Jumatano, 2 Machi 2016

Maisha ya Maombi !



Neno La Msingi 1Wathesalonike 5;17 “Ombeni Bila kukoma” Pamoja na kuwa Mstari huu tunaoutafakari una maneno matatu tu Ombeni Bila kukoma  ni muhimu kufahamu kuwa una uzito mkubwa sana  unaoelezea namna maisha ya mkristo au mtu aliyeokoka  anavyopaswa kuwa  yaani maisha ya mkristo ni maisha ya kuomba bila kukoma au kuacha. Tutajifunza somo hili kwa kuzingatia vipengele viwili vifuatavyo;-

Kuacha kuomba ni kuacha Ukristo
§  Umuhimu wa maombi kwa Mkristo.
§  Kielelezo cha Bwana Yesu 

Umuhimu wa maombi kwa Mkristo.
Mkristo akiacha kuomba anakuwa ameacha kuishi maisha ya kikristo, Kuacha kuomba ni kuacha ukristo, wako watu wengine ambao wanajiona wa kiroho sana na kwa sababu hiyo hawaoni umuhimu wa kuomba tena Yesu Kristo alikuwa wa Kiroho kuliko mtu awaye yote  alikuwa ni mtume mkuu na kuhani mkuu Waebrania 3;1 alikuwa pia ni Nabii mkuu Luka 7;16 alikuwa mwinjilisti mkuu ambaye watu walikuwa wanakimbilia na kutafuta mahubiri yake hata pale ambapo alitaka kupumzika, na Katika maombezi yake hakuna mgonjwa aliyekuja kwa Yesu asipokee uzima Luka 8;40, Marko 6;30-34 Mathayo 9;35, alikuwa ni mchungaji mkuu Waebania 13;20, alikuwa mwalimu aliyetoka kwa Mungu Yohana 3;2 zaidi ya yote alikuwa mwana wa Mungu  na anaitwa Mungu mkuu Waebania 14;14 Tito 2;13,   Pamoja na kuwa wa kiroho na huduma kubwa kiasi hiki Yesu hakuacha kuomba  naye ametuachia kielelezo.

Kielelezo cha Bwana Yesu.
Bwana yesu alikuwa mwombaji aliishi maisha ya maombi na hakuacha kuomba kila siku Bwana yesu aliomba na kila wakati nafasi ilipopatikana naye ametuachia kielelezo Alfajiri na Mapema  alifanya maombi Marko 1;35, wakati mwingine mchana aliacha huduma za muhimu na kwenda kuomba  Luka 5;15-16, wakati mwingine alikesha usiku kucha  katika kumuomba Mungu Luka 6;12 alijitenga na wanafunzi wake  akapiga magoto akaomba Luka 22;41,aliomba na kulia sana machozi Wabrania 5;7 aliomba wakati Fulani mpaka hari (jasho) lake likawa kama matone ya Damu Luka 22;43-44, Yesu aliishi maisha ya maombi, kama tunataka kutenda kazi alizozitenda na zaidi  kama alivyosema yeye Yohana 4;12 ni muhimu kufahamu kuwa haiwezekani kuzitenda kazi hizo bila ya kuwa waombaji, hatuna budi kuomba  kama Yesu ili kuzifanya kazi hizo ni kumba kwa namna hii ndiko kunakomfanya mtukutumiwa na Mungu kwa kazi za ajabu Mungu hafurahuiwi na mtu awaye yote asiyeishimaisha ya maombi kutokuishi maisha ya maombi so tu ni sawa na kuacha ukristo lakini ni kiburi kwani twaonyesha kuwa tunajitegemea jambo ambalo linamuhuzunisha mno Mungu 2Wakoritho 1;8-9, Pasipo Yesu Kristo sisi hatuwezi kufanya jambo lolote hata kama ni dogo kiasi gani Yohana 15;5 tukiishi maisha ya maombi Mungu anapendezwa na ndiyo shara ya kuwa tunamtegemea Yeye, mara kadhaa tunaonywa kwamba endapo tutaacha kuomba tutajikuta tukiingia majarini lakini kama tukiomba Mungu atatuepusha na majarib hayo Marko 14;38-40, 

Ni muhimu kukumbuka wakati wote kuombeana sisi kwa sisi kila siku Yakobo 5;16 na kuwaombea watakatifu wote  ili wasipepetwe na Ibilisi kama ngano waefeso 6;18 Luka 22;31-32 na pia kuwaombea wenye dhambi ili kwamba Mungu awape wokovu Warumi 10;1 ni muhimu pia kumombea Mchungaji wetu ili apewe usemi na Mungu katika kuubiri na kufundisha na pia ili apete kutumiwa kipekee aanapotuombea 1Wathesalonike 5;25,Waefeso 6;18-19, Matendo 4:29-30.

Hakuna maoni: