Jumatano, 16 Novemba 2022

Jinsi ya kuwa Adui wa Roho Mtakatifu!


Isaya 63:9-10Katika mateso yao yote yeye aliteswa, na malaika wa uso wake akawaokoa; kwa mapenzi yake, na huruma zake, aliwakomboa mwenyewe; akawainua, akawachukua siku zote za kale. Lakini wakaasi, wakamhuzunisha Roho yake Mtakatifu; kwa hiyo akawageukia, akawa adui, akapigana nao.”


Utangulizi:

Ni muhimu kufahamu kuwa Mungu wetu ni mwingi wa rehema huruma na neema, Sifa za Mungu wetu kamwe haziwezi kulinganishwa na mwingine awaye yote, Musa alipotaka kumjua Mungu Mungu alijifunua kwake kwa sifa nzuri zenye kuwavutia sana wanadamu zinazoashiria kuwa Mungu ni mwema mno ona

Kutoka 34:6-7 “BWANA akapita mbele yake, akatangaza, BWANA, BWANA, Mungu mwingi wa huruma, mwenye fadhili, si mwepesi wa hasira, mwingi wa rehema na kweli; mwenye kuwaonea huruma watu elfu elfu, mwenye kusamehe uovu na makosa na dhambi; wala si mwenye kumhesabia mtu mwovu kuwa hana hatia kamwe; mwenye kuwapatiliza watoto uovu wa baba zao, na wana wa wana wao pia, hata kizazi cha tatu na cha nne.”  

Unaona tunamwabudu na kumtumikia Mungu mwenye huruma nyingi, mwenye fadhili, na si mwepesi wa Hasira mwingi wa rehema na kweli nani mwenye kuonea watu huruma hii ni sifa kubwa sana ya Mungu aliye baba na muumba kwetu sifa hii na tabia hii ya uungu iko kwa Mungu etu ambaye amejifunua kwetu kama Baba, mwana na Roho Mtakatifu, yeye ni mwingi wa huruma kama maandiko yanenavyo 

Zaburi 145:7-9 “Watalihubiri kumbukumbu la wema wako mkuu. Wataiimba haki yako. Bwana ana fadhili, ni mwingi wa huruma, Si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema, Bwana ni mwema kwa watu wote, Na rehema zake zi juu ya kazi zake zote.”

Hata hivyo pamoja na wingi huu wa rehema na neema na huruma za Mungu wetu, ni ukweli ulio wazi kwamba maandiko yanatuonya sana sana sana kutokumkosea ROHO MTAKATIFU Onyo hili limerudiwa tena na tena kama tahadhari kubwa sana katika maandiko ya kwamba katika maisha yetu kama mtunataka kufurahia neema ya Mungu na uwepo wake basi katika ufunuo wa Mungu wetu hasa kuhusiana na ROHO MTAKATIFU tunaonywa sana kutokumfanyia dhambi au kasirani ROHO MTAKATIFU hii maana yake ni nini maana yake mtu anaweza kutengeneza uadui na Roho Mtakatifu na akajikuta yuko matatani.  Katika nafsi hizi tatu kwa mujibu wa mafundisho ya Yesu mwenyewe tunaweza kumkosea Mungu baba na Mwana pia na mlango wa neema ukapatikana lakini tahadhari kubwa inatolewa kuhusu kumkosea ROHO MTAKATIFU.

Mathayo 12:31-32 “Kwa sababu hiyo nawaambia, Kila dhambi na kila neno la kufuru watasamehewa wanadamu, ila kwa kumkufuru Roho hawatasamehewa. Naye mtu ye yote atakayenena neno juu ya Mwana wa Adamu atasamehewa, bali yeye atakayenena neno juu ya Roho Mtakatifu hatasamehewa katika ulimwengu wa sasa, wala katika ule ujao.”

Unaona maneno hayo ni maneno ya Bwana wetu Yesu Kristo ambaye anatuonya sana namna ya kujihadhari ili tusiweze kuwa na uadui na Roho Mtakatifu kwani tunaweza kujikuta katika wakati Mgumu  hii maana yake ni nini maana yake tunaweza kujikuta tunamtenda dhambi Mungu Roho Mtakatifu na akageuka na kuwa adui yetu na kupigana nasi!          

Namna ya kutengeneza uadui na Roho Mtakatifu.

Taasisi nyingi leo zinazomtaja Mungu, na zilizokuwa na nguvu sana duniani zilianza kupoteza umaarufu wake mara baada ya kuanza kupingana na kazi za Roho Mtakatifu na kufanikiwa kutengeneza uadui naye, ni jambo la kusikitisha kwamba katika nchi nyingi za ulaya na ikiwemo Uingereza makanisa mengi sana yaliyokuwa taasisi kubwa yamebakiwa na majengo ambayo mengine yamenunuliwa na kuwa misikiti au kuwa maduka au majumba ya makumbusho na pia kuwa makasino lakini ukichunguza kwa kina chanzo kikubwa cha kufikia hatua hiyo ni kupoteza uamsho na kufikia ngazi ya kufanikiwa kuwa na uadui na Roho Mtakatifu! Uwepo wa Roho Mtakatifu una nafasi kubwa sana katika maisha yetu na mafanikio yetu ya kimwili na kiroho hata hivyo hatuna budi kuzingatia tahadhari zilizotolewa na Mungu kwa neno lake kuhusu Mungu Roho Mtakatifu ni namna gani tunaweza kutengeneza uadui na Roho Mtakatifu

1.       Angalieni msimtie Kasirani -  kumtia kasirani maana yake ni kumuudhi kwa sababu ya manunguniko na malalamiko na kutokuamini, wakati tunapokuwa tumeokolewa hatuna budi kufahamu kuwa ni kazi ya roho Mtakatifu kutuongoza na kutusaidia yeye ni msaada ulio karibu sana anafanya kazi katika kiwango kile kile ambacho angekifanya Kristo akiwa katikati yetu yeye huitwa msaidizi Yohana 14:16 – 18 Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine, ili akae nanyi hata milele; ndiye Roho wa kweli; ambaye ulimwengu hauwezi kumpokea, kwa kuwa haumwoni wala haumtambui; bali ninyi mnamtambua, maana anakaa kwenu, naye atakuwa ndani yenu. Sitawaacha ninyi yatima; naja kwenu.”

 

Unaona Mpango wake Mungu ni kuwa pamoja nasi, Pamoja na kuwa Yesu alipaa Mbinguni lakini hakutuacha yatima ametuletea Msaidizi yaani Roho Wake mtakatifu ili akae nasi ni rafiki wa karibu na ni kiongozi wetu hivyo hatupaswi kumtia kasirani ona

 

Kutoka 23:20-22Tazama, mimi namtuma malaika aende mbele yako, ili akulinde njiani na kukupeleka mpaka mahali pale nilipokutengezea. Jitunzeni mbele yake, mwisikize sauti yake; wala msimtie kasirani; maana, hatawasamehe makosa yenu; kwa kuwa jina langu limo ndani yake. Lakini ukiisikiza sauti yake kweli, na kuyatenda yote ninenayo mimi; ndipo mimi nitakuwa ni adui wa adui zako, na mtesi wa hao wakutesao.”

 

Ni muhimu kufahamu kuwa malaika anayetajwa hapa na Bwana kwamba atawaongoza wana wa Israel na kuwa wajihadhari wasimtie Kasirani ni ROHO MTAKATIFU Yeye katika agano la kale anaitwa malaika wa uso wake kama unavyoweza kuona katika andiko la Msingi

 

Isaya 63:9-10Katika mateso yao yote yeye aliteswa, na malaika wa uso wake akawaokoa; kwa mapenzi yake, na huruma zake, aliwakomboa mwenyewe; akawainua, akawachukua siku zote za kale. Lakini wakaasi, wakamhuzunisha Roho yake Mtakatifu; kwa hiyo akawageukia, akawa adui, akapigana nao.”

 

Unaweza kuona maonyo ya kibiblia kwamba tunaweza kumkosea ROHO MTAKATIFU kwa kumtia kasirani na hatimaye akageuka na kuwa adui na kupigana nasi, haya yalifanywa na wana wa Israel walipookolewa kutoka Misri lakini njiani mara kwa mara walimkosea Mungu Roho Mtakatifu kwa kufanya maovu ambayo yaliwafanya waangamizwe jangwani  ona

  
1Wakoritho 10:1-11Kwa maana, ndugu zangu, sipendi mkose kufahamu ya kuwa baba zetu walikuwa wote chini ya wingu; wote wakapita kati ya bahari; wote wakabatizwa wawe wa Musa katika wingu na katika bahari; wote wakala chakula kile kile cha roho; wote wakanywa kinywaji kile kile cha roho; kwa maana waliunywea mwamba wa roho uliowafuata; na mwamba ule ulikuwa ni Kristo. Lakini wengi sana katika wao, Mungu hakupendezwa nao; maana waliangamizwa jangwani. Basi mambo hayo yalikuwa mifano kwetu, kusudi sisi tusiwe watu wa kutamani mabaya, kama wale nao walivyotamani. Wala msiwe waabudu sanamu, kama wengine wao walivyokuwa; kama ilivyoandikwa, Watu waliketi kula na kunywa, kisha wakasimama wacheze. Wala msifanye uasherati, kama wengine wao walivyofanya, wakaanguka siku moja watu ishirini na tatu elfu. Wala tusimjaribu Bwana, kama wengine wao walivyomjaribu, wakaharibiwa na nyoka. Wala msinung'unike, kama wengine wao walivyonung'unika, wakaharibiwa na mharabu. Basi mambo hayo yaliwapata wao kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ili kutuonya sisi, tuliofikiliwa na miisho ya zamani

 

Unaona? Wana wa Israel kwa rehema na huruma za Mungu waliokolewa kutoka utumwani Misri kwa nia nzuri ya upendo wa Mungu ili kusudi awapeleke katika nchi ya mkanaani akawape raha na maziwa na asali na kila walichokitamani, hata hivyo katika namna ya kushangaza sana utaweza kuona walimuhuzunisha Mungu na kumtia kasirani Roho wa Mungu na hatimaye wakaangamizwa jangwani.

 

Ni kwa sababu ya somo hili Paulo mtume anasema mambo hayo yaliwapata wao kwa jinsi ya mifano ili kutuonya sisi tuliofikiwa na miisho ya zamani hizi yaani zamani hizi ni zama hizi ambapo ROHO MTAKATIFU Yuko kazini hapa duniani akifanya kazi pamoja nasi, kwa msingi huo basi kanisa au taasisi yoyote inayomtaja Mungu kama haitajali kutunza uwepo wa ROHO MTAKATIFU kwa heshima kubwa ni ukweli ulio wazi kuwa tutakuwa na uadui naye!

 

2.       Wala Msimuhuzunishe - Namna nyingine ambayo tunaweza kujenga uadui na Roho Mtakatifu ni Pamoja na kumuhuzunisha ona Waefeso 4:30 “Wala msimhuzunishe yule Roho Mtakatifu wa Mungu; ambaye kwa yeye mlitiwa muhuri hata siku ya ukombozi.”  Kumuhuzunisha ROHO MTAKATIFU huambatana na kumkasirisha  neno la kiyunani linalotumika kuhusiana na kumuhuzunisha ROHO MTAKATIFU Katika kiyunani ni LYPEITE Kwa kiingereza ni Cause Grief Ambalo maana yake ni kumsababishia MAJONZI hili ni wimbi zito la masikitiko na kukasirishwa kunakotokana na kupingwa kunakosababishwa na ugumu wa mioyo ya watu kwa makusudi jambo la namna hii lilimtokea Masihi pale watu walipiokuwa wanataka asiponye mtu kwa sababu ni siku ya sabato Marko 3:4-5 “Akawauliza, Ni halali siku ya sabato kutenda mema, au kutenda mabaya? Kuponya roho au kuiua? Wakanyamaza. Akawakazia macho pande zote kwa hasira, akiona huzuni kwa ajili ya ugumu wa mioyo yao, akamwambia yule mtu, Nyosha mkono wako. Naye akaunyosha; mkono wake ukawa mzima tena.”        Katika taasisi mbalimbali na madhehebu mbalimbali ya Kikristo wakati mwingine wamekuweko watu ambao kwa makusudi kabisa wanapinga na kazi za Roho Mtakatifu katika taasisi au maisha ya mtu, wako watu wanaweza kupinga maombi, wanaweza kupinga uponyaji au hata ustawi wa tabia njema iliyoko ndani ya Mtu ambayo imetokana na kazi za ROHO MTAKATIFU shughuli kama hizo zinamuhuzunisha sana Mungu Pale katika Marko 5:6 ukisoma utaona viongozi wa dini sio tu walichukizwa na Yesu kuponya siku ya sabato lakini vilevile walikuwa na makusudi ya kumuangamiza! Wako watu pia wanaopinga na mahubiri, au muhubiri au kazi zinazofanywa na wahubiri wa Injili,  nimefanya kazi ya kichungaji miaka 12, na kufundisha vyo vya Biblia miaka 12 na pia kuongoza taasisi ya kielimu kwa shule ya seminari miaka 10 na mara kadhaa nimeona watu wakishindana na ROHO MTAKATIFU wazi wazi na wakati mwingine nilidhani wananichukia mimi jambo ambalo nimeshalizoea lakini kumbe niligundua baadaye kuwa kazi ile ambayo Roho wa Mungu ameiweka ndani yangu ilikuwa inapingwa vikali, sio hivyo tu mahali popote ambako watu wanaishi kwa MANENO MAOVU, UCHUNGU, GHADHABU, HASIRA KELELE NA MATUKANO NA UBAYA WA KILA NAMNA  Hayo nayo hayo nayo ni sababu kubwa ya kusababisha MAJONZI kwa ROHO MTAKATIFU hili ndio tukio lililopelekea Paulo Mtume kuwataka Kanisa la Efeso wawe mbali na maswala ya aina hiyo kwani ndiyo yanayopelekea kuhuzunika kwa Majonzi kwa ROHO MTAKATIFU jambo ambalo litapelekea aliache kanisa, aondoke au asifanye kazi tena na hapo uadui nay eye huwa unaweza kufikia kikomo. Waefeso 4:29-31 “Neno lo lote lililo ovu lisitoke vinywani mwenu, bali lililo jema la kumfaa mwenye kuhitaji, ili liwape neema wanaosikia. Wala msimhuzunishe yule Roho Mtakatifu wa Mungu; ambaye kwa yeye mlitiwa muhuri hata siku ya ukombozi.Uchungu wote na ghadhabu na hasira na kelele na matukano yaondoke kwenu, pamoja na kila namna ya ubaya;”

 

3.       Msimzimishe Roho1Wathesalonike 5:19 “Msimzimishe Roho;” Ni muhimu kukumbuka kuwa  katika kumueleze ROHO MTAKATIFU  moja ya alama zinazotumika keelezea utendaji wa Roho Mtakatifu ni pamoja na MOTO, wote tunaweza kuwa na ufahamu juu ya umuhimu wa Moto katika maisha ya Mwanadamu, tunajua kuwa maendeleo makubwa ya mwanadamu yalichangiwa pia na ugunduzi wa Moto, Roho wa Krito vilevile hufanya kazi kama Moto katika maisha ya waaminio

 

Isaya 4:3-4 “Tena itakuwa ya kwamba yeye aliyebaki katika Sayuni, na yeye aliyeachwa ndani ya Yerusalemu, ataitwa mtakatifu; yaani, kila mmoja aliyeandikwa miongoni mwa hao walio hai ndani ya Yerusalemu; hapo Bwana atakapokuwa ameuosha uchafu wa hao binti za Sayuni na kuisafisha damu ya Yerusalemu kati yake, kwa roho ya hukumu na kwa roho ya kuteketeza.”

 

Unaona maandiko yanatufundisha wazi kuwa utendaji wa Roho Mtakatifu ni kama mfano wa Moto hufanya kazi ya kuichoma mioyo yetu na kuteketeza yasiyofaa ndani yetu ili tuweze kuwa watakatifu, upendo wa Mungu huwaka ndani yetu, upendo wa kuhubiri, kuabudukumtumikia Mungu kwa uaminifu, kufanya maombi, kuwasaidia wengine moto huo wa kihuduma ndani yetu huwashwa na ROHO MTAKATIFU tangu anapokuja ndani yetu ona Matendo 2:3-4 “Kukawatokea ndimi zilizogawanyikana, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao. Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema kwa lugha nyingine, kama Roho alivyowajalia kutamka.” 

 

Unaona hii ni Ishara ya Roho wa Mungu kuwasha moto wa uamsho ndani yetu ili tumpende Mungu na wenzetu, kwa msingi huo hatupasw kamwe kuuzima moto huo, Neno linalotumika katika maneno ya kiyunani kuhusu KUZIMA  ni neno SBENNUMI – “sben-noo-mee” kwa kiingereza to extinguish  ambalo maana yake ni tendo endelevu la kuzima moto, msimzimishe ROHO kanisa ua taasisi au mtu binafsi anaweza kuendelea kuuzimisha moto wa Roho Mtakatifu kwa kukosa furaha, kuacha kuomba, kuacha kushukuru, kupinga unabii, kupinga mapenzi ya Mungu, kupinga mambo mema na kutokujitenga na uovu au ubaya wa kila namna haya ndio mojawapo ya maswala yanayochangia kumzimisha ROHO WA BWANA ona 1Wathesalonike 5:14-22 “Ndugu, twawasihi, waonyeni wale wasiokaa kwa utaratibu; watieni moyo walio dhaifu; watieni nguvu wanyonge; vumilieni na watu wote. Angalieni mtu awaye yote asimlipe mwenziwe mabaya kwa mabaya; bali siku zote lifuateni lililo jema, ninyi kwa ninyi na kwa watu wote. Furahini siku zote; ombeni bila kukoma; shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu. Msimzimishe Roho; msitweze unabii; jaribuni mambo yote; lishikeni lililo jema; jitengeni na ubaya wa kila namna.”        Unaona kwa mujibu wa maelezo na maonyo ya Mtume Paulo matukio yote hayo yakifanyika kwa waamini na taasisi za kidini tunamfanya Roho wa Mungu auzunike na kwa sababu hiyo tunatengeneza uadui na Mungu nay eye atatutapika na matokeo yake taasisi au watu binafsi wanapoa ona

 

Ufunuo 3:13-22 “Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa. Na kwa malaika wa kanisa lililoko Laodikia andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye Amina, Shahidi aliye mwaminifu na wa kweli, mwanzo wa kuumba kwa Mungu. Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto. Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu. Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi. Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona. Wote niwapendao mimi nawakemea, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu. Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami. Yeye ashindaye, nitampa kuketi pamoja nami katika kiti changu cha enzi, kama mimi nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba yangu katika kiti chake cha enzi. Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa

 

Unaona kwa msingi huo kama watu watauzima moto wa Roho kwaajili ya sababu mbalimbali tulizojifunza hapo juu ni ahadi ya ROHO MTAKATIFU mwenyewe ya kuwa watatutapika, yeye hapenzi watu vuguvugu, yeye anatutaka tutubu na kama hatutafanya hivyo hakuna kingine tunachoweza kuzawadiwa bali tutapoteza Rehema na neema yake na kujikuta tumeunda uadui na Roho Mtakatifu. Nisikilize Mungu habadiliki, tabia ya Mungu ni ileile sisi wanadamu hubadilika Kabla ya gharika ya wakati wa Nuhu iliyofutilia mbali wanadamu wengi na kumuacha Nuhu na familia yake wanadamu walitenda maovu, walijaa uovu waliacha kumsikiliza ROHO MTAKATIFU kwa kufanya uovu na kuwaza kufanya mabaya kila wakati hivyo walimuhuzunisha na walimzimisha pia na walishindana  naye nadhani ni pale alipokuwa akiwashauri kuwa wema na wao wakapuuzia  Mwanzo 6:3-6BWANA akasema, Roho yangu haitashindana na mwanadamu milele, kwa kuwa yeye naye ni nyama; basi siku zake zitakuwa miaka mia na ishirini. Nao Wanefili walikuwako duniani siku zile; tena, baada ya hayo, wana wa Mungu walipoingia kwa binti za binadamu, wakazaa nao wana; hao ndiyo waliokuwa watu hodari zamani, watu wenye sifa. BWANA akaona ya kuwa maovu ya mwanadamu ni makubwa duniani na kwamba kila kusudi analowaza moyoni mwake ni baya tu sikuzote. BWANA akaghairi kwa kuwa amemfanya mwanadamu duniani, akahuzunika moyo” unaona madhara watu waliposhinda ana Roho ya Mungu, miaka ya kuishi mwanadamu ilipunguzwa, Mungu aklijuta kumuumba mwanadamu, rehema zake na huruma zake zikafikia mpaka akahuzunika akawafuta wanadamu, watu wanaopinga ana mapenzi ya Mungu, taasisi zinazopigana na kusudi la Mungu, na watu wenye tabia endelevu ya kushinda ana kazi ya Mungu kupitia roho Mtakatifu watapunguziwa maisha, watafutwa kwa sababu wameamua kuwa adui wa Mungu

 

4.       Msimpinge Roho Mtakatifu – Matendo 7:51-52 “Enyi wenye shingo gumu, msiotahiriwa mioyo wala masikio, siku zote mnampinga Roho Mtakatifu; kama baba zenu walivyofanya, na ninyi ni vivyo hivyo. Ni yupi katika manabii ambaye baba zenu hawakumwudhi? Nao waliwaua wale waliotabiri habari za kuja kwake yule Mwenye Haki; ambaye ninyi sasa mmekuwa wasaliti wake, mkamwua;”            Namna nyingine ya kuwa adui wa Roho Mtakatifu ni kumpinga ni neno gumu na lenye kusikitisha sana kadiri nilipokuwa naendelea kujifunza somo hili nilikuwa nawaza maoyoni hivi somo hili ni sehemu ya INJILI kweli au kuwatisha watu? Lakini Roho Mtakatifu akanikumbusha maeno ya BWANA YESU na haya ya STEFANO kwa habari ya ROHO MTAKATIFU maonyo ya kucheza naye hayana utani wala mchezo kabisa, hakuna mzaha linapokuja swala la kucheza na Roho Mtakatifu lugha ya kimaandiko ni kali na ngumu na haina mzaha! Kumpinga Roho Mtakatifu ni dhambi nyingine ambayo wanadamu wanaweza kumtendea Mungu aidha walioamini au hata wasioamini maadamu tu utaingia kwenye anga zake na kumpinga madhara yake yatakuhusu, Kumpinga Roho Mtakatifu katika lugha ya kiyunani linatumika neno ANTIPIPTO ambalo kiingereza chake ni resist au oppose kwa kuwa Roho Mtakatifu hawezi kuonekana kwa macho ya kibinadamu

 

Yohana 14:16-17 “Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine, ili akae nanyi hata milele; ndiye Roho wa kweli; ambaye ulimwengu hauwezi kumpokea, kwa kuwa haumwoni wala haumtambui; bali ninyi mnamtambua, maana anakaa kwenu, naye atakuwa ndani yenu.”          

 

Sasa unawezaje kumpinga yeye usiyemuona kwa macho, ukweli ni wazi kuwa kumpinga ROHO MTAKATIFU Huambatana na kuwapinga watumishi wake, wale wanaobeba ujumbe wake NI YUPI KATIKA MANABII AMBAYE BABA ZENU HAWAKUMWUUDHI Wayahudi walipinga ana Musa, walipinga ana manabii, walimpinga yesu Kristo waliwapimga mitume na hata kuwaua walipinga maneno yale na ujumbe ule ambao waliubeba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu, Roho wa Mungu leo anaweza kugeuka adui na akapigana nasi kama tu tunazuia kazi mzake na kupinga ujumbe wake huku tukiwadharau na kuwapiga na kuwapinga watumishi wake na kushindana na kazi yake hiki ndicho ambacho mafarisayo na Masadukayo walikifanya na wayahudi wengi wenye wivu walishindana sana na wajumbe wa injili hata wakitaka wasihubiri wala kumtaja Yesu ona

 

Matendo 4:1-10 “Hata walipokuwa wakisema na watu wale, makuhani na akida wa hekalu na Masadukayo wakawatokea, wakifadhaika sana kwa sababu wanawafundisha watu na kuhubiri katika Yesu ufufuo wa wafu.Wakawakamata, wakawaweka gerezani hata asubuhi; kwa kuwa imekwisha kuwa jioni. Lakini wengi katika hao waliosikia lile neno waliamini; na hesabu ya watu waume ikawa kama elfu tano.Hata asubuhi wakubwa na wazee na waandishi wakakusanyika Yerusalemu, na Anasi Kuhani Mkuu, na Kayafa pia, na Yohana na Iskanda, na wote wale waliokuwa jamaa zake Kuhani Mkuu.Walipowaweka katikati wakawauliza, Kwa nguvu gani na kwa jina la nani ninyi mmefanya haya? Ndipo Petro, akijaa Roho Mtakatifu, akawaambia, Enyi wakubwa wa watu na wazee wa Israeli, kama tukiulizwa leo habari ya jambo jema alilofanyiwa yule mtu dhaifu, jinsi alivyoponywa, jueni ninyi nyote na watu wote wa Israeli ya kuwa kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, ambaye ninyi mlimsulibisha, na Mungu akamfufua katika wafu, kwa jina hilo mtu huyu anasimama ali mzima mbele yenu.”     

 

Matendo 5:14-39 “walioamini wakazidi kuongezeka kwa Bwana, wengi, wanaume na wanawake; hata ikawa katika njia kuu hutoa nje wagonjwa, na kuwaweka juu ya majamvi na magodoro, ili Petro akija, ngawa kivuli chake kimwangukie mmojawapo wao. Nayo makutano ya watu wa miji iliyoko kandokando ya Yerusalemu wakakutanika, wakileta wagonjwa, nao walioudhiwa na pepo wachafu; nao wote wakaponywa. Akaondoka Kuhani Mkuu na wote waliokuwa pamoja naye, (hao ndio walio wa madhehebu ya Masadukayo), wamejaa wivu, wakawakamata mitume wakawaweka ndani ya gereza; lakini malaika wa Bwana akafungua milango ya gereza usiku, akawatoa, akasema, Enendeni mkasimame hekaluni mkawaambie watu maneno yote ya Uzima huu. Nao waliposikia wakaenda alfajiri hekaluni, wakaanza kufundisha. Akaja Kuhani Mkuu nao waliokuwa pamoja naye, wakawakutanisha watu wa baraza, na wazee wote wa wana wa Israeli, wakatuma watu gerezani ili wawalete. Hata watumishi walipofika hawakuwaona gerezani, wakarudi wakatoa habari, wakisema, Gereza tumeikuta imefungwa salama, nao walinzi wamesimama mbele ya mlango; lakini tulipoufungua hatukukuta mtu ndani.  Basi jemadari wa hekalu na wakuu wa makuhani waliposikia haya, wakaingiwa na shaka kwa ajili yao, litakuwaje jambo hilo. Mtu mmoja akaja akawapasha habari ya kwamba, Watu wale mliowaweka gerezani wako ndani ya hekalu, wamesimama wakiwafundisha watu. Ndipo yule jemadari akaenda pamoja na watumishi, wakawaleta, lakini si kwa nguvu, kwa maana waliogopa watu wasije wakawapiga kwa mawe. Walipowaleta, wakawaweka katika baraza. Kuhani Mkuu akawauliza, akisema, Je! Hatukuwaamuru ninyi kwa nguvu, msifundishe kwa jina hili? Nanyi, tazameni, mmeijaza Yerusalemu mafundisho yenu, na mnataka kuileta damu ya mtu yule juu yetu. Petro na mitume wakajibu, wakisema, Imetupasa kumtii Mungu kuliko wanadamu. Mungu wa baba zetu alimfufua Yesu, ambaye ninyi mlimwua mkimtundika katika mti. Mtu huyo Mungu amemtukuza kwa mkono wake wa kuume, awe Mkuu na Mwokozi, awape Waisraeli toba na msamaha wa dhambi. Na sisi tu mashahidi wa mambo haya, pamoja na Roho Mtakatifu ambaye Mungu amewapa wote wamtiio.Wao waliposikia wakachomwa mioyo yao; wakafanya shauri kuwaua. Lakini mtu mmoja, Farisayo, jina lake Gamalieli, mwalimu wa torati, mwenye kuheshimiwa na watu wote, akasimama katika baraza, akaamuru mitume wawekwe nje kitambo kidogo, akawaambia, Enyi waume wa Israeli, jihadharini jinsi mtakavyowatenda watu hawa. Kwa sababu kabla ya siku hizi aliondoka Theuda, akijidai ya kuwa yeye ni mtu mkuu, watu wapata mia nne wakashikamana naye; naye aliuawa na wote waliomsadiki wakatawanyika wakawa si kitu. Baada ya mtu huyo aliondoka Yuda Mgalilaya, siku zile za kuandikiwa orodha, akawavuta watu kadha wa kadha nyuma yake, naye pia akapotea na wote waliomsadiki wakatawanyika. Basi sasa nawaambia, Jiepusheni na watu hawa, waacheni; kwa kuwa shauri hili au kazi hii ikiwa imetoka kwa binadamu, itavunjwa, lakini ikiwa imetoka kwa Mungu hamwezi kuivunja; msije mkaonekana kuwa mnapigana na Mungu.”

 

Wakati wote unaposoma kitabu cha Matendo ya Mitume ambacho kimsingi ndio tunasoma kwa kina na mapana na marefu utendaji wa Roho wa Mungu ndio utaweza kuona jinsi watu kadha wa kadhaa walivyoweza kupinga ana kazi ya Mungu na wajumbe wa ile kazi na hiki ndicho anachokikemea STEFANO na kuwaonya wayahudi kwamba waache kumpinga ROHO MTAKATIFU   ikiwa ni pamoja na kushupaza shingo zao. Kumpinga Roho Mtakatifu na kazi zake au watumishi wake leo limekuwa moja wapo ya Dhambi inayopelekea Mungu kuwaacha watu wake Roho Mtakatifu leo anapingwa sana na waliokoka na wasiookoka yako mashirika leo na wako watu leo wamefilisika kiroho na wanafanya kila jitihana waweze kuinuka tena lakini inashindikana sababu kubwa ni kupinga ana Roho wa Mungu, watu wanapinga uamsho, wanapinga ujazo wa Roho, wanapinga miujiza, wanapinga wajumbe wa Mungu, wanahakikisha kuwa mnakuwa na usumbufu na mnakosa utulivu ili mradi tu kuharibu hali ya kiroho na injili. Ukitaka kuwa adui wa ROHO MTAKATIFU hakikisha kuwa unapinga anaye, yeye aliye na sikio na alisikie neno hili.

 

5.       Usimwambie uongo Roho Mtakatifu - Matendo 5:3-5 “Petro akasema, Anania, kwa nini Shetani amekujaza moyo wako kumwambia uongo Roho Mtakatifu, na kuzuia kwa siri sehemu ya thamani ya kiwanja? Kilipokuwa kwako, hakikuwa mali yako? Na kilipokuwa kimekwisha kuuzwa, thamani yake haikuwa katika uwezo wako? Ilikuwaje hata ukaweka neno hili moyoni mwako? Hukumwambia uongo mwanadamu, bali Mungu. Anania aliposikia maneno haya akaanguka, akafa. Hofu nyingi ikawapata watu wote walioyasikia haya.”  Kumwambia uongo ROHO MTAKATIFU  ni mojawapo ya dhambi mbaya ambayo nyakati za kanisa la kwanza ilisababisha watu kufa mara moja, lakini hata leo watu wanaweza kutengeneza uadui na ROHO WA MUNGU kwa mtindo unaofanana na Anania na Safira kimsingi watu hawa walifanya unafiki, walikuwa wakiigiza jambo ambalo sio sahihi mbele za Mungu kwanza tuichambue asili ya dhambi yao

 

Kulikuwa na mpango wa watu kuishi kwa umoja na kwa pamoja na kwaajili ya kanisa watu wengi walikuwa wakiuza mali zao na kukabidhi kwa mitume kwa kusudi la kuwasaidia wengine moja ya watu waliofanya hayo na kupata umaarufu na sifa kubwa katika kanisa ni Barnabas ona

 

Matendo 4:34-37 “Wala hapakuwa na mtu mmoja miongoni mwao mwenye mahitaji; kwa sababu watu wote waliokuwa na viwanja au nyumba waliviuza, wakaileta thamani ya vitu vile vilivyouzwa,wakaiweka miguuni pa mitume; kila mtu akagawiwa kwa kadiri ya alivyohitaji. Na Yusufu, aliyeitwa na mitume Barnaba, (maana yake, Mwana wa faraja), Mlawi, asili yake ni mtu wa Kipro, alikuwa na shamba akaliuza, akaileta fedha, akaiweka miguuni pa mitume.”

 

Nadhani ni kutokana na watu kadhaa kusifiwa na mitume kwa moyo wao wa utoaji tayari Anania na Safira nao walipata msukumo wa kufanya hivyo lakini nadhani wakiwa na nia ya kujipatia sifa tu, kutoa mali zako na kuziuza kwaajili ya utoaji wa kanisa halikuwa tatizo, na hata kuzuia sehemu ya fedha kwaajili ya familia haikuwa tatizo, kama Petro Mtume alivyohoji

 

Matendo 5:4 “Kilipokuwa kwako, hakikuwa mali yako? Na kilipokuwa kimekwisha kuuzwa, thamani yake haikuwa katika uwezo wako? Ilikuwaje hata ukaweka neno hili moyoni mwako? Hukumwambia uongo mwanadamu, bali Mungu.”               

 

Swala kubwa lilikuwa kumdanganya ROHO MTAKATIFU na kumjaribu, Shetani alikuwa ameshamjaza Anania na mkewe nia ovu nia yao ilikuwa ni kutaka sifa, kutoka katika jamii ya kanisa, wao waliwaambia mitume kuwa wametoa vyote kumbe kuna ambacho walijifichia, walikuwa wakijaribu kuwadanganya watu hasa wa jamii ya kanisa kumbe kiuhalisia walikuwa wakimdanganya ROHO MTAKATIFU ona

 

Matendo 5:3-5 “Petro akasema, Anania, kwa nini Shetani amekujaza moyo wako kumwambia uongo Roho Mtakatifu, na kuzuia kwa siri sehemu ya thamani ya kiwanja? Kilipokuwa kwako, hakikuwa mali yako? Na kilipokuwa kimekwisha kuuzwa, thamani yake haikuwa katika uwezo wako? Ilikuwaje hata ukaweka neno hili moyoni mwako? Hukumwambia uongo mwanadamu, bali Mungu. Anania aliposikia maneno haya akaanguka, akafa. Hofu nyingi ikawapata watu wote walioyasikia haya.”

 

Mungu alikusudia kanisa lake liwe kama mfano wake yeye aliyetuumba ni agizo la kibiblia kwamba tuuvue kabisa utu wa kale na kuacha kabisa kuambiana uongo angalia Wakolosai 3:9-10 “Msiambiane uongo, kwa kuwa mmevua kabisa utu wa kale, pamoja na matendo yake; mkivaa utu mpya, unaofanywa upya upate ufahamu sawasawa na mfano wake yeye aliyeuumba.”

 

Leo hii sio ajabu watu kuambiana uongo, kumekuwa na watu waogo na wadanganyaji kuliko nyakati za kanisa la Kwanza, kumekuwa na wimbi kubwa la watu wanafiki na wanaotaka sifa na kujijengea jina katika jamii kupitia umaarufu feki, vyovyote iwavyo kusema uongo ni ishara iliyo wazi kuwa Ibulisi ambaye ni baba wa uongo anatawala ona

 

Yohana 8:44 “Ninyi ni wa baba yenu, Ibilisi, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; kwa sababu yeye ni mwongo, na baba wa huo.”

 

Kwa misingi hii unaweza kuona ya kuwa kama unadanganya watu na kutaka sifa na kudanganya watumishi wa Mungu ni wazi kuwa unatengeneza uadui na ROHO MTAKATIFU jambo ambalo litakugharimu.

 

6.       Kumfanyia Jeuri Roho wa Neema – Waebrania 10:26-29 “Maana, kama tukifanya dhambi kusudi baada ya kuupokea ujuzi wa ile kweli, haibaki tena dhabihu kwa ajili ya dhambi; bali kuna kuitazamia hukumu yenye kutisha, na ukali wa moto ulio tayari kuwala wao wapingao.Mtu aliyeidharau sheria ya Musa hufa pasipo huruma, kwa neno la mashahidi wawili au watatu. Mwaonaje? Haikumpasa adhabu iliyo kubwa zaidi mtu yule aliyemkanyaga Mwana wa Mungu, na kuihesabu damu ya agano aliyotakaswa kwayo kuwa ni kitu ovyo, NA KUMFANYIA JEURI ROHO WA NEEMA?Nyakati za agano la kale mtu aliyeivunja sharia ya Musa aliuawa pasipo huruma

 

Hesabu 15:30-35 “Lakini mtu afanyaye neno lo lote kwa kusudi, kama ni mzalia, kama ni mgeni, huyo amtukana Bwana; na mtu huyo atakatiliwa mbali na watu wake. Kwa sababu amelidharau neno la Bwana, na kuyavunja maagizo yake; mtu huyo atakatiliwa mbali, uovu wake utakuwa juu yake. Kisha wakati huo wana wa Israeli walipokuwako jangwani, wakamwona mtu mmoja akikusanya kuni siku ya Sabato. Hao waliomwona akikusanya kuni wakamleta kwa Musa na Haruni, na kwa mkutano wote. Nao wakamweka kifungoni, maana, lilikuwa halijasemwa atakalotendwa. Bwana akamwambia Musa, Mtu huyo lazima atauawa; mkutano wote watampiga kwa mawe huko nje ya marago.”

 

Agano jipya ni agano lililobora zaidi ya lile la agano la kale kama mtu angeliweza kuuawa kwaajili ya kuvunja sharia katika agano la kale ni zaidi sana mtu anapoivunja sharia ya kifalme katika agano jipya kama asemavyo mwandishi wa kitabu cha Waebrania, Mwandishi anatoa maonyo makali sana kuhusiana na ukengeufu, kurudi nyuma na kumkana Yesu Kristo jambo ambalo ni kinyume na utendaji mzima wa Roho Mtakatifu ambaye hufanya kazi ya kuwapa watu neema ili watubu na kumuamini Yesu kwa msingi huo mtu anapoifanya shingo yake kuwa ngumu na kutukana maswala kadhaa ya wokovu na kuukana anajiweka kwenye uadui na Roho wa Kristo nani sawa kabisa na kumfanyia Jeuri ROHO WA NEEMA kwa msingi huo kufanya dhambi kusudi, kunaleta hukumu yenye kutisha kwa sababu kufanya hivyo ni kumfanyia jeuri yeye.

 

7.       Kumkufuru Roho Mtakatifu. – Kilele cha juu zaidi katika dhambi zinazoweza kumfanya mtu kuwa na uadui na Roho Mtakatifu ni kumkufuru, neno Kukufuru katika lugha ya Kiyunani linatumika neno Blasphemia – sawa na neno Blasyphemy katika kiingereza ambalo maana yake ni kusema maneno mabaya au kuzungumza vibaya kuhusu Mungu, jambo hili limezungumzwa na Bwana wetu Yesu Kristo Mwenyewe

 

Mathayo 12:31-32 “Kwa sababu hiyo nawaambia, Kila dhambi na kila neno la kufuru watasamehewa wanadamu, ila kwa kumkufuru Roho hawatasamehewa. Naye mtu ye yote atakayenena neno juu ya Mwana wa Adamu atasamehewa, bali yeye atakayenena neno juu ya Roho Mtakatifu hatasamehewa katika ulimwengu wa sasa, wala katika ule ujao.”

 

Dhambi ya kumkufuru Roho Mtakatifu ndio dhambi pekee ambayo haina msamaha kwa mujibu wa maelekezo ya Yesu kristo, na ndio maana utaweza kuona kumekuweko na maonyo ya kutosha kuhusu kuacha kutenda dhambi kinyume na mapenzi ya ROHO MTAKATIFU,  ukimkufuru Roho umefanya dhambi ya milele, kukufuru ni hali ya kuzungumza mabaya, au kutukana na kuudhi maswala yote Matakatifu yanayohusiana na Mungu Yesu alitoa maonyio ya namna hii katika mazingira ambayo mafarisayo walikuwa wanapinga kazi zote za Mungu alizokuwa akizifanya hata kufikia ngazi ya kutukana na kusema ya kuwa kazi hizo za kiungu zinafanywa na shetani kupoitia Yesu ona

Mathayo 12:22-32 “Wakati ule akaletewa mtu mwenye pepo, kipofu, naye ni bubu; akamponya, hata yule bubu akanena na kuona.  Makutano wote wakashangaa, wakasema, Huyu siye mwana wa Daudi? Lakini Mafarisayo waliposikia, walisema, Huyu hatoi pepo, ila kwa Beelzebuli mkuu wa pepo. Basi Yesu akijua mawazo yao, akawaambia, Kila ufalme ukifitinika juu ya nafsi yake, hufanyika ukiwa; tena mji au nyumba yo yote ikifitinika juu ya nafsi yake, haitasimama. Na Shetani akimtoa Shetani, amefitinika juu ya nafsi yake; basi ufalme wake utasimamaje? Na mimi nikitoa pepo kwa Beelzebuli, je! Wana wenu huwatoa kwa nani? Kwa sababu hiyo hao ndio watakaowahukumu. Lakini mimi nikitoa pepo kwa Roho wa Mungu, basi ufalme wa Mungu umekwisha kuwajilia. Ama awezaje mtu kuingia ndani ya nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuviteka vyombo vyake, asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu? Ndipo atakapoiteka nyumba yake. Mtu asiye pamoja nami yu kinyume changu; na mtu asiyekusanya pamoja nami hutapanya. Kwa sababu hiyo nawaambia, Kila dhambi na kila neno la kufuru watasamehewa wanadamu, ila kwa kumkufuru Roho hawatasamehewa. Naye mtu ye yote atakayenena neno juu ya Mwana wa Adamu atasamehewa, bali yeye atakayenena neno juu ya Roho Mtakatifu hatasamehewa katika ulimwengu wa sasa, wala katika ule ujao.

 

Matendo na maneno yote anayosemewa na kutendewa Roho Mtakatifu kilele chake kinakamilika katika kumkufuru na hivyo kila wakati inapotokea anahuzunishwa, anazimishwa, anaongopewa, anapingwa, anafanyiwa jeuri, anafanyiwa kasirani kielele chake ni kuondoka, kuacha, kutokujishughulisha na ninyi tena na kutokusababisha moyo wa toba utokee na hatimaye kusababisha kuhesabika kana kwamba umekufuruau umemkufuru, Ndio maana leo tunaweza kuiona watu wengi, makanisa mengi na taasisi nyingi zimechwa na ROHO WA BWANA  kwa sababu hawakuzingatia maswala kadhaa yanayimuhuzunisha Mungu ROHO MTAKATIFU  na kumfikisha katika hatua ya kuondoka na kwenda mbali nasi.

Hitimisho:

Kuondoka kwa Roho Mtakatifu katika maisha yetu sio tu kunatutengenezea uadui naye lakini inshara ya kuondoka kwa utukufu wa Mungu, mar azote maandiko yameeleza kuwa wanadamu wamepungukiwa na utukufu wa Mungu mara baada ya kutenda dhambi Warumi 3:23  kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu;” Utukufu wa Mungu unakuwepo kwetu kwa ukamilifu wakati ambapo Roho wa Mungu akiwa hai ndani yetu, akiwa anatenda kazi akiwa anatuongoza, ikiwa tunamsikiliza, lakini tunaelezwa kuwa tunapomuasi anageuka anakuwa adui anapigigana nasi, kwa kuwa Roho Mtakatifu ni Mungu ieleweke wazi kuwa nafsi hii katika utatu wa Mungu inapokasirishwa na kufikia hatua ya kupigana nasi ujue hakuna mwamuzi tena

 

1Samuel 2:22-25. “Basi Eli alikuwa mzee sana; naye alisikia habari za mambo yote ambayo wanawe waliwatenda Waisraeli; na jinsi walivyolala na wanawake waliokuwa wakitumika mlangoni pa hema ya kukutania. Akawaambia, Mbona mnatenda mambo kama hayo? Maana nasikia habari za matendo yenu mabaya kwa watu hawa wote. Sivyo hivyo, wanangu, kwa maana habari hii ninayoisikia si habari njema; mnawakosesha watu wa Bwana. Mtu mmoja akimkosa mwenzake, Mungu atamhukumu; lakini mtu akimkosa Bwana, ni nani atakayemtetea? Lakini hawakuisikia sauti ya baba yao, kwa sababu Bwana amekusudia kuwaua.”  

 

Inapofikia ngazi Mungu mwenye rehema na neema nyingi mwingi wa huruma na asiye mwepesi wa Hasira anafikia ngazi ya kumuua mtu ujue jambo hilo limekuwa machukizo makubwa kwa Mungu wetu, unapokuwa na uadui na Mungu kinachofuata ni kifo na wakati huo huo Mungu anaweza kuamua kukuacha na kuondoa utukufu wake hakuna jambo baya duniani kama kupungukiwa na utukufu wa Mungu. Israel walipokuwa wamemtenda dhambi ukweli ni kuwa utukufu wa Mungu ulikuwa ukiondoa hatua kwa hatua na hatimaye ukaenda katika inchi ya mbali ona katika kitabu cha Ezekiel uwepo wa Mungu ulikuwa ukiondoka taratibu kutoka katika patakatifu hata kwenye kizingiti, kutoka kizingitini hata ukutani, kutoka ukutani hata mlimani na kutoka mlimani hata ukaldayo katika nchi ya utumwa

Ezekiel 10: 4. “Utukufu wa BWANA ukapaa kutoka kwa kerubi yule, ukasimama juu ya kizingiti cha nyumba; nayo nyumba ikajazwa na lile wingu, na ua ulikuwa umejaa mwangaza wa utukufu wa BWANA.,”

Ezekiel 10:18-19. “Kisha huo utukufu wa BWANA ukatoka pale juu ya kizingiti cha nyumba, ukasimama juu ya makerubi.Nao makerubi wakainua mabawa yao, wakapaa juu kutoka katika dunia machoni pangu, hapo walipotoka nje, nayo magurudumu yakawa kando yao; wakasimama mahali pa kuingilia pa mlango wa upande wa mashariki wa nyumba ya BWANA; na utukufu wa Mungu wa Israeli ulikuwa juu yao.”                

Ezekiel 11:23-25. “Utukufu wa BWANA ukapaa juu toka katikati ya mji, ukasimama juu ya mlima wa upande wa mashariki wa mji. Na roho hiyo ikaniinua, ikanichukua katika maono, kwa nguvu za roho ya Mungu, hata Ukaldayo, kwa watu wale wa uhamisho. Basi maono niliyoyaona yakaniacha. Ndipo nikawaambia watu wa uhamisho habari ya mambo yote aliyonionyesha BWANA.” 

Kadiri watu wa Mungu wanapofanya machukizo ya aina mbalimbali, Mungu huupunguza utukufu wake na kuondoka kidogo kidogo utukufu wa Mungu ni sihara ya uwepo wa Mungu ni uwepo wa Roho wake Mtakatifu, Israel walipotenda ya kuchukiza uwepo huo uliondoka na kwenda utumwani Babeli na ndipo sa unapoweza kuona watu waliokuwa utumwani walikuwa na nguvu na uwezo mkubwa sana wa Kiroho na Mungu alitukuzwa lakini Israel panyewe pakabaki ukiwa, Mtu wa Mungu wewe ndio hekalu la Mungu je utukufu wa Mungu umeondoka na kufikia ngazi gani kama utukufu umekuacha na kwenda Babeli huna budi kulia na kutubu, Leo hii mtakapoisikia sauti yake msiifanye mioyo yenu kuwa Migumu. Chunga sana hakuna jambo baya duniani kama kutengwa mbali na uso wa Mungu hakuna jambo linatisha duniani kama kumuasi Roho Mtakatifu na kumuacha akawa adui yetu na kupoigana nasi Bwana ampe neema kila mmoja wetu asiwe adui wa ROHO MTAKATIFU KATIKA JINA LA YESU AMEN.

Na. Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye hekima.      



Maoni 3 :

Bila jina alisema ...

Habari Mtazamaji wangu mheshimiwa, naandika makala hii kuueleza ulimwengu jinsi Dr.diamond alivyomrudisha mpenzi wangu wa zamani kwangu, hii ndio sababu ya mimi kuchukua jukumu la kumshukuru mwigizaji huyu mkubwa anayeitwa Dr diamond kwa sababu kupitia wimbo wake. nisaidie maisha yangu yalizidi kujawa na mapenzi na nafurahi kusema kuwa Ex Boyfriend wangu ambaye tumeachana na mimi kwa kipindi cha miaka 3 alirudi kwangu akiniomba nikubaliwe, Hili lilikuwa tukio la kushtua kwani kabla sijawasiliana na Dr. diamonf ndiye niliyemsihi Ex Boyfriend wangu arudi kwangu lakini kwa msaada wa Dr.diamond sasa uhusiano wangu umerejeshwa. Unaweza pia kuwa na uhusiano bora ikiwa tu utamtumia barua pepe: ( drdiamondTemple@gmail.com ) WhatsApp +2349130958968

Mkuu wa Wajenzi Mwenye Hekima alisema ...

Ukurasa huu umewekwa wakfu kwaajili ya Kuwaelekeza watu kwa Mungu ambaye ndiye msaada wetu mkuu, Maandiko yanasema Mungu kwetu sisi Ni kimbilio na Ngu vu msaada uonekanao tele wakati wa Mateso, hivyo kama yuko mwanadamu anatumia ukurasa huu, kujitangaza kuwa anaweza kuwasaidia wanadamu basi Mwanadamu huyo anamkufuru Mungu na ukurasa huu hautawajibika kwa mtu anayetegemea ushirikina badala ya kumtegemea Mungu, Maandiko yanasema amelaaniwa Mtu yule amtegemeaye mwanadamu na kumfanya kuwa kinga yake

Bila jina alisema ...

Mtumishi Asante kwa somo zuri lakini kwa kuwa blog ni yako naamini unaweza kufuta huo ujumbe wa anaejitangaza, hivyo nashauri uufute, barikiwa sana