Jumapili, 25 Novemba 2018

Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba

Wafilipi 4:6-7 “Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu. Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu."
 
 Unapokuwa umemtegemea Mungu huna sababu ya kuogopa Yeye yu pamoja nawe Zaburi 118:6

Utangulizi:
Neno usijisumbue lilikuwa ni moja ya Misingi mikubwa katika Mafundisho ya Bwana Yesu Mathatyo 6:25, 34 zinasema “Kwa sababu hiyo nawaambieni, Msisumbukie maisha yenu, mle nini au mnywe nini; wala miili yenu, mvae nini. Maisha je! Si zaidi ya chakula, na mwili zaidi ya mavazi?, Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake.”

Msisumbuke!

Mungu katika mapenzi yake hataki sisi tusumbuke yaani tujiumize kwa mashaka na wasiwasi kama wasioamini, Usumbufu huu ni usumbufu wa Moyo uitwao “ANXIETY”ambalo maana yake ni kuogopa au kuhofia au kutetemeka kwaajili ya jambo fulani linalohuisiana na maisha, Kama tutafikiri kwa akili zetu za kibinadamu kwa jambo lolote gumu katika maisha yetu ni dhahiri kuwa tutazama katika masumbufu na mashaka , lakini kama tutamshirikisha Mungu ukweli wa kimaandiko ni kuwa tutakuwa juu ya mashaka yetu

Mithali 3:5-6 “.Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote, Wala usizitegemee akili zako mwenyewe; Katika njia zako zote mkiri yeye, Naye atayanyosha mapito yako.”

Watakatifu waliotutangulia walikuwa na ufahamu wa kutosha kuwa kila unapokutana na changamoto za aina yoyote hupaswi kujisumbua katika jambo lolote zaidi ya kuomba na kumshukuru Mungu yaani kumfanyia bwana ibada, Petro huenda alikuwa na ujuzi na uzoefu kuwa kila changamoto mitume waliweza kuikabili kwa maombi, walipofadhaika walimwambia Mungu,lakini sio hivyo tu bali hata manabii walipokuwa na changamoto waliweza kuomba Ndugu zango hata leo maombi ndio ufunguo wa kukomesha aina yoyote ya mashaka na wasiwasi, hofu na kuleta majibu ya maswali magumu katika masha yetu.

1. Tumtwike yeye fadhaa zetu zote 1Petro 5:6-7Basi nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake; huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu.” Mtume Petro alikuwa na ujuzi wa kutosha kuwa kila unapokutana na changamoto zozote unapaswa kumtwika Mungu swala hilo kisha kustarehe ku “relax” ni wazi kuwa mitume na watakatifu waliotutangulia walikuwa na uelewa huu wazi kuwa linapokuja swala linalosumbua moyo unalipeleka katika maombi kisha unaamini kuwa Mungu atashughulikia na ni kweli atalishughulikia! Unaona angalia walivyofanya walipokutana na changamoto hapa chini katika Matendo 4;24-31 waliomba na Mungu aliwatia nguvu.

2. Matendo 4:24-31Nao waliposikia, wakampazia Mungu sauti zao kwa moyo mmoja, wakisema, Mola, wewe ndiwe Mungu, ndiwe uliyefanya mbingu na nchi na bahari na vitu vyote vilivyomo; nawe ulinena kwa Roho Mtakatifu kwa kinywa cha babaetu Daudi, mtumishi wako, Mbona mataifa wamefanya ghasia, Na makabila wametafakari ubatili? Wafalme wa dunia wamejipanga, Na wakuu wamefanya shauri pamoja Juu ya Bwana na juu ya Kristo wake. Maana ni kweli, Herode na Pontio Pilato pamoja na Mataifa na watu wa Israeli, walikusanyika katika mji huu juu ya Mtumishi wako mtakatifu Yesu, uliyemtia mafuta, ili wafanye yote ambayo mkono wako na mashauri yako yamekusudia tangu zamani yatokee. Basi sasa, Bwana, yaangalie matisho yao; ukawajalie watumwa wako kunena neno lako kwa ujasiri wote, ukinyosha mkono wako kuponya; ishara na maajabu vifanyike kwa jina la Mtumishi wako mtakatifu Yesu. Hata walipokwisha kumwomba Mungu, mahali pale walipokusanyika pakatikiswa, wote wakajaa Roho Mtakatifu, wakanena neno la Mungu kwa ujasiri.”

3. Daniel 6:10Hata Danieli, alipojua ya kuwa yale maandiko yamekwisha kutiwa sahihi, akaingia nyumbani mwake, (na madirisha katika chumba chake yalikuwa yamefunguliwa kukabili Yerusalemu;) akapiga magoti mara tatu kila siku, akasali, akashukuru mbele za Mungu wake, kama alivyokuwa akifanya tokea hapo.” Unaweza kuona pia kwa Daniel ni wazi kuwa ni mapenzi ya Mungu kwamba tusijisumbue katika neno lolote, tusiogope lolote, tuombe Mungu hata kama swala hilo liko kinyume na serikali, liko kinyume na wafalme, madam liko kinyume na mapenzi ya Mungu wewe omba tu kisha Mungu atalijibu mtegemee yeye, relax kama mtu aliyeruka na parachute.

Ushindi wetu na uthabiti wetu uko katika maombi na kumtegemea Mungu na sio kuogopa, na Ukiisha kumuomba Mungu furahi na kutulia.

Na mkuu wa wajenzi mwenye Hekima
Rev. Innocent Kamote

Hakuna maoni: