Alhamisi, 3 Februari 2022

Jinsi ya kuzidi kuwa Hodari.

Matendo 9:22 “Sauli akazidi kuwa hodari, akawatia fadhaa Wayahudi waliokaa Dameski, akithibitisha ya kuwa huyu ndiye Kristo


Utangulizi:

Tunasoma Katika maandiko ya kwamba watu wengi wanaotajwa kama mashujaa wa Imani katika biblia, kwamba walikuwa hodari ona katika

Waebrania 11:32-34 “Nami niseme nini tena? Maana wakati usingenitosha kuleta habari za Gideoni na Baraka na Samsoni na Yeftha na Daudi na Samweli na za manabii; ambao kwa imani walishinda milki za wafalme, walitenda haki, walipata ahadi, walifunga vinywa vya simba, walizima nguvu za moto, waliokoka na makali ya upanga. Walitiwa nguvu baada ya kuwa dhaifu, walikuwa hodari katika vita, walikimbiza majeshi ya wageni.”

Kwa msingi huo ni kama kusema watu wote wenye mafanikio na wanaondelea kufanikiwa katika ulimwengu walikuwa na uhodari ndani mwao na huu uhodari pia unaweza kuzidi zaidi na zaidi, maandiko yanatueleza kuwa Sauli akazidi kuwa hodari hii maana yake ni kuwa alikuwa hodari na akaendelea kuwa hodari, kuwa hodari na hata kujilinda na kuendelea katika uhodari huo sio jambo jepesi, kuna mambo ambayo ukiyafanya utazidi kuwa hodari katika maisha yako, kabla ya kuzungumiza jinsi ya kuzidi kuwa hodari, ni muhimu kwetu tukajifunza somo hili jinsi ya kuzidi kuwa Hodari kwa kuzingatia vipengele viwili vifuatavyo:-

·         Maana ya neno Hodari

·         Jinsi ya kuzidi kuwa Hodari

Maana ya Neno Uhodari:-

Neno hodari limetajwa mara kadhaa katika maandiko, Kila mtu anayetajwa katika maandiko anatajwa vilevile kuwa alikuwa na uhodari hususani wale wote ambao walikuwa maarufu na ambao Mungu aliwatumia kwa viwango vya juu katika maandiko kwa mfano tunasoma katika

Matendo 7:22 “Musa akafundishwa hekima yote ya Wamisri, akawa hodari wa maneno na matendo.”

Unaona tunasoma kuwa Musa alifundishwa Hekima yote ya Wamisri, akawa Hodari wa maneno na matendo, kwa msingi huo basi ili tuweze kufanikiwa katika maisha yetu na tusiweze kuharibikiwa hatuna budi kuhakikisha ya kwamba katika kila  Nyanja ya maisha yetu tunapaswa kuwa na uhodari, na kuzidi.

Matendo 18:24-26 Basi Myahudi mmoja, jina lake Apolo, mzalia wa Iskanderia, mtu wa elimu, akafika Efeso; naye alikuwa hodari katika maandiko. Mtu huyo alikuwa amefundishwa njia ya Bwana; na kwa kuwa roho yake ilikuwa ikimwaka, alianza kunena na kufundisha kwa usahihi habari za Yesu; naye alijua ubatizo wa Yohana tu.  Akaanza kunena kwa ujasiri katika sinagogi; hata Prisila na Akila walipomsikia wakamchukua kwao, wakamweleza njia ya Bwana kwa usahihi zaidi.”

Kwa hiyo utaona hivyo tena na tena katika maandiko kila wakati neno uhodari likijirudia tena na tena kwa watu waliokuwa na kitu cha ziada kwa msingi huo ni muhimu kwetu kuwa na ufahamu wa kutosha ili tuweze kujua ni nini maana ya neno hodari au na kwanini agizo la Mungu katika maandiko linatutaka kuwa hodari ona

 Joshua 1:6-7 “Uwe hodari na moyo wa ushujaa, maana ni wewe utakayewarithisha watu hawa nchi hii niliyowaapia baba zao ya kwamba nitawapa. Uwe hodari tu na ushujaa mwingi, uangalie kutenda sawasawa na sheria yote aliyokuamuru Musa mtumishi wangu; usiiache, kwenda mkono wa kuume, au wa kushoto, upate kufanikiwa sana kila uendako.”:-

Sasa basi ni nini maana ya kuwa Hodari? Manoneo yanayotumika katika maandiko kuelezea maana ya kuwa hodari katika lugha ya kiingereza ni pamoja na:-

Be strong and Courageous Be powerful ambalo maneno mengine yanayorumika sambaba na neno hili ni Capable, Forceful, Mighty, Potent, powerful, Fit na kadhalika, Hata hivyo neno hilo katika lugha ya kivita waebrania wanatumia neno “MARSHAL” ambalo mara nyingi au chache hutumika kwa maofisa wa jeshi wa ngazi ya juu kabisa wenye weledi wa kufanya mambo ya kupita kawaida, au kufanya mambo zaidi ya jinsi ulivyofundishwa katika Nyanja ya kijeshi ni Fidel Marshal – is the most senior military rank, or ordinary senior to the General officer ranks, usually it is the highest rank ina an army, and such few persons are appointed to it  Kwa hiyo tunapozungumzia mtu Hodari ni yule anayefanya mambo kwa weledi, au kwa ubora zaidi ya jinsi alivyoelekezwa na kufundishwa !  kwa hiyo maandiko yanapozungumzia wale mashujaa wa imani kuwa walikuwa hodari maana yake walikuwa na rank za juu zaidi za kijeshi, walifanya mambo kwa weledi kwa viwango vya juu zaidi ya jinsi ya walivyofundishwa

Waebrania 11:32-34 “Nami niseme nini tena? Maana wakati usingenitosha kuleta habari za Gideoni na Baraka na Samsoni na Yeftha na Daudi na Samweli na za manabii; ambao kwa imani walishinda milki za wafalme, walitenda haki, walipata ahadi, walifunga vinywa vya simba, walizima nguvu za moto, waliokoka na makali ya upanga. Walitiwa nguvu baada ya kuwa dhaifu, walikuwa hodari katika vita, walikimbiza majeshi ya wageni.”

 Kwa msingi huo sasa Mungu anatutaka na sisi tuwe hodari, lakini kama ni mahodari sasa tuzidi kuwa hodari unaona sasa basi ni kwa jinsi gani tunaweza kuzidi kuwa Hodari?

1.      Uwe mtu wa Haki 

A man of integrity he is or she is a person who is value what is honest, true, noble, trustworthy, kind and right ahead of Personal gain yaani ni mtu mwenye kupenda kweli, mwenye kustahi, mwenye kutenda haki, msafi asiye na lawama, mwema na mwenye sifa njema

 Waefeso 4:8 “Hatimaye, ndugu zangu, mambo yo yote yaliyo ya kweli, yo yote yaliyo ya staha, yo yote yaliyo ya haki, yo yote yaliyo safi, yo yote yenye kupendeza, yo yote yenye sifa njema; ukiwapo wema wo wote, ikiwapo sifa nzuri yo yote, yatafakarini hayo.”

Mtu wa haki anatembea na uwepo wa Mungu, au Mungu hufanya masikani yake au atadumu katika vizazi vyake atadumu katika uwepo wa Mungu atakaa katika masikani za Mungu atafanikiwa

Zaburi 15:1-3 “Bwana, ni nani atakayekaa Katika hema yako? Ni nani atakayefanya maskani yake Katika kilima chako kitakatifu? Ni mtu aendaye kwa ukamilifu, Na kutenda haki. Asemaye kweli kwa moyo wake, Asiyesingizia kwa ulimi wake. Wala hakumtenda mwenziwe mabaya, Wala hakumsengenya jirani yake.”

Unapochunguza maisha ya watu Hodari utaweza kuona moja ya sifa wanayotajwa kuwa nayo ni kutenda haki, hawakuwa na hila ndani yao andiko lile katika Waebrania linasisitiza kuwa mashujaa wa imani walitenda haki sasa basi ikiwa tutaishi maisha ya haki tutazidi kuwa hodari kwa sababu Mungu atatubariki ona

Zaburi 119:1 -3Heri walio kamili njia zao, Waendao katika sheria ya Bwana. Heri wazitiio shuhuda zake, Wamtafutao kwa moyo wote. Naam, hawakutenda ubatili, Wamekwenda katika njia zake.”

2.      Uwe na dhamiri Njema 

Ni muhimu kufahamu kuwa watu Hodari vilevile ni watu wanaokuwa na dhamiri njema, kila unalilifanya unalifanya bila unafiki, Maandiko yanawataka wakristo kuwa na dhamiri njema ni muhimu kukumbuka kuwa Mungu hatahukumu matendo ya nje Mungu anaangalia ndani ya moyo na kupima dhamiri yetu, Neno dhamiri katila lugha ya kiyunani ni SUNOIDA Neno hili limetajwa mara 34 katika agano jipya mara nne katika injli na kitabu cha matendo ya mitume lakini mara 30 katika nyaraka ka Mtume Paulo wakati wote akisisitiza watu kuwa na dhamiri njema, kutokufanya jambo kwaajili ya unafiki,  ona

1Timotheo 1:5-6 “Walakini mwisho wa agizo hilo ni upendo utokao katika moyo safi na dhamiri njema, na imani isiyo na unafiki. Wengine wakiyakosa hayo wamegeukia maneno ya ubatili

1Timotheo 1:18-20 “Mwanangu Timotheo, nakukabidhi agizo hilo liwe akiba, kwa ajili ya maneno ya unabii yaliyotangulia juu yako, ili katika hayo uvipige vile vita vizuri; uwe mwenye imani na dhamiri njema, ambayo wengine wameisukumia mbali, wakaangamia kwa habari ya Imani.  Katika hao wamo Himenayo na Iskanda, ambao nimempa Shetani watu hao, ili wafundishwe wasimtukane Mungu.”

Matendo 23:1 ”Paulo akawakazia macho watu wa baraza, akasema, Ndugu zangu, mimi kwa dhamiri safi kabisa nimeishi mbele za Mungu hata leo hivi.”

Matendo 24:16 “Nami ninajizoeza katika neno hili niwe na dhamiri isiyo na hatia mbele za Mungu na mbele ya watu siku zote

1Timotheo 3:8-10 “Vivyo hivyo mashemasi na wawe wastahivu; si wenye kauli mbili, si watu wa kutumia mvinyo sana, si watu wanaotamani fedha ya aibu.wakiishika siri ya imani katika dhamiri safi. Hawa pia na wajaribiwe kwanza; baadaye waitende kazi ya shemasi, wakiisha kuonekana kuwa hawana hatia.”

Muda usingeweza kutosha kuona namna maandiko yanavyokazia tena na tena swala la kuwa na Dhamiri njema SUNOIDA kumfikiri Mungu na wanadamu 2Wakoritho 8:20-21 “Tukijiepusha na neno hili, mtu asije akatulaumu kwa habari ya karama hii tunayoitumikia; tukitangulia kufikiri yaliyo mema, si mbele za Bwana tu, ila na mbele ya wanadamu.”

3.      Endelea kujisomea siku zote 

Ni muhimu kufahamu kuwa watu waliokuwa hodari vilevile na wanaozidi kuwa Hodari huwa wanasoma na wanajiendeleza katika maarifa, maandiko yanaonyesha kuwa kadiri mtu anavyosoma ndivyo anavyoongeza ufahamu wake zaidi ona

Mathayo 24:15 “Basi hapo mtakapoliona chukizo la uharibifu, lile lililonenwa na nabii Danieli, limesimama katika patakatifu (asomaye na afahamu),

Kusoma kunaleta ugunduzi wa siri nyingi sana za kimaandiko Nabii Daniel aligundua kuwa siku za kukaa kwao utumwani zilitabiriwa kuwa ni miaka 70 na hivyo kwa kusoma vitabu alighundua kuwa wakati huo umefika na akaanza kumuomba Mungu ona

 Daniel 9:1-3 “Katika mwaka wa kwanza wa Dario, mwana wa Ahasuero, wa uzao wa Wamedi, aliyetawazwa kuwa mfalme juu ya milki ya Wakaldayo; katika mwaka wa kwanza wa kumiliki kwake, mimi Danieli, kwa kuvisoma vitabu, nalifahamu hesabu ya miaka, ambayo neno la Bwana lilimjia Yeremia nabii, ya kuutimiza ukiwa wa Yerusalemu, yaani, miaka sabini. Nikamwelekezea Bwana Mungu uso wangu, ili kutaka kwa maombi, na dua, pamoja na kufunga, na kuvaa nguo za magunia na majivu.”

Unaona kumbe Nabii Daniel aligundua baadhi ya mambo kwa kusoma na akaingiza kumuomba Mungu, ziko siri nyingi zimefichwa katika vitabu, hivyo watu wanaozigundua ni wale wanaosoma asomaye na afahamu, watu wengi huwa wanashangazwa sana na hekima kubwa aliyokuwa nayo Paulo Mtume lakini ukichunguza kwa undani utagundua kuwa mpaka anakuwa mzee alikuwa ni mtu mwenye tabia ya kupenda kujisomea, hakufikiri kuwa amekwisha kufika lakini mara kwa mara alitaka kujiendeleza na alikuwa na tabia ya kujisomea ona,

2Timotheo 4:13 “Lile joho nililoliacha kwa Karpo huko Troa, ujapo ulilete, na vile vitabu, hasa vile vya ngozi.”           

Je wewe unajisomea? Unaongeza maarifa kwa kupenda kujisomea? Kusoma kunaongeza maarifa na maarifa yanaongeza ujuzi na ujuzi unaleta weledi na kukufanya wewe kuwa Hodari.

4.      Fanya maamuzi sahihi 

Moja ya mambo ambayo yanawaletea watu wengi sana majuto katika maisha yao ni pamoja na swala zima la kufanya uamuzi, wako watu wengi sana ambao wanajutia maamuzi waliyoyafanya na wanahitaji second chance, lakini imeshindikana kwa sababu ya maamuzi yao! Mashujaa wa imani kila walipotaka kufanya jambo hawakutumia akili zao, waliuliza kutoka kwa Bwana

1Samuel 23:1-3 “Kisha wakamwambia Daudi, kusema, Angalia, Wafilisti wanapigana vita juu ya Keila na kuiba nafaka sakafuni mwa kupuria. Basi Daudi akamwuliza Bwana, kusema, Je! Niende nikawapige hao Wafilisti? Naye Bwana akamwambia Daudi, Nenda ukawapige Wafilisti, na kuuokoa Keila. Ila watu wake Daudi wakamwambia, Tazama, sisi tunaogopa hapa katika Yuda; je! Si zaidi tukienda Keila juu ya majeshi ya Wafilisti? Basi Daudi akamwuliza Bwana tena, Naye Bwana akamjibu, akasema, Ondoka, ukashukie Keila; kwa kuwa nitawatia hao Wafilisti mikononi mwako.”

1Samuel 23:9-13 “Naye Daudi alifahamu ya kuwa Sauli amemkusudia mabaya; akamwambia Abiathari, kuhani, Lete hapa hiyo naivera. Ndipo Daudi akasema, Ee Bwana, Mungu wa Israeli, mimi mtumwa wako nimesikia hakika ya kuwa Sauli anataka kuja huku Keila, ili kuuharibu mji kwa ajili yangu. Je! Watu wa Keila watanitoa, nitiwe mkononi mwake? Je! Sauli atashuka, kama mtumwa wako alivyosikia? Ee Bwana, Mungu wa Israeli, nakusihi, umwambie mtumwa wako. Naye Bwana akamjibu, Atashuka. Ndipo Daudi akasema, Je! Watu wa Keila watanitia mimi na watu wangu mkononi mwake Sauli? Bwana akasema, Watakutia. Basi Daudi na watu wake, ambao wapata kama mia sita, wakaondoka na kutoka Keila, wakaenda po pote walipoweza kwenda. Kisha Sauli akaambiwa ya kwamba Daudi amekimbia toka Keila; akaacha kutoka nje"

1Samuel 30:8-9 “Daudi akauliza kwa Bwana, akasema, Je! Nikiwafuata jeshi hili, nitawapata? Naye akamjibu, Fuata; kwa kuwa hakika utawapata, nawe hukosi utawapokonya wote. Basi Daudi akaenda, yeye na wale watu mia sita waliokuwa pamoja naye, nao wakakifikilia kijito Besori, ambapo wale walioachwa nyuma walikaa.”

Unaona Daudi kila alipokuwa anataka kufanya jambo aliuliza kutoka kwa Bwana, kwanini alikuwa anafanya hivi ni ili aweze kufanya maamuzi sahihi bila kutumia au kutegemea akili zake yeye mwenyewe maandiko yanasema hivi katika Mithali3:5-6 “Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote, Wala usizitegemee akili zako mwenyewe; Katika njia zako zote mkiri yeye, Naye atayanyosha mapito yako. Usiwe mwenye hekima machoni pako; Mche Bwana, ukajiepushe na uovu.”

5.      Hakikisha unakuwa mnyenyekevu.

Wengi wetu tunatabia ya kupuuzia hali ya kuwa kujinyenyekeza, Mungu anapotuinua tunainuka na kiburi, na kwa sababu hiyo inakuwa ngumu kwetu kufundishika na hata kuonyeka, hasa pale tunapofikiri kuwa labda tuna akili kuliko wengine, au tunaweza kujidhani kuwa sisi ni kitu  maandiko yanaonya sana tabia ya kujiinua na kujikweza na yanatufundisha kuwa wanyenyekevu, unyenyekevu huwa unalipa, Yesu Kristo Bwana wetu aklifanikiwa sana kwa sababu alikuwa mnyenyekevu na Mungu akamuadhimisha mno

Wafilipi 2:3-11 “Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake. Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine.  Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu; ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho; bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu; tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba. Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina; ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi; na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI BWANA, kwa utukufu wa Mungu Baba.”

Kanuni ya Mungu ya kumpeleka mtu juu ni mtu huyo kujishusha, kujinyenyekeza, Yesu mwenyewe alisema hivi katika Luka 14:8-11 “Ukialikwa na mtu arusini, usiketi katika kiti cha mbele; isiwe kwamba amealikwa mtu mwenye kustahiwa kuliko wewe, akaja yule aliyewaalika wewe na yeye, na kukuambia, Mpishe huyu! Ndipo utakapoanza kwa haya kushika mahali pa nyuma. Bali ukialikwa, nenda ukaketi mahali pa nyuma, ili ajapo yule aliyekualika akuambie, Rafiki yangu, njoo huku mbele zaidi; ndipo utakapokuwa na utukufu mbele ya wote walioketi pamoja nawe. Kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa.”

Watu wengi sana duniani wanabadilika mno wanapopata madaraka au kibali, au pale Mungu anapokuwa amekusudia kuwapeleka kwenye ngazi nyingine, wanapokuwa wamefanikiwa hujisahau na kuwa na kiburi kiasi cha kutokytaka kuwasikiliza wengine, hata watu wa Mungu huonekana kuwa wajinga na hawawezi kusikilizwa katika nafasi yao

2Mambo ya Nyakati 26:16-20 “Lakini alipokuwa na nguvu, moyo wake ulitukuka, hata akafanya maovu, akamwasi Bwana, Mungu wake; kwani aliingia hekaluni mwa Bwana, ili afukize uvumba juu ya madhabahu ya kufukizia. Azaria kuhani akaingia nyuma yake, na pamoja naye makuhani themanini wa Bwana, mashujaa; wakamzuia Uzia mfalme, wakamwambia, Si haki yako, Uzia, kumfukizia Bwana uvumba, ila ni haki ya makuhani wana wa Haruni, waliofanywa wakfu, ili wafukize uvumba; toka katika patakatifu; kwa kuwa umekosa; wala haitakuwa kwa heshima yako kutoka kwa Bwana, Mungu. Akaghadhibika Uzia; naye alikuwa na chetezo mkononi cha kufukizia uvumba; naye hapo alipowaghadhibikia makuhani, ukamtokea ukoma katika paji la uso wake mbele ya makuhani nyumbani mwa Bwana karibu na madhabahu ya kufukizia. Azaria kuhani mkuu na makuhani wote wakamtazama, na angalia, alikuwa na ukoma pajini mwa uso, wakamtoa humo upesi; hata na yeye mwenyewe akafanya haraka kutoka, kwa sababu Bwana amempiga.” 

Unaona hii ni kanuni kubwa sana ya mafanikio kwa mashujaa wa imani, wengi walifanikiwa kwa sababu walifahamu umuhimu wa kuwa wanyenyekevu, na wengine tunawasoma kuwa kwa sababu ya kiburi waliasi na kupatwa na mabaya kanuni za Mungu hazidanganyi kuwa kijapo kiburi ndipo ijapo aibu Mithali 11:2 “Kijapo kiburi ndipo ijapo aibu; Bali hekima hukaa na wanyenyekevu.” Ni kwaajili ya haya sasa Ndipo Mungu anatutaka katika neno lake tuwe wanyenyekevu, ukijinyenyekeza neema ya Mungu inakuwa kubwa sana, lakini kama hatutajua kanuni ya kujinyenyekeza Mungu atapinga anasi yeye mwenyewe kwani ukiwa na kiburi unashughulikiwa na Mungu 1Petro 5:5 “Vivyo hivyo ninyi vijana, watiini wazee. Naam, ninyi nyote jifungeni unyenyekevu, mpate kuhudumiana; kwa sababu Mungu huwapinga wenye kiburi, lakini huwapa wanyenyekevu neema.”

6.      Uwe mwaminifu.

Hakuna jambo Muhimu katika maisha ya mwanadamu kama uaminifu, kila mtu duniani anapenda mtu mwaminifu, hata mume mzinzi au mke mzinzi bado anataka apatiwe uaminifu kutoka kwa mwenziwe, Maandiko yanatutaka tuwe waaminifu, tena tuwe waaminifu hta kufa

Ufunuo 2:10 “Usiogope mambo yatakayokupata; tazama, huyo Ibilisi atawatupa baadhi yenu gerezani ili mjaribiwe, nanyi mtakuwa na dhiki siku kumi. Uwe mwaminifu hata kufa, nami nitakupa taji ya uzima.

Kuwa mwaminifu ni kujidhabihu, ni kujitoa, commitment- kiyunani DESMEFSI ambalo kwa tafasiri ya kiingereza ni imprisonment - kujifunga au kufanya maamuzi magumu mfano hutafanya jambo Fulani mapaka jambo Fulani limefanikiwa:-

1Samuel 6:9-11 “Ndipo Yese akampitisha Shama. Naye akasema, wala Bwana hakumchagua huyu. Yese akawapitisha wanawe saba mbele ya Samweli. Samweli akamwambia Yese, Bwana hakuwachagua hawa. Kisha Samweli akamwambia Yese, Watoto wako wote wapo hapa? Naye akasema, Amesalia mdogo wao, na tazama, anawachunga kondoo. Basi Samweli akamwambia Yese, Tuma watu, wamlete; kwa sababu hatutaketi hata atakapokuja huku.”

Matendo 23:12 “Kulipopambauka, Wayahudi wakafanya mapatano, wakajifunga kwa kiapo kwamba hawatakula wala hawatakunywa hata wamwue Paulo.”

Esta 4:15-16 “Basi Esta akawatuma ili wamjibu Mordekai, Uende ukawakusanye Wayahudi wote waliopo hapa Shushani, mkafunge kwa ajili yangu; msile wala kunywa muda wa siku tatu, usiku wala mchana, nami na wajakazi wangu tutafunga vile vile; kisha nitaingia kwa mfalme, kinyume cha sheria; nami nikiangamia, na niangamie.”

Kwa msingi huo kuwa mwaminifu kuna maana ya kujifunga, lakini pia kusimamia kitu mpaka kifanikiwe kwamba iwe ni jambo kubwa au kwamba ni jambo dogo, kwa mujibu wa mafundisho ya Yesu Kristo yeye alisisitiza kuwa uaminifu pia unapimwa katika kuanzia na mambo madogo madogo sana Yesu anaamini kuwa mtu akiwa muaminifu katika jambo lililo dogo anaweza kuwa mwaminifu katika jambo lililo kubwa zaidi

Luka 16:10-12 “Aliye mwaminifu katika lililo dogo sana, huwa mwaminifu katika lililo kubwa pia; na aliye dhalimu katika lililo dogo, huwa dhalimu katika lililo kubwa pia. Basi, kama ninyi hamkuwa waaminifu katika mali ya udhalimu, ni nani atakayewapa amana mali ya kweli? Na kama hamkuwa waaminifu katika mali ya mtu mwingine, ni nani atakayewapa iliyo yenu wenyewe?

 Watu wengi sana wameshindwa kuwa hodari katia nafasi walizo nazo na vipawa walivyo navyo kwa sababu tu wameshindwa kuwa waaminifu, Mungu anahitaji watu ambao ni waaminifu Uaminifu ni tabia ya Mungu ili sisi nasi tuwe kama baba wa Mbinguni hatuna budi kuwa na tabia hii ya uungu kwa kuwa waaminifu na Mungu atatufanikisha

Zaburi 145:17 “Bwana ni mwenye haki katika njia zake zote, Na mwenye fadhili juu ya kazi zake zote.”

Kwa msingi huo Mungu anatutaka sisi nasi tuwe waaminifu kwa kuingia katika ushirika wa mwanawe ona

1Wakoritho 1:9 “Mungu ni mwaminifu ambaye mliitwa na yeye mwingie katika ushirika wa Mwanawe, Yesu Kristo Bwana wetu.”

7.      Lazima uwe na uvumilivu

Watu hodari vilevile ni wavumilivu, au wenye subira ni vigumu sana kuwa na mafanikio kwa njia rahisi rahisi, mafanikio yanawakuta watu wenye uwezo mkubwa katika uvumilivu, tunaambiwa kuwa manqabii wote walikuwa wavumilivu sana lakini vilevile tunaambiwa kuwa Ayubu alikuwa mvumilivu, Mungu anapoona uvumilivu wetu hatimaye anatukumbuka na kutufadhili ona

Yakobo 5: 10-11 “Ndugu, watwaeni manabii walionena kwa jina la Bwana, wawe mfano wa kustahimili mabaya, na wa uvumilivu. Angalieni, twawaita heri wao waliosubiri. Mmesikia habari ya subira yake Ayubu, mmeuona mwisho wa Bwana ya kwamba Bwana ni mwingi wa rehema, mwenye huruma.”

Hakuna mafanikio ya kufumba na kufumbua, wala mafanikio hayaji kwa usiku mmoja, watu wote waliofanikiwa duniani walikuwa na tabia ya uvumilivu, kujifunza kuwa wavumilivu kutatuletea hali ya kuzaa matunda, ukitaka kuwa na afya imara lazima ufanye mazoezi, mazoezi sio kitu kitamu, utakimbia, utabeba vitu vizito, utatembea na kufanya hili ama lile mambo ambayo yanahitaji nidhambu ya hali ya juu, kwa ufupi uvumilivu ni nidhamu ya hali ya juu, kila jambo litahitaji uvumilivu Yesu katika mfano wake ule wa mbegu alionyesha wazi kuwa hata zile zinazozaa matunda huwa hazizai bila uvumilivu ona

Luka 8:11-15 “Na huo mfano, maana yake ni hii; Mbegu ni neno la Mungu. Wale wa karibu na njia ndio wasikiao, kisha huja Ibilisi akaliondoa hilo neno mioyoni mwao, wasije wakaamini na kuokoka. Na wale penye mwamba ndio wale ambao wasikiapo hulipokea lile neno kwa furaha; nao hawana mizizi, huamini kitambo kidogo, na wakati wa kujaribiwa hujitenga. Na zilizoanguka penye miiba ni wale waliosikia, na katika kuenenda kwao husongwa na shughuli na mali, na anasa za maisha haya, wasiivishe lo lote. Na zile penye udongo mzuri, ndio wale ambao kwa unyofu na wema wa mioyo yao hulisikia neno, na kulishika; kisha huzaa matunda kwa kuvumilia.”

Yakobo anatoa mfano wa Mkulima anavyovumilia mpaka kupata mazao, hakuna kazi ngumu sana duniani kama kulima hasa kama ni kilimo kile cha kutumia mikono lakini ukifuatilia maisha ya wakulima utaweza kuona na kujifunza kuwa ni watu wenye imani na subira wanasubiri mpaka wakati wa Mavuno ufike, sisi nasi hatuna budi kuwa wavumilivu na waaminifu na kufanya majukumu yetu ambayo Mungu ametupa na kwa uvumilivu mkubwa tutafikia malengo na mafanikio na kuzidi kuwa hodari.

Yakobo 5:7 “Kwa hiyo ndugu, vumilieni, hata kuja kwake Bwana. Tazama, mkulima hungoja mazao ya nchi yaliyo ya thamani, huvumilia kwa ajili yake hata yatakapopata mvua ya kwanza na ya mwisho.”

Unaona kwa msingi huo kila kitu kinahitaji uvumilivu, malezi yanahitaji uvumilivu, uanafunzi unahitaji uvumilivu, ualimu unahitaji uvumilivu, uongozi unahitaji uvumilivu, na kila tukifanyacho kinahitaji uvumilivu, kwa msingi huo ili tuwezer kufanikiwa katika kila eneo la maisha yetu hatuna budi kuwa na uvumilivu, na tunapovumilia tutaendelea kuwa hodari zaidi na zaidi.

8.      Jenga mazingira ya kuhitajika.

Maandiko yanasema hivi katika kitabu cha Mithali 14:4 “Zizi ni safi ambapo hapana ng'ombe; Bali nguvu za ng'ombe zaleta faida nyingi.”

Maandiko yanatufundisha kuwa Ngombe wana faida kuwa sana japo wakiwepo zizizni inaweza kuonekana kuwa wanachafua, na wakiwa hawapo yaweza kuonekana kuwa zizi ni safi, lakini ni afadhali kuwa nao kwa sababu wana faida kubwa sana , wao hulima na kusababisha mazao, tutupa nyama, hutupa maziwa, hutupa ngozi na kadhalika, kimsingi tunajifunza umuhimu wa watu wenye bidii, Mungu anataka ufanye kazi kwa bidii na kuwa mwenye faida ili ikiwezekana watu wakuhitaji, watu maarufu katika Biblia waliitwa watu ambao ulimwengu haukustahili kuwa nao

Waebrania 11:32-38 “Nami niseme nini tena? Maana wakati usingenitosha kuleta habari za Gideoni na Baraka na Samsoni na Yeftha na Daudi na Samweli na za manabii;        ambao kwa imani walishinda milki za wafalme, walitenda haki, walipata ahadi, walifunga vinywa vya simba, walizima nguvu za moto, waliokoka na makali ya upanga. Walitiwa nguvu baada ya kuwa dhaifu, walikuwa hodari katika vita, walikimbiza majeshi ya wageni. Wanawake walipokea wafu wao waliofufuliwa. Lakini wengine waliumizwa vibaya hata kuuawa, wasikubali ukombozi, ili wapate ufufuo ulio bora; wengine walijaribiwa kwa dhihaka na mapigo, naam, kwa mafungo, na kwa kutiwa gerezani; walipigwa kwa mawe, walikatwa kwa misumeno, walijaribiwa, waliuawa kwa upanga; walizunguka-zunguka wakivaa ngozi za kondoo na ngozi za mbuzi; walikuwa wahitaji, wakiteswa, wakitendwa mabaya; (watu ambao ulimwengu haukustahili kuwa nao), walikuwa wakizunguka-zunguka katika nyika na katika milima na katika mapango na katika mashimo ya nchi.”      

Popote ulipo jitume kwa bidii ili watu waone umuhimu wako, uwe na ubunifu, na uwezo wa kujenga mpango utakaofanya wewe uhitajike na uonekane umuhimu wako katika jamiii ona

 Mwanzo 41:33-38 “Basi, Farao na ajitafutie mtu wa akili na hekima amweke juu ya nchi ya Misri. Farao na afanye hivi, tena akaweke wasimamizi juu ya nchi, na kutwaa sehemu ya tano katika nchi ya Misri, katika miaka hii saba ya kushiba. Na wakusanye chakula chote cha miaka hii myema ijayo, wakaweke akiba ya nafaka mkononi mwa Farao wakakilinde kuwa chakula katika miji. Na hicho chakula kitakuwa akiba ya nchi kwa ajili ya miaka hiyo saba ya njaa, itakayokuwa katika nchi ya Misri, nchi isiharibike kwa njaa. Neno hilo likawa jema machoni pa Farao, na machoni pa watumwa wake wote.  Farao akawaambia watumwa wake, Tupate wapi mtu kama huyu, mwenye roho ya Mungu ndani yake?”

9.      Usiogope 

Hofu ni mojawapo ya kifungo kikubwa sana, Mungu hafurahii watu wanaoogopa, mtu anayeogopa  na siyejaribu ni kizuizi kikubwa sana na ndio maana mara kwa mara utaweza kuona Mungu akiwataka watu wake wasiogope Yoshua 1:5-9 “Hapatakuwa mtu ye yote atakayeweza kusimama mbele yako siku zote za maisha yako; kama nilivyokuwa pamoja na Musa, ndivyo nitakavyokuwa pamoja na wewe; sitakupungukia wala sitakuacha. Uwe hodari na moyo wa ushujaa, maana ni wewe utakayewarithisha watu hawa nchi hii niliyowaapia baba zao ya kwamba nitawapa. Uwe hodari tu na ushujaa mwingi, uangalie kutenda sawasawa na sheria yote aliyokuamuru Musa mtumishi wangu; usiiache, kwenda mkono wa kuume, au wa kushoto, upate kufanikiwa sana kila uendako. Kitabu hiki cha torati kisiondoke kinywani mwako, bali yatafakari maneno yake mchana na usiku, upate kuangalia kutenda sawasawa na maneno yote yaliyoandikwa humo; maana ndipo utakapoifanikisha njia yako, kisha ndipo utakapositawi sana. Je! Si mimi niliyekuamuru? Uwe hodari na moyo wa ushujaa; usiogope wala usifadhaike; kwa kuwa Bwana, Mungu wako, yu pamoja nawe kila uendako.”  

Kwa nini Mungu alimsisitiza Yoshua asiogope kwa sababu woga uliwkosesha Israel Inchi ya kanaani kwa miaka mingi sana walikosa urithi wao, watu wengin wanaotaka mtu asijaribu au mtu asifanikiwe hujaribu kutumia hofu kama njia ya kukuwekea utisho ili uogope na usifanya majaribio, katika wapelelezi wale walioipepeleza ichi ya kanaani kumi kati yao walileta habari ya hofu na kuwatisha watu kiasi cha watu kuogopa na kujikosesha nchi ya maziwa na asali

Hesabu 14:1-9 “Mkutano wote wakapaza sauti zao wakalia; watu wakatoka machozi usiku ule. Kisha wana wa Israeli wote wakamnung'unikia Musa na Haruni; mkutano wote wakawaambia, Ingekuwa heri kama tungalikufa katika nchi ya Misri, au, ingekuwa heri kama tungalikufa katika jangwa hili. Mbona Bwana anatuleta mpaka nchi hii ili tuanguke kwa upanga? Wake zetu na watoto wetu watakuwa mateka; je! Si afadhali turudi Misri? Wakaambiana, Na tumweke mtu mmoja awe akida, tukarudi Misri. Ndipo Musa na Haruni wakaanguka kifudifudi mbele ya mkutano wa kusanyiko la wana wa Israeli. Na Yoshua mwana wa Nuni, na Kalebu mwana wa Yefune, waliokuwa miongoni mwao walioipeleleza nchi, wakararua nguo zao; wakanena na mkutano wote wa wana wa Israeli wakasema, Nchi ile tuliyopita kati yake ili kuipeleleza, ni nchi njema mno ya ajabu. Ikiwa Bwana anatufurahia, atatuingiza katika nchi hii atupe iwe yetu, nayo ni nchi yenye wingi wa maziwa na asali. Lakini msimwasi Bwana, wala msiwaogope wale wenyeji wa nchi, maana wao ni chakula kwetu; uvuli uliokuwa juu yao umeondolewa, naye Bwana yu pamoja nasi; msiwaogope.”

Unaona Wana wa Israel walishaogopa mno wakati wao wanaogopa kumbe wakanaani nao walikuwa wamewaogopa muda mrefu sana na hakuna ujasiri uliokuwa umesalia ndani yao, wakati mwingine tunajikosesha Baraka za Mungu kwetu kwa sababu ya hofu ona

Joshua 2:1-11 “Yoshua, mwana wa Nuni, akawatuma watu wawili kutoka Shitimu kwa siri, ili kupeleleza, akawaambia, Enendeni mkaitazame nchi hii, na Yeriko. Wakaenda wakafika nyumbani kwa kahaba mmoja jina lake aliitwa Rahabu, wakalala huko. Mfalme wa Yeriko akaambiwa, kusema, Tazama, watu wawili wa wana wa Israeli wameingia humu leo usiku, ili kuipeleleza nchi. Mfalme wa Yeriko akatuma watu kwa Rahabu, akasema, Watoe watu wale waliokuja kwako, walioingia ndani ya nyumba yako, maana wamekuja ili kuipeleleza nchi. Yule mwanamke akawatwaa wale watu wawili, akawaficha, akasema, Naam, wale watu walikuja kwangu, lakini sikujua walikotoka; ikawa kama wakati wa kufungwa lango la mji, kulipokuwa giza, watu wale wakatoka, wala sijui walikokwenda; wafuateni upesi, maana mtawapata. Lakini yeye alikuwa amewapandisha darini, akawaficha kwa mabua ya kitani, aliyokuwa ameyatandika juu ya dari. Basi hao watu wakawafuata kwa njia iendayo Yordani mpaka vivukoni; na mara wale watu waliowafuatia walipokwisha kutoka, wakalifunga lango.Tena kabla hawajalala akawaendea juu darini, akawaambia wale wanaume, Mimi najua ya kuwa Bwana amewapa ninyi nchi hii, na ya kuwa hofu imetuangukia mbele yenu, na ya kuwa wenyeji wote wa nchi wanayeyuka mbele yenu. Maana tumesikia jinsi Bwana alivyoyakausha maji ya bahari ya Shamu mbele yenu, hapo mlipotoka Misri, tena mambo hayo mliyowatendea wafalme wawili wa Waamori waliokuwa huko ng'ambo ya Yordani, yaani, Sihoni na Ogu, mliowaangamiza kabisa. Na mara tuliposikia hayo mioyo yetu iliyeyuka, wala haukusalia ujasiri wo wote katika mtu awaye yote, kwa sababu yenu; kwa kuwa Bwana, Mungu wenu, yeye ndiye Mungu, katika mbingu juu na katika nchi chini.”

Hebu jaribu kuwaza wakati Israel wakiwaogopa wanaowaogopa! Wakanaani walishashikwa na hofu tangu waliposikia matendo makuu ya Mungu lakini warithi wa ile Inchi nyaani waisrael wenyewe walikuwa wanaogopa na iliwachukua miaka 40 kuingia katika inchi ya kaanaani lakini tatioz kubwa likichangiwa na kutokuamini kwao! Kila mtu anayetaka kuwa hodari zaidi inampasa kujifunza kutokuogopa!

10.  Futa msamiati haiwezekani.

Watu wote waliofanikiwa katika maandiko ni wale waliokuwa hawana msamiati wa haiwezekani, msamiati huu sio msamiati wa kiungu hata siku moja Mungu hajawahi kuzungumza kokote kuwa kuna kitu kisichowezekana hususani kama utamshirikisha na yeye

Mathayo 19:26 “Yesu akawakazia macho, akawaambia, Kwa wanadamu hilo haliwezekani; bali kwa Mungu yote yawezekana.”

Mwanzo 18:9-14 “Wakamwambia, Yu wapi Sara mkeo? Akasema, Yumo hemani. Akamwambia, Hakika nitakurudia wakati huu huu mwakani, na tazama, Sara mkeo atapata mwana wa kiume. Sara akasikia mlangoni pa hema iliyokuwapo nyuma yake. Basi Ibrahimu na Sara walikuwa wazee, na umri wao mkubwa, na Sara alikuwa amekoma katika desturi ya wanawake. Kwa hiyo Sara akacheka moyoni mwake, akisema, Niwapo mkongwe, nitapata furaha, na bwana wangu mzee? BWANA akamwambia Ibrahimu, Mbona Sara amecheka akisema, Mimi kweli nitazaa mwana, nami ni mzee? Kuna neno gani lililo gumu la kumshinda BWANA? Kwa muhula wake nitakurudia, wakati huu huu mwakani, na Sara atapata mwana wa kiume.”

Yeremia 32:27 “Tazama, mimi ni Bwana, Mungu wa wote wenye mwili; je! Kuna neno gumu lo lote nisiloliweza?

Kwa msingi huo tunachopaswa sisi ni kujiungamanisha na Mungu ili tuweze kutenda mambo makubwa sana Zaburi 60:12 “Kwa msaada wa Mungu tutatenda makuu, Maana Yeye atawakanyaga watesi wetu.”

Zaburi 108:13 “Kwa msaada wa Mungu tutatenda makuu, Maana Yeye atawakanyaga watesi wetu.”

11.   Kumbuka kuukomboa wakati.

Kulitumikia kusudi lolote la Mungu hapa Duniani kumbuka limewekwa katika muda, kwa msingi huo Maandiko yanatutaka vilevile kuwa na hekima ya jinsi na namna ya kuukomboa wakati, kumbuka kuwa kila mwanadamu anayeishi ulimwenguni ana masaa 24 kwa siku, ana siku saba kwa wiki siku 30 kwa mwezi na Miezi 12 kwa mwaka sawa na siku 365, lakini moja ya tatizo kubwa tulilonalo wanadamu ni kutokuujua wakati na kutokujua namna ya kuzitumia nyakati

Luka 19:41-44 “
Alipofika karibu aliuona mji, akaulilia, akisema, Laiti ungalijua, hata wewe katika siku hii, yapasayo amani! Lakini sasa yamefichwa machoni pako. Kwa kuwa siku zitakuja, adui zako watakapokujengea boma, likuzunguke; watakuzingira na kukuhusuru pande zote; watakuangusha chini wewe na watoto wako ndani yako, wasikuachie jiwe juu ya jiwe, kwa sababu hukutambua majira ya kujiliwa kwako.”         

Yesu aliulilia mji wa Yerusalem ambao ulibomolewa vibaya mwaka wa 70 baada ya Kristo yaani kama miaka 27 baadaye na sababu kubwa ya kubomolewa kwao ni ka sababu hawakujua majira yaani Muda wa kutembelewa na Mungu walipuuza waklimkataa Yesu walimsulubisha na wakati ulifika walijuta lakini wakati huo muda ulikuwa umekwisha kwenda, kila mtu anayetaka kuwa mhodari katika maisha yake lazima ajue kuukomboa wakati, mtu anayeukomboa wakati katika maandiko anaitwa mtu mwenye hekima ona Waefeso 5:15-17 “
Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima; mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu. Kwa sababu hiyo msiwe wajinga, bali mfahamu ni nini yaliyo mapenzi ya Bwana.” Biblia ya kingereza na NIV inafananisha Muda na nafasi ya bahati OPPORTUNITY –  Kwa KIYUNANI Efkairia maana yake – a time or set of circumstances that makes it possible to do something, yaani ni muda au wakati ambapo unapata mazingira ya kuweza kufanya jambo, kwahiyo matumizi ya muda na matumizi ya nafasi za kipekee ambazo ulipaswa kuzitumia vema, kwa hiyo tiofauti yatu na watu wengine ni sio kwa sababu wao wana muda mwingi zaidi bali kwa sababu wao wana ujuzi wa kutumia nafasi

Muhubiri 3:1-8 “
Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu. Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa; Wakati wa kupanda, na wakati wa kung'oa yaliyopandwa; Wakati wa kuua, na wakati wa kupoza; Wakati wa kubomoa, na wakati wa kujenga; Wakati wa kulia, na wakati wa kucheka; Wakati wa kuomboleza, na wakati wa kucheza; Wakati wa kutupa mawe, na wakati wa kukusanya mawe; Wakati wa kukumbatia, na wakati wa kutokumbatia; Wakati wa kutafuta, na wakati wa kupoteza; Wakati wa kuweka, na wakati wa kutupa; Wakati wa kurarua, na wakati wa kushona; Wakati wa kunyamaza, na wakati wa kunena; Wakati wa kupenda, na wakati wa kuchukia; Wakati wa vita, na wakati wa amani.”

Kwa msingi huo kujua nyakati kunaweza kutusaidia kujua nini litupasalo kufanya wana wa Israel walifanikiwa sana hasa nyakati za utawala la Daudi kwa vile lilikuweko kabila la wana wa isakari ambao walikuwa na ujuzi wa nyakati na nini kiwapasacho watu kufanya kwa wakati huo ona

1Nyakati 12:32 “
Na wa wana wa Isakari, watu wenye akili za kujua nyakati, kuyajua yawapasayo Israeli wayatende; vichwa vyao walikuwa watu mia mbili na ndugu zao wote walikuwa chini ya amri yao.”

Kwa msingi huo kila mtu anayetaka mafanikio ni lazima aelewe na ajue namna na jinsi ya kuutmia wakati ni hekima kuutumia wakati vizuri! Na ujinga kupoteza muda na kutokujua namna na jinsi ya kuutumia wakati, Bwana na ampe neema kila mmoja wetu ajue jinsi anavyopaswa kuutumia wakati ili tusijute baadaye katika jina la Yesu amen.

12.  Fanya kazi kwa bidii.

Unapofuatilia maisha ya watu waliofanikiwa katika maandiko, utagundua pia kuwa watu hao walikuwa wachapa kazi, hawakuwa wavivu, wote tunafahamu kuwa kazi ya kwanza aliyopewa Adamu haikuwa kuabudu, Mungu alimuweka Mwanadamu katika bustani ya edeni ili afanye kazi ona Mwanzo 2:15 “BWANA Mungu akamtwaa huyo mtu, akamweka katika bustani ya Edeni, ailime na kuitunza.”, kulima na kutunza sio kazi nyepesi, kwa msingi huo utaweza kugundua kuwa Mungu alimtaka mwanadamu afanye kazi, hata maumbile ya kiulimwengu yanaonyesha mkazo wa kufanya kazi katika siku saba ambazo Mungu ametupa utaweza kuona ametoa siku sita za kufanya kazi na siku moja utamkumbuka bwana Mungu wako ona

Kutoka 35:1-2 “Musa akakutanisha mkutano wote wa wana wa Israeli, na kuwaambia, Maneno aliyoyausia BWANA ni haya, kwamba myafanye. Fanyeni kazi siku sita, lakini siku ya saba itakuwa siku takatifu kwenu; ni Sabato ya kustarehe kabisa kwa BWANA; mtu awaye yote atakayefanya kazi yo yote katika siku hiyo atauawa

kwa hiyo utaweza kuona ni kama kwa kiwango Fulani hivi neno la Mungu linatutaka tufanye kazi kanuni hii ya kufanya kazi imewafanya watu wa mataifa ya Asia kubarikiwa na kufanikiwa kwa haraka sana, nilipotembelea Marekani nilikuta jamii kubwa ya wakazi wa marekani katika jimbo la Viginia ni wakorea na wanapendwa sana na wamarekani kwa sababu ni wachapa kazi, hata nchi yao imeendelea sana kwa sababu wako aggressive ni wenye juhudi katika kufanya kazi Maandiko yako kinyume na uvivu na yanamtaka kila mmoja afanye kazi kwa bidii na mkazo huu umedhihirika hata kwa mkazo ulio wazi kuwa asiyefanya kazi kula na asile ona

2Wathesalonike 3:10-12 “Kwa kuwa hata wakati ule tulipokuwapo kwenu tuliwaagiza neno hili, kwamba ikiwa mtu hataki kufanya kazi, basi, asile chakula.Maana twasikia kwamba wako watu kwenu waendao bila utaratibu, hawana shughuli zao wenyewe, lakini wanajishughulisha na mambo ya wengine. Basi twawaagiza hao, na kuwaonya katika Bwana Yesu Kristo, watende kazi kwa utulivu na kula chakula chao wenyewe.

Unaona kwa msingi huo kutokufanya kazi ni dhambi, Mungu anataka watu wafanye kazi zao, kila mmoja awe na shughuli yake mwenyewe ya kufanya, na kuhakikisha kuwa anajituma, maandiko yanaionyesha kuwa kuna mafanikio makubwa kama watu watafanya kazi kwa bidii, iko wazi kuwa kila mtu anayefanya kazi kwa bidii na kwa kujitoa anafanikiwa, tunafahamu yako mapito na pia kuwa wakati mwingine haiku wazi kwa sababu wako watu wanafanya kazi kwa bidii nab ado hayaonekani mafanikio, nii ni sehemu ndogo ya matokeo ya kimaisha lakini Biblia inatuongoza kwamba bado ni agizo la Mungu kufanya kazi kwa bidii, tunapofanya kazi kwa bidii bila kujali imani zetu na kabila zetu na rangi zetu ni wazi kuwa Mungu anasimama karibu nasi, kwa hiyo fanya kazi hata kama hujui Mungu yuko kwenye hatua gani kukutokea

Mithali 12:24 “Mkono wa mwenye bidii utatawala; Bali mvivu atalipishwa kodi.” Neno la Mungu linatutaka tufanye kazi na kutunza familia zetu na jama zetu kama mtu anashindwa hata kuitunza familia yake maandiko yanasema ni mbaya kuliko asiye na imani ona

1Timotheo 5:8 “Lakini mtu ye yote asiyewatunza walio wake, yaani, wale wa nyumbani mwake hasa, ameikana Imani, tena ni mbaya kuliko mtu asiyeamini Paulo mtume pamoja na kuwa Muhubiri wa injili alihakikisha kuwa wakati mwingine anafanya kazi kwa bidii ili kujipatia mahitaji yake yeye alijua wazi kuwa ni heri kutoa kuliko kupokea

Matendo 20:33-35 “Sikutamani fedha wala dhahabu, wala mavazi ya mtu. Ninyi wenyewe mnajua ya kuwa mikono yangu hii imetumika kwa mahitaji yangu na ya wale waliokuwa pamoja nami. Katika mambo yote nimewaonyesha ya kuwa kwa kushika kazi hivi imewapasa kuwasaidia wanyonge, na kuyakumbuka maneno ya Bwana Yesu, jinsi alivyosema mwenyewe, Ni heri kutoa kuliko kupokea Lakini maandiko pia yanataka tujifunze kutoka kwa chungu au mchwa kwamba wanafanya kazi ka bidii na wanajiwekea akiba hata kwa wakati wa kiangazi au nukame ona

Mithali 6:6-11 “Ewe mvivu, mwendee chungu, Zitafakari njia zake ukapate hekima. Kwa maana yeye hana akida, Wala msimamizi, wala mkuu, Lakini hujiwekea akiba ya chakula wakati wa jua; Hukusanya chakula chake wakati wa mavuno. Ewe mvivu, utalala hata lini? Utaondoka lini katika usingizi wako? Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, Bado kukunja mikono upate usingizi! Hivyo umaskini wako huja kama mnyang'anyi, Na uhitaji wako kama mtu mwenye silahahatuna budi kuhakikisha kuwa kila tulifanyalo tunalifanya kwa bidii na tunashuhudia mafanikio makubwa sana katika utendaji wetu wa kazi na maisha yetu.

13.  Usiache kumtegemea Mungu

Maandiko yanaonyesha kudumu kwetu na kuendelea kusimama kwetu ni kwa kumtegemea Mungu na kumtumaini mtu anayemtegemea Mungu anafananishwa na mlima sayuni hatatikisika milele

Zaburi 152: 1-5 “Wamtumainio Bwana ni kama mlima Sayuni, Ambao hautatikisika, wakaa milele. Kama milima inavyouzunguka Yerusalemu, Ndivyo Bwana anavyowazunguka watu wake, Tangu sasa na hata milele. Kwa maana fimbo ya udhalimu Haitakaa juu ya fungu la wenye haki; Wenye haki wasije wakainyosha Mikono yao kwenye upotovu. Ee Bwana, uwatendee mema walio wema, Nao walio wanyofu wa moyo. Bali wao wanaozigeukia njia zao zilizopotoka, Bwana atawaondoa pamoja na watenda maovu. Amani ikae na Israeli.”

Mashujaa wote wa imani walioendelea kuwa hodari zaidi walimtegemea Mungu na kamwe hawakuwategemea wanadamu, mara unapo mfanya mwanadamu kuwa kinga yako na kumdaharau Bwana ukweli ni kuwa unajiweka katika laana na hautafanikiwa

Yeremia 17:5-7 “Bwana asema hivi, Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, Amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake Na moyoni mwake amemwacha Bwana. Maana atakuwa kama fukara nyikani, Hataona yatakapotokea mema; Bali atakaa jangwani palipo ukame, Katika nchi ya chumvi isiyokaliwa na watu. Amebarikiwa mtu yule anayemtegemea Bwana, Ambaye Bwana ni tumaini lake. Maana atakuwa kama mti uliopandwa kando ya maji, Uenezao mizizi yake karibu na mto; Hautaona hofu wakati wa hari ujapo

Kwa msingi huo pamoja na mambo mengine yote hatuna budi kuhakikisha kuwa tunamtegemea Mungu katika njia zetu zote na maandiko yanatuasa kwamba wala tusizitegemee akili zetu wenyewe

Mithali 3:5-6 “
Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote, Wala usizitegemee akili zako mwenyewe; Katika njia zako zote mkiri yeye, Naye atayanyosha mapito yako.”

Mambo yanapokuwa magumu neno la Mungu linatuagiza kuomba na kumtwika yeye fadhaa zetu zote ona

1Petro 5:6-7 “
Basi nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake; huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenuhakuna sababu ya kufadhaika

Wafilipi 4:6 “Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu

Ni imani yangu kuwa kanuni hizi zitamsaidia kila mtu anayetaka kuwa hodari zaidi katika Nyanja mbalimbali ukiyajua hayo heri wewe ukiyatenda

Yohana 13:17 “
Mkiyajua hayo, heri ninyi mkiyatenda

Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima!

Jumatatu, 31 Januari 2022

Haki huinua Taifa !


Mithali 14:34 “Haki huinua taifa; Bali dhambi ni aibu ya watu wo wote.”



Utangulizi:

Ni muhimu kufahamu kuwa maandiko yanatupa siri ya mafanikio makubwa sana katika maisha yetu ya kila siku na maisha ya kila mtu na maisha ya taifa lolote lile kwamba; Ili tuweze kuwa na ustawi tunapaswa kuwa watu wa haki, Mungu hawezi kumvumilia mtu au taifa lolote ikiwa watu wa taifa hilo wataacha na uadilifu na kumkataa Mungu, siri ya nguvu na mafanikio ya mtu watu jamii na taifa lolote iko katika kutenda uadilifu na kuyaishi mapenzi ya Mungu na wala sio nguvu za kijeshi na uchumi, siri ya mafanikio ya kweli iko kwenye uadilifu na kutenda haki, Taifa lolote likiandaa mipango na mikakati ya kiadilifu na ya kumcha Mungu na kumuheshimu na kukaa katika uadilifu kila kitu kitafanikiwa kwa mujibu wa maandiko Mithali 14:34 Haki huinua taifa; Bali dhambi ni aibu ya watu wo wote.” Tutajifunza somo hili Haki huinua taifa kwa kuzingatia vipengele vitatu vifuatavyo:- 

1.       Maana ya Taifa

2.       Jinsi haki inavyoinua taifa na Dhambi inavyoleta aibu

3.       Haki huinua taifa 

Maana ya Taifa

Ni muhimu kufahamu kuwa katika maandiko lugha inayotumika kumaanisha taifa inatumika katika maana pana sana unapoangalia maana ya Taifa kwa kiingereza yaani Nation maana yake katika Dictionary inasomeka hivi National means People who possess a common kinship, a social or political group and simply a people, kwa kiyunani ni Ethnos au Ethinic, ni jamii au watu wanaotokana na mtu, au kabila au dini au lugha na kadhalika, Kwa mfano watu wanaweza kuzaliwa na baba mmoja na mama mmoja au hata wakawa mapacha lakini katika jicho la kiungu hao wanaweza kuwa mataifa mawili tofauti na kabila mbili tofauti unaona!

Mwanzo 25:21-23 Isaka akamwomba BWANA kwa ajili ya mke wake, maana alikuwa tasa. Naye BWANA akamwitikia, na Rebeka mkewe akachukua mimba. Watoto wakashindana tumboni mwake. Naye akasema, Ikiwa ni hivi, kuishi kwanifaa nini? Akaenda kumwuliza BWANA. BWANA akamwambia, Mataifa mawili yamo tumboni mwako, Na kabila mbili za watu watafarakana tangu tumboni mwako. Kabila moja litakuwa hodari kuliko la pili, Na mkubwa atamtumikia mdogo.”      

Unaona na pia unaweza kuiona lugha ya aina hii ikitumiwa na Yesu katika Mathayo 24:6-7 “Nanyi mtasikia habari za vita na matetesi ya vita; angalieni, msitishwe; maana hayo hayana budi kutukia; lakini ule mwisho bado. Kwa maana taifa litaondoka kupigana na taifa, na ufalme kupigana na ufalme; kutakuwa na njaa, na matetemeko ya nchi mahali mahali.”  

Kwa msingi huo sasa Taifa linaweza kuwa ni jamii ya watu wanaotokana na mtu mmoja mmoja, taifa ni watu wa karibu sana wakati ufalme na ufalme inaweza kuwa ni mipaka ya kiserikali, kwa hiyo Mungu yu aweza kumuona au kumuita mtu mmoja na mtu huyo akamfanya kuwa taifa, yaani kama wewe ni mtenda haki na unampendeza Mungu wewe ni asili ya taifa Mungu yu aweza kukufanya wewe kuwa taifa kubwa ona

Mwanzo 12:1-3 “BWANA akamwambia Abramu, Toka wewe katika nchi yako, na jamaa zako, na nyumba ya baba yako, uende mpaka nchi nitakayokuonyesha; nami nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, na kukubariki, na kulikuza jina lako; nawe uwe baraka; nami nitawabariki wakubarikio, naye akulaaniye nitamlaani; na katika wewe jamaa zote za dunia watabarikiwa.”

Kwa msingi huo tunapozungumzia taifa tunamzungumzia mtu mmoja mmoja, na jamii au kabila au kundi la watu wa aina filani walio karibu sana hilo ndio taifa, na ufalme ni jamii ya watu wanaopakana kiserikali, kwa hiyo kila mmoja anapaswa kuwa mtenda haki na kuishi maisha ya kumcha Mungu kwa sababu Mungu hashindwi kukufanya wewe kuwa taifa kwa sababu taifa linaanzia na mtu mmoja kama Mungu akipendezwa nawe anaweza kukufanya kuwa taifa na kama Mungu akichukizwa nawe anaweza kukufuta ona

Kutoka 32:7-14BWANA akamwambia Musa, Haya! Shuka; kwa maana watu wako uliowatoa katika nchi ya Misri wamejiharibu nafsi zao, wamepotoka upesi kuiacha ile njia niliyowaamuru, wamejifanyizia ndama ya kuyeyusha wakaiabudu na kuitolea dhabihu, wakasema, Hiyo ndiyo miungu yako, Ee Israeli, iliyokutoa katika nchi ya Misri. Tena BWANA akamwambia Musa, Mimi nimewaona watu hawa, na tazama, ni watu wenye shingo ngumu basi sasa niache, ili hasira zangu ziwake juu yao, niwaangamize, nami nitakufanya wewe uwe taifa kuu. Musa akamsihi sana BWANA, Mungu wake, na kusema, BWANA, kwa nini hasira zako kuwaka juu ya watu wako uliowaleta kutoka nchi ya Misri kwa uweza mkuu, na kwa mkono wenye nguvu? Kwa nini Wamisri kunena, wakisema, Amewatoa kwa kuwatenda uovu, ili apate kuwaua milimani, na kuwaondoa watoke juu ya uso wa nchi? Geuka katika hasira yako kali, ughairi uovu huu ulio nao juu ya watu wako. Mkumbuke Ibrahimu, na Isaka, na Israeli, watumishi wako, ambao uliwaapia kwa nafsi yako, na kuwaambia, Nitazidisha kizazi chenu mfano wa nyota za mbinguni; tena nchi hii yote niliyoinena nitakipa kizazi chenu nao watairithi milele. Na BWANA akaughairi ule uovu aliosema ya kwamba atawatenda watu wakeunaweza kuona kwa msingi huo sasa swala la kutenda haki au kwa lugha nyingine nyepesi kutembea katika mapenzi ya Mungu halianzi na mtu Fulani tu linaanza na wewe na mimi

Jinsi haki inavyoinua taifa na Dhambi inavyoleta aibu

Maandiko sasa yanatuonyesha kupitia wana wa Israel na maisha yao kwamba pale watu walipotenda haki na walipotembea katika njia za Mungu, Mungu aliwafanya kuwa imara na pale watu walipoziacha njia za Mungu, na kuyaacha mapenzi yake  Mungu aliwaacha waanguke katika mikono ya adui zao na kunyanyaswa vibaya  ona kwa mfano

Waamuzi 2:11-23 Wana wa Israeli walifanya yaliyokuwa ni maovu mbele za macho ya Bwana, nao wakawatumikia Mabaali.Wakamwacha Bwana, Mungu wa baba zao, aliyewaleta kutoka katika nchi ya Misri, wakafuata miungu mingine, baadhi ya miungu ya watu wale waliokaa karibu nao pande zote, wakajiinamisha mbele yao; wakamkasirisha Bwana, akaghadhibika. Wakamwacha Bwana, wakamtumikia Baali na Maashtorethi. Hasira ya Bwana ikawaka juu ya Israeli, naye akawatia katika mikono ya watu waliowateka nyara, akawauza na kuwatia katika mikono ya adui zao pande zote; hata wasiweze tena kusimama mbele ya adui zao. Kila walikokwenda mkono wa Bwana ulikuwa juu yao kuwatenda mabaya, kama Bwana alivyosema, na kama Bwana alivyowaapia; nao wakafadhaika sana. Kisha Bwana akawainua waamuzi, waliowaokoa na mikono ya watu hao waliowateka nyara. Lakini hawakuwasikiliza hao waamuzi wao, maana walifanya uasherati kwa kuifuata miungu mingine, wakajiinamisha mbele yao; wakageuka upesi, na kuiacha njia ile waliyoiendea baba zao, waliozitii amri za Bwana bali wao hawakufanya hivyo. Na wakati Bwana alipowainulia waamuzi, ndipo Bwana alikuwa pamoja na mwamuzi huyo, akawaokoa na mikono ya adui zao siku zote za mwamuzi huyo; maana Bwana alighairi kwa ajili ya kuugua kwao kwa sababu ya watu wale waliowaonea na kuwasumbua. Lakini ikawa, wakati alipokufa mwamuzi huyo, wakarudi nyuma wakafanya maovu kuliko baba zao, kwa kuifuata miungu mingine ili kuitumikia, na kuinama mbele yao; hawakuacha matendo yao, wala njia zao za ukaidi. Basi hasira ya Bwana ikawaka juu ya Israeli, naye akasema, Kwa kuwa taifa hili wamelihalifu agano langu nililowaamuru baba zao, wala hawakuisikiliza sauti yangu; mimi nami tokea sasa sitalifukuza taifa mojawapo la hayo aliyoyaacha Yoshua alipokufa; ili kwa njia ya hayo nipate kuwajaribu Israeli, kwamba wataishika njia ya Bwana kwenda katika njia hiyo, au sivyo. Basi Bwana akawaacha mataifa yale, wala hakuwafukuza kwa upesi, wala hakuwatia katika mikono ya Yoshua.”

Unaweza kuona kwamba pale watu wa Mungu walipoziacha njia za Mungu na kuishi kwa dhuluma na  wakajifanyia kila wanachokiona kuwa chema katika macho yao  Mungu aliwadhibu vikali sana na kuwaacha katika mikono ya adui zao ili washughulikiwe na wakati mwingine aliruhusu wachukuliwe mateka na kwenda utumwani  na sio hivyo tu akliwaacha wadhalilike na kufedheheka nah ii ndio aibu kubwa iliyokuwa inawapata pale wanapoacha njia za Mungu ambayo ndio haki ya Mungu.

2Wafalme 17:6-12 “Katika mwaka wa kenda wa Hoshea, huyo mfalme wa Ashuru akautwaa Samaria, akawahamisha Israeli mpaka Ashuru, akawaweka katika Hala na Habori, karibu na mto wa Gozani, na katika miji ya Wamedi. Yalitukia hayo kwa sababu wana wa Israeli walikuwa wametenda dhambi juu ya Bwana, Mungu wao, aliyewaleta kutoka katika nchi ya Misri watoke chini ya mkono wa Farao mfalme wa Misri, wakawaacha miungu mingine. Wakaziendea sheria za mataifa, ambao Bwana aliwafukuza mbele ya wana wa Israeli, na sheria za wafalme wa Israeli walizozifanya. Tena, wana wa Israeli wakafanya kwa siri mambo yasiyokuwa mema juu ya Bwana, Mungu wao, wakajijengea mahali pa juu katika miji yao yote, kutoka mnara wa walinzi hata katika miji yenye boma. Wakajisimamishia nguzo na maashera juu ya kila mlima mrefu, na chini ya kila mti wenye majani mabichi; wakafukiza uvumba huko katika kila mahali pa juu, kama mataifa walivyofanya, ambao Bwana aliwafukuza mbele yao; wakaunda mambo mabaya, ili wamkasirishe Bwana; wakatumikia sanamu, ambazo Bwana aliwakataza, akasema, Msitende jambo hili.”

Pale Israel walipotubu na kucha dhambi zao na kutembea katika mapenzi ya Mungu Mungu aliwasaidia aliwapa Mwokozi, alileta ukombozi na kuwapa amani na kuondoa masumbufu yote

 Waamuzi 3:9-11 “Kisha wana wa Israeli walipomlingana Bwana, Bwana akawainulia wana wa Israeli mwokozi, aliyewaokoa, yaani, Othnieli mwana wa Kenazi, ndugu mdogo wa Kalebu. Roho ya Bwana ikamjilia juu yake, naye akawa mwamuzi wa Israeli; akatoka kwenenda vitani, naye Bwana akamtia huyo Kushan-rishathaimu, mfalme wa Mesopotamia, mkononi mwake; na mkono wake ukamshinda Kushan-rishathaimu. Nayo nchi ikawa na amani muda wa miaka arobaini. Kisha Othnieli, mwana wa Kenazi, akafa.” Unaweza kuona hii ndio kanuni ya Mungu, Mungu hawezi kukuinua na kukutumia katika hali ya uovu, hatunabudi kutubu, kujinyenyekesha mbele za Mungu na kumlingana Mungu yaani kutembea katika njia zake tukifanya hivyo hatutaingia katika aibu na fedhea ya aina yoyote ile na Mungu atakuwa pamoja nasi na tutakuwa na uhakika wa ulinzi wa kudumu wala Bwana hatatuuza tuumizwe na adui zetu

Haki huinua taifa

Mithali 14:15-34 “Mjinga huamini kila neno; Bali mwenye busara huangalia sana aendavyo. Mwenye hekima huogopa, akajitenga na uovu; Bali mpumbavu ana ufidhuli, na kujitumai. Yeye aonaye hasira upesi atatenda kwa ujinga; Na mtu mwenye hila mbaya huzirwa. Wajinga hurithi upumbavu; Bali wenye busara huvikwa taji ya maarifa. Wabaya huinama mbele ya wema, Na wasio haki malangoni mwao wenye haki. Maskini huchukiwa hata na jirani yake; Bali tajiri ana rafiki wengi. Amdharauye mwenzake afanya dhambi; Bali amhurumiaye maskini ana heri. Je! Hawakosi wawazao mabaya? Bali fadhili na kweli zina wao wawazao mema. Katika kila kazi mna faida; Bali maneno ya midomo huleta hasara tu. Taji ya wenye hekima ni mali zao; Bali upumbavu wa wajinga ni upumbavu tu. Shahidi wa kweli huponya nafsi za watu; Bali atoaye uongo hudanganya. Kumcha Bwana ni tumaini imara; Watoto wake watakuwa na kimbilio. Kumcha Bwana ni chemchemi ya uzima, Ili kuepukana na tanzi za mauti. Utukufu wa mfalme ni wingi wa watu wake; Bali uchache wa watu ni uharibifu wa mkuu wao. Asiye mwepesi wa hasira ana fahamu nyingi; Bali mwenye roho ya hamaki hutukuza upumbavu. Moyo ulio mzima ni uhai wa mwili; Bali husuda ni ubovu wa mifupa. Amwoneaye maskini humsuta Muumba wake; Bali yeye awahurumiaye wahitaji humheshimu. Mtu mbaya husukumwa chini katika kutenda mabaya kwake; Bali mwenye haki ana matumaini katika kufa kwake. Hekima hukaa katika moyo wake mwenye ufahamu; Bali yaliyo ndani ya wapumbavu hudhihirika. Haki huinua taifa; Bali dhambi ni aibu ya watu wo wote.”

Suleimani katika kitabu cha Mithali anaonyesha wazi namna mtu mwenye haki anavyoweza kufanikiwa na namna watu waovu wanavyoweza kujikuta katika mashaka kinachosisitizwa katika maandiko hapa ni kwamba wale wanaomkataa Mungu na kuacha kutenda haki na kuendelea na uovu wanafanya ujinga ambao utawaharibia maisha na wale wanaomkubali Mungu na njia zake wanajipatia hekima na maarifa  na kujitengenezea ulinzi wa uhakika , kwa msingi huo neno la Mungu linapozungumza kuhusu taifa linatuzungumzia wewe na mimi na baadaye jamii yetu na jamii ya dunia kwa ujumla lakini kanuni hii inaanza kufanya kazi kwa mtu mmoja mmoja

Mithali 3:5 -8 “Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote, Wala usizitegemee akili zako mwenyewe; Katika njia zako zote mkiri yeye, Naye atayanyosha mapito yako. Usiwe mwenye hekima machoni pako; Mche Bwana, ukajiepushe na uovu. Itakuwa afya mwilini pako, Na mafuta mifupani mwako.” Ukiyajua hayo Heri wewe ukiyatenda!

Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima

Jumatatu, 24 Januari 2022

Ni nani atakayewashitaki wateule


Warumi 8:31-33 “Basi, tuseme nini juu ya hayo? Mungu akiwapo upande wetu, ni nani aliye juu yetu? Yeye asiyemwachilia Mwana wake mwenyewe, bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote, atakosaje kutukirimia na mambo yote pamoja naye? Ni nani atakayewashitaki wateule wa Mungu? Mungu ndiye mwenye kuwahesabia haki.  Ni nani atakayewahukumia adhabu? Kristo Yesu ndiye aliyekufa; naam, na zaidi ya hayo, amefufuka katika wafu, naye yuko mkono wa kuume wa Mungu; tena ndiye anayetuombea. Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Je! Ni dhiki au shida, au adha, au njaa, au uchi, au hatari, au upanga?  Kama ilivyoandikwa, ya kwamba, Kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa, Tumehesabiwa kuwa kama kondoo wa kuchinjwa. Lakini katika mambo hayo yote tunashinda, na zaidi ya kushinda, kwa yeye aliyetupenda. Kwa maana nimekwisha kujua hakika ya kwamba, wala mauti, wala uzima, wala malaika, wala wenye mamlaka, wala yaliyopo, wala yatakayokuwapo, wala wenye uwezo, wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, wala kiumbe kinginecho chote hakitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu Bwana wetu.”



Utangulizi:

Ni muhimu kufahamu kuwa moja ya kazi muhimu anayoifanya shetani katika maisha yetu ya kila siku, ukiacha kututia majaribuni pia anafanya kazi ya kutushitaki mara tunapoangukia katika majaribu, yeye anaitwa Mshitaki wetu  na kazi hii huifanya usiku na mchana ona katika

Ufunuo 12:10 “Nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema, Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana ametupwa chini mshitaki wa ndugu zetu, yeye awashitakiye mbele za Mungu wetu, mchana na usiku.”  Unaona Mwandishi wa kitabu cha ufunuo anaonyesha kushindwa kwa Mshitaki huyu katika ulimwengu wa roho, lakini ni wazi maandiko yanatukumbusha kuwa shetani nimshitaji wetu  kwa kiingereza  The Accuser” kwa hiyo waweza kuona wazi kuwa ibilisi ni mshitaki wetu, Petro anawaonywa Wakristo kuwa makini usiku na mchana ni kama anasema wasilale wawe waangalifu kwa sababu huyu mshitaki yuko kazini akituwinda kama Simba ona 1Petro 5:8 “Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze.” Tutajifunza somo hili kwa kuzingatia vipengele vitatu vifuatavyo:-

·         Maana ya neno Mshitaki wetu:-

·         Ni nani atakaye washitaki wateule:-

·         Madhara ya kuwashitaji wateule:-

Maana ya neno mshitaki.

Ni muhimu kufahamu kuwa Paulo Mtume anaonyesha kwanza uwazi kuhusu ukarimu mkuu wa Mungu kwa wateule wake  na jinsi anavyotuhesabia haki na namna alivyotupenda ona

Warumi 3:23-26 “kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu; wanahesabiwa haki bure kwa neema yake, kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu; ambaye Mungu amekwisha kumweka awe upatanisho kwa njia ya imani katika damu yake,ili aonyeshe haki yake ,kwa sababu ya kuziachilia katika ustahimili wa MUNGU dhambi zote zilzotangulia kufanywa. apate kuonyesha haki yake wakati huu, ili awe mwenye haki na mwenye kumhesabu haki yeye amwaminiye Yesu.”

Na pia unaweza kuona katika Yohana 3:16-18 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. Maana Mungu hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye. Amwaminiye yeye hahukumiwi; asiyeamini amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu.”       

Upendo wa Mungu kwa wateule ni mkuu sana kiasi ambacho hakutuachilia mwanaye wa pekee asiyekuwa na dhambi kwaajili yetu na kwa sababu hiyo Mungu hashindwi, kutukarimia na mambo mengine lakini Paulo mtume anakwenda ndani zaidi katika lugha ya kimahakama kwamba licha ya rehema na upendo wa Mungu wa kutukomboa lakini vilevile sio rahisi mtu kufanikiwa kuwashitaki watele wa Mungu hii ni ile hali ya mtu kusimama mahakamani na kuendesha mashitaka ya kutaka wewe usikubaliwe na Mungu, Maneno yanayotumika hapo katika lugha ya Kiyunani ni Kategoros kwa kiingereza Prosecutor  -  A person who institutes legal proceedings against someone ! or a Person who claims that someone has committed an Offence or done something wrong , ni mtu anayeendesha mashitaka kwaajili ya mtuhumiwa ili ahukumiwe  na kuonekana na hatia , Nyakati za agano la kale  wayahudi waliamini hivyo ya kuwa shetani hufanya kazi ya kuwashitaki watu wa Mungu ili waonekane kuwa na hatia ona kwa mfano

Ayubu 1:6-11 “Ilikuwa, siku moja ambayo hao wana wa Mungu walikwenda kujihudhurisha mbele za Bwana, Shetani naye akaenda kati yao. Bwana akamwuliza Shetani, Umetoka wapi wewe? Ndipo Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Natoka katika kuzunguka-zunguka duniani, na katika kutembea huku na huku humo. Kisha Bwana akamwuliza Shetani, Je! Umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Kwa kuwa hapana mmoja aliye kama yeye duniani, mtu mkamilifu na mwelekevu, mwenye kumcha Mungu na kuepukana na uovu. Ndipo Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Je! Huyo Ayubu yuamcha Bwana bure? Wewe hukumzingira kwa ukigo pande zote, pamoja na nyumba yake, na vitu vyote alivyo navyo? Kazi za mikono yake umezibarikia, nayo mali yake imeongezeka katika nchi Lakini nyosha mkono wako sasa, uyaguse hayo yote aliyo nayo, naye atakukufuru mbele za uso wako.

Unaweza kuona pia katika tukio linguine mfano Zakaria 3:1-7 “Kisha akanionyesha Yoshua, kuhani mkuu, amesimama mbele ya malaika wa Bwana, na Shetani amesimama mkono wake wa kuume ili kushindana naye. Bwana akamwambia Shetani, Bwana na akukemee Ewe Shetani; naam, Bwana, aliyechagua Yerusalemu, na akukemee; je! Hiki si kinga kilichotolewa motoni? Basi, Yoshua alikuwa amevaa nguo chafu sana, naye alikuwa akisimama mbele ya malaika. Naye huyo akajibu, akawaambia wale waliosimama mbele yake, akisema, Mvueni nguo hizi zenye uchafu. Kisha akamwambia yeye, Tazama, nimekuondolea uovu wako, nami nitakuvika mavazi ya thamani nyingi. Nikasema, Na wampige kilemba kizuri kichwani pake. Basi, wakampiga kilemba kizuri kichwani pake, wakamvika mavazi; naye malaika wa Bwana akasimama karibu. Kisha malaika wa Bwana akamshuhudia Yoshua, akisema, Bwana wa majeshi asema hivi, Kama ukienda katika njia zangu, na kama ukishika maagizo yangu, ndipo utakapoihukumu nyumba yangu, nawe utazilinda nyua zangu, nami nitakupa nafasi ya kunikaribia kati yao wasimamao karibu.”

Kwa msingi huo wanadamu wengi wanakuwa na hofu, na kutembea kwa kutokujiamini kwa sababu wanajua kuwa wana hatia na kuwa shetani akiwashitani katika kesi ni kuwa hawatatoboa, sio hivyo tu lakini hata pale itakapotokea huna hatia kama Ayubu bado shetani atahakikisha kuwa anakuchongea kwa Mungu ili upate shida ni kwaajili ya haya Paulo mtume anauliza kwa hoja zenye nguvu kubwa sana kuwa ni nani atakayewashitaki wateule ?  nan i nani atawahukumia adhabu? Yesu yuko mkono wa Kuume wa Mungu na kwa bei ya mauti yake ametukomboa na anatutetea kwa baba yake ili wewe na mi mi tuokolewe!

Ni nani atakaye washitaki wateule:-

Kama jinsi tulivyoweza kuona maana ya Mshitaki, vilevile kugundua kuwa ni shetani lakini vilevile shetani hutumia sana mioyo yetu kutuhukumu, kule kujua kuwa tumetenda dhambi kunatuuma sana moyoni na wakati mwingine tunaweza kumfikiri Mungu vibaya kwa kudhani kuwa hataweza kutukubali na kutuhesabia haki, kutokana na namna na jinsi tulivyomkosea, sio hivyo tu wakati mwingine pia tunaweza kusikia mashitaka kutoka kwa wanadamu wenzetu wakituhukumu kutokana na kosa hili au lile

Yohana 8:2-7 “Hata asubuhi kulipokucha akaingia tena hekaluni, na watu wote wakamwendea; naye akaketi, akawa akiwafundisha. Waandishi na Mafarisayo wakamletea mwanamke aliyefumaniwa katika uzinzi, wakamweka katikati. Wakamwambia, Mwalimu, mwanamke huyu amefumaniwa alipokuwa akizini. Basi katika torati, Musa alituamuru kuwapiga kwa mawe wanawake namna hii; nawe wasemaje?  Nao wakasema neno hilo wakimjaribu, ili wapate sababu ya kumshitaki. Lakini Yesu akainama, akaandika kwa kidole chake katika nchi. Nao walipozidi kumhoji, alijiinua, akawaambia, Yeye asiye na dhambi miongoni mwenu na awe wa kwanza wa kumtupia jiwe

Kwa hiyo shetani anaweza kutushitaki, mioyo yetu inaweza kutushitaki lakini hata watu wengine wanaweza kutushitaki na kisha kutuhukumu, Paulo sasa ana jenga hoja kwa kuwa Mungu ametupenda upeo akatuokoa na kutusamehe dhambi zetu ni nani atakaye washitaki wateule ?  Paulo anajenga hoja hii kwa vile anakumbuka kuwa mtu akimuamini Yesu hakuna hukumu iwayo yote inaweza kuwa na nguvu juu yake, kwa kufa kwa yesu pale msalabani hati za mashitaka na hukumu zimeharibiwa hivyio hakuna copy of judgement Wakolosai 2:13-15 “Na ninyi mlipokuwa mmekufa kwa sababu ya makosa yenu na kutokutahiriwa kwa mwili wenu, aliwafanya hai pamoja naye, akiisha kutusamehe makosa yote; akiisha kuifuta ile hati iliyoandikwa ya kutushitaki kwa hukumu zake, iliyokuwa na uadui kwetu; akaiondoa isiwepo tena, akaigongomea msalabani; akiisha kuzivua enzi na mamlaka, na kuzifanya kuwa mkogo kwa ujasiri, akizishangilia katika msalaba huo.”

Mtu akimuamini Yesu Kristo dhambi zake zinasamehewa ya kale yanapita na tazama kila kitu kina kuwa kipya

2Wakoritho 5: 17 “Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya.”

Hii maana yake ni kuwa kila aina ya mashitaka kwa mtu wa Mungu au kwa watu wa Mungu lazima yataanguka na kusambara tika na hayatafanikiwa ni Mungu ndiye anayetuhesabia haki, Mungu muumba wa ulimwengu, ni yeye anayemtangaza mtu kuwa na haki, kwa malipo ya ukombozi unaotokana na kazi ya Yesu Pale msalabani, ambaye amekwishalipa gharama ya dhambi zetu, ni yeye aliyeteswa badala yetu ni yeye aliyekufa naye yuko mkono wa kuume wa Nguvu mbinguni hivyo kikla anayemuamini anahesabiwa haki, kwa hiyo hatusimami kwa sababu ya shetani, au mioyo yetu au watu, twasimama kwa sababu Mungu yuko pamoja nasi na anatutetea kupitia kazi ya Bwana Yesu Pale Msalabani.

Madhara ya kuwashitaji wateule:-

Watu wa Mungu hawashitakiwi, unapojaribu kuwashitaki watu wa Mungu ni wewe ndiye utakayeumbuka, ukimhukumu mtu wa Mungu wewe ndiye utakayekuja kuonekana una hukumu na hatia maandiko yanaonya vikali sana swala zima la kuhukumiana  na yana ahadi ya kuwa hakuna mtu atakayekuhukumu akafanikiwa :-

·         Isaya 54:17 “Kila silaha itakayofanyika juu yako haitafanikiwa na kila ulimi utakaoinuka juu yako katika hukumu utauhukumu kuwa mkosa. Huu ndio urithi wa watumishi wa Bwana, na haki yao inayotoka kwangu mimi, asema Bwana.”

·         Mtu wa Mungu hata kama unamuna anaharibu sio jukumu lako kuhukumu  ni hatari sana kumuhukumu mtu wa Mungu kwa Mungu mwenyewe biblia inaonya vikali ona Warumi 14:4 “Wewe u nani unayemhukumu mtumishi wa mwingine? Kwa bwana wake mwenyewe yeye husimama au huanguka. Naam, atasimamishwa, kwa kuwa Bwana aweza kumsimamisha.”

·         Kushitaki na kumuhukumu mtu mwingine ni kujifanya wewe ni Mungu ni kuchukua nafasi ya Mungu ni kujikweza kuliko kukubwa sana ni kujifanya ya kuwa wewe ndiwe mwenye hatima ya maisha ya mtu mwingine Yakobo 4:12 “Mtoa sheria na mwenye kuhukumu ni mmoja tu, ndiye awezaye kuokoa na kuangamiza. U nani wewe umhukumuye mtu mwingine? Maandiko ni kama yanaonya vikali sana swala zima la kuhukumu watu wengine na kuna madhara makubwa sana kwa kuwa wewe sio Mungu

·         Kuhukumu wengine kutakufanya ukataliwe  au uonekane sio kitu Warumi 11:1-3 “Basi, nauliza, Je! Mungu aliwasukumia mbali watu wake? Hasha! Kwa kuwa mimi nami ni Mwisraeli, mmoja wa wazao wa Ibrahimu, mtu wa kabila ya Benyamini. Mungu hakuwasukumia mbali watu wake aliowajua tokea awali. Au hamjui yale yaliyonenwa na maandiko juu ya Eliya? Jinsi anavyowashitaki Waisraeli mbele za Mungu, Bwana, wamewaua manabii wako, wamezibomoa madhabahu zako, nami nimesalia peke yangu, nao wananitafuta roho yangu. Lakini ile jawabu ya Mungu yamwambiaje? Nimejisazia watu elfu saba wasiopiga goti mbele ya Baali.”

Ndugu yangu Mungu ni mkubwa kuliko mioyo yetu, hakuna sababu ya kutembea kwa huzuni iwapo moyo wako unamtegemea Yesu, makosa ya kibinadamu yanaweza kuweko lakini tukimuomba Mungu msamaha kwa neema yake ataturehemu, na zaidi sana Mungu ni muhimu kuendelea na Yesu, kumshika na kumuamini dhambi kubwa sana kuliko yote ni kukataa neema ya Mungu kwa kumkana Yesu Kristo Mathayo 10:32-33 “Basi, kila mtu atakayenikiri mbele ya watu, nami nitamkiri mbele za Baba yangu aliye mbinguni. Bali mtu ye yote atakayenikana mbele ya watu, nami nitamkana mbele za Baba yangu aliye mbinguni.”

Na Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima

Rev. Innocent Kamote.

Jumatatu, 20 Desemba 2021

Nayahesabu mambo yote kuwa hasara kwaajili ya Kristo!


Wafilipi 3:4-11 “Walakini mimi ningeweza kuutumainia mwili. Mtu ye yote akijiona kuwa anayo sababu ya kuutumainia mwili, mimi zaidi. Nalitahiriwa siku ya nane, ni mtu wa taifa la Israeli, wa kabila ya Benyamini, Mwebrania wa Waebrania, kwa habari ya kuishika torati, ni Farisayo, kwa habari ya juhudi, mwenye kuliudhi Kanisa, kwa habari ya haki ipatikanayo kwa sheria sikuwa na hatia. Lakini mambo yale yaliyokuwa faida kwangu, naliyahesabu kuwa hasara kwa ajili ya Kristo. Naam, zaidi ya hayo, nayahesabu mambo yote kuwa hasara kwa ajili ya uzuri usio na kiasi wa kumjua Kristo Yesu, Bwana wangu; ambaye kwa ajili yake nimepata hasara ya mambo yote nikiyahesabu kuwa kama mavi ili nipate Kristo; tena nionekane katika yeye, nisiwe na haki yangu mwenyewe ipatikanayo kwa sheria, bali ile ipatikanayo kwa imani iliyo katika Kristo, haki ile itokayo kwa Mungu, kwa imani; ili nimjue yeye, na uweza wa kufufuka kwake, na ushirika wa mateso yake, nikifananishwa na kufa kwake; ili nipate kwa njia yo yote kuifikia kiyama ya wafu



Utangulizi:

Kwa watu au kampuni zinazofanya biashara neno hasara na faida ni maneno ya karibu sana katika misamiati ya kila siku ya maisha ya biashara, Kila wakati wanajua mwenendo wa biashara zao endapo wanapata faida au wanapata hasara, kusimama au kuendelea kwa Biashara yoyote ile kunategemeana na faida inayopatikana au hasara inayopatikana, kuendelea kwa biashara Fulani kunategemeana sana na jinsi biashara hiyo inavyoingiza faida, Marabi wa kiyahudi wengi walikuwa wanafahamu swala hili  la kibiashara nao wakalitumia katika kuainisha jambo lililo na umuhimu na lisilo na umuhimu  mfano utaweza kuona Mathayo 16:26 “Kwani atafaidiwa nini mtu akiupata ulimwengu wote, na kupata hasara ya nafsi yake? Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake?”

Katika somo letu la msingi Paulo mtume anatumia mtindo huo huo kuonyesha maswala ya msingi kwake na maswala yasiyo ya msingi, Wafilipi 3:7-8 “Lakini mambo yale yaliyokuwa faida kwangu, naliyahesabu kuwa hasara kwa ajili ya Kristo. Naam, zaidi ya hayo, nayahesabu mambo yote kuwa hasara kwa ajili ya uzuri usio na kiasi wa kumjua Kristo Yesu, Bwana wangu; ambaye kwa ajili yake nimepata hasara ya mambo yote nikiyahesabu kuwa kama mavi ili nipate Kristo;Unapofanya uchunguzi wa kimaandiko utaweza kuona kuwa hasara na faida inayozungumziwa hapa ni mambo ambayo ni ya msingi na mambo ambayo sio ya msingi, na hii inatusaidia sisi nasi leo kujihoji na kutafakari kuwa ni mambo gani tunayapa kipaumbele kama mambo ya msingi na mambo yapi hatuyapi kipaumbele yaani mambo yasiyo ya msingi katika maisha!. Kwaajili ya hayo hapo tutaweza kugundua mambo yaliyo na faida kwetu na mambo yasiyo na faida kwetu, Paulo mtume aliyahesabu mambo yote yasiyo na faida kama hasara na kuyahesabu kuwa kama mavi kutokana na faida ya kumpata Yesu. Ni mambo gani hayo ya msingi ambayo aliyazingatia kisha baadaye akayaacha na kuona ni afadhali kupata hasara iwa mambo ambayo mwanzoni alifikikuwa yana faida kwake:-

1.       Dini za wazazi wetu.

 

Kama kuna jambo litawapa hasara kubwa sana watu wengi ni pamoja na kung’ang’ania dini za wazazi wao, hizi ni zile imani ambazo tumezirithi kutoka kwa wazazi wetu, imani hizi zitatuleta katika hasara kubwa badala ya faida, Paulo Mtume alikuwa akipambana vikali na watu waliokuwa wakihubiri dini ya kiyahudi na kufikiri kuwa ni dini bora zaidi kuliko kumpata Yesu, ni ukweli ulio wazi na dhahiri kuwa hakuna urithi wa kiroho, hali ya kiroho ya kila mtu inategemeana na yeye anavyokutana na Mungu kwa binafsi na sio kwa sababu ya wazazi, wake nyakati za namna hiyo kwa sasa haziko tena, watu wengi leo hii wako katika madhehebu au dini Fulani kwa sababu tu eti babu yake baba yake na ndugu zake wote walizaliwaga humo, kwa hiyo mtu yuko tayari kwenda Motoni na kutokumkubali Kristo kwa sababu tu anaiona dini ya baba zake kuwa ina faida, Wayahudi wengi sana walidhani kuwa Mungu atawahesabia haki kwa sababu wao ni watoto wa Ibrahimu, Yesu aliwajibu wazi kuwa huwezi kuwa mtoto wa Ibrahimu kisha ukawa muuaji, kwa vyovyote vile wayahudi hawakujua kuwa tayari wamekuwa na baba mwingine

 

Yohana 8:39-44 “Wakajibu, wakamwambia, Baba yetu ndiye Ibrahimu! Yesu akawaambia, Kama mngekuwa watoto wa Ibrahimu, mngezitenda kazi zake Ibrahimu. Lakini sasa mnatafuta kuniua mimi, mtu ambaye nimewaambia iliyo kweli, niliyoisikia kwa Mungu. Ibrahimu hakufanya hivyo. Ninyi mnazitenda kazi za baba yenu. Ndipo walipomwambia, Sisi hatukuzaliwa kwa zinaa; sisi tunaye Baba mmoja, yaani, Mungu. Yesu akawaambia, Kama Mungu angekuwa baba yenu, mngenipenda mimi; kwa maana nalitoka kwa Mungu, nami nimekuja; wala sikuja kwa nafsi yangu, bali yeye ndiye aliyenituma. Mbona hamyafahamu hayo niyasemayo? Ni kwa sababu ninyi hamwezi kulisikia neno langu. Ninyi ni wa baba yenu, Ibilisi, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; kwa sababu yeye ni mwongo, na baba wa huo.”   

 

Wayahudi wengi walijifikiri wako sahihi kwa sababu baba yao ni Ibrahimu, walidhani hali ya kiroho inaweza kurithiwa kwa jinsi ya mwili na kwa kushika mapokeo ya baba zao, Lakini Yesu alikuwa akiwajulisha kuwa huwezi kurithi hali ya kiroho bila kuamua kufuata mambo ya rohoni wewe mwenyewe, Paulo mtume anaonyesha hali kama hiyo kuwa kabla hajamjua Yesu alifikiri kuwa ana haki zote vilevile kama wayahudi wengine naye alikuwa mwenye bidii sana katika maswala ya imani akijua kuwa yatampa faida kubwa sana kwa kumpendeza Mungu kupitia taratibu za baba zake na mila za kwao na madhehebu ya kwao na kupitia vyuo vyao, lakini alipomfahamu Yesu alifahamu kuwa yale mambo ya kwanza aliyokuwa akiyashikilia na kufikiri kuwa na faida sasa anaachana nayo na kuyaiona kuwa ni hasara ukilinganisha na uzuri wa kumpokea Kristo:-

 

Wafilipi 3:3-7 “Maana sisi tu tohara, tumwabuduo Mungu kwa Roho, na kuona fahari juu ya Kristo Yesu, wala hatuutumainii mwili. Walakini mimi ningeweza kuutumainia mwili. Mtu ye yote akijiona kuwa anayo sababu ya kuutumainia mwili, mimi zaidi.Nalitahiriwa siku ya nane, ni mtu wa taifa la Israeli, wa kabila ya Benyamini, Mwebrania wa Waebrania, kwa habari ya kuishika torati, ni Farisayo, kwa habari ya juhudi, mwenye kuliudhi Kanisa, kwa habari ya haki ipatikanayo kwa sheria sikuwa na hatia. Lakini mambo yale yaliyokuwa faida kwangu, naliyahesabu kuwa hasara kwa ajili ya Kristo.”

 

Paulo anaonyesha kuwa yeye kama ni kuitumainia Dini aliitumainia sana, alitahiriwa siku ya nane kama dini yao ilivyoagiza,  alikuwa ni muisraeli yaani ni myahudi kama walivyo wayahudi wengine, alizaliwa katika kabila la Benjamin, alikuwa mwebrania halisi, na alikuwa wa madhehebu ya mafarisayo na aliishika torati, na aliliudhi kanisa na kuwatesa wakristo akifikiri kuwa ni sawa kwa mujibu wa dini yao, na aliishika torati hasa na kuwa kwa habari ya kuishika torati hakuwa na dhambi yoyote, Paulo anaonyesha jinsi alivyokuwa jemadari wa kuishi maisha ya haki kwa niaba ya dini yake  na aliipigania.

 

·         Aliishika torati tangu utoto, yeye alipitia mafunzo ya sharia chini ya mkufunzi aliyeheshimika sana na wayahudi aliyeitwa Gamaliel ona

 

Matendo 22:3 “Mimi ni mtu wa Kiyahudi, nalizaliwa Tarso, mji wa Kilikia, ila nililelewa katika mji huu, miguuni pa Gamalieli, nikafundishwa sheria ya baba zetu kwa usahihi, nikawa mtu wa jitihadi kwa Mungu kama ninyi nyote mlivyo leo hivi;”

 

Matendo 5:34 “Lakini mtu mmoja, Farisayo, jina lake Gamalieli, mwalimu wa torati, mwenye kuheshimiwa na watu wote, akasimama katika baraza, akaamuru mitume wawekwe nje kitambo kidogo,”

 

Gamaliel alikuwa ni Rabbi aliyeheshimika sana, kusoma kwake ni kama kusoma chuo kikuu kilichoheshimika sana kwa wakati huo kwa kuwa alikuwa ni Mwalimu wa sharia aliyebobea sana katika madhehebu ya mafarisayo, na Paulo mtume alikuwa mwanafunzi wa mkufunzi huyu wa kiyahudi. Lakini hata hivyo alipompata Yesu degree zake za dini ya kiyahudi alizihesabu kuwa si kitu au ni hasara ukilinganisha na kumpata Yesu Kristo!

 

·         Alikuwa Farisayo yaani moja ya madhehebu yaliyokuwa yakiheshimika sana kwa mitazamo mikali sana na iliyohesabika kama dini sahihi zaidi  Matendo 26:5 “wakinijua sana tangu mwanzo, kama wakipenda kushuhudia, ya kwamba nalikuwa Farisayo kwa kuifuata madhehebu ya dini yetu iliyo sahihi kabisa.”

 

·         Kwa habari ya wivu zeal yaani imani kali Paulo alikuwa na imani kali kiasi cha kutumika kuliudhi kanisa ona

 

Wafilipi 3:6 “kwa habari ya juhudi, mwenye kuliudhi Kanisa, kwa habari ya haki ipatikanayo kwa sheria sikuwa na hatia”. 

 

Matendo 8:3 “Sauli akaliharibu kanisa, akiingia kila nyumba, na kuwaburuta wanaume na wanawake na kuwatupa gerezani.”

 

Matendo 9:1-2 “Lakini Sauli, akizidi kutisha na kuwaza kuwaua wanafunzi wa Bwana, akamwendea Kuhani Mkuu, akataka ampe barua za kuenda Dameski zilizoandikwa kwa masinagogi, ili akiona watu wa Njia hii, waume kwa wake, awafunge na kuwaleta Yerusalemu

                               

·         Kwa asili alikuwa myahudi ni wa uzao wa Ibrahimu

·         Kwa asili alikuwa mbenjamin kabila mojawapo halisi la kiyahudi

·         Kwa asili alikuwa mwebrania wa waebrania, yaani alizaliwa akiwa mwebrania kweli kweli na kiutamaduni yeye ni mwebrania kwelikweli ambapo napo hakuwa na sababu ya kubagulika  Palulo mtume anaonyesha kuwa alikuwa amekamilika idara zote kwa habari ya dini, yeye sio tu alimcha Mungu bali pia alikuwa tayari kuuwa  na kuwatesa na kuwafunga wale wote aliodhani kuwa  hawamchi Mungu kwa mujibu wa dini yake, Paulo mtume alikuwa mtu aliyejitoa katika dini yake kuliko kawaida huu ulikuwa ni wakati ambapo hakuwa amemjua Yesu,  maisha yake ya awali katika dini yake yalikuwa ya muhimu na ya faida kwa wakati huo akijua ya kuwa anaingiza kwake na kwa Mungu wake, Lakini sasa alipobaini ya kuwa kwa Yesu kunalipa zaidi akabadili kibao na kuhesabu yale ya zamani kuwa hayana faida kama kumpata Yesu

 

Wafilipi 3:7 “Lakini mambo yale yaliyokuwa faida kwangu, naliyahesabu kuwa hasara kwa ajili ya Kristo. Naam, zaidi ya hayo, nayahesabu mambo yote kuwa hasara kwa ajili ya uzuri usio na kiasi wa kumjua Kristo Yesu, Bwana wangu; ambaye kwa ajili yake nimepata hasara ya mambo yote nikiyahesabu kuwa kama mavi ili nipate Kristo;”     

 

Unaweza kuona wako watu ambao wanadhani imani walizozirithi zina faida kubwa sana kwao na hawataki kuachana nazo kwa sababu ni mila, kwa sababu ndugu zao wote ni wa aina hiyo, hawataki kuziachia wakidhani kuwa yana faida kwao, wako wenye kuabudu mizimu, wako wenye kushika dini Fulani na desturi za aina Fulani, au imani zao zimewafikisha mahali Fulani, labda wamesomea maswala kadhaa katika imani zao, wana degree, wana phd, wana diploma za aina mbalimbali, wana heshima, wana wivu kwaajili ya miungu yao, wanaheshimika katika dini zao, wamepewa vyeo ni wazee wa kanisa, wamehiji maeneo matakatifu wako karibu na viongozi wakubwa wa kidini  wanaamini kuwa wamewekeza kwa faida na kiwango kikubwa sana katika dini zao, vyovyote vile iwavyo Paulo mtume alipobaini kuwa Yesu, analipa aliachana na kila kitu na kuyahesabu yote kuwa ni hasara  na kuwa faida kubwa ni kumpata Yesu!

Paulo mtume alikuwa amejifunza ya kuwa hakuna mtu anaweza kuokolewa kwa matendo yake mema au sifa zake za zamani, Mungu hatuhesabii haki kwa sababu ya wema na matendo mazuri tuliyoyafanya katika dini zetu

Warumi 3:20-24 “kwa sababu hakuna mwenye mwili atakayehesabiwa haki mbele zake kwa matendo ya sheria; kwa maana kutambua dhambi huja kwa njia ya sheria. Lakini sasa, haki ya Mungu imedhihirika pasipo sheria; inashuhudiwa na torati na manabii; ni haki ya Mungu iliyo kwa njia ya imani katika Yesu Kristo kwa wote waaminio. Maana hakuna tofauti; kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu; wanahesabiwa haki bure kwa neema yake, kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu;”

Tunaishi katika ulimwengu wa pongezi, na wengi wanadhani kwa kufanya vizuri wanaweza kukubalika kwa Mungu na wanadamu pia lakini ukweli unabaki palepale kwamba mafanikio ya kiroho yanapatikana kwa kumuamini Yesu tu, tunapofanya mema tukumbuke maelekezo ya Yesu ya kuwa tumefanya tu yatupasayo kufanywa, Luka 17:10 “Vivyo hivyo nanyi, mtakapokwisha kuyafanya yote mliyoagizwa, semeni, Sisi tu watumwa wasio na faida; tumefanya tu yaliyotupasa kufanya.” Kutumainia lolote nje ya Yesu Kristo ni kutumainia hasara.

2.       Mila na desturi za baba zetu.

Jambo linguine kubwa litakalowatesa wengi na kuwapeleka Motoni ni kushika mila na desturi za baba zao au babu zao, Jambo hili vilevile liliwaathiri wayahudi, walidhani ya kuwa wanaweza kuokolewa kupitia mila zao na hivyo walishika sana mila zao na desturi kiasi cha kusahahu kujua Mungu anataka nini kwao kuna watu wengi sana leo wanayashika mapokeo ya madhehebu yao, mila na desturi za wazee wao na kuacha kuliangalia neno la Mungu kwa undani hii ilikuwa shida kubwa kwa wayahudi wa kawaida na kwa Paulo Mtume pia Mathayo 15:1-3 “Ndipo Mafarisayo na waandishi toka Yerusalemu walipomwendea Yesu wakisema, Mbona wanafunzi wako huyahalifu mapokeo ya wazee, kwa maana hawanawi mikono walapo chakula. Akajibu, akawaambia, Mbona ninyi nanyi huihalifu amri ya Mungu kwa ajili ya mapokeo yenu?Yesu alikemea vikali sana na kuiita tabia hii kuwa ni ya kinafiki alionya vikali kutokuhubiri neno la Mungu na kuhubiri mila na desturi ambayo kwa lugha nyingine aliyaita maagizo ya wanadamu au mapokeo ya wanadamu ona Mathayo 15:7-9 “Enyi wanafiki, ni vema alivyotabiri Isaya kwa habari zenu, akisema, Watu hawa huniheshimu kwa midomo; Ila mioyo yao iko mbali nami. Nao waniabudu bure, Wakifundisha mafundisho Yaliyo maagizo ya wanadamuNabii Yohana aliwaonya vikali na mapema wayahudi kuwa kujifikiri ya kuwa wanaye baba ndiye Ibrahimu bila kufungua mioyo yao na kumpokea masihi kwa imani ona Mathayo 3:7-10 “Hata alipoona wengi miongoni mwa Mafarisayo na Masadukayo wakiujia ubatizo wake, aliwaambia, Enyi wazao wa nyoka, ni nani aliyewaonya ninyi kuikimbia hasira itakayokuja? Basi zaeni matunda yapasayo toba; wala msiwaze mioyoni mwenu kwamba, Tunaye baba, ndiye Ibrahimu; kwa maana nawaambia ya kwamba Mungu aweza katika mawe haya kumwinulia Ibrahimu watoto. Na shoka limekwisha kuwekwa penye mashina ya miti; basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni.” Swala la mila na desturi lilisumbua mno nyakati za kanisa la kwanza na linasumbua hata leo, watu wengi wameacha kweli ya neno la Mungu na wanasumbuliwa na mafundisho na mapokeo ya wanadamu na hivyo wanaweza kujikuta kuwa wanapata hasara kwa kufuata desturi za kidhehebu, kimila na taratibu zilizowekwa na wanadamu, Paulo aliyashika sana mapokeo ya baba zake ona Wagalatia 1:14 “Nami naliendelea katika dini ya Kiyahudi kuliko wengi walio hirimu zangu katika kabila yangu, nikajitahidi sana katika kuyashika mapokeo ya baba zangu.” Hata hivyo baada ya kumjua Kristo aliliasa kanisa kuachana na aina hii ya Elimu yenye kupotosha ambayo kismingi sio neno la Kristo Wakolosai 2:8 “Angalieni mtu asiwafanye mateka kwa elimu yake ya bure na madanganyo matupu, kwa jinsi ya mapokeo ya wanadamu, kwa jinsi ya mafundisho ya awali ya ulimwengu, wala si kwa jinsi ya Kristo.” Ukristo utakuwa na nguvu kubwa sana kama watu wataacha mapokeo ya kujifunza kulishika neno la Mungu ambalo kimsingi ni kumjua Yesu Kristo jambo hili ndio lenye faida kubwa sana kuliko tunavyoweza kufikiri.          

Faida kubwa iko katika kumjua Yesu Kristo

Tangu nyakati za nabii Yeremia maandiko yalionyesha kuwa jambo lanye faida kubwa na la kujivunia ni kumjua Yesu, Mungu anataka tujivunie kumjua yeye zaidi ya kitu kingine chochote!

Yeremia 9:23-24 “Bwana asema hivi, Mwenye hekima asijisifu kwa sababu ya hekima yake, wala mwenye nguvu asijisifu kwa sababu ya nguvu zake, wala tajiri asijisifu kwa sababu ya utajiri wake; bali ajisifuye na ajisifu kwa sababu hii, ya kwamba ananifahamu mimi, na kunijua, ya kuwa mimi ni Bwana, nitendaye wema, na hukumu, na haki, katika nchi; maana mimi napendezwa na mambo hayo, asema Bwana,”       

Paulo anaiona faida kwa kumjua Yesu Kristo Wafilipi 3:8 “Naam, zaidi ya hayo, nayahesabu mambo yote kuwa hasara kwa ajili ya uzuri usio na kiasi wa kumjua Kristo Yesu, Bwana wangu; ambaye kwa ajili yake nimepata hasara ya mambo yote nikiyahesabu kuwa kama mavi ili nipate Kristo;”

Hili ndio jambo lenye faida kubwa mno, kumjua Yesu, kuwa na uhusiano naye na zaidi sana hata kutamani kwenda kukaa naye milele na milele Wafilipi 3:9-10 “tena nionekane katika yeye, nisiwe na haki yangu mwenyewe ipatikanayo kwa sheria, bali ile ipatikanayo kwa imani iliyo katika Kristo, haki ile itokayo kwa Mungu, kwa imani; ili nimjue yeye, na uweza wa kufufuka kwake, na ushirika wa mateso yake, nikifananishwa na kufa kwake;Kumjua Yesu kristo kuna faida kubwa sana, kumjua yeye kunaaanza na kusoma habari zake, ili tuziamini na kwa kumuamini yeye tunakuwa na uzima tena uzima wa milele ona Yohana 20:30-31 “Basi kuna ishara nyingine nyingi alizozifanya Yesu mbele ya wanafunzi wake, zisizoandikwa katika kitabu hiki. Lakini hizi zimeandikwa ili mpate kuamini ya kwamba Yesu ndiye Kristo, Mwana wa Mungu; na kwa kuamini mwe na uzima kwa jina lake

Muhimu

Wafilipi 3:10-11 “ili nimjue yeye, na uweza wa kufufuka kwake, na ushirika wa mateso yake, nikifananishwa na kufa kwake; ili nipate kwa njia yo yote kuifikia kiyama ya wafu.”

Kuna mambo mengi ambayo tungependa kuyajua duniani kwa sababu tunataka kuitawala dunia,na kuyajua mazingira yetu ya sasa na kukabiliana na changamoto za ulimwengi huu kila mmoja ana mengi ambayo kwayo anaweza kuyaona kuwa yana faida nyingisana, hata katika maisha tunatoa kipaumbele kwa mambo tunayodhani na kufikiri kuwa ni ya Muhimu na yana faida kubwa sana kama ilivyiokuwa kwa Paulo mtume hata hivyo tunapaswa kumuelewa kuwa kwa nini alitamani sana kumuona Kristo Paulo alikuwa na uelelewa kuwa kumjua Yesu Kristo lilikuwa jambo lenye faida pan asana na hivyo aliyahesabu mabo mengine yote kuwa ni hasara na kuyafafnanisha na mavi, ili kumpata Kristo

Rev. Innocent Samuel Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima!