Mwanzo 15:1-5. “Baada ya mambo hayo neno la
BWANA likamjia Abramu katika njozi, likinena, Usiogope, Abramu, Mimi ni ngao
yako, na thawabu yako kubwa sana. Abramu akasema, Ee Bwana MUNGU, utanipa nini,
nami naenda zangu hali sina mtoto, na atakayeimiliki nyumba yangu ni huyu
Eliezeri, Mdameski? Abramu akasema, Tazama, hukunipa uzao, na mtu aliyezaliwa
nyumbani mwangu ndiye mrithi wangu. Nalo neno la BWANA likamjia likinena, Huyu
hatakurithi, bali atakayetoka katika viuno vyako ndiye atakayekurithi. Akamleta
nje, akasema, Tazama sasa mbinguni, kazihesabu nyota, kama ukiweza kuzihesabu.
Akamwambia, Ndivyo utakavyokuwa uzao wako.”
Utangulizi:
Katika aya tulizosoma hapo juu,
tunataarifiwa kuwa Mungu alimtembelea Abrahamu katika njozi na kumpa maneno ya
kutia moyo, wakati huu Abrahamu alikuwa hana mtoto bado na umri wake ulikuwa
umeenda sana na mke wake pia alikuwa mzee, na sasa anawaza kuacha urithi wake
kwa Eliezeri mtumishi wake, kimsingi Abrahamu alikuwa amekata tamaa, na Mungu
alikuja kumpasha habari za muhimu sana ambazo zilikuwa zinapita uwezo wa
kufikiri kwake, wakati Abrahamu alikuwa anafikiri juu ya mtoto mmoja tu, Mungu
alikuwa anafikiri uzao mwingi sana kama nyota za angani, Yeye alimleta Abrahamu
nje na kumpa kazi ya kuzihesabu nyota na kisha alimhakikishia kuwa ndivyo
utakavyokuwa uzao wake! Ahadi hii ya kipekee inazungumzia kuzidishwa kusikoweza
kuhesabika, wema na kibali kikubwa sana cha Mungu kwa Abrahamu, na urithi wa
kiroho usio na mipaka na hivyo kama wewe ni mtoto wa Abraham kwa ahadi na kwa imani
maono haya yanaashiria kuwa wewe sio wa kawaida kama unavyoweza kudhani na
Baraka za Mungu kwako hazina mipaka na kuwa hauko duniani kwa hasara, una
ushawishi mkubwa na uwepo wako unachangia kitu Fulani duniani, wewe ni nuru
inayong’aa gizani, umeinuliwa juu sana wewe si wa kawaida, maono haya hayaleti
ujumbe wa uzao tu kwa Abrahamu bali pia yanaleta ujumbe kwetu kuwa sisi ni
watoto wa namna gani katika uhusiano wetu na Mungu ona
1Petro 2:9-10 “Bali ninyi ni mzao mteule,
ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza
fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu;
ninyi mliokuwa kwanza si taifa, bali sasa ni taifa la Mungu; mliokuwa hamkupata
rehema, bali sasa mmepata rehema.”
Wafilipi 2:14-15. “Yatendeni mambo yote
pasipo manung'uniko wala mashindano, mpate kuwa wana wa Mungu wasio na lawama,
wala udanganyifu, wasio na ila kati ya kizazi chenye ukaidi, kilichopotoka;
ambao kati ya hao mnaonekana kuwa kama mianga katika ulimwengu,”
Leo basi tutachukua muda wetu
kujifunza kile Mungu anazungumza na Abrahamu kutuhusu sisi pamoja na wana wa
Abrahamu wengineo na kile ambacho Mungu alikuwa anamaanisha katika ujumbe wake
kwa Abrahamu na kwetu tutajifuza somo hili “Nyota za Abrahamu” kwa kuzingatia vipengele muhimu vitatu
vifuatavyo:-
·
Maana ya
Nyota za Abrahamu
·
Nyota za
Abrahamu
·
Jinsi ya
kuwa nyota za Abrahamu
Maana ya Nyota za Abrahamu.
Mwanzo 15:1-5. “Baada ya mambo hayo neno la
BWANA likamjia Abramu katika njozi, likinena, Usiogope, Abramu, Mimi ni ngao
yako, na thawabu yako kubwa sana. Abramu akasema, Ee Bwana MUNGU, utanipa nini,
nami naenda zangu hali sina mtoto, na atakayeimiliki nyumba yangu ni huyu
Eliezeri, Mdameski? Abramu akasema, Tazama, hukunipa uzao, na mtu aliyezaliwa
nyumbani mwangu ndiye mrithi wangu. Nalo neno la BWANA likamjia likinena, Huyu
hatakurithi, bali atakayetoka katika viuno vyako ndiye atakayekurithi. Akamleta
nje, akasema, Tazama sasa mbinguni, kazihesabu nyota, kama ukiweza kuzihesabu.
Akamwambia, Ndivyo utakavyokuwa uzao wako.”
Ni muhimu kufahamu kuwa asili ya
ndoto hii ambayo Mungu alisema na Abrahamu ina uhusiano mkubwa na watoto wa
Abrahamu wa kiroho zaidi kuliko watoto wa Abrahamu wa kimwili, kumbuka kuwa hii
ilikuwa ni mara nyingine tena zaidi Mungu akizungumza na Abrahamu kuhusu uzao,
hasa kwa sababu ya hali yake ya kutokuwa na watoto, Mungu alizungumza kwa namna
mbili tofauti na ni lazima namna zote mbili tuzielewe vema, anapozungumza na
Abrahamu kuhusu uzao mwingi na uzao wa kimwili au kibaiolojia Mungu anamwambia
Abrahamu kuwa uzao wako utakuwa mwingi kama Mchanga au kama mavumbi ya nchi!
Mwanzo 13:14-18 “BWANA akamwambia Abramu,
alipokwisha kutengana na Lutu, Inua sasa macho yako, ukatazame kutoka hapo
ulipo, upande wa kaskazini, na wa kusini na wa mashariki na wa magharibi;maana
nchi hii yote uionayo, nitakupa wewe na uzao wako hata milele.Na uzao wako
nitaufanya uwe kama mavumbi ya nchi; hata mtu akiweza kuyahesabu mavumbi ya
nchi, uzao wako nao utahesabika. Ondoka, ukatembee katika nchi hii katika
mapana yake, na marefu yake, maana nitakupa wewe nchi hiyo. Basi Abramu
akajongeza hema yake, akaja akakaa kwenye mialoni ya Mamre, nayo ni miti
iliyoko Hebroni, akamjengea BWANA madhabahu huko.”
Hesabu 23:8-10 “Nimlaanije, yeye ambaye
Mungu hakumlaani? Nimshutumuje, yeye ambaye Bwana hakumshutumu? Kutoka kilele
cha majabali namwona; Na kutoka milimani namtazama; Angalia, ni watu wakaao
peke yao, Wala hawatahesabiwa pamoja na mataifa. Ni nani awezaye kufanya idadi
ya mavumbi ya Yakobo, Au kuhesabu robo ya Israeli? Na nife kifo chake mwenye
haki, Na mwisho wangu uwe mfano wa mwisho wake.”
Mwanzo 32:10-12 “mimi sistahili hata kidogo
hizo rehema zote na kweli yote uliyomfanyia mtumwa wako; maana nalivuka mto huo
wa Yordani na fimbo yangu tu, na sasa nimekuwa matuo mawili.Uniokoe sasa na
mkono wa ndugu yangu, mkono wa Esau, maana mimi namwogopa, asije akanipiga, na
mama pamoja na wana. Nawe ulisema, Hakika nitakutendea mema, nami nitafanya
uzao wako uwe kama mchanga wa bahari, usiohesabika kwa kuwa mwingi.”
Mungu anazungumza na Abrahamu
katika fungu hili akumuahidi watoto wa mwilini, wale watakaoirithi nchi pale
mashariki ya kati, watoto hawa wanawakilishwa na mavumbi ya nchi, mchanga au
mchanga wa bahari, na hapo katika lugha za kinabii wanazungumziwa watoto wa
Abrahamu wa kimwili wa kidunia wanaweza
kuwa Wayahudi na Waarabu wa kawaida wasiookoka, kwa hiyo tunafunuliwa hapa
katika maandiko kuwa Abrahamu ana watoto wa aina mbili wa mwilini na watoto wa
kiroho, au waliozaliwa kwa mwili na wale waliozaliwa kwa Ahadi, tunafahamu kuwa
baada ya kifo cha Sara Abraham alikuwa na watoto wengine kupitia Ketura ambao
ni Zimran. Yokshan, Medani, Midiani
Ishbaki na Shua ambao wengi wanaunda falme za kiarabu mashariki ya kati
hata hivyo Ishamel na Isaka ndio wanaotumika zaidi kitheolojia kutufunza watoto
hao wa aina mbili wa Abrahamu, yaani mmoja wa mwilini na mwingine wa ahadi,
mmoja wa mjakazi na mwingine wa Muungwana, sasa hawa wanawakilishwa na mavumbi
na nyota, mavumbi ni wale wa mwilini na Nyota ni wale wa Rohoni, au wa ahadi.
Wagalatia 4:22-23 “Kwa maana imeandikwa ya
kuwa, Ibrahimu alikuwa na wana wawili mmoja kwa mjakazi, na mmoja kwa
mwungwana. Lakini yule wa mjakazi alizaliwa kwa mwili, yule wa mwungwana kwa
ahadi.”
Kwa hiyo maana ya maono ya nyota
za Abrahamu hapo, wanazungumziwa watoto wa kiroho wa Abrahamu wana wa ahadi,
wale wanaomwamini Mungu kama Abrahamu alivyomwamini Mungu akahesabiwa kuwa na
haki, hawa ni wale waliookoka waliomwamini Yesu kama Bwana na mwokozi kutoka
kila mahali duniani wawe ni Wayahudi au Wayunani vyovyote kama wamemuamini
Bwana Yesu kwa imani hao ni wana wa Ibrahimu wanaotajwa kama nyota
Wagalatia 3:6-9 “Kama vile Ibrahimu
alivyomwamini Mungu akahesabiwa haki.Fahamuni basi, ya kuwa wale walio wa imani,
hao ndio wana wa Ibrahimu.Na andiko, kwa vile lilivyoona tangu zamani kwamba Mungu
atawahesabia haki Mataifa kwa imani, lilimhubiri Ibrahimu habari njema zamani,
kusema, Katika wewe Mataifa yote watabarikiwa. Basi hao walio wa imani
hubarikiwa pamoja na Ibrahimu aliyekuwa mwenye imani.”
Kwa hiyo Mungu anapozungumza na
Abrahamu kwa habari ya watoto wa Mwilini anamuahidi uzao kama mavumbi ya nchi
na anapozungumza naye kuhusu watoto wa kiroho anazungumza na Abrahamu kwa ahadi
ya kuhesabia nyota, kwa hiyo nyota za Abrahamu ni watoto wake wa kiroho yaani
wewe na mimi tuliookoka tulio mwamini Yesu na kuhesabiwa haki kwa imani sisi
ndio “Nyota za Abrahamu” kwa hiyo
katika ahadi ya uzao kwa Ibrahimu kumbuka kuna uzao kama nyota za angani na
uzao kama mchanga wa bahari au mavumbi ya nchi hii inatofautisha watoto wa mwilini
na watoto wa rohoni wa Ibrahimu mwenye
kusikia na asikie! Mungu anaahidi kuwabariki watoto hao wote
Mwanzo 22:16-18. “akasema, Nimeapa kwa
nafsi yangu asema BWANA, kwa kuwa umetenda neno hili, wala hukunizuilia mwanao,
mwanao wa pekee, katika kubariki nitakubariki, na katika kuzidisha nitauzidisha
uzao wako KAMA NYOTA ZA MBINGUNI, na KAMA MCHANGA ULIOKO PWANI; na uzao wako
utamiliki mlango wa adui zao; na katika uzao wako mataifa yote ya dunia
watajibarikia; kwa sababu umetii sauti yangu.”
Nyota za Abrahamu.
Mwanzo 15:1-5. “Baada ya mambo hayo neno la
BWANA likamjia Abramu katika njozi, likinena, Usiogope, Abramu, Mimi ni ngao
yako, na thawabu yako kubwa sana. Abramu akasema, Ee Bwana MUNGU, utanipa nini,
nami naenda zangu hali sina mtoto, na atakayeimiliki nyumba yangu ni huyu
Eliezeri, Mdameski? Abramu akasema, Tazama, hukunipa uzao, na mtu aliyezaliwa
nyumbani mwangu ndiye mrithi wangu. Nalo neno la BWANA likamjia likinena, Huyu
hatakurithi, bali atakayetoka katika viuno vyako ndiye atakayekurithi. Akamleta
nje, akasema, Tazama sasa mbinguni, kazihesabu nyota, kama ukiweza kuzihesabu.
Akamwambia, Ndivyo utakavyokuwa uzao wako.”
Kimsingi katika maono haya Mungu
alikuwa anafanya agano na Abrahamu kuwa atakuwa na watoto wa agano au watoto wa
ahadi, au watoto wa imani ambao watakuwa na uwezo mkubwa sana na wenye Baraka
za kudumu, watakuwa ni watoto ambao hawawezi kueleweka kwa hesabu za
kibinadamu, watakuwa na ushawishi mkubwa duniani, watatoa muelekeo, wataipa
dunia nuru, watatofautishwa na giza, wao hawatakuwa wa kawaida, wasioweza
kuwekewa mipaka, wasiohesabika, watoto hao ni sisi na uweza wao unaelezewa
katika maandiko kwa njia ya kipeke
1. Ni watoto wa Imani – Abrahamu alikuwa
katika mashaka makubwa sana , umri unaenda mkewe amezeeka na anawasiwasi kuhusu
warithi wake, Lakini kwa Mungu hiyo haikuwa shida alikuwa amekusudia kumpa
Abrahamu watoto wa aina zote watoto wa mwilini na watoto wa rohoni na wote
wangekuwa wengi sana wa mwilini kama mchanga wa bahari na wa kiroho au wa Imani
kama nyota za mbinguni ona:-
Mwanzo
22:16-18. “akasema, Nimeapa kwa nafsi yangu asema
BWANA, kwa kuwa umetenda neno hili, wala hukunizuilia mwanao, mwanao wa
pekee,katika kubariki nitakubariki, na katika kuzidisha nitauzidisha uzao wako
KAMA NYOTA ZA MBINGUNI, na KAMA MCHANGA ULIOKO PWANI; na uzao wako utamiliki
mlango wa adui zao; na katika uzao wako mataifa yote ya dunia watajibarikia;
kwa sababu umetii sauti yangu.”
Watoto wanaofananishwa na Nyota za mbinguni ni watoto
wa kiroho ni watoto wa Imani, hawa sio wale wanaozaliwa kwa damu na nyama bali
ni wale wanaozaliwa kwa imani wale waliomwamini Mungu kama Ibrahimu aliyomwamini
Mungu na kuhesabiwa kuwa haki.
Wagalatia 3:6-9
“Kama vile Ibrahimu alivyomwamini Mungu akahesabiwa
haki.Fahamuni basi, ya kuwa wale walio wa imani, hao ndio wana wa Ibrahimu.Na
andiko, kwa vile lilivyoona tangu zamani kwamba Mungu atawahesabia haki Mataifa
kwa imani, lilimhubiri Ibrahimu habari njema zamani, kusema, Katika wewe
Mataifa yote watabarikiwa.Basi hao walio wa imani hubarikiwa pamoja na Ibrahimu
aliyekuwa mwenye imani.”
2. Ni watoto wasio na mipaka - Akamleta
nje, akasema, Tazama sasa mbinguni, kazihesabu nyota, kama ukiweza kuzihesabu.
Akamwambia, Ndivyo utakavyokuwa uzao wako, Mungu alimtoa Abrahamu nje, ilikuwa
nje ya hema yake, ilikuwa nje ya kuta za nyumba, ilikuwa nje ya dunia, ilikuwa nje ya mipaka ya kimazingira, ilikuwa
nje ya fikra finyu, inayoishia kwenye anga la dunia, akamwangalisha juu,
alimtazamisha mbinguni akamuamuru ahesabie nyota kama ataweza akamwambia ndivyo
utakavyokuwa uzao wako, Mungu alikuwa anasema na Abrahamu kuwa wazao wake Nyota za Abrahamu hawatakuwa na mipaka,
wala hawawezi kuhesabiwa kwa hesabu za kidunia wala za kibinadamu, mtu yeyote
anayetaka kuangalia mambo kwa upana haangalii mambo ya duniani pekee,
anaangalia yaliyo juu, watoto wa Abrahamu au nyota za Abrahamu huangalia mambo
kwa upana, wanaona mbali, hawaangalii vya muda wanaaangalia vya milele,
hawafikri yaliyo katika nchi pekee wanafikiri yaliyo juu, huwezi kuwawekea
mipaka watu wenye mtazamo unaozidi mtazamo wa kidunia, nyota hazikai katika
anga hili nyota zinakaa mbali ziko juu sana na ni kubwa mno
Wakolosai 3:1-2
“Basi mkiwa mmefufuliwa pamoja na Kristo,
yatafuteni yaliyo juu Kristo aliko, ameketi mkono wa kuume wa Mungu. Yafikirini
yaliyo juu, siyo yaliyo katika nchi.”
2Wakorintho
4:16-18. “Kwa hiyo hatulegei; bali ijapokuwa utu
wetu wa nje unachakaa, lakini utu wetu wa ndani unafanywa upya siku kwa siku.
Maana dhiki yetu nyepesi, iliyo ya muda wa kitambo tu, yatufanyia utukufu wa
milele uzidio kuwa mwingi sana; tusiviangalie vinavyoonekana, bali
visivyoonekana. Kwa maana vinavyoonekana ni vya muda tu; bali visivyoonekana ni
vya milele.”
3. Ni watoto wenye wito wa mbinguni – Nyota
za Abrahamu ni watoto wa Imani wa Ibrahimu ambao wameitwa na Mungu kwaajili ya
wito mkuu wa Mungu wa maisha yasiyokuwa ya kawaida kusudi lao si la kidunia
kusudi lao ni la kimbingu, ni watu ambao wenyeji wao uko mbinguni wao wako
ulimwenguni lakini sio wa ulimwengu huu,
Waebrania
3:1-2. “Kwa hiyo, ndugu watakatifu, wenye
kuushiriki mwito wa mbinguni, mtafakarini sana Mtume na Kuhani Mkuu wa maungamo
yetu, Yesu, aliyekuwa mwaminifu kwake yeye aliyemweka, kama Musa naye
alivyokuwa, katika nyumba yote ya Mungu.”
Wafilipi 3:20-21
“Kwa maana sisi, wenyeji wetu uko mbinguni; kutoka
huko tena tunamtazamia Mwokozi, Bwana Yesu Kristo; atakayeubadili mwili wetu wa
unyonge, upate kufanana na mwili wake wa utukufu, kwa uweza ule ambao kwa huo
aweza hata kuvitiisha vitu vyote viwe chini yake.”
Yohana 15:18-19.
“Iwapo ulimwengu ukiwachukia, mwajua ya kuwa
umenichukia mimi kabla ya kuwachukia ninyi. Kama mngekuwa wa ulimwengu,
ulimwengu ungewapenda walio wake; lakini kwa kuwa ninyi si wa ulimwengu, bali
mimi naliwachagua katika ulimwengu, kwa sababu hiyo ulimwengu huwachukia.”
4. Ni watoto wenye hekima isiyo ya dunia hii –
Watoto wa Abrahamu au nyota za Abrahamu ni wenye kutoa muongozo. Wanatoa nuru
na wako tofauti na wana wa giza, tofauti na wana siasa na watawala wa dunia hii
hekima waliyonayo wanaitumia kuwavuta wengi na kuwaongoza katika kuishi maisha
ya haki, Nyota zinaashiria ushawishi wenye manufaa, zinaashiria uwezo wa juu wa
kimtazamo, mawazo mapana na hekima ya hali ya juu, hekima isiyokuwa ya
kawaida, isiyo ya duania hii, hekima
iliyohifadhiwa kwaajili yetu tu
Daniel 12:3 “Na walio na hekima watang'aa kama mwangaza wa anga; na
hao waongozao wengi kutenda haki watang'aa kama nyota milele na milele.”
1Wakorintho
2:6-7 “Walakini iko hekima tusemayo kati ya
wakamilifu; ila si hekima ya dunia hii, wala ya hao wanaoitawala dunia hii,
wanaobatilika; bali twanena hekima ya Mungu katika siri, ile hekima
iliyofichwa, ambayo Mungu aliiazimu tangu milele, kwa utukufu wetu; “
Yakobo 3:15-17
“Hekima hiyo siyo ile ishukayo kutoka juu, bali ni
ya dunia, ya tabia ya kibinadamu, na Shetani. Maana hapo palipo wivu na ugomvi
ndipo palipo machafuko, na kila tendo baya. Lakini hekima itokayo juu, kwanza
ni safi, tena ni ya amani, ya upole, tayari kusikiliza maneno ya watu, imejaa
rehema na matunda mema, haina fitina, haina unafiki.”
5. Ni watoto wa Nuru – Nyota zina sifa
maalumu na sifa mojawapo ni kung’aa gizani, na hivyo kuziwezesha kung’aa usiku
zadi wakati dunia ikiwa giza, dunia inapokuwa imeharibiwa na giza la dhambi,
giza la kutokuyajua mapenzi ya Mungu, giza la kutokuona mbele, giza la
kutokumfahamu Mungu watoto wa Abrahamu ambao ni nyota huiangaza Dunia hawa ni
wana wa Nuru na kamwe sio wana wa giza, kazi yao ni kuleta ufumbuzi, ni
kuiangazia dunia isiwe na ukiwa, isiwe na giza, isipoteze ladha na isiwe yenye kutisha
Mathayo 5:14-16
“Ninyi ni nuru ya ulimwengu. Mji hauwezi kusitirika
ukiwa juu ya mlima. Wala watu hawawashi taa na kuiweka chini ya pishi, bali juu
ya kiango; nayo yawaangaza wote waliomo nyumbani.Vivyo hivyo nuru yenu na iangaze
mbele ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye
mbinguni.”
1Wathesalonike
5:4-5 “Bali ninyi, ndugu, hammo gizani, hata siku
ile iwapate kama mwivi. Kwa kuwa ninyi nyote mmekuwa wana wa nuru, na wana wa
mchana; sisi si wa usiku, wala wa giza.”
6. Ni watoto wenye uwezo wa kutangaza
fadhili/utukufu wa Mungu – Nyota za Abrahamu maisha yao ni ya ushindi na
ushuhuda, tabia zao na matendo yao humtukuza Mungu, na shuhuda zao zinatangaza
fadhili za Mungu, Kama jinsi maandiko yasemavyo kuwa moja ya kazi za anga au
mbingu ni kuhubiri utukufu wa Mungu hivyo ndivyo uzao wa Abrahamu yaani nyota
za Abrahamu hutangaza fadhili na utukufu wa Mungu
Zaburi 19:1-4 “Mbingu zauhubiri utukufu wa Mungu, Na anga laitangaza
kazi ya mikono yake. Mchana husemezana na mchana, Usiku hutolea usiku
maarifa.Hakuna lugha wala maneno, Sauti yao haisikilikani. Sauti yao imeenea
duniani mwote, Na maneno yao hata miisho ya ulimwengu. Katika hizo ameliwekea
jua hema,”
1Petro 2:9-10 “Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa
takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye
aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu; ninyi mliokuwa
kwanza si taifa, bali sasa ni taifa la Mungu; mliokuwa hamkupata rehema, bali sasa
mmepata rehema.”
7. Ni watoto wasioweza kurogeka wala kulaanika
– Nyota za Abrahamu ni watoto waliobarikiwa ambao nguvu za giza, uchawi na
waganga hauwawezi, wao wanalindwa na nguvu za Mungu awaye yote atakayejaribu
kufanya lolote la kichawi au la kiganga kwa lengo la kuwadhuru watoto wa
Abrahamu wa Imani atashughulikiwa na Mungu mwenyewe. Watoto wa duniani wanaweza
kurogwa kwa kuchukua Mchanga wa mbinguni utachukua nini huwezo kuchota nyao za
watoto wa mbinguni, huwezi kufukia kitu kwao ukatoboa hawarogeki!
Hesabu 23:7-9 “Akatunga mithali yake, akasema, Balaki amenileta kutoka
Aramu, Mfalme wa Moabu kutoka milima ya mashariki, Njoo! Unilaanie Yakobo,
Njoo! Unishutumie Israeli. Nimlaanije, yeye ambaye Mungu hakumlaani?
Nimshutumuje, yeye ambaye Bwana hakumshutumu? Kutoka kilele cha majabali
namwona; Na kutoka milimani namtazama; Angalia, ni watu wakaao peke yao, Wala
hawatahesabiwa pamoja na mataifa.”
Hesabu 23:18-24
“Naye akatunga mithali yake, akasema, Ondoka
Balaki, ukasikilize; Nisikilize, Ee mwana wa Sipori; Mungu si mtu, aseme uongo;
Wala si mwanadamu, ajute; Iwapo amesema, hatalitenda? Iwapo amenena,
hatalifikiliza? Tazama, nimepewa amri kubariki, Yeye amebariki, nami siwezi
kulitangua. Hakutazama uovu katika Yakobo, Wala hakuona ukaidi katika Israeli.
Bwana, Mungu wake, yu pamoja naye, Na sauti kuu ya mfalme i katikati yao. Mungu
amewaleta kutoka Misri, Naye ana nguvu kama nguvu za nyati. Hakika hapana
uchawi juu ya Yakobo, Wala hapana uganga juu ya Israeli. Sasa habari za Yakobo
na Israeli zitasemwa, Ni mambo gani aliyoyatenda Mungu! Tazama, watu hawa
wanaondoka kama simba mke, Na kama simba anajiinua nafsi yake, Hatalala hata
atakapokula mawindo, Na kunywa damu yao waliouawa.”
8. Watawashinda adui zao – Hakuna adui
atakayeweza kusimama kinyume na Nyota za Abrahamu, Neno la Mungu la kinabii
limeahidi ushindi dhidi ya adui wote wanaowazunguka watoto wa Abrahamu,
watakata pembe za adui zao, watawavunja
vunja wana wote wa ghasia, Uzao huu utamiliki mlango wa adui zao
Hesabu 24:16-19
“Asema, yeye asikiaye maneno ya Mungu, Na kuyajua
maarifa yake Aliye Juu. Yeye aonaye maono ya Mwenyezi, Akianguka kifudifudi,
amefumbuliwa macho, Namwona, lakini si sasa; Namtazama, lakini si karibu; Nyota
itatokea katika Yakobo Na fimbo ya enzi itainuka katika Israeli; Nayo
itazipiga-piga pembe za Moabu, Na kuwavunja-vunja wana wote wa ghasia. Na Edomu
itakuwa milki Seiri pia itakuwa milki, waliokuwa adui zake; Israeli
watakapotenda kwa ushujaa.Mwenye kutawala atakuja toka Yakobo, Atawaangamiza
watakaobaki mjini.”
Mwanzo 22:16-18. “akasema, Nimeapa kwa nafsi yangu asema BWANA, kwa kuwa umetenda neno hili, wala hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee, katika kubariki nitakubariki, na katika kuzidisha nitauzidisha uzao wako KAMA NYOTA ZA MBINGUNI, na KAMA MCHANGA ULIOKO PWANI; na uzao wako utamiliki mlango wa adui zao; na katika uzao wako mataifa yote ya dunia watajibarikia; kwa sababu umetii sauti yangu.”
Jinsi ya kuwa nyota za Abrahamu
Ni muhimu kuwa na uelewa na
ufahamu kuwa Nyota za Abrahamu sio swala la ndoto na maono ya kawaida Nyota za
Abrahamu leo ni mimi na wewe, Nyota za Abrahamu ni wana wa angani ni wana wa
ahadi, Abrahamu ana wana wa aina mbili Nyota na Vumbi, wewe mwenyewe unaweza
kuchagua kuwa mwana wa Abrahamu kwa maisha yako unaishije? Unaangaza au
umefichwa, umefufuka au umezikwa, ni wa chini au ni wa juu wewe ni wa ulimwengu
huu au wewe sio wa ulimwengu huu, wewe ni mwana wa Nuru au u mwana wa giza unaishi kwa Imani au kwa kuona? una mchango
duniani kwa kuangaza au huangazi, kama wewe ni mwana wa Abrahamu Nyota za Abrahamu
utaenenda kwa Imani na sio kwa kuona, pale ambapo dunia inasema haiwezekani
watu wa Mungu wanasema inawezekana, wana wa Abrahamu ni watoto wenye Imani,
wanaishi wakimpendeza Mungu kwa Imani, hakuna jambo lenye mipaka Mbinguni,
wakiroga mavumbi ya ardhi sisi haturogeki mpaka upande mbinguni, ukituweka
kwenye giza tunang’aa,. Sisi ni wana wa ahadi ahatukuzaliwa kwa mwili, sisi ni
wa maono ya kimbinguni na sio ya kidunia huwezi kumuwekea mipaka kwa uhuru tulio
nao angani, unataka kuwa mwana wa Abrahamu ambaye ni Nyota hapa duniani uokoke
leo, unataka kuwa Mwana wa Abrahamu mavumbi usiokoke ukanywagwe duniani.
2Wakorintho 5:7-9 “(Maana twaenenda kwa
imani, si kwa kuona.) Lakini tuna moyo mkuu; nasi tunaona ni afadhali
kutokuwamo katika mwili na kukaa pamoja na Bwana. Kwa hiyo, tena, ikiwa tupo
hapa, au ikiwa hatupo hapa, twajitahidi kumpendeza yeye”
Luka 19:8-10 “Zakayo akasimama, akamwambia
Bwana, Tazama, Bwana, nusu ya mali yangu nawapa maskini, na ikiwa
nimenyang'anya mtu kitu kwa hila namrudishia mara nne.Yesu akamwambia, Leo
wokovu umefika nyumbani humu, kwa sababu huyu naye ni mwana wa Ibrahimu. Kwa
kuwa Mwana wa Adamu alikuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea.”
Zakayo alikuwa Myahudi, lakini
alikuwa uzao wa Abrahamu upande wa mavumbi, lakini alipookolewa Yesu alisema
huyu naye ni mwana wa Ibrahimu, ukimkubali Yesu kuanzia leo unakuwa mwana wa
Ibrahimu, ukiendelea kung’ang’ania dini kama mafarisayo unapoteza sifa ya kuwa
mwana wa Ibrahimu, Wayahudi wengi waligeuka kuwa wana wa Ibilisi na wana wa
mavumbi na kamwe hawakuwa nyota ya Abrahamu kwa sababu dini iliwageuza wakawa
na roho mbaya na wauaji, wenye kujihesabia haki na wala hawakutenda mapenzi ya
Mungu unataka kuwa Nyota za Abrahamu toka gizani leo uje nuruni, Mwombe Mungu
uokolewe! Ukiokoka na kumwamini Yesu wewe ni nyota!
Yohana 8:39-44 “Wakajibu, wakamwambia, Baba
yetu ndiye Ibrahimu! Yesu akawaambia, Kama mngekuwa watoto wa Ibrahimu,
mngezitenda kazi zake Ibrahimu.Lakini sasa mnatafuta kuniua mimi, mtu ambaye
nimewaambia iliyo kweli, niliyoisikia kwa Mungu. Ibrahimu hakufanya hivyo.
Ninyi mnazitenda kazi za baba yenu. Ndipo walipomwambia, Sisi hatukuzaliwa kwa
zinaa; sisi tunaye Baba mmoja, yaani, Mungu. Yesu akawaambia, Kama Mungu
angekuwa baba yenu, mngenipenda mimi; kwa maana nalitoka kwa Mungu, nami
nimekuja; wala sikuja kwa nafsi yangu, bali yeye ndiye aliyenituma. Mbona
hamyafahamu hayo niyasemayo? Ni kwa sababu ninyi hamwezi kulisikia neno langu.
Ninyi ni wa baba yenu, Ibilisi, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda.
Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna
hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; kwa sababu
yeye ni mwongo, na baba wa huo.”
Wafilipi 2:14-15. “Yatendeni mambo yote
pasipo manung'uniko wala mashindano, mpate kuwa wana wa Mungu wasio na lawama,
wala udanganyifu, wasio na ila kati ya kizazi chenye ukaidi, kilichopotoka;
ambao kati ya hao mnaonekana kuwa kama mianga katika ulimwengu,”
Rev. Innocent Samuel Kamote
Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima!

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni