Jumanne, 7 Januari 2025

Msimwite Mtu Baba Duniani!


Mathayo 23:8-10 “Bali ninyi msiitwe Rabi, maana mwalimu wenu ni mmoja, nanyi nyote ni ndugu. Wala msimwite mtu baba duniani; maana Baba yenu ni mmoja, aliye wa mbinguni. Wala msiitwe viongozi; maana kiongozi wenu ni mmoja, naye ndiye Kristo.




Utangulizi:

Moja ya maonyo aliyoyatoa Yesu Kristo Kiongozi mkuu wa wokovu wetu kwa wanafunzi wake ni pamoja na kuacha kutafuta heshima kutoka kwa wanadamu na au kuwapa wanadamu heshima isiyostahili, Yesu aliwakumbusha wanafunzi wake kuwa wao ni ndugu, yaani kaka na dada katika Bwana, kwa hivyo wakristo ni familia moja ya Mungu, na Mungu pekee ndiye baba yetu,  lakini zaidi ya yote aliwaonya wasimuite mtu rabi wala baba duniani wala kiongozi, kwa kuwa baba yetu ni mmoja aliye wa mbinguni na Mwalimu wetu ni mmoja ndiye Yesu na wala tusiitwe viongozi, kwa hiyo kamwe hatupaswi kutafuta heshima, wala kumpa mtu heshima ambayo hastahili na badala yake kuhakikisha tunawatumikia watu,  na kuwa heshima na utukufu ni mali ya Mungu Baba yetu.

Marko 10:42-45 “Yesu akawaita, akawaambia, Mwajua ya kuwa wale wanaohesabiwa kuwa wakuu wa Mataifa huwatawala kwa nguvu, na wakubwa wao huwatumikisha. Lakini haitakuwa hivyo kwenu; bali mtu anayetaka kuwa mkubwa kwenu, atakuwa mtumishi wenu, na mtu anayetaka kuwa wa kwanza wenu, atakuwa mtumwa wa wote. Kwa maana Mwana wa Adamu naye hakuja kutumikiwa, bali kutumika, na kutoa nafsi yake iwe fidia ya wengi.”

Mafundisho ya Yesu Kristo ni tofauti sana na mafundisho ya ulimwengu huu, watu wa ulimwengu huu wanatafuta kutambulika, wanatafuta umaarufu na heshima kubwa na kutawala, na kutumikisha au kutumikiwa,lakini Kristo anasisitiza unyenyekevu, kujishusha na kuwatumikia watu, na wale wanaojinyenyekeza wawapo duniani watainuliwa katika ufalme wa Mungu, Leo tutachukua muda sasa kujifunza kwa kina na mapana na marefu somo hili zuri lenye na lenye mabishano makubwa sana lenye kichwa“Msimwite mtu Baba duniani” kwa kuzingatia vipengele viwili vifuatavyo:-


Asili na matumizi ya neno Baba.

Msimwite Mtu Baba Duniani!. 


Asili na matumizi ya neno Baba.

Ni muhimu kufahamu kuwa itakuwa ni vigumu sana kuelewa kwanini Yesu anawaonya wanafunzi wake wasimwite mtu Baba hapa duniani, kama hatutaelewa kuwa katika Biblia yaani neno la Mungu jina hilo baba lilikuwa lina maana gani, na lilikuwa linatumikaje hususani katika tamaduni za kiebrania, ni muhimu kufahamu kuwa:- 

Neno baba katika lugha ya asili ya Kiebrania linatumika kama neno “Abh” “abea” au “av” na katika Kiyunani ni “Patēr” kwa kiingereza “Father” na katika lugha ya kiaram ni “Abba” ambalo maana yake ni mtu anayeaanzisha jambo ambalo anafikiri kuwa ni sahihi na anahakikisha linaendelea kuwepo, Baba ni mmiliki, Baba ni Mwanzilishi, Baba ni Mlinzi, Mzazi wa kiume, Baba ni mwenye mamlaka ya uzima au kifo, Baba ni muheshimiwa. (Upholder, the owner, Founder, Protector, A male ancestor, Respect). Katika maandiko yaani nyakati za agano la kale na agano jipya pia Neno baba lilipotumika liligusa maeneo hayo muhimu katika maneno hayo niliyoyataja hapo juu. Lakini neno la kiaramu “Abba” linahusika na uhusiano wa ndani zaidi wa kifamilia sawa na neno “Papa” au “Daddy” Hebu sasa tuchukue muda wa kutosha kuangalia jinsi neno Baba lilivyokuwa likitumika katika maandiko:-

Mzazi au mlezi wa kiume  “Abh”– Jina baba au neno baba katika tamaduni za kiebrania na warumi lilikuwa lina uhusiano wa moja kwa moja na Mzazi mwanaume ambaye ana uhusiano wa damu au uhusiano wa kibailojia wa moja kwa moja na wahusika kama ni watoto wa kiume au wa kike, kwa hiyo matumizi ya neno baba yalimaanisha moja kwa moja baba mzazi, mwanaume ambaye anahusika kukuzaa kibaiolojia kama mzazi wa damu, na hata babu yako na babu yake baba yako nao waliweza kuunganishwa katika kundi hilo kumaanisha baba zako yaani watu ambao ni sababu ya wewe kuwepo duniani, ni waanzilishi wa asili yako ya kimwili duniani, ni sababu ya wewe kuweko kwako duniani, ni damu yako, hawa Mungu anawatambua na ameamuru waheshimiwe na kuna Baraka za kufanya hivyo ikiwa ni pamoja na kupewa siku nyingi za kuishi na heri duniani, Kimsingi hawa ukiwaita baba hakuna shida na Yesu hakukataza tukio la aina hii kwa sababu hii ni kawaida na mzazi au mlezi wa familia yako anastahili heshima hii, kwa hiyo hakuna dhambi wala kosa kumuita mzazi wako baba hii ni heshima yake na ni agizo la Mungu katika maandiko kuwa wazazi wetu wanastahili kuheshimiwa. Kwa hiyo matumizi baba kwa mtu aliyekuzaa au kukulea hayana shida katika katazo la Yesu Kristo.


Kutoka 20:12 “Waheshimu baba yako na mama yako; siku zako zipate kuwa nyingi katika nchi upewayo na BWANA, Mungu wako.” (Neno linalotumika hapo ni âb au av)


Matendo 7:32 “Mimi ni Mungu wa baba zako, Mungu wa Ibrahimu, na Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo. Musa akatetemeka, asithubutu kutazama.” (Neno linalotumika hapa ni Patēr au Patriachs)


1Wafalme 11:42-43 “Na siku alizotawala Sulemani katika Yerusalemu juu ya Israeli wote zilikuwa miaka arobaini. Naye Sulemani akalala na baba zake, akazikwa katika mji wa Daudi baba yake; na Rehoboamu mwanawe akatawala mahali pake.” (Neno linalotumika hapa ni âb au av)


Mababa hawa wa duniani wana mamlaka nyingi, ikiwa ni pamoja na kukuzaa, kukulea, kukupa elimu, kukupa chakula, kukutoa uoe au uolewe, kukulinda, kukuongoza, kukutia moyo, kukuelimisha, kukufundisha, pamoja na kukurithisha, Baba wa waabudu miungu zamani  walikuwa na mamlaka ya kuwatoa watoto wao kafara kwa miungu hivyo kuonyesha kuwa baba wa kibaiolojia pia alikuwa ana mamlaka ya uhai wako na kifo chako, Sawa tu na Ibrahimu alivyotaka kumtoa Isaka, au Yeftha alivyomtoa binti yake, hii ni mamlaka nzito sana aliyo nayo baba, Baba hawa wanaweza kukuonya, kukukemea, kukudekeza, kukuadhibu, kukufundisha hekima, kukurithisha Imani, kushughulika na mahitaji yako kukuhurumia  na hata kuwa rafiki na kadhalika. hawa ni baba wa miili yetu. Ni mababa wa kibaiolojia hawa wana haki ya kuitwa Baba. Kuitwa baba ni heshima yao maalumu na wala sio ya kuitafuta wamepewa na Mungu, kwa hiyo baba hawa huitwa baba wa miili yetu, na Mungu ni baba wa roho zetu. Unaweza kuona:-


Waebrania 12:7-9 “Ni kwa ajili ya kurudiwa mwastahimili; Mungu awatendea kama wana; maana ni mwana yupi asiyerudiwa na babaye? Basi kama mkiwa hamna kurudiwa, ambako ni fungu la wote, ndipo mmekuwa wana wa haramu ninyi, wala si wana wa halali. Na pamoja na hayo tulikuwa na baba zetu wa mwili walioturudi, nasi tukawastahi; basi si afadhali sana kujitia chini ya Baba wa roho zetu na kuishi? ” 


Zaburi 103:13 “Kama vile baba awahurumiavyo watoto wake, Ndivyo Bwana anavyowahurumia wamchao.


Kwa hiyo maana ya kwanza ya neno baba ni mzazi wa kiume aliyekuzaa au aliyekulea na kuku-kuza, baba ambaye mna asili ya damu na hata yule anayeweza kukuasili ili uwe mwanaye na kadhalika na wale waliohusika katika malezi yako baba mlezi hii ni kawaida. Na hao wanastahili kuitwa baba lakini ni baba wa miili yetu na kwa habari za kiroho, Mungu ndiye baba yetu, anaitwa Baba wa roho zetu unaweza kuona!.


Mwanzilishi – Jina au neno baba pia katika maandiko linatumika kumuelezea mwanzilishi au aliyeweka msingi wa jambo Fulani, aidha kiulimwengu, au kitaifa, au kiimani, au kitabia au kifalsafa au kuweka miongozo, kwa hiyo waanzilishi wa kitu fulani au jambo Fulani au hata waanzilishi wa taifa, katika maandiko waliitwa baba wa hicho alichokianzisha yaani mgunduzi, au mwanzilishi au  sababu au chanzo cha hiyo tabia au jambo, mwanzilishi au mgunduzi wa jambo fulani linaweza kuwa jema au baya hapa duniani  huyo naye katika maandiko aliitwa baba mfano:-


ImaniWarumi 4:11-12. “Naye aliipokea dalili hii ya kutahiriwa, muhuri ya ile haki ya imani aliyokuwa nayo kabla hajatahiriwa; apate kuwa BABA YAO WOTE WAAMINIO, ijapokuwa hawakutahiriwa, ili na wao pia wahesabiwe haki; tena awe baba ya kutahiriwa, kwa wale ambao si waliotahiriwa tu, bali pia wanazifuata nyayo za imani yake baba yetu Ibrahimu aliyokuwa nayo kabla hajatahiriwa.


Ibrahimu anaitwa baba wa Imani, kwa sababu ndiye mtu wa kwanza kuwasiliana na Mungu aliye hai baada ya miaka mingi sana tangu nyakati za Nuhu, na hivyo kuwa sababu ya watu wengi kumwamini Mungu na kumjua Mungu aliye hai na imani kubwa duniani zikiwemo ya kiyahudi, kikristo na nyinginezo ambazo mzizi wake ni nabii Ibrahimu zinakubali na zinamtambua Ibrahimu kama baba wa Imani yaani mwanzilishi wa Imani yetu kwa Mungu na ndiye mgunduzi wa uhusiano na Mungu wa kweli duniani.


Uongo na dhambiYohana 8:44 “Ninyi ni wa baba yenu, Ibilisi, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; kwa sababu yeye ni mwongo, na baba wa huo.”


Hapa shetani anatajwa kama baba wa uongo, na mwanzilishi wa uongo duniani, ambaye hakuna kweli ndani yake yeye ni mwongo na baba wa huo, yaani shetani ndiye asili au mwanzilishi wa uongo, kwa hiyo neno baba hapa linatumika kuonyesha chanzo, asili au mwanzilishi, mwanzilishi wa uongo ni baba wa huo uongo.

 

Mgunduzi, au mwanzilishi (Meyased) – Mwanzo 4:20-22 “Ada akamzaa Yabali; huyo ndiye baba yao wakaao katika hema na kufuga wanyama. Na jina la nduguye aliitwa Yubali; huyo ndiye baba yao wapigao kinubi na filimbi. Sila naye akamzaa Tubal-kaini, mfua kila chombo cha kukatia, cha shaba na cha chuma; na umbu lake Tubal-kaini alikuwa Naama.” 


Hapa Yabali anatajwa kama asili au mwanzilishi wa kukaa katika mahema na kufuga wanyama, na Yubali ni mwanzilishi wa wapiga muziki yaani kinubi na filimbi, na Tubal-Kaini yeye ni mwanzilishi au mgunduzi wa vyombo vya kukatia vya chuma na shaba au mgunduzi wa silaha 


Aidha katika hali ya isiyokuwa ya kawaida Marekani walimuita George Washington na Abraham Lincoln kama Baba labda kwa sababu ya Washington kuwa mwanzilishi wa taifa hilo, na Lincoln kuwa mtu muhimu katika kujinga Marekani iliyotulia, India walimuita Mahatma Ghand, na Tanzania Mwalimu Nyerere kuwa baba wa mataifa yao, heshima hii kamwe hawajawahi kujipa wala kujiita wenyewe, lakini watu waliwaita hivyo kwa sababu labda ni waanzilishi wa mataifa yao, hatupati kuungwa mkono moja kwa moja kutoka katika maandiko kama wanaweza kufaa kuitwa hivyo kama waanzilishi.  


Uhusiano wa karibu na kihisia – katika tamaduni za kiebrania pia kama mtu alikuwa na uhusiano wa karibu sana na wewe wa kawaida na wa kihisia, waliweza pia kutumia neno baba, watu hawa sio tu walikuwa na uhusiano wa kihisia bali pia uhusiano wa uaminifu ambao unahusisha kujitoa na kushika ahadi na mwenye kumtunza mtu kwa ndani sana Neno la kiebrania linalotumika hapo ni “Masculine” maneno mengine yanayotumika kuelezea aina hii ya uhusiano wa kibaba ni Khesed – anayekutunza, Ahav - anayekupenda, Kesher – zaidi ya rafiki, Kirvah mnayetofautiana kiumri na Yada – unayemjua au unayemuingilia kimwili, hii hutumiwa sana na wanawake kuwaita waume zao baba, Paulo mtume alikuwa na uhusiano wa karibu na kanisa la Korintho na uhusiano wa kihisia kwa hiyo alitumia neno baba hapa kama mtu anayejali na kulilinda kanisa kwaajili ya mafundisho sahihi, na alimuita Timotheo mwanaye katika picha ya uhusiano kama huo, ukaribu na ufahamu wa kile anachiokifundisha zaidi.


1Wakorintho 4:15-17 “Kwa kuwa ijapokuwa mna waalimu kumi elfu katika Kristo, walakini hamna baba wengi. Maana mimi ndimi niliyewazaa katika Kristo Yesu kwa njia ya Injili. Basi, nawasihi mnifuate mimi. Kwa sababu hii nimemtuma Timotheo kwenu, aliye mwanangu mpendwa, mwaminifu katika Bwana, atakayewakumbusha njia zangu zilizo katika Kristo, kama vile nifundishavyo kila mahali katika kila kanisa.”


Paulo mtume alikuwa ndiye mwanzilishi wa kanisa la Korintho na aliwazaa watoto wa kiroho kupitia injili, na aliruhusu walimu wengine kutoka sehemu mbalimbali kufundisha katika kanisa la Korintho, lakini kutokana na uchungu aliokuwa nao na kutokana na kuwepo kwa walimu wa uongo aliwasihi wao kumfuata yeye kama anavyomfuata Kristo, na ama kumfuata Timotheo ambaye ni mwanae mwaminifu katika bwana, hii ilikuwa lugha ya kisamiati yenye lengo la kutaka kuweka wazi kwa wakorintho namna na jinsi wanavyotakiwa kupokea mafundisho kwa walimu wote lakini wakisheshimu mafundisho ya Msingi ya mwanzilishi wa kanisa hilo na kijana wake, lakini kielelezo ikiwa ni kama wanavyomfuata Kristo, hapa hapakua na agizo endelevu la Paulo kuitwa Baba, hivyo hajapingana Bwana.


Kwa hiyo neno kla kiebrania pia meyased linafaa kutumika hapa kama mwanzilishi, mwanzilishi wa kanisa la Korintho, kwa kiyunani megiasménos, yaani kuwazaa kwa njia ya nguvu za Mungu (injili) wao kuwa kanisa. Na katika uhusiano wa Paulo na Timotheo, Paulo alimuita Timotheo mwanae kwa sababu ya umri, malezi na namna alivyoshughulika na kijana huyu kwa uhusiano wa ndani sana hata kutahiriwa kwa Timotheo ona 


Matendo 16:1-3 “Basi akafika Derbe na Listra, na hapo palikuwa na mwanafunzi mmoja jina lake Timotheo, mwana wa mwanamke Myahudi aliyeamini; lakini babaye alikuwa Myunani. Mtu huyo alishuhudiwa vema na ndugu waliokaa Listra na Ikonio. Paulo akamtaka huyo afuatane naye, akamtwaa akamtahiri kwa ajili ya Wayahudi waliokuwako pande zile; kwa maana wote walijua ya kuwa babaye ni Myunani.” 


Paulo mtume alikuwa na uhusiano wa karibu na Timotheo, na hivyo alimuita mwanangu, hii ilikuwa ni katika kudumisha uhusiano waliokuwa nao binafsi “TEKNON” katika mandiko ya kiyunani uhusiano wa baba na mwanae, hii ilikuwa katika uhalisia wa huduma zao na sio kuwa Paulo alitafuta heshima au kuliagiza kanisa kumuite yeye Baba, wakati wote Paulo alijiita Mtumwa wa Yesu Kristo “Doulos” akimaanisha kuwa yeye ni mtumwa wa Yesu Kristo na sio baba kumbuka hilo, alijitoa maisha yake kutumikia na wala sio kutumikiwa kwa hiyo matumizi na ubaba hapa hayakumaanisha mitume waitwe baba.


Katika mahusiano hayo ya kiumri pia utaweza kumuonya mtume Yohana nadhani kwa sababu ya umri au utu uzima aliokuwanao yeye naye alikuwa akitumia lugha ya kuwaita washirika watoto, hii ni kwa sababu ya umri ona 


1Yohana 2:1 “Watoto wangu wadogo, nawaandikia haya ili kwamba msitende dhambi. Na kama mtu akitenda dhambi tunaye Mwombezi kwa Baba, Yesu Kristo mwenye haki, naye ndiye kipatanisho kwa dhambi zetu; wala si kwa dhambi zetu tu, bali na kwa dhambi za ulimwengu wote.”


Biblia ya kiingereza ya “Complete Jewish Bible” inatumia neno “Wanangu” yenyewe inasema hivi “My Children, Iam writing you these things so that you won’t sin. But if anyone does sin, we heve Yeshua the Messiah, the Tzaddik, who pleads our cause with the Father”


Muumba au kiini Adonai (Lord or Master) – Waefeso 1:17 “Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa utukufu, awape ninyi roho ya hekima na ya ufunuo katika kumjua yeye;”


Ayubu 38:28-29 “Je! Mvua ina baba? Au ni nani aliyeyazaa matone ya umande? Barafu ilitoka katika tumbo la nani? Na sakitu ya mbinguni ni nani aliyeizaa?


Neno baba pia linatumika kama neno Lord yaani Bwana mkubwa, na Master yaani Mwalimu au kwa kiibrania Adonai hii ikiwa na maana ya Bwana wa Mabwana, au Bwana wa viumbe vyote kwa hiyo huyu ni chanzo cha uhai wa kimwili na kiroho na hivyo neno Adonai bila shaka lina sifa ya kutumiwa kwa Mungu peke yake

Kiongozi wa kiroho au nabii – Nyakati za agano la kale kiongozi wa kiroho kama nabii aliitwa baba pia hii ni kabla ya katazo la Yesu Kristo wakati wa agano jipya, lakini waitaji walilia hivyo kutoka moyoni si kwa agizo la manabii kama ilivyo leo, lakini hii pia ilitokana na uhusiano wa karibu na kihisia, wakati mwingine sio wachungaji na watumishi wa Mungu wanaojiita baba na ndio maana agizo la Yesu Kristo linasisitiza “Msimwite mtu baba duniani”, hii maana yake nini inawahusu sana waitaji, manabii hata hivyo walikuwa wanyenyekevu na hawakuchukulia kuitwa baba kama heshima ya kuidai, lakini watu wa Mungu wenyewe kwa hiyari waliwaita baba, sasa tunalo katazo kutoka kwa Yesu Kristo Msimwite mtu baba duniani. 


2Wafalme 2:11-13 “Ikawa, walipokuwa wakiendelea mbele na kuongea, tazama! Kukatokea gari la moto, na farasi wa moto, likawatenga wale wawili; naye Eliya akapanda mbinguni kwa upepo wa kisulisuli. Naye Elisha akaona, akalia, Baba yangu, baba yangu, gari la Israeli na wapanda farasi wake! Asimwone tena kabisa; akashika mavazi yake mwenyewe, akayararua vipande viwili. Kisha akaliokota lile vazi la Eliya lililomwangukia, akarudi, akasimama katika ukingo wa Yordani.”


2Wafalme 13:14 “Basi Elisha alikuwa ameshikwa na ugonjwa wake uliomwua; naye Yehoashi mfalme wa Israeli akatelemka amtazame, akamlilia mbele yake, akasema, Baba yangu! Baba yangu! Gari la Israeli na wapanda farasi wake! ” 


Kuitwa baba kama tamaduni au mapokeo  -  Aidha Kanisa Catholic, Othodoxy, Anglican na Lutherran huwaita viongozi wao wa kidini Babakwa mujibu wa tamaduni zao au mapokeo yao, na madai yao makubwa ni ushirikiano au uhusiano wa karibu ulioko kati ya washirika na makuhani wa makanisa hayo wito huu ulipata nguvu katika karne za kati maarufu kama Middle Ages wakati wa utambuzi wa viongozi wa kiroho, kama makuhani Mapadre walipopewa heshima hii ya kuitwa baba na maaskofu wakiitwa Papa, watetezi wa hoja hii, ya kuwaita viongozi wa kiroho baba, wanamadai kuwa hata baadhi ya mitume waliitwa hivyo baba mfano


Yohana 2:1 “Watoto wangu wadogo, nawaandikia haya ili kwamba msitende dhambi. Na kama mtu akitenda dhambi tunaye Mwombezi kwa Baba, Yesu Kristo mwenye haki,”


1Timotheo 1:18 “Mwanangu Timotheo, nakukabidhi agizo hilo liwe akiba, kwa ajili ya maneno ya unabii yaliyotangulia juu yako, ili katika hayo uvipige vile vita vizuri;”


1Petro 5:12-13 “Kwa mkono wa Silwano, ndugu mwaminifu kama nionavyo, nimewaandikia kwa maneno machache, kuonya na kushuhudia ya kuwa hii ndiyo neema ya kweli ya Mungu. Simameni imara katika hiyo. Mwenzenu mteule hapa Babeli awasalimu, na Marko mwanangu.” 


Makanisa mengi leo ukiacha Catholic na Othodoxy wameanza kuwa na kusimika wanawake kuwa makasisi, Anglican na lutheran sasa siku hizi wana wachungaji wengi wanawake na makanisa mengi ya kipentekoste pia yamekuwa yakisimika makasisi wanawake, wachungaji wanawake n ahata kuwaruhusu kuhudumu na kuchunga makanisa wao wanaitwaje sasa katika heshima hii, tuwaite Mama, au tuwaite baba?  Utamaduni na mapokeo hapa yanasemaje Jibu la swali hilo unaweza kubaki nalo kichwani? 


Msimwite Mtu Baba Duniani! 

Yesu aliposema katika Mathayo 23:9 “Wala msimwite mtu baba duniani; maana Baba yenu ni mmoja, aliye wa mbinguni.” Alikuwa anazungumza moja kwa moja kwa wanafunzi wake na kinyume na waandishi yaani walimu waliobobea katika torati pamoja na mafarisayo yaani viongozi wa dini na baraza la Sanhedrin, kimsingi watu hawa walikuwa na tabia ya kujitukuza sana na kutafuta kuheshimiwa sana na watu wote, kuheshimiwa sio kubaya ni sehemu ya maagizo ya maandiko lakini walipenda sana kuheshimiwa na kutafuta umaarufu na heshima hiyo kwa nguvu na kimazingira, Baraza la wazee wakipenda kuitwa baba na waandishi wakipenda kuitwa Rabbi, kimsingi ndani yao hakukuwa na tabia ya unyenyekevu lakini walijawa na tamaa ya kutafuta heshima na waliitengenezea mazingira ya kuipata, mtu alikuwa asipowaita baba hawaridhiki na wanaweza kumuona kama anadharau, mioyoni mwao walijisikia heshima kubwa sana kuitwa baba, Rabbi na Viongozi na vichwa vilivimba, na Kimsingi Yesu alikuwa akiwaona mpaka nia ya ndani moyoni mwao na tabia zao

Marko 12:38-40 “Akawaambia katika mafundisho yake, Jihadharini na waandishi, wapendao kutembea wamevaa mavazi marefu, na kusalimiwa masokoni, na kuketi mbele katika masinagogi, na viti vya mbele katika karamu; ambao hula nyumba za wajane, na kwa unafiki husali sala ndefu; hawa watapata hukumu iliyo kubwa.”

Matendo 7:1-3 “Kuhani Mkuu akasema, Je! Mambo hayo ndivyo yalivyo? Naye akasema, Ndugu zangu na baba zangu, sikilizeni: Mungu wa utukufu alimtokea baba yetu Ibrahimu, alipokuwa katika Mesopotamia, kabla hajakaa Harani, akamwambia, Toka katika nchi yako na katika jamaa zako, ukaende hata nchi nitakayokuonyesha.”

Mafarisayo na Waandishi walipenda kuitwa Rabbi na Baba, na kila aina ya heshima ya hadharani ambako kimsingi wangeweza kuheshimika, walijifikiria wenyewe kuwa ni watu wa kuheshimika na ni walimu wakubwa na ndio maana Yesu alitumia nafasi hii kuwafundisha wanafunzi wake kuwa kinyume na tabia isiyo ya mfano ya kutafuta heshima, kama walivyo wao mafarisayo na sio hivyo tu aliwakataza wanafunzi wake kutokumuita mtu awaye yote Baba au Rabi,  Alisisitiza kuwa wakristo Mwalimu wao ni mmoja tu Bwana Yesu na baba yao ni Mmoja tu Baba wa mbinguni, tofauti na hilo wakristo wote ni ndugu, kaka na dada katika Bwana na wote ni familia ya Mungu. Baba yetu wa Kiroho ni Mungu peke yake tulipofanyika kuwa wana wa Mungu baada ya kumpokea Yesu kama Bwana na mwokozi wa maisha yetu, tulifanyika wana wa Mungu kwa uwezo wa Roho Mtakatifu kwa hiyo kuzaliwa kwetu kwa upya ni matokeo ya kazi ya Roho Mtakatifu na wala sio ya mwanadamu yeyote yule.

Tangu kuokolewa kwetu sisi sote tumekuwa wanafunzi wa Yesu na kila siku tunajifunza, Mwalimu wetu mkuu ni Yesu Kristo na Roho Mtakatifu kwa hiyo sisi sio Rabbis, wala mafundisho yetu asili yake sio sisi bali ni Yesu Kristo mwenyewe na Roho Mtakatifu. Kumbuka neno lile naye alitoa wengine hii maana yake yeye ndiye asili ya watumishi

Waefeso 4:11-13 “Naye alitoa wengine kuwa mitume, na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wainjilisti na wengine kuwa wachungaji na waalimu; kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, hata kazi ya huduma itendeke, hata mwili wa Kristo ujengwe; hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na kumfahamu sana Mwana wa Mungu, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo;”

Kristo Yesu ndiye anayetoa huduma ya kitume, kinabii, kiinjilisti, kichungaji na kialimu, wote hawa wanaongozwa na Roho Mtakatifu chanzo cha mafundisho yao ni Kristo mwenyewe na Roho Mtakatifu, kila aina ya mafundisho ya neno la Mungu asili yake ni Roho Mtakatifu yeye ndiye asili ya mafundisho yetu, Yesu alisema atakapokuja Roho wa Kweli atatufundisha na kwa sababu hiyo katika kanisa Roho wa Mungu amekuwa akitumia watu kufundisha kweli zake na kuyafunua maandiko.

Yohana 14:26 “Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba atampeleka kwa jina langu, atawafundisha yote, na kuwakumbusha yote niliyowaambia.” 

Kristo anatufundisha kuwa badala ya kutafuta heshima miongoni mwa wanadamu sisi tunapaswa kuwa watumishi wa watu, unyenyekevu ni sehemu muhimu sana inayoweza kumfanya Mungu Roho Mtakatifu kuendelea kuleta mafundisho kwetu na kutufunulia jumbe zake kwaajili ya mwili wa Kristo, sisi au mimi na wewe sio chanzo cha mafundisho hayo bali Yesu mwenyewe, Mafarisayo na waandishi walijiweka katika nafasi ya kujifikiri kuwa wao ndo chanzo cha mafundisho na kuwa mafunuo ya kweli yanatoka kwao na wao ndio wenye mamlaka ya kuamuru mtu afundishe, wasipo kuidhinisha watahakikisha haukubaliki, hivyo wakakutana na fundisho hili zito kutoka kwa Yesu Kristo. Ni kwa nini hasa Yesu alitoa fundisho hili ambalo ni kama siku za karibuni kanisa linajisahau na kuanza tena kuwaita viongozi wa kiroho baba? Mimi niiteni Mchungaji tu inanitosha kwa nini Yesu alikataza? Hapa ziko sababu:-

Kumpa Mungu heshima anayoistahili – Yesu alikuwa anataka kukazia ukweli kwamba Baba wa mbinguni ndiye baba wa kweli wa watu wote waliomuamini Bwana Yesu na kumpokea kama Bwana na mwokozi wao, Hakuna mtu mwingine anayeweza kuichukua nafasi hiyo au hata kujipa nafasi hii, Yaani ya kumuita mtu mwingine baba katika maswala ya kiroho, Heshima ya baba wa kiroho ni heshima ya Mungu baba peke yake, ikiwa mtumishi wa Mungu awaye yote atajiita baba au watu wanamuita baba anajiweka katika hatari ya kuichukua heshima ya Mungu baba au utukufu wake, kwa hiyo ni lazima tuwaelimishe watu wasituite mtu baba. 


Malaki 1:6 “Mwana humheshimu baba yake, na mtumishi humcha bwana wake; basi, kama mimi ni baba yenu, heshima yangu iko wapi? Na kama mimi ni bwana wenu, kicho changu ki wapi? Bwana wa majeshi awauliza ninyi, enyi makuhani, mnaolidharau jina langu. Nanyi mwasema, Tumelidharau jina lako kwa jinsi gani? ” 


Isaya 42:6-8 “Mimi, Bwana, nimekuita katika haki, nami nitakushika mkono, na kukulinda, na kukutoa uwe agano la watu, na nuru ya mataifa; kuyafunua macho ya vipofu, kuwatoa gerezani waliofungwa, kuwatoa wale walioketi gizani katika nyumba ya kufungwa. Mimi ni Bwana; ndilo jina langu; na utukufu wangu sitampa mwingine, wala sitawapa sanamu sifa zangu.”


Yesu anatoa tahadhari kwa kusisitiza kwamba baba wa mbinguni ndiye baba wa kweli na halisi wa watu waliookolewa au walioamini, na kwamba hakuna mtu mwingine anayeweza kuichukua nafasi hiyo, kwa hiyo unapomuita mtu mwingine baba katika maana ya heshima ya kiroho, maana yake unampa mtu heshima ambayo inamstahili Mungu pekee, Mwenyewe ana hoji kama mimi ni Baba yenu heshima yangu iko wapi? 


Kuzuia mamlaka makubwa juu ya watu – Kwaasili Mungu alipomuumba mwanadamu alikusudia wanadamu kutawala viumbe vyote, lakini sio watu kuwatawala watu, Waandishi na mafarisayo walikuwa wamejenga mfumo wa kidini ambao ulikuwa unawapa mwanya wa wao kuwa na mamlaka kubwa juu ya maisha ya watu ni wao ndio walikuwa wanaamua hata nani aishi na nani auawe, inapofikia hatua ya mwanadamu kujipa mamlaka mpaka ya kuamua ni nani atakula au nani atakaa na njaa, nani atamuoa nani, na nani ataolewa na nani?  Mungu huwa anachukizwa na hali hiyo, Mwanadamu sio mtawala wa mwanadamu mwenzake lakini ni msimamizi tu, na ndio maana mitume hawakuwahi kutengeneza mifumo ya kiutawala bali mifumo ya kimaongozi, hakuna aliyekuwa mkubwa miongoni mwa wanafunzi Yesu., Mungu ni Mungu wa utaratibu na mifumo ya kisimamizi haina shida kwake lakini kumbuka hata wazee waliochaguliwa kumsaidia Musa katika uongozi, hawajawahi kuitwa baba, wala mitume hawajawahi popote pale kujiita baba na walipotumia neno baba au mwanangu au watoto wangu wadogo, hawakutumia maneno hayo katika mtazamo wa ubora bali katika mtazamo wa uhusiano.Musa ni nabii mkubwa sana aliyekuwa na uhusiano mkubwa na wa karibu na Mungu lakini hatuoni kokote katika maandiko akiitwa baba. Badala yake yeye alimuita Mungu baba.


Mwanzo 1:28-31 “Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi. Mungu akasema, Tazama, nimewapa kila mche utoao mbegu, ulio juu ya uso wa nchi yote pia, na kila mti, ambao matunda yake yana mbegu; vitakuwa ndivyo chakula chenu; na chakula cha kila mnyama wa nchi, na cha kila ndege wa angani, na cha kila kitu kitambaacho juu ya nchi, chenye uhai; majani yote ya miche, ndiyo chakula chenu; ikawa hivyo. Mungu akaona kila kitu alichokifanya, na tazama, ni chema sana. Ikawa jioni ikawa asubuhi, siku ya sita.”


Kumbukumbu 32:6 “Je! Mnamlipa Bwana hivi, Enyi watu wapumbavu na ujinga? Je! Yeye siye baba yako aliyekununua? Amekufanya, na kukuweka imara.”


Matendo 12:20-23 “Naye Herode alikuwa amewakasirikia sana watu wa Tiro na Sidoni; wakamwendea kwa nia moja, na wakiisha kufanya urafiki na Blasto, mwenye kukitunza chumba cha mfalme cha kulalia, wakataka amani; kwa maana nchi yao ilipata riziki kwa nchi ya mfalme. Basi siku moja iliyoazimiwa, Herode akajivika mavazi ya kifalme, akaketi katika kiti cha enzi, akatoa hotuba mbele yao. Watu wakapiga kelele, wakisema, Ni sauti ya Mungu, si sauti ya mwanadamu. Mara malaika wa Bwana akampiga, kwa sababu hakumpa Mungu utukufu; akaliwa na chango, akatokwa na roho.”


Herode alifikia hatua ya kuamua mtu wa kufa na mtu wa kuachiwa huru, alifikia hatua ya kuamua nani akae na njaa na nani anufaike na Mungu alimsubiria hapo baada ya kuwafunga mitume na kumuua Yakobo na kutaka kumuua Petro na kutawala watu wa Tiro na Sidoni kwa kuamua kuwanyima chakula maana wanaishi kwa mkono wake, Mungu alichukizwa na hatua hii, wakristo lazima tufikie ngazi ya kujihadhari sana kuwa na mamlaka juu ya watu, sisi ni viongozi tu wa kiroho, ni wasimamizi tu, hatuna mamlaka juu ya maisha ya watu, Mungu ametuweka kama watumishi ili tuwahudumie watu wa Mungu, na hili halimaanishi watu wa Mungu waache kuwaheshimu viongozi wa kiroho, hapana lakini sisi hatupaswi kutukuzwa, wala kujitukuza.


Kujifunza njia ya unyenyekevu – Katika tukio hili pia Bwana Yesu alikuwa akifundisha kuhusu umuhimu wa unyenyekevu, kuwakataza wanafunzi wake kuitwa baba au rabi au kiongozi alikuwa akiwaelekeza kinyume na mafarisayo na masadukayo na waandishi ya kuwa katika njia ya ufalme wa Mungu hakuna nafasi yoyote ya kujivuna na kujiona au kufikiri ya kuwa tuko juu kuliko wengine, Mungu kumuita mtu katika huduma ya  kitume, kinabii, kiinjilisti, kichungaji, na ualimu aliweka ndani mwetu huduma, na nyakati za leo uko utaratibu mzuri wa kimaongozi katika kanisa kama mtu ni Askofu mkuu ita tu Askofu mkuu, kama ni askofu wa jimbo ita tu askofu wa jimbo, kama ni mwangalizi ita tu mwangalizi, kama ni mchungaji ita tu mchungaji, ni mtume ita tu mtume, ni nabii ita tu nabii, na mwinjilisti ita tu mwinjilisti na mchungaji ita tu mchungaji, ni Mwalimu ita tu Mwalimu, ni padre ita tu padre, ni kuhani itatu tu kuhani, ni paroko ita tu paroko usimuite mtu baba, Hakuna  mahali popote katika maandiko ya agano jipya ambapo wakristo walimuita mtu baba, huduma hizo zenyewe ni heshima tosha maana zimetoka kwa Mungu, usianze na baba askofu, baba mchungaji, baba paroko, unaanza kujiingiza katika anga lingine wakati dhambi iliyomuangusha shetani ikiwa ni kiburi, sifa zilizomuinua Yesu Kristo na kumfanya awe na jina kuu kuliko yote ilikuwa ni tabia ya unyenyekevu. 


Ezekiel 28:11-17 “Ulikuwa ndani ya Adeni, bustani ya Mungu; kila jiwe la thamani lilikuwa kifuniko chako, akiki, na yakuti manjano, na almasi, na zabarajadi, na shohamu, na yaspi, na yakuti samawi, na zumaridi, na baharamani, na dhahabu; kazi ya matari yako na filimbi zako ilikuwa ndani yako; katika siku ya kuumbwa kwako zilitengenezwa tayari. Wewe ulikuwa kerubi mwenye kutiwa mafuta afunikaye; nami nalikuweka hata ukawa juu ya mlima mtakatifu wa Mungu, umetembea huko na huko kati ya mawe ya moto. Ulikuwa mkamilifu katika njia zako tangu siku ile ulipoumbwa, hata uovu ulipoonekana ndani yako. Kwa wingi wa uchuuzi wako watu walikujaza udhalimu ndani yako, nawe umetenda dhambi; kwa sababu hiyo nimekutoa kwa nguvu katika mlima wa Mungu, kama kitu kilicho najisi; nami nimekuangamiza, Ewe kerubi ufunikaye, utoke katika mawe hayo ya moto. Moyo wako uliinuka kwa sababu ya uzuri wako; umeiharibu hekima yako kwa sababu ya mwangaza wako; nimekutupa chini, nimekulaza mbele ya wafalme, wapate kukutazama.”


Wafilipi 2:5-11“Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu; ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho; bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu; tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba. Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina; ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi; na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI BWANA, kwa utukufu wa Mungu Baba.”


Yesu hakumaanisha kuwa tusiwaite baba zetu wa kutuzaa kuwa baba, maandiko yanaposema tuwahehimu wazazi moja wapo ya sehemu ya heshima hiyo ni kuwaita kwa majina yao mzazi wa kiume baba na mzazi wa kike mama na tunapaswa kuwaheshimu. Wala Yesu hajafundisha kuwa tuache kuwaheshimu viongozi wetu wa kidini na kiimani na wa kiserikali tunapaswa kuwaheshimu sawasawa na madaraka ambayo Mungu amewapa na kuwanyenyekea 


1Timotheo 5:17 “Wazee watawalao vema na wahesabiwe kustahili heshima maradufu; hasa wao wajitaabishao kwa kuhutubu na kufundisha.”


Neno watawalao katika lugha ya kiyunani linalotumika hapo ni “Proistēmi” maana yake kwa kiingereza ni to preside – to be in a position of authority in a meeting or gathering, na neno lingine ni rule – governing au conducting a procedure, kwa Kiswahili kutawala kunakotajwa hapo ni mtu mwenye mamlaka ya kuongoza mkutano au kanisa, au kuendesha utaratibu, kwa msingi huo maandiko hayazungumzii kudhibiti “control” na watumishi wa Mungu wameonywa kuacha tabia ya kujifanya mabwana (Boss) katika mitaa yao


1Petro 5:1-3 “Nawasihi wazee walio kwenu, mimi niliye mzee, mwenzi wao, na shahidi wa mateso ya Kristo, na mshirika wa utukufu utakaofunuliwa baadaye; lichungeni kundi la Mungu lililo kwenu, na kulisimamia, si kwa kulazimishwa, bali kwa hiari kama Mungu atakavyo; si kwa kutaka fedha ya aibu, bali kwa moyo. WALA SI KAMA WAJIFANYAO MABWANA JUU YA MITAA YAO, bali kwa kujifanya vielelezo kwa lile kundi. 


Petro anaeleza Mungu anavyotaka watu waongozwe si kama tujifanyao mabwana juu ya mitaa bali vielelezo kwa kundi, neno hilo mabwana maana yake “Boss” ambao lina tafasiri mbaya sana, na tunapoitwa baba ni kama tunaelekea huko, uongozi wa kikristo unatupa tahadhari sana kujilinda na kujihami kiasi cha kutokuangukia katika lawama na mtego wa ibilisi, mtego wa ibilisi ni kiburi na majivuno na hukumu ya ibilisi ni anguko linalotokana na kiburi na majivuno au kujiinua na hivyo kutupiliwa mbali nje ya neema ya Mungu


1Timotheo 3:6-7 “Wala asiwe mtu aliyeongoka karibu, asije akajivuna akaanguka katika hukumu ya Ibilisi. Tena imempasa kushuhudiwa mema na watu walio nje; ili asianguke katika lawama na mtego wa Ibilisi.”


Njia iliyo bora wakati wote ni kujifunza unyenyekevu kutoka moyoni na kuwa na tahadhari, shetani anaweza kuwatumia washirika wetu kutuingiza katika mtego wa ibilisi kwani wakati mwingine ni wao ndio wanaotuita baba hivyo hatuna budi kulikataa hilo na kuwafundisha kwamba ukiniita tu Mchungaji hiyo imetosha ni heshima kubwa na kuwa kuniita baba ni kunipalia makaa, tunaye baba mmoja baba wa roho zetu, Mungu.


Kujilinda na kujiweka katika nafasi ya Mungu – Mafarisayo na waandishi walijikweza mno kiasi cha kujiweka katika ngazi ya kutumikiwa na sio kuwatumikia watu, kujiinua sana kungewaweka katika hatari ya kujiweka katika nafasi ya Mungu, Bwana Yesu alikuwa anataka kututahadharisa na hilo, aidha Yesu alikuwa akionyesha tofauti ya mafundisho yake na yale ya ulimwengu huu, watu wa ulimwengu huu wanatafuta kujikweza na mwisho wa siku watahukumiwa na kutupwa chini, lakini wale wanaotubu na kunyenyekea watainuliwa 


Mathayo 18:1-4 “Saa ile wanafunzi wakamwendea Yesu wakisema, Ni nani basi aliye mkuu katika ufalme wa mbinguni? Akaita mtoto mmoja, akamweka katikati yao, akasema, Amin, nawaambia, Msipoongoka na kuwa kama vitoto, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni. Basi, ye yote ajinyenyekeshaye mwenyewe kama mtoto huyu, huyo ndiye aliye mkuu katika ufalme wa mbinguni.”


Marko 9:35 “Akaketi chini, akawaita wale Thenashara akawaambia, Mtu atakaye kuwa wa kwanza atakuwa wa mwisho kuliko wote, na mtumishi wa wote.


1Petro 5:5-6 “Vivyo hivyo ninyi vijana, watiini wazee. Naam, ninyi nyote jifungeni unyenyekevu, mpate kuhudumiana; kwa sababu Mungu huwapinga wenye kiburi, lakini huwapa wanyenyekevu neema.Basi nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake;” 

Neno la Mungu linawataka wanafunzi wote wa Yesu kujivika unyenyekevu, na unyenyekevu wa kweli sio maigizo ni unyenyekevu kutoka ndani, kila mtu ajione na kujifunza kuwa hastahili mbele za Mungu na kuwa mtumwa wa wengine, mtu mnyenyekevu anatambua ya kuwa anayafanya yote kwa neema ya Mungu, unyenyekevu sio tabia rahisi kama tunavyodhani sababu kubwa ni kuwa kinyume cha unyenyekevu ni majivuno na kiburi jambo ambalo ndio dhambi ya ndani zaidi ya mwanadamu, ambayo shetani aliwaingizia wanadamu. 


Mwanzo 3:4-5 “Nyoka akamwambia mwanamke, Hakika hamtakufa, kwa maana Mungu anajua ya kwamba siku mtakayokula matunda ya mti huo, mtafumbuliwa macho, nanyi MTAKUWA KAMA MUNGU, mkijua mema na mabaya.” 


Shetani alitamani kuwa kama Mungu na ni aina hii ya wazo aliingiza kwa wanadamu na wakamkosea Mungu, kwa msingi huo ni lazima tuchukue tahadhari kuwa neno lolote, cheo chochote na nafasi yoyote ile ambayo anayestahili ni Mungu sisi ni lazima tujifunze kuwa mbali nayo, na sasa kwa bahati isiyo njema katazo hili la wanadamu kuitwa baba limetolewa na Yesu mwenyewe, je unataka kuabudiwa? Jilinde tujilinde na namna yoyote ile ya kutaka kuchukua nafasi ya Mungu, Yesu alihakikisha wakati wote nafasi ya ubaba inakwenda kwa anayestahili na ukichunguza katika maandiko Yesu ndiye anayeongoza kwa kutumia neno baba kuliko mtu awaye yote, Yesu amemtaja Mungu kwa kutumia neno baba mara zaidi ya 165 katika injili pekee mkazo huu sio wa kijinga, wala wa kupuuziwa wakati katika maandiko mengine ya kiyahudi ikiwepo agano la kale watu wamemtaja Mungu kama baba mara 15 tu, hii sio kwa sababu tu Yesu alikuwa mwana wa Mungu, bali kwa sababu Yesu alitaka uhusiano wa wanafunzi wake kwa Mungu uwe hivyo na kuwa mwenye sifa ya kuitwa baba ni Mungu peke yake.


Mathayo 23:8-12 “Bali ninyi msiitwe Rabi, maana mwalimu wenu ni mmoja, nanyi nyote ni ndugu.Wala msimwite mtu baba duniani; maana Baba yenu ni mmoja, aliye wa mbinguni. Wala msiitwe viongozi; maana kiongozi wenu ni mmoja, naye ndiye Kristo. Naye aliye mkubwa wenu atakuwa mtumishi wenu.Na ye yote atakayejikweza, atadhiliwa; na ye yote atakayejidhili, atakwezwa


Yohana 14:6-11 “Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi. Kama mngalinijua mimi, mngalimjua na Baba; tangu sasa mnamjua, tena mmemwona. Filipo akamwambia, Bwana, utuonyeshe Baba, yatutosha.Yesu akamwambia, Mimi nimekuwapo pamoja nanyi siku hizi zote, wewe usinijue, Filipo? Aliyeniona mimi amemwona Baba; basi wewe wasemaje, Utuonyeshe Baba? Husadiki ya kwamba mimi ni ndani ya Baba, na Baba yu ndani yangu? Hayo maneno niwaambiayo mimi siyasemi kwa shauri langu; lakini Baba akaaye ndani yangu huzifanya kazi zake. Mnisadiki ya kwamba mimi ni ndani ya Baba, na Baba yu ndani yangu; la! Hamsadiki hivyo, sadikini kwa sababu ya kazi zenyewe.”


Wakati wote Yesu alihakikisha anamtambua baba yake na alimuita baba katika maeneo mengi sana, leo hii ukitaja baba basi lazima ufafanue ni yupi anazungumzwa, yaani yuko mwanadamu fulani tu mwenye madhaifu kibao anajiita baba, Mungu na atusaidie, ikiwa watu wanatuita hivyo tunaweza kuwafundisha na tunaweza kuwakataza na kuwafunulia maandiko ili wasituingize mtegoni, nao pia wasiingie mtegoni.


Matendo 14:8-15 “Na huko Listra palikuwa na mtu mmoja, dhaifu wa miguu, kiwete tangu tumboni mwa mamaye, ambaye hajaenda kabisa. Mtu huyo alimsikia Paulo alipokuwa akinena; ambaye akamkazia macho na kuona ya kuwa ana imani ya kuponywa, akasema kwa sauti kuu, Simama kwa miguu yako sawasawa. Akasimama upesi akaenda. Na makutano walipoona aliyoyafanya Paulo wakapaza sauti zao, wakisema kwa Kilikaonia, Miungu wametushukia kwa mifano ya wanadamu. Wakamwita Barnaba, Zeu, na Paulo, Herme, kwa sababu ndiye aliyekuwa mnenaji. Kuhani wa Zeu ambaye hekalu lake lilikuwa mbele ya mji, akaleta ng'ombe na taji za maua hata malangoni, akitaka kutoa dhabihu pamoja na makutano. Walakini mitume Barnaba na Paulo, walipopata habari, wakararua nguo zao, wakaenda mbio wakaingia katika makutano, wakipiga kelele, wakisema, Akina bwana, mbona mnafanya haya? Sisi nasi tu wanadamu hali moja na ninyi; twawahubiri habari njema, ili mgeuke na kuyaacha mambo haya ya ubatili na kumwelekea Mungu aliye hai, aliyeumba mbingu na nchi na bahari na vitu vyote vilivyomo;”


Roho Mtakatifu hutuelekeza wa kumuita baba – Ni muhimu kufahamu kuwa watu wote waliompokea Yesu Kristo kama Bwana na mwokozi wa maisha yao na kuamini katika kazi aliyoifanya pale msalabani wanapewa neema ya kufanyika watoto wa Mungu, watu hawa wanazaliwa kwa mapenzi ya Mungu na sio ya mtu au mwili kwa sababu hiyo ni wana wa Mungu, kwa hiyo Mungu Roho Mtakatifu huwaelekeza watoto wake nani wa kumuita baba ona  


Yohana 1:12-13 “Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake; waliozaliwa, si kwa damu, wala si kwa mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, bali kwa Mungu.”


Sio hivyo tu Biblia inatufundisha kuwa Roho Mtakatifu huweka mzigo ndani yetu kumuita Mungu baba kwa sababu yeye ndiye aliyewazaa kiroho kwa mapenzi yake na anatujulisha kuwa Mungu ndiye baba yetu na ya kuwa uhusiano wa karibu sana tulio nao watu tuliookolewa na Mungu ni uhusiano wa baba na mwana wake


Wagalatia 4:4-7 “Hata ulipowadia utimilifu wa wakati, Mungu alimtuma Mwanawe ambaye amezaliwa na mwanamke, amezaliwa chini ya sheria, kusudi awakomboe hao waliokuwa chini ya sheria, ili sisi tupate kupokea hali ya kuwa wana. Na kwa kuwa ninyi mmekuwa wana, Mungu alimtuma Roho wa Mwanawe mioyoni mwetu, aliaye, Aba, yaani, Baba. Kama ni hivyo, wewe si mtumwa tena bali u mwana; na kama u mwana, basi, u mrithi kwa Mungu.”


Warumi 8:14-15 “Kwa kuwa wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu, hao ndio wana wa Mungu. Kwa kuwa hamkupokea tena roho wa utumwa iletayo hofu; bali mlipokea roho ya kufanywa wana, ambayo kwa hiyo twalia, Aba, yaani, Baba.”


Warumi 8:15-16 “Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu; na kama tu watoto, basi, tu warithi; warithi wa Mungu, warithio pamoja na Kristo; naam, tukiteswa pamoja naye ili tupate na kutukuzwa pamoja naye.”


Abba”  ni neno linalotumika katika kiyunani kuonyesha uhusiano wa ndani zaidi wa mtu na baba yake ni neno lililolotumiwa na watoto wadogo kuita baba zao waliowazaa, Roho Mtakatifu tunapookoka anaweka hiyo hali ndani yetu tuliookolewa kuelekeza neno baba kwa Mungu wetu aliyetuumba na kutuokoa, kuonyesha uhusiano wa ndani tulio nae kama watoto wake, sasa basi ikiwa Roho Mtakatifu hutuelekeza sisi kumuita Mungu baba yetu, swali ni nani anayetuelekeza kumuita mtu wa kawaida ambaye ni kiongozi wa kiroho nani anatuelekeza kumuita baba? Usinijibu swali hilo! Ubaba wote wa mbinguni na duniani unaelekezwa wapi?


Waefeso 3:14-15 “Kwa hiyo nampigia Baba magoti, ambaye kwa jina lake ubaba wote wa mbinguni na wa duniani unaitwa,”


Kristo alikazia sana kutuelekeza kwa baba – Kama ilivyo kwa Roho wa Mungu kutufundisha na kutuelekeza wa kumuita baba, ni ukweli ulio wazi kuwa katika maandiko Yesu Kristo katika maisha na mafundisho yake alikazia sana sana sana neno baba akilielekeza kwa Mungu baba, kulikuwa na sababu maalumu sana za Yesu kulikazia hili, na ziko sababu maalumu za Roho Mtakatifu kutufundisha kumuita Mungu kama baba yetu, Kama Yesu ni kiongozi mkuu wa wokovu wetu na kama kweli tunafuata nyayo zake utaweza kuona akikazia katika maeneo mbalimbali katika maandiko akikazia kuhusu ubaba wa Mungu wetu.


Mathayo 11:25-27 “Wakati ule Yesu akajibu, akasema, Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye hekima na akili, ukawafunulia watoto wachanga. Naam, Baba, kwa kuwa ndivyo ilivyopendeza mbele zako. Akasema, Nimekabidhiwa vyote na baba yangu; wala hakuna amjuaye Mwana, ila Baba; wala hakuna amjuaye Baba, ila Mwana, na ye yote ambaye Mwana apenda kumfunulia.”


Marko 14:35-36 “Akaendelea mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, akiomba ya kuwa, ikiwezekana, saa hiyo imwepuke.Akasema, Aba, Baba, yote yawezekana kwako; uniondolee kikombe hiki; walakini, si kama nitakavyo mimi, bali utakavyo wewe.”


Luka 23:34 “Yesu akasema, Baba, uwasamehe, kwa kuwa hawajui watendalo. Wakagawa mavazi yake, wakipiga kura.”


Yohana 14:6-10 “Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi. Kama mngalinijua mimi, mngalimjua na Baba; tangu sasa mnamjua, tena mmemwona. Filipo akamwambia, Bwana, utuonyeshe Baba, yatutosha. Yesu akamwambia, Mimi nimekuwapo pamoja nanyi siku hizi zote, wewe usinijue, Filipo? Aliyeniona mimi amemwona Baba; basi wewe wasemaje, Utuonyeshe Baba? Husadiki ya kwamba mimi ni ndani ya Baba, na Baba yu ndani yangu? Hayo maneno niwaambiayo mimi siyasemi kwa shauri langu; lakini Baba akaaye ndani yangu huzifanya kazi zake.”


Yohana 17:1-5 “Maneno hayo aliyasema Yesu; akainua macho yake kuelekea mbinguni, akasema, Baba, saa imekwisha kufika. Mtukuze Mwanao, ili Mwana wako naye akutukuze wewe; kama vile ulivyompa mamlaka juu ya wote wenye mwili, ili kwamba wote uliompa awape uzima wa milele.Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma. Mimi nimekutukuza duniani, hali nimeimaliza kazi ile uliyonipa niifanye. Na sasa, Baba, unitukuze mimi pamoja nawe, kwa utukufu ule niliokuwa nao pamoja nawe kabla ya ulimwengu kuwako.”


Yohana 17:21-26 “Wote wawe na umoja; kama wewe, Baba, ulivyo ndani yangu, nami ndani yako; hao nao wawe ndani yetu; ili ulimwengu upate kusadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma. Nami utukufu ule ulionipa nimewapa wao; ili wawe na umoja kama sisi tulivyo umoja. Mimi ndani yao, nawe ndani yangu, ili wawe wamekamilika katika umoja; ili ulimwengu ujue ya kuwa ndiwe uliyenituma, ukawapenda wao kama ulivyonipenda mimi.Baba, hao ulionipa nataka wawe pamoja nami po pote nilipo, wapate na kuutazama utukufu wangu ulionipa; kwa maana ulinipenda kabla ya kuwekwa msingi ulimwengu. Baba mwenye haki, ulimwengu haukukujua; lakini mimi nalikujua, na hao wamejua ya kuwa ndiwe uliyenituma. Nami naliwajulisha jina lako, tena nitawajulisha hilo; ili pendo lile ulilonipenda mimi liwe ndani yao, nami niwe ndani yao.”


Mitume walielekeza watu kwa baba – Unapoangalia katika nyaraka zote za maelekezo na mafundisho ya mitume utaweza kuona wakilitii agizo la Yesu Kristo kwa kumtaja Mungu kama Baba, kwa hiyo ni wazi kuwa mamlaka ya ubaba ilipelekwa kwa usahihi kwa Mungu baba mwenyewe na wala sio kwa wanadamu, Wazo la ubaba wa Mungu halikuwa na Msingi sana katika agano la kale , lakini limekuwa ni jambo la msingi sana katika nyakati za gano jipya, huku Yesu akilitilia mkazo sana kuonyesha ni mapenzi ya Mungu, Baba aitwe baba, kwa hiyo utaweza kuona mitume waliukazia ubaba huu kuliko tunavyofikiri kumbuka kuwa mitume walikuwa makini sana, Yesu alifanya hivyo ili sisi tushike hili na kulitumia, labda limesahaulika lakini huu ndio wakati sahihi sasa wa kulikumbusha kanisa msituite baba, tunaye baba mmoja tu ndiye Mungu muumba.


1Wakorintho 8:6 “lakini kwetu sisi Mungu ni mmoja tu, aliye Baba, ambaye vitu vyote vimetoka kwake, nasi tunaishi kwake; yuko na Bwana mmoja Yesu Kristo, ambaye kwake vitu vyote vimekuwapo, na sisi kwa yeye huyo.”


1Wakorintho 1:3 “Neema na iwe kwenu na amani, zitokazo kwa Mungu Baba yetu, na kwa Bwana Yesu Kristo.”


Wagalatia 4:6 “Na kwa kuwa ninyi mmekuwa wana, Mungu alimtuma Roho wa Mwanawe mioyoni mwetu, aliaye, Aba, yaani, Baba.”


Warumi 1:7 “kwa wote walioko Rumi, wapendwao na Mungu, walioitwa kuwa watakatifu. Neema na iwe kwenu na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu, na kwa Bwana Yesu Kristo.”


Waefeso 5:19-21 “mkisemezana kwa zaburi na tenzi na nyimbo za rohoni, huku mkiimba na kumshangilia Bwana mioyoni mwenu; na kumshukuru Mungu Baba sikuzote kwa mambo yote, katika jina lake Bwana wetu Yesu Kristo; hali mnanyenyekeana katika kicho cha Kristo.”


Wakolosai 1:2 “kwa ndugu watakatifu, waaminifu katika Kristo, walioko Kolosai. Neema na iwe kwenu, na amani, zitokazo kwa Mungu Baba yetu.”


2Yohana 1:9 “Kila apitaye cheo, wala asidumu katika mafundisho ya Kristo, yeye hana Mungu. Yeye adumuye katika mafundisho hayo, huyo ana Baba na Mwana pia.”


1Yohana 2:1 “Watoto wangu wadogo, nawaandikia haya ili kwamba msitende dhambi. Na kama mtu akitenda dhambi tunaye Mwombezi kwa Baba, Yesu Kristo mwenye haki,“


1Yohana 4:14 “Na sisi tumeona na kushuhudia ya kuwa Baba amemtuma Mwana kuwa Mwokozi wa ulimwengu.


Yakobo 1:17 “Kila kutoa kuliko kwema, na kila kitolewacho kilicho kamili, hutoka juu, hushuka kwa Baba wa mianga; kwake hakuna kubadilika, wala kivuli cha kugeuka-geuka.”


1Wathesalonike 1:1-2 “Paulo, na Silwano, na Timotheo, kwa kanisa la Wathesalonike, lililo katika Mungu Baba, na katika Bwana Yesu Kristo. Neema na iwe kwenu na amani. Twamshukuru Mungu siku zote kwa ajili yenu nyote, tukiwataja katika maombi yetu.” 


Hitimisho


Msimwite mtu baba Duniani. Ni agizo la Bwana Yesu lililo la muhimu sana, Yesu alitaka kila mkristo aelewe  kuwa uhusiano wetu na Mungu ni wa karibu zaidi, Mungu ni Baba yetu na heshima yake kubwa ni ubaba wake ambao kimsingi heshima hii haipaswi kutolewa kwa mwingine kirahisi, kwa msingi huo katika maisha yetu ya kiroho tunaye baba mmoja tu ndiye Mungu. Nanyi msalipo semeni, Baba yetu uliye mbinguni ona:-


Mathayo 6:9-12 “Basi ninyi salini hivi; Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe, Ufalme wako uje, Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni.Utupe leo riziki yetu.Utusamehe deni zetu, kama sisi nasi tuwasamehevyo wadeni wetu. Na usitutie majaribuni, lakini utuokoe na yule mwovu. [Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu, na utukufu, hata milele. Amina.]


Yesu alitaka watu wote waelewe kuwa Mungu pekee ndiye baba naye alikuja kutupa kielelezo tukifuate wengine wote wanaobaki ni watumishi wa Mungu kwaajili ya maisha yetu ya kiroho, ni wasimamizi tu, hawana mamlaka ya kutawala wanadamu, wana mamlaka ya kusimamia, heshima ya u baba ni ya Mungu pekee, Waandishi na mafarisayo walikuwa wamejenga mfumo ambao kwa bahati mbaya sana miaka ya hivi karibuni unarudi kwa kasi, mifumo inayowaruhusu wao kuwa na mamlaka makubwa juu ya watu, Yesu alitaka watu wasiwategemee viongozi wa kidini, Yesu alikataa mfumo huo na kuwakumbusha watu kuwa wanapaswa kumtegemea Mungu pekee. Aidha Yesu alitaka watu wawe wanyenyekevu na kuacha kujipa majina makubwa kwani kwa makusudi ya kupata heshima, uhusiano wetu na viongozi wa kidini na wao ni watu hauwezi kuwa uhusiano wa karibu kama uhusiano wetu na Mungu Baba, Hivyo ni Mungu pekee ndiye baba yetu, najua kuna watu wanaweza kuchukizwa na fundisho hili, lakini ni ukweli ulio wazi hatuwezi kuwa na akili au hekima kumzidi Yesu Kristo, kama Yesu amekataza wewe una nini? Endelea kujiita baba lakini yatakayokukuta mie simo, kazi yangu ni kukufunulia kweli za neno la Mungu na ni juu yako kuelewa, kutii au kuasi kukubali au kubisha. Lakini ukweli uko wazi kuwa washirika wengi sana nyakati za leo wanatuita baba, kila mahali ninakoenda nikijitambulisha kama mchungaji watu wanaita baba, ukweli sijawahi kuwakataza lakini moyoni ninapata taabu sana kwanini wakristo wanaacha kuniita mchungaji wananiita baba? Au kwa nini waniite baba mchungaji wakati nadhani ukiniita mchungaji tu inatosha, Ni ukweli ulio wazi kuwa mimi najua kuwa hawakuwa wamejifunza neno na agizo la Yesu na kulifikiri kwa kina lakini ilivyo ni kwamba hata Yesu hatumuiti baba, iweje Yesu aje akute mimi naitwa baba jina ambalo yeye hajawahi kulitumia wala Roho Mtakatifu hajawahi kutuongoza tumuite Yesu baba, wala mitume hawajafundisha wakristo kumuita mtu baba, wala biblia haijaelekeza kumuita mtu baba, alafu hapa kuna mtu mwanadamu tunamuita baba? Yesu Kristo mpaka dakika ya mwisho akiwa anapaa bado alikuwa akimtaja Mungu baba kama baba ona hii


Matendo 1:4-8 “Hata alipokuwa amekutana nao aliwaagiza wasitoke Yerusalemu, bali waingoje ahadi ya Baba, ambayo mlisikia habari zake kwangu; ya kwamba Yohana alibatiza kwa maji, bali ninyi mtabatizwa katika Roho Mtakatifu baada ya siku hizi chache. Basi walipokutanika, wakamwuliza, wakisema, Je! Bwana, wakati huu ndipo unapowarudishia Israeli ufalme? Akawaambia, Si kazi yenu kujua nyakati wala majira, Baba aliyoyaweka katika mamlaka yake mwenyewe. Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi.”


Kwa hiyo sasa itakuwaje? Kanisa hatuna budi kutubu, na kuacha mara moja kuwaita watumishi wa Mungu wowote wale Baba, watumishi wa Mungu ni lazima tukatae kuitwa baba, na ni muhimu kuwafundisha watu wote duniani kuacha mara moja kutuita baba, hivi hujawahi kujiuliza ni kwanini Mashehe na mamufti na viongozi wakubwa wa dini kama ya kiislamu hawawaiti viongozi wao wa dini baba?  na sasa wengine tumeenda mbali sana mpaka tuna BABA MTAKATIFU. Hii ni kufuru kubwa sana narudia tena hii ni kufuru kubwa sana narudia mara ya tatu hii ni kufuru kubwa sana, Shetani kuna mahali anataka kutupeleka taratibu bila sisi kujielewa, ile ile tabia yake ya kutaka kuwa kama Mungu anaipanda kwetu na kutuingizia bila kujua mwisho majina yote ya Mungu yatakuwa ndio ya wanadamu ni lazima tuwe makini na hili ndilo Mungu alinituma niweze kuwaonya watu, angalia kwa mujibu wa Yesu Kristo BABA MTAKATIFU ni nani? Ona:- 


Yohana 17:11-12. “Wala mimi simo tena ulimwenguni, lakini hawa wamo ulimwenguni, nami naja kwako. BABA MTAKATIFU, kwa jina lako ulilonipa uwalinde hawa, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo. Nilipokuwapo pamoja nao, mimi naliwalinda kwa jina lako ulilonipa, nikawatunza; wala hapana mmojawapo wao aliyepotea, ila yule mwana wa upotevu, ili andiko litimie.”


Makanisa yanayoongoza kwa kuita wachungaji na makuhani wao baba ni pamoja na Catholics, Orthodox, Anglican na Lutheran kwa bahati mbaya siku hizi hata watu waliookoka wameanza kuwaita wachungaji baba, Hata Haruni alikuwa ni kuhani mkuu lakini Wayahudi hawakumuita baba, kule kuchaguliwa tu na Mungu umtumikie ni heshima kubwa sana na inatosha. 


Lakini ni kwanini Catholics, Orthodox, Anglican na Lutheran huwaina makuhani wao na viongozi wao wa dini Baba? Akijibu swali hili Padre Colin Wen ambaye ni kuhani wa kikatoliki yeye alijibu hivi!


“Sio vibaya kabisa kumuita mtu mwingine baba sawa na katazo la Kristo katika Mathayo 23:9 yeye alisema kuwa mstari huu, unaweza kuwa umetafasiriwa vibaya kwa kuzingatia muktadha wa kile alichokuwa anakisema Bwana Yesu, Yesu hapa alikuwa anakemea tabia ya waandishi namafarisayo ambao waliweka mkazo wa kutafuta heshima hata kuliko utumishi wao kwa Mungu, Padre Colin Wen anaendelea kueleza kuwa ni kweli tuna baba mmoja tu wa mbinguni lakini makuhani wa kidini na wengine wanaoitwa baba wanatumia jina hili kwa sababu wanahusika katika ubaba huo kupitia utumishi wao,  na hivyo sio vibaya wakiitwa baba, wao sio baba kimamlaka lakini wanamuwakilisha baba mbinguni, kama jinsi ambavyo wao sio baba wa kimwili, aliongeza kuwa hata kuwaita baba viongozi wa kiroho maaskofu na makunani sio kitu ambacho kimeibuka siku za karibuni  kwani hata Paulo mwenyewe anasema 


1Wakorintho 4:14-15 “Siyaandiki hayo ili kuwatahayarisha; bali kuwaonya kama watoto niwapendao. Kwa kuwa ijapokuwa mna waalimu kumi elfu katika Kristo, walakini hamna baba wengi. Maana mimi ndimi niliyewazaa katika Kristo Yesu kwa njia ya Injili.”


Kwa maelezo hayo anasema Paulo alijiona kuwa anafiti kabisa kujiita baba na akaeleza kuwa katika maandiko Petro, Paulo na Yohana wote waliwaona waamini wao kama watoto katika mtazamo wa kuwaona wao kuwa ni familia yao na kuwa uhusiano waliokuwa nao ulikuwa ni kama uhusiano wa baba na mwana anasema Petro alimuita Marko mwanangu , na Yohana akiwaita wakristo wanae


1Petro 5:12-13 “Kwa mkono wa Silwano, ndugu mwaminifu kama nionavyo, nimewaandikia kwa maneno machache, kuonya na kushuhudia ya kuwa hii ndiyo neema ya kweli ya Mungu. Simameni imara katika hiyo. Mwenzenu mteule hapa Babeli awasalimu, na Marko mwanangu.”


1Yohana 2:1-2 “Watoto wangu wadogo, nawaandikia haya ili kwamba msitende dhambi. Na kama mtu akitenda dhambi tunaye Mwombezi kwa Baba, Yesu Kristo mwenye haki, naye ndiye kipatanisho kwa dhambi zetu; wala si kwa dhambi zetu tu, bali na kwa dhambi za ulimwengu wote.” 


Anaeleza kuwa tabia hii iliendelea kuwa tabia ya kanisa kwa nyakati zote za maisha ya kanisa na akaeleza ndio maana Askofu mkuu wa kanisa Catholic anatumia jina Papa kama ilivyo kwa kiongozi wa kanisa la Coptic la huko Misri tangu enzi na enzi, Je hoja hizi zinajitosheleza? Kujenga fundisho? Kuwa watumishi wa Mungu wanaushiriki ubaba katika huduma na kwa sababu hiyo kuitwa kwao baba sio tatizo? Padre Colin Wen anaona kuwa japo wao sio baba wa kibailojia, lakini wanashiriki ubaba kila siku katika huduma kuanzia ubatizo na sakramenti nyinginezo na anaeleza kuwa kila siku katika huduma yake anashiriki ubaba huo na anauona na anasema anapoitwa baba inamkubusha kuwa yeye ni nani”. Mwisho wakumnukuu.


Kwa mtazamo wangu mimi naona Padre Colin Wen hoja zake hazina mashiko, kitendo cha kuchaguliwa tu na Mungu kuwa kuhani au Padre tayari kwa Mungu ni heshima kubwa sana, wangeridhika tu kuitwa Padre, au kuhani, au kasisi, na siew engine Mchungaji inatosha lakini nionavyo mimi kuna mstari mwembamba sana kati ya katazo la Yesu Kristo na utetezi wa kuitwa baba tunaoutaka na mtazamo mpana wa kibiblia, Petro kumuita Marko mwanangu, au Paulo kumuita Timotheo mwanangu, au Yohana kuwaita wakristo wanae, inaweza kuwa sio tatizo kwanza kwa sababu ya ukaribu mkubwa wa kimahusiano walio nao Petro na Marko na hali kadhalika Paulo na Timotheo, kama nilivyotangulia kufafanua hapo juu kwenye jinsi na namna neno baba lilivyoelezewa maana zake, lakini pia Umri wao ukilinganisha na washirika waliokuwepo wakati huo mfano Yohana alikuwa mzee sana ukilinganisha na washirika waliokuwako wakati huo kwa umri wake kutumia neno mwanangu haikuwa kitu cha kushangaza. Paulo na Timotheo walikuwa na ukaribu kiasi ambacho Timotheo alitahiriwa nadhani chini ya mamlaka ya Paulo na kama sio Paulo mwenyewe, wao walikuwa na uhusiano wa karibu na kihisia. 


Matendo 16:1-3 “Basi akafika Derbe na Listra, na hapo palikuwa na mwanafunzi mmoja jina lake Timotheo, mwana wa mwanamke Myahudi aliyeamini; lakini babaye alikuwa Myunani. Mtu huyo alishuhudiwa vema na ndugu waliokaa Listra na Ikonio. Paulo akamtaka huyo afuatane naye, akamtwaa akamtahiri kwa ajili ya Wayahudi waliokuwako pande zile; kwa maana wote walijua ya kuwa babaye ni Myunani.”


Kwa hiyo unaweza kuona uhusiano wa Paulo na Timotheo ulikuwa wa ndani kiasi ambacho Timotheo kuitwa mwanangu na Paulo halikuwa jambo la kushangaza, sina Muda sana wa kuzungumzia Marko Kwa Petro, Lakini wote tunajua jinsi ambavyo Petro alifahamiana na Marko tangu akiwa kijana mdogo katika jengo lililokuwako Yerusalem siku ya Pentekoste, na historia ya kanisa inaonyesha uhusiano huo, aidha ukubwa wa umri wa Yohana ambaye aliishi siku nyingi kuwaita wanae washirika pia sio jambo la kushangaza, na zaidi ya yote katazo la Kristo msimuite mtu baba, lilikuwa kwa wanafunzi wa Yesu tusimuite mtu baba duniani, sisi sasa ndio wanafunzi wa Yesu na swala hilo linatuhusu, lakini hatujakatazwa kumuita mtu mwanangu. Katazo linawahusu watu wasituite baba, tunaweza kujenga hoja za kimaandiko na Roho Mtakatifu Mwalimu mkuu anaweza kutufafanulia kama ni haki kuitwa baba katika uhusiano wa kiroho! Kwa sababu Baba ndiye Mwanzilishi wa Maisha yetu sifa ya Ubaba ni sifa ya Mungu peke yake na sio sisi, makasisi wa kikatoliki waitwe Padre, maksaisi wa kiprotestant na waitwe wachungaji, na majina mengineyo lakini hata hivyo swala la kuitwa baba katika uhusiano wa Kiroho linatuweka katika wakati mgumu ambao hakuna hoja ya kimaandiko ya kututetea.



Na Rev. Innocent Samuel Kamote


Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima

Jumatano, 1 Januari 2025

Kurejeshwa kwa miaka ya hasara!


Yoel 2:25-27 “Nami nitawarudishia hiyo miaka iliyoliwa na nzige, na parare, na madumadu, na tunutu, jeshi langu kubwa nililotuma kati yenu. Nanyi mtakula chakula tele na kushiba, na kulihimidi jina la Bwana, Mungu wenu, aliyewatendea mambo ya ajabu; na watu wangu hawatatahayari kamwe. Nanyi mtajua ya kuwa mimi ni katikati ya Israeli, na ya kuwa mimi ndimi Bwana, Mungu wenu, wala hakuna mwingine; na watu wangu hawatatahayari kamwe.




Utangulizi:

Ni muhimu kufahamu kuwa wakati mwingine katika maisha ya mwanadamu duniani huwa kunakuwa na maafa yanayojitokeza katika nyanja mbalimbali za mifumo ya kimaisha, maafa hayo yanaweza kuwa ya kiroho, kisiasa, kiuchumi na kimwili. Aidha aina hizi za maafa sio ngeni kwa ulimwengu na kwa watu wa Mungu likiwemo taifa la Israel, Wana wa Israel walikuwa na ufahamu wa kina kuhusiana na aina hizi za maafa zilizokuwa zimewakuta na kuwapata katika taifa lao, na hivyo walikuwa na ujuzi wa kutafasiri na kuelewa kwa kina kile ambacho manabii walikizungumza kwa uwazi au kwa mafumbo na hii iliwasaidia kutambua mpango na makusudi ya Mungu katika maisha yao sawa na Maneno ya manabii. Nabii Yoeli alikuwa moja ya manabii walioweza kuainisha wazi na kuijulisha jamii yake kwa habari ya maafa hayo au majanga lakini sio hivyo tu njia ya kuondoa majanga hayo na namna ambavyo Mungu angeyakomesha maafa hayo na kuwapa miaka ya neema au ya urejesho

Yoeli 1:2-4 “Sikieni haya, enyi wazee; Sikilizeni, enyi wenyeji wote wa nchi. Je! Mambo haya yamekuwako katika siku zenu, Au katika siku za baba zenu? Waarifuni watoto wenu habari yake, Watoto wenu wakawaambie watoto wao, Na watoto wao wakakiambie kizazi kingine. Yaliyosazwa na tunutu yameliwa na nzige; na yaliyosazwa na nzige yameliwa na parare; na yaliyosazwa na parare yameliwa na madumadu.”

Unaona hapo nabii alitangaza maafa ya kiroho, kisiasa na kiuchumi kwa wana wa Israel na kisha baadaye aliwapa njia ya namna ya kufanya ili kurejesha neema ya Mungu katika maisha yao na kisha alitangaza kurejeshwa kwa miaka hiyo ya hasara, ujumbe huu leo uko wazi kwaajili ya ulimwengu, Israel, Kanisa, taifa, jamii, familia na kila mtu mmoja mmoja kwa nafasi yake na maisha yake kwa hiyo ni muhimu kuzingatia kile ambacho Mungu anataka kusema nasi leo jambo litakaloutaufanya mwaka mpya huu  na miaka mingine kwako kuwa mwaka wa neema kuliko majira na nyakati ulizozipitia katika maisha yako, kwa sababu hiyo Leo tutajifunza somo hili “Kurejeshwa kwa miaka ya hasara” kwa kuzingatia vipengele vitatu vifuatavyo:- 


Kutangazwa kwa miaka ya hasara.

Namna ya kuondoa miaka ya hasara. 

Kurejeshwa kwa miaka ya hasara


Kutangazwa kwa miaka ya hasara

Nabii Yoel alipokea ujumbe wake kama neno la Mungu kwa utawala wa Yuda lakini pia ukiuhusu ulimwengu wote, Yoeli alikuwa na makusudi makubwa matatu tu, kutangaza hukumu ya Mungu inayokuja kwa utawala wa Yuda, kuwaita watu pamoja ili waweze kumrudia Mungu kwa toba na kutangaza neema ya Mungu Kwa watu wake wanapokubali kujinyenyekeza, anapotangaza ujumbe wake nabii huyu hususani katika eneo la kwanza lakutangaza hukumu ya Mungu, kimsingi nabii anazungumza kuwa hukumu hii ya Mungu kwa watu wake itahusu, maswala yote muhimu ya mwanadamu, kiroho, kisiasa na kiuchumi, kuwa endapo watu wake Mungu wangeendelea katika mfumo wa maisha ya kutokujali kuhusu Mungu, Mungu angeinua taifa lenye nguvu, au mataifa adui yenye nguvu yatakayoishambulia Yuda na kuleta maafa katika taifa lao, hali ya kiroho ya Taifa, kanisa, familia na mtu mmoja mmoja ina mchango mkubwa sana katika kuamua mustakabali wa kisiasa na kiuchumi katika maisha ya taifa, kanisa na mtu awayeyote yule.

Yoeli 1:2-4 “Sikieni haya, enyi wazee; Sikilizeni, enyi wenyeji wote wa nchi. Je! Mambo haya yamekuwako katika siku zenu, Au katika siku za baba zenu? Waarifuni watoto wenu habari yake, Watoto wenu wakawaambie watoto wao, Na watoto wao wakakiambie kizazi kingine. Yaliyosazwa na tunutu yameliwa na nzige; na yaliyosazwa na nzige yameliwa na parare; na yaliyosazwa na parare yameliwa na madumadu.”

Tangazo la nabii Yoeli limewasumbuwa watafasiri wengi wa Biblia hususani katika pigo la tunutu, nzige, parare na madumadu, hii ni kwa sababu nabii alitumia mfano wa wadudu waharibifu wa mazao kuzungumzia uharibifu wa kisiasa, kiuchumi na kiroho kwa watu wa taifa lake, Yuda.  Israel kama ilivyo hapa Afrika huwa tunafahamu kuwa ziko nyakati ambapo, katika secta za kilimo hutokea wadudu waharibifu wa mazao ambao kimsingi husababisha hasara kubwa sana na hata kuleta njaa na uharibifu mkubwa wa mazao ya chakula, wadudu hao Kwa kawaida huvamia kama jeshi, na wanajulikana kama tunutu, nzige, parare na madumadu, kwa hiyo Yoeli anawatumia wadudu hawa kutangaza miaka ya hasara kiroho, kisiasa na kiuchumi. Kimsingi Yoel hazungumzii wadudu halisi bali anazungumzia Mataifa mabaya ambayo yataivamia Israel na mataifa hayo yatakuwa yameruhusiwa na Mungu kuwaumiza na kuwaletea hali ngumu kwa sababu ya dhambi zao, Yoeli anatumia uzoefu wa wadudu waharibifu wa mazao kuwakilisha uharibifu wa taifa, kisiasa, kiuchumi na ambako kumesababishwa na hali yao ya kiroho.

Muda wa hasara ungeweza kuhusisha uharibifu katika maeneo kadhaa, kiuchumi, kisiasa, na kiroho muda huo hapa umeitwa miaka, lakini ni nyakati na majira ambayo Mungu amekusudia upite ko sio lazima iwe miaka:-

Kiuchumi – Watu  walioishi siku nyingi na wale watakaoishi siku nyingi yaani wenye uzoefu ambao nabii anawataja kama wazee watakuwa wanafahamu maafa ya kiuchumi yanayosababishwa na wadudu waharibifu kama tunutu, nzige, parare na madumadu, Yoeli aliwadhihirishia wazee yaani wenye uzoefu kufikiri na kutafakari kuwa hali kama hiyo kama umewahi kwako katika nyakati zao, wajitafakari kwani hali ambayo ingewakuta hata wazee, na wenyeji wa nchi wasingeliweza kuamini kwani lilikuwa ni pigo la kiuchumi la kihistoria ambalo halijawahi kutokea katika maisha yao

Yoeli 1:2-4 “Sikieni haya, enyi wazee; Sikilizeni, enyi wenyeji wote wa nchi. Je! Mambo haya yamekuwako katika siku zenu, Au katika siku za baba zenu? Waarifuni watoto wenu habari yake, Watoto wenu wakawaambie watoto wao, Na watoto wao wakakiambie kizazi kingine. Yaliyosazwa na tunutu yameliwa na nzige; na yaliyosazwa na nzige yameliwa na parare; na yaliyosazwa na parare yameliwa na madumadu.”

Tunutu hawa ni jamii ya panzi/nzige wakiwa katika hatua ya kuwa kama buu au kiwavi, hapa kwetu wanaitwa viwavi jeshi kwa kawaida hawa ni waharibifu sana viwavi wanapovamia shamba kwa muda mfupi huwa wanashambulia Matunda au maua ambayo yanaelekea kuzaa matunda na hivyo kusababisha tunda lisizaliwe au kama tunda limezaliwa lioze kwa hiyo wadudu hawa huharibu MATUNDA ya mimea yaliyozaliwa au yanayotaka kuzaliwa

Nzige hawa ni jamii ya panzi ambao huruka kwa makundi makubwa sana yenye kutisha nao pia kama viwavi jeshi huweza kushambulia MAJANI ya mazao na kusababisha uharibifu mkubwa wa mazao, na kuleta njaa na kuathiri uchumi wa watu

Parare ni jamii ya panzi ambao nao kimsingi huweza kushambualia MATAWI na vijiti na kuvitafuna na kuozesha kabisa, kama mmea unaweza kushambuliwa na nzige na kisha wasije hawa parare mmea unaweza kupata nguvu na kustawi tena lakini wakija parare wao hula kabisa matawi na kuacha miti ikiwa imesalia kama kijiti kilichosimama, kikavu na  kuharibu kabisa ustawi wa mmea na kusababisha majanga ya njaa

Madumadu wao huja kumalizia MTI wenyewe na kuutafuna mpaka kubakiza shina tu, lakini kama haitoshi Madumadu huwa wanaharufu mbaya kama utawakanyaga na kuwauwa wao ni wakubwa zaidi na ni wanye kutia kinyaa kabisa sehemu nyingine panzi hawa jamii ya madumadu huitwa panzia kunuka kwa hiyo endapo Mungu angeruhusu wadudu hao kuivamia inchi ukweli ni kuwa hali ya uchumi wanchi au taifa au kanisa au mtu mmoja mmoja ingwakuwa iko katika hali ngumu wao humalizia kabisa mmea na kuua


Kisiasa – Yoeli aliendelea kuweka wazi kuwa hukumu ya Mungu kwa watu wa Mungu isingelikuwa ya kiuchumi pekee, bali ingelihusu pia hali ya kisiasa ambayo ingewatesa Israel kwa ukoloni tofauti na ule waliowahi kuusikia huko Misri, Mungu angeleta hukumu ya kisiasa ambako Israel na Yuda wangekwenda utumwani na kuwa chini ya tawala kubwa za dunia za nyakati hizo Falme hizo zingeinuka kutoka kaskazini mwa Yuda na kusababisha maafa sawa tu na wadudu waharibifu wanavyoweza kushambulia mti au mazao, mataifa hayo yanatajwa kama mataifa nyenye nguvu na wenye jeshi kubwa na wakali na wangeharibu watu wa Mungu na kuwachukua na kuwapeleka utumwani na wangeondoa kabisa ustawi wa kiroho na kimwili na kiuchumi wa taifa la Mungu na wangejaribu kuwatawanya kabisa Wayahudi ona 


Yoeli 1:6-7 “Maana taifa limepanda juu ya nchi yangu, Lenye nguvu, tena halina hesabu; Meno yake ni kama meno ya simba, Naye ana magego ya simba mkubwa. Ameuharibu mzabibu wangu; ameuvunja mtini wangu; ameyaambua magamba yake kabisa; ameuangusha chini; matawi yake yamefanywa kuwa meupe.”


Tunutu – Wangewakilisha utawala wa Ashuru na Babeli (900-600BC) Israel wangepoteza utawala wa kisiasa chini ya dola kubwa ya Ashuru na Yuda wangepoteza utawala wa kisiasa chini ya utawala wa Babeli, Amani na utulivu pamoja na furaha ya Israel au watu wa Mungu ingeweza kutoweshwa kabisa na mataifa hayo yenye nguvu 


Yoel 1:10-12 “Shamba limeharibika, nchi inaomboleza; maana nafaka imeharibika, divai mpya imekauka, mafuta yamepunguka. Tahayarini, enyi wakulima; Pigeni yowe, enyi watunzaji wa mizabibu; Kwa ajili ya ngano na shayiri, Maana mavuno ya mashamba yamepotea. Mzabibu umesinyaa, mtini nao umevia; Nao mkomamanga na mtende na mtofaa; Naam, miti yote ya mashamba imekauka; Maana furaha imekauka katika wanadamu.”


Nzige – Wangewakilisha utawala uliofuata baada ya kuanguka kwa utawala wa Babeli ambao ni Waamedi na Waajemi (550-331BC) kimsingi hawa nao wangeendeleza uharibifu ule ule ulioanzishwa na tunutu, wao wangeendelea kula majani na magamba ya mti na kuuacha mti huu ukiwa uchi na chini ya aibu, kubwa sana na hatari ya kifo cha mti husika.


Parare –Wangewakilisha utawala wa Wayunani/Wagiriki (800-146 BC) wao wangesababisha ukimya kabisa kwa wana wa Israel na wangeweza kubalisha kabisa mtazamo wao na kuwaingizia elimu na falsafa na mitazamo mipya kutokana na Maendeleo ya kielimu waliyokuwa nayo wayunani, Parare walikula kabisa matawi na kuufanya mti usionekane tena wala kujulikana kuwa ni mti wa namna gani na mti ungepoteza sura yake 


Madumadu – wanawakilisha utawala wa kisiasa wa Warumi, (31 BC-476 AD) Israel wote wangekuwa chini ya utumwa  na kutiwa unajisi na watu hawa, ambao wangemsulubisha hata masihi, na kuiharibu kabisa Yerusalem na kuwaondoa kabisa wayahudi na kuwatawanya Dunia nzima wasiwepo katika nchi ya Yuda kabisa kwa hiyo sio tu kuwa Matunda ya mti yangeliwa, au majani ya mti yangeliwa au matawi na maganda yake yangeliwa lakini mti ungeliwa kabisa na kuozeshwa na kuharibiwa mpaka shinani Warumi ndio waliowaondoa Israel na kuwatawanya wayahudi wengi duniani na kuwahamisha Israel kabisa lakini pia walimsulubisha Masihi 


Kiroho – uharibifu ambao ulifanywa na mataifa haya sio tu ulihusu uchumi na siasa lakini vile vile ulihusu swala zima la kiroho, uchumi unapoguswa na siasa inapoguswa hali ya kiroho haiwezi kuwa salama kwa hiyo Yoeli anaonyesha kuwa hata Imani iliguswa katika maafa hayo aliyoyatabiri, Inawezekana wakati mwingine sio mara zote hali ya kiroho ikiwa mbovu ikasababisha hali ya uchumi na siasa pia kuwa mbovu, au hali ya uchumi na siasa ikiwa mbovu, wito wa kuweka sawa ya maswala kiroho yanaweza kurejesha uponyaji wa kitaifa, kisisasa na kiuchumi, Yoeli anaonyesha kuwa mapigo hayo pia yaliunganishwa na hali ya kiroho.


Yoeli 1: 13-14 “Jikazeni mkaomboleze, enyi makuhani; Pigeni yowe, enyi wahudumu wa madhabahu; Njoni mlale usiku kucha katika magunia, Enyi wahudumu wa Mungu wangu; Kwa kuwa sadaka ya unga na sadaka ya kinywaji Zimezuiwa katika nyumba ya Mungu wenu.Takaseni saumu, iteni kusanyiko la dini, Wazee na wakusanye wenyeji wote wa nchi; Waende nyumbani kwa Bwana, Mungu wenu, Na kumlilia Bwana,”


Tunutu – Wanasahambulia “TUNDA LA ROHO” au matunda ya kiroho, ile hali njema ya watu wa Mungu kuwa na upendo, furaha, Amani, uvumilivu. Utu wema, fadhili, uaminifu, upole na kiasi katika jamii sasa imetoweka imeliwa na tunutu, Yoeli analiona taifa na kanisa kuwa limepoteza haki, limepoteza ile hali ya kuwa na sifa ya watu wacha Mungu, dhuluma kila mahali, kiburi na majivuno, unibafsi na choyo, chuki na mafarakano, uchawi na uadui ndio ambao unachukua nafasi sasa na kuondoa upendo wa kwanza, sio hivyo tu kunaupungufu mkubwa wa matendo ya ajabu, miujiza na uponyaji pamoja na utendaji wa karama za Roho Mtakatifu, kanisa limeachwa jeupee na maombi ya dhati na kuugua hayapo. 


Yoeli 1:7 “Maana taifa limepanda juu ya nchi yangu, Lenye nguvu, tena halina hesabu; Meno yake ni kama meno ya simba, Naye ana magego ya simba mkubwa.”


Ufunuo 2:4-5 “Lakini nina neno juu yako, ya kwamba umeuacha upendo wako wa kwanza.Basi, kumbuka ni wapi ulikoanguka; ukatubu, ukayafanye matendo ya kwanza. Lakini, usipofanya hivyo, naja kwako, nami nitakiondoa kinara chako katika mahali pake, usipotubu.”


Nzige – Inawakilisha kutoweka kwa “NENO LA MUNGU”, Hapa hakuna unabii na hali ya neno la Mungu limekuwa adimu, zaidi ya yote kuchakachuliwa kwa Neno na tafasiri zake halali, kila mmoja anatafasiri neno anavyojisikia na unabii unafifia, ni manabii wachache sana labda Daniel tu walioweza kusema chochote walipokuwa utumwani Babeli, lakini wakati wa utawala wa Uajemi na uamedi, hakukuwa tena na nabii na ukimya ukatawala kwa muda mrefu, katika maafa ya kiroho yanayoweza kuwakumba watu wa Mungu ni pamoja na kutokuwepo kwa unabii ambao kimsingi unatoa mwelekeo wa watu wa Mungu na kuwatia moyo, aidha kama hakuna wahudumu halali wa neno la Mungu wanaowasaidia watu wa Mungu kujua NENO, jamii ya watu wa Mungu inaathirika na kuwa kama imevuliwa nguo, Neno la Mungu ndilo linalochochea utendaji wa Roho Mtakatifu. Kwa hiyo wakati neno la Bwana linapokuwa adimu, Roho wa Mungu hutulia na hivyo kuzimishwa.


Mwanzo 1:2 “Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji; Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji.”


1Samuel 3:1 “Basi, mtoto Samweli akamtumikia Bwana mbele ya Eli. Na neno la Bwana lilikuwa adimu siku zile; hapakuwa na mafunuo dhahiri.”


Yoeli 1:16-17 “Je! Chakula hakikukatiliwa mbali mbele ya macho yetu? Naam, furaha na kicheko mbali na nyumba ya Mungu wetu? Mbegu zinaoza chini ya udongo wake; ghala zimeachwa ukiwa; mabanda yamevunjika; kwa maana nafaka imekauka.”


Parare – wenyewe wanahusika na kupotea kwa UTAKATIFU Parare wanahusika na uharibifu  na wakati huu wanaharibu kabisa matawi na maganda ya mti, wanaharibu muonekano halisi wa mti, hii inaashiria kuondoka kwa hofu ya Mungu, watu kuacha kuishi kwa uadilifu na mwenendo wa njia za Mungu, watu hawawezi tena kuushinda ulimwengu, wala hakuna tena mahubiri yanayozungumia au kuelekeza watu kuishi maisha matakatifu, wala watumishi wa Mungu wanaokemea dhambi kwa viwango vya juu, hakuna tena mtu na nayeweza kukaza kama na kuhubiri Utakatifu kama walivyofanya mitume ona

1Petro 1:15-16 “bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote; kwa maana imeandikwa, Mtakuwa watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu.”


2Timotheo 2:19 “Lakini msingi wa Mungu ulio imara umesimama, wenye muhuri hii, Bwana awajua walio wake. Na tena, Kila alitajaye jina la Bwana na auache uovu.”


Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao;” 


Madumadu – Mti umeliwa mpaka shinani na unaoza hii ni hali ya kutoweka kwa matumaini na ni wakati ambapo imani imekwisha na ni kipindi cha GIZA/KUFA KIROHO – kila kitu kimekufa na limebaki jina tu, uko uwezekano wa taifa, au kanisa au mtu fulani mmoja mmoja kubakia na jina tu lakini hali ya kiroho inakuwa imekufa kabisa mmea hauna matunda, hauna majani, na matawi yameliwa na shina lake linabaki limeoza, katika hali kama hiyo hakuna matunda ya kiroho, Neno la Mungu limechakachuliwa, hakuna msisitizo wa kujaa nguvu za Roho Mtakatifu, hakuna mkazo wa utakatifu na uchafu unabaki katika kanisa, kuchukulina na dunia, hakuna haki, upendeleo unachukua nafasi, majungu masengenyi na Kila aina ya ubaya na hata kuuana na kurogana mwili mwili mwili unakuwa katika nafasi ya kiroho, hakuna imani. Watu wamepoteza umakini wa kimaadili na wameleweshwa katika anasa na upatikanaji wa mali za duniani 


Yoel 1:5 “Levukeni, enyi walevi, mkalie; Pigeni yowe, ninyi nyote mnywao divai; Kwa sababu ya divai mpya; Maana umekatiliwa mbali na vinywa vyenu.” 


Ufunuo 3:1 “Na kwa malaika wa kanisa lililoko Sardi andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye na hizo Roho saba za Mungu, na zile nyota saba. Nayajua matendo yako, ya kuwa una jina la kuwa hai, nawe umekufa.”


Luka 18:8 “Nawaambia, atawapatia haki upesi; walakini, atakapokuja Mwana wa Adamu, je! Ataiona imani duniani?


Kwa hiyo tunaweza kuona jinsi nabii Yoeli alivyokuwa akiionya jamii dhidi ya ujio wa miaka ya hasara, Mungu alikuwa amempa neno la maonyo na kuwaonya watu wake dhidi ya uharibifu na maafa ya kiuchumi, kisiasa na kiroho, huu ni ujumbe kwa ulimwengu mzima kwa kila taifa na kanisa na mtu mmoja mmoja, wakati wote kila taifa litakapopuuzia maswala ya Mungu ni lazima ijulikane wazi kuwa Mungu ataondoa mkono wake na kumruhusu yule alaye aweze kuharibu kila kitu, Ustawi wa taifa lolote na kanisa familia na mtu mmoja mmoja unategemeana na namna tunavyompa Mungu heshima katika kila eneo, kama tutaruhusu ufisadi, mmomonyoko wa uadilifu rushwa na dhuluma kila mahali, tujue wazi kabisa Mungu ataiondoa heshima yake katika kanisa au taifa  Mithali 14:34 “Haki huinua taifa; Bali dhambi ni aibu ya watu wo wote.” Hata hivyo ikiwa hali kama hizo zimelikuta taifa, au kanisa au mtu binafsi bado liko tumaini kwa kuwa Mungu ni mwingi wa rehema na si mwepesi wa hasira ni Mungu ambaye hatatulipa sawasawa na makosa yetu yeye kama Baba anavyowahurumia watoto wake ndivyo Anavyowahurumia wale wamchao naye anatoa njia ya kufanya ili kuondoa miaka ya hasara au kwa lugha nyingine muda wa hasara, hilo linatupa neema ya kutafakari kipengele cha pili.


Namna ya kuondoa miaka ya hasara

Ni ukweli ulio wazi kuwa licha ya nabii Yoeli kutoa maonyo kwa watu wa Mungu juu ya kupatwa na mambo mabaya au juu ya taifa kupitia miaka ya hasara nabii Yoeli anatoa wito wa kutubu ili Mungu aweze kuleta uamsho, na ufufuo na urejesho kwa miaka iliyoliwa na tunutu, nzige, parare, na madumadu, wakati wowote tunapotaka kuona Mungu akiliponya kanisa, taifa au watu wake katika Nyanja zote za kisiasa, kiuchumi na kiroho, ni silaha za kiroho pekee ndizo zinazoweza kuleta uponyaji wa mazingira yote makubwa na silaha hiyo ni unyenyekevu na toba ya kweli na hiki ndicho anachokisema Yoeli

Yoeli 1:13-14 “Jikazeni mkaomboleze, enyi makuhani; Pigeni yowe, enyi wahudumu wa madhabahu; Njoni mlale usiku kucha katika magunia, Enyi wahudumu wa Mungu wangu; Kwa kuwa sadaka ya unga na sadaka ya kinywaji Zimezuiwa katika nyumba ya Mungu wenu. Takaseni saumu, iteni kusanyiko la dini, Wazee na wakusanye wenyeji wote wa nchi; Waende nyumbani kwa Bwana, Mungu wenu, Na kumlilia Bwana,” 

Yoeli 2:12-17 “Lakini hata sasa, asema Bwana, nirudieni mimi kwa mioyo yenu yote, na kwa kufunga, na kwa kulia, na kwa kuombolea; rarueni mioyo yenu, wala si mavazi yenu, mkamrudie Bwana, Mungu wenu; kwa maana yeye ndiye mwenye neema, amejaa huruma; si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema, naye hughairi mabaya. N'nani ajuaye kwamba hatarudi na kugeuka, na kutuachia baraka nyuma yake, naam, sadaka ya unga, na sadaka ya kinywaji, kwa Bwana, Mungu wenu? Pigeni tarumbeta katika Sayuni, Takaseni saumu, kusanyeni kusanyiko kuu; Kusanyeni watu, litakaseni kusanyiko, Kusanyeni wazee, kusanyeni watoto, Na hao wanyonyao maziwa; Bwana arusi na atoke chumbani mwake, Na bibi arusi katika hema yake. Hao makuhani, wahudumu wa Bwana, na walie Kati ya patakatifu na madhabahu, Na waseme, Uwaachilie watu wako, Ee Bwana, Wala usiutoe urithi wako upate aibu, Hata mataifa watawale juu yao; Kwani waseme kati ya watu, Yuko wapi Mungu wao?” 

Wakati wowote hali inapokuwa mbaya katika jambo lolote nabii anatoa wito kwa watu wa Mungu kutubu kwa kumlilia Mungu, na kumuomba Mungu kwa kufunga na kuomba,  na hata kukesha usiku na mchana, wito huu unatolewa kwa watu wote kuanzia kwa makuhani yaani watumishi wa Mungu mpaka watu wengine wote, Nabii anaonyesha kuwa hii ndio namna ya kiroho ambayo Mungu alikuwa amemuagiza kuwa watu wafanye hivyo, akiwakumbusha kuwa Mungu ni wa neema na rehema  na kuwa amejaa huruma wala sio mwepesi wa hasira, na kuwa yeye hughairi mabaya, hii ndio njia iliyotumiwa na mataifa yote hata ya kipagani katika kujiokoa na hasira za Mungu pale zilipotangazwa

Yona 3:4-10 “Yona akaanza kuuingia mji mwendo wa siku moja, akapaza sauti yake, akasema, Baada ya siku arobaini Ninawi utaangamizwa. Basi watu wa Ninawi wakamsadiki Mungu; wakatangaza kufunga, wakajivika nguo za magunia, tangu yeye aliye mkubwa hata aliye mdogo. Habari ikamfikia mfalme wa Ninawi, naye akaondoka katika kiti chake cha enzi, akavua vazi lake, akajivika nguo za magunia, na kuketi katika majivu.Naye akapiga mbiu, akatangaza habari katika mji wa Ninawi, kwa amri ya mfalme na wakuu wake; kusema, Mwanadamu asionje kitu, wala mnyama wala makundi ya ng'ombe, wala makundi ya kondoo; wasile, wala wasinywe maji; bali na wafunikwe nguo za magunia, mwanadamu na mnyama pia, nao wakamlilie Mungu kwa nguvu, naam, na wageuke, kila mtu akaache njia yake mbaya, na udhalimu ulio mikononi mwake. Ni nani ajuaye kwamba Mungu hatageuka na kughairi, na kuiacha hasira yake kali, ili msiangamizwe? Mungu akaona matendo yao, ya kuwa wameiacha njia yao mbaya. Basi Mungu akalighairi neno lile baya, ambalo alisema atawatenda; asilitende.” 

Biblia imejaa mifano na maandiko ya kutosha yanayoonyesha kuwa kila wakati Mungu alipotaka kuadhibu au hata alipoadhibu toba ilileta mabadiliko makubwa, Bwana yuko tayari kughairi kila aina ya uovu alioukusudia au kuuruhusu endapo tu tutaitikia kwa toba kile ambacho neno la Mungu limetuagiza kukifanya hii ni kwa mtu mmoja mmoja, kwa taifa na kwa kanisa pia na watu wowote wanaotaka kuona mkono wa Mungu wa rehema ukiwa juu yao, ikiwa unaona wazi kuwa unapita katika miaka/muda iliyoliwa na tunutu, nzige, parare na madumadu basi changamkia agizo la toba na acha maovu yako nawe utaona uamsho mkubwa, mapinduzi makubwa ya kiuchumi, kisiasa na kiroho na mvua ya Baraka itanyesha juu yako., 

Unabii. Kuhusu 2025 na kuendelea!

Wakati Mungu ananipa ujumbe huu alitaka niseme wazi na mataifa ya Malawi na Kenya na Tanzania, alitaka pia niseme na ulimwengu na mtu mmoja mmoja lakini zaidi sana Malawi na Kenya, huku Tanzania ikijifunza kutoka katika unabii huo, “Mungu ameniambia kwa habari ya Malawi na Kenya, Kwamba siku za karibuni aliinua viongozi wacha Mungu katika mataifa hayo, yaani marais ambao wanamjua Mungu na wameokoka, lakini amenimeambia pamoja na hayo nchi hizo zinahali mbaya ya maporomoko makubwa ya kiroho, na kwa sababu hiyo uharibifu mkubwa unazipata nchi hizo, watapata majanga ya kawaida ya asili na njaa na mporomoko mkubwa ya kiuchumi na vurugu za hapa na pale, lakini sababu kubwa ni kuwakumbusha maraisi hao kuirudisha nchi ya Malawi na Kenya katika kilele, cha uchaji wa Mungu, hizi ni nchi ambazo Mungu alizikusudia ziwe nchi za kiinjilisti na kimisheni, lakini zimeacha wajibu huo na hivyo wanapaswa kutubu na wakifanya hivyo kutakuwa shwari Malawi na Kenya, Malawi Umisheni, Kenya Uinjilisti Kwa Tanzania Mungu amekuchagua kuwa Mwalimu wa neno la Mungu na mafundisho sahihi, lakini Mungu anaionya Tanzania kuwa nayo imeanza kuruhusu mafundisho potofu kuenea na injili imechakachuliwa katika taifa hili, Mungu anaionya Tanzania na kanisa la Tanzania kusimama imara katika kusimamia kweli ya Mungu vinginevyo iko hukumu nzito italijia taifa hili, lakini wakitubu na kila mtu akiisimamia kweli na kuacha kuichuja injili Tanzania itakuwa mfano wa kuigwa Afrika, aidha matukio ya kidunia yatakayojitokeza katika miaka hii kuanzia 2025, kutakuwa na uamsho mkubwa sana wa kasi katika Israel, katika jamii ya wayahudi, kiu ya kuwa taifa kubwa itaongezeka na kiu ya kulijenga Hekalu itawajia kwa nguvu, Israel itaendelea kuwa na nguvu kubwa sana na hakutakuwa na mtu wa kuwanyamazisha katika kile wanachotaka kukifanya Duniani, kutakuwa na maendeleo makubwa sana kwa Taifa la Saud Arabia, Jordan na Misri, lakini taifa la Iran litafifia sana kwa nguvu zake, kutakuwa na utulivu mkubwa sana katika taifa la Syria na watu wake watatulia na kujali katika kujijenga wenyewe kiuchumi na kimaendeleo na hawatatamani vita tena milele, viongozi wengi wa dunia wenye asili ya kidikteta wataangushwa madarakani, kutakuweko na viongozi wengi wenye kupigiwa kura za kutokuwa na Imani nao na wengi kuondolewa madarakani kwa kura za kibunge na maandamano ya wananchi, kutakuwa na uamsho mkubwa sana katika nchi ya Msumbiji, watanzania na wakenya wengi watahubiri Msumbiji na kuwa na makanisa makubwa sana, miujiza mingi na wahubiri wakubwa sana watapatikana Msumbiji na watu wengi watakuwa wakisafiri kwenda Msumbiji kwaajili ya maombi na maombezi, Aidha kutakuwa na watu wenye misimamo mikali wengi sana katika Imani ambao watakuwa na uelewa wa kumcha Mungu kwa viwango vya juu bila unafiki na watakuwa na wivu wa bwana hawa watainuka kwa wingi hususani Tanzania, aidha Muhubiri wa kimataifa aitwaye Bushiri huko Malawi, atang’ara sana  na kuwa tegemeo la watu wengi, Mungu atamtumia kwa viwango vikubwa sana na ninaambiwa atakuwa ni mtu mwenye upendo mwingi sana mimi simjui na simfuatilii sana, lakini Mungu atamtumia katika kilele chake”  Mwisho

Kurejeshwa kwa miaka ya hasara 

Yoeli sio tu kuwa alitangaza hukumu ya Mungu, lakini alionyesha njia ya kumrejea Mungu na kama hayo hayatoshi Yoeli anaonyesha na kutabiri kurejeshwa kwa hali ya kiroho na Baraka za Mungu ambazo kimsingi asili yake ni rohoni akionyesha kuwa Mungu atawahurumia watu wake na kusikia wivu kwaajili yao na kwa sababu hiyo atawajibu watu wake na kuwaponya kiroho, kimwili na kisiasa

Kiuchumi - Yoel 2:18-19 “Hapo ndipo Bwana alipoona wivu kwa ajili ya nchi yake, akawahurumia watu wake. Bwana akajibu, akawaambia watu wake; Tazameni, nitawaletea nafaka, na divai, na mafuta, nanyi mtashiba kwa vitu hivyo; wala sitawafanya tena kuwa aibu kati ya mataifa;”

KisiasaYoel 2:20-22 “lakini jeshi lililotoka kaskazini nitaliondolea mbali nanyi, nami nitalifukuza mpaka nchi ya ukame na ukiwa; sehemu yake iliyo mbele itaingia katika bahari ya mashariki, na sehemu yake iliyo nyuma itaingia katika bahari ya magharibi; na uvundo wake utapanda juu, na harufu yake mbaya itapanda juu, kwa sababu ametenda mambo makubwa.Ee nchi, usiogope; furahi na kushangilia; kwa kuwa Bwana ametenda mambo makuu.Msiogope, enyi wanyama wa kondeni; maana malisho ya jangwani yanatoa miche, na huo mti unazaa matunda yake, mtini na mzabibu inatoa nguvu zake.”

KirohoYoel 2:23-27 “Furahini, basi, enyi wana wa Sayuni, mkamfurahie Bwana, Mungu wenu; kwa kuwa yeye huwapa ninyi mvua ya masika, kwa kipimo cha haki, naye huwanyeshea mvua, mvua ya masika, na mvua ya vuli, kama kwanza. Na sakafu za kupepetea zitajaa ngano, na mashinikizo yatafurika kwa divai na mafuta.Nami nitawarudishia hiyo miaka iliyoliwa na nzige, na parare, na madumadu, na tunutu, jeshi langu kubwa nililotuma kati yenu.Nanyi mtakula chakula tele na kushiba, na kulihimidi jina la Bwana, Mungu wenu, aliyewatendea mambo ya ajabu; na watu wangu hawatatahayari kamwe.Nanyi mtajua ya kuwa mimi ni katikati ya Israeli, na ya kuwa mimi ndimi Bwana, Mungu wenu, wala hakuna mwingine; na watu wangu hawatatahayari kamwe.”

Hatimaye – Yoel 2:28-29 “Hata itakuwa, baada ya hayo, ya kwamba nitamimina roho yangu juu ya wote wenye mwili; na wana wenu, waume kwa wake, watatabiri, wazee wenu wataota ndoto, na vijana wenu wataona maono; tena juu ya watumishi wenu, wanaume kwa wanawake, katika siku zile, nitamimina roho yangu.”

Hatimaye Mungu ataleta uamsho mkubwa sana na kurejesha tena matunda ya roho, karama za Roho Mtakatifu na utendaji mkubwa wa Mungu, kila eneo la ustawi wa maisha ya mwanadamu litaimarika hii itatokea kwa taifa, itatokea kwa kanisa na ustawi wa mtu mmoja mmoja kwa kadiri anavyojitoa kwa Mungu na hiki ndio bwana anachotaka kukiona kama tutatudumu katika utakatifufu na imani na kuishi katika uweza na nguvu za Roho Mtakatifu basi tegemea Ustawi huu, tukidumu katika unyenyekevu na uaminifu  na kuwa mbali na ukaidi hakuna mtu atakaye tahayarika, Mungu atatuhurumia, na Roho wa Mungu atamwagwa kwa wingi na karama na madhihirisho yataachiwa katika kanisa na watu watakiri wazi kuwa Mungu yu katikati yenu.

Wishes Happy new year to you All, love you

Na. Rev. Mkombozi Samuel Kamote 

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima.


Jumapili, 29 Desemba 2024

Wale waliokwenda katika giza wameona nuru kuu!


Isaya 9:1-2 “Lakini yeye aliyekuwa katika dhiki hatakosa changamko. Hapo kwanza aliiingiza nchi ya Zabuloni na nchi ya Naftali katika hali ya kudharauliwa, lakini zamani za mwisho ameifanya kuwa tukufu, karibu na njia ya bahari; ng'ambo ya Yordani, Galilaya ya mataifa. Watu wale waliokwenda katika giza Wameona nuru kuu; Wale waliokaa katika nchi ya uvuli wa mauti, Nuru imewaangaza.”




Utangulizi:

Moja ya habari za kinabii za kutia moyo na kuleta tumaini kwa jamii ni pamoja na ujio wa Masihi, Yesu Kristo Mwana wa Mungu aliye hai ambaye angeleta Nuru kwa watu waliokuwa gizani, na kuwaangazia tumaini watu waliokaa katika inchi ya uvuli wa mauti, Kimsingi giza pamoja na uvuli wa mauti ni hatia, hukumu, ni kupoteza tumaini, ni kuishi mbali na Mungu, ni kukosa muelekeo, pamoja na mateso yanayoambatana na kukata tamaa ambavyo vinawasumbua wanadamu kila iitwapo leo, kuzaliwa kwa Yesu Kristo kungekuwa ni sehemu muhimu ya kutimia kwa unabii huu ambao kimsingi ni habari njema zenye kuleta tumaini la Rehema kuu za Mungu kwa watu wote, kimsingi Kristo Yesu alipokuja Duniani alijitangaza rasmi kuwa yeye ni Nuru ya ulimwengu.

Yohana 8:12 “Basi Yesu akawaambia tena akasema, Mimi ndimi nuru ya ulimwengu, yeye anifuataye hatakwenda gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima.”

Nuru ni ishara ya wema wa Mungu kwa wanadamu, na giza ni ishara ya uovu uonevu na utendaji wa ibilisi, Maisha ya Bwana wetu Yesu Kristo ni Nuru inayong’aa gizani, ambayo imekuja ulimwenguni kwa kusudi la kuwapa tumaini na kuwaondoa hofu wale wote waliokuwa wanakabiliwa na giza la uovu na uvuli wa Mauti. Wakati Yesu anazaliwa kimsingi watu walikuwa wamechoka sana, walikuwa wamekata tamaa, ukiacha ukoloni mzito  wa Warumi uliokuwa ukiwatawala kiserikali, maisha yao yalijawa na mateso, kukata tamaa na kufunikwa na giza la kiroho, miaka mingi karibu 400 ilikuwa imepita kukiwa na ukimya bila ya kuweko kwa nabii wala neno la Mungu la Dhahiri kwaajili yao, tumaini lilikuwa limebaki moja tu, kusubiri kutimizwa kwa unabii wa kuhusu kuja kwa Masihi, kiu yao hii inaonekana wazi hata Yohana alipokuwa ameanza kuhubiri ubatizo wake wa toba Maswali mengi yalielekea katika  kiu na hamu na shauku ya kumtamani Masihi ili aweze kukomesha mateso yao.

Yohana 1:20-23 “Naye alikiri, wala hakukana; alikiri kwamba, Mimi siye Kristo. Wakamwuliza, Ni nini basi? U Eliya wewe? Akasema, Mimi siye. Wewe u nabii yule? Akajibu, La. Basi wakamwambia, U nani? Tuwape majibu wale waliotupeleka. Wanenaje juu ya nafsi yako? Akasema, Mimi ni sauti ya mtu aliaye nyikani, Inyosheni njia ya Bwana! Kama vile alivyonena nabii Isaya.”              

Kwa nini kulikuwa na maswali mengi sana kwa Yohana Mbatizaji, kwa sababu watu walikuwa wamechoka sana na sasa walikuwa wakimtazamia Masihi aje kuwakomboa na kuwatoa katika maisha yaliyogubikwa na giza nene, tunapoadhimisha kuzaliwa kwa Yesu Kristo, neno la Mungu linatukumbusha kuwa hatupaswi tena kuishi maisha ya mashaka, ya kukata tamaa, ya kutokuwa na matumaini, maisha ya machozi, na kuweko gizani, kwa sababu Nuru imekuja ulimwenguni, kimsingi sio Israel pekee waliokuwa wakimtarajia masihi lakini mataifa yote duniani ujio wa masihi ungekuwa ni habari njema za kuleta matumaini makubwa sana na kuondoa hofu.

Luka 2:8-14 “Na katika nchi ile ile walikuwako wachungaji wakikaa makondeni na kulinda kundi lao kwa zamu usiku.Malaika wa Bwana akawatokea ghafula, utukufu wa Bwana ukawang'aria pande zote, wakaingiwa na hofu kuu.Malaika akawaambia, Msiogope; kwa kuwa mimi ninawaletea habari njema ya furaha kuu itakayokuwa kwa watu wote; maana leo katika mji wa Daudi amezaliwa, kwa ajili yenu, Mwokozi, ndiye Kristo Bwana.Na hii ndiyo ishara kwenu; mtamkuta mtoto mchanga amevikwa nguo za kitoto, amelala katika hori ya kulia ng'ombe. Mara walikuwapo pamoja na huyo malaika, wingi wa jeshi la mbinguni, wakimsifu Mungu, na kusema, Atukuzwe Mungu juu mbinguni, Na duniani iwe amani kwa watu aliowaridhia.”                 

Tutajifunza somo hili Wale waliokwenda katika giza wameona nuru kuu. Kwa kuzingatia vipengele viwili muhimu vifuatavyo:-

 

·         Maana ya kwenda katika giza na kukaa katika nchi ya uvuli wa mauti

·         Wale waliokwenda katika giza wameona Nuru kuu!

 

Maana ya kwenda katika giza na kukaa katika nchi ya uvuli wa mauti

Neno kwenda katika giza, katika lugha ya kiebrania linatumika neno “chôshek” kwa kiingereza “destruction” kwa Kiswahili kukaa katika “uharibifu” au kukaa katika uovu, Kabla ya ujio wa Yesu Kristo watu waliishi katika giza kubwa la kiroho, watu walikuwa hawana mwelekeo na hawaijui njia kwa sababu hiyo giza lilitawala na ukiwa ulikuwa juu ya nchi, Nguvu za wakuu wa giza ndizo zilizokuwa zinatawala ulimwengu, matendo ya giza yalikuwa yanatawala ulimwengu, Giza lilitawala kabla ya Nuru ya injili kuwazukia watu hivyo watu walikuwa wanaenenda gizani, watu walikuwa hawawezi wala hawana njia ya kurejesha uhusiano wao na Mungu ambao uliharibika tangu anguko la wazazi wetu Adam na Eva, Ni ujio wa Yesu Kristo ndio ulioleta Nuru ulimwenguni.

-          Yohana 4:4-10 “Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu. Nayo nuru yang'aa gizani, wala giza halikuiweza. Palitokea mtu, ametumwa kutoka kwa Mungu, jina lake Yohana. Huyo alikuja kwa ushuhuda, ili aishuhudie ile nuru, wote wapate kuamini kwa yeye. Huyo hakuwa ile nuru, bali alikuja ili aishuhudie ile nuru. Kulikuwako Nuru halisi, amtiaye nuru kila mtu, akija katika ulimwengu. Alikuwako ulimwenguni, hata kwa yeye ulimwengu ulipata kuwako, wala ulimwengu haukumtambua

 

-          Wakolosai 1:12-14 “mkimshukuru Baba, aliyewastahilisha kupokea sehemu ya urithi wa watakatifu katika nuru. Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake; ambaye katika yeye tuna ukombozi, yaani, msamaha wa dhambi;”

 

-          1Yohana 1:5-7 “Na hii ndiyo habari tuliyoisikia kwake, na kuihubiri kwenu, ya kwamba Mungu ni nuru, wala giza lo lote hamna ndani yake.Tukisema ya kwamba twashirikiana naye, tena tukienenda gizani, twasema uongo, wala hatuifanyi iliyo kweli; bali tukienenda nuruni, kama yeye alivyo katika nuru, twashirikiana sisi kwa sisi, na damu yake Yesu, Mwana wake, yatusafisha dhambi yote.”

 

-          Mika 7:7-8 “Lakini mimi, nitamtazamia Bwana; nitamngojea Mungu wa wokovu wangu; Mungu wangu atanisikia. Usifurahi juu yangu, Ee adui yangu; niangukapo, nitasimama tena; nikaapo gizani, Bwana atakuwa nuru kwangu.”                  

 

-          Zaburi 88:3-12 “Maana nafsi yangu imeshiba taabu, Na uhai wangu umekaribia kuzimu. Nimehesabiwa pamoja nao washukao shimoni; Nimekuwa kama mtu asiye na msaada. Miongoni mwao waliokufa nimetupwa, Kama waliouawa walalao makaburini. Hao ambao Wewe huwakumbuki tena, Wametengwa mbali na mkono wako. Mimi umenilaza katika shimo la chini, Katika mahali penye giza vilindini. Ghadhabu yako imenilemea, Umenitesa kwa mawimbi yako yote. Wanijuao umewatenga nami; Umenifanya kuwa chukizo kwao; Nimefungwa wala siwezi kutoka. Jicho langu limefifia kwa ajili ya mateso Bwana, nimekuita kila siku; Nimekunyoshea Wewe mikono yangu. Wafu je! Utawafanyia miujiza? Au waliofariki watasimama na kukuhimidi? Fadhili zako zitasimuliwa kaburini? Au uaminifu wako katika uharibifu? Miujiza yako itajulikana gizani? Au haki yako katika nchi ya usahaulifu?

 

Unapozisoma aya kadhaa za kibiblia hapo juu utaweza kugundua kuwa Giza ni baya sana na giza lina uhusiano wa karibu sana na mauti, giza humfanya mtu asiwe na msaada, giza ni sawa na mtu aliyetupwa miongoni mwa watu waliokufa, giza ni kukosa tumaini la kimwili na kiroho, giza ni kama kuwa shimoni, giza linakufanya usipambanue kati ya kifo na uhai, giza linamfanya mtu apoteze kibali, giza linamfanya mtu awe chukizo, giza linamfanya mtu asifurahie maisha kwa hiyo giza ni njia ya uovu, giza ni uharibifu, giza ni kuwa chini ya ukoloni wa kiroho, wa kimwili, wa kisiasa, wa kiuchumi, giza humfanya mwanadamu aishi kwa mashaka na kwa kubahatisha, mtu aliye gizani haoni mbele yake kukoje zaidi ya kuona giza, maisha ya dhambi, na ukosefu mkubwa wa kimaadili ni kutembea katika giza, giza pia linawakilisha hukumu, giza linawakilisha hofu na msahaka, giza ni bumbuwazi, giza kuchanganyikiwa na kutokuona.

Kutoka 10:21-23 “BWANA akamwambia Musa, Nyosha mkono wako kuelekea mbinguni, kuwe giza juu ya nchi ya Misri, watu wapapase-papase gizani. Basi Musa akaunyosha mkono wake kuelekea mbinguni; kukawa na giza nene katika nchi yote ya Misri muda wa siku tatu; hawakupata kuonana mtu na mwenziwe, wala hakuondoka mtu mahali alipokuwa muda wa siku tatu; lakini wana wa Israeli wote walikuwa na mwanga makaoni mwao.”

Sio hivyo tu Giza liliwakilisha hali ya mauti, au uvuli wa mauti “sheol” Msiba, kaburi au kuzimu yaani mwanadamu kupita katika msongo mkubwa wa mawazo wa kutokujua nini cha kufanya sawa tu na mtu aliyekuzimu, Katika Israel pia yalikuweko mapango ya kutisha ambapo watu waliokuwa wakichunga wanyama wakati mwingine walipenya katika mapango hayo ya kutisha kwa kusudi la kutokea katika eneo la kuwapa malisho wanyama wao ambayo pia waliyaita uvuli wa mauti, mapito mazito na huzuni unazozipitia ambazo hujui zitaisha lini ni giza, lakini ukiwa na Yesu ambaye ni Nuru ya ulimwengu utapita ukiwa salama kama mwandishi wa zaburi alivyoimba:-

Zaburi 23:4 “Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji.”

Kwa hiyo hali zote hizo zilikuwa zinaashiria kuwa mtu aliyepoteza uhusiano na Mungu na hana namna wala hajui njia ya kuurejesha ni sawa tu na mtu anayepita katika giza, na kuenenda katika uvuli wa mauti, Ujio wa Yesu Kristo kwakweli ulikuwa unaleta nuru kwa wale waliokuwa katika giza, wote waliokuwa wanapita katika mashaka na wote waliopoteza uhusiano wao na Mungu wangeweza kupata tumaini kwa upya kupitia ujio wa Yesu Kristo mwokozi na msaidizi wetu mkuu.               

Wale waliokwenda katika giza wameona nuru kuu!

Ujio wa Yesu Kristo ulikuwa ni wenye kuleta matumaini makubwa sana kwa wanadamu, kile alichokisema nabii Isaya miaka karibu na zaidi ya 700 kabla ya kuzaliwa kwa Kristo, ukweli ni kuwa alipozaliwa Yesu Kristo Nuru halisi ilikuwa imeingia sio tu Israel wala sio tu katika nchi za Zabuloni na Naftali na wala sio tu katika Galilaya lakini pia kwa ulimwengu mzima

Mathayo 4:13-16 “akatoka Nazareti, akaja akakaa Kapernaumu, mji ulioko pwani, mipakani mwa Zabuloni na Naftali; ili litimie neno lililonenwa na nabii Isaya, akisema, Nchi ya Zabuloni na nchi ya Naftali, Njia ya bahari, ng'ambo ya Yordani, Galilaya ya mataifa,Watu wale waliokaa katika giza Wameona mwanga mkuu, Nao waliokaa katika nchi na uvuli wa mauti Mwanga umewazukia.”

Luka 1:78-79 “Kwa njia ya rehema za Mungu wetu, Ambazo kwa hizo mwangaza utokao juu umetufikia, Kuwaangaza wakaao katika giza na uvuli wa mauti, Na kuiongoza miguu yetu kwenye njia ya amani.”

Ujio wa Yesu Kristo duniani unamuondoa kila amwaminiye yeye katika kuenenda gizani na kukabiliana na kutembea katika uvuli wa mauti bila kuogopa, Yesu Kristo mwenyewe alijitangaza kuwa yeye ndiye nuru ya ulimwengu na kuwa kila atakayemfuata yeye atakuwa na nuru na uzima wa milele, maisha yako hayatakuwa gizani tena.

Yohana 8:12 “Basi Yesu akawaambia tena akasema, Mimi ndimi nuru ya ulimwengu, yeye anifuataye hatakwenda gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima.”

Kila mwanadamu anayeumwa na kuugua, kila mwanadamu asiye na kazi, kila mwanadamu aliyekata tamaa, kila mwanadamu mwenye misiba, kila mwanadamu anayeumizwa na hatia ya dhambi, kila mwanadamu anayejisikia upweke kwa sababu ametengwa mbali na Mungu, kila mwanadamua ambaye mahusiano yake yako katika vita, kila mwanadamu ambaye hana furaha mahali pa kazi, kila mwanadamu ambaye haabudu katika roho na kweli, kila mwanadamu ambaye hana utulivu wa nafsi, mwili na roho, kila mwanadamu ambaye yuko katika machafuko, kila mwanadamu ambaye dini yake haimpi tumaini la kweli, wala mungu wake hajishughulishi na mahitaji yake, kila aliye na huzuni, misiba na changamoto za aina mbali mbali na kila anaeyeelemewa na mizigo ya namna mbalimbali huyo yumo gizani, Habari njema ni kuwa Yesu Kristo ndiye nuru ya ulimwengu, yeye anaweza kuyaleta na kuyajenga matumaini ya kweli ya mwanadamu na kuondoa hali zote za kuvunjika moyo na kukata tamaa, yeye ndiye Nuru halisi, sio ile nuru ambayo watu waliandama mwezi na kuushangilia unapotoka gizani, huitaji tena kuandama mwezi na kuushangilia sasa nuru halisi ni Yesu Kristo mwana wa Mungu aliye hai, hivyo katika majira haya ya kukumbuka siku ya kuzaliwa kwa masihi lazima tuwatangazie ya kuwa Nuru imekuja ulimwenguni na ni wakati sasa wa kuifuata nuru  

Wakolosai 2:16-17 “Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au sabato; mambo hayo ni kivuli cha mambo yajayo; bali mwili ni wa Kristo.”

Ujio wa Yesu Kristo unatupa tumaini na kurejesha uhai – Ukimuamini Yesu Kristo yeye ataitupilia mbali hofu, atakuweka huru mbali na hatia ya dhambi, atakurudishia matumaini yaliyopotea na safari yako ya kupita katika uvuli wa mauti na badala yake nawe nuru kuu itakuzukia hutakuwa gizani tena.

Yohana 12:46 “Mimi nimekuja ili niwe nuru ya ulimwengu, ili kila mtu aniaminiye mimi asikae gizani.”

Ujio wa Yesu Kristo na kazi ile aliyokuja kuikamilisha imetuwezesha kuwa na mamlaka dhidi ya giza, giza sasa halituwezi kwa sababu nuru ina nguvu kuliko giza nasi tunayo mamlaka ya kuyakemea matendo yote ya giza.

Yohana 1:4-5 “Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu. Nayo nuru yang'aa gizani, wala giza halikuiweza.”

Waefeso 5:11-14. “Wala msishirikiane na matendo yasiyozaa ya giza, bali myakemee; kwa kuwa yanayotendeka kwao kwa siri, ni aibu hata kuyanena. Lakini yote yaliyokemewa hudhihirishwa na nuru maana kila kilichodhihirika ni nuru. Hivyo husema, Amka, wewe usinziaye, Ufufuke katika wafu, Na Kristo atakuangaza.”

Ujio wa Yesu Kristo kama nuru unatuhakikishia wema wa Mungu katika maisha yetu kuwa hatutakuja kuwa watumwa wa hofu, nuru ni njema, nuru ni kweli, nuru ni usalama, nuru ni maisha, nuru ni uwepo wa Mungu, Bwana akiwa nuru yako maana yake ni wokovu wako na nguvu zako na hakuna jeshi linaloweza kujipanga kupigana nawe na hata wakipigana nawe hutaogopa.

Zaburi 27:1-3 “Bwana ni nuru yangu na wokovu wangu, Nimwogope nani? Bwana ni ngome ya uzima wangu, Nimhofu nani? Watenda mabaya waliponikaribia, Wanile nyama yangu, Watesi wangu na adui zangu, Walijikwaa wakaanguka. Jeshi lijapojipanga kupigana nami, Moyo wangu hautaogopa. Vita vijaponitokea, Hata hapo nitatumaini.”

Ujio wa Yesu Kristo kama Nuru unatukumbusha kuifanya kazi yake wakati nuru hiyo inawaka, kila mtu aliyeokolewa amepewa wajibu wa kuisambaza nuru ulimwenguni, kuamka na kuitangaza injili na kuwafanya mataifa yote kuwa wanafunzi agizo la kimaandiko linamtaka kila mmoja kufanya kazi na kuinuka na kuangaza nuru kila mahali kusiko na tumaini.

Yohana 9:4-5 “Imetupasa kuzifanya kazi zake yeye aliyenipeleka maadamu ni mchana, usiku waja asipoweza mtu kufanya kazi.Muda nilipo ulimwenguni, mimi ni nuru ya ulimwengu.”

Isaya 60:1-3 “Ondoka, uangaze; kwa kuwa nuru yako imekuja, Na utukufu wa Bwana umekuzukia. Maana, tazama, giza litaifunika dunia, Na giza kuu litazifunika kabila za watu; Bali Bwana atakuzukia wewe, Na utukufu wake utaonekana juu yako. Na mataifa wataijilia nuru yako, Na wafalme kuujia mwanga wa kuzuka kwako.”

Nuru inatukumbusha kuishi maisha matakatifu, kila mtu aliyeokolewa anapaswa kuwa mfano wa kuigwa na kuwaonyesha wengine njia, hatuwezi kuwa na madai kuwa tunamfuata Yesu kisha tukajificha, hatuwezi kuwa na madai ya kuwa tunamfuata Yesu kisha tukaishi kinyume naye Yesu alikuwa mtakatifu, kuishi maisha matakatifu ni agizo la kibiblia, hatuwezi kuacha kulihubiri na kulikazia, wala hatuwezi kuishi maisha ya dhambi kwa kisingizio cha neema, Nuru yake Yesu Kristo ni neema ya kutuwezesha kuishi maisha matakatifu chini ya msaada wake kwa hiyo matendo yetu mema yanapaswa kuiangazia dunia ili kila mmoja aweze kuona na kumtukuza baba wa Mbinguni, kwa sababu hiyo hatuna budi kutembea kama watoto wa nuru kwa kuishi maisha matakatifu.

Mathayo 5:14-16 “Ninyi ni nuru ya ulimwengu. Mji hauwezi kusitirika ukiwa juu ya mlima. Wala watu hawawashi taa na kuiweka chini ya pishi, bali juu ya kiango; nayo yawaangaza wote waliomo nyumbani.Vivyo hivyo nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni.”

Waefeso 5:8-9 “Kwa maana zamani ninyi mlikuwa giza, bali sasa mmekuwa nuru katika Bwana; enendeni kama watoto wa nuru, kwa kuwa tunda la nuru ni katika wema wote na haki na kweli;”

Nuru inatukumbusha kuhusu Nguvu za Mungu, za uumbaji na utendaji, wakati nguvu za uonevu zikiitwa nguvu za giza, Nguvu za Mungu ni nguvu za Nuru, wakati wowote kunapokuwa na giza ukiweka mwanga giza hutoweka haraka na kukimbia, kunapokosekana utaratibu na kuwepo kwa machafuko Nuru ikija utaratibu unakaa mahali pake na giza lote linakimbia, andiko linasema Nuru hung’aa gizani wala giza halikuiweza, Wakati huu tunapoadhimisha ujio wa Yesu Kristo Duniani na kushangilia kuzaliwa kwake, tujue ya kuwa ujio wake umekuwa na faida kubwa sana katika maisha yetu, Nguvu za giza hazituwezi tena, sisi tumehamishwa kabisa na kuokolea kabisa katika nguvu za giza na kutuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa mwana wa pendo lake, kwa hiyo nguvu zozote za uonevu wa kishateni hazituwezi, wala giza halikuiweza nuru, tuyakemee matendo yote yasiyozaa ya giza, tuiitie nuru wakati wote tunapokuwa na mashaka, au vita Bwana akiwa nuru yetu kamwe hatupaswi kuogopa, kwa kuwa sisi sasa ni miongoni mwa watu waliokaa katika giza na nuru imetuzukia, ni miongoni mwa watu waliokaa katika nchi ya uvuli wa mauti na nuru imetuangazia.

Wakolosai 1:13-14 “Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake; ambaye katika yeye tuna ukombozi, yaani, msamaha wa dhambi;”

Yohana 1:4-5 “Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu. Nayo nuru yang'aa gizani, wala giza halikuiweza.”

1Yohana 3:8 “atendaye dhambi ni wa Ibilisi; kwa kuwa Ibilisi hutenda dhambi tangu mwanzo. Kwa kusudi hili Mwana wa Mungu alidhihirishwa, ili azivunje kazi za Ibilisi.”

 

Na. Rev. Innocent Samuel Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima.

Jumatano, 25 Desemba 2024

Amekirimiwa jina lile lipitalo kila jina!


Wafilipi 2:9-11 “Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina; ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi; na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI BWANA, kwa utukufu wa Mungu Baba.”



Utangulizi:

Ni majira ambayo leo Wakristo wote nchini wanaungana na wakristo wenzao ulimwengu kusheherekea sikukuu ya kuzaliwa kwa masihi yaani “Chrismas”, Ujio wa Masihi “Yesu Kristo” una maana pana sana kwa mustakabali wa maisha ya mwanadamu, kuja kwa Yesu Kristo duniani ni zawadi kubwa sana kwani ujio wake unaambatana na faida kubwa sana. Isaya alitabiri kuwa ni zawadi ya mtoto wa kiume ambaye ndani yake kuna msaada mkubwa sana wa uungu ambao una faida kubwa sana kwa maisha ya mwadamu.

Isaya 9:6-7 “Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina Lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani. Maongeo ya enzi yake na amani Hayatakuwa na mwisho kamwe, Katika kiti cha enzi cha Daudi na ufalme wake; Kuuthibitisha na kuutegemeza Kwa hukumu na kwa haki, Tangu sasa na hata milele. Wivu wa Bwana wa majeshi ndio utakaotenda hayo.”

Moja ya zawadi kubwa inayoambatana na ujio wa Masihi ni pamoja na kukirimiwa jina lile lipitalo majina yote, jina ambalo lina faida kubwa sana katika maisha ya mwanadamu, na hili ndilo ambalo tutalijadili katika siku hii ya leo, ili kujikumbusha Baraka kubwa ambayo Mungu amewapa wanadamu kupitia Bwana Yesu lakini zaidi sana pia kupitia jina lake Matendo 2:21 “Na itakuwa kila atakayeliitia jina la Bwana ataokolewa.”

Warumi 10:11-13 “Kwa maana andiko lanena, Kila amwaminiye hatatahayarika. Kwa maana hakuna tofauti ya Myahudi na Myunani; maana yeye yule ni Bwana wa wote, mwenye utajiri kwa wote wamwitao; kwa kuwa, Kila atakayeliitia Jina la Bwana ataokoka.”

Jina la Yesu lina umuhimu kwaajili ya wokovu wetu, katika mazingira yote yanayohitaji msaada wa kiungu, jina hili lina nguvu, lina uwezo wa kubadilisha maisha ya watu kwa vizazi vyote, lina siri ya ajabu, lina uwezo wa kuvunja minyororo ya dhambi na kutufungulia malango ya mbinguni, jina hili linatufunulia mamlaka kubwa ya kiungu na kutuonyesha upendo mkubwa wa Mungu kwa wanadamu na kwa sababu hiyo katika msimu huu wa sikukuu ya kuzaliwa kwa masihi sisi tutachukua muda kuangalia umuhimu wa jina hili la Yesu, tutajifunza somo hili Amekirimiwa jina lile lipitalo kila jina kwa kuzingatia vipengele vitatu vifuatavyo:-


·         Umuhimu wa jina katika neno la Mungu.

·         Siri kubwa katika jina la Yesu.

·         Amekirimiwa jina lile lipitalo kila jina.                 

 

Umuhimu wa jina katika neno la Mungu.

Ni muhimu kufahamu kuwa kwa mujibu wa tamaduni za kibiblia, Majina hayakuwa yanatolewa kama jina tu, Majina yalikuwa ni tangazo linaloendana na tabia na mwenendo wa muhusika, majina yalikuwa ni picha halisi ya kinabii yenye kufunua kusudi la Mtu huyo kupewa jina, aidha majina pia yalikuwa yanatabiri kilele cha maisha ya mtu husika na wakati mwingine jina la mtu lilibadilishwa kwa kusudi la kubadilisha muelekeo wa maisha ya mtu huyo kutoka katika lile kusudi la kwanza la kupewa jina hilo, kwa mfano Mungu alipomuita Abrahamu, ambaye alikuwa anaitwa Abram alibadilisha jina lake hilo kuwa Abrahamu, Abram ikiwa na maana ya baba aliyeinuliwa, au mwana wa mfalme, na Abraham ikiwa na maana ya Baba wa Mataifa, au baba wa wafalme wengi, kwa hiyo Mungu alibadili jina la mwana wa mfalme, kuwa baba wa wafalme, Mungu alimpa jina linaloonyesha kuwa mwana mfalme huyu atakuwa ni baba wa wafalme wengi sana maarufu Duniani, Hali kadhalika Mungu alibadili jina la Sarai kuwa Sara.

Mwanzo 17:1-6 “Abramu alipokuwa mtu wa miaka tisini na kenda, BWANA akamtokea Abramu, akamwambia, Mimi ni Mungu Mwenyezi, uende mbele yangu, ukawe mkamilifu. Nami nitafanya agano langu kati ya mimi na wewe, nami nitakuzidisha sana sana. Abramu akaanguka kifudifudi. Mungu akamwambia, akasema, Mimi, agano langu nimefanya nawe, nawe utakuwa baba wa mataifa mengi, wala jina lako hutaitwa tena Abramu, lakini jina lako litakuwa Ibrahimu, kwani nimekuweka uwe baba wa mataifa mengi. Nitakufanya uwe na uzao mwingi sana, nami nitakufanya kuwa mataifa, na wafalme watatoka kwako.”

Mwanzo 17:15-16 “Mungu akamwambia Ibrahimu, Sarai mkeo, hutamwita jina lake Sarai, kwa kuwa jina lake litakuwa Sara.Nami nitambariki, na tena nitakupa mwana kwake, naam, nitambariki, naye atakuwa mama wa mataifa, na wafalme wa kabila za watu watatoka kwake.”

Mungu alibadilisha jina la Abramu kuwa Abrahamu kwa sababu Mungu alikusudia kubadilisha mustakabali wa maisha ya Abrahamu na kumfanya kubwa Baraka kubwa kwa dunia ili kwamba kuputia yeye mataifa yote yaweze kubarikiwa, na kama mtu atakuwa kinyume na Abrahamu angeweza kumlaani naye angelaaniwa, kwa hiyo unaweza kuona jinsi maisha ya Abrahamu yalivyogeuzwa na Mungu kuwa maisha ambayo yanaweza kumgusa kila mtu duniani

Mwanzo 12:1-3 “BWANA akamwambia Abramu, Toka wewe katika nchi yako, na jamaa zako, na nyumba ya baba yako, uende mpaka nchi nitakayokuonyesha; nami nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, na kukubariki, na kulikuza jina lako; nawe uwe baraka; nami nitawabariki wakubarikio, naye akulaaniye nitamlaani; na katika wewe jamaa zote za dunia watabarikiwa.”

Unaweza kuona, katika mpango huo huo wa kuleta Baraka kwa Dunia nzima Mungu alilazimika kubadili jina la Yakobo mjukuu wa Abrahamu kuwa Israel, ili kubadilisha mustakabali wa maisha ya Yakobo na kumbadilisha kuwa kitu kingine

Mwanzo 32:26-28 “Akasema, Niache, niende, maana kunapambazuka. Akasema, Sikuachi, usiponibariki. Akamwuliza, Jina lako n'nani? Akasema, Yakobo. Akamwambia, Jina lako hutaitwa tena Yakobo, ila Israeli, maana umeshindana na Mungu, na watu, nawe umeshinda.”

Kwa msingi huo utakubaliana nami kuwa ni ukweli usiopingika kimaandiko kuwa majina yalihusika kwa sehemu kubwa kuhusisha uweza wa Mtu tabia na mustakabali wa maisha yajayo, kwa hiyo kila mkristo anapaswa kukumbuka jambo hili kwamba tuwape watoto wetu majina mazuri kwaajili ya mustakabali mwema wa maisha yao ya baadaye na kamwe tusiruhusu wakawa na majina yenye kuwakilisha uchungu, au machungu ya maisha, hasa kama watoto hao hawahusiki na hilo walilolipitia wazazi, kwa mfano wakati Benjamin anazaliwa mama yake akiwa katika hali ya kufa alimpa jina Benon akiwakilisha mwana wa uchungu wake, lakini Yakobo alilibadilisha jina hilo mara moja jina likimaanisha mwana  wa mkono wake wa kuume ona:-

Mwanzo 35;16-18 “Wakasafiri kutoka Betheli, hata ukabaki mwendo wa kitambo tu kufika Efrathi, Raheli akashikwa na utungu wa kuzaa, na utungu wake ulikuwa mzito. Ikawa alipokuwa anashikwa sana na utungu, mzalisha akamwambia, Usiogope, maana sasa utamzaa mwanamume mwingine. Ikawa hapo katika kutoa roho yake, maana alikufa, akamwita jina lake Benoni, lakini babaye alimwita Benyamini.”

Katika hali kama hiyo majina ya Mungu katika maandiko yanafunua asili, tabia na uhusiano ulioko kati ya Mungu na wanadamu, Mfano mtu alipofadhiliwa na Mungu alimwita Mungu wa fadhili zangu Yehovah Yire, au mtu alipohakikishiwa Amani na Mungu alimuita Yehovah Shalom akikubali Amani ya Mungu, majina hayo sio tu yanamfunua Mungu bali yanatukaribisha kwake yakituonyesha kuwa Mungu anaweza kujitokeza kwetu pia sawasawa na mahitaji yetu, sasa jina la Yesu linafunua ufunuo mkamilifu wa Mungu kwa mahitaji yetu yote wanadamu kutokea upande wowote wa kiroho, nafsi, na mwili na kutufundisha au kutufunulia ukamilifu wote wa Mungu na kusudi lake kwa wanadamu.


Siri kubwa katika jina la Yesu.

Sasa tunapokuja kuangalia kuhusu jina la Yesu, utaweza kuona kuwa jina hili lilitangulia kutolewa kama zawadi kwa wanadamu wakati wa maandalizi ya kuzaliwa kwake yeye mwenyewe, jina hili lilikuja kama habari njema kwa Yusufu kuwajulisha watu wote Duniani kuwa mtoto huyu mwanaume ambaye tumepewa kama zawadi ukiacha shughuli zote za ukombozi na mafundisho yake yote jina lake tu ni msaada tosha kwa wanadamu na jina hili lilikuja vilevile wakati wa kuzaliwa kwake, kwa hiyo mojawapo ya zawadi kubwa kabisa katika siku za kuzaliwa kwa Masihi ni pamoja na jina lake ambalo ni jina lipitalo majina yote.

Mathayo 1:20-25 “Basi alipokuwa akifikiri hayo, tazama, malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto, akisema, Yusufu, mwana wa Daudi, usihofu kumchukua Mariamu mkeo, maana mimba yake ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu. Naye atazaa mwana, nawe utamwita jina lake Yesu, maana, yeye ndiye atakayewaokoa watu wake na dhambi zao. Hayo yote yamekuwa, ili litimie neno lililonenwa na Bwana kwa ujumbe wa nabii akisema, Tazama, bikira atachukua mimba, Naye atazaa mwana; Nao watamwita jina lake Imanueli; Yaani, Mungu pamoja nasi. Naye Yusufu alipoamka katika usingizi, alifanya kama malaika wa Bwana alivyomwagiza; akamchukua mkewe; asimjue kamwe hata alipomzaa mwanawe; akamwita jina lake YESU.”

Jina Yesu kwaasili limetokana na jina “JESUS” la kiingereza ambalo lina mzizi mkuu kutoka katika lugha ya kilatini, na kwa kiyunani, “IESOUS” ambalo asili yake ni jina la kiibrania “yehōshuaYEHOSHUA au JOSHUA ambalo maana yake ni “MUNGU MWOKOZI” jina la Yesu lina maana pana katika kiibrania zinazojumuisha

Yeshua – yaani Mwokozi

Yoshua – yaani muunganiko wa maneno makuu mawili

·         Yah – ambalo ni kifupi cha neno la kiibrania ambalo lilikuwa katika mfumo wa herufi zisizo na silabii yaani Tetragrammaton zijulikanazo kama YHWH au YAHWEH

·         Yasha – ambalo maana yake wokovu au ukombozi Kwa hiyo jina la Yesu maana yake Yohova ni mwokozi,  kwa hiyo unapolitaja jina hili unaita mamlaka yote ya kiungu kwaajili ya kuleta msaada wa kiungu kokote uliko iwe ni mbinguni, duniani au kuzimu jina hili lina nguvu na mamlaka kubwa ya kusababisha ukombozi katika eneo husika, Mungu mwenyewe anashuka katika historia ya mwanadamu na kuukomboa uumbaji wake

Kwa hiyo jina la Yesu, linatimiza uhitaji mzima wa ukombozi wa mwanadamu ulioahidiwa katika agano la kale, kama Yoshua aliwaingiza wana wa Israel katika inchi ya mkanaani basi Yesu anawaingiza wanadamu wote duniani wamwaminio katika pumziko la uzima wa milele, kwa hiyo jina hili sio tu linawaokoa wanadamu na dhambi zao, bali pia na madhara ya dhambi, magonjwa na utumwa wa kila namna ambao wanadamu wanatumikishwa na zaidi ya yote kumkomboa mwanadamu na mauti ya milele, jina hili ni zaidi ya kazi za ukombozi, ni jina linaloachilia mamlaka ya kimbingu kushuka na kushughulika na mahitaji ya wanadamu duniani.

Luka 2:9-11 “Na katika nchi ile ile walikuwako wachungaji wakikaa makondeni na kulinda kundi lao kwa zamu usiku.Malaika wa Bwana akawatokea ghafula, utukufu wa Bwana ukawang'aria pande zote, wakaingiwa na hofu kuu. Malaika akawaambia, Msiogope; kwa kuwa mimi ninawaletea habari njema ya furaha kuu itakayokuwa kwa watu wote; maana leo katika mji wa Daudi amezaliwa, kwa ajili yenu, Mwokozi, ndiye Kristo Bwana.”

Jina la Yesu haliondoi majina majina ya Mungu yaliyotumiwa wakati wa agano la kale lakini linayatimiza, wakati wa agano la kale Mungu alijifunua kidogo kidogo kwa vipande vipande kupitia jina lake mfano Yehova Rapha ilimaanisha, wokovu katika uponyaji, na Yehova Nisi ilimaanisha wokovu katika vita hivi vilikuwa ni vipande vipande vya ukombozi ambapo Mungu alijifunua kwa sehemu tu kulingana na uhitaji wa mtu kwa wakati huo, kwa hiyo ufunuo kuhusu jina la Mungu ulikuwa ni kwa sehemu, sivyo ilivyo katika jina la Yesu, hili linafunua wokovu kamili, ni kifurushi kamili chenye kujitosheleza katika nyanja zote, kama muumba, asili yake, wajibu wake kwa viumbe wake, na kadhalika kwa hiyo Yesu ni ufunuo kamili  wa Mungu.

Waebrania 1:1-4 “Mungu, ambaye alisema zamani na baba zetu katika manabii kwa sehemu nyingi na kwa njia nyingi, mwisho wa siku hizi amesema na sisi katika Mwana, aliyemweka kuwa mrithi wa yote, tena kwa yeye aliufanya ulimwengu. Yeye kwa kuwa ni mng'ao wa utukufu wake na chapa ya nafsi yake, akivichukua vyote kwa amri ya uweza wake, akiisha kufanya utakaso wa dhambi, aliketi mkono wa kuume wa Ukuu huko juu; amefanyika bora kupita malaika, kwa kadiri jina alilolirithi lilivyo tukufu kuliko lao.”

Isaya 45:22-23 “Niangalieni mimi, mkaokolewe, enyi ncha zote za dunia; maana mimi ni Mungu; hapana mwingine.Kwa nafsi yangu nimeapa, neno hili limetoka kinywani mwangu katika haki, wala halitarudi, ya kwamba mbele zangu kila goti litapigwa, kila ulimi utaapa.”

Wafilipi 2:9-11 “Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina; ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi; na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI BWANA, kwa utukufu wa Mungu Baba.”

Kwa msingi huo kila unabii katika Mungu uliotabiriwa katika agano la kale umekuja kutimizwa katika agano jipya kupitia jina la Yesu na kwa sababu hiyo tena hatuna jina lingine litupasalo sisi kuokolewa kwalo isipokuwa jina la Yesu tu,

Matendo 4:10-12 “jueni ninyi nyote na watu wote wa Israeli ya kuwa kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, ambaye ninyi mlimsulibisha, na Mungu akamfufua katika wafu, kwa jina hilo mtu huyu anasimama ali mzima mbele yenu. Yeye ndiye jiwe lile lililodharauliwa na ninyi waashi, nalo limewekwa kuwa jiwe kuu la pembeni.Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo.”


Amekirimiwa jina lile lipitalo kila jina

Wafilipi 2:9-11 “Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, AKAMKIRIMIA JINA LILE LIPITALO KILA JINA; ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi; na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI BWANA, kwa utukufu wa Mungu Baba.”

Yesu Kristo sasa ni jina lipitalo majina yote kwa vitu vyote vya mbinguni na vya duniani na kuzimu neno LIPITALO katika kiyunani linatumika neno HUPER kimatamshi Hoo-per, huupa ambalo tafasiri yake kwa kiingereza ni Beyond across, Superior to more than, above, very chiefest, Exceeding, highly more than, very highly, jina lililo juu zaidi ya kawaida, Bora kupita yote, liko juu, la juu zaidi, limepitiliza kuliko kawaida, liko juu mno, Kwa hiyo nguvu iliyokuwa ikifunuliwa kupitia jina Yehova au Yahweh sasa inakaa katika Yesu kwa ukamilifu wake wote, bila kupuuzia majina ya agano la kale kuhusu Mungu, jina la Yesu sasa linabeba ufunuo mkamilifu wa mamlaka ya kiungu na wokovu wa mwanadamu kwahiyo ni kusema ukitoa pepo kwa jina la YEHOVA halitatoka lakini ukitoa kwa jina la Yesu litaondoka, jina hili hata shetani analijua, matumizi sahihi ya jina hili huwakilisha Serikali, ufalme, dola, mamlaka na utawala  na hivyo Pepo wakilisikia lazima wakimbie. Ni Mungu mwenyewe ambaye amempa Yesu jina hili na ametaka alitambulishe kwa wanadamu kwaajili ya kuwasaidia

Yohana 17:11-12 “Wala mimi simo tena ulimwenguni, lakini hawa wamo ulimwenguni, nami naja kwako. Baba mtakatifu, kwa jina lako ulilonipa uwalinde hawa, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo. Nilipokuwapo pamoja nao, mimi naliwalinda kwa jina lako ulilonipa, nikawatunza; wala hapana mmojawapo wao aliyepotea, ila yule mwana wa upotevu, ili andiko litimie.”              

Jina la Yesu likitumika katika matamshi yoyote yawe ya Kiswahili, kiebrania, au kiyunani na kingereza nguvu yake inabakia vilevile halichuji endapo tu utamaanisha Yesu huyu wa Nazareth tunayehubiri habari zake jina hili lina nguvu, lina mamlaka, uwezo wa kuokoa na kufanya mambo makubwa unapoliitia maana yake unaiita serikali ya mbinguni kutoa msaada katika eneo husika

Jina hili linaokoa - Matendo 2:21 “Na itakuwa kila atakayeliitia jina la Bwana ataokolewa.”

Jina hili kanisa limeamriwa kuliamini – 1Yohana 3:23 “Na hii ndiyo amri yake, kwamba tuliamini jina la Mwana wake Yesu Kristo, na kupendana sisi kwa sisi, kama alivyotupa amri.”

Jina hili lina mamlaka ya kuamuru lolote - Marko 16:17-18 “Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya; watashika nyoka; hata wakinywa kitu cha kufisha, hakitawadhuru kabisa; wataweka mikono yao juu ya wagonjwa, nao watapata afya.”

Jina hili huitiwa na makanisa yote ya kweli – 1Wakorintho 1:2 “Na hii ndiyo amri yake, kwamba tuliamini jina la Mwana wake Yesu Kristo, na kupendana sisi kwa sisi, kama alivyotupa amri.”

Jina hili lilitumiwa na mitume kuponya na kufanya miujiza mbalimbali.

Matendo 3:6, “Lakini Petro akasema, Mimi sina fedha, wala dhahabu, lakini nilicho nacho ndicho nikupacho. Kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, simama uende.”

Matendo 4:10 “jueni ninyi nyote na watu wote wa Israeli ya kuwa kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, ambaye ninyi mlimsulibisha, na Mungu akamfufua katika wafu, kwa jina hilo mtu huyu anasimama ali mzima mbele yenu.”

Jina hili mitume na kanisa la kwanza walilitumia katika kuhubiri

Matendo 8:12 “Lakini walipomwamini Filipo, akizihubiri habari njema za ufalme wa Mungu, na jina lake Yesu Kristo, wakabatizwa, wanaume na wanawake.”

Matendo 9:27-29 “Lakini Barnaba akamtwaa, akampeleka kwa mitume, akawaeleza jinsi alivyomwona Bwana njiani, na ya kwamba alisema naye, na jinsi alivyohubiri kwa ushujaa katika Dameski kwa jina la Yesu. Naye akawa pamoja nao katika Yerusalemu akiingia na kutoka. Akahubiri kwa jina la Bwana kwa ushujaa, akinena na kuhojiana na Wayahudi wa Kiyunani. Nao wakajaribu kumwua.”                    

Jina hili ni ulinzi na kimbilio – Mithali 18:10 “Jina la Bwana ni ngome imara; Mwenye haki huikimbilia, akawa salama.”

Jina hili lilitumiwa na mitume kufukuza pepo wabaya.

Matendo 16:18 “Akafanya hayo siku nyingi. Lakini Paulo akasikitika, akageuka akamwambia yule pepo, Nakuamuru kwa jina la Yesu Kristo, mtoke huyu. Akamtoka saa ile ile.” 

Jina hili lilaleta Amani – Yohana 16:23-24 “Tena hsiku ile hamtaniuliza neno lo lote. Amin, amin, nawaambia, Mkimwomba Baba neno lo lote atawapa kwa jina langu.Hata sasa hamkuomba neno kwa jina langu; ombeni, nanyi mtapata; furaha yenu iwe timilifu.”

Jina hili ni kibali cha kujibiwa maombi – Yohana 14:13-15 “Nanyi mkiomba lo lote kwa jina langu, hilo nitalifanya, ili Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Mkiniomba neno lo lote kwa jina langu, nitalifanya.”

Jina hili Mitume walikuwa tayari hata kulifia

Matendo 15:25-26 “sisi tumeona vema, hali tumepatana kwa moyo mmoja, kuwachagua watu na kuwapeleka kwenu pamoja na wapendwa wetu Barnaba na Paulo, watu waliohatirisha maisha yao kwa ajili ya jina la Bwana wetu Yesu Kristo.”               

Matendo 21:12-13  “Basi tuliposikia haya, sisi na watu wa mahali pale, tukamsihi asipande kwenda Yerusalemu.Ndipo Paulo alipojibu, Mnafanya nini, kulia na kunivunja moyo? Kwa maana mimi, licha ya kufungwa, ni tayari hata kuuawa katika Yerusalemu kwa ajili ya jina lake Bwana Yesu.”  

Jina hili linavuta uwepo wa Mungu – Mathayo 18:19-20 “Tena nawaambia, ya kwamba wawili wenu watakapopatana duniani katika jambo lo lote watakaloliomba, watafanyiwa na Baba yangu aliye mbinguni.Kwa kuwa walipo wawili watatu wamekusanyika kwa jina langu, nami nipo papo hapo katikati yao.”

Kwa hiyo watu wa Mungu tuna wajibu wa kulitumia jina la Yesu katika jambo lolote, najua yako mafundisho mengi duniani hata yale yanayofundisha watu kutumia damu ya Yesu na kuinyunyiza kwa Imani, maandiko yameelekeza katika changamoto yoyote ile tutumie jina la Yesu, Shetani asikudanganye kutumia kingine tumia jina la Yesu moja kwa moja, maandiko yametuagiza kulitumia katika maombi, kulitumia kwaajili ya uponyaji, kulitumia katika vita vya kiroho, na kulitumia katika kuabudu, tumeagizwa ya kuwa lolote tulifanyalo kwa neno au kwa tendo tulifanye kwa jina la Yesu, tunapoliitia jina hili utendaji wa serikali ya mbinguni unahamia pale jina hili linapotajwa na kutimiliza matakwa yetu kwa utukufu wa Mungu, wajibu wetu ni kulitumia jina la Yesu kwa Imani, kwa heshima, kwa kulitumainia na kulitegemea, kwa kulitangaza kwa ujasiri, na kuishi sawasawa na heshima ya jina hilo, kwani jina hili ndio ufunuo mkamilifu wa upendo na wokovu wa mwanadamu kutoka kwa Mungu, jina hili lilifichwa nyakati za agano la kale na kufunuliwa kwetu wa kizazi hiki katika wakati huu wa neema hivyo ni zawadi ya kipekee ambayo hatuna budi kuitumia kwa mustakabali wa maisha yetu, unapoadhimisha kuzaliwa kwa Yesu Kristo basi kumbuka tumepewa jina kuu kuliko yote! Na ingawa amekirimiwa jina hili, kimsingi tumekarimiwa sisi kwa matumizi yake, kwa changamoto zozote zile unazokutana nazo katika maisha liitie jina la Yesu na utayafurahia maisha, omba kwa jina la Yesu, kemea kwa jina la Yesu, Amini  na ishi kwa  kulitegemea jina la Yesu.

Wakolosai 3:16-17. “Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana kwa zaburi, na nyimbo, na tenzi za rohoni; huku mkimwimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu. Na kila mfanyalo, kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Mungu Baba kwa yeye.”

Maadui wa Yesu Kristo akiwepo shetani wakati wote hawatataka kulisikia jina hili likitumika na wakati wote watalikataa kama wanavyomkataa, Yesu Kristo mwenyewe, Shetani anatamani sana kama ikiwezekana jina hili lisiwepo au litumike lingine kwa sababu anaijua nguvu iliyomo katika jina hili. Nakusihi sana wakati huu tunapoadhimisha kuzaliwa kwa Yesu Kristo kumbuka kuwa Mungu ametukirimia sio zawadi tu ya maisha yake ya ukombozi kwa wanadamu lakini ametukirimia pia jina hili zuri ambalo tunaweza kulitumia kwa mustakabali wa maisha yetu. Lakini hata manabii wa uongo watalitumia jina hili kwa kusudi la kuwadanganya wateule hivyo hatuna budi kuwa makini, si kila anayelitumia atakuwa ni mtu mzuri au mtu sahihi.

Mathayo 7:21 “Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.”

Matendo 4:18 “Wakawaita, wakawaamuru wasiseme kabisa wala kufundisha kwa jina la Yesu.”

Matendo 5:40-42 “Wakakubali maneno yake; nao walipowaita mitume, wakawapiga, wakawaamuru wasinene kwa jina lake Yesu; kisha wakawaacha waende zao. Nao wakatoka katika ile baraza, wakifurahi kwa sababu wamehesabiwa kuwa wamestahili kuaibishwa kwa ajili ya Jina hilo.Na kila siku, ndani ya hekalu na nyumbani mwao, hawakuacha kufundisha na kuhubiri habari njema za Yesu kwamba ni Kristo.”  

 

Na. Rev. Mkombozi Samuel Kamote

Mkuu wa Wajenzi mwenye Hekima