Jumatano, 2 Machi 2016

Jinsi ya Kuhudumia watu wenye Uhitaji



Leo tutachukua Muda kutafakari namna na jinsi ya kumuhudumia mtu mwenye matatizo, watu wenye matatizo ni kama ile wagonjwa waliolazwa mahospitalini, au waloko majumani, watu waliorudi nyuma na kukata tamaa kwaajili ya wokovu, watu wanaopitia mateso kwaajili ya wokovu watu waliofiwa na kadhalika lengo la kujifnza jinsi ya kuwahudumia ni kwa makusudi ya kuwachukulia mizigo yao ili wote tufike mbinguni Wagalatia 6;2 ,1wakoritho 12;25-27. Tutajifunza somo hili kwa kuzingatia yafuatayo;-

      Huduma ya Masaidiano katika kanisa ni ya muhimu hasa nyakayti hizi za mwisho                 


  •  Jinsi ya kuwafikia watu wenye Matatizo
  • Namna ya kuwahudumia wenye matatizo ya aina mbalimbali.


Jinsi ya kuwahudumia watu wenye Matatizo.
Endapo tunagundua kuwa mwenzetu katika imani anaanza kulegea au amepatwa na tatizo tunapaswa kumsaidia kwa kumpa msaada wa kiroho kwanza  kwa kumlisha neon la Mungu na hatimaye  tutaangalia msaada wowote wa kimwil kulingana natatizo alilonalo  kutokana na neema tuliyonayo 2wakoritho 8;11-12 tutamfuatilia mwenzetu huku tukizingatia mahusiano ya kijinsia  ili injili yetu isitukanwe na kuwa kwazo la kuwafungia wau Ufalme wa Mungu, Tunawaendea watu wenye matatizo kwa upole huku tukiwa kwanza tumewaombea kwa uzito mkubwa Wakolosai 1;9,4;2-3 tutamomba Mungu ili kwamba atupe hekima ya kuwaendea na kuzungumza nao na kasha ndipo tutaanza kutoa msaada wa kiroho na kimwili kama Mungu atakavyotuongoza.

Namna ya kuwahudumia wenye matatizo ya aina mbalimbali.
1.       Jinsi ya kuwahudumia wagonjwa wa aina mbalimbali
Tuwajulishe kuwa Mungu hajawaacha kwa sababu wanafanya mapenzi ya Mungu Zaburi 37;25 Ayubu alipokuwa katika hali mbaya ya kutisha aliyacheka maangamizo na njaa kwa sababu alijua  kuwa hii ilikuwa njia ya Mungu kumpa daraja la juu  na ndivyo ilivyokuwa Ayubu 42;10-17 Tuwatie Moyo na kuwaambia Bwana aliyachukua magonjwa yetu na udhaifu wa kila namna  kwa hiyo wajipe moyo kwa kuwa Mungu anakwenda kuwafungua Isaya 53;4-5, Mathayo 8;17 Mungu alipomuinua mkwewe Petro alipokuwa amelala hoi kitandani atakuinua na wewe katika jina la Yesu Luka 4;38-39 Baada ya kumtia moyo inatupasa kumuombea na kumsaidia shughuli za kimwili.

2.       Jinsi ya kuwahudumia wanaopitia mateso kwaajili ya Wokovu
Kanisa ni lazima litafute kila namna ya kuwatia moyo kwa neno la Mungu wale wanaopitia mateso ni muhimu kwao kufahamu kuwa tukiteswa kwaajili ya Kristo tuna heri maana tutapokea taji ya Uzima tukivumilia mpaka mwisho 1Petro 4; 12-16 Yakobo 1; 12 Ni muhimu kufahamu kuwa tukimfuata Yesu Kristo ambaye ndiye kielelzo chetu tutachukiwa, kuudhiwa na kudharauliwa pia tutaeswa na kuonewa na kunenwa mabaya  hii sio ajabu hiki ni kipimo tu kinachoashiria kuwa sasa tuko na Mungu na kuwa shetani ameudhiwa na uamuzi wetu hasa  kwa msingi huio tusizimie roho  na kumpa tena shetani ushindi kwa kukata tamaa kwa sababu ya mateso haya ya muda mfupi lakini tuitegemee neema na kumshinda shetani kwa kuitegemea neema na kuendelea katika imani  1Petro2;19-25 waebrania 2;18,Warumi 8;35-39 wafilipi 1;29-30

3.       Jinsi ya kuwahudumia watu waliofwa kwa ujumla
Tuwatie moyo na kuwafariji kwa maandiko kama haya 1Wathesalonike 4; 13-17 Kutoka katika uso wa dunia sio kitu cha ajabu ni njia ya Mungu ya kumpeleka mtu pazuri zaidi akiwa amejiandaa  hapa hapa duniani Mwanzo 3;19 Duniani sisi wote ni wapitaji tu Ndio maana tunapaswa kujiandaa kwa makao ya milele na Mungu Amosi 4;12 1Petro 2;11.

4.       Jinsi ya kuwatia moyo waliokata tamaa kimaisha.
Ni muhimu kuwatia moyo wapendwa wa aina hiyo kwamba wasibabaike wala kufadhaika  na wala wasiogope  maana bwana anasema ujapopita katika  maji mengi hayata kugharikisha  kwa kuwa Bwana atakuwa pamoja nawe Isaya 43;1-5,41;10 Mungu hawezi kukusahau Isaya 49;14-16 kinachotakiwa ni kutokujisumbukia  nafsi zetu maana Bwana anajua kuwa tuna haja  na yote hayo ila anatpa msingi wa kutafuta kwanza ufalme wa ungu na kisha haja zetu zijulikane na Mungu  na tumuombe Mungu bila kukata tama Bwana ataushindia  Luka 12; 21-31 Wafilipi 4;4-7

5.       Jinai ya kuwahudumia waliorudi nyuma.
Mtu anaporudi nyuma anapaswa kuendewa kwa upole na Upendo na kumwambia kuwa bado Mungu anakupenda na anahitaji ukawe naye baadaye Mbingun kwenye raha ya milele na milele, Petro aliporudi nyuma kwa kumkana mara tatu alitubu kwa majonzi na kutambua kuwa shetani alimdanganya, Bwana alipomtokea tena na kumtumia sana kwaajili ya ufalme wake, wewe nawe kumbuka wapi ulikoanguka ukatubu na kuurudia upendo wako wa kwanza Ezekiel 3;19-20,21;18;20-22 tunapochukua mzigo mkubwa  kuwafuatilia wale waliorudi nyuma sisi tunajiwekea Baraka  na kufutiwa wingi wa dhambi Yakobo 5; 19-20 Lakini tuwe macho ili kwamba adui naye asije akatutupata kwa kutumia huyu aliyerudi nyuma na kututeka Wagalatia 6;1-2. 

6.       Jinsi ya kuwatia moyo walio wavivu wa Ibada
Ni muhimu kutumuia maandiko kama Luka 12;16-21,Yakobo 4;13-16 na Mathayo 16;26-27 kwa kusudi la kuwakumbusha umuhimu wa kuhudhuria Ibada hili ni jambo la msingi linalodhihirisha uhai wa kiroho wa kila Mwamini.

Agizo la Kujihadhari na Manabii wa Uongo!



Yesu Kristo alifundisha katika mafundisho yake umuhimu wa kujihadhari na Manabii wa uongo Mathayo 7;15 kwa kukosa kuwa na ufahamu katika neno la Mungu tunaweza kujikuta tunachukuliwa na uongo wa shetani kwa kuikimbia kweli na kwenda mbali kabisa na neno la Mungu hata hivyo namna ya kuwatambua manabii wa uongo ni jambo linaloweza kukuchanganya kama hutakuwa na ufahamu kuhusu Neno la Mungu ni kwa msingi huo sasa leo tutachukua Muda  kujifunza neno la Mungu linasema nini uhusu manabii wa uongo ili tupate kujihadahri sawasawa na neno la Mungu.tutajifunza somo hili kwa kuzingatia vipengele viwili vifuatavyo;-


Muhubiri huyu hapaswi kugusa chini wakati wa mahubiri hushinda juu ya migongo ya washirika

§  Maana ya neno Nabii
§  Jinsi ya kuwatambua manabii wa uongo.

Maana ya neno Nabii.
Neno nabii lmejitokeza zaidi ya mara mia 300 katika agano la kale na mara 100 katika agano jipya katika agano la kale neno hili lilitumika kama Navi au Nabi ambalo maana yake mtu mwenye uwezo wa kupokea neno la Mungu na kulifikisha kwa watu, walifanya kazi ya kuzungumza mambo ya Mungu kwa wakati ulioko, uliopita na ujao, kwa ufupi leo tunaweza kusema kuwa manabii ni wanenaji kwa niaba ya Mungu au  watumishi wa Mungu wanaohubiri yale yaliyo haki na yale ambayo sio haki mbele za Mungu hao ndio manabii wa kweli Waefeso 4;11 nabii wa kweli kwa kawaida anakuwa na sifa kuu mbili A. atafundisha maneno ya kweli ya Mungu bila kuchuja kwa namna yoyote ile bila kujali cheo au sifa ya mtu na atafundisha njia ya Mungu kwa Usahii bila upendeleo Yohana 3;34, Mathayo 22;16, Wagalatia 2;4-6.B. Maisha yake yataonyesha matunda ya Kristo na ya Roho Mtakatifu maana Mungu anayemwakilisha ni Mtakatifu kwa hivyo maisha yake yataendana na yale anayoyafundisha  kila siku Matendo 1;1 Warumi 2;21-25 Wagalatia 5;22-25 pale tunapoona sifa izi kuu na nyinginezo sawasawa na neno la Mungu  ndipo tunapoweza kujua kuwa huyu ni nabii wa kweli  tuliyoipokea.

Jinsi ya kuwatambua manabii wa uongo.
Maandiko yanatupa mwanga wa kutosha kuweza kuwatambua manabii wa uongo kama anavyo tufundisha Bwana wetu Yesu Kristo. Katika Mathayo 7;15-20 anasema tutawatambua kwa MATUNDA yao matunda ya manabii wa uongo kwa mujibu wa maandiko nikama ifuatavyo;-
a.       Manabii wa uongo hufundisha UONGO na katika maandiko wanaitwa mikia, Kufundisha uongo ni kufundisha yale ambayo hayako kwenye Biblia au yale ambayo Biblia haikumaanisha badala yeke watafundisha hadithi zilizotungwa na wanadamu na katiba zao hata kama ziko kinyume na neno la Mungu linatuonya  kuwa mbali nao katika jina la Yesu, tujihadhari kabisa Isaya 9;15-16, 2Petro 2;1-4.
b.      Manabii wa uongo hukiri kwa vinywa vyao kuwa wanamjua Mungu lakini kwa Matendo yao wanamkana  ni wenye machukizo na uovu wote Tito 1;16 watakuwa ni watu ambao wanashika Biblia au vitabu vya kidini na kwenda huko na huko kuhubiri dini lakini ukiangalia maisha yao ni ya uasherati, Uzinzi, usengenyaji, uongo, ushirikina, fitina, faraka na uadui  haya ni baadhi ya matunda ya mwili Wagalatia 5;22
c.       Manabii wa uongo kamwe hawakiri kuwa Yesu ni mwana wa Mungu ila wanasema ni mwanadamu tu sawa na wengine 1Yohana 4;1-4
d.      Manabii wa uongo hukataa neema ya wokovu iliyokuja kwa mkono wa Yesu Kristo na hufundisha na kuwaambia watu kuwa watafika mbinguni kwa matendo Fulani ya sheria, Nyakati za leo hatuko chini ya sheria ya Musa ili tuko chini ya sheria ya kifalme ya Yesu Kristo ambayo tunawezeshwa na Yesu mwenyewe Tito 2;11-12 Wagalatia 5;4 2;16 Yohana 1;16-17, 2Petro 2;1-2.
e.      Manabii wa uongo huwaambia watu amani tu hata kama yale waliyoyafanya yako kinyume na neno la Mungu, manabii hao kusudi lao au mungu wao hasa ni tumbo Yeremia 23;16-17 Warumi 16;17-18 wafilipi 3;18-19. Fedha ndio lengo lau kuu wanatajirika kupitia washirika masikini ambao labda wangehitaji msaada kutoka kwao.
f.        Manabii wa uongo watasifiwa na watu wote na kutakuwa hakuna upinzani wowote wa kunenwa vibaya au vinginevyo. Nabii wa kweli kunakuwa na mchanganyo wa utukufu na aibu na kunenwa mabaya  Luka 6;20-26 angalia sifa za nabii wa kweli 2Wakoritho 6;4-10,Yohana 7;20,8:48.
g.       Manabii wa uongo hawaongozi na neno la Mungu ila wanaongozwa na mapokeo ya kibinadamu tu ndoto na maono ya uongo Wakolosai 2; 18-19, Marko 7;6-7,13. n.k.
Ni muhimu basi kujihadhari na kutokuwakubali walete upuuzi wao au kuanza kubishana nao 2Timotheo 2; 14, 23-24, waefeso 5;4 Mungu atupe neema ya kutokukubali kupotea. Lazima watumishi wenye kudai kuwa wanaihubiri kweli waishi sawa na injili, tunafahamu kuwa yako matatizo ya kibinadamu na udhaifu wa kibinadamu lakini manabii wa uongo kwa makusudi kabisa lengo lao ni kujitajirisha wao wenyewe wengine kuwaona ni gharama kubwa sana kuliko kumuona Yesu, washirika wanateseka mpaka wakiponyoka katika kanisa lao wanajisikia Huru Mungu awasaidie watu wake walioteswa na kundi kubwa la manabii wenye kujikinai na kutabiri uongo

Maisha ya Maombi !



Neno La Msingi 1Wathesalonike 5;17 “Ombeni Bila kukoma” Pamoja na kuwa Mstari huu tunaoutafakari una maneno matatu tu Ombeni Bila kukoma  ni muhimu kufahamu kuwa una uzito mkubwa sana  unaoelezea namna maisha ya mkristo au mtu aliyeokoka  anavyopaswa kuwa  yaani maisha ya mkristo ni maisha ya kuomba bila kukoma au kuacha. Tutajifunza somo hili kwa kuzingatia vipengele viwili vifuatavyo;-

Kuacha kuomba ni kuacha Ukristo
§  Umuhimu wa maombi kwa Mkristo.
§  Kielelezo cha Bwana Yesu 

Umuhimu wa maombi kwa Mkristo.
Mkristo akiacha kuomba anakuwa ameacha kuishi maisha ya kikristo, Kuacha kuomba ni kuacha ukristo, wako watu wengine ambao wanajiona wa kiroho sana na kwa sababu hiyo hawaoni umuhimu wa kuomba tena Yesu Kristo alikuwa wa Kiroho kuliko mtu awaye yote  alikuwa ni mtume mkuu na kuhani mkuu Waebrania 3;1 alikuwa pia ni Nabii mkuu Luka 7;16 alikuwa mwinjilisti mkuu ambaye watu walikuwa wanakimbilia na kutafuta mahubiri yake hata pale ambapo alitaka kupumzika, na Katika maombezi yake hakuna mgonjwa aliyekuja kwa Yesu asipokee uzima Luka 8;40, Marko 6;30-34 Mathayo 9;35, alikuwa ni mchungaji mkuu Waebania 13;20, alikuwa mwalimu aliyetoka kwa Mungu Yohana 3;2 zaidi ya yote alikuwa mwana wa Mungu  na anaitwa Mungu mkuu Waebania 14;14 Tito 2;13,   Pamoja na kuwa wa kiroho na huduma kubwa kiasi hiki Yesu hakuacha kuomba  naye ametuachia kielelezo.

Kielelezo cha Bwana Yesu.
Bwana yesu alikuwa mwombaji aliishi maisha ya maombi na hakuacha kuomba kila siku Bwana yesu aliomba na kila wakati nafasi ilipopatikana naye ametuachia kielelezo Alfajiri na Mapema  alifanya maombi Marko 1;35, wakati mwingine mchana aliacha huduma za muhimu na kwenda kuomba  Luka 5;15-16, wakati mwingine alikesha usiku kucha  katika kumuomba Mungu Luka 6;12 alijitenga na wanafunzi wake  akapiga magoto akaomba Luka 22;41,aliomba na kulia sana machozi Wabrania 5;7 aliomba wakati Fulani mpaka hari (jasho) lake likawa kama matone ya Damu Luka 22;43-44, Yesu aliishi maisha ya maombi, kama tunataka kutenda kazi alizozitenda na zaidi  kama alivyosema yeye Yohana 4;12 ni muhimu kufahamu kuwa haiwezekani kuzitenda kazi hizo bila ya kuwa waombaji, hatuna budi kuomba  kama Yesu ili kuzifanya kazi hizo ni kumba kwa namna hii ndiko kunakomfanya mtukutumiwa na Mungu kwa kazi za ajabu Mungu hafurahuiwi na mtu awaye yote asiyeishimaisha ya maombi kutokuishi maisha ya maombi so tu ni sawa na kuacha ukristo lakini ni kiburi kwani twaonyesha kuwa tunajitegemea jambo ambalo linamuhuzunisha mno Mungu 2Wakoritho 1;8-9, Pasipo Yesu Kristo sisi hatuwezi kufanya jambo lolote hata kama ni dogo kiasi gani Yohana 15;5 tukiishi maisha ya maombi Mungu anapendezwa na ndiyo shara ya kuwa tunamtegemea Yeye, mara kadhaa tunaonywa kwamba endapo tutaacha kuomba tutajikuta tukiingia majarini lakini kama tukiomba Mungu atatuepusha na majarib hayo Marko 14;38-40, 

Ni muhimu kukumbuka wakati wote kuombeana sisi kwa sisi kila siku Yakobo 5;16 na kuwaombea watakatifu wote  ili wasipepetwe na Ibilisi kama ngano waefeso 6;18 Luka 22;31-32 na pia kuwaombea wenye dhambi ili kwamba Mungu awape wokovu Warumi 10;1 ni muhimu pia kumombea Mchungaji wetu ili apewe usemi na Mungu katika kuubiri na kufundisha na pia ili apete kutumiwa kipekee aanapotuombea 1Wathesalonike 5;25,Waefeso 6;18-19, Matendo 4:29-30.

Dhambi ya kuacha kuwaombea wengine!



1Samuel 12; 23 “Walakini mimi hasha! Nisimtende Bwana dhambi kwa kuacha kuwaombea ninyi” Ni maneno ya nabii aliyeheshimika sana katika Israel ambaye Mungu alipendezwa naye sana Samuel alikuwa na ufunuo ulio sahii machoni kwa Mungu kuwa kutokuwaombea Israel ni dhambi ambayo yeye hangelipenda aifanye aliwaombea Israel. Kwa Msingi huo tutajifunza somo hili kwa kuzingatia vipengele viwili vifuatavyo;-



 Kwa nabii Samuel kutokuwaombea wengine ni dhambi



§  Dhambi ya kuacha kuwaombea wengine
§  Faida za kuwaombea wengine.

Dhambi ya kuacha kuwaombea wengine.
Kutokuwaombea wengine ni dhambi, mbele za Mungu dhambi yoyote ile inaweza kutupelekea kupata hukumu isiyo njema Mafndisho mengi kuusu maombi hayajaundwa katika namna ya mfumo wa kujiombea wenyewe tu angalia mfano Mathayo 6; 9-13, ….Utupe leo riziki yetu, utusamehe makosa yetu…usitutie majaribuni…. Lugha inayotumika katika maombi sio lugha ya kibinafsi yaani unipe leo riziki yangu, unisamehe dhambi zangu…usinitie majaribuni… Ni muhimu kwa kila mtu aliyeokoka kuwa na ufahamu kuwa Mungu hapendezwi na ubinafsi katika maombi anataka tuombeane, hu ni mfano ulio wazi kuwa Yesu alituombea sisi  hata kabla ya kuzaliwa Yohana 17;15-20 Maombi mengi ya wakristo hayajibiwi kwa sababu wanaangalia yetu wenyewe Wafilipi 2;4. Samuel aligundua siri ya ajabu kuwa kuacha kuwaombea wengine ni dhambi ingawa yeye alikuwa kuhani, sisi nasi ni ukuhani mteule, taifa takatifu watu wa milki ya Mungu kwa msingi huo nasi tunaweza kuliitia jina la bwana kwaajili ya wengine.
Faida za kuwaombea wengine.
Tunapouwa na Muda wa kuwaombea wengine tunapata faida kubwa sana katika ulimwengu wa Roho, tunavikwa silaha zote za Mungu pale tunapokumbuka kuwaombea wengine kimwili na Kiroho ni muhimu kufahamu kuwa maombi ambayo ni tishio kwa shetani ni yale yanayolenga  kuujenga ufalme wa Mungu na mapenzi a Mungu ili yatimizwe ndani yetu na mengine yanapaswa kufuata baadaye Waefeso 6;11,18-20 tunapoomba kwa uzito mkubwa siku zote kwaajili ya washirika wenzetu Mungu atatubariki upeo na kutupa ushindi dhidi ya adui yetu shetani Wakolosai 4;2-3 , tunapoomba kwa uzito kwaajili ya Mchungaji wetu Mungu atatubariki upeo na kutupa thawabu warumi 15;30-31,1Wathesalonike 5;25, pia ni muhimu kuomba kwaajili ya Ndugu na jamaa na majirani katika maeneo yetu ili kwamba Mungu awaokoe na ufalme wa Mungu uongezeka kuna tahwabu kubwa Mbinguni Warumi 9;1-5.
Nykati za kanisa la kwanza  kanisa lilikuwa na nguvu kubwa na lilikuwa na mamlaka dhidi ya adui kwa sababu hawakuwa na ubinafsi na kwa sababu hiyi Mungu alifanya mambo ya kutisha na kushangaza Matendo 2;43-47, 5;12-16. Wenzetu nyakati za kanisa la kwanza waliushinda umimi walikubali kuangalia mambo ya wenzao waebrania 10; 32-36 inawezekana bado hatujaona mambo makubwa ya kutisha na kushangaza katika huduma zetu kwa sababu Mungu hakai katika ubinafsi ni muhimu kufahamu kuwa maombi yanayompendeza Mungu ni maombi yanayohusiana na kuwaombea wengine.

Makusudi Ya kuokolewa !



Neno la Msingi Kutoka 10;3. “…………Bwana Mungu wa Waebrania asema hivi……..……Wape watu wangu ruhusa waende zao ili wanitumikie”


 Mungu ametuokoa kwa kusudi la Kumtumikia

§  Makusudi ya kuokolewa.
§  Faida za kumtumikia Mungu.

Makusudi ya kuokolewa.
Ni muhimu kufahamu kuwa mambo yaliyowapata wana wa Israel walipokuwa Misri na kuokolewa kwao hatimaye kuingia kanaani ulikuwa ni mfano kwetu kutuonya sisi tuliofikiwa na miisho ya zamani hizi 1Wakoritho 10;11 moja ya kjambo kubwa tunallojifunza kutka kwao ni uweza wa Mungu wa kuokoa Pamoja na moyo Mgumu wa Farao, ni wazi kuwa sisi nasi tumeokolewa kama ilivyokuwa kwa wana wa Israel Jukumu letu kubwa la kuokolewa kwetu kama ilivyokuwa kwa wana wa Israel ni ili TUMTUMIKIE Bwana  kusudi hili lilitajwa na kurudiwa tena na tena katika maandiko kwa msisitizo mkubwa. Kutoka 4; 22-23, 7; 16, 8;1, 8;20, 9;1, 9;13, 10; 3, 10; 24-26.  Sisi nasi hatuna budi kufahamu kuwa makusudimakubwa ya kuokolewa kwetu ni ili tumtumikie Mungu kama mtu aliyeokolewa haoni furaha ya kumtumikia Mungu ni kwa kutokujua ulitendalo na Bwana hana furaha na mtu wa aina hiyo.Kwa kukosa kuelewa makusudi ya kuokolewa watu wengine hawachukulii uzito swala la kumtumkia Mungu ni wazi kuwa kutokumtumikia Mungu kuna tuweka katika hali ya kujitafutia madhara lakini kwa kumtumkia Mungu kunakuwa na faida nyingi sana 

Faida za kumtumikia Mungu
Yesu aliahidi kuwa mtu akimtumikia pale atakapokuweko na mtumishi wake atakuwepo Yohana 12; 26 kwa msingi huo ikiwa tunataka kumuona Mungu akiwa pamoja nasi, ni muhimukufahamu kuwa baada ya kuokolewa tunapaswa kumtumikia Munmgu na kukumbuka ya kuwa kuna thawabu kubwa kwa watu watakaomtumikia Mungu mtu anakuwa wa thamani zaidi nyumbani kwa Mungu kwa kadiri anavyotumika kama ilivyo kwa chombo kinachotumiwa Nyumbani Mungu hutubariki kwa Baraka mbalimbali ikiwa tutayatoa maishayetu kumtumikia Yeye

§  Kutoka 23;25-26  atabariki chakula maji na kutuondolea magonjwa
§  Isaya 65;13-14  Luka 9;2-3,22;35 Hatutapungukiwa na kitu wakati wengine wakipungukiwa

Unaweza kumtumikia Mungu kwa namna gani? kwa kualika watu wengine kuja Ibadani, kushuhudia wengine habari ya wokovu, kufuatilia watoto wachanga kiroho ili kuhakikisha kuwa tunawafundisha na kuwasaidia kukua, kumtumikia Mungu kwa kuimba kwaya na kuhudhuria ibada pia kuitikia wito wa kumtumikia Bwana katika ngazi ya kichungaji kwa msingi huo ni vema tunapokuwa tumetambua umuhimu wa wa kumtumikia Munu basi hatuna budi kuhakikisha kuwa tunaongeza bidii ya utumishi kwa bidii kwani amelaaniwa kila aifanyaye kazi ya Bwana kwa ulegevu Warumi 12;11,Yeremia 48;10 kwa kufanya hivyo Baraka nyingi zinatungoja.