Jumatatu, 15 Mei 2017

Je Hapana Zeri Katika Gileadi? (Zeri ya Gilead)

Mstari wa Msingi: Yeremia 8: 22 “Je Hapana Zeri katika Gilead? Huko Hakuna tabibu? Mbona basi haijarejea afya ya Binti ya watu wangu?

 Mmea aina ya zeri kama unavyoonekana katika Picha

Ni muhimu kufahamu kwamba hapa duniani hakuna jambo lolote Gumu lisilo na majibu, kila jambo na kila tatizo lina majibu yake na ufumbuzi wake, Magonjwa hali kadhalika yanaweza kutibiwa kwa tiba za aina mbali mbali, Mungu aliwapa wanadamu mimea ambayo ndani yake aliweka nguvu za uponyaji kwaajili ya matibabu ya aina mbali mbali.

Nyakati za Biblia watu walitumia pia madawa yatokanayo na mimea kutibu magonjwa na mateso ya aina mbalimbali, kulikuwa na miti mingi sana iliyotumika kama tiba, kabla ya kuanza kutumia zaidi kemikali ambazo nyingi zina uharibifu mkubwa katika mwili wa wanadamu na hivyo kuchangia udhaifu mkubwa wa aina binadamu walioko leo juu ya uso wa nchi. Moja ya miti maarufu sana iliyotumika kwa tiba katika Israel na mashariki ya kati ulikuwa ni mmea ujulikanao kama Zeri ambao ulikuwa unapatikana kanaani na katika mji wa Gilead.

Zeri ni nini hasa?

Zeri kwa kiingereza (BALM) ulikuwa ni mmea ambao ulikuwa maarufu sana nyakati za Biblia mmea huu ulipatikana katika nchi ya milimamilima iliyokuwa nga’mbo ya Jordan iliyojulikana kama milima ya Gilead, mmea huu uliuzwa kwa bei kubwa sana na wafanya biashara wa zamani waliokuwa matajiri walitajirika kwa kuuza zeri, 

Mwanzo 37:25 “Nao wakakaa kitako kula chakula; wakainua macho yao, wakaona, msafara wa Waishmaeli wanakuja wakitoka Gileadi na ngamia zao, wakichukua ubani na ZERI na manemane, wakisafiri kuvichukua mpaka Misri.” 

Unaweza kuona aidha katika nyakati za Biblia kama mtu anakupenda sana na kukuheshimu sana moja ya zawadi ya ngazi ya juu kabisa ambayo mtu anageweza kukupatia ilikuwa ni pamoja na ZERI angalia
Mwanzo 43:11 “Israeli, baba yao, akawaambia, Kama ndivyo, fanyeni hivi; twaeni tunu za nchi katika vyombo vyenu, mkamchukulie mtu huyo zawadi, ZERI kidogo, na asali kidogo, ubani, na manemane, na jozi, na lozi”.

Kwa nini Zeri ilikuwa bidhaa ya thamani na zawadi kubwa sana, Zeri ilikuwa na sifa ya kuponya majeraha yote ya mwili “recovering” na vidonda mbalimbali pia vikiwemo vidonda vya kuumwa na nyoka, aidha watu pia waliitumia zeri katika kuhifadhia mwili wa mwanadamu aliyekufa usioze, Hivyo kama dawa nyingine zote zingeshindwa kutibu jeraha la mtu ndipo sasa ili kuokoa maisha yake ilipaswa kuitafuta Zeri kwa vile hii ilijulikana kama dawa isiyoshindwa hata hivyo dawa hii ilikuwa ghali sana ingekugharimu kuuza vyote ulivyo navyo ili kutibiwa na wataalamu wa Gilead upate kupona. Dawa hii likuwa haishindwi kutibu jambo kama mtu anetibiwa na dawa zote na ikashindikana watu walimshauri aende Gilead kwa wataalamu kataumie Zer.

Yeremia 46:11Panda uende Gileadi, ukatwae zeri, Ee binti, bikira wa Misri; unatumia dawa nyingi bure tu; hupati kupona kamwe.” 

Ni wazi kuwa kama mtu angetumia dawa bila mafanikio dawa ya mwisho ingekuwa Zeri ni zeri tu ndiyo ambayo ingeweza kutibu maumivu aliyoyapata mtu".

Yeremia 51:8Babeli umeanguka na kuangamia ghafula; mpigieni yowe; twaeni zeri kwa maumivu yake; ili labda apate kuponywa

Katika namna ya kushangaza sana hata hivyo yalikuweko magonjwa ambayo yalikuwa ahayasikii dawa yaani magonjwa sugu, ilipotokea kuwa mgonjwa haonyeshi badiliko, kila mara alionekana yuko vilevile hapati kugangwa lilikuwa ni jambo la kushangaza sana kusikia Zeri imeshindwa au wataalamu wa Gilead wameshindwa, katika mstari wa Msingi Yeremia alikuwa anazungumzia tatizo la kiroho na tabia ya wana wa Israel ambao walishindwa kutubu na kubadilika kiasi cha kufikia ngazi ya kuhukumiwa na Mungu, Nabii alikuwa akiomboleza na kujiuliza kuwa dawa isiyoshindwa imekosekana? Matabibu wa Gilead hawako, Yeremia alikuwa anamaanisha kuweko kwa toba na manabii, Israel walishindwa kuwasikiliza manabii na pia walikosa moyo wa toba nJe hapana zeri katika Gilead? Na Matabibu maana naona afya ya watu wangu haijarejea?

Kimsingi zeri ya Gilead ilikuwa ghali sana na hata hivyo haikuweza kuponya majeraha mengine yaliyowasibu watu.

Marko 5:25-28Na mwanamke mmoja mwenye kutoka damu muda wa miaka kumi na miwili, na kuteswa mengi kwa mikono ya matabibu wengi, amegharimiwa vitu vyote alivyo navyo, kusimfae hata kidogo, bali hali yake ilizidi kuwa mbaya, aliposikia habari za Yesu, alipita katika mkutano kwa nyuma, akaligusa vazi lake; maana alisema, Nikiyagusa mavazi yake tu, nitapona

Zeri ulikuwa ni mti halisi lakini vilevile ulikuwa ni picha ya Yesu Kristo, katika muujiza huu alioufanya Yesu ni dhahiri biblia inatuonyesha zeri kutoka mbinguni, inatuonyesha mwanaume mwenye uwezo wa kumfanya mtu akawa recovered akapona akawa kamili, unaweza kuhangaika huko na kule kwaajili ya mahitaji yako, kwaajili ya afya yako ya kimwili na kiroho, kwaajili ya majeraha ya moyo wako, kwaajili ya majeraha ya adui zako, kwaajili ya majeraha ya ndoa na kazini na shuleni na hata kanisani, unaweza kuangaika huku na kule kwaajili ya mahitaji yako ya aina mbalimbali lakini lao ninakutangazia kuwa iko dawa isiyoshindwa Dawa hii ni Yesu Kristo peke yake yeye anaweza yote kwake hakuna linaloshindikana ni dawa ya waliokata tamaa, dawa ya waliojeruhiwa na kudharaulika, ni dawa ya maisha yetu, feature yetu haiku mikononi mwa wanadamu, iko mikononi mwa Yesu tu, huyu ndio wa kumkimbilia, huyu ndio wa kumpapatikia, huyu ndio wa kumtazama kwa kila unalokaboliana nalo katika maisha katika masomo, katika ndoa, kazini nk. Mwangalie Yesu na utafanikiwa yeye ni zaidi ya zeri ya Gilead ni Zawadi ya upendo wa hali ya juu kutoka kwa Mungu baba 

Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa mwanawe wa Pekee ili kila amwaminiye asipotee bali awe na uzima wa milele.

Na. Innocent Kamote
Mkuu wa Wajenzi Mwenye Hekima

Ijumaa, 5 Mei 2017

Kama Mlivyonena Ndivyo nitakavyowafanyia!


Katika maandiko haya,(HESABU 13:25-33; 14:1-12,26-32),

Hesabu 14:26-32 “Kisha Bwana akanena na Musa na Haruni, na kuwaambia,  Je! Nichukuane na mkutano mwovu huu uninung'unikiao hata lini? Nimesikia manung'uniko ya wana wa Israeli, waninung'unikiayo.  Waambieni, Kama niishivyo, asema Bwana, hakika yangu kama ninyi mlivyonena masikioni mwangu, ndivyo nitakavyowafanyia ninyi;”

Hesabu 13:25-33 “Wakarejea baada ya kuipeleleza nchi, mwisho wa siku arobaini. . Wakaenda wakafika kwa Musa, na kwa Haruni, na kwa mkutano wote wa wana wa Israeli, katika jangwa la Parani, huko Kadeshi; wakawaletea habari, wao na mkutano wote, wakawaonyesha matunda ya nchi.  Wakamwambia wakasema, Tulifika nchi ile uliyotutuma, na hakika yake, ni nchi yenye wingi wa maziwa na asali, na haya ndiyo matunda yake.  Lakini watu wanaokaa katika nchi ile ni hodari, na miji yao ina maboma, nayo ni makubwa sana; na pamoja na hayo tuliwaona wana wa Anaki huko.  Amaleki anakaa katika nchi ya Negebu; na Mhiti, na Myebusi, na Mwamori wanakaa katika milima, na Mkanaani anakaa karibu na bahari; na kando ya ukingo wa Yordani.  Kalebu akawatuliza watu mbele ya Musa, akasema, Na tupande mara, tukaitamalaki; maana twaweza kushinda bila shaka. Bali wale watu waliopanda pamoja naye wakasema, Hatuwezi kupanda tupigane na watu hawa; kwa maana wana nguvu kuliko sisi.    Wakawaletea wana wa Israeli habari mbaya ya ile nchi waliyoipeleleza, wakasema, Ile nchi tuliyopita kati yake ili kuipeleleza, ni nchi inayowala watu wanaoikaa; na watu wote tuliowaona ndani yake ni watu warefu mno.  Kisha, huko tuliwaona Wanefili, wana wa Anaki, waliotoka kwa hao Wanefili; tukajiona nafsi zetu kuwa kama mapanzi; nao ndivyo walivyotuona sisi.”

Hesabu 14:1-12 “1. Mkutano wote wakapaza sauti zao wakalia; watu wakatoka machozi usiku ule. Kisha wana wa Israeli wote wakamnung'unikia Musa na Haruni; mkutano wote wakawaambia, Ingekuwa heri kama tungalikufa katika nchi ya Misri, au, ingekuwa heri kama tungalikufa katika jangwa hili. Mbona Bwana anatuleta mpaka nchi hii ili tuanguke kwa upanga? Wake zetu na watoto wetu watakuwa mateka; je! Si afadhali turudi Misri? Wakaambiana, Na tumweke mtu mmoja awe akida, tukarudi Misri.Ndipo Musa na Haruni wakaanguka kifudifudi mbele ya mkutano wa kusanyiko la wana wa Israeli.  Na Yoshua mwana wa Nuni, na Kalebu mwana wa Yefune, waliokuwa miongoni mwao walioipeleleza nchi, wakararua nguo zao; wakanena na mkutano wote wa wana wa Israeli wakasema, Nchi ile tuliyopita kati yake ili kuipeleleza, ni nchi njema mno ya ajabu.  Ikiwa Bwana anatufurahia, atatuingiza katika nchi hii atupe iwe yetu, nayo ni nchi yenye wingi wa maziwa na asali. Lakini msimwasi Bwana, wala msiwaogope wale wenyeji wa nchi, maana wao ni chakula kwetu; uvuli uliokuwa juu yao umeondolewa, naye Bwana yu pamoja nasi; msiwaogope. Lakini mkutano wote wakaamuru wapigwe kwa mawe. Ndipo utukufu wa Bwana ukaonekana katika hema ya kukutania, mbele ya wana wa Israeli wote. Bwana akamwuliza Musa, Je! Watu hawa watanidharau hata lini? Wasiniamini hata lini? Nijapokuwa nimefanya ishara hizo zote kati yao.  Nitawapiga kwa tauni, na kuwaondolea urithi wao, nami nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, kisha yenye nguvu kuliko wao.  


Utangulizi:
Ni muhimu kufahamu kuwa ulimi wa Mwanadamu una nguvu ya kusababisha madhara makubwa na pia kuleta uponyaji mkubwa, kwa kuwa wanadamu wameumbwa kwa sura na mfano wa Mungu, Mungu aliuumba ulimwengu kwa Neno tu alitamka na ikawa, wakati wote utendaji wetu na matukio yetu katika maisha yanatokana nay ale tunayoyazungumza Mithali 18:20-21Tumbo la mtu litajazwa matunda ya kinywa chake; Atashiba mazao ya midomo yake. Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi; Na wao waupendao watakula matunda yake”Kama hivi ndivyo ni jambo la msingi sana kujichunga ni kitu gani tunakizungumza na kukitamka kwa vile tunaweza kuumba jambo hilo.

Kumbuka hata wokovu wetu unapatikana kwa kumuamini Yesu moyoni na kwa kumkiri kwa kinywa na ni kwa kinywa tu tunaweza kuliitia jina la Bwana na kupata msaada Warumi 10:9-13  Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka. Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu.  Kwa maana andiko lanena, Kila amwaminiye hatatahayarika.  Kwa maana hakuna tofauti ya Myahudi na Myunani; maana yeye yule ni Bwana wa wote, mwenye utajiri kwa wote wamwitao; kwa kuwa, Kila atakayeliitia Jina la Bwana ataokoka.

Kwa msingi huo kama tunataka kuwa mbali na mauti na kama tunataka kuleta uzima katika maisha yetu ni lazima tuwe na semi zilizo na manufaa katika maisha yetu na hata ya wengine

Jambo la kujifunza:
Wana wa Israeli wanatumia ulimi kuzungumza maneno kama haya "AHERI TUNGALIKUFA KATIKA JANGWA HILI" na maneno kama "HATUWEZI".Mungu akasema atawafanyia hivyo walivyosema na kweli walikufa katika jangwa hilo.

Kalebu Mwana wa Yefune na Yoshua Mwana wa Nuni walisema maneno ya ushindi kama haya "TWAWEZA KUSHINDA BILA SHAKA na BWANA YU PAMOJA NASI".

Tunajifunza juu ya makundi mawili.Kundi la kwanza ambao ndio wengi wanazungumza maneno HASI NA YA KUSHINDWA na kweli walishindwa.

Kundi la pili ambao ni wachache sana wanazungumza maneno ya CHANYA YA KUSHINDA na kweli walishinda na kuingia nchi ya ahadi.

Watu wa Mungu ikiwa Mungu anatufanyia jambo sawa na ukiri wetu, ikiwa uzima na mauti uko katika uwezo wa ulimi wetu, ikiwa kwa ulimi tunaweza kukiri na hata kupata wokovu ni muhimu kwetu ,KWA KILA JAMBO TUZUNGUMZE MANENO CHANYA  YA KUSHINDA sawasawa na Neno la Mungu,NA BWANA mwenye kutushindia atakuwa pamoja nasi kufanikisha yote kiroho na kimwili.

MANENO TUNAYOSEMA NDIYO BWANA ANAYOTUFANYIA YAWE MEMA AU MABAYA!Maana anasema CHAGUENI HIVI LEO!(YOSHUA 24:14-15;WAFILIPI 2:13;WARUMI 8:31-32,37-39;WAFILIPI 4:13).Mungu aweke mlinzi vinywani mwetu ili sikuzote tuzungumze maneno ya kuumba ushindi katika Jina la Yesu Kristo.(ZABURI 141:1-3)

Ni imani yangu kuwa Tangu sasa utatumia kinywa chako vema na kujizungumzia ushindi, acha kujizungumzia kukata tamaa, jizungumzie mambo mema wazungumzie wengine mema  Na mungu atatubariki sawasawa na ukiri wetu.

Sources. Rev.George Swenya Full Gospel Bible Fellowship Church Tanga.

Ukarabati: Rev. Innocent Kamote Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima

Ijumaa, 28 Aprili 2017

Kazi za Roho Mtakatifu katika Kanisa!


Andiko la Msingi: Matendo 1:8Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi.”


 Hii hapo juu ni picha (symbol) ya Roho Mtakatifu na sio Roho Mtakatifu

Utangulizi.

Hali ya kanisa la leo imekuwa dhaifu kuliko Nyakati za kanisa la Kwanza, Kanisa lilikusudiwa na Mungu kuwa Chombo kikuuu cha ukombozi wa wanadamu Baada ya kazi njema iliyofanywa na Yesu Msalabani, Mungu analitegemea kanisa kuwa kama Waamuzi, watetezi, wakombozi, makuhani, wafalme na askari wa mstari wa mbele katika kuwatetea wanyonge, walioonewa na waliosetwa katika vifungo vya Ibilisi, na kukemea uovu, kuikosoa serikali na kuonyesha njia kwa ulimwengu!

Luka 4: 18-19Roho wa Bwana yu juu yangu, Kwa maana amenitia mafuta kuwahubiri maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, Na vipofu kupata kuona tena, Kuwaacha huru waliosetwa, Na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa.”

Kanisa lilipaswa kufanya kazi hizo alkizozitaja Yesu na kuzitabiri Isaya hapo Juu, ikiwa Roho wa Mungu yuko juu yetu, ikiwa ametupaka Mafuta, lakini jiulize leo hii je kazi zinazofanywa na kanisa ndizo hizo hapo juu? Leo kanisa limejaa watu wengi wenye Stresses yaani migandamizo, lina watu wengi wasio waaminifu bila kujali kuwa wako ngazi gani za kiroho, yale ambayo zamani tulikuwa tunayaona na kuyashuhudia yakifanywa na watu tuliowaita Mataifa watu wasiomjua Mungu, tuliokuwa tukiwalilia waokolewe, wamjue Mungu wamgeukie Mungu sasa ndio yanafanywa na Kanisa, Je ni mara ngapi kanisa limekaa kimya watu wanapoonewa, Mauaji yanapotokea Duniani, vita vinavyoendelea, matishio ya umwagikaji wa damu na dhuluma za kila aina je leo ni nani anaifanya kazi hii? Nani anasimamia haki za binadamu zinazoendana sawa na Neno la Mungu? Kwa nini tumefikia hapa tulipofikia? Kuna na mambo mengi sana sitaki kuyazungumza hapa lakini wewe unayajua kuhusu hali ya kanisa la leo! Ni ya kushangaza, ni kweli ziko huduma za kinabii na mitume na miujiza ambayo inatendeka na najua inatendeka kwa nguvu za Roho Mtakatifu, lakini je uadilifu? Uko? Je Hakuna ulevi, uongo, picha za ngono, chuki, uadui, uchawi, ushirikina, masengenyo, uasherati na zinaa, je hatutoi muda mwingi kwa simu zetu, tablets, na laptop, zaidi kuliko kwa Mungu na familia zetu, hali ni mbaya mno sasa, Turudi kukazia kazi za Roho Mtakatifu ndani ya kanisa, tutajifunza somo hili kwa kuzingatia vipengele viwili vifuatavyo:-

1.       Roho Mtakatifu ni Nani?

2.       Kazi za Roho Mtakatifu Katika ya Kanisa

Roho Mtakatifu Ni nani?

Katika Maandiko Roho Mtakatifu anaelezewa vema kama Nafsi kamili  inayojitegemea yeye ni BWANA yaani ni Mungu 2Wakoritho 3:17-18 17. Basi 'Bwana' ndiye Roho; walakini alipo Roho wa Bwana, hapo ndipo penye uhuru. Lakini sisi sote, kwa uso usiotiwa utaji, tukiurudisha utukufu wa Bwana, kama vile katika kioo, tunabadilishwa tufanane na mfano uo huo, toka utukufu hata utukufu, Waebrania  9:14 Roho Mtakatifu ni wa Milele tunaelezwa katika maandiko “basi si zaidi damu yake Kristo, ambaye kwamba kwa Roho wa milele alijitoa nafsi yake kwa Mungu kuwa sadaka isiyo na mawaa, itawasafisha dhamiri zenu na matendo mafu, mpate kumwabudu Mungu aliye hai?” kuwepo milele ni sifa ya uungu, 1Petro 1:2, Roho Mtakatifu ni Mungu kama ilivyo kwa Baba na Mwana kwa msingi huo hatupaswi kumfikiri Roho mtakatifu kama nguvu tu au hamasa Fulani, ana sifa za nafsi anafikiri, Warumi 8:27 ana hisia Warumi 15:30 ana maamuzi 1Wakoritho 12:11 na ana uwezowa kupenda na kufurahia ushirika , alitumwa na Mungu Baba kuleta uwepo wa kiungu kwa washirika ili tufurahie ushirika wetu na Kristo Yohana 14:16-18,26, kwaajili ya hayo Kanisa linapaswa kukumbuka kuwa Roho ni Mungu na ni nafsi na nilazima tuhakikisha anaunganishwa mioyoni mwetu, na kuwa anastahili kuabudiwa kupendwa na kusikilizwa Marko 1:11

Kazi za Roho Mtakatifu katika Kanisa.

1.       Yeye ndio njia ya wokovu anayetushawishi kwa habari ya haki dhambi na hukumu Yohana 16:7-8 Sasa basi ni vigumu kwa kanisa kujisikia hukumu na kufa kwa dhamiri kama Roho Mtakatifu hapewi nafasi ya kutosha katika kuifanya kazi ya kutuhukumu kwa habari ya dhambi, kutuonyesha kuna hukumu kubwa ijayo endapo hatutatubu na kutushuhudia namna ya kutenda haki.
2.       Anafunua kweli kuhusu Kristo Yohana 14:16,26,
3.       Anatuzaa kwa upya Yohana 3:3-6
4.       Anatufanya washirika wa mwili wa Kristo 1Wakoritho 12:13
5.       Anatutakasa  Warumi 8:9, IWakoritho 6:19
6.       Anatuthibitishia kuwa sisi ni wana wa Mungu Warumi 8:16
7.       Anatusaidia katika kuabudu Matendo 8:26-27
8.       Anatufanya tumtukuze Yesu Kristo Wagalatia 5:22-23,1Petro
9.       Anazalisha neema ya Kristo inayotufanya tuwe na sifa zinazomtukuza Kristo Wagalatia 5:22-23, 1Petro 1:2
10.   Ni Mwalimu  na hutuongoza katika kweli yote  Yohana 16: 13, 14:26, 1Wakoritho 2:9-16
11.   Aanamfunua Yesu kwetu na kutuongoza katika kuwa na ushirika na Yeye Yohana 14:16-18,16:14
12.   Anapanda upendo wa Mungu siku zote ndani yetu  Warumi 5:5
13.   Anatupa Furaha faraja na msaada Yohana 14:16, 1Thesalonike 1:6
14.   Ni njia ya huduma na hututia nguvu kwaajili ya huduma, shuhuda na utangazaji wa Neno la Mungu Matendo 1:8, 4:31 na hutenda miujiza Matendo 2:43;3:2-8, 5:15, 6:8, 10:38
15.   Anatoa Karama za Roho kwa kusudi la kulijenga Kanisa 1Wakoritho 12-14
16.   Analijenga Kanisa Waefeso 2:22, anatia moyo kuabudu Wafilipi 3:3
17.   Anaongoza katika Umisheni Matendo 13:2, anateua waamini Matendo 20:28
18.   Anapaka Mafuta watumishi Matendo 2:4 1Wakoritho 2:4
 
Hitimisho!
Kama ikiwa Roho wa Mungu hufanya kazi hizo zote kanisa halipaswi kumdharau, upungufu mkubwa unaolikumba kanisa la leo unatokana na sababu tu za kumzimisha Roho Mtakatifu, Ni lazima kanisa limpe Roho Mtakatifu kipaumbele kama linataka kuwa hai nnapozungumza kanisa namaanisha kila mtu aliyeokolewa anayemwamini Yesu anapaswa kuzingatia haya ili Kazi za Mungu ziweze kufanyikakatika kiwango ambacho Mungu amekikusudia na sio chini ya kiwango.

Mkuu wa Wajenzi mwenye Hekima

Rev. Innocent Kamote. 0718990796

Jumanne, 18 Aprili 2017

Malaika wa Pasaka!



Mstari wa Msingi: Marko 16:1-8, Mathayo 28:1-10

Hata sabato ilipokwisha, ikipambazuka siku ya kwanza ya juma, Mariamu Magdalene, na Mariamu yule wa pili, walikwenda kulitazama kaburi. Na tazama, palikuwa na tetemeko kubwa la nchi; kwa sababu malaika wa Bwana alishuka kutoka mbinguni, akaja akalivingirisha lile jiwe akalikalia. Na sura yake ilikuwa kama umeme, na mavazi yake meupe kama theluji. Na kwa kumwogopa, wale walinzi wakatetemeka, wakawa kama wafu. Malaika akajibu, akawaambia wale wanawake, Msiogope ninyi; kwa maana najua ya kuwa mnamtafuta Yesu aliyesulibiwa. Hayupo hapa; kwani amefufuka kama alivyosema. Njoni, mpatazame mahali alipolazwa. Nanyi nendeni upesi, mkawaambie wanafunzi wake, Amefufuka katika wafu. Tazama, awatangulia kwenda Galilaya; ndiko mtakakomwona. Haya, nimekwisha waambia. Wakaondoka upesi kutoka kaburini, kwa hofu na furaha nyingi, wakaenda mbio kuwapasha wanafunzi wake habari.  Na tazama, Yesu akakutana nao, akisema, Salamu! Wakakaribia wakamshika miguu, wakamsujudia. Kisha Yesu akawaambia, Msiogope; enendeni, mkawaambie ndugu zangu waende Galilaya, ndiko watakakoniona.


              
Utangulizi:

Inaonekana wazi wakati wote Mungu anapokuwa na Tangazo muhimu sana kwa wanadamu, hutuma ujumbe wake kupitia Malaika, wakati mwingine Malaika wa habari muhimu alijitambulisha kwa jina na wakati mwingine Hakujitambulisha, vyovyote vile iwavyo malaika hao walileta ujumbe Muhimu kwa wanadamu mfano:- 

·         Mungu alituma Malaika kutangaza kuzaliwa kwa Samson Waamuzi 13
·         Mungu alituma Malaika kutangaza kuzaliwa kwa Yohana Mbatizaji Luka 1
·         Mungu alituma Malaika kutangaza kuzaliwa kwa Yesu Kristo Luka 2:8-11
·         Mungu alituma Malaika kushughulika na tatizo la Sodoma na Gomora Mwanzo 19
·         Mungu alimtuma Malaika wa Pasaka wakati wa Ukombozi wa wana wa Israel Misri 12:29

·     Na Mara hii Yesu anapofufuka Malaika wa Pasaka anakuja tena akiwa na ujumbe mzito ambao tutachukua Muda kuutafakari leo.

Malaika wa Pasaka anawatokea kinamama walikuja Kaburini wakiwa wamekata tamaa na wenye fadhaa kubwa sana, walitoka wakiwa hawajua hata ni nani atakayewaondolea jiwe waendelee na kazi ya kupaka mafuta mwili wa Yesu, lilikuwa ni jambo la hatari na lenye kuogopesha mno, lakini Malaika wa Pasaka alikuwa na ujumbe muhimu sana 

1.       Aliwaambia Msiogope.
Inawezekana kina mama waliokwenda Kaburini walishituka zaidi walipoona kijana huyu mwenye mavazi meupe, na waliogopa mno lakini ujumbe wa kwanza wanaoupokea kutoka kwa malaika wa pasaka ni kutokuogopa Mungu wakati wote anataka watu wake wasiogope na wawe na amani, wakati wote haijalishi tunazungukwa na mazingira ya namna gani, Malaika hakutaka kina mama na dunia nzima kwa ujumla itawaliwe na Hofu, hofu ni adui mkuu wa amani, kila mtu anayesheherekea Pasaka anapaswa kuwa Mbali na Hofu, Kama mauti ilimpata Yesu Kristo naye amefufuka hatupaswi kuogopa tena Milele Ufunuo 1:17-18, 2Timotheo 1:3, 8, Dunia ya leo imejawa na Hofu, Huko Syria hivi Karibuni Marekani imepiga Bomu kubwa sana kubwa mno, hali ya hofu inaongezeka , Hapa nchini kule Pwani Polisi kumi wameuawa ambao ni walizni wa amani nchini hii inaongeza Hofu, Kule Korea Kaskazini na Marekani wamekuwa na mikwara ya kustaajabisha wakitaka kupigana hali hizi zote zinaoneza hofu duniani na kuifanya Dunia isiwe mahali pa Amani ni lazima jitihada zifanyike katika kuhakikisha Amani inatawala Duniani na watu wanaondoka katika maisha ya hofu.

2.       Amefufuka Katika wafu.
Malaika anataka kuthibitisha kuwa Yesu alisulubiwa, na alikufa na kuwa amefufuka maana yake yu hai, Ufunuo 1:17-18 Yesu yu Hai milele na milele, kama kuna jambo ambalo shetani hapendi kulisikia ni ushahidi ulio wazi kuwa Yesu amefufuka, hii ndio tofauti yake na waanzilishi wote wa dini na falsafa mbalimbali duniani, wote waliandika historian a wakapita sivyo ilivyo kweke Yesu Kristo yeye yuko hai milele, ulikuwa ni ujumbe wa kutia moyo kwa kina mama hawa walikuwa wamenunua mafuta ya kuupaka mwili wa Yesu usizoe, aendelee kuwepokuwepo kaburini, Lakini Neno la malaika lilikuja kuondoa mashaka kwao na kuwajulisha kuwa hata mafuta yenu ya kumpaka Merehemu hayana kazi tena huyu mwanamume yu hai.Aidha malaika alikuwa amewakumbusha Maneno aliyoyasema Yesu kuwa atafufuka hii maana yake ni kuwa Yesu aliitimiza ahadi, viongozi wazuri ni wale wanaotimiza ahadi zao mara baada ya Uchaguzi kama ilivyo kwa Pombe Joseph Magufuli anatimiza ahadi nyingi sana alizowaahidi watanzania, lakini nitoe wito kwake kuendelea kudhibiti mfumo wa Bei ya chakula kwani imepanda mmno na kipato cha watanzania hakitoshelezi katika kukabiliana na kupanda kwa unga na vyakula vinginevyo.

3.       Hayuko Hapa
Malaika aliwaambia wanawake hawa wawe watalii wa kwanza wa kulitembelea Kaburi la Yesu lililotupu, aliwaambia Patazameni mahali walipomuweka, hata leo unaweza kwenda kupatazama mahali walipomuweka Hayupo tena, yuko Hai, Kaburi lake ni ushahidi wazi hata leo kuwa Yesu Kristo amefufuka na tayari yuko busy na majukumu ya kutuombea kama kuhani mkuu

4.       Nendeni Mkwawaambie wanafunzi wake na Petro
Habari njema kwa wanafunzi wote wa Yesu. Lakini pia maalumu kwa Petro, Petro na Yesu walikuwa tayari wameachana pabaya Petro alikuwa tayari amemkana Yesu Mara tatu wakati anasulubiwa Malaika ametumwa kulete ujumbe wa ufufuo kwa wanafunzi wote wa Yesu na maalumu kwa Petro pia, Mungu alitaka kuthibitisha kuwa ameshamsamehe Petro kabisa na kuwa sasa ana uhusiano naye mkubwa na wa kipekee zaidi, Habari njema za ufufuo zinawagusa hata wale ambao walikuwa wamemkana Yesu, Yesu kipakee anaonyesha kuhusika na rafiki zake wote na hata wale waliomkataa kivitendo na kwa kiapo

Malaika alikuwa na ujumbe uliobeba Kuondoa Hofu, Kuleta Matumaini, Msamaha na uthibitisho kuwa tutamuona Yesu aliyefufuka, Kila kiongozi wa kisiasa kuanzia ngazi ya kata anapaswa kuhakikisha wanainchi wanaishi mbali na Hofu, tuache kuwatisha wanainchi, Lazima kila kiongozi alete habari za matumaini na kututhibitishia hali halisi ya tumaini hilo Yesu alikuwa ni kiongozi aliyetoka tunmaini na alilithibitisha, aliposema yeye ni ufufuo na uzima alifuua wafu lakini pia alifufuka kwelikweli, aliweza kusamehe na kuwahesabu wale waliomkosea kama rafiki maalumu na sio maadui zake, viongozi wa leo hawapaswi kujenga hali ya uadui na raia wake, ahadi zake zilikuwa za kweli hakutoa matumaini hewa.

Na mkuu wa Wajenzi Mwenye Hekima
Rev. Innocent Kamote.