Jumatano, 2 Machi 2016

Agizo la Kujihadhari na Manabii wa Uongo!



Yesu Kristo alifundisha katika mafundisho yake umuhimu wa kujihadhari na Manabii wa uongo Mathayo 7;15 kwa kukosa kuwa na ufahamu katika neno la Mungu tunaweza kujikuta tunachukuliwa na uongo wa shetani kwa kuikimbia kweli na kwenda mbali kabisa na neno la Mungu hata hivyo namna ya kuwatambua manabii wa uongo ni jambo linaloweza kukuchanganya kama hutakuwa na ufahamu kuhusu Neno la Mungu ni kwa msingi huo sasa leo tutachukua Muda  kujifunza neno la Mungu linasema nini uhusu manabii wa uongo ili tupate kujihadahri sawasawa na neno la Mungu.tutajifunza somo hili kwa kuzingatia vipengele viwili vifuatavyo;-


Muhubiri huyu hapaswi kugusa chini wakati wa mahubiri hushinda juu ya migongo ya washirika

§  Maana ya neno Nabii
§  Jinsi ya kuwatambua manabii wa uongo.

Maana ya neno Nabii.
Neno nabii lmejitokeza zaidi ya mara mia 300 katika agano la kale na mara 100 katika agano jipya katika agano la kale neno hili lilitumika kama Navi au Nabi ambalo maana yake mtu mwenye uwezo wa kupokea neno la Mungu na kulifikisha kwa watu, walifanya kazi ya kuzungumza mambo ya Mungu kwa wakati ulioko, uliopita na ujao, kwa ufupi leo tunaweza kusema kuwa manabii ni wanenaji kwa niaba ya Mungu au  watumishi wa Mungu wanaohubiri yale yaliyo haki na yale ambayo sio haki mbele za Mungu hao ndio manabii wa kweli Waefeso 4;11 nabii wa kweli kwa kawaida anakuwa na sifa kuu mbili A. atafundisha maneno ya kweli ya Mungu bila kuchuja kwa namna yoyote ile bila kujali cheo au sifa ya mtu na atafundisha njia ya Mungu kwa Usahii bila upendeleo Yohana 3;34, Mathayo 22;16, Wagalatia 2;4-6.B. Maisha yake yataonyesha matunda ya Kristo na ya Roho Mtakatifu maana Mungu anayemwakilisha ni Mtakatifu kwa hivyo maisha yake yataendana na yale anayoyafundisha  kila siku Matendo 1;1 Warumi 2;21-25 Wagalatia 5;22-25 pale tunapoona sifa izi kuu na nyinginezo sawasawa na neno la Mungu  ndipo tunapoweza kujua kuwa huyu ni nabii wa kweli  tuliyoipokea.

Jinsi ya kuwatambua manabii wa uongo.
Maandiko yanatupa mwanga wa kutosha kuweza kuwatambua manabii wa uongo kama anavyo tufundisha Bwana wetu Yesu Kristo. Katika Mathayo 7;15-20 anasema tutawatambua kwa MATUNDA yao matunda ya manabii wa uongo kwa mujibu wa maandiko nikama ifuatavyo;-
a.       Manabii wa uongo hufundisha UONGO na katika maandiko wanaitwa mikia, Kufundisha uongo ni kufundisha yale ambayo hayako kwenye Biblia au yale ambayo Biblia haikumaanisha badala yeke watafundisha hadithi zilizotungwa na wanadamu na katiba zao hata kama ziko kinyume na neno la Mungu linatuonya  kuwa mbali nao katika jina la Yesu, tujihadhari kabisa Isaya 9;15-16, 2Petro 2;1-4.
b.      Manabii wa uongo hukiri kwa vinywa vyao kuwa wanamjua Mungu lakini kwa Matendo yao wanamkana  ni wenye machukizo na uovu wote Tito 1;16 watakuwa ni watu ambao wanashika Biblia au vitabu vya kidini na kwenda huko na huko kuhubiri dini lakini ukiangalia maisha yao ni ya uasherati, Uzinzi, usengenyaji, uongo, ushirikina, fitina, faraka na uadui  haya ni baadhi ya matunda ya mwili Wagalatia 5;22
c.       Manabii wa uongo kamwe hawakiri kuwa Yesu ni mwana wa Mungu ila wanasema ni mwanadamu tu sawa na wengine 1Yohana 4;1-4
d.      Manabii wa uongo hukataa neema ya wokovu iliyokuja kwa mkono wa Yesu Kristo na hufundisha na kuwaambia watu kuwa watafika mbinguni kwa matendo Fulani ya sheria, Nyakati za leo hatuko chini ya sheria ya Musa ili tuko chini ya sheria ya kifalme ya Yesu Kristo ambayo tunawezeshwa na Yesu mwenyewe Tito 2;11-12 Wagalatia 5;4 2;16 Yohana 1;16-17, 2Petro 2;1-2.
e.      Manabii wa uongo huwaambia watu amani tu hata kama yale waliyoyafanya yako kinyume na neno la Mungu, manabii hao kusudi lao au mungu wao hasa ni tumbo Yeremia 23;16-17 Warumi 16;17-18 wafilipi 3;18-19. Fedha ndio lengo lau kuu wanatajirika kupitia washirika masikini ambao labda wangehitaji msaada kutoka kwao.
f.        Manabii wa uongo watasifiwa na watu wote na kutakuwa hakuna upinzani wowote wa kunenwa vibaya au vinginevyo. Nabii wa kweli kunakuwa na mchanganyo wa utukufu na aibu na kunenwa mabaya  Luka 6;20-26 angalia sifa za nabii wa kweli 2Wakoritho 6;4-10,Yohana 7;20,8:48.
g.       Manabii wa uongo hawaongozi na neno la Mungu ila wanaongozwa na mapokeo ya kibinadamu tu ndoto na maono ya uongo Wakolosai 2; 18-19, Marko 7;6-7,13. n.k.
Ni muhimu basi kujihadhari na kutokuwakubali walete upuuzi wao au kuanza kubishana nao 2Timotheo 2; 14, 23-24, waefeso 5;4 Mungu atupe neema ya kutokukubali kupotea. Lazima watumishi wenye kudai kuwa wanaihubiri kweli waishi sawa na injili, tunafahamu kuwa yako matatizo ya kibinadamu na udhaifu wa kibinadamu lakini manabii wa uongo kwa makusudi kabisa lengo lao ni kujitajirisha wao wenyewe wengine kuwaona ni gharama kubwa sana kuliko kumuona Yesu, washirika wanateseka mpaka wakiponyoka katika kanisa lao wanajisikia Huru Mungu awasaidie watu wake walioteswa na kundi kubwa la manabii wenye kujikinai na kutabiri uongo

Maoni 1 :

Unknown alisema ...

hakika blog hii imenisaidia

ubarikiwe sana Mtumishi wa Mungu

ushauri wangu: kama upo uwezekano wa kutengeneza APP,naomba unda....tutabarikiwa zaidi!