Jumatatu, 7 Novemba 2022

Enda ukawapige Amaleki !


1Samuel 15:1-3 “Wakati huo Samweli akamwambia Sauli, Bwana alinipeleka nikutie mafuta, uwe mfalme wa watu wake Israeli; basi sasa, isikilize sauti na maneno ya Bwana. Bwana wa majeshi asema hivi, Nimeyatia moyoni mwangu mambo hayo Amaleki waliyowatenda Israeli, jinsi walivyowapinga njiani, hapo walipopanda kutoka Misri. Basi sasa enda ukawapige Amaleki, na kuviharibu kabisa vitu vyote walivyo navyo, wala msiwaachilie; bali waueni, mwanamume na mwanamke, mtoto naye anyonyaye, ng'ombe na kondoo, ngamia na punda. 



Utangulizi:

Mapema sana miaka mingi Mungu alikuwa amemuahidi rafiki yake Abrahamu kuwa atampa nchi ya mkanaani, lakini alimueleza wazi kuwa atayatimiza haya katika kizazi cha nne wakati huo uovu wa wakanaani utakuwa umefikia kiwango cha juu ona

Mwanzo 15:13-16 “BWANA akamwambia Abramu, Ujue hakika ya kwamba uzao wako utakuwa mgeni katika nchi isiyo yake, watawatumikia watu wale, nao watateswa muda wa miaka mia nne. Hata na taifa lile, watakaowatumikia, nitawahukumu; baadaye watatoka na mali mengi. Lakini wewe utakwenda kwa baba zako kwa amani, utazikwa katika uzee mwema. Na kizazi cha nne kitarudi hapa, maana haujatimia uovu wa Waamori bado.”

Unaona moja ya makabila ambayo uovu wao ulikuwa umefikia kiwango ni pamoja na waamaleki ambao kimsingi Mungu alikasirishwa nao kwa sababu ndio walikuwa wa kwanza kupinga na kusudi la Mungu kwa kupingana ana kusudi la Mungu kwa kutaka kwiazuia wana wa Israel njiani ili wasiweze kwenda katika nchi ya mkanaani ona

Kutoka 17:14 “BWANA akamwambia Musa, Andika habari hii katika kitabu iwe ukumbusho, kisha ihubiri masikioni mwa Yoshua; ya kuwa nitaufuta ukumbusho wa Amaleki kabisa, usiwe tena chini ya mbingu.”

Mungu alikasirishwa na Amaleki na alikusudia kuwafuta wasiwepo milele kwa sababu ya uovu wao na moja ilikuwa ni kuwauzia wana wa Israel wasiende kwa amani katika nchi ya kanaani lakini pili ni kwa kutokuwahurumia watu wanyonge waliokuwa wamechoka jangwani wagonjwa na waliokuwa wamechoka jangwani

Kumbukumbu la Torati 25:17-19 “Kumbuka aliyokufanya Amaleki katika njia mlipokuwa mkitoka Misri; jinsi alivyokukuta katika njia, akapiga katika watu wako walioachwa nyuma, wote waliokuwa wanyonge nyuma yako, ulipokuwa umechoka na kuzimia; wala asimche Mungu.  Basi itakuwa, hapo atakapokwisha kukupumzisha Bwana, Mungu wako, katika adui zako wote walio kando-kando, katika nchi akupayo Bwana, Mungu wako, iwe urithi uimiliki, ndipo uufute ukumbuko wa Amaleki chini ya mbingu; usisahau.”

Kwaajili ya hayo Mungu alikuwa anataka kumbukumbu ya watu hawa wasiofaa iondolewe kabisa milele katika uso wa ardhi na kwa bahati njema agizo hili alipewa mfalme Sauli ambaye kwa bahati mbaya na kwa kukosa utii aliwabakiza kinyume na maagizo ya torati jambo lililolata laana Mungu anapotupa agizo ni lazima yuhakikishe kuwa tunalitimiza kwa usahihi na hatupaswi kuhurumia chochote kinachowekwa mbele yetu maandiko yanasema amelaaniwa mtu yule aifanyaye kazi ya Mungu kwa ulegevu ona

Yeremia 48:10 10. “Na alaaniwe mtu afanyaye kazi ya Bwana kwa ulegevu; na alaaniwe auzuiaye upanga wake usimwage damu.”

Mungu anachokitaka kwetu leo ni kuhakikisha kuwa tunaangamiza kabisa kila kizuizi tunachokutana nacho kisibaki katika kumbukumbu zetu kuwa tuna kitu tumebakiza hakikisha unafutilia mbali kila kikwazo, kinachokukabili, iwe ni mitihani ya kidato cha pili au kidato cha nne au cha sita amaa lolote linalokusibu hakikisha kuwa unatimiza wala usishindwe wala usiuhurumia wala usibakize kama Sauli, leo ni siku yak o na wiki hii ni wiki yako kuhakikisha kuwa unampiga mwamaleki sio kwa ulegevu bali kwa bidii ukijua ya kuwa unamtumikia Mungu,

Warumi 12:11 “kwa bidii, si walegevu; mkiwa na juhudi katika roho zenu; mkimtumikia Bwana;”

Kutokutii agizo la kumtumikia Mungu na kufanya kinyume na maagizo yake kunaweza kutuleta katika wakati mgumu wa kukataliwa kama Sauli na kurfananishwa na waasi au wachawi, Sauli alipoteza nafasi ya kutimiza mapenzi ya Mungu alipofanya vile alivyotaka yeye,

1Samuel 15:7-11 “Sauli akawapiga Waamaleki, toka Havila uendapo Shuri, unaokabili Misri. Akamkamata Agagi, mfalme wa Waamaleki, yu hai, akawaangamiza hao watu wote kwa upanga. Lakini Sauli na watu wake wakamwacha Agagi hai, na katika kondoo walio wazuri, na ng'ombe, na vinono, na wana-kondoo, na cho chote kilicho chema, wala hawakukubali kuwaangamiza; bali cho chote kilichokuwa kibaya na kibovu, ndicho walichokiangamiza kabisa. Ndipo neno la Bwana likamjia Samweli, kusema, Najuta kwa sababu nimemtawaza Sauli awe mfalme; maana amerudi nyuma, asinifuate, wala hakufanya nilivyomwamuru. Samweli akasikitika, akamlilia Bwana usiku kucha.”

Leo hii Mungu anamtuma kila mmoja kwenda kuyatimiza mapenzui yake na kuhakikisha kuwa anaangamiza kila kikwazo kinachozuia mafanikio yake kwa asilimia 100, Na tukifanya hivyo Mungu hatasikitika badala yake atatufurahia kwani tunatimiza mapenzi yake kupiia kila kilichoko moyoni mwake ambacho kimeandikwa katika neno lake weka bidii katika kila ulifanyalo ukijua ya kuwa unayatenda mapenzi ya Mungu, soma kwa bidii, fanya kazi kwa bidii, acha majungu, acha unafiki, acha kuigiza, kila mmoja na amtangulize Mungu mbele na bwana atampa neema kila mmoja wetu na kumfanikisha katika jina la Yesu Amen           

Na Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye hekima.

Hakuna maoni: