Jumanne, 11 Aprili 2023

Mama tazama mwanao


Yohana 19:26-27 “Basi Yesu alipomwona mama yake, na yule mwanafunzi aliyempenda amesimama karibu, alimwambia mama yake, Mama, tazama, mwanao. Kisha akamwambia yule mwanafunzi, Tazama, mama yako. Na tangu saa ile mwanafunzi yule akamchukua nyumbani kwake.”


Utangulizi

Moja ya maneno saba aliyoasema Bwana Yesu pale msalabani ni Pamoja na Maneno haya Mama tazama mwanao, neno hili ni moja ya neno Muhimu sana linalotukumbusha wajibu wetu Muhimu sana wa kuhakikisha kuwa wazazi wetu na jamii yetu na familia zetu zinajengewe uhakika wa maisha ya baadaye hata pale wakati sisi tunapokuwa hatupo, leo tutachukua muda kujifunza kwa undani kwa kina na mapana na marefu kuhusiana na maana ya maneno haya, hata hivyo ni muhimu kama ilivyo kwa masomo yote ya mfululizo wa maneno saba ya Kristo pale Msalabani kujikumbusha maneno yote sana kwa mfululizo wake kisha tutaendelea na uchambuzi wa neno husika leo, Maneno yote sana ya Msalabani ni pamoja na :-

·         Baba uwasamehe kwa maana hawajui walitendalo Luka 23:34

·         Amin nakuambia leo hii utakuwa pamoja nani peponi Luka 23:43

·         Mama tazama mwanao, mwana tazama mama yako Yohana 19:26-27

·         Mungu wangu Mungu wangu mbona umeniacha Mathayo 27:46

·         Nina kiu Yohana 19:28

·         Imekwisha Yohana 19:30

·         Baba mikononi mwako naiweka roho yangu Luka 23:46

Tutajifunza somo hili, Mama tazama mwanao kwa kuzingatia maeneo makuu matatu yafuatayo:-

*      Utata kuhusu Ndugu wa Yesu Kristo

*      Kwa nini Mariam mikononi mwa Yohana ?

*      Mama tazama mwanao

Utata kuhusu Ndugu wa Yesu Kristo.

Yohana 19:26-27 “Basi Yesu alipomwona mama yake, na yule mwanafunzi aliyempenda amesimama karibu, alimwambia mama yake, Mama, tazama, mwanao. Kisha akamwambia yule mwanafunzi, Tazama, mama yako. Na tangu saa ile mwanafunzi yule akamchukua nyumbani kwake.”

Kabla ya kuzungumzia umuhimu na maana ya maneno ya Bwana Yesu ya awamu ya tatu Mama tazama mwanao… Ni muhimu kwanza tukaondoa utata wa kitheolojia unaotoka na msimamo wa kanisa katoliki na msimamo wa makanisa ya kipentekoste kuhusu Maana ya mstari huu!

Katika mtazamo wa kikatoliki wao wanajenga hoja ya kuwa mstari huu wa Yesu akiwa msalabani kumwambia Mama tazama mwanao Kisha akamwambia yule mwanafunzi, Tazama mama yako, Na tangu saa ile Mwanafunzi yule akamchukua nyumbani kwake, ni suhahidi wazi kuwa Mariamu hakuwa na watoto wengine zaidi ya Yesu, wakatoliki wanajenga hoja kuwa ni jambo la kushangaza kumuona Yesu akimkabidhi mama yake kwa Mtu mwingine mbali na watoto wake mariamu kama mama huyo angelikuwa na watoto wengine kwa hiyo kwao mstari huu ni ushidi ulio wazi kuwa Mariamu hakuwa na watoto wengine tofauti na wapentekoste wanavyodai!

Katika mtazamo wa kipentekoste ni wazi na dhahiri kuwa kulikuwepo sababu maalumu za Yesu kumkabidhi mama yake Kwa mwanafunzi aliyempenda sana ambaye kiushahidi mwanafunzi huyu ni Yohana, ukweli wa kuweko ndugu za Yesu kristo sio ukweli na mtazamo wa kipentekoste bali ni ukweli na mtazamo wa Biblia yenyewe Maandiko yanaionyesha wazi kuwa Yesu alikuwa na ndugu zake wa kuzaliwa mara baada ya yeye kuzaliwa nao walikuwa ni Yakobo, Yusufu, Simoni na Yuda pamoja na dada zake wawili ona :-

Mathayo 13:53-56 “Ikawa Yesu alipoimaliza mifano hiyo, alitoka akaenda zake. Na alipofika nchi yake, akawafundisha katika sinagogi lao, hata wakashangaa, wakasema, Huyu amepata wapi hekima hii na miujiza hii? Huyu si mwana wa seremala? Mamaye si yeye aitwaye Mariamu? Na nduguze si Yakobo, na Yusufu, na Simoni, na Yuda? Na maumbu yake wote hawapo hapa petu? Basi huyu amepata wapi haya yote?

Biblia imeweka wazi kuwa Yesu Kristo alikuwa na ndugu zake na imetueleza kuwa mwanzoni nduguze walikuwa bado hawajamuamini, na pia mara kwa mara walimtembelea kutaka kumuona hata wakati akiwa anawahudumia watu ona

Mathayo 12:46-47 “Alipokuwa katika kusema na makutano, tazama, mama yake na ndugu zake walikuwa wakisimama nje, wataka kusema naye. Mtu mmoja akamwambia, Tazama, mama yako na ndugu zako wamesimama nje, wanataka kusema nawe.”

Marko 3:31-32 “Wakaja mamaye na nduguze; wakasimama nje, wakatuma mtu kumwita. Na makutano walikuwa wameketi, wakimzunguka, wakamwambia, Tazama, mama yako na ndugu zako wako nje, wanakutafuta.”

Luka 8:19-20 “Wakamwendea mama yake na ndugu zake, wasiweze kumkaribia kwa sababu ya mkutano. Akaletewa habari akiambiwa, Mama yako na ndugu zako wamesimama nje wakitaka kuonana nawe.”

Yohana 7:1-10 “Na baada ya hayo Yesu alikuwa akitembea katika Galilaya; maana hakutaka kutembea katika Uyahudi, kwa sababu Wayahudi walikuwa wakitafuta kumwua. Na sikukuu ya Wayahudi, Sikukuu ya Vibanda, ilikuwa karibu. Basi ndugu zake wakamwambia, Ondoka hapa, uende Uyahudi, wanafunzi wako nao wapate kuzitazama kazi zako unazozifanya. Kwa maana hakuna mtu afanyaye neno kwa siri, naye mwenyewe ataka kujulikana. Ukifanya mambo haya, basi jidhihirishe kwa ulimwengu. Maana hata nduguze hawakumwamini. Basi Yesu akawaambia, Haujafika bado wakati wangu; ila wakati wenu sikuzote upo. Ulimwengu hauwezi kuwachukia ninyi; bali hunichukia mimi, kwa sababu mimi naushuhudia ya kuwa kazi zake ni mbovu. Kweeni ninyi kwenda kula sikukuu; mimi sikwei bado kwenda kula sikukuu hii, kwa kuwa haujatimia wakati wangu. Naye alipokwisha kuwaambia hayo, alikaa vivi hivi huko Galilaya. Hata ndugu zake walipokwisha kukwea kuiendea sikukuu, ndipo yeye naye alipokwea, si kwa wazi bali kana kwamba kwa siri.”

Matendo 1:13-14 “Hata walipoingia, wakapanda orofani, walipokuwa wakikaa; Petro, na Yohana, na Yakobo, na Andrea, Filipo na Tomaso, Bartholomayo na Mathayo, Yakobo wa Alfayo, na Simoni Zelote, na Yuda wa Yakobo.Hawa wote walikuwa wakidumu kwa moyo mmoja katika kusali, pamoja nao wanawake, na Mariamu mama yake Yesu, na ndugu zake.”

Wagalatia 1:18-19 “Kisha, baada ya miaka mitatu, nalipanda kwenda Yerusalemu ili nionane na Kefa, nikakaa kwake siku kumi na tano. Lakini sikumwona mtume mwingine, ila Yakobo, ndugu yake Bwana.    

Kwa hiyo tunapoyachunguza maandiko unaweza kuona kuwa yanabainisha wazi kuwa Yesu alikuwa na ndugu wa kibailojia ndugu wa damu ndugu wa kuzaliwa mara baada yaye ye kuzaliwa kwa uwezo wa Roho Mtakatifu, kwa msingi huo ni dhahiri ya kuwa Yesu alikuwa na ndugu,  na ndio maana utaweza kuona kwa asili wanapotajwa wanatajwa wakiwa pamoja na mama yao, wakatio mwingine wakatoliki wamefikiri kuwa ndugu hao wa Yesu ni binamu zake lakini iko wazi kuwa hao hawakuwa binamu zake Neno la asili la kiyunani linalotumika katika maandiko kuelezea maana ya Ndugu ni Adelphos au Delphus ambalo maana yake connective particle au Morphological ties Neno hilo Ndugu limetumika mara 346 katika Biblia likimaanisha Ndugu wa damu au ndugu wa tumbo Moja wakati ndugu wa kiimani limetumika mara 226 kwa msingi huo Yesu alikuwa na ndugu wa damu na wa kuzaliwa baada ya kuzaliwa yeye kwa muujiza nduguze wa karibu walizaliwa Nduhu hao wa Yesu wanatajwa katika maandiko baada ya Yesu kuzaliwa na sio kabla kwa kuwa wangeweza kutajwa wakati Yusufu alipoenda Bethelehemu au walipokimbilia Misri au wakati wa kurudi Nazarethi kwa msingi huo Maandiko yanabainisha wazi kuwa Yesu alikuwa na ndugu zake wa damu na wa kuzaliwa mwenye sikio la kusikia na alisikie neno hili.

*      Kwa nini Mariam mikononi mwa Yohana ?

Swali kubwa wanalouliza wengi ni kuwa kama Yesu alikuwa na ndugu zake iweje Yesu amkabidhi Mariama kwa Mwanafunzi wake aliyempenda aitwaye Yohana? Jibu ni rahisi sana Yohana ndiye mwanafunzi pekee aliyekuwa karibu sana na Msalaba pamoja na Mariamu mama yake Yesu wakati wanafunzi wengine walikimbia au walikuwa wakiangalia kwa mbali sana

Mathayo 26:58 “Na Petro akamfuata kwa mbali mpaka behewa ya Kuhani Mkuu, akaingia ndani, akaketi pamoja na watumishi, auone mwisho.”

Mathayo 27:55-56 “Palikuwa na wanawake wengi pale wakitazama kwa mbali, hao ndio waliomfuata Yesu toka Galilaya, na kumtumikia.Miongoni mwao alikuwamo Mariamu Magdalene, na Mariamu mama yao Yakobo na Yusufu, na mama yao wana wa Zebedayo.”

Marko 15:40-41 “Palikuwako na wanawake wakitazama kwa mbali; miongoni mwao alikuwamo Mariamu Magdalene, na Mariamu mama yao Yakobo mdogo na Yose, na Salome; hao ndio waliofuatana naye huko Galilaya, na kumtumikia; na wengine wengi waliopanda pamoja naye mpaka Yerusalemu.”

Luka 23:49 “Na wote waliojuana naye, na wale wanawake walioandamana naye toka Galilaya, wakasimama kwa mbali, wakitazama mambo hayo.”

Wakati injili zote zikithibitisha kuwa watu wote walikuwa mbali sana na Yesu wakati wa mateso yake habari njema ni kuwa waliokuwako karibu kabisa na msalaba kiasi cha kusikia maneno ya Yesu akizungumza ni Mariamu mama yake Yesu na Yohana mwanafunzi mpendwa wa Yesu Kristo  ona

 Yohana 19:26-27 “Basi Yesu alipomwona mama yake, na yule mwanafunzi aliyempenda amesimama karibu, alimwambia mama yake, Mama, tazama, mwanao. Kisha akamwambia yule mwanafunzi, Tazama, mama yako. Na tangu saa ile mwanafunzi yule akamchukua nyumbani kwake.”

Yesu alipokuwa msalabani aliweza kumuona mama yake na yule mwanafunzi aliyempenda amesimama karibu unaona jukumu la kumuangalia Mariamu mama yake Yesu alipewa Yohana na Jukumu la Mama kumuona Yohana kama mwanae walipewa kwa sababu ndio waliokuwa karibu na Yesu na sio vinginevyo, wakati wa mateso  na majaribu watu muhimu ni wale wanaokuwa karibu na wewe na sio wale wanaokuwa mbali na wewe

*      Mama tazama mwanao

Ukiacha sababu ya Yesu kumuona Yohana na mama yake kuwa karibu kiasi cha kuweza kuzungumza nao na kuwapa majukumu ya kutunzana maneno haya mama tazama mwanao na mwana tazama mama yako, ni fundisho lililowazi kuwa Yesu pamoja na mambi mengine alikuwa anaijali famlia yake, Historia ya kimasimulizi ya kale inaona wazi kuwa huenda Yusufu baba mlezi wa Yesu Kristio na baba mzazi wa ndugu zake Yesu huenda atakuwa alifariki kitambo kidogo kabla ya kusulubiwa kwa Yesu na huenda kuwa ni kwa muda Fulani Yesu alikuwa ndio nguzo ya Familia na ndio maana utaweza kuona ndugu zake na mama yake mara kadhaa walikuwa wakimuendea, Sasa Yesu Yuko Msalabani alimkabidhi mama yake kwa Yohana na kumtaka amuangalie na pia alimkabidhi Mariamu kwa Yohana ili wawe na ushirika naye

Agizo hili linatukumbusha wote majukumu yetu ya kuwaangalia wanafamilia wote na kuhakikisha tunawatunza,  kukabidhiwa kwa Mariamu kwa Yohana ni sawa na kukabidhiwa kwa wanafunzi wote na Yesu angeagiza hivyuo kwa owte kanma wote wangekuwa karibu naye Mungu hana upendeleo, baadaye tunamuona Yesu akiwaoa wanafunzi wake majukumu kadhaa akionyesha kuwa amewaamini, mfano alimwambia Petro Lisha kondoo zangu lakini pia aliwaambia wanafunzi wote waihubiri injili na kuwa anagekuwa pamoja nao zaidi ya yote tunawaona wanafunzi wote baadaye wakiwa na Mariamu mama yake Yesu na nduguze wakiwa na ushirika mmoja wote kwa pamoja, 

Matendo 1:13-14 “Hata walipoingia, wakapanda orofani, walipokuwa wakikaa; Petro, na Yohana, na Yakobo, na Andrea, Filipo na Tomaso, Bartholomayo na Mathayo, Yakobo wa Alfayo, na Simoni Zelote, na Yuda wa Yakobo.Hawa wote walikuwa wakidumu kwa moyo mmoja katika kusali, pamoja nao wanawake, na Mariamu mama yake Yesu, na ndugu zake.”

Unaona Katika majira ya Pasaka ni muhimu kila mmoja kukumbuka kuwa karibu na familia na kuangaliana na kutunzana lakini ni wakati wa kujikumbusha umuhimu wa kuwa karibu na wale wanaopitia changamoto za aina mbalimbali, na wakati wote kuhakikisha kuwa tunawakumbuka wazazi wetu na kuwapa msaada wa karibu unaowezekana heshima hii ni ya Muhimu wakati wote tunapokuwa hai.

Na Rev. Innocent Samuel Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima



Leo hivi utakuwa pamoja nami Peponi!


Luka 23:39-43 “Na mmoja wa wale wahalifu waliotungikwa alimtukana, akisema, Je! Wewe si Kristo? Jiokoe nafsi yako na sisi. Lakini yule wa pili akamjibu akamkemea, akisema, Wewe humwogopi hata Mungu, nawe u katika hukumu iyo hiyo? Nayo ni haki kwetu sisi, kwa kuwa tunapokea malipo tuliyostahili kwa matendo yetu; bali huyu hakutenda lo lote lisilofaa. Kisha akasema, Ee Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako. Yesu akamwambia, Amin, nakuambia, leo hivi utakuwa pamoja nami peponi.”


Utangulizi

Wote tunafahamu kuwa Mateso na hukumu ya kusulubiwa na kufia Msalabani halikuwa tukio Jepesi, lilikuwa tukio gumu na la maumivu mengi ya kimwili, kisaikolojia na kiroho, Yesu alisulubiwa akiwa hana hatia wala hakuwa amefanya kosa lolote, wote tunajua sasa ya kuwa alisulubiwa na kuteswa kwaajili ya dhambi zetu, lakini kwa wakati ule wa mateso haikuwa rahisi kueleweka namna hiyo, akiwa Msalabani Pale Golgotha Yesu alisulubiwa pamoja na wanyang’anyi wawili, ambao kimsingi wao walikuwa na hatia! Lakini katika namna ya kushangaza wahalifu hao mmoja alijiunga katika kumshutumu Bwana Yesu na Mwingine kumtetea

Luka 23:36-43 “Wale askari nao wakamfanyia dhihaka, wakimwendea na kumletea siki, huku wakisema, Kama wewe ndiwe mfalme wa Wayahudi, ujiokoe mwenyewe. Na juu yake palikuwa na anwani; HUYU NDIYE MFALME WA WAYAHUDI. Na mmoja wa wale wahalifu waliotungikwa alimtukana, akisema, Je! Wewe si Kristo? Jiokoe nafsi yako na sisi. Lakini yule wa pili akamjibu akamkemea, akisema, Wewe humwogopi hata Mungu, nawe u katika hukumu iyo hiyo? Nayo ni haki kwetu sisi, kwa kuwa tunapokea malipo tuliyostahili kwa matendo yetu; bali huyu hakutenda lo lote lisilofaa. Kisha akasema, Ee Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako. Yesu akamwambia, Amin, nakuambia, leo hivi utakuwa pamoja nami peponi.”

Tukio hili linapelekea Yesu kutamka neno la pili Muhimu miongini mwa maneno saba aliyoyatamka akiwa msalabani, kwa kujikumbusha maneno mengine aliyoyatamka Yesu akiwa Msalabani ni Pamoja na :-

·         Baba uwasamehe kwa maana hawajui walitendalo Luka 23:34

·         Amin nakuambia leo hivi utakuwa pamoja nani peponi Luka 23:43

·         Mama tazama mwanao, mwana tazama mama yako Yohana 19:26-27

·         Mungu wangu Mungu wangu mbona umeniacha Mathayo 27:46

·         Nina kiu Yohana 19:28

·         Imekwisha Yohana 19:30

·         Baba mikononi mwako naiweka roho yangu Luka 23:46

Uchambuzi kuhusu Neno “Leo hivi utakuwa pamoja nami Peponi”

Ni muhimu sana kufahamu kuwa Maneno hayo ya pili yaliyotamkwa na Yesu pale msalabani kwa mtu yule aliyekuwa muhalifu, yana uzito mkubwa sana linapokuja swala la wanafunzi wa kimaandiko wenye kufikiri sana, watafasiri wengi wa maandiko wanaweka hoja ngumu zinazopelekea mstari huu wakati mwingine usiwe mstari mwepesi kutafasirika ona kwa mfano Maneno hayo yanasomeka hiviYesu akamwambia, Amin, nakuambia, leo hivi utakuwa pamoja nami peponiwataalamu wa maandiko wakati mwingine kwa sababu ya kufikiri sana wanajenga hoja kuwa Yesu alikata roho na kufa na kuzikwa na siku ya tatu akafufuka  na akaonekana mara kadhaa duniani kwa watu mbalimbali mpaka alipopaa, kwa msingi huo inawezekanaje Yesu kuwa Pamoja na muhalifu yule Peponi siku ileile, kwa sababu hiyo waoa wanajenga hoja kwamba kwa vile Maandiko ya awali hayakuwa na vituo wala koma huenda maneno maneno ya Yesu yalitakiwa yasomoke hivi Yesu akamwambia, Amin nakuambia leo hivi, utakuwa pamoja nami peponikwa hiyo wataalamu hao wa maandiko hifikiri kuwa kulikuwa na makosa kuweka koma mbele ya neno Amin na neno nakuambia na kuwa sentensi …AMIN NAKUAMBIA LEO HIVI, Yalikuwa ni sentesi moja na hivyo kuifanya ahadi ya Yesu iwe ni neno UTAKUWA PAMOJA NAMI PEPONI, kuweka neno LEO HIVI UTAKUWA PAMOJA NAMI PEPONI Kungeweza kupotosha maana halisi ya tafasiri ya maandiko hayo, Kwa tafasiri hiyo wao wanaamini ya kuwa Yesu alikuwa anamthibitishia Mwizi yule aliyemuamini kuwa anayioyasema ni hakika kwamba atakuwa naye Peponi, Kwahiyo uthibitisho huo wa Yesu kusema ukweli umebebwa na neno …AMIN NAKUAMBIA LEO HIVI ni kwamba Yesu alikuwa anamueleza ukweli wa kuweko kwake peponi mtu yule anayemuamini, lakini haikuwa lazima kuwa Yesu alikuwa anamaanisha kuwa angekuwa naye peponi siku ileile!

Wakati mwingine kufikiri sana na kutumia akili sana kunaweza kuleta upotofu katika maandiko, ushahidi wa kibiblia kutoka katika biblia nyingine unathibitisha wazi kuwa koma iliwekwa mahali sahihi vilevioe kama ilivyowekwa katika Biblia ya kiswahili ya Union version Mfano

·         Biblia ya Kiingereza ya KJV inasema “Verily I say unto thee, To day shalt thou be with me in paradise”

·         Biblia ya kiingereza ya Amplified inasema “Assuredly I tell you, today you will be with me in Paradise”

·         Biblia ya kiingereza ya RSV inasema “And he said to him truly, I say to you, today you will be with me in paradise”

Unaweza kuona tafasiri zote za Biblia zimeweka Koma katika eneo sahihi na kama ilivyo ada ni kweli kuwa Yesu kila alipotaka kuzungumza neno lenye mantiki kubwa sana alitumia neno Amin Nakuambia, na neno la namna hiyo limerejewa katika biblia zaidi ya  mara 76 hata hivyo katika maeneo yote hayo hajawahi kutumia neno LEO,  Kwa msingi huo ni wazi kabisa kuwa Yesu alikuwa akisisitiza kuwa Peponi na Mtu yule kuanzia siku ile ile Angekuwa naye Peponi.

Ni ukweli ulio wazi kuwa Yesu aliposulubiwa na kufa na kuzikwa mwili wake uliwekwa Kaburini, Lakini Nafsi yake na Roho yake alikabidhi kwa Mungu baba na hivyo alikuwa mbinguni au Paradiso tangu wakati ule Luka 23:46 “Yesu akalia kwa sauti kuu, akasema, Ee Baba, mikononi mwako naiweka roho yangu.”  Maneno ya Yesu yako wazi na hayahitaji tafakari pana inakayoweza kututoa nje ya maana halisi japo kufikiri kama mhivi ni kuzuri na kunapanua ufahamu lakini ni ukweli usiopingika kuwa Mwivi yule alipata tiketi ya kuwa na Yesu Peponi tangu siku ile ile.

Leo hivi utakuwa pamoja nani peponi.

Ni ahadi ya uhakika ya kuwa kila anayermkubali Yesu Mungu mwenyewe anatuhakikishia kuwa atakuwa pamoja nasi Peponi, haijalishi kuwa ulikuwa muovu kiasi gani, hatujaelezwa wazi kuwa muhalifu huyu alikuwa amefanya makosa gani lakini iko wazi kuwa kama mtu amehukumiwa kuuawa bila shaka hakuwa mtu mwenye kufaa tena katika jamii, mhalifu huyu sio tu alistahili kuuawa lakini alikuwa hastahili hata kuwekwa Gerezani, kwa vyovyote vile akuwa muovu, mtu huyu hata toba yake ilikuwa sio toba ya kueleweka lakini ni ukweli ya kuwa alikuwa anajua kuwa yuko Msalabani kwa makosa yake naya kuwa anastahili kupata yanayompata, lakini pia alikuwa anatambua kazi ya Yesu pale Msalabani alijua wazi kuwa yeye hakuwa na hatia kama wao na alitambua kuwa Yesu anao ufalme na kuwa sio mwanadamu wa kawaida na alijiombea kukumbukwa katuika ufalme huo, Yesu alimkakikishia kuwa atakuwa pamoja naye peponi, Yesu aliteseka Msalabani si kwa sababu yake ilikuwa ni kwaajili ya dhambi zetu

Isaya 53:3-5 “Alidharauliwa na kukataliwa na watu; Mtu wa huzuni nyingi, ajuaye sikitiko; Na kama mtu ambaye watu humficha nyuso zao, Alidharauliwa wala hatukumhesabu kuwa kitu. Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu; Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa, Amepigwa na Mungu, na kuteswa. Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona

Na kwa msingi huo toba ya muhalifu yule kama ilivyo kwetu sisi ilikuwa ni ahadi thabiti yay a kweli yenye kutuhakikishia wote tunaomkiri Yesu hadharani ya kuwa Mungu atakuwa pamoja nasi na sisi tunakuwa pamoja naye, hakuna mtu mbaya kiasi cha kutokuweza kusafishwa au kusamehewa na kusafishwa kwa Damu ya Yesu!, hakuna jambo la msingi kama kuingia peponi tunaweza kuona wivu kwa jamaa huyu Msalabani laki Kristio ameahidi kuwa kila amuaminiye hatatahayarika katika msimu huu wa Pasaka ni Muhimu basi kwa kila mmoja wetu kusogelea Msalabani na kutubu na kumkiri Kristo ili tupate uhakika wa neema yake ya kutupa kibali cha kuingia naye peponi

Na Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima!



Baba uwasamehe, kwa kuwa hawajui watendalo!

 

Luka 23:33-37 “Na walipofika mahali paitwapo Fuvu la Kichwa, ndipo walipomsulibisha yeye, na wale wahalifu, mmoja upande wa kuume, na mmoja upande wa kushoto. Yesu akasema, BABA, UWASAMEHE, KWA KUWA HAWAJUI WATENDALO. Wakagawa mavazi yake, wakipiga kura. Watu wakasimama wakitazama. Wale wakuu nao walikuwa wakimfanyia mzaha, wakisema, Aliokoa wengine; na ajiokoe mwenyewe, kama ndiye Kristo wa Mungu, mteule wake. Wale askari nao wakamfanyia dhihaka, wakimwendea na kumletea siki, huku wakisema, Kama wewe ndiwe mfalme wa Wayahudi, ujiokoe mwenyewe



Utangulizi:

Mojawapo kati ya usemi wenye maana sana kati ya semi saba za Yesu alizozisema akiwa msalabani na ambazo zinatajwa katika sehemu mbalimbali za injili, ni pamoja ya usemi huo wa muhimu ni usemi wa Kwanza wenye Neno BABA UWASAMEHE KWA MAANA HAWAJUI WALITENDALO ambalo leo katika msimu huu wa pasaka tutachukua muda kulijadili kwa undani na kupata maana Muhimu sana iliyokusudiwa, maneno mengine kati ya maneno saba aliyoyasema Yesu msalabani ni pamoja na:-

1.       Baba uwasamehe kwa maana hawajui walitendalo Luka 23:34

2.       Amin nakuambia leo hii utakuwa pamoja nani peponi Luka 23:43

3.       Mama tazama mwanao, mwana tazama mama yako Yohana 19:26-27

4.       Mungu wangu Mungu wangu mbona umeniacha Mathayo 27:46

5.       Nina kiu Yohana 19:28

6.       Imekwisha Yohana 19:30

7.       Baba mikononi mwako naiweka roho yangu Luka 23:46

BABA UWASAMEHE KWA MAANA HAWAJUI WALITENDALO.

Leo ni siku ya ijumaa kuu, ni siku ambayo wakristo wote duniani, tunaungana katika kuadhimisha na kukumbuka kusulubiwa kwa Yesu Kristo huko Golgota miaka zaidi ya 2000 iliyopita katika siku hii basi basi sisi tutachukua Muda kuangalia usemi huu wa Kwanza katika maneno saba yaliyozungumzwa na Yesu Pale Msalabani wakati wa mateso yake , Neno hili ni miongoni mwa maneno saba ya Yesu akiwa matesoni ambayo yamekusanywa kutoka maeneo mbalimbali ya vitabu vya injili na hili mojawapo tutaangalia umuhimu wake katika msimu huu wa Pasaka. Hapa tunazungumzia Msamaha.

Kila mmoja wetu kwa namna moja ama nyingine amewahi kujeruhiwa moyo na mtu mwingine, kila mmoja amewahi kujeruhiwa na kuathiriwa kiakili, kihisia na hata kimwili, na kwa sababu hiyo tunaweza kujawa na maumivu ya aina Fulani mioyoni mwetu, ama uchungu wa aina Fulani, vyovyote vile iwavyo ukomavu wa kiroho katika maisha yetu ya ukristo unapimwa na namna tunavyoweza kusamehe, uwezo wa kusamehe ukiwa pamoja nasi  unatuwezesha kuishi kwa furaha na amani duniani na huku tukiwa huru bila kifungo chochote endapo tutakuwa na uwezo wa kusamehe wengine.

Yesu Kristo akiwa Msalabani aliangalia chini na kutafakari katika hali ya ukimya akiwaangalia wote waliokuwa wanahusika katika kumtesa, Askari ambao walisimamia mateso yake wakigawana nguo yake kwa kuipigia kura, Yesu hakuwahi kutenda neno lolote ovu, siku zote alikuwa akiwafundisha watu neno la Mungu na kuwaponya watu magonjwa yao, aliwahudumia watu akifufua, akiponya, akilisha akihurumia na kurehemu, hata hivyo kwajili ya wivu wakuu wa dini walikusudia kumuua, waliandaa mpango mkakati wa kumuua, walitoa rushwa kwa Yuda ili aweze kumsaliti, waliandaa mashahidi wa uongo ili wamshitaki, walimuweka katima mikono ya wenye dhambi ili asulubiwe, hakimu aliyekuwepo alipindisha hukumu ilihali akijua wazi kuwa Yesu hakuwa na hatia, zaidi ya yote aliamuru Yesu apigwe mijeledi

Yohana 19:1-6 “Basi ndipo Pilato alipomtwaa Yesu, akampiga mijeledi. Nao askari wakasokota taji ya miiba, wakamtia kichwani, wakamvika vazi la zambarau. Wakawa wakimwendea, wakisema, Salamu! Mfalme wa Wayahudi! Wakampiga makofi. Kisha Pilato akatokea tena nje, akawaambia, Mtu huyu namleta nje kwenu, mpate kufahamu ya kuwa mimi sioni hatia yo yote kwake. Ndipo Yesu alipotoka nje, naye amevaa ile taji ya miiba, na lile vazi la zambarau. Pilato akawaambia, Tazama, mtu huyu! Basi wale wakuu wa makuhani na watumishi wao walipomwona, walipiga kelele wakisema, Msulibishe! Msulibishe! Pilato akawaambia, Mtwaeni ninyi basi, mkamsulibishe; kwa maana mimi sioni hatia kwake.”

Ni ukweli usiopingika kuwa Yesu aliharibiwa sana kiasi ambacho ilikuwa ni ngumu kumtamani sawa kabisa na alivyotabiri Isaya katika Isaya 53:2-5Maana alikua mbele zake kama mche mwororo, Na kama mzizi katika nchi kavu; Yeye hana umbo wala uzuri; Na tumwonapo hana uzuri hata tumtamani. Alidharauliwa na kukataliwa na watu; Mtu wa huzuni nyingi, ajuaye sikitiko; Na kama mtu ambaye watu humficha nyuso zao, Alidharauliwa wala hatukumhesabu kuwa kitu. Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu; Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa, Amepigwa na Mungu, na kuteswa. Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona.”

Pamoja na mateso haya na suluba kali pia walimfanyia dhihaka za namna nyingi, mateso yake yamerekodiwa na Mel Gobson katika filamu yake ijulikanayo kama Passion of Jesus ambayo wayahudi walipoiona kwa mara ya kwanza waliikataa na kusema kuwa inaweza kuchochea chuki kati ya wakristo na wayahudi wakifikiri kuwa Mel Gibson ametia chumvi, lakini kitaalamu Mel Gibson ameonyesha karibu robo tatu tu ya mateso halisi aliyoyapata Kristo, mateso mengine :-

Yohana 19:23-24, “Nao askari walipomsulibisha Yesu, waliyatwaa mavazi yake, wakafanya mafungu manne, kwa kila askari fungu lake; na kanzu nayo. Basi kanzu ile haikushonwa, ilikuwa imefumwa yote pia tangu juu. Basi wakaambiana, Tusiipasue, lakini tuipigie kura, iwe ya nani. Ili litimie andiko lile linenalo, Waligawanya nguo zangu, Na vazi langu wakalipigia kura. Basi ndivyo walivyofanya wale askari.

Mathayo 27:27-31 “Ndipo askari wa liwali wakamchukua Yesu ndani ya Praitorio, wakamkusanyikia kikosi kizima.Wakamvua nguo, wakamvika vazi jekundu. Wakasokota taji ya miiba, wakaiweka juu ya kichwa chake, na mwanzi katika mkono wake wa kuume; wakapiga magoti mbele yake, wakamdhihaki, wakisema, Salamu, Mfalme wa Wayahudi! Kisha wakamtemea mate, wakautwaa ule mwanzi, wakampiga-piga kichwani. Walipokwisha kumdhihaki, wakalivua lile vazi, wakamvika mavazi yake, wakamchukua kumsulibisha.

Wahalifu wawili waliokuwa kulia kwake na kushoto kwake wakimshutumu, Mathayo 27:44, “Pia wale wanyang'anyi waliosulibiwa pamoja naye walimshutumu vile vile.” Viongozi wa dini waliofanya fitina na kutengeneza ushahidi wa uongo na kushinikiza kwamba Yesu asulubiwe na waliokuwa wakimdhihaki Mathayo 27:41-43,“Kadhalika na wale wakuu wa makuhani wakamdhihaki pamoja na waandishi na wazee, wakisema, Aliokoa wengine, hawezi kujiokoa mwenyewe. Yeye ni mfalme wa Israeli; na ashuke sasa msalabani, nasi tutamwamini. Amemtegemea Mungu; na amwokoe sasa, kama anamtaka; kwa maana alisema, Mimi ni Mwana wa Mungu

Hakimu Pilato ambaye alifahamu kabisa kuwa Yesu hakuwa na hatia, lakini akapindisha kesi haya yote na ile aina ya mateso kwa mwana wa Mungu, kungeweza kwa namna yoyote ile kuleta hisia za maumivu, uchungu, kinyongo, kisasi, ugumu wa moyo, hasira, ghadhabu, ubaridi, kujihami na kuhakikisha kuwa unawashughulikia wote waliokutenda uovu, Lakini Bwana Yesu anatangaza kusamehe na kuwaombea wakosaji wote kwa BABA KUWA WASAMEHEWE, Hali hii inaashiria uwezo mkubwa wa ukomavu mkubwa wa kiroho aliokuwa nao Yesu wa kutangaza Msamaha, ni ngazi ya juu sana ya Rehema na upendo, kwamba hata katika hali ngumu kama hii ya kuteseka bado Yesu anatangaza Msamaha dhidi ya maadui zake ! wote tunafahamu kuwa msamaha sio jambo rahisi, lakini katika msimu huu wa Pasaka Bwana Yesu anatukumbusha kwamba tunapaswa kuachilia na kutangaza msamaha kwa wote waliotukosea lakini vilevile kuwaomba radhi wale ambao tumewakosea, wakati huu wa Kwaresma ni wakati wa kuachilia ni wakati wa kusamehe ni wakati wa kuonyesha kuwa tumekomaa kiroho na kiakili na kuwa kusamehe ndio njia ya juu kabisa ya kuonyesha tabia ya uungu na ukomavu wetu, tusamehe.!

Kusamehe ni nini hasa?

Kusamehe ni kuachilia, unaachilia mambio yaende, unaacha kuhesabu ubaya uliofanyiwa unaufunika kwa kuendelea kupenda, unaacha kutafuta kulipa kisasi au nkulipiwa kisasi, unaondoa moyoni mwako hali ya kumfikiri mtu aliyekukosea unajiweka huru mbali na kifungo cha aina yoyote cha kuwa na mtu moyoni, unamuhurumia mtu, unachukuliana naye, unamuhesabu kuwa yeye ni dhaifu, hivyo unamuachilia

Faida za kusamehe

·         Unadumisha mahusiano, mahusiano yanakuwa mazuri, Ndoa inakuwa nzuri, unampata ndugu yako

·         Unaiweka akili yako kufikiri mambo ya msingi na kuzungumza mambo ya msingi

·         Unajiweka huru kutoka kwenye migandamizo na msongo wa mawazo

·         Unakuwa na afya nzuri, unakuwa mwenye furaha, hutakuwa na pressure, hutaugua magonjwa ya moyo, na unakuwa mtu mwenye uwezio wa juu wa kujitambua

·         Kusamehe kunakufanya wewe nawe usamehewe na Mungu

Mathayo 18:21-35Kisha Petro akamwendea akamwambia, Bwana, ndugu yangu anikose mara ngapi nami nimsamehe? Hata mara saba? Yesu akamwambia, Sikuambii hata mara saba, bali hata saba mara sabini. Kwa sababu hii ufalme wa mbinguni umefanana na mfalme mmoja aliyetaka kufanya hesabu na watumwa wake. Alipoanza kuifanya, aliletewa mtu mmoja awiwaye talanta elfu kumi.Naye alipokosa cha kulipa, bwana wake akaamuru auzwe, yeye na mkewe na watoto wake, na vitu vyote alivyo navyo, ikalipwe ile deni.Basi yule mtumwa akaanguka, akamsujudia akisema, Bwana, nivumilie, nami nitakulipa yote pia. Bwana wa mtumwa yule akamhurumia, akamfungua, akamsamehe ile deni. Mtumwa yule akatoka, akamwona mmoja wa wajoli wake, aliyemwia dinari mia akamkamata,akamshika koo,akisema Nilipe uwiwacho.Basi mjoli wake akaanguka miguuni pake, akamsihi, akisema, Nivumilie, nami nitakulipa yote pia. Lakini hakutaka, akaenda, akamtupa kifungoni, hata atakapoilipa ile deni. Basi wajoli wake walipoyaona yaliyotendeka, walisikitika sana, wakaenda wakamweleza bwana wao yote yaliyotendeka. Ndipo bwana wake akamwita, akamwambia, Ewe mtumwa mwovu, nalikusamehe wewe deni ile yote, uliponisihi; nawe, je! Haikukupasa kumrehemu mjoli wako, kama mimi nilivyokurehemu wewe? Bwana wake akaghadhibika, akampeleka kwa watesaji, hata atakapoilipa deni ile yote. Ndivyo na Baba yangu wa mbinguni atakavyowatenda ninyi, msiposamehe kwa mioyo yenu kila mtu ndugu yake.”

Kutokusamehe hasara zake

Hakuna sababu ya kuwabeba watu moyoni, hii hali kiroho inakuweka wewe mwenyewe gerezani na kukunyima furaha, dua, sala, sadaka na maombi yetu vinakutana na kikwazo kama hatujawasamehe wengine Mathayo 6:12 “Utusamehe deni zetu, kama sisi nasi tuwasamehevyo wadeni wetu.” Mathayo 6:14-15 “Kwa maana mkiwasamehe watu makosa yao, na Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi.Bali msipowasamehe watu makosa yao, wala Baba yenu hatawasamehe ninyi makosa yenukuna hasara nyingi sana za kiroho na kimwili kama watu hawatasamehe na kuna faida nyingi sana kama watu watasamehe.Lakini kama mtu hatasamehe yafuatayo yatamkabili:-

·         Unakuwa na moyo wenye uchungu, huwezi kufurahia mahusiano hata katika ndoa

·         Unakuwa na mawazo mabaya kwa kudhani Fulani ni adui yako

·         Utakuwa na mgandamizo wa mawazo

·         Unafungua mlango wa kuvamiwa na mapepo, unafukuza uwepo wa Mungu

·         Unazuia Baraka za Mungu na kufanya ibada zako zikataliwe

Bwana na ampe neema kila Mmoja wetu, kuwa na uwezo wa kusamehe ili tuweze kuwa wana wa Mungu sawasawa na mafundisho ya Bwana wetu Yesu!

 

Na. Rev. Innocent Kamote.

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima.

Jumanne, 28 Machi 2023

Mungu Katikati ya shida zako !


Zaburi 138:6-8 “Ingawa Bwana yuko juu, amwona mnyenyekevu, Naye amjua mwenye kujivuna tokea mbali. Nijapokwenda kati ya shida utanihuisha, Utanyosha mkono juu ya hasira ya adui zangu, Na mkono wako wa kuume utaniokoa. Bwana atanitimilizia mambo yangu; Ee Bwana, fadhili zako ni za milele; Usiziache kazi za mikono yako.”



Utangulizi:

Duniani ni mahali ambapo pana changamoto za aina mbalimbali ambazo kila mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke atakutana nazo, wakati mwingine tutakutana na hali ngumu sana ama upinzani mzito sana, au magonjwa makubwa ya kusumbua au kuwa na ndoto kubwa  ambazo tunatafuta namna ya kuzitimiza, na changamoto nyinginezo nyingi, na wakati mwingine hali Fulani za kukatisha tamaa na kuvunja moyo na ama wakati mwingine ukiwa katika vita kali sana, katika ndoa, katika kazi, katika masomo, katika biashara, katika mashamba, katika mifugo na katika mahusiano taabu hizi zote Yesu Kristo anazifahamu na anajua ya kuwa tunazipitia na alitutaka tujipe moyo kwa sababu yeye amezishinda kwaajili yetu. 

Yohana 16:33 “Hayo nimewaambieni mpate kuwa na amani ndani yangu. Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu.” 

Yesu anazungumza maneno haya kwa sababu anatambua wazi kuwa wakati mwingine tunaweza kujiona kama tuna mapungufu Fulani nani kama hatutoshi wala hatustahili hata kufanyiwa muujiza, lakini ni muhimu sana kukumbuka ya kuwa Mungu yuko pamoja nasi yeye anaitwa Emmanuel yaani Mungu pamoja nasi na wakati tunapopitia kila aina ya changamoto na mambo yoyote yanayotukabili yeye yuko pamoja nasi, alikuwa pamoja na Yesu Kristo katika mateso yake na alihakikisha anamfufua, na hakumuacha kaburini, wakati Daudi anakabiliana na jitu kubwa kuliko uwezo wake Mungu alikuwa pamoja naye, wakati Paulo na Sila wakiwa gerezani ni yeye aliyafungua milango ya gereza, wakati Danieli anatupwa katika tundu la Simba ni yeye aliyekuweko kufunga makanwa ya simba, na wakati Shadrak, Meshak na Abednego wakitupwa kwenye tanuri la moto mkali ni yeye ndiye aliyejiunga nao wasiunguzwe jambo kubwa la msingi ni kukumbuka tu ya kuwa Mungu yuko kati kati ya shida zako. 

Zaburi 138:6-8 “Ingawa Bwana yuko juu, amwona mnyenyekevu, Naye amjua mwenye kujivuna tokea mbali. Nijapokwenda kati ya shida utanihuisha, Utanyosha mkono juu ya hasira ya adui zangu, Na mkono wako wa kuume utaniokoa. Bwana atanitimilizia mambo yangu; Ee Bwana, fadhili zako ni za milele; Usiziache kazi za mikono yako.” 

Katika mistari hii ya msingi hususani mstari ule wa saba yaani Zaburi ya 138:7 “Nijapokwenda kati ya shida utanihuisha, Utanyosha mkono juu ya hasira ya adui zangu, Na mkono wako wa kuume utaniokoa.  Mungu nanatufundisha kupitia mtumishi wakeMwandishi wa zaburi hii ya kuwa yeye huwa katikakati ya shida zetu mstari huu katika lugha ya kiingereza Biblia ya NIV husomeka hiviThough I walk in the midst of trouble, you preserve my life you stretch out your hand against the anger of my foes with your hand you save meambapo katika tafasiri yangu naweza kusema Mstari huu unasema hivi NINAPOPITA KATIKATI YA TAABU/SHIDA UNANYOOSHA MKONO WAKO KUNIOKOA NA HASIRA ZA ADUI ZANGU, Yaani maana yake katikati ya shida Mungu anakuwepo, na anatoa msaada kwaajili ya utukufu wake hii maana yake ni nini ? sio kila wakati Mungu atakutoa nje ya shida lakini wakati mwingine atakuacha uingie katika shida na changamoto mbalimbali kisha ataweka mkono wake kwaajili ya utukufu wake, kwa sababu hiyo jambo kubwa la Msingi na la kukumbuka ni kuwa Bwana yuko pamoja nawe bila kujali hali unayoipitia, kuokolewa katika shida sio jambo la Msingi sana kama Mungu kuwa pamoja nawe, Mungu kuwa pamoja nawe hilo ndio jambo kubwa na la msingi, 

Isaya 43:1-2 “Lakini sasa, Bwana aliyekuhuluku, Ee Yakobo, yeye aliyekuumba, Ee Israeli, asema hivi, Usiogope, maana nimekukomboa; nimekuita kwa jina lako, wewe u wangu. Upitapo katika maji mengi nitakuwa pamoja nawe; na katika mito, haitakugharikisha; uendapo katika moto, hutateketea; wala mwali wa moto hautakuunguza.” 

Unaona haijalishi kuna dhuruba kiasi gani kama Mungu yuko pamoja nawe hakuna kitakachoshindikana kwaajili ya utukufu wake, Mungu atatokeza muujiza kwa sababu yumo katikati ya shida yako pamoja nawe 

Kumbuka kuwa 

1.       Wakati Suleiman anaanza kutawala alikuwa na hofu kuwa anawezaje kuongoza taifa kubwa na watu wengi kama wale, baba yake alikuwa mtu wa vita na mtu aliyemtegemea Mungu, hivyo Mungu alimsaidia Suleimani kuwa na hekima ya namna ya kuingia na kutoka na mambo yakawa shwari 

2.       Mungu hakumuwacha Yesu asisulubiwe lakini alimfufua siku ya tatu, hakumwacha mtakatifu wake aonje uharibifu

3.       Mungu hakumwacha Nyangumi asimmeze Yona na badala yake alimsababisha nyangumi amtapike Yona siku ya tatu

4.       Mungu hakumuacha Daniel asiingizwe kwenye tundu la Simba badala yake aliyafunga makanwa ya simba

5.       Mungu hakuwaacha Shadrak na Meshak na Abednego wasitupwe katika tanuru la Moto lakini badala yake alijiunga nao katikati ya Moto ili usiwateteze

6.       Mungu hakuwaacha Paulo na Silas wasipigwe na kutupwa gerezani lakini badala yake aliwaacha wakafungwa gerezani na baadaye akayafungua malango ya magereza na vifungo vyake   

Changamoto kubwa katika maisha yetu sio kutokupitia changamoto bali ni kumuomba Mungu awe pamoja nasi hili ndilo jambo la Msingi Yesu aliahidi ya kuwa atakuwa pamoja nasi hata ukamilifu wa dahari, na alihahidi kuwa tunapokutanika wawili au watatu kwa ajili ya jina lake atakuwa pamoja nasi, Hakuna jambo la msingi duniani kama kuwa na Mungu, Muulize jirani yako una Mungu ukiwa na Mungu una kila kitu!, Changamoto yako sio kubwa kuliko Mungu tunayemtumikia na kumuabudu, Bwana ampoe neema kila mmoja wetu kuwa na Mungu wakati tunapopita katika siku za kujaribiwa kwetu katika jina la Yesu Kristo amen! 

Na Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima!



Alhamisi, 23 Machi 2023

Chanda cha Mungu !


Kutoka 8: 16 -19 “BWANA akamwambia Musa, Mwambie Haruni, Nyosha fimbo yako, ukayapige mavumbi ya nchi, ili kwamba yawe chawa katika nchi yote ya Misri. Nao wakafanya; Haruni akaunyosha mkono wake na fimbo yake, na kuyapiga mavumbi ya nchi, nayo yakawa chawa juu ya wanadamu na juu ya wanyama; mavumbi yote ya nchi yakawa ni chawa katika nchi yote ya Misri. Hao waganga nao wakafanya mfano wa hayo kwa uganga wao, ili kwamba walete chawa, lakini wasiweze; nako kulikuwa na chawa juu ya wanadamu, na juu ya wanyama. Ndipo wale waganga wakamwambia Farao, Jambo hili ni chanda cha Mungu; na moyo wake Farao ukawa mgumu asiwasikize; vile vile kama BWANA alivyonena.”




Utangulizi:

Neno Chanda cha Mungu limejitokeza au kutajwa katika Biblia ya Kiebrania kama neno “etsba” kimatamshi “ets-bah” na kutajwa katika Biblia ya kiingereza ya King James Version mara 32  na kwa lugha ya kiyunani ni “Daktulos” kimatamshi ni Dak-too-los  ambalo Katika Biblia ya kiingereza ya King James Version limetajwa mara 8, maneno yote hayo katika lugha ya kiibrania na kiyunani yanamaanisha kidole cha Mungu, Neno ambalo kinabii linahusiana na Utendaji wa Roho Mtakatifu, hata hivyo Pamoja na neno hilo kutajwa mara kadhaa, limeonekana kwa uwazi katika matukio kadhaa likitumika kwa namna kali zaidi ya maeneo mengine.

·         Kidole cha Mungu wakati wa Farao.

·         Kidole cha Mungu Katika mlima wa Sinai.

·         Kidole cha Mungu wakati wa Beltshaza.

·         Kidole cha Mungu na wakati wa Huduma ya Yesu.

Kidole cha Mungu wakati wa Farao!

Neno kidole cha Mungu linajitokeza kwa mara ya kwanza katika lugha za kinabii, kutokana na uandishi wa Musa katika kitabu cha kutoka mara baada ya Musa na Haruni kuamuriwa na Mungu kuachilia pigo la tatu, Mapigo haya yalikuwa ni amri ya Mungu ili kumlazimisha Farao kuwaachia wana wa Israel waende zao kwa sababu walikaa katika inchi ya Misri na katika hali ya utumwa kwa zaidi ya miaka 400, Mungu alimuelekeza Musa kumuamuru Haruni kunyoosha fimbo yake ili kuyapiga mavumbi ya nchi yapate kuwa chawa katika inchi yote ya Misri

Kutoka 8:16-17BWANA akamwambia Musa, Mwambie Haruni, Nyosha fimbo yako, ukayapige mavumbi ya nchi, ili kwamba yawe chawa katika nchi yote ya Misri. Nao wakafanya; Haruni akaunyosha mkono wake na fimbo yake, na kuyapiga mavumbi ya nchi, nayo yakawa chawa juu ya wanadamu na juu ya wanyama; mavumbi yote ya nchi yakawa ni chawa katika nchi yote ya Misri.”

Kwa kawaida kila Muujiza ambao Musa na Haruni waliufanya kwa jina la Mungu, utaweza kuona wachawi wa kimisri nao waliigiza hasa kwa miujiza ya mwanzoni walipojaribu kuuigiza muujiza huu kwa uchawi wao na kushindwa ndipo walipotamka wenyewe kwa midomo yao kumueleza Farao kuwa hiki ni chanda cha Mungu,

Kutoka 8:18-19 “Hao waganga nao wakafanya mfano wa hayo kwa uganga wao, ili kwamba walete chawa, lakini wasiweze; nako kulikuwa na chawa juu ya wanadamu, na juu ya wanyama. Ndipo wale waganga wakamwambia Farao, Jambo hili ni CHANDA CHA MUNGU; na moyo wake Farao ukawa mgumu asiwasikize; vile vile kama BWANA alivyonena.”  Hapo ndipo tunapouona uweza wa Mungu katika kutenda miujiza ya kupita kawaida dhidi ya miujiza ya kichawi na ya kimazingaombwe, Mungu ana uwezo mkubwa sana, anapukusudia kutukomboa katika utumwa wa anina yoyote ile ni lazima tumuitie yeye kwa uweza wa Roho wake Mtakatifu ambaye ndiye chanda cha Mungu atatutoa katika mikandamizo ya aina yoyote ile                            

Kidole cha Mungu Katika mlima wa Sinai.

Eneo lingine ambapo tunaona maandiko yakitaja chanda cha Mungu ni katika Mlima wa Sinai wakati Mungu alipokuwa anataka kumpa Musa Amri na sharia zake ili awafundishe watu wake, wakati Amri Kumi za Msingi zilipokuwa zinaandikwa tunaelezwa kuwa amri hizo ziliandikwa kwa kidole cha Mungu yaani Chanda cha Mungu

Kutoka 31:18 “Hapo BWANA alipokuwa amekwisha zungumza na Musa katika mlima wa Sinai, akampa hizo mbao mbili za ushuhuda, mbao mbili za mawe, zilizoandikwa kwa chanda cha Mungu.”

Musa analikumbuka tukio hilo la amri na sharia za Mungu kuandikwa kwa kidole chake wakati alipokuwa anawaandikia kitabu kingine cha kumbukumbu la Torati ona katika

Kumbukumbu la Torati 9:9 -10 “Na hapo nilipokwea mlimani kwenda kuzipokea mbao za mawe, nazo ni mbao za agano Bwana alilofanya nanyi, ndipo nikakaa mle mlimani siku arobaini usiku na mchana; sikula chakula wala kunywa maji. Bwana akanipa zile mbao mbili za mawe zimeandikwa kwa kidole cha Mungu; na juu yake yameandikwa maneno mfano wa yote aliyosema nanyi Bwana mle mlimani toka kati ya moto siku ya mkutano.”  

Haikuwa lazima kuwa labda Mungu aliandika ka ma wanadamu waandikavyo kwa kuwa Mungu ni Roho lakini haipingiki kuwa uwezo wake wa utendaji ROHO MTAKATIFU alisababisha kwa muujiza mkubwa sharia zake za msingi kuwepo katika mawe yale, ni ukweli usiopingika kuwa kama Roho Mtakatifu aliweza kuziandika sharia za Mungu katika mawe hashindwi kuziandika sharia zake katika mioyo yetu neno la Mungu linaeleza wazi kuwa uko wakati ambapo Mungu ataziandika sheria zake katika mioyo yetu  

2 Wakoritho 3:2-3  Ninyi ndinyi barua yetu, iliyoandikwa mioyoni mwetu, inajulikana na kusomwa na watu wote; mnadhihirishwa kwamba mmekuwa barua ya Kristo tuliyoikatibu, iliyoandikwa si kwa wino, bali kwa Roho wa Mungu aliye hai; si katika vibao vya mawe, ila katika vibao ambavyo ni mioyo ya nyama.”  

Unaona Roho Mtakatifu yaani utendaji wa Mungu ulioandika sharia kwa kidole cha Moto katika mlima wa Sinai yu aweza kuandika sheria zake na kuweka mwako wa moto katika mioyo yetu ili tumtii Mungu, tunaweza kusoma mapenzi ya Mungu leo kutoka Moyoni kwa kuelekezwa na kufundishwa na Roho Mtakatifu

1Yohana 3:21-24 “Wapenzi, mioyo yetu isipotuhukumu, tuna ujasiri kwa Mungu; na lo lote tuombalo, twalipokea kwake, kwa kuwa twazishika amri zake, na kuyatenda yapendezayo machoni pake. Na hii ndiyo amri yake, kwamba tuliamini jina la Mwana wake Yesu Kristo, na kupendana sisi kwa sisi, kama alivyotupa amri. Naye azishikaye amri zake hukaa ndani yake yeye naye ndani yake. Na katika hili tunajua ya kuwa anakaa ndani yetu, kwa huyo Roho aliyetupa.”

 Utendaji wa Mungu ndani yetu unaweza kuihuisha sharia ya Mungu ndani yetu na kutugeuza kuwa mfano wa kuigwa kwa kila mtu duniani, hata kama ulimwengu unaweza kuwa umeharibika kwa kiwango gani Roho Mtakatifu ndani yetu atatuongoza na kutuhifadhi na kuionya mioyo yetu na kutuelekeza katika sharia ya Mungu wetu sharia ya kifalme sharia ya Roho wa Uzima kwa sababu hiyo sisi sasa hatuongozwi na sharia ile ya kimwili iletayo mauti bali twaongozwa na sharia ya Roho wa Uzima ulio katika Kristo Yesu.

Warumi 8:1-4Sasa, basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu. Kwa sababu sheria ya Roho wa uzima ule ulio katika Kristo Yesu imeniacha huru, mbali na sheria ya dhambi na mauti. Maana yale yasiyowezekana kwa sheria, kwa vile ilivyokuwa dhaifu kwa sababu ya mwili, Mungu, kwa kumtuma Mwanawe mwenyewe katika mfano wa mwili ulio wa dhambi, na kwa sababu ya dhambi, aliihukumu dhambi katika mwili; ili maagizo ya torati yatimizwe ndani yetu sisi, tusioenenda kwa kufuata mambo ya mwili, bali mambo ya roho.”      

Kidole cha Mungu wakati wa Beltshaza.

Eneo lingine ambapo tunauona utendaji wa Mungu kama Kidole chake ni wakati wa kipindi cha utawala wa mfalme Mpumbavu aliyeitwa Belshaza mfalme huyu hakujua ya kuwa Mungu ndiye anayeweka watu madarakani, yeye aliamuru vyombo vilivyokuwa vimetekwa kutoka Hekalu lililokuwako Yerusalem, na baba yake Mfalme mkuu Nebukadreza ambaye baadaye alimuheshimu sana Mungu wa Israel, lakini Belshaza yeye alikuwa na dharau hakuthamini vyombo vile vya Hekaluni ambavyo kimsingi vilikuwa vimewekwa wakfu, chombo kinapokuwa kimewekwa Wakfu maana yake Roho wa Mungu anakuwa amevitenga na kuviheshimu lakini Beslshaza badala yake yeye aliamua kuvidhalilisha kwa kuvinywea pombe ona katika

Daniel 5:1-4 “Belshaza, mfalme, aliwafanyia wakuu wake elfu karamu kubwa akanywa divai mbele ya elfu hao. Belshaza, alipokuwa akionja ile divai, akaamuru wavilete vile vyombo vya dhahabu na fedha, ambavyo baba yake, Nebukadreza, alivitoa katika hekalu lililokuwako Yerusalemu; ili kwamba mfalme, na wakuu wake, na wake zake, na masuria wake, wapate kuvinywea. Basi wakavileta vile vyombo vya dhahabu, vilivyotolewa katika hekalu la nyumba ya Mungu lililokuwako Yerusalemu; na mfalme na wakuu wake, na wake zake, na masuria wake, wakavinywea. Wakanywa divai, wakaisifu miungu ya dhahabu, na ya fedha, na ya shaba, na ya chuma, na ya mti, na ya mawe.”

Ukweli ni wazi kuwa tukio hili lilimuuzunisha sana Mungu wa Israel, Mungu hawezi kukubali vyombo vyake alivyovoweka wakfu kwa kuvitakasa vitumike kinyume na makusudi ya Mungu aliye hai, wakati tukio hili lililpokuwa likiendelea mfalme aliona katika ukuta kiganja cha mkono kikiandika kwa vidole vya kibinadamu kumtangazia mfalme huyu hukumu yake kwa haraka ona

Daniel 5:5-6 “Saa iyo hiyo vikatokea vidole vya mkono wa mwanadamu, vikaandika katika chokaa ya ukuta wa nyumba ya enzi ya mfalme, mahali palipokikabili kinara; naye mfalme akakiona kitanga cha ule mkono ulioandika. Ndipo uso wa mfalme ukambadilika; fikira zake zikamfadhaisha; viungo vya viuno vyake vikalegea; magoti yake yakagongana.”

 Jambo hili lilikuwa jambo la kutisha sana lugha ya kibiblia hapo VIUNGO VYA VIUNO VYAKE VIKALEGEA ni lugha ya kiungwana kuwa mfalme alijinyea na kujiharishia kwa hofu, tabia mbaya aliyokuwa nayo na dhadhau yake dhidi ya mambo ya Mungu ilikuwa sasa inashughulikiwa na utendaji wa Mungu mwenyewe, vidole hivyo vya Mungu vilikuwa vimentangazia hukumu ya Mungu na hukumu yake ilikuwa ni kifo kwa sababu amevuka mpaka Daniel ambaye ndiye alikuja kuyatafasiri maneno yale alisema

Daniel 5: 22-30 “Na wewe, mwanawe, Ee Belshaza, hukujinyenyekeza moyo wako, ijapokuwa ulijua hayo yote. Bali umejiinua juu ya Bwana wa mbingu; nao wamevileta vyombo vya nyumba yake mbele yako; na wewe, na wakuu wako, na wake zako, na masuria wako, mmevinywea; nawe umeisifu miungu ya fedha na ya dhahabu na ya shaba, na ya chuma, na ya mti, na ya mawe; wasioona, wala kusikia, wala kujua neno lo lote; na Mungu yule, ambaye pumzi yako i mkononi mwake, na njia zako zote ni zake, hukumtukuza. Ndipo kile kitanga cha ule mkono kikaletwa kutoka mbele zake, na maandiko haya yameandikwa. Na maandiko yaliyoandikwa ni haya; MENE, MENE, TEKELI, NA PERESI. Na tafsiri ya maneno haya ni hii; MENE, Mungu ameuhesabu ufalme wako na kuukomesha. TEKELI, umepimwa katika mizani nawe umeonekana kuwa umepunguka. PERESI, ufalme wako umegawanyika, nao wamepewa Wamedi na Waajemi. Ndipo Belshaza akatoa amri, nao wakamvika Danieli mavazi ya rangi ya zambarau, wakatia mkufu wa dhahabu shingoni mwake, wakapiga mbiu kutangaza habari zake, ya kwamba yeye ni mtu wa tatu katika ufalme. Usiku uo huo Belshaza, mfalme wa Wakaldayo, akauawa.”

Ni ukweli usiopingika ya kuwa vidole vile vilikuwa ni vidole vya Mungu wazo hili katika Daniel lilikuwa ni wazo linalofanana kabisa na wazo la kile kidole kilichoandika Sheria za Mungu wakati wa Musa, lakini hapa chanda cha Mungu kinashughulika na mtawala mwenye kiburi na majivuno na dharau kuhusu Maswala ya Mungu, Mungu huwapinga wenye kiburi linapokuja swala la Mtu ana kiburi Roho wa Mungu na utendaji wake unafanya kazi ya kuhukumu na kupinga na wale wanaokataa mambo ya Mungu, wakati mwingine watu wanapingana na watumishi wa Mungu na kufikiri au kudhani kuwa watakuwa salama Mungu hawezi kukubali jambo kama hilo litendeke

Zaburi 105:14-15 “Hakumwacha mtu awaonee, Hata wafalme aliwakemea kwa ajili yao. Akisema, Msiwaguse masihi wangu, Wala msiwadhuru nabii zangu.” Wako watu wanadharau neno la Mungu, wanadharau ibada, wanadharau watumishi wa Mungu, wanadharau wakristo, wanadharau wokovu, wanadharau miujiza, na kila kazi zinazofanywa na Roho Mtakatifu ukweli ni wazi kuwa kidole cha Mungu chanda cha Mungu pia kitahusika katika kuleta hukumu haraka kwa wenye kiburi na majivuno Mungu huwapinga wenye kiburi bali huwapa wanyenyekevu neema.

Kidole cha Mungu na wakati wa Huduma ya Yesu.

Wakati wa Huduma ya Yesu Krito duniani neno chanda cha Mungu linaonekana kutumiwa na Bwana Yesu Kristo mwenyewe, Hii ni baada ya kuwa amemponya kwa muujiza mtu aliyekuwa na pepo bubu na kziwi, Mafarisayo na wapinzani wa Yesu Kristo walikosoa vikali miujiza iliyokuwa ikifanywa na Bwana Yesu na kudai kuwa anatoa pepo na kufanya miujiza kwa nguvu za Belzebuli ona

Mathayo 12:22-24 “Wakati ule akaletewa mtu mwenye pepo, kipofu, naye ni bubu; akamponya, hata yule bubu akanena na kuona. Makutano wote wakashangaa, wakasema, Huyu siye mwana wa Daudi? Lakini Mafarisayo waliposikia, walisema, Huyu hatoi pepo, ila kwa Beelzebuli mkuu wa pepo.”

Katika kuwajibu hoja yao Mafarisayo na wapinzani wa kazi za Mungu Roho Mtakatifu ambaye ndiye nguvu ya utendaji iliyokuwa ikitenda kazi ndani ya Kristo, Yesu alieleza wazi kuwa hakuna ufalme unaweza kujipinga wenyewe na hivyo shetani hawezi kuwatoa mashetani, Bali yeye anayafanya anayoyafanya kwa chanda cha Mungu akimaanisha miujiza yote na kazi zote za utoaji wa pepo ni matokeo ya kazi za Roho Mtakatifu atendaye kazi ndani yake na ndani yetu pia

Luka 11:20 “Lakini, ikiwa mimi natoa pepo kwa kidole cha Mungu, basi ufalme wa Mungu umekwisha kuwajilia.” Mathayo 12:24-28 “Lakini Mafarisayo waliposikia, walisema, Huyu hatoi pepo, ila kwa Beelzebuli mkuu wa pepo. Basi Yesu akijua mawazo yao, akawaambia, Kila ufalme ukifitinika juu ya nafsi yake, hufanyika ukiwa; tena mji au nyumba yo yote ikifitinika juu ya nafsi yake, haitasimama.  Na Shetani akimtoa Shetani, amefitinika juu ya nafsi yake; basi ufalme wake utasimamaje? Na mimi nikitoa pepo kwa Beelzebuli, je! Wana wenu huwatoa kwa nani? Kwa sababu hiyo hao ndio watakaowahukumu. Lakini mimi nikitoa pepo kwa Roho wa Mungu, basi ufalme wa Mungu umekwisha kuwajilia.”

Katika maandiko yote hayo ya injili Yesu anasisitiza kuwa anazifanya kazi za Mungu kwa utendaji wa Mungu ulioko ndani yake chanda cha Mungu, yaani Roho Mtakatifu, hii ndio nguvu ile ile iliyotenda kazi katika muujiza wa kusababisha chawa na ndio nguvu, iliyoandika amri za Mungu katika mbao za mawe, na ndio nguvu iliyoandika hukumu katika ukuta kushughulika na Belshaza, Kidole cha Mungu au chanda cha Mungu ni uweza wa Mungu usio na mipaka ni ngubvu za Mungu ni upako utendao kazi, Hakuna chombo cha kibinadamu kinachoweza kupingana na nguvu za kiungu zitendazo kazi za kiungu, hakuna wachawi wanaweza kushindana na nguvu hizo, hakuna utawala unaweza kupoingana na nguvu hizo, hakuna mwanasayansi anaweza kupinga a na nguvu hizo wala hakuna hekima inayozidi hekima ya Chanda cha Mungu ni chanda cha Mungu ndicho kinachotumika kuponya magonjwa kwa wenye shida za aina mbalimbali na kushughulika na mahitaji yote ya aina binadamu.

Kidole cha Mungu sio tu kinatenda miujiza ya uponyaji, lakini pia kinatangaza rehema na msamaha kwa wenye dhambi na kutukinga na wale waliotukusudia mabaya

Yohana 8:3-8Waandishi na Mafarisayo wakamletea mwanamke aliyefumaniwa katika uzinzi, wakamweka katikati. Wakamwambia, Mwalimu, mwanamke huyu amefumaniwa alipokuwa akizini. Basi katika torati, Musa alituamuru kuwapiga kwa mawe wanawake namna hii; nawe wasemaje? Nao wakasema neno hilo wakimjaribu, ili wapate sababu ya kumshitaki. Lakini Yesu akainama, akaandika kwa kidole chake katika nchi. Nao walipozidi kumhoji, alijiinua, akawaambia, Yeye asiye na dhambi miongoni mwenu na awe wa kwanza wa kumtupia jiwe. Akainama tena, akaandika kwa kidole chake katika nchi.”

Wakati watu wanapoorodhesha list ya dhambi zetu ili tuhukumiwe na Mungu, kidole cha Mungu kinaweza kunadika rehema kwaajili yetu kinaweza kuandika dhambi ya kila mmoja ya wale wanaotushitaki, kidole cha Mungu kina uwezo wa kubatilisha hati za mashitaka wakati wote Neno la Mungu linapoonesha kidole cha Mungu kimehusika mahali lazima tujue kuwa ni uweza wa Mungu ni utendaji wa Mungu Roho Mtakatifu akiwa kazini. Kamwe hatupaswi kuogopa kitu, wala kuhofia kitu. Wala hatupaswi kuwaogopa wale watupingao na kwanza wanaonywa waache kucheza na chanda cha Mungu! Aidha chanda cha Mungu kinahusika na uumbaji kuonyesha utendaji wa Mungu uliokuwako wakati wa uumbaji ona

Zaburi 8:1-3 “Wewe, MUNGU, Bwana wetu Jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote! Wewe umeuweka utukufu wako mbinguni; Vinywani mwa watoto wachanga na wanyonyao Umeiweka misingi ya nguvu; Kwa sababu yao wanaoshindana nawe; Uwakomeshe adui na mijilipiza kisasi.Nikiziangalia mbingu zako, kazi ya vidole vyako, Mwezi na nyota ulizoziratibisha;”

Hitimisho

Hivi nilivyo na hivyo ulivyo ni matokeo ya kazi yake Mungu wetu, adui zako wakikutisha waambie hivi nilivyo ni chanda cha Mungu, chanda cha Mungu kinaweza kutuelekeza katika sharia yake, katika hukumu zake, katika utendaji wake wa miujiza, katika utendaji wa nguvu zake na uwezo wake dhidi ya wapinzani wetu, wakati wote tunaweza kumkumbusha Mungu ya kuwa tunahitaji kidole chake kihusike katika kila eneo la maisha yetu na kuleta mpenyo kila amahali pale tunahitaji mpenyo

Na Rev. Innocent Samuel Kamote.

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima.