Ijumaa, 25 Desemba 2020

Kupimwa kwa kazi ya kila mtu !

1Wakoritho 3:10-15 “Kwa kadiri ya neema ya Mungu niliyopewa, mimi, kama mkuu wa wajenzi mwenye hekima, naliuweka msingi, na mtu mwingine anajenga juu yake. Lakini kila mtu na aangalie jinsi anavyojenga juu yake. Maana msingi mwingine hakuna mtu awezaye kuuweka, isipokuwa ni ule uliokwisha kuwekwa, yaani, Yesu Kristo. Lakini kama mtu akijenga juu ya msingi huo, dhahabu au fedha au mawe ya thamani, au miti au majani au manyasi, kazi ya kila mtu itakuwa dhahiri. Maana siku ile itaidhihirisha, kwa kuwa yafunuliwa katika moto; na ule moto wenyewe utaijaribu kazi ya kila mtu, ni ya namna gani. Kazi ya mtu aliyoijenga juu yake ikikaa, atapata thawabu. Kazi ya mtu ikiteketea, atapata hasara; ila yeye mwenyewe ataokolewa; lakini ni kama kwa moto” 

 

 


 


 

Utangulizi:

 

 

Ni muhimu kufahamu kuwa katika ulimwengu tulionao Mungu alimleta kila mtu Duniani kwa kusudi la kutimiza wajibu Fulani katika maisha yake,  kwa sababu hiyo  siku ya hukumu kila mmoja atatoa hesabu ya kazi au kusudi alilolifanya hakutakuwa na kisingizio kuwa hili linanipata kwa sababu ya Fulani, wote tutatioa hesabu mbele za Mungu na kila mtu atabeba mzigo wake kulingana na kazi au namna alivyotimiza  wajibu na kusudi lake duniani ona.;- 

 

Wagalatia 6:4-5 “Lakini kila mtu na aipime kazi yake mwenyewe, ndipo atakapokuwa na sababu ya kujisifu ndani ya nafsi yake tu, wala si kwa mwenzake. Maana kila mtu atalichukua furushi lake mwenyewe. 

 

Tutajifunza so mo hili kwa kuzingatia vipengele vitatu vifuatavyo:-

 

·         Umuhimu wa kutimiza kusudi la Mungu!

·         Mifano ya watu waliotimiza kusudi la Mungu kwa uaminifu!.

·         Faida za kutimiza kusudi la Mungu!

 

Umuhimu wa kutimiza kusudi la Mungu!

 

Kwa msingi huo ni muhimu kwa kila mmoja wetu kuhakikisha kuwa anajua ni kwa nini yuko Duniani na amekuja kufanya nini duniani, kisha pambana kwa kila namna uwezavyo kuhakikisha kuwa unafikia lengo na kusudi kubwa la Mungu jkukuleta duniani, Katika maandiko Daudi anatajwa kama mtu aliyeweza kutimiza kusudi au shauri lote la Mungu, hakuondoka duniania akiwa amebakiza kazi fulani alihakikisha kuwa anaitimiza yote yaliyomo katika moyo wa Mungu na hata alitaka kuzidisha!

 

Matendo 13:36 “Kwa maana Daudi, akiisha kulitumikia shauri la Mungu katika kizazi chake, alilala, akawekwa pamoja na baba zake, akaona uharibifu.

 

Shauri l Mungu maana yake ni Kusudi lote la Mungu, kila mmoja anao wajibu wa kutimiza kusudi lote la Mungu, kuhakikisha kuwa unamaliza vema unahitimisha kazi yako vema, unatenda vema kusudi la Mungu, kama ni kuhubiri ni lazima tuhakikishe kuwa tunahubiri kusudi lote la Mungu, kama ni kuchunga tunachunga kwa kusudi lote la Mungu kama ni kufundisha tunafundisha kama Mungu anavyokusudia, kama ni kusoma tunasoma kama Mungu alivyokusudia, kama ni kuhubiri injili unahubiri kama Mungu alivyokusudia na kama ni kuongoza unaongoza kama Mungu alivyokusudia, Paulo Mtume alipohubiri injili aliweka wazi kuwa aliwahubiria watu kile ambacho Mungu alikusudia na hivyo  alihubiri kusudi lote la Mungu!

 

 Matendo 20:25-27 “Na sasa, tazameni, mimi najua ya kuwa ninyi nyote niliowahubiria ufalme wa Mungu, nikienda huko na huko, hamtaniona uso tena. Kwa hiyo nawashuhudia wote siku hii ya leo, ya kuwa mimi sina hatia kwa damu ya mtu awaye yote. Kwa maana sikujiepusha na kuwahubiria habari ya kusudi lote la Mungu.”

 

Mifano ya watu waliotimiza kusudi la Mungu kwa uaminifu!.

 

Wako watu mbalimbali katika maandiko ambao wanatajwa kuwa walitimiza makusudi ya Mungu kwa uaminifu na walitioa hesabu na kujifanyia tathimini;-

 

1.       Yesu mwenyewe alijifanyia tathimini na kutoa Ripoti kuwa amemaliza kusudi lote la Mungu, ukiacha kuwa siku ya kusulubiwa kwake alisema IMEKWISHA yaani alitimiza makusudi yote ya Mungu lakini vilevile alitoa hesabu ya kile ambacho baba alikuwa amemuagiza kukitimiza na kwa uhakikika kabisa alikuwa ameyatimiza hivyo kama asemavyo mwenyewe katika  injili ona ;-Yohana 17:1-13 “Maneno hayo aliyasema Yesu; akainua macho yake kuelekea mbinguni, akasema, Baba, saa imekwisha kufika. Mtukuze Mwanao, ili Mwana wako naye akutukuze wewe; kama vile ulivyompa mamlaka juu ya wote wenye mwili, ili kwamba wote uliompa awape uzima wa milele. Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma. Mimi nimekutukuza duniani, hali nimeimaliza kazi ile uliyonipa niifanye.  Na sasa, Baba, unitukuze mimi pamoja nawe, kwa utukufu ule niliokuwa nao pamoja nawe kabla ya ulimwengu kuwako. Jina lako nimewadhihirishia watu wale ulionipa katika ulimwengu; walikuwa wako, ukanipa mimi, na neno lako wamelishika. Sasa wamejua ya kuwa yote uliyonipa yatoka kwako. Kwa kuwa maneno uliyonipa nimewapa wao; nao wakayapokea, wakajua hakika ya kuwa nalitoka kwako, wakasadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma. Mimi nawaombea hao; siuombei ulimwengu; bali hao ulionipa, kwa kuwa hao ni wako; na wote walio wangu ni wako, na walio wako ni wangu; nami nimetukuzwa ndani yao. Wala mimi simo tena ulimwenguni, lakini hawa wamo ulimwenguni, nami naja kwako. Baba mtakatifu, kwa jina lako ulilonipa uwalinde hawa, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo. Nilipokuwapo pamoja nao, mimi naliwalinda kwa jina lako ulilonipa, nikawatunza; wala hapana mmojawapo wao aliyepotea, ila yule mwana wa upotevu, ili andiko litimie.  Na sasa naja kwako; na maneno haya nayasema ulimwenguni, ili wawe na furaha yangu imetimizwa ndani yao.”

 

2.       Paulo Mtume alihakikisha kuwa ametimiza kusudi lote la Mungu na kwa ujasiri kabisa alimuekleza Timotheo kuwa anasubiri taji yaani thawabu kubwa kwa sababu alikamilisha kile alichokusudiwa na Mungu kwa uaminifu mkubwa kwa mapambano na kwa mwendo mrefu na aliukamilisha  ona 2Timotheo 4;6-8 “Kwa maana, mimi sasa namiminwa, na wakati wa kufariki kwangu umefika. Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda;  baada ya hayo nimewekewa taji ya haki, ambayo Bwana, mhukumu mwenye haki, atanipa siku ile; wala si mimi tu, bali na watu wote pia waliopenda kufunuliwa kwake.”

 

3.       Musa alikuwa mwaminifu katika kazi yote nya Mungu, maana yake alikamilisha jukumu lake duniani, Musa alilitumikia kusudi la Mungu mpaka akasahau kifo, ilibidi Mungu amkubushe kwamba apande kwake mlimani akafe kwa sababu alikuwa mwaminifu mpaka sekunde ya mwisho Waebrania 3:5 “Na Musa kweli alikuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Mungu kama mtumishi, awe ushuhuda wa mambo yatakayonenwa baadaye;

 

4.       Yoshua alikuwa kiongozi mkubwa jemadari na shujaa alitimiza makusudi ya Mungu hadi  mwisho na kuhakikisha kuwa anaonyesha msimamo wake hata kwa wana wa Israek kuwa yeye na nyumba yake wameamua kwa dhati kuwa watamtumikia Mungu aliye hai ona Yoshua 24:14-18 “Basi sasa mcheni Bwana, mkamtumikie kwa unyofu wa moyo na kwa kweli; na kuiweka mbali miungu ambayo baba zenu waliitumikia ng'ambo ya Mto, na huko Misri; mkamtumikie yeye Bwana. Nanyi kama mkiona ni vibaya kumtumikia Bwana, chagueni hivi leo mtakayemtumikia; kwamba ni miungu ile ambayo baba zenu waliitumikia ng'ambo ya Mto, au kwamba ni miungu ya wale Waamori ambao mnakaa katika nchi yao; lakini mimi na nyumba yangu tutamtumikia Bwana. Hao watu wakajibu wakasema, Hasha! Tusimwache Bwana, ili kuitumikia miungu mingine;  kwa maana Bwana, Mungu wetu, yeye ndiye aliyetupandisha sisi na baba zetu kutoka nchi ya Misri; kutoka nyumba ya utumwa; naye ndiye aliyezifanya ishara zile kubwa mbele ya macho yetu, na kutulinda katika njia ile yote tuliyoiendea, na kati ya watu wa mataifa yote tuliopita katikati yao. Bwana ndiye aliyewafukuza watu wa mataifa yote watoke mbele yetu, naam, Waamori waliokaa katika nchi hii; basi, kwa sababu hiyo sisi nasi tutamtumikia Bwana, maana yeye ndiye Mungu wetu.”               

 

5.       Nabii Samuel aliishi maisha ya haki, hakudhuklumu mtu na mbele ya watu wote alijipambanua kuwa hakuwa na tatizo na Mtu he was a man of integrity   alihitmisha akiwa na ujasiri kuwa hakuwahi kumuonea mtu wala kumdhulumu mtu na kuwa alihitimisha akiwa na mikono safi je wewe unahitimisha vipi katika utumishi wako, je watu watakumbuka namna ulivyowaliza? Na kuwaonea na kuwatendea mabaya? Samuel alimaliza vema ona  katika 1Samuel 12:3-5 “Nami nipo hapa; basi, mnishuhudie mbele za Bwana, na mbele ya masihi wake,nalitwaa ng`ombe wa nani? au nalitwaa punda wa nani? au ni nani niliye mdhulumu? Ni nani niliyemwonea? Au kwa mkono wa nani nimepokea rushwa inipofushe macho? Nami nitawarudishia ninyi. Nao wakasema, hukutudhulumu, wala hukutuonea, wala hukupokea kitu kwa mkono wa mtu awaye yote. Akawaambia, Bwana ni shahidi juu yenu, na masihi

 

6.       Henoko alikuwa mwaminifu alitembea na Mungu, mwandishi wa kitabu cha mwanzo anamfanyia tathimini Henoko na kumuonyesha kuwa mtu wa tofauti, yeye licha ya kuzaa kama wengine licha ya kuishi maisha marefu alitembea na Mungu kiasi Mungu aliamua kumfanya kuwa malaika

 

Mwanzo 5:8-14 “ Siku zote za Sethi ni miaka mia kenda na kumi na miwili, akafa. Enoshi akaishi miaka tisini, akamzaa Kenani. Enoshi akaishi baada ya kumzaa Kenani miaka mia nane na kumi na mitano, akazaa wana, waume na wake. Siku zote za Enoshi ni miaka mia kenda na mitano, akafa. Kenani akaishi miaka sabini, akamzaa Mahalaleli. Kenani akaishi baada ya kumzaa Mahalaleli miaka mia nane na arobaini, akazaa wana, waume na wake. Siku zote za Kenani ni miaka mia kenda na kumi, akafa. Mahalaleli akaishi miaka sitini na mitano, akamzaa Yaredi. Mahalaleli akaishi baada ya kumzaa Yaredi miaka mia nane na thelathini, akazaa wana, waume na wake. Siku zote za Mahalaleli ni miaka mia nane na tisini na mitano, akafa. Yaredi akaishi miaka mia na sitini na miwili, akamzaa Henoko. Yaredi akaishi baada ya kumzaa Henoko miaka mia nane, akazaa wana, waume na wake.  Siku zote za Yaredi ni miaka mia kenda na sitini na miwili, akafa. Henoko akaishi miaka sitini na mitano, akamzaa Methusela. Henoko akaenda pamoja na Mungu baada ya kumzaa Methusela miaka mia tatu, akazaa wana, waume na wake. Siku zote za Henoko ni miaka mia tatu na sitini na mitano. Henoko akaenda pamoja na Mungu, naye akatoweka, maana Mungu alimtwaa.”

 

Hao walikuwa ni baadhi ya watu muhimu katika biblia ambao walijifanyia tathimini katika maisha yao na kutimiza makusudi ya Mungu vema, kila mmoja anapaswa kutimiza wajibu wake vema, tukikumbuka na kuelewa ya kuwa tutatoa hesabu mbele za Mungu, katia Nyanja yoyote ambayo Mungu amekuita unapaswa kuhakikisha kuwa unafanya vema, Florence Nightingale mwanzilishi wa uuguzi duniani alisimama vema katika kusudi lake mpaka leo anakumbukwa kwa kazi yake katika siku ya wauguzi duniani,  ni vema kila mmoja akafanya vema, mainjinia wasipunje, viwango vya barabara za lami hata kwa chepe moja la kokoto, Mizani za wafanya biashara ziwe za haki, madaktari na wafanye kwa uadilifu, Walimu wafundishe kwa bidii na wanafunzi wasome kwa bidii ni wakati wa kila mmoja kutimiza wajibu wake vema ili mbele za Mungu anwanadamu tuonekane kuwa na haki na kuepuka hukumu wakati kazi zetu zitakapopimwa!

 

Faida za kutimiza kusudi la Mungu!

 

Mungu ataipima kazi ya kila mmoja wetu kama lisemavyo neon la msingi, kila mmoja anapaswa kujifanyia tathimini kama anafanya kwa ubora kile ambacho Mungu amekusudia ndani yake, katika hukumu za Mungu ziko hukumu za aina nne Mungu aatakazowahukumu wanadamu

 

1.       Present judgment – hukumu iliyoko sasa kama mtu hajampokea Yesu hajamuamini huyo kwa sasa tunapozungumza ujumbe huu amekwisha kuhukumiwa angalia Yohana 3:16-18 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. Maana Mungu hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye.  Amwaminiye yeye hahukumiwi; asiyeamini amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu.” Ili kuepuka hukumu hii basi mwanadamu anapaswa kumuamini Yesu

 

2.       Hukumu ya adhabu Warumi 8:1 Sasa, basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu.” Hukumu hii ni hukumu ya aibu hukumu ya adhabu kwa kiyunani inaitwa KRI MA Mungu atafunua siri zote za uovu za wale wasiomuamini Mungu na wale waliotenda vibaya ona Muhubiri 12:14 “Kwa maana Mungu ataleta hukumuni kila kazi, pamoja na kila neno la siri, likiwa jema au likiwa baya.” Mungu atafupisha maisha au hata kazi za mtu asiyetenda vema hakikisha kuwa unatenda vema

 

3.       Hukumu isiyo ya adhabu Warumi 8:1 “Sasa, basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu.” Hii ni hukumu ya watakatifu, pamoja na neema ya kuingia mbinguni Mungu atamlipa kila mmoja sawa na kazi njema aliyoitenda kazi hizo zitajaribiwa kwa moto  kama ni ya majani, miti na nyasi itateketea na haitaleta heshima kwetu, lakini pamoja na kumuamini Yesu tunapaswa kutenda vema hukumu hii kwa kiyunani inaitwa KRINO ni hukumu isiyo ya adhabu kwa wale walio katika Kristo lakini kazi ya kila mmoja itapimwa, Yesu ataketi katika kiti cha Enzi kiitwacho Bema na kutoa thawabu kwa kazi zetu1Wakoritho 3:10-15 “Kwa kadiri ya neema ya Mungu niliyopewa, mimi, kama mkuu wa wajenzi mwenye hekima, naliuweka msingi, na mtu mwingine anajenga juu yake. Lakini kila mtu na aangalie jinsi anavyojenga juu yake. Maana msingi mwingine hakuna mtu awezaye kuuweka, isipokuwa ni ule uliokwisha kuwekwa, yaani, Yesu Kristo. Lakini kama mtu akijenga juu ya msingi huo, dhahabu au fedha au mawe ya thamani, au miti au majani au manyasi, kazi ya kila mtu itakuwa dhahiri. Maana siku ile itaidhihirisha, kwa kuwa yafunuliwa katika moto; na ule moto wenyewe utaijaribu kazi ya kila mtu, ni ya namna gani. Kazi ya mtu aliyoijenga juu yake ikikaa, atapata thawabu. Kazi ya mtu ikiteketea, atapata hasara; ila yeye mwenyewe ataokolewa; lakini ni kama kwa moto  

 

4.       Mungu anajua, un predictable judgment hii ni hukumu isiyotabirika   Warumi 14:4 ” Wewe u nani unayemhukumu mtumishi wa mwingine? Kwa bwana wake mwenyewe yeye husimama au huanguka. Naam, atasimamishwa, kwa kuwa Bwana aweza kumsimamisha.“Yeye ni Bwana ana maamuzi yake kama unavyokwenda kwa hakimu anaweza kuamua lolote kama apendavyo mwenyewe hakuna mtu anayejua rehema za Mungu, haiyamkini bwana anaweza kutyangaza rehema kwa mtu, yeyote au hata kwa watu wote kwani utamwambia nini yeye si ndio Mungu? Ndio anaweza kuamua lolote utamfanya nini aliamua utamuuliza nini, Tufanye kazi zetu kwa bidii kwani maandiko yamesema iko thawabu kubwa sana waongoze wengi katika kutenda haki nawe utafaidika!

 

Daniel 12;3  Na walio na hekima watang'aa kama mwangaza wa anga; na hao waongozao wengi kutenda haki watang'aa kama nyota milele na milele.

 

Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima

0718990796

Upendo mwingi!

Yoahan 15:13 “Hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake.”



Utangulizi:

Moja ya maagizo ya mwisho kabisa ya Yesu Kristo kwa wanafunzi wake kabla ya kuteswa, kufa na kufufuka ilikuwa ni kuhakikisha kuwa wanafunzi wake wanakuwa na upendo, wote tunafahamu kuhusu kupenda, lakini Yesu hakutaka tu tuwe tunapenda lakini alitaka wawe na upendo mwingi sana, unaweza kujiuliza upendo mwingi ni upendo wa namna gani? Biblia nyingine za Kiswahili zinatumia neno upendo mkuu, biblia ya kiingereza inatumia neno “The Great love” ambalo ka Kiswahili ni Upendo mwingi au upendo mkuu! Kwanini Yesu anazungumzia upendo mwingi kwani kuna upendo kidogo au mchache ndio kuna upendo kamili “Perfect Love au “sacrificial love” na upendo mwingine wenye upungufu!

Katika Lugha ya kiyunani neno upendo linaelezewa vizuri, sana kwa kuzingatia maeneo manne

1.       Phileo – Huu ni upendo au uhusiano wa kirafiki, unampenda mtu kwa sababu ni rafiki yako mahusiano yenu ni ya kirafiki, upendo huu una mipaka, kwa sababu unaweza kufa unaweza kuharibika ndio maana unaweza kuona watu wanafarakana na wanaweza hata kusalitiana na urafiki ukageuka kuwa uadui mkubwa

2.       Storge – Huu ni Upendo au uhusiano wa kindugu, unampenda mtu kwa sababu ni ndugu yako, mna uhusiano wa damu, uhusiano wa kubaiolojia ni babam ni mama, ni mama mdogo ni baba mdogo, ni binamu, ni shangazi, ni babu, ni bibi na kadhalika upendo huu pia una mipaka na unaweza kuharibika na ndugu wakageuka kuwa maadui wakubwa sana

3.       Eros – Huu ni upendo au uhusiano wa kimapenzi, ni upendo wa asili ya kibinadamu ambao mvutio wake unatokana na mapenzi, so unaweza kumpenda mtu kwa sababu ana usio mzuri, hana malolo, Yakobo alimpenda Raheli kuliko Leah kwa sababu Lea alikuwa na macho dhaifu alikuwa na malolo, unaweza kumpenda mtu kwa sababu ana makalio makubwa, mazito, hips za kutikisa dunia, ana chuchu zilizosimama, saa sita ni mkwaju wa nguvu umbo namba nane, potable au ana mzigo mzito wa kitikisa dunia na kadhalika huu ni upedno wenye hisia za kimapenzi

4.       Agape – Upendo huu sasa ndio unaoitwa upendo mwingi, ni upendo wenye kujitoa sacrificial love , upendo huu ni mgumu kuwa nao, ni watu wachahce sana wanaweza kuwa na upendo kama huu, Yesu aliuita upendo huu kuwa ni upendo mkuu, ni upendo mwingi, unahusisha kupenda mpaka kuyatia maisha yako kwaajili yaw engine Yohana 3:16 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele upendo huu mtu akiwa nao ndio tunasema amekomaa kiroho, ni upendo ambao una sifa za kipekee 1Wakoritho 15:1-13Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao. Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, si kitu mimi. Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, kama sina upendo, hainifaidii kitu. Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni; haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya; haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli; huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote. Upendo haupungui neno wakati wo wote; bali ukiwapo unabii utabatilika; zikiwapo lugha, zitakoma; yakiwapo maarifa, yatabatilika. Kwa maana tunafahamu kwa sehemu; na tunafanya unabii kwa sehemu; lakini ijapo ile iliyo kamili, iliyo kwa sehemu itabatilika. Nilipokuwa mtoto mchanga, nalisema kama mtoto mchanga, nalifahamu kama mtoto mchanga, nalifikiri kama mtoto mchanga; tokea hapo nilipokuwa mtu mzima, nimeyabatilisha mambo ya kitoto. Maana wakati wa sasa tunaona kwa kioo kwa jinsi ya fumbo; wakati ule tutaona uso kwa uso; wakati wa sasa nafahamu kwa sehemu; wakati ule nitajua sana kama mimi nami ninavyojuliwa sana. Basi, sasa inadumu imani, tumaini, upendo, haya matatu; na katika hayo lililo kuu ni upendo.”

 

Ukomavu wetu wa juu sana Kiroho utajulikana pale tunapokuwa tayari kuyatoa maisha yetu kwaajili ya wengine 

 

Yuda - Mwanzo 44:1-34,·  Alikuwa mwenye upendo mwingi sana alikuwa tayari kufa kwaajili ya kuitunza familia yake na baba yake na kwaajili ya ndugu zake

Daudi - 2Samuel 18:31-33·   alikuwa na upendo mwingi kiasi ambacho alilia kwaajili ya Absalom mwanaye japokuwa yeye alikuwa amekusudia kumuua baba yake

 

Yesu Kristo Yohana 15:13:- “Hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake· kwa ajili ya rafiki zake”.

 

1. Daktari mmoja wa Uingereza aitwaye Will Pooley alikuwa ni moja ya madaktari waliokuwa mstari wa mbele Nchini “Sierra Leone” huko walikuwa na wenzake wengi wakipambana na wagonjwa wa EBOLA na virusi vyake katika harakati hizo Madaktari wengi sana na Manesi wengi sana wakiwemo wa Afrika Magharibi waliambukizwa virusi vya ebola wakati walipokuwa wakiwauguza wagonjwa na wengi wao walikufa Ugonjwa utokanao na kirusi cha Ebola ni ugonjwa hatari wenye uwezo wa kusababisha kifo kwa asilimia 90. Shirika la afya duniani, WHO katikatovuti yake inasema kwa mara ya kwanza ulibainika mwaka 1976 huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC na Sudan. Chanzo cha kirusi hiki hadi sasa hakijulikani lakini popo aina ya (Pteropodidae) wanaonekana kuwa wabebaji wa kirusi hicho, kwa mujibu wa ushahidi uliopo sasa. Maambukizi hupatikana kwa kila aina ya majimaji yanayotoka katika mwili wa binadamu ni ugonjwa hatari na unaoua kwa haraka na hauna tiba Will Pooley alipoupata ugonjwa huu alirejeshwa katika ndege maalumu na kuanza kutibiwa chini ya uangalizi maalumu huko uingereza Jambo la kushangaza ni kuwa baada ya kupona kwa bahati tu Will Pooley alitangaza nia yake ya kurudi tena Sierra Leone kusaidiana na wenzake kupambana na ugonjwa huo. Mtu huyu aliwashangaza wengi sana na kuwaogopedha wengi sana akiwa amepona kwa asilimia 100%alisema atarudi Africa kusaidia zaidi maana alizaliwa kwaajili ya hayo, jambo hili lilimfanya aandikwe kama shujaa na mwanadamu mwenye uwezo wa kujitoa kwa kiwango cha juu.

 

2. Maximilian Kolbe alikuwa ni Padre aliyetokea Poland aliuawa kama mfungwa tarehe 14 August 14,1941, Jeshi la wa NAZI waligundua kuwa baadhi ya wafungwa wamejaribu kutoroka na hivyo waliamua kuwaua wafungwa kadhaa, walijaribu kuwaua kwa njia mbalimbali, na hivyo walichagua wafungwa 10 ili wauawe na kifo chao kiliamuriwa kuwa kifo cha njaa, wafungwa waliamuriwa kujitoa mmoja mmoja yeye mwenyewe na mfungwa wa kwanza kuchaguliwa alijulikana kama Franciszek Gajowinczek mfungwa huyu alipochaguliwa alilia kwa huzuni kubwa akimtaja mkewe, watoto wake na familia yake na kusikitika kuwa hatowaona tena kutokana na swala hili Maximillian alisimama na kusogea mbele na kuomba afe yeye kwa niaba ya Franciszek ombi lake lilikubaliwa, wafungwa waliwekwa kizuizini kwa muda wa siku kadhaa bila kula wengine walikunywa mikojo yao ili waweze kuishi, Maximillian alikaa kwa wiki mbili bila kufa huku wengine wote wakiwa wamekufa, walimchoma sindano ya kufa hakufa na hivyo waliamua kukata kichwa Pope John Paul II alimtangaza kuwa Mtakatifu kutokana na moyo wake

 

3. Mifano hii inatusaidia kujua kile ambacho Bwana wetu Yesu amekifanya Pale alipojibu kuwa kwaajili ya haya Nalizaliwa alikuwa akimkumbusha Pilato kuwa yeye amekuja kuwafia wanadamu, amekuja kuwaonyesha upendo wa Mungu jinsi ulivyo Isaya 53:1-5 “Ni nani aliyesadiki habari tuliyoileta? Na mkono wa Bwana amefunuliwa nani? Maana alikua mbele zake kama mche mwororo, Na kama mzizi katika nchi kavu; Yeye hana umbo wala uzuri; Na tumwonapo hana uzuri hata tumtamani. Alidharauliwa na kukataliwa na watu; Mtu wa huzuni nyingi, ajuaye sikitiko; Na kama mtu ambaye watu humficha nyuso zao, Alidharauliwa wala hatukumhesabu kuwa kitu. Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu; Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa, Amepigwa na Mungu, na kuteswa. Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona.” Huu ni upendo mkubwa sana Yesu alikufa kwaajili yetu, Hatuna budi kuhakikisha kuwa tunasimama upande wake siku zote za maisha yetu, tusihesabu damu yake ya thamani kuwa kitu cha hovyo tudumu katika wokovu na kuwa wavumilivu kwaajili ya Mungu wetu.”

Na Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima

Jumatatu, 23 Novemba 2020

Mzeituni umeao katika nyumba ya Mungu!

Zaburi 52:8 “Bali mimi ni kama mzeituni Umeao katika nyumba ya Mungu. Nazitumainia fadhili za Mungu milele na milele.”



Utangulizi:

Ni muhimu kufahamu kuwa Mungu katika hekima yake alipouumba ulimwengu, aliiuumba ili uwe zawadi kubwa kwa wanadamu,  na aliweka miti na mimea kwaajili ya uhai na utatuzi wa matatizo ya kiafya kwa wanadamu, kwa msingi huo basi utaweza kuona kuwa, Miti ina uhusiano mkubwa wa uhai maisha na hata nafsi ya mwanadamu Lakini miti pia ina uhusiano wa kiroho na maisha ya mwanadamu. Mungu aliitoa miti na mimea kama zawadi kwa wanadamu kwaajili ya kunufaisha maisha yao ona Mwanzo 1:29 “Mungu akasema, Tazama, nimewapa kila mche utoao mbegu, ulio juu ya uso wa nchi yote pia, na kila mti, ambao matunda yake yana mbegu; vitakuwa ndivyo chakula chenu;

Katika miti au miche ambayo ilitolewa kama zawadi kwa wanadamu moja ya mti wa ajabu sana wenye nguvu za mwilini na rohoni ni mti wa Mzeituni, mti huu ni malimbuko ya amani ya dunia ni ni mti wa kwanza kutajwa mara baada ya gharika wakati wa nabii Nuhu, ukiacha mti wa mtini ambao ulitajwa mapema sana mara baada ya anguko la mwanadamu ona Mwanzo 8:6-12 “Ikawa baada ya siku arobaini, Nuhu akalifungua dirisha la safina, alilolifanya; akatoa kunguru, naye akatoka akaenda huko na huko, hata maji yakakauka juu ya nchi. Kisha akatoa njiwa, aone kwamba maji yamepunguka usoni pa nchi; bali yule njiwa hakuona mahali pa kutua kwa wayo wa mguu wake, akamrudia Nuhu safinani, maana maji yalikuwa juu ya uso wa nchi yote; naye akanyosha mkono, akamtwaa, akamwingiza mle safinani. Akangoja na siku saba tena; kisha akamtoa yule njiwa katika safina mara ya pili, njiwa akamjia jioni, na tazama, alikuwa na jani bichi la mzeituni kinywani mwake, ambalo amelitunda, basi Nuhu akajua ya kwamba maji yamepunguka juu ya nchi. Akangoja na siku saba tena, akamtoa yule njiwa; naye asimrudie tena kamwe.

Mungu aliweka uwezo wa ajabu katika mti huu, na miongoni mwa miti inayofanya kazi ya kuleta heshima kwa Mungu na wanadamu Mzeituni ni mojawapo ni mti  wa kwanza katika miti hiyo  maarufu ya kibiblia angalia Waamuzi 9:8-12 “Siku moja miti ilitoka ili kuutia mmoja mafuta uwe mfalme juu yao; ikauambia mti mzeituni, Tawala wewe juu yetu. Lakini huo mzeituni ukaiambia, Je! Niache mafuta yangu, ambayo kwangu mimi watu wamheshimu Mungu na wanadamu, ili niende nikayonge-yonge juu ya miti? Kisha miti ikauambia mtini, Njoo wewe, utawale juu yetu. Lakini huo mtini ukaiambia, Je! Niuache utamu wangu, na matunda yangu mazuri, niende nikayonge-yonge juu ya miti? Kisha miti ikauambia mzabibu, Njoo wewe, utawale juu yetu.

Sifa za mti wa Mzeituni!

Moja ya sifa ya mti wa Mzeituni ni kuwa ni mti wenye uwezo mkubwa sana wa kustahimili ukame, lakini ni mti usioweza kufa, ni mti wenye uwezo wa kufufuka, mizizi yake ina uwezo mkubwa sana wa kwenda chini na kujiunganisha na maji, kwa sababu hiyo sio rahisi kuuua mzeituni, ukitaka kuuua lazima uchomoe mizizi yake na kuitenganisha na maji huko ardhini, hapo ndipo utaweza kuua, unaweza kuifyekelea mbali lakini baada ya muda fulani unachipua tena!

Mti huu ulitumika nyakati za Agano la kale kusimika watu waliokusudiwa kuwa watumishi wa Mungu katika Nyanja mbalimbali, kama Wafalme, Makuhani na manabii, ili mtu aweze kumtumikia Mungu katika nafasi hizo alipakwa mafuta ya mzeituni kwa maelekezo ya Mungu na maisha ya mtu huyo yalibadilika sana, Makanisa makubwa ya zamani kama Anglican na Kanisa Katoliki huyatumia mafuta ya mzeituni katika ibada za kipaimara na wakati wa kusimika viongozi wa kanisa wakiwemo makuhani wa madhehebu hayo, hii ni kwa sababu wanakumbuka huduma za kikuhani za kupoaka mafuta zilizokuwa zikifanywa na makuhani au manabii nyakati za agano la kale mifano ifuatayo itakusaidia kuelewa uhusiano wa kiroho ulioko kati ya mwanadamu na upako wa mafuta ya mzeituni unaokaribisha nguvu za Mungu Roho Mtakatifu! Ona  

1Samuel 10:1-7 “Ndipo Samweli akatwaa kichupa cha mafuta, akayamimina kichwani pake, akambusu, akasema, Je! Bwana hakukutia mafuta [uwe mkuu juu ya watu wake Israeli? Nawe utamiliki watu wa Bwana, na kuwaokoa na mikono ya adui zao; kisha hii itakuwa ishara kwako ya kuwa Bwana amekutia mafuta] uwe mkuu juu ya urithi wake.Utakapoondoka kwangu leo, utakutana na wanaume wawili karibu na kaburi la Raheli, katika mpaka wa Benyamini huko Selsa; nao watakuambia, Punda hao uliokwenda kuwatafuta wameonekana; na tazama, baba yako ameacha kufikiri habari za punda, anafikiri habari zenu, akisema, Nifanye nini kwa ajili ya mwanangu? Kisha utakwenda mbele kutoka hapo, na kufika kwa mwaloni wa Tabori, na hapo watu watatu watakutana nawe, wanaokwea kumwendea Mungu huko Betheli, mmoja anachukua wana-mbuzi watatu, na mwingine anachukua mikate mitatu, na mwingine anachukua kiriba cha divai; nao watakusalimu na kukupa mikate miwili; nawe utaipokea mikononi mwao. Baada ya hayo utafika Gibea ya Mungu, hapo palipo na ngome ya Wafilisti; kisha itakuwa, utakapofika mjini, utakutana na kundi la manabii wakishuka kutoka mahali pa juu, wenye kinanda, na tari, na kinubi, na filimbi mbele yao, nao watakuwa wakitabiri; na roho ya Bwana itakujilia kwa nguvu, nawe utatabiri pamoja nao, nawe UTAGEUZWA KUWA MTU MWINGINE. Basi, hapo ishara hizi zitakapokutukia, fanya kama uonavyo vema; kwa kuwa Mungu yu pamoja nawe.

1Samuel 16:1-13Bwana akamwambia Samweli, Hata lini utamlilia Sauli, ikiwa mimi nimemkataa asiwamiliki Israeli? Ijaze pembe yako mafuta, uende, nami nitakupeleka kwa Yese, Mbethlehemi; maana nimejipatia mfalme katika wanawe. Samweli akasema, Nawezaje kwenda? Sauli akipata habari, ataniua. Basi Bwana akasema, Chukua ndama pamoja nawe, ukaseme, Nimekuja ili kumtolea Bwana dhabihu. Ukamwite Yese aje kwenye dhabihu, nami nitakuonyesha utakayotenda; nawe utamtia mafuta yule nitakayemtaja kwako. Samweli akafanya hayo aliyosema Bwana, akaenda Bethlehemu. Wakaja wazee wa mji kumlaki, wakitetemeka, nao wakasema, Je! Umekuja kwa amani? Naye akasema, Naam, kwa amani; nimekuja kumtolea Bwana dhabihu; jitakaseni; njoni pamoja nami kwenye dhabihu. Akawatakasa Yese na wanawe, akawaita kwenye dhabihu.  Ikawa walipokuja, alimtazama Eliabu, akasema, Yakini masihi wa BWANA yupo hapa mbele zake.Lakini Bwana akamwambia Samweli, Usimtazame uso wake, wala urefu wa kimo chake; kwa maana mimi nimemkataa. Bwana haangalii kama binadamu aangaliavyo; maana wanadamu huitazama sura ya nje, bali Bwana huutazama moyo. Ndipo Yese akamwita Abinadabu, akampitisha mbele ya Samweli. Naye akasema, Bwana hakumchagua huyu. Ndipo Yese akampitisha Shama. Naye akasema, wala Bwana hakumchagua huyu. Yese akawapitisha wanawe saba mbele ya Samweli. Samweli akamwambia Yese, Bwana hakuwachagua hawa. Kisha Samweli akamwambia Yese, Watoto wako wote wapo hapa? Naye akasema, Amesalia mdogo wao, na tazama, anawachunga kondoo. Basi Samweli akamwambia Yese, Tuma watu, wamlete; kwa sababu hatutaketi hata atakapokuja huku. Basi akatuma mtu, naye akamleta kwao. Naye alikuwa mwekundu, mwenye macho mazuri, na umbo lake lilikuwa la kupendeza. Bwana akasema, Ondoka, umtie mafuta; maana huyu ndiye. Ndipo Samweli akaitwaa pembe yenye mafuta, akamtia mafuta kati ya ndugu zake; na ROHO YA BWANA IKAMJILIA DAUDI KWA NGUVU tangu siku ile. Basi Samweli akaondoka, akaenda zake Rama.”           

Katika Agano jipya ishara ya kupakwa mafuta inaweza kuwa mafuta halisi ya mzeituni au kuwekewa mikono na mtumishi wa Mungu aliyepakwa mafuta aliyewekwa wakfu, sio lazima yawe mafuta kama yale yaliyokaa katika pembe lakini Mchungaji aliyepakwa mafuta anaweza kukuwekea mikono na kutamka kusudi la kukuwekea mikono na ikawa sawa kabisa na kupakwa mafuta, lakini hata akikupaka mafuta halisi ya zeituni, bado uweza utakuwa uleule wa kuwekea mikono au kupakwa mafuta, Ndio maana Yesu hakuwekewa mikono lakini alipakwa mafuta na Mungu mwenyewe mara baada ya kubatizwa na Yohana Mbatizaji, mtu anapowekwa wakfu kwa kupakwa mafuta anakuwa mtu mwenye uweza wa kiungu ndani yake na kumfanya kuwa mtu wa tofauti! Ona tangazao la Yesu la kuwa mpakwa mafuta;-

Luka 4:18-19 “Roho wa Bwana yu juu yangu, Kwa maana amenitia mafuta kuwahubiri maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, Na vipofu kupata kuona tena, Kuwaacha huru waliosetwa, Na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa.”

Mungu anaporuhusu katika kanuni zake uwekewe mikono au upakwe mafuta unakuwa na uweza wa kiwokovu ndani yako na mungu anakupoa neema inayokuwezesha kuwatetea wengina na kutimiza majukumu yako ambayo Mungu anakuwa ameyakusudia

Mzeituni umeao katika nyumba ya Mungu!

Zaburi 52:1-9

Kwa nini kujisifia uovu, Ewe jabari? Wema wa Mungu upo sikuzote.

Ulimi wako watunga madhara, Kama wembe mkali, Ewe mwenye hila

Umependa mabaya kuliko mema, Na uongo kuliko kusema kweli.

Umependa maneno yote ya kupoteza watu, Ewe ulimi wenye hila.  

Lakini Mungu atakuharibu hata milele; Atakuondolea mbali; Atakunyakua hemani mwako; Atakung'oa katika nchi ya walio hai.

Nao wenye haki wataona; Wataingiwa na hofu na kumcheka;

Kumbe! Huyu ndiye mtu yule, Asiyemfanya Mungu kuwa nguvu zake.

 Aliutumainia wingi wa mali zake, Na kujifanya hodari kwa madhara yake.

Bali mimi ni kama mzeituni Umeao katika nyumba ya Mungu.

Nazitumainia fadhili za Mungu milele na milele.

Nitakushukuru milele kwa maana umetenda; Nitalingojea jina lako kwa kuwa ni jema; Mbele ya wacha Mungu wako.

 

Katika msitari wetu wa Msingi Mwandishi anaonyesha ya kuwa yuko mtu wa hila, mtu mwenye kiburi mwenye uwezo wa kupoteza watu, muovu  inaonekana mtu huyu ana madhara ni hodari na mwenye nguvu, anawaandama wanadamu anapigana nao ana hila bila shaka ni wazi kabisa mtu huyu ni Ibilisi anasimama kushindana na makusudi ya Mungu ndani ya kila mmoja wetu anataka kutuahribia anataka kutuumiza anataka kuweka jeraha katika mioyo yetu, anataka tushindwe, anazuia mafanikio yetu, anapoingana na makusudi ya mungu ndani yetu na ndani ya mwandishi wa zaburi hii ambaye ni Daudi.  Mwandishi anamkumbusha  mtu huyo (Shetani) kuwa Yuko Mungu mwenye nguvu kushinda yeye, anauwezo wa Kumuharibu milele, anauwezo wa kumfutilia mbali, na ana uwezo wa kumng’oa na Daudi anatabiri kuwa wenye haki watamcheka!  Watashangaa kwanini mtu huyu wa kiburi hakumfanya Mungu kuwa nguvu yake? Kwa nini alitumainia mali zake na kujifanya hodari kumbe hana nguvu! Daudi anaeleza kuwa mtu anayemtegemea Mungu anayeutumainia  wema wa Mungu anayetambua kuwa Mungu ni mwema siku zote yaani hata wakati wa nyakati ngumu au ndani ya jambo gumu bado Mungu ni mwema tu! Hao ni sawa na Mzeituni uliopandwa katika nyumba ya Mungu,  yaani wale wanaomtegemea Mungu na kuzitumainia nguvu zake  watamea katika nyumba ya Mungu yaani katika uwepo wa Mungu watastawi watahuishwa, kwa sababu wanategemea fadhili za Mungu wanalitizamia jina lile jema yaani jina la Yesu, hawa hawatatikiswa wala hawataogopa, wakikatwa wanachipua tena! huwezi kuwazibia wameunganishwa mizizi yao na chemichemi ya uzima na chanzo cha uhai ambaye ni Mungu!,  watu walioungwa na chemichemu ya uzima wanautazamia wema wa Mungu siku zote Zaburi 52:1, hao hawawezi kutikiswa hawaogopi wana jina wanalolitumainia wanakaa katika uwepo wa Mungu wanazitumainia fadhili za Mungu milele na milele hawa ni watu wasiowezekana

Ndugu  tunalo tumaini lisiloweza kutikiswa sisi ni kama Mzeituni unaomea katika nyumba ya Mungu. Kila anayemtegemea Mungu na anayezitegemea fadhili zake hapaswi kuogopa, hatupaswi kufadhaika maana sisi kama ilivvyo kwa daudi ni mzeituni unaomea katika Nyumba ya Mungu, Mizeituni huwa haifi, mizeituni huwa inadumu milele, mizizi yake imeungwa na chemic hemi za chini sana za maji, ili tutoweke ni mpaka wachomoe mizizi inayotuunganisha na fadhili za Mungu, Usiogope!

 

Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa Wajenzi mwenye Hekima

0718990796

Jumapili, 8 Novemba 2020

Hamjui yatakayokuwako kesho!

Mstari wa Msingi: Yakobo 4:13-15 “Haya basi, ninyi msemao, Leo au kesho tutaingia katika mji fulani na kukaa humo mwaka mzima, na kufanya biashara na kupata faida; walakini hamjui yatakayokuwako kesho. Uzima wenu ni nini? Maana ninyi ni mvuke uonekanao kwa kitambo, kisha hutoweka. Badala ya kusema, Bwana akipenda, tutakuwa hai na kufanya hivi au hivi.”


Utangulizi:

Mojawapo ya swali muhimu sana ambalo kila mwanadamu mwenye akili timamu huwa anajiuliza ni kuhusu kesho  “future”  kwamba itakuwaje kesho, nini kinafuata baada ya haya? Nini kinakuja, nini kitatokea wiki ijayo, mwezi ujao, mwaka ujao na wakati mwingine tunaona giza, na kujiuliza je tutakuwa na furaha au tutakuwa na dhuruba? Ni nani anaishikilia kesho yetu? Je napaswa kuwa na matumaini au kuogopa?


Itakuwaje mtihani unaokuja mbele yetu? Tutapata habari gani, itakuwaje matokeo ya uchaguzi wa, nani atashinda na itakuwaje akishinda fulani? Itakuwaje kazini, itakuwaje ndoa yangu, itakuwaje marafiki zangu, itakuwaje familia yangu? Itakuwaje afya yangu? Itakuwaje nikistaafu? Itakuwaje nikiachwa?


Watu wengi sana wanaogopa sana kuhusu maisha yajayo na kwa sababu hii ingawa wanajua umuhimu wa maswali hayo lakini kutokana na hofu au woga kisaikolojia watu wengi huwa wanapotezea swali hili Muhimu ili kupata unafuu na kutuliza maumivu yake, Mungu anajua kwamba swala kuhusu kesho ni swali tata sana kwa wanadamu na hataki tuogope wala kujisumbua hususani tunapokuwa na uhusiano mwema na yeye  Yesu Kristo anawatoa hofu kabisa waaumini wake akitaka jambo hili lisiwasumbue ona


Mathayo 6:31-34 “Msisumbuke, basi, mkisema, Tule nini? Au Tunywe nini? Au Tuvae nini? Kwa maana hayo yote Mataifa huyatafuta; kwa sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hayo yote. Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa. Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake.”


Kwa kuwa Mungu anajua kuwa swala la kesho itakuwaje ni swala zito kwa wanadamu Maandiko yanawafundisha watu wa Mungu namna inavyowapasa kuenenda, watu wenye kiburi na watu wasiomjua Mungu huwa wana uhakika sana na maisha ya kesho kunakosababishwa na majivuno na kiburi.


Neno la Mungu linaonya kujisifu kuhusu kesho!


Watu wasiomjua Mungu huwa na tabia ya kujisifu na kujivuna kuhusu Kesho! Jambo ambalo neno la Mungu limeonya sana kwa njia nyingi na kwa mifano mingi wako watu ambao hujivunia kesho kana kwamba wanajua yatakayotukia kesho Biblia inaonya vikali sana kuhusu maisha yajayo au kuhusu kesho ona Mithali 27:1 “Usijisifu kwa ajili ya kesho; Kwa maana hujui yatakayozaliwa na siku moja.Wako watu hujivunia kuhusu kesho kana kwamba wana uhakika nayo na wanamuweka pembeni Mungu katika mipango yao na makusudi yake, Neema yake na wema wake  wako watu ambao walisahau kuwa kila kitu na kila jambo liko kwenye mikono ya Mungu, Mungu ana namna yake ya kuwanyoosha watu wenye kiburi


Ø Daniel 4:28-33 “Hayo yote yakampata mfalme Nebukadreza. Baada ya miezi kumi na miwili, alikuwa akitembea ndani ya jumba la kifalme katika Babeli. Mfalme akanena, akasema, Mji huu sio Babeli mkubwa nilioujenga mimi, uwe kao langu la kifalme, kwa uwezo wa nguvu zangu, ili uwe utukufu wa enzi yangu? Hata neno lile lilipokuwa katika kinywa cha mfalme, sauti ilikuja kutoka mbinguni, ikisema, Ee mfalme Nebukadreza, maneno haya unaambiwa wewe; Ufalme huu umeondoka kwako.Nawe utafukuzwa mbali na wanadamu, na makao yako yatakuwa pamoja na wanyama wa kondeni; utalishwa majani kama ng'ombe, na nyakati saba zitapita juu yako, hata utakapojua ya kuwa Aliye juu ndiye anayemiliki katika ufalme wa wanadamu, naye humpa amtakaye, awaye yote. Saa iyo hiyo jambo hilo likatimizwa, likampata Nebukadreza; alifukuzwa mbali na wanadamu, akala majani kama ng'ombe, na mwili wake ulilowa maji kwa umande wa mbinguni, hata nywele zake zikakua, zikawa kama manyoya ya tai, na kucha zake kama kucha za ndege.“

 

Ø Matendo 12:20-23 “Naye Herode alikuwa amewakasirikia sana watu wa Tiro na Sidoni; wakamwendea kwa nia moja, na wakiisha kufanya urafiki na Blasto, mwenye kukitunza chumba cha mfalme cha kulalia, wakataka amani; kwa maana nchi yao ilipata riziki kwa nchi ya mfalme. Basi siku moja iliyoazimiwa, Herode akajivika mavazi ya kifalme, akaketi katika kiti cha enzi, akatoa hotuba mbele yao. Watu wakapiga kelele, wakisema, Ni sauti ya Mungu, si sauti ya mwanadamu. Mara malaika wa Bwana akampiga, kwa sababu hakumpa Mungu utukufu; akaliwa na chango, akatokwa na roho.


Ø Luka 12: 15-21 “Akawaambia, Angalieni, jilindeni na choyo, maana uzima wa mtu haumo katika wingi wa vitu vyake alivyo navyo. Akawaambia mithali, akisema, Shamba la mtu mmoja tajiri lilikuwa limezaa sana; akaanza kuwaza moyoni mwake, akisema, Nifanyeje? Maana sina pa kuyaweka akiba mavuno yangu. Akasema, Nitafanya hivi; nitazivunja ghala zangu, nijenge nyingine kubwa zaidi, na humo nitaweka nafaka yangu yote na vitu vyangu. Kisha, nitajiambia, Ee nafsi yangu, una vitu vyema vingi ulivyojiwekea akiba kwa miaka mingi; pumzika basi, ule, unywe, ufurahi. Lakini Mungu akamwambia, Mpumbavu wewe, usiku huu wa leo wanataka roho yako! Na vitu ulivyojiwekea tayari vitakuwa vya nani?Ndivyo alivyo mtu ajiwekeaye nafsi yake akiba, asijitajirishe kwa Mungu.”  

 

Ø Mjezi wa Meli ya TITANIC  ambayo ilikuwa meli ya kifahari sana iliyokuwa na viwanja vya mpira, kumbi za starehe na mabwawa ya kuogelea alipoulizwa kuhusu uimara wa meli hiyo alijigamba na kusema hata Mungu hawezi kuizamisha, meli hii ilizama siku ya nne tu tangu ilipoanza safari kutoka Uingereza baada ya kugonga mwamba wa barafu katika bahari ta Atlantic  mnamo asubuhi ya tarehe 15/04.1912, Meli hii ilikuwa na abiria wapatao 2240 na kati yao zaidi ya 1500 walipoteza maisha, hatujui kesho yetu, kila aina ya kile tunachokifikia duniani hatuna budi kukumbuka kuwa ni kwa neema ya Mungu tu!


Mifano hii yote katika Biblia imeandikwa ili kutuonya sisi wanadamu ya kwamba hatuna kesho, kujilimbikizia mali na kuwa na choyo hakuongezei uzima wetu duniani, kila aina ya mafanikio tuliyionayo hayatokani na uwezo wetu ni neema ya Mungu  na wema wake ona Paulo mtume ndiye mtume aliyefanya kazi kubwa kuliko mitume wote lakini wakati wote alikumbuka kuwa alifanya chini ya neema ya Mungu na sio uwezo wake ona  1Wakoritho 15:10 “Lakini kwa neema ya Mungu nimekuwa hivi nilivyo; na neema yake iliyo kwangu ilikuwa si bure, bali nalizidi sana kufanya kazi kupita wao wote; wala si mimi, bali ni neema ya Mungu pamoja nami.Tunapaswa kuhakikisha kuwa tunaitegemea neema ya Mungu na kumtukuza yeye katika kila jambo na kumtanguliza yeye, kila mmoja anapaswa kuhakikisha anajilinda na kiburi kwa vile maisha hayako katika mikono yetu! Na Hatujui yatakayokuwako Kesho!


Hamjui yatakayokuwako kesho! 


Hakuna ajuaye kesho, Kesho iko katika mikono ya Mungu, Mungu anajua yote kuhusu kesho, Mungu anajua kila kitakachotokea anajua kitakachotokea kesho, wiki ijayo, mwezi ujao na miaka ijayo kwa hiyo kesho iko katika mikono ya Mungu Isaya 46:9-10 “kumbukeni mambo ya zamani za kale; maana mimi ni Mungu, wala hapana mwingine; mimi ni Mungu, wala hapana aliye kama mimi; nitangazaye mwisho tangu mwanzo, na tangu zamani za kale mambo yasiyotendeka bado; nikisema, Shauri langu litasimama, nami nitatenda mapenzi yangu yote.” Mungu anautangaza mwisho tangu mwanzo, Mungu anakujua na wewe nawe anajua unayoyahitaji anajua utakuwa nani anajua atakayeolewa na wewe anajua utakayemuoa anajua utakuwa na watoto wangapi anajua mwanzo na hata mwisho wa maisha yetu, alitambua mwisho wa Yusufu na kuutangaza kwa njozi kabla,  Mungu alikuwa anajua kuwa mavazi ya Yesu yatapigiwa kura miaka 1000 kabla ya Yesu Daudi alitabiri kitakachompata Yesu ona Zaburi 22:18 “Wanagawanya nguo zangu, Na vazi langu wanalipigia kura.” na Mathayo 27:35 “Walipokwisha kumsulibisha, waligawa mavazi yake, wakipiga kura; [ili litimie neno lililonenwa na nabii, Waligawa nguo zangu kati yao, na juu ya vazi langu walipiga kura.]”  Mungu anaweza kutuambia hata leo akitaka kuhusu kesho yetu na hivyo kama tunamtegemea na kumuamini tunapaswa kuwa na unyenyekevu na kumtegemea yeye na kumtanguliza yeye na kumuomba yeye, Kesho yetu iko mikononi mwa Mungu hatupaswi kusahau hilo yeye amakuwepo tangu mwanzo na yuko hata milele, Yesu ni yeye yule jana leo na milele anajua kila kitu kitakachotokea  na anampango mwema kwa aajili ya kila mmoja anayemtanguliza na kumtegemea yeye Warumi 8:28-30 “Nasi twajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao katika kuwapatia mema, yaani, wale walioitwa kwa kusudi lake. Maana wale aliowajua tangu asili, aliwachagua tangu asili wafananishwe na mfano wa Mwana wake, ili yeye awe mzaliwa wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi. Na wale aliowachagua tangu asili, hao akawaita; na wale aliowaita, hao akawahesabia haki; na wale aliowahesabia haki, hao akawatukuza.” 


Mkumbuke Mungu katika mipango yako yote. 


Ni muhimu kufahamu kuwa maandiko yanatufundisha kwamba tunapaswa kumtanguliza Mungu mbele katika kila jambo, katiia mipango yetu maono yetu ndote zetu na kazi zetu tunapaswa kumuomba Mungu na kumtanguliza yeye na hatupaswi kuzitegemea na kujivunia akili zetu wenyewe, Watu wenye kiburi hawa na choyo wadhalimu hujisifia tama zao na hawataki kumkumbuka wala kumtanguliza Mungu kwa namna yoyote ile Zaburi 10:2-3 “Kwa kiburi chake asiye haki mnyonge anafuatiwa kwa ukali; Na wanaswe kwa hila zizo hizo walizoziwaza. Maana mdhalimu hujisifia tamaa ya nafsi yake, Na mwenye choyo humkana Bwana na kumdharau.” 


Na. Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima !

0718990796