Jumanne, 11 Aprili 2023

Leo hivi utakuwa pamoja nami Peponi!


Luka 23:39-43 “Na mmoja wa wale wahalifu waliotungikwa alimtukana, akisema, Je! Wewe si Kristo? Jiokoe nafsi yako na sisi. Lakini yule wa pili akamjibu akamkemea, akisema, Wewe humwogopi hata Mungu, nawe u katika hukumu iyo hiyo? Nayo ni haki kwetu sisi, kwa kuwa tunapokea malipo tuliyostahili kwa matendo yetu; bali huyu hakutenda lo lote lisilofaa. Kisha akasema, Ee Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako. Yesu akamwambia, Amin, nakuambia, leo hivi utakuwa pamoja nami peponi.”


Utangulizi

Wote tunafahamu kuwa Mateso na hukumu ya kusulubiwa na kufia Msalabani halikuwa tukio Jepesi, lilikuwa tukio gumu na la maumivu mengi ya kimwili, kisaikolojia na kiroho, Yesu alisulubiwa akiwa hana hatia wala hakuwa amefanya kosa lolote, wote tunajua sasa ya kuwa alisulubiwa na kuteswa kwaajili ya dhambi zetu, lakini kwa wakati ule wa mateso haikuwa rahisi kueleweka namna hiyo, akiwa Msalabani Pale Golgotha Yesu alisulubiwa pamoja na wanyang’anyi wawili, ambao kimsingi wao walikuwa na hatia! Lakini katika namna ya kushangaza wahalifu hao mmoja alijiunga katika kumshutumu Bwana Yesu na Mwingine kumtetea

Luka 23:36-43 “Wale askari nao wakamfanyia dhihaka, wakimwendea na kumletea siki, huku wakisema, Kama wewe ndiwe mfalme wa Wayahudi, ujiokoe mwenyewe. Na juu yake palikuwa na anwani; HUYU NDIYE MFALME WA WAYAHUDI. Na mmoja wa wale wahalifu waliotungikwa alimtukana, akisema, Je! Wewe si Kristo? Jiokoe nafsi yako na sisi. Lakini yule wa pili akamjibu akamkemea, akisema, Wewe humwogopi hata Mungu, nawe u katika hukumu iyo hiyo? Nayo ni haki kwetu sisi, kwa kuwa tunapokea malipo tuliyostahili kwa matendo yetu; bali huyu hakutenda lo lote lisilofaa. Kisha akasema, Ee Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako. Yesu akamwambia, Amin, nakuambia, leo hivi utakuwa pamoja nami peponi.”

Tukio hili linapelekea Yesu kutamka neno la pili Muhimu miongini mwa maneno saba aliyoyatamka akiwa msalabani, kwa kujikumbusha maneno mengine aliyoyatamka Yesu akiwa Msalabani ni Pamoja na :-

·         Baba uwasamehe kwa maana hawajui walitendalo Luka 23:34

·         Amin nakuambia leo hivi utakuwa pamoja nani peponi Luka 23:43

·         Mama tazama mwanao, mwana tazama mama yako Yohana 19:26-27

·         Mungu wangu Mungu wangu mbona umeniacha Mathayo 27:46

·         Nina kiu Yohana 19:28

·         Imekwisha Yohana 19:30

·         Baba mikononi mwako naiweka roho yangu Luka 23:46

Uchambuzi kuhusu Neno “Leo hivi utakuwa pamoja nami Peponi”

Ni muhimu sana kufahamu kuwa Maneno hayo ya pili yaliyotamkwa na Yesu pale msalabani kwa mtu yule aliyekuwa muhalifu, yana uzito mkubwa sana linapokuja swala la wanafunzi wa kimaandiko wenye kufikiri sana, watafasiri wengi wa maandiko wanaweka hoja ngumu zinazopelekea mstari huu wakati mwingine usiwe mstari mwepesi kutafasirika ona kwa mfano Maneno hayo yanasomeka hiviYesu akamwambia, Amin, nakuambia, leo hivi utakuwa pamoja nami peponiwataalamu wa maandiko wakati mwingine kwa sababu ya kufikiri sana wanajenga hoja kuwa Yesu alikata roho na kufa na kuzikwa na siku ya tatu akafufuka  na akaonekana mara kadhaa duniani kwa watu mbalimbali mpaka alipopaa, kwa msingi huo inawezekanaje Yesu kuwa Pamoja na muhalifu yule Peponi siku ileile, kwa sababu hiyo waoa wanajenga hoja kwamba kwa vile Maandiko ya awali hayakuwa na vituo wala koma huenda maneno maneno ya Yesu yalitakiwa yasomoke hivi Yesu akamwambia, Amin nakuambia leo hivi, utakuwa pamoja nami peponikwa hiyo wataalamu hao wa maandiko hifikiri kuwa kulikuwa na makosa kuweka koma mbele ya neno Amin na neno nakuambia na kuwa sentensi …AMIN NAKUAMBIA LEO HIVI, Yalikuwa ni sentesi moja na hivyo kuifanya ahadi ya Yesu iwe ni neno UTAKUWA PAMOJA NAMI PEPONI, kuweka neno LEO HIVI UTAKUWA PAMOJA NAMI PEPONI Kungeweza kupotosha maana halisi ya tafasiri ya maandiko hayo, Kwa tafasiri hiyo wao wanaamini ya kuwa Yesu alikuwa anamthibitishia Mwizi yule aliyemuamini kuwa anayioyasema ni hakika kwamba atakuwa naye Peponi, Kwahiyo uthibitisho huo wa Yesu kusema ukweli umebebwa na neno …AMIN NAKUAMBIA LEO HIVI ni kwamba Yesu alikuwa anamueleza ukweli wa kuweko kwake peponi mtu yule anayemuamini, lakini haikuwa lazima kuwa Yesu alikuwa anamaanisha kuwa angekuwa naye peponi siku ileile!

Wakati mwingine kufikiri sana na kutumia akili sana kunaweza kuleta upotofu katika maandiko, ushahidi wa kibiblia kutoka katika biblia nyingine unathibitisha wazi kuwa koma iliwekwa mahali sahihi vilevioe kama ilivyowekwa katika Biblia ya kiswahili ya Union version Mfano

·         Biblia ya Kiingereza ya KJV inasema “Verily I say unto thee, To day shalt thou be with me in paradise”

·         Biblia ya kiingereza ya Amplified inasema “Assuredly I tell you, today you will be with me in Paradise”

·         Biblia ya kiingereza ya RSV inasema “And he said to him truly, I say to you, today you will be with me in paradise”

Unaweza kuona tafasiri zote za Biblia zimeweka Koma katika eneo sahihi na kama ilivyo ada ni kweli kuwa Yesu kila alipotaka kuzungumza neno lenye mantiki kubwa sana alitumia neno Amin Nakuambia, na neno la namna hiyo limerejewa katika biblia zaidi ya  mara 76 hata hivyo katika maeneo yote hayo hajawahi kutumia neno LEO,  Kwa msingi huo ni wazi kabisa kuwa Yesu alikuwa akisisitiza kuwa Peponi na Mtu yule kuanzia siku ile ile Angekuwa naye Peponi.

Ni ukweli ulio wazi kuwa Yesu aliposulubiwa na kufa na kuzikwa mwili wake uliwekwa Kaburini, Lakini Nafsi yake na Roho yake alikabidhi kwa Mungu baba na hivyo alikuwa mbinguni au Paradiso tangu wakati ule Luka 23:46 “Yesu akalia kwa sauti kuu, akasema, Ee Baba, mikononi mwako naiweka roho yangu.”  Maneno ya Yesu yako wazi na hayahitaji tafakari pana inakayoweza kututoa nje ya maana halisi japo kufikiri kama mhivi ni kuzuri na kunapanua ufahamu lakini ni ukweli usiopingika kuwa Mwivi yule alipata tiketi ya kuwa na Yesu Peponi tangu siku ile ile.

Leo hivi utakuwa pamoja nani peponi.

Ni ahadi ya uhakika ya kuwa kila anayermkubali Yesu Mungu mwenyewe anatuhakikishia kuwa atakuwa pamoja nasi Peponi, haijalishi kuwa ulikuwa muovu kiasi gani, hatujaelezwa wazi kuwa muhalifu huyu alikuwa amefanya makosa gani lakini iko wazi kuwa kama mtu amehukumiwa kuuawa bila shaka hakuwa mtu mwenye kufaa tena katika jamii, mhalifu huyu sio tu alistahili kuuawa lakini alikuwa hastahili hata kuwekwa Gerezani, kwa vyovyote vile akuwa muovu, mtu huyu hata toba yake ilikuwa sio toba ya kueleweka lakini ni ukweli ya kuwa alikuwa anajua kuwa yuko Msalabani kwa makosa yake naya kuwa anastahili kupata yanayompata, lakini pia alikuwa anatambua kazi ya Yesu pale Msalabani alijua wazi kuwa yeye hakuwa na hatia kama wao na alitambua kuwa Yesu anao ufalme na kuwa sio mwanadamu wa kawaida na alijiombea kukumbukwa katuika ufalme huo, Yesu alimkakikishia kuwa atakuwa pamoja naye peponi, Yesu aliteseka Msalabani si kwa sababu yake ilikuwa ni kwaajili ya dhambi zetu

Isaya 53:3-5 “Alidharauliwa na kukataliwa na watu; Mtu wa huzuni nyingi, ajuaye sikitiko; Na kama mtu ambaye watu humficha nyuso zao, Alidharauliwa wala hatukumhesabu kuwa kitu. Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu; Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa, Amepigwa na Mungu, na kuteswa. Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona

Na kwa msingi huo toba ya muhalifu yule kama ilivyo kwetu sisi ilikuwa ni ahadi thabiti yay a kweli yenye kutuhakikishia wote tunaomkiri Yesu hadharani ya kuwa Mungu atakuwa pamoja nasi na sisi tunakuwa pamoja naye, hakuna mtu mbaya kiasi cha kutokuweza kusafishwa au kusamehewa na kusafishwa kwa Damu ya Yesu!, hakuna jambo la msingi kama kuingia peponi tunaweza kuona wivu kwa jamaa huyu Msalabani laki Kristio ameahidi kuwa kila amuaminiye hatatahayarika katika msimu huu wa Pasaka ni Muhimu basi kwa kila mmoja wetu kusogelea Msalabani na kutubu na kumkiri Kristo ili tupate uhakika wa neema yake ya kutupa kibali cha kuingia naye peponi

Na Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima!



Hakuna maoni: