Jumapili, 24 Septemba 2017

Rafiki aliye na Msaada!

Mstari wa Msingi: Yohana 15:13 “Hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake

Injli Maalumu kwa Watoto. Waacheni watoto wadogo waje kwangu msiwazuie kwa maana watoto kama hawa Ufalme wa Mungu ni wao!


Sungura mmoja mcheshi sana aliishi msituni, kutokana na ucheshi wake aliweza kujipatia marafiki wengi sana wenye nguvu na maarufu sana aliwapenda na kujivunia sana Marafiki zake

Siku moja sungura Mcheshi alikumbana na kundi la mbwa mwitu wakali ambao walikusudia kumla, Sungura mcheshi aliogopa sana na alikimbilia kwa moja ya marafiki zake kwa kusudi la kutafuta msaada, haraka sana alikimbilia kwa swala dume rafki yake wa karibu na kumwambia tafadhali rafiki yangu mpendwa nisaidie kuna kundi la mbwa mwitu wakali wamekudia kunila nyama, najua unaweza kuwafukuzia mbali kupitia pembe zako ndefu ulizo nazo.

Swala alijibu na kusema ni kweli nina pembe ndefu na ninaweza kuwashambulia mbwa mwitu kwa pembe zangu lakini nina shughuli nyingi sana tafadhali mwambie Dubu akusaidie.

Sungura mcheshi alikimbilia kwa Dubu na kumwambia Tafadhali rafiki wewe una nguvu za kutosha niokoe kutoka kwa mbwa mwitu hawa wakali tafadhali, wafukuze tafadhali alimuomba Dubu

Dubu alimjibu, pole sana rafiki yangu nina njaa na nimechoka sana nahitaji kutafuta namna ya kula tafadhali muombe tumbili akusaidie.

Sungura mcheshi alimuendea tumbili, tembo, na nyati na rafiki zake wengine lakini hakuna aliyemsaidia

Alitambua kuwa anapaswa kutafuta namna ya kujitoa katika tatizo hilo mwenyewe, aliamua kupambana na hali yake na kuliitia jina la Mungu aliyemuumba, na kumwambia ee Mungu wagu je uliniumba ili nije kuwa kitowewo cha wengine duniani? ndipo Mungu akamjibu na akamuelekeza kuchimba shimo na kujificha kimyaa ikawa kila Sungura anapoona hali ya Hatari hukimbilia shini ya shimo lile na kuwa salama na kuokoka, Ndipo mbwa mwitu waliendelea kufukuza wanyama wengine na walimkosa Sungura, aliyekuwa salama chini ya shimo!

Sungura alijifunza kumtegemea aliyemuumba kwaajili ya kutunza uhai wake na sio kuwategemea rafiki zake, sungura alitambua kuwa mwenye uchungu na yeye ni yule aliyemuumba tu!

Yeremia 17:5 “Bwana asema hivi, Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, Amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake Na moyoni mwake amemwacha Bwana. Maana atakuwa kama fukara nyikani, Hataona yatakapotokea mema; Bali atakaa jangwani palipo ukame, Katika nchi ya chumvi isiyokaliwa na watu. Amebarikiwa mtu yule anayemtegemea Bwana, Ambaye Bwana ni tumaini lake. Maana atakuwa kama mti uliopandwa kando ya maji, Uenezao mizizi yake karibu na mto; Hautaona hofu wakati wa hari ujapo, Bali jani lake litakuwa bichi; Wala hautahangaika mwaka wa uchache wa mvua, Wala hautaacha kuzaa matunda.

Tunajifunza: “Kumtegemea Mungu na kumfanya aliyetuumba kuwa rafiki yetu wa Kweli”
Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima

Rev. Innocent Kamote
Yesu kwetu ni rafiki,
Huambiwa haja pia,
Tukiomba kwa Babaye
Maombi asikia,
Lakini twajikosesha,
Twajitweka vibaya,
Kwamba tukimwomba Mungu,
Dua atasikia.

Una dhiki na maonjo?
Una mashaka pia?
Haifai kufa moyo,
Dua atasikia.
Hakuna mwingine mwema
Wa kutuhurumia
Atujua tu dhaifu,
Maombi asikia.

Je, hunazo hata nguvu,
Huwezi kwendelea?
Ujapodharauliwa,
Ujaporushwa pia,
Watu wangekudharau,
Wapendao dunia
Hukwambata mikononi,
Dua atasikia

Hakuna maoni: