifu japo kwa Mariamu huenda tukio hilo lilikuwa likijirudia kwa mara nyingine kwani Raoho wa Mungu alikuwa juu yake mapema zaidi ili aweze kukabidiwa jukumu la Kumbeba Bwana Yesu.

Kwa mujibu ya masimulizi ya kihistoria hasa ya wakatoliki na makanisa ya Othodox wanaamini kuwa mwili wake ulinyakuliwa Mbinguni moja kwa moja lakini swala hili linaitwa “Assumption” yaani inasadikiwa tu lakini hakuna uthibitisho wa moja kwa moja, Masimulizi mengine yanaeleza kuwa huenda alikuweko mpaka mwaka wa 70 AD wayahudi walipotawanywa na kupoteana na kutokuweko kwa uhakika kuwa ni wapi alifia, Mtume Yohana alipewa jukumu la kumlea Mariam lakini hata hivyo hajawahi kueleza lolote kuhusu Mwisho wake aidha baadhi ya wanawe kama Yuda aliyeandika waraka na Yakobo pia  ndugu zake bwana hawajawahi kueleza lolote kuhusu mama yao.
Mariamu anaheshimika na watu wengi sana na mamilioni ya watu wanaamini kuwa ni moja ya watakatifu muhimu sana katika dini, wengine wanaamini kuwa amewahi kuwatokea kimuujiza katika karne kadhaa, makanisa ya Othodox na Catholic na Anglican na Lutheran yanaamini kuwa kwa kuwa yesu ni Mungu na alizaliwa na Mariam basi Mariamu ni mama wa Mungu, baadhi ya mashirika ya kikatoliki kama Marian wao wanaamini na kumuita kuwa ni mama wa Mungu na wanaamini kuwa hata yeye kama ilivyo kwa yesu Kristo hakuwa na dhambi na kuwa alizaliwa pasipokuwa na dhambi, siwezi kusema lolote katika hili lakini ukweli ni kuwa Quran pia imemkubali sana Maryam na kuonyesha heshima kubwa sana juu yake akitetewa kuwa hakuwa na dhambi tofauti na mama wa Muhamad ambaye hatajwi kabisa katika kitabu hichi ukicha khadithi.

Pamoja na ubora wote huu kuhusu Mariamu na utakatifu wake kwetu sisi na kwangu mimi Mariamu ni mtakatifu kama walivyo watakatifu wote katika biblia, nakubali kuwa Yesu alimuheshimu sana mama yake lakini vilevile sisi nasi tunamuheshimu sana na kama mbingu zilivyomuheshimu sana kuwa ni Mtakatifu hilo hatuna mashaka nalo, kila mtu anaweza kuwa kama Mariamu tu kama tukiyashika maneno ya Mungu Yesu alisema “MAMA NA NDUGU ZANGU NI AKINA NANI? NI WALE WANAOLISIKIA NENO LA MUNGU NA KULISHIKA”  ni imani yangu pia kuwa furaha atakayokuwa nayo Mariamu inaweza kuwa furaha ya kila mmoja anayelisikia neno la Mungu na kulishika Yesu akasema  alipoulizwa ni furaha gani aliyonayo mwanamke aliyekuzaa na kukulea alijibu AMA NI FURAHA GANI WALIYONAYO WANAOLISIKIA NENO LA MUNGU NA KULITII” 

Katika kitabu cha matendo Mariamu anaonekana akiwa muombaji sawa na waombaji wengine kama Petro na wengineo, mariamu amebarikiwa hatuna shaka na hilo, Mariamu ytuko mbinguni kama watakatifu wengine hatuna shaka na hilo, Lakini Mariamu sio njia na kweli na uzima, yeye sio njia ya kumfikia Mungu aliye hai, yeye sio njia ya kutumika kutuombea kwa baba mbinguni, yeye sio mama wa Mungu, wala sio mke wa Mungu, yeye aliendelea kuwa mke wa Yusufu na alizaa watoto sita zaidi ukiacha Yesu mwanawe wa kwanza aliyemzaa kwa muujiza soma Mathayo 13:54-56Na alipofika nchi yake, akawafundisha katika sinagogi lao, hata wakashangaa, wakasema, Huyu amepata wapi hekima hii na miujiza hii? Huyu si mwana wa seremala? Mamaye si yeye aitwaye Mariamu? Na nduguze si YAKOBO, NA YUSUFU, NA SIMONI, NA YUDA? Na MAUMBU  (Dada zake) yake wote hawapo hapa petu? Basi huyu amepata wapi haya yote?”

Kama u mwanafunzi wa Biblia utaona wazi kuwa ndugu zake Yesu wametajwa katika Biblia Yakobo. Yusufu, Simoni na Yuda yaaninkaka wane na neno maumbu maana yeke dada zake ambao inakisiwa walikuwa wawili hivyo jumla ya wana wa Mariamu ni Saba na aliozaa na Yusufu ni sita, so kama Mariamu ni mama wa Mungu basi pia ni mama wa wanadamu! Kumbuka ni Yesu pekee ndie alikuwa mwana wa miujiza na yusufu aliendelea kuzaa na kufurahia maisha yake na Mariam inasadikiwa tu kuwa Yusufu alifariki mapema zaidi.

Wakati watu wanakazania kumuomba Mariamu ni muhimu kujikumbusha kuwa Mariamu alikuwa akimuomba Yesu pamoja na wanafunzi wake aliungana nao katika maombi Matendo ya Mitume 1:12-14Kisha wakarudi kwenda Yerusalemu kutoka mlima ulioitwa wa Mizeituni, ulio karibu na Yerusalemu, wapata mwendo wa sabato.Hata walipoingia, wakapanda orofani, walipokuwa wakikaa; Petro, na Yohana, na Yakobo, na Andrea, Filipo na Tomaso, Bartholomayo na Mathayo, Yakobo wa Alfayo, na Simoni Zelote, na Yuda wa Yakobo. Hawa wote walikuwa wakidumu kwa moyo mmoja katika kusali, pamoja nao wanawake, na Mariamu mama yake Yesu, na ndugu zake.” Unaona Mariamu mama yake Yesu na ndugu zake walikuwa miongoni mwa watu waombaji waliokuwa wakimuomba Mungu kwa jina la Yesu, dhana inayojengwa na baadhi ya watu wanaotaka kupotoshja maandiko wakisema kuwa Mariamu ni muombezi wanajenga hoja kupitia muujiza wa kana ya Galilaya wakati Yesu alipohudhuria harusini na kisha watu wakatindikiwa na Divai, Mariamu alikuja kumuomba Yesu na kumpa taarifa ya kutoikuweko kwa Divai Yesu hakukubali kwa urahisi kwani mariamu alitaka Yesu atumie uwezo wake wa kimuuijiza kabla ya wakati wa Mungu, hata hivyo alimuomba kwa imani na kuwagiza wanafunzi wake kuwa atakalowaagiza walifanye dhana hii haitufundishi kumuomba mariamu aku kumfanya mariamu kuwa ni muombezi bali inatufundisha kuwa tukiwa na uhitaji wowote ni lazima tumweleze Bwana yesu kwa imani naye ataenda Yohana  2:1-9Na siku ya tatu palikuwa na arusi huko Kana, mji wa Galilaya; naye mama yake Yesu alikuwapo. Yesu naye alikuwa amealikwa arusini pamoja na wanafunzi wake. Hata divai ilipowatindikia, mamaye Yesu akamwambia, Hawana divai. Yesu akamwambia, Mama, tuna nini mimi nawe? Saa yangu haijawadia. Mamaye akawaambia watumishi, Lo lote atakalowaambia, fanyeni. Basi kulikuwako huko mabalasi sita ya mawe, nayo yamewekwa huko kwa desturi ya Wayahudi ya kutawadha, kila moja lapata kadiri ya nzio mbili tatu. Yesu akawaambia, Jalizeni mabalasi maji. Nao wakayajaliza hata juu. Akawaambia, Sasa tekeni, mkampelekee mkuu wa meza. Wakapeleka. Naye mkuu wa meza alipoyaonja yale maji yaliyopata kuwa divai, (wala asijue ilikotoka, lakini watumishi walijua, wale walioyateka yale maji),” 

Ni muhimu kufahamu kuwa Yesu Kristo ni Mkuu kuliko Mariam, neema aliyopewa Mariamu ilikuwa ni kushiriki Baraka kubwa ya kumleta masihi Duniani, Lakini Mungu hajamfanya Mariamu kuwa mwombezi kwa sababu zozote zile Makuhani waombezi wote katika uyahudi walikuwa wanaume, Mariamu hakuwa nabii kama ilivyokuwa kwa Miriam wa agano la kale aliyekuwa Dada wa Musa na Haruni,  alikuwa ni mwanamke shujaa jasiri na mwenye imani katika kutunza neno na ahadi za Mungu, Mungu hajawahi kumfanya Mariamu kuwa malkia wa Mbinguni wala hajawahi kumfanya mariamu kuwa sehemu ya ibada, Mariam atasikitika sana kama atarudi duniani na kukuta akuombwa na kuabudiwa kama Mungu kwa unyenyekevu aliokuwa nao angeshangaa kukuta kufuru hii.

Njia pekee ya kumfikia Mungu ni Yesu naye ndiye kipatanisho pekee kati ya Mungu na wanadamu, 1Yohana 2:1-2Watoto wangu wadogo, nawaandikia haya ili kwamba msitende dhambi. Na kama mtu akitenda dhambi tunaye Mwombezi kwa Baba, Yesu Kristo mwenye haki, naye ndiye kipatanisho kwa dhambi zetu; wala si kwa dhambi zetu tu, bali na kwa dhambi za ulimwengu wote.” 

Unapotumia Muda wako kumuomba Mungu kupitia Mariamu unapoteza lengo la maombi yako huku ukiwa na nia nzuri lakini sio ya kimaandiko ni vema dua zetu na maombi yetu tukamuombababa wa Mbinguni kwa njia ya mwanae Yesu Kristo pekee

Yohana 16:23-24Tena siku ile hamtaniuliza neno lo lote. Amin, amin, nawaambia, Mkimwomba Baba neno lo lote atawapa KWA JINA LANGU.  Hata sasa hamkuomba neno KWA JINA LANGU; ombeni, nanyi mtapata; furaha yenu iwe timilifu.”
 
Wengi hawana furaha hawajawahi nkufurahia uwepo wa Mungu na utendaji wa Mungu kwa sababu hawajawahi kuomba kwa jina la Yesu wamedanganywa na kudanganyika wakiomba kupitia majina mengine Yesu Mwenye yu ashauri hivi Yohana 14:13-14Nanyi mkiomba lo lote kwa jina langu, hilo nitalifanya, ili Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Mkiniomba neno lo lote kwa jina langu, nitalifanya”: ni jambo la kusikitisha sana katika Karne hii ya uwazi na ukweli yautafiti na ujuzi ya hekima na maarifa neno la mungu liko wazi kila mahali bado kuna watu wanatumia jina la Mariamu katika maombezi, ni malizie kwa kusema kuwa Roho Mtakatifu ndiye anayetuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa.

Kama hujui kuomba ruhusu Roho Mtakatifu akufundisha kuomba maana yeye ndio muombezi mkuu na sio Mariamu Warumi 8:26-27 “Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa. Na yeye aichunguzaye mioyo aijua nia ya Roho ilivyo, kwa kuwa huwaombea watakatifu kama apendavyo Mungu.” 

Ni imani yangu kuwa utaifahamu kweli nayo itakuweka Huru katika jina la Yesu Kristo aliye hai amen!

Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima