Alhamisi, 21 Julai 2016

Ujumbe: Kustahimili Mapingamizi makuu


Waebrania 12:3
Maana mtafakarini sana yeye aliyeyastahimili mapingamizi makuu namna hii ya watendao dhambi juu ya nafsi zao, msije mkachoka, mkizimia mioyoni mwenu”.

Ulimwengu huu ni ulimwengu wa mapingamizi, ni ulimwengu ambao kadiri kunavyokucha vipingamizi vya aina mbalimbali, Yesu aliweza kuyashinda mapingamizi nyote na ndio maana mwandishi wa kitabu cha Waebrania anataka tumtafakari sana Yesu ambaye alishinda mapingamizi makuu sana 

 "Dhoruba Katika Maisha zisikubabaishe na kukusumbua Yesu alizishinda mtafakari yeye"

Ulimwengu huu tulionao ni ulimwengu ambao unazidi kuwa wenye kutisha siku hadi siku na watu wanapoteza matumaini kabisa  Jonathan Park alitunga shairi hili kuuzungumzia ulimwengu huu na kusema 

·         Ni ulimwengu ambao mtu Fulani mahali Fulani amepoteza tumaini
·         Ni ulimwengu ambao mtu fulani mahali Fulani Ndugu kwa ndigu wanauana
·         Ni ulimwengu ambao mtu Fulani mahali Fulani anauawa kwaajili ya ngozi ya ragi yake
·         Ni ulimwengu ambao mtu Fulani mahali fulanmi anaona Fedha ni za muhimu kuliko imani, familia na marafiki
·         Ni ulimwengu ambao mahali Fulani serikali inatumia nguvu zake kuwatendea mabaya raia wake
·         Ni ulimwengu ambao mahali Fulani hawaruhusiwi hawaruhusiwi kuabudu Mungu au imani uitakayo
·         Ni ulimwengu ambao mahali Fulani mtu Fulani anamuua mwingine kwa jina la Allah
·         Ni ulimwengu ambao mahali Fulani mtu Fulani anamuua mwingine kwa jila la Mungu
·         Ni ulimwengu ambao mahali Fulani sehemu Fulani huwezi kutembea bila milio ya risasi kusikika
·         Ni ulimwengu ambao mahali Fulani mtu Fulani anakimbia nchi yake kutafuta maisha
·         Ni ulimwengu ambao mahali Fulani mtu Fulani anakimbia nchi yake na anakumbana na kifo
·         Ni ulimwengu ambao mahali Fulani baba anamtandika mtoto wake mpaka hawezi kutembea
·         Ni ulimwengu ambao mahali Fulani mama anamtupa mtoto wake wa kuzaa kwa vile eti hawezi kumtunza
·         Ni ulimwengu ambao maneno ya mtu au ahadi za mtu zimekuwa sio za muhimu tena
·         Ni ulimwengu ambao mwalimu anamwambia mwanafunzi huwezi kitu kabisa
·         Ni ulimwengu ambao watu wanasalitiana na marafiki wanakuwa maadui
·         Ni ulimwengu ambao vijana wanakata tamaa na kujiua
·         Ni ulimwengu ambao unakimbilia polisi au mahakamani upate haki unaishia kudhulumiwa
·         Ni ulimwengu ambao mtu Fulani anapatwa na mabaya wengine wanafurahi
·         Ni ulimwengu ambao unamwahisha mgonjwa hospitali ili kuokoa maisha yake anakufa kwa kukosa huduma za wahudumu wasio na haraka
·         Ni ulimwengu ambao mjomba anamuharibu mtoto wa dada yake mwenyewe kwa ulawiti
·         Ni ulimwengu ambao wanaume kwa wanaume wanaoana na wana wake kwa wanawake
·         Ni ulimwengu ambao watu hawaaminiani tena 

Hi jinsi gani tunaweza kustahimili hali hizi zote zenye kukatisha tamaa? 2 Timotheo 2:3, 8 Biblia inasema hivi “Ushiriki taabu pamoja name kama aksari mwema wa Kristo Yesu; Mkumbuke Yesu Kristo, aliyefufuka katika wafu, wa uzao wa Daudi kama inenavyo injili yangu”

Kwa nini maandiko yanatutaka tumtafakari Yesu tunapopitia mambo magumu  ni kwa sababu sehemu Fulani hapa ulimwenguni kuna tumaini tumaini hilo linapatikana kwa Yesu, kama sehemu moja ya ulimwengu ni Gisa sehemu ya pili kuna Nuru Yesu ni Nuru ya Ulimwengu  Yohana 1:5 “ Nayo Nuru yang’aa Gizani, wala giza halikuiweza, Yohana 12:46 “ Mimi nimekuja ili niwe Nuru ya ulimwengu, ili kila aniaminiye mimi asikae gizani”

Tukiyafikiria haya tunaweza kuzimia mioyoni mwetu, yaani tunaweza kukata tamaa na kuona kuwa ulimwengu umekuwa sio mahali salama tena pa kukalika lakini tukimtafakari sana Yesu ambaye alishindamap[ingamizi makuu namna hii, Hatutachoka wala kukata tamaa wala kuzimia moyo.

Hakuna maoni: