Ijumaa, 10 Machi 2017

Kwa nini Naipenda Israel kwanini Naipenda Yerusalem!



Zaburi 137:5,6Eee Yerusalem nikikusahau wewe Mkono wangu wa kuume na usahau, Ulimi wangu na uganadamane na Kaakaa la kinywa changu nisipokukumbuka, Nisipoikuza Yerusalemu zaidi ya furaha yangu iliyo kuu

 Pichani Jiji la yerusalem Maarfuru kama old Jerusalem ikionekana katika utukufu wake
 
UMUHIMU WA KUIPENDA ISRAEL. (JERUSALEM)

Mji wa Yerusalem ambao ni mji mkuu wa Israel ni mji muhimu sana katika maswala ya kisiasa kiimani na kiusalama mjii huu ni picha ya mji halisi ulioko peponi au mbinguni ambao ni makao makuu ya serikali ya Mungu Mbinguni, 

Mungu ana mji ulioko Juu mbinguni na mji huu unaitwa Yerusalem Wagalatia 4:25- 26Maana Hajiri ni kama mlima Sinai ulioko Arabuni, umelingana na Yerusalem wa sasa kwa kuwa anatumika pamoja na watoto, Bali Yerusalem wa juu ni mwungwana naye ndiye mama yetu sisi” 

Katika maandiko hayo Paulo mtume anaonyesha kuwa kuna Yerusalem ya Duniani naya mbinguni miji yote hii ni makao makuu ya serikali ya Mungu aliye hai, Yerusalem iliyoko Israel ni makao makuu ya Mungu Duniani na Yerusalem ulioko mbinguni ni makao makuu ya serikali ya Mungu.

Mji huu ni wa muhimu sana wengi waliotambua siri ya umuhimu wa mji huu wanaupenda na watakatifu waliotutangulia waliomba wasiisahau Yerusalem Zaburi 137:5,6Eee Yerusalem nikikusahau wewe Mkono wangu wa kuume na usahau, Ulimi wangu na uganadamane na Kaakaa la kinywa changu nisipokukumbuka, Nisipoikuza Yerusalemu zaidi ya furaha yangu iliyo kuu

 unaweza kuona Yerusalemu ni zaidi ya furaha ya watakatifu

Kama ilivyo kwa almasi katika kiti cha sofa ndivyo ulivyo mji wa Yerusalem mji huu ukokatikati ya vilele vya Safu ya milima ya Yudea (Uyahudi) na kwa ujumla ni katikati ya Dunia kijiografia, maisha na hatima ya wanadamu wote duniani iko au imefungamanishwa na mji huu wa kipekee, Tangu wakati wa Ibrahim nabii Israel imekuwa ni makao makuu ya ukombozi wa Mwanadamu, wakati huu dunia inapoelekea ukingoni Israel inaanza kuwa ngome tena ya kufunua makusudi ya Utawala wa Mungu duniani na ngoma ya kuchezwa mbele ya wanadamu na malaika.

Wakristo na hata wasio wakristo wanapaswa kuwa na uelewa wa kutosha Kuhusu Israel na Jerusalem na uhusiano wetu kiimani Biblia inaonyesha upekee wa hali ya juu kuhusu Israel na Yerusalem na kukosa ufahamu huu kunaweza kutunyima Baraka za kipekee zilizofichwa kuhusu inchi hii na mji huu

Nchi yangu na Mji wangu!

Zaburi ya 21:1 “Biblia inasema Nchi na vyote viijazavyo ni mali ya Bwana, Dunia na wote wakaao ndani yake. “ unaweza kuona Biblia inatufundisha kuwa nchi na vyote viijazavyo ni mali ya Bwana na Dunia yote na watu wote, hivyo kuna uweli kuwa kila inchi ni ya Mungu na kila taifa ni la Mungu na watu wote ni wa Mungu katika ujumla wake, lakini katika upekee wake Israel na mji wake mkuu Yerusalem ni Mji mtakatifu wa Mungu na ushahidi wa kimaandiko upo kuthibitisha kuwa kuna utofauti kwa nchi hii na mji huu

1.    Unaitwa mji Mtakatifu “Amka, amka, jivike nguvu zako, Ee Sayuni; Jivike mavazi yako mazuri, Ee Yerusalemu, MJI MTAKATIFU; Kwa maana tokea sasa hataingia ndani yako Asiyetahiriwa, wala aliye najisi.” Biblia inasema katika Isaya 52:1
 
2.    Yesu mwenyewe aliupenda mji huu licha ya kuutolea Machozi katika mafundisho yake aliuita mji wa Mfalme mkuu angalia Mathayo 5:35Tena mmesikia watu wa kale walivyoambiwa, Usiape uongo, ila mtimizie Bwana nyapo zako;    34. lakini mimi nawaambia, Usiape kabisa; hata kwa mbingu, kwa maana ndicho kiti cha enzi cha Mungu;35. wala kwa nchi, kwa maana ndiyo pa kuwekea miguu yake; wala kwa YERUSALEMU, KWA MAANA NDIO MJI WA MFALME MKUU” Yesu anatambua kuwa mji huu ndio makao yake makuu, mfalme mkuu ni yeye, mji huu ni wake unawezaje kusema kuwa unampenda Yesu kisha unachukia mji wake na serikali yake na makao yake makuu?

3.    Kiti cha enzi cha Mungu Yeremia 3:17 Wakati ule watauita Yerusalemu kiti cha enzi cha Bwana; na mataifa yote watakusanyika huko Yerusalemu, kwa ajili ya jina la Bwana; wala hawatakwenda tena kwa ukaidi wa moyo wao mbaya.”

4.    Mungu aliahidi kuliweka Jina lake pale Yerusalem milele soma 2Nyakati 33:4 Biblia inasema ”Akajenga madhabahu katika nyumba ya Bwana, napo ndipo alipopanena Bwana, Katika Yerusalemu litakuwako jina langu milele

5.    Maandiko yako wazi kuwa Mungu anajivunia Yerusalem angalia Zaburi 87:1-3 Biblia inasema “Msingi wake upo Juu ya milima mitakatifu. Bwana ayapenda malango ya Sayuni Kuliko maskani zote za Yakobo. Umetajwa kwa mambo matukufu, Ee Mji wa Mungu.”

6.    Yerusalem ni sababu ya Furaha Isaya 65:19 Nami nitaufurahia Yerusalemu, nitawaonea shangwe watu wangu; sauti ya kulia haitasikiwa ndani yake tena, wala sauti ya kuomboleza.”

7.    Isaya alisema kwaajili ya Yerusalem yaani sayuni sitanyamaza Isaya 62:31. Kwa ajili ya Sayuni sitanyamaza, na kwa ajili ya Yerusalemu sitatulia, hata haki yake itakapotokea kama mwangaza, na wokovu wake kama taa iwakayo. 2. Na mataifa wataiona haki yako, na wafalme wote watauona utukufu wako; nawe utaitwa jina jipya, litakalotajwa na kinywa cha Bwana. 3. Nawe utakuwa taji ya uzuri katika mkono wa Bwana, na kilemba cha kifalme mkononi mwa Mungu wako.” Unaweza kuona jinsi mji huu uliyounganishwa na shughuli za kinabii na kiimani wote waliokuwa wakimpenda Mungu kwa dhati waliipenda Yerusalem kwa dhati vilevile

8.    Unabii unaonyesha kuwa siku za mwisho watu wengi sana wataitembelea Israel yaani wataitembelea Yerusalem makundi kwa makundi Isaya 2:3 “1. Hili ni neno aliloliona Isaya mwana wa Amozi katika habari za Yuda na Yerusalemu. 2. Na itakuwa katika siku za mwisho, mlima wa nyumba ya Bwana utawekwa imara juu ya milima, nao utainuliwa juu ya vilima; na mataifa yote watauendea makundi makundi.  3. Na mataifa mengi watakwenda na kusema, Njoni, twende juu mlimani kwa Bwana, nyumbani kwa Mungu wa Yakobo, naye atatufundisha njia zake, nasi tutakwenda katika mapito yake maana katika Sayuni itatoka sheria, na neno la Bwana katika Yerusalemu. 4. Naye atafanya hukumu katika mataifa mengi, atawakemea watu wa kabila nyingi; nao watafua panga zao ziwe majembe, na mikuki yao iwe miundu; taifa halitainua upanga juu ya taifa lingine, wala hawatajifunza vita tena kamwe. 5. Enyi wa nyumba ya Israeli, njoni, twende katika nuru ya Bwana”.Unaona unabii wa Isaya watu wote wataiendea Yerusalem huko ndiko itokako amani ya watu wote huko ndio asili nya Neno la Mungu, huku ndio asili ya mafundissho yote Yerusalem Yerusalem!

Mungu hajamaliza na Yerusalem ya Asili

Ni muhimu kwa kila mkristo kuwa na uelewa huu kuwa Mungu hajamaliza kazi yake na mji huu Yerusalem wa Duniani, nasema hivi kwa sababu mtu anaweza kujenga Hoja za kimaandiko kuwa isis kama Ibrahimu tunautazamia mji wenye misingi ambao mwenye kuujenga na kuubuni ni Mungu, akiwa na maana ya Yerusalem ya Mbinguni  sawa na Waebrania 11:10 ambapo Biblia inasema “Kwa imani Ibrahimu alipoitwa aliitika, atoke aende mahali pale atakapopapata kuwa urithi; akatoka asijue aendako. 9. Kwa imani alikaa ugenini katika ile nchi ya ahadi, kama katika nchi isiyo yake, akikaa katika hema pamoja na Isaka na Yakobo, warithi pamoja naye wa ahadi ile ile. 10. Maana alikuwa akiutazamia mji wenye misingi, ambao mwenye kuubuni na kuujenga ni Mungu.” 

Maandiko yanaonyesha kuwa Ibrahim kwa Imani alikuwa akiutazamia Mji wa Mbinguni kwa vyovyote vile Yerusalem wa Mbinguni, Pia tunaweza kuona msisitizo wa Paulo Mtume kwa Wafilipi 3:20Kwa maana sisi, wenyeji wetu uko mbinguni; kutoka huko tena tunamtazamia Mwokozi, Bwana Yesu Kristo;” na tunaambiwa kuwa Yerusalem wa Mbinguni ndio mama wa yote Waebrania 12:22 na kuwa kila aliyeamini ameungamanishwa na Sayuni ya Mbinguni au Yerusalem ya Mbinguni  Bali ninyi mmeufikilia mlima Sayuni, na mji wa Mungu aliye hai, Yerusalemu wa mbinguni, na majeshi ya malaika elfu nyingi,”

Na Kama haitoshi Yesu mwenyewe alionyesha kuwa ndani ya agano jipya watu wangefurahia uwepo wa Mungu katika roho na kweli ikiwa na maana ya ibada halisi haitategemea Hekalu Yerusalem wala mlima Fulani kwa vile Mungu anataka kuabudiwa katika roho na kweli angalia Yohana 4:21-24 “Yesu akamwambia, Mama, unisadiki, saa inakuja ambayo hamtamwabudu Baba katika mlima huu, wala kule Yerusalemu. Ninyi mnaabudu msichokijua; sisi tunaabudu tukijuacho; kwa kuwa wokovu watoka kwa Wayahudi. Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu.  Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli”. 

Kama utaviangalia kwa makini vifungu vyote vya maandiko hapo juu unaweza kudhani kuwa Mungu hana kazi tena na mji wa Yerusalem wa sasa na Taifa la Israel, unaweza kufikiri kuwa makusudi yake yamekwisha 

Lakini turudi tena katika Mathayo 5: 35 Tena mmesikia watu wa kale walivyoambiwa, Usiape uongo, ila mtimizie Bwana nyapo zako; 34. lakini mimi nawaambia, Usiape kabisa; hata kwa mbingu, kwa maana ndicho kiti cha enzi cha Mungu;35. wala kwa nchi, kwa maana ndiyo pa kuwekea miguu yake; wala kwa YERUSALEMU, KWA MAANA NDIO MJI WA MFALME MKUU” Yesu anaonyesha kuwa tusiape kwa Yerusalem kwa maana ndio mji wa Mfalme mkuu hii ina maana gani kwa nini asiseme kwa vile ulikuwa mji wa mfalme mkuu? Kwanini Mungu Hajamaliza kazi yeke na mji huu wa Yerusalem wa asili

Yesu alisema Yerusalem utakanyagwa na mataifa kwa kitambo Luka 21:24 “…..Na Yerusalemu utakanyagwa na Mataifa, hata majira ya Mataifa yatakapotimia” 

“Kama Maandiko yametoa nafasi ya kukanyaga Israel na Yerusalem naamini ni vema wakristo tukaitumia nafasi hiyo ya kwenda Israel na kutembelea nchi hiyo ya kipekee kwani utakuja wakati itakuwa ngumu sana kuitembelea Israel hata kama utakuwa na uwezo huo” huu ni mtazamo wa kinabii wa mkuu wa wajenzi hapa.

Maneno hayo ya kinabii yanamaanisha kuwa mataifa wataukanyaga kwa muda na hatimeye mjii huu utarejeshwa katika utukufu wake , Yesu Kristo atakaporudi katika utukufu wake atasimamisha serikali yake kutoka mji huu na kutawala akiwa MFALMA WA WAFALME NA BWANA WA MABWANA Kutoka Israel Yerusalem angalia

 Zekaria 14:4, 9Na siku hiyo miguu yake itasimama juu ya mlima wa Mizeituni, unaoelekea Yerusalemu upande wa mashariki, nao mlima wa Mizeituni utapasuka katikati yake, upande wa mashariki na upande wa magharibi; litakuwako huko bonde kubwa sana; na nusu ya mlima ule utaondoka kwenda upande wa kaskazini, na nusu yake itaondoka kwenda upande wa kusini. , Naye Bwana atakuwa Mfalme juu ya nchi yote; siku hiyo Bwana atakuwa mmoja, na jina lake moja” 

Kwa hiyo iko wazi kuwa mjii huu bado uko na uhusiano mkubwa na maswala ya kiimani ni wazi kuwa kuna Baraka za kimungu kama tunautakia mafanikio, na hata ingawa kunaweza kusiwe na Uhusiano wa kiibada na Israel au Yerusalem lakini huwezi kukataa kuwa kuna ahadi za mafanikio kwa wanaoiombea Israel na wamnaoutakia mema Yerusalem

Utakieni Yerusalem Amani!

Zaburi ya 122 :6-9 inasema hivi:- “Utakieni Yerusalemu amani; Na wafanikiwe wakupendao;. Amani na ikae ndani ya kuta zako, Na kufanikiwa ndani ya majumba yako. Kwa ajili ya ndugu zangu na rafiki zangu Niseme sasa, Amani ikae nawe.  Kwa ajili ya nyumba ya Bwana, Mungu wetu, Nikutafutie mema

Biblia inaamuru “Utakieni Yerusalem Amani” na inaunganisha Baraka kubwa na wale waipendao Yerusalem wafanikiwe wakupendao, Mema yataambatana na kila Mkristo na mtu aiye mkristo anayeitakia Mema Israel na Yerusalem

Mungu anataka tufurahi pamoja na Israel Isaya 65:18 , 19 a na 66:10-13 Biblia inasema haya

“18. Lakini furahini, mkashangilie daima, kwa ajili ya hivi niviumbavyo; maana, tazama, naumba Yerusalemu uwe shangwe, na watu wake wawe furaha. 19. Nami nitaufurahia Yerusalemu, nitawaonea shangwe watu wangu; sauti ya kulia haitasikiwa ndani yake tena, wala sauti ya kuomboleza. 10. Furahini pamoja na Yerusalemu, shangilieni kwa ajili yake, ninyi nyote mmpendao; furahini pamoja naye kwa furaha, ninyi nyote mliao kwa ajili yake; 11. mpate kunyonya, na kushibishwa kwa maziwa ya faraja zake, mpate kukama, na kufurahiwa kwa wingi wa utukufu wake. 12. Maana Bwana asema hivi, Tazama, nitamwelekezea amani kama mto, na utukufu wa mataifa kama kijito kifurikacho, nanyi mtapata kunyonya; mtabebwa; na juu ya magoti mtabembelezwa. 13. Mfano wa mtu ambaye mama yake amfariji, ndivyo nitakavyowafariji ninyi; nanyi mtafarijiwa katika Yerusalemu.”

Yesu aliipenda Yerusalem kiasi cha kuulilia mji huu, Nehemia aliugua na kufunga na kuomba kwaajili ya Yerusale, Yesu anaitamani Yerusalem mpango wake ni kuukumbatia ni kuukusanya kama kuku akusanyavyo vifaranga vyake! Mathayo 23:37Ee Yerusalemu, Yerusalemu, uwauaye manabii, na kuwapiga kwa mawe wale waliotumwa kwako! Ni mara ngapi nimetaka kuwakusanya pamoja watoto wako, kama vile kuku avikusanyavyo pamoja vifaranga vyake chini ya mabawa yake, lakini hamkutaka! “ Yerusalem walikataa mapenzi ya Mungu kwa kumkataa masihi na kumsulubisha nje ya mji huu, lakini Mungu anawatamani sana Israel na ni mapenzi ya Mungu waokolewe na mjii huu kwa vyovyote vila ndio utakuja kuwa makao makuu ya Masihi Yesu.

Siri ya tai ya rangi ya blue katika shati Jeupe!
 

Kwa nini Viongozi katika Israel na Marekani huvaa tai ya rangi ya Blue? Ngoja nikuambie siri ya tai ya rangi ya blue na Nyekundu kwa Marekani, Bendera ya marekani ina rangi nyeupe, Nyekundu na blue, Chama cha republican huwakilihwa na rangi nyekundu na chama cha democratic huwakilishwa na rangi ya blue hii ni alama kubwa sana kwa taifa lao, wanapovaa tai viongozi wao huvaa kuonyesha uzalendo wa taifa lao katika maswala ya kitaifa

Pia kwa vile wamarekani wana uhusiano mkubwa sana na Israel pia kuvaa tai ya blue kwao humaanisha wazi kuipenda na kuiunga mkono Taifa la kiyahudi, Wayahudi bendera yao ni yeupe na ina mistari ya blue na nyota ya Mfalme Daud iliwa na rangi ya blue hivyo viongozi wa kitaifa kwao huvaa tai ya blue
Uganda bendera yao ina rangi nyekundu,mkenya pia na nyeusi na njano, Rais Museven hupenda kuvaa tai ya Manjano kwa vile ni rangi ya taifa lao katika bendera yao
Ukiona kiongozi wa kitaifa katika taifa ambalo halijamwaga Damu amevaa tai nyekundu maana yake huvaa tu bila kuzingatia amevaa kwa maana gani

Tai ya blue ikivaliwa na mtu anayejua maandiko humaanisha wazi kuwa anaipenda Israel, scafu na kadhalika kwa msingi huo kama unaipenda Israel katika kuonyesha mapenzi yako kwa taifa hilo vaa tai ya blue kuna siri kubwa katika jambo hilo kwaajili ya kuonyesha unaiunga mkono Israel
Kwa bahati njema kwa watanzania tai ya blue pia itakuwa ni sehemu ya Bedera yetu katika zile rangi nne mamarufu kwa hiyo tai ya blue itamaanisha uzalendo kwa taifa lako lakini kiroho Israel, hii ni siahara nyingine ya kuipenda sayuni.

Ujumbe na Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima
Rev. Innocent Kamote.

Jumatatu, 27 Februari 2017

Mkono wa Bwana!


Mstari wa Msingi: Isaya 53:1Ni nani aliyesadiki habari tuliyoileta? Na mkono wa Bwana amefunuliwa nani?”


Kware kama wanavyoonekana Pichani ni ndege watamu sana na wenye afya ya ajabu 

Utangulizi:

Neno mkono linapotumika katika maandiko humaanisha utendaji au uweza, Na tunapoona neno Mkono wa Mungu moja kwa moja humaanisha uweza na utendaji wa Mungu, yako mambo kadhaa katika maisha yetu hayawezi kufanikiwa kama mkono wa Mungu hautakuwa juu yako ama kuwa pamoja nawe, Katika maandiko tunamuona Naomi akilia akiamini kuwa alipatwa na mikasa mbalimbali mibaya kwa sababu Bwana ameondoa mkono wake juu yake 

(Ruthu 1:11-13) “Naye Naomi akasema, Enyi wanangu, mrejee; kwani kufuatana na mimi? Je! Mimi ninao watoto wa kiume tena tumboni mwangu, hata wawe waume zenu? Enyi wanangu, mrejee; nendeni zenu; kwa kuwa mimi ni mzee, siwezi kupata mume tena. Kama ningesema, Natumaini; kama ningepata mume hata usiku huu, na kuzaa watoto wa kiume;  je! Mngesubiri hata watakapokuwa watu wazima? Mngejizuia msiwe na waume? La, sivyo, wanangu; maana ni vigumu kwangu kuliko kwenu, kwa sababu mkono wa Bwana umetoka juu yangu”.  
     
kwa msingi huo Nyakati za Biblia watu wengi waliofanikiwa walifahamu kuwa mkono wa Bwana uko pamoja nao, Hakuwezi kuwa na mafanikio ya aina yoyote kama Mkono wa Bwana ukitupungukia, lakini uko ushindi mkubwa sana kama Mungu akiunyoosha mkono wake kutenda jambo.

Uweza wa mkono wa Bwana

·         Mkono wa Mungu ukinyoosha kila kilicho kigumu kinashughulikiwa Kutoka 3:19-20 Biblia inasema hivi “19. Nami najua ya kuwa huyo mfalme wa Misri hatawapa ruhusa mwende zenu, la, hata kwa mkono wa nguvu. Nami nitaunyosha mkono wangu, na kuipiga Misri kwa ajabu zangu zote, nitakazofanya kati yake, kisha baadaye atawapa ruhusa kwenda.” 

·         Mkono wa Bwana ukinyooshwa hakuna jambo gumu la kumshinda Hesabu 11:4-15, 18-23, 31-32. “4. Kisha mkutano wa wafuasi waliokuwa kati yao, wakashikwa na tamaa; wana wa Israeli nao wakalia tena, wakasema, N'nani atakayetupa nyama tule? 5. Twakumbuka samaki tuliokula huko Misri bure; na yale matango, na matikiti, na mboga, na vitunguu, na vitunguu saumu; 6. lakini sasa roho zetu zimekauka; hapana kitu cho chote; hatuna kitu cha kutumaini isipokuwa hii mana tu. 7. Na hiyo mana ilikuwa mfano wa chembe za mtama na kuonekana kwake kulikuwa kama kuonekana kwake bedola. 8. Watu wakazunguka-zunguka na kuikusanya, kisha wakaisaga kwa mawe ya kusagia, au kuitwanga katika vinu, kisha wakaitokosa nyunguni, na kuandaa mikate; na tamu yake ilikuwa kama tamu ya mafuta mapya. 9. Umande ulipoyaangukia marago wakati wa usiku, hiyo mana ilianguka pamoja nao. 10. Basi Musa akawasikia watu wakilia katika jamaa zao zote, kila mtu mlangoni pa hema yake; na hasira za Bwana zikawaka sana; Musa naye akakasirika. 11. Musa akamwambia Bwana, Mbona umenitenda uovu mimi mtumishi wako? Kwa nini sikupata neema machoni pako, hata ukanitwika mzigo wa watu hawa wote juu yangu? 12. Je! Ni mimi niliyewatungisha mimba watu hawa wote je! Ni mimi niliyewazaa, hata ikawa wewe kuniambia, Haya, wachukue kifuani mwako, mfano wa baba mwenye kulea achukuavyo mtoto anyonyaye, uende nao mpaka nchi uliyowaapia baba zao? 13. Nipate wapi nyama ya kuwapa watu hawa wote? Kwani wanililia, wakisema Tupe nyama, tupate kula. 14. Mimi siwezi kuwachukua watu hawa wote peke yangu, kwa kuwa ni mzigo mzito sana wa kunishinda. 15. Na kama ukinitenda hivi, nakuomba uniulie mbali, kwamba nimepata fadhili mbele ya macho yako; nami nisiyaone haya mashaka yangu.”

“18. Kisha uwaambie watu hawa, Jitakaseni nafsi zenu kabla ya kesho, nanyi mtakula nyama; kwa maana mmelia masikioni mwa Bwana, mkisema, Ni nani atakayetupa nyama, tule? Maana huko Misri tulikuwa na uheri. Basi kwa sababu hiyo Bwana atawapa nyama, nanyi mtakula. 19. Hamtakula siku moja, wala siku mbili, wala siku tano, wala siku kumi, wala siku ishirini; 20. lakini mtakula muda wa mwezi mzima, hata hapo nyama hiyo itakapotoka katika mianzi ya pua zenu, nanyi mtaikinai, kwa sababu mmemkataa Bwana aliye kati yenu, na kulia mbele zake, mkisema, Tulitoka Misri kwa maana gani? 21. Musa akasema, Watu hawa ambao mimi ni kati yao, ni watu sita mia elfu waendao kwa miguu; nawe umesema, Nitawapa nyama, ili wale muda wa mwezi mzima. 22. Je! Makundi ya kondoo na ng'ombe yatachinjwa kwa ajili yao, ili kuwatosha? Au samaki wote wa baharini watakusanywa pamoja kwa ajili yao, ili kuwatosha? 23. Bwana akamwambia Musa, Je! Mkono wa Bwana umepungua urefu wake? Sasa utaona kwamba neno langu litatimizwa kwako, au sivyo.”

“31. Kisha upepo ukavuma kutoka kwa Bwana, nao ukaleta kware kutoka pande za baharini, nao ukawaacha wakaanguka karibu na kambi, kama kiasi cha mwendo wa siku moja upande huu, na kama kiasi cha mwendo wa siku moja upande huu, kuizunguka, nao wakafikilia kiasi cha dhiraa mbili juu ya uso wa nchi. 32. Watu wakaondoka mchana huo wote, na usiku huo wote, na siku ya pili yote, kuwakusanya hao kware; yeye aliyepata ya upungufu kuliko wenziwe alipata kiasi cha homeri kumi; nao wakawaanika wote kando-kando ya kambi kuizunguka pande zote.”            

Dhiraa mbili  (2 Cubic )ni sawa na Futi Tatu kwenda juu au mita moja, na mwendo wa siku nzima ni sawa na KM.

Siri ya Mkono wa Bwana

·         Isaya anauliza Ni nani aliyesadiki Habari tuliyoileta na mkono wa Bwana amefunuliwa nani? Kisha isaya anaeleza habari za Yesu Kristo na mateso yake ambayo yameleta ukombozi mkuu kwa wanadamu

·         Ni wazi kuwa Biblia inapozungumzia juu ya mkono wa Bwana inaeleza siri iliyo wazi kuwa Yesu ndio mkono wa Bwana ni wazi kuwa ukiiamini injili, Habari njema na kuiamini kazi iliyofanyika msalabani kwamba ni kwaajili yetu, na kuwa Yesu ametunukiwa jina kuu kuliko yote nay a kuwa tukiliitia jina lake tunaokolewa

·         Hakuna jambo litakalokuwa Gumu kwetu, hakuna jambo linaloshindikana Mkono wa Bwana utafunuliwa kwako tu, mweke Yesu mbele, kubali kazi zake usimkatae Yesu utauona uwezo wake, Musa alilia alikata tamaa wanataka Nyama, nitoe wapi nyama Kama nimepata fadhili machoni pako inatosha Heri nife, inawezekana umefikia pointi ngumu sana katika maisha yako, kwamba sasa Mungu uko wapi, kwanini haya yanatokea, heri uniuwe kabala ya aibu hii, yatosha baba lakini nakuthibitishia leo kuwa Mkoo wa Bwana haujapunguka urefu wake

·         Yeye alisema niite nami nitakuitika na kukuonyesha Mambo makubwa na Magumu usiyoyajua

Kizuizi kwa Mkono wa Bwana
·         Isaya 59:1-2 1. “Tazama, mkono wa Bwana haukupunguka, hata usiweze kuokoa wala sikio lake si zito, hata lisiweze kusikia; 2. lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia”. 

 Biblia inaonyesha wazi kuwa ni dhambi tu ndio inaweza kumfanya Mungu aionyeshe mkono wake na ni maovu tu ndio yanayoweze kumfanya asisikie sasa dawa ya hili ni rahisi, lazima tukubali kutubu na Yesu anatusubiri na tukiungama yeye ni mwaminifu na atatusamehe kabisa 1Yohana 1:9 “Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote.”

Na Mkuu wa Wajenzi mwenye Hekima
Rev. Innocent Kamote.

Alhamisi, 23 Februari 2017

WALIO PAMOJA NASI NI WENGI KULIKO WALE WALIO PAMOJA NAO.



ANDIKO LA MSINGI: 2WAFALME 6:15-16 “.Hata asubuhi na mapema mtumishi wake yule mtu wa Mungu alipoondoka, na kwenda nje, kumbe! Pana jeshi la watu, na farasi na magari, wameuzingira mji ule. Mtumishi wake akamwambia, Ole wetu! Bwana wangu, tufanyeje?  Akamjibu, Usiogope; maana walio pamoja nasi ni wengi kuliko wale walio pamoja nao.”

Utangulizi:

Ni muhimu kwa kila Mkristo kuwa na ufahamu kwamba ulimwengu wa kiroho ni halisi, na kuwa kama tulivyojifunza, kwamba kuna vita vya kiroho katika ulimwengu wa roho, kwamba ziko pande mbili zinazoshindana, upande wa Mungu na Shetani na kuwa wakati mwingine vita hii hujitokeza katika hali halisi ya mwilini.

Ili ushindi wetu uweze kuwa Dhahiri,ni muhimu kuwa na uelewa wa kutosha namna na jinsi ambavyo ulimwengu war oho unavyotenda kazi, ujuzi huu wakati wote utakufanya utembee katika ushindi na kuwa mbali na hofu ya jambo lolote linalohsindana nawe.
Nabii Elisha alikuwa moja ya manabii muhimu sana katika Israel, hii ilitokana na uwezo wake mkubwa sana katika kuuona ulimwengu war oho na kujua kila kinachoendelea upande wa maadui wa Israel, kutokana na umuhimu wake siku alipougua na kukaribia kufa, mfalme alilia san asana na kusema “ Baba yangu baba yangu Gagari la Israel na Mpanda farasi wake” 2 Wafalme 13:14 Biblia inesema

Basi Elisha alikuwa ameshikwa na ugonjwa wake uliomwua; naye Yehoashi mfalme wa Israeli akatelemka amtazame, akamlilia mbele yake, akasema, Baba yangu! Baba yangu! Gari la Israeli na wapanda farasi wake!

Kilio hiki kilikuwa kina maanisha mtu huyu anayekufa alikuwa ni wa muhimu kwa Israel kuliko jeshi zima, Elisha alikuwa ametumiwa na Mungu sio tu kama Nabii lakini pia kama Mlinzi na mtetezi wa Izrael na Mfalme pia, Mfalme alijua kuwa kufa kwa Elisha ni sawa na kutoweka kwa Jeshi la Ulinzi la Israel kwa sababu kadhaa wa kadhaa.

·         Elisha alikuwa ni zaidi ya Idara ya Usalama wa taifa kwa Marekani, tunaweza kusema alikuwa ni zaidi ya FBI au CIA, alikuwa na uwezo wa kuona maadui na mipango yao zaidi ya rada kali sana katika Israel inayoitwa “GREEN PINE” Rada hii ina uwezo wa kuhisi hatari kwa zaidi ya KM 400, Elisha alikuwa ni zaidi ya Green Pine”


Pichani ni Rada aina ya Green Pine ambayo imegunduliwa na kuundwa na Jeshi la Israel pekee

·         Ulinzi wa Elisha ulikuwa ni zaidi ya “IRON DOME” hii ni silaha nzito yenye uwezo wa kuhisi mashambilizi ya adui na kufyatua makombora ya kudhoofisha makombora ya adui kabla hayajaleta madhara

 Pichani ni silaha aina ya Irone Dome ni silaha iliyogunduliwa Israel ina uwezo mkubwa sana wa kulinda na kuharibu mashambulizi dhidi ya silaha za adui na vituo vyao

·         Elisha alikuwa ni zaidi ya “DELILAH CRUISE MISSILE” yenye uwezo wa kupiga km 250 ikiwa na uzito wa kg 187 au “PROTECTOR USV RAFAEL” ambazo ni boti zenye uwezo wa kufanya kazi ya boti 9-11 za kijeshi na inauwzo wa kutumiwa na watu sita na kufanya kazi nyingi kwa wakati mmoja, umuhimu wa silaha hizo zote nzito zinazotumiwa na Jeshi la Israel kwa wakati wa sasa zilikuwa sawa na Elisha mmoja tu umuhimu wake kwa ufahamu kuhusu silaha hizo Google Top 10 Most Powerful weapons of Israel pia unaweza kupitia Defencyclopedia.com)

Pichani ni Israel Rafael Protector USV ni chombo chenye uwezo mkubwa sana na chenye kufanya kazi nyingi katika Jeshi la Israel

 Kwa nini Elisha alikuwa wa Muhimu kiasi hicho?

2Wafalme 6:8-14 Biblia inasema “Basi, mfalme wa Shamu alikuwa akifanya vita na Israeli. Akafanya mashauri na watumishi wake, akasema, Kituo changu kitakuwapo mahali fulani. Yule mtu wa Mungu akapeleka habari kwa mfalme wa Israeli, kusema, Jihadhari, usipite mahali fulani; kwa sababu ndiko wanakoshukia Washami. Mfalme wa Israeli akapeleka watu mpaka mahali pale alipoambiwa na yule mtu wa Mungu, na kuhadharishwa; akajiokoa nafsi yake, si mara moja, wala si mara mbili. Basi mfalme wa Shamu moyo wake ukamfadhaika sana kwa ajili ya jambo hili; akawaita watumishi wake, akawaambia, Je! Hamtanionyesha, ni mtu yupi miongoni mwenu aliye upande wa mfalme wa Israeli?, Mmojawapo wa watumishi wake akasema, La, bwana wangu, mfalme; lakini Elisha, yule nabii aliye katika Israeli, humwambia mfalme wa Israeli maneno uyanenayo katika chumba chako cha kulala.  Akasema, Enendeni, mkamwangalie aliko, nipate kupeleka watu kwenda kumchukua. Akaambiwa ya kwamba, Tazama, yuko Dothani. Kwa hiyo akapeleka huko farasi, na magari, na jeshi kubwa; wakafika usiku, wakauzingira mji ule pande zote.”

Unaposona kifungu hicho utaweza kuona umuhimu wa Elisha kwa Israel uwezo wake wa kuona mambo katika ulimwengu war oho ulimpa ujasiri mkubwa kiasi cha kuliteka Jeshi zima la madui wa Shamu, Kijana wake Elisha alikuwa haoini katika ulimwengu wa Kiroho na hiyo aliogopa sana lakini Elisha alimtia moyo asiogope

Kuna watu wengi sana wanaogopa tena wanaogopa nguvu za giza, au wanapoona mapambano ya vita za aina mbalimbali kwa jinsi ya mwili wanaogopa sana woga wao ni kama wa mtumishi wa Elisha shida yao ni kutokuujua ulimwengu wa Kiroho ulivyo

-          Mtu anaweza kuogopa Hirizi tu
-          Mtu anweza kuogopa kuwa ametumiwa njiwa
-          Mtu anwexza kuogopa milio ya Bundi tu wakati wa usiku
-          Mtu anaweza kuogopa akisikia vitu vinatembea juu ya dali au bati
-          Mtu anaweza kuogopa kusikia milio ya Mapaka
-          Mtu anaweza kuogopa kwa sababu tu ameota ndoto mbaya
-          Mtu anaweza kuogopa kwa sababu tu ya nguvu za giza au wachawi na wapiga madogoli
-          Mtu anaweza kuogopa kwa sababu ya vitisho vya aina mbalimbali duniani

Ukijujua ulimwengu wa Roho kwamba tunazungukwa na majeshi ya Malaika hutaweza kuogopa Elisha alikuwa anajua kuwa analindwa na nguvu za kupita kawaida, Malaika wenye farasi za moto walikuwa wamemzingira pande zote, ikiwa Elisha wa agano la kale alikuwa analindwa kiasi hiki sisi nasi tunalindwa na nguvu za Mungu, Zaburi 3:5-6, 27:3 Waebrania 1:14 Roho watumikao kuwahudumia wale watakaourithi wokovu wapo kutuhudumia na kutulinda hivyo hatupaswi kuogopa

 2Wafalme 6; 16-17 “Akamjibu, Usiogope; maana walio pamoja nasi ni wengi kuliko wale walio pamoja nao. Elisha akaomba, akasema, Ee Bwana, nakusihi, mfumbue macho yake, apate kuona. Bwana akamfumbua macho yule mtumishi; naye akaona; na tazama, kile kilima kilikuwa kimejaa farasi na magari ya moto yaliyomzunguka Elisha pande zote.”
 Pichani ni silaha ya Mashambulizi iliyogunduliwa Israel iitwayo "Delilah Cruise Missile"

Mungu akikufungua macho ukaona namna unavyolindwa na majeshi ya Malaika hutaweza kuogopa Daudi akasema Jeshi lijapojipanga kupigana name Moyo wangu hautaogopa”