Alhamisi, 6 Oktoba 2016

Uhusiano wa Kanisa na Israel


Wakristo wengi hawaelewi uhusiano ulioko kati ya Kanisa na Taifa la Israel Ni muhimu kufgahamu kuwa hatuwezi kuepuka nlabda kwa shingo ngumu kuwa kwa namna yoyote ile uhusiano ulioko kati ya kanisa yaani wakristo na wana wa Israel kuwa tuna uhusiano katika ilimwengu wa Roho ingawa tunaweza tusiwe na uhusiano wa kitaifa au kibalozi lakini katika Mungu Israel wanaungwa mojakwa moja na Kanisa Tutajifunza somo hili kwa kuzingatia vipengele  vitatu vifuatavyo;- 

  • ·         Israel imewekwa wakfu
  • ·         Kwa nini niipende Israel
  • ·         Uhusiano wa Kanisa na Isarel

Israel imewekwa wakfu.

Neno wakfu au kuwekwa wakfu maana yake ni kutenga kitu au watu au kutakasa kitu au mtu ili atumike kwa utukufu wa Mungu na si vinginevyo au kulaani kisitumike kwa namna nyingine isipokuwa Mungu tu na kwa sababu hiyoi kitu au mtu anapokuwa amewekwa wakfu anafanyika kuwa mali ya Mungu Kutoka 13;2, 29;1

     Katika maana hiyo basi ni muhimu kufahamu kuwa Israel ni Taifa au kabila na jamaa ambayo imewekwa wakfu, imeteuliwa  na kutengwa  kwa kusudi maalumu hivyo wao ni mali ya Mungu Kumbukumbu 14;2,4;20,Zaburi 135;4. Israel ni Taifa la Mungu na Yerusalem  ni mji wake mtakatifu na kamwe Mungu hawezi kuwasahahu mji hu na inchi hii na watu wake Zaburi 137;5-6, Mungu wa Israel ndiye Mungu tunayemuabudu  wokovu tulio nao umetoka kwa wayahudi, Masihi tunayemwadhimisha alikuwa myahudi na ametoka kwa wayahudi, hata mifumo ya ibada zetu tumerithi kwa wayahudi na Biblia tuliyo nayo kwa sehemu kubwa imeandikwa na wayahudi na manabii wote tunaowaamini ni wa jamii ya kiytahudi  kwa msingi huo kanisa linapaswa kuwa na uzalendo wa kisayuni kwa wana wa Israel na kuonyesha kuwapewnda na kuwajali na kuwa wanatuhusu, Leo hii vyomboi vya habari  na jamii ya watu wengine wa kisiasa na ulimwengu wa Kiislamu wamekuwa na mtazamo duni na hafifu dhidi ya Israel  na hivyo kuichukia na wakati mwingine kuilaani katika vitendo kadhaa jambo hili linapaswa kuchukuliwa kwa umakini na watu wanayoyajua maandiko Hili ni taifa masihi na ni taifa la Mungu  ardhi hii aliyopewa Ibrahimu alipewa na Mungu kwa hiyo kila mkristo anapaswa kuielewa siri hii na kuipenda Israel

Kwanini niipende Israel

1.       Kuipenda Israel ni kumpenda Mungu

Amri iliyo kuu kuliko zote ni kumpenda Bwana Mungu Kumbukumbu 6;5, kama tunampenda Mungu kwa dhati , bila hska pia tutapenda kile anachokipenda  na kuchukia anacho kichukia , Maandiko yanaonyesha kuwa Mungu anaipedna Israel na mji wake Yerusalem Zaburi 87;1-2 Labda mtu atasema sisi wenyeji wetu uko mbinguni na kama Abrahamu tunautazamia mji wenye misingi ambao mwenye kuubuni na kuujenga ni Mungu  Waebrania 11;10, Wafilipi 3;20,Wagalatia 4;26 dhana hiyo ni kweli kabisa  kila mkristo anajua kuwa kuna mji Yerusalemu ya mbinguni na Yesu alisema Yerusalemu huu wa sasa hatuwezi kukwea na kwenda kuabudu Yohana 4;21-24 Lakini Maneno ya Bwana yesu yanshitua zaidi unaposoma katika Mathayo 5;34-35 kluwa usiape kwa Yerusalem nmaana ndio mji wa mfalme mkuu (Yaani Mungu) na Yesu alisema kuwa mji huu utakanyagwa na mataifa kwa wakati tu Luka 21;24 uko wakati ambapo Heshima na utukufu wa Mungu utarudi na Mungu mwenyewe ataiatawala Dunia  nzima kuanzia hapa Israel Zekaria 14;4,9.


Pichani ni jiji la Yerusalem ambalo wayahudi wameapa hautagawanywa milele ,Upande wa kushoto ni Msikiti (The Dome of Rock) ukiwa umejengwa mahali ambapo palikuwa ni Hekalu la Wayahudi, hapo ni mahali makini wayahudi hawajapagusa bado,Waislamu huamini ndipo alipopaa Muhamad kwenda mbinguni (Uongo mtupu),na ni kibla ya kwanza kabla ya Makka.Ukouwezekano kwa wayahudi wenye msimamo mkali wa kidini kulijenga tena hekalu hilo mahali hapa 
(Picha kwa hisani ya maktaba ya Mwandishi wa somo Innocent Samuel Kamote.)

2.       Kuipenda Israel ni ufunguo wa mafanikio

Mungu amekuwa mwema kwa Israel kwa karibu miaka 1720 hivi Waisrael hawakuweko katika inchi yao mpaka mwaka wa 1948 waliporudi ambapo mji wao mkuu kwa wati huo ulikuwa ni Tel-aviv-Jafa ambao una bandari na wakati huo Yerusalemu haukuwa mikononi mwao Leo mji huu uko mikononi mwao Mungu ameanza kuirehemu Israel sawa na Zaburi ya 102;13-14 katika wakati huu ambapo Israel inazungukwa na mataifa adui wasio watakia mema hata kidogo ni muhimu kuipenda Israel na kuwaombea amani  kwani kwa kufanya hivi tunaruhusu Baraka biunafsi na za taifa letu kwa ujumla Zaburi 122;1-9

3.       Kwa sababu kanisa ni tawi na Israel ni shina yaani (asili).

Mkristo awaye tyote na mchungaji au kikundichochote cha faragha wanapaswa kutambua kuwa Israel ndio shina la wokovu wetu  au ni sawa na tawi lililopandikizwa katika shina ambalo ka asili ni Israel Warumi 11;11-21  Mungu anatuionya kanisa kuwa sisi ni tawi tu lililopandikizwa na Israel ndio shina halisi, kutokutii kwao na kumkatraa maishi kumeleta wokovu mkubwa kwa amataifa mengine kluweza kufurahia neema hii ya wokovu na baraka zitakuwa kubwa zaidi kama wakitii, kwa msingi huo kutokuipenda Israel ni kuchukia asili huku sisi tukiwa ni tawi tu lililopandikizwa Yesu alionyesha dhahiri kuwa wokovu wetu asili yake unatoka kwa wayahudi Yohana 4;22  Biblia yote kuanzia Mwanzo mpaka Malaki ambayo tunaiita Agano la kale  ni kitabu cha Mungu kwetu lakini kwa asili ni Biblia ya waebrania yaani wayahudi kwa msingi huo huwezi kamwe kumteganisha Mkristo na Myahudi adui wa wayahudi lazimam pia anakuwa ni adui wa wakristo anayetaka kuifuta Israel Bila shaka pia atataka kuufutilia mbali ukristo kwa msingi hio kila mkristo anawajibika kuikumbuka Israel

4.       Kuilaani Israel ni kujilaani na kuibariki Israel ni kujibariki

Tangu mwanzo Mungu alipomuita Ibrahimu ambaye ndiye baba wa Taifa hili alimtamkia Baraka zitakazoambatana na wale watakaombariki lakini pia Mungu aliweka laana kwa wale watakaomlaani Ibrahimu Mwanzo 12;1-3,26;1-6,28;10-15 Baraka hizio na matamko haya yanawahusu Israel hata leo kwa msingi huo kila mtu anapaswa kufahamu kuwa Mungu yuko nyuma ya maswala yote ya Israel tangu wakati wa Ibarahimu na uzao wake  wale watakaomnenea mema watabarikiwa na wale wanaomnenea vibaya watalaaniwa. Tafuta ukaone katika historia wale wote waliowahi kuitishia Israel waliishia wapi na Historia itakuambia kuilaani Israel ni kujiweka katika hatari

Uhusiano wa Kanisa na Israel.

Tumeona kwa namna Fulani uhusiano ulioko katia ya Israel na kanisa mwanzoni tulipokuwa tunazungumzia kwanini niipende Israel, Kanisa linapaswa kuelewa kuwa Mungu yuko pamoja na Israel na kuwa tunauhusiano mmoja kama tulivyoona sisi nasi tunapaswa kuhakikisha kuwa katika shughuli zetu za kimisheni pia tunawalenga wayahudi ili nao waokolewe Paulo mtume alikuwa na huruma sana dhidi ya ndugu zake hawa yaani wayahudi ambao sisi pia ni ndugu zetu  kwamba waokolewe na alikuwa akiwaombea sana Soma warumi 10;1 sisi nasi tunapaswa kuhakikisha kuwa tunawahubiria wokovu kwa kawaida kunakuwa na kitu cha ziada sana myahudi anapookoka wengi waliookolewa wametumiwa sana na Mungu aktika kuupanua Ufalme wake akiwemo Muhubiri maarufu Mourice Cerrulo na Benny Hinny Mungu na alisaidie kanisa kukumbuka kuwa na mkakati maalumu kuomba na kuhakikisha kuwa injili inawafikia wao pia aidha ni muhimu kanisa kuwaombea viongozi wetu wa kitaifa kuwa makini na kauli zao za kisiasa wanazozitamka dhidi ya Utendaji wowote wa kisiasa wa Israel, Wamarekani wengi wanaifahamu siri hiyo, kama unailaani Israel kasha unakwenda Marekani kuomba misaada ambao wao kuybarikiwa kwao kunatokana na kuwafanyia mema wayahudi je unadhani utafaidika au umasikini utaendelea kutufunika tu, wayahudi ni Ndugu zetu, Mungu wao ni Mungu wetu, manabii wao ni manbabii wetu, Mwokozi wao ni mwokozi wetu Biblia yao ni Biblia yetu, tumaini lao ni tumaini letu, mji wao ni mji wetu nukombozi wao ni ukombozi wetu tunauhusiano wa kudumu na Israel

somo limeandaliwa na 

Rev. Innocent Kamote
Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima

Maoni 2 :

MANOTI alisema ...

Mchungaji, asante kwa kazi njema inayoleta baraka. Kila kazi inayokusudiwa kuleta baraka huwa ngumu. Hata ilimgharimu Mwana wa Mungu kuutoa uhai wake ili kuleta ukombozi kwa watu. Somo la Israeli linalenga kumletea mtu baraka, kwa hiyo haiwezi kuwa kazi nyepesi, ina changamoto zake. Nimenufaika sana na somo hili.
Asante
Manoti

Unknown alisema ...

Hallelujah Hakika nimepata kitu kuhusu Israel ni mhimu sana kulifundisha kanisa kuhusu kanisa na Israel,
Barikiwa sana Mtumishi wa MUNGU
Ni Mimi Pastor Wilson Chiusa