Jumatatu, 13 Februari 2017

Mshitaki wa Ndugu zetu!



Andiko la Msingi: Ufunuo 12:10Nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema, Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana ametupwa chini MSHITAKI wa ndugu zetu, yeye AWASHITAKIYE mbele za Mungu wetu, mchana na usiku.”


Marko 15:3Nao wakuu wa Makuhani walikuwa WAKIMSHITAKI mambo mengi



Ni muhimu kufahamu kuwa shetani ndiye adui mkuu wa kila mwanadamu na kwa watu wa Mungu, Naye hufanya kazi kwa mbinu mbalimbali katika kuwashambulia wanadamu na watu wa Mungu moja ya mbinu kuu anayoitumia katika kufanya mashambulizi kwetu ni kutushitaki, au kutushutumu au kutulaumu, Leo tutachukua muda kutafakari kwa kina moja ya mbinu hii anayoitumia shetani kutushambulia ili asipate kutushinda kwa kukosa kuzijua Fikra zake au mbinu zake katika Jina la Yesu. 2Wakoritho 2:11Shetani asije akapata kutushinda kwa maana hatukosi kuzijua fikira zake.” Tutajifunza somo hili kwa kuzingatia vipengele vitatu vifuatavyo:-

·         Maana ya neno Mshitaki.
·         Makusudi makuu ya mshitaki wetu.
·         Jinsi ya kumshinda Mshitaki wetu.

Maana ya neno Mshitaki.
Neno mshitaki kwa asili linatokana na neno la Kiyunani “Kategoros” au “Kategor” ambalo kwa kiingereza ni “An accuiser” which means one who blames another, or charges another with crime ambalo maana yake ni “Yeye mwenye kutafuta na kuinua lawama kwa Mwingine” au yeye mwenye kushitaki mwingine kwa uhalifu, Unaweza kuona ni katika namna ya kushangaza sana shetani mwenyewe au kupitia maajenti wake huitumia mbinu hii katika kuhakikisha anabomoa kazi ya injili, au sifa za mtu, au kanisa, ili lisiweze kukubalika kwa wasioamini au kuwafanya walioamini kupungukiwa na imani. Neno hili limetajwa mara kadhaa katika biblia likionyesha kusudi la Ibilisi au maajenti wake wakilifanya kwa kusudi la kuharibu mpango wa Mungu!. Mfano:-

Yohana 8:10 Biblia inasema hivi “Yesu akajiinua asimwone mtu ila yule mwanamke, akamwambia Mwanamke, wako wapi wale WASHITAKI wako? Je Hakuna aliyekuhukumu kuwa na Hatia? Akamwambia  Hakuna Bwana Yesu akamwambia, Wala mimi sikuhukumu. Enenda zako wala usitende dhambi tena” 

Katika kifungu hicho hapo juu mwanamke huyu alikamatwa katika kosa la zinaa na kwa mujibu wa Torati wazinzi walipaswa kupigwa mawe hata kufa, hata hivyo katika nyakati hizi serikali ya Warumi ndio ilikuwa inatawala Dunia na Israel pia, wao walikuwa wamepiga marufuku mtu yeyote kuendesha hukumu ya kifo isipokuwa serikali ya Rumi, katika kisa hicho hapo juu shetani aliitumia dhambi ya mwanamke huyu na washitaki wake ili kumtega Yesu aingie katika mtego wa kuruhusu hukumu ya kifo na hatimaye Yesu apate kushitakiwa unaona? Kisa kinaonekana kumlenga mtu mwingine lakini ndani yake kinamlenga Yesu Kristo ili ashitakiwe yeye, Mungu alimpa Hekima namna ya kuwasaidia wote akiwemo mwanamke huyo, shetani ndiye mshitaki wetu mkuu kumbuka, swala la kumtega Yesu ili aingie hatiani lilikuwa ni swala la kila siku la shetani na maajenti wake ili wapate kisa cha kumshitaki

Mathayo 12:10Na tazama yumo mtu mwenye mkono umepooza: wakamwuliza, wakisema Ni halali kuponya  watu siku ya Sabato? Wapate KUMSHITAKI.”

Marko3:2Wakamvizia ili kuona kama atamponya siku ya sabato wapate KUMSHITAKI

Marko 12:13-15Wakatuma baadhi ya Mafarisayo na Maherodi, ili wamnase kwa maneno, Kumnasa kwa maneno maana yake wapate namna ya KUMSHITAKI

Marko 15:3Nao wakuu wa Makuhani walikuwa WAKIMSHITAKI mambo mengi
Muda usingeliweza kutosha kuweza kuangalia maandiko mengi zaidi yanayoonyesha neno hilo Mshitaki linavyotumiwa katika Biblia katika maeneo mengoi sana kote huko shetani akitafuta hatia dhidi ya watu wa Mungu.

Makusudi makuu ya Mshitaki wetu!
Shetani kuitwa mshitaki wetu sio jambo geni katika agano jipya tangu zamani hizi zimekuwa sifa zake kubwa na tabia yake kuu mno, shetani ameonekana katika maandiko mengi ya kale akifanya kazi ya kuwashitaki wenye haki mfano katika :-

Ayubu 1:6-11 Bilia inasema hivi “Ilikuwa, siku moja ambayo hao wana wa Mungu walikwenda kujihudhurisha mbele za Bwana, Shetani naye akaenda kati yao. Bwana akamwuliza Shetani, Umetoka wapi wewe? Ndipo Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Natoka katika kuzunguka-zunguka duniani, na katika kutembea huku na huku humo. Kisha Bwana akamwuliza Shetani, Je! Umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Kwa kuwa hapana mmoja aliye kama yeye duniani, mtu mkamilifu na mwelekevu, mwenye kumcha Mungu na kuepukana na uovu. Ndipo Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Je! Huyo Ayubu yuamcha Bwana bure? Wewe hukumzingira kwa ukigo pande zote, pamoja na nyumba yake, na vitu vyote alivyo navyo? Kazi za mikono yake umezibarikia, nayo mali yake imeongezeka katika nchi. Lakini nyosha mkono wako sasa, uyaguse hayo yote aliyo nayo, naye atakukufuru mbele za uso wako.  
       
Ayubu 2:1-5 Biblia inasema hivi “Tena kulikuwa na siku hao wana wa Mungu walipokwenda kujihudhurisha mbele za Bwana, Shetani naye akaenda kati yao, ili kujihudhurisha mbele za Bwana. Bwana akamwuliza Shetani, Umetoka wapi? Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Natoka katika kuzunguka-zunguka duniani, na katika kutembea huku na huku humo. Bwana akamwuliza Shetani, Je! Umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Kwa kuwa hapana mmoja aliye kama yeye duniani, mtu mkamilifu na mwelekevu, mwenye kumcha Mungu na kuepukana na uovu; naye hata sasa anashikamana na utimilifu wake, ujapokuwa ulinichochea juu yake, ili nimwangamize pasipokuwa na sababu. Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Ngozi kwa ngozi, naam, yote aliyo nayo mtu atayatoa kwa ajili ya uhai wake. Lakini sasa nyosha mkono wako, uuguse mfupa wake na nyama yake, naye atakukufuru mbele za uso wako. Bwana akamwambia Shetani, Tazama, yeye yumo mkononi mwako; lakini tunza tu uhai wake

Zekaria 3:1-5Kisha akanionyesha Yoshua, kuhani mkuu, amesimama mbele ya malaika wa Bwana, na Shetani amesimama mkono wake wa kuume ili kushindana naye. Bwana akamwambia Shetani, Bwana na akukemee Ewe Shetani; naam, Bwana, aliyechagua Yerusalemu, na akukemee; je! Hiki si kinga kilichotolewa motoni? Basi, Yoshua alikuwa amevaa nguo chafu sana, naye alikuwa akisimama mbele ya malaika. Naye huyo akajibu, akawaambia wale waliosimama mbele yake, akisema, Mvueni nguo hizi zenye uchafu. Kisha akamwambia yeye, Tazama, nimekuondolea uovu wako, nami nitakuvika mavazi ya thamani nyingi. Nikasema, Na wampige kilemba kizuri kichwani pake. Basi, wakampiga kilemba kizuri kichwani pake, wakamvika mavazi; naye malaika wa Bwana akasimama karibu”.
1Nyakati 21:1Tena shetani akasimama juu ya Israeli, akamshawishi Daudi kuwahesabu Israeli.”

Unaweza kuona kazi za shetani katika vifungu vyote vya maandiko hapo juu kwa nini shetani hutumia lawama, mashitaka, na masingizio kwa wanadamu na kwa jamii ya wenye haki ambao maandiko yanawaita Ndugu zetu yaani waamini? Kusudi kubwa ni kuharibu sifa na kuvunjilia mbali ushawishi walionao waamini katika jamii ili Mungu azomewe na kazi zake za ukombozi zionekane kuwa bure, Hii ndio imekuwa sifa ya Shetani na maajenti wake siku zake zote Kazi hii Maandiko yanaonyesha kuwa shetani huifanya Usiku na Mchana

Kwa kutumia maandiko hayo utaweza kuliona wazi kusudi la shetani kuwashitaki wateule
Ø  Anamshitaki Daudi ili Israel wapigwe wakataliwe na Mungu, Mungu awakasirikie watu wake na wapate hasara na shetani kufurahia angamizo la watu wa Mungu
Ø  Anamshitaki Zakaria ili asihesabiwe haki, aonekane hana sifa kwa Mungu aliyemchagua
Ø  Anamshitaki Ayubu kuonyesha kuwa mungu haabudiwi tupu, kwamba watu wake wanamuabudu kwa sababu Mungu amewapa Maisha mema, ili ionekanane kwamba binadamu akikosa kitu hawezi kumuweka Mungu mbele.
Ø  Kushitaki pia huja kwa kusudi la kutuletea Mateso katika jamii, akipata kitu cha kutusingizia na tukauhumiwa tutateseka sana kwaajili ya Kristo.
Ø  Anataka kuharibu mioyo yetu na kutujengea mazingira ya kuwa wenye hatia na usijione kuwa unastahili. Kisha upoteze Haki zako. Na kuleta aibu kubwa
Ø  Jumla ya yote ni ili karama tunayoitumikia iweze kulaumiwa yaani watu waone kuwa hakuna wokovu

Jinsi ya kumshinda Mshitaki wetu.

1.      Biblia inaonya kwamba tuwe na kiasi na wenye kukesha! 1Petro 5:8Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa MSHITAKI wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze.” Njia pekee ya Kumshinda ni kuishi maisha ya kiasi, Mungu alituokoa ili tupate kuishi kwa kiasi, tusizidiwe na mambo ya ulimwengu huu kiasi ya kwamba yatatutoa katika mapenzi yake na adui akapata sababu ya kulaumu, Tito 2:11-12 Biblia inasema hivi “Maana neema ya Mungu iwaokoayo wanadamu wote imefunuliwa; nayo yatufundisha kukataa ubaya na tamaa za kidunia; tupate kuishi kwa kiasi, na haki, na utauwa, katika ulimwengu huu wa sasa;” Unaweza kuona Mungu anatutaka tuishi kwa kiasi na kwa haki adi Yetu shetani asipate la kutushitaki Mungu anapokuwa ametuokoa anatupa nguvu dhidi ya mamlaka na utawala wa shetani na shetani hawezi kufurahia kuanguka kwetu au kupatikana kwetu katika lawama ni njia yake ya kututamani ili kwamba turejee katika utawala wake, njia pekee ni kujitia nidhamu ni kuishi kwa kiasi.

2.      Biblia inatukumbusha namna nyingine ya kumshinda mshitaki wetu ni kuendelea kumwangalia Yesu Kristo ambaye kwa upendo wake mkubwa alitufia msalabani na zaidi ya yote ndiye anayetuombea, lazima tujue kuwa ni vigumu kutenganishwa na upendo huu Warumi 8:33- 39Ni nani atakayewashitaki wateule wa Mungu? Mungu ndiye mwenye kuwahesabia haki. Ni nani atakayewahukumia adhabu? Kristo Yesu ndiye aliyekufa; naam, na zaidi ya hayo, amefufuka katika wafu, naye yuko mkono wa kuume wa Mungu; tena ndiye anayetuombea. Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Je! Ni dhiki au shida, au adha, au njaa, au uchi, au hatari, au upanga? Kama ilivyoandikwa, ya kwamba, Kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa, Tumehesabiwa kuwa kama kondoo wa kuchinjwa. Lakini katika mambo hayo yote tunashinda, na zaidi ya kushinda, kwa yeye aliyetupenda. Kwa maana nimekwisha kujua hakika ya kwamba, wala mauti, wala uzima, wala malaika, wala wenye mamlaka, wala yaliyopo, wala yatakayokuwapo, wala wenye uwezo, wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, wala kiumbe kinginecho chote hakitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu”.     Ni nani atakayewashitaki wateule wa Mungu, Mungu ndiye mwenye kuwahesabia haki, iko wazi kuwa haki tuliyonayo sio haki yetu wenyewe ni haki inayotokana na Kristo, ni muhimu kwetu kuendelea kuwa kuishi kwa imani na kuendelea kuaminikatika upendo wake nayeye mwenyewe atamkemea Shetani, kama ilivyokuwa kwa kuhani mkuu Zekaria, Shetani alipomshitaki Malaika alimtetea na kumtaka bwana amkemee, lazima tuendelee kumwangalia Yesu kama mtetezi wetu aliye hai.

3.       Damu ya Yesu ni jibu lingine la kumshinda mshitaki wetu, Yohana 12:10-11Nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema, Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana ametupwa chini mshitaki wa ndugu zetu, yeye awashitakiye mbele za Mungu wetu, mchana na usiku. Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo, na kwa neno la ushuhuda wao; ambao hawakupenda maisha yao hata kufa. Kama tukiwa na hisia za hatia tusiogope hatia sio jambo baya kusudi lake ni kutuleta katika toba, na toba hii inatupa wepesi wa kusamehewa na kuitumia damu ya Yesu kwa imani iliyomwagika msalabani tu narudi katika kuhesabiwa haki na shetani anapoteza nafasi ya kutushitaki.
4.      Yesu Kristo ni mpatanishi wetu Ni lazima tuelewe kuwa tunaye mpatanishi anayestahili yeye ndiye anayeweza kusimama mahali palipobomoka kati yetu na Mungu na kutupatanisha hatupaswi kuogopa turudi kwa mung mara tunapogundua kuwa tumemkosea na Kristo kama wakili wetu anatuombea kwa baba na kutupatanisha na Mungu kabla ibilisi hajapata la kutushitaki 1Yohana 2:1-2Watoto wangu wadogo, nawaandikia haya ili kwamba msitende dhambi. Na kama mtu akitenda dhambi tunaye Mwombezi kwa Baba, Yesu Kristo mwenye haki,  naye ndiye kipatanisho kwa dhambi zetu; wala si kwa dhambi zetu tu, bali na kwa dhambi za ulimwengu wote.” 

        Hatupaswi kuogopa na kufikiri kuwa kila kitu kimeisha eti kwa sababu tulikosea jambo la msingi ni kurudi kwa Mungu na pia kuelewa kuwa tunaye mpatanishi na atafanyia upatanisho na Mungu.

5.      Usishitaki watu wa Mungu bali uwaombee, watu wengi wa Mungu hasa wana tabia ya kushutumu sana wanapoona makosa ya wengine badala ya kuwaombea Mungu kamwe hafurahii tabia ya aina hiyo, Mungu anaweza kukuhukumu wewe kwa vile unageuka na kusimama katika nafasi ya shetani kosa kama hili liliwahi kufanywa na Nabii Eliya Warumi 11: 2-4Mungu hakuwasukumia mbali watu wake aliowajua tokea awali. Au hamjui yale yaliyonenwa na maandiko juu ya Eliya? Jinsi anavyowashitaki Waisraeli mbele za Mungu, Bwana, wamewaua manabii wako, wamezibomoa madhabahu zako, nami nimesalia peke yangu, nao wananitafuta roho yangu. Lakini ile jawabu ya Mungu yamwambiaje? Nimejisazia watu elfu saba wasiopiga goti mbele ya Baali”. Wakristo ni lazima wajifunze kuombeana na kusamehe kwa haraka kutokusamehe kwa haraka ni kumpa ibilisi nafasi Efeso 4:26-27 inasema “Mwe na hasira, ila msitende dhambi; jua lisichwe na uchungu wenu bado haujawatoka; wala msimpe Ibilisi nafasi.” Shetani anapataje nafasi ni kwa watu kutokusameheana nah ii inaweza kumpa yeye wakati wa kutushitaki kwa kulijua hili Paulo mtume aliagiza msamaha kwa ndugu aliyefanya dhambi na kupokea maonyo, alilisihi kanisa kumsamehe mtu huyo, kwani kama wasingelifanya hilo shetani angeweza kuwashinda angalia 2Wakoritho 2:10-11Lakini kama mkimsamehe mtu neno lo lote, nami nimemsamehe; kwa maana mimi nami, ikiwa nimemsamehe mtu neno lo lote, nimemsamehe kwa ajili yenu mbele za Kristo, Shetani asije akapata kutushinda; kwa maana hatukosi kuzijua fikira zake.” Unaweza kuona kumbe kutokusamehe kunaweza kumpa ushindi mshitaki wetu ni lazima tuwe wenye kusamehe na kutokuwashutumu na kuwalaumu wengine, na badala yake kuwaombea vinginevyo shetani atapata nafasi kwetu pia.
Itaendelea na Rev. Innocent Kamote Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima!

Alhamisi, 26 Januari 2017

Mfano wa tai ayashukiaye Mawindo!


Andiko: Ayubu 9: 25 -26 Biblia inasema “ Basi siku zangu zina mbio kuliko Tarishi; Zakimbia wala hazioni mema, Zimepita kama merikebu ziendazo mbio; Mfano wa tai ayashukiayemawindo.”



Leo tutachukua muda kutafakari kwa kina somo kuhusu Mfano wa tai ayashukiaye Mawindo, Ni muhimu kuwa na ufahamu kuwa Mungu aliviumba viumbe vingi duniani kwa makusudi mbali mbali lakini mojawapo ya kusudi kuu ni kutufunza mambo mbalimbali ya msingi, Tai ni moja ya Ndege au kiumbe ambaye biblia imezungumza sifa zake kwa kina na mapana na marefu na tunaweza kujifunza mambo kadhaa ya muhimu kutoka kwa kiumbe hiki.
Kuna usemi wa wahenga kuwa ndege wa aina moja huruka pamoja, Usemi huu kwa Tai ni tofauti tai wanaruka pekeyo na wanafurahia kuruka juu sana, sifa zake zinawekwa katika Biblia kwa vile ni ndege mwenye sifa za kipakee ni ndege asiyeshindwa na ukubwa wa mawindo yake.
Kwa nini Biblia inampa Tai sifa za hali ya juu sana ni muhimu kwetu kujifunza sifa zake na kuzilinganisha na maisha yetu.

1.       Tai ni wenye uwezo mkubwa wa kuona mbali.



Ayubu 39:27-29 Biblia inasema hivi “ Je! Tai hupaa juu kwa amri yako, Na kufanya kioto chake mahali pa juu?  Hukaa jabalini, ndiko kwenye malazi yake, Juu ya genge la jabali, na ngomeni. Toka huko yeye huchungulia mawindo; Macho yake huyaangalia toka mbali.”

Tai kama utamfanyia uchunguzi na kumchungulia kwa mbali ni ndege makini sana Biblia inamsifia kuwa “macho yake huyaangalia mawindo toka mbali” ndi ndege hodari katika kuwinda macho yake amebarikiwa uwezo wa kuona mbali sana na anaona kwa uwazi kabisa inasemekana anauwezo wa kumuona mwenzake akiwa Maili 50 kwa uwazi kabisa! Jambo hili linatufundisha nini? Naamini unaweza kupata picha Fulani

Mamia ya watu hodari wamewahi kuishi duniania na kupita wakiwemo watu maarufu sana duniani na viongozi wakubwa

Ili dunia iweze kuwa na Mafanikio makubwa sana inahitaji watu na viongozi wenye uwezo wa kuona mbali sana, Abraham Lincoln rais wa 16 wa Marekani aliongoza katika wakati mgumu sana wenye matatizo mengi na inchi ikiwa katika vita vya wenyewe kwa wenyewe, lakini ndiye aliyefanikiwa kuweka misingi ya umoja na kukomesha utumwa na kuifanya Marekani iwe kama ilivyo leo,

Ili dunia iweze kuwa na mafanikio ni lazima iwe na watu wenye uwezo wa kuona mbali, wanaoangalia faida za mbeleni za kwao na za kizazi kinachokuja badala yao
·         Watu wasio na maono ya mbali wanaweza kutugawa kupitia dini na ukabila
·         Watu waioona mbali hawajali kutunza Mazingira
·         Watu wasioona mbali hawaogopi kuharibu mahusiano
·         Watu wasioona mbali hawaogopi kuua wanyama kama tembo kwa faida yao
·         Watu wasioona mbali hawaogopi kufanya Ufisadi kwa kuifilisi nchi
·         Watu wasioona mbali hawafikiri kujisomea kwa bidii
·         Watu wasioona mbali hawafikiri kujiwekea akiba
·         Watu wasioona mbali hawafikiri kuhusu maisha yao baada ya kufa duniani
Awaye yote aliye kama tai atakuwa na ujuzi wa kuona mbali na kuzingatia faida za siku zijazo kuliko kuangalia leo. Unayaona mwindo yako kwa mbali. Ni lazima tuwe na maono makubwa yaliyopimwa kwa kina na yatakayoleta faida kubwa na matokeo makubwa katika jamii.

2.       Tai ni ndege wasioogopa Mawindo.


Tai ni ndege asiyeogopa hata kidogo, wakati wote anapambana kuhakikisha anashinda, atapambana kuhakikisha anapata mawindo yake au anatawala,unapoangalia sinema za maisha ya tai utaweza kuona  hawaogopi mawindo haijalishi mawindo yao ni makubwa kiasi gani hata kama ni mbuzi ambaye anaonekana kuwa mkubwa kuliko uwezo wake tai ni lazima atabeba, wana ujuzi mkubwa wa kuwinda na ni mahodari, tai haogopi
Ni muhimu kufahamu kuwa kama unataka kufanikiwa katika maisha haya usiogope kufanya jambo gumu, usiogope kukabiliana na watu wakubwa au waliokuzidi umri, hakikisha kuwa unakipigania kile unachokipenda,
·         Usiogope kupigania unachokipenda
·         Usiogope kusimama katika kweli hata kama itakuletea madhara
·         Usiogope ukubwa wa tatizo unalopambana nalo pigania mpaka kieleweke
·         Usiogope ugumu wa masomo unayosoma
·         Usiogope au kuonea aibu aina ya kazi unayoifanya
·         Lengo lako kuu ni kuhakikisha unafanikiwa
·         Usiogope mateso utakayoyapata kwaajili ya imani au kile unachokipigania
·         Usiogope kuanzisha huduma au kufungua kanisa, usiogope kuwa mmisionary, usiogope kugombea urais kama Mungu anataka ufanye jambo kwa faida yako lifanye
·         Uisogope kufanya lolote ili kufafikia malengo yako, Tai hawaogopi mawindo yao hata kama anachokiwinda ni kikubwa kuliko umbile lake.

3.       Tai ni Hodari hawaogopi Dhuruba.


Ukitaka kujua uhodari wa Tai utaweza kuuona wakati wa dhoruba, wakati huu ndege wengine wote hukimbia na kujificha kwa kuogopa dhoruba , kwa tai mambo ni tofauti anafunua mbawa zake na kuzitanua na kupaa kwenda juu zaidi, taia wanatabia ya kutumia dhoruba kwa faida, wakati ndege wa kawaida wakiogopa, ni muhimu kufahamu kuwa watu wanaolinganishwa na tai hawakimbii changamoto zozote bali huzitumia changamoto kusimama na kuongeza viwango, Mungu anataka watu wasiokimbia changamoto bali wenye uwezo wa kukabiliana nazo huku wakisimama katika kusudi au kuelekea juu zaidi

4.       Tai wanaruka juu sana.



Ndege huyu ndiye anayejulikana kama mfalme wa ana inasemekana tai wanauwezo wa kuruka juu kiasi cha fiti 10,000, katika kiwango hicho hutaweza kumuona ndege mwingine na ukimuona ni lazima atakuwa tai, Tai haruki wala kutafutiza chakula pamoja na njiwa, alisema Dr, Myles Munroe Marehemu, alisema wakati njiwa wakiwa ardhini wanacgakuachakua siku nzima na kulalamika, Taia hawanung’uniki, hawapigi kelele, wanapaa juu sana wakisubiri mawindo wakisubiri nafasi waweze kuitumia, watu wakuu duniani ni wale wanaotatua matatizo na sio wanaolalamika, wanatumia nafasi na changamoto yoyote kama tai dhoruba inapotokea.

5.       Tai hawali kibudu
Ni muhimu kufahamu kuwa sifa nyingine ya tai ni pamoja na kutokula kibudu tai hawali wasichokiua wenyewe, siku zote wanakula nyama ya mawindo yao wenyewe, wanakula nyma safi na mpya hivi ndivyo watu wakuu katika dunia wanavyopaswa kuwa
Watu wakubwa duniani hukaa na watu wenye mawazo mapana na wenye kufikiri na wenye uwezo wa kuamua, watu hodari wasiokata tamaa, hawa ndio watu wanaoweza kulete mabadiliko makubwa Duniani, watu wenye uwezo wa kuleta badiliko unapowasikiliza au kukaa nao karibu, watu wenye ushawishi
Kamwe usipoteze muda na watu wanaopoteza muda
Kamwe usipoteze muda na watu wenye kusengenya
Kamwe usipoteze muda na watu wasio na imani
Kamwe usipoteze muda na watu wenye kuzungumzia wengine
Kamwe usipoteze muda na watu wenye kupiga majungu na fitina
Kamwe usipoteze muda na watu ambao kuanguka kwa wengine ndio furaha yao
Kamwe usipoteze muda na watu wenye kuhukumu
Kamwe usipoteze muda na watu wenye mitazamo hasi wenye kujihusisha na rushwa na uovu hivyo ni vibudu, tafuta vya kwako mwenyewe mawindo yako mwenyewe.



Tai anayekula Mizoga!
Ni muhimu kufahamu kuwa tai tunayemzungumzia hapa  mwenye sifa tulizozitaja anaitwa Eagle huyu hali mizoga na taia anayetajwa katika Mathayo 24:28 huyu ndiye taia anayekula mizoga huyu anaitwa VULTURE
§  Mathayo 24:28Kwa kuwa popote ulipo mzoga ndipo watakapokusanyika tai”
§   Matthew 24: 28 "Whenever there is carcass, there the VULTURE will gather” NIV.
§  Matthew 24: 28 "For wheresoever' the carcase  is there will eagles be gathered together KJV
Tai anayekula Mizoga haitwi “Eagle” anaitwa  “Vulture”
Huyu ni aina nyingine ya tai ambaye hupatikana mashariki ya kati nyikanani na katika mbuga za wanyama Afrika tai huyu ndiye anayekula mizoga kiingereza sahii anaitwa VULTURE huyu ndiye ambaye Yesu anazungumza katika injili ya Mathayo  

Tai aina ya Vulture ndiye anayekula Mizoga na sio Tai aina ya Eagle

6.       Tai wanauwezo wa kujitia nguvu mpya
Zaburi 103:4-5 “ Akusamehe maovu yako yote, Akuponya magonjwa yako yote,  Aukomboa uhai wako na kaburi, Akutia taji ya fadhili na rehema, Aushibisha mema uzee wako, Ujana wako ukarejezwa kama tai;”


Isaya 40:31 “Bali wao wamngojeao Bwana watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia.”
 
Moja ya tabia ya tai ya kushangaza sana ni uwezo wake wa kujitia nguvu kwa upya ukiacha kuwa wanauwezo wa kuona mbali lakini wana maisha marefu inasemekana Tai anapofikisha miaka 30 anakuwa anachakaa na manyoya yake yanakuwa yamezeeka hivyo kuathiri uwezo wake wa kiutendaji, inapofikia hivyo tai hakati tamaa ya kuishi badala yake hutafuta kilele kikubwa cha mlima na kutulia kwa miezi mitano anagonga mdomo wake katika mawe ya miamba na kungoa ngozi ya juu, hujinyonyoa manyoa nyake yote wakati huu ajajigomoa na kuanza kuwa na manyoya mapya mdomo mpya na magamba mapya jambo hili humfanya tai awe na uwezo wa kurejexza uhai wake kwa miaka mingine 30-40, Ndo maana biblia inasema ujana wako utarejezwa kama tai
 Watu wenye akili ni watu wanaoweza kujitafakari na kuangalia yote waliyoyafanya katika maisha yao liwe jema au baya linapokuwa baya unaachana nalo  wanatafuta nini lililo jema na lipi wanaweza kuliendeleza na jipya gani wanaweza kuenda nalo, na kujifunza jambo jipya la kufanya siku hadi siku.
Kamwe sukubali kudumaaa
Usikubali kubaki vilevile siku zote

7.       Tai wanatoa mafunzo kwa vifaranga vyao


Amini usiamini tai wanaotoa mafunzo kwa vijana wao, tai wanafikiriwa kuwa ni ndege katili sana wakati wa kutoa mafunzo na kama hujui makusudi yao unaweza kukubaliana kuwa ni ndege wakatili, jambo moja la kushangaza kuhusu tai ni uwezo wake wa kutoa mafunzo kwa vifaranga vyake, utafiti unaonyesha kuwa hakuna aina ya ndege mwenye mvuto na mpole kama tai kwa watoto wake kushinda tai
Mama wa tai anapogundua kuwa wakati umefika kwa vifaranga vyake kujifunza kuruka, anawabeba vifaranga wake mgongoni na kupanua mbawa zake anaruka juu sana kisha anajiondoa kutoka kifaranga chake na kukiachia kiangukekinapoanguka kinajifunza kuruka akiona kinaogopa na kinataka kuanguka anakidaka na kukirejeza katika kiota chake, atafanya hivyo mpaka kimejifunza kuruka.

Watu wakubwa sana duniani sio mabosi, wakati wote wanawafanya wengine kukua katika jamii na wanawapa changamoto lakini wanawasaidia kukua na kujiamini na kuendelea kuwapa maelekezo wengine mpaka wameweza kufanya vilevile kama wao wafanyavyo.

Rev. Innocent Kamote
Mkuu wa Wajenzi mwenye Hekima
0718990796