Jumapili, 9 Mei 2021

Wewe u mwana wa mwanamke mwingine!

Waamuzi 11:1-2 “Basi huyo Yeftha, Mgileadi, alikuwa mtu shujaa sana, naye alikuwa ni mwana wa mwanamke kahaba; Gileadi akamzaa Yeftha. Mkewe huyo Gileadi akamzalia wana; na hao wana wa mkewe hapo walipokuwa wamekua wakubwa wakamtoa Yeftha, na kumwambia, Wewe hutarithi katika nyumba ya babaetu; kwa sababu wewe u mwana wa mwanamke mwingine.”



Utangulizi:


Wewe u mwana wa mwanamke mwingine! Yalikuwa ni maneno ya kukatisha tamaa yaliyotolewa kwa kijana shujaa aliyejulikana kama Yeftha, Mwandishi wa kitabu cha Waebrania katika agano Jipya anamtaja kama mojawapo wa mashujaa wa imani ona Waebrania 11:32-34Nami niseme nini tena? Maana wakati usingenitosha kuleta habari za Gideoni na Baraka na Samsoni na Yeftha na Daudi na Samweli na za manabii; ambao kwa imani walishinda milki za wafalme, walitenda haki, walipata ahadi, walifunga vinywa vya simba,walizima nguvu za moto, waliokoka na makali ya upanga. Walitiwa nguvu baada ya kuwa dhaifu, walikuwa hodari katika vita, walikimbiza majeshi ya wageni.”

Yeftha ni moja ya waamuzi wakubwa miongoni mwa waamuzi wanaotajwa katika Biblia, waamuzi walikuwa ni viongozi wa mpito waliotumiwa na Mungu, kuwasaidia Israel walipokuwa hawana mfalme tangu kufa kwa Yoshua mpaka kupakwa mafuta kwa mfalme wa Kwanza aliyeitwa Sauli, Jina Yeftha maana yake ni ni Bwana atafanya njia, au Bwana atafungua.

Yeftha alikataliwa na ndugu zake, baada ya kifo cha baba yake kwa sababu eti alizaliwa na mwanamke Kahaba, sababu hii inawezekana kabisa ilitokana na sifa zake kuwa alikuwa mtu mwema tene mwenye ujuzi kuhusu Mungu na hodari sana, alikuwa ni shujaa, kuzaliwa kwake na mwanamke kahaba haikuwa sababu yay eye kukata tama katika maisha yake, alijiendeleza kitabia na kuwa mtoto mwema sana kuliko wenzake kwa wivu walimkataa kwa maneno mabaya ya ubaguzi kuwa yeye ni mwana wa mwanamke mwingine hii haikuwa sababu ya kumzuia Yeftha ambae aliamua kwenda kuishi katika mji mwingine ulioitwa Tobu, watu wote hohehahe walimkusanyikia na kuishi Pamoja naye,  Israel walipoonewa na wana wa Ammoni na kuteswa vibaya walimkumbuka Yeftha na wakatuma wazee kumuomba Yeftha aje kuwa shujaa wao, naye kwa neema ya Mungu akijazwa Roho Mtakatifu, na kuonyesha ujuzi wake katika Torati na historia ya wana wa Israel alikubali kuja na kuwatetea na kuwaokoa dhidi ya wana wa Amoni ona


Waamuzi 11:4-11 “Ikawa baadaye, wana wa Amoni wakapigana na Israeli. Ikatukia, hapo wana wa Amoni walipopigana na Israeli, wazee wa Gileadi wakaenda kumtwaa huyo Yeftha katika ile nchi ya Tobu; wakamwambia Yeftha, Njoo wewe uwe kichwa chetu, ili tupate kupigana na wana wa Amoni. Yeftha akawaambia wazee wa Gileadi, Je! Ninyi hamkunichukia mimi na kunifukuza nitoke katika nyumba ya baba yangu? Basi kwani kunijilia hivi sasa wakati mlio katika taabu?  Wazee wa Gileadi wakamwambia Yeftha, Kwa ajili ya hayo sasa tumegeuka kukuelekea wewe tena, ili uende pamoja nasi na kupigana na wana wa Amoni, nawe utakuwa kichwa chetu juu ya wenyeji wote wa Gileadi. Basi Yeftha akawaambia wazee wa Gileadi Kwamba mwanirejeza kwetu tena ili kupigana na wana wa Amoni, naye Bwana akiwatoa mbele yangu, je! Mimi nitakuwa kichwa chenu? Wazee wa Gileadi wakamwambia Yeftha, Yeye Bwana atakuwa shahidi kati yetu; hakika yetu tutafanya sawasawa na neno lako. Ndipo Yeftha akaenda pamoja na wazee wa Gileadi, na hao watu wakamfanya awe kichwa, tena mkuu, juu yao; naye Yeftha akanena maneno yake yote mbele ya Bwana huko Mispa.”


Licha ya kufanywa kiongozi na mwamuzi wa Israel ni wazi kuwa Yefhta aliijua sharia alitenda haki na hata vita yake na namna alivyokuwa anajenga hoja alijenga kwa haki, akiitumia torati, Yeftha hakuwa na makosa ni baba yaka ndiye aliyezaa na mwanamke kahaba, lakini kigezo hiki cha kilitumiwa na ndugu zake kumkataa na kumbagua, huenda jambo hili pia liliingiliwa na wazee kwa kuwa katika Israel maamuzi yasingelifanyika bila wazee kuingilia kati wote wakiwa wametiwa upofu na wivu tu, uwezo wa Yeftha katika kulijua neno la Mungu unaonekana wazi kwa hoja anazozijenga dhidi ya mfalme wa wana wa Amoni kabla hajampa mkon’goto ona

Waamuzi 11:11-28 “Ndipo Yeftha akaenda pamoja na wazee wa Gileadi, na hao watu wakamfanya awe kichwa, tena mkuu, juu yao; naye Yeftha akanena maneno yake yote mbele ya Bwana huko Mispa. Basi Yeftha akatuma wajumbe waende kwa mfalme wa wana wa Amoni akasema, Je! Wewe una nini nami, hata umenijilia kupigana juu ya nchi yangu? Mfalme wa wana wa Amoni akawajibu hao wajumbe wa Yeftha Kwa sababu Israeli waliitwaa nchi yangu, hapo walipokwea kutoka katika nchi ya Misri, tokea Arnoni mpaka Yaboki, na hata Yordani; basi sasa rudisha hizo nchi tena pasipo matata. Yeftha akatuma wajumbe mara ya pili waende kwa huyo mfalme wa wana wa Amoni; akamwambia, Yeftha akuambia hivi; Israeli hakuitwaa nchi ya Moabu, wala nchi ya wana wa Amoni; lakini hapo walipokwea kutoka Misri, na Israeli walienenda katika bara hata kuifikilia Bahari ya Shamu, na kufikilia Kadeshi; ndipo Israeli wakatuma wajumbe waende kwa mfalme wa Edomu, wakisema, Nakuomba sana unipe ruhusa nipite katika nchi yako; lakini mfalme wa Edomu hakusikia. Ni vivyo wakampelekea wajumbe mfalme wa Moabu; wala yeye hakukubali; basi Israeli wakakaa katika Kadeshi. Kisha akaenda nyikani na kuizunguka hiyo nchi ya Edomu, na nchi ya Moabu, nao wakapita upande wa mashariki wa nchi ya Moabu, wakapanga marago upande wa pili wa Arnoni; wala hawakuingia ndani ya mpaka wa Moabu, kwa maana Arnoni ilikuwa ni mpaka wa Moabu. Kisha Israeli wakatuma wajumbe waende kwa Sihoni mfalme wa Waamori, mfalme wa Heshboni: Israeli wakamwambia, Twakuomba utupe ruhusa tupite katika nchi yako, mpaka mahali pangu. Lakini huyo Sihoni hakuwaamini Israeli ili wapite ndani ya mpaka wake; bali Sihoni akawakutanisha watu wake wote, nao wakapanga kambi katika Yahasa, wakapigana na Israeli. Bwana, Mungu wa Israeli, akamtia Sihoni na watu wake wote mikononi mwa Israeli, nao wakawapiga; basi Israeli wakaimiliki hiyo nchi ya Waamori, wenye kukaa nchi hiyo. Nao wakaumiliki mpaka wote wa Waamori, tokea Arnoni hata Yaboki, tokea hiyo bara hata Yordani. Basi sasa yeye Bwana, Mungu wa Israeli, amewapokonya Waamori watoke mbele ya watu wake Israeli, na wewe wataka kuwatamalaki? Je! Wewe hutakitamalaki hicho ambacho huyo Kemoshi mungu wako akupa kukitamalaki? Kadhalika, awaye yote ambaye Bwana, Mungu wetu, amemfukuza atoke mbele yetu hao ndio tutakaowatamalaki. Na wewe sasa, je! U mwema kuliko Balaki mwana wa Sipori, huyo mfalme wa Moabu, kwa lo lote? Je! Yeye alishindana na Israeli, au kupigana nao? Wakati Israeli waliokuwa wakikaa Heshboni na miji yake, na katika Aroeri na miji yake, na katika miji hiyo yote iliyo huko kando ya Arnoni, muda wa miaka mia tatu; mbona ninyi hamkuipata tena katika majira hayo? Basi mimi sikukufanyia wewe dhambi, lakini wewe unanitenda uovu kwa kupigana nami; yeye Bwana, yeye Mwamuzi, na awe mwamuzi hivi leo kati ya wana wa Israeli na wana wa Amoni. Lakini mfalme wa wana wa Amoni hakuyasikiza hayo maneno ya Yeftha aliompelekea.”



inaonyesha wazi jinsi alivyokuwa mtu wa haki na mwenye ujuzi wa neno la Mungu, Mungu alimjaza kwa Roho wake na kusikiliza dua yake na maombi yake akamuwezesha kuwaokowa wana wa Israel kwa kuwapiga wana wa amoni ona 


Waamuzi 11:29-33 “Ndipo roho ya Bwana ikamjilia juu yake Yeftha, naye akapita katika Gileadi na Manase, akapita na katika Mispa ya Gileadi, na kutoka hapo Mispa ya Gileadi akapita kuwaendea wana wa Amoni. Naye Yeftha akamwekea Bwana nadhiri, akasema, Kwamba wewe utawatia wana wa Amoni mkononi mwangu kweli, ndipo itakuwa ya kwamba, kile kitakachotoka katika milango ya nyumba yangu kunilaki, hapo nitakaporudi na amani kutoka kwa hao wana wa Amoni, kitu hicho kitakuwa ni cha Bwana, nami nitakisongeza kiwe sadaka ya kuteketezwa. Basi Yeftha akavuka kuwaendea wana wa Amoni ili kupigana nao; naye Bwana akawaua mkononi mwake. Akawapiga kutoka Aroeri hata kufikilia Minithi, miji ishirini, na mpaka Abel-keramimu, akawapiga kwa machinjo makuu mno. Basi hivyo wana wa Amoni walishindwa mbele ya wana wa Israeli.”


Ni dhahiri kuwa Yeftha alikuwa amekubalika na Mungu, sio lazima wakati wote tukubalike kwa wanadamu, lakini Mungu akikukubali na kuweka mkono wake lazima mlango uliofungwa na wanadamu utafunguliwa tu , lazima bwana atafanya njia, Kujitoa kwa Yeftha kwa Mungu na uaminifu wake kwa Mungu hakujawahi kufikiwa na myahudi wala mkristo awaye yote yeye ni mtuwa pekee aliyeweka nadhiri ngumu sana na kuitimiza, japokuwa kuna mgogoro mubwa wa kimjadala kuhusu Nadhiri yake, lakini ni ukweli usiopingika kuwa mwana huyu wa kahaba, mtoto wa mwanamke mwingine alikuwa vizuri kwa Mungu wake kuliko wana wengine, Ni kitu gani tunaweza kujifunza kutoka kwake ni kuwa hatupaswi kukata tama katika maisha,  kila kikwazo katika maisha yetu tunaweza kukitumia kuwa nafasi ya kipekee kutupeleka katika hatua nyingine:- Hatupaswi kukatishwa tamaa na jambo lolote!


Mwanzilishi wa Kampuni ya kutengeneza injini za aina mbalimbali ikiwemo magari, pikipiki, jenereta na mashine za pump za kumwagilia na kuoshea magari Chini Japan aliyejulikana kama SOICHIRO HONDA alizaliwa mwaka 17 November 1906  na alifariki mwaka 5 August 1991 akiwa na miaka 84 Kampuni yake iliitwa Honda Motor Company ltd. Aliondoka nyumbani akiwa na miaka 15 tu na akaanza kuwa fundi wa kutengeneza magari na kuuza vifaa nya magari vilivyotumika, alikuwa nimmtu mchapakazi sana na alipenda sana magari, na kutamani kuwa fundi wa kuyatengeneza, lakini hata hivyo alikataliwa kwa sababu na mambo yalikuwa magumu kwa sababu hakuwa na Elimu yeyote, wenzake walimpa kazi ya kuwapikia chakula na kusafisha duka la spea za magari. Aliamua kujiendeleza mwenyewe ili kuendeleza kipawa chake alijiunga na timu ya mbio za magari, lakini wakati Fulani alianguka na kupata ajali ambayo ilimjeruhi mwili wake na hakuweza kuendelea tena,  na akaachana na swala la mbio za magari, Baada ya kupona Soichiro alianza kutengeneza Piston rings kwa uwezo wake, alizipeleka kwa kampuni ya TOYOTA ili awauzie, lakini walimfukuzilia mbali kwa aibu, walikataa kabia uvumbuzi wake wakisema ni wa hali ya chini, kukataliwa kwake hakukumfanya ake chini aliendelea kukazana na kuamua kuanzisha kiwanda chake hatimaye aliweza, leo hii ndio mtu mwenye pikipiki imara sana kuliko aina nyingine ya pikipiki duniani.

Mungu hamtupi mja wake, Hijalishi umetiokea katika ukoo gani, au jamii gani au una historia mbaya kiasi gani, wala haijalishi watu wanasema nini juu yako, jambo kubwa la kuuliangalia ni Mungu anasema nini juu yako, tunaweza kupitia katika hali ya kukataliwa, Lakini hilo lisitutishe tumpe Mungu nafasi ya kutuonyesha nini kiko mbele yetu, Na kwa neema na uweza wa Roho Mtakatifu Bwana atakufanya uwe kimbilio la Ndugu zako na jamaa zako wote walipokupuuzia  na kukudharau watakuja wakuinamie kumbuka jiwe walilolikataa waashi hilo limekuwa jiwe kuu la msingi Yeftha aliambiwa wewe u mwana wa mwanmke mwingine, ni kama wanamwambia wewe sio ndugu yetu halisi, lakini baadaye walikwenda kumuhitaji na kuhitaji msaada wake!


Na Rev. Innocent Samuel Kamote.

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima.



Jumatatu, 3 Mei 2021

Unapokutana na Mitihani!


Kumbukumbu La Torati 8:15-16 “aliyekuongoza katika jangwa lile kubwa lenye kitisho, lenye nyoka za moto na nge, nchi ya kiu isiyokuwa na maji; aliyekutolea maji katika mwamba mgumu, aliyekulisha jangwani kwa mana, wasiyoijua baba zako; apate kukutweza, apate kukujaribu, ili kukutendea mema mwisho wako.”



Utangulizi:

Wakati mwingine ili Mungu aweze kutuimarisha na kutukomaza ili kutupeleka katika kusudi lake alilolikusidia basi hutupitisha katika majaribu ya aina mbalimbali kwaajili ya kutufundisha hali kama hii hututokea katika siku za maisha yetu tuwapo duniani na zaidi sana katika maisha ya shuleni, maisha ya uanafunzi huwa yanahitimishwa kwa mitihani, huwezi kumtenganisha mwanafunzi na mitihani hata kidogo, mtihani ndio unaoamua hatima ya mwanafunzi na kumpeleka katika kiwango kingine cha kusudi la utumishi wake duniani.

Ni msimu mwingine tena wa mitihani, kwa majuma kadhaa sasa wanafunzi wetu watakuwa wanakaa kwaajili ya mitihani yao, ambayo kimsingi vilevile itaamua hatima ya maisha yao ya baadaye, kwa hivyo wote tunakubaliana kuwa ni wakati muhimu sana, Mitihani ni sehemu ya kipimo cha yale tuliyojifunza na uwezo wetu wa kuelewa lakini sio hivyo tu ndiyo inayotupeleka juu kuelekea hatua nyingine ya kielimu katika maisha, kwa msingi huo kama wanafunzi tutakuwa tumewahi kukutana na mitihani ya aina mbalimbali kama hii tunayokutana nayo sasa, Pamoja na uzuri na umuhimu wa mitihani wakati wa mitihani ndio wakati ambao wanafunzi wengi hujikuta katika msongo mkubwa wa mawazo na kufikiri itakuwaje, Je tunawezaje kuikabili mitihani, Neno la Mungu linatupa kanuni za kutusaidia namna na jijnsi ya kushinda wakati wa mitihani Roho wa Mungu aliniambia nisema haya kwa wanafunzi wanofanya mitihani wakati huu.

1.       Hesabia kuwa ni wakati wa furaha  #

 

Yakobo 1:2 “Ndugu zangu, hesabuni ya kuwa ni furaha tupu, mkiangukia katika majaribu mbalimbali;” Hapo Biblia inazungumzia kufurahi wakati tunapopitia katika majaribu ya aina mbalimbali, Biblia inazungumzia kihalisia habari ya changamoto kadhaa katika maisha ya ukristo na maisha ya duniani kwa ujumla, lakini kwa vile imesema majaribu mbalimbali mimi nataka kuweka majaribu kama mtihani, nataka kuitumia kanuni ileile ya jambo lile-lile ambalo huwa ni jaribu katika maisha huwa ni changamoto huwa linatuhuzunisha na kutuondolea furaha kuwataka wanafunzi wafahamu kuwa wakati wa mitihani japo wanatumia sana akili, na wanapaswa kuongeza umakini mkubwa, wanakesha bongo zinachoka lakini wafahamu vilevile kuwa sio wakati wa kuhuzuinika ni wakati wa kufurahi, ni wakati wa kujiachia katika neema ya Mungu na kuondoa hofu kabisa kila mmoja akijua kuwa mtihani una faida kubwa na kuwa utampeleka katika ngazi ya juu zaidi hivyo wakati kama huo sio wa kulia na kuumia bali ni wakati wa furaha relax.

 

2.       Fanya kwa utukufu wa Mungu.

 

Maandiko yanatufundisha kuwa lolote tulifanyalo kwa neno au kwa tendo, tulifanye kwa utukufu wa Mungu

1Wakoritho 10:31 “Basi, mlapo, au mnywapo, au mtendapo neno lo lote, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu.”

Hatufanyi mtihani kwaajili ya mashindano, hatushindani na mtu, tunafanya lolote tulifanyalo kwaajili ya kumpa Mungu utukufu, kwa msingi huo hakikisha kuwa Mungu anakwenda kutukuzwa kwa kile unachokwenda kukifanya, acha mashindano, usishindane na mtu, wala shule yako isifanye mashindano na shule nyingine,usiogope pia unapoona mwenzako ameandika sana na kujaza kurasa haimaanishi kuwa ndio amejaza point, usiogope, mwenzako anapoongeza booklet ya kujibia usipasuke moyo na kudhani kuwa labda mambo ni mazuri kwake wala na wewe usiige kwa sababu balada ya kwenda kwenye point unaweza kujikuta unajaza blaablaa kwa sababu ya kutaka kuwa kama Fulani kumbuka kuwa unafanya mtihani kwa kusudi la kumpendeza Mungu, hivyo usijilinganishe na mwingine endapo wasimamizi wa mtihani wanaruhusu mtu kutoka haraka wewe usitoke kwa haraka unapoona kuna mtu kamaliza wewe fuata muda uliopangwa katika ratiba na mtihani wako ukikumbuka kuwa wewe uko pale kwa kusudi la kumpendeza Mungu na sio wanadamu

2Wakoritho2:9 “Kwa hiyo, tena, ikiwa tupo hapa, au ikiwa hatupo hapa, twajitahidi kumpendeza yeye.”

Vyovyote vile jitahidi kuufanya mtihani wako kwa kusudi la kumpendeza Mungu, Mungu anakuona, anajua hitaji lako, anajua wazazi wako wamewekeza kiasi gani anajua walimu wako wamejitahidi kiasi gani sasa wakati wa mtihani hakikisha kuwa unafanya mtihani kwa kusudi la kumpendeza yeye, na kusudi lako kubwa liwe kwamba Mungu atukuzwe kwa matokeo mema ya mtihani wako!

 

3.       Mwamini Mungu!

 

Sisi hatuingii katika chumba cha mtihani kama wapagani,au kama watu wasio na imani au matumaini tunaingia tukiwa na Mungu aliye hai, ni lazima tumtangulize Mungu mbele na ili tumpendeze yeye lazima tuwe na imani naye Maandiko yanasema pasipo imani haiwezekani kumpendeza,  kwa hiyo ingia katika chumba chako cha mtihani ukiamini na kujua wazi kuwa yuko Mungu na kuwa hatakuacha

Waebrania 11:6 “Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao.”

Mafanikio yetu na kuthibitika kwetu kutakuja tu endapo tutamuamini Mungu, na kwa kuwa sisi tunamtumaini yeye ni dhahiri kuwa tutafanikiwa

2Nyakati 20:20 “Wakaamka asubuhi na mapema, wakaenda nje katika jangwa la Tekoa; nao walipokuwa wakitoka, Yehoshafati akasimama, akasema, Nisikieni, enyi Yuda nanyi wenyeji wa Yerusalemu; mwaminini Bwana, Mungu wenu, ndivyo mtakavyothibitika; waaminini manabii wake, ndivyo mtakavyofanikiwa.”
Hakuna mtu amemuamini Mungu kisha Mungu akamuacha hivihivi tu!

 

4.       Fanya mtihani kwa jina la Yesu

Mtu anaweza kujiuliza Je naweza kutumia jina la Yesu kufanya mtihani ndio Jina la Bwana ni ngome imara mwenye haki huikimbilia akawa salama ona

Mithali 18:10 “Jina la Bwana ni ngome imara; Mwenye haki huikimbilia, akawa salama.”
Yesu mwenyewe alisisitiza kuwa tukiomba lolote kwa jina lake baba wa Mbinguni atalitenda ona

Yohana 14:13-14 “Nanyi mkiomba lo lote kwa jina langu, hilo nitalifanya, ili Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Mkiniomba neno lo lote kwa jina langu, nitalifanya.”
Tunaweza kulitumia Jina la Yesu kila wakati katika taabu yoyote naye atatusaidia, hili ndio jila lenye kuleta msaada ndio jina linaloweza kutuokoa bila kujali historia zetu au wapi tumetokea Biblia inasema kila, nakazia tena KILA, yaani bila kujali wewe ni nani, ni wa kabila gani, ni wa ukoo gani, ni wa taifa gani, ni wa dini gani bila kujali haki yako unapoliitia jina hili litaleta wokovu ulio sawa na mahitaji yako ona

Matendo 2:21 “Na itakuwa kila atakayeliitia jina la Bwana ataokolewa.”
Wengine wanaweza wasikubaliane nami kwamba tunaweza kulitumia jina la Yesu katika mambo mazito sio kulichezea katika mitihani, nisikilize mitihani ndio inayoamua hatima ya maisha yetu, hivyo wakati wa mitihani sio wakati wa mchezo, tunamuhitaji Mungu na tunamuhitaji Bwana Yesu wakati wa mitihani yetu kwa msingi huo ni muhimu kwetu tukafanya mtihani huo kwa jina la Yesu, Biblia imesema lolote tufanyalo nakazia tena LOLOTE tufanyalo ukiwemo mtihani tulifanye kwa jina la Yesu ona

Wakolosai 3:17 “Na kila mfanyalo, kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Mungu Baba kwa yeye.”
Unaona kumbe maandiko yanatutia Moyo kuwa tunaweza kufanya kila tunachokifanya kwa jina la Yesu, iwe kwa neno au kwa tendo, ikiwa watakatifu waliotutangulia katika agano la kale walifanya vita kwa jina la Bwana je kuna dhambi gani kufanya mtihani kwa jina la Bwana wa majeshi?

5.       Usiibe/. Wala usifanye udanganyifu!.

 

Kutoka 20:15-16 “Usiibe, Usimshuhudie jirani yako uongo.” Ni amri mbili ambazo zinafuatana katika maandiko, na katika amri Kumi, wote tunajua madhara ya udanganyifu, tunafahamu namna dunia ilivyoingia katika huzuni kubwa sana kwa sababu ya udanganyifu, shetani alipofanikiwa kumdanganya hawa alisababisha uharibifu mkubwa, wakati wa mitihani shetani hatakosa kuwajaribu watu walio dhaifu, usikubali kujaribiwa, usikubali kumpa shetani nafasi, Biblia inasema wala msimpe ibilisi nafasi, nafasi moja tu inaweza kusambaratisha na kuharibu maisha yako, hairuhusiwi kufanya udanganyifu wa aina yeyote wakati wa mtihani, Mungu anataka tuwe waaminifu tu, hivyo basi jitahidi kutumia akili zako na kumtegemea Mungu, hakuna msaada unaoweza kupewa na walimu wako wala mtu yeyote wala mzazi wako zaidi ya msaada ule waliokusaidia kukulipia ada na kukufundisha, hivyo uwe na bidii, ukaufanye mtihani ule kwa akili zako mwenyewe na kwa msaada wa Mungu aliye hai, wala usiibe wala usifanye udanganyifu ambao unaweza kuwa na madhara makubwa kwako, lakini vilevile kwa shule yako na kwa wenzako, na pia kusababisha hasara kwa taifa na kuitia dosari wilaya yako mkoa wako na kadhalika, hivyo tusijaribu kwa namna yoyote ile kufanya udanganyifu kwaajili ya utukufu wa Mungu!, Mungu atatukuzwa vipi kama tumeibia, Mungu atatukuzwa tu kama tulisoma kwa bidii, tukamuomba , tukamtegemea na kumuamini naye akatusaidia basi.

 

6.       Muombe Mungu!

 

Wako watu ambao wanadharau maombi, wanadhani kuwa hayana msaada wowote wala kitu chochote cha ziada hususani linapokuja swala la Mtihani, dhana hii ni ya kijinga, Hatupaswi kuzitumainia akili zetu wenyewe japokuwa kutumia akili sio dhambi, akili ni karama ya kwanza ambayo mwanadamu amepewa na Mungu, tuna haki ya kuitumia, lakini ni kosa kubwa sana kukataa masaada wa Mungu wakati wa jaribio lililoko mbele yetu, Neno la Mungu linasema tusijisumbue katika jambo lolote bali kwa kuomba ona

Wafilipi 4:6-7 “Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu. Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu.”  

Maombi ni silaha ya kipekee ambayo tunaweza kuitumia katika nyakati zote na kwa jambo lolote, hatuna budi kuliamini neno la Mungu na kuomba, Yesu mwenyewe alipokuwa anakabiliwa na Mtihani wa kufa msalabani aliomba na malaika wa Bwana wakaja kumtia nguvu, inawezekana mtihani wenyewe ukawa sio tatizo lakini hofu yetu, kukosa kwetu amani, kuogopa kukawa ndio tatizo kwa hiyo ni muhimu kuomba ili tuhifadhiwe mioyo yetu na nia yetu na amani ya Mungu ipitayo akili zote itatuhifadhi.

 

7.       Usiogope

 

Hofu ya mitihani ni moja ya maumivu na homa kubwa sana ya wanafunzi wakati wa mtihani, wakati wa mtihani watu wengi hujiuliza itakuwaje, mioyo inawadunda watu wanaogopa, namimi pia nimefanya mitihani katiika viwango mbalimbali vya msingi, sekondari, vyuoni na katika kozi nyinginezo, nimejiona na nimeona pia watu wengi wakiogopa mitihani, Hata wachungaji katika vyuo vya Biblia huogopa mitihani, woga sio mzuri, woga unaweza kuchelewesha kufikia kusudi la Mungu ndani yako, katika Kiwango “level” ya chuo nilipokuwa na chukua digrii ya ualimu, ilikuwa ni ruhusa kutokufanya mtihani kama unaona hauko tayari na maandalizi yako sio mazuri, lakini pia ilikuwa ruhusa kurudia mtihani ukifeli, sikupenda kurudia mtihani nilitamani kufaulu mara moja nitakapoufanya mtihani wangu, lakini mara kadhaa niliahirisha kufanya mtihani kwa kutokujiamini kuwa laba maandalizi yangu hayatoshi hivyo nilihairisha mara kwa mara,lakini mwisho nikaona mbona ninapoteza Muda, mbona ninajichelewesha kufikia kusudi la Mungu analotaka kunitumia kwalo? Nikamuamini Mungu nikaomba, Mungu aliponitia nguvu kufanya nilikasirika na kuamua kuifanya yote bila kujali nilifanikiwa kuimaliza kwa wepesi sana, hata hivyo nilikuja najishangaa kwa nini niliogopa sasa, niliogopa nini kumbe mbiona inawezekana, ni kwa sababu waliita chuo kikuu kwa hiyo nilidhani sio mahali pa mchezo na kuwa kila kitu ni kigumu kumbe inawezekana kama wengine walivyoweza. Kuogopa kunaweza kuchelewesha lile ambalo Mungu alikuwa amelikusudia kwetu, Hofu ni mbaya, wana wa Israel walipoogopa walishindwa kuirithi nchi ya kanaani kwa wakati iliokusudiwa na hivyo ikawagharimu miaka mingi,

Hesabu 14:1-9 “Mkutano wote wakapaza sauti zao wakalia; watu wakatoka machozi usiku ule. Kisha wana wa Israeli wote wakamnung'unikia Musa na Haruni; mkutano wote wakawaambia, Ingekuwa heri kama tungalikufa katika nchi ya Misri, au, ingekuwa heri kama tungalikufa katika jangwa hili. Mbona Bwana anatuleta mpaka nchi hii ili tuanguke kwa upanga? Wake zetu na watoto wetu watakuwa mateka; je! Si afadhali turudi Misri? Wakaambiana, Na tumweke mtu mmoja awe akida, tukarudi Misri. Ndipo Musa na Haruni wakaanguka kifudifudi mbele ya mkutano wa kusanyiko la wana wa Israeli. Na Yoshua mwana wa Nuni, na Kalebu mwana wa Yefune, waliokuwa miongoni mwao walioipeleleza nchi, wakararua nguo zao; wakanena na mkutano wote wa wana wa Israeli wakasema, Nchi ile tuliyopita kati yake ili kuipeleleza, ni nchi njema mno ya ajabu. Ikiwa Bwana anatufurahia, atatuingiza katika nchi hii atupe iwe yetu, nayo ni nchi yenye wingi wa maziwa na asali. Lakini msimwasi Bwana, wala msiwaogope wale wenyeji wa nchi, maana wao ni chakula kwetu; uvuli uliokuwa juu yao umeondolewa, naye Bwana yu pamoja nasi; msiwaogope.”

Wakati wote linapokuja swala lolote linalotupa changamoto Fulani hatupaswi kuogopa, tunapaswa kuona kama Kalebu na Yoshua kuwa kama Bwana yuko pamoja nasi hakuna linaloweza kusimama kinyume nasi, tunaliitia jina la Bwana katika shida zetu na tunaingia katika chumba cha mtihani tukiwa na imani kuwa yuko pamoja nasi

Zaburi 118:5-9 “Katika shida yangu nalimwita Bwana; Bwana akanijibu akaniweka panapo nafasi. Bwana yuko upande wangu, sitaogopa; Mwanadamu atanitenda nini? Bwana yuko upande wangu, msaidizi wangu, Kwa hiyo nitawaona wanaonichukia wameshindwa. Ni heri kumkimbilia Bwana Kuliko kuwatumainia wanadamu. Ni heri kumkimbilia Bwana. Kuliko kuwatumainia wakuu.”

Unaona mwandishi wa zaburi ana ushujaa mwingi sana kwa sababu ana uhakika kuwa Bwana yuko upande wake sisi nasi Mungu yuko pamoja nasi kwa hiyo hatupaswi kuogopa na ushindi ni dhahiri kuwa utakuwa upande wetu ona

Warumi 8:31 “Basi, tuseme nini juu ya hayo? Mungu akiwapo upande wetu, ni nani aliye juu yetu?”

 

8.       Fanya kwa bidii.

 

Kama jinsi ambavyo tumeiona kuwa mtihani ni nafasi, ni nafasi kwa sababu ndio unaoamua hatima ya maisha yetu, na kutupeleka kule kwenye utume ambao Mungu ametuitia kuufanya duniani kwa hiyo “it is an opportunity” ni fursa kwa msingi huo hatuna budi kuhakikisha kuwa tunaufanya vizuri sana

Muhibiri 9:10 “Lo lote mkono wako utakalolipata kulifanya, ulifanye kwa nguvu zako; kwa kuwa hakuna kazi, wala shauri, wala maarifa, wala hekima, huko kuzimu uendako wewe.”

Unaona maandiko yanatutia moyo kufanya kila kitu kwa ufasaha, hakikisha unaandika vizuri, unapangilia vizuri, unaonyesha machakato wa namna na jinsi ulivyopata majibu, nenda kwenye pointi kama hakuna cha kuelezea usipige blaablaa nyingi, kumbuka huufanyi mtihani kwaajili ya kuwapendeza wanadamu bali kwaajili ya utukufu wa Mungu, hivyo mambo ya Mungu hayapaswi kufanywa kwa upuuzi, hivyo fanya kazi yako vema.

 

9.        Jipumzishe! (Relax)

 

Mwanzo 2:1-3 “Basi mbingu na nchi zikamalizika, na jeshi lake lote. Na siku ya saba Mungu alimaliza kazi yake yote aliyoifanya; akastarehe siku ya saba, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoifanya. Mungu akaibarikia siku ya saba, akaitakasa kwa sababu katika siku hiyo Mungu alistarehe, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoiumba na kuifanya.”

Kama tumemuomba Mungu na kuzingatia yote yale ambayo Mungu ametupa kuyafanya yaani tumejisomea sana, tulikesha sana, tulifunga na kuomba, tunamuamini Mungu hatuogopi tuna uhakika kuwa Mungu yuko upande wetu basi “Relax” usijisumbue pumzisha akili zako acha kuwa na msongo wa mawazo, uwe na utulivu, wala hata usijadili kitu na mtu utakapotoka nje hasa kwa mtihani ambao umekwisha kuumaliza, tafakari na utulie na upumzike hii nayo ni kanuni ya kiungu unapomaliza kufanya assignment ambayo Mungu amekupa unahitaji kupumzika “Relax”

Yona 4: 5-6 “Ndipo Yona akatoka mjini, akaketi upande wa mashariki wa mji, akajifanyia kibanda huko, akakaa chini yake uvulini, hata aone mji ule utakuwaje. Na Bwana Mungu aliweka tayari mtango, akaufanya ukue juu ya Yona, ili uwe kivuli juu ya kichwa chake, na kumponya katika hali yake mbaya. Basi Yona akafurahi sana kwa sababu ya ule mtango.”

 

10.   Chochea karama iliyoko ndani yako kwa kuwekewa Mikono

 

Nilitaka kumalizia mahubiri yangu na poit namba 9 tu lakini Roho wa Mungu akanitaka niweke hii ya kuwekewa Mikono, unapofika wakati wa Mtihani kama hivi ni muhimu kufahamu kuwa kila mtu, kila kijana kila mtoto, Mungu ameweka kitu ndani yake, lakini wakati mwingine hakiwezi kujitokeza bila kuwekewa Mikono, hii ni sihara ya maombezi yenye kuleta neema kubwa sana japo sio lazima, lakini ni kanuni bora ya kimaandiko, kama sio tatizo mchungaji na aweke mikono juu ya wale wanaokwenda kufanya mitihani yao, inahitajika neema, kuwekea mikono mtu hufanya hekima na maarifa ya kiungu yawe juu yake ona

Kumbukumbu la Torati 34:9 “Na Yoshua, mwana wa Nuni, alikuwa amejaa roho ya hekima; maana Musa alikuwa amemwekea mikono yake juu yake; wana wa Israeli wakamsikiliza, wakafanya kama Bwana alivyomwamuru Musa.”


Mmmh kumbe basi mtu anapowekewa Mikono karama zilizojificha ndani yake huibuka na kumpa neema ya kuwa na hekima na maarifa kama ilivyokuwa kwa Musa alimuwekea mikono Yoshua na Paulo mtume alimuwekea mikono Timotheo, mtu anapowekewa mikono aidha roho ya woga huondoka na amani ya Mungu humkalia hivyo uko umuhimu wa kuwawekea mikono watahiniwa endapo mazingira na muda unaruhusu kufanya hivyo kwa watumishi husika Kama Paulo alivyofanya kwa Timotheo. ona

2Timotheo 1:6-7 “Kwa sababu hiyo nakukumbusha, uichochee karama ya Mungu, iliyo ndani yako kwa kuwekewa mikono yangu. Maana Mungu hakutupa roho ya woga, bali ya nguvu na ya upendo na ya moyo wa kiasi.”

 

Uongezewe neema!

 

Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima!

Alhamisi, 29 Aprili 2021

Atakaye kupenda Maisha

1Petro 3:10-12Kwa maana, Atakaye kupenda maisha, Na kuona siku njema, Auzuie ulimi wake usinene mabaya, Na midomo yake isiseme hila. Na aache mabaya, atende mema; Atafute amani, aifuate sana. Kwa kuwa macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, Na masikio yake husikiliza maombi yao; Bali uso wa Bwana ni juu ya watenda mabaya.”



Utangulizi:

Ni muhimu kufahamu; kwamba ni vigumu sana kuyapenda maisha hususani nyakati ambazo tunapitia maswala magumu, watu wengi wanapopitia nyakati ngumu sana katika maisha yao huwa wanatamani kufa na au wanakata tamaa kabisa hata kufikia hatua ya kufikiri kuwa Mungu hawajali na kujishughulisha tena na maisha yao, Je umewahi kupitia maswala magumu sana katika maisha hata kufikia ngazi ya kukata tamaa na kutamani kufa  au kufikiria kuwa Mungu hakujali? watu wengi wamewahi kufikiri hivyo, hata mimi pia katiika vipindi Fulani mbalimbali,  maisha sio kitu rahisi lakini maisha ni ya muhimu sana, maisha yana changamoto nyingi sana lakini bado maisha yanabaki kuwa ni ya muhimu mno!.  Mtume Petro anawaandikia Wakrito ambao walikuwa wanapitia nyakati za Mateso na nyakati ngumu sana na anatoa ushauri unaokwenda sambamba na Zaburi  iliyoandikwa na Mfalme Daudi kuhusu Maisha:-


Zaburi 34:12-16 “Ni nani mtu yule apendezwaye na uzima, Apendaye siku nyingi apate kuona mema? Uuzuie ulimi wako na mabaya, Na midomo yako na kusema hila. Uache mabaya ukatende mema, Utafute amani ukaifuatie. Macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, Na masikio yake hukielekea kilio chao. Uso wa Bwana ni juu ya watenda mabaya, Aliondoe kumbukumbu lao duniani.”


Petro anaunga mkono kile kilichosemwa na Daudi au anahubiri kitabu cha zaburi ya 34:12-16 akionyesha ni namna gani watu wa Mungu wanapopita katika magumu wanapaswa kuyatazama maisha, Petro pamoja na Daud mwandishi wa Zaburi wanatutia moyo kuwa na imani kwa ahadi za Mungu wakati wote hata wakati tunapopitia changamoto za aina mbalimbali katika maisha  na kuendelea kuyapenda maisha ili Mungu atukuzwe wakati wa Magumu yetu, tunaonyesha ukomavu na imani badala ya kuchukizwa nayo kama ilivyokuwa kwa Suleimani mwandishi wa kitabu cha Muhubiri ambaye aliyaiona maisha kuwa jambo lisilo na maana na hasa maisha ya mtu wa kawaida asiye na imani huyaona maisha kama kujilisha upepo, Maisha yana maana kubwa sana hata pamoja na magumu unayoyapitia! Hivyo hatuna budi kuyapenda:-


Petro anaona kuwa ziko kanuni ambazo angaweza kutushauri wote tunaoishi bila kujali kuwa tunaishi katika mazingira mazuri au mabaya kiasi gani lakini Maisha ni zawadi ni neema ambayo Mungu ametupa hivyo wakati wote tuwapo duniani, tunapaswa kumshukuru Mungu kwa imani sasa katika kanuni hizo Petro anatuasa kwanza


1.       Kuuzuia ulimi usinene mabaya !

 

Ni muhimu kufahamu kuwa ulimi ndio kiungo chepesi zaidi kutumika katika maisha ya mwanadamu,  mtu mwenye ukomavu na busara au mtu mkamilifu ni yule mwenye uwezo wa kujua namna na jinsi ya kuutunza Ulimi, na kuutumia Biblia inaonyesha ya kuwa kiungo hiki kinabeba mamlaka kubwa sana katika maisha yetu ikiwa ni pamoja na uzima na mauti ona Mithali 18:20-21 “Tumbo la mtu litajazwa matunda ya kinywa chake; Atashiba mazao ya midomo yake. Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi; Na wao waupendao watakula matunda yake.” Kwa haraka sana ni ulimi ndio unaoweza kutubadilishia hali ya ulimwengu wetu kuwa wa furaha au wa amani, kuyatawala mazingira ama kutawaliwa kutengeneza hali ya hewa au kuiharibu, kunung’unika au kushangilia mwenendo wetu mbele za Mungu na wanadamu unaweza kuathiriwa au kuwekwa sawa kwa ulimi! Maneno ni silaha yenye nguvu sana inayoweza kuinua watu au kuwaharibu watu! Patro ananyesha wazi kuwa tunaweza sana kujizuia maisha yetu na dhuruba za ulimwengu kama endapo tu tutaweza kuzuia ndimi zetu ona Mithali 21:23 “Mtu azuiaye kinywa chake na ulimi wake, Atajilinda nafsi yake na taabu.” Uwezo wa kuchagua nini cha kuzungumza na nini cha kutokuzungumza uko katika uchaguzi wetu, lakini wakati wote ni muhimu sana kukumbuka namna na jinsi tunavyoutumia ulimi, Ni vigumu sana kumsoma na kumjua kwa undani mtu asiyezungumza, mara tu unapozungumza ndipo watu wanapoweza kukujua wewe ni nani nani mtu wa namna gani, Maneno yetu yanafichua kile kilichoko ndani yetu  Moja ya hukumu watakayohukumiwa wanadamu mbele za Mungu ni pamoja na kile wanachokizungumza Mathayo 12:33-37 “Ufanyeni mti kuwa mzuri na matunda yake kuwa mazuri; au ufanyeni mti kuwa mbaya na matunda yake mabaya, kwa maana kwa matunda yake mti hutambulikana. Enyi wazao wa nyoka, mwawezaje kunena mema, mkiwa wabaya? Maana, kinywa cha mtu huyanena yaujazayo moyo wake. Mtu mwema katika akiba njema hutoa mema; na mtu mbaya katika akiba mbaya hutoa mabaya. Basi, nawaambia, Kila neno lisilo maana, watakalolinena wanadamu, watatoa hesabu ya neno hilo siku ya hukumu. Kwa kuwa kwa maneno yako utahesabiwa haki, na kwa maneno yako utahukumiwa.” Ni kutokana na hekina na ujuzi wake Petro kuhusu Maisha yeye anaona ni vema kutuasa kutikunena na hasa kunena mabaya, kila mtu mwenye hekima anapaswa kujua yampasayo kunena na ikiwezekana azungumze maneno ya kujenga sio mabaya au yenye hila ndani yake, Dhambi nyingi tunazozifanya na namna tunavyowazunguzia watu kwa wema au kwa ubaya kwa kujenga au kwa kuibomoa tunatumia ulimi, karibu kila iana ya dhambi ni lazima itauhusisha ulimi, kwa msingi huo Daudi na Patro wanatutaka sisi kuutumia ulimi kuleta uponyaji duniani na sio kuharibu Mithali 12:17-19 “ Atamkaye maneno ya kweli hufunua haki; Bali shahidi wa uongo hutamka hila. Kuna anenaye bila kufikiri, kama kuchoma kwa upanga; Bali ulimi wa mwenye haki ni afya. Mdomo wa kweli utathibitishwa milele; Bali ulimi wa uongo ni wa kitambo tu.” Kama hakuna sababu ya kuzungumza ni vema kutokuzungumza kuliko kuzungumza maneno ya kubomoa, kuna thawabu kubwa sana Mbinguni kwa watu wa Mungu ambao watakuwa na ujuzi wa namna na jinsi ya kuutumia ulimi, na ni vema vile vile kwa pamoja tukiwa tunatafakari na kujadili mambo yaliyo mazuri, yaliyo ya staha, yenye kujenga , yenye wema, yenye kupendeza, yenye sifa nzuri hayo ndio maswala ya kuyajadili na ndivyo neno la Mungu linavyotutaka Wafilipi 4:8 “Hatimaye, ndugu zangu, mambo yo yote yaliyo ya kweli, yo yote yaliyo ya staha, yo yote yaliyo ya haki, yo yote yaliyo safi, yo yote yenye kupendeza, yo yote yenye sifa njema; ukiwapo wema wo wote, ikiwapo sifa nzuri yo yote, yatafakarini hayo.”        Tukitafakari mambo mema tutazungumza mambo mema na tutaufanya ulimwengu uwe mahali pema pa kuishi na vilevile katika maisha yajayo baada ya kufa tutakuwa na wakati mwema na Mungu, kwa msingi huo basi kanuni ya kwanza ya kutufanya tuishi maisha mazuri  na kuufurahia uumbaji wa Mungu na kuona siku njema ni kuzungumza mambo mazuri yaliyo mema kwa msingi huo basin i vema mno tukaangalia kile Daudi alikisema na kile ambacho Petro alikihubiri kwamba kama tunapenda maisha na kutaka kuwa na siku njema katika kipindi hiki kifupi sana ambacho Mungu ametupa kuwepo duniani basi ni vema tunayapokea maisha kwa shukurani, kwa tabia njema tukiwa tumejaa neema na kuhakikisha kuwa tunawajenga wengine kwa utukufu wa Mungu baba! Matumizi ya ulimi yanatujengea kanuni kubwa na njema na nzuri ya kuyafurahia maisha kwa hiyo kuna umuhimu wa kujilinda na kujihami tusinene mabaya, tusihukumu kwa haraka na kuhakikisha kuwa tunatenda mema, Neno la Mungu linatutaka kwamba hata kama tunaishi katika nyakati ambazo kila mtu anazungumza mabaya ni wakristo pekee na watu weme na wenye hekima wanaoweza kuufanya ulimwengu kuwa mahali pema kwa kuzungumza maneno mema na mazuri ya neema na tukatae kabisa kutumika kama chombo cha shetani kwa kuuujaza ulimwengu maneno mabaya hata kama tunapitia mambo magumu Wakolosai 4:5-6 “Enendeni kwa hekima mbele yao walio nje, mkiukomboa wakati. Maneno yenu yawe na neema siku zote, yakikolea munyu, mpate kujua jinsi iwapasavyo kumjibu kila mtu.” Tunapozungumza haya unaweza kujiuliza kwamba sasa nitafanyaje maana huenda mimi niko miongoni mwa watu wenye midomo michafu sana yaani katika watu ambao wana majibu mabaya mimi nimo, katika watu ambao wanajua kunya kwa mdomo, wanajua kutema vyondo na mimi nimo na sasa nimeyaharibu maisha yangu kwa kuzungumza yasiyopaswa nawezaje kuwa mwema tena? Usiogope kama uliutumia ulimi wako vibaya kabla hatujafika katika hatua nyingine yako mambo muhuimu ya kufanya :-

 

a.       Muombe Mungu akutakase Moyo wako, akili zako na maneno yako:

 

Ni vigumu kuishi maisha matakatifu na kumpendeza Mungu kama maneno yetu ni mabaya meneno yetu ni kipimo ya kile kilichoko moyoni mwetu, akilini kwetu na ndio huwa kinadhihirishwa kwa kusema kwetu ona Luka 6:45 “Mtu mwema katika hazina njema ya moyo wake hutoa yaliyo mema, na mtu mwovu katika hazina mbovu ya moyo wake hutoa yaliyo maovu; kwa kuwa mtu, kinywa chake hunena yale yaujazayo moyo wake.”  Yesu anaonyesha wazi kuwa kile tunachokinena ni matokeo ya kile kilichoko moyoni, Kwa msingi huo basi hatuna budi kumuomba Mungu atusafishe na kututakasa, mioyo yetu, akili zetu na maneno yetu, Mungu akitusamehe na kutusafisha maneno yetu yatakuwa na nguvu ya kuumba mambo mema kwaajili ya Mungu Ona Isaya 6:1-7 “Katika mwaka ule aliokufa mfalme Uzia nalimwona Bwana ameketi katika kiti cha enzi, kilicho juu sana na kuinuliwa sana, na pindo za vazi lake zikalijaza hekalu. Juu yake walisimama maserafi; kila mmoja alikuwa na mabawa sita; kwa mawili alifunika uso wake, na kwa mawili alifunika miguu yake, na kwa mawili aliruka. Wakaitana, kila mmoja na mwenzake, wakisema, Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu, ni Bwana wa majeshi; dunia yote imejaa utukufu wake. Na misingi ya vizingiti ikatikisika kwa sababu ya sauti yake aliyelia, nayo nyumba ikajaa moshi. Ndipo niliposema, Ole wangu! Kwa maana nimepotea; kwa sababu mimi ni mtu mwenye midomo michafu, nami ninakaa kati ya watu wenye midomo michafu; na macho yangu yamemwona Mfalme, Bwana wa majeshi. Kisha mmoja wa maserafi wale akaruka akanikaribia; naye alikuwa na kaa la moto mkononi mwake, ambalo alikuwa amelitwaa kwa makoleo toka juu ya madhabahu; akanigusa kinywa changu kwa kaa hilo, akaniambia, Tazama, hili limekugusa midomo yako, na uovu wako umeondolewa, na dhambi yako imefunikwa.” Isaya ni nabii aliyetumiwa sana na Mungu, Lakini kabla ya kutumwa alijitakasa alitubia uovu wake na Mungu akamtakasa kinywa chake na ndipo akamtumia, hatuna budi kuhakikisha kuwa tunaomba na kujitakasa ili kwamba Mungu aweze kuyalinda mawazo yetu na kutulinda na uharibifu. Kumbuka kwamba tumeumbwa kwa sura na mfano wa Mungu, Mungu aliuumba ulimwengu huu kwa neno tu na mara kadhaaa laifanya miujiza kwa kutamkqa neno ona Mwanzo 18:10-14 “Akamwambia, Hakika nitakurudia wakati huu huu mwakani, na tazama, Sara mkeo atapata mwana wa kiume. Sara akasikia mlangoni pa hema iliyokuwapo nyuma yake. Basi Ibrahimu na Sara walikuwa wazee, na umri wao mkubwa, na Sara alikuwa amekoma katika desturi ya wanawake. Kwa hiyo Sara akacheka moyoni mwake, akisema, Niwapo mkongwe, nitapata furaha, na bwana wangu mzee? BWANA akamwambia Ibrahimu, Mbona Sara amecheka akisema, Mimi kweli nitazaa mwana, nami ni mzee? Kuna neno gani lililo gumu la kumshinda BWANA? Kwa muhula wake nitakurudia, wakati huu huu mwakani, na Sara atapata mwana wa kiume.” Unaweza kuona Mungu hapa anatamka neno na lile neno linakuwa kama vile alivyotamka, sisi nasi tumeumbwa kwa mfano wake Mungu akikitakasa kinywa chetu na kujifunza nidhamu ya kutunza kinywa tutakuwa na mamlaka katika matamshi yetu nan a kusababisha uumbaji, mimi ni Mwalimu pia wa chuo cha Biblia chuo cha Biblia kibiblia huitwa chuo cha manabii, hivyo nafundisha manabii pia ni Mwalimu wa manabii ili nabii aweze kuwa na mamlaka anapaswa kuwa na kinywa safi ili kinywqa cheke kiwe na mamlaka na ndio maana kabala Mungu hajamtumia nabii isaya alimtakasa kinywa cheke kisha akaweka neno lake hivyo isaya akatabiri mambo mengi kuhusu masihi na yakatimia, Manabii wengi walikuwa wakijitunza vinywa vyao na hivyo vinywa vyao vikawa na mamlaka kubwa sana ona, Nabii Elisha alitamka tu kama Mungu alivyomtamkia Sara na kile alichokinena kikatimia  2Wafalme 4:16-17 “Akasema, Panapo wakati huu mwakani, utamkumbatia mwana. Akasema, La! Bwana wangu, wewe mtu wa Mungu, usiniambie mimi mjakazi wako uongo. Yule mwanamke akachukua mimba, akazaa mtoto mume wakati uo huo mwakani, kama Elisha alivyomwambia.”Elisha anatufundisha kuwa tunaweza kutamka kitu kama Mungu nqa kikawa vilevile kwaajili ya hayo tujnaina kuwa kuna umuhimu mkubwa sana wa kuomba kutakaswa ili kwamba vivywa vyetu viweze kuwa na mamlaka ona 1Wafalme 17:1 “Basi Eliya Mtishbi, wa wageni wa Gileadi, akamwambia Ahabu, Kama Bwana, Mungu wa Israeli, aishivyo, ambaye ninasimama mbele zake, hakutakuwa na umande wala mvua miaka hii, ila kwa neno langu.” “2 Wafalme 6:24-30 “Ikawa baada ya hayo, Ben-hadadi mfalme wa Shamu akakusanya majeshi yake yote, akakwea akauhusuru Samaria. Njaa ikawa kuu huko Samaria; na tazama, wakauhusuru, hata kichwa cha punda kikapata kuuzwa kwa vipande themanini vya fedha, na kibaba cha mavi ya njiwa kwa vipande vitano vya fedha. Ikawa mfalme wa Israeli alipokuwa akipita ukutani, mwanamke mmoja akamwita akisema, Unisaidie, bwana wangu, mfalme. Akasema, Bwana asipokusaidia, nikusaidieje mimi? Ya sakafuni, au ya shinikizoni? Mfalme akamwambia, Una nini? Akajibu, Mwanamke huyu aliniambia, Mtoe mtoto wako, tumle leo, na mtoto wangu tutamla kesho. Basi, tukamtokosa mtoto wangu, tukamla; nikamwambia siku ya pili, Mtoe mtoto wako, tumle; naye amemficha mtoto wake.  Ikawa, mfalme alipoyasikia maneno ya huyo mwanamke, aliyararua mavazi yake; (naye alikuwa akipita juu ya ukuta;) na watu wakaona, na tazama, alikuwa amevaa magunia ndani mwilini mwake.Tatizo la Njaa hapa lilikuwa kubwa sana mpaka yakatokea hayo yaliyotokea lakini Elisha alitamka neno la matumaini ambalo ni vigumu kuamini kuwa linaweza kutokea katika mazingira kama yale lakini kwakuwa kinywa chake kilikuwa na mamlaka Mungu aliweza kutekeleza kile alichokisema ona 2 Wafalme 7:1-2 “Elisha akasema, Lisikieni neno la Bwana; Bwana asema hivi, Kesho panapo saa hii, kipimo cha unga mzuri kitauzwa kwa shekeli, na vipimo viwili vya shayiri kwa shekeli, langoni pa Samaria. Basi yule akida, ambaye mfalme alikuwa akitegemea mkono wake, akamjibu yule mtu wa Mungu, akasema, Tazama, kama Bwana angefanya madirisha mbinguni, je! Jambo hili lingewezekana? Akamwambia, Angalia, wewe utaliona kwa macho yako, lakini hutakula.”  Hali kama hii hata sisi tunaoishi zamani za siku hizi zama za agano jipya tunaweza kabisa kutumia ndimi zetu kwa mamlaka makubwa endapo tutakubali Mungu atutakase ndimi zetu na kututuimia Matendo 3:6 “Lakini Petro akasema, Mimi sina fedha, wala dhahabu, lakini nilicho nacho ndicho nikupacho. Kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, simama uende.” Kwa msingi huo tunaona kuwa kuna faida kubwa sana kuwa na nidhamu kwa kutunza ndimi zetu na kutakaswa kwa ndimi zetu ili kwamba vinywa vyetu viweze kutumiwa na Mungu kwa mamlaka iliyokubwa zaidi, hata Pepo huwa wanatii watu wanaojua kutumia vinywa vyao vyema .

 

 

b.      Omba kwamba Mungu ailinde dhamiri yako:

 

Ni muhimu kuyapima maneno yetu kabla ya kuyazungumza, Ni muhimu kwetu kumuomba Mungu azilinde dhamiri zetu ili kwamba wakati wote tukusudie kuzungumza mambo mazuri wakati wote tunapokusudia kuzungumza na kama ni mazingira ambayo hatupaswi kusema lolote itakuwa vema basi tukanyamaza au kumuomba Mungu atulinde vinywa vyetu ona Zaburi 19:14 “Maneno ya kinywa changu, Na mawazo ya moyo wangu, Yapate kibali mbele zako, Ee Bwana, Mwamba wangu, na mwokozi wangu.” Mara kwa mara wanadamu tunapenda, na kulalamika hususani mbele ya rafiki zetu, wanfanyakazi, wanafunzi, wageni na kaedhalika kwa kawaida hakuna mwanadamu anayefurahia kimsingi kusikia malalamiko yetu, malalamiko huinajisi mioyo, kwa msingi huo ni vema sana tukazuia vinywa vyetu lakini kwa kuwa hatuwezi basin a tumuombe Mungu kama mwandishi wa zaburi ili kwamba Mungu atusaidie kila tunalolizungumza lipate kibali mbele za Mungu!, Watu wengi sana wanafikiri kuwa Musa hakwenda kanaani kwa sababu aliupiga mwamba hapana Musa alizunguimza yasiyofaa Zaburi 106:32-33 “Wakamghadhibisha penye maji ya Meriba, Hasara ikampata Musa kwa ajili yao, Kwa sababu waliiasi roho yake, Akasema yasiyofaa kwa midomo yake.” Wana wa Israel kwa sababu ya kunungunika kwao mara kwa mara walimkosesha Musa na kumfanya Musa kutamka mambo yasiyofaa na kwa sababu hiyo, hakuruhusiwa kuingia Kanaani.


Ni muhimu kukumbuka kuwa maandiko yanatuambia katika wingi wa maneno hapakosi kuwa na maovu kwa msingi huo ni muhimu kumuomba Mungu atupe akili ya kijizuia Mithali 10:19 “Katika wingi wa maneno hapakosi kuwa na maovu; Bali yeye azuiaye midomo yake hufanya akili.” Kama wewe ni mropokaji sana katika maneno ni muhimu sana kumuomba Mungu akuwekee walinzi katika kinywa chako maneno yasikuchomoke tu kama risasi katika bunduki iliyokwisha kutenguliwa kitufe Zaburi 141:1-3 “Ee Bwana, nimekuita, unijie hima, Uisikie sauti yangu nikuitapo.  Sala yangu ipae mbele zako kama uvumba, Kuinuliwa mikono yangu kama dhabihu ya jioni.  Ee Bwana, uweke mlinzi kinywani pangu, Mngojezi mlangoni pa midomo yangu.” Unaweza kuona mfano kwa watakatifu waliotutangulia walijua hatari ya kuropoka walitaka Mungu aweke mngojezi katika vinywa vyao, sisi nasi hatuna budi kumuomba Mungu aweke walinzi kwenye vinywa vyetu

 

c.       Tujifunze kuzungumza maneno ya kujenga:

 

Neno la Mungu linatufundisha ya kuwa tunaweza kutumia vinywa vyetu kujenga, na hilo ndilo kusudi kubwa la Mungu kutuweka Duniani, Biblia inaonya kuwa haifai kuzungumza maneno ya kubomoa, ulimi unafananishwa na chemichemi, hakuna chemichemi moja inayoweza kutoa aina mbili za maji yaani kama ni maji ya chumvi itakuwa ya chumvi na kama ni maji matamu itakuwa maji matamu ona Yakobo 3:10-11 “Katika kinywa kile kile hutoka baraka na laana. Ndugu zangu, haifai mambo hayo kuwa hivyo. Je! Chemchemi katika jicho moja hutoa maji matamu na maji machungu?”  Yakobo anataka kama tunazungumza jambo basi tuzungumze kwa kusudi la kujenga, kwa msingi huo uko umuhimu wa kumuomba Mungu atuongoze na kutusaidia ili tuzungumze maneno ambayo yatamjengea heshima yeye  Waefeso 4:29 “ Neno lo lote lililo ovu lisitoke vinywani mwenu, bali lililo jema la kumfaa mwenye kuhitaji, ili liwape neema wanaosikia.”  Kumbe tunapaswa kuzungumza maneno mema yanayomfaa mwenye uhitaji kufaa mana yeke kujenga kutia ujasiri, kutia moyo, kuleta tumaini, kuwatoa watu kwenye maumivu, kuwaendeleza kuwahuisha na kuwainua,wakati wote tujihadhari na mambo ushirika au maneno yatakayoharibu 1Wakoritho 15:33 “Msidanganyike; Mazungumzo mabaya huharibu tabia njema.” Aidha biblia inatutaka tusiwe watu wa mizaha kupitiliza Mithali inaonya kuwa kuna hukumu ambazozimewekwa tayari kwa wenye mizaha Mithali 19:28-29 “Shahidi asiyefaa kitu hudhihaki hukumu, Na vinywa vya wasio haki humeza uovu. Hukumu zimewekwa tayari kwa wenye mzaha; Na mapigo kwa mgongo wa wapumbavu.”    Biblia inatufundisha kuwa wako vijana 42 ambao walipomuona nabii Elisha ambaye alikuwa na upaa walimchokoza kwa kumtania  na akachukizwa na jambo hilo kiasi ambacho nabii aliweza kuamuru Dubu ambaye aliwararua vijana wale ona 1Wafalme 2:23-24 “Akakwea kutoka huko mpaka Betheli; naye alipokuwa akienda njiani, wakatoka vijana katika mji, wakamfanyizia mzaha, wakamwambia, Paa wewe mwenye upaa! Paa wewe mwenye upaa! Akatazama nyuma akawaona, akawalaani kwa jina la Bwana. Wakatoka dubu wawili wa kike mwituni, wakawararua vijana arobaini na wawili miongoni mwao.Kwa msingi huo tumeona kwa mujibu wa Petro kuwa ili mtu aweze kufurahia maisha na kuona siku njema anapaswa auzuie ulimi wake usinene mabaya au midomo yake isiseme hila na kwamba ni vema kutumia ulimi kwa kuijenga jamii hapo tutayafurahia maisha.

 

2.       Na midomo yake isiseme hila!

 

Mojawapo ya tabia ambazo zimeumiza watu wengi sana duniani ni pamoja na hila au kutenda hila au kusema hila Biblia ya kiingereza imetumia neno GUILE kuzungumzia hila ambalo tafasiri zake ni pamoja na Deceit, au cunning ambalo maana yake ni mbinu za kudanganya, au kwa lugha nyingine ni kufanyiwa utapeli, udanganyifu, ujanja wenye nia ya kudanganya Biblia ya Kiswahili inatumia neno hilo HILA, Mungu anapendezwa sana na mtu ambaye hana hila ona Zaburi 32:1-2 “Heri aliyesamehewa dhambi, Na kusitiriwa makosa yake. Heri Bwana asiyemhesabia upotovu, Ambaye rohoni mwake hamna hila.” Kristo Yesu alipokuwa akiwachagua wanafunzi wake alimuona mmoja wa wanafunzi wake akija na alimsifia kuwa ni Myahudi kwelikweli ambaye hakuna hila ndani yake ona Yohana 1:47-48 “Basi Yesu akamwona Nathanaeli anakuja kwake, akanena habari zake, Tazama, Mwisraeli kweli kweli, hamna hila ndani yake. Nathanaeli akamwambia, Umepataje kunitambua? Yesu akajibu, akamwambia, Kabla Filipo hajakuita, ulipokuwapo chini ya mtini nilikuona.” 


Sasa basi ili tuweze kuyafurahia maisha neno la Mungu linatuonya kuwa tujihadhari na hila katika maisha yetu, tuhakikishe kuwa rohoni mwetu hakuna hila ili tuweze kumpendeza Bwana, Yakobo ni mfano wa mtu aliyekuwa na hila, jina lake pia maana yake ni mwenye hila alitumia hila kumlaghai kaka yake Esau ili kupata haki ya uzaliwa wa kwanza ona Mwanzo 25:29-34 “Yakobo akapika chakula cha dengu. Esau akaja kutoka nyikani, naye alikuwa amechoka sana. Esau akamwambia Yakobo, Tafadhali, unipe hicho chakula chekundu nile, kwa kuwa ninazimia mimi. Kwa hiyo walimwita jina lake Edomu. Yakobo akamwambia, Kwanza niuzie leo haki yako ya mzaliwa wa kwanza. Esau akasema, Tazama, mimi ni karibu kufa, itanifaa nini haki hii ya uzazi? Yakobo akamwambia, Uniapie kwanza. Naye akamwapia, akamwuzia Yakobo haki yake ya mzaliwa wa kwanza. Yakobo akampa Esau mkate na chakula cha dengu, naye akala, akanywa, kisha akaondoka, akaenda zake. Hivyo Esau akaidharau haki yake ya mzaliwa wa kwanza.” Licha Yakobo kufanya hila kuupata haki ya mzaliwa wa kwanza pia alitumia hila kupata Baraka kutoka kwa baba yake, Mwanzo 27:19-20 “Yakobo akamwambia babaye, Mimi ni Esau, mzaliwa wako wa kwanza, nimefanya kama ulivyoniambia. Ondoka, tafadhali, ukae kitako, ule mawindo yangu, ili roho yako inibariki. Isaka akamwuliza mwanawe, Imekuwaje umepata upesi namna hii, mwanangu? Akasema, Kwa sababu BWANA, Mungu wako, amenifanikisha.”  Hata hivyo Hila alizokuwa nazo zilimtokea puani katia maisha yake, aliishi maisha ya kudanganywa nay eye kwa miaika Mingi sana kazi kubwa ilifanyika ya kumbadilisha kutoka kuacha hila na kuwa Israel, ni kweli hila zinaweza kukufanikisha kwa kitambo na kutupa kile tunachofikiri itatupa Lakini Mungu kwa namna yoyote ile hawezi kukubali kuibariki hila na mwisho wa siku lazima tuvuine kile tulichokipanda Mwanzo 29:16-26 “Labani alikuwa na binti wawili, jina la mkubwa ni Lea, na jina la mdogo ni Raheli. Naye Lea macho yake yalikuwa dhaifu, lakini Raheli alikuwa mzuri wa umbo, na mzuri uso. Yakobo akampenda Raheli akasema, Nitakutumikia miaka saba kwa kumpata Raheli, binti yako mdogo. Labani akasema, Afadhali nikupe wewe kuliko mtu mwingine; kaa kwangu. Yakobo akatumika miaka saba kwa kumpata Raheli. Ikawa machoni pake kama siku chache tu kwa vile alivyompenda. Yakobo akamwambia Labani, Nipe mke wangu, maana siku zangu zimetimia; niingie kwake. Labani akakusanya watu wote wa mahali pale, akafanya karamu. Ikawa wakati wa jioni akamtwaa Lea, binti yake, akamletea Yakobo, naye akaingia kwake. Labani akampa Lea mjakazi wake Zilpa, awe mjakazi wake. Ikawa, kulipokuwa asubuhi, kumbe! Ni Lea. Akamwambia Labani, Nini hii uliyonitenda? Sikukutumikia kwa Raheli? Mbona umenidanganya? Labani akasema, Havitendeki hivi kwetu, kumtoa mdogo kabla ya mkubwa;” Hila sio njema na wakati wote inapotajwa katika Biblia haielezwi kama kitu kizuri hakuna uzuri wowote katika hila , Hila siku zote inahusishwa na kazi za ibilisi ona 2wakoritho 11:3 “Lakini nachelea; kama yule nyoka alivyomdanganya Hawa kwa hila yake, asije akawaharibu fikira zenu, mkauacha unyofu na usafi kwa Kristo.Mungu ni mwaminifu naye anapendezwa nasi tukiwa na tabia inayofanana na yeye hivyo anatoa wito kwetu kuwa watu wasio na hila, Yesu Kristo mwenyewe hakuwa na hila ona 1Petro 2:21-22 “Kwa sababu ndio mlioitiwa; maana Kristo naye aliteswa kwa ajili yenu, akawaachia kielelezo, mfuate nyayo zake. Yeye hakutenda dhambi, wala hila haikuonekana kinywani mwake”. Hila ndio moja ya dhambo mbaya ya kuepukwa Pale Yesu alipomwambia Nathaniel kuwa hakuna hila ndani yake alikuwa amemaanisha kuwa ni mtu mwenye kiwango cha juu sana cha uadilifu, Bwana ampe neema kila mmoja wetu kuwa mbali na hila katika jina la Yesu amen

 

3.       Na aache mabaya:

 

Wito wa Mungu wakati wote kwa watu wake ni kuacha mabaya, ili mtu aweze kuwa na siku njema aweze kuufurahia uumbaji na utendaji wa Mungu ni lazima aacha mabaya, Neno kuacha mabaya katika lugha nyingine linatumika neno “Let him eschew evil” Lugha hii ina maana ya kujiepusha na maovu mfano imetumika pia katiika Ayubu 1:1 “Palikuwa na mtu katika nchi ya Usi, jina lake alikuwa akiitwa Ayubu; mtu huyo alikuwa mkamilifu na mwelekevu, ni mmoja aliyemcha Mungu, na kuepukana na uovu.”  Ingawa hatuwezi wakati wote kuepuka kukutana na changamoto mbalimbali lakini hatuna budi kuhakikisha kuwa wakati wote tunaendelea kuwa na huruma na upendo kwa jamii, na hakuna matu anayeweza kuishi maisha ya raha moja kwa moja tuwapo duniani lakini ili tuweze kuyafurahia maisha maisha ya uzima wa milele mbinguni basin i lazima tujiepushe au kuacha mabaya hii ndio njia itakayotupatia maisha mema, Kumbuka Petro alikuwa anawaandikia wakristo waliokuwa wanapoitia katika mateso, kwa hivyo kwao hazikuwa siku njema lakini alikuwa akizungumza kuwa uvumilivu wao utawaleta hatimaye katika kufurahia siku njema kwa hivyo aliwaasa wasiache njia “ekklineo” – wasiende nje ya njia njema, Zaburi 1:1-6 “Heri mtu yule asiyekwenda Katika shauri la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wakosaji; Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha. Bali sheria ya Bwana ndiyo impendezayo, Na sheria yake huitafakari mchana na usiku. Naye atakuwa kama mti uliopandwa Kandokando ya vijito vya maji, Uzaao matunda yake kwa majira yake, Wala jani lake halinyauki; Na kila alitendalo litafanikiwa. Sivyo walivyo wasio haki; Hao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo. Kwa hiyo wasio haki hawatasimama hukumuni, Wala wakosaji katika kusanyiko la wenye haki. Kwa kuwa Bwana anaijua njia ya wenye haki, Bali njia ya wasio haki itapotea.Ni wito wa kiungu wakati wote kuwaita watu wageuke na kuacha njia zao mbaya ili aweze kuwaponya na kuwabariki Ezekiel 33:11 “Waambie, Kama mimi niishivyo, asema Bwana MUNGU, SIKUFURAHII kufa kwake mtu mwovu; bali aghairi mtu mwovu, na kuiacha njia, yake mbaya, akaishi. Ghairini, ghairini, mkaache njia zenu mbaya; mbona mnataka kufa, Enyi nyumba ya Israeli? ” ni ahadi ya Mungu kila wakati kuwabariki watu na kuwatendea mema iwapo wataacha njia mabaya 2Nyakati 7:14 “ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha, na kuomba, na kunitafuta uso, na kuziacha njia zao mbaya; basi, nitasikia toka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao, na kuiponya nchi yao.” Biblia inatutia moyo kuwa rehema za Mungu ziko haijalishi kwamba umewahi kuwa muovu kwa kiwango gani lakini ukibadilisha njia yako leo Mungu yuko tayari kuyabariki maisha yako na kuanza nawe ukurasa mbaya maandiko yamesisitiza wakati wote kuacha njia mbaya, kuishi maisha ya toba kila wakati na kuendelea kumpendeza yeye Isaya 55:6-8 “Mtafuteni Bwana, maadamu anapatikana, Mwiteni, maadamu yu karibu; Mtu mbaya na aache njia yake, Na mtu asiye haki aache mawazo yake; Na amrudie Bwana, Naye atamrehemu; Na arejee kwa Mungu wetu, Naye atamsamehe kabisa. Maana mawazo yangu si mawazo yenu, wala njia zenu si njia zangu; asema Bwana.

 

4.       Atende mema!.

 

Petro anaonekana kuathiriwa sana na usomaji wa zaburi, kwani anarejea tena katika kile ambacho alinukuu kutoka katika Zaburi ya Daudi ambayo mara kadhaa imesisitiza kuwa sasa kwa kuwa tumeacha mabaya na tutende mema ona Zaburi 37:1-4 “Usikasirike kwa sababu ya watenda mabaya, Usiwahusudu wafanyao ubatili. Maana kama majani watakatika mara, Kama miche mibichi watanyauka. Umtumaini Bwana ukatende mema, Ukae katika nchi, upendezwe na uaminifu. Nawe utajifurahisha kwa Bwana, Naye atakupa haja za moyo wako.” Ona pia Zaburi 37: 27-28 “Jiepue na uovu, utende mema, Na kukaa hata milele.     Kwa kuwa Bwana hupenda haki, Wala hawaachi watauwa wake. Wao hulindwa milele, Bali mzao wa wasio haki ataharibiwa.” Mara kadhaa maandiko yameonyesha kile ambacho Mungu anakitaka kwetu na ambacho ni kutenda mema Mika 6:8 “Ee mwanadamu, yeye amekuonyesha yaliyo mema; na Bwana anataka nini kwako, ila kutenda haki, na kupenda rehema, na kwenda kwa unyenyekevu na Mungu wako!

 

5.       Atafute amani.

 

Mwisho Petro anataka tuitafute amani, kwa kweli neno la Mungu Biblia kwa mukhtasari ni kitabu cha amani, ili mtu awe kamili anapaswa kuwa na amani na Mungu na amani na wanadamu, hili ndio agizo la kibiblia, Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao;Amani ina faida kubwa sana kwetu tunapotaka kustawisha uhusiano wetu kwa Mungu na wanadamu, hatuwezi kuwa sawa na Mungu kama hatuna amani na mtu fulani 1Yohana 4:20-21 “Mtu akisema, Nampenda Mungu, naye anamchukia ndugu yake, ni mwongo; kwa maana asiyempenda ndugu yake ambaye amemwona, hawezi kumpenda Mungu ambaye hakumwona. Na amri hii tumepewa na yeye, ya kwamba yeye ampendaye Mungu, ampende na ndugu yake.” Mke na Mume wasipokaa kwa akili na kuhakikisha kuwa wana amani maombi yao yanaweza kuzuiwa 1Petro 3:7 “Kadhalika ninyi waume, kaeni na wake zenu kwa akili; na kumpa mke heshima, kama chombo kisicho na nguvu; na kama warithi pamoja wa neema ya uzima, kusudi kuomba kwenu kusizuiliwe.Watu wanapokosa amani kati yao na akama hawajatengeneza au kupatana jambo hilo husima a kama ukuta katika ain azote za ibada ikiwepo sadaka Mathayo 5:23-24 “Basi ukileta sadaka yako madhabahuni, na huku ukikumbuka ya kuwa ndugu yako ana neno juu yako, iache sadaka yako mbele ya madhabahu, uende zako, upatane kwanza na ndugu yako, kisha urudi uitoe sadaka yako.” Yesu alimaanisha wazi kuwa hatuwezi kupokea Baraka zozote zile kama tumevuruga amani, hivyo ni muhimu kupatana na mashitaki wako upesi ili asizuie Baraka zako katika ulimwengu wa Roho, Maagizo ya kibiblia yanatutaka tuitafute sana amani kwa sababu kuna gharama kubwa sana kuipata, amani inapaswa kutafutwa kwa bidii, Yakobo alikuwa amemuuzi kaka yake Esau kiasi ambacho Esau aliapa kuwa atamuua, jambo hili lilisabababisha akimbie mbali ujombani, lakini huko nako hakuwa na amani maisha yake yalikuwa taabuni kwa sababu Esaua angemuua na Esau aliposikia kuwa Yakobo anakuja alikuja na kikosi cha askari mia nne huu ulikuwa wakati mbaya sana katika maisha ya Yakobo na hapa ndipo alipoutafuta uso wa Mungu na vilevile alitafuta msamaha wa kweli kutoka kwa Esau ona Mwanzo 32: 1-8 “Yakobo akashika njia yake na malaika wa Mungu wakakutana naye. Naye Yakobo alipowaona, alisema, Hili ni jeshi la Mungu. Akapaita mahali pale, Mahanaimu. Basi, Yakobo akapeleka wajumbe mbele yake kwenda kwa Esau nduguye mpaka nchi ya Seiri katika nyika ya Edomu. Akawaagiza akisema, Mwambieni hivi bwana wangu, Esau, Hivi ndivyo asemavyo mtumwa wako, Yakobo; Nimekaa ugenini kwa Labani, na kukawia huko hata sasa, nami nina ng'ombe, na punda, na kondoo, na watumwa, na vijakazi; nami nimepeleka watu nimpashe bwana wangu habari, nipate neema machoni pako. Wale wajumbe wakarudi kwa Yakobo wakisema, Tulifika kwa ndugu yako, Esau, naye anakuja kukulaki, na watu mia nne pamoja naye.Ndipo Yakobo akaogopa sana, na kufadhaika sana, akawagawanya watu waliopo pamoja naye, na kondoo, na ng'ombe, na ngamia, wawe matuo mawili. Akasema, Akija Esau kwa kundi la kwanza, akalipiga, kundi litakalosalia litaokoka.Ni wazi kuwa Esau angekuja kufanya vita na Yakobo na yakobo aliogopa na aliamua kumuomba Mungu usiku ule na Mungu alimuelekeza namna ya kupata amani ilimgharimu sana lakini alifabya bidii ili aweze kuwa na amani na ndugu yake, kila atakaye kupenda maisha yaani maisha haya nay ale yajayo hana budi kujikita katika kuitafuta amani kwa bidii, Yakobo aliiitafuta sana na Mungu akamfanikisha  Mwanzo 33:1-11 “Yakobo akainua macho yake, akaona, na tazama, Esau anakuja na watu mia nne pamoja naye. Akawagawanyia Lea, na Raheli, na wale vijakazi wawili, wana wao. Akawaweka hao vijakazi na wana wao mbele, na Lea na wanawe nyuma yao, na Raheli na Yusufu mwisho. Akapita mwenyewe mbele yao, akainama mpaka nchi mara saba, hata alipomkaribia ndugu yake. Esau akaja mbio kumlaki, akamkumbatia, na kumwangukia shingoni, akambusu; nao wakalia. Akainua macho yake, akawaona wale wanawake na watoto, akauliza, Ni nani hawa walio pamoja nawe? Akasema, Ni watoto Mungu aliompa mtumwa wako kwa neema yake. Ndipo wale vijakazi, na wana wao, wakakaribia wakainama.Lea naye, na wanawe, wakakaribia wakainama. Baadaye Yusufu na Raheli wakakaribia, wakainama. Akasema, Kundi hili lote nililolikuta, maana yake ni nini? Akasema, Kunipatia kibali machoni pa bwana wangu.  Esau akasema, Ninayo tele, ndugu yangu, uliyo nayo na yawe yako. Yakobo akasema, Sivyo; kama nimekubalika machoni pako tafadhali upokee zawadi yangu mkononi mwangu, iwapo nimeona uso wako kama kuona uso wa Mungu, ukapendezwa nami. Pokea, tafadhali, mbaraka wangu, ulioletewa, kwa sababu Mungu amenineemesha, na kwa sababu ninavyo hivi vyote Akamshurutisha, naye akapokea.”

 

1Petro 3:10-12Kwa maana, Atakaye kupenda maisha, Na kuona siku njema, Auzuie ulimi wake usinene mabaya, Na midomo yake isiseme hila. Na aache mabaya, atende mema; Atafute amani, aifuate sana. Kwa kuwa macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, Na masikio yake husikiliza maombi yao; Bali uso wa Bwana ni juu ya watenda mabaya.”

 

Na. Rev. Innocent Kamote.

Mkuu wa Wajenzi mwenye Hekima!

Jumanne, 20 Aprili 2021

Mtetezi wangu yu hai

Mstari wa msingi: Ayubu 19:25-27Lakini mimi najua ya kuwa Mteteaji wangu yu hai, Na ya kuwa hatimaye atasimama juu ya nchi. Na baada ya ngozi yangu kuharibiwa hivi, Lakini, pasipokuwa na mwili wangu nitamwona Mungu; Nami nitamwona mimi nafsi yangu, Na macho yangu yatamtazama, wala si mwingine. Mtima wangu unazimia ndani yangu


.”


Utangulizi:

Lakini mimi najua mteteaji wangu yu hai - ni moja ya vifungu vilivyojipoatia umaarufu mkubwa sana katika Biblia na kuvutia mioyo ya watu wengi sana na kutolewa maoni mbalimbali, na wataalamu mbalimbali wa neno la Mungu na watafasiri wengi wa Biblia, huku wengi wakivutiwa na kifungu hiki cha Ayubu 19:25-27 hasa kwa vile kifungu hiki kina uhusiano mkubwa sana na unabii wa kuja Masihi. Lakini sio hivyo tu kifungu hiki kina mvuto mkubwa saa kwa sababu kinapandisha imani zetu. Leo tutachukua muda kwa ufupi kujifunza kuhusiana na kile ambacho Mungu anataka kusema nasi kupitia kifungu hiki.


Kimsingi kitabu cha  Ayubu ni kitabu cha kwanza kati ya vitabu vya Mashairi ya kiibrania, kikifuatiwa na Zaburi, Mithali, Muhubiri na Wimbo uliobora Lakini vitabu hivi pia  ni vitabu vya  Kifalsafa.  Kitabu cha Ayubu chenyewe kina uhusiano mkubwa sana na falsafa ya Mateso na hasa kikiwa na maswali kwa nini mwenye haki ateseke? Lakini kama haitoshi pia kinatabiri mateso ya Yesu ambaye hakuwa na dhambi lakini aliteseka kwa kusudi la kuwakomboa wanadamu, Katika kitabu hiki tunaona kwa undani sana mateso mazito yaliyompata Ayubu na kimsingi Mateso haya yalikuwa na sababu ambayo kwa wakati huo wa Ayubu hakuwa anajua nini kilikuwa kinaendelea katika ulimwengu wa roho, Mateso yake kwa kiwango kikubwa yalichangiwa na wivu, dhuluma na uonevu wa shetani, kama tunavyotahadharishwa leo katika maandiko  Ona 1Petro 5:8 “Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze.” Shetani alileta uonevu huu kwa mtu wa Mungu hata pamoja na kuwa mtu huyu aliishi maisha ya haki, Maandiko yanaonyesha wazi kuwa Ayubu alikuwa mtu wa haki na kwa sababu hiyo mateso yake hayakuwa kwamba ni kwa sababu amemkosea Mungu! Lakini maandiko yanaonyesha wazi kuwa ni kwa sababu ya mshitaki wetu shetani namna na jinsi anavyofanya kazi katika ulimwengu wa roho!


Mateso ya Ayubu:-

 

Ø  Ayubu aliishi maisha ya haki ona Ayubu 1:1-3Palikuwa na mtu katika nchi ya Usi, jina lake alikuwa akiitwa Ayubu; mtu huyo alikuwa mkamilifu na mwelekevu, ni mmoja aliyemcha Mungu, na kuepukana na uovu. Kisha walizaliwa kwake wana saba, na binti watatu. Mali yake nayo yalikuwa ni kondoo elfu saba, na ngamia elfu tatu, na jozi za ng'ombe mia tano, na punda wake mia tano, na watu wa nyumbani wengi sana; basi hivi mtu huyo alikuwa ni mkuu sana kuliko watu wote wa upande wa mashariki.      

 

Ø  Asili ya Mateso ya Ayubu yalitokana na mashitaka ya Shetani katika ulimwengu wa roho ona Ayubu 1:6-12Ilikuwa, siku moja ambayo hao wana wa Mungu walikwenda kujihudhurisha mbele za Bwana, Shetani naye akaenda kati yao. Bwana akamwuliza Shetani, Umetoka wapi wewe? Ndipo Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Natoka katika kuzunguka-zunguka duniani, na katika kutembea huku na huku humo.Kisha Bwana akamwuliza Shetani, Je! Umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Kwa kuwa hapana mmoja aliye kama yeye duniani, mtu mkamilifu na mwelekevu, mwenye kumcha Mungu na kuepukana na uovu. Ndipo Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Je! Huyo Ayubu yuamcha Bwana bure? Wewe hukumzingira kwa ukigo pande zote, pamoja na nyumba yake, na vitu vyote alivyo navyo? Kazi za mikono yake umezibarikia, nayo mali yake imeongezeka katika nchi. Lakini nyosha mkono wako sasa, uyaguse hayo yote aliyo nayo, naye atakukufuru mbele za uso wako. Bwana akamwambia Shetani, Tazama, yote aliyo nayo yamo katika uwezo wako; lakini usinyoshe mkono wako juu yake yeye mwenyewe. Basi Shetani akatoka mbele za uso wa Bwana.”

 

Ø  Shetani alimuonea Ayubu kupitia mali zake ona Ayubu 1:13-19Bwana akamwambia Shetani, Tazama, yote aliyo nayo yamo katika uwezo wako; lakini usinyoshe mkono wako juu yake yeye mwenyewe. Basi Shetani akatoka mbele za uso wa Bwana.Ilitukia siku moja hao wanawe na binti zake walipokuwa wakila na kunywa divai katika nyumba ya ndugu yao mkubwa,mjumbe akamfikilia Ayubu na kumwambia, Hao ng'ombe walikuwa wakilima, na punda walikuwa wakilisha karibu nao; mara Waseba wakawashambulia, wakawachukua wakaenda nao; naam, wamewaua hao watumishi kwa makali ya upanga, mimi peke yangu nimepona, mimi tu, kukuletea habari. Huyo alipokuwa akali akinena, akatokea na mwingine, na kusema, Moto wa Mungu umeanguka kutoka mbinguni na kuwateketeza kondoo, na wale watumishi, na kuwaangamiza; mimi peke yangu nimepona, mimi tu, kukuletea habari. Huyo alipokuwa akali akinena, akatokea na mwingine, na kusema, Wakaldayo walifanya vikosi vitatu, wakawaangukia ngamia, wakaenda nao, naam, wamewaua wale watumishi kwa makali ya upanga; mimi peke yangu nimepona, mimi tu, kukuletea habari. Huyo alipokuwa akali akinena, akatokea na mwingine, na kusema, Wanao na binti zako walikuwa wakila na kunywa divai katika nyumba ya ndugu yao mkubwa; mara, tazama, upepo wenye nguvu ukatoka pande za jangwani, ukaipiga hiyo nyumba pembe zake nne, nayo ikawaangukia hao vijana, nao wamekufa; na mimi peke yangu nimepona, mimi tu, kukuletea habari.

 

Ø  Shetani alimuonea Ayubu kupitia afya yake aliiharibu kabisa afya ya Ayubu kwa sababu Ayubu alikuwa ma majipu mabaya yaliyokuwa yakioza na kufumba na kupasuka kila eneo la mwili wake  

     Ayubu 2:7-10 “Basi Shetani akatoka mbele za uso wa Bwana, akampiga Ayubu na majipu mabaya tangu wayo wa mguu hata utosi wa kichwa.Naye akashika kigae cha kujikunia; akaketi majivuni. Ndipo mkewe akamwambia, Je! Wewe hata sasa washikamana na utimilifu wako? Umkufuru Mungu, ukafe. Lakini yeye akamwambia, Wewe wanena kama mmoja wa hao wanawake wapumbavu anenavyo. Je! Tupate mema mkononi mwa Mungu, nasi tusipate na mabaya? Katika mambo hayo yote Ayubu hakufanya dhambi kwa midomo yake.”           

Ø  Watu na rafiki zake Ayubu waliposikia yaliyompata walifunga safari kuja kumtia moyo lakini walipoona kwa mbali hali halisi ya maisha ya Ayubu waliomboleza kwa kulia sana na kurarua mavazi yao, huku wakirusha michanga juu, inasemekana kwa siku saba wote walikaa kimya na hakuna aliyeweza kuzungumza lolote yaani walishindwa unaanzia wapi kumfariji kwani yaoikuwa ni majanga makubwa mno ona  


Ayubu 2:11-13 “Basi ikawa hao rafikize Ayubu watatu walipopata habari ya mabaya hayo yote yaliyomfikilia, wakaja kila mtu kutoka mahali pake; nao ni Elifazi Mtemani, na Bildadi Mshuhi, na Sofari Mnaamathi; wakapatana pamoja ili waende kumlilia Ayubu na kumtuliza moyo. Basi walipovua macho yao, nao wakali mbali, wasimtambue, wakainua sauti zao na kulia; kila mmoja akararua joho yake, wakarusha mavumbi juu ya vichwa vyao kuelekea mbinguni. Kisha wakaketi nchi pamoja naye muda wa siku saba, mchana na usiku, wala hapana mmoja aliyenena naye neno lo lote; kwa maana waliona ya kuwa mashaka yake aliyo nayo ni makuu mno.”    

 

Ø  Mateso ya Ayubu yalizidi kiasi cha kufikia kiwango cha kuilaani siku yake ya kuzaliwa ona Ayubu 3:1-4 “Baada ya hayo Ayubu akafunua kinywa chake, na kuilaani siku yake. Ayubu akajibu, na kusema; Na ipotelee mbali ile siku niliyozaliwa mimi, Na ule usiku uliosema, Mtoto mume ametungishwa mimba. Siku hiyo na iwe giza; Mungu asiiangalie toka juu, Wala mwanga usiiangazie.”Ayubu alitamani kama angekufa tangu tumboni ili aweze kupumzika aliyaona maisha ya dunia hii kuwa ni maisha yasiyofaa hata kidogo Mstari wa 11-13 unasema hivi “Mbona si kufa mimi tokea mimbani? Mbona nisitoe roho hapo nilipotoka tumboni? Mbona hayo magoti kunipokea? Au hayo maziwa, hata nikanyonya? Maana hapo ningelala na kutulia; Ningelala usingizi; na kupata kupumzika;

 

Ø  Pamoja na mates ohayo yote inasemekana kuwa Ayubu alikimbiwa na watu wote waliokuwa karibu naye tunaelezwa wazi mwanzoni kuwa watu wengi sana walimjia Ayubu alipokuwa na uwezo ona Ayubu 1:3 “Mali yake nayo yalikuwa ni kondoo elfu saba, na ngamia elfu tatu, na jozi za ng'ombe mia tano, na punda wake mia tano, na watu wa nyumbani wengi sana; basi hivi mtu huyo alikuwa ni mkuu sana kuliko watu wote wa upande wa mashariki.” Lakini Ayubu alipopatwa na majanga na umasikini kila mtu alimkimbia ona Ayubu 19:13-21 “Amewaweka ndugu zangu mbali nami, Na wanijuao wametengwa nami kabisa. Watu wa mbari yangu wamekoma, Na rafiki zangu niwapendao wamenisahau. Wakaao nyumbani mwangu, na vijakazi vyangu, wanihesabu kuwa mgeni; Mimi ni mgeni machoni pao. Namwita mtumishi wangu, wala haniitikii, Ingawa namsihi kwa kinywa changu. Pumzi zangu ni kama za mgeni kwa mke wangu, Nami ni machukizo kwa ndugu zangu. Hata watoto wadogo hunidharau; Nikiondoka, huninena. Wasiri wangu wote wanichukia; Na hao niliowapenda wamenigeukia. Mfupa wangu unagandamana na ngozi yangu na nyama yangu, Nami nimeokoka na ngozi ya meno yangu tu. Nihurumieni, nihurumieni, enyi rafiki zangu, Kwa maana mkono wa Mungu umenigusa.”

 

Ø  Ayubu alikuwa na Machungu mengi sana Moyoni na alifikiri kuwa mambo yote hayo maovu na mabaya yanatoka kwa Mungu alimlaumu muumba wake ona Ayubu 6:2-4 “ Laiti uchungu wangu ungepimwa, Na msiba wangu kutiwa katika mizani pamoja! Kwa kuwa sasa ungekuwa mzito kuliko mchanga wa bahari; Kwa hiyo maneno yangu yamekuwa ya haraka. Kwa kuwa mishale ya huyo Mwenyezi i ndani yangu, Na roho yangu inainywa sumu yake; Vitisho vya Mungu vimejipanga juu yangu.

 

Mtetezi wangu yu hai!:-

Kutokana na uoenvu huu wa shetani Ayubu alielewa kuwa alikuwa anaonewa na kudhulumiwa na Ibilisi alifahamu kuwa nimshitaki wetu yuko kazini na anamchochea Muumba ilia pate kufanya haya aliyoyafanya shetani, hata hivyo pamoja na changamoto zote hizo imani yake Ayubu haikutindika aliamini ya kuwa mteteaji wake yu hai nay a kuwa hatimaye ataismama juu ya nchi kumtetea

Ni muhimu kufahamu kuwa neno linalotrumika hapa kwa Mteteaji wangu katika kiingereza linasomeka kama “redeemer” katika lugha ya kiebrania neno linalotumika hapo ni ni Ga’al au Go’ al ambalo lilitumika kumaanisha mtu mwenye kulipia gharama ya hasara zote ulizozipata, au aliyekulipia gharama za shamba lililouzwa, au mali iliyopotea, au anayekukomboa kutoka katika umasikini kwa mfano ulipoteza shamba lako kwa umasikini kisha akaja ndugu yako aliye karibu akalilipia na kukurudishia huyu sasa ndiye aliyeitwa Ga’al au Go’ al   kwa kizigua Mkombozi, ona kwa mfano Mambo ya walawi 25:25-26 “Kwamba nduguyo amekuwa maskini, na kuuza sehemu ya milki yake, ndipo jamaa yake aliye karibu naye atakuja, naye ataikomboa ile aliyoiuza nduguye. Na kama mtu hana atakayeikomboa, naye mwenyewe amepata mali na kujiona kuwa anayo ya kutosha kuikomboa;” Neno hilo pia lilitumika kwa mtu aliyechukuliwa utumwani kisha mtu akaja kumnunua kwa kusudi la kumkomboa unaweza kuliona katika Kutoka 6:6 na Isaya 43:1 ona Kutoka 6:6 “Basi waambie wana wa Israeli, Mimi ni YEHOVA, nami nitawatoa ninyi mtoke chini ya mizigo ya Wamisri, nami nitawaokoa na utumwa wao, nami nitawakomboa kwa mkono ulionyoshwa, na kwa hukumu kubwa;” pia angalia Isaya 43:1 “Lakini sasa, Bwana aliyekuhuluku, Ee Yakobo, yeye aliyekuumba, Ee Israeli, asema hivi, Usiogope, maana nimekukomboa; nimekuita kwa jina lako, wewe u wangu.”

Mpendwa haijalishi umekosa furaha na amani mara ngapi, haijalishi umedhulumiwa mara ngapi, haujalishi umefanyiwa fitina mara ngapi, haijalishi umeteseka kwa muda gani, hajalishi shetani amekuonea kwa kiwango gani, haijalishi kwamba una onewa na magonjwa na mateso kwa kiwango gani , haijalishi wazee wa kanisa nwanakukandamiza kwa kiwango gani, hajalishi manabii wamekudhulumu kwa kiwango gani, hajalishi unapitia changamoto za aina gani, haijalishi umeibiwa mara ngapi, haijalishi umelizwa mara ngapi, haijalishi una huzuni kwa kiasi gani  leo natangaza ya kuwa Mkombozi wetu yu hai, Ayubu aliamini ya kuwa siku moja atasimama atatokea juu ya uso wa nchi na kumtetea mimi natangaza kuwa amekwishakutokea, namtangaza metetaji wetu yuko hai na kuwa ameketi mkono wa kuume wa nguvu; Mbinguni na anafuatulia kwa ukaribu maumivu na mateso unayoyapitia, nakutaarifu kuwa mbingu zina taarifa ya kile unapitia, Mbingu zinataarifa ya kile familia yako inapitia, mama yako na baba yako na wazazi wako na ndugu zako kila wanalolipitia na kile unapitia katika ndoa yako na popote pale nakutangazia kuwa Yuko mkombozi yuko mtetezi haijalishi ni huzuni kiasi gani tunapitia lakini nataka tumuamini kuwa anajua hali zetu na kuwa hatupaswi kuogopa lolote,  na kuwa atalipa atatulipia machungu yote na machozi yote na huzuni zote tutalipiwa tu Mungu yuko atatulipia, Mtetezi wetu yu hai aatashughulika hatupaswi kuogopa ametuita kwa jina lake ametukomboa kwa mkono wake yu haiiiiii!

Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa Wajenzi mwenye Hekima