Jumatatu, 8 Mei 2023

Furaha ya Bwana ni nguvu zetu !


Nehemia 8:9-11 “Naye Nehemia, ndiye aliyekuwa Tirshatha, na Ezra kuhani, mwandishi, na Walawi waliowafundisha watu, wakawaambia watu wote, Siku hii ni takatifu kwa Bwana, Mungu wenu; msiomboleze wala msilie. Maana watu wote walilia, walipoyasikia maneno ya torati. Kisha akawaambia, Enendeni zenu, mle kilichonona, na kunywa kilicho kitamu, tena mpelekeeni sehemu yeye asiyewekewa kitu; maana siku hii ni takatifu kwa Bwana wetu; wala msihuzunike; kwa kuwa furaha ya Bwana ni nguvu zenu. Hivyo Walawi wakawatuliza watu wote, wakasema, Nyamazeni, kwa maana siku hii ni takatifu; wala msihuzunike.”




Utangulizi:

Ni muhimu kujikumbusha wazi Kwamba Mwanadamu katika maumbile yake ni kiumbe chenye Hisia, “Human being is Emotional being” Na kwa sababu ya kuumbwa tukiwa na hisia wakati mwingine tunaweza kukutana na kupanda au kushuka kwa hisia zetu katika maisha ya kila siku, kuna wakati tunaweza kupenda na kuna wakati tunaweza kuchukia, wakati mwingine tunaweza kuwa na furaha na wakati mwingine tunaweza kuwa na huzuni, wakati mwingine kujiamini na wakati mwingine wasiwasi, wakati mwingine ujasiri wakati mwingine hofu, hii ni hali ya kawaida ya maumbile ya mwanadamu, Hisia zetu zinatusaidia kukabiliana na mazingira yetu, kama tutakuwa na siku nzuri tunaweza kuwa na furaha na kama siku hiyo inaweza kuwa mbaya tunaweza kuwa na fadhaa, timu tunazoshabikia zikipata ushindi tunaitikia kwa kufurahi, timu tunazoshabikia zikishindwa tunaitikiwa kwa kuwa na huzuni, tunapopata zawadi za kushitukizwa tunafurahi, tunapopata habari za huzuni, tunahuzunika, ni Muhimu kufahamu kuwa sio mapenzi ya Mungu kuwahuzunisha watu wake ona

Maombolezo 3:31-33 “Kwa kuwa Bwana hatamtupa mtu Hata milele. Maana ajapomhuzunisha atamrehemu, Kwa kadiri ya wingi wa huruma zake. Maana moyo wake hapendi kuwatesa wanadamu. Wala kuwahuzunisha

Tutajifunza somo hili FURAHA YA BWANA NI NGUVU ZENU Kwa kuzingatia vipengele vitatu vifuatavyo:- 

·         Maana ya  Neno Furaha

·         Mafundisho ya Neno la Mungu kuhusu Furaha

·         Furaha ya Bwana ni nguvu zenu.

Maana ya neno Furaha

Neno Furaha katika Biblia ya kiingereza linasomeka kama JOY na tafasiri ya neno JOY katika kamusi ya kiingereza JOY – “The climax of Great pleasure and happiness”, or Feeling great pleasure and happiness, Katika Lugha ya kibiblia inayotumika katika uhusiano na neno hilo, Kwa Kiibrania ni “CHEDVAH” ambalo tafasiri yake ni Gladness au rejoicing  - a state of well – being, and contentment  katika kiyunani ni “CHARA” ni hali ya kuwa na furaha, na kuona kuwa mambo yako vizuri na kuridhika kuwa hakuna wasiwasi hata kama Mazingira hayaonyeshi kuwa hivyo, Ni uwezo wa kushinda mazingira ya kuhuzunisha na kuonyesha ukomavu hata kama mazingira hayo hayaonyeshi au kutia moyo kufurahi.

Mafundisho ya neno la Mungu kuhusu Furaha

Kama tulivyoona maana ya neno furaha hapo juu, Neno la Mungu linatufundisha kuwa furaha hii sio furaha ya kawaida furaha hii inaitwa furaha ya Bwana

Nehemia 8:10Kisha akawaambia, Enendeni zenu, mle kilichonona, na kunywa kilicho kitamu, tena mpelekeeni sehemu yeye asiyewekewa kitu; maana siku hii ni takatifu kwa Bwana wetu; wala msihuzunike; kwa kuwa furaha ya Bwana ni nguvu zenu.”

Ukiifahamu furaha hii nakuhakikishia kuwa maisha yako hayatakuwa kama yalivyo na hasa kama tutahakikisha kuwa tunatembea katika furaha hiyo siku zote za maisha yetu! Furaha hii inatokana na Mungu mwenyewe ona

Wagalatia 5:22 “Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu,

Kwa mujibu wa maandiko furaha hii haitokani na hisia zetu, Furaha hii ni tunda la Roho Mtakatifu katika maisha yetu ya kila siku, Ni furaha inayotoka kwa Mungu mwenyewe, ni furaha kutoka kwa Roho Mtakatifu, furaha hii ikiwa ndani ya Mtu huwa haijalishi mazingira yakoje, Furaha hii inaangalia mbele ya mapingamizi, haikufanyi kuchoka wala haikufanyi uzimie moyo ona

Waebrania 12:2-3 “tukimtazama Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake aliustahimili msalaba na kuidharau aibu, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu. Maana mtafakarini sana yeye aliyeyastahimili mapingamizi makuu namna hii ya watendao dhambi juu ya nafsi zao, msije mkachoka, mkizimia mioyoni mwenu.”         

Furaha hii sio inayotokana na hisia ni furaha inayotokana na karama ya Mungu kwa watu wake inaambatana na uwezo mkubwa sana wa kuvumilia na kukufanya uwe wa kawaida katika mazingira yoyote

Warumi 5:3-5 “Wala si hivyo tu, ila na mfurahi katika dhiki pia; mkijua ya kuwa dhiki, kazi yake ni kuleta saburi; na kazi ya saburi ni uthabiti wa moyo; na kazi ya uthabiti wa moyo ni tumaini; na tumaini halitahayarishi; kwa maana pendo la Mungu limekwisha kumiminwa katika mioyo yetu na Roho Mtakatifu tuliyepewa sisi.”

Kuna utamu Fulani kama utasoma kifungu hiki katika lugha ya kiingereza kwa wale wanaokifahamu kidogo ona

Romans 5:3-5 “Not only so, but we also rejoice in our Sufferings, because we know that suffering produces perseverance, Perseverance character and character hope and hope does not disappoint us because, God has poured out his love into our hearts by the Holy Spirit whom he has given us

Unaona kwa hiyo ni furaha inayotokana na upendo wa Mungu uliomiminwa kwetu na Roho Mtakatifu, hivyo hata wakati wa mateso utawezxa kuona bado furaha hiyo inatawala na haiondolewi na chochote kwa sababu inatazama mbele ya mateso ambako kuna utuklufu mkubwa !

Furaha hiyo sio ya muda, sio ya hisia haitokanani na hali ya mazingira kwamba leo nimepata au nimekosa wala haiwi sawa na ya waliovuna mashamba na zabibu  wala ya maadui zetu ambayo hiyo ni ya kitambo tu , Furaha hii inatoka kwa Bwana na inazidi furaha ya kawaida ona

Zaburi 4:7-8 “Umenitia furaha moyoni mwangu, Kupita yao wanapozidishiwa nafaka na divai. Katika amani nitajilaza na kupata usingizi mara, Maana Wewe, Bwana, peke yako, Ndiwe unijaliaye kukaa salama.”

Furaha ya Bwana ni Nguvu zetu !

Baada ya kuwa tumeona maana ya Furaha na jinsi maandiko yanavyoielezea furaha hiyo sasa turudi katika Mistari ya msingi kwa nini Nehemia anasema furaha ya Bwana ni Nguvu yenu?

  Nehemia 8:9-11 “Naye Nehemia, ndiye aliyekuwa Tirshatha, na Ezra kuhani, mwandishi, na Walawi waliowafundisha watu, wakawaambia watu wote, Siku hii ni takatifu kwa Bwana, Mungu wenu; msiomboleze wala msilie. Maana watu wote walilia, walipoyasikia maneno ya torati. Kisha akawaambia, Enendeni zenu, mle kilichonona, na kunywa kilicho kitamu, tena mpelekeeni sehemu yeye asiyewekewa kitu; maana siku hii ni takatifu kwa Bwana wetu; wala msihuzunike; kwa kuwa furaha ya Bwana ni nguvu zenu. Hivyo Walawi wakawatuliza watu wote, wakasema, Nyamazeni, kwa maana siku hii ni takatifu; wala msihuzunike.”

Israel walikuwa wamepelekwa katika utumwa kihistoria na utumwa huo haukuwa mzuri, wanakumbuka historia chungu ya utumwa wao, na sasa Mungu alikuwa amewapa neema ya kurejea katika nchi yao, na chini ya Zerubabeli walikuwa wamelijenga tena Hekalu, na chini ya Nehemia walikuwa wameujenga ukuta wa Yerusalem na  Nehemia akiungana na Ezra, Ezra aliwasomea watu Torati na kuwakumbusha maneno yote ya Mungu, na hivyo Israel waligundua kuwa walikuwa kinyume na maagizo ya Mungu walikuwa wamekengeuka walisahau maagizo ya Bwana hivyo walipoyasikia maneno ya tarati walilia sana na kuhuzunika, walilia machozi, walijihukumu kuwa huenda wamemkose Mungu na labda walitaka kuomboleza  badala ya kulia na kuomboleza Nehemia aliwaambia hapana hakuna sababu ya kulia na kuomboleza badala yake  walitakiwa kufurahia na kuchinja vitu vinono na kufanya sikukuu unaona :-

Nehemia 8:10-12 “Kisha akawaambia, Enendeni zenu, mle kilichonona, na kunywa kilicho kitamu, tena mpelekeeni sehemu yeye asiyewekewa kitu; maana siku hii ni takatifu kwa Bwana wetu; wala msihuzunike; kwa kuwa furaha ya Bwana ni nguvu zenu. Hivyo Walawi wakawatuliza watu wote, wakasema, Nyamazeni, kwa maana siku hii ni takatifu; wala msihuzunike. Na watu wote wakaenda zao kula na kunywa, na kuwapelekea watu sehemu, na kufanya furaha nyingi, kwa sababu walikuwa wameyafahamu maneno yale waliyohubiriwa.”

Kwa kawaida watu wanapokuwa katika huzuni wanafunga na kuomba, wanalia, wanagalagala kwenye majivu na kuvaa magunia, hii ndio ilikuwa nia ya watu, walidhani kuwa kila wakati wanapaswa kuomboleza, unapogundua kuwa umekosea sio kila wakati unapaswa kulia na kuhuzunika na kuomboleza na kufunga na kuomba, unapopita katika magumu sio kila wakati unapaswa kutumia njia ileile  wakati mwingine unachohitaji ni kupiga kelele za shangwe ni kufurahi ni kujisamehe ni kumuachia Mungu atende kazi yake, kile kitendo tu cha kujua kuwa umekosea ni tayari kazi ya Roho Mtakatifu imefanyika ndani mwako wakati mwingine nenda kachinje ule ufurahi kafanye sikukuu! Adui yetu shetani anataka kuona tunalia tu wakati wote anatarajia tuwe katika taharuki tu lakini iko siri mwamini Mungu ya kuwa atakupa siku yenye furaha kila aunapoamka asubihi usiitarajie siku yako wiki yako mwezi wako mwaka wako kuwa mbaya wewe mwambie Mungu aachilie ile karama yake na tunda lake la furaha hilo linatosha sana kutuweka huru

Zaburi 118:24 “Siku hii ndiyo aliyoifanya Bwana, Tutashangilia na kuifurahia.”

Nisikilize kama Nehemia aliweza kugundua katika nyakati za agano la kale kwamba badala ya watu kulia, badala ya kuhuzunika, badaya ya kufunga na kuomba na kuvaa magunia na kujipaka majivu, Basi wanaweza kutumia silaha ya kufurahia kula pamoja kugawa vyakula kutoa kwa niaba kwaajili ya wengine kwa sababu fuaraha ya Bwana itawapa nguvu, Ni furaha kutioka kwa Roho wake Mtakatifu, kwa hiyo katika changamoto zozote unazozipitia usiangalie mazingira wewe furahi,  Mungu anatupenda kiasi kwamba alimtoa Yesu kufa msalabani kwa niaba yetu, kwa hiyo sio mwakati wetu tena kubeba mateso, ni wakati wetu kufurahi, Hakuna wa kutukwaza,

Hitimisho !

Unawezaje kuwa na furaha ya Bwana katika maisha yako?

-          Hakikisha kuwa unawapoa watu vitu, Matendo 20:35 “Katika mambo yote nimewaonyesha ya kuwa kwa kushika kazi hivi imewapasa kuwasaidia wanyonge, na kuyakumbuka maneno ya Bwana Yesu, jinsi alivyosema mwenyewe, Ni heri kutoa kuliko kupokea.” Kutoa kwa kawaida huwa kunaleta furaha, Ne heri kutoa kuliko kupokea, katika andiko la Msingi Nehemia aliwaambia watu wakatioe wawape wakle ambao hawana kitu ili watu wafurahie pamoja kumbe katika kutoa utaweza kuona furaha ya Bwana ndani yako!

-          Kaa katika uwepo wa Mungu 1Nyakati 16:27 “Heshima na adhama ziko mbele zake; Nguvu na furaha zipo mahali pake.”

-          Jawa na wingi wa shukurani, Msifu Mungu  Zaburi 43:4 “Hivyo nitakwenda madhabahuni kwa Mungu, kwa Mungu aliye furaha yangu na shangwe yangu; Nitakusifu kwa kinubi, Ee MUNGU, Mungu wangu.”

-          Uwe mtu wa ibada na kumujua Mungu Zaburi 122:1 “Nalifurahi waliponiambia, Na twende nyumbani kwa Bwana”.

Furaha ya bwana ni Nguvu zetu kwa sababu inatupa amani ya kweli ambayo huwezi kuipata katika mitandao ya kijamii, huwezi kuipata kwa fedha, huwezi kuipata kwa marafiki, kwa kwenda pikiniki, kwa kufanya ngono, kwa kula madawa ya kulevya, kwa kunywa pombe, kwa kucheza disco hayo yanaweza kukupa furaha ya muda lakini iliyojawa na majuto, Furaha ya kweli unaweza kuipata ndani ya Yes utu!

Na Rev. Innocent Samuel Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima!

Hakuna maoni: