Alhamisi, 29 Aprili 2021

Atakaye kupenda Maisha

1Petro 3:10-12Kwa maana, Atakaye kupenda maisha, Na kuona siku njema, Auzuie ulimi wake usinene mabaya, Na midomo yake isiseme hila. Na aache mabaya, atende mema; Atafute amani, aifuate sana. Kwa kuwa macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, Na masikio yake husikiliza maombi yao; Bali uso wa Bwana ni juu ya watenda mabaya.”



Utangulizi:

Ni muhimu kufahamu; kwamba ni vigumu sana kuyapenda maisha hususani nyakati ambazo tunapitia maswala magumu, watu wengi wanapopitia nyakati ngumu sana katika maisha yao huwa wanatamani kufa na au wanakata tamaa kabisa hata kufikia hatua ya kufikiri kuwa Mungu hawajali na kujishughulisha tena na maisha yao, Je umewahi kupitia maswala magumu sana katika maisha hata kufikia ngazi ya kukata tamaa na kutamani kufa  au kufikiria kuwa Mungu hakujali? watu wengi wamewahi kufikiri hivyo, hata mimi pia katiika vipindi Fulani mbalimbali,  maisha sio kitu rahisi lakini maisha ni ya muhimu sana, maisha yana changamoto nyingi sana lakini bado maisha yanabaki kuwa ni ya muhimu mno!.  Mtume Petro anawaandikia Wakrito ambao walikuwa wanapitia nyakati za Mateso na nyakati ngumu sana na anatoa ushauri unaokwenda sambamba na Zaburi  iliyoandikwa na Mfalme Daudi kuhusu Maisha:-


Zaburi 34:12-16 “Ni nani mtu yule apendezwaye na uzima, Apendaye siku nyingi apate kuona mema? Uuzuie ulimi wako na mabaya, Na midomo yako na kusema hila. Uache mabaya ukatende mema, Utafute amani ukaifuatie. Macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, Na masikio yake hukielekea kilio chao. Uso wa Bwana ni juu ya watenda mabaya, Aliondoe kumbukumbu lao duniani.”


Petro anaunga mkono kile kilichosemwa na Daudi au anahubiri kitabu cha zaburi ya 34:12-16 akionyesha ni namna gani watu wa Mungu wanapopita katika magumu wanapaswa kuyatazama maisha, Petro pamoja na Daud mwandishi wa Zaburi wanatutia moyo kuwa na imani kwa ahadi za Mungu wakati wote hata wakati tunapopitia changamoto za aina mbalimbali katika maisha  na kuendelea kuyapenda maisha ili Mungu atukuzwe wakati wa Magumu yetu, tunaonyesha ukomavu na imani badala ya kuchukizwa nayo kama ilivyokuwa kwa Suleimani mwandishi wa kitabu cha Muhubiri ambaye aliyaiona maisha kuwa jambo lisilo na maana na hasa maisha ya mtu wa kawaida asiye na imani huyaona maisha kama kujilisha upepo, Maisha yana maana kubwa sana hata pamoja na magumu unayoyapitia! Hivyo hatuna budi kuyapenda:-


Petro anaona kuwa ziko kanuni ambazo angaweza kutushauri wote tunaoishi bila kujali kuwa tunaishi katika mazingira mazuri au mabaya kiasi gani lakini Maisha ni zawadi ni neema ambayo Mungu ametupa hivyo wakati wote tuwapo duniani, tunapaswa kumshukuru Mungu kwa imani sasa katika kanuni hizo Petro anatuasa kwanza


1.       Kuuzuia ulimi usinene mabaya !

 

Ni muhimu kufahamu kuwa ulimi ndio kiungo chepesi zaidi kutumika katika maisha ya mwanadamu,  mtu mwenye ukomavu na busara au mtu mkamilifu ni yule mwenye uwezo wa kujua namna na jinsi ya kuutunza Ulimi, na kuutumia Biblia inaonyesha ya kuwa kiungo hiki kinabeba mamlaka kubwa sana katika maisha yetu ikiwa ni pamoja na uzima na mauti ona Mithali 18:20-21 “Tumbo la mtu litajazwa matunda ya kinywa chake; Atashiba mazao ya midomo yake. Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi; Na wao waupendao watakula matunda yake.” Kwa haraka sana ni ulimi ndio unaoweza kutubadilishia hali ya ulimwengu wetu kuwa wa furaha au wa amani, kuyatawala mazingira ama kutawaliwa kutengeneza hali ya hewa au kuiharibu, kunung’unika au kushangilia mwenendo wetu mbele za Mungu na wanadamu unaweza kuathiriwa au kuwekwa sawa kwa ulimi! Maneno ni silaha yenye nguvu sana inayoweza kuinua watu au kuwaharibu watu! Patro ananyesha wazi kuwa tunaweza sana kujizuia maisha yetu na dhuruba za ulimwengu kama endapo tu tutaweza kuzuia ndimi zetu ona Mithali 21:23 “Mtu azuiaye kinywa chake na ulimi wake, Atajilinda nafsi yake na taabu.” Uwezo wa kuchagua nini cha kuzungumza na nini cha kutokuzungumza uko katika uchaguzi wetu, lakini wakati wote ni muhimu sana kukumbuka namna na jinsi tunavyoutumia ulimi, Ni vigumu sana kumsoma na kumjua kwa undani mtu asiyezungumza, mara tu unapozungumza ndipo watu wanapoweza kukujua wewe ni nani nani mtu wa namna gani, Maneno yetu yanafichua kile kilichoko ndani yetu  Moja ya hukumu watakayohukumiwa wanadamu mbele za Mungu ni pamoja na kile wanachokizungumza Mathayo 12:33-37 “Ufanyeni mti kuwa mzuri na matunda yake kuwa mazuri; au ufanyeni mti kuwa mbaya na matunda yake mabaya, kwa maana kwa matunda yake mti hutambulikana. Enyi wazao wa nyoka, mwawezaje kunena mema, mkiwa wabaya? Maana, kinywa cha mtu huyanena yaujazayo moyo wake. Mtu mwema katika akiba njema hutoa mema; na mtu mbaya katika akiba mbaya hutoa mabaya. Basi, nawaambia, Kila neno lisilo maana, watakalolinena wanadamu, watatoa hesabu ya neno hilo siku ya hukumu. Kwa kuwa kwa maneno yako utahesabiwa haki, na kwa maneno yako utahukumiwa.” Ni kutokana na hekina na ujuzi wake Petro kuhusu Maisha yeye anaona ni vema kutuasa kutikunena na hasa kunena mabaya, kila mtu mwenye hekima anapaswa kujua yampasayo kunena na ikiwezekana azungumze maneno ya kujenga sio mabaya au yenye hila ndani yake, Dhambi nyingi tunazozifanya na namna tunavyowazunguzia watu kwa wema au kwa ubaya kwa kujenga au kwa kuibomoa tunatumia ulimi, karibu kila iana ya dhambi ni lazima itauhusisha ulimi, kwa msingi huo Daudi na Patro wanatutaka sisi kuutumia ulimi kuleta uponyaji duniani na sio kuharibu Mithali 12:17-19 “ Atamkaye maneno ya kweli hufunua haki; Bali shahidi wa uongo hutamka hila. Kuna anenaye bila kufikiri, kama kuchoma kwa upanga; Bali ulimi wa mwenye haki ni afya. Mdomo wa kweli utathibitishwa milele; Bali ulimi wa uongo ni wa kitambo tu.” Kama hakuna sababu ya kuzungumza ni vema kutokuzungumza kuliko kuzungumza maneno ya kubomoa, kuna thawabu kubwa sana Mbinguni kwa watu wa Mungu ambao watakuwa na ujuzi wa namna na jinsi ya kuutumia ulimi, na ni vema vile vile kwa pamoja tukiwa tunatafakari na kujadili mambo yaliyo mazuri, yaliyo ya staha, yenye kujenga , yenye wema, yenye kupendeza, yenye sifa nzuri hayo ndio maswala ya kuyajadili na ndivyo neno la Mungu linavyotutaka Wafilipi 4:8 “Hatimaye, ndugu zangu, mambo yo yote yaliyo ya kweli, yo yote yaliyo ya staha, yo yote yaliyo ya haki, yo yote yaliyo safi, yo yote yenye kupendeza, yo yote yenye sifa njema; ukiwapo wema wo wote, ikiwapo sifa nzuri yo yote, yatafakarini hayo.”        Tukitafakari mambo mema tutazungumza mambo mema na tutaufanya ulimwengu uwe mahali pema pa kuishi na vilevile katika maisha yajayo baada ya kufa tutakuwa na wakati mwema na Mungu, kwa msingi huo basi kanuni ya kwanza ya kutufanya tuishi maisha mazuri  na kuufurahia uumbaji wa Mungu na kuona siku njema ni kuzungumza mambo mazuri yaliyo mema kwa msingi huo basin i vema mno tukaangalia kile Daudi alikisema na kile ambacho Petro alikihubiri kwamba kama tunapenda maisha na kutaka kuwa na siku njema katika kipindi hiki kifupi sana ambacho Mungu ametupa kuwepo duniani basi ni vema tunayapokea maisha kwa shukurani, kwa tabia njema tukiwa tumejaa neema na kuhakikisha kuwa tunawajenga wengine kwa utukufu wa Mungu baba! Matumizi ya ulimi yanatujengea kanuni kubwa na njema na nzuri ya kuyafurahia maisha kwa hiyo kuna umuhimu wa kujilinda na kujihami tusinene mabaya, tusihukumu kwa haraka na kuhakikisha kuwa tunatenda mema, Neno la Mungu linatutaka kwamba hata kama tunaishi katika nyakati ambazo kila mtu anazungumza mabaya ni wakristo pekee na watu weme na wenye hekima wanaoweza kuufanya ulimwengu kuwa mahali pema kwa kuzungumza maneno mema na mazuri ya neema na tukatae kabisa kutumika kama chombo cha shetani kwa kuuujaza ulimwengu maneno mabaya hata kama tunapitia mambo magumu Wakolosai 4:5-6 “Enendeni kwa hekima mbele yao walio nje, mkiukomboa wakati. Maneno yenu yawe na neema siku zote, yakikolea munyu, mpate kujua jinsi iwapasavyo kumjibu kila mtu.” Tunapozungumza haya unaweza kujiuliza kwamba sasa nitafanyaje maana huenda mimi niko miongoni mwa watu wenye midomo michafu sana yaani katika watu ambao wana majibu mabaya mimi nimo, katika watu ambao wanajua kunya kwa mdomo, wanajua kutema vyondo na mimi nimo na sasa nimeyaharibu maisha yangu kwa kuzungumza yasiyopaswa nawezaje kuwa mwema tena? Usiogope kama uliutumia ulimi wako vibaya kabla hatujafika katika hatua nyingine yako mambo muhuimu ya kufanya :-

 

a.       Muombe Mungu akutakase Moyo wako, akili zako na maneno yako:

 

Ni vigumu kuishi maisha matakatifu na kumpendeza Mungu kama maneno yetu ni mabaya meneno yetu ni kipimo ya kile kilichoko moyoni mwetu, akilini kwetu na ndio huwa kinadhihirishwa kwa kusema kwetu ona Luka 6:45 “Mtu mwema katika hazina njema ya moyo wake hutoa yaliyo mema, na mtu mwovu katika hazina mbovu ya moyo wake hutoa yaliyo maovu; kwa kuwa mtu, kinywa chake hunena yale yaujazayo moyo wake.”  Yesu anaonyesha wazi kuwa kile tunachokinena ni matokeo ya kile kilichoko moyoni, Kwa msingi huo basi hatuna budi kumuomba Mungu atusafishe na kututakasa, mioyo yetu, akili zetu na maneno yetu, Mungu akitusamehe na kutusafisha maneno yetu yatakuwa na nguvu ya kuumba mambo mema kwaajili ya Mungu Ona Isaya 6:1-7 “Katika mwaka ule aliokufa mfalme Uzia nalimwona Bwana ameketi katika kiti cha enzi, kilicho juu sana na kuinuliwa sana, na pindo za vazi lake zikalijaza hekalu. Juu yake walisimama maserafi; kila mmoja alikuwa na mabawa sita; kwa mawili alifunika uso wake, na kwa mawili alifunika miguu yake, na kwa mawili aliruka. Wakaitana, kila mmoja na mwenzake, wakisema, Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu, ni Bwana wa majeshi; dunia yote imejaa utukufu wake. Na misingi ya vizingiti ikatikisika kwa sababu ya sauti yake aliyelia, nayo nyumba ikajaa moshi. Ndipo niliposema, Ole wangu! Kwa maana nimepotea; kwa sababu mimi ni mtu mwenye midomo michafu, nami ninakaa kati ya watu wenye midomo michafu; na macho yangu yamemwona Mfalme, Bwana wa majeshi. Kisha mmoja wa maserafi wale akaruka akanikaribia; naye alikuwa na kaa la moto mkononi mwake, ambalo alikuwa amelitwaa kwa makoleo toka juu ya madhabahu; akanigusa kinywa changu kwa kaa hilo, akaniambia, Tazama, hili limekugusa midomo yako, na uovu wako umeondolewa, na dhambi yako imefunikwa.” Isaya ni nabii aliyetumiwa sana na Mungu, Lakini kabla ya kutumwa alijitakasa alitubia uovu wake na Mungu akamtakasa kinywa chake na ndipo akamtumia, hatuna budi kuhakikisha kuwa tunaomba na kujitakasa ili kwamba Mungu aweze kuyalinda mawazo yetu na kutulinda na uharibifu. Kumbuka kwamba tumeumbwa kwa sura na mfano wa Mungu, Mungu aliuumba ulimwengu huu kwa neno tu na mara kadhaaa laifanya miujiza kwa kutamkqa neno ona Mwanzo 18:10-14 “Akamwambia, Hakika nitakurudia wakati huu huu mwakani, na tazama, Sara mkeo atapata mwana wa kiume. Sara akasikia mlangoni pa hema iliyokuwapo nyuma yake. Basi Ibrahimu na Sara walikuwa wazee, na umri wao mkubwa, na Sara alikuwa amekoma katika desturi ya wanawake. Kwa hiyo Sara akacheka moyoni mwake, akisema, Niwapo mkongwe, nitapata furaha, na bwana wangu mzee? BWANA akamwambia Ibrahimu, Mbona Sara amecheka akisema, Mimi kweli nitazaa mwana, nami ni mzee? Kuna neno gani lililo gumu la kumshinda BWANA? Kwa muhula wake nitakurudia, wakati huu huu mwakani, na Sara atapata mwana wa kiume.” Unaweza kuona Mungu hapa anatamka neno na lile neno linakuwa kama vile alivyotamka, sisi nasi tumeumbwa kwa mfano wake Mungu akikitakasa kinywa chetu na kujifunza nidhamu ya kutunza kinywa tutakuwa na mamlaka katika matamshi yetu nan a kusababisha uumbaji, mimi ni Mwalimu pia wa chuo cha Biblia chuo cha Biblia kibiblia huitwa chuo cha manabii, hivyo nafundisha manabii pia ni Mwalimu wa manabii ili nabii aweze kuwa na mamlaka anapaswa kuwa na kinywa safi ili kinywqa cheke kiwe na mamlaka na ndio maana kabala Mungu hajamtumia nabii isaya alimtakasa kinywa cheke kisha akaweka neno lake hivyo isaya akatabiri mambo mengi kuhusu masihi na yakatimia, Manabii wengi walikuwa wakijitunza vinywa vyao na hivyo vinywa vyao vikawa na mamlaka kubwa sana ona, Nabii Elisha alitamka tu kama Mungu alivyomtamkia Sara na kile alichokinena kikatimia  2Wafalme 4:16-17 “Akasema, Panapo wakati huu mwakani, utamkumbatia mwana. Akasema, La! Bwana wangu, wewe mtu wa Mungu, usiniambie mimi mjakazi wako uongo. Yule mwanamke akachukua mimba, akazaa mtoto mume wakati uo huo mwakani, kama Elisha alivyomwambia.”Elisha anatufundisha kuwa tunaweza kutamka kitu kama Mungu nqa kikawa vilevile kwaajili ya hayo tujnaina kuwa kuna umuhimu mkubwa sana wa kuomba kutakaswa ili kwamba vivywa vyetu viweze kuwa na mamlaka ona 1Wafalme 17:1 “Basi Eliya Mtishbi, wa wageni wa Gileadi, akamwambia Ahabu, Kama Bwana, Mungu wa Israeli, aishivyo, ambaye ninasimama mbele zake, hakutakuwa na umande wala mvua miaka hii, ila kwa neno langu.” “2 Wafalme 6:24-30 “Ikawa baada ya hayo, Ben-hadadi mfalme wa Shamu akakusanya majeshi yake yote, akakwea akauhusuru Samaria. Njaa ikawa kuu huko Samaria; na tazama, wakauhusuru, hata kichwa cha punda kikapata kuuzwa kwa vipande themanini vya fedha, na kibaba cha mavi ya njiwa kwa vipande vitano vya fedha. Ikawa mfalme wa Israeli alipokuwa akipita ukutani, mwanamke mmoja akamwita akisema, Unisaidie, bwana wangu, mfalme. Akasema, Bwana asipokusaidia, nikusaidieje mimi? Ya sakafuni, au ya shinikizoni? Mfalme akamwambia, Una nini? Akajibu, Mwanamke huyu aliniambia, Mtoe mtoto wako, tumle leo, na mtoto wangu tutamla kesho. Basi, tukamtokosa mtoto wangu, tukamla; nikamwambia siku ya pili, Mtoe mtoto wako, tumle; naye amemficha mtoto wake.  Ikawa, mfalme alipoyasikia maneno ya huyo mwanamke, aliyararua mavazi yake; (naye alikuwa akipita juu ya ukuta;) na watu wakaona, na tazama, alikuwa amevaa magunia ndani mwilini mwake.Tatizo la Njaa hapa lilikuwa kubwa sana mpaka yakatokea hayo yaliyotokea lakini Elisha alitamka neno la matumaini ambalo ni vigumu kuamini kuwa linaweza kutokea katika mazingira kama yale lakini kwakuwa kinywa chake kilikuwa na mamlaka Mungu aliweza kutekeleza kile alichokisema ona 2 Wafalme 7:1-2 “Elisha akasema, Lisikieni neno la Bwana; Bwana asema hivi, Kesho panapo saa hii, kipimo cha unga mzuri kitauzwa kwa shekeli, na vipimo viwili vya shayiri kwa shekeli, langoni pa Samaria. Basi yule akida, ambaye mfalme alikuwa akitegemea mkono wake, akamjibu yule mtu wa Mungu, akasema, Tazama, kama Bwana angefanya madirisha mbinguni, je! Jambo hili lingewezekana? Akamwambia, Angalia, wewe utaliona kwa macho yako, lakini hutakula.”  Hali kama hii hata sisi tunaoishi zamani za siku hizi zama za agano jipya tunaweza kabisa kutumia ndimi zetu kwa mamlaka makubwa endapo tutakubali Mungu atutakase ndimi zetu na kututuimia Matendo 3:6 “Lakini Petro akasema, Mimi sina fedha, wala dhahabu, lakini nilicho nacho ndicho nikupacho. Kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, simama uende.” Kwa msingi huo tunaona kuwa kuna faida kubwa sana kuwa na nidhamu kwa kutunza ndimi zetu na kutakaswa kwa ndimi zetu ili kwamba vinywa vyetu viweze kutumiwa na Mungu kwa mamlaka iliyokubwa zaidi, hata Pepo huwa wanatii watu wanaojua kutumia vinywa vyao vyema .

 

 

b.      Omba kwamba Mungu ailinde dhamiri yako:

 

Ni muhimu kuyapima maneno yetu kabla ya kuyazungumza, Ni muhimu kwetu kumuomba Mungu azilinde dhamiri zetu ili kwamba wakati wote tukusudie kuzungumza mambo mazuri wakati wote tunapokusudia kuzungumza na kama ni mazingira ambayo hatupaswi kusema lolote itakuwa vema basi tukanyamaza au kumuomba Mungu atulinde vinywa vyetu ona Zaburi 19:14 “Maneno ya kinywa changu, Na mawazo ya moyo wangu, Yapate kibali mbele zako, Ee Bwana, Mwamba wangu, na mwokozi wangu.” Mara kwa mara wanadamu tunapenda, na kulalamika hususani mbele ya rafiki zetu, wanfanyakazi, wanafunzi, wageni na kaedhalika kwa kawaida hakuna mwanadamu anayefurahia kimsingi kusikia malalamiko yetu, malalamiko huinajisi mioyo, kwa msingi huo ni vema sana tukazuia vinywa vyetu lakini kwa kuwa hatuwezi basin a tumuombe Mungu kama mwandishi wa zaburi ili kwamba Mungu atusaidie kila tunalolizungumza lipate kibali mbele za Mungu!, Watu wengi sana wanafikiri kuwa Musa hakwenda kanaani kwa sababu aliupiga mwamba hapana Musa alizunguimza yasiyofaa Zaburi 106:32-33 “Wakamghadhibisha penye maji ya Meriba, Hasara ikampata Musa kwa ajili yao, Kwa sababu waliiasi roho yake, Akasema yasiyofaa kwa midomo yake.” Wana wa Israel kwa sababu ya kunungunika kwao mara kwa mara walimkosesha Musa na kumfanya Musa kutamka mambo yasiyofaa na kwa sababu hiyo, hakuruhusiwa kuingia Kanaani.


Ni muhimu kukumbuka kuwa maandiko yanatuambia katika wingi wa maneno hapakosi kuwa na maovu kwa msingi huo ni muhimu kumuomba Mungu atupe akili ya kijizuia Mithali 10:19 “Katika wingi wa maneno hapakosi kuwa na maovu; Bali yeye azuiaye midomo yake hufanya akili.” Kama wewe ni mropokaji sana katika maneno ni muhimu sana kumuomba Mungu akuwekee walinzi katika kinywa chako maneno yasikuchomoke tu kama risasi katika bunduki iliyokwisha kutenguliwa kitufe Zaburi 141:1-3 “Ee Bwana, nimekuita, unijie hima, Uisikie sauti yangu nikuitapo.  Sala yangu ipae mbele zako kama uvumba, Kuinuliwa mikono yangu kama dhabihu ya jioni.  Ee Bwana, uweke mlinzi kinywani pangu, Mngojezi mlangoni pa midomo yangu.” Unaweza kuona mfano kwa watakatifu waliotutangulia walijua hatari ya kuropoka walitaka Mungu aweke mngojezi katika vinywa vyao, sisi nasi hatuna budi kumuomba Mungu aweke walinzi kwenye vinywa vyetu

 

c.       Tujifunze kuzungumza maneno ya kujenga:

 

Neno la Mungu linatufundisha ya kuwa tunaweza kutumia vinywa vyetu kujenga, na hilo ndilo kusudi kubwa la Mungu kutuweka Duniani, Biblia inaonya kuwa haifai kuzungumza maneno ya kubomoa, ulimi unafananishwa na chemichemi, hakuna chemichemi moja inayoweza kutoa aina mbili za maji yaani kama ni maji ya chumvi itakuwa ya chumvi na kama ni maji matamu itakuwa maji matamu ona Yakobo 3:10-11 “Katika kinywa kile kile hutoka baraka na laana. Ndugu zangu, haifai mambo hayo kuwa hivyo. Je! Chemchemi katika jicho moja hutoa maji matamu na maji machungu?”  Yakobo anataka kama tunazungumza jambo basi tuzungumze kwa kusudi la kujenga, kwa msingi huo uko umuhimu wa kumuomba Mungu atuongoze na kutusaidia ili tuzungumze maneno ambayo yatamjengea heshima yeye  Waefeso 4:29 “ Neno lo lote lililo ovu lisitoke vinywani mwenu, bali lililo jema la kumfaa mwenye kuhitaji, ili liwape neema wanaosikia.”  Kumbe tunapaswa kuzungumza maneno mema yanayomfaa mwenye uhitaji kufaa mana yeke kujenga kutia ujasiri, kutia moyo, kuleta tumaini, kuwatoa watu kwenye maumivu, kuwaendeleza kuwahuisha na kuwainua,wakati wote tujihadhari na mambo ushirika au maneno yatakayoharibu 1Wakoritho 15:33 “Msidanganyike; Mazungumzo mabaya huharibu tabia njema.” Aidha biblia inatutaka tusiwe watu wa mizaha kupitiliza Mithali inaonya kuwa kuna hukumu ambazozimewekwa tayari kwa wenye mizaha Mithali 19:28-29 “Shahidi asiyefaa kitu hudhihaki hukumu, Na vinywa vya wasio haki humeza uovu. Hukumu zimewekwa tayari kwa wenye mzaha; Na mapigo kwa mgongo wa wapumbavu.”    Biblia inatufundisha kuwa wako vijana 42 ambao walipomuona nabii Elisha ambaye alikuwa na upaa walimchokoza kwa kumtania  na akachukizwa na jambo hilo kiasi ambacho nabii aliweza kuamuru Dubu ambaye aliwararua vijana wale ona 1Wafalme 2:23-24 “Akakwea kutoka huko mpaka Betheli; naye alipokuwa akienda njiani, wakatoka vijana katika mji, wakamfanyizia mzaha, wakamwambia, Paa wewe mwenye upaa! Paa wewe mwenye upaa! Akatazama nyuma akawaona, akawalaani kwa jina la Bwana. Wakatoka dubu wawili wa kike mwituni, wakawararua vijana arobaini na wawili miongoni mwao.Kwa msingi huo tumeona kwa mujibu wa Petro kuwa ili mtu aweze kufurahia maisha na kuona siku njema anapaswa auzuie ulimi wake usinene mabaya au midomo yake isiseme hila na kwamba ni vema kutumia ulimi kwa kuijenga jamii hapo tutayafurahia maisha.

 

2.       Na midomo yake isiseme hila!

 

Mojawapo ya tabia ambazo zimeumiza watu wengi sana duniani ni pamoja na hila au kutenda hila au kusema hila Biblia ya kiingereza imetumia neno GUILE kuzungumzia hila ambalo tafasiri zake ni pamoja na Deceit, au cunning ambalo maana yake ni mbinu za kudanganya, au kwa lugha nyingine ni kufanyiwa utapeli, udanganyifu, ujanja wenye nia ya kudanganya Biblia ya Kiswahili inatumia neno hilo HILA, Mungu anapendezwa sana na mtu ambaye hana hila ona Zaburi 32:1-2 “Heri aliyesamehewa dhambi, Na kusitiriwa makosa yake. Heri Bwana asiyemhesabia upotovu, Ambaye rohoni mwake hamna hila.” Kristo Yesu alipokuwa akiwachagua wanafunzi wake alimuona mmoja wa wanafunzi wake akija na alimsifia kuwa ni Myahudi kwelikweli ambaye hakuna hila ndani yake ona Yohana 1:47-48 “Basi Yesu akamwona Nathanaeli anakuja kwake, akanena habari zake, Tazama, Mwisraeli kweli kweli, hamna hila ndani yake. Nathanaeli akamwambia, Umepataje kunitambua? Yesu akajibu, akamwambia, Kabla Filipo hajakuita, ulipokuwapo chini ya mtini nilikuona.” 


Sasa basi ili tuweze kuyafurahia maisha neno la Mungu linatuonya kuwa tujihadhari na hila katika maisha yetu, tuhakikishe kuwa rohoni mwetu hakuna hila ili tuweze kumpendeza Bwana, Yakobo ni mfano wa mtu aliyekuwa na hila, jina lake pia maana yake ni mwenye hila alitumia hila kumlaghai kaka yake Esau ili kupata haki ya uzaliwa wa kwanza ona Mwanzo 25:29-34 “Yakobo akapika chakula cha dengu. Esau akaja kutoka nyikani, naye alikuwa amechoka sana. Esau akamwambia Yakobo, Tafadhali, unipe hicho chakula chekundu nile, kwa kuwa ninazimia mimi. Kwa hiyo walimwita jina lake Edomu. Yakobo akamwambia, Kwanza niuzie leo haki yako ya mzaliwa wa kwanza. Esau akasema, Tazama, mimi ni karibu kufa, itanifaa nini haki hii ya uzazi? Yakobo akamwambia, Uniapie kwanza. Naye akamwapia, akamwuzia Yakobo haki yake ya mzaliwa wa kwanza. Yakobo akampa Esau mkate na chakula cha dengu, naye akala, akanywa, kisha akaondoka, akaenda zake. Hivyo Esau akaidharau haki yake ya mzaliwa wa kwanza.” Licha Yakobo kufanya hila kuupata haki ya mzaliwa wa kwanza pia alitumia hila kupata Baraka kutoka kwa baba yake, Mwanzo 27:19-20 “Yakobo akamwambia babaye, Mimi ni Esau, mzaliwa wako wa kwanza, nimefanya kama ulivyoniambia. Ondoka, tafadhali, ukae kitako, ule mawindo yangu, ili roho yako inibariki. Isaka akamwuliza mwanawe, Imekuwaje umepata upesi namna hii, mwanangu? Akasema, Kwa sababu BWANA, Mungu wako, amenifanikisha.”  Hata hivyo Hila alizokuwa nazo zilimtokea puani katia maisha yake, aliishi maisha ya kudanganywa nay eye kwa miaika Mingi sana kazi kubwa ilifanyika ya kumbadilisha kutoka kuacha hila na kuwa Israel, ni kweli hila zinaweza kukufanikisha kwa kitambo na kutupa kile tunachofikiri itatupa Lakini Mungu kwa namna yoyote ile hawezi kukubali kuibariki hila na mwisho wa siku lazima tuvuine kile tulichokipanda Mwanzo 29:16-26 “Labani alikuwa na binti wawili, jina la mkubwa ni Lea, na jina la mdogo ni Raheli. Naye Lea macho yake yalikuwa dhaifu, lakini Raheli alikuwa mzuri wa umbo, na mzuri uso. Yakobo akampenda Raheli akasema, Nitakutumikia miaka saba kwa kumpata Raheli, binti yako mdogo. Labani akasema, Afadhali nikupe wewe kuliko mtu mwingine; kaa kwangu. Yakobo akatumika miaka saba kwa kumpata Raheli. Ikawa machoni pake kama siku chache tu kwa vile alivyompenda. Yakobo akamwambia Labani, Nipe mke wangu, maana siku zangu zimetimia; niingie kwake. Labani akakusanya watu wote wa mahali pale, akafanya karamu. Ikawa wakati wa jioni akamtwaa Lea, binti yake, akamletea Yakobo, naye akaingia kwake. Labani akampa Lea mjakazi wake Zilpa, awe mjakazi wake. Ikawa, kulipokuwa asubuhi, kumbe! Ni Lea. Akamwambia Labani, Nini hii uliyonitenda? Sikukutumikia kwa Raheli? Mbona umenidanganya? Labani akasema, Havitendeki hivi kwetu, kumtoa mdogo kabla ya mkubwa;” Hila sio njema na wakati wote inapotajwa katika Biblia haielezwi kama kitu kizuri hakuna uzuri wowote katika hila , Hila siku zote inahusishwa na kazi za ibilisi ona 2wakoritho 11:3 “Lakini nachelea; kama yule nyoka alivyomdanganya Hawa kwa hila yake, asije akawaharibu fikira zenu, mkauacha unyofu na usafi kwa Kristo.Mungu ni mwaminifu naye anapendezwa nasi tukiwa na tabia inayofanana na yeye hivyo anatoa wito kwetu kuwa watu wasio na hila, Yesu Kristo mwenyewe hakuwa na hila ona 1Petro 2:21-22 “Kwa sababu ndio mlioitiwa; maana Kristo naye aliteswa kwa ajili yenu, akawaachia kielelezo, mfuate nyayo zake. Yeye hakutenda dhambi, wala hila haikuonekana kinywani mwake”. Hila ndio moja ya dhambo mbaya ya kuepukwa Pale Yesu alipomwambia Nathaniel kuwa hakuna hila ndani yake alikuwa amemaanisha kuwa ni mtu mwenye kiwango cha juu sana cha uadilifu, Bwana ampe neema kila mmoja wetu kuwa mbali na hila katika jina la Yesu amen

 

3.       Na aache mabaya:

 

Wito wa Mungu wakati wote kwa watu wake ni kuacha mabaya, ili mtu aweze kuwa na siku njema aweze kuufurahia uumbaji na utendaji wa Mungu ni lazima aacha mabaya, Neno kuacha mabaya katika lugha nyingine linatumika neno “Let him eschew evil” Lugha hii ina maana ya kujiepusha na maovu mfano imetumika pia katiika Ayubu 1:1 “Palikuwa na mtu katika nchi ya Usi, jina lake alikuwa akiitwa Ayubu; mtu huyo alikuwa mkamilifu na mwelekevu, ni mmoja aliyemcha Mungu, na kuepukana na uovu.”  Ingawa hatuwezi wakati wote kuepuka kukutana na changamoto mbalimbali lakini hatuna budi kuhakikisha kuwa wakati wote tunaendelea kuwa na huruma na upendo kwa jamii, na hakuna matu anayeweza kuishi maisha ya raha moja kwa moja tuwapo duniani lakini ili tuweze kuyafurahia maisha maisha ya uzima wa milele mbinguni basin i lazima tujiepushe au kuacha mabaya hii ndio njia itakayotupatia maisha mema, Kumbuka Petro alikuwa anawaandikia wakristo waliokuwa wanapoitia katika mateso, kwa hivyo kwao hazikuwa siku njema lakini alikuwa akizungumza kuwa uvumilivu wao utawaleta hatimaye katika kufurahia siku njema kwa hivyo aliwaasa wasiache njia “ekklineo” – wasiende nje ya njia njema, Zaburi 1:1-6 “Heri mtu yule asiyekwenda Katika shauri la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wakosaji; Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha. Bali sheria ya Bwana ndiyo impendezayo, Na sheria yake huitafakari mchana na usiku. Naye atakuwa kama mti uliopandwa Kandokando ya vijito vya maji, Uzaao matunda yake kwa majira yake, Wala jani lake halinyauki; Na kila alitendalo litafanikiwa. Sivyo walivyo wasio haki; Hao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo. Kwa hiyo wasio haki hawatasimama hukumuni, Wala wakosaji katika kusanyiko la wenye haki. Kwa kuwa Bwana anaijua njia ya wenye haki, Bali njia ya wasio haki itapotea.Ni wito wa kiungu wakati wote kuwaita watu wageuke na kuacha njia zao mbaya ili aweze kuwaponya na kuwabariki Ezekiel 33:11 “Waambie, Kama mimi niishivyo, asema Bwana MUNGU, SIKUFURAHII kufa kwake mtu mwovu; bali aghairi mtu mwovu, na kuiacha njia, yake mbaya, akaishi. Ghairini, ghairini, mkaache njia zenu mbaya; mbona mnataka kufa, Enyi nyumba ya Israeli? ” ni ahadi ya Mungu kila wakati kuwabariki watu na kuwatendea mema iwapo wataacha njia mabaya 2Nyakati 7:14 “ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha, na kuomba, na kunitafuta uso, na kuziacha njia zao mbaya; basi, nitasikia toka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao, na kuiponya nchi yao.” Biblia inatutia moyo kuwa rehema za Mungu ziko haijalishi kwamba umewahi kuwa muovu kwa kiwango gani lakini ukibadilisha njia yako leo Mungu yuko tayari kuyabariki maisha yako na kuanza nawe ukurasa mbaya maandiko yamesisitiza wakati wote kuacha njia mbaya, kuishi maisha ya toba kila wakati na kuendelea kumpendeza yeye Isaya 55:6-8 “Mtafuteni Bwana, maadamu anapatikana, Mwiteni, maadamu yu karibu; Mtu mbaya na aache njia yake, Na mtu asiye haki aache mawazo yake; Na amrudie Bwana, Naye atamrehemu; Na arejee kwa Mungu wetu, Naye atamsamehe kabisa. Maana mawazo yangu si mawazo yenu, wala njia zenu si njia zangu; asema Bwana.

 

4.       Atende mema!.

 

Petro anaonekana kuathiriwa sana na usomaji wa zaburi, kwani anarejea tena katika kile ambacho alinukuu kutoka katika Zaburi ya Daudi ambayo mara kadhaa imesisitiza kuwa sasa kwa kuwa tumeacha mabaya na tutende mema ona Zaburi 37:1-4 “Usikasirike kwa sababu ya watenda mabaya, Usiwahusudu wafanyao ubatili. Maana kama majani watakatika mara, Kama miche mibichi watanyauka. Umtumaini Bwana ukatende mema, Ukae katika nchi, upendezwe na uaminifu. Nawe utajifurahisha kwa Bwana, Naye atakupa haja za moyo wako.” Ona pia Zaburi 37: 27-28 “Jiepue na uovu, utende mema, Na kukaa hata milele.     Kwa kuwa Bwana hupenda haki, Wala hawaachi watauwa wake. Wao hulindwa milele, Bali mzao wa wasio haki ataharibiwa.” Mara kadhaa maandiko yameonyesha kile ambacho Mungu anakitaka kwetu na ambacho ni kutenda mema Mika 6:8 “Ee mwanadamu, yeye amekuonyesha yaliyo mema; na Bwana anataka nini kwako, ila kutenda haki, na kupenda rehema, na kwenda kwa unyenyekevu na Mungu wako!

 

5.       Atafute amani.

 

Mwisho Petro anataka tuitafute amani, kwa kweli neno la Mungu Biblia kwa mukhtasari ni kitabu cha amani, ili mtu awe kamili anapaswa kuwa na amani na Mungu na amani na wanadamu, hili ndio agizo la kibiblia, Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao;Amani ina faida kubwa sana kwetu tunapotaka kustawisha uhusiano wetu kwa Mungu na wanadamu, hatuwezi kuwa sawa na Mungu kama hatuna amani na mtu fulani 1Yohana 4:20-21 “Mtu akisema, Nampenda Mungu, naye anamchukia ndugu yake, ni mwongo; kwa maana asiyempenda ndugu yake ambaye amemwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hakumwona. Na amri hii tumepewa na yeye, ya kwamba yeye ampendaye Mungu, ampende na ndugu yake.” Mke na Mume wasipokaa kwa akili na kuhakikisha kuwa wana amani maombi yao yanaweza kuzuiwa 1Petro 3:7 “Kadhalika ninyi waume, kaeni na wake zenu kwa akili; na kumpa mke heshima, kama chombo kisicho na nguvu; na kama warithi pamoja wa neema ya uzima, kusudi kuomba kwenu kusizuiliwe.Watu wanapokosa amani kati yao na akama hawajatengeneza au kupatana jambo hilo husima a kama ukuta katika ain azote za ibada ikiwepo sadaka Mathayo 5:23-24 “Basi ukileta sadaka yako madhabahuni, na huku ukikumbuka ya kuwa ndugu yako ana neno juu yako, iache sadaka yako mbele ya madhabahu, uende zako, upatane kwanza na ndugu yako, kisha urudi uitoe sadaka yako.” Yesu alimaanisha wazi kuwa hatuwezi kupokea Baraka zozote zile kama tumevuruga amani, hivyo ni muhimu kupatana na mashitaki wako upesi ili asizuie Baraka zako katika ulimwengu wa Roho, Maagizo ya kibiblia yanatutaka tuitafute sana amani kwa sababu kuna gharama kubwa sana kuipata, amani inapaswa kutafutwa kwa bidii, Yakobo alikuwa amemuuzi kaka yake Esau kiasi ambacho Esau aliapa kuwa atamuua, jambo hili lilisabababisha akimbie mbali ujombani, lakini huko nako hakuwa na amani maisha yake yalikuwa taabuni kwa sababu Esaua angemuua na Esau aliposikia kuwa Yakobo anakuja alikuja na kikosi cha askari mia nne huu ulikuwa wakati mbaya sana katika maisha ya Yakobo na hapa ndipo alipoutafuta uso wa Mungu na vilevile alitafuta msamaha wa kweli kutoka kwa Esau ona Mwanzo 32: 1-8 “Yakobo akashika njia yake na malaika wa Mungu wakakutana naye. Naye Yakobo alipowaona, alisema, Hili ni jeshi la Mungu. Akapaita mahali pale, Mahanaimu. Basi, Yakobo akapeleka wajumbe mbele yake kwenda kwa Esau nduguye mpaka nchi ya Seiri katika nyika ya Edomu. Akawaagiza akisema, Mwambieni hivi bwana wangu, Esau, Hivi ndivyo asemavyo mtumwa wako, Yakobo; Nimekaa ugenini kwa Labani, na kukawia huko hata sasa, nami nina ng'ombe, na punda, na kondoo, na watumwa, na vijakazi; nami nimepeleka watu nimpashe bwana wangu habari, nipate neema machoni pako. Wale wajumbe wakarudi kwa Yakobo wakisema, Tulifika kwa ndugu yako, Esau, naye anakuja kukulaki, na watu mia nne pamoja naye.Ndipo Yakobo akaogopa sana, na kufadhaika sana, akawagawanya watu waliopo pamoja naye, na kondoo, na ng'ombe, na ngamia, wawe matuo mawili. Akasema, Akija Esau kwa kundi la kwanza, akalipiga, kundi litakalosalia litaokoka.Ni wazi kuwa Esau angekuja kufanya vita na Yakobo na yakobo aliogopa na aliamua kumuomba Mungu usiku ule na Mungu alimuelekeza namna ya kupata amani ilimgharimu sana lakini alifabya bidii ili aweze kuwa na amani na ndugu yake, kila atakaye kupenda maisha yaani maisha haya nay ale yajayo hana budi kujikita katika kuitafuta amani kwa bidii, Yakobo aliiitafuta sana na Mungu akamfanikisha  Mwanzo 33:1-11 “Yakobo akainua macho yake, akaona, na tazama, Esau anakuja na watu mia nne pamoja naye. Akawagawanyia Lea, na Raheli, na wale vijakazi wawili, wana wao. Akawaweka hao vijakazi na wana wao mbele, na Lea na wanawe nyuma yao, na Raheli na Yusufu mwisho. Akapita mwenyewe mbele yao, akainama mpaka nchi mara saba, hata alipomkaribia ndugu yake. Esau akaja mbio kumlaki, akamkumbatia, na kumwangukia shingoni, akambusu; nao wakalia. Akainua macho yake, akawaona wale wanawake na watoto, akauliza, Ni nani hawa walio pamoja nawe? Akasema, Ni watoto Mungu aliompa mtumwa wako kwa neema yake. Ndipo wale vijakazi, na wana wao, wakakaribia wakainama.Lea naye, na wanawe, wakakaribia wakainama. Baadaye Yusufu na Raheli wakakaribia, wakainama. Akasema, Kundi hili lote nililolikuta, maana yake ni nini? Akasema, Kunipatia kibali machoni pa bwana wangu.  Esau akasema, Ninayo tele, ndugu yangu, uliyo nayo na yawe yako. Yakobo akasema, Sivyo; kama nimekubalika machoni pako tafadhali upokee zawadi yangu mkononi mwangu, iwapo nimeona uso wako kama kuona uso wa Mungu, ukapendezwa nami. Pokea, tafadhali, mbaraka wangu, ulioletewa, kwa sababu Mungu amenineemesha, na kwa sababu ninavyo hivi vyote Akamshurutisha, naye akapokea.”

 

1Petro 3:10-12Kwa maana, Atakaye kupenda maisha, Na kuona siku njema, Auzuie ulimi wake usinene mabaya, Na midomo yake isiseme hila. Na aache mabaya, atende mema; Atafute amani, aifuate sana. Kwa kuwa macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, Na masikio yake husikiliza maombi yao; Bali uso wa Bwana ni juu ya watenda mabaya.”

 

Na. Rev. Innocent Kamote.

Mkuu wa Wajenzi mwenye Hekima!

Jumanne, 20 Aprili 2021

Mtetezi wangu yu hai

Mstari wa msingi: Ayubu 19:25-27Lakini mimi najua ya kuwa Mteteaji wangu yu hai, Na ya kuwa hatimaye atasimama juu ya nchi. Na baada ya ngozi yangu kuharibiwa hivi, Lakini, pasipokuwa na mwili wangu nitamwona Mungu; Nami nitamwona mimi nafsi yangu, Na macho yangu yatamtazama, wala si mwingine. Mtima wangu unazimia ndani yangu


.”


Utangulizi:

Lakini mimi najua mteteaji wangu yu hai - ni moja ya vifungu vilivyojipoatia umaarufu mkubwa sana katika Biblia na kuvutia mioyo ya watu wengi sana na kutolewa maoni mbalimbali, na wataalamu mbalimbali wa neno la Mungu na watafasiri wengi wa Biblia, huku wengi wakivutiwa na kifungu hiki cha Ayubu 19:25-27 hasa kwa vile kifungu hiki kina uhusiano mkubwa sana na unabii wa kuja Masihi. Lakini sio hivyo tu kifungu hiki kina mvuto mkubwa saa kwa sababu kinapandisha imani zetu. Leo tutachukua muda kwa ufupi kujifunza kuhusiana na kile ambacho Mungu anataka kusema nasi kupitia kifungu hiki.


Kimsingi kitabu cha  Ayubu ni kitabu cha kwanza kati ya vitabu vya Mashairi ya kiibrania, kikifuatiwa na Zaburi, Mithali, Muhubiri na Wimbo uliobora Lakini vitabu hivi pia  ni vitabu vya  Kifalsafa.  Kitabu cha Ayubu chenyewe kina uhusiano mkubwa sana na falsafa ya Mateso na hasa kikiwa na maswali kwa nini mwenye haki ateseke? Lakini kama haitoshi pia kinatabiri mateso ya Yesu ambaye hakuwa na dhambi lakini aliteseka kwa kusudi la kuwakomboa wanadamu, Katika kitabu hiki tunaona kwa undani sana mateso mazito yaliyompata Ayubu na kimsingi Mateso haya yalikuwa na sababu ambayo kwa wakati huo wa Ayubu hakuwa anajua nini kilikuwa kinaendelea katika ulimwengu wa roho, Mateso yake kwa kiwango kikubwa yalichangiwa na wivu, dhuluma na uonevu wa shetani, kama tunavyotahadharishwa leo katika maandiko  Ona 1Petro 5:8 “Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze.” Shetani alileta uonevu huu kwa mtu wa Mungu hata pamoja na kuwa mtu huyu aliishi maisha ya haki, Maandiko yanaonyesha wazi kuwa Ayubu alikuwa mtu wa haki na kwa sababu hiyo mateso yake hayakuwa kwamba ni kwa sababu amemkosea Mungu! Lakini maandiko yanaonyesha wazi kuwa ni kwa sababu ya mshitaki wetu shetani namna na jinsi anavyofanya kazi katika ulimwengu wa roho!


Mateso ya Ayubu:-

 

Ø  Ayubu aliishi maisha ya haki ona Ayubu 1:1-3Palikuwa na mtu katika nchi ya Usi, jina lake alikuwa akiitwa Ayubu; mtu huyo alikuwa mkamilifu na mwelekevu, ni mmoja aliyemcha Mungu, na kuepukana na uovu. Kisha walizaliwa kwake wana saba, na binti watatu. Mali yake nayo yalikuwa ni kondoo elfu saba, na ngamia elfu tatu, na jozi za ng'ombe mia tano, na punda wake mia tano, na watu wa nyumbani wengi sana; basi hivi mtu huyo alikuwa ni mkuu sana kuliko watu wote wa upande wa mashariki.      

 

Ø  Asili ya Mateso ya Ayubu yalitokana na mashitaka ya Shetani katika ulimwengu wa roho ona Ayubu 1:6-12Ilikuwa, siku moja ambayo hao wana wa Mungu walikwenda kujihudhurisha mbele za Bwana, Shetani naye akaenda kati yao. Bwana akamwuliza Shetani, Umetoka wapi wewe? Ndipo Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Natoka katika kuzunguka-zunguka duniani, na katika kutembea huku na huku humo.Kisha Bwana akamwuliza Shetani, Je! Umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Kwa kuwa hapana mmoja aliye kama yeye duniani, mtu mkamilifu na mwelekevu, mwenye kumcha Mungu na kuepukana na uovu. Ndipo Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Je! Huyo Ayubu yuamcha Bwana bure? Wewe hukumzingira kwa ukigo pande zote, pamoja na nyumba yake, na vitu vyote alivyo navyo? Kazi za mikono yake umezibarikia, nayo mali yake imeongezeka katika nchi. Lakini nyosha mkono wako sasa, uyaguse hayo yote aliyo nayo, naye atakukufuru mbele za uso wako. Bwana akamwambia Shetani, Tazama, yote aliyo nayo yamo katika uwezo wako; lakini usinyoshe mkono wako juu yake yeye mwenyewe. Basi Shetani akatoka mbele za uso wa Bwana.”

 

Ø  Shetani alimuonea Ayubu kupitia mali zake ona Ayubu 1:13-19Bwana akamwambia Shetani, Tazama, yote aliyo nayo yamo katika uwezo wako; lakini usinyoshe mkono wako juu yake yeye mwenyewe. Basi Shetani akatoka mbele za uso wa Bwana.Ilitukia siku moja hao wanawe na binti zake walipokuwa wakila na kunywa divai katika nyumba ya ndugu yao mkubwa,mjumbe akamfikilia Ayubu na kumwambia, Hao ng'ombe walikuwa wakilima, na punda walikuwa wakilisha karibu nao; mara Waseba wakawashambulia, wakawachukua wakaenda nao; naam, wamewaua hao watumishi kwa makali ya upanga, mimi peke yangu nimepona, mimi tu, kukuletea habari. Huyo alipokuwa akali akinena, akatokea na mwingine, na kusema, Moto wa Mungu umeanguka kutoka mbinguni na kuwateketeza kondoo, na wale watumishi, na kuwaangamiza; mimi peke yangu nimepona, mimi tu, kukuletea habari. Huyo alipokuwa akali akinena, akatokea na mwingine, na kusema, Wakaldayo walifanya vikosi vitatu, wakawaangukia ngamia, wakaenda nao, naam, wamewaua wale watumishi kwa makali ya upanga; mimi peke yangu nimepona, mimi tu, kukuletea habari. Huyo alipokuwa akali akinena, akatokea na mwingine, na kusema, Wanao na binti zako walikuwa wakila na kunywa divai katika nyumba ya ndugu yao mkubwa; mara, tazama, upepo wenye nguvu ukatoka pande za jangwani, ukaipiga hiyo nyumba pembe zake nne, nayo ikawaangukia hao vijana, nao wamekufa; na mimi peke yangu nimepona, mimi tu, kukuletea habari.

 

Ø  Shetani alimuonea Ayubu kupitia afya yake aliiharibu kabisa afya ya Ayubu kwa sababu Ayubu alikuwa ma majipu mabaya yaliyokuwa yakioza na kufumba na kupasuka kila eneo la mwili wake  

     Ayubu 2:7-10 “Basi Shetani akatoka mbele za uso wa Bwana, akampiga Ayubu na majipu mabaya tangu wayo wa mguu hata utosi wa kichwa.Naye akashika kigae cha kujikunia; akaketi majivuni. Ndipo mkewe akamwambia, Je! Wewe hata sasa washikamana na utimilifu wako? Umkufuru Mungu, ukafe. Lakini yeye akamwambia, Wewe wanena kama mmoja wa hao wanawake wapumbavu anenavyo. Je! Tupate mema mkononi mwa Mungu, nasi tusipate na mabaya? Katika mambo hayo yote Ayubu hakufanya dhambi kwa midomo yake.”           

Ø  Watu na rafiki zake Ayubu waliposikia yaliyompata walifunga safari kuja kumtia moyo lakini walipoona kwa mbali hali halisi ya maisha ya Ayubu waliomboleza kwa kulia sana na kurarua mavazi yao, huku wakirusha michanga juu, inasemekana kwa siku saba wote walikaa kimya na hakuna aliyeweza kuzungumza lolote yaani walishindwa unaanzia wapi kumfariji kwani yaoikuwa ni majanga makubwa mno ona  


Ayubu 2:11-13 “Basi ikawa hao rafikize Ayubu watatu walipopata habari ya mabaya hayo yote yaliyomfikilia, wakaja kila mtu kutoka mahali pake; nao ni Elifazi Mtemani, na Bildadi Mshuhi, na Sofari Mnaamathi; wakapatana pamoja ili waende kumlilia Ayubu na kumtuliza moyo. Basi walipovua macho yao, nao wakali mbali, wasimtambue, wakainua sauti zao na kulia; kila mmoja akararua joho yake, wakarusha mavumbi juu ya vichwa vyao kuelekea mbinguni. Kisha wakaketi nchi pamoja naye muda wa siku saba, mchana na usiku, wala hapana mmoja aliyenena naye neno lo lote; kwa maana waliona ya kuwa mashaka yake aliyo nayo ni makuu mno.”    

 

Ø  Mateso ya Ayubu yalizidi kiasi cha kufikia kiwango cha kuilaani siku yake ya kuzaliwa ona Ayubu 3:1-4 “Baada ya hayo Ayubu akafunua kinywa chake, na kuilaani siku yake. Ayubu akajibu, na kusema; Na ipotelee mbali ile siku niliyozaliwa mimi, Na ule usiku uliosema, Mtoto mume ametungishwa mimba. Siku hiyo na iwe giza; Mungu asiiangalie toka juu, Wala mwanga usiiangazie.”Ayubu alitamani kama angekufa tangu tumboni ili aweze kupumzika aliyaona maisha ya dunia hii kuwa ni maisha yasiyofaa hata kidogo Mstari wa 11-13 unasema hivi “Mbona si kufa mimi tokea mimbani? Mbona nisitoe roho hapo nilipotoka tumboni? Mbona hayo magoti kunipokea? Au hayo maziwa, hata nikanyonya? Maana hapo ningelala na kutulia; Ningelala usingizi; na kupata kupumzika;

 

Ø  Pamoja na mates ohayo yote inasemekana kuwa Ayubu alikimbiwa na watu wote waliokuwa karibu naye tunaelezwa wazi mwanzoni kuwa watu wengi sana walimjia Ayubu alipokuwa na uwezo ona Ayubu 1:3 “Mali yake nayo yalikuwa ni kondoo elfu saba, na ngamia elfu tatu, na jozi za ng'ombe mia tano, na punda wake mia tano, na watu wa nyumbani wengi sana; basi hivi mtu huyo alikuwa ni mkuu sana kuliko watu wote wa upande wa mashariki.” Lakini Ayubu alipopatwa na majanga na umasikini kila mtu alimkimbia ona Ayubu 19:13-21 “Amewaweka ndugu zangu mbali nami, Na wanijuao wametengwa nami kabisa. Watu wa mbari yangu wamekoma, Na rafiki zangu niwapendao wamenisahau. Wakaao nyumbani mwangu, na vijakazi vyangu, wanihesabu kuwa mgeni; Mimi ni mgeni machoni pao. Namwita mtumishi wangu, wala haniitikii, Ingawa namsihi kwa kinywa changu. Pumzi zangu ni kama za mgeni kwa mke wangu, Nami ni machukizo kwa ndugu zangu. Hata watoto wadogo hunidharau; Nikiondoka, huninena. Wasiri wangu wote wanichukia; Na hao niliowapenda wamenigeukia. Mfupa wangu unagandamana na ngozi yangu na nyama yangu, Nami nimeokoka na ngozi ya meno yangu tu. Nihurumieni, nihurumieni, enyi rafiki zangu, Kwa maana mkono wa Mungu umenigusa.”

 

Ø  Ayubu alikuwa na Machungu mengi sana Moyoni na alifikiri kuwa mambo yote hayo maovu na mabaya yanatoka kwa Mungu alimlaumu muumba wake ona Ayubu 6:2-4 “ Laiti uchungu wangu ungepimwa, Na msiba wangu kutiwa katika mizani pamoja! Kwa kuwa sasa ungekuwa mzito kuliko mchanga wa bahari; Kwa hiyo maneno yangu yamekuwa ya haraka. Kwa kuwa mishale ya huyo Mwenyezi i ndani yangu, Na roho yangu inainywa sumu yake; Vitisho vya Mungu vimejipanga juu yangu.

 

Mtetezi wangu yu hai!:-

Kutokana na uoenvu huu wa shetani Ayubu alielewa kuwa alikuwa anaonewa na kudhulumiwa na Ibilisi alifahamu kuwa nimshitaki wetu yuko kazini na anamchochea Muumba ilia pate kufanya haya aliyoyafanya shetani, hata hivyo pamoja na changamoto zote hizo imani yake Ayubu haikutindika aliamini ya kuwa mteteaji wake yu hai nay a kuwa hatimaye ataismama juu ya nchi kumtetea

Ni muhimu kufahamu kuwa neno linalotrumika hapa kwa Mteteaji wangu katika kiingereza linasomeka kama “redeemer” katika lugha ya kiebrania neno linalotumika hapo ni ni Ga’al au Go’ al ambalo lilitumika kumaanisha mtu mwenye kulipia gharama ya hasara zote ulizozipata, au aliyekulipia gharama za shamba lililouzwa, au mali iliyopotea, au anayekukomboa kutoka katika umasikini kwa mfano ulipoteza shamba lako kwa umasikini kisha akaja ndugu yako aliye karibu akalilipia na kukurudishia huyu sasa ndiye aliyeitwa Ga’al au Go’ al   kwa kizigua Mkombozi, ona kwa mfano Mambo ya walawi 25:25-26 “Kwamba nduguyo amekuwa maskini, na kuuza sehemu ya milki yake, ndipo jamaa yake aliye karibu naye atakuja, naye ataikomboa ile aliyoiuza nduguye. Na kama mtu hana atakayeikomboa, naye mwenyewe amepata mali na kujiona kuwa anayo ya kutosha kuikomboa;” Neno hilo pia lilitumika kwa mtu aliyechukuliwa utumwani kisha mtu akaja kumnunua kwa kusudi la kumkomboa unaweza kuliona katika Kutoka 6:6 na Isaya 43:1 ona Kutoka 6:6 “Basi waambie wana wa Israeli, Mimi ni YEHOVA, nami nitawatoa ninyi mtoke chini ya mizigo ya Wamisri, nami nitawaokoa na utumwa wao, nami nitawakomboa kwa mkono ulionyoshwa, na kwa hukumu kubwa;” pia angalia Isaya 43:1 “Lakini sasa, Bwana aliyekuhuluku, Ee Yakobo, yeye aliyekuumba, Ee Israeli, asema hivi, Usiogope, maana nimekukomboa; nimekuita kwa jina lako, wewe u wangu.”

Mpendwa haijalishi umekosa furaha na amani mara ngapi, haijalishi umedhulumiwa mara ngapi, haujalishi umefanyiwa fitina mara ngapi, haijalishi umeteseka kwa muda gani, hajalishi shetani amekuonea kwa kiwango gani, haijalishi kwamba una onewa na magonjwa na mateso kwa kiwango gani , haijalishi wazee wa kanisa nwanakukandamiza kwa kiwango gani, hajalishi manabii wamekudhulumu kwa kiwango gani, hajalishi unapitia changamoto za aina gani, haijalishi umeibiwa mara ngapi, haijalishi umelizwa mara ngapi, haijalishi una huzuni kwa kiasi gani  leo natangaza ya kuwa Mkombozi wetu yu hai, Ayubu aliamini ya kuwa siku moja atasimama atatokea juu ya uso wa nchi na kumtetea mimi natangaza kuwa amekwishakutokea, namtangaza metetaji wetu yuko hai na kuwa ameketi mkono wa kuume wa nguvu; Mbinguni na anafuatulia kwa ukaribu maumivu na mateso unayoyapitia, nakutaarifu kuwa mbingu zina taarifa ya kile unapitia, Mbingu zinataarifa ya kile familia yako inapitia, mama yako na baba yako na wazazi wako na ndugu zako kila wanalolipitia na kile unapitia katika ndoa yako na popote pale nakutangazia kuwa Yuko mkombozi yuko mtetezi haijalishi ni huzuni kiasi gani tunapitia lakini nataka tumuamini kuwa anajua hali zetu na kuwa hatupaswi kuogopa lolote,  na kuwa atalipa atatulipia machungu yote na machozi yote na huzuni zote tutalipiwa tu Mungu yuko atatulipia, Mtetezi wetu yu hai aatashughulika hatupaswi kuogopa ametuita kwa jina lake ametukomboa kwa mkono wake yu haiiiiii!

Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa Wajenzi mwenye Hekima   


Alhamisi, 25 Machi 2021

Kifo Katika Mpango wa Mungu!

Ayubu 14:5 “Kwa kuwa siku zake zimeamriwa, hesabu ya miezi yake unayo wewe, Nawe umemwekea mipaka yake asiyoweza kuipita;”


Utangulizi:

Kumekuwepo na mijadala mbalimbali, mitazamo na falsafa kuhusu kifo!, Baadhi wakiamini kuwa kila kifo ni mapenzi ya Mungu, wengine wanaamini kama Mungu akiamua usife huwezi kufa na akiamua ufe unakufa, na wengine wakiamini kuwa kila mwanadamu ana siku zake zilizoamriwa kuishi duniani na zikikamilika anaondoka, wengine wanaamini kuwa Mungu huwa anahuzunika sana mtu anapokufa kama sisi  nasi tunapohuzunika matukio ya kifo yanapotokea, lakini kwa sababu tunaishi katika ulimwengu wa dhambi Mungu huruhusu kifo kutokea Ni muhimu kufahamu kuwa ni neno la Mungu pekee yaani Biblia inayoweza kutupa majibu ya maswali yetu kuhusu kifo na maana halisi ya kifo kinapotokea! Lakini ni lazima kwanza tufahamu kuwa Mungu hapendi kuwatesa wanadamu wala kuwahuzunisha ona

 

Maombolezo 3:31-33 “Kwa kuwa Bwana hatamtupa mtu Hata milele. Maana ajapomhuzunisha atamrehemu, Kwa kadiri ya wingi wa huruma zake. Maana moyo wake hapendi kuwatesa wanadamu. Wala kuwahuzunisha.”

Kifo katika mpango wa Mungu!

Ni muhimu kufahamu kuwa Mungu katika mpango wake hakuwa amekusudia kifo kiwepo katika maisha ya mwanadamu, na ndio maana kwa asili hakuna mwanadamu anayekubali au kukipenda kifo kwa sababu kimsingi sio maumbile ya asili yetu Mungu alimuumba mwanadamu ili aishi milele na ndio maana kifo kimekuwa kinampa taabu sana mwanadamu kwa maana haukuwa mpango wala mapenzi kamili ya Mungu



Muhubiri 3:10-11 “Nimeiona taabu ambayo Mungu amewapa wanadamu, ili kutaabika ndani yake. Kila kitu amekifanya kizuri kwa wakati wake; tena ameiweka hiyo milele ndani ya mioyo yao; ila kwa jinsi mwanadamu asivyoweza kuivumbua kazi ya Mungu anayoifanya, tangu mwanzo hata mwisho.” 


Kifo na taabu zake kimekuja kama matokeo ya kuasi kwa mwanadamu, kwa hiyo Mungu alimuwekea mwanadamu uchaguzi kuchagua uzima au mauti kupitia kutii au kuasi na kwa bahati mbaya mwanadamu akaasi na hapo ndipo ilipokuja adhabu ya kifo ambayo Mungu alikuwa amemuonya nayo Adamu ona


Mwanzo 2:15-17 “BWANA Mungu akamtwaa huyo mtu, akamweka katika bustani ya Edeni, ailime na kuitunza. BWANA Mungu akamwagiza huyo mtu, akisema, Matunda ya kila mti wa bustani waweza kula, walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika.”


Kwa msingi huo kifo kipo Duniani leo kwa sababu ya kuasi kwa mwanadamu mmoja baba yetu Adamu na mama yetu Eva kwa sababu sisi tulikuwa viunoni mwao wakati wana wanaasi na kwa sababu hiyo wanadamu wote wanaonja mauti ona


Warumi 5:12 “Kwa hiyo, kama kwa mtu mmoja dhambi iliingia ulimwenguni, na kwa dhambi hiyo mauti; na hivyo mauti ikawafikia watu wote kwa sababu wote wamefanya dhambi;”


kwa hiyo kifo kiliingia ulimwenguni kwa sababu ya dhambi na kikawafikia watu wote kwa nini kwa sababu wote tulikuwa katika viuno vya wazazi hao kwa msingi huo tuwe wema au tuwe waovu ni lazima tutaionja mauti, Kama mwanadamu hangelifanya dhambi, muda wetu wa kutimiza makusudi ya Mungu Duniani ungekuwa kama umekamilika Mungu angetutwaa kwenda mbinguni kukaa naye bila kuonja mauti ona

Mwanzo 5:24 “Henoko akaenda pamoja na Mungu, naye akatoweka, maana Mungu alimtwaa


.” Huu ndio ulikuwa mpango kamili wa Mungu (Perfect will of God), kwa msingi huo kifo sio mpango kamili wa Mungu bali ni matokeo ya dhambi ambayo yameruhusiwa na Mungu (permissive will of God).sasa kifo kimekuwepo na Mungu aliandaa mpango mwingine wa kukikomesha wakati wa utimilifu wa dahari utakapowadia.

Je kila kifo kinachotokea ni mpango wa Mungu?

Swali hili linaweza kuwa na majibu NDIO na HAPANA kulingana na mazingira ya kifo chenyewe kwa mujibu wa neno la Mungu sio kila kifo kinachotokea ni mpango wa Mungu wala sio mapenzi yake kamili, Maandiko ynashuhudia wazi kuwa Mungu hapendi wala hafurahii kufa kwake mtu mwenye dhambi! Ona

Ezekiel 33:11 “Waambie, Kama mimi niishivyo, asema Bwana MUNGU, SIKUFURAHII kufa kwake mtu mwovu; bali aghairi mtu mwovu, na kuiacha njia yake mbaya, akaishi. Ghairini, ghairini, mkaache njia zenu mbaya; mbona mnataka kufa, Enyi nyumba ya Israeli?


kwa hiyo kumbe linapokuja swala la Mtu kufa Mungu hapendi afe mtu mwenye dhambi, Mungu hafurahii kufa kwake mtu muovu, Mungu anatamani mtu awe ametubu, awe amegeuka na kuacha njia mbaya kabla ya kifo ili waweze kuungana naye, haya ndio mapenzi kamili kwa kila mwanadamu na ndio maana wakati mwingine Mungu huwaacha waovu kwa kitambo na kuwavumilia ili yamkini ikiwezekana wafikie wakati wa kutubu ona


2Petro 3:9 “. Bwana hakawii kuitimiza ahadi yake, Kama wengine wanavyokudhani kukawia, bali huvumilia kwenu, maana HAPENDI mtu ye yote apotee, bali wote wafikilie toba”.


kwa hiyo Mungu hapendi, na hafurahii na hivyo kuna nyakati huwacheklewesha waovu wasife kwa haraka au wasife kabla hawajafikia toba, kwa hiyo kuna mazingira ambayo kwayo Mungu hatafurahia au hafurahii kufa kwa mtu hususani mtu mwenye dhambi. Kwa hiyo Mungu husubiri mtu aifikie toba mtu ageuke na kuiacha njia yake mbaya

Hata hivyo kifo ni kanuni, ni kanuni ya adhabu kwa kitokumtii Mungu, kifo kama kanuni ya adhabu ya kutokumtii Mungu ni hitimisho la hatua kadhaa zisizochukuliwa katika hatua ya dhambi, angalia andiko hili kwa mfano


Yakobo 1:14-15 “Lakini kila mmoja hujaribiwa na tamaa yake mwenyewe huku akivutwa na kudanganywa. Halafu ile tamaa ikiisha kuchukua mimba huzaa dhambi, na ile dhambi ikiisha kukomaa huzaa mauti.”


Kanuni ya kifo ni dhambi kuna namna ambavyo Mungu katika hekima yake anakiruhusu kifo kwa nafi yenye dhambi, japo kifo sio mapenzi yake kamili lakini ni mshahara wa dhambi kwa hiyo kama nafsi itajaribiwa dhambini na kukawia kufanya toba na kwa bahati mbaya hatuwezi kujua muda ambao Mungu anatupa wa toba kanini ya kifo ambayo ni dhambi ikikomaa inaleta mauti kwa hiyio Mungu pia huruhusu mtu kufa endapo nafsi ya mtu huyo itatenda dhambi ona mfano


Ezekiel 18:20-23 “Roho itendayo dhambi, ndiyo itakayokufa; mwana hatauchukua uovu wa baba yake, wala baba hatauchukua uovu wa mwanawe, haki yake mwenye haki itakuwa juu yake, na uovu wake mwenye uovu utakuwa juu yake. Lakini mtu mbaya akighairi, na kuacha dhambi zake zote alizozitenda, na kuzishika amri zangu zote, na kutenda yaliyo halali na haki, hakika ataishi, hatakufa. Dhambi zake zote alizozitenda hazitakumbukwa juu yake hata mojawapo; katika haki yake aliyoitenda ataishi. Je! Mimi ninafurahia kufa kwake mtu mwovu? Asema Bwana MUNGU; si afadhali kwamba aghairi, na kuiacha njia yake, akaishi?” 


Unaona hivyo basi kutokana na kanuni Fulani za dhambi zinapoendelea kutendwa na nafsi basi Mungu huweza kuruhusu Dhambi hiyo kusababisha kifo na kukatiza uhai wa nafsi husika kwa ain azote za uzima huu na ule ujao 


Kutoka 21:14,-16 “Lakini, mtu akimwendea mwenziwe kwa kujikinai, kusudi apate kumwua kwa hila; huyo utamwondoa hata madhabahuni pangu, auawe. Ampigaye baba yake au mama yake, sharti atauawa.Yeye amwibaye mtu, na kumwuza, au akipatikana mkononi mwake, sharti atauawa huyoKatika mazingira kama kifo kinachotokea hapa ni mpango wa Mungu katika mantiki kwamba uovu umepelekea kufa, tama imepelekea nafsi itendayo dhambi kufa, kwa hiyo sio mapenzi ya Mungu mtu kufia katika dhambi, lakini ni mwanadamu anapokuwa na ukaidi Fulani kinyume na amri za Mungu mungu huruhusu mtu huyo kufa. Kwa hiyo yako mazingira jibu linaweza kuwa ndio na yako mazingira jibu linaweza kuwa sio!

Kwa mfano sio mapenzi ya Mungu kwa watoto wasiowahehimu wazazi wao kufa kabla ya wakati ona Waefeso 6:1-3 “Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika Bwana, maana hii ndiyo haki. Waheshimu baba yako na mama yako; amri hii ndiyo amri ya kwanza yenye ahadi, Upate heri, ukae siku nyingi katika dunia.” Kumbe ni mapenzi ya Mungu kwamba watoto wawaheshimu wazazi wao ili siku zao zipate kuwa nyingi tena na za heri duniani, Lakini mtoto ambaye atamlaani baba yake au mama yake Mungu ameamuru apigwe kwa mawe mpaka kufa, kwa lugha nyingine maisha ya mtoto asiyewaheshimu wazazi yatafupishwa 


Kutoka 21:15, 17 “Ampigaye baba yake au mama yake, sharti atauawa. Yeye amwapizaye baba yake au mama yake, sharti atauawa.” kwa hiyo ni wazi kuna mazingira ya aina fulani Mungu hataki mtu afe kwa dhambi na kuna mazingira fulani Mungu huruhusu mtu afe kwa sababu ya dhambi.

Je Mungu hujisikiaje wanapokufa watu wengi?

Swala lingine nyeti ni je Mungu hujisikiaje wanapokufa watu kwa wingi? Kimaandiko bado Mungu huuzunishwa sana wanapokufa watu wengi wakiwa dhambini, Mungu huuzunishwa dhambi inapozidi na hivyo huweza kuruhusu maangamizi mfano 


Mwanzo 6:5-7 “BWANA akaona ya kuwa maovu ya mwanadamu ni makubwa duniani na kwamba kila kusudi analowaza moyoni mwake ni baya tu sikuzote. BWANA akaghairi kwa kuwa amemfanya mwanadamu duniani, akahuzunika moyo. BWANA akasema, Nitamfutilia mbali mwanadamu niliyemwumba usoni pa nchi; mwanadamu na mnyama, na kitambaacho na ndege wa angani; kwa maana naghairi ya kwamba nimewafanya.” 


Wakati wa Nuhu Mungu aliufutilia ulimwengu kwa gharika kwa sababu ya kuongezeka kwa maasi, kimsingi Mungu hafurahii udhalimu na uovu unaofanywa na watu, hapendi watu wafe lakini dhambi hupelekea Mungu kuruhusu vifo.


Dunia inaweza kukabiliwa na majanga kama watu hawatatubu, mji au nchi au taifa kama halitamjali Mungu Mungu anaweza kuachilia roho ya mauti ikafanya kazi yake na kuleta madhara kwa watu wema na wabaya wote wakaathirika kutokana na ule ukaidi wa kibinadamu wa kufa kwa dhamiri na kutaka kuendelea kuishi katika maisha ya dhambi ona 


Mwanzo 18:20 “BWANA akasema, Kwa kuwa kilio cha Sodoma na Gomora kimezidi, na dhambi zao zimeongezeka sana,” 

Dhuluma na uharibifu wa dhambi uliofanywa na watu wa Sodoma na Gomora ulimsukuma Mungu kuruhusu miji hiyo kuangamizwa kwa wingi wao, Kimsingi watu wengi wa mji au taifa wanapomgeukia Mungu na kuomba rehema zake kwa toba na kuacha njia yao mbaya Mungu huwarehemu watu hao ona 

Yona 3:11-10 “Neno la Bwana likamjia Yona mara ya pili, kusema, Ondoka, uende Ninawi, mji ule mkubwa; ukaihubiri habari nitakayokuamuru. Basi Yona akaondoka, akaenda Ninawi, kama Bwana alivyonena. Basi Ninawi ulikuwa mji mkubwa mno, ukubwa wake mwendo wa siku tatu. Yona akaanza kuuingia mji mwendo wa siku moja, akapaza sauti yake, akasema, Baada ya siku arobaini Ninawi utaangamizwa. Basi watu wa Ninawi wakamsadiki Mungu; wakatangaza kufunga, wakajivika nguo za magunia, tangu yeye aliye mkubwa hata aliye mdogo. Habari ikamfikia mfalme wa Ninawi, naye akaondoka katika kiti chake cha enzi, akavua vazi lake, akajivika nguo za magunia, na kuketi katika majivu. Naye akapiga mbiu, akatangaza habari katika mji wa Ninawi, kwa amri ya mfalme na wakuu wake; kusema, Mwanadamu asionje kitu, wala mnyama wala makundi ya ng'ombe, wala makundi ya kondoo; wasile, wala wasinywe maji; bali na wafunikwe nguo za magunia, mwanadamu na mnyama pia, nao wakamlilie Mungu kwa nguvu, naam, na wageuke, kila mtu akaache njia yake mbaya, na udhalimu ulio mikononi mwake. Ni nani ajuaye kwamba Mungu hatageuka na kughairi, na kuiacha hasira yake kali, ili msiangamizwe? Mungu akaona matendo yao, ya kuwa wameiacha njia yao mbaya. Basi Mungu akalighairi neno lile baya, ambalo alisema atawatenda; asilitende.” 


 Ni wazi kuwa Ninawi ulikuwa mji mkubwa yaani wenye watu wengi na waliishi maisha ya dhambi na dhambi hiyo ilifikia mstari wa kuwaletea mauti lakini walipogeuka na kutubu Mungu aliwasamehe na kifo kikaahirishwa kwao, hii ni ahadi ya Mungu kwa miji yoye, nchi zote na mataifa yote ya kuwa watu wafikilie toba na kuwa watu wakigeuka kuacha njia zao mbaya Rehema za Mungu zitakuwa juu ya watu hao ona 


2Nyakati 7:13-14 “Nikizifunga mbingu isiwe mvua, tena nikiamuru nzige kula nchi, au nikiwapelekea watu wangu tauni; ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha, na kuomba, na kunitafuta uso, na kuziacha njia zao mbaya; basi, nitasikia toka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao, na kuiponya nchi yao.” Kumbe basi yanapotokea majanga ya aina mbalimbali, na matukio yenye kuua watu wengi na matukio mengone ya asili yanayodhuru wanadamu na kuumiza wengi haimaanishi tu kuwa watu wale wanaweza kuwa waovu kuliko wale wanaobaki salama lakini kwa Mungu wakati wote matukio hayo yanakuwa ni wito wa toba kwa watu wote wapate kumgeukia Mungu ona 


Luka 13:1-5 “Na wakati uo huo walikuwapo watu waliompasha habari ya Wagalilaya wale ambao Pilato alichanganya damu yao na dhabihu zao. Akawajibu akawaambia, Je! Mwadhani ya kwamba Wagalilaya hao walikuwa wenye dhambi kuliko Wagalilaya wote, hata wakapatwa na mambo hayo? Nawaambia, Sivyo; lakini msipotubu, ninyi nyote mtaangamia vivyo hivyo. Au wale kumi na wanane, walioangukiwa na mnara huko Siloamu, ukawaua, mwadhani ya kwamba wao walikuwa wakosaji kuliko watu wote waliokaa Yerusalemu? Nawaambia, Sivyo; lakini msipotubu, ninyi nyote mtaangamia vivyo hivyo.” 


Kwahiyo hata yanapotokea majanga katika upande wa Mungu inabaki vilevile Mungu hafurahii kufa kwa wenye dhambi na angepeda wafikie toba lakini ni wazi kwetu kuwa yanapotokea majanga na kuchukua watu wengi, sisi tunaosalia hatuna budi kukaa katika toba na kuacha njia mbaya tukikumbuka kuwa wale walioangamia sio kuwa walikuwa wabaya kuliko sisi.                            

Heri wafu wafao katika Bwana !

Ufunuo 14:13 “Nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, Andika, Heri wafu wafao katika Bwana tangu sasa. Naam, asema Roho, wapate kupumzika baada ya taabu zao; kwa kuwa matendo yao yafuatana nao.”

Kifo ni jambo la kuhuzunisha sana lakini ni tamko la Mungu, kwa hiyo Mungu hawezi kuwa kinyume na neno lake kwa sababu hiyo kifo kitamchukua mtu awaye yote mwema au muovu, kwa wakati wake ambao Mungu ameukusudia chini ya Mbingu, Yesu alipokuwa duniani alidhihirisha kuwa anahuzunishwa na kufa mtu tena hata wale waliokuwa rafiki zake ona Yohana 11:35 “Yesu akalia machozi.” Yesu alilia kwa sababu alihuzunishwa na kifo cha mtu wa karibu na rafiki yake yaani maana yake anahuzunishwa na kila mtu anayemuamini na anayeishi maisha ya haki bila kujali mtu huyo amekufa katika umri wa namna gani. Lakini Maandiko yanaeleza kuwa Heri wafu wafao katika Bwana yaani bila kujali umri au miaka lakini kama mtu huyo amekufa akiwa na imani katima Mungu akiamini kuwa yesu ni Bwana mtu huyo ana Baraka kubwa sana na maandiko yanaonyesha kuwa anapata pumziko baada ya taabu

Kwa sili andiko hilo ni matokeo ya maonyo kwa watu waovu ambao maandiko yanaonyesha kuwa wao wanapokufa hawatakuwa na nafasi ya kupumzika na badala yake watapata taabu sana Ufunuo 14:11 “Na moshi wa maumivu yao hupanda juu hata milele na milele, wala hawana raha mchana wala usiku, hao wamsujuduo huyo mnyama na sanamu yake, na kila aipokeaye chapa ya jina lake.”


Maandiko hayo yanaonyesha kwa asili wale watakaokufa wakati wa dhiki kuu, na tofauti yake kati ya wale watakaokufa kwa imani na wale watakaokuwa wamemuabudu mpinga kristo, Lakini maandiko hayo kuwa katika muktadha wa nyakati za dhiki kuu, hayaachi uole ukweli ulio wazi wa hata sasa kwamba wale wanaomuamini Yesu watapata raha na wale wasiomuamini watapata taabu sana kwani hayo ni matokeo yanayotokea haraka sana mara mtu anapokufa na aina ya maisha aliyoishi huamua hatima ya maisha yake ya umilele mara moja baada ya kufa ona Waebrania 9:27 “Na kama vile watu wanavyowekewa kufa mara moja, na baada ya kufa hukumu;” Maandiko ynaonyesha wazi kuwa mara baada ya kufa hukumu hujitokeza pale pale kwa aidha kwenda katika raha au kwenda katika mateso mtu aliyemuamini Bwana Yesu anasamehewa na kuwanywa kuwa kiumbe kipya 2Wakoritho 5:17 “Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya.” Watu hawa ambao neema ya Mungu imefunuliwa kwao watapata raha nafsini mwao kama maandiko yasemavyo Mathayo 11:28-29. Kwa hiyo anapokufa mtu mcha Mungu Mungu hufurahia anahuzunika anapoona wale walioko duniani wanalia na wanahuzunika na huhuzunika pamoja nao lakini mtu wa Mungu anapokufa kuna faidha kubwa sana na Mungu hufurahia mauti yake maandiko yanatuambia ina thamani kama nini mauti ya wacha Mungu wake ona Zaburi 116:15 “Ina thamani machoni pa Bwana Mauti ya wacha Mungu wake.” Haijalishi mtu wa Mungu atakufa katika mazingira ya aijna gani vyovyote vile kama Mungu ameruhusu mauti hiyo ina thamani kubwa sana mbele za Mungu aliyekuwa Askofu wa Antiokia aliuawa wakati wa mateso ya Decian askofu huyu ambaye katika historia ya kanisa aliitwa Babylas alikufa akiwa anaimba zaburi hii ina thamani machoni pa Bwana Mauti ya wacha Mungu wake!, Mtume Paulo aliungana na wazo kama hili kuhusu mauti ya mtu wa Mungu yeye alihesabu hivi kwake yaani kwa mtu kama yeye kuishi ni Kristo na kufa ni faida ona 


Wafilipi 1:21-24 21.Kwa maana kwangu mimi kuishi ni Kristo, na kufa ni faida. Ila ikiwa kuishi katika mwili, kwangu mimi ni matunda ya kazi; basi nitakalolichagua silitambui. Ninasongwa katikati ya mambo mawili; ninatamani kwenda zangu nikae na Kristo maana ni vizuri zaidi sana; bali kudumu katika mwili kwahitajiwa zaidi kwa ajili yenu” kumbe basi kufa katika imani kwa mtu wa Mungu na kwa watu wema ni busara ya Mungu ambaye anakwenda kuwapumzisha na kukaa pamoja na wao, bila kujali ni mazingira gani anakuchukua nani katika umri gani anakuchukua kwa msingi huo kwa uelewa mwembamba kifo ni kupoteza katika akili za kibinadamu na hasa anapokufa mtu mwema lakini kwa uelewa mpana kifo cha mtu mwema kina thamani kubwa sana kwa Mungu, Mara kadhaa wakati mwingine nimeshangazwa na Kocha wa mpira wa miguu anaweza kumtoa mtu ambaye amefunga magoli mengi siku hiyo au mwenye uchu wa kufunga zaidi, na ukatamani aendelee kucheza kwa vile unakuwa na matumaini naye lakini unashangaa kocha anamtoa! Unaweza kumtukana au kumlaumu lakini kwa nini anatolewa kocha ndiye anayejua Katika Biblia kama kuna mtu binafsi nisingelipenda Mungu amchukue Mapema ni Stefano mimi nahizi kuwa angakuwa muhubiri mkubwa na alikuwa ni mtu muhimu, mitume walimtegemea sana na alikuwa na uwezo wa juu sana kulitetea kanisa lakini Mungu kama Mungu aliruhusu Stefano auawe kwa kupigwa mawe na kuwa mtu wa kwanza kuifia Imani, hivyo wakati mwingine Mungu hufanya mambo kama apendavyo yeye na hata hivyo wanatheolojia wanajua faida ya kifo cha Stefano lakini pia tunaijua Furaha ya Yesu aliyesimama kumpokea Stefano!

Je mtu akifa ni kweli kuwa siku yake imefika?

Tumewasikia watu mara kadhaa wakisema mara baada ya mtu kufa kuwa siku yake imefika, au amemaliza kazi iliyokusudiwa au siku yako ikifika bwana hakuna cha kuzia na kadhalika na kadhalika je Mungu amekusudia mwanadamu awe na wakati Fulani muafaka wa kuishi? Je kuna uwezekano wa siku kufupizwa au kuongezwa na nini faida zake na makusudi yake? Maandiko yanatufundisha wazi kuwa kwaajili ya dhambi umri wa kuishi mwanadamu umefupizwa ona Mwanzo 6:1-3 “Ikawa wanadamu walipoanza kuzidi usoni pa nchi na wana wa kike walizaliwa kwao, wana wa Mungu waliwaona hao binti za wanadamu ya kuwa ni wazuri; wakajitwalia wake wo wote waliowachagua. BWANA akasema, Roho yangu haitashindana na mwanadamu milele, kwa kuwa yeye naye ni nyama; basi siku zake zitakuwa miaka mia na ishirini.              


Mwanzoni wanadamu waliweza kuishi hata karne 9 yaani miaka mia tisa na kitu na mwanadamu aliyepata kuishi miaka mingi zaidi aliitwa Methusela yeye aliishi miaka 969 katika rekodi za Biblia ona Mwanzo 5:27 “Siku zote za Methusela ni miaka mia kenda na sitini na kenda, akafa.” Kutokana na kuongezeka kwa maasi duniani Mungu aliipunguza miaka ya kuishi mwanadamu na kuwa 120 kama tuonavyo katika maandiko, hivyo 120 ndio kiwango cha wastani wa juu zaidi ambao mwanadamu anaweza kuishi, Wakati wana wa Israel wakiwa Jangwani kutokana na kuasi kwao mara kwa mara Mungu aliwapunguzia wao wana wa Israel Miaka ya kuishi hususani wale walikuwa jangwani wakati wa Musa na miaka yao ikakadiriwa kuwa kati ya 70-80 ona Zaburi 90:10 “Siku za miaka yetu ni miaka sabini, Na ikiwa tuna nguvu miaka themanini; Na kiburi chake ni taabu na ubatili, Maana chapita upesi tukatokomea mara.” Musa aliyasema maneno hayo wakati wa hukumu ya wana wa Israel ambao walikuwa wanakufa jangwani kwa sababu ya kutokumuamini Mungu, lakini kibiblia swala la msingi linabakia kuwa wastani wa mwanadamu kuishi ni kati ya miaka “70-120” hata hivyo hii haimaanishi kuwa ni lazima mwanadamu afiikishe miaka hiyo au kwamba anayekufa chini ya umri huo ni muovu hapana hata kidogo bado maisha ya mwanadamu yanabaki kuwa katika mipaka aliyoiweka Mungu! Kama itafikiriwa kuwa mtu akifa chini ya umri huo amekufa kijana basin i vema kuyafikiri maisha ya Yesu ambaye alipokuwa duniani aliishi miaka 33 tu, au kufikiri maisha ya Nabii Yohana mbatizaji ambaye aliishi miaka 30 tu na akauaawa! Ni Mungu tu ndiye anayejua kwanini na lini kifo kitokee kwa mtu kwa sababu zake mwenyewe, siku za mwanadamu za kuishi kwa ujumla sio nyingi kama hata kama mtu ataishi 120 bado ni siku zenye kupita haraka mno. Kwa mujibu wa maandiko 

Ayubu 14:1-2 “Mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke Siku zake za kuishi si nyingi, naye hujaa taabu. Yeye huchanua kama vile ua, kisha hukatwa; Hukimbia kama kivuli, wala hakai kamwe” mwandishi mwingine wa Biblia anayafananisha maisha ya mwanadamu kama vile maua, maua na majani ndio mfano wa vitu vyenye muda mfuoi sana wa kuishi, ni kama wanasema muda tuliopewa ni mdogo sana ona 

Zaburi 103:15 “Mwanadamu siku zake zi kama majani; Kama ua la kondeni ndivyo asitawivyo.” Pia maisha ya mwanadamu yanafananishwa na kivuli yaani kitu kinachopita na kutoweka kwa haraka sana Zaburi 144:4 “Binadamu amefanana na ubatili, Siku zake ni kama kivuli kipitacho.” 

Katika namna ya kibinadamu wengi tunaweza kufikiri kuwa maisha ya duniani ni matamu sana lakini kwa Mungu katika uwepo wake ndio kuzuri zaidi, Mungu amepangilia na kuweka mipaka katika maisha ya mwanadamu kwamba ukifika wakati huo aliouweka mwanadamu ataondoka tu kwa sababu siku zake zimeamriwa zimeratibiwa ziko programed kwamba huyu zitakuwa hizi tu 


Ayubu 14:5 “Kwa kuwa siku zake zimeamriwa, hesabu ya miezi yake unayo wewe, Nawe umemwekea mipaka yake asiyoweza kuipita;kwa hiyo iko wazi kuwa Mungu ameweka mpaka katika maisha yetu ambao huo hatuwezi kuuvuka iwe tuna pesa kiasi gani, wema kiasi gani na kadhalika aidha pia Mungu huweza kuitimiza ile iliyokusudiwa au kuipunguza maika iliyokusudiwa kwa wanadamu kwa sababu zake na kanuni zake mfano 


Kutoka 23:25-26 “Nanyi mtamtumikia BWANA, Mungu wenu, naye atakibarikia chakula chako, na maji yako; nami nitakuondolea ugonjwa kati yako. Hapatakuwa na mwenye kuharibu mimba, wala aliye tasa, katika nchi yako; na hesabu ya siku zako nitaitimiza.” Aidha Mungu anaweza kuhakikisha kuwa miaka iliyokusudiwa kwa mtu inatimizwa au anaweza kuiongeza lakini pia anaweza kuipunguza kutokana na kanuni mbalimbali za maisha na neno lake mfano Mithali 10:27 “Kumcha Bwana kwaongeza siku za mtu; Bali miaka yao wasio haki itapunguzwa.         


Kila mwanadamu anatamani sana kuishi muda mrefu sana lakini wakati mwingine Mungu hutuepusha na mambo kadhaa na dhiki au mambo mabaya ambayo yeye hangependa ukumbane nayo Hezekia alikuwa moja ya wafalme wazuri ambaye Mungu alitaka kumchukua mapema lakini aliomba Mungu amuongezee muda wa kuishi na Mungu alimuongezea muda wa miaka 15 2Wafalme 20:1-6 “Siku hizo Hezekia akaugua, akawa katika hatari ya kufa. Isaya, nabii, mwana wa Amozi, akamjia akamwambia, Bwana asema hivi, Tengeza mambo ya nyumba yako; maana utakufa, wala hutapona. Basi Hezekia akajigeuza, akaelekeza uso wake ukutani, akamwomba Bwana akasema,Nakusihi, Bwana, ukumbuke sasa, jinsi nilivyokwenda mbele zako katika kweli na kwa moyo mkamilifu, na kutenda yaliyo mema machoni pako. Hezekia akalia sana sana. Ikawa, kabla Isaya hajatoka katika mji wa kati, neno la Bwana likamjia, kusema, Rudi, ukamwambie Hezekia, mkuu wa watu wangu, Bwana, Mungu wa Daudi baba yako asema hivi, Nimeyasikia maombi yako, na kuyaona machozi yako; tazama, nitakuponya; siku ya tatu utapanda nyumbani kwa Bwana. Tena, nitazizidisha siku zako, kiasi cha miaka kumi na mitano, nami nitakuokoa wewe, na mji huu, na mkono wa mfalme wa Ashuru, nami nitaulinda mji huu kwa ajili yangu, na kwa ajili ya Daudi, mtumishi wangu.” 


Hata hivyo jambo la kushangaza ni kuwa baada ya miaka hiyo ya nyongeza Hezekia alipata mtoto na ambaye aliwaongoza watu kufanya mambo mabaya sana na kufanya machukizo mabaya zaidi ambayo hata baba yake angalikuwa hai asingeliweza kuyavumilia mauozo hayo ona 2Wafalme 21:9 “Walakini hawakusikia; naye Manase akawakosesha wafanye mabaya, kuliko mataifa Bwana aliowaharibu mbele za wana wa Israeli.” 

Ni kama kusema afadhali Hezekia angelikubali kwenda kwa bwana wakati wake ulipofika kuliko miaka aliyoongezwa. Wakati mwingine Mungu katika hekima yake hufanya mambo kwa manufaa makubwa sana anayoyajua mwenyewe kwaajili ya hayo ni vigumu kumuuliza Mungu kwanini, kwanini hili litokee, lakini tunapaswa kumshukuru Mungu kwa kila jambo na kutokumkufuru Mungu linapofanyika tukio lenmye kushangaza tuendelee kumuamini yeye katika njia zake zote na tusizitegemee akili zetu wenyewe 

Mithali 3:5-6 “Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote, Wala usizitegemee akili zako mwenyewe; Katika njia zako zote mkiri yeye, Naye atayanyosha mapito yako.” Wakati mwingine Mungu anaweza kumchukua mtu mwema akapumzike nyumbani kwa kusudi la kumuepusha na machukizo ya aina Fulani bila kujali njia itakayotumika kwa kuondoka kwake, 


Isaya 57:1 “Mwenye haki hupotea, wala hakuna atiaye hayo moyoni; na watu watauwa huondolewa, wala hakuna afikiriye ya kuwa mwenye haki ameondolewa asipatikane na mabaya.” Mungu anaweza kumchukua mtu ili kumuepusha na mabaya au maumivu makali au ulemavu, au kupooza na maswala mengine mengi,Jambo kubwa la msingi ni kila mmoja kuwa tayari kwa kifo wakati wowote tangu siku unapozaliwa Hata hivyo Yesu Ndiye mwenye funguo yaani mamlaka na kifo na hivyo hutaweza kuondoka mpaka Mungu ameruhusu Shetania anaweza kutujaribu kwa kiwangochochote kile lakini hana ruhusa kuondoa uhai wetu mpaka Mungu mwenyewe afanye hivyo 


Ayubu 2:6 “Bwana akamwambia Shetani, Tazama, yeye yumo mkononi mwako; lakini tunza tu uhai wake” Ufunuo 1:17-18 “Nami nilipomwona, nalianguka miguuni pake kama mtu aliyekufa. Akaweka mkono wake wa kuume juu yangu, akisema, Usiogope, Mimi ni wa kwanza na wa mwisho, na aliye hai; nami nalikuwa nimekufa, na tazama, ni hai hata milele na milele. Nami ninazo funguo za mauti, na za kuzimu.”        

Adui wa mwishio atakayeangamizwa ni kifo:

1Wakoritho 15:26  Adui wa mwisho atakayebatilishwa ni mautiHatimaye Yesu Kristo ambaye ana mamlaka dhidi ya kifo na mauti na ambaye alionja mauti ya msalabani na kuishinda kwa kufufuka siku ya tatu mwisho wa dahari atambatilisha adui huyu ambaye amekuwa akisumbua kili zetu na kutuchukulia wapendwa wetu na kutuondolea tumaini duniani na kutufanya tuione dunia kuwa haina maana na ni batili na kutukatisha tamaa na kutufanya tuishi kwa hofu,  habari njema ni kuwa Mungu ataibatilisha mauti yaani kifo na hakitakuwepo tena mjadala wake utafungwa na Mungu mwenyewe kwa kutupa uzima wa milele na kujibu maswali yote ya msingi kuhusu Kifo, kwa sasa kifo ni siri ya ajabu, na Mungu ndiye aijuaye.

Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima!


Ijumaa, 5 Machi 2021

Kumbuka aliyokufanya Amaleki !


Kumbukumbu 25:17-19 Kumbuka aliyokufanya Amaleki katika njia mlipokuwa mkitoka Misri; jinsi alivyokukuta katika njia, akapiga katika watu wako walioachwa nyuma, wote waliokuwa wanyonge nyuma yako, ulipokuwa umechoka na kuzimia; wala asimche Mungu. Basi itakuwa, hapo atakapokwisha kukupumzisha Bwana, Mungu wako, katika adui zako wote walio kando-kando, katika nchi akupayo Bwana, Mungu wako, iwe urithi uimiliki, ndipo uufute ukumbuko wa Amaleki chini ya mbingu; usisahau.”


Utangulizi:

Moja ya matukio mabaya sana ambayo Israel walitakiwa kuyakumbuka Daima ni pamoja na ukatili mkubwa waliofanyiwa na wana wa amaleki (Amaleki). Musa analikumbuka sana tukio hili baya na la kinyama na anawaandikia Israel na kumkumbusha Joshua kutokulisahau tukio hili baya na la kinyama  lililopata kufanywa na Wamaleki!. Wana wa Israel walikuwa wamefanyiwa mambo ya kikatili sana katika nchi ya Misri, waliteswa na kutumikishwa katika utumwa mkubwa na mzito kwa muda wa zaidi ya miaka 400, waliugua na kulia na kibinadamu haingekuwa rahisi mtu awaye yote kuwaondoa katika utumwa huo mzito isipokuwa tu pale ambapo Mungu alikuja kuingilia kati unawezakuona.


Kutoka 3;7-10 BWANA akasema, Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri, nami nimekisikia kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao; maana nayajua maumivu yao; nami nimeshuka ili niwaokoe na mikono ya Wamisri, niwapandishe kutoka nchi ile, hata nchi njema, kisha pana; nchi ijaayo maziwa na asali; hata mahali pa Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi.Basi, tazama, kilio cha wana wa Israeli kimenifikilia; tena nimeyaona hayo mateso ambayo Wamisri wanawatesa. Haya, basi, nitakutuma sasa kwa Farao, ili upate kuwatoa watu wangu, hao wana wa Israeli, katika Misri.


Huu ndio ulikuwa mpango wa Mungu na mapenzi kamili ya Mungu, kwamba awakomboe wana wa Israel na kuwafikisha katika nchi ya mkanaani nchi iliyojawa maziwa na asali, aweze kuwafariji na kuwafundisha mapenzi yake ili kwamba kupitia wao jamaa zote za dunia zipate kubarikiwa kupitia mwana wake mpendwa Yesu Kristo ambaye kinabii angetokea Israel na kuwa ishara ya kuaminiwa duniani kote, kwa hiyo Taifa hili lilikuwa limebeba mpango na mapenzi kamili ya Mungu, Mungu aliwapitisha katika jangwa hili zito na la kutisha apate kuwafundisha imani na kumtegemea yeye ili wawe watu wake Lakini wakiwa njiani pamoja na vikwazo vingi walivyokuwa wamekutana navyo walitokewa kabila hili la jangwani waliojulikana kama Amaleki watu hawa walifanya vita na Israel, Kitabu cha kutoka kimetuficha sababu ya vita hii kinaeleza tu walivyotokea na kupigana na Israel na Yoshua akatumwa kuwapiga kwa msaada wa maombi ya Musa unawezakuona katika

Aliyoyafanya Amaleki:-

Kutoka 17:8-14 Wakati huo Waamaleki wakatokea, wakapigana na Israeli huko Refidimu. Musa akamwambia Yoshua, Tuchagulie watu, ukatoke upigane na Waamaleki; kesho nitasimama juu ya kilele kile, na ile fimbo ya Mungu nitakuwa nayo mkononi mwangu. Basi Yoshua akafanya kama Musa alivyomwambia, akapigana na Amaleki; na Musa na Haruni na Huri wakapanda juu ya kile kilima. Ikawa, Musa alipouinua mkono wake, Israeli walishinda; na alipoushusha mkono wake, Amaleki walishinda. Lakini mikono ya Musa ilikuwa mizito; basi wakatwaa jiwe, wakaliweka chini yake akalikalia. Haruni na Huri wakaitegemeza mikono yake, mmoja upande huu na mmoja upande huu; mikono yake ikathibitika hata jua lilipokuchwa. Yoshua akawaangamiza Amaleki na watu wake kwa ukali wa upanga. BWANA akamwambia Musa, Andika habari hii katika kitabu iwe ukumbusho, kisha ihubiri masikioni mwa Yoshua; ya kuwa nitaufuta ukumbusho wa Amaleki kabisa, usiwe tena

Mungu anakasirishwa sana na tendo la Amaleki kushindana na Israel na akaagiza kuwa Musa ni lazima alihubiri jambo hili kwa Yoshua na  wana wa Israel walikumbuke tukio hili milele, aliambiwa aliweke tukio hili katika kitabu cha kumbukumbu ukumbusho kuwa kizazi cha Amaleki kitashughulikiwa siku zote mpaka kifutike kabisa duniani, sababu kubwa ni kuwa kilikuwa kizazi cha watu katili sana hawakuwa na huruma hawakuwaonea huruma watu waliotoka katika mateso kwa muda mrefu sana waliotakiwa kuhurumiwa waliostahili kuhurumiwa  na waliokuwa wanahitaji msaada, watu waliokuwa wanahitaji msaada na huruma na huduma na kutiwa moyo na msaada wa kibinadamu ambao Mungu alikuwa amefungua mlango kuwatoa katika mateso amaleki walikosa utu kabisa hawakuwahurumia watu ambao walistahili kibinadamu kuhurumiwa, hawakuwahurumia wanyonge, hawakuwahurumia watu waliokuwa wamechoka na kuzimia wala hawakumuhofu Mungu na kwa tukio hili Musa analiweka vizuri katika kitabu cha kumbukumbu la Torati kwamba Amaleki kwamba Israel walikuwa wamewaacha nyuma watu wanyonge wagonjwa na wenye uhitaji wa namna mbalimbali ili labda huenda wapate huduma za kitabibu, maji na huduma nyinginezo lakini Amaleki aliwapiga bila kujali ilihali wakijua kuwa ni watu wanaohitaji huduma na msaada wa kibinadamu ona.

Kumbukumbu 25:18. jinsi alivyokukuta katika njia, akapiga katika watu wako walioachwa nyuma, wote waliokuwa wanyonge nyuma yako, ulipokuwa umechoka na kuzimia; wala asimche Mungu

 Tukio hili halikuwa tukio lenye kuheshimu ubinadamu, watu wanapokuwa vitani sharia za kivita zinakataza kushambulia maeneo ya kiraia, lakini mbaya zaidi kushambulia hospitali au sehemu zinazotoa huduma za kijamii, wanawake watoto na raia, lakini sio hivyo tu wakati wa vita taifa lile linalopigana linapaswa kuhakikisha kuwa wanajali utu na ndio maana utaweza kuona baadhi ya mataifa wanapokuwa na vita na wananchi wakapata shida ya njaa huwa wanatoa msaada wa chakula na madawa, Katika ulimwengu huu ulio haribika ni dhambi kubwa sana kumuongezea mtu tatizo ilihali yeye mwenyewe ana tatizo au anatoka katika matataizo, kwaajili ya shida zetu, wamekuwepo watu katika jamii ambao matendo yao ni kama waamaleki, badala ya kuwasaidia watu wanyonge wenyewe wamekuwa kikwazo kikubwa sana  kwa watu hao wanyonge, mtu ni mgonjwa anahitaji msaada ana matatizo wanaweza kuwako hata wahubiri au watoa huduma kama hospitalini ambao watadai fedha kutokana na huduma wanayoitoa, mtu anaweza kuwa mlemavu lakini watu wakamuhuzunisha na kumjeruhi roho yake kwa kumuongezea masimango, mtu anaweza kuwa mjamzito akakutana na huduma na maneno ya kukatisha tamaa huko leba wanakojifungulia, mtu anaweza kuwa yatima watu wakawatumia yatima hao kwa manufaa yao, mtu anaweza kuwa mlemavu, kipofu au mwenye ualbino na watu wakawatumia hao kwa manufaa yao wenyewe, mtu anaweza kuwa mjane  anahitaji msaada lakini ujane wake ukatumika kwa manufaa ya wengine, ukatili wa kijinsia, uonevu kwa wanyonge kutokujali, kukosa utu na lugha mbovu sehemu za huduma ni maswala ambayo yanaweza kufanywa na watu ambao wanaweka kwazo kama walivyo Amaleki ambao kwa makusudi kabisa walishindana na kusudi la Mungu la kuwapeleka watu katika nchi ya mkanaani lakini pia kwa kuwaonea wanyinge, jambo hili linahifadhiwa katika kumbukumbu za Mungu na ndipo Mungu hujitakia kisasi, na kuwa na vita na jamii ya watu hao milele, dhuluma na uonevu unawekwa katika kumbukumbu za Mungu na ni lazima vilipiwe ni kwaajili ya haya miaka mingi baadaye Mungu alimtaka mfalme Sauli kuwafutilia mbali Amaleki kwa sababu ya uovu wao lakini hata hivyo Mfalme Sauli alimuudhi sana Mungu kwa sababu alishindwa kuyatii maneno ya Musa mtumishi wake na agizo la Mungu na mapenzi yake ya kutaka kujilipizia kisasi dhidi ya Amaleki

Muhukumu wa ulimwengu lazima atende haki;-

1Samuel 15:1-19 Wakati huo Samweli akamwambia Sauli, Bwana alinipeleka nikutie mafuta, uwe mfalme wa watu wake Israeli; basi sasa, isikilize sauti na maneno ya Bwana. Bwana wa majeshi asema hivi, Nimeyatia moyoni mwangu mambo hayo Amaleki waliyowatenda Israeli, jinsi walivyowapinga njiani, hapo walipopanda kutoka Misri. Basi sasa enda ukawapige Amaleki, na kuviharibu kabisa vitu vyote walivyo navyo, wala msiwaachilie; bali waueni, mwanamume na mwanamke, mtoto naye anyonyaye, ng'ombe na kondoo, ngamia na punda. Ndipo Sauli akawaita watu, akawahesabu huko Telemu, askari waliopanda farasi mia mbili elfu, na watu wa Yuda kumi elfu.  Sauli akaufikilia mji wa Amaleki, akauvizia bondeni. Sauli akawaambia Wakeni, Haya! Enendeni zenu, mkashuke ili kujitenga na Waamaleki, nisije nikawaangamiza ninyi pamoja nao; maana mliwatendea wana wa Israeli mema, walipopanda kutoka Misri. Basi hao Wakeni wakaondoka, wakajitenga na Waamaleki. Sauli akawapiga Waamaleki, toka Havila uendapo Shuri, unaokabili Misri. Akamkamata Agagi, mfalme wa Waamaleki, yu hai, akawaangamiza hao watu wote kwa upanga. Lakini Sauli na watu wake wakamwacha Agagi hai, na katika kondoo walio wazuri, na ng'ombe, na vinono, na wana-kondoo, na cho chote kilicho chema, wala hawakukubali kuwaangamiza; bali cho chote kilichokuwa kibaya na kibovu, ndicho walichokiangamiza kabisa. Ndipo neno la Bwana likamjia Samweli, kusema, Najuta kwa sababu nimemtawaza Sauli awe mfalme; maana amerudi nyuma, asinifuate, wala hakufanya nilivyomwamuru. Samweli akasikitika, akamlilia Bwana usiku kucha. Samweli akaondoka asubuhi na mapema ili aonane na Sauli; Samweli akaambiwa ya kwamba, Sauli alifika Karmeli, na tazama, akajisimamishia ukumbusho, akageuka, akapita, akatelemkia Gilgali. Samweli akamwendea Sauli; naye Sauli akamwambia, Ubarikiwe na Bwana, nimeitimiza amri ya Bwana. Samweli akasema, Maana yake nini, basi, hiki kilio cha kondoo masikioni mwangu, na huu mlio wa ng'ombe ninaousikia? Sauli akasema, Wamewaleta kutoka kwa Waamaleki; maana watu waliwaacha hai kondoo na ng'ombe walio wazuri, ili wawatoe dhabihu kwa Bwana, Mungu wako, nao waliosalia tumewaangamiza kabisa. Ndipo Samweli akamwambia Sauli, Ngoja, nami nitakuambia neno aliloniambia Bwana usiku huu. Naye akamwambia, Haya, sema. Basi Samweli akasema, Ingawa ulikuwa mdogo machoni pako mwenyewe, je! Hukufanywa kuwa kichwa cha kabila za Israeli? Naye Bwana akakutia mafuta uwe mfalme wa Israeli. Kisha Bwana akakutuma safarini, akasema, Enenda ukawaangamize kabisa wale Waamaleki wenye dhambi, upigane nao hata watakapoangamia. Mbona, basi, hukuitii sauti ya Bwana, bali ukazirukia nyara ukafanya yaliyo maovu machoni pa Bwana?

Onyo kwa watu wenye dhukluma:-

Kuwatumiwa wanyonge kwa manufaa yakio mwenyewe ni dhambi kubwa sana, Mungu anachukizwa na udhalimu wa kila namna maandiko yanasema wala wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu, Kitendo cha waameleki kuwazuia Israel wasiende kulitimiza kusudl la Mungu kilikuwa ni kitendo cha kutokujali mpangio wa Mungu, laziki tendo la kuwaonea watu wanyonge na kuwatendea uahlifu liliwekwa katika kumbukumbu za Mungu, lakini tendo la kuwahurumia amaleki na kutiokuangamiza au kumlipizia Bwana kisasi sawasawa na neno lake kulikofanywa na Sauli kulimuudhi sana Mungu, Maana yake ni kuwa Mungu hatakubali mtu awaye yote aliye mnyonge na mnyenyekevu aonewe kupita kawaida, ni lazima ataliweka jambo hilo katika kumbukumbu na kujitakia kisasi milele,

Warumi 12:19 Wapenzi, msijilipize kisasi, bali ipisheni ghadhabu ya Mungu; maana imeandikwa, Kisasi ni juu yangu mimi; mimi nitalipa, anena Bwana.”

Mungu alitunza uovu wa wana wa Amekeli na alikusudia kujilipizia kisasi, na ole wake mtu yule ambaye atawaacha waameleki, Dhambi yao ilikuwa kubwa , walikuwa waonevu, walikuwa wenye dhuluma, walikuwa wasiojali utu, waliwaonea wanyinge, walishindana na kusudi la Mungu, kuna mambo unaweza kuyafanya kuna ukatili unaweza kuufanya lakini sio kwa watu wanyonge ambao maisha yao yalikuwa ya taabu na Mungu aliwasaidia dhidi ya wamisri,  watu waliohitaji huruma kufarijiwa kuinuliwa na kutiwa moyo, Mungu asingeliweza kupuuzia hata kidogo, Lazima atawangalia wanyonge

Isaya 66:2 Maana mkono wangu ndio uliofanya hivi vyote, vitu hivi vyote vikapata kutokea, asema Bwana; lakini mtu huyu ndiye nitakayemwangalia, mtu aliye mnyonge, mwenye roho iliyopondeka, atetemekaye asikiapo neno langu.”

Mungu ni lazima atatenda haki Mwanzo 18:25b ………. "Hasha: Mhukumu ulimwengu wote asitende haki?

Mungu atakulipa endapo unaonewa kwa haki na kudhukumiwa hebu mlilie Mungu lalama mbele zake omba na kuliitia jina lake na kisha utaona ukuu wa Mungu katika maisha yako, wale wanaoowatumia wanyionge kwa manufaa yao tubu na achana na unevu wa kila namna Mungu asije akakuhukumu!

Rev. Innocent Kamote
Mkuu wa wajenzi Mwenye Hekima