Jumanne, 5 Februari 2019

“Ukialikwa na mtu Harusini ! ”

Mstari wa Msingi: Luka 14:7-11
 
Akawaambia mfano wale walioalikwa, alipoona jinsi walivyochagua viti vya mbele; akisema, Ukialikwa na mtu arusini, usiketi katika kiti cha mbele; isiwe kwamba amealikwa mtu mwenye kustahiwa kuliko wewe, akaja yule aliyewaalika wewe na yeye, na kukuambia, Mpishe huyu! Ndipo utakapoanza kwa haya (AIBU) kushika mahali pa nyuma. Bali ukialikwa, nenda ukaketi mahali pa nyuma, ili ajapo yule aliyekualika akuambie, Rafiki yangu, njoo huku mbele zaidi; ndipo utakapokuwa na utukufu mbele ya wote walioketi pamoja nawe.  Kwa maana kila ajikwezaye atadhiliwa, naye ajidhiliye atakwezwa.”



Utangulizi:

Maandiko matakatifu yanatufundisha namna bora ya kuishi katika ulimwengu huu, na kupata mafanikio, moja ya njia iliyo bora zaidi ya kuishi maisha ya furaha na amani ni pamoja na kuishi maisha ya unyenyekevu, pamoja na kuwaheshimu watu wengine au watu wote, Maandiko yanasema katika.

 Wafilipi 2:3Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake.

Yesu Kristo katika kufundisha kwake alipenda sana kutumia mifano ya aina mbalimbali kwaajili ya kufundisha watu kuhusu ufalme wa Mungu, na ili watu waweze kuelewa alitumia story pamoja na matukio mbalimbali halisi yaliyotokea kuwafundisha watu maisha na ufahamu kuhusu utendaji wa Mungu na tabia zake ili waweze kuishi kwa amani, Ingawa Yesu alitumia mifano lakini mifano hii ilibeba maana kubwa sana na za kweli kuhusu maisha.

Katika kifungu cha Maandiko tunayosoma leo, Katika Luka 14, Yesu alikuwa amealikwa katika chakula cha jioni na moja ya maafisa wakubwa sana wa Mafarisayo, Watu wengine wengi sana walikuwepo au walialikwa pia, kulikuwa na watu muhimu wengi sana wastahiki na pia watu wengine wengi waliokuwa na nyadhifa mbalimbali  na wale ambao bila shaka walijifikiri kuwa ni wa muhimu sana, walipokuwa wakiingia Yesu alikuwa akifuatilia kila kilichokuwa kinaendelea, wengi walikwenda kukaa moja kwa moja kwenye viti maalumu vya Meza kuu, hatujui nini kilitokea lakini Yesu alipata somo la kuwafundisha wanafunzi wake,  kwa kile kilichotokea kwani tunaweza kukiona japokuwa mwandishi hakukigusia wazi inawezekana wengi walikwenda kukaa mahali ambapo huenda hapakuwa pameandaliwa kwa ajili yao  na hivyo haikuwa sahihi kwao kukaa, na inawezekana baadaye walihamisha na kupelekwa katika viti vya kawaida na hawakujisikia vizuri, (Zamani hakukuwa na utaratibu wa kuweka majina mezani, Lakini aliyepanga viti na meza yaani mwenyeji ndiye aliyekuwa na jibu moyoni kuwa nani anastahili kukaa wapi). Yesu anatumia tukio hili kutufundisha jinsi njia ya unyenyekevu ilivyo ya muhimu sana katika maisha yetu ya kila siku na zaidi sana katika ufalme wa Mungu.

Kuna nukuu nyingi sana duniani zinazotufundisha kuhusu umuhimu wa unyenyekevu na hapa nimechagua chache:-

Mtakatifu Augustino alisema “it was Pride that Changed the Angels to be devils and its humility that makes man as Angels” yaani “Ni kiburi kilichowafanya malaika kuwa pepo na ni unyenyekevu unaowafanya wanadamu kuwa kama malaika

Thomas Merton alisema “Pride makes us artificial and humility makes us really” kwamba “kiburi hutufanya kuwa fake na unyenyekevu hutufanya kuwa halisi

Rev. Innocent Kamote “Many ways may let people down, but have never ever seen humility letting someone down njia nyingi zinaweza kuwaangusha watu chini lakini sijawahi ona unyenyekevu ukiwaangusha mtu chini

Unaweza kuona Yesu anataka tuelewe kanuni za ufalme wa Mungu na kanuni za maisha haya, ni wazi kuwa mgeni hajui kuwa anapaswa kukaa katika kiti gani, ni lazima asubiri kukaribisha mwenyeji ndiye anayejua, Katika ufalme wa Mungu mwenyeji wetu ni Yesu, ni uhusiano wetu na mwenyeji wetu ndio utakaoamua kuwa ni kiti gani tutakalia, wako wengine wanajifikiri kuwa ni bora, kutokana na Dini zao, au madhehebu yao, au elimu zao, au kabila zao, au familia wanayotokea, au mkoa, au kutokana na huduma aliyo nayo, au kwa sababu anatumiwa sana na Mungu kufanya miujiza mikubwa, mtu anaweza akapiga hesabu zake kichwani mwake akajidhani kuwa yeye ni  wa muhimu kuliko wengine, Ni mwenyeji wetu Yesu ndiye ana mamlaka ya kuhamisha watu viti, anaweza kukuambia ndugu kakae mbele au anaweza kukuambia ndugu kakaye nyuma!

Mwanafunzi anapokwenda shuleni, anakuwa amekuja kujifunza, amekuja kukaa chjini ya walimu amekuja kufuata maelekezo, amekuja kufuata program zote za shule,  na hivyo wanafunzi wa aina hii hukubali kukaa chini ya walimu kwa unyenyekevu na kukubali kufundishika, wanakaa chini wanajifunza na kutafuta majibu ya maswala husika huku wakitii kila wanachoagizwa, Mwanafunzi yeyote ambaye anajidhani kuwa yuko smatter kuliko mwalimu wake, huwa na kiburi hawawezi kukubali kufuata maelekezo ya walimu wao wala program za shule na hatimaye matokeo yataeleza baadaye who is more smatter?

Yesu Kristo alikuwa ni mwana wa Mungu, lakini aliishi maisha ya unyenyekevu, alikuwa mtii alikubali kuelekezwa na alihukumiwa na alikubali kutii mpango wa Mungu na kumtii hata katika mauti ya msalaba ambayo ni mauti ya aibu sana kutokana na uwezo wake mkubwa wa unyenyekevu Mungu amemuadhimisha mno.


Wafilipi 2:4-11 “Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine. Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu; ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho; bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu; tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba. Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina;ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi; na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI BWANA, kwa utukufu wa Mungu Baba

Ili Mungu atuinue na kutuheshimu katika kanuni za ufalme wa Mungu njia ya kuwa wa muhimu sana ni kujishusha sana, njia ya kupanda juu sana ni kuwa mnyenyekevu sana ukikumbuka kuwa kuwa mnyenyekevu hakumaanishi kuwa wewe ni mjinga bali ni hekima ya Mungu ya hali ya juu ni njia ambayo Yesu aliichagua katika maisha na akatuachia kielelezo tuifuate kwani ina mafanikio makubwa sana.

Zaburi 138: 6 “Ingawa Bwana yuko juu, amwona mnyenyekevu, Naye amjua mwenye kujivuna tokea mbali.

Mithali 18:12 “Kabla ya uharibifu moyo wa mwanadamu hujivuna; Na kabla ya heshima hutangulia unyenyekevu.”

Warumi 12:16 “Mpatane nia zenu ninyi kwa ninyi. Msinie yaliyo makuu, lakini mkubali kushughulishwa na mambo manyonge. Msiwe watu wa kujivunia akili.

Aidha Yesu alikuwa anataka tujifunze kuwaheshimu wengine na kutambua uweza wa wengine, mwaka 18th April 1980 ilikuwa nisiku ya Zimbabwe kupata uhuru wake kutoka kwa Muingereza, katika siku hiyo walialikwa wageni maarufu kabisa duniani akiwemo Rais maarufu wa Tanzania Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, pamoja na mambo mengine, Zimbabwe ilimualika Mwanamziki maarufu wa muziki wa Regge duniani 

Robert Nesta "Bob" Marley (6 Februari 1945 - 11 Mei 1981) yaye alikuwa mwimbaji na mwanamuziki muhimu kutoka nchini Jamaika. Alivuma hasa kunako miaka ya 1970 na 1980.  Ambaye ameweza kuifanya staili ya muziki wa reggae kuwa maarufu sana duniani. Muziki wake mwingi ulikuwa unazungumzia dini ya Rastafari ambayo yeye alikuwa anaifuata. Kuna baadhi ya nyimbo zake zinahusu masuala ya dini na zingine siasa.

Katika wakati wa kusalimiana Mwalimu Julius Nyerere alipopeana mkono na mwanamuzik Bob Marley hakuwa amependezwa naye kwani alionekana kuwa mtu rafu asiyekata nyele zake na kama mvuta bangi hivi, lakini katika wakati Mwanamuziki huyo alipotumbuiza ndipo mwalimu Nyerere alipokwenda kumkumbatia na kumkubali mwanamziki huyo kutokana na nyimbo zake nzuri zenye kuhamasisha fikra za kiukombozi wimbo mojawapo muhimu ulikuwa ni pamoja na wimbo kuhusu Zimbabwe ambao ulikuwa na maneno yenye hamasa ya hali ya juu, yaliyodhihirisha kuwa Bob alikuwa msanii mahiri mwana mapinduzi aliyeipenda afrika kwa dhati kutoka Moyoni.

Every man gotta right to decide his own destiny
And in this judgment there is no partiality
So arm in arms, with arms
We'll fight this little struggle
'Cause that's the only way
We can overcome our little trouble

No more internal power struggle
We come together to overcome the little trouble
Soon we'll find out who is the real revolutionary
'Cause I don't want my people to be contrary

To divide and rule could only tear us apart
In everyman chest, there beats a heart
So soon we'll find out who is the real revolutionary
And I don't want my people to be tricked by mercenaries

Maneno haya na uwezo mkubwa alioonyesha mwanamuziki huyo ulimfanya Mwalimu Julius Nyerere amualike Bob Marley kuitembelea Tanzania lakini kabla ya kuitembelea Tanzania Bob alifariki kwa ugunjwa wa Kansa ambapo May 11 1981 alifariki Dunia, Bob alipowasili Zimbabwe alitumia ndege ya Boeing 777 na vyombo vyake vya music vilikuwa na uzito wa tani 21. 

Kila mwanadamu Dunainai ana kitu cha ziada ndani yake na kwa sababuhiyo tunapaswa kuwaheshimu wenzetu na kutambua kuwa wana umuhimu mkubwa duniani kulinga ana nafasi zao

Rev. Innocent Kamote.

Mkuu wa wajenzi mwenye hekima.

Jumatatu, 21 Januari 2019

Operesheni Lutu !

Adiko la Msingi: Mwanzo 14:14-16 “Abramu aliposikia ya kwamba nduguye ametekwa mateka, akawapa silaha vijana wake, waliozaliwa katika nyumba yake, watu mia tatu na kumi na wanane, akawafuata mpaka Dani. Akajipanga apigane nao usiku, yeye na watumwa wake, akawapiga, akawafukuza mpaka Hoba, ulioko upande wa kushoto wa Dameski. Naye akarudisha mali zote, akamrudisha na Lutu nduguye na mali zake, na wanawake pia, na watu.”


Utangulizi:

Nimetumia neno operesheni ambalo kwa kawaida ni neno linalotumika katika kampeni mbalimbali za kivita, mfano Tanzania,ilipokwenda kukomboa visiwa vya Anjuan wakati wa utawala wa Kikwete ile iliitwa Operasheni Demokrasi, Israel ilipokwenda kukomboa wayahudi kule Uganda wakati wa idd Amin kampeni ile iliitwa Operasheni Entebbe au wakati wa kurejesha Waethiopia wenye asili ya Kiyahudi ambao inasadikiwa kuwa walikuwa watoto wa Suleiman iliitwa operesheni SOLOMON sasa Abrahamu alipigana vita kumkomboa Lutu ndio maana nimeiita Operesheni Lutu sasa tuendelee na somo 

Ni muhimu kufahamu kwamba maandiko matakatifu yanatukumbusha katika Wagalatia 5:13b kwa mba tutumikiane kwa Upendo, “bali tumikianeni kwa upendo” moja ya maeneo yanayotufundisha kuhusu maisha ya Abraham ni pamoja na kifungu hiki muhimu tulichokipitia leo,kifungu hiki kinatukumbusha jinsi Abrahamu alivyokuwa mwenye kujali sana Maisha ya ndugu zake na jamaa zake. Lakini vilevile tunajifunza mambo mengine Makubwa sana kuhusu Mtu huyu wa Mungu ambayo yatatupa uweza mpana wa kufukiri kuhusu utendaji wa Mungu katika maisha yake.

Wengi wetu tunaposikia kuhusu Maisha ya Abrahamu mara kadhaa tunaweza kukumbuka matukio yake ya kidhaifu kama kusema uongo kwa kusudi la kulinda uhai wake kwa kumtaja Sara kama dada yake jambo lililohatarisha kupoteza ndoa yake, Lakini vilevile tunaweza kukumbuka ushujaa wake wa kukubali kuitikia wito wa Mungu na kukubali kuitii Sauti yake kwenda Katika nchi ya Kanaani, aidha tunaweza kukumbuka ushujaa wake wa kuthubutu kumtoa Isaka kama sadaka ya kuteketezwa mpaka malaika akamzuia, Pamoja na umuhimu wa Maswala hayo Leo ni muhimu tukajikumbusha kuwa Ibrahimu vilevile alikuwa mtu wa Vita, alikuwa mpiganaji Hodari mwenye mbinu kali sana za kivita, Abrahamu alikuwa mpiganaji.

Abrahamu si baba wa imani tu laikini ni baba wa vita!

Biblia inatufunulia siri hii kuhusu maisha ya Abrahamu kama mtu wa vita na jemadari kwa habari tunayoweza kuiona katika Mwanzo 14:1-4. Ni muhimu kufahamu kuwa sio tu kuwa Abraham alikuwa mpole tu lakini vilevile alikuwa ni Jemadari wa vita ni mpiganaji, Lakini alikuwa na Moyo wa kuwasaidia wengine, Mungu anapokuwa amekuita kuwa Baraka kwa wengine maana yake pia amekuita kuwapigania wengine Abrahamu anaonekana kuwa shujaa wa kipekee alipoingia katika vita ya kumuokoa Lutu Nduguye.

Mwanzo 14:1-4Ikawa siku za Amrafeli mfalme wa Shinari, na Arioko mfalme wa Elasari, na Kedorlaoma mfalme wa Elamu na Tidali mfalme wa Goimu, walifanya vita na Bera mfalme wa Sodoma na Birsha mfalme wa Gomora, na Shinabu mfalme wa Adma, na Shemeberi mfalme wa Seboimu, na mfalme wa Bela, ndio Soari. Hawa wote wakakutana panapo bonde la Sidimu, kwenye Bahari ya Chumvi. Miaka kumi na miwili walimtumikia Kedorlaoma, hata mwaka wa kumi na tatu wakaasi.”

Maandiko yanaonyesha kuwa kulikuwa na vita za kifalme wafalme Amrafel, Arioko, Elasari, Kedorlaoma na tidal yaani combine ya Majeshi ya wafalme watano(5) walioungana walikuja kupigana na Birsha, Shinabu, Shemeberi, na mfalme wa Bela jumla ya wafalme (4) sababu kuu ya wafalme hawa wanne walikuwa wamekataa kuendelea kulipa Kodi ya mfale Kedorlaoma wa Elamu aliyekuwa kinara wa utawala huo, hii ilikuwa vita kali katika nchi ya kanaani hususani kusini ya Israel liliko bonde la nchi ya chumvi lililojulikana kama bonde la Siddim, wafalme hao wanne walikuwa watumwa kwa miaka 12 lakini sasa wakaasi, hivyo Kedorlaoma alikuja kuwashambulia akiwa na wafalme kadhaa wanaomuunga mkono.

Mwanzo 14:5-7 “Na mwaka wa kumi na nne akaja Kedorlaoma na wafalme waliokuwa pamoja naye, wakawapiga Warefai katika Ashteroth-karnaimu, na Wazuzi katika Hamu, na Waemi katika Shawe-kiryathaimu, na Wahori katika mlima wao Seiri, mpaka Elparani iliyo karibu na jangwa. Kisha wakarudi wakaja mpaka Enmisfati, ndio Kadeshi, wakapiga nchi yote ya Waamaleki, na Waamori waliokaa Hasason-tamari. Mfalme wa Sodoma, na mfalme wa Gomora, na mfalme wa Adma, na mfalme wa Seboimu, na mfalme wa Bela, ndio Soari, wakatoka wakapanga vita panapo bonde la Sidimu; wapigane na Kedorlaoma mfalme wa Elamu, na Tidali mfalme wa Goimu, na Amrafeli mfalme wa Shinari, na Arioko mfalme wa Elasari, wafalme wanne juu ya wale watano. Na bonde la Sidimu lilikuwa limejaa mashimo ya lami. Nao wafalme wa Sodoma na Gomora wakakimbia, wakaanguka huko, nao waliosalia wakakimbia milimani. Wakachukua mali zote za Sodoma na Gomora na vyakula vyao vyote, wakaenda zao.

Kinara wa vita hivi alikuwa ni mfalme KEDORLAOMA yeye aliongoza muungano wa majeshi ya kifalme kwa zaidi ya wafalme wanne na kabla ya kuanza na hawa watano walifagia miji mingina na kuwapiga vibaya wote waliokuwa kinyume nao na walipofika katika miji ya Sodoma na Gomora wafalme hao watano pia yaliwakuta magumu na wote walikimbia mbele ya ufalme huu wenye nguvu. Nani angeweza kuwatetea wafalme hao watano na wengine wote chini ya KEDORLAOMA? Hakuna mtu aliyeweza kusimama mbele yake.

Kosa kuu la KEDORLAOMA

Pamoja na ushindi mkubwa aliokuwa nao KEDORLAOMA alifanya kosa ambalo liliweza kumfanya ajutie utendaji wake kosa hili lilikuwa kumgusa Lutu Mwanzo 14:8-10, walichukua Mateka kila kitu lakini pia walimchukua Lutu na mali zake na watoto wake na watu wake wote aliokuwa nao, Lutu alikuwa amefiwa na baba yake na hivyo alilelewa na Abrahamu, Abrahamu hangeweza kumuacha Lutu, amekulia kwake tangu utoto wake kusumbuliwa kwake kulileta maumivu makubwa sana kwa Abrahamu naye alipopata habari aliona aweze kufanya jambo.

Mwanzo 14:11-12 Biblia inasema “Wakachukua mali zote za Sodoma na Gomora na vyakula vyao vyote, wakaenda zao. Wakamtwaa Lutu, mwana wa nduguye Abramu, aliyekaa huko Sodoma, na mali yake, wakaenda zao.”

Abrahamu aliamuru Majeshi yake kwaajili ya Lutu.

Mwanzo 14:13-19 “Mtu mmoja aliyeponyoka akaenda, akampasha habari Abramu Mwebrania; naye amekaa panapo mialoni ya Mamre, yule Mwamori, ndugu ya Eshkoli, na ndugu ya Aneri, na hao walikuwa wamepatana na Abramu. Abramu aliposikia ya kwamba nduguye ametekwa mateka, akawapa silaha vijana wake, waliozaliwa katika nyumba yake, watu mia tatu na kumi na wanane, akawafuata mpaka Dani. Akajipanga apigane nao usiku, yeye na watumwa wake, akawapiga, akawafukuza mpaka Hoba, ulioko upande wa kushoto wa Dameski. Naye akarudisha mali zote, akamrudisha na Lutu nduguye na mali zake, na wanawake pia, na watu. Abramu aliporudi kutoka kumpiga Kedorlaoma na wale wafalme waliokuwa pamoja naye, mfalme wa Sodoma akatoka amlaki katika bonde la Shawe, nalo ni Bonde la Mfalme. Na Melkizedeki mfalme wa Salemu akaleta mkate na divai, naye alikuwa kuhani wa Mungu Aliye juu sana. Akambariki, akasema, Abramu na abarikiwe na Mungu Aliye juu sana, Muumba mbingu na nchi.

Mungu alimpa neema kubwa Abrahamu, alikuwa na vijana “318” ambao wao walikuwa wamejifunza vita Biblia inasema hawa wote walizaliwa katika nyumba yake hii ni wazi kuwa walilelewa na Ibrahimu, na ni wazi kuwa Ibrahimu alikuwa amewafunza kuhusu Mungu ushujaa wao ulikuwa umetokana na Mungu aliye juu Neema ya Mungu ilikuwa juu yao haiwezekani katika akili za kawaida Mtu mmoja aweze kupiga wafalme wanne waliokuwa na ushindi mkubwa wa ajabu, na wafalme wanne walikuwa wamekimbia Lakini Abrahamu na vijana wake 318 tu waliwapiga vibaya kundi kubwa la watu wenye uzoefu wa vita, siri kuu ya ushindi wa Abrahamu ilikuwa ni Muujiza wa Mungu, lakini vilevile alifanya sehemu yake alipigana na Mungu aliwaongezea hekima namna ya kupambana.

Abrahamu alifanikiwa kuwafuatia na kuwavamia maadui na aliweza kufanikiwa kuwapokonya malizote walizozipora kwa wafalme wanne na zaidi ya yote Abrahamu alikuwa anamtaka Lutu awe salama, aliwafukuza maadui kwa zaidi ya maili 50

Abrahamu alifanya mashambulizi makali wakati wa usiku, hakupigana mchana, laziki zaidi ya yote aliwagawa vijana wake makundi makundi na wakaanza kushambulia kutoka sehemu mbalimbali, maadui walichanganyikiwa wakidhani ya kuwa ulikuwa uvamizi mkubwa sana na hivyo walikimbia na kuachia kila kitu hivyo Abrahamu alimshinda KEDORLAOMA, Abrahamu alirejea nyumbani na ushindi. Alirudi na vijana wote waliwa salama na alirejea na mali zote na alifanikiwa kumuokoa Lutu.

Wafalme kadhaa wakaja kumlaki

Mmoja alifikiri ushindi wa Abrahamu unatokana na vijana wake “318” na akasema Mwanzo 14:21-22Mfalme wa Sodoma akamwambia Abramu, Nipe mimi hao watu, na hizo mali uchukue wewe. Abramu akamwambia mfalme wa Sodoma, Nimeinua mkono wangu kwa BWANA, Mungu Aliye juu sana, Muumba mbingu na nchi

Lakini Mfalme mwingine aliyekuwa Kuhani wa Mungu aliya juu sana alijua siri ya ushindi wa Abrahamu

Mwanzo 14:17-20 “Abramu aliporudi kutoka kumpiga Kedorlaoma na wale wafalme waliokuwa pamoja naye, mfalme wa Sodoma akatoka amlaki katika bonde la Shawe, nalo ni Bonde la Mfalme. Na Melkizedeki mfalme wa Salemu akaleta mkate na divai, naye alikuwa kuhani wa Mungu Aliye juu sana. Akambariki, akasema, Abramu na abarikiwe na Mungu Aliye juu sana, Muumba mbingu na nchi. Ahimidiwe Mungu Aliye juu sana, aliyewatia adui zako mikononi mwako. Abramu akampa fungu la kumi la vitu vyote

Siri kubwa ya ushindi wa maisha yetu hautokani na uwezo wetu na akili zetu, bali inatokana na uwezo na uhodari wetu katika Mungu, ni lazima tujifunze kupambana na kushinda vita zote za kiroho, na kujitegemeza katika uwepo wake na adui zetu watakimbia, Ibrahimu alikuwa ni mpole sana lakini linapokuja swala la kuchokozwa na kuguswa kwa maisha ya nduguze alihakikisha kuwa anapigana kwa hali na mali huku akimshirikisha Mungu.

Ni ukweli ulio wazi kuwa tunapokuwa na Moyo wa kuwajali wengine Mungu hutubariki na kutupa neema na Baraka tele, Abrahamu hakuweza kusema Lutu shauri yake si amejitenga nani mwenyewe lakini bado alitaka kuhakikisha usalama wa Lutu na jirani zake unakuwepo na hivyo alimtetea Lutu hii ndio operesheni Lutu.

mfalme wa Sodoma alitamani kumpa Ibrahu Mali zake ili achukue vijana 318, Ibrahimu hakukubali, wako watu wa mataifa ya kigeni wakati mwingine wanatulazimisha Afrika kufuata tabia zao mbaya kwa makusudi ya kutuingiza katika mtego wa kukosa uadilifu, tukatae misaada hiyo na tuendelee kumtegemea Mungu anatubariki na kutusaidia. 

Na mkuu wa wajenzi mwenye Hekima. 

Rev. Innocent Kamote

Jumanne, 27 Novemba 2018

“Kama wakitenda Mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?”

Mstari wa Msingi: Luka 23:27-31

Mkutano mkubwa wa watu wakamfuata, na wanawake waliokuwa wakijipiga vifua na kumwombolezea.Yesu akawageukia, akasema, Enyi binti za Yerusalemu, msinililie mimi, bali jililieni nafsi zenu na watoto wenu. Kwa maana tazama, siku zitakuja watakaposema, Heri walio tasa, na matumbo yasiyozaa, na maziwa yasiyonyonyesha. Ndipo watakapoanza kuiambia milima, Tuangukieni, na vilima, Tufunikeni. Kwa kuwa kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?”

 “Kama wakitenda Mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?”

Utangulizi:

Leo nataka tuchukue Muda kutafakari kwa kina kuhusu usemi huu wa Yesu Kristo, Kwa kuwa kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?”  Usemi huu ambao ni usemi mzito sana na unaweza kuwa mgumu katika kuutafasiri kwa namna nyepesi nyepesi, Usemi huu ni usemi wa kitaaluma katika maswala ya semi za “Marabbi” na “Manabii” Ni usemi mzito uliojaa unabii, maana na maonyo na ndani yake kuna maana nzito sana ukilinganisha na mfumo wa maisha ya sasa tuliyonayo katika ulimwengu, lakini vilevile katika maisha ya kila mmoja wetu, Bwana na atupe neema kuuangalia usemi huu kwa undani, hata tuweze kupata, maana inayokusudiwa! Na kujifunza kutoka kwa Mwalimu mkuu Roho Mtakatifu!Katika jina la Yesu Kristo Amen.

Maana ya mti mbichi.
Mstari wa 31 Kwa kuwa wakitenda mambo haya katika mti mbichi, -  Kimsingi mti mbichi unaotajwa hapa na Yesu ni mti mwema mti wenye kuzaa matunda “Productive tree” mti ambao unaonekana kuwa una faida kubwa sana kibiblia mti huu unaitwa mti wa uzima angalia Ufunuo 2:7Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye, nitampa kula matunda ya mti wa uzima, ulio katika bustani ya Mungu”. Ufunuo 22:2Katikati ya njia kuu yake. Na upande huu na upande huu wa ule mto, ulikuwapo mti wa uzima, uzaao matunda, aina kumi na mbili, wenye kutoa matunda yake kila mwezi; na majani ya mti huo ni ya kuwaponya mataifa.” 14, “Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake”. 19 “Na mtu ye yote akiondoa lo lote katika maneno ya unabii wa kitabu hiki, Mungu atamwondolea sehemu yake katika ule mti wa uzima, na katika ule mji mtakatifu, ambao habari zake zimeandikwa katika kitabu hiki.” 

Mti mbichi hapa unawakilisha Yesu Kristo, ambaye ndio mti wa uzima, wenye kuzaa matunda, kupitia kazi ya ukombozi na huruma zake amekuwa akiwaponya watu na kuwatendea mema, amekuwa mzuri na mwenye moyo mzuri, aliwafundisha watu neno la Mungu kwa huruma zake, aliwalisha watu wenye njaa, aliwaponya wenye ukoma, vipofu, walemavu na watu wenye shida na maatatizo ya aina mbalimbali, lakini pasipo huruma wakuu wa makuhani walimkabidhi kwa askari wa Kirumi watu wa mataifa wasiotahiriwa, ili wamsulubishe japokuwa Pilato hakuona dhambi yoyote ndani yake, hakuwa na hatia yoyote Yesu hakutenda dhambi yoyote lakini alifanyiwa tukio baya sana, alipigwa mijeledi, alitemewa mate, alivunjiwa heshima, alifedheheshwa, alinyanyashwa, alivishwa taji ya miiba japo kuwa alikuwa mwema Pilato alitoa hukumu ya kifo dhidi ya mtu ambaye mwenyewe alihakikisha kuwa hana hatia, lakini alitendewa mambo yasiyofaa, Yesu alikuwa akiwawazia mema, alikuwa akiwapenda, alikuwa akiwahurumia lakini aliteswa na kudhulumiwa uhai wake vibaya pasipo hatia yoyote, Yesu kristo alimtii Mungu kwa viwango vya juu zaidi hakuwa na dhambi Yohana 8;46 Je, kuna ye yote miongoni mwenu awezaye kunithibitisha kuwa nina dhambi? Kama nawaambia yaliyo kweli, mbona hamniamini?” Kama Yesu Kristo mti wenye faida wenye kuzaa matunda wenye kutii na kutenda mema wenye kweli yote amepita katika wakati mgumu namna hii siku ya mtu mbaya au mti mbaya kupita katika hukumu utakuwa ni wakati mbaya sana, ikiwa watu wa Mungu wanaokoka kwa shida, asiye wa Mungu atapata taabu sana 1Petro 4:18 “Na mwenye haki akiokoka kwa shida, Yule asiyemcha Mungu na mwenye dhambi ataonekana wapi? ”
 
Maana ya Mti mkavu.

31.b Itakuwaje kwa mti mkavu – Kwa upande mwingine mti mkavu inazungumzia kibiblia mti usio na matunda na mti usiozaa matunda “un Productive tree” unawakilisha watu wasiomcha Mungu, mti usio na faida mti usiozaa matunda au mti usiozaa matunda mazuri Mathayo 3:10Na shoka limekwisha kuwekwa penye mashina ya miti; basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni.” 

Luka 13:7-9 “Akamwambia mtunzaji wa shamba la mizabibu, Tazama, miaka mitatu hii naja nikitafuta matunda juu ya mtini huu, nisipate kitu; uukate, mbona hata nchi unaiharibu?  Akajibu akamwambia, Bwana, uuache mwaka huu nao, hata niupalilie, niutilie samadi; nao ukizaa matunda baadaye, vema! La, usipozaa, ndipo uukate”.

Mti mkavu unawakilisha watu waiozaa matunda, watu wabaya wasiomcha Mungu, wenye dhuluma waliojaa wivu kama mafarisayo na wakuu wa makuhani waliomsulubisha Yesu Kristo, pamoja na wote waliokataa neema ya Mungu lakini pia kwa lugha ya kinabii mti mkavu ni nabii wa uongo na mpinga Kristo.

Onyo kwa wanaomkataa Yesu!

Luka 23:27-31 “27.Mkutano mkubwa wa watu wakamfuata, na wanawake waliokuwa wakijipiga vifua na kumwombolezea. 28. Yesu akawageukia, akasema, Enyi binti za Yerusalemu, msinililie mimi, bali jililieni nafsi zenu na watoto wenu. 29. Kwa maana tazama, siku zitakuja watakaposema, Heri walio tasa, na matumbo yasiyozaa, na maziwa yasiyonyonyesha. 30. Ndipo watakapoanza kuiambia milima, Tuangukieni, na vilima, Tufunikeni.

Lakini vilevile katika jamii tunao watu wenye nia mbovu wasio wema ingawa wakati mwingine unaweza kushangaa watu wema wakafanyiwa vitu vibaya sana vya kusikitisha na ukajiuliza je itakuwaje kwa watu wabaya, Muda unakuja kwa wabaya pia kuhukumiwa na hukumu yao itakuwa mbaya sana, kama Mungu anaweza kumuadhibu mwana wake mpendwa Yesu, na kumuacha achinjwe kama kondoo wa kafara na watu wema wakawa wanamlilia na kumuhurumia Yesu aliwaonya kuwa afadhali waache kumlilia yeye na waanze kulia na kuomboleza kwaajili ya watoto wao, Yeye kristo anauawa kwaajili ya faida ya watakaomwamini, kifo chake ni ushindi dhidi ya adui zake, kifo chake kinaleta uzima wa milele  na wokovu kwa wote watakaomwamini, kwa sababu hiyo hakuna sababu ya kulia na kuomboleza kwaajili ya Kristo, lakini iko sababu ya kulia na kuomboleza kwaajili ya nafsi zetu na watoto wetu hususani kama tutaikataa neema ya Mungu.

Hata hivyo kinabii vilevile Yesu alikuwa akizungumza na wayahudi ambao wangeuawa na kuteswa vibaya na Warumi hao hao miaka michache kwa sababu ya kumkataa Yesu wayahudi walijuta sana kile ambacho Yesu alikuwa amewaonya kilitimizwa mwaka wa 70 BK. Ilikuwa ni kilio na kusaga meno. Ni muhimu kukumbuka kuwa kama mti mbichi na mti mkavu itatiwa moto ukweli ni kuwa mti mkavu utawaka na kuteketea na kusahaulika ukilinganisha na mti mbichi.

Ni ukweli ulio wazi kuwa baada ya Yesu kutabiri hili kwenye mwaka wa 33BK tunaelezwa katika historia kuwa mwaka wa 70 BK yaani (70-33=37) yaani miaka 37 baada ya maneno ya Yesu Askari wa kirumi waliizingira Yerusalem na kuwanza kuwaua wayahudi chini ya utawala wa Kaisari TITUS baada ya uasi wa mwaka 66 Israel walipotaka kuwa na serikali huru, Yerusalem uliharibiwa vibaya, Hekalu lilichomwa kwa moto na halikujengwa tena mpaka naandaa ujumbe huu, wayahudi waliuawa kila upande chini ya Jemadari aliyeitwa Tiberius Julius Alexander , Wayahudi waliuawa kijiji kwa kijiji na kumalizikia katika kijiji kilichoitwa Masada ambako wayahudi walijiua wenyewe wakikataa kwenda utumwani, hali ilikuwa mbaya sana na wayahudi walitawanyika dunia nzima mpaka mwaka wa 1949 may walipopata uhuru na kujitangaza tena kama taifa pekee la kiyahudi lililoko hadi leo, hii ilikuwa ni hukumu mbaya na yenye kutisha kama alivyoonya Bwana Yesu.

Wito wa Kimungu unamtaka kila mtu duniani atubu, ajirekebishe aache dhambi, ikiwa Mungu aliruhusu mwana wake Mpendwa Yesu Kristo achubuliwe na kudhihakiwa na kufa kifo kibaya na cha aibu Msalabani, huku kwa hakika hakuwa mwenye dhambi, alikuwa mti mbichi sembuse mimi na wewe leo, tusiofaa kitu, tulio mti mkavu, Bila unyenyekevu na toba ya kweli ni wazi kuwa hatutaweza kustahimili siku ya kuadhibiwa kwetu, ni lazima kama taifa tutubu, tuache uovu, tuzae matunda unabii huuwa Yesu Kristo bado unafanya kazi hata sasa kwa kila mtu na kwa kila Taifa, Kama humuamini Yesu wewe hutaweza kustahimili Hasira  ya Mungu, angalia dhuluma, uonevu, wizi, uasherati,zinaa, mmommonyoko mkubwa wa uadilifu ulioko kwa dunia ya sasa, uovu unapoonekana akama sifa ya kujivunia.

Mataifa yaliyoendelea yaliyokuwa yanajulikana kama mataifa ya Kikristo mabunge na viongozi na hata wa kidini angalia walivyopigwa upofu kuruhusu ndoa za jinsia moja, kutokukemea matendo ya usagaji na ushoga, angalia mataifa ya Kiislam yasiyotenda haki na kuruhusu injili ya Kristo kuhubiriwa kwao, au kuruhusu uhuru wa kuabudu, utapeli uliokithiri na ufisadi hizi zote zinatufanya kuwa mti mkavu ambao hautaweza kustahimili, Hukumu ya moto wa Mungu itakapofika, kukandamiza wanyonge, dhuluma kwa wajane na yatima, dhuluma za mipaka ya mashamba na viwanja, dhuluma za hati za nyumba na viwanja, vilio kila mahali, mauaji yenye utata haya yote utafika wakati ambapo Mungu mwenye haki hatoweza kuyafumbia macho, siasa makanisani, uchawi, na ushirikina kampenzi za kimwili nyakati za chaguzi hata za kidini, kuonewa na kudhulumiwa kwa watu wema haya yote yanaandaa mti mkavu kuwashwa moto.

“Kama wakitenda Mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?” Yesu aliwaonya kina mama wa Yerusalem kuwa wasilie kwaajili yake bali walilie nafsi zao na watoto wao, Dunia nakutangazia ni wakati wa kujililia na kuililia nafsi za watoto wetu, leo ni taabu ukizaa mtoto wa kiume tabu ukizaa wa kike taabu  Mungu na aingilia kati na kuwaponya watu wake, usijifikiri kuwa wewe utapenya, hakuna upenyo dhiki ya Yerusalem iliwapata wema na waovu, lakini zaidi sana wale waliomkataa Kristo, Kama humuamini Yesu ndugu wewe ni mti mkavu, kama ungali unaishi katika dhambi ndugu wewe ni mti mkavu na kama wametenda yale kwa mti mbichi itakuwaje kwa mti mkavu? Kristo anasema siku ile watu watasema heri matumbo yasiyozaa,  na maziwa yasiyonyonyesha,watu wataiambia milima na vilima tuangukieni na kutufunika bila toba hali hii inaweza kumkuta mtu awaye yote.

“Kama wakitenda Mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?”
Rev. Innocent Kamote
Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima.

Jumapili, 25 Novemba 2018

Watapigana nawe lakini Hawatakushinda!


Mstari wa Msingi: Yeremia 1:19Nao watapigana nawe; lakini hawatakushinda; maana mimi nipo pamoja nawe, asema Bwana, ili nikuokoe.”



Pichani ndege za Jeshi la Anga la Israel (IAF) Israel Air Force  tayari kwa mashambulizi dhidi ya adui wa Israel

Utangulizi:

Nabii Yeremia alikuwa moja ya manabii aliyepata ahadi nyingi sana za Mungu za kutia moyo, na sababu kubwa ni kuwa pia alikuwa ni nabii aliyepitia changamoto nyingi sana katika maisha, hususani upinzani mkubwa sana kwa ujumbe aliokuwa akiutoa, ambao kimsingi haukuwa wake bali ulikuwa ni ujumbe kamili wa Mungu dhidi ya watu wake kwa kinya cha nabii Yeremia.

Mungu mwenye upendo mwingi na rehema alikuwa anajua wazi kuwa mtumishi wake atapitia changamoto, kubwa na nyingi dhidi ya ujumbe wake wa kinabii aliokuwa anautoa ambao kimsingi haungeweza kuwafurahisha watu wayahudi kwa vile huenda walidhani kuwa Yeremia anatabiri kinyume na watu wa Mungu, mji wa Mungu na Hekalu la Mungu, aidha alionekana kama anawatukuza wakaldayo ambao kimsingi walikuwa ni adui wa Israelk na mataifa mengine.

Kutokana na ugumu wa kazi hii mapema sana Mungu alimuahidi Yeremia kuwa atakuwa pamoja naye, Mungu kuwa pamoja na Yeremia ulikuwa ni ujumbe wazi kuwa Mungu mwokozi wa wanadamu angekuwa pamoja naye, hii ilieleweka wazi kwa Yeremia kuwa ushindi uko pamoja naye, uwepo wa Mungu unapokuwa na mtu awaye yote ni vigumu sana kumshinda mtu wa namna hiyo, Kama Mungu amesema mtu huyu niko naye tayari mtu huyo ni mshindi, uwepo wa Mungu ni ushindi, uwepo wa Mungu ni ulinzi, uwepo wa Mungu bwana wa majeshi ni ishara iliyowazi kuwa hata kuwe na jeshi kubwa namna gani litasambaratika kabisa na hii ndio maana ya “ Immanuel” Isaya 7:14Kwa hiyo Bwana mwenyewe atawapa ishara. Tazama, bikira atachukua mimba, atazaa mtoto mwanamume, naye atamwita jina lake Imanueli.” Unaweza kuona Katika mstari wa Msingi Mungu alimuahidi Nabii Yeremia  mambo ya msingi makuu matatu ambayo anamuahidi kila mtu wake leo kama yeremia wa sasa au kama mtu unayepitia mambi magumu au uko kwenye vita ngumu kama ile aliyokuwa akiipitia Yeremia.

1.       Watapigana naye (au watashindana naye) Lakini hawatakushinda, watapigana nawe hii ina maana ya Muungano mkubwa wa maadui, ya kwamba adui sio mmoja tu, wanaweza kuwa wengi wanaweza kuwa ni timu kubwa ya watu walioungana kwa nia moja kuweza kukufutilia mbali, na wewe unaweza kusalia peke yako, Hili lisikupe shida lisikutese angalia Waamuzi 20:11Basi waume wote wa Israeli walikutana pamoja juu ya mji huo, walikuwa wanashikamana pamoja kama mtu mmoja.” Kuna wakati adui wataungana na kuwa kama mtu moja wakiwa na lengo au kusudi la kupigana nawe hivi ndivyo ilivyokuwa kwa Yeremia, Israel na hata wewe pia lakini Mungu ameahidi kuwa HAWATAKUSHINDA. 2Mambo ya nyakati 20:1- 15 “Ikawa baadaye, wana wa Moabu, na wana wa Amoni, na pamoja nao baadhi ya Wameuni, wakaja juu ya Yehoshafati vitani. Wakaja watu waliomwambia Yehoshafati, wakisema, Wanakuja jamii kubwa juu yako watokao Shamu toka ng'ambo ya bahari; na tazama, wako katika Hasason-tamari (ndio En-gedi).Yehoshafati akaogopa, akauelekeza uso wake amtafute Bwana; akatangaza mbiu ya watu kufunga katika Yuda yote. Yuda wakakusanyika pamoja ili wamtafute Bwana; hata kutoka miji yote ya Yuda wakaja kumtafuta Bwana. Yehoshafati akasimama kati ya kusanyiko la Yuda na Yerusalemu, nyumbani mwa Bwana, mbele ya ua mpya; akasema, Ee Bwana, Mungu wa baba zetu, si wewe uliye Mungu mbinguni? Tena si wewe utawalaye falme zote za mataifa? Na mkononi mwako mna uweza na nguvu, asiweze mtu ye yote kusimama kinyume chako. Si wewe, Ee Mungu wetu, uliyewafukuza wenyeji wa nchi hii mbele ya watu wako Israeli, ukawapa wazao wa Ibrahimu rafiki yako hata milele? Nao walikaa humo, wamekujengea patakatifu pa jina lako humo, wakisema, Yakitujia mabaya, upanga, hukumu, au tauni, au njaa, tutasimama mbele ya nyumba hii, na mbele zako, (maana jina lako limo katika nyumba hii), na kukulilia katika shida yetu, nawe utasikia na kuokoa. Na sasa, tazama, wana wa Amoni, na Moabu, na wa mlima Seiri, ambao hukuwaacha Israeli waingie katika nchi yao, walipotoka nchi ya Misri; lakini wakawageukia mbali, wasiwaharibu; tazama, jinsi wanavyotulipa, wakija kututupa toka milki yako, uliyoturithisha. Ee Mungu wetu, je! Hutawahukumu? Maana sisi hatuna uwezo juu ya jamii kubwa hii, wanaotujia juu yetu; wala hatujui tufanyeje; lakini macho yetu yatazama kwako. Wakasimama Yuda wote mbele za Bwana, pamoja na wadogo wao, na wake zao, na watoto wao. Ndipo Yahazieli mwana wa Zekaria, mwana wa Benaya, mwana wa Yeieli, mwana wa Matania, Mlawi, wa wana wa Asafu, akajiliwa na roho ya Bwana, katikati ya kusanyiko; akasema, Sikieni, Yuda wote, nanyi mkaao Yerusalemu, na wewe mfalme Yehoshafati; Bwana awaambia hivi, Msiogope, wala msifadhaike kwa ajili ya jeshi kubwa hili; kwani vita si yenu bali ni ya Mungu.”

2.       Hawatakushinda; Maana yake ni kuwa hawataweza, hawatakuweza, yaani hata kama watatumia silaha kubwa na za kisasa namna gani, yaani hata kama watatumia uchawi, yaani hata kama watajikita na  kuleketa watu waliobobea kiasi gani Mungu ameahidi kuwa hawatakushinda Yeremia 15:20-21Nami nitakufanya kuwa kama ukuta wa boma la shaba juu ya watu hawa; nao watapigana nawe; lakini hawatakushinda; maana mimi nipo pamoja nawe, ili nikuokoe, na kukuponya, asema Bwana. Nami nitakuokoa na mkono wa watu wabaya, nami nitakukomboa katika mkono wao wenye kutisha.” Unaweza kuona kumbe hata adui awe mwenye kutisha kiasi gani Mungu ameahidi kutokoa na mikono ya watu wabaya na kutukomboa kwa mkono wenye kutisha, licha ya ushindi mkubwa sana Mungu atakaotupa dhidi ya adui zetu Pia mungu ameahidi kuwa watapata aibu ambayo haitasahaulika  hii ni kwa sababu Mungu atakuwa pamoja nasi  Yeremia 20:10-11.Maana nimesikia mashutumu ya watu wengi; hofu ziko pande zote. Rafiki zangu wote, wanaonivizia nisite, husema, Mshitaki, nasi tutamshitaki, huenda akahadaika, nasi tutamshinda, tutajilipiza kisasi kwake. Lakini Bwana yu pamoja nami, mfano wa shujaa mwenye kutisha; kwa hiyo hao wanaonionea watajikwaa, wala hawatashinda; watatahayarika sana. Kwa sababu hawakutenda kwa akili, wataona aibu ya milele, ambayo haitasahauliwa kamwe.” 

3.       Kwa kuwa mimi nipo pamoja nawe: Siri kubwa ya ushindi ambayo kila muumini anaweza kuwa nayo ni kwakuwa Bwana Mungu yuko pamoja naye Yeremia 1:8 “Usiogope kwa sababu ya hao maana mimi nipo pamoja nawe nikuokoe, asema Bwana.” Wakati wote Mungu anapokuwa pamoja nasi uwepo wake unaleta ushindi katika maisha yetu, Mungu anapokuwa pamoja nasi yeye anakuwa ndio ushindi wetu, na mlinzi wetu hatuna budi kutembea kifua mbela tukijua kuwa Bwana yu pamoja nasi 2Timotheo 4:17-18Lakini Bwana alisimama pamoja nami akanitia nguvu, ili kwa kazi yangu ule ujumbe utangazwe kwa utimilifu, hata wasikie Mataifa yote; nami nikaokolewa katika kinywa cha simba. Bwana ataniokoa na kila neno baya, na kunihifadhi hata nifike ufalme wake wa mbinguni. Utukufu una Yeye milele na milele. Amina.”  
            
Hitimisho!

Ahadi hii kimsingi haikuwa tu kwaajili ya Yeremia pekee, Ahadi hii ni agano kwa watu wote wanaomtumaini Bwana, ni ahadi kwa Taifa la Israel na ni ahadi kwa kanisa na ni ahadi kwa kila Mtu wa Mungu, Katika Israel wote tunakumbuka kuwa mara kadhaa mataifa pinzani yanayoizunguka Israel wakiwahi kutaka kuifuta na kuikusudia mabaya, Misri, Jordan, Lebanon, Syria na Iraq waliwahi kukusudia mabaya dhidi ya Israel lakini walibamizwa vibaya na kusambaratishiwa mbali, watapigana nawe lakini hawatakushinda, Ndugu mpendwa kama tunamtumaini Mungu na kutembea katika uwepo wake hatupaswi kuogopa kitu, Hakuna atakayeweza kutushinda, hata kama maadui wataungana na kuwa kundi kubwa la watu au jeshi kubwa litasambaratishwa hatupaswi kuogopa kwa sababu tumemtumaini Mungu naye ametuahidi kuwa yuko pamoja nasi ili atuokoe na wale waliotukusudia mabaya watotaoka wakiwa wanatahayari, wamesambaratika, wamerudhishwa nyuma, Mpendwa liamini neno lake uone kama Mungu ninayekuhubiri habari zake atakuaibisha, Muaminini Mungu waaminini manabii wake ndipo mtakapothibitika.

Na mkuu wa wajenzi mwenye Hekima.

Rev. Innocent Kamote
0718990796/0781394550

Moto wa Kigeni!


Walawi 10:1-2Na Nadabu na Abihu, wana wa Haruni, wakatwaa kila mtu chetezo chake, wakatia moto ndani yake, wakatia na uvumba, nao wakatoa moto wa kigeni mbele ya BWANA, ambao yeye hakuwaagiza. Kisha moto ukatoka hapo mbele za BWANA, nao ukawala, nao wakafa mbele za BWANA.”


Utangulizi:

Mojawapo ya matukio mazito ya kutisha ambayo yamerekodiwa katika Biblia hususani wakati wa agano la kale ni pamoja na tukio la kifo cha wana wa Haruni Nadabu na Abihu, Hili ni tukio lenye kutisha na kuogofya kama lilivyokuwa tukio la kifo cha Anania na Safira katika Agano jipya. Tukio hili kwa mujibu wa maandik lilisababishwa na tendo la Nadabu na Abihu kutoa Moto wa Kigeni mbele za Bwana, kutoa moto wa kigeni kuna maanisha nini hasa? Hili ndilo jambo la msingi na kuliangalia kwa undani na kujifunza katika nyakati zetu leo kuwa lina maanisha nini.

Maana ya Moto wa Kigeni.

Neno moto wa kigeni Katika Biblia ya kiebrania linatajwa kama “esh zarah” Kwa kiingereza “Alien Fire” yaani moto ulio tofauti na maagizo “Strange fire” Jambo ambalo liko kinyume na kawaida, Jambo lisiloagizwa, jambo lililo kinyume na mamlaka, Jambo lisilojali heshima au utukufu wa Mungu, tukio la aina hii ndilo limeitwa moto wa kigeni. Yaani wana wa Haruni walifanya jambo ambalo halikuagizwa na Mungu. Biblia ya kiingereza ya King James Version KJV na New American Standard Bible NASB yanatumia neno “Strange Fire” na Biblia ya kiingereza ya New International Version NIV inatumia neno “unauthorized fire” Kwa hiyo Mungu sio tu alikataa sadaka yao (Ibada yao) lakini aliwaangamiza kwa moto na kifo kwa kutokufuata maagizo yake.

Moto wa Mungu na Moto wa Kigeni.

Ni muhimu kufahamu kuwa Biblia imetaja aina mbili za Moto, kwanza kulikuwa na Moto uliotoka kwa Mungu na pili Nadabu na Abihu walitumia moto wa kigeni

Unaposoma maandiko katika Mambo ya walawi 9:22-24 “Kisha Haruni akainua mikono yake na kuielekeza kwa hao watu, akawabariki; kisha akashuka akisha isongeza sadaka ya dhambi, na sadaka ya kuteketezwa, na sadaka za amani. Kisha Musa na Haruni wakaingia ndani ya hema ya kukutania, kisha wakatoka nje, na kuwabarikia watu; na huo utukufu wa BWANA ukawatokea watu wote. Kisha moto ukatoka hapo mbele za BWANA, na kuiteketeza sadaka ya kuteketezwa, na yale mafuta juu ya madhabahu; watu wote walipouona huo moto wakapiga kelele wakainama kifudifudi.

Huu ulikuwa Moto ulioshuka kutoka kwa Mungu, Mto huu ulitokana na Musa na haruni pamoja na wanawe kufuata maelekezo yote ambayo Mungu alikuwa amewapa jinsi na namna ya kumuabudu, Moto huu ulileta Baraka kubwa sana kwa watu wa Mungu, Haruni kuhani mkuu aliwabariki watu, Mto huu uliposhuka watu waliuona walipiga kelele za utukufu kwa Mungu na waliinama na kumuabudu Mungu, Huu ulikuwa moto wa ushindi

Unaposoma maandiko Katika Mambo ya walawi 10:1-2 “Na Nadabu na Abihu, wana wa Haruni, wakatwaa kila mtu chetezo chake, wakatia moto ndani yake, wakatia na uvumba, nao wakatoa moto wa kigeni mbele ya BWANA, ambao yeye hakuwaagiza. Kisha moto ukatoka hapo mbele za BWANA, nao ukawala, nao wakafa mbele za BWANA” 

Biblia haijaweka wazi kwamba Nadabu na Abihu walitumia aidha moto waliotumia walichukua kutoka nje au kama huu ulikuwa Moto uleule ambao ulishuka kutoka kwa Mungu lakini safari hii ulitumiwa na Nadabu na Abihu kwaajili ya kuwashia vyetezo vya kufukizia uvumba, Moto ukashuka kutoka kwa Munngu ukawaua nao wakafa, Moto huu ulisababishwa na Nadabu na Abihu kuasi na kutokufuata maelekezo ya Mungu na hivyo Haukuleta utukufu kwa Mungu na badala yake ulileta laana majuto na majonzi, ulikuwa ni moto wa hukumu, vyovyote vile kama walitumia moto wa Mungu au walitumia Moto kutoka nje ni wazi kuwa hawakuwa wanyenyekevu kutaka maelekezo kutoka kwa Mungu kwamba vyetezo vilipaswa kutumia moto wa aina gani, uwazi ni kuwa hawakuwa wamepokea maelekezo hivyo waliwasha moto usiamriwa na Mungu hawakufuata maelekezo,lakini pia kulikuwa na sababu kadhaa zifuatazo:-

Nabadu na Abihu waliuawa kwa sababu kadhaa zifuatazo za kibiblia.

1. Waliasi na kutokufuata maelekezo sahihi waliyopewa na Mungu na hivyo walishindwa kuonyesha heshima kwa Mungu Walawi 10: 3Ndipo Musa akamwambia Haruni, Jambo hili ni hilo BWANA alilolinena, akisema, Nitatakaswa mimi katika hao wanikaribiao, nami nitatukuzwa mbele ya watu hao wote. Haruni akanyamaza kimya.”

2. Hawakumuheshimu Mungu; Walihudhuria ibada waliwa wamelewa na hivyo walishindwa kukumbuka maagizo ya Mungu kwa usahihi Walawi 10: 8-9 “Kisha BWANA akanena na Haruni, na kumwambia, Usinywe divai wala kileo cho chote, wewe, wala wanao pamoja nawe, hapo mwingiapo ndani ya hema ya kukutania, ili kwamba msife; amri hii itakuwa ni amri ya milele katika vizazi vyenu; kisha, mpate kupambanua kati ya yaliyo matakatifu na hayo yaliyo ya siku zote, na kati ya yaliyo najisi na hayo yaliyo safi;” Ni wazi kuwa tabia yao ya ulevi wa pombe na kuingia katika nyumba ya Bwana ndiko kulikopelekea wasitiikwa usahihi maagizo ya Mungu na Mungu aliwashughulikia kwa hukumu yenye kutisha iliyopelekea kufutwa kwao.

Fundisho:

Kwa kifo cha hukumu ya Nadabu na Abihu kwaajili ya Moto wao wa kigeni , Mungu anamfundisha kila mmoja wetu kuwa Mungu hakubalkiani na namna yoyote ya uasi na kuvunjamaagizo yake, Hatupaswi kuwa na kiburi na kujifikiri kuwa tuna hati miliki ya Mungu, Hakuna jambo baya duniani kama uasi, Biblia haikubaliana kabisa na uasi wa aina yoyote kwa sababu zozote zile, Mungu anataka atukuzwe na sisi au kupitia sisi katika mazingira yoyote yale, hakuna sababu yoyote ambayo inaweza kukubaliwa na Mungu ya kutufanya sisi tuasi, Hata kama tunaonewa Mungu yupo na atatulipia, lakini kuonewa kwetu kusiwe sababu ya kumuasi Mungu na kuacha Mungu atukanwe kupitia maisha yetu.

Mungu anaijua mioyo yetu vema Ni sadaka ya utii na unyenyekevu tu inayoweza kutuletea Baraka kutoka kwake na kuuleta utukufu wake, Lakini hatuwezi kumtolea Mungu Sadaka ya Kiburi na kutokutii kisha Mungu atuvumilie tu, Mungu huwapinga wenye kiburi na kuwapa neema wanyenyekevu, Tunaponyenyekea kwake na kumtii Mungu hutubariki na kutukubali, lakini linapokuja swala la Utukufu na Heshima yake Mungu hawezi kukubali kuona vinaharibiwa
Mungu anachukizwa sana na watu wasiofuata maelekezo yake , watu wasiofuata maelekezo ya Mungu maana yake wamekataa kuwa chini ya utawala wa Mungu na hivyo Mungu huwadhibu au kuwakataa.

1Samuel 15:22-23 “Naye Samweli akasema, je! Bwana huzipenda sadaka za kuteketezwa na dhabihu Sawasawa na kuitii sauti ya Bwana? Angalia, kutii ni bora kuliko dhabihu, Na kusikia kuliko mafuta ya beberu. Kwani kuasi ni kama dhambi ya uchawi, Na ukaidi ni kama ukafiri na vinyago; Kwa kuwa umelikataa neno la Bwana, Yeye naye amekukataa wewe usiwe mfalme.” 

Popote pale unapoona watu wanachochea kuasi uongozi wa shule, au serikali, au wazazi au Mungu, au mamlaka fahamu kwa haraka kuwa hao wanatumia moto wa kigeni na kuwa hukumu ya Mungu haiko mbali, popote pale ambapo injili ya aina nyingine inahubiriwa na sio ile tuliyowahubiri mjue ya kuwa huo ni moto wa kigeni,Mafundisho potofu yaliyo kinyume na mpango halkisi wa Mungu ni moto wa kigeni, Mungu hatoruhusu Heshima yake iharibiwe kwa kufuata kile watu wanachokitaka na sio kile Mungu alichoagiza, Popote pale ambapo watu wanafungisha ndoa za jinsia moja au wanakubali kwa namna yoyote maswala ua ushoga na usagaji huo ni moto wa kigeni, Popote pale ambapo wanapinga watoto kuadhibiwa kwa fimbo, au walimu kushika fimbo kwaajili ya kuwaelekeza watoto sawasawa na neno la Mungu huo ni moto wa kigeni, ppopote pale wanapotumia mziki ambao sio wa kupiga moja kwa moja wakati wa kumsifu Mungu huo ni moto wa kigeni, popote pale ambapo watu wanaoongoza ibada wanavaa nusu uchi huo nao ni moto wa kigeni na utaharibu maisha yetu, utatuua hautaleta utukufu wa Mungu, kwetu utatunyima Baraka zilizokusudiwa kwetu, ni lazima tutubu kwa dhati na kumuomba Mungu atusamehe kila inapotokea mbegu ya uasi dhidi ya Mungu katikati yetu na kila linapotokea swala linalofanywa ambalo liko kinyume na Maagizo ya Mungu.

Musa alikuwa ni nabii aliyeheshimika sana na Mungu lakini Mungu hakumuachia aingie kanaani pale aliposhindwa kutii maagizo ya Mungu, ni lazima watu wa Mungu waogope kufuata maelekezo mengine ambayo sio ya neno lake.

Kumbukumbu 34:10 “Wala hajainuka tena katika Israeli nabii kama Musa, ambaye Bwana alimjua uso kwa uso;”

Pamoja na ukuu wote aliokuwa nao Musa aliadhibiwa vikali pale aliposhindwa kuyatii maagizo ya Mungu .

Hesabu 20: 7-13 “Bwana akasema na Musa, akinena, Twaa ile fimbo, ukawakusanye mkutano, wewe na Haruni ndugu yako, ukauambie mwamba mbele ya macho yao utoe maji yake, nawe utawatokezea maji katika mwamba, na hivyo utawanywesha maji mkutano na wanyama wao. Musa akaitwaa hiyo fimbo kutoka mbele za Bwana kama alivyomwamuru. Musa na Haruni wakawakusanya kusanyiko mbele ya mwamba, akawaambia, Sikieni sasa, enyi waasi; je! Tuwatokezee maji katika mwamba huu? Musa akainua mkono wake akaupiga ule mwamba kwa fimbo yake mara mbili; maji yakatoka mengi, mkutano wakanywa na wanyama wao pia. Bwana akamwambia Musa na Haruni, Kwa kuwa hamkuniamini mimi, ili kunistahi mbele ya macho ya wana wa Israeli, basi kwa sababu hiyo, hamtawaingiza kusanyiko hili katika ile nchi niliyowapa. Maji haya ni maji ya Meriba; kwa sababu wana wa Israeli waliteta na Bwana, naye alijionyesha kuwa mtakatifu kati yao”.

Mtu anayeweza kufurahia Baraka za Mungu kwa vyovyote vile atakuwa mtu yule ambaye anafuata maagizo ya Mungu na kuyashika vilevile bila kuangalia mkono wa kushoto au wa kiume, ni muhimu kukaza injili tuliyoipokea na kukaa katika utuu na maagizo ya Bwana, 

Joshua 1:5-8 “Hapatakuwa mtu ye yote atakayeweza kusimama mbele yako siku zote za maisha yako; kama nilivyokuwa pamoja na Musa, ndivyo nitakavyokuwa pamoja na wewe; sitakupungukia wala sitakuacha. Uwe hodari na moyo wa ushujaa, maana ni wewe utakayewarithisha watu hawa nchi hii niliyowaapia baba zao ya kwamba nitawapa. Uwe hodari tu na ushujaa mwingi, uangalie kutenda sawasawa na sheria yote aliyokuamuru Musa mtumishi wangu; usiiache, kwenda mkono wa kuume, au wa kushoto, upate kufanikiwa sana kila uendako. Kitabu hiki cha torati kisiondoke kinywani mwako, bali yatafakari maneno yake mchana na usiku, upate kuangalia kutenda sawasawa na maneno yote yaliyoandikwa humo; maana ndipo utakapoifanikisha njia yako, kisha ndipo utakapositawi sana. Je! Si mimi niliyekuamuru? Uwe hodari na moyo wa ushujaa; usiogope wala usifadhaike; kwa kuwa Bwana, Mungu wako, yu pamoja nawe kila uendako.” 

Mungu atupe neema leo kukumbuka kufuata maagizo ya Mungu na kuyatii katika jina la Yesu Kristo wa Nazareth mwana wa Mungu aliye hai, Amen!

Rev. Innocent Kamote.

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima.

0718990796

Hata sasa Bwana ametusaidia!


1Samuel 7:12 “Ndipo Samweli akatwaa jiwe, na kulisimamisha kati ya Mispa na Sheni, akaliita jina lake Eben-ezeri, akisema, Hata sasa Bwana ametusaidia.


Utangulizi:
Ni muhimu kufahamu kuwa wana wa Israel, waliwahi kupigwa vibaya sana na kusambaratishwa mbele ya adui zao, swalala Israel kushindwa lilikuwa swala la aibu kubwa sana katika maisha yao, Wao walitambua kuwa Mungu yuko pamoja nao na hivyo isingeliweza kuwa rahisi kwao kushindwa vita, lakini bilia inaonyesha kuwa Israel walipigwa vibaya na wazee walifikiri kuwa endapo watalileta sanduku la agano labda huenda wangeweza kupata ushindi hata hivyo safari hii walipigwa vibaya na hata sanduku la agano lilichukuliwa mateka
1Samuel 4:1-11 “[Ikawa siku zile Wafilisti walikusanyika ili kupigana na Israeli,] nao Waisraeli wakatoka juu ya Wafilisti kwenda vitani;wakatua karibu na Ebenezeri ,nao Wafilisti wakatua huko Afeki. Nao Wafilisti wakajipanga juu ya Israeli; na walipopigana, Israeli wakapigwa mbele ya Wafilisti; wakauawa watu wa jeshi lao lililokuwa uwandani wapata watu elfu nne. Hata watu walipofika kambini, wazee wa Israeli wakasema, Mbona Bwana ametupiga leo mbele ya Wafilisti? Twende tukalilete sanduku la agano la Bwana toka Shilo hata huku, lije kati yetu, na kutuokoa katika mikono ya adui zetu. Basi wakatuma watu kwenda Shilo, nao wakalileta toka huko sanduku la agano la Bwana wa majeshi, akaaye juu ya makerubi; na Hofni na Finehasi, wana wawili wa Eli, walikuwako huko pamoja na sanduku la agano la Mungu. Na sanduku la agano la Bwana lilipoingia kambini, Israeli wote wakapiga kelele kwa sauti kuu, hata nchi ikavuma. Nao Wafilisti waliposikia mshindo wa zile kelele, walisema, Maana yake nini mshindo wa kelele hizi kubwa katika kambi ya Waebrania? Wakatambua ya kuwa sanduku la Bwana limefika kambini. Wafilisti wakaogopa, maana walisema, Mungu ameingia kambini. Wakasema, Ole wetu! Kwani halijawa jambo kama hili tangu hapo. Ole wetu! Ni nani atakayetuokoa na mkono wa miungu hawa walio hodari? Hawa ndio miungu waliowapiga Wamisri kwa mapigo ya kila namna jangwani. Iweni hodari, na kufanya kiume enyi Wafilisti, msije mkawa watumwa wa Waebrania, kama wao walivyokuwa watumwa wenu; fanyeni kiume, mkapigane nao. Wafilisti wakapigana nao, Israeli wakapigwa, wakakimbia kila mtu hemani kwake; wakauawa watu wengi sana; maana katika Israeli walianguka watu thelathini elfu wenye kwenda vitani kwa miguu. Hilo sanduku la Mungu Likatwaliwa; na Hofni na Finehasi, wale wana wawili wa Eli, wakauawa.”
Unaweza kuona tukio hili la kusikitisha ambalo lilitokea kabla Samuel hajawa Mwamuzi wa Israel, lilikuwa tukio la kusikitisha na lililoleta simanzi kubwa sana kwa wana wa Israel, jambo hili liliwapa kujitafakari kwa nini wamepoteza ushindi katika maisha yao! Israel waligundua siri ya kushindwa kwao vibaya katika vita hii na hivyo chini ya Samuel walijipanga tena kuutafuta uso wa Mungu wa Israel, kwani sababu ilikuwa wazi kuwa kushindwa kwao kulitokana na maisha yao ya kuabudu miungu na kumuacha Mungu wa kweli, sasa Israel walitambua kuwa wamekosa na hivyo walianza kutafuta ushindi. Kanuni za ushindi.

Mungu aliweza kuwajilia tena baada ya kufuata kanuni kadhaa na kuweza kuwasaidia na kuwapa Ushindi.
1Samuel 7:3-12Basi Samweli akawaambia nyumba yote ya Israeli, akasema, Ikiwa mnamrudia Bwana kwa mioyo yenu yote, basi, iondoleeni mbali miungu migeni, nayo Maashtorethi yatoke kwenu, mkamtengenezee Bwana mioyo yenu, mkamtumikie yeye peke yake; naye atawaokoa katika mikono ya Wafilisti. Ndipo wana wa Israeli wakayaondoa Mabaali na Maashtorethi, wakamtumikia Bwana peke yake. Samweli akasema, Wakusanyeni Israeli wote Mispa, nami nitawaombea ninyi kwa Bwana. Wakakusanyika huko Mispa, wakateka maji na kuyamimina mbele za Bwana; wakafunga siku ile, wakasema huko, Tumemfanyia Bwana dhambi. Samweli akawaamua wana wa Israeli huko Mispa. Hata Wafilisti waliposikia ya kuwa wana wa Israeli wamekusanyika huko Mispa, mashehe wa Wafilisti walipanda juu ili kupigana na Israeli. Nao wana wa Israeli waliposikia, wakawaogopa Wafilisti. Wana wa Israeli wakamwambia Samweli, Usiache kumlilia Bwana, Mungu wetu, kwa ajili yetu, kwamba atuokoe na mikono ya Wafilisti. Ndipo Samweli akatwaa mwana-kondoo mchanga, akamtolea Bwana sadaka ya kuteketezwa nzima; Samweli akamlilia Bwana kwa ajili ya Israeli; Bwana akamwitikia. Hata Samweli alipokuwa akiitoa hiyo sadaka ya kuteketezwa, Wafilisti wakakaribia ili kupigana na Israeli; walakini Bwana akapiga ngurumo, mshindo mkubwa sana, juu ya Wafilisti siku ile, akawafadhaisha; nao wakaangamizwa mbele ya Israeli.Nao watu wa Israeli wakatoka Mispa, wakawafuatia Wafilisti, wakawapiga, hata walipofika chini ya Beth-kari. Ndipo Samweli akatwaa jiwe, na kulisimamisha kati ya Mispa na Sheni, akaliita jina lake Eben-ezeri, akisema, Hata sasa Bwana ametusaidia. Hivyo Wafilisti walishindwa, wasiingie tena ndani ya mipaka ya Israeli; na mkono wa Bwana ulikuwa juu ya Wafilisti siku zote za Samweli. Nayo miji ile Wafilisti waliyokuwa wamewapokonya Waisraeli ilirudishwa tena kwa Israeli, tokea Ekroni mpaka Gathi; na Waisraeli wakauokoa mpaka wake mikononi mwa Wafilisti. Tena kulikuwa na amani kati ya Israeli na Waamori. Naye huyo Samweli akawaamua Israeli siku zote za maisha yake.”
Unaweza kuona Israel walipata ushindi mkubwa baada ya kuchukua hatua za kurejea katika kanuni za kimungu zilizowapa ushindi.
1. Waloimrudia Bwana kwa Moyo yaani walitubu na kuacha dhambi zao hususani za kuabudu miungu.
2. Walimtumikia Mungu yaani walimuabudu kwa moyo safi.
3. Waliteka maji na kuyamimina mbele za Bwana – kumimina maji ni lugha ya fumbo ambayo maana yake ni kuanguka chini na kuomba Zaburi 22:14 “Nimemwagika kama maji, Mifupa yangu yote imeteguka, Moyo wangu umekuwa kama nta, Na kuyeyuka ndani ya mtima wangu.” Hivyo Israel walianguka chini na kufanya maombi ya unyenyekevu yaliyoambatana na kufunga.
4. Walimuomba Samuel Nabii awaombeee kwa Mungu na kuwa asiache kuwa mwombezi katikati yao Samuel aliwaombea na Mungu alimjibu.
5. Kisha Maadui wa Israel waliinuka tena na safari hii walipigwa vibaya na kutolewa nje kabisa.
Ni ukweli ulio wazi kuwa Mungu aliwasaidia sana Israel, katika mji uleule mahali walipopigwa vibaya waliwashinda adui zao na kuwapiga vinbaya na kujikomboa, ni ukweli uliowazi kuwa Samuel alijua kuwa Mungu nsasa ameanza kuwasaidia watu wake, na alitaka kuweka kumbukumbu ya ushindi ule kwa jiwe alilolisimamisha na Kupaita mahali Pale EBEN-EZER yaani hata sasa Mungu ametusaidia.
Je maisha yako ni ya ushindi? Ni wapi umekwama Mungu anakupa nafasi ya kumrudia yeye na kuumimina moyo wako kwake, ni muhimu kukumbuka kuwa tunaye mwomnbezi, Yesu Kristo yeye ni Jiwe lililo hai, yeye ni muombezi wetu anatuombea na atatupa ushindi tukiwa naye hakuna kitu kitaweza kusimama mbele yetu, Israel waliwezakupata ushindi na adui hakuweza kusimama mbele yao siku zote za Samuel, Tunaweza kuwa na ushindi tukiwa na kuhani mwombezi aliyeketi mkono wa kuume wa Mungu baba naye anatuombea siku zote yeye ndiye kipatanisho kati yetu na Mungu, yeye ndiye chanzo cha ushindi wetu, Yeye ni Ebenezaer Jiwe la ushindi wetu, hata kama kulikuwa na historia ya kushindwa yeye Mungu wetu atatupa ushindi, na kuifuta historia ya kushindwa kwetu na kuwa ushindi wetu.
Na Rev. Innocent Kamote.
Mkuu wa Wajenzi mwenye Hekima.

Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba

Wafilipi 4:6-7 “Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu. Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu."
 
 Unapokuwa umemtegemea Mungu huna sababu ya kuogopa Yeye yu pamoja nawe Zaburi 118:6

Utangulizi:
Neno usijisumbue lilikuwa ni moja ya Misingi mikubwa katika Mafundisho ya Bwana Yesu Mathatyo 6:25, 34 zinasema “Kwa sababu hiyo nawaambieni, Msisumbukie maisha yenu, mle nini au mnywe nini; wala miili yenu, mvae nini. Maisha je! Si zaidi ya chakula, na mwili zaidi ya mavazi?, Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake.”

Msisumbuke!

Mungu katika mapenzi yake hataki sisi tusumbuke yaani tujiumize kwa mashaka na wasiwasi kama wasioamini, Usumbufu huu ni usumbufu wa Moyo uitwao “ANXIETY”ambalo maana yake ni kuogopa au kuhofia au kutetemeka kwaajili ya jambo fulani linalohuisiana na maisha, Kama tutafikiri kwa akili zetu za kibinadamu kwa jambo lolote gumu katika maisha yetu ni dhahiri kuwa tutazama katika masumbufu na mashaka , lakini kama tutamshirikisha Mungu ukweli wa kimaandiko ni kuwa tutakuwa juu ya mashaka yetu

Mithali 3:5-6 “.Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote, Wala usizitegemee akili zako mwenyewe; Katika njia zako zote mkiri yeye, Naye atayanyosha mapito yako.”

Watakatifu waliotutangulia walikuwa na ufahamu wa kutosha kuwa kila unapokutana na changamoto za aina yoyote hupaswi kujisumbua katika jambo lolote zaidi ya kuomba na kumshukuru Mungu yaani kumfanyia bwana ibada, Petro huenda alikuwa na ujuzi na uzoefu kuwa kila changamoto mitume waliweza kuikabili kwa maombi, walipofadhaika walimwambia Mungu,lakini sio hivyo tu bali hata manabii walipokuwa na changamoto waliweza kuomba Ndugu zango hata leo maombi ndio ufunguo wa kukomesha aina yoyote ya mashaka na wasiwasi, hofu na kuleta majibu ya maswali magumu katika masha yetu.

1. Tumtwike yeye fadhaa zetu zote 1Petro 5:6-7Basi nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake; huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu.” Mtume Petro alikuwa na ujuzi wa kutosha kuwa kila unapokutana na changamoto zozote unapaswa kumtwika Mungu swala hilo kisha kustarehe ku “relax” ni wazi kuwa mitume na watakatifu waliotutangulia walikuwa na uelewa huu wazi kuwa linapokuja swala linalosumbua moyo unalipeleka katika maombi kisha unaamini kuwa Mungu atashughulikia na ni kweli atalishughulikia! Unaona angalia walivyofanya walipokutana na changamoto hapa chini katika Matendo 4;24-31 waliomba na Mungu aliwatia nguvu.

2. Matendo 4:24-31Nao waliposikia, wakampazia Mungu sauti zao kwa moyo mmoja, wakisema, Mola, wewe ndiwe Mungu, ndiwe uliyefanya mbingu na nchi na bahari na vitu vyote vilivyomo; nawe ulinena kwa Roho Mtakatifu kwa kinywa cha babaetu Daudi, mtumishi wako, Mbona mataifa wamefanya ghasia, Na makabila wametafakari ubatili? Wafalme wa dunia wamejipanga, Na wakuu wamefanya shauri pamoja Juu ya Bwana na juu ya Kristo wake. Maana ni kweli, Herode na Pontio Pilato pamoja na Mataifa na watu wa Israeli, walikusanyika katika mji huu juu ya Mtumishi wako mtakatifu Yesu, uliyemtia mafuta, ili wafanye yote ambayo mkono wako na mashauri yako yamekusudia tangu zamani yatokee. Basi sasa, Bwana, yaangalie matisho yao; ukawajalie watumwa wako kunena neno lako kwa ujasiri wote, ukinyosha mkono wako kuponya; ishara na maajabu vifanyike kwa jina la Mtumishi wako mtakatifu Yesu. Hata walipokwisha kumwomba Mungu, mahali pale walipokusanyika pakatikiswa, wote wakajaa Roho Mtakatifu, wakanena neno la Mungu kwa ujasiri.”

3. Daniel 6:10Hata Danieli, alipojua ya kuwa yale maandiko yamekwisha kutiwa sahihi, akaingia nyumbani mwake, (na madirisha katika chumba chake yalikuwa yamefunguliwa kukabili Yerusalemu;) akapiga magoti mara tatu kila siku, akasali, akashukuru mbele za Mungu wake, kama alivyokuwa akifanya tokea hapo.” Unaweza kuona pia kwa Daniel ni wazi kuwa ni mapenzi ya Mungu kwamba tusijisumbue katika neno lolote, tusiogope lolote, tuombe Mungu hata kama swala hilo liko kinyume na serikali, liko kinyume na wafalme, madam liko kinyume na mapenzi ya Mungu wewe omba tu kisha Mungu atalijibu mtegemee yeye, relax kama mtu aliyeruka na parachute.

Ushindi wetu na uthabiti wetu uko katika maombi na kumtegemea Mungu na sio kuogopa, na Ukiisha kumuomba Mungu furahi na kutulia.

Na mkuu wa wajenzi mwenye Hekima
Rev. Innocent Kamote