Jumatano, 2 Machi 2016

Dhambi ya kuacha kuwaombea wengine!



1Samuel 12; 23 “Walakini mimi hasha! Nisimtende Bwana dhambi kwa kuacha kuwaombea ninyi” Ni maneno ya nabii aliyeheshimika sana katika Israel ambaye Mungu alipendezwa naye sana Samuel alikuwa na ufunuo ulio sahii machoni kwa Mungu kuwa kutokuwaombea Israel ni dhambi ambayo yeye hangelipenda aifanye aliwaombea Israel. Kwa Msingi huo tutajifunza somo hili kwa kuzingatia vipengele viwili vifuatavyo;-



 Kwa nabii Samuel kutokuwaombea wengine ni dhambi



§  Dhambi ya kuacha kuwaombea wengine
§  Faida za kuwaombea wengine.

Dhambi ya kuacha kuwaombea wengine.
Kutokuwaombea wengine ni dhambi, mbele za Mungu dhambi yoyote ile inaweza kutupelekea kupata hukumu isiyo njema Mafndisho mengi kuusu maombi hayajaundwa katika namna ya mfumo wa kujiombea wenyewe tu angalia mfano Mathayo 6; 9-13, ….Utupe leo riziki yetu, utusamehe makosa yetu…usitutie majaribuni…. Lugha inayotumika katika maombi sio lugha ya kibinafsi yaani unipe leo riziki yangu, unisamehe dhambi zangu…usinitie majaribuni… Ni muhimu kwa kila mtu aliyeokoka kuwa na ufahamu kuwa Mungu hapendezwi na ubinafsi katika maombi anataka tuombeane, hu ni mfano ulio wazi kuwa Yesu alituombea sisi  hata kabla ya kuzaliwa Yohana 17;15-20 Maombi mengi ya wakristo hayajibiwi kwa sababu wanaangalia yetu wenyewe Wafilipi 2;4. Samuel aligundua siri ya ajabu kuwa kuacha kuwaombea wengine ni dhambi ingawa yeye alikuwa kuhani, sisi nasi ni ukuhani mteule, taifa takatifu watu wa milki ya Mungu kwa msingi huo nasi tunaweza kuliitia jina la bwana kwaajili ya wengine.
Faida za kuwaombea wengine.
Tunapouwa na Muda wa kuwaombea wengine tunapata faida kubwa sana katika ulimwengu wa Roho, tunavikwa silaha zote za Mungu pale tunapokumbuka kuwaombea wengine kimwili na Kiroho ni muhimu kufahamu kuwa maombi ambayo ni tishio kwa shetani ni yale yanayolenga  kuujenga ufalme wa Mungu na mapenzi a Mungu ili yatimizwe ndani yetu na mengine yanapaswa kufuata baadaye Waefeso 6;11,18-20 tunapoomba kwa uzito mkubwa siku zote kwaajili ya washirika wenzetu Mungu atatubariki upeo na kutupa ushindi dhidi ya adui yetu shetani Wakolosai 4;2-3 , tunapoomba kwa uzito kwaajili ya Mchungaji wetu Mungu atatubariki upeo na kutupa thawabu warumi 15;30-31,1Wathesalonike 5;25, pia ni muhimu kuomba kwaajili ya Ndugu na jamaa na majirani katika maeneo yetu ili kwamba Mungu awaokoe na ufalme wa Mungu uongezeka kuna tahwabu kubwa Mbinguni Warumi 9;1-5.
Nykati za kanisa la kwanza  kanisa lilikuwa na nguvu kubwa na lilikuwa na mamlaka dhidi ya adui kwa sababu hawakuwa na ubinafsi na kwa sababu hiyi Mungu alifanya mambo ya kutisha na kushangaza Matendo 2;43-47, 5;12-16. Wenzetu nyakati za kanisa la kwanza waliushinda umimi walikubali kuangalia mambo ya wenzao waebrania 10; 32-36 inawezekana bado hatujaona mambo makubwa ya kutisha na kushangaza katika huduma zetu kwa sababu Mungu hakai katika ubinafsi ni muhimu kufahamu kuwa maombi yanayompendeza Mungu ni maombi yanayohusiana na kuwaombea wengine.

Hakuna maoni: