Jumanne, 8 Novemba 2022

Kufa afavyo Mpumbavu!


2Samuel 3:33-34Ndipo mfalme akamwomboleza Abneri, akasema, Ilimpasaje Abneri kufa afavyo mpumbavu? Mikono yako haikufungwa, Wala miguu yako haikutiwa pingu; Aangukavyo mtu mbele ya wana wa uovu, ndivyo ulivyoanguka. Na watu wote wakaongeza kumlilia.” 



Utangulizi:

Abner alikuwa ni binamu na mkuu wa majeshi ya ulinzi wa Jeshi la Mfalme Sauli, Jina lake limejitokeza katika maandiko vilevile kama Abner mwana wa Ner jina lake maana yake baba yangu ni Ner  na neno Ner maana yake ni Mwanga au Nuru!, Mkuu huyu wa majeshi alitumika na Sauli na Jonathan na hata baada ya kifo chake alikuwa mwaminifu kwa Mtoto wa Sauli aliyeitwa Ishboshethi hivyo tunapata picha ya kuwa wakati wote wa vita vya Sauli na Daudi Abner ndiye aliyekuwa akiongoza mapambano hayo lakini kwa neema ya Mungu siku hadi siku Nyumba ya Sauli ilizidi kudhoofika dhidi ya Nyumba ya Daudi kama yanenavyo maandiko.

2Wafalme 3:1 “Basi kulikuwa na vita siku nyingi kati ya nyumba ya Sauli na nyumba ya Daudi; Daudi akaendelea akasitawi, lakini nyumba ya Sauli ikaendelea kudhoofika.”

Hata hivyo kutokana na kutambua mapenzi ya Mungu, Abner alitambua wazi kuwa Mungu alikuwa amekusudia Daudi awe mfalme tangu miaka mingi alipopakwa mafuta na Samuel Nabii, lakini kibishibishi upande wa Sauli walikuwa wanachelewesha au kushindana na makusudi ya Mungu, hatimaye Abner aliamua kuwa atasaidia kumkabidhi Daudi ufalme baada ya kugombea mwanamke kati yake na Ishboshethi mwana wa Sauli.

2Wafalme 3:6-9 “Ikawa, wakati vilipokuwapo vita kati ya nyumba ya Sauli na nyumba ya Daudi, Abneri akajipatia nguvu nyumbani kwa Sauli. Basi Sauli alikuwa na suria, jina lake akiitwa Rispa, binti Aya; Ishboshethi akamwuliza Abneri, Kwa nini umeingia kwa suria ya babangu? Basi Abneri akakasirika kwa maneno ya Ishboshethi, akasema, Je! Mimi ni kichwa cha mbwa, aliye wa Yuda? Hata leo hivi nawafanyia fadhili nyumba ya Sauli babako, na ndugu zake, na rafiki zake, nisikutie wewe mkononi mwa Daudi; nawe hata hivyo wanitia hatiani leo kwa mwanamke huyu. Mungu amfanyie Abneri vivyo, na kuzidi, nisipomtendea Daudi kama vile Bwana alivyomwapia;”

Kwa hiyo unaweza kupata picha kuwa kwa kiwango fulani kikubwa Abner alikuwa ni kikwazo kikubwa kwa mapenzi ya Mungu kwa Daudi kutimia akitetea upande wa Sauli na watoto wake na pia kumbe alijua mapenzi ya Mungu kuwa Mungu alimuapia Daudi Ufalme lakini kwa makusudi alikuwa akipingana na mapenzi ya Mungu na kuchelewesha kusudi la Mungu juu ya Daudi ashukuriwe Mungu kuwa makusudi yake hayawezi kuzuilika, Mungu aliutumia ugomvi wao na Ishbotheth kutimiza Mpango wake na Abner sasa alikuwa katika njia ya Mungu akijua wazi kuwa anatimiza mapenzi ya Mungu.

Abner na mapenzi ya Mungu.

Abner alifahamu kuwa kama amekosana na Ishbotheth mwana wa Sauli na kujipa nguvu yeye mwenyewe kwa vyovyote vile atakayepambana na Daudi angekuwa yeye, uso kwa uso, kwa ujumla Jemedari huyu alikuwa na tatizo la kiburi moyoni mwake maandiko yanaposema alijipatia nguvu katika nyumba ya Sauli maana yake alijiinua yeye mwenyewe

2Wafalme 3:6-7 “Ikawa, wakati vilipokuwapo vita kati ya nyumba ya Sauli na nyumba ya Daudi, Abneri akajipatia nguvu nyumbani kwa Sauli. Basi Sauli alikuwa na suria, jina lake akiitwa Rispa, binti Aya; Ishboshethi akamwuliza Abneri, Kwa nini umeingia kwa suria ya babangu?

Unaona akajipatia nguvu nyumbani mwa Sauli hii maana yake kibiblia alianza kujiinua alianza kuwa na kiburi, kuchukua mke au suria katika mila za kifalme kulikuwa hakuna tofauti na kujifanya mfalme au kutaka ufalme ona, 1Wafalme 2:13-23 “Ndipo Adonia mwana wa Hagithi akaja kwa Bath-sheba mamaye Sulemani. Naye akasema, Je! Umekuja kwa amani? Naye akajibu, Kwa amani. Tena akasema, Nina shauri ninalotaka kukuambia. Naye akamwambia, Sema. Basi akasema, Wajua ya kwamba ufalme ulikuwa wangu, na Israeli wote wakaniwekea nyuso zao ili nimiliki mimi; walakini sasa ufalme umegeuka kuwa wake ndugu yangu; kwa maana ulikuwa wake kutoka kwa Bwana. Basi sasa nina haja moja ninayokuomba, usinikataze hiyo. Naye akamwambia, Sema. Akasema, Nena, nakusihi, na Sulemani, mfalme, (kwa kuwa hawezi kukukataza neno), kwamba anioze Abishagi, Mshunami. Naye Bath-sheba akasema, Vema; nitasema na mfalme kwa ajili yako. Basi Bath-sheba akaingia kwa mfalme Sulemani, aseme naye kwa ajili ya Adonia. Naye mfalme akainuka kwenda kumlaki, akamwinamia, akaketi katika kiti chake cha enzi; kisha akaagiza awekewe kiti cha enzi mamaye mfalme; naye akaketi mkono wake wa kuume. Ndipo akasema, Haja moja ndogo nakuomba; usinikataze. Mfalme akamwambia, Omba, mama; kwa kuwa siwezi kukukataza neno. Naye akasema, Nataka Adonia, ndugu yako, aozwe Abishagi, Mshunami. Akajibu mfalme Sulemani akamwambia mamaye, Na mbona wamtakia Adonia Abishagi, Mshunami? Umtakie na ufalme pia; kwa kuwa yeye ni ndugu yangu mkubwa; naam, umtakie yeye, na Abiathari kuhani, na Yoabu mwana wa Seruya. Ndipo mfalme Sulemani akaapa kwa Bwana, akasema, Mungu anifanyie hivyo, na kuzidi, isipokuwa Adonia amenena neno hili juu ya uhai wake mwenyewe.” hivyo ili Daudi atawale ilikuwa lazima Abner ashughulikiwe, naye akijua yatakayompata baada ya kuasi nyumba ya Sauli sasa anakuja na mpango wa kukabidhi mamlaka ya kifalme kwa Daudi, lilikuwa wazo jema na mapenzi ya Mungu, lakini ni yeye ndiye aliyekuwa anachelewesha kusudi la Mungu, sasa anataka kurudisha mamlaka kwa Daudi.

2Wafalme 3:9-10 “Mungu amfanyie Abneri vivyo, na kuzidi, nisipomtendea Daudi kama vile Bwana alivyomwapia; kuupitisha ufalme toka nyumba ya Sauli, na kukisimamisha kiti cha Daudi juu ya Israeli, na juu ya Yuda, toka Dani mpaka Beer-sheba.”

Abner alikuwa mtu mwenye kujiamini kupita kawaida yeye alijifanya kuwa ni Mungu, pamoja na kuwa aliapa kwa Mungu lakini anapotumia neno KUUPITISHA UFALME TOKA NYUMBA YA SAULI NA KUKISIMAMISHA KITI CHA DAUDI JUU YA ISRAEL NA JUU YA YUDA hii ilikuwa ni kazi ambayo haifanyiki kibinadamu neno kupitisha Katika kiingereza linasomeka kama “To translate” ambalo katika kiebrania maana yake ni Abar likisomeka kama AW-BAR ambalo maana yake ni ni sawa na kutenga au kusababisha au kuweka wakfu au kuhamisha kimsingi hayo yanaweza kufanywa na Mungu tu ona Wakolosai 1:13 “Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake;”  unaweza kuona Lugha hiyo pia katika Waebrania 11:5 “Kwa imani Henoko alihamishwa, asije akaona mauti, wala hakuonekana, kwa sababu Mungu alimhamisha; maana kabla ya kuhamishwa alikuwa ameshuhudiwa kwamba amempendeza Mungu.” Kwa hiyo kumamisha au kupitisha ni kumtoa mtu katika hali moja na kumpeleka katika hali nyingine hii ni kazi ya Mungu na sio ya Mwanadamu. Ni wazi kuwa kamanda huyu alikuwa na kiburi.

Abner vilevile alikuwa ni mtu hatia ya damu ya shujaa anayeitwa Asahel, Huyu alikuwa moja ya watu mashujaa aliyekuwa na mbio za kufukuzia maadui kama mbio za kulungu, katika mashujaa watatu waliotoka kwa Seruya waliojulikana kama wana wa Seruya Asahel alikuwa ni hodari lakini zaidi sana aliyekuwa na uwezo wa kukimbiza adui, Asahel alikuwa akimkimbiza Abner na kwaajili ya kujihami Abneri alimshihi sana aache kumfuatilia lakini Asahel alikaza na kwa sababu hiyo yeye alimuua ona

2Samuel 18-28 Na wana watatu wa Seruya walikuwako huko, Yoabu, na Abishai, na Asaheli; na Asaheli alikuwa mwepesi wa miguu kama kulungu. Naye Asaheli akamfuatia Abneri; na katika kwenda kwake hakugeuka kwenda mkono wa kuume wala mkono wa kushoto katika kumfuatia Abneri. Basi Abneri akatazama nyuma yake, akasema, Ni wewe, Asaheli? Akajibu, Ni mimi. Basi Abneri akamwambia, Geuka mkono wa kuume au mkono wa kushoto, ukamshike mmoja wa vijana, ukazitwae silaha zake. Lakini Asaheli hakukubali kugeuka na kuacha kumfuata. Abneri akamwambia Asaheli mara ya pili, Geuka, acha kunifuatia mimi; kwa nini nikupige hata chini? Hapo ningewezaje kuinua uso wangu mbele ya Yoabu, ndugu yako? Lakini akakataa kugeuka; kwa hiyo Abneri akampiga tumboni kwa ncha ya nyuma ya mkuki wake, ule mkuki ukamtoka kwa nyuma; naye akaanguka hapo, akafa papo hapo; ikawa, watu wote waliofika hapo, alipoanguka Asaheli na kufa, wakasimama. Ila Yoabu na Abishai wakamfuatia Abneri; na jua likachwa hapo walipoufikilia mlima wa Ama, uelekeao Gia, katika njia ya nyika ya Gibeoni. Nao wana wa Benyamini wakakusanyika pamoja nyuma ya Abneri, wakawa kikosi kimoja, wakasimama juu ya mlima. Ndipo huyo Abneri akamwita Yoabu, akasema, Je! Upanga uwale watu sikuzote? Je! Hujui ya kwamba utakuwa uchungu mwisho wake? Basi itakuwa hata lini usijewaamuru watu warudi na kuacha kuwafuatia ndugu zao? Naye Yoabu akasema, Aishivyo Mungu, usingalinena, basi asubuhi wangalikwenda zao, wasiwafuatie kila mtu ndugu yake. Basi Yoabu akapiga tarumbeta, na watu wote wakasimama, wasiwafuatie Israeli tena, wala hawakupigana tena.” Mtu aliyeua mtu mwingine alipaswa kusalimisha maisha yake katika mojawapo ya miji sita ya makimbilio ili mwenye kujilipiza kisasi kwaajili ya nduguye aije akamuua, Hata hivyo Abneri hakuweza kujali maelekezo hayo ya torati kwa vile alikuwa akijiamini kutokana na umahiri wake katika vita

Agano la Abner na Daudi.

Pamoja na madhaifu makubwa aliyokuwa nayo Abner, huyu pia alikuwa ni jemadari wa vita, alikuwa ni mzoefu wa vita shujaa na kamanda mwenye nguvu sana lakini pia alikuwa mpenda amani na mwangalifu mno, katika uwezo wa kujihami,  ulifika wakati akaona pia kuwa sasa Israel wanahitaji amani.

2Samuel 3:12-16 “Basi Abneri akatuma wajumbe kwa Daudi mahali alipokuwapo, akisema, Nchi hii ni ya nani? Fanya agano nami, na tazama, mkono wangu utakuwa pamoja nawe, ili kuwaleta Israeli wote kwako. Daudi akasema, Vema, nitafanya agano nawe, lakini nina sharti moja nitakalo kwako, nalo ni hili; Hutaniona uso wangu, isipokuwa uniletee Mikali, binti Sauli, hapo ujapo kuniona uso wangu. Basi Daudi akatuma wajumbe kwa Ishboshethi, mwana wa Sauli, kusema, Nipe mke wangu Mikali, niliyemposa kwa govi mia za Wafilisti. Basi Ishboshethi akatuma watu, akamnyang'anya Paltieli, mwana wa Laishi, mumewe, mwanamke huyo. Huyo mumewe akafuatana naye, akiendelea na kulia, akamfuata mpaka Bahurimu. Ndipo Abneri akamwambia, Haya, rudi. Naye akarudi.”

Kwa kuwa ilikuwa ni desturi ya Israel mtu anapofanya agano lazima wawekeana masharti Daudi aliitumia nafasi hiyo kumdai Abner ili aweze kumona uso wake amletee mke wa ujana wake aliyemuoa kwa gharama ya givi za wafilisti 100 lakini yeye aliua 200 ambaye alikuwa ni mikali Binti wa Sauli jambo ambalo Abner alilitii,  hii ilikuwa picha halisi ya kuwa Abner kweli alikuwa anataka amani Jambo hili lilimpendeza Daudi, hata hivyo Daudi hakuwa anahitaji sana Nguvu ya Abner kwani vijana wa Daudi walikuwa wameshaonyesha uwezo mkubwa sana kivita kumzidi yeye ona

2Samuel2:14-17 “Abneri akamwambia Yoabu, Tafadhali vijana hawa na waondoke na kucheza mbele yetu. Yoabu akasema, Haya! Na waondoke. Basi wakaondoka, wakaenda upande wa pili kwa hesabu yao watu kumi na wawili wa Benyamini, na wa Ishboshethi, mwana wa Sauli na watu kumi na wawili wa watumishi wa Daudi. Wakakamatana, kila mtu akimshika mwenziwe kichwa chake, na kutia upanga wake katika ubavu wa mwenzake; wakaanguka pamoja; hata mahali pale pakaitwa Helkath-hasurimu, napo ni katika Gibeoni. Vita vile vilikuwa vikali sana siku ile; naye Abneri akashindwa, na watu wa Israeli, mbele ya watumishi wa Daudi.”

Hata hivyo swala la kuwa na amani ya pamoja lilikuwa ni wazo zuri na mapenzi ya Mungu hivyo Daudi alilikubali na alimkubali Abneri kama mtu mwenye akili na mwema na aliyekubali kushindwa na kukubali mpango wa Mungu.    

Kufa afavyo Mpumbavu!

Abneri alikuja Hebron ili aweze kuonana na Daudi na kufanya patano naye 2 Samuel 3:20-23 “Basi Abneri akamwendea Daudi huko Hebroni, na watu ishirini pamoja naye. Daudi akamfanyia karamu Abneri, na watu wote waliokuwa pamoja naye. Kisha Abneri akamwambia Daudi, Nitaondoka, niende zangu; nami nitamkusanyia bwana wangu mfalme Israeli wote, ili wafanye agano nawe, ukamiliki juu ya wote inaowatamani roho yako. Basi Daudi akamruhusu Abneri; naye akaenda zake kwa amani. Na tazama, watumishi wa Daudi pamoja na Yoabu walitoka jeshini, wakaleta mateka mengi pamoja nao; lakini Abneri hakuwako Hebroni kwa Daudi; maana alikuwa amemruhusu, naye amekwisha kwenda zake kwa amani. Hata Yoabu, na jeshi lote waliokuwa pamoja naye, walipofika, watu wakamwambia Yoabu, wakisema, Abneri, mwana wa Neri, alikuja kwa mfalme, naye amemruhusu, naye amekwenda zake kwa amani.”

Daudi aliamini kuwa yalikuwa ni mapatano ya kweli na kuwa Abneri sasa anakwenda kuwakusanya watu kwaajili ya Daudi ili wafanye patano naye na kumfanya mfalme kwa njia ya amani, Hata hivyo Kamanda mkuu wa majeshi ya Daudi alikuwa hayuko wakati hilo likifanyika na kwa medani za kivita Yoabu hakuamini kuwa Abneri alikuwa na nia ya dhati ya kufanya hivyo yeye alikumbuka kuwa huyu ndiye alikuwa mpinzani mkubwa wa kuzuia kusudi la Mungu na iweje leo aweze kuwa mwema aidha Yoabu alikuwa na ufahamu kuwa Abneri pia alikuwa na kisasi cha damu ya kumuua Asaheli Ndugu yake, Yoabu alisikitika kuwa ni kwanini Abneri amekuja na Daudi anamuachia aende zake kwa amani inawezekanaje mtu mwenye nia ovu kesho akawa na nia njema? Hivyo Yoabu aliagiza kuwa Abneri arudi akidhani ya kuwa ameitwa tena na Daudi kumbe Yoabu alitaka kujilipizia kisasi kwaajili ya Ndugu yake ona

2Samuel 3:24-27 “Basi Yoabu akamwendea mfalme, akasema, Umefanyaje? Tazama, Abneri amekuja kwako; mbona umemruhusu, naye amekwisha kwenda zake?  Wewe wamjua Abneri, mwana wa Neri, ya kuwa alikuja ili kukudanganya, apate kujua kutoka kwako, na kuingia kwako, akajue yote uyatendayo. Naye Yoabu alipotoka kwa Daudi, akapeleka wajumbe kumfuata Abneri, wakamrudisha kutoka kisima cha Sira; lakini Daudi alikuwa hana habari. Basi Abneri alipokuwa amerudi Hebroni, Yoabu akamchukua kando hata katikati ya lango, ili aseme naye kwa faragha; akampiga mkuki wa tumbo huko, hata akafa; kwa ajili ya damu ya Asaheli, ndugu yake.”

Tukio hili lilimsikitisha sana Daudi, kwani lingeweza kuhesabika ya kuwa amechukua ufalme kwa upanga, hata hivyo Daudi alifahamu kuwa Abneri hakuwa na nia ya uovu, hivyo alilaani vikali tukio la Yoabu. Na kumlaani Yoabu pamona na nyumba yake kwa kumuua mtu ambaye alikuwa anataka amani, Daudi aliitisha mbiu ya maombolezo lilikuwa ni tukio la kusikitisha sana Hata hivyo katika maombolezo hayo Daudi hakumlaumu yeyote bali alimlaumu Abneri mwenyewe kwa kufa kipumbavu ona

2Samuel 3:28-34 “Hata baadaye Daudi aliposikia, akasema, Mimi na ufalme wangu hatuna hatia milele mbele za Bwana, kwa sababu ya damu ya Abneri, mwana wa Neri; na imwangukie Yoabu kichwani pake, na nyumba yote ya babaye, tena hiyo nyumba ya Yoabu isikose kuwa na mtu mwenye kutoka damu, au aliye na ukoma, au mwenye kutegemea fimbo, au mwenye kuanguka kwa upanga au mwenye kuhitaji chakula. Basi Yoabu, na Abishai nduguye, walimwua Abneri, kwa sababu yeye alimwua ndugu yao Asaheli katika vita huko Gibeoni. Kisha Daudi alimwambia Yoabu, na watu wote waliokuwa pamoja naye, Rarueni nguo zenu, mkajivike nguo za magunia, mkamlilie Abneri. Naye mfalme Daudi akaifuata jeneza. Wakamzika Abneri katika Hebroni; naye mfalme akapaza sauti yake, akalia kaburini kwa Abneri, nao watu wote wakalia. Ndipo mfalme akamwomboleza Abneri, akasema, Ilimpasaje Abneri kufa afavyo mpumbavu? Mikono yako haikufungwa, Wala miguu yako haikutiwa pingu; Aangukavyo mtu mbele ya wana wa uovu, ndivyo ulivyoanguka. Na watu wote wakaongeza kumlilia.”

Kwa nini Daudi amsikitikie Abneri kuwa amekufa kipumbavu?  Hii ni kwa sababu Abneri aliuawa pembeni kidogo tu ya lango la mji wa Hebroni, Mji wa  Hebroni ulikuwa ni mji wa makimbilio, miji ya makimbilio ilikuwa ni miji maalumu iliyotengwa kwaajili ya kutunza uhai wa mtu aliyeua kwa bahati mbaya, Abneri alikuwa amemuua Asaheli hivyo ilikuwa rahisi kwa mtu mwenye kutaka kisasi cha damu ya ndugu yake kumuua na mahali sahihi na salama ni kwenye moja ya miji ya makimbilio na Hebron ulikuwa ni mojawapo ya miji hiyo, hii ni miji ambayo muuaji angekimbilia humo angekula angevaa na kuishi salama miji hii iliwekwa na Mungu kwa sababu hiyo!

Hesabu 35:9-16 “Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia, Nena na wana wa Israeli, uwaambie, Mtakapovuka mto wa Yordani na kuingia nchi ya Kanaani, Ndipo mtajiwekea miji iwe miji ya makimbilio kwa ajili yenu; ili kwamba mwenye kumwua mtu, pasipo kukusudia kumwua, apate kukimbilia huko. Na hiyo miji itakuwa kwenu kuwa makimbilio, kumkimbia mwenye kutwaa kisasi, ili asiuawe mwenye kumwua mtu, hata atakaposimama mbele ya mkutano ahukumiwe. Na hiyo miji mtakayowapa itakuwa kwenu ni miji sita ya makimbilio. Mtawapa miji mitatu ng'ambo ya pili ya Yordani, na miji mitatu mtawapa katika nchi ya Kanaani; miji hiyo itakuwa ni miji ya makimbilio. Miji hiyo sita itakuwa miji ya makimbilio kwa ajili ya wana wa Israeli, na kwa ajili ya mgeni, na kwa ajili ya huyo aketiye kati yao hali ya ugeni; ili kila amwuaye mtu, naye hakukusudia kumwua, apate kukimbilia huko. Lakini kama alimpiga kwa chombo cha chuma, akafa, ni mwuaji huyo; mwuaji hakika yake atauawa.”

·         Ni miji iliyowekwa na Mungu kwaajili ya usalama wa kila mtu.

·         Ni miji iliyowekwa na Mungu kwaajili ya kupate neema ya kutokuuawa

·         Ni miji iliyowekwa na Mungu ikiwa na mamlaka ya kuokoa

·         Ni miji iliyowekwa na Mungu kwa makusudi ya kutunza uhai

·         Ni miji Iliyokuwa maarufu na iliyojulikana sana na kila mtu aliijua

·         Ni miji iliyowekwa na Mungu kutoa mahitaji ya kutosha kwa kila anayekimbilia

·         Ni miji iliyokuwa imeandaliwa kwa maelekezo ya Mungu

·         Ni miji ambayo njia zake hazikufungwa

·         Miji hii ilikuwa sita tu katika nchi nzima ya Israel

 

1.       Kadesh – maana yake Haki

2.       Shekemu – mabega maana yake nguvu za Mungu

3.       Hebron -  maana yake Ushirika

4.       Bezeri – maana yake Ngome

5.       Ramoth – maana yake juu

6.       Na Golan – Maana yake Furaha

Kwa hiyo ilihitajika hatua moja tu kujikinga ndani ya mji wa Hebron, kwa mtu aliyekuwa shujaa, aliyepigana vita vingi sana, jemadari, anakujaje kufa wakati wa amani tena hatua chache tu kutoka lango la mji unaoweza kuokoa, tena akiwa na silaha zake, tena akiwa hajatiwa pingu, tena akiwa hajafungwa miguu wala mikono, tena akiwa hajachukua tahadhari ya aina yoyote,  Komandoo anawezaje kufa kirahisi namna ile, kimsingi yako mambo ambayo yako katika uwezo wetu ambayo tulitakiwa kuchukua hatua moja tu na hiyo ingetuweka mahali salama, Mungu ametupa Mwokozi, ametupa Yesu Kristo aliye haki yetu, aliye na nguvu za kiungu za kutusaidia ambaye anahitaji ushirika na kila mtu, ambaye ni ngome imara, ambaye yuko mkono wa kuume wa Mungu mbinguni ambaye ni furaha yetu, yuko tayari kutoa neema kwa kila mtu, yuko tayari kuokoa, yuko tayari kutuhifadhi na kutunza uhai wetu, anatoa kila kitu ni msaada ulio karibu, yuko tayari kumsaidia kila mtu hata bila kujali umefanya dhambi kiasi gani yuko tayari kusamehe na kukuhifadhi ni kifo cha kujitakia kufa bila kumpokea Yesu, ni aibu kukaa karibu na injili na kushindwa kuchukua hatua moja tu itakayostawisha usalama wako milele, ndani ya mji yuko mfalme ambaye anataka amani na wewe anakuamini hata kama watu hawakuamini, iweje leo ushindwe kuchukua hatua, ndugu yangu ni aibu ni kufa kipumbavu kama tutashindwa kumtumia Yesu aliyetupa kila kitu katika maisha yetu, ni hatua moja tu ya maombi, ni hatua moja tu ya kufunga, ni hatua moja tu ya kukumbuka kuwa liko lango la Hebron ni kuingia tu hakuna wa kukuzuia hupaswi kufa kipumbavu!  Na huwezi kuwa salama nje ya mji wa makimbilio! Kamanda mwenye akili na mwenye kujua mapenzi ya Mungu na mtu ambaye aklikuwa na nguvu na mzoezu wa vita ilikuwaje akafa kipumbavu, leo hii yako magonjwa mengine kama yakituua ni kwa sababu tumejitakia, maandiko yanasema kila atakayeliitia jina la Bwana ataokoka, tena yanasema nimekukimbilia wewe bwana nisiabike milele, mtu mweye akili na hekima kama wewe huwezi kuangamia ilihali unajua ya kuwa Yesu ni kimbilio na msaada wetu, heri leo kama utayatoa maisha yako kwake na kukubali msaada mkubwa utokao kwake !

Na Rev. Innocent Samuel Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima!

Heri wenye Upole !


Mathayo 5:1-5 “Naye alipowaona makutano, alipanda mlimani; na alipokwisha kuketi, wanafunzi wake walimjia; akafumbua kinywa chake, akawafundisha, akisema, Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao. Heri wenye huzuni; Maana hao watafarijika. Heri wenye upole; Maana hao watairithi nchi.”


Utangulizi.

Nimekuwa kiongozi na Mchunjaji kwa Muda mrefu sana nimemtumikia Mungu kwa karibu robo tatu ya maisha yangu yote sasa, nimekutana na changamoto nyingi na za aijna mbalimbali, Pia nimewahi kupigana vita za aina mbalimbali za kiroho na naweza kukiri wazi kuwa hakuna vita nimewahi kushindwa kwa sababu wakati wote nilipopigana nalimtafuta Bwana ili awe upande wangu kwanza kwa hiyo ushindi wangu umetokana na Bwana mwenyewe kunipigania!, Moja ya changamoto kubwa kutoka kwa watu wanaonipiga vita katika uongozi wangu ni pamoja na kunishutumu kuwa mimi sifai kwa sababu ni MPOLE sikuhuzunika lakini hili lilinipa kutafakari kwani Upole ni sifa mbaya kwa mwanadamu? Au ni sifa Njema? Hili lilinifanya nianze kurejea katika maandiko na kuanza kujifunza kwa kina na mapana na marefu ili nipate kujua kuhusiana na UPOLE. Viongozi wakubwa sana katika maandiko wanaelezwa kuwa walikuwa wapole akiwemo Musa ona katika Hesabu 12:3 “Basi huyo mtu, huyo Musa, alikuwa mpole sana zaidi ya wanadamu wote waliokuwa juu ya uso wa nchi.” Unaona lakini sio hivyo tu Yesu akitoa mwaliko wa watu wenye kuelemewa na changamoto mbalimbali anajitaja mwenyewe kuwa ni mpole na mnyenyekevu wa Moyo unaweza kuona katika Mathayo 11:28-29 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha. Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu; Upole ni nini hasa je ni sababu ya kulaumiwa? Ni sifa mbaya? Ama ni sifa njema? Hili swala litupa nafasi ya kutafakari kwa kina na mapana na marefu katika somo hili katika jina la Yesu Kristo amen!

Maana ya Upole!

Katika hutuba maarufu sana ya Yesu Kristo inayojulikana kama Hutuba ya Mlimani, Yesu alifundisha pamoja na mafundisho mengine mafundisho ya HERI kama nane hivi ambazo kwa kiingereza zinaitwa Beatitudes ambalo maana yake ni “Supreme Blessedness” yaani mtu aliyebarikiwa sana sasa katika moja ya sifa hizo za watu waliobarikiwa sana mojawapo ni UPOLE kwa hiyo Mathayo 5:5 “Heri wenye upole; Maana hao watairithi nchi.” Maana yake wamebarikiwa sana wenye upole maana hao watairithi nchi kwa hiyo UPOLE ni Baraka UPOLE ni neema ya Mungu ya ngazi ya juu sana, lakini ni lazima nan i muhimu kuelewa maana na neno hilo UPOLE

Neno upole linalotumika katika Kiswahili kwenye Biblia ya kiingereza linasomeka kama MEEK ambalo kwa ujumla linabeba maana tajiri sana ambazo kimsingi zinaweza kukomba matunda yote ya roho yanayotajwa katika maandiko MEEK - MILD, SUBMISSIVE, MODERATE, QUITE, GENTLE, LONG-SUFFERING, PATIENT. Maneno hayo yote yanayozingumzia upole kama MEEK katika unyambulisho wake yanatupa picha pana sana kuwa mtu mwenye upole kwa vyovyote vile ni mtu mkamilivu na momavu na katika maswala ya kiroho ni mtu wa ngazi ya juu sana kwani ameweza kubeba matunda mengi ya rohoni ona maana hizo kwanza 

MILD – MTARATIBU, SUBMISSIVE – MTIIFU, MNYENYEKEVU, MODERATE – MTU WA WASTANI (KIASI), ULINGANIFU USAWA, QUITE MKAMILIFU, GENTLE – MUUNGWANA, LONG-SUFFERING – MVUMILIFU, ASIYEKASIRIKA KWA HARAKA, PATIENCE – ALIYE NA SUBIRA.

Unaona kwa hiyo tunaposoma katika kitabu cha Wagalatia 5:22-23 “Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria.

Aina hii ya upole Yakobo aliita Upole wa hekima Yakobo 3: 13 “N'nani aliye na hekima na ufahamu kwenu? Na aonyeshe kazi zake kwa mwenendo wake mzuri, katika upole wa hekima”.

Aidha neno hili katika Biblia ya kiyunani linatumika kama neno PRAUS au PRAEIS ambalo tafasiri yake ni MILD  ikimaanisha mtu mwenye uwezo wa kujishusha kwa Mungu na wanadamu, au mtu mwenye uwezo wa kutumia nguvu na mamlaka lakini akawa na subira kwa faida ya wengine, Kimsingi hii ilikuwa sifa kubwa sana ya viongozi wa kibiblia na hata mfalme Daudi alikuwa miongoni mwa watu wa namna  hata alipotafuta kuuawa na Sauli aliyekuwa anamchukia sana yeye hakufanya haraka kumdhuru waola kujitakia kisasi hata pale ambapo Mungu alimwambia kufanya hivyo yeye alisubiri wakati muafaka wa Mungu hii ona

Zaburi 37:10-13 “Maana bado kitambo kidogo asiye haki hatakuwapo, Utapaangalia mahali pake wala hatakuwapo. Bali wenye upole watairithi nchi, Watajifurahisha kwa wingi wa amani. Asiye haki hunuia mabaya juu ya mwenye haki, Na kumsagia meno yake. Bwana atamcheka, Maana ameona kwamba siku yake inakuja.”

Unaona kwa msingi huo ni vema ikaeleweka wazi kuwa Upole sio udhaifu bali Nguvu za Mtu mwenye uwezo  chini ya udhibiti wa Nguvu za Mungu, kwa hiyo mtu Mpole ni mtu anayeachia mambo chini ya udhibiti wa Mungu, ili Mungu mwenyewe achukue hatua za haki, ni mtu ambaye hajifikiri kuwa bora nje ya neema ya Mungu, upole ni hali ya kufikiri kuwa nguvu zetu na mamlaka yetu ina mipaka ya kufikiri katika Mungu kwa nia njema kuliko kuitikia haraka kwa hasira za kibinadamu Yakobo 1:20 “kwa maana hasira ya mwanadamu haiitendi haki ya Mungu.” Mtu mwenye upole hutembea katika neema ya Mungu na hanaga mpango wa kunia makuu kuliko impasavyo kunia.

Warumi 12:3 “Kwa maana kwa neema niliyopewa namwambia kila mtu aliyeko kwenu asinie makuu kupita ilivyompasa kunia; bali awe na nia ya kiasi, kama Mungu alivyomgawia kila mtu kiasi cha imani.”

Heri wenye upole!

Maana yake kuna amebarikiwa sana Mtu mwenye upole hii maana yake ni kuwa kuna faida kubwa sana za upole kama ifuata vyo:-

ü  Watu wenye upole ni watu waliobarikiwa kwa kiwango kikubwa Mathayo 5:5 “Heri wenye upole; Maana hao watairithi nchi.” Hii maana yake ni nini maana yake ni kuwa na uhusiano na Muumba wa mbingu na Nchi, urithi mtu huupata kutokwa kwa yule eliyemzaa au aliyekuandikisha uupate kwa sababu ya wema wake mtu akiwa mpole maana yake anafanana na Mungu ni mwana wa Mungu hivyo anastahili urithi, Ni Mungu ndiye aliyeumba mbingu nan chi na hivyo kuwa mwanae kwa sababu ya upole kwa msingi huo lazima tutarajie Baraka za Mungu hata pale atakapoiumba mbingu mpya nan chi mpya Mungu atawarithisha watoto wake

 

ü  Watu wenye upole hutetewa na Mungu Hesabu 12:1-9 “Kisha Miriamu na Haruni wakamnenea Musa kwa sababu ya mwanamke Mkushi aliyekuwa amemwoa; maana, alikuwa amemwoa mwanamke Mkushi. Wakasema, Je! Ni kweli Bwana amenena na Musa tu? Hakunena na sisi pia? Bwana akasikia maneno yao. Basi huyo mtu, huyo Musa, alikuwa mpole sana zaidi ya wanadamu wote waliokuwa juu ya uso wa nchi. Bwana akanena ghafula na Musa, na Haruni na Miriamu, na kuwaambia, Tokeni nje ninyi watatu, mwende hemani mwa kukutania. Basi hao watatu wakatoka nje. Bwana akashuka katika nguzo ya wingu akasimama pale mlangoni pa Hema, akawaita Haruni na Miriamu, nao wakatoka nje wote wawili. Kisha akawaambia, Sikizeni basi maneno yangu; Akiwapo nabii kati yenu, Mimi, Bwana, nitajifunua kwake katika maono, Nitasema naye katika ndoto. Sivyo ilivyo kwa mtumishi wangu, Musa; Yeye ni mwaminifu katika nyumba yangu yote; Kwake nitanena mdomo kwa mdomo, Maana, waziwazi wala si kwa mafumbo; Na umbo la Bwana yeye ataliona. Mbona basi ninyi hamkuogopa Kumnenea mtumishi wangu, huyo Musa? Hasira za Bwana zikawaka juu yao; naye akaenda zake.”

 

ü  Watu wenye upole hudumu muda mrefu katika nafasi zao na katika maisha Zaburi 37:10-13 “Maana bado kitambo kidogo asiye haki hatakuwapo, Utapaangalia mahali pake wala hatakuwapo. Bali wenye upole watairithi nchi, Watajifurahisha kwa wingi wa amani. Asiye haki hunuia mabaya juu ya mwenye haki, Na kumsagia meno yake. Bwana atamcheka, Maana ameona kwamba siku yake inakuja.” Unaona kama unataka kudumu Muda mrefu uwe mwenye haki, kama watu wapole kuna stori moja ya kuchekesha kuhusu Meno na Ulimi, siku moja ulimi ulimwambia Mungu kuwa tafadhali umeniweka mimi katika wito wangu pamoja na meno na meno ni mgumu kuliko mimi kwa hiyo mara kwa mara katika kutimiza wajibu wetu meno amekuwa akinumiza na kuniacha na majeraha nikipona tena baada ya Muda meno hufanya hivyo hivyo ndipo Mungu akamjibu meno kazi yenu ni ya muda tu lakini wewe ulimi ni wa muda mrefu zaidi kuliko meno hivyo ni lazima ujifunze kuvumilia, baada ya miaka 70 au 80 hivi ya maisha yenu uje unipe majibu, baada ya muda huo kupita kumbe meno mengi yalioza na kung’oka lakini ulimi ulibaki, ni wazi kabisa kama maandiko yasemavyo aggressive people shall not live longer but Mild people will live more than normal ,  watu wakali hawadumu lakini watu wapole hudumu, in the workplace the arrogant and powerful seems to win but in the end they  lose alisema mtu mmoja kazini watu jeusi na wanaojiinua huonekana kama washindi lakini mwishoni wanyenyekevu ndio wanaoshinda, Ni changamoto kubwa sana kuachia mamlaka zetu na nguvu zetu katika mikono ya Mungu na kujinyenyekesha, tunaweza kuona raja kwa kitambo kutumia mamlaka zetu, kufukuza watu, kumarisha watu lakini ni ukweli ulio wazi kuwa hatima yake ni huzuni, hawafanikiwi katika lolote watu jeuri hawana marafiki wala hata wakipata fedha hawatosheki, wanaweza kudhani kuwa wanaumiliki ulimwengu lakini ni ukweli kuwa ulimwengu unawamiliki, Mwanamke na mwanaume wanaojikweza na kutaka kuonyesha nguvu zao huishia katika aibu na upweke hakuna mtu anaweza kuwa na urafiki na mtu jeuri!, wanawake huvutiwa sana na mwanaume mpole. Mwaname mkali hawezi kufaidi lolote hata katika ndoa yake! Mithali 22:24-25 “Usifanye urafiki na mtu mwenye hasira nyingi; Wala usiende na mtu wa ghadhabu nyingi; Usije ukajifunza njia zake; Na kujipatia nafsi yako mtego.”

 

ü  Upole unakaribisha uwepo wa Mungu Isaya 66:1-2 “Bwana asema hivi, Mbingu ni kiti changu cha enzi, na dunia ni mahali pa kuweka miguu yangu; mtanijengea nyumba ya namna gani? Na mahali pangu pa kupumzikia ni mahali gani? Maana mkono wangu ndio uliofanya hivi vyote, vitu hivi vyote vikapata kutokea, asema Bwana; lakini mtu huyu ndiye nitakayemwangalia, mtu aliye mnyonge, mwenye roho iliyopondeka, atetemekaye asikiapo neno langu.” Uwepo wa Mungu unakaa na watu wanyenyekevu wanyonge na wapole bila upole nafsi ya mwanadamu inakuwa katika mgogoro wa ndani, inasababisha hasira, kuchanganyikiwa, uchungu, na kukosa utulivu,  Upole unaweka mambo sawa na kupunguza mawimbi, unaleta utaratibu wakati wa machafuko unaponya nafsi na kutiisha mawimbi, Lazima mwanadamu akumbuke kuwa yeye ni mavumbi, ukikumbuka kuwa wewe ni udongo itakusaidia, Upole unaleta furaha na amani ya kweli, kama Mungu akiwa na ghadhabu na hasira kama tulizonazo sisi kwa wengine tungekuwa wapi leo? Watu wengine hata wakisikia masengenyo tu  mahali wanakurupuka na kufanya maamuzi hata bila kufanya uchunguzi wa kina na wa kutosha  je Mungu anekuwa mwepesi wa hasira kama wewe na mimi ingekuwaje ?

 

ü  Upole ni alama ya ukomavu wa kiroho Wagalatia 5:22-23 “Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria.” Hakuna jambo linachosha duniani kama kuchunga wakristo wa Mwilini yaani wakristo ambao hawajakomaa kiroho au waliodumaa, Paulo mtume alisikitishwa sana na Kanisa lililodumaa na la wakristo wa mwilini kwani jamii hii ya wakristo wana taabu sana kuliko hata wapagani kutokana na kufarakana na kugombana na kufanya mambo ya ajabu yanayotukanisha ukristo 1Wakorintho 3:1-3 “Lakini, ndugu zangu, mimi sikuweza kusema nanyi kama na watu wenye tabia ya rohoni, bali kama na watu wenye tabia ya mwilini, kama na watoto wachanga katika Kristo. Naliwanywesha maziwa sikuwalisha chakula; kwa kuwa mlikuwa hamjakiweza. Naam, hata sasa hamkiwezi, kwa maana hata sasa ninyi ni watu wa tabia ya mwilini. Maana, ikiwa kwenu kuna husuda na fitina, je! Si watu wa tabia ya mwilini ninyi; tena mnaenenda kwa jinsi ya kibinadamu?  unaona watu waliokomaa kiroho hawana muda wa majungu, fitina na husuda na maswala mengine, UPOLE ni alama muhimu sana kwa mtu aliyekomaa kiroho, lakini mtu wa tabia ya mwilini asiyekomaa kiroho hawezi kuwa na utulivu, kwa sababu hana matunda ya rohoni!

 

Hitimisho:

Ni mmuhimu kuelewa kuwa tunaweza kumuomba Mungu atupe upole kama jinsi ambavyo tunaomba Mambo mengine Yakobo 1:5 “Lakini mtu wa kwenu akipungukiwa na hekima, na aombe dua kwa Mungu, awapaye wote, kwa ukarimu, wala hakemei; naye atapewa.” Ingawa Yakobo hapo  anaelezea swala la kuomba Hekima ni muhimu pia kujua kuwa Upole ni Hekima kwa hiyo tunapoomba Hekima tunaweza kupokea na upokle ndani yake hekima ya kiungu ikoje? Yakobo 3:17-18 “Lakini hekima itokayo juu, kwanza ni safi, tena ni ya amani, ya upole, tayari kusikiliza maneno ya watu, imejaa rehema na matunda mema, haina fitina, haina unafiki. Na tunda la haki hupandwa katika amani na wale wafanyao amani.” Kumbe tunaweza kuiomba Hekima hii iliyojaaa amani, rehema, matendo mema na iko tayari kusikiliza kwa hiyo ni lazima tumuombe Mungu atupe upole. Martin Luther King Alipingana na ubaguzi uliokuwepo Marekani, alitaka watu wote wahesabike kuwa sana alifanya maandamano ya amani hakuwahi kufanya vurugu wala kuruhusu wafuasi wake kufanya fujo akitumia falsafa ya Mahatma Ghandi ya non-violence resistance, kupinga maswala yasiyo haki bila kumwaga Damu, hii maana yake ni kuwa alikuwa Mpole Bwana na ampe neema kila mmoja wetu kuwa mpole katika jina la Yesu Kristo, kwa hiyo ieleweke wazi kuwa Upole sio udhaifu upole ni sifa kubwa na ya kipekee sana katika uhusiano wetu na Mungu, hivyo wale wanaonishutumu kuwa mimi ni Mpole sasa nimewaelewa vema asanteni!

 

Na Rev. Innocent Samuel Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima     

Jumatatu, 7 Novemba 2022

Enda ukawapige Amaleki !


1Samuel 15:1-3 “Wakati huo Samweli akamwambia Sauli, Bwana alinipeleka nikutie mafuta, uwe mfalme wa watu wake Israeli; basi sasa, isikilize sauti na maneno ya Bwana. Bwana wa majeshi asema hivi, Nimeyatia moyoni mwangu mambo hayo Amaleki waliyowatenda Israeli, jinsi walivyowapinga njiani, hapo walipopanda kutoka Misri. Basi sasa enda ukawapige Amaleki, na kuviharibu kabisa vitu vyote walivyo navyo, wala msiwaachilie; bali waueni, mwanamume na mwanamke, mtoto naye anyonyaye, ng'ombe na kondoo, ngamia na punda. 



Utangulizi:

Mapema sana miaka mingi Mungu alikuwa amemuahidi rafiki yake Abrahamu kuwa atampa nchi ya mkanaani, lakini alimueleza wazi kuwa atayatimiza haya katika kizazi cha nne wakati huo uovu wa wakanaani utakuwa umefikia kiwango cha juu ona

Mwanzo 15:13-16 “BWANA akamwambia Abramu, Ujue hakika ya kwamba uzao wako utakuwa mgeni katika nchi isiyo yake, watawatumikia watu wale, nao watateswa muda wa miaka mia nne. Hata na taifa lile, watakaowatumikia, nitawahukumu; baadaye watatoka na mali mengi. Lakini wewe utakwenda kwa baba zako kwa amani, utazikwa katika uzee mwema. Na kizazi cha nne kitarudi hapa, maana haujatimia uovu wa Waamori bado.”

Unaona moja ya makabila ambayo uovu wao ulikuwa umefikia kiwango ni pamoja na waamaleki ambao kimsingi Mungu alikasirishwa nao kwa sababu ndio walikuwa wa kwanza kupinga na kusudi la Mungu kwa kupingana ana kusudi la Mungu kwa kutaka kwiazuia wana wa Israel njiani ili wasiweze kwenda katika nchi ya mkanaani ona

Kutoka 17:14 “BWANA akamwambia Musa, Andika habari hii katika kitabu iwe ukumbusho, kisha ihubiri masikioni mwa Yoshua; ya kuwa nitaufuta ukumbusho wa Amaleki kabisa, usiwe tena chini ya mbingu.”

Mungu alikasirishwa na Amaleki na alikusudia kuwafuta wasiwepo milele kwa sababu ya uovu wao na moja ilikuwa ni kuwauzia wana wa Israel wasiende kwa amani katika nchi ya kanaani lakini pili ni kwa kutokuwahurumia watu wanyonge waliokuwa wamechoka jangwani wagonjwa na waliokuwa wamechoka jangwani

Kumbukumbu la Torati 25:17-19 “Kumbuka aliyokufanya Amaleki katika njia mlipokuwa mkitoka Misri; jinsi alivyokukuta katika njia, akapiga katika watu wako walioachwa nyuma, wote waliokuwa wanyonge nyuma yako, ulipokuwa umechoka na kuzimia; wala asimche Mungu.  Basi itakuwa, hapo atakapokwisha kukupumzisha Bwana, Mungu wako, katika adui zako wote walio kando-kando, katika nchi akupayo Bwana, Mungu wako, iwe urithi uimiliki, ndipo uufute ukumbuko wa Amaleki chini ya mbingu; usisahau.”

Kwaajili ya hayo Mungu alikuwa anataka kumbukumbu ya watu hawa wasiofaa iondolewe kabisa milele katika uso wa ardhi na kwa bahati njema agizo hili alipewa mfalme Sauli ambaye kwa bahati mbaya na kwa kukosa utii aliwabakiza kinyume na maagizo ya torati jambo lililolata laana Mungu anapotupa agizo ni lazima yuhakikishe kuwa tunalitimiza kwa usahihi na hatupaswi kuhurumia chochote kinachowekwa mbele yetu maandiko yanasema amelaaniwa mtu yule aifanyaye kazi ya Mungu kwa ulegevu ona

Yeremia 48:10 10. “Na alaaniwe mtu afanyaye kazi ya Bwana kwa ulegevu; na alaaniwe auzuiaye upanga wake usimwage damu.”

Mungu anachokitaka kwetu leo ni kuhakikisha kuwa tunaangamiza kabisa kila kizuizi tunachokutana nacho kisibaki katika kumbukumbu zetu kuwa tuna kitu tumebakiza hakikisha unafutilia mbali kila kikwazo, kinachokukabili, iwe ni mitihani ya kidato cha pili au kidato cha nne au cha sita amaa lolote linalokusibu hakikisha kuwa unatimiza wala usishindwe wala usiuhurumia wala usibakize kama Sauli, leo ni siku yak o na wiki hii ni wiki yako kuhakikisha kuwa unampiga mwamaleki sio kwa ulegevu bali kwa bidii ukijua ya kuwa unamtumikia Mungu,

Warumi 12:11 “kwa bidii, si walegevu; mkiwa na juhudi katika roho zenu; mkimtumikia Bwana;”

Kutokutii agizo la kumtumikia Mungu na kufanya kinyume na maagizo yake kunaweza kutuleta katika wakati mgumu wa kukataliwa kama Sauli na kurfananishwa na waasi au wachawi, Sauli alipoteza nafasi ya kutimiza mapenzi ya Mungu alipofanya vile alivyotaka yeye,

1Samuel 15:7-11 “Sauli akawapiga Waamaleki, toka Havila uendapo Shuri, unaokabili Misri. Akamkamata Agagi, mfalme wa Waamaleki, yu hai, akawaangamiza hao watu wote kwa upanga. Lakini Sauli na watu wake wakamwacha Agagi hai, na katika kondoo walio wazuri, na ng'ombe, na vinono, na wana-kondoo, na cho chote kilicho chema, wala hawakukubali kuwaangamiza; bali cho chote kilichokuwa kibaya na kibovu, ndicho walichokiangamiza kabisa. Ndipo neno la Bwana likamjia Samweli, kusema, Najuta kwa sababu nimemtawaza Sauli awe mfalme; maana amerudi nyuma, asinifuate, wala hakufanya nilivyomwamuru. Samweli akasikitika, akamlilia Bwana usiku kucha.”

Leo hii Mungu anamtuma kila mmoja kwenda kuyatimiza mapenzui yake na kuhakikisha kuwa anaangamiza kila kikwazo kinachozuia mafanikio yake kwa asilimia 100, Na tukifanya hivyo Mungu hatasikitika badala yake atatufurahia kwani tunatimiza mapenzi yake kupiia kila kilichoko moyoni mwake ambacho kimeandikwa katika neno lake weka bidii katika kila ulifanyalo ukijua ya kuwa unayatenda mapenzi ya Mungu, soma kwa bidii, fanya kazi kwa bidii, acha majungu, acha unafiki, acha kuigiza, kila mmoja na amtangulize Mungu mbele na bwana atampa neema kila mmoja wetu na kumfanikisha katika jina la Yesu Amen           

Na Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye hekima.

Kuupiga mateke mchokoo !


Matendo 26:12-15Basi katika kazi hiyo nilipokuwa nikienda Dameski, mwenye mamlaka na maagizo ya wakuu wa makuhani; Ee Mfalme, ndipo wakati wa adhuhuri njiani naliona nuru inatoka mbinguni ipitayo mwangaza wa jua, ikinimulikia mimi, na wale waliofuatana nami pande zote. Tukaanguka nchi sote, nikasikia sauti ikisema nami kwa lugha ya kiebrania, Sauli! Sauli! Mbona waniudhi? Ni vigumu kwako kuupiga mateke mchokoo. Nami nikasema, Wewe u nani, Bwana? Bwana akaniambia, Mimi ni Yesu, ambaye wewe unaniudhi.”



Utangulizi:

Paulo mtume alikuwa ni kiongozi wa mateso ya wakristo mapema sana Kanisa likiwa katika hatua za awali, akiwakilisha mafarisayo pamoja na baraza la mahakama kuu ya kiyahudi iliyoitwa Senhedrin katika kuhakikisha kuwa wanawasambaratisha wakristo, yeye alisimamia kuuawa kwa Shemasi maarufu wa nyakati za kanisa la Kwanza aliyeitwa Stefano ona

Matendo 7:57-60 “Wakapiga kelele kwa sauti kuu, wakaziba masikio yao, wakamrukia kwa nia moja,wakamtoa nje ya mji, wakampiga kwa mawe. Nao mashahidi wakaweka nguo zao miguuni pa kijana mmoja aliyeitwa Sauli. Wakampiga kwa mawe Stefano, naye akiomba, akisema, Bwana Yesu, pokea roho yangu. Akapiga magoti, akalia kwa sauti kuu, Bwana, usiwahesabie dhambi hii. Akiisha kusema haya akalala. Na Sauli alikuwa akiona vema kwa kuuawa kwake.”

Baada ya mpango wake huu kufanikiwa mtu huyu aliendelea na hila za kutaka kulisambaratisha kanisa hasa kwa kuwatesa na kuwaburuza mahakamani na kuwatia gerezani  watu wa njia ile yaani wanaomuamini Bwana Yesu, na mpango wake huu ulikuwa ni tishio kubwa sana kwa kanisa  na kwa kweli maandiko yanaeleza kuwa aliliharibu kanisa kiasi ambacho waamini walitawanyika na waliobaki walikuwa ni mitume tu ona

Matendo 8:1-3 “Siku ile kukatukia adha kuu ya kanisa lililokuwa katika Yerusalemu; wote wakatawanyika katika nchi ya Uyahudi na Samaria, isipokuwa hao mitume. Watu watauwa wakamzika Stefano, wakamfanyia maombolezo makuu. Sauli akaliharibu kanisa, akiingia kila nyumba, na kuwaburuta wanaume na wanawake na kuwatupa gerezani.

Kama hilo halitoshi alipoona mpango wake umefanikiwa aliongeza mpango wa kwenda mbali nje ya Yerusalem ili nako akatekeleze mpango wake wa kuwatesa watakatifu na kuliharibu kanisa na sasa alikuwa anaelekea Dameski akiwa na kibali cha mahakama kuu ya kiyahudi kufanya hivyo, wakati huu sio akiwaza kuwafunga tu na hata kuwaua ona

Matendo 9:1-2 “Lakini Sauli, akizidi kutisha na kuwaza kuwaua wanafunzi wa Bwana, akamwendea Kuhani Mkuu, akataka ampe barua za kuenda Dameski zilizoandikwa kwa masinagogi, ili akiona watu wa Njia hii, waume kwa wake, awafunge na kuwaleta Yerusalemu.”

Ni katika mazingira kama haya ya utekelezaji wake wa nia ovu ya kusambaratisha Kanisa ndipo Yesu alipomtokea na kumkemea, vikali. Huku akimuonya kwamba aache kuupiga mateke Mchokoo!

Maana ya neno Mchokoo!

Matendo 26:12-15Basi katika kazi hiyo nilipokuwa nikienda Dameski, mwenye mamlaka na maagizo ya wakuu wa makuhani; Ee Mfalme, ndipo wakati wa adhuhuri njiani naliona nuru inatoka mbinguni ipitayo mwangaza wa jua, ikinimulikia mimi, na wale waliofuatana nami pande zote. Tukaanguka nchi sote, nikasikia sauti ikisema nami kwa lugha ya kiebrania, Sauli! Sauli! Mbona waniudhi? Ni vigumu kwako kuupiga mateke MCHOKOO. Nami nikasema, Wewe u nani, Bwana? Bwana akaniambia, Mimi ni Yesu, ambaye wewe unaniudhi.”

Neno Mchokoo katika biblia ya kiyunani linasomeka kama KENTRON ambalo kwa kiingereza ni Prick ambayo maana yake ni katikati centre au kwa lugha rahisi ni “NCHA” kali Ncha hii inaweza kuwa ya mkuki, mti wa kuchonga, au ncha ya panga au kisu,  kwa mujibu wa masimulizi ya kale wakulima wa zamani waliokuwa wanalima kwa kutumia jembe la kukokotwa na Ngo’mbe walikuwa wanaandaa fimbo ndefu yenye ncha kali na kumtegeshea mnyama kama Ngombe anapolima kama analeta ubishi au kiburi au upinzani anapopiga mateke angeweza kuumizwa nakitu hicho chenye ncha kali na hivyo angeweza kuacha mara moja tabia yake ya kushindana na mkulima, Paulo mtume alikuwa anakabiliwa na adhabu kali kutoka kwa Yesu Kristo ambaye ndiye mwanzilishi wa Kanisa, Paulo mtume alikuwa akishindana na Kusudi la Mungu ambalo kwa vyovyote vile lingweza kuleta madhara makubwa sana katika maisha yake kama hangelitubu na kugeuka na kumuhubiri Kristo, kuendelea kuwaua au kuwatesa wakristo, na kuwatia gerezani ilikuwa ni kushindana na kazi au agizo la Mungu mwenyewe,  hili liwe onyo sio kwa Paulo tu lakini kwa watu wote ambao kwa kiburi na kwa ujeuri hushindana na maagizo ya Mungu, hakuna mtu anayeweza kushindana na Mpango wa Mungu na kufanikiwa

Matendo 5:34-39 “Lakini mtu mmoja, Farisayo, jina lake Gamalieli, mwalimu wa torati, mwenye kuheshimiwa na watu wote, akasimama katika baraza, akaamuru mitume wawekwe nje kitambo kidogo, akawaambia, Enyi waume wa Israeli, jihadharini jinsi mtakavyowatenda watu hawa. Kwa sababu kabla ya siku hizi aliondoka Theuda, akijidai ya kuwa yeye ni mtu mkuu, watu wapata mia nne wakashikamana naye; naye aliuawa na wote waliomsadiki wakatawanyika wakawa si kitu. Baada ya mtu huyo aliondoka Yuda Mgalilaya, siku zile za kuandikiwa orodha, akawavuta watu kadha wa kadha nyuma yake, naye pia akapotea na wote waliomsadiki wakatawanyika. Basi sasa nawaambia, Jiepusheni na watu hawa, waacheni; kwa kuwa shauri hili au kazi hii ikiwa imetoka kwa binadamu, itavunjwa, lakini ikiwa imetoka kwa Mungu hamwezi kuivunja; msije mkaonekana kuwa mnapigana na Mungu.”

Mtu awaye yote ambaye anashindana na kupingana na kazi ya Mungu au jambo au shauri ambalo Mungu mwenyewe ni sababu kwa vyovyote vile anaupiga mateke mchokoo, Paulo alipokuwa anajaribu kulisambaratisha kanisa na kuonekana kama anafanikiwa kuwaudhi na kuwaumiza watakatifu,  alikuwa ni kama mtu anayejiumiza mwenyewe, wako watu wengi leo hii katika taasisi mbalimbali, makanisa, madhehebu na sehemu nyingine ambako adui wao wa kwanza ni wale wanaomcha Mungu, wanaweza kukutengenezea zengwe, wanaweza kukupiga vita, wanaweza kukudhukumu na kukuwekea vikwazo, wakidhani ya kuwa kwa kufanya hivyo watakukwamisha wewe lakini kwa bahati mbaya sana wanajiumiza wenyewe, Haya yalikuwa ni maonyo ya Yesu Kristo mwenyewe kumbuka kumbe Kristo yuko serious na kila aina ya binadamu anayeshindana na makusudi ya Mungu!

Kuupiga mateke mchokoo !

Ni muhimu kukumbuka kuwa makusudi ya Bwana hayawezi kuzuilika Ayubu 42:1-2 “Ndipo Ayubu akamjibu Bwana, na kusema. Najua ya kuwa waweza kufanya mambo yote, Na ya kuwa makusudi yako hayawezi kuzuilika.” Kila mwanadamu, mtu au awaye yote ambaye anashindana na kusudi la kiungu hapa Duniani anaupiga teke mchokoo na hatafanikiwa, kwa sababu unashindana na Mungu mwenyewe, sikiliza unaweza kusema kuwa hii sio injili kwa vile tunaishi katika agano Jipya lakini ngoja nikukumbushe kuwa maneno haya ni ya Yesu Mwenyewe akimuonya Paulo Mtume kuwa linapokuja swala la kuliudhi kanisa na kupambana ana kusudi la Mungu au hata mtu ambaye yuko katika kulitekeleza kusudi la Mungu hii iko wazi kabisa kuwa unashindana na Yesu Mwenyewe kumbuka maonyo haya ni makali Sauli Sauli mbona waniudhi? Kuna mmstari ambao ulikuwa unamfikia muhusika na kuwa ulikuwa umefikia wakati kuwa aidha aokoke au afe. Kushindana na Wakristo ni kuupiga teke mchokoo, kupamba ana kanisa ni kuupiga teke mchokoo, kushindana na watu wa Mungu ni kuupiga teke mchokoo na kushinda na mtu ambaye yuko kwenye kuyatimiza mapenzi ya Mungu ni kuupiga teke mchokoo na matokeo yake ni maumivu makali na makubwa zaidi

Madhaya ya kuupiga mateke Mchokoo!

Maandiko yananyesha wazi kuwa Mungu hawezi kuvumilia kwa namna yoyote mtu awaye yote ashindane na Kusudi lake na wote walioshindana na kusudi la Mungu aidha ndani ya mtu au taasisi zake Mungu aliwashughulikia vikali, ashukuriwe Mungu kuwa Paulo Mtume alielewa baadaye kuwa anashinda na Mapenzi ya Mungu na alitubu na kubadilika na kulitumikia shauri la Mungu, Lakini uzoefu wa kimaandiko unaonyesha kuwa Mungu hupigania mpango wake na watu wake pia, wako watu walishindana na Daniel na kumfanyia fitina ili kuathiri kusudi la Mungu ndani yake lakini badala ya Daniel kudhurika wao ndio walijikuta wako taabuni. 

Daniel 6:1-24 “Ilimpendeza Dario kuweka juu ya ufalme maliwali mia na ishirini, wawe juu ya ufalme wote; na juu yao akaweka wakubwa watatu, na Danieli alikuwa mmoja wao; ili maliwali hawa watoe hesabu kwao, mfalme asipate hasara. Basi Danieli huyo alipata sifa kuliko wakubwa na maliwali, kwa kuwa roho bora ilikuwa ndani yake; naye mfalme akaazimu kumweka juu ya ufalme wote. Basi mawaziri na maamiri wakatafuta sana kupata sababu za kumshitaki Danieli kwa habari za mambo ya ufalme; lakini hawakuweza kuona sababu wala kosa; kwa maana alikuwa mwaminifu, wala halikuonekana kosa wala hatia ndani yake. Ndipo wale watu wakasema, Hatutapata sababu ya kumshitaki Danieli huyo, tusipoipata katika mambo ya sheria ya Mungu wake. Basi wale mawaziri na maamiri wakakusanyika pamoja mbele ya mfalme, wakamwambia hivi, Mfalme Dario, uishi milele. Mawaziri wote wa ufalme, na manaibu, na maamiri, na madiwani, na maliwali wamefanya shauri pamoja ili kuweka amri ya kifalme; na kupiga marufuku, ya kwamba mtu ye yote atakayeomba dua kwa Mungu awaye yote, au kwa mtu awaye yote, katika muda wa siku thelathini, ila kwako, Ee mfalme atatupwa katika tundu la simba. Sasa, Ee mfalme, piga marufuku, ukatie sahihi maandiko haya, yasibadilike, kama ilivyo sheria ya Wamedi na Waajemi, isiyoweza kubadilika. Basi mfalme Dario akayatia sahihi maandiko yale, na ile marufuku. Hata Danieli, alipojua ya kuwa yale maandiko yamekwisha kutiwa sahihi, akaingia nyumbani mwake, (na madirisha katika chumba chake yalikuwa yamefunguliwa kukabili Yerusalemu;) akapiga magoti mara tatu kila siku, akasali, akashukuru mbele za Mungu wake, kama alivyokuwa akifanya tokea hapo.Basi watu hao wakakusanyika pamoja, wakamwona Danieli akiomba dua, na kusihi mbele za Mungu wake. Ndipo wakakaribia, wakasema mbele ya mfalme katika habari ya ile marufuku ya mfalme; Je! Hukuitia sahihi ile marufuku, ya kwamba kila mtu atakayeomba dua kwa Mungu awaye yote, au kwa mtu awaye yote, katika muda wa siku thelathini, ila kwako, Ee mfalme, atatupwa katika tundu la simba? Mfalme akajibu, akasema, Neno hili ni kweli, kama ilivyo sheria ya Wamedi na Waajemi isiyoweza kubadilika.  Basi wakajibu, wakasema mbele ya mfalme, Yule Danieli, aliye mmoja wa wana wa wale waliohamishwa wa Yuda, hakujali wewe, Ee mfalme, wala ile marufuku uliyoitia sahihi, bali aomba dua mara tatu kila siku. Basi mfalme aliposikia maneno haya alikasirika sana, akakaza moyo wake ili kumponya Danieli; akajitaabisha kumwokoa hata jua likachwa. Ndipo watu wale wakakusanyika pamoja mbele ya mfalme, wakamwambia mfalme, Ee mfalme, ujue ya kuwa ni sheria ya Wamedi na Waajemi, lisibadilike neno lo lote lililo marufuku, wala amri yo yote iliyowekwa na mfalme. Basi mfalme akatoa amri, nao wakamleta Danieli, wakamtupa katika tundu la simba. Mfalme akanena, akamwambia Danieli, Mungu wako unayemtumikia daima, yeye atakuponya.  Likaletwa jiwe, likawekwa mdomoni mwa lile tundu; naye mfalme akalitia muhuri kwa muhuri yake mwenyewe, na kwa muhuri ya wakuu wake, lisibadilike neno lo lote katika habari za Danieli. Kisha mfalme akaenda nyumbani kwake, akakesha usiku kucha, akafunga; na vinanda havikuletwa mbele yake; na usingizi wake ukampaa. Asubuhi mfalme akaondoka mapema, akaenda kwa haraka mpaka penye lile tundu la simba. Naye alipolikaribia lile tundu, akamlilia Danieli kwa sauti ya huzuni; mfalme akanena; akamwambia Danieli, Ee Danieli, mtumishi wa Mungu aliye hai, je! Mungu wako, unayemtumikia daima, aweza kukuponya na simba hawa? Ndipo Danieli akamwambia mfalme, Ee mfalme, uishi milele. Mungu wangu amemtuma malaika wake, naye ameyafumba makanwa ya simba, nao hawakunidhuru; kwa kuwa mbele zake mimi nalionekana kuwa sina hatia; tena, mbele yako, Ee mfalme, sikukosa neno. Basi mfalme akafurahi sana, akaamuru wamtoe Danieli katika lile tundu. Ndipo Danieli akatolewa katika lile tundu, wala dhara lo lote halikuonekana mwilini mwake, kwa sababu alikuwa anamtumaini Mungu wake. Mfalme akaamuru, nao wakawaleta wale watu waliomshitaki Danieli, wakawatupa katika tundu la simba, wao, na watoto wao,”

 Unaona wale waliokuwa wakishindana na Daniel katika maisha yake na kusudi la Mungu lilioko ndani yake ni wenyewe ndio waliokuja kuangamia badala ya Daniel, Mungu akufanyie hivyo na kuzidi dhidi ya adui zako wanaoukuandama na kutaka kupigana na kusudi la Mungu lililoko ndani yako!, Maandiko yanaonyesha pia kuwa Mungu alikuwa amekusudia kuwarithisha Israel Nchi ya mkanaani akiwa amewabariki tangu enzi za baba yao Ibrahimu na Isaka na Yakobo, lakini mfalme wa Moabu aliyeitwa Balaki alimuita mtu mmoja aje kuilaani Israel kinyume na kusudi la Mungu huku nako ni kushindana na kusudi la Mungu ni kuupiga mateke mchokoo, Balaamu aliamua kwenda kuilaani Israel lakini mpango wake ulipingwa vikali na malaika mpaka Punda akasema naye na sio hivyo tu badala ya kulaani alijikuta anatamka Baraka ona

Hesabu 23-7-8 “Akatunga mithali yake, akasema, Balaki amenileta kutoka Aramu, Mfalme wa Moabu kutoka milima ya mashariki, Njoo! Unilaanie Yakobo, Njoo! Unishutumie Israeli. Nimlaanije, yeye ambaye Mungu hakumlaani? Nimshutumuje, yeye ambaye Bwana hakumshutumu?

Unaona Balaamu alijikuta anawabariki Israel na kuwashuindwa kuwalaani au kuwashutumu, lazima ufikie wakati ambapo maadui wa ukristo au watumishi wa Mungu au mtu awaye yote wa Mungu waache kushindana nasi kwani kufanya hivyo ni kujichimbia shimo lao wenyewe Mithali 26:27 “Achimbaye shimo atatumbukia mwenyewe; Naye abingirishaye jiwe litamrudia.” Kila anayeshindana nawe hatafanikiwa kila anayekupiga vita anajipiga vita mwenyewe na kila anayekushutumu shutuma hizo zitamrudia kila anayeshindana na kusudi la Mungu lililoko ndani yako anaupiga vita mchokoo na ataumia mwenyewe!

Na. Rev. Innocent Samuel Kamote

Mkuu wa wajensi mwenye Hekima!

Jina la Bwana ni Ngome imara !


Mithali 18:10-14 “Jina la Bwana ni ngome imara; Mwenye haki huikimbilia, akawa salama. Mali ya mtu tajiri ni mji wake wa nguvu; Ni kama ukuta mrefu katika mawazo yake. Kabla ya uharibifu moyo wa mwanadamu hujivuna; Na kabla ya heshima hutangulia unyenyekevu. Yeye ajibuye kabla hajasikia, Ni upumbavu na aibu kwake. Roho ya mtu itastahimili udhaifu wake; Bali roho iliyovunjika nani awezaye kuistahimili?


Utangulizi:

Kifungu cha mistari ya msingi kwa ujumla kinazungumzia ulinzi unaopatikana kwa Mungu jinsi ulivyo Muhimu kuliko ulinzi wa matajiri, au moyo  wa mwanadamu ulioharibika au wenye kiburi na majivuno,  Mwenye Hekima hapa anataka kufafanua jambo la muhimu na la msingi kwamba usalama na ulinzi unaopatikana kwa Mungu ni wa msingi sana kuliko ule tunaoufikiria kibinadamu na moyoni mwetu! Na kwa sababu hiyo kulitumainia Jina la Mungu ni kwa Muhimu zaidi ya marafiki, mioyo yetu na kiburi cha kibinadamu! Lakini hakuna mtu anayemtegemea Mungu au jina lake kisha Mungu akamuacha aaibike ona

Yeremia 17:5-9 “Bwana asema hivi, Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, Amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake Na moyoni mwake amemwacha Bwana. Maana atakuwa kama fukara nyikani, Hataona yatakapotokea mema; Bali atakaa jangwani palipo ukame, Katika nchi ya chumvi isiyokaliwa na watu. Amebarikiwa mtu yule anayemtegemea Bwana, Ambaye Bwana ni tumaini lake. Maana atakuwa kama mti uliopandwa kando ya maji, Uenezao mizizi yake karibu na mto; Hautaona hofu wakati wa hari ujapo, Bali jani lake litakuwa bichi; Wala hautahangaika mwaka wa uchache wa mvua, Wala hautaacha kuzaa matunda. Moyo huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote, una ugonjwa wa kufisha; nani awezaye kuujua?

Kwa msingi huo ni wazi kuwa maandiko yanatuasa kuwa kumtumainia Mungu na jina lake ni jambo la msingi na la muhimu sana kuliko kuitegemea Hekima ya kibinadamu au kujivunia mitazamo ya kibinadamu na utajiri wa Dunia hii.

Maana ya Neno Ngome!

Nyakati za Biblia watu walipokuwa wanajenga miji, walihakikisha kuwa miji yao vilevile inazungukwa na kuta kubwa ngumu na imara kwa kusudi la kuhakikisha ulinzi na usalama wa watu wote pamoja na mfalme wa mji ule ili ustawi wa watu uweze kuendelea kuwepo, aidha juu ya kuta hizo askari walikuwa wakizunguka zunguka kufanya matembezi ya kiulinzi na pia kulikuwa na minara mirefu ambayo pia ilikuwa na walinzi waliokaa kwa zamu kwaajili ya kuangalia usalama wa mji na wakati mwingine kutoa taarifa kwa wananchi na serikali kuhusiana na usalama wao, kwa msingi huo uimara wa mji ulitegemea sana na Ngome za miji hiyo zikoje Miji mingi katika nchi ya Kanaani ilikuwa imejengwa kwa ngome imara zisizopenyeka kwa ulaini ambazo pia ziliitwa boma kwa jina lingine  ona

Yoshua 19:35-39 “Na miji yenye boma ilikuwa ni hii, Sidimu, na Seri, na Hamathi, na Rakathi, na Kinerethi; na Adama, na Rama, na Hazori; na Kedeshi, na Edrei, na Enhasori; na Ironi, na Migdal-eli, na Horemu, na Bethanathi, na Bethshemeshi; miji kumi na kenda, pamoja na vijiji vyake. Huu ndio urithi wa kabila ya wana wa Naftali kwa kuandama jamaa zao; miji hiyo pamoja na vijiji vyake.”

Ngome au boma katika miji ilikuwa ni alama kubwa sana ya kuonyesha ulinzi na nguvu kwaajili ya miili, akili, uwezo, utajiri, ushawishi, ulinzi, uadilifu, nguvu, uthabiti, afya, uwezo wa kutokuvamiwa na kuonewa, uhakika, uimara, na uwezo wa kutoa mahitaji ya watu, na usalama,  kwa hiyo kila kitu ambacho kilikuwa kinahifadhiwa na wenye miji yenye boma ndio katika Jina la Mungu navyo vinapatikana endapo kila mwanadamu atalitumainia na kulikimbilia. 

Jina la Bwana ni ngome Imara.

Mfalme Sulemani anaposema Jina la Bwana Ni ngome imara mwenye haki hukimbulia akawa salama ana maanisha nini?  Nyakati za Biblia jina lilikuwa lina maana pana sana kuliko tunavyoweza kufikiri katika siku za leo, jina lilikuwa linatambulisha uwezo na mamlaka ya kila kitu alichokuwa nacho Mtu, au mwenye jina, Jina la bwana ni Ngome imara neno Bwana hapo lilikuwa linasomeka kama YAHWEH na hii ilikuwa inafunua uhalisia na ukweli wote kuhusu sifa zake zote alizokuwa nazo Mungu, kwa hiyo jina lilifunua tabia na sifa alizokuwa nazo, kwa hiyo jila la Mtu lilikuwa linauwezo wa kukupa picha nzima ya anayetajwa katika jina hilo, kwa mfano Mungu alipojifunua kwa Musa kuhusu jina lake alikuwa anamaanisha maswala kadhaa yafuatayo:-

Kutoka 34:5-7 “BWANA akashuka ndani ya lile wingu, akasimama pamoja naye huko, akalitangaza jina la BWANA. BWANA akapita mbele yake, akatangaza, BWANA, BWANA, Mungu mwingi wa huruma, mwenye fadhili, si mwepesi wa hasira, mwingi wa rehema na kweli; mwenye kuwaonea huruma watu elfu elfu, mwenye kusamehe uovu na makosa na dhambi; wala si mwenye kumhesabia mtu mwovu kuwa hana hatia kamwe; mwenye kuwapatiliza watoto uovu wa baba zao, na wana wa wana wao pia, hata kizazi cha tatu na cha nne.”

Jina la Mungu wetu linafunua uwezo wake na mamlaka yake na yale yote ambayo Mungu wetu anaweza kutufadhili kwayo, kwa msingi huo kama Mungu ana uwezo wote ni wazi kuwa jina lake linapita vyote ni jina ambalo liko juu mno kwa uweza na mamlaka na kwa msaada wowote ule

1.       Jina hili lilo juu mno Zaburi 148:11-13 “Wafalme wa dunia, na watu wote, Wakuu, na makadhi wote wa dunia. Vijana waume, na wanawali, Wazee, na watoto; Na walisifu jina la Bwana, Maana jina lake peke yake limetukuka; Adhama yake i juu ya nchi na mbingu.”

 

2.       Jina hili linafunua ya kuwa yeye anamiliki na kuwa hakuna mfalme wala taifa linaloweza kusimama mbele yake kila anayesikia matendo yake anatetetmeka Yoshua 2:9-11 “akawaambia wale wanaume, Mimi najua ya kuwa Bwana amewapa ninyi nchi hii, na ya kuwa hofu imetuangukia mbele yenu, na ya kuwa wenyeji wote wa nchi wanayeyuka mbele yenu. Maana tumesikia jinsi Bwana alivyoyakausha maji ya bahari ya Shamu mbele yenu, hapo mlipotoka Misri, tena mambo hayo mliyowatendea wafalme wawili wa Waamori waliokuwa huko ng'ambo ya Yordani, yaani, Sihoni na Ogu, mliowaangamiza kabisa. Na mara tuliposikia hayo mioyo yetu iliyeyuka, wala haukusalia ujasiri wo wote katika mtu awaye yote, kwa sababu yenu; kwa kuwa Bwana, Mungu wenu, yeye ndiye Mungu, katika mbingu juu na katika nchi chini.”

 

3.       Ni jina ambalo kwalo linaokoa Yoeli 2:32Na itakuwa ya kwamba mtu awaye yote atakayeliita jina la Bwana ataponywa; kwa kuwa katika mlima Sayuni na katika Yerusalemu watakuwako watu watakaookoka, kama Bwana alivyosema; na katika mabaki, hao awaitao Bwana.”       Warumi 10:13 “kwa kuwa, Kila atakayeliitia Jina la Bwana ataokoka.” Matendo 2:21 “Na itakuwa kila atakayeliitia jina la Bwana ataokolewa.”

 

4.       Ni jina ambalo ukilitumia kwenye maombi kuomba lolote utajibiwa ona Yohana 14:12-14 “Amin, amin, nawaambieni, Yeye aniaminiye mimi, kazi nizifanyazo mimi, yeye naye atazifanya; naam, na kubwa kuliko hizo atafanya, kwa kuwa mimi naenda kwa Baba. Nanyi mkiomba lo lote kwa jina langu, hilo nitalifanya, ili Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Mkiniomba neno lo lote kwa jina langu, nitalifanya.

                 

5.       Ni jina lenye uwezo wa kutiisha kila kitu chini yake Wafilipi 2:9-11 “Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina; ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi; na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI BWANA, kwa utukufu wa Mungu Baba.” 

 

6.       Jina hili ni ngome ya kumfanya adui asikupate Zaburi 61:2-3 “Ee Mungu, ukisikie kilio changu, Uyasikilize maombi yangu. Toka mwisho wa nchi nitakulilia nikizimia moyo, Uniongoze juu ya mwamba nisioweza kuupanda. Kwa maana ulikuwa kimbilio langu, Ngome yenye nguvu adui asinipate.”

 

Hitimisho

Kwa msingi huo sasa iwapo unakabiliwa na hali yoyote ya hatari, iwe ya kimwili au kiroho, kiakili au kisaikolojia  na hatari nyingine za aina yoyote maandiko yanatushauri kuwa ni hekima kulikimbilia jina la Bwana kwani jina hilo linatoa usalama, usalama maana yake ni kuwa katika ulinzi, kulindwa na madhara, au kuawa, au kujeruhiwa, au kupotea, na nhatari nyingine yoyote, Jina  la Mungu wetu liko juu ya kila jina maana yake liko juu ya mamlaka zote, ni salama kwa ulinzi, ni salama kwa kulikimbilia ni salama kwa kulitegemea, ni nguvu yetu, ni katika jina hili ndiko kuliko na usalama wa kweli na ulinzi wa uhakika, jina la Bwana ni ngome imara maana yake hatupaswi kuogopa kama tunaumwa, hatupaswi kuchanganyikiwa kama tuna huzuni, hatupaswi kuogopa wakitutisha, hatupaswi kuhofia tuwapo, dhaifu, tunapolemewa na au tunapokuwa na uchumi dhaifu, tunapopatwa na matisho ya aina yoyote ukweli ni kwamba wakati wowote hatuna budi kukumbuka ya kuwa ni jina la Yesu ndilo ngome imara hapo ndipo tunapoweza kukimbilia na kuliitia jina lake kwa msaada tunaouhitaji, Jina lake linawakilisha kila tunachokihitaji, iwe, Upendo, Rehema, Neema, Nguvu, Haki, na zaidi, Watakatifu waliotutangulia walilitegemea na kuliitia wakati wote na Mungu akawasaidia ni hekima kubwa kumkimbilia Mungu, ni ujinga kutegemea wanadamu, na tujiachie katika mikono yake ili tuwe salama kwani hakuna sababu ya kuogopa

Mithali 29:25 “Kuwaogopa wanadamu huleta mtego; Bali amtumainiye Bwana atakuwa salama.”

Na Rev. Innocent Samuel Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima !