Alhamisi, 24 Februari 2022

Katika habari ya Madhehebu hiyo inanenwa vibaya!


Matendo ya Mitume 28:17-22Ikawa baada ya siku tatu akawaita wakuu wa Wayahudi wakutane, hata walipokutanika akawaambia, Ndugu zangu, ningawa sikufanya neno kinyume cha watu wetu wala neno lililopingamana na desturi za baba zetu, nalitiwa katika mikono ya Warumi, hali nimefungwa, tokea Yerusalemu. Na hao walipokwisha kuniuliza-uliza walitaka kunifungua, kwa maana hapakuwa na sababu yo yote kwangu ya kuuawa. Lakini Wayahudi walipotoa hoja juu ya shauri hili nalishurutishwa kutaka rufani kwa Kaisari. Si kwamba nalikuwa na neno la kuwashitaki watu wa taifa langu. Basi kwa ajili ya hayo, nimewaita mje kunitazama na kusema nami; kwa maana nimefungwa kwa mnyororo huu kwa ajili ya tumaini la Israeli. Wale wakamwambia, Sisi hatukupata nyaraka zenye habari zako kutoka Uyahudi, wala hapana ndugu hata mmoja aliyefika hapa na kutupasha habari, au kunena neno baya juu yako. Lakini tunataka kusikia kwako uonavyo wewe; kwa maana katika habari za madhehebu hiyo imejulikana kwetu kwamba inanenwa vibaya kila mahali.”


Utangulizi:

Ni muhimu kufahamu kuwa Paulo mtume alitamani sana Kufika Rumi kwa miaka mingi, Mji wa Rumi ndio ulikuwa makao makuu ya Utawala wa waroma wakati wa ufalme mkubwa wa Kaisari, watu wengi sana waliishi katika mji mkuu wa Rumi, na wayahudi wengi sana, hivyo Paulo alitamani kuwa katika safari zake za injili vilevile aweze kufika Rumi, na alimuomba Mungu ili aweze kufika huko nako, unaweza kuona katika

Warumi 1:9-12Kwa maana Mungu, nimwabuduye kwa roho yangu katika Injili ya Mwana wake, ni shahidi wangu jinsi niwatajavyo pasipo kukoma, siku zote katika sala zangu, nikiomba nije kwenu hivi karibu, Mungu akipenda kuifanikisha safari yangu. Kwa maana ninatamani sana kuwaona, nipate kuwapa karama ya rohoni, ili mfanywe imara; yaani, tufarijiane mimi na ninyi, kila mtu kwa imani ya mwenzake, yenu na yangu.”

Unaweza kuona kwa hiyo kuwa kiu kubwa ya Mtume Paulo ilikuwa siku moja aweze kuonana na wayahudi walioko Rumi ili aweze kuonana nao, iliposhindikana kufika Rumi kwa wakati aliotamani aliwaandikia waraka, Paulo aliamua kuwaandikia waraka huu ili kuweka mafundisho Muhimu sana kuhusu Wokovu na ukombozi wa Bwana wetu Yesu Kristo, lakini vilevile kanisa la Rumi na wayahudi walioko huko na wale walioamini wapate kujua injili aliyokuwa akiihubiri, Rumi ndio ulikuwa mji mkuu wa ulimwengu wa wakati ule na ulikuwa ni mji wenye watu wengi sana wakiwepo wayahudi, Paulo aliutamani mji huu kwa kuwa ulikuwa ni hazina ambayo baadaye ilikuja kutumika kueneza injili ya Kristo Duniani kwa kujua ubora wa mji huu na umuhimu wa huduma ya Paulo Mtume kwa watu wa Rumi, Shetani alijaribu kwa kila hila kuzuia injili kupitia Paulo mtume  na kupingana naye kwa namna na mazingira Magumu sana asifike katika mji wa Rumi na hivyo kulikuwa na mazingira magumu sana 

Matendo 27:1-44 “Tukapanda katika merikebu ya Adramitio iliyokuwa tayari kusafiri mpaka miji ya pwani za Asia, tukatweka; Aristarko, Mmakedonia wa Thesalonike, akiwa pamoja nasi. Siku ya pili tukawasili Sidoni; Yulio akamfadhili sana Paulo akampa ruhusa kwenda kwa rafiki zake, apate kutunzwa. Kutoka huko tukatweka, tukasafiri chini ya Kipro ili kuukinga upepo, kwa maana pepo zilikuwa za mbisho. Tulipopita bahari ya upande wa Kilikia na Pamfilia, tukafika Mira, mji wa Likia. Na huko yule akida akakuta merikebu ya Iskanderia, tayari kusafiri kwenda Italia, akatupandisha humo. Tukasafiri polepole kwa muda wa siku nyingi, tukafika mpaka Nido kwa shida; na kwa sababu upepo ulikuwa ukituzuia tukapita chini ya Krete, tukaikabili Salmone.Tukaipita kwa shida, pwani kwa pwani, tukafika mahali paitwapo Bandari Nzuri. Karibu na hapo pana mji uitwao Lasea. Na wakati mwingi ulipokwisha kupita, na safari ikiwa ina hatari sasa, kwa sababu siku za kufunga zilikuwa zimekwisha kupita, Paulo akawaonya, akawaambia, Wanaume, naona kwamba safari hii itakuwa na madhara na hasara nyingi, si ya shehena na merikebu tu, ila na ya maisha yetu pia. Lakini yule akida akawasikiliza nahodha na mwenye merikebu zaidi ya yale aliyoyasema Paulo.Na kwa sababu bandari ile ilikuwa haifai kukaa wakati wa baridi, wengi wao wakatoa shauri la kutweka kutoka huko ili wapate kufika Foinike, kama ikiwezekana, na kukaa huko wakati wa baridi; nayo ni bandari ya Krete, inaelekea kaskazini-mashariki na kusini-mashariki. Na upepo wa kusi ulipoanza kuvuma kidogo, wakidhani ya kuwa wamepata waliyoazimu kupata, wakang'oa nanga, wakasafiri karibu na Krete pwani kwa pwani. Baada ya muda mchache ukavuma upepo wa nguvu wa namna ya tufani, uitwao Eurakilo, merikebu iliposhikwa, na kutoweza kushindana na upepo, tukaiacha tukachukuliwa. Na tukipita upesi karibu na kisiwa kidogo kiitwacho Kauda tukadiriki kuikweza mashua; lakini kwa shida. Walipokwisha kuikweza wakatumia misaada, wakaikaza merikebu kwa kupitisha kamba chini yake, nao wakiogopa wasije wakakwama katika fungu liitwalo Sirti, wakatua matanga wakachukuliwa vivi hivi. Na kwa maana tulikuwa tukipigwa sana na ile tufani, siku ya pili yake wakaanza kuitupa shehena baharini. Siku ya tatu wakatupa vyombo vya merikebu kwa mikono yao wenyewe. Jua wala nyota hazikuonekana kwa muda wa siku nyingi, na tufani kuu ikatushika, basi tukakata tamaa ya kuokoka. Na walipokuwa wamekaa wakati mwingi bila kula chakula, Paulo akasimama katikati yao, akasema, Wanaume, iliwapasa kunisikiliza mimi na kutokung'oa nanga huko Krete, na kupata madhara haya na hasara hii. Sasa nawapeni shauri, iweni na moyo mkuu, kwa maana hapana hata nafsi mmoja miongoni mwenu atakayepotea, ila merikebu tu. Kwa maana usiku huu wa leo malaika wa Mungu yule ambaye mimi ni wake, naye ndiye nimwabuduye, alisimama karibu nami, akaniambia, Usiogope, Paulo, huna budi kusimama mbele ya Kaisari; tena, tazama, Mungu amekupa watu wote wanaosafiri pamoja nawe. Basi, wanaume, changamkeni; kwa sababu namwamini Mungu, ya kwamba yatakuwa vile vile kama nilivyoambiwa. Lakini hatuna budi kupwelewa katika kisiwa kimoja.  Hata usiku wa kumi na nne ulipofika, tulipokuwa tukichukuliwa huko na huko katika bahari ya Adria, kama usiku wa manane baharia wakadhani ya kuwa wanaikaribia nchi kavu. Wakatupa bildi wakapata pima ishirini, wakaendelea kidogo wakatupa bildi tena, wakapata pima kumi na tano. Wakachelea tusije tukapwelewa mahali penye miamba, wakatupa nanga nne za tezi, wakaomba kuche. Na baharia walipotaka kukimbia na kuiacha merikebu, wakiishusha mashua baharini kana kwamba wanataka kutupa nanga za omo, Paulo akawaambia akida na askari, Hawa wasipokaa ndani ya merikebu hamtaweza kuokoka. Basi askari wakazikata kamba za mashua, wakaiacha ianguke. Na kulipokuwa kukipambauka Paulo akawasihi wote wale chakula, akisema, Leo ni siku ya kumi na nne kungoja na kufunga, hamkula kitu cho chote. Basi nawasihi mle chakula, maana itakuwa kwa wokovu wenu; kwa maana hapana hata unywele wa kichwa cha mmoja wenu utakaopotea. Alipokwisha kusema hayo akatwaa mkate, akamshukuru Mungu mbele yao wote akaumega akaanza kula. Ndipo wakachangamka wote, wakala chakula wenyewe. Na sisi tuliokuwa ndani ya merikebu tulipata watu mia mbili na sabini na sita. Walipokwisha kushiba wakaipunguza shehena ya merikebu, wakiitupa ngano baharini. Kulipokucha hawakuitambua ile nchi, ila waliona hori yenye ufuo, wakashauriana kuiegesha merikebu huko, kama ikiwezekana. Wakazitupilia mbali zile nanga, na kuziacha baharini, pamoja na kuzilegeza kamba za sukani, wakalitweka tanga dogo ili liushike upepo, wakauendea ule ufuo. Lakini wakafikia mahali palipokutana bahari mbili, wakaiegesha merikebu, omo ikakwama ikakaa isitikiswe, bali tezi ilikuwa imefumuliwa kwa nguvu za mawimbi.  Shauri la askari lilikuwa kuwaua wafungwa, mtu asiogelee na kukimbia. Bali akida, akitaka kumponya Paulo, akawazuia, wasifanye kama walivyokusudia, akawaamuru wale wawezao kuogelea wajitupe kwanza baharini, wafike nchi kavu; nao waliosalia, hawa juu ya mbao na hawa juu ya vitu vingine vya merikebu. Na hivyo watu wote wakapata kuifikilia nchi

Hatimaye Paulo mtume alifika katika mji huu wa Rumi akiwa mfungwa lakini vilevile kwa shida kubwa sana wakinusurika kifo kwa njia zote dhoruba njaa na majanga makubwa sana mwishoe Paulo aliingia Rumi akiwa mfungwa wan je katika nyumba mojawapo chini ya ulinzi wa akida aliyeitwa Julius, akiwa katika vifungo vya minyororo. Na ndipo wazee wa kiyahudi walipokuja na kumsalimu lakini wakitaka kujua kwanini dhehebu hili linanenwa vibaya! Tutajifunza somo hili kwa kuzingatia vipengele vikuu viwili vifuatavyo:-

·         Katika habari ya Madhehebu hiyo inanenwa vibaya!

·         Kwa nini Dhehebu hili linanenwa vibaya!

Katika habari ya Madhehebu hiyo inanenwa vibaya!

Kwa bahati njema kama tulivyoona katika utangulizi wazee na viongozi wakuu wa wayahudi waliokaa Rumi walikuja kumtembelea na kumjulia hali, na kukutana naye katika nyumba aliyokuwa amefungwa, Naye aliwaelezea mkasa mzima wa namna alivyo singiziwa maneno ya uongo na jinsi alivyotaka kuuawa na akaamua kuyaokoa maisha yake kwa kukata rufaa kuja Rumi kwa kaisari hata hivyo wazee wa kiyahudi kule Rumi hawakuwa na taarifa yoyote kuhusu kesi yake na kile kilichokuwa kimeendelea juu yake

Matendo 28:17-21 “Ikawa baada ya siku tatu akawaita wakuu wa Wayahudi wakutane, hata walipokutanika akawaambia, Ndugu zangu, ningawa sikufanya neno kinyume cha watu wetu wala neno lililopingamana na desturi za baba zetu, nalitiwa katika mikono ya Warumi, hali nimefungwa, tokea Yerusalemu. Na hao walipokwisha kuniuliza-uliza walitaka kunifungua, kwa maana hapakuwa na sababu yo yote kwangu ya kuuawa. Lakini Wayahudi walipotoa hoja juu ya shauri hili nalishurutishwa kutaka rufani kwa Kaisari. Si kwamba nalikuwa na neno la kuwashitaki watu wa taifa langu. Basi kwa ajili ya hayo, nimewaita mje kunitazama na kusema nami; kwa maana nimefungwa kwa mnyororo huu kwa ajili ya tumaini la Israeli. Wale wakamwambia, Sisi hatukupata nyaraka zenye habari zako kutoka Uyahudi, wala hapana ndugu hata mmoja aliyefika hapa na kutupasha habari, au kunena neno baya juu yako.”

Wazee wa kitahudi pale Rumi hawakuwa na neno lolote kuhusu Paulo Mtume na walikiri kuwa hawakuwahi kupata hata barua kuhusu Paulo mtume zilizotoka uyahudi, na hawa wayahudi waliosafiri kutoka Israel hawakuwahi kmzungumzia Paulo Mtume lakini jambo moja tu walitaka kujua habari ya dhehebu, kitu walichotaka kukisikia kutoka kwa Paulo na kutaka uhakika kutoka kwake ni habari ya dhehebu lake kuwa linanenwa vibaya kila mahali

Matendo 28:22 “Lakini tunataka kusikia kwako uonavyo wewe; kwa maana katika habari za madhehebu hiyo imejulikana kwetu kwamba inanenwa vibaya kila mahali.”

Wazee wa kiyahudi walikuwa wamechoshwa kusikia kuwa kuna mamdhehebu mengi yametokea miongoni mwa wayahudi na yanajulikana kila mahali lakini katika habari ya Madhehebu hii habari imetukfikia kuwa inanenwa vibaya kila mahali, Wazee walimuuliza Paulo mtume swali hili kwa sababu yeye hakuwa maarufu na watu walimchukia kiasi cha kutokutaka kuzungumza habari zake, yeye alikuwa ni mtu aliyechukiwa na Wayahudi wote kila mahali hata huko Asia uturuki ya leo, kila mahali alikokwenda sio yeye tu watu wote waliomuhubiri Kristo walichukiwa na kuuawa wayahudi walifikiri kuwa ukristo unaondoa taratibu zao na desturi zao

Matendo 6:8-14 8. “Na Stefano, akijaa neema na uwezo, alikuwa akifanya maajabu na ishara kubwa katika watu. Lakini baadhi ya watu wa sinagogi lililoitwa sinagogi la Mahuru, na la Wakirene, na la Waiskanderia, na la wale wa Kilikia na Asia, wakaondoka na kujadiliana na Stefano; lakini hawakuweza kushindana na hiyo hekima na huyo Roho aliyesema naye. Hata wakashawishi watu waliosema, Tumemsikia mtu huyu akinena maneno ya kumtukana Musa na Mungu. Wakawataharakisha watu na wazee na waandishi, wakamwendea, wakamkamata, wakampeleka mbele ya baraza. Wakasimamisha mashahidi wa uongo waliosema, Mtu huyu haachi kusema maneno ya kufuru juu ya mahali hapa patakatifu na juu ya torati; maana tumemsikia akisema kwamba Yesu huyo Mnazareti atapaharibu mahali hapa, na kuzibadili desturi tulizopewa na Musa.”

Wayahudi walimuua Stefano kwa sababu alimuhubiri Kristo akiyatumia maandiko kuthibitisha kuwa Yesu ni Masihi, wayahudi walimshitaki Paulomtume pia kuwa ameingiza watu wa mataifa Hekaluni

Matendo 21:27-29 “Basi zile siku saba zilipokuwa karibu kutimia, Wayahudi waliotoka Asia wakamwona ndani ya hekalu, wakawataharakisha watu wote, wakamkamata,wakapiga kelele, na kusema, Enyi wanaume wa Israeli, tusaidieni. Huyu ndiye mtu yule afundishaye watu wote kila mahali kinyume cha taifa letu na torati na mahali hapa. Tena, zaidi ya haya, amewaingiza Wayunani katika hekalu, akapatia unajisi mahali hapa patakatifu. Kwa maana walikuwa wamemwona Trofimo, Mwefeso, pamoja naye mjini, ambaye walidhania ya kuwa Paulo amemwingiza katika hekalu.”          

Pia unaweza kuona kuwa wayahudi kutoma Asia walimfanyia fujo kubwa Paulo mtume kule Thesalonike Wakati Paulo mtume na Sila walipoihubiri injili, wayahudi walijaa wivu kuiona mafanikio ya injili na wakawafuatia kwa ukaribu na kufanya ghasia kubwa sana ona

Matendo 17:1-14 “Wakiisha kupita kati ya Amfipoli na Apolonia wakafika Thesalonike, ambapo palikuwa na sinagogi la Wayahudi. Na Paulo, kama ilivyokuwa desturi yake, akaingia mle walimo, akahojiana nao kwa maneno ya maandiko sabato tatu, akiyafunua na kuwaeleza ya kwamba ilimpasa Kristo kuteswa, na kufufuka katika wafu; na ya kwamba, Yesu huyu ninayewapasha ninyi habari zake ndiye Kristo. Wengine miongoni mwao wakaamini, wakashikamana na Paulo na Sila; na Wayunani waliomcha Mungu, wengi sana, na wanawake wenye cheo si wachache. Na Wayahudi wakaona wivu, wakajitwalia watu kadha wa kadha katika watu ovyo wasio na sifa njema, nao wakakutanisha mkutano, wakafanya ghasia mjini, wakawaendea watu wa nyumba ya Yasoni, wakataka kuwapeleka mbele ya watu wa mji; na walipowakosa, wakamkokota Yasoni na baadhi ya ndugu mbele ya wakubwa wa mji, wakipiga kelele, wakisema, Watu hawa walioupindua ulimwengu wamefika huku nako, na Yasoni amewakaribisha; na hawa wote wanatenda mambo yaliyo kinyume cha amri za Kaisari, wakisema na kwamba yupo mfalme mwingine, aitwaye Yesu. Wakafadhaisha ule mkutano na wakubwa wa mji walipoyasikia hayo. Nao walipokwisha kumtoza dhamana Yasoni na wenziwe wakawaacha waende zao. Mara hao ndugu wakawapeleka Paulo na Sila usiku hata Beroya. Nao walipofika huko wakaingia katika sinagogi la Wayahudi. Watu hawa walikuwa waungwana kuliko wale wa Thesalonike, kwa kuwa walilipokea lile neno kwa uelekevu wa moyo, wakayachunguza maandiko kila siku, waone kwamba mambo hayo ndivyo yalivyo. Basi watu wengi miongoni mwao wakaamini, na wanawake wa Kiyunani wenye cheo, na wanaume si wachache. Lakini Wayahudi wa Thesalonike walipopata habari ya kwamba neno la Mungu linahubiriwa na Paulo hata katika Beroya, wakaenda huko nako wakawachafua na kuwafadhaisha makutano. Mara hiyo wale ndugu wakampeleka Paulo aende zake mpaka pwani; bali Sila na Timotheo wakasalia huko.”         

Ukristo na wahubiri wa kweli hawakuweza kukubalika kirahisi, Paulo mtume na washirika wake walipingwa kila mahali, nyakati za kanisa la kwanza injili haikuwa rahisi, ibilisi aliwatumia wayahudi kuhakikisha kuwa wanafanya fujo na kuharibu kabisa mpango wa Mungu hata kwa kukodi,  watu wasio na sifa njema ili mradi tu kuharibu haklinya hewa, na kuuahribu Ukristo, Wayahudi kutoa sehemu mbalimbali duniani walikuwa wamekwenda Yerusalem mara kadhaa katika siku kuu mbalimbali  na inawezekana walikutana na Wayahudi kutoa Asia ambao waliwatahadharisha kuhusu Ukristo kuwa ni madhehebu yasiyofaa kuna wakati ambapo hata Kaisari aliwafukuza wakristo waondoke Rumi kwa sababu ilifikiriwa kuwa wana imani tofauti mwaka wa 49AD Baada ya Kristo ona

Matendo 18:1-2 “Baada ya mambo hayo, Paulo akatoka Athene akafika Korintho. Akamwona Myahudi mmoja, jina lake Akila, mzalia wa Ponto; naye amekuja kutoka nchi ya Italia siku za karibu, pamoja na Prisila mkewe, kwa sababu Klaudio amewaamuru Wayahudi wote watoke Rumi, naye akafikilia kwao;”

Hata hivyo habari njema ni kuwa Wayahudi wa Rumi na hawakumpokea Paulo kwa fujo na hivyo walimsikiliza na hawakumshutumu kwa lolote lakini walitaka kusikia kutoka kwake, kuwa hawa watu wayahudi wanaomuhubiri Yesu kuwa ni masihi awathibitishie maana kila mahali hawa wanaomuhubiri Kristo kwa dhati wananenwa vibaya kila mahali hu ni uzushi au ni ukweli, huyu Masihi mnayemuhubiri ni kweli au ni uzushi? Hivyo walitaka kusikia Kutoka kwa Paulo Mtume kwamba hiki sasa ndio chanzo cha ukweli wa habari zote ambazo tumekuwa tukizisikia tunataka kusikia kutoka kwako hii ikoje katika habari ya madhehebu hii inanenwa vibaya

Kwa nini Dhehebu hili linanenwa vibaya!

1.       Walimuhubiri Christo.

 

Kristo Yesu, mateso yake kufa kwake na kufufuka kwake ilikuwa ndio kiini kiku cha ujumbe wa wahubiri wa nyakati za kanisa la kwanza, Nyakati za kanisa la kwanza wahubiri waliwaelekeza watu kwa Yesu, wakliwathibitishia wayahudi kwa wayunani kuwa Kristo ni Bwana, mahubiri yenye nguvu kupita yote ni yale ambayo kiini cha ujumbe wake ni Yesu, waelekeze watu kwa Yesu, sio dhebu lako, sio kwa mchungaji wako, waimarishe watu wasimame imara katika imani wakimtegemea Yesu, Paulo mtume na timu yake ya umisheni na uinjilisti hawakupeleka khadithi kwa watu walipeleka neno la Mungu, hawakupeleka hekima za wanadamu, walilihubiri neno lililothibitishwa kwa ishara na miujiza ya jina la Yesu  jambo hili liliwafanya kunenwa vibaya kila mahali. Ona;-

 

1Wakoritho 1:22-24 “Kwa sababu Wayahudi wanataka ishara, na Wayunani wanatafuta HEKIMA; BALI SISI TUNAMHUBIRI KRISTO, ALIYESULIBIWA; kwa Wayahudi ni kikwazo, na kwa Wayunani ni upuzi; bali kwao waitwao, Wayahudi kwa Wayunani, ni Kristo, nguvu ya Mungu, na hekima ya Mungu

 

Dhehebu au mtu awaye yote anayemuhubiri Kristo hawezi kufurahiwa, shetani hawezi kufurahi watu wamuhubiri Kristo shetani anataka mahubiri ya aina nyingine anataka watu wahubiri uponyaji na wa mwilini ambao ni wa kitambo na  mafanikio ya mwilini ambayo pia ni ya kitambo, lakini ile injili ya kweli ya kuwaelekeza watu kwa Yesu, na kubadilisha desturi za watu waache tabia mbaya, waishi maisha matakatifu, waache uchawi, waache ushirikina, wabadilike biashara ya uaguzi iharibike kamwe shetani haitaki injili ya aina hiyo wala hawezi kuikubali, unapomuhubiri Kirsto Kuzimu hakuwezi kufurahia na ndio maana nyakati za Kanisa la kwanza waliigundua siri kwamba nguvu ya kweli iko katika kumuhubiri Kristo, hivyo kila Muhubiri wa nyakati za kanisa la kwanza alipohubiri Kristo ndio ilikuwa kiini cha somo lake  na matokeo yalikuwa makubwa sana nay a kushangaza ona

 

Matendo 5:42 “Na kila siku, ndani ya hekalu na nyumbani mwao, hawakuacha kufundisha na kuhubiri habari njema za YESU KWAMBA NI KRISTO.”

 

Matendo 8:4-5 “Lakini wale waliotawanyika wakaenda huko na huko wakilihubiri neno. Filipo akatelemka akaingia mji wa Samaria, AKAWAHUBIRI KRISTO.”         

 

Matendo 4:18-20 “Wakawaita, wakawaamuru wasiseme kabisa wala kufundisha KWA JINA LA YESU. Petro na Yohana wakawajibu wakawaambia, Kwamba ni haki mbele za Mungu kuwasikiliza ninyi kuliko Mungu, hukumuni ninyi wenyewe; maana sisi hatuwezi kuacha kuyanena mambo tuliyoyaona na kuyasikia.”

 

Mahali popote au dhehebu lolote au taasisi yoyote ambapo Yesu anatajwa na kuelezewa vema, shetani hawezi kukubali mahali hapo panenwe vizuri, Jina la Yesu lina nguvu uwezo na mamlaka ya kuokoa na kuwaelimisha watu na kuwastaarabisha na kuwaponya na kuwaleta katika kiwango kikinge, kwa sababu hiyo kila mahali ambapo Kirtso anahubiriwa kwa dhati mahali hapo hapawezi kunenwa vema! Wapanene vema kwa lipi ilihali biashara zao zinaharibiwa, biashara ya tabia mbaya na ukahaba, na wizi, na ulevi na mapinduzi makubwa yanatokea watafurahishwa vipi, ni kwaajili ya haya katika habari ya madhehebu hiyo inanenwa vema!

 

2.       Walikazia kuwa viwango visivyo vya ulimwengu huu.

 

Kanisa au dhehebu tamu ni lile ambalo wahubiri wake wanakazia viwango, wanawaelekeza watu kuishi kwa viwango vya juu zaidi vya kibiblia, hawalichuji neno la Mungu wala kulighoshi wanakaza, injili za kina Paulo mtume zilikaza wazi wazi wala msiifuatishe namna ya dunia hii ona

Warumi 12:2 “Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.”

 

Watu au wakristo wanaoishi kwa viwango vya juu anavyovitaka Kristo na wahubiri wakikazia viwango anacvyovotaka Kristo shetani hawezi kufurahia, dunia haiwezi kukuinena vema, utasikia wanajifanya watakatifu sana sio wanajifanya maandiko yanatuita sisi ni watakatifu, hatupaswi kuishi chini ya kiwango  sisi sio wa ulimwengu huu na hivyo usufikiri kuwa dunia itakukubali, ikukubali kwa lipi, ikuunge mkono kwa lipi lazima unenwe vibaya

 

Yohana 15:18 -19 “Iwapo ulimwengu ukiwachukia, mwajua ya kuwa umenichukia mimi kabla ya kuwachukia ninyi. Kama mngekuwa wa ulimwengu, ulimwengu ungewapenda walio wake; lakini kwa kuwa ninyi si wa ulimwengu, bali mimi naliwachagua katika ulimwengu, kwa sababu hiyo ulimwengu huwachukia.”

Sisi tumechaguliwa na Yesu, na sisi sio wa ulimwengu huu, hatuwezi kukubaliwa na ulimwengu, Mkristowa kweli ukiona unakubalika tu kila mahali lazima ujihoji, sisi sio wa kawaida Yesu ametuambia lazima ulimwengu utuchukie na kama utatuchukia utatunena vizuri kwa lipi ? sisi ni ukuhani mteule, taifa takatifu watu wa miliki ya Mungu, tumeitwa kutoka gizani sisi ni nuru giza hakliwezi kuwa na furaha na sisi hata kidogo, hivyo kama wanasengenya wasengenye sana, kama wanaroga waroge sana, kama wanakosoa wakosoe sana katika habari ya madhehebu hii inanenwa vibaya hii

 

1Petro 2:9 -10 “Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu; ninyi mliokuwa kwanza si taifa, bali sasa ni taifa la Mungu; mliokuwa hamkupata rehema, bali sasa mmepata rehema.”

 

Unaona kumbe kama dhehebu au kanisa au wahubiri na waamini wataishi maisha ya kiwango kile Mungu alichotuitia ulimwengu hauwezi kufurahia hata kidogo, watufurahie kwa lipi kama hatuna urafiki na dunia

 

Yakobo 4:4 “Enyi wazinzi, hamjui ya kwamba kuwa rafiki wa dunia ni kuwa adui wa Mungu? Basi kila atakaye kuwa rafiki wa dunia hujifanya kuwa adui wa Mungu.”            

 

Unaona nyakati za kanisa la kwanza watu walikuwa serious hawakuwa na mchezo walivunja urafiki na dunia, hawakuwa na mahusiano ya kijinga na watu wasioamini, unadhani dunia ingewakubalije, unadhani wangesifiwa unadhani wangenenwa vema?

 

2Wakoritho 6:14-18 “Msifungiwe nira pamoja na wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa; kwa maana pana urafiki gani kati ya haki na uasi? Tena pana shirika gani kati ya nuru na giza? Tena pana ulinganifu gani kati ya Kristo na Beliari? Au yeye aaminiye ana sehemu gani pamoja na yeye asiyeamini? Tena pana mapatano gani kati ya hekalu la Mungu na sanamu? Kwa maana sisi tu hekalu la Mungu aliye hai; kama Mungu alivyosema, ya kwamba, Nitakaa ndani yao, na kati yao nitatembea, nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu. Kwa hiyo, Tokeni kati yao, Mkatengwe nao, asema Bwana, Msiguse kitu kilicho kichafu, Nami nitawakaribisha. Nitakuwa Baba kwenu, Nanyi mtakuwa kwangu wanangu wa kiume na wa kike

Yesu alieleza wazi kuwa kwa kumfuata yeye na kumuamini hali haiwezi kuwa nzuri kwa dunia lazima watatuchukia, watatutesa, watatuua, na tunaweza kuchukiwa na mataifa yote kwaajili ya Kristo,

 

Mathayo 24:9 “Wakati huo watawasaliti ninyi mpate dhiki, nao watawaua; nanyi mtakuwa watu wa kuchukiwa na mataifa yote kwa ajili ya jina langu.”

Moyo wangu unalibeba jina la Yesu unamuamini Yesu, nimejitenga na dunia, nimevunja urafiki na watu waovu, naishi maisha ya mfano nakazaia utakatifu naonyesha namna tunavyotakiwa kuvaa kwa nidhamu, naonyesha namna inavyotupasa kuabudu kumuheshimu Mungu naelekeza watu kwa Yesu, naishi maisha ya kiwango kisha unatarajia dunia inipende inipende kwa lipi?  Katika habari ya madhehebu hii imejulikana kwetu kuwa inanenwa vibaya kila mahali!

 

3.       Waliihubiri kweli!

 

Wanadamu huwa wanachukia ukweli, watu wengi hawapendi kuambiwa ukweli, ukitaka kuchukiwa wewe uwe tu msema kweli, utaona, watu wana mambo yao na wanataka wasiambiwe, ukiwaambia tu tayari unakosana nao kwa sababu watu wanapenda uongo na wanataka kudanganywa na ndio maana utaina imani za ajabu ajabu zenye usanii mwingi zinakubalika na kujaza watu wengi, wewe nyoosha maelezo utaona kimsingi tunapomuhubiri Yesu tunahubiri ukweli yeye ndio njia na kweli na uzima Yohana 14:6 “Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.” Tunapolihubiri neno la Mungu na kulitumia kwa halali tunaihubiri kweli Yohana 17:17 “Uwatakase kwa ile kweli; neno lako ndiyo kweli.” Kwa msingi huo unapotaka kuwa na uadui na watu na ukitaka watu wakuchukie wewe uwe msema kweli, moja ya sababu ya Ndugu zake Yusufu kumchukia na hata kutaka kumuua ukiacha ndoto zake ni kwa sababu Yusufu alikuwa mkweli alipopeleka ripoti ya mambo yao kwa baba yake aliipeleka kama ilivyo

Mwanzo 37:2-4 “Hivi ndivyo vizazi vya Yakobo. Yusufu, aliyekuwa mwenye miaka kumi na saba, alikuwa akichunga kondoo pamoja na ndugu zake; naye alikuwa kijana pamoja na wana wa Bilha, na wana wa Zilpa, wake wa baba yake. Yusufu akamletea baba yao habari zao mbaya. Basi Israeli akampenda Yusufu kuliko wanawe wote, maana ni mwana wa uzee wake, akamfanyia kanzu ndefu. Ndugu zake wakaona ya kuwa baba yao anampenda kuliko ndugu zake wote, wakamchukia, wala hawakuweza kusema naye kwa amani.”

Nyakati za Kanisa la kwanza wahubiri hawakuwapaka watu mafuta kwa mgongo wa chupa walipeleka injili kavukavu na ukweli wake wote bila kuichuja jambo hili liliwafanya waonekane kuwa maadui ona Wagalatia 4:16 “Je! Nimekuwa adui wenu kwa sababu nawaambia yaliyo kweli?   watu katika ulimwengu huu wana mambo yao na yana faida klatika akili zao na hivyo sio rahisi kukubali mabadiliko anapotokea mtu kuwaambia ukweli wanachukia, dunia ya leo inahitaji kuhubiriwa kweli, mitume walihubniri ukweli, manabii walisema ukweli, wengine waliuawa kwa sababu ya kusema ukweli madhahebu haya yalinenwa vibaya kila mahali kwa sababu watu hawataki kuambiwa ukweli ona

 

Warumi 1:16-22 “Kwa maana siionei haya Injili; kwa sababu ni uweza wa Mungu uuletao wokovu, kwa kila aaminiye, kwa Myahudi kwanza, na kwa Myunani pia. Kwa maana haki ya Mungu inadhihirishwa ndani yake, toka imani hata imani; kama ilivyoandikwa, Mwenye haki ataishi kwa imani. Kwa maana ghadhabu ya Mungu imedhihirishwa kutoka mbinguni juu ya uasi wote na uovu wa wanadamu waipingao kweli kwa uovu. Kwa kuwa mambo ya Mungu yanayojulikana yamekuwa dhahiri ndani yao, kwa maana Mungu aliwadhihirishia. Kwa sababu mambo yake yasiyoonekana tangu kuumbwa ulimwengu yanaonekana, na kufahamika kwa kazi zake; yaani, uweza wake wa milele na Uungu wake; hata wasiwe na udhuru; kwa sababu, walipomjua Mungu hawakumtukuza kama ndiye Mungu wala kumshukuru; bali walipotea katika uzushi wao, na mioyo yao yenye ujinga ikatiwa giza. Wakijinena kuwa wenye hekima walipumbazika;” Pale stefano alipowaambia watu ukweli walimsagia meno na wakamuua kwanini basi dhehebu linalohubiri kweli lisinenwe vibaya kila mahali.

 

4.        Shetani amepofusha fikra zao:

 

Kuna mambo mengi sana yanayowafanya watu wawe vipofu wa kiroho, wakati mwingine shetani, wakati mwingine kiburi, wakati mwingine ujinga, wakati mwingine kupuuzia, wakati mwingine kuongozwa na viongozi vipofu, wakati mwingine kufuata mkumbo, wakati mwingine kurithi na kadhalika, au kwa kuifuata kawaida ya ulimwengu huu,  unapkuwa kipofu kwa sababu yoyote ile kati ya hizo huwezi kuona Yesu katika ubora wake kwa sababu maarifa yako na ujuzi wako unapigwa upofu ili usihifahamu kweli ambayo inatabia ya kukuweka huru

 

Yohana 8:31-32 “Basi Yesu akawaambia wale Wayahudi waliomwamini, Ninyi mkikaa katika neno langu, mmekuwa wanafunzi wangu kweli kweli; tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru.” Kazi mojawapo kubwa anayoifanya shetani pamoja na nyenzo zake nyingine ni kupofusha fikra na hivyo kuwafanya watu wawe wagumu na wawe vipofu ili wasimjue Yesu na nuru ya injili isiwazukie

 

2Wakoritho 4:3-4 “Lakini ikiwa injili yetu imesitirika, imesitirika kwa hao wanaopotea; ambao ndani yao mungu wa dunia hii AMEPOFUSHA FIKIRA ZAO wasioamini, isiwazukie nuru ya injili ya utukufu wake Kristo aliye sura yake Mungu.”  Unaona watu ambao fikra zao zimepofushwa na ibilisi hawawezi kuona utamu wa injili ya Bwana Yesu wao wataipinga tu wao ni vipofu hawawezi kuona ni watu wa dunia hii wanafuata kawaida ya ulimwengu huu wako chini ya mkuu wa anga hili ambaye anatenda kazi kwa wana wa kuasi waefeso 2:1-2 “Nanyi mlikuwa wafu kwa sababu ya makosa na dhambi zenu; ambazo mliziendea zamani kwa kuifuata kawaida ya ulimwengu huu, na kwa kumfuata mfalme wa uwezo wa anga, roho yule atendaye kazi sasa katika wana wa kuasi;” unaona kwa msingi huo hawawezi kamwe kuisifia kazi ya injili na badala yake itanenwa vibaya kila mahali, wengine kwa sababu ya kiburi na wengine kwa sababu ya kukaa chini ya viongozi wasioifahamu kweli na kupata mafundisho potofu Mathayo 15:14 “Waacheni; hao ni viongozi vipofu wa vipofu. Na kipofu akimwongoza kipofu mwenzake, watatumbukia shimoni wote wawili.” Kwa msingi huo wakati mwingine sio rahisi mtu wa kawaida kujua maswala haya ya muhimu ya kiroho ni kwaajili ya haya utaweza kuona katika habari ya madhehebu hii inanenwa vibaya kila mahali.

 

5.       Kwa sababu ya tabia ya mwilini                .

 

Kristo Yesu amekuja kuwakomboa watu kwa jinsi ya Rohoni, ukiisha kusamehewa dhambi pia unaponywa kwa msingi huo asili ya ukombozi wetu inaanzia rohoni, neno linapohubiriwa ni mpaka mtu wa rohoni asikie ndipo na wa kawaida anaweza kuelewa kwa msingi huo mtu wa mwilini hawezi kuyatambua mambo ya Roho wa Mungu

 

1Wakoritho 2:13-15 “Nayo twayanena, si kwa maneno yanayofundishwa kwa hekima ya kibinadamu, bali yanayofundishwa na Roho, tukiyafasiri mambo ya rohoni kwa maneno ya rohoni. Basi mwanadamu wa tabia ya asili hayapokei mambo ya Roho wa Mungu; maana kwake huyo ni upuzi, wala hawezi kuyafahamu, kwa kuwa yatambulikana kwa jinsi ya rohoni. Lakini mtu wa rohoni huyatambua yote, wala yeye hatambuliwi na mtu.”

 

Injili ni swala la kiroho, hivyo uwezo wa kufasiri maswala ya rohoni unamuhitaji Mungu ambaye ni Roho unahitaji msaada wa Roho Mtakatifu, ni vigumu kwa ulimwengu kuitambua haya nan i vigumu kwa watu wa mwilini kuyatambua haya, ulimwengu haujui kuwa Mungu Roho Mtakatifu yupo, haujui kuwa Roho Mtakatifu yuko kazini, haujui kuwa yeye ni roho wa kweli, na hawawezi kumpokea maana hawamuoni 

 

Yohana 14:16-20 “Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine, ili akae nanyi hata milele; ndiye Roho wa kweli; ambaye ulimwengu hauwezi kumpokea, kwa kuwa haumwoni wala haumtambui; bali ninyi mnamtambua, maana anakaa kwenu, naye atakuwa ndani yenu. Sitawaacha ninyi yatima; naja kwenu. Bado kitambo kidogo na ulimwengu haunioni tena; bali ninyi mnaniona. Na kwa sababu mimi ni hai, ninyi nanyi mtakuwa hai. Siku ile ninyi mtatambua ya kuwa mimi ni ndani ya Baba yangu, nanyi ndani yangu, nami ndani yenu.”

 

Kuifahamu injili, na kumfahamu Yesu kristo hakuji kwa akili za kibinadamu ni hekima inayotoka kwa Mungu hivyo wanadamu wa kawaida huona kuwa ni ujinga na upuuzi swala zima la injili na kwa sababu hiyo hawawezi kuzungumza jema kuhusu Ukristo sahihi

 

1Wakoritho 1:18-20 “     Kwa sababu neno la msalaba kwao wanaopotea ni upuzi, bali kwetu sisi tunaookolewa ni nguvu ya Mungu. Kwa kuwa imeandikwa, Nitaiharibu hekima yao wenye hekima, Na akili zao wenye akili nitazikataa. Yu wapi mwenye hekima? Yu wapi mwandishi? Yu wapi mlete hoja wa zamani hizi? Je! Mungu hakuifanya hekima ya dunia kuwa ni upumbavu?

 

6.       Dunia inamchukia Mungu

 

Kwa kawaida dunia iko kinyume na Mungu na inamchukia Mungu, Nyakati za kanisa la kwanza waliwaelekeza watu kwa Mungu na kulitangaza jina la Mungu, Dunia haimtaki Yesu na inamchukia Yesu na inachukia jina lake nyakati za kanisa la kwanza walimtangaza Yesu na walitii agizo lake la kuipeleka injili, Yesu alikwisha kuonya kuwa wale waifanyao kazi hiyo kwa dhati na kwa moyo watachukiwa udhihirisho wa chuki hiyo ni pamoja na kunenwa vibaya Mathayo 10:22 “Nanyi mtakuwa mkichukiwa na watu wote kwa ajili ya jina langu; lakini mwenye kuvumilia hata mwisho, ndiye atakayeokoka,” unaona ni wazi kuwa Yesu alijua kuwa wanafunzi wake wa kweli watachukiwa  na watachukiwa kwaajili ya jina lake ni wazi kabisa kuwa Yesu anajua kuwa kwa chuki hizo watu hawawezi kulinenea vizuri kanisa la kweli nah ii ni kwa sababu ulimwengu unamchukia Mungu na hivyo sio ajabu kuchukia mali yake

 

Yohana 15:18 -19 “Iwapo ulimwengu ukiwachukia, mwajua ya kuwa umenichukia mimi kabla ya kuwachukia ninyi. Kama mngekuwa wa ulimwengu, ulimwengu ungewapenda walio wake; lakini kwa kuwa ninyi si wa ulimwengu, bali mimi naliwachagua katika ulimwengu, kwa sababu hiyo ulimwengu huwachukia                 

 

Maandiko yako wazi kuwa watu wa ulimwengu huu ni waovu, wenye tama, wenye chuki, wenye wivu, wauaji, wagomvi, wadanganyifu, matapeli, wachawi, wasengenyaji, wambeya, wenye kumchukia Mungu, wenye kiburi na majivuno, wenye kujisifu, wasiotii wazazi wao, wenye nia mbaya wenye ujuzi wa kutenda maovu kuliko mema, wenye kuvunja mapatano, wasio na huruma wenye mioyo mibovu wasiotii wazazi unategemea watu kama hawa watalipenda kanisa ambalo liko kinyume na  njia zao, linakemea uovu na kuonyesha njia ya haki sio rahisi

 

Warumi 1:28-30 “Na kama walivyokataa kuwa na Mungu katika fahamu zao, Mungu aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa, wayafanye yasiyowapasa. Wamejawa na udhalimu wa kila namna, uovu na tamaa na ubaya; wamejawa na husuda, na uuaji, na fitina, na hadaa; watu wa nia mbaya, wenye kusengenya,wenye kusingizia, wenye kumchukia Mungu, wenye jeuri, wenye kutakabari, wenye majivuno, wenye kutunga mabaya, wasiowatii wazazi wao, wasio na ufahamu, wenye kuvunja maagano, wasiopenda jamaa zao, wasio na rehema; ambao wakijua sana hukumu ya haki ya Mungu, ya kwamba wayatendao hayo wamestahili mauti, wanatenda hayo, wala si hivyo tu, bali wanakubaliana nao wayatendao  na maandiko yanaonyesha wazi kuwa pia huenda  wako watu wengi wanaomchukia Mungu pasipo sababuna pia wanaowachukia watu wa Mungu pasipo sababu ni wengi Daudi alichukiwa pasipo sababu alikuwa na maadui wengi ijapokuwa hakuwa mtenda maovu ona  Zaburi 69:4 “Wanaonichukia bure ni wengi Kuliko nywele za kichwa changu. Watakao kunikatilia mbali wamekuwa hodari, Adui zangu kwa sababu isiyo kweli. Hata mimi nalilipishwa kwa nguvu Vitu nisivyovichukua”. Dunia inamchukia Mungu na neno lake kwa sababu linawashuhudia kuwa ni waovu Yohana 7:7 “Ulimwengu hauwezi kuwachukia ninyi; bali hunichukia mimi, kwa sababu mimi naushuhudia ya kuwa kazi zake ni mbovuunaona kanisa la kwanza hawakukubali kukalia kimya uovu waliukemea waliushuhudia kuwa haukuwa sahihi waliwaonyesha njia, hali kadhalika kazi hii ndio aliyoifanya Yesu alikema unafiki wa kidini, alionya na kuelekeza ibada sahihi na namna sahihi ya kumuabudu Mungu je unatarajia kama kanisa au dhebu litayatenda haya au mimi na wewe tutayafanya haya je tutanenwa vizuri kila mahali? Katika habari ya madhehebu hiyo imejulikana kwetu kuwa inanenwa vibaya.

 

7.       Kumfuata Yesu sio rahisi.

Nyakati za kanisa la kwanza mafundishi kuhusu dhiki nha udhia yalikuwa ni mojawapo ya nguzio muhimu sana ya Ukristo, wakristio waliteseka kwa namna na kwa njia mbali mbali ilikuwa kama kuchagua injili ni kuchagua njia ya mateso na mitume waliweka wazi hili kama msingi wa mafundisho yao na ya Kristo

 

Matendo 14:21-22 “Hata walipokwisha kuihubiri Injili katika mji ule, na kupata wanafunzi wengi, wakarejea mpaka Listra na Ikonio na Antiokia, wakifanya imara roho za wanafunzi na kuwaonya wakae katika ile Imani, na ya kwamba imetupasa kuingia katika ufalme wa Mungu kwa njia ya dhiki nyingi.”

 

1Petro 1:6 -7 “Mnafurahi sana wakati huo, ijapokuwa sasa kwa kitambo kidogo, ikiwa ni lazima, mmehuzunishwa kwa majaribu ya namna mbalimbali; ili kwamba kujaribiwa kwa imani yenu, ambayo ina thamani kuu kuliko dhahabu ipoteayo, ijapokuwa hiyo hujaribiwa kwa moto, kuonekane kuwa kwenye sifa na utukufu na heshima, katika kufunuliwa kwake Yesu Kristo”.

 

Unaona tangu mwanzo Yesu alikuwa amekwisha kuonya kuwa kufuata yeye sio lele mama nyakati za leo injili zilizojaa mitaani ni za mafanikio na vitu vya duniani, injili za nyakati zetu  mkazo ulikuwa ni huu hapa IMETUPASA KUINGIA KATIKA UFALME WA MUNGU KWA NJIA YA DHIKI NYINGI, injili  za leo ni kutesa duiniani na mbinguni ahaaaa tunapoteza muelekeo sio kuwa naunga mkono mateso hakuna mtu anapenda mateso lakini sisi ambao tumepata rata commitment zetu ni tofauti sana na zile wanazopata watu wanaopitia shida kwa ukweli Yesu hakuonyesha kuwa kazi ya injili ni lele,mama Luka 14:26-27 “Kama mtu akija kwangu naye hamchukii baba yake, na mama yake, na mke wake, na wanawe, na ndugu zake waume na wake; naam, na hata nafsi yake mwenyewe, hawezi kuwa mwanafunzi wangu. Mtu ye yote asiyeuchukua msalaba wake na kuja nyuma yangu, hawezi kuwa mwanafunzi wangu”.  Lakini watu wengi sana leo wanajihurumia na wanapoutazama Ukristo wa kweli na kuona msimamo wa aina hii ni wazi kabisa kuwa hawawezi kuzungumza mazuri kwa kuona watu ambao wana misimamo mikali na wanasonga mbele bila kujali kuwa wanapitia changamoto gani watu ambao wako tayari kuzipoteza nafsi zao kuliko kuziokoa Mathayo 16:24-26 “Wakati huo Yesu aliwaambia wanafunzi wake, Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake, anifuate. Kwa kuwa mtu atakaye kuiokoa nafsi yake, ataipoteza; na mtu atakayepoteza nafsi yake kwa ajili yangu, ataiona. Kwani atafaidiwa nini mtu akiupata ulimwengu wote, na kupata hasara ya nafsi yake? Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake?   

 

Misimamo hii na misingi hii ndio ilikuwa misimamo ya Paulo mtuma na ilikuwa ni misimamo ya injili waliyoihubiri na ilikuwa misimamo ya kanisa la nyakati za kanisa la kwanza ni kwaajili ya haya watu wa ulimwengu ule walichukizwa na misimamo yao na kuona kuwa watu hawa wanaupindua ulimwengu na kubadili desturi za kilimwengu na kuuleta umayi kwa Yesu hivyo shetani alitumia silaya ya kuinena vibaya lakini wazee wa kirumi waliomfuata Paulo wao walikuwa waungwana na wenye hekima hawakutaka kusikia tu walimuuliza Paulo mtume mwenyewe wakitaka kusikia kutoka kwake kwanini katika habari ya madhehebu hii inannenwa vibaya ?

 

Bwana atupe neema kanisa la leo ili tusinenwe vibaya kwa ubaya badala yake tunanene vibaya kwa sababu ya viwango vya kujitoa kwetu kwa Mungu kuwa vya hakli ya njuu kiasi cha kuuchanganya ulimwengu, ni maombi yangu kuwa tutasimama imara na kuendelea kuipeleka injili mpaka Yesu afurahi barikiwa!

 

Na mkuu wa wajenzi mwenye Hekima

Rev. Innocent Kamote



Hakuna maoni: