Jumanne, 28 Juni 2016

Birthday iliyonifanya nitumbuliwe na mke wangu!


Week iliyopita nilikuwa na birthday yangu lakini mke wangu, watoto wangu hata wazazi wangu wote hawakunitakia heri ya kuzaliwa.

 Mke wangu mara baada ya kunikuta nimechizika kwenye sofa!
 
Nilienda kazini lakini hakuna hata mfanyakazi hata mmoja aliyenitakia heri ya kuzaliwa, nilipokuwa naingia ktk ofisi yangu katibu muhtasi wangu (secretary) akaniambia "Happy birthday bosi wangu" hapo ndipo nilijihisi wa maalumu (special) mnoo.
 
Akaniomba mchana twende tukapate lunch pamoja! Nilimkubalia na kuona kuwa hakuna maana hata ya kuwaza nyumbani tena, Tulienda na baada ya lunch akanialika nyumbani kwake anakoishi nalo niliona halina shida hata nikikawia kurudi nyumbani haijalishi.
 
Tulienda kwake na tulipoingia kwake akaniambia kwa sauti ya mahaba "Naomba niende chumbani kwa dakika moja narudi sasa hivi"  alisikika akibembeleza kimahaba nilijibu sawa huku nikiwa na mchecheto mno na kiroho kilianza kwenda kwa kasi.

Nilijua wazi kuwa huyu demu atakuwa ameni mind na huenda anakwenda kujiandaa kwa sex na mimi, na nilihisi atarejea akiwa ameondoa suti yake nzuri aliyokuwa amevaa siku hiyo na kwa vyovyote atarejea akiwa katika hali ya kunipa mahaba mazito

Sasa, kutokana na kujawa na mawazo ya kingono nilikuwa tayari nimejiandaa kumpokea kwa mahaba mazito na tayari kujibu shambulizi lolote la kimapenzi mara mara atakaporudi!
 
Alitoka baada ya dakika tano hivi alirejea akiwa amebeba keki ya birthday  Lakini kama haitoshi huku alikuwa ameambatana  na mke wangu, watoto wangu, mama yangu,Msichana wetu wa kazi na baadhi ya rafiki zangu wote wakisema  kwa nguvu sana SUPRISEEE!!!
 
Na nilikuwa nikisubiri katika sofa pale sebuleni NIKIWA NSHAVUA SURUALI NA PEPO LA NGONO LISHENIPANDA!
 
Masikini mie! Mawazo ya Ngono yameniponza! 

Kwa akili zako finyu unadhani nitakuwa nimejitumbua au nimetumbuliwa?
 
Hapa ninapozungumza mwenzenu Sina mke hivi sasa na heshima yangu iko jalalani!.

"Heri wenye Moyo safi maana hao watamuona Mungu" Mathayo 5:8 

Na Kirima Gs Baba God!
Edited by Rev. Kamote Mkuu wa wajenzi Mwenye Hekima!

Hakuna maoni: