Alhamisi, 6 Oktoba 2016

Uhusiano wa Kanisa na Israel


Wakristo wengi hawaelewi uhusiano ulioko kati ya Kanisa na Taifa la Israel Ni muhimu kufgahamu kuwa hatuwezi kuepuka nlabda kwa shingo ngumu kuwa kwa namna yoyote ile uhusiano ulioko kati ya kanisa yaani wakristo na wana wa Israel kuwa tuna uhusiano katika ilimwengu wa Roho ingawa tunaweza tusiwe na uhusiano wa kitaifa au kibalozi lakini katika Mungu Israel wanaungwa mojakwa moja na Kanisa Tutajifunza somo hili kwa kuzingatia vipengele  vitatu vifuatavyo;- 

  • ·         Israel imewekwa wakfu
  • ·         Kwa nini niipende Israel
  • ·         Uhusiano wa Kanisa na Isarel

Israel imewekwa wakfu.

Neno wakfu au kuwekwa wakfu maana yake ni kutenga kitu au watu au kutakasa kitu au mtu ili atumike kwa utukufu wa Mungu na si vinginevyo au kulaani kisitumike kwa namna nyingine isipokuwa Mungu tu na kwa sababu hiyoi kitu au mtu anapokuwa amewekwa wakfu anafanyika kuwa mali ya Mungu Kutoka 13;2, 29;1

     Katika maana hiyo basi ni muhimu kufahamu kuwa Israel ni Taifa au kabila na jamaa ambayo imewekwa wakfu, imeteuliwa  na kutengwa  kwa kusudi maalumu hivyo wao ni mali ya Mungu Kumbukumbu 14;2,4;20,Zaburi 135;4. Israel ni Taifa la Mungu na Yerusalem  ni mji wake mtakatifu na kamwe Mungu hawezi kuwasahahu mji hu na inchi hii na watu wake Zaburi 137;5-6, Mungu wa Israel ndiye Mungu tunayemuabudu  wokovu tulio nao umetoka kwa wayahudi, Masihi tunayemwadhimisha alikuwa myahudi na ametoka kwa wayahudi, hata mifumo ya ibada zetu tumerithi kwa wayahudi na Biblia tuliyo nayo kwa sehemu kubwa imeandikwa na wayahudi na manabii wote tunaowaamini ni wa jamii ya kiytahudi  kwa msingi huo kanisa linapaswa kuwa na uzalendo wa kisayuni kwa wana wa Israel na kuonyesha kuwapewnda na kuwajali na kuwa wanatuhusu, Leo hii vyomboi vya habari  na jamii ya watu wengine wa kisiasa na ulimwengu wa Kiislamu wamekuwa na mtazamo duni na hafifu dhidi ya Israel  na hivyo kuichukia na wakati mwingine kuilaani katika vitendo kadhaa jambo hili linapaswa kuchukuliwa kwa umakini na watu wanayoyajua maandiko Hili ni taifa masihi na ni taifa la Mungu  ardhi hii aliyopewa Ibrahimu alipewa na Mungu kwa hiyo kila mkristo anapaswa kuielewa siri hii na kuipenda Israel

Kwanini niipende Israel

1.       Kuipenda Israel ni kumpenda Mungu

Amri iliyo kuu kuliko zote ni kumpenda Bwana Mungu Kumbukumbu 6;5, kama tunampenda Mungu kwa dhati , bila hska pia tutapenda kile anachokipenda  na kuchukia anacho kichukia , Maandiko yanaonyesha kuwa Mungu anaipedna Israel na mji wake Yerusalem Zaburi 87;1-2 Labda mtu atasema sisi wenyeji wetu uko mbinguni na kama Abrahamu tunautazamia mji wenye misingi ambao mwenye kuubuni na kuujenga ni Mungu  Waebrania 11;10, Wafilipi 3;20,Wagalatia 4;26 dhana hiyo ni kweli kabisa  kila mkristo anajua kuwa kuna mji Yerusalemu ya mbinguni na Yesu alisema Yerusalemu huu wa sasa hatuwezi kukwea na kwenda kuabudu Yohana 4;21-24 Lakini Maneno ya Bwana yesu yanshitua zaidi unaposoma katika Mathayo 5;34-35 kluwa usiape kwa Yerusalem nmaana ndio mji wa mfalme mkuu (Yaani Mungu) na Yesu alisema kuwa mji huu utakanyagwa na mataifa kwa wakati tu Luka 21;24 uko wakati ambapo Heshima na utukufu wa Mungu utarudi na Mungu mwenyewe ataiatawala Dunia  nzima kuanzia hapa Israel Zekaria 14;4,9.


Pichani ni jiji la Yerusalem ambalo wayahudi wameapa hautagawanywa milele ,Upande wa kushoto ni Msikiti (The Dome of Rock) ukiwa umejengwa mahali ambapo palikuwa ni Hekalu la Wayahudi, hapo ni mahali makini wayahudi hawajapagusa bado,Waislamu huamini ndipo alipopaa Muhamad kwenda mbinguni (Uongo mtupu),na ni kibla ya kwanza kabla ya Makka.Ukouwezekano kwa wayahudi wenye msimamo mkali wa kidini kulijenga tena hekalu hilo mahali hapa 
(Picha kwa hisani ya maktaba ya Mwandishi wa somo Innocent Samuel Kamote.)

2.       Kuipenda Israel ni ufunguo wa mafanikio

Mungu amekuwa mwema kwa Israel kwa karibu miaka 1720 hivi Waisrael hawakuweko katika inchi yao mpaka mwaka wa 1948 waliporudi ambapo mji wao mkuu kwa wati huo ulikuwa ni Tel-aviv-Jafa ambao una bandari na wakati huo Yerusalemu haukuwa mikononi mwao Leo mji huu uko mikononi mwao Mungu ameanza kuirehemu Israel sawa na Zaburi ya 102;13-14 katika wakati huu ambapo Israel inazungukwa na mataifa adui wasio watakia mema hata kidogo ni muhimu kuipenda Israel na kuwaombea amani  kwani kwa kufanya hivi tunaruhusu Baraka biunafsi na za taifa letu kwa ujumla Zaburi 122;1-9

3.       Kwa sababu kanisa ni tawi na Israel ni shina yaani (asili).

Mkristo awaye tyote na mchungaji au kikundichochote cha faragha wanapaswa kutambua kuwa Israel ndio shina la wokovu wetu  au ni sawa na tawi lililopandikizwa katika shina ambalo ka asili ni Israel Warumi 11;11-21  Mungu anatuionya kanisa kuwa sisi ni tawi tu lililopandikizwa na Israel ndio shina halisi, kutokutii kwao na kumkatraa maishi kumeleta wokovu mkubwa kwa amataifa mengine kluweza kufurahia neema hii ya wokovu na baraka zitakuwa kubwa zaidi kama wakitii, kwa msingi huo kutokuipenda Israel ni kuchukia asili huku sisi tukiwa ni tawi tu lililopandikizwa Yesu alionyesha dhahiri kuwa wokovu wetu asili yake unatoka kwa wayahudi Yohana 4;22  Biblia yote kuanzia Mwanzo mpaka Malaki ambayo tunaiita Agano la kale  ni kitabu cha Mungu kwetu lakini kwa asili ni Biblia ya waebrania yaani wayahudi kwa msingi huo huwezi kamwe kumteganisha Mkristo na Myahudi adui wa wayahudi lazimam pia anakuwa ni adui wa wakristo anayetaka kuifuta Israel Bila shaka pia atataka kuufutilia mbali ukristo kwa msingi hio kila mkristo anawajibika kuikumbuka Israel

4.       Kuilaani Israel ni kujilaani na kuibariki Israel ni kujibariki

Tangu mwanzo Mungu alipomuita Ibrahimu ambaye ndiye baba wa Taifa hili alimtamkia Baraka zitakazoambatana na wale watakaombariki lakini pia Mungu aliweka laana kwa wale watakaomlaani Ibrahimu Mwanzo 12;1-3,26;1-6,28;10-15 Baraka hizio na matamko haya yanawahusu Israel hata leo kwa msingi huo kila mtu anapaswa kufahamu kuwa Mungu yuko nyuma ya maswala yote ya Israel tangu wakati wa Ibarahimu na uzao wake  wale watakaomnenea mema watabarikiwa na wale wanaomnenea vibaya watalaaniwa. Tafuta ukaone katika historia wale wote waliowahi kuitishia Israel waliishia wapi na Historia itakuambia kuilaani Israel ni kujiweka katika hatari

Uhusiano wa Kanisa na Israel.

Tumeona kwa namna Fulani uhusiano ulioko katia ya Israel na kanisa mwanzoni tulipokuwa tunazungumzia kwanini niipende Israel, Kanisa linapaswa kuelewa kuwa Mungu yuko pamoja na Israel na kuwa tunauhusiano mmoja kama tulivyoona sisi nasi tunapaswa kuhakikisha kuwa katika shughuli zetu za kimisheni pia tunawalenga wayahudi ili nao waokolewe Paulo mtume alikuwa na huruma sana dhidi ya ndugu zake hawa yaani wayahudi ambao sisi pia ni ndugu zetu  kwamba waokolewe na alikuwa akiwaombea sana Soma warumi 10;1 sisi nasi tunapaswa kuhakikisha kuwa tunawahubiria wokovu kwa kawaida kunakuwa na kitu cha ziada sana myahudi anapookoka wengi waliookolewa wametumiwa sana na Mungu aktika kuupanua Ufalme wake akiwemo Muhubiri maarufu Mourice Cerrulo na Benny Hinny Mungu na alisaidie kanisa kukumbuka kuwa na mkakati maalumu kuomba na kuhakikisha kuwa injili inawafikia wao pia aidha ni muhimu kanisa kuwaombea viongozi wetu wa kitaifa kuwa makini na kauli zao za kisiasa wanazozitamka dhidi ya Utendaji wowote wa kisiasa wa Israel, Wamarekani wengi wanaifahamu siri hiyo, kama unailaani Israel kasha unakwenda Marekani kuomba misaada ambao wao kuybarikiwa kwao kunatokana na kuwafanyia mema wayahudi je unadhani utafaidika au umasikini utaendelea kutufunika tu, wayahudi ni Ndugu zetu, Mungu wao ni Mungu wetu, manabii wao ni manbabii wetu, Mwokozi wao ni mwokozi wetu Biblia yao ni Biblia yetu, tumaini lao ni tumaini letu, mji wao ni mji wetu nukombozi wao ni ukombozi wetu tunauhusiano wa kudumu na Israel

somo limeandaliwa na 

Rev. Innocent Kamote
Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima

Jumamosi, 24 Septemba 2016

Umuhimu wa maombi wakati wa mambo magumu!



Andiko la msingi: Zaburi 46:1-2Mungu kwetu sisi ni kimbilio na Nguvu, Msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso, kwa hiyo hatutaogopa ijapobadilika nchi, Ijapotetemeka milima moyoni mwa Bahari

              Gereza ambalo Paulo na Sila walifungwa wakaomba na vifungo vikaachia huko Philipi


Utangulizi.
Kwa mujibu wa Mafundisho ya kibiblia kuhusu Maombi, Biblia inatoa maelekezo kwamba imetupasa kumuomba Mungu siku zote bila kukata tamaa Luka 18:1Akawaambia mfano ya kwamba imewapasa kumwomba Mungu siku zote , wala wasikate tamaa” kwa lugha nyingine imetupasa kumuomba Mungu siku zote bila kukoma 1Wathesalonike 5:17Ombeni bila kukoma” ni wazi kuwa  Biblia inatia moyo kuwa waombaji na kila siku kumuomba Mungu na kushukuru, ni katika hali zote na kwa namna yoyote imetupasa kuomba Maombi ni muhimu sana katika maisha yetu, na katika kudumisha uhusiano wetu na Mungu, Yesu alikuwa Muombaji, hatuna budi kuunganisha ucha Mungu wetu na maombi, kuacha maombi ni sawa na kuacha Ukristo!

Lakini kila mmoja anaweza kujiuliza kwa nini leo mkuu wa wajenzi anataka au anazungumzia Umuhimu wa maombi wakati wa mambo Magumu, Kwa ujumla maombi yanapaswa kuwa sehemu na tabia ya kila amwaminiye Yesu Kristo, Na pamoja na hayo binafsi sipendi kuomba wakati wa mambo magumu, nafurahia sana kuomba wakati wa amani, hata hivyo kibiblia wakati wa mambo magumu sio wakati wa kuacha kuomba ni wakati wa kuongeza bidii katika kuomba. Biblia inatufundisha kuwa nyakati za Kanisa la kwanza wakristo wa Karne ya kwanza walikuwa waombaji, sehemu kuu ya ibada ya kawaida ya kanisa ilikuwa ni maombi, waliomba Mungu siku zote, Biblia inasema walikuwa wakidumu kwa moyo mmoja katika kusali Matendo 2:14Hawa wote walikuwa wakidumu kwa moyo mmoja katika kusali,pamoja nao wanawake, na Mariamu mama yake Yesu na ndugu zake” Unaona! Biblia inaonyesha kuwa wanafunzi na mama yake Yesu na ndugu zake walidumu katika kuomba hii ndio ilikuwa tabia ya nyakati za kanisa la kwanza.

Lakini hata hivyo tunaweza kuona katika biblia Kanisa la kwanza wakiongeza Maombi zaidi wakati wa mambo magumu, kama andiko la msingi pale juu linaonyesha kuwa Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, ni msaada utakaoonekana tele wakati wa Mateso, hii maana yake ni kuwa ni lazima na ni muhimu kuliitia jina la bwana zaidi wakati wa mateso na majaribu Matendo 4:23-31 Biblia inasema

 “23. Hata walipofunguliwa, wakaenda kwa watu wao, wakawapasha habari ya mambo yote waliyoambiwa na wakuu wa makuhani na wazee. 24. Nao waliposikia, wakampazia Mungu sauti zao kwa moyo mmoja, wakisema, Mola, wewe ndiwe Mungu, ndiwe uliyefanya mbingu na nchi na bahari na vitu vyote vilivyomo; 25. nawe ulinena kwa Roho Mtakatifu kwa kinywa cha babaetu Daudi, mtumishi wako, Mbona mataifa wamefanya ghasia, Na makabila wametafakari ubatili? 26. Wafalme wa dunia wamejipanga, Na wakuu wamefanya shauri pamoja Juu ya Bwana na juu ya Kristo wake. 27. Maana ni kweli, Herode na Pontio Pilato pamoja na Mataifa na watu wa Israeli, walikusanyika katika mji huu juu ya Mtumishi wako mtakatifu Yesu, uliyemtia mafuta, 28. ili wafanye yote ambayo mkono wako na mashauri yako yamekusudia tangu zamani yatokee. 29. Basi sasa, Bwana, yaangalie matisho yao; ukawajalie watumwa wako kunena neno lako kwa ujasiri wote, 30. ukinyosha mkono wako kuponya; ishara na maajabu vifanyike kwa jina la Mtumishi wako mtakatifu Yesu. 31. Hata walipokwisha kumwomba Mungu, mahali pale walipokusanyika pakatikiswa, wote wakajaa Roho Mtakatifu, wakanena neno la Mungu kwa ujasiri.”

 Unaweza kuona Kumbe wakati wa majaribu na mateso pia ni wakati mzuri wa kuongeza bidii na kumuomba Mungu kwa nguvu zaidi, Muda usingeliweza kutosha kwa nyongeza ya mifano zaidi ya kibiblia lakini biblia inaonyesha pia Paulo na Sila walipokuwa Gerezani yaani wakati wa mateso waliendelea kukazia ibada Matendo 16:25Lakini panmapo usiku wa manane Paulo na Sila walikuwa wakimwomba Mungu na kumwimbia nyimbo za kumsifu na wafungwa wengine walikuwa wakisikiliza” unaona ukiendelea kusoma utaweza kuona ni nini kilitokea Mungu alipowajibu maombi yao hivyo Biblia inatufundisha kuwa tusikate tamaa na kuwa hata wakati wa mambo magumu inatupasa kuomba 

1.       Kwa nini inatupasa kumuomba Mungu hata wakati wa Mambo Magumu
2.       Maombi ni msaada kutoka kwa Mungu wakati wa mambo Magumu Zaburi 3:3-8;34:4
1.Bwana, watesi wangu wamezidi kuwa wengi, Ni wengi wanaonishambulia, 2. Ni wengi wanaoiambia nafsi yangu, Hana wokovu huyu kwa Mungu. 3. Na Wewe, Bwana, U ngao yangu pande zote, Utukufu wangu na mwinua kichwa changu. 4. Kwa sauti yangu namwita Bwana Naye aniitikia toka mlima wake mtakatifu. 5. Nalijilaza nikalala usingizi, nikaamka, Kwa kuwa Bwana ananitegemeza. 6. Sitayaogopa makumi elfu ya watu, Waliojipanga juu yangu pande zote. 7. Bwana, uinuke, Mungu wangu, uniokoe, Maana umewapiga taya adui zangu wote; Umewavunja meno wasio haki. 8. Wokovu una Bwana; Baraka yako na iwe juu ya watu wako.

3.       Maombi ndio njia ya Mungu ya kutulinda na nguvu na utendaji wa yule muovu Mathayo 6:13, Efeso 6:12.
4.       Maombi ndio njia pekee ya kutuletea amani tunapokutana na Magumu na hali za kutisha na kukatisha tamaa Wafilipi 4:4-7
5.       Maombi yanaweza kupindulia mbali vikwazo vya aina zote Marko 11:23-24
6.       Maombi ndio njia ya kututia moyo wakati wa kuvunjika Moyo Wakolosai 1:9-11
7.       Maombi yana nguvu ya kuhairisha jambo baya Esta 4:15-17, Daniel 2:13-19
8.       Maombi ndio njia ya kupokea nguvu za kiroho na ujasiri wakati wa vita za kiroho Matendo 4:23-31

Bila shaka sasa unaweza kuona na kuamini kupitia maandiko, kuwa wakati wa mateso na Mapito na mambo magumu ya aina yoyote ile, huo sio wakati wa kukata tamaa na kuacha kuomba ni wakati wa kuzidisha maombi na kumtegemea Mungu, Na Mungu hujitokeza  kwa viwango vikubwa tukionyesha kumtegemea yeye katika maombi wakati wa Mahitaji yetu katika wakati mgumu.

Rev. Innocent Kamote
Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima.

Jumapili, 18 Septemba 2016

MUNGU SI MTU ASEME UONGO


Wengi wetu tutakuwa tunafahamu kuwa Mungu wetu ana tabia ya uaminifu na mkweli anapokuwa ameahidi jambo ni muhimu kufahamu kuwa atalifanya (2 Koritho 1;20,)Biblia inasema hivi:-

“Maana ahadi zote za Mungu zilizopo katika yeye ni Ndiyo; tena kwa hiyo katika yeye ni Amin; Mungu apate kutukuzwa kwa sisi.”

 Tabia za Mungu kamwe haziwezi kufananishwa na za wanadamu ambao wao hugeuka geuka kwa sababu ya kigeugeu

 (Yakobo 1;17)Biblia inasema hivi:-  Kila kutoa kuliko kwema, na kila kitolewacho kilicho kamili, hutoka juu, hushuka kwa Baba wa mianga; kwake hakuna kubadilika, wala kivuli cha kugeuka-geuka.”

Kwa msingi huo basi hatupaswi hatupaswi kumdhani Mungu kuwa ni kama mwanadamu yeye anapohaidi au kusema ni lazima atatenda  na kulifikiliza na kamwe hawezi kujuta kama mwanadamu kuwa kwanini alihaidi YEYE SI MTU HATA ASEME UONGO Hesabu 23;19,katika kujifunza kwetu kuhusu uaminifu wa Mungu leo tutaangalia mfano wa maisha ya Yusufu tangu Mungu alipomuahidi kwa ndoto kuwa atawatawala ndugu zake  Hali ilikuwa tofauti kana kwamba ndoto za Yusufu zinakwenda kupotelea mbali je mambo yalikuaje? Miaka kumi na mitatu ilipita na ahadi za Mungu zikatimizwa angalia mchoro huu.

Maelezo kutoka katika picha ya Grafu ya maisha ya Yusufu



·         Mwanzo 37;5-11- Yusufu alipewa Ndoto Na Mungu kuwa atakuwa Kiongozi mkubwa kiasi ambacho Nduguze watamuinamia
·         Mwanzo 37;18-22 – Ndugu wa Yusufu kwa wivu uliosukumwa na Ibilisi walitaka kumuua
·         Mwanzo 37;26-27- Mungu alimuokoa Yusufu na Kifo kwa wazo la Yuda la kumuuza Ndugu yao
·         Mwanzo 39;2-6  - Yusufu alinunuliwa na Potifa Kamanda wa Jeshi la farao na kuwa mkubwa
·         Mwanzo 39;7-20  - Majaribu Makubwa yalimpata kwa kusingiziwa kubaka na akafungwa
·         Mwanzo 39;21-23  - Mungu aliyatunza maisha yake Gerezani akawa kiongozi wa wafungwa
·      Mwanzo 41;40,42,42;5-6,43;26 – Mungu aliiitimiza Ndoto ya Yusufu Na akawa mkubwa na nduguze walimsujudia ilichukua miaka 13 kwa ndoto ya Yusufu kuwa kweli, Mungu alitunza ahadi yake Mungu si Mtu hata aseme uongo  

    Kijana Yusufu akiwa anatupwa shimoni kwa kusudi la mkuuawa, na kijana Yusufu akiwa anauzwa utumwani
   Yusufu akisimikwa kumsaidia farao kama makamu wa rais wa Taifa kubwa Duniani nyakati hizo
 
 Mambo yatupasayo Kufanya
1. Kuendelea Kumuamini Mungu ( Yusufu alimuamini Mungu katika maisha yake)
2. Kuendelea kuwa mwaminifu Yusufu hakutaka kumtenda Mungu dhambi ambazo zingeweza kuharibu Ndoto yake, hata ingawa Mungu ni Mwaminifu katika upande wetu sisi nasi tunahitaji kutunza uaminifu wetu kwake kusudi aweze kutubariki
3. Ni lazima tuwe wavumilivu hakuna ahadi ya Mungu ambayo haitatimizwa kwetu, lakini kwa uvumilivu tutazipata ahadi, ni lazima tuwe kama wakulima ambao huvumilia tangu mvua ya kwanza



Waebrania 6:13-18 "13. Kwa maana Mungu, alipompa Ibrahimu ahadi, kwa sababu alikuwa hana mkubwa kuliko yeye mwenyewe wa kumwapa, aliapa kwa nafsi yake, 14.akisema, Hakikayangu kubariki nitakubariki, na kuongeza nitakuongeza. 15. Na hivyo kwa kuvumilia akaipata ile ahadi. 16. Maana wanadamu huapa kwa yeye aliye mkuu kuliko wao; na kwao ukomo wa mashindano yote ya maneno ni kiapo, kwa kuyathibitisha.  17. Katika neno hilo Mungu, akitaka kuwaonyesha zaidi sana warithio ile ahadi, jinsi mashauri yake yasivyoweza kubadilika, alitia kiapo katikati;  18. ili kwa vitu viwili visivyoweza kubadilika, ambavyo katika hivyo Mungu hawezi kusema uongo, tupate faraja iliyo imara, sisi tuliokimbilia kuyashika matumaini yale yawekwayo mbele yetu;"  

 Yakobo 5:7-8."7. Kwa hiyo ndugu, vumilieni, hata kuja kwake Bwana. Tazama, mkulima hungoja mazao ya nchi yaliyo ya thamani, huvumilia kwa ajili yake hata yatakapopata mvua ya kwanza na ya mwisho.   8. Nanyi vumilieni, mthibitishe mioyo yenu, kwa maana kuja kwake Bwana kunakaribia

Jumamosi, 3 Septemba 2016

MADHARA YA KUWAGUSA MASIHI WA BWANA.


Mstari wa Msingi: Zaburi 105: 14-15 Biblia inasema “Hakumwacha mtu awaonee, Hata wafalme aliwakemea kwaajili yao. Akisema, Msiwaguse masihi wangu wala msiwadhuru nabii zangu

Kupakwa mafuta kuliunganisha unganisho la Kiroho na uwezo wa kufanya kazi uliyoitiwa na Mungu

He allowed no man to do them wrong Amplified, He allowed no one to oppress NIV, He permitted no one to do them wrong NKJV

Kusudi la Somo:- (uwakumbushe watu kunyenyekea kwa wenye uwezo na mamlaka  na kutii na kuwa tayari kwa kila kazi njema Tito 3:1)

Watu wote duniani waliookoka na wasiookoka wanapaswa kuwa na ufahamu na kuwa na hekima juu ya ujumbe huu muhimu katika maisha yao ili wasije wakajikuta wanapoteza Neema ya Mungu na kuwa na maisha yaliyojawa na mikosi na mapigo mazito yasiyoweza kuzuilika kwa sababu ya kutokuwa na ufahamu katika neno la Mungu na tukajikuta tunamchukiza Mungu, Bwana na ampe neema na hekima kila mmoja wetu kuwa na ufahamu katika somo hili katika jina la Yesu amen. Tutajifunza somo hili kwa kuzingatia vipengele vine vifuatavyo:-
 
·         Maana ya Neno  masihi
·         Onyo la kutokuwagusa masihi wa Bwana
·         Madhara ya kuwagusa masihi wa Bwana
·         Jinsi ya kufanya.

MAANA YA NENO MASIHI

Neno masihi limetokana na neno la kiibrania MESIAH au MESSIAS  na limejitokeza kwa mara ya kwanza katika 1Samuel 2:10, ambalo maana yake ni mtiwa mafuta au mwenye kuwekwa wakfu kwa kutiwa mafuta ili awe Kuhani, Mfalme au nabii, kwa kiyunani ni Kristo, Neno masihi mahali hapo linatumika katika mazingira tofauti sana na ile tunayoitumia kwa Bwana Yesu Kristo, Nyakati za Agano la kale mtu alipochaguliwa na Mungu kuwa kuhani, mfalme au nabii aliwekwa wakfu kwa kutiwa mafuta na hivyo kuitwa masihi, mafuta hayo yaliyomiminwa juu yao kwa jinsi ya mwili yaliwakilisha maswala muhimu katika jinsi ya kiroho 1Samuel 16:1-13, Roho Mtakatifu alishuka juu ya mtu aliyepakwa mafuta kumuwezesha mtu huyo, kuwa na uwezo wa kiungu na wa kupita kawaida katika kuyatimiza majukumu yake, ilifanyika hivyo katika nyakati za agano la kale kwa vile Roho Mtakatifu alikuwa hajaja maalumu bado, Nyakati za sasa hatutiwi mafuta katika namna ya kimwili, Lakini Roho wa Mungu mwenyewe ndiye anayemchagua mtu kwa utumishi alioukusudia  na kumpaka Mafuta Matendo 13:1-3, aidha pia katika agano jipya watumishi wa Mungu wanapowekewa mikono na kubarikiwa wanakuwa wametiwa mafuta katika namna ya rohoni, Kumbuka kuwa ni Mungu mwenyewe ndiye anayechagua “Nitengeeni Barnaba na Saul kwa kazi ile niliyowaitia” watu wa Mungu

Mafuta ilikuwa na hata sasa ni alama ya Roho Mtakatifu, mtu alipopakwa mafuta Roho alimuwezesha kuwa na vipaji vya kiroho vya kuweza kutimiza jukumu alilokabidhiwa, Mfano Yesu Kristo kama Masihi hakupakwa mafuta kwa jinsi ya mwili, lakini alijiliwa na Roho Mtakatifu na kuongozwa katika kuyatekeleza majukumu yake Luka 3:21-22,4:1,18-19 Kupakwa mafuta kwa Yesu Kristo kulimfanya awe na uwezo wa kipekee katika kuitimiza huduma yake hivyo Yesu ni Masihi ni mpakwa mafuta ni Kristo, Mtu anapomwamini Yesu kuwa bwana na mwokozi wamaisha yake Roho wa Mungu anakaa ndani yake kwa hivyo kibiblia mafuta yanakaa ndani yake 1Yohana 2:26-27, Yohana 14:25-26, hivyo watu waliookolewa ni wapakwa mafuta roho Mtakatifu anakaa ndani yetu 1Wakoritho 3:10, Hata hivyo kutoka miongoni mwao Roho Mtakatifu ambaye ndiye Bwana wa Mavuno, huwaita watu katika huduma Matedno 13:2, watumishi wa Mungu wanaoitwa katika huduma maalumu za utumishi, Roho wa Mungu anakuwa juu yao kwaajili ya kutimiza huduma waliyoitiwa, kwa hiyo nao huitwa wapakwa mafuta, wapakwa mafuta hao wanakuwa wametumwa na Mungu na hivyo huyanena maneno ya Mungu Yohana 3:24 wao huubiri kweli yote kwa ujasiri bila kuichakachua injili, watasimamia kweli yote huku wenyewe wakiwa kielelezo cha injili wanayoihubiri, watakemea, wataonya, watatia moyo na hawatahubiri khadihi za kutungwa na wanadamu Mathayo 5:48, watahubiri utakatifu 1Petro 1:13-16,Waebrania 12:14 watafanya na kutenda kama Yesu Kristo mwenyewe, Masihi wa Bwana wanaishi kwa haki na utauwa, bila kuwa na lawama zilizo na ukweli 1Wakoritho 1:11, 1Wathesalonike 2:10, Biblia inasema tutawatambua kwa matunda yao.

Aidha masihi wa Bwana watafanya kazi ya kulitetea jina la Bwana lisichafuliwe au kutukanwa, Manabii makuhani na manabii nyakati za agano la kale hawakujali sana watu maadui zao wanasema nini juu yao bali, walijali sana maaduin au watu waliokuwa wakitaka au kumkufuru Mungu.

Masihi wa Bwana watahubiri Utakatifu, Ni  muhimu kufahamu kuwa shetani hawezi  kuhubiri  utakatifu na ni rahisi kupambambanua kati ya mtumishi wa shetani na  Mtumishi wa Mungu, sifa  mojawapo ya Mtumishi wa shetani ni kuhubiri maneno yake. ( maneno yao) na  watajifanya ni watumishi  wa haki na watahubiri   mambo   ambayo ukiwauliza kwa wameyapata wapi au yameandikwa wapi, watakuambia  hii  ndiyo  sheria au desturi ya kanisa:  watajitungia mambo yao  na  hawataihubiri  neno, shetani kamwe hawezi   kuhubiri  utakatifu   na watumishi wa shetani  hawawezi  kamwe  kuishi  katika  utakatifu  na akawa  kielelezo  na hawezi  kuwafanya  watu waokolewe na  kukaa  katika  usafi  na utakatifu: (shetani hawezi kumtoa  shetani )

ONYO LA KUTOKUWAGUSA MASIHI  WA BWANA. Zaburi 105: 14- 15,  I Nyakati  16: 21-22
Ni muhimu kufahamu kuwa Maandiko matakatifu yanatoa maonyo na yamejaa mafundisho na mifano ya kutosha yanayotoa maonyo dhidi ya kuwagusa masihi wa Bwana

Kuwagusa huku ni pamoja  na kuwasengenya, kuwanena  vibaya, kuwachafulia huduma zao ili waonekane  wabaya  hawafai kama walivyomchafua  Yesu  kwa  kusema  anatoa pepo kwa Nguvu za mkuu wa pepo Bezelzebul, kuwadhalilisha, mbele za  watu  wengine  kuwalia huduma zao ,  kuwaua moja kwa moja  au kuwadhuru kwa mabaya au kuwatukana huko ni kuwagusa  masihi wa Bwana au kuwanyanyasa, kuwavunjia Heshima, kuwadhulumu, na kuwatendea mabaya  kumgeuza  mkewe, hata  kama ni mfalme  atashughulikiwa  atadhibitiwa na  Mungu Zakaria 2: 8  kuwagusa hawa ni kugusa  mboni  ya jicho la Mungu;  Hivyo hata kama sisi ni  wachungaji tunapaswa kuangalia walio juu  yetu  kwani wao  ni masihi wa Bwana. Kwa nini Biblia inaonya kutokuwagusa masihi wa Bwana au wapakwa mafuta?

1.       Wao ni Mawakili wa Mungu- Tito. 1:7,8,9 “Maana imempasa askofu(mwangalizi) awe mtu asiyeshitakiwa neno, kwa kuwa ni wakili wa Mungu; asiwe mtu wa kujipenda nafsi yake, asiwe mwepesi wa hasira, asiwe mlevi wala mgomvi, asiwe mpenda mapato ya aibu; bali awe mkaribishaji, mpenda wema,mwenye kiasi,mwenye haki, mtakatifu,mwenye kudhibiti nafsi yake, akilishika lile neno la imani vilevile kama alivyofundishwa,apate kuweza kuwaonya watu kwa mafundisho yenye uzima, na kuwashinda wenye kupinga.”

2.       Hawajichukulii wenyewe heshima hii Waebrania 5:4 “Na hapana mtu ajitwaliaye mwenyewe Heshima hii ila yeye aitwaye na Mungu kama vile Haruni

3.       Biblia imeagiza kuwatii na kuwanyenyekea wanaotuongoza Waebrania 13:17 “watiini wenye kuwaongoza  na kuwanyenyekea  maana wao wanakesha kwaajili ya roho zenu, kama watu watakaotoa hesabu, ili kwamba wafanye hivyo kwa furaha wala si kwa kuugua maana isingeliwafaa ninyi

4.       Mungu huwaheshimu watu wanaomtumikia Yohana 12:26 “Mtu akinitumikia na anifuate nami nilipo na mtumishi wangu atakakapokuwepo, tena mtu akinitumikia Baba atamheshimu

MADHARA YA KUWAGUSA MASIHI WA BWANA.

Muda usingetutosha kuweza kuangalia mifano  mmoja moja katika Biblia juu ya watu waliowagusa masihi wa Bwana na kushughulikiwa kwa makini na Mungu alivyoonyesha  ghadhabu juu yao hata hivyo tutaangalia mifano kadhaa:

1.       MARIAMU: (Hesabu 12: 1- 9) Miriamu alikuwa nabii mke lakini alinena vibaya juu ya uongozi wake Musa na  alishughulikiwa kwa kupigwa ukoma.

2.       FARAO:  Alichukua mke wa Ibrahimu kwa kutumia mamlaka ya kifalme alivyokuwa nayo na alishughulikiwa kwa mapigo mazito sana.( Mwanzo. 12: 14- 17

3.       ABIMELEKI:  Alipotamani kumchukua Sarai mke wa Ibrahim Mungu alimtandika( MWANZO 20: 1- 4, 6-8,14)

4.       YEROBOAMU: ( I Falme 13: 1- 4

5.       ASKARI WALIOTAKA KUMKAMATA  ELIYA  Bila kuonnyesha unyenyekevu  ( 2 Falme 1: 5- 15)

6.       WATU WALIOMFANYIA MZAHA ELISHA  yaani vijana waliomtania Upara wake (2 Falme 2: 23- 25)

7.       MWAMLEKI Aliyejidai kuwa ameuua  SAULI ( 2  Samwel 1: 1-16)

8.       Herode Baada ya Kumuua Yakobo Matendo 12: 1-4,20-24

JINSI YA KUFANYA.

-          Ni muhimu kufahamu kuwa Mungu anaheshimu sana mafuta na kwa sababu hiyo si vema kupuuzia mafuta yaliyo juu ya watumishi wake kwani kwa kufanya hivyo kuna madhara yawezayo kutupata
-          Ni muhimu pia kufahamu kuwa kupakwa mafuta haipaswi kuwa sababu ya kuwafanya wapakwa mafuta hao kutokuishi sawa na maadili ya injili na Neno la Mungu
-          Ni muhimu kuomba kwa ajili ya wapakwa mafuta kwa sababu nao ni wanadamu

Na Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima
Rev. Innocent Kamote
Nilijifunza kutoka kwa Bishop Zachary Kakobe, Miaka zaidi ya 20 iliyopita.