Jumapili, 10 Julai 2016

Ujumbe: Watu huninena mimi kuwa ni nani?


Marko 8:27-30 “27. Akatoka Yesu na wanafunzi wake, wakaenda kwenye vijiji vya Kaisaria-Filipi; na njiani akawauliza wanafunzi wake, akasema, Watu huninena mimi kuwa ni nani? 28. Wakamjibu, Yohana Mbatizaji; wengine, Eliya; wengine, Mmojawapo wa manabii. 29. Naye akawauliza, Na ninyi mnasema ya kuwa mimi ni nani? Petro akamjibu, akamwambia, Wewe ndiwe Kristo. 30. Akawaonya wasimwambie mtu habari zake.”



Utangulizi:

Wengi wetu huwa kuna mahali tumeanzia tunapotaka kujifunza kitu au jambo Fulani, Leo tunataka kujifunza kwa kina kuhusu Yesu Kristo, tunaweza iujifunza habari za Yesu katika namna ileile ambayo tunajifunza habari za watu wengine, tutajibu swali Watu huninena mimi kuwa ni nani? Kwa kusudi la kumfahamu Yesu Kristo, Tutajifunza somo hili kwa kuzingatia vipengele vitatu vifuatavyo:-

Ushahidi wa kutoka kwa wanadamu kuhusu Yesu Kristo
Ushahidi wa kutoka kwa Malaika kuhusu Yesu Kristo
Ushahidi wa kutoka kwa Yesu Kristo

Ushahidi wa kutoka kwa wanadamu kuhusu Yesu Kristo

1.      Matha Yohana 11:27
2.      Petrer Mathayo 16:16; 2Peter 1:16-17
3.      Yohana Yohana 1:1-3, Yohana 1:14, IYohana 1:1-2, Yohana 20:30-31
4.      Thomas Yohana 20:28
5.      Ndugu zake Yohana 7:5; 1Wakoritho 15:7, Wagalatia 1:19, Yakobo 1:1 Yuda 1
6.      Mama yake Matendo 1:14

Ushahidi wa kutoka kwa Malaika Kuhusu Yesu Kristo

1.      Kundi la malaika Luka 2:11
2.      Gabriel Luka 1:32
3.      Kutoka kwa Baba yake  “Huyu ni Mwanangu Mpendwa”Luka 1:32. Mathayo 17:5 na Matendo 2:22

Ushahidi wa kutoka kwa Yesu Kristo Mwenyewe

1.      Mimi ni njia na kweli na uzima Yohana 14;16
2.      Mimi ndio Ufufuo na uzima Yohana 11:25
3.      Kabla Ibrahimu ahajakuwako mimi niko Yohana 8:58

Hitimisho:
1.      Basi Yesu sio mwanadamu wa Kawaida
2.      Yesu sio Mzushi
3.      Yesu sio Muongo
4.      Yesu ni mwana wa Mungu
5.      Yesu ni Mungu na Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima!

Hakuna maoni: