Jumamosi, 31 Agosti 2024

Ubatizo wa Roho Mtakatifu:-


Mathayo 3:11-12 “Kweli mimi nawabatiza kwa maji kwa ajili ya toba; bali yeye ajaye nyuma yangu ana nguvu kuliko mimi, wala sistahili hata kuvichukua viatu vyake; yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.  Ambaye pepeto lake li mkononi mwake, naye atausafisha sana uwanda wake; na kuikusanya ngano yake ghalani, bali makapi atayateketeza kwa moto usiozimika.”




Utangulizi:

Ubatizo wa Roho Mtakatifu ni uzoefu wa kiroho unaotokea kwa mtu aliyeokoka kumuwezesha mtu huyo kupokea uwepo wa Roho Mtakatifu unaoambatana na nguvu za Mungu na ujasiri unaomuwezesha mtu huyo kuzungumza neno la Mungu kwa ujasiri, huku akithibitishwa na kunena kwa lugha pamoja na kupokea vipawa na karama nyinginezo, Ubatizo wa Roho Mtakatifu umetajwa kwa mara ya kwanza na Yohana mbatizaji katika vitabu vya injili.

Mathayo 3:11-12 “Kweli mimi nawabatiza kwa maji kwa ajili ya toba; bali yeye ajaye nyuma yangu ana nguvu kuliko mimi, wala sistahili hata kuvichukua viatu vyake; yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.  Ambaye pepeto lake li mkononi mwake, naye atausafisha sana uwanda wake; na kuikusanya ngano yake ghalani, bali makapi atayateketeza kwa moto usiozimika.”

Marko 1:7-8 “Akahubiri akisema, Yuaja nyuma yangu aliye na nguvu kuliko mimi, ambaye mimi sistahili kuinama na kuilegeza gidamu ya viatu vyake. Mimi niliwabatiza kwa maji; bali yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu.”

Luka 3:16-17 “Yohana alijibu akawaambia wote, Kweli mimi nawabatiza kwa maji; lakini yuaja mtu mwenye nguvu kuliko mimi, ambaye mimi sistahili kuilegeza gidamu ya viatu vyake; yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto; ambaye pepeo lake li mkononi mwake, naye atausafisha sana uwanda wake, na kuikusanya ngano ghalani mwake, bali makapi atayateketeza kwa moto usiozimika.”  

Madhehebu mbalimbali ya Kikristo yanatafasiri ubatizo wa Roho Mtakatifu katika mitazamo tofauti tofauti kulingana na elimu zao za kitheolojia (Experimental Theology)

1.       Wapentekoste na wanacharismatic - kuwa ubatizo huu unatokea kwa mtu aliyeokoka yaani aliyemuamini Bwana Yesu na kumkubali kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yake na, kufuatiwa na kupokea uwepo na nguvu za Roho Mtakatifu ambazo kimsingi zinathibitishwa na kunena kwa lugha mpya hii ndio alama ya kwanza inayothibitisha uwepo wa Roho wa Mungu ndani ya mtu na umuhimu wa kuishi maisha yenye nguvu za Roho Mtakatifu na kupelekea kuwa bora katika nia zetu za kuabudu na kumtumukia Mungu.

 

2.       Madhehebu ya kiinjili na kiprotestant - wao wanaamini kuwa ubatizo huu unatokea mara tu mtu anapokuwa amempokea Yesu, mara mtu anapompokea Yesu, wanaamini kuwa ni kazi ya Roho Mtakatifu kusababisha kuzaliwa upya kwa mtu huyo na hivyo anakaa ndani yake na hawaamini kuwa wokovu na uwepo wa Roho au Ubatizo wa Roho Mtakatifu ni vitu vinaweza kutenganishwa.

 

3.       Wakatoliki  na waanglikana wa High Church wanaamini kumpokea Roho Mtakatifu tu ni tukio la kisakrament (Kipaimara), wao wanaona kuwa uwepo wa Roho Mtakatifu ni tukio endelevu la maisha ya kila siku na tukio la kukua na kukomaa katika utakatifu na huduma.               

 

Kibiblia ubatizo huu wa Roho Mtakatifu ni moja ya ahadi Muhimu sana aliyoiahidi Mungu baba na Bwana wetu Yesu Kristo, ambapo wanafunzi wa Yesu Kristo walipaswa kusubiri kwanza pale Yerusalem mpaka wavikwe uwezo huu kutoka mbinguni.

Luka 24:49 “Na tazama, nawaletea juu yenu ahadi ya Baba yangu; lakini kaeni humu mjini, hata mvikwe uwezo utokao juu.”     

Matendo 1:4-5, 8 “Hata alipokuwa amekutana nao aliwaagiza wasitoke Yerusalemu, bali waingoje ahadi ya Baba, ambayo mlisikia habari zake kwangu; ya kwamba Yohana alibatiza kwa maji, bali ninyi mtabatizwa katika Roho Mtakatifu baada ya siku hizi chache.8 Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi.”

Kwa hiyo unaweza kuona kuwa ni ubatizo wa ahadi kimaandiko na ni tukio ambalo Yesu aliwaelekeza wanafunzi wake kulisubiria na Yesu alilitofautisha na wokovu pamoja na ubatizo wa maji,  na wanafunzi wa Yesu walisubiria ahadi hii  na walijazwa au walibatizwa kwa  Roho Mtakatifu na kuanza kusema kwa lugha nyingine.

Matendo 2:1-4 “Hata ilipotimia siku ya Pentekoste walikuwako wote mahali pamoja. Kukaja ghafula toka mbinguni uvumi kama uvumi wa upepo wa nguvu ukienda kasi, ukaijaza nyumba yote waliyokuwa wameketi. Kukawatokea ndimi zilizogawanyikana, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao. Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema kwa lugha nyingine, kama Roho alivyowajalia kutamka.”

Haikuishia hapo tu kwani baadaye tunawaona wanafunzi wakiwa na mabadiliko makubwa sana wakiwa pia na karama na vipawa mbalimbali na wakimtumikia Mungu kwa nguvu na ujasiri mwingi pia wakiwa moto sana kuanzia Matendo 3 na kuendelea, jambo lililopelekea watu wengi kuokoka na kukua kwa kanisa na uhai wa kanisa unaoendelea mpaka leo.

Kwa msingi huo basi leo tutachukua Muda kujifunza kwa kina na mapana na marefu kuhusu Ubatizo wa Roho Mtakatifu kwa kuzingatia vipengele muhimu vitatu vifuatavyo:-



·         Maana ya ubatizo wa Roho Mtakatifu.

·         Mtu aliyebatizwa kwa Roho Mtakatifu.

·         Jinsi ya kupokea Ubatizo wa Roho Mtakatifu.



Maana ya ubatizo wa Roho Mtakatifu;

Maandiko yanatufundisha ya kuwa kila mtu aliyeokolewa anakuwa na Roho Mtakatifu ndani yake, hii ni kwa sababu tukio zima la mtu kumkiri Yesu na kumpokea kama bwana na mwokozi kupitia kazi aliyoifanya Msalabani ni tukio linalosababishwa na Roho Mtakatifu, kwa hiyo kuzaliwa mara ya pili ni kuzaliwa kwa roho na kuungwa katika mwili wa Kristo, kwa Msingi huo basi ni muhimu kufahamu kuwa, Ndani ya kila mtu aliyeokolewa Roho wa Mungu yupo na hivyo kila aaminiye amefanyika kuwa mali ya Mungu.

Yohana 16:7-11 “Lakini mimi nawaambia iliyo kweli; yawafaa ninyi mimi niondoke, kwa maana mimi nisipoondoka, huyo Msaidizi hatakuja kwenu; bali mimi nikienda zangu, nitampeleka kwenu. Naye akiisha kuja, huyo atauhakikisha ulimwengu kwa habari ya dhambi, na haki, na hukumu. Kwa habari ya dhambi, kwa sababu hawaniamini mimi; kwa habari ya haki, kwa sababu mimi naenda zangu kwa Baba, wala hamnioni tena; kwa habari ya hukumu, kwa sababu yule mkuu wa ulimwengu huu amekwisha kuhukumiwa.”

Warumi 8:9 “Lakini ikiwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu, ninyi hamwufuati mwili; bali mwaifuata roho. Lakini mtu awaye yote asipokuwa na Roho wa Kristo, huyo si wake.”

Wagalatia 4:5-6 “Na kwa kuwa ninyi mmekuwa wana, Mungu alimtuma Roho wa Mwanawe mioyoni mwetu, aliaye, Aba, yaani, Baba. Kama ni hivyo, wewe si mtumwa tena bali u mwana; na kama u mwana, basi, u mrithi kwa Mungu.”

Wakati huu Roho Mtakatifu atafanya kazi na mwamini katika kiwango tofauti tofauti kwa kadiri ya neema ya Mungu ndani ya waamini, viwango hivi ni sawa na ngazi za ujazo wa maji kutoka kiwango kimoja hadi kiwango kingine, viwango hivyo vinachangiwa na utii, kujitoa, maombi, kufunga na maisha kwa ujumla ambapo kila mmoja anakuwa na kiwango chake viwango hivi tunaweza kuelezea vizuri kwa kutumia maono ya mfano wa nabii Ezekiel.

Ezekiel 47:1-5 “Baadaye akanileta tena mpaka lango la nyumba; na tazama, maji yalitoka chini ya kizingiti cha nyumba, kwa njia ya mashariki, maana upande wa mbele wa nyumba ulielekea upande wa mashariki; nayo maji yakashuka toka chini ya upande wa kuume wa nyumba, upande wa kusini wa madhabahu. Ndipo akanileta nje kwa njia ya lango upande wa kaskazini, akanizungusha kwa njia ya nje mpaka lango la nje, kwa njia yake iliyoelekea mashariki; na tazama, maji yalitoka upande wa kuume. Na alipotoka mtu yule, mwenye uzi wa kupimia mkononi mwake, kwenda masharikini, akapima dhiraa elfu, akanivusha maji yale; maji yakafika mpaka viweko vya miguu. Kisha akapima dhiraa elfu, akanivusha maji yale, maji yakafika mpaka magoti. Kisha akapima dhiraa elfu, akanivusha, maji yakafika mpaka viuno. Kisha akapima dhiraa elfu, yakawa mto nisioweza kuuvuka; maana maji yamezidi, maji ya kuogelea, mto usiovukika.”

Ezekiel Katika maono haya anajaribu kuelezea kiwango au viwango mbalimbali vya ujazo wa Roho Mtakatifu kutofautisha na ubatizo wa Roho Mtakatifu, viwango hivyo vinategemeana na ukuaji wa kila mwamini kutoka hatua moja kwenda hatua nyingine, na kila mwamini anaweza kuongezea kiwango chake yeye mwenyewe kwa kujitoa kwa Mungu kwa hiyo uko uhusiano wa ukuaji wa kiroho na ujazo wa Roho Mtakatifu, mfano ni kutoka maji ya kiwango cha viwiko vya miguu, kisha maji ya magotini, kisha maji ya kiunoni, kisha mto usioweza kuvukika  Ezekiel alikuwa anazungumzia ukuaji wa kiroho wa muumini na uhusiano wake na ujazo wa Roho Mtakatifu, kwa hiyo mtu anaweza kuwa na Roho Mtakatifu tangu alipookoka kwa sehemu, lakini akawa hajajazwa au hajabatizwa katika kiwango cha kufurika ambacho ndio kinaitwa Ubatizo. Mtu anayebatizwa kwa Roho Mtakatifu ni mtu mwingine ni mtu wa tofauti sana ni mtu wa viwango vya juu sana , ni mtu ambaye uungu unakaa ndani yake kama tutakavyoona.

Wanafunzi wa Yesu walikuwa na kiwango cha uwepo wa Roho Mtakatifu wakati wakiwa na Yesu Kristo, kwa hiyo yako mambo waliweza kuyafanya, lakini katika kiwango cha chini na cha kawaida mfano kutoa Pepo, kufunuliwa kumjua Yesu, kusikiliza mafundisho yake na kadhalika walimpokea Roho Mtakatifu kwa sehemu, kwa hiyo walifanya kazi mbalimbali za Mungu kwa kiwango hicho.

Yohana 20:21-22 “Basi Yesu akawaambia tena, Amani iwe kwenu; kama Baba alivyonituma mimi, mimi nami nawapeleka ninyi. Naye akiisha kusema hayo, akawavuvia, akawaambia, Pokeeni Roho Mtakatifu.”

Luka 9:1-2 “Akawaita wale Thenashara, akawapa uwezo na mamlaka juu ya pepo wote na kuponya maradhi. Akawatuma wautangaze ufalme wa Mungu, na kupoza wagonjwa.”

Luka 10:1,17-19 “1.Basi, baada ya hayo Bwana aliweka na wengine, sabini, akawatuma wawili wawili wamtangulie kwenda kila mji na kila mahali alipokusudia kwenda mwenyewe.” 17-19 “Ndipo wale sabini waliporudi kwa furaha, wakisema, Bwana, hata pepo wanatutii kwa jina lako. Akawaambia, Nilimwona Shetani, akianguka kutoka mbinguni kama umeme. Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru.”

Mathayo 16:15-17 “Akawaambia, Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani? Simoni Petro akajibu akasema, Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai. Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni”  

Kwa hiyo utaweza kuona kuwa wanafunzi wa Yesu walipokea Roho Mtakatifu wakati wakiwa na Yesu, walitumwa kuhubiri, walitoa pepo, walitetemesha utawala wa shetani, waliweza pia kupokea mafunuo mbalimbali kwa sababu walikuwa na Roho wa Mungu ndani yao, na Yesu aliwatumia lakini ilikuwa katika kiwango cha chini sana, kiwango cha kawaida na ni wanafunzi hao hao Yesu anawagiza wasianze kuifanya kazi hiyo mpaka wamepokea uwezo kutoka juu, mpaka wamejiliwa na Roho Mtakatifu, mpaka wamebatizwa kwa Roho Mtakatifu ona

Luka 24:49 “Na tazama, nawaletea juu yenu ahadi ya Baba yangu; lakini kaeni humu mjini, hata mvikwe uwezo utokao juu.”     

Matendo 1:4-5, 8 “4-5,Hata alipokuwa amekutana nao aliwaagiza wasitoke Yerusalemu, bali waingoje ahadi ya Baba, ambayo mlisikia habari zake kwangu; ya kwamba Yohana alibatiza kwa maji, bali ninyi mtabatizwa katika Roho Mtakatifu baada ya siku hizi chache.” 8 “Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi.”

Kwa hiyo ubatizo wa Roho Mtakatifu ni zaidi ya ujazo, ni zaidi ya kuvikwa, ni zaidi ya kupokea, ujazo una viwango vya viwiko, magoti, kiuno, lakini ubatizo unahusisha maji yasiyovukika ni aidha uzame na ufie humo uzikwe humo, mtu anapobatizwa kwa maji huwa anazamishwa analowekwa kila kitu chake mwili wake, nafsi yake, roho yake na mpaka nguo zake analowa chapa chapa, anafia kwenye maji anazikwa kwenye maji, anazamishwa, kwa hiyo ubatizo wa Roho Mtakatifu maana yake ni nini  Neno ubatizo linatusaidia kwa sehemu kujua kinachozungumzwa hapo katika lugha ya kibiblia !

Neno ubatizo limetokana na neno la kiingereza Baptism ambalo kwa asili limetokana na neno la Kiyunani cha zamani Baptizein ambalo maana yake kuzamisha to immerse, dip in water, kuzamisha katika maji, kwa hiyo neno hilo ubatizo wa Roho Mtakatifu maana yake ni kuzamishwa katika Roho Mtakatifu!, aidha nguo za kitani nyeupe zilipokuwa zikilowekwa ili zipate rangi ya zambarau au nyekundu, zilizamishwa katika maji yaliyochemka na rangi hiyo na kutoka nguo hiyo ikiwa imebadilika rangi, yaani nguo ya kitani ingepoteza rangi yake nyeupe na kuwa na rangi ambayo nguo hiyo imechovya, kitendo hicho pia kinaitwa ubatizo, sasa maana ile ile inayotumika katika ubatizo wa maji sasa ndio inatumika katika ubatizo wa Roho Mtakatifu, kwa hiyo nawashauri walimu wa neno la Mungu kutumia neno ubatizo zaidi kuliko ujazo, au kuvikwa au kupokea nguvu au kujaa Roho Mtakatifu, japokuwa maneno hayo yote Ujazo na kuvikwa na kupokea yana maana moja lakini msamiati ulio bora zaidi utumike kubatizwa.

Kwa hiyo Neno ubatizo linapotumika pamoja na Roho Mtakatifu maana yake ni ile ile kuzamishwa katika Roho kwa hiyo kila kitu cha mtu anayebatizwa katika Roho Mtakatifu kina uwepo wa Mungu mtu analowa Roho Mtakatifu kwenye kila kitu mwili wake, nasfi yake, mavazi yake, mawazo yake, sauti yake, kivuli chake, jasho lake kila kitu, anafia ndani ya Roho Mtakatifu anabobea analowa maana yake mpaka mifupa ya mtu mwenye Roho wa Mungu ina jaa uwepo wa Mungu ndio maana Elisha alipokufa watu, walitupia mwili katika kaburi lake na ule mwili ulipogusa mifupa ya Elisha ukafufuka angalia:-

2Wafalme 13:20-21 “Elisha akafa, nao wakamzika. Basi vikosi vya Wamoabi wakaingia katika nchi mwanzo wa mwaka. Ikawa, walipokuwa wakimzika mtu, angalia, waliona kikosi; wakamtupa yule mtu kaburini mwa Elisha; mara yule maiti alipoigusa mifupa ya Elisha, alifufuka, akasimama kwa miguu.”

Kwa hiyo mtu aliyebatizwa kwa Roho Mtakatifu sio mtu wa kawaida, hawi wa kawaida, anaweza kupigwa mawe na akavumilia, hawi yeye anayeishi, anaweza kupaa kwenda mji mwingine, anaweza hata kivuli chake kikasababisha miujiza kwa sababu kila kitu kimelowa uwepo wa Mungu, wakati mwingine hata mazingira ya mtu aliyebatizwa kwa Roho Mtakatifu huwa na uwepo wa Roho Mtakatifu, Ubatizo wa Roho Mtakatifu ni kiwango cha maji yasiyovukika, unazama, unalowa, unapoteza uhai unapotea huwi wa ulimwengu huu hata kidogo watu wanaweza kudhani miungu imewashukia kwa jinsi ya kibinadamu sijui unanielewa?

Matendo 14:8-15 “Na huko Listra palikuwa na mtu mmoja, dhaifu wa miguu, kiwete tangu tumboni mwa mamaye, ambaye hajaenda kabisa. Mtu huyo alimsikia Paulo alipokuwa akinena; ambaye akamkazia macho na kuona ya kuwa ana imani ya kuponywa, akasema kwa sauti kuu, Simama kwa miguu yako sawasawa. Akasimama upesi akaenda. Na makutano walipoona aliyoyafanya Paulo wakapaza sauti zao, wakisema kwa Kilikaonia, Miungu wametushukia kwa mifano ya wanadamu. Wakamwita Barnaba, Zeu, na Paulo, Herme, kwa sababu ndiye aliyekuwa mnenaji. Kuhani wa Zeu ambaye hekalu lake lilikuwa mbele ya mji, akaleta ng'ombe na taji za maua hata malangoni, akitaka kutoa dhabihu pamoja na makutano. Walakini mitume Barnaba na Paulo, walipopata habari, wakararua nguo zao, wakaenda mbio wakaingia katika makutano, wakipiga kelele, wakisema, Akina bwana, mbona mnafanya haya? Sisi nasi tu wanadamu hali moja na ninyi; twawahubiri habari njema, ili mgeuke na kuyaacha mambo haya ya ubatili na kumwelekea Mungu aliye hai, aliyeumba mbingu na nchi na bahari na vitu vyote vilivyomo;”

Kwa hiyo watu waliobatizwa kwa Roho Mtakatifu wana kitu cha ziada  na ndio maana hata lugha inaweza kubadilika na wakaanza kusema kwa lugha mpya kwa nini uwepo wa Mungu unashuka katika kile eneo la mtu aliyebatizwa kwa Roho Mtakatifu, hiyo ndio maana ya ubatizo wa Roho Mtakatifu. Kama ukichukua chupa iliyojaa maji unakitumia kama kielelezo cha ujazo wa Roho Mtakatifu maana yake ujazo wa chupa hautoshi kuelezea ubatizo wa Roho Mtakatifu maana yake ni nini maana yake Roho anakuwepo mpaka kwenye chupa yenyewe na kifuniko chake !


Mtu aliyebatizwa kwa Roho Mtakatifu:

1.       Anakuwa na uhusiano wa ndani sana na Mungu – Kwa kawaida mtu ambaye amebatizwa kwa Roho Mtakatifu anaumbiwa kiu na hamu na shauku ya kuwa na uhusiano wa ndani sana na Mungu na kiu yake ya kumtafuta Mungu inakuwa kubwa anaweza kujisikia kuendelea kuutafuta uso wa Mungu hata kama ibada ya kawaida imeisha, wao watataka kuongea na Mungu watatafakari, wanakuwa kama hawana kiasi katika swala la kuutafuta uso wa Mungu wanakaa muda mrefu sana kwenye maombi, kiu yao ni uwepo wa Mungu.Roho wa Mungu ndani yao anawapa neema ya kuomba kwa kuugua kama waombolezaji.

 

a.       Yoshua Mwana wa Nuni: Kutoka 33:10-11 “Watu wote wakaiona nguzo ya wingu ikisimama penye mlango wa hema; watu wote wakaondoka wakasujudu, kila mtu mlangoni pa hema yake.Naye BWANA akasema na Musa uso kwa uso, kama vile mtu asemavyo na rafiki yake. Kisha akageuka akarejea hata maragoni; bali mtumishi wake Yoshua, mwana wa Nuni, naye ni kijana, hakutoka mle hemani.”

 

b.      Daudi – Zaburi 27:1-6 “Bwana ni nuru yangu na wokovu wangu, Nimwogope nani? Bwana ni ngome ya uzima wangu, Nimhofu nani? Watenda mabaya waliponikaribia, Wanile nyama yangu, Watesi wangu na adui zangu, Walijikwaa wakaanguka. Jeshi lijapojipanga kupigana nami, Moyo wangu hautaogopa. Vita vijaponitokea, Hata hapo nitatumaini. Neno Moja nimelitaka kwa Bwana, Nalo ndilo nitakalolitafuta, Nikae nyumbani mwa Bwana Siku zote za maisha yangu, Niutazame uzuri wa Bwana, Na kutafakari hekaluni mwake.”

       

c.       Daniel: Daniel 6:4-11 “Basi mawaziri na maamiri wakatafuta sana kupata sababu za kumshitaki Danieli kwa habari za mambo ya ufalme; lakini hawakuweza kuona sababu wala kosa; kwa maana alikuwa mwaminifu, wala halikuonekana kosa wala hatia ndani yake. Ndipo wale watu wakasema, Hatutapata sababu ya kumshitaki Danieli huyo, tusipoipata katika mambo ya sheria ya Mungu wake. Basi wale mawaziri na maamiri wakakusanyika pamoja mbele ya mfalme, wakamwambia hivi, Mfalme Dario, uishi milele.  Mawaziri wote wa ufalme, na manaibu, na maamiri, na madiwani, na maliwali wamefanya shauri pamoja ili kuweka amri ya kifalme; na kupiga marufuku, ya kwamba mtu ye yote atakayeomba dua kwa Mungu awaye yote, au kwa mtu awaye yote, katika muda wa siku thelathini, ila kwako, Ee mfalme atatupwa katika tundu la simba. Sasa, Ee mfalme, piga marufuku, ukatie sahihi maandiko haya, yasibadilike, kama ilivyo sheria ya Wamedi na Waajemi, isiyoweza kubadilika. Basi mfalme Dario akayatia sahihi maandiko yale, na ile marufuku. Hata Danieli, alipojua ya kuwa yale maandiko yamekwisha kutiwa sahihi, akaingia nyumbani mwake, (na madirisha katika chumba chake yalikuwa yamefunguliwa kukabili Yerusalemu ;) akapiga magoti mara tatu kila siku, akasali, akashukuru mbele za Mungu wake, kama alivyokuwa akifanya tokea hapo. Basi watu hao wakakusanyika pamoja, wakamwona Danieli akiomba dua, na kusihi mbele za Mungu wake.”

 

d.      Paulo mtume na timu yake ya umisheni: Matendo 16:12-16 “na kutoka hapo tukafika Filipi, mji wa Makedonia, mji ulio mkuu katika jimbo lile, mahali walipohamia Warumi; tukawa katika mji huu, tukikaa siku kadha wa kadha. Hata siku ya sabato tukatoka nje ya lango, tukaenda kando ya mto, ambapo tukadhani ya kuwa pana mahali pa kusali; tukaketi, tukasema na wanawake waliokutana pale. Mwanamke mmoja, jina lake Lidia, mwenye kuuza rangi ya zambarau, mwenyeji wa Thiatira, mcha Mungu, akatusikiliza, ambaye moyo wake ulifunguliwa na Bwana, ayatunze maneno yaliyonenwa na Paulo. Hata alipokwisha kubatizwa, yeye na nyumba yake, akatusihi, akisema, Kama mmeniona kuwa mwaminifu kwa Bwana, ingieni nyumbani mwangu mkakae. Akatushurutisha.Ikawa tulipokuwa tukienda mahali pale pa kusali, kijakazi mmoja aliyekuwa na pepo wa uaguzi akatukuta, aliyewapatia bwana zake faida nyingi kwa kuagua.”

 

e.       Watu wa Mungu - Zekaria 12:10 “Nami nitawamwagia watu wa nyumba ya Daudi, na wenyeji wa Yerusalemu, roho ya neema na kuomba; nao watamtazama yeye ambaye walimchoma; nao watamwombolezea, kama vile mtu amwombolezeavyo mwanawe wa pekee; nao wataona uchungu kwa ajili yake, kama vile mtu aonavyo uchungu kwa ajili ya mzaliwa wake wa kwanza.”

 

2.       Wanasumbuliwa sana kueneza injili: - Mtu aliyebatizwa kwa Roho Mtakatifu ndani yake kunakuwa na kiu ya kutaka kuieneza injili, kwa wengine hawahisi utulivu mioyoni mwao wanawiwa kwa hiyo wanasukumwa kushuhudia, wanasukumwa kulisema neno la Mungu na hawawezi kukaa kimya

 

a.       Matendo 17:14-17 “Mara hiyo wale ndugu wakampeleka Paulo aende zake mpaka pwani; bali Sila na Timotheo wakasalia huko. Lakini wale waliomsindikiza Paulo wakampeleka mpaka Athene; nao wakiisha kupokea maagizo kuwapelekea Sila na Timotheo, ya kwamba wasikawie kumfuata, wakaenda zao. Paulo alipokuwa akiwangojea huko Athene na kuona jinsi mji ule ulivyojaa sanamu, roho yake ilichukizwa sana ndani yake. Basi katika sinagogi akahojiana na Wayahudi na waliomcha Mungu, na wale waliokutana naye sokoni kila siku.”

 

b.      Apolo Matendo 18:24-26 “Basi Myahudi mmoja, jina lake Apolo, mzalia wa Iskanderia, mtu wa elimu, akafika Efeso; naye alikuwa hodari katika maandiko. Mtu huyo alikuwa amefundishwa njia ya Bwana; na kwa kuwa roho yake ilikuwa ikimwaka, alianza kunena na kufundisha kwa usahihi habari za Yesu; naye alijua ubatizo wa Yohana tu. Akaanza kunena kwa ujasiri katika sinagogi; hata Prisila na Akila walipomsikia wakamchukua kwao, wakamweleza njia ya Bwana kwa usahihi zaidi.”

 

3.       Wanakuwa na uwezo mkubwa sana wa kukabiliana na changamoto – Mtu aliyebatizwa kwa Roho Mtakatifu anakuwa na uwezo mkubwa sana wa kukabiliana na changamoto yoyote inayokuja mbele zake na haogopi kitu na wako tayari hata kufa kwaajili ya injili

 

a.       Matendo 21:10-13 “Basi tulipokuwa tukikaa huko siku nyingi, nabii mmoja jina lake Agabo akashuka kutoka Uyahudi. Alipotufikia akautwaa mshipi wa Paulo, akajifunga miguu na mikono, akasema, Roho Mtakatifu asema hivi, Hivyo ndivyo Wayahudi wa Yerusalemu watakavyomfunga mtu mwenye mshipi huu, nao watamtia katika mikono ya watu wa Mataifa. Basi tuliposikia haya, sisi na watu wa mahali pale, tukamsihi asipande kwenda Yerusalemu. Ndipo Paulo alipojibu, Mnafanya nini, kulia na kunivunja moyo? Kwa maana mimi, licha ya kufungwa, ni tayari hata kuuawa katika Yerusalemu kwa ajili ya jina lake Bwana Yesu.”

 

b.      Matendo 4:18-20 “Wakawaita, wakawaamuru wasiseme kabisa wala kufundisha kwa jina la Yesu.Petro na Yohana wakawajibu wakawaambia, Kwamba ni haki mbele za Mungu kuwasikiliza ninyi kuliko Mungu, hukumuni ninyi wenyewe; maana sisi hatuwezi kuacha kuyanena mambo tuliyoyaona na kuyasikia.”          

 

4.       Wanafanya mambo makubwa ya kushangaza na kupita kawaida – watu waliobatizwa kwa Roho Mtakatifu wanakuwa na karama na vipawa na uweza wa kiungu unaowawezesha kufanya mambo ya kutisha na kushangaza katika viwango vikubwa sana

 

a.       Matendo 5:12-15 “Na kwa mikono ya mitume zikafanyika ishara na maajabu mengi katika watu; nao wote walikuwako kwa nia moja katika ukumbi wa Sulemani; na katika wote wengine hapana hata mmoja aliyethubutu kuambatana nao; ila watu waliwaadhimisha; walioamini wakazidi kuongezeka kwa Bwana, wengi, wanaume na wanawake; hata ikawa katika njia kuu hutoa nje wagonjwa, na kuwaweka juu ya majamvi na magodoro, ili Petro akija, ngawa kivuli chake kimwangukie mmojawapo wao.”           

 

b.      Matendo 6:8-10 “Na Stefano, akijaa neema na uwezo, alikuwa akifanya maajabu na ishara kubwa katika watu.Lakini baadhi ya watu wa sinagogi lililoitwa sinagogi la Mahuru, na la Wakirene, na la Waiskanderia, na la wale wa Kilikia na Asia, wakaondoka na kujadiliana na Stefano; lakini hawakuweza kushindana na hiyo hekima na huyo Roho aliyesema naye.”

 

c.       Matendo 19:11-12 “Mungu akafanya kwa mikono ya Paulo miujiza ya kupita kawaida; hata wagonjwa wakaletewa leso na nguo zilizotoka mwilini mwake, magonjwa yao yakawaondokea, pepo wachafu wakawatoka.”

 

d.      Paulo na Barnaba – Matendo 17:2-6 “Na Paulo, kama ilivyokuwa desturi yake, akaingia mle walimo, akahojiana nao kwa maneno ya maandiko sabato tatu, akiyafunua na kuwaeleza ya kwamba ilimpasa Kristo kuteswa, na kufufuka katika wafu; na ya kwamba, Yesu huyu ninayewapasha ninyi habari zake ndiye Kristo. Wengine miongoni mwao wakaamini, wakashikamana na Paulo na Sila; na Wayunani waliomcha Mungu, wengi sana, na wanawake wenye cheo si wachache. Na Wayahudi wakaona wivu, wakajitwalia watu kadha wa kadha katika watu ovyo wasio na sifa njema, nao wakakutanisha mkutano, wakafanya ghasia mjini, wakawaendea watu wa nyumba ya Yasoni, wakataka kuwapeleka mbele ya watu wa mji; na walipowakosa, wakamkokota Yasoni na baadhi ya ndugu mbele ya wakubwa wa mji, wakipiga kelele, wakisema, Watu hawa walioupindua ulimwengu wamefika huku nako,”

 

5.       Watu waliobatizwa kwa Roho Mtakatifu wanakuwa na ukarimu na uwezo wa kujitoa kwa hali ya juu, wanauwezo wa kutoa mali zao kwaajili ya injili, hutumii nguvu wala ushawishi kuwataka watoe, wanajua kujitoa, ukiona ni mpaka upige sarakasi ndio watu wajitoe ujue watu hao bado maji yao ni ya kisigino bado hayajajaa

 

a.       Matendo 4:31-37 “Hata walipokwisha kumwomba Mungu, mahali pale walipokusanyika pakatikiswa, wote wakajaa Roho Mtakatifu, wakanena neno la Mungu kwa ujasiri. Na jamii ya watu walioamini walikuwa na moyo mmoja na roho moja; wala hapana mmoja aliyesema ya kuwa kitu cho chote alicho nacho ni mali yake mwenyewe; bali walikuwa na vitu vyote shirika. Na mitume wakatoa ushuhuda wa kufufuka kwake Yesu kwa nguvu nyingi, na neema nyingi ikawa juu yao wote. Wala hapakuwa na mtu mmoja miongoni mwao mwenye mahitaji; kwa sababu watu wote waliokuwa na viwanja au nyumba waliviuza, wakaileta thamani ya vitu vile vilivyouzwa, wakaiweka miguuni pa mitume; kila mtu akagawiwa kwa kadiri ya alivyohitaji.Na Yusufu, aliyeitwa na mitume Barnaba, (maana yake, Mwana wa faraja), Mlawi, asili yake ni mtu wa Kipro, alikuwa na shamba akaliuza, akaileta fedha, akaiweka miguuni pa mitume.”

 

b.      Wafilipi 4:15-19 “Nanyi pia, ninyi wenyewe mnajua, enyi Wafilipi, ya kuwa katika mwanzo wa Injili, nilipotoka Makedonia, hakuna kanisa lingine lililoshirikiana nami katika habari hii ya kutoa na kupokea, ila ninyi peke yenu. Kwa kuwa hata huko Thesalonike mliniletea msaada kwa mahitaji yangu, wala si mara moja. Si kwamba nakitamani kile kipawa, bali nayatamani mazao yanayozidi kuwa mengi, katika hesabu yenu. Lakini ninavyo vitu vyote na kuzidi, tena nimejaa tele; nimepokea kwa mkono wa Epafrodito vitu vile vilivyotoka kwenu, harufu ya manukato, sadaka yenye kibali, impendezayo Mungu. Na Mungu wangu atawajazeni kila mnachokihitaji kwa kadiri ya utajiri wake, katika utukufu, ndani ya Kristo Yesu.”          

 

6.       Hawasumbuliwi na wachawi  na badala yake wao ndio huwa juu ya wachawi

 

a.       Wagalatia 5:18-21 Lakini mkiongozwa na Roho, hampo chini ya sheria. Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi, ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.”

       

b.      Matendo 8:5-13 “Filipo akatelemka akaingia mji wa Samaria, akawahubiri Kristo. Na makutano kwa nia moja wakasikiliza maneno yale yaliyosemwa na Filipo walipoyasikia na kuziona ishara alizokuwa akizifanya. Kwa maana pepo wachafu wakawatoka wengi waliopagawa nao, wakilia kwa sauti kuu; na watu wengi waliopooza, na viwete, wakaponywa. Ikawa furaha kubwa katika mji ule. Na mtu mmoja, jina lake Simoni, hapo kwanza alikuwa akifanya uchawi katika mji ule, akiwashangaza watu wa taifa la Wasamaria, akisema ya kuwa yeye ni mtu mkubwa. Wote wakamsikiliza tangu mdogo hata mkubwa, wakisema, Mtu huyu ni uweza wa Mungu, ule Mkuu. Wakamsikiliza, kwa maana amewashangaza muda mwingi kwa uchawi wake. Lakini walipomwamini Filipo, akizihubiri habari njema za ufalme wa Mungu, na jina lake Yesu Kristo, wakabatizwa, wanaume na wanawake. Na yeye Simoni mwenyewe aliamini akabatizwa, akashikamana na Filipo; akashangaa alipoziona ishara na miujiza mikubwa inayotendeka.”

       

c.       Matendo 19:17-21 “Habari hii ikajulikana na Wayahudi wote na Wayunani waliokaa Efeso, hofu ikawaingia wote, na jina la Bwana Yesu likatukuzwa. Na wengi wa wale walioamini wakaja wakaungama, wakidhihirisha matendo yao. Na watu wengi katika wale waliotumia mambo ya uganga wakakusanya vitabu vyao, wakavichoma moto mbele ya watu wote; wakafanya hesabu ya thamani yake, wakaona ya kwamba yapata fedha hamsini elfu. Hivyo ndivyo neno la Bwana lilivyozidi na kushinda kwa nguvu. Mambo hayo yalipokwisha kumalizika, Paulo akaazimu rohoni mwake, akiisha kupita katika Makedonia na Akaya, aende Yerusalemu, akisema, Baada ya kuwako huko, yanipasa kuuona na Rumi pia.”


 Jinsi ya kupokea Ubatizo wa Roho Mtakatifu.

1.       Fahamu ya kuwa anayebatiza kwa Roho Mtakatifu Ni Bwana Yesu mwenyewe, Na ubatizo huu ni mpango wa Mungu, ni ahadi ya Mungu kwa waaminio kwa hiyo kila mmoja anastahili kupokea kwa Imani na kufungua moyo wake kuhakikisha kuwa maisha yake yanajaa na kufunikwa na uwepo wa Mungu Roho Mtakatifu sawa na neno lake lisemavyo:-

 

a.       Mathayo 3:11 “Kweli mimi nawabatiza kwa maji kwa ajili ya toba; bali yeye ajaye nyuma yangu ana nguvu kuliko mimi, wala sistahili hata kuvichukua viatu vyake; yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.”

 

b.      Ubatizo huu ni ahadi ya Mungu mwenyewe kwa kila mtu amwaminiye

Yoel 2:28 “Hata itakuwa, baada ya hayo, ya kwamba nitamimina roho yangu juu ya wote wenye mwili; na wana wenu, waume kwa wake, watatabiri, wazee wenu wataota ndoto, na vijana wenu wataona maono;”

       

Luka 24:49 “Na tazama, nawaletea juu yenu ahadi ya Baba yangu; lakini kaeni humu mjini, hata mvikwe uwezo utokao juu.”

 

Matendo 2:38-39 “Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu. Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie.”

 

c.       Lazima uwe na nia ya kutumika – Ubatizo wa Roho Mtakatifu ni kwaajili ya utumishi, Roho wa Mungu anatabia ya kutaharakisha watu kwaajili ya utumishi, Pale tunapokuwa tayari kwa huduma na kukubali kutumika huku na huko Roho Mtakatifu atakuwa radhi nasi, Ubatizo huu hauwafai watu ambao wakataa tu, unawafaa watu ambao wako tayari kwa kazi kwa sababu Roho Hatakupa kutulia

 

Waamuzi 13:24-25 “Basi yule mwanamke akamzaa mtoto mwanamume akamwita jina lake Samsoni, mtoto huyu akakua, Bwana akambarikia. Roho ya Bwana ikaanza kumtaharakisha katika Mahane-dani, katikati ya Sora na Eshtaoli.”

 

Yeremia 47:6-7 “Ee upanga wa Bwana, Siku ngapi zitapita kabla hujatulia? Ujitie katika ala yako; Pumzika, utulie. Utawezaje kutulia, Ikiwa Bwana amekupa agizo? Juu ya Ashkeloni na juu ya pwani, Ndipo alipoyaamuru hayo.”

 

d.      Kwa maombi bila kuchoka

Luka 18:9-13 “Nami nawaambia, Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa. Kwa kuwa kila aombaye hupokea; naye atafutaye huona; naye abishaye atafunguliwa. Maana ni yupi kwenu aliye baba, ambaye mwanawe akimwomba mkate, atampa jiwe au samaki, badala ya samaki atampa nyoka? Au akimwomba yai, atampa nge? Basi, ikiwa ninyi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! Baba aliye mbinguni hatazidi sana kuwapa Roho Mtakatifu hao wamwombao?

 

e.      Lazima uwe na imani

Maswala yote ya kiroho yanapokelewa kwa Imani, wakati wote mt akiwa na mashaka hawezi kupokea kitu kutoka kwa Mungu, kwani pasipo Imani haiwezekani kumpendeza Mungu, kwa hiyo Mtu anayemuhitaji Roho wa Mungu ni lazima aombe kwa Imani,

 

Waebrania 11:6 “Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao.”

 

Wagalatia 3:2 “Nataka kujifunza neno hili moja kwenu. Je! Mlipokea Roho kwa matendo ya sheria, au kwa kusikia kunakotokana na imani?

 

Kwa hiyo baada ya kujifunza namna hii na kusikia neno la Mungu kuhusu Ubatizo wa Roho Mtakatifu unapaswa kuamini na kuatendea kazi yale yote ambayo umeyasikia na ninakuhakikishia hutakuwa ulivyo.

       

Na Rev. Innocent Samuel Kamote

Mkuu wa wajenzi Mwenye hekima        

Hakuna maoni: