Jumatano, 2 Machi 2016

Makusudi Ya kuokolewa !



Neno la Msingi Kutoka 10;3. “…………Bwana Mungu wa Waebrania asema hivi……..……Wape watu wangu ruhusa waende zao ili wanitumikie”


 Mungu ametuokoa kwa kusudi la Kumtumikia

§  Makusudi ya kuokolewa.
§  Faida za kumtumikia Mungu.

Makusudi ya kuokolewa.
Ni muhimu kufahamu kuwa mambo yaliyowapata wana wa Israel walipokuwa Misri na kuokolewa kwao hatimaye kuingia kanaani ulikuwa ni mfano kwetu kutuonya sisi tuliofikiwa na miisho ya zamani hizi 1Wakoritho 10;11 moja ya kjambo kubwa tunallojifunza kutka kwao ni uweza wa Mungu wa kuokoa Pamoja na moyo Mgumu wa Farao, ni wazi kuwa sisi nasi tumeokolewa kama ilivyokuwa kwa wana wa Israel Jukumu letu kubwa la kuokolewa kwetu kama ilivyokuwa kwa wana wa Israel ni ili TUMTUMIKIE Bwana  kusudi hili lilitajwa na kurudiwa tena na tena katika maandiko kwa msisitizo mkubwa. Kutoka 4; 22-23, 7; 16, 8;1, 8;20, 9;1, 9;13, 10; 3, 10; 24-26.  Sisi nasi hatuna budi kufahamu kuwa makusudimakubwa ya kuokolewa kwetu ni ili tumtumikie Mungu kama mtu aliyeokolewa haoni furaha ya kumtumikia Mungu ni kwa kutokujua ulitendalo na Bwana hana furaha na mtu wa aina hiyo.Kwa kukosa kuelewa makusudi ya kuokolewa watu wengine hawachukulii uzito swala la kumtumkia Mungu ni wazi kuwa kutokumtumikia Mungu kuna tuweka katika hali ya kujitafutia madhara lakini kwa kumtumkia Mungu kunakuwa na faida nyingi sana 

Faida za kumtumikia Mungu
Yesu aliahidi kuwa mtu akimtumikia pale atakapokuweko na mtumishi wake atakuwepo Yohana 12; 26 kwa msingi huo ikiwa tunataka kumuona Mungu akiwa pamoja nasi, ni muhimukufahamu kuwa baada ya kuokolewa tunapaswa kumtumikia Munmgu na kukumbuka ya kuwa kuna thawabu kubwa kwa watu watakaomtumikia Mungu mtu anakuwa wa thamani zaidi nyumbani kwa Mungu kwa kadiri anavyotumika kama ilivyo kwa chombo kinachotumiwa Nyumbani Mungu hutubariki kwa Baraka mbalimbali ikiwa tutayatoa maishayetu kumtumikia Yeye

§  Kutoka 23;25-26  atabariki chakula maji na kutuondolea magonjwa
§  Isaya 65;13-14  Luka 9;2-3,22;35 Hatutapungukiwa na kitu wakati wengine wakipungukiwa

Unaweza kumtumikia Mungu kwa namna gani? kwa kualika watu wengine kuja Ibadani, kushuhudia wengine habari ya wokovu, kufuatilia watoto wachanga kiroho ili kuhakikisha kuwa tunawafundisha na kuwasaidia kukua, kumtumikia Mungu kwa kuimba kwaya na kuhudhuria ibada pia kuitikia wito wa kumtumikia Bwana katika ngazi ya kichungaji kwa msingi huo ni vema tunapokuwa tumetambua umuhimu wa wa kumtumikia Munu basi hatuna budi kuhakikisha kuwa tunaongeza bidii ya utumishi kwa bidii kwani amelaaniwa kila aifanyaye kazi ya Bwana kwa ulegevu Warumi 12;11,Yeremia 48;10 kwa kufanya hivyo Baraka nyingi zinatungoja.

Hakuna maoni: