Jumapili, 24 Januari 2021

Nyumba juu ya Mwamba!


Mathayo 7:24-27Basi kila asikiaye hayo maneno yangu, na kuyafanya, atafananishwa na mtu mwenye akili, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba; mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, isianguke; kwa maana misingi yake imewekwa juu ya mwamba. Na kila asikiaye hayo maneno yangu asiyafanye, atafananishwa na mtu mpumbavu, aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga; mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, ikaanguka; nalo anguko lake likawa kubwa.


Utangulizi:

Kristo Yesu alipokuwa duniani aliishi kama mtenda kazi awaye yote  katika Bwana akiwa na karama na vipawa mbalimbali vya Roho moja ya karama aliyokuwa nayo ilikuwa ni karama ya ualimu,uwezo wake na mamlaka aliyokuwa nayo katika kufundisha iliwafanya wale waliomsikiliza wakubwa kwa wadogo kushangazwa sana na uweza wake wa kufundisha ona

Mathayo 7:28-29 “Ikawa, Yesu alipoyamaliza maneno hayo, makutano walishangaa mno kwa mafundisho yake; kwa maana alikuwa akiwafundisha kama mtu mwenye amri, wala si kama waandishi wao
”.

Makutano wengi walifurahishwa sana na kukubaliana na mafundisho yake, lakini sio wao tu hata watu wakubwa na wenye cheo na mamlaka walimkubali Yesu kuwa ni Mwalimu wa kweli na kuwa Mungu yuko pamoja naye ona

Yohana 3:1-2 “Basi palikuwa na mtu mmoja wa Mafarisayo, jina lake Nikodemo, mkuu wa Wayahudi.Huyo alimjia usiku, akamwambia, Rabi, twajua ya kuwa u mwalimu, umetoka kwa Mungu; kwa maana hakuna mtu awezaye kuzifanya ishara hizi uzifanyazo wewe, isipokuwa Mungu yu pamoja naye.

Moja ya sifa kubwa sana ya Yesu Katika mafundisho yake ilikuwa ni uwezo wake wa kutumia mifano iliyo hai inayoeleweka vema kama daraja la kuwasaidia wpte waliomzunguka kumuelewa kwa wepesi, Mafundisho ya Yesu yalieleweka kwa watu wa kila Nyanja wakiwemo wasomo na watu wa kawaida, alitumia mifano mbali mbali iliyojumuisha maisha ya kila siku ya jamii yake nay a watu wake mfano alizungumza mifanyo ya Nyanja ya uvuvi, afya, mizabibu, mashamba, mbweha, matajiri na masikini, ndege, maisha ya kawaida, fedha lakini vilevile katika maswala ya ujenzi kama ilivyo katika mfano huu tutakaouchambua leo!

Makusudi makuu ya Yesu kutumia mifano ilikuwa ni kuleta uelewa wa ndani zaidi kwa wasikilizaji wake na kuleta matokeo makubwa ikiwemo kubadilisha maisha yao na kuwasaidia kuelewa makusudi ba mpango wa Mungu kwetu!

Mfano wa Mjenzi mwenye Hekima na Mjenzi mpumbavu.

Mfano huu Yesu aliweza kuuelezea kama kilele cha Mafunisho yake akitaka wale walioyasikia mafundisho yake waweze kuyafanyia kazi, kwa hiyo ulikuwa ni mfano unaosimama kama msumari wa moto kugongelea umuhimu wa kuishi kile ambacho yeye amekifundisha, Yesu alikuwa Carpenter yaani mjenzi alikulia na kujifunza maswala ya ujenzi, na hivyo alifahamu kuwa nyumba imara huwa inajengwa namna gani, uimara wa nyumba ni msingi wake  aidha uende chini sana au ujengwe juu ya Mwamba, lakini sio hivyo tu iwe na uwezo wa kustahimili mikimikiki ya Mafuriko, maji na pepo kali,

Yesu alikuwa akikazia mfano huu kuwataka wote wanaomuamini, wajue kuwa hawajamaliza kazi, Mwanafunzi makini wa Yesu Kristo ni yule anayejifunza kusikia na kutii au kuyafanyia kazi mafundisho ya Yesu Kristo ona

Luka 6:46-49
Na kwa nini mnaniita, Bwana, Bwana, walakini hamyatendi nisemayo? Kila mtu ajaye kwangu, na kuyasikia maneno yangu na kuyatenda, nitawaonyesha mfano wake. Mfano wake ni mtu ajengaye nyumba, na kuchimba chini sana, na kuweka msingi juu ya mwamba; na kulipokuja gharika, mto uliishukia nyumba ile kwa nguvu, usiweze kuitikisa; kwa kuwa imejengwa vizuri. Lakini yule aliyesikia ila hakutenda, mfano wake ni mtu aliyejenga nyumba juu ya ardhi pasipokuwa na msingi, mto ukaishukia kwa nguvu, ikaanguka mara; na maangamizi yake nyumba ile yakawa makubwa.

Neno la Mungu linatuagiza kuwa watendaji wa neno na sio wasikiaji tu, nykati za leo kumekuwepo na wimbi kubwa sana la wakristo ambao msingi wao hauko katika neno la Mungu, na wahubiri pia msingi wao uko katika miujiza tu na matyokeo yake wameendelea kuwa wachanga wakichukuliwa huku na huko na upepo wa kila namna wa Elimu, Kusudi la kuwepo kwa karama zote tano za huduma ni ili mwili wa Kristo ujengwe watu wakomae wafikie kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo wasiwe watu wa kuyumbishwa huku na kule ona

Waefeso 4:11-15
Naye alitoa wengine kuwa mitume, na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wainjilisti na wengine kuwa wachungaji na waalimu; kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, hata kazi ya huduma itendeke, hata mwili wa Kristo ujengwe; hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na kumfahamu sana Mwana wa Mungu, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo; ili tusiwe tena watoto wachanga, tukitupwa huku na huku, na kuchukuliwa na kila upepo wa elimu, kwa hila ya watu, kwa ujanja, tukizifuata njia za udanganyifu. Lakini tuishike kweli katika upendo na kukua hata tumfikie yeye katika yote, yeye aliye kichwa, Kristo.” Unaona Karama zote za huduma zimetolewa kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, kwa kusudi la kuwajenga watu wakomae, Leo hii watu wengi wamekuwa wakifukuzia miujiza, akiinuka muhubiri huyu na miujiza wanahama huku na kule kwa sababu hawana msingi katika neno, lakini hata wahubiri pia wameshindwa kubalance/ kuweka sawa mzani sikatai kuwa miujiza ni ya muhimu sana na ndio maana hata Yesu aliifanya lakini kulitendea kazi neno la Mungu ni muhimu zaidi kuliko miujiza Biblia inaonya watu wanaofanya muujiza lakini hawayafanyi wala kuyaishi yale Kristo anayoyataka ona  maonyo ya yesu mwenyewe

Mathayo 7:21-23 “Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni. Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu.”
 

Kipimo kikubwa cha uendeleaji mwema wa Kikristo ni kulitendea kazi neno na sio vinginevyo, watu wanapaswa sasa kuwa na kiu ya kutafuta kujifunza neno la Mungu kuliko kuhangaika huku na kule wakitafuta miujiza ambayo ni ya kitoto tu kwani ni ya Muda mfupi na wale waitendao na hata wanaotenda hufariki dunia, Mkristo mkomavu ni yule anayejifunza neno la Mungu na kukaa katika neno huku akilifanyia kazi kinyume na hapo ni kujidanganya ona


Yakobo 1:22-25 “Lakini iweni watendaji wa neno, wala si wasikiaji tu, hali mkijidanganya nafsi zenu. Kwa sababu mtu akiwa ni msikiaji wa neno tu, wala si mtendaji, mtu huyo ni kama mtu anayejiangalia uso wake katika kioo. Maana hujiangalia, kisha huenda zake, mara akasahau jinsi alivyo. Lakini aliyeitazama sheria kamilifu iliyo ya uhuru, na kukaa humo, asiwe msikiaji msahaulifu, bali mtendaji wa kazi, huyo atakuwa heri katika kutenda kwake.”
  

Unaona neno la Mungu halitaki blaablaa wala unafiki linataka watu walitendee kazi, hiyo ndio akili kinyume cha hapo ni upumbavu, Neno la Mungu linatupa changamoto leo kuwa tusiwe wasikiaji tu bali tuwe watendaji, ni muhimu kujikumbusha kuwa kutoa pepo na kutoa unabii pekee hakutoshi, kwa kuingia katika ufalme wa Mungu wote tunapewa wito wa kulifanyia kazi neno, na kisha wote wenye karama za huduma yaani walimu, wachungaji, wainjilishi, manabii na mitume tumeitwa kuimarisha kanisa na kulijenga na sio kufanya miujiza peke yake, waamini nanyi mnapaswa kujifunza neno la Mungu na kukaa katika hilo, watu wanapaswa kumjua Yesu, huduma zetu zinapaswa kumtambulisha yesu zaidi kuliko sisi wenyewe, huduma zetu ziwaelekeze watu kwa Yesu, tusiwe busy kutafuta umaarufu au kufanya miujiza na hatimaye tukawa maarufu kumshinda Yesu, tunapaswa kuwa makini ili katika huduma zetu tufanyazo kipaumbele kisiwe sisi bali Yesu! Mkazo wetu uwe kuyatendea kazi yale Bwana aliyotuangiza hata kama si kwa ukamilifu lakini huo ndio uwe mwelekeo wetu Kama tunampenda Yesu tutazishika amri zake

Yohana 14:15 “Mkinipenda, mtazishika amri zangu.”
Mfano wa mjenzi ni mfano rahisi kueleweka kwamba mwanafunzi imara ni yule anayesikiliza na kutii walimu wake na kuyatendea kazi yake anayoagizwa, tukiishi hivyo na tukimuomba Mungu then Mungu atafanya sehemu yake na neema yake itakuwa juu yetu, Yohana 13;17 “ Mkiyajua hayo, heri ninyi mkiyatenda.”

Mathayo 7:24-27Basi kila asikiaye hayo maneno yangu, na kuyafanya, atafananishwa na mtu mwenye akili, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba; mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, isianguke; kwa maana misingi yake imewekwa juu ya mwamba. Na kila asikiaye hayo maneno yangu asiyafanye, atafananishwa na mtu mpumbavu, aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga; mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, ikaanguka; nalo anguko lake likawa kubwa.

Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima!




Jumapili, 17 Januari 2021

Wapandao kwa machozi watavuna kwa kelele za furaha!

Zaburi 126:1-6Bwana alipowarejeza mateka wa Sayuni, Tulikuwa kama waotao ndoto. Ndipo kinywa chetu kilipojaa kicheko, Na ulimi wetu kelele za furaha. Ndipo waliposema katika mataifa, Bwana amewatendea mambo makuu.  Bwana alitutendea mambo makuu, Tulikuwa tukifurahi. Ee Bwana, uwarejeze watu wetu waliofungwa, Kama vijito vya Kusini. Wapandao kwa machozi Watavuna kwa kelele za furaha. Ingawa mtu anakwenda zake akilia, Azichukuapo mbegu za kupanda. Hakika atarudi kwa kelele za furaha, Aichukuapo miganda yake.”

Utangulizi:

Zaburi ya 126 ni mojawapo ya zaburi zilizoitwa zaburi za kupandia yaani ziliimbwa wakati watu wanapanda kwenda nyumbani mwa bwana Hekaluni aidha pia ni zaburi ya kihistoria inayoelezea maisha  ya wana wa Israel hususani Wayahudi waliorudi kutoka uhamishoni Babeli, Wayahudi hao walichukuliwa mateka wakati wa Mfalme Nebukadreza kwa kusudi la kuwatumikisha hivyo waliishi uhamishoni kama watumwa walifanyishwa kazi kwa faida ya taifa la wakaldayo, Hata hivyo baada ya miaka kadhaa kupita Mungu aliwajia tena watu wake na kuwaletea ukombozi, yaani walirejea katika nchi yao kwa amri ya mfalme Koreshi, makundi matatu ya wayahudi walirejea nyumbani kundi la Kwanza wakati wa Zerubabel na kundi la pili wakati wa Ezra na la tatu wakati wa Nehemia  hivyo inaaminika kuwa zaburi hii inaaminika iliimbwa na wana wa Asafu waliorejea kutoka uhamishoni wakati wa Ezra ona

Ezra 2:1-2, 41. “1. Basi hawa ndio wana wa wilaya, waliokwea kutoka katika ule uhamisho wa hao waliokuwa wamechukuliwa, ambao Nebukadneza, mfalme wa Babeli, aliwachukua mateka mpaka Babeli, nao wakarudi Yerusalemu na Yuda, kila mtu mjini kwake; 2. ndio hawa waliokuja pamoja na Zerubabeli, Yoshua, Nehemia, Seraya, Reelaya, Mordekai, Bilshani, Mispari, Bigwai, Rehumu, na Baana. Hii ndiyo hesabu ya wanaume wa watu wa Israeli; 41 Waimbaji; wana wa Asafu, mia moja ishirini na wanane.”


Wimbo huu ulijulikana kama wimbo wa kupandia yaani wayahudi walikuwa wakiuimba kila wakati walipokuwa wakipanda kwenda Yerusalemu kuabudu Hekaluni,  Kumbuka kuwa Nyumba ya Mungu yaani Hekalu lilijengwa juu yam lima yaani sayuni na hivyo mara kwa mara mtu alipoenda nyumbani kwa Bwana ilikuwa ni kama anapanda, Zaburi hii ilitungwa na wana wa Asafu wakati wa Ezara  na wimbo huu ulitumika katika maeneo makuu matatu kushukuru, kuomba na kutia moyo

1.       Kama njia ya kumshukuru Mungu kwa wale waliokuwa wamerejea kutoka utumwani  kwamba Mungu alikuwa amewatendea mambo makubwa sana amewakomboa amewapa uhuru, nyakati za ukoloni wa kizamani mataifa yenye nguvu walipowateka watu waliwachukua kuwa watumwa katika nchi zao, ni watu wa ulaya kama Wayunani na warumi ndio walioanzisha iana ya utumwa au utawala wa kumtawala mtu katika taifa lake lakini wakaldayo na mataifa ya kale waliua watu na wengine waliwahamisha  hivyo kurudi nyumbani hasa wayahudi  kurudi Israel kwao ni Muujiza mkubwa sana ni kurudi katyika uwepo wa Mungu ni jambo la kushangaza mataifa hivyo katika zaburi hii wanashukuru kurejea nyumbani

Zaburi 126:2-3
unaonyesha “Ndipo kinywa chetu kilipojaa kicheko, Na ulimi wetu kelele za furaha. Ndipo waliposema katika mataifa, Bwana amewatendea mambo makuu. Bwana alitutendea mambo makuu, Tulikuwa tukifurahi.


2.   Aidha wimbo huu pia ulitumika kuwaombea dua na kuwatia moyo  na kuwataka wale ambao bado walikuwa wamesalia huko utumwani kuendelea kumuomba Mungu ili nao waweze kutoka katika utumwa  walikumbuka kuwa wako ndugu zao ambao bado hawajarejea hivyo walitoa wito na kumsihi Bwana awarejeza ndugu zao walioko kifungoni utumwani nchi ya mbali  ona   

       Zaburi126:4Ee Bwana, uwarejeze watu wetu waliofungwa, Kama vijito vya Kusini.”

3.  Na eneo la tatu lilitumika kuwatia moyo watu wote waliokuwa wanapitia shida za aina yoyote na changamoto za aina yoyote katika maisha kuwa maisha yao wanayoyapitia ya aina yoyote ile yanafananishwa na maisha ya mkulima na kuwa mtu awaye yote anapopitia taabu na machungu ya aina Fulani ni lazima aelewe kuwa wakati huo katika maandiko unafananishwa na wakati wa kupanda, kupanda kunajumuisha maandalizi ya shamba, kulima na kukatua ardhi  na ujuzi wa nyakati kwamba mvua zitaanza lini? huu ni wakati wa taabu na shida ambayo inahitaji uvumilivu  na kwa kweli wakati wa kuandaa shamba mpaka kupanda ndio wakati Mgumu sana kwa mkulima kuliko wakati wa kuvuna, wakati wa kuandaa shamba na kupanda wakulima wengi hawaonekani mjini wala nyumbani, wanaamka mapema sana kwenda shambani ili walime kabla jua halijawa kali, wakulima hupata taabu sana wanapojiandaa kupanda kwa huku wakijua kuwa uko wakati watafurahia mavuno hivyo kipindi hiki ni kipindi cha machozi.  Wana wa Asafu wanafananisha kipindi cha kupanda kama kipindi cha machozi na wakati wa kuvuna kama wakati wa furaha,  ona

Zaburi 126:5-6 Wapandao kwa machozi Watavuna kwa kelele za furaha.Ingawa mtu anakwenda zake akilia, Azichukuapo mbegu za kupanda. Hakika atarudi kwa kelele za furaha, Aichukuapo miganda yake.”

Ni muhimu kufahamu hili kuwa maisha ya mwanadamu yana nyakati tofauti tofauti na kila wakati una umuhimu wake na wakati mwingine wakati mmoja una maana sana kwaajili ya wakati mwingine na kila wakati ni muhimu mno  kwa msingi huo ni muhimu kufahamu majira na nyakati ili uweze kujipanda vema kujua kuwa wakatio huu ni wa kupanda au wa kuvuna ukichanganya nyakati utapata tabu sana !  huwezi kuishi maisha ya mavuno wakati wa kipindi cha kupanda ukifanya hivyo utapata hasara kubwa sana ona

Muhubiri 3:1-8 “Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu. Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa; Wakati wa kupanda, na wakati wa kung'oa yaliyopandwa; Wakati wa kuua, na wakati wa kupoza; Wakati wa kubomoa, na wakati wa kujenga; Wakati wa kulia, na wakati wa kucheka; Wakati wa kuomboleza, na wakati wa kucheza; Wakati wa kutupa mawe, na wakati wa kukusanya mawe; Wakati wa kukumbatia, na wakati wa kutokumbatia; Wakati wa kutafuta, na wakati wa kupoteza; Wakati wa kuweka, na wakati wa kutupa; Wakati wa kurarua, na wakati wa kushona; Wakati wa kunyamaza, na wakati wa kunena; Wakati wa kupenda, na wakati wa kuchukia; Wakati wa vita, na wakati wa amani.”

Maisha yetu yanapofananishwa na nyakati zozote za taabu katika Biblia wakati huo unafananishwa na wakati wa kupanda “it’s a labour time” ni wakati wa taabu ni wakati wa subira ni wakati wa uvumilivu, wakulima huwa wanajitoa muhanga sana wakati wa kupanda yaani kuandaa mashamba kukatua ardhi huku wakivizia wakati sahihi wa kufanya hivyo, sasa wanadamu wenye akili timamu wanapaswa kujua ni namna gani watacheza au wataenenda na mapigo ya huo wakati, huwezi kuishi wakati wa kupanda kama ndio wakati wa kuvuna ni lazima ujue nyakati kwani wakati mmoja hutengeneza wakati mwingine, mtu akiishi kwa anasa wakati wa kupanda atakuwa na msiba wakati wa mavuno, maana wenzake walivumilia wakajitoa kupanda hivyo wakati wa mavuno watafurahi, wakati wa kupanda ni wakati wa subira na uvumilivu wala sio wakati wa kupendeza, maandiko yanavyotuasa wakati wote tutapopitia changamoto zinazotuonyesha kuwa ni kama tuko katika wakati wa kulia, au tuko katika wakati wa kufanya kazi  ni wakati ambao unahitaji uvumilivu kwani hatimaye Mungu ataleta mvua na mazao yatakua na tutavuna kwa furaha kubwa on

Yakobo 5:7-8,,10 -11 “7. Kwa hiyo ndugu, vumilieni, hata kuja kwake Bwana. Tazama, mkulima hungoja mazao ya nchi yaliyo ya thamani, huvumilia kwa ajili yake hata yatakapopata mvua ya kwanza na ya mwisho. 8. Nanyi vumilieni, mthibitishe mioyo yenu, kwa maana kuja kwake Bwana kunakaribia.10-11 “10. Ndugu, watwaeni manabii walionena kwa jina la Bwana, wawe mfano wa kustahimili mabaya, na wa uvumilivu.11. Angalieni, twawaita heri wao waliosubiri. Mmesikia habari ya subira yake Ayubu, mmeuona mwisho wa Bwana ya kwamba Bwana ni mwingi wa rehema, mwenye huruma.”

Kimsingi neno la Mungu linatujuza kuwa uko wakati Mungu atatutendea mema, jambo kubwa la msingi ni kujua nyakati ni kuwa na hekima na ujuzi kwamba wakati huu ni wakati wa  namna gani na ni jambo gani tunapaswa kulifanya  tusiishi kizemba kumbuka  katika Israel kulikuwa na Kabila moja waliojulikana kama wana wa Isakari hawa waliitwa watu wenye akili sana na kazi yao kubwa walikuwa ni watu wenye kujua nyakati sio tu kujua nyakati bali pia kujua jambo gani linapaswa kutendeka kwa wakati huo ona

1Nyakati 12:32 “Na wa wana wa Isakari, watu wenye akili za kujua nyakati, kuyajua yawapasayo Israeli wayatende; vichwa vyao walikuwa watu mia mbili na ndugu zao wote walikuwa chini ya amri yao
”. 

Kila mmoja wetu anapaswa kujua nyakati na kuwa na akili kama wana wa isakari kujua nini kinatupasa kutenda kwa wakati, mwezi januari mpaka machi ni miezi muhimu sana kwa wanafunzi na walimu kujipanga kufundisha kwa bidii na kujifunza kwa bidii  katika wakati huu wa mwanzo kama hatutajua yatupasayo kufanya tukajifanya tunacheka na kumbe ni wakati wa kulia  tunaweza kujikuta tunakosea, mkulima anapaswa kujua wakati huwezi kupanda wakati wa hari, kama mwanafunzi anataka kustarehe wakati anajua wazi ni wakati wa kujisomea kwa bidii wakati wake wa mavuno utakuwa wakati wa majuto matokeo yatakapotoka anaweza kulia badala ya kufurahi kwa vile hakufahamu ni wakati gani alipaswa kusoma kwa bidii, wote tunajua kuwa ni mbaya sana mwanafunzi kuja na simu shuleni, wazazi pia wanapaswa kufahamu, unampa mtoto simu aje nayo shuleni atasomaje? Hii ni sawa na kuutumia wakati vibaya au kutokujua wakai na jambo la kufanya kwa wakati huo, huwezi kuchanganya masomo na mapenzi, au uvutaji wa bangi na tabia za ajabu ajabu wakati ukiwa mwanafunzi au kutumia ulevi au kufanya biashara ni dhahiri kuwa huo sio wajati wa kufanya hayo kila mmoja anapaswa kufahamu kuwa kuna wakati wa kupanda wakati huu huwa kama wakati mchungu lakini kuna wakati wa kuvuna huu ni wakati ambapo tutayafurahia matunda ya kazi zetu, tunapoanza shughuli za kila aina mwanzoni mwa mwaka huu basi na tufanye kazi kwa bidii sana kama tupandao,lipa ada ya shule kama uliila wakati wa disemba hukujua kuwa kuna januari hukutofautisha wakati wa kupanda na wakati wa kuvuna? Ahaa ulivuna kabla ya kupanda sisi tutakudai ada ya shule tu!  Wakati ukiwa shuleni mwanafunzi  tujisiomee kwa bidii, tuhudhurie kazini kwa bidii, tuombe na kufanya ibada na  kila lililowajibu wetu kwa bidii tukijua wazi kuwa wapandao kwa machozi watavuna kwa kelele za furaha  na Mungu atatupa wakati wa faraja hatatuacha tuumie tu atakuwa pamoja nasi na tutafurahia uwepo wake kwa nguvu na ushujaa mwingi ataleta mvua yaani neema atayakuza mapando yetu na atatupa wakati wa mavuno, wakati wa matokeo mazuri, wakati wa kuvuna kwa hiyo ni muhimu kwetu tunapoendelea na wiki hii ya kazi ndani ya mwaka huu 2021 tujitoe kwa ngubvu zetu zote tukijua ya kuwa wapandao kwa machozi watavuna kwa kelele za furaha !   .

Wimbo wa Marehemu Fanuel sedekia unatukumbusha umuhimu wa kujua Majira na nyakati na kuzitumia kwa utukufu wa Mungu:-

Nitaimba haleluya asubuhi, nitaimba haleluya Mchana, nitaimba haleluya jioni haleluya na hata usiku X2, Muhubiri anasema kila jambo na wakati wake; wa kupanda na kuvuna wa kulia na kucheka x2  Haleluya nina wimbo; wa kila  wakati na kila majira wimbo wa nyakati zote na marira yote;  wimbo huo ni Haleluya Nitaimba haleluya asubuhi, nitaimba haleluya Mchana, nitaimba haleluya jioni haleluya na hata usiku X2,  – Fanuel Sedekia

Na Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima       

Jumapili, 27 Desemba 2020

Usimwambie Yakobo neno la heri wala la Shari!

Mwanzo 31:24 “Mungu akamjia Labani, Mshami, katika ndoto ya usiku, akamwambia, Ujihadhari, usimwambie Yakobo neno la heri wala la shari.     


Utangulizi:

Je umewahi kupitia mambo magumu katika maisha yako mpaka unaamua kukimbia? Umewahi kupitia mitihani mizito mpaka unaamua kufanya maamuzi magumu?  Maisha ya Yakobo yaani Israel duniani hayakuwa mepesi kama tunavyoweza kufikiri, alipitia mambo magumu mno, alipitia maisha ya taabu na dhiki kuliko Ibrahimu na Isaka baba zake ona

Mwanzo 47:7-9 “Yusufu akamleta Yakobo babaye ndani akamweka mbele ya Farao Yakobo akambariki Farao.  Farao akamwuliza Yakobo, Je! Siku za miaka ya maisha yako ni ngapi? Yakobo akamjibu Farao, Siku za miaka ya kusafiri kwangu ni mia na thelathini; siku za miaka ya maisha yangu zimekuwa chache, tena za taabu, wala hazikufikilia siku za miaka ya maisha ya baba zangu katika siku za kusafiri kwao.”

Moja ya maeneo ambayo huenda Israel aliyakumbuka katika taabu alizozipitia ni pamoja na maisha yake  ya ujombani, alikokuwa akimtumikia Laban Mjomba wake, Hatimaye Yakobo na wake zake na wanae waliamua kuondoka kwa mjomba kwa kutoroka bila hata kuaga kwa kuhofia kuwa huenda Labani atamuonea tena Yakobo kama alivyomuonea siku zote za maisha yake, Hata hivyo Labani aligundua kutoroka kwa Yakobo na kuwa msafara wake ulikuwa ukielekea Gilead akamuwahi na kumkuta baada ya wiki nzima

Mwanzo 31:21-23 “Basi akakimbia yeye na yote aliyokuwa nayo; akaondoka akauvuka mto, akaelekeza uso wake kwenda mlima wa Gileadi. Hata siku ya tatu Labani akaambiwa ya kwamba Yakobo amekimbia, akatwaa ndugu zake pamoja naye, akamfuata mwendo wa siku saba. Akampata katika mlima wa Gileadi.”

Hatuwezi kujua kuwa Labani alikusudia kumfanya nini Yakobo? Hatujui nini kilikuwa katika akili zake lakini bila shaka alikuwa amenogowa na utumishi wa Yakobo, alitamani kuendelea kumfanya yakobo kuwa mtumwa wake siku zote, hakufikiri wala kutamani kuona kuwa siku moja Yakobo anakuwa huru, anamuabudu Mungu wa baba zake kwa uhuru, ana kuwa na kabila zake mwenyewe, anajitawala na kutimiza hivyo kusudi la Mungu, labani alikuwa ni muabudu miungu, hakuweza kujua kusudi la Mungu ndani ya Yakobo. Lakini alikuwa na hisia zilizowazi kuwa mtu huyu anaye Mungu aliye hai, anajua na kufahamu kuwa Yakobo alitajirika kwa jasho lake huku Mungu wa baba zake akiwa ameweka mkono wake kumbariki mtu huyu aliyeonewa na kupangiwa maisha tangu siku ya kwanza, Labani asingeweza kukubali hata kidogo kumuachia Yakobo kama farao alivyokataa kuwaachia wana wa Israel Kule misri baadaye, Yako mambo ambayo ulimwengu hauwezi kukubali kutuachia wala shetani hakubali kukuachia kwa sababu uweza wa Mungu uko juu yako na adui zako wanafaidika na uwepo wako, Africa wazungu hawawezi kukubali kukuachia ujitawale hawawezi kukuacha uchakate kila ulicho nacho kwa sababu wanafaidika na utumwa wako, wakati mwingine ili tuweze kuwa huru katika eneo Fulani ni mpaka Mungu aingilie kati, na Mungu huingilia kati pale anapoona tu mechoshwa na hali hiyo, hata hivyo Labani hangekubali na hivyo Mungu wa Israel aliingilia kati na kumuonya katika ndoto kwamba Usimwambie Yakobo neno la heri wala la Shari!

Kwa Lugha nyingine usiiingilie kati kusudi la Mungu lililoko ndani yakem usimzuie, Yakobo ni lazima aishi kanaani, ni lazima aende katika nchi ya ahahdi ndani yake kuna kusudi Yeye anajua na Mungu anajua kwa hiyo umemtafuta umemuona lakini lazima umuache aende zake usmwambie la heri wala la shari katika uamuzi wake huu unasikia labani? Labani alikuwa amefikisha Hatua ambayo angeingia kwenye ugimzi na Mungu, alikuwa akimuonea Yakobo mara kadhaa na inawezekana kabisa pia alitaka kumdhuru wakati ulikuwa umefika sasa Yakobo lazima awe huru, na Labani achague kurejea katika nchi yake ama akutane na mkono wa Mungu! Ona

Mwanzo 31:6-16 “Nanyi mmejua ya kwamba kwa nguvu zangu zote nimemtumikia baba yenu. Na baba yenu amenidanganya, akabadili mshahara wangu mara kumi; lakini Mungu hakumwacha kunidhuru. Aliposema, Walio na madoadoa watakuwa mshahara wako, wanyama wote wakazaa madoadoa. Aliposema, Walio na milia watakuwa mshahara wako, ndipo wanyama wote wakazaa wenye milia.  Hivi Mungu akamnyang'anya mali yake baba yenu, na kunipa mimi. Ikawa, wakati wale wanyama walipochukua mimba, naliinua macho yangu nikaona katika ndoto, na tazama, mabeberu waliowapanda hao wanyama walikuwa na milia, na madoadoa, na marakaraka. Na malaika wa Mungu akaniambia katika ndoto, Yakobo! Nikasema, Mimi hapa. Akasema, Inua, basi, macho yako, ukaone; mabeberu wote wanaopanda wanyama wana milia, na madoadoa, na marakaraka; maana nimeona yote aliyokutendea Labani. Mimi ni Mungu wa Betheli, huko ulikotia mafuta nguzo, na kuniwekea nadhiri. Sasa ondoka, toka katika nchi hii, urudi mpaka nchi ile uliyozaliwa. Raheli na Lea wakajibu, wakamwambia, Je! Imetubakia sehemu au urithi katika nyumba ya baba yetu? Hakutufanya kama wageni, maana ametuuza, naye amekula fedha zetu kabisa? Maana mali yote ambayo Mungu amemnyang'anya baba yetu, mali hiyo ndiyo yetu na ya wana wetu. Basi yo yote Mungu aliyokuambia, uyafanye.

Unaona unaposoma kifungu hicho unaweza kuona  na kupata picha ya kuwa maisha ya Yakobo, hayakuwa rahisi, kulikuwa na kila aina ya ukatili   na uonevu kutoka ujombani,  Labani alijaribu kwa kila namna kumfanya yakobo awe mtumwa wake wa kudumu, mtumwa wa maisha yake yote, Mungu alikuwa ni shahidi wa kile Labani alikuwa anamfanyia Yakobo, ni jambo la kushangaza kwamba mjomba wako mwenyewe kaka wa mama yako anakuwa kikwazo cha kusudi la Mungu maishani mwako sasa ilikuwa lazima Yakobo aende Nyumbani, aende alikozaliwa arudi Betheli kwenye nyumba ya Mungu, anede kwenye kusudi la Mungu, aende kwa baba yake aende akamuabudu Mungu wa baba yake katika nchi ya ahadi, Mungu mwenyewe alisema aende na kuwa atakuwa pamoja naye

Mwanzo 31:2-3 “Yakobo akaona uso wa Labani, ya kuwa hakumtazama vema kama jana na juzi. BWANA akamwambia Yakobo, Urudi mpaka nchi ya baba zako na kwa jamaa zako, nami nitakuwa pamoja nawe.”

Inaonekana kulikuwa na hali ngumu katika nyumba ya labani na ni wazi kuwa Israel alikuwa mvumilivu mno, ziko hali zinaweza kukuta mpaka majirani wakaona jinsi unavyoteseka na kuvumilia, ziko hali zinaweza kukukuta mpaka Mungu mwenyewe anakuambia sasa toka na kuwa nitakuwa pamoja nawe

Ni Mungu pia aliyemshauri Yakobo kurejea na ni Mungu aliyemuahidi atakuwa pamoja naye, yakobo alitoroka kama mahusiano yalikuwa mema haiwezekani kutoroka kwa mjomba lakini kutoroka huku kimya kimya kunaashiria kuwa hakli haikuwa nzuri ujombani, Labani anagundua bila shaka anamfuatilia Yakobo akiwa na hasira kali, akiwa amekusudia kumdhuru na kumfanyia jambo baya sana Lakini Mungu wa wote wenye mwili alimkemea Labani alimuonya katika ndoto alimtokea na kumueleza waziwazi Usimwambie Yakobo neno la heri wala la Shari! Ndio  kuna watu ni wakorofi, hatuwawezi kwa akili zetu na unyonge wetu, ndio wenye nguvu, ndio waliotuajiri ndio wajomba zetu lakini Mungu akiwa upande wako hatakuacha uonewe, atamkemea kila mtu anayesimama kinyume na kusudi la Mungu ndani yako kumbuka

Zaburi 105:14-15 “Hakumwacha mtu awaonee, Hata wafalme aliwakemea kwa ajili yao.  Akisema, Msiwaguse masihi wangu, Wala msiwadhuru nabii zangu.

Haijalishi audi zako wana uwezo kiasi gani, wana nguvu kiasi gani, wana uzoefu kiasi gani wana mali kwa kiasi gani vyovyote iwavyo Bwana atawakemea Mungu alimkemea Labani  kwaajili ya Yakobo, Mungu atamkemea kila mmoja anayesimama kinyume nawe kwa kuwa wewe umtumishi wake, Labani ni lazima akumbuke kuwa hawezi kushindana na kusudi la Mungu lililo ndani yako Lazima akumbuke jinsi Mungu alivyomuonya na kusema naye, ana nguvu ana uwezo anaweza kukudhuru lakini Bwana amesema naye ajihadhari asiseme le heri wala la shari nini kingemtokea unajua unaelewa hakuna mtu anaweza kushindana na kusudi la Mungu hata kidogo Labani angeshughulikiwa lakini afadhali alikumbuka maonyo ya Mungu ona

Mwanzo 31:25-29. “Labani akamfikia Yakobo, na Yakobo alikuwa amepiga hema zake katika mlima, na Labani na ndugu zake wakapiga hema zao katika mlima wa Gileadi.Labani akamwambia Yakobo, Umefanya nini? Umenihadaa, ukawachukua binti zangu kama mateka waliotwaliwa kwa upanga. Mbona umekimbia kwa siri ukanihadaa, wala hukuniambia, nipate kuagana nawe uende zako kwa furaha, na nyimbo, na ngoma, na kinubi?Wala hukuniacha niwabusu wanangu, na binti zangu; basi umetenda upumbavu. Ninao uwezo mkononi mwangu wa kukufanyia madhara; lakini Mungu wa baba yako usiku huu ameniambia, akisema, Ujihadhari, usimwambie Yakobo neno la heri wala la shari.

Nakuombea neema kwa Mungu, wewe unayeteseka kwa sababu mbali mbali, natamka maneno ya kinabii juu yako dhidi ya adui zako dhidi ya wanaokuonea dhidi ya wenye kutunga hila juu yako, kwamba wakuache wajihadhai wasinenen neno la Kheri wala la shari juu yako!  Wewe una Mungu aliye hai, wewe hauabudu vinyago, wewe una kusudi la Mungu ndani yako nasema wakuache nasema wakuache nasema wasikusimange nasema wasikusengenye nasema kwa lugha ya kinabii nawakemea wenye kukusudia mdhara juu yako wasinene wasipange la kheri wala la shari wakumbuke neno hili kwani Mungu yule yule wa Israel Mungu yuleyule wa Yakobo na baba yetu Isaka na Ibrahimu huyu huyo ndiye mtetezi wetu, huyo huyo ndiye atakayefanya njia , huyo huyo ndiye  jemedari wetu, huyo huyo hataacha mtu atuoneee hata kama ni wenye uwezo na mamlaka atawakemea

Baraka za Mungu yule nimuabuduye na ziwe na kila aneysoma waraka huu, Bwana kubariki na kuwa upande wako, wasinene la Kheri wala la shari dhidi yako katika jina la Yesu Kristo wa Nazareth amen

Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima!

Familia takatifu !

Andiko la Msingi: Luka 2:41-49 “41. Basi, wazee wake huenda Yerusalemu kila mwaka, wakati wa sikukuu ya Pasaka. 42. Na alipopata umri wake miaka kumi na miwili, walipanda kama ilivyokuwa desturi ya sikukuu; 43. na walipokwisha kuzitimiza siku, wakati wa kurudi kwao, yule mtoto Yesu alibaki nyuma huko Yerusalemu, na wazee wake walikuwa hawana habari. 44. Nao wakadhani ya kuwa yumo katika msafara; wakaenenda mwendo wa kutwa, wakawa wakimtafuta katika jamaa zao na wenzao; 45. na walipomkosa, wakarejea Yerusalemu, huku wakimtafuta. 46. Ikawa baada ya siku tatu wakamwona hekaluni, ameketi katikati ya waalimu, akiwasikiliza na kuwauliza maswali. 47. Nao wote waliomsikia walistaajabia fahamu zake na majibu yake. 48. Na walipomwona walishangaa, na mama yake akamwambia, Mwanangu, mbona umetutenda hivi? Tazama, baba yako na mimi tulikuwa tukikutafuta kwa huzuni.49. Akawaambia, Kwani kunitafuta? Hamkujua ya kuwa imenipasa kuwamo katika nyumba ya Baba yangu?”



Utangulizi:

Ni muhimu kufahamu kuwa mara baada ya sikukuu ya krismas Kanisa huwa linasheherekea siku ya familia takatifu, Tayari Yesu Kristo amezaliwa na tayari imekuwa familia kamili, Yenye baba, Mama na mtoto, hii sasa ni familia ya watu wanaomcha Mungu, Familia ndio asili ya kila kitu, hakuwezi kuwa na taifa pasipo familia, hakuwezi kuwa na kabila pasipo familia, hatuwezi kuwa na viongozi wazuri wasiotoka katika familia, hatuwezi kuwa na watetea haki, waamuzi, wanamapinduzi,  manabii, na wachungaji ambao kwa namna moja ama nyingine hawajatokana na familia, hivyo familia ndio taasisi ya kwanza kabisa kabla ya kuweko kwa taasisi nyingine, Kwa msingi huo basi ili tuweze kuwa na kila jambo zuri, lazima jambo hilo lianzie katika familia, Leo tutachukua muda kujifunza namna familia ya Yesu, ambayo ilimjumuisha Mariamu, mama yake na Yusufu Baba yake mlezi na kijana mtoto Yesu. Hii ilikuwa ni familia ambayo imeleta Baraka kubwa sana duniani na hivyo kuna mambo ya kujifunza

1.       Hakuna familia isiyokuwa na Changamoto.

Ni muhimu kufahamu kuwa kila familia inapitia changamoto zake, Familia ya Yesu ilipitia changamoto za aina mbalimbali, Lakini kutokana na kumtanguliza Mungu, Mungu aliwatoa katika changamoto hizo:-

 

a.       Walipitia katika umasikini uliokithiri ;-

 

Kabla ya Yesu kuzaliwa ni wazi kabisa kuwa Yusufu na Mariamu hawakuwa na uchumi mzuri, walikuwa na ukata, usafiri waliotumia ulikuwa usafiri wa punda,  sadaka walizokuwa wakitoa Hekaluni ilikuwa ni njiwa wawili ambayo ni sadaka ya chini mno iliyotolewa na watu waliokuwa masikini, Hata hivyo umasikini huu haukuwa sababu ya manung’uniko kwao, wala sababu ya kuiba, au kutapeli, au kukopa na kutokurudisha, au kuomba omba, waliweza kuvumilia na kuendelea kumtegemea Mungu huku wakifanya kazi kwa bidii, Maisha yao yalibadilika baadaye baada ya sadaka ya Mamajusi waliotoa dhahabu, uvumba na manemane hivyo ndio viliweza kuibadili hali ya familia hii iliyomtegemea Mungu, Wakristo lazima tujifunze kuwa wavumilivu na kuusubiri wakati wa Mungu wa kutufanikisha bila kupitia short cut kwani Mungu ana majira na nyakati za kutubariki, Familia hii ilivumilia magumu na changamoto walizozipitia mpaka Mamajusi walipotoa zawadi zilizowatajirisha sana ona

Mathayo 2:10-12 “10. Nao walipoiona ile nyota, walifurahi furaha kubwa mno. 11. Wakaingia nyumbani, wakamwona mtoto pamoja na Mariamu mamaye, wakaanguka wakamsujudia; nao walipokwisha kufungua hazina zao, wakamtolea tunu; dhahabu na uvumba na manemane. 12. Nao wakiisha kuonywa na Mungu katika ndoto wasimrudie Herode, wakaenda zao kwao kwa njia nyingine.”


Tunaimba kwamba mjini mwaka mfalme Daudi palikuwa zizi nyoge... Yesu alizaliwa katika hali ya unyonge lakini maisha ya uvumilivu na subira ilibadilisha maisha ya familia yake na wakawa sasa wana uwezo wa kwenda Misri na kuishi huko kwa muda wakijikimu maisha yao, Lazima kila familia iwe na uvumilivu, usijilinganisha na watu wengine mtegemee Mungu, na Mungu atawabariki

 

b.      Walimsikiliza Mungu (Walitii mapenzi ya Mungu):-

 

 

Familia takatifu lazima iwe na uwezo wa kumsikiliza Mungu, Kumsikiliza Mungu ni kulisikiliza neno lake, kusikiliza watumishi wake na kuhudhuria ibada, Familia hii iliweza kudumu kwa sababu ilikuwa familia ya wazazi ambao wote walikuwa na uwezo wa kumsikiliza Mungu, kuliko kusikiliza maneno ya watu wa mtaani, Yusufu alipoona Mariamu ana Mimba biblia inasema aliamua kumuacha kwa siri! Unaona lakini mapema sana Malaika wa Bwana alimuonya Yusufu asimuache mariamu mkewe, ona katika

Mathayo 1:19-21 “19. Naye Yusufu, mumewe, kwa vile alivyokuwa mtu wa haki, asitake kumwaibisha, aliazimu kumwacha kwa siri. 20. Basi alipokuwa akifikiri hayo, tazama, malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto, akisema, Yusufu, mwana wa Daudi, usihofu kumchukua Mariamu mkeo, maana mimba yake ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu. 21. Naye atazaa mwana, nawe utamwita jina lake Yesu, maana, yeye ndiye atakayewaokoa watu wake na dhambi zao.

Unaona Kama Yusufu angekuwa ni mwenye kusikiliza maneno ya watu wa mitaani ndoa yake ingevunjika mapema na familia hii isingekuwa Baraka kwa dunia, Familia takatifu ni lazima iwe familia inayosikiliza maneno ya Mungu na kufuata uongozi wa Mungu, ni kwa kujua unyenyekevu na usikivu wa Yusufu, Mungu alisema na Yusufu tena kupitia malaika wake ili kukimbilia Misri na kuyalinda au kuyatunza maisha ya Yesu asiuawe na Herode ona 

Mathayo 2:13-14 “13. Na hao walipokwisha kwenda zao, tazama, malaika wa Bwana alimtokea Yusufu katika ndoto, akasema, Ondoka, umchukue mtoto na mama yake, ukimbilie Misri, ukae huko hata nikuambie; kwa maana Herode anataka kumtafuta mtoto amwangamize. 14. Akaondoka akamchukua mtoto na mama yake usiku, akaenda zake Misri;

Unaona ni maisha ya usikivu wa Yusufu ulioweza kumfanya Mariamu na mtoto Yesu kuwa salama kule misri na kuepuka kifo kutoka kwa Herode, Leo hii familia nyingi zinaharibika na watoto wanaenea mitaani wakipoteza muelekeo, au hata wakikosa kusoma kwa sababu ya wazazi waliokosa usikivu kwa Mungu na kwa wazazi, vijana wengi wanaishi vile wanavyojisikia na kujibu kile wanachojisikia na hata wazazi wamekosa kuwa mfano bora kwa kuigwa na watoto wao kwa sababu ya kutikumcha Mungu, Yusufu, na Mariam na Yesu walikuwa ni familia ya mfano katika kumcha Mungu.

 

c.       Walimuabudu Mungu;’-

 

Mstari wa msingi tuliousoma unasema “Basi, wazee wake huenda Yerusalemu kila mwaka,” Unajua maana yake nini hawakukosa ibada kuu katika hekalu lililokuwako Yerusalem, wazee wake maana yake wazazi wake kila mwaka walikwenda Hekaluni kusali na hawakuenda wenyewe walikwenda na vijana wao akiwemo Yesu, wao wenyewe walimuabudu Mungu lakini waliwafundisha watoto wao kumuabudu Mungu na kumpenda jambo hili lilijenga uhusiano mkubwa wa Yesu na Mungu baba wa Mbinguni, kiasi ambacho licha ya Yesu kuwaheshimu wazazi wake alimuona Mungu baba wa Mbinguni kuwa baba yake

Luka 2:48-49 “48. Na walipomwona walishangaa, na mama yake akamwambia, Mwanangu, mbona umetutenda hivi? Tazama, baba yako na mimi tulikuwa tukikutafuta kwa huzuni. 49. Akawaambia, Kwani kunitafuta? Hamkujua ya kuwa imenipasa kuwamo katika nyumba ya Baba yangu?

tuwafunze watoto wetu wajue kuwa japo sisi ni wazazi wao lakini wanaye baba wa Mbinguni wamsikilize, wamtiii wampende wamuabudu familia takatifu lazima wajijenge tabia ya kuabudu. Kuimba, kuomba, kusoma neno la Mungu na kuhudhuria makusanyiko ya ibada na kujifunza na kudumisha uhusiano na Mungu ni jukumu la kila familia kuhimizana na kutiana moyo, kumuheshimu Mungu.

 

d.      Walipeleka watoto shule

 

Katika desturi za kiyahudi kijana aliyefikisha miaka 12 alikuwa tayari amefunzwa kuijua Torati na kufanya kazi za kujitegemea, wengine walijivunza uvuvi, wengine ukulima, wengine ujenzi na wengine kushoma mahema kama Paulo mtume, Yesu alikuwa na ujuzi wa torati na alikuwa amejifunza ujenzi “Carpenter” hii iliwajengea watoto uwezo wa kujiamini na kukabiliana na changamoto mbalimbali za maisha Hivyo Yesu alijengewa kupenda kujifunza na alikuwa msikivu kwa walimu wake na alikuwa mdadisi aliuliza maswali ona

“Luka 2:45-47 45. na walipomkosa, wakarejea Yerusalemu, huku wakimtafuta. 46. Ikawa baada ya siku tatu wakamwona hekaluni, ameketi katikati ya waalimu, akiwasikiliza na kuwauliza maswali. 47. Nao wote waliomsikia walistaajabia fahamu zake na majibu yake.”

Familia takatifu na iliyo njema inapaswa kuhakikisha kuwa watoto wao wanapata Elimu nzuri, na wanakuwa na uwezo wa kujitegemea wanaweza kufanya kazi mbalimbali, na wanakuwa na ujuzi wa maadili na sheria za ukoo na familia zao, leo hii tunaona kuna mmomonyoko mkubwa wa uadilifu lakini ni kwa sababu tatizo kubwa limeanzia katika ngazi ya familia, wazazi wanapaswa kuwa kitu kimoja na kuhakikisha kuwa wote kwa pamoja wanawajengea watoto uwezo wa kijitegemea ili watoto hao wasigeuke kuwa mzigo kwetu endapo hatutawaandaa vema Yesu alijengewa uwezo mkubwa sana na hatimaye akawa Mwalimu mwema alikuwa na wanafunzi 12 maalumu na wanafunzi wengine wengi, aliuitwa RABBI yaani Mwalimu, uwezo wake mkubwa wa kufundisha ulitokana na uwezo wake mkubwa wa kujifunza, kawaulize walimu hakuna Mwalimu mzuri ambaye sio mwanafunzi mzuri, Lazima tuwajengee uwezo wa kielimu watoto wetu

 

e.      Waliwalea watoto wao katika uadilifu

 

Tunasoma hivi katika Luka 2:52 “Naye Yesu akazidi kuendelea katika hekima na kimo, akimpendeza Mungu na wanadamu.

Swali jepesi la kujiuliza je watoto wetu leo na familia zetu leo zinampendeza Mungu na wanadamu? Tunaambiwa Yesu alizidi kukua akiwa na hekima lakini vilevile akimpendeza Mungu na wanadamu, Je tunampendeza Mungu na wanadamu, hii haiwezi kutokea kama hatutakuwa chuo cha maadili kwa vijana wetu, ni muhimu kuwafunza watoto wetu, na kuwalea katika uadilifu, tikifanya hivi tutakuwa na watoto wenye muelekeo thabiti katika taifa letu, leo hii tujnashuhudia mmomonyoko mkubwa waa maadili lakini sababu kubwa ni kuanzia ngazi ya familia kutokujali uadilifu na mwenendo mwema kwa watoto wetu.

 

f.        Walijali Ndugu jamaa na kule walikozaliwa/kulelewa

 

“Human being is a social being” Mungu hakutuuumba tuishi kama kisiwa, aluiposema si vema mtu huyu awe peke yake alimaanisha wanadamu tunahitajiana wakati mwingine ili uweze kujengeka unapaswa kuwa na muda wa kusikiliza wengine na hapo ndipo tunapoweza kujengwa na kukua au kutiana moyo, Mariam alipopata ujauzito wa ajabu malaika alimueleza kuwa jamaa yako  Elizabeth pia ana mimba ya mtoto wa kiume, kusudi kubwa ilikuwa ili Mariamu aweze kutiwa moyo kustahimili kile kilichomtokea hivyo Mariamu alimtembela Elizabeth ona

Luka 1:36-44 “36. Tena, tazama, jamaa yako Elisabeti naye amechukua mimba ya mtoto mwanamume katika uzee wake; na mwezi huu ni wa sita kwake yeye aliyeitwa tasa; 37. kwa kuwa hakuna neno lisilowezekana kwa Mungu. 38. Mariamu akasema, Tazama, mimi ni mjakazi wa Bwana; na iwe kwangu kama ulivyosema. Kisha malaika akaondoka akaenda zake. 39. Basi, Mariamu akaondoka siku hizo, akaenda hata nchi ya milimani kwa haraka mpaka mji mmoja wa Yuda, 40. akaingia nyumbani kwa Zakaria akamwamkia Elisabeti. 41. Ikawa Elisabeti aliposikia kule kuamkia kwake Mariamu, kitoto kichanga kikaruka ndani ya tumbo lake; Elisabeti akajazwa Roho Mtakatifu; 42. akapaza sauti kwa nguvu akasema, Umebarikiwa wewe katika wanawake, naye mzao wa tumbo lako amebarikiwa. 43. Limenitokeaje neno hili, hata mama wa Bwana wangu anijilie mimi? 44. Maana sauti ya kuamkia kwako ilipoingia masikioni mwangu, kitoto kichanga kikaruka kwa shangwe ndani ya tumbo langu.


Unaoma Mariamu anamtembelea Elizabeth anajifunza mambo mablimbali kutoka kwa mwanamke mzee mwenye uzoefu wa kutembea na Mungu, na hivyo anajifunza mambo mbalimbali Mariamu kutoka kwa watu wa rika linguine je leo hii wanawake watu wazima huwafunza wanawake vijana ? je watu hutembeleana nyakati  za leo? Je watu hutembelea kule walikozaliwa au kulelelwa familia zenye upendo hutembeleana Yesu pia alitembelea Nazareth kule alikolelewa na kuwafundisha mambo makubwa ya Mungu ona

Luka 4:16-21 “16. Akaenda Nazareti, hapo alipolelewa; na siku ya sabato akaingia katika sinagogi kama ilivyokuwa desturi yake, akasimama ili asome.17. Akapewa chuo cha nabii Isaya, akakifungua chuo, akatafuta mahali palipoandikwa, 18. Roho wa Bwana yu juu yangu, Kwa maana amenitia mafuta kuwahubiri maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, Na vipofu kupata kuona tena, Kuwaacha huru waliosetwa, 19. Na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa. 20. Akakifunga chuo, akamrudishia mtumishi, akaketi; na watu wote waliokuwamo katika sinagogi wakamkazia macho. 21. Akaanza kuwaambia, Leo maandiko haya yametimia masikioni mwenu.


Yesu alienda Nazareth kule alikolelewa, Ni muhimu kukumbuka na nyumbani, watu wengi sana wanapofanikiwa hawakumbuki nyumbani, watu wengi wa Tanga waliosoma zamani walitawanyika huko na huko na kusaidia watu wengine na kuwaelimisha lakini waliisahau Tanga,  wabunge wengi  hukumbuka nyumbani wajkati wa kupiga kura, Yesu pamoja na umaarufu wake wote na alikuwa Mungu hakuweza kusahau kule alikolelewa, tunawashangaa wachaga tu wanapoenda nyumbani msimu wa sikukuu, hebu na sisi tujifunze na kukumbuka kuenda kule tulikolelelwa na kukulia na kuwa Baraka kwao pia

Tuwe tayari kujitoa kwa wengine

Kusudi kubwa la Yesu kuzaliwa ni ili awaokoe watu wake na dhambi zao Yusufu alielezwa hili mapema ona

Mathayo 1:20-21 “20. Basi alipokuwa akifikiri hayo, tazama, malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto, akisema, Yusufu, mwana wa Daudi, usihofu kumchukua Mariamu mkeo, maana mimba yake ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu. 21. Naye atazaa mwana, nawe utamwita jina lake Yesu, maana, yeye ndiye atakayewaokoa watu wake na dhambi zao.”


Yusufu alielezwa mapema kuwa Yesu ni mwokozi, familia ina wajibu wa kulea vijana na kukuza viongozi ambao watakuwa faida si kwaajili yao tu bali kwaajili ya ulimwengu mzima Mariamu pia alijulishwa kuwa mtoto wake sio wake pekee bali amewekwa kwaajili ya wenginona

Luka 2:34-35 “34. Simeoni akawabariki, akamwambia Mariamu mama yake, Tazama, huyu amewekwa kwa kuanguka na kuinuka wengi walio katika Israeli, na kuwa ishara itakayonenewa. 35. Nawe mwenyewe, upanga utaingia moyoni mwako, ili yafunuliwe mawazo ya mioyo mingi.

  
Ilikuwa wazi kuwa Mungu aliwaamini Mariamu na Yusufu kuwa walezi wa kiongozi mkubwa ambaye atakuwa Baraka kubwa kwa ulimwengu ni mwokozi wa ulimwengu, kama familia hatuna budi kuwatunza wanafamilia wote na kuwasaidia kutimiza ndoto zao ili makusudi yote ya Mungu yapate kutimizwa ndani mwao, nani ajuaye kuwa mtoto uliyembeba ni Raisi ajaye, ni Mwalimu ajayem, ni daktari ajaye, Mungu ana makusudi na kila aliyezaliwa na hakunanayezaliwa kwa bahati mbaya hivyo tuendelee kuwa na ustawi katima familia zetu ili Mungu ajiinulie watumishi wake kutioka katika familia zetu watakaokuwa Baraka kwa wengine

Yohana 13:17 “Mkiyajua hayo heri ninyi mkiyatenda!”

Bwana Mungu awabariki na kuwafadhili tunapoadhimisha siku ya familia takatifu katika jina la Baba na Mwana na Roho Mtakatifu amina

Na. Rev. Innocent Samuel Kamote

Mkuu wa Wajenzi mwenye Hekima!

0718990796

Ijumaa, 25 Desemba 2020

Mfalme wa Amani!


 Isaya 9:6-7 “ Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani. Maongeo ya enzi yake na amani Hayatakuwa na mwisho kamwe, Katika kiti cha enzi cha Daudi na ufalme wake; Kuuthibitisha na kuutegemeza Kwa hukumu na kwa haki, Tangu sasa na hata milele. Wivu wa Bwana wa majeshi ndio utakaotenda hayo.“      


Utangulizi:

Leo ni sikukuu ya Christmas wakristo kote nchini wanaungana na waktristo wote duniani katika kuadhimisha siku hii maalumu ya kukumbuka kuzaliwa kwa Masihi, na mwokozi wa ulimwengu, Yesu Kristo kulikotokea huko Bethelehemu Israel zaidi ya miaka 2000 iliyopita. Katika siku hii muhimu ni muhimu kwetu tukajikumbusha mambo kadhaa kumuhusu Yesu Kristo.

Andiko letu la Msingi  Isaya 9:6-7 “ Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani. Maongeo ya enzi yake na amani Hayatakuwa na mwisho kamwe, Katika kiti cha enzi cha Daudi na ufalme wake; Kuuthibitisha na kuutegemeza Kwa hukumu na kwa haki, Tangu sasa na hata milele. Wivu wa Bwana wa majeshi ndio utakaotenda hayo.“

Kimsingi yalikuwa ni maneno ya nabii Isaya aliyetabiri kuzaliwa kwa mwokozi wa ulimwengu miaka  zaidi ya 700 kabla ya kuzaliwa kwa  Yesu, Isaya anamuona masihi kama kiongozi mkubwa sana na mwenye uwezo mkubwa wa kutatua matatizo na changamoto mbalimbali walizonazo wanadamu, Nyakati za Biblia wafalme ndio ambao walikuwa wanatakiwa kutatua changamoto zozote zilizowakumba watu wao na walipaswa kuwatatulia matatizo yao na kutioa ufumbuzi ona mfano

2Wafalme 6:24-30 “Ikawa baada ya hayo, Ben-hadadi mfalme wa Shamu akakusanya majeshi yake yote, akakwea akauhusuru Samaria. Njaa ikawa kuu huko Samaria; na tazama, wakauhusuru, hata kichwa cha punda kikapata kuuzwa kwa vipande themanini vya fedha, na kibaba cha mavi ya njiwa kwa vipande vitano vya fedha. Ikawa mfalme wa Israeli alipokuwa akipita ukutani, mwanamke mmoja akamwita akisema, Unisaidie, bwana wangu, mfalme. Akasema, Bwana asipokusaidia, nikusaidieje mimi? Ya sakafuni, au ya shinikizoni? Mfalme akamwambia, Una nini? Akajibu, Mwanamke huyu aliniambia, Mtoe mtoto wako, tumle leo, na mtoto wangu tutamla kesho. Basi, tukamtokosa mtoto wangu, tukamla; nikamwambia siku ya pili, Mtoe mtoto wako, tumle; naye amemficha mtoto wake. Ikawa, mfalme alipoyasikia maneno ya huyo mwanamke, aliyararua mavazi yake; (naye alikuwa akipita juu ya ukuta;) na watu wakaona, na tazama, alikuwa amevaa magunia ndani mwilini mwake.

unaweza kuona kwa hiyo kuwa mfalme halikuwa jambo rahisi, ilikuwa ni lazima uwe na uwezo wa kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili watu, hata leo viongozi wakubwa wanapotembelea maeneo mbali mbali huzomewa risala na kuelezwa changamoto kubwa mbalimbali zinazowakabili wananchi na wanatakiwa kuzitatua, hapo moja ya wafalme alishindwa kutatua changamoto na kuamua kufunga na kuomba kwa kuvaa magunia maana yake tatizo lilikuwa kubwa sana

Mungu alizungumza na manabii kuwa atakuja kiongozi mkubwa sana atakayetatua changamoto mbali mbali za watu wake sio katika Israel tu bali dunia nzima huyu ndiye masihi, tunapoadhimisha kuzaliwa kwake leo tunapaswa kukumbuka kuwa Mungu ametupa kiongozi mwenye uwezo wa kutatua changamoto za aina mbalimbali ulimwenguni na kwa wanadamu wote na huyu si mwingine ni Yesu Kristo.

Isaya anamuelezea kiongozi huyu kuwa ni mwenye uwezo na mamlaka kubwa  na kuwa atatua changamoto nyingi zinazowakabili wanadamu na moja ya changamoto kubwa inayowakabili  wanadamu ni kukosekana kwa amani na utulivu mioyoni mwao na ndio maana Yesu anaitwa Mfalme wa Amani, kwanini mfalme wa amani

Ni muhimu kufahamu kuwa tunapozungumzia amani hii inayozingumziwa katika maandiko;-

Tunazungumziia ustawi, utulivu starehe amani na mafanikio makubwa ya mwanadamu ambayo asili yake ni Mungu, Amani hii ilikuwepo katika bustani ya Eden kabla ya anguko la mwanadamu, lakini baada ya anguko la mwanadamu amani hii ilitoweka Neno linalotumiska kuielezea amani hii katika lugha ya kiebrania ni SHALOM, neno shalom maana yake ni amani na ustawi na mafanikio ya kiunghu katika Nyanja zote, Waaarabu wanatumia neno SALAM,  kwa kiaramu linatumika neno SALEMI, ni maneno yanayofanana sana katika lugha ya kiebrania, kiarabu na Kiswahili, kwa Kiswahili tunalo neno SALAMA  ni hali ya amani, ni hali ya kuwa mbakli na masumbufu, ni hali ya kuwa na utulivu, Daudi alipigana sana vita katika maisha yake yote mpaka Mungu akamuita mtu wa Damu, Lakini mwanaye Suleimani hakukuwa na vita wakati wake, SULEMANI, SOLOMON maana yake ni utulivu na ustawi,  Yerusalem maana yake ni mji wa amani, Dar es Salaam maana yake ni bandari ya amani, jina la mji wa mzizima Dare s Salaam lilitolewa na sultan Baraghash aliyekuwa anatawala Zanzibar na pwani na alitoa jina hilo kwa mji wa mzuizima kwa sababu aliamini badari hii ni mahali salama mno na patulivu

Isaya anazungumzia kuwa masihi anazaliwa duniani kwa kusudi na malengo ya kuleta utulivu kwa wanadamu, utulivu huu ni ustawi wa mwanadamu katika Nyanja zote  na ndio maana siku Yesu alipozaliwa malaika waliimba wimbo huu  kuonyesha kuwa kiongozi mkubwa mwokozi wa ulimwengu atakayetatua matatizo na kuleta majibu na ufumbuzi wote wa mwanadamu amezaliwa na atatoa amani kwa watu wote atakaowakubali

Luka 2:8-18 “Na katika nchi ile ile walikuwako wachungaji wakikaa makondeni na kulinda kundi lao kwa zamu usiku. Malaika wa Bwana akawatokea ghafula, utukufu wa Bwana ukawang'aria pande zote, wakaingiwa na hofu kuu. Malaika akawaambia, Msiogope; kwa kuwa mimi ninawaletea habari njema ya furaha kuu itakayokuwa kwa watu wote;  maana leo katika mji wa Daudi amezaliwa, kwa ajili yenu, Mwokozi, ndiye Kristo Bwana. Na hii ndiyo ishara kwenu; mtamkuta mtoto mchanga amevikwa nguo za kitoto, amelala katika hori ya kulia ng'ombe. Mara walikuwapo pamoja na huyo malaika, wingi wa jeshi la mbinguni, wakimsifu Mungu, na kusema, Atukuzwe Mungu juu mbinguni, Na duniani iwe amani kwa watu aliowaridhia. Ikawa, malaika hao walipoondoka kwenda zao mbinguni, wale wachungaji waliambiana, Haya, na twendeni mpaka Bethlehemu, tukalione hilo lililofanyika, alilotujulisha Bwana. Wakaenda kwa haraka wakamkuta Mariamu na Yusufu, na yule mtoto mchanga amelala horini.  Walipomwona wakatoa habari waliyoambiwa juu ya huyo mtoto. Wote waliosikia wakastaajabu kwa hayo waliyoambiwa na wachungaji.”

Kila mtu anayemwamini Yesu anapewa amani hii moyoni mwake ni amani ambayo hata upatwe na changamoto ya aina gani wewe unakuwa na imani kuwa nitatoka nitatoboa kwa sababu ninaye mfalme ambaye ana uwezo wa ajabu mno anayetoa amani tofauti na jinsi ulimwengu utoavyo  amani anayotupa Kristo ni amani ya pekee nay a tofauti sana ona Yesu anatuachia mani hii Yohana 14:27 “Amani nawaachieni; amani yangu nawapa; niwapavyo mimi sivyo kama ulimwengu utoavyo. Msifadhaike mioyoni mwenu, wala msiwe na woga. “              

Hatupaswi kufadhaika wala kuogopa kwa sababu Yesu ametuachia mani, na yeye ndiye mfalme wa amani, tunapoadhimisha kuzaliwa kwake leo, hatuna budi kuhakikisha kuwa tunaruhusu amani yake itawale katika mioyo yetu na kila mahali hatupaswi kufadhaika kwa jambo lolote tunapokuwa na fadhaa, udhaifu, magonjwa, changamoto na lolote lile ambalo linatuondolea amani yetu, tunaweza kumueleza Yesu Kristo mfalme wa amani yetu na akaweza kabisa kutatua na kushughulikia yala yanayotukanili na kutupa amani ya kweli, Nikutakie sikukuu njema ya Christmas

 

Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima

Kupimwa kwa kazi ya kila mtu !

1Wakoritho 3:10-15 “Kwa kadiri ya neema ya Mungu niliyopewa, mimi, kama mkuu wa wajenzi mwenye hekima, naliuweka msingi, na mtu mwingine anajenga juu yake. Lakini kila mtu na aangalie jinsi anavyojenga juu yake. Maana msingi mwingine hakuna mtu awezaye kuuweka, isipokuwa ni ule uliokwisha kuwekwa, yaani, Yesu Kristo. Lakini kama mtu akijenga juu ya msingi huo, dhahabu au fedha au mawe ya thamani, au miti au majani au manyasi, kazi ya kila mtu itakuwa dhahiri. Maana siku ile itaidhihirisha, kwa kuwa yafunuliwa katika moto; na ule moto wenyewe utaijaribu kazi ya kila mtu, ni ya namna gani. Kazi ya mtu aliyoijenga juu yake ikikaa, atapata thawabu. Kazi ya mtu ikiteketea, atapata hasara; ila yeye mwenyewe ataokolewa; lakini ni kama kwa moto” 

 

 


 


 

Utangulizi:

 

 

Ni muhimu kufahamu kuwa katika ulimwengu tulionao Mungu alimleta kila mtu Duniani kwa kusudi la kutimiza wajibu Fulani katika maisha yake,  kwa sababu hiyo  siku ya hukumu kila mmoja atatoa hesabu ya kazi au kusudi alilolifanya hakutakuwa na kisingizio kuwa hili linanipata kwa sababu ya Fulani, wote tutatioa hesabu mbele za Mungu na kila mtu atabeba mzigo wake kulingana na kazi au namna alivyotimiza  wajibu na kusudi lake duniani ona.;- 

 

Wagalatia 6:4-5 “Lakini kila mtu na aipime kazi yake mwenyewe, ndipo atakapokuwa na sababu ya kujisifu ndani ya nafsi yake tu, wala si kwa mwenzake. Maana kila mtu atalichukua furushi lake mwenyewe. 

 

Tutajifunza so mo hili kwa kuzingatia vipengele vitatu vifuatavyo:-

 

·         Umuhimu wa kutimiza kusudi la Mungu!

·         Mifano ya watu waliotimiza kusudi la Mungu kwa uaminifu!.

·         Faida za kutimiza kusudi la Mungu!

 

Umuhimu wa kutimiza kusudi la Mungu!

 

Kwa msingi huo ni muhimu kwa kila mmoja wetu kuhakikisha kuwa anajua ni kwa nini yuko Duniani na amekuja kufanya nini duniani, kisha pambana kwa kila namna uwezavyo kuhakikisha kuwa unafikia lengo na kusudi kubwa la Mungu jkukuleta duniani, Katika maandiko Daudi anatajwa kama mtu aliyeweza kutimiza kusudi au shauri lote la Mungu, hakuondoka duniania akiwa amebakiza kazi fulani alihakikisha kuwa anaitimiza yote yaliyomo katika moyo wa Mungu na hata alitaka kuzidisha!

 

Matendo 13:36 “Kwa maana Daudi, akiisha kulitumikia shauri la Mungu katika kizazi chake, alilala, akawekwa pamoja na baba zake, akaona uharibifu.

 

Shauri l Mungu maana yake ni Kusudi lote la Mungu, kila mmoja anao wajibu wa kutimiza kusudi lote la Mungu, kuhakikisha kuwa unamaliza vema unahitimisha kazi yako vema, unatenda vema kusudi la Mungu, kama ni kuhubiri ni lazima tuhakikishe kuwa tunahubiri kusudi lote la Mungu, kama ni kuchunga tunachunga kwa kusudi lote la Mungu kama ni kufundisha tunafundisha kama Mungu anavyokusudia, kama ni kusoma tunasoma kama Mungu alivyokusudia, kama ni kuhubiri injili unahubiri kama Mungu alivyokusudia na kama ni kuongoza unaongoza kama Mungu alivyokusudia, Paulo Mtume alipohubiri injili aliweka wazi kuwa aliwahubiria watu kile ambacho Mungu alikusudia na hivyo  alihubiri kusudi lote la Mungu!

 

 Matendo 20:25-27 “Na sasa, tazameni, mimi najua ya kuwa ninyi nyote niliowahubiria ufalme wa Mungu, nikienda huko na huko, hamtaniona uso tena. Kwa hiyo nawashuhudia wote siku hii ya leo, ya kuwa mimi sina hatia kwa damu ya mtu awaye yote. Kwa maana sikujiepusha na kuwahubiria habari ya kusudi lote la Mungu.”

 

Mifano ya watu waliotimiza kusudi la Mungu kwa uaminifu!.

 

Wako watu mbalimbali katika maandiko ambao wanatajwa kuwa walitimiza makusudi ya Mungu kwa uaminifu na walitioa hesabu na kujifanyia tathimini;-

 

1.       Yesu mwenyewe alijifanyia tathimini na kutoa Ripoti kuwa amemaliza kusudi lote la Mungu, ukiacha kuwa siku ya kusulubiwa kwake alisema IMEKWISHA yaani alitimiza makusudi yote ya Mungu lakini vilevile alitoa hesabu ya kile ambacho baba alikuwa amemuagiza kukitimiza na kwa uhakikika kabisa alikuwa ameyatimiza hivyo kama asemavyo mwenyewe katika  injili ona ;-Yohana 17:1-13 “Maneno hayo aliyasema Yesu; akainua macho yake kuelekea mbinguni, akasema, Baba, saa imekwisha kufika. Mtukuze Mwanao, ili Mwana wako naye akutukuze wewe; kama vile ulivyompa mamlaka juu ya wote wenye mwili, ili kwamba wote uliompa awape uzima wa milele. Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma. Mimi nimekutukuza duniani, hali nimeimaliza kazi ile uliyonipa niifanye.  Na sasa, Baba, unitukuze mimi pamoja nawe, kwa utukufu ule niliokuwa nao pamoja nawe kabla ya ulimwengu kuwako. Jina lako nimewadhihirishia watu wale ulionipa katika ulimwengu; walikuwa wako, ukanipa mimi, na neno lako wamelishika. Sasa wamejua ya kuwa yote uliyonipa yatoka kwako. Kwa kuwa maneno uliyonipa nimewapa wao; nao wakayapokea, wakajua hakika ya kuwa nalitoka kwako, wakasadiki ya kwamba wewe ndiwe uliyenituma. Mimi nawaombea hao; siuombei ulimwengu; bali hao ulionipa, kwa kuwa hao ni wako; na wote walio wangu ni wako, na walio wako ni wangu; nami nimetukuzwa ndani yao. Wala mimi simo tena ulimwenguni, lakini hawa wamo ulimwenguni, nami naja kwako. Baba mtakatifu, kwa jina lako ulilonipa uwalinde hawa, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo. Nilipokuwapo pamoja nao, mimi naliwalinda kwa jina lako ulilonipa, nikawatunza; wala hapana mmojawapo wao aliyepotea, ila yule mwana wa upotevu, ili andiko litimie.  Na sasa naja kwako; na maneno haya nayasema ulimwenguni, ili wawe na furaha yangu imetimizwa ndani yao.”

 

2.       Paulo Mtume alihakikisha kuwa ametimiza kusudi lote la Mungu na kwa ujasiri kabisa alimuekleza Timotheo kuwa anasubiri taji yaani thawabu kubwa kwa sababu alikamilisha kile alichokusudiwa na Mungu kwa uaminifu mkubwa kwa mapambano na kwa mwendo mrefu na aliukamilisha  ona 2Timotheo 4;6-8 “Kwa maana, mimi sasa namiminwa, na wakati wa kufariki kwangu umefika. Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda;  baada ya hayo nimewekewa taji ya haki, ambayo Bwana, mhukumu mwenye haki, atanipa siku ile; wala si mimi tu, bali na watu wote pia waliopenda kufunuliwa kwake.”

 

3.       Musa alikuwa mwaminifu katika kazi yote nya Mungu, maana yake alikamilisha jukumu lake duniani, Musa alilitumikia kusudi la Mungu mpaka akasahau kifo, ilibidi Mungu amkubushe kwamba apande kwake mlimani akafe kwa sababu alikuwa mwaminifu mpaka sekunde ya mwisho Waebrania 3:5 “Na Musa kweli alikuwa mwaminifu katika nyumba yote ya Mungu kama mtumishi, awe ushuhuda wa mambo yatakayonenwa baadaye;

 

4.       Yoshua alikuwa kiongozi mkubwa jemadari na shujaa alitimiza makusudi ya Mungu hadi  mwisho na kuhakikisha kuwa anaonyesha msimamo wake hata kwa wana wa Israek kuwa yeye na nyumba yake wameamua kwa dhati kuwa watamtumikia Mungu aliye hai ona Yoshua 24:14-18 “Basi sasa mcheni Bwana, mkamtumikie kwa unyofu wa moyo na kwa kweli; na kuiweka mbali miungu ambayo baba zenu waliitumikia ng'ambo ya Mto, na huko Misri; mkamtumikie yeye Bwana. Nanyi kama mkiona ni vibaya kumtumikia Bwana, chagueni hivi leo mtakayemtumikia; kwamba ni miungu ile ambayo baba zenu waliitumikia ng'ambo ya Mto, au kwamba ni miungu ya wale Waamori ambao mnakaa katika nchi yao; lakini mimi na nyumba yangu tutamtumikia Bwana. Hao watu wakajibu wakasema, Hasha! Tusimwache Bwana, ili kuitumikia miungu mingine;  kwa maana Bwana, Mungu wetu, yeye ndiye aliyetupandisha sisi na baba zetu kutoka nchi ya Misri; kutoka nyumba ya utumwa; naye ndiye aliyezifanya ishara zile kubwa mbele ya macho yetu, na kutulinda katika njia ile yote tuliyoiendea, na kati ya watu wa mataifa yote tuliopita katikati yao. Bwana ndiye aliyewafukuza watu wa mataifa yote watoke mbele yetu, naam, Waamori waliokaa katika nchi hii; basi, kwa sababu hiyo sisi nasi tutamtumikia Bwana, maana yeye ndiye Mungu wetu.”               

 

5.       Nabii Samuel aliishi maisha ya haki, hakudhuklumu mtu na mbele ya watu wote alijipambanua kuwa hakuwa na tatizo na Mtu he was a man of integrity   alihitmisha akiwa na ujasiri kuwa hakuwahi kumuonea mtu wala kumdhulumu mtu na kuwa alihitimisha akiwa na mikono safi je wewe unahitimisha vipi katika utumishi wako, je watu watakumbuka namna ulivyowaliza? Na kuwaonea na kuwatendea mabaya? Samuel alimaliza vema ona  katika 1Samuel 12:3-5 “Nami nipo hapa; basi, mnishuhudie mbele za Bwana, na mbele ya masihi wake,nalitwaa ng`ombe wa nani? au nalitwaa punda wa nani? au ni nani niliye mdhulumu? Ni nani niliyemwonea? Au kwa mkono wa nani nimepokea rushwa inipofushe macho? Nami nitawarudishia ninyi. Nao wakasema, hukutudhulumu, wala hukutuonea, wala hukupokea kitu kwa mkono wa mtu awaye yote. Akawaambia, Bwana ni shahidi juu yenu, na masihi

 

6.       Henoko alikuwa mwaminifu alitembea na Mungu, mwandishi wa kitabu cha mwanzo anamfanyia tathimini Henoko na kumuonyesha kuwa mtu wa tofauti, yeye licha ya kuzaa kama wengine licha ya kuishi maisha marefu alitembea na Mungu kiasi Mungu aliamua kumfanya kuwa malaika

 

Mwanzo 5:8-14 “ Siku zote za Sethi ni miaka mia kenda na kumi na miwili, akafa. Enoshi akaishi miaka tisini, akamzaa Kenani. Enoshi akaishi baada ya kumzaa Kenani miaka mia nane na kumi na mitano, akazaa wana, waume na wake. Siku zote za Enoshi ni miaka mia kenda na mitano, akafa. Kenani akaishi miaka sabini, akamzaa Mahalaleli. Kenani akaishi baada ya kumzaa Mahalaleli miaka mia nane na arobaini, akazaa wana, waume na wake. Siku zote za Kenani ni miaka mia kenda na kumi, akafa. Mahalaleli akaishi miaka sitini na mitano, akamzaa Yaredi. Mahalaleli akaishi baada ya kumzaa Yaredi miaka mia nane na thelathini, akazaa wana, waume na wake. Siku zote za Mahalaleli ni miaka mia nane na tisini na mitano, akafa. Yaredi akaishi miaka mia na sitini na miwili, akamzaa Henoko. Yaredi akaishi baada ya kumzaa Henoko miaka mia nane, akazaa wana, waume na wake.  Siku zote za Yaredi ni miaka mia kenda na sitini na miwili, akafa. Henoko akaishi miaka sitini na mitano, akamzaa Methusela. Henoko akaenda pamoja na Mungu baada ya kumzaa Methusela miaka mia tatu, akazaa wana, waume na wake. Siku zote za Henoko ni miaka mia tatu na sitini na mitano. Henoko akaenda pamoja na Mungu, naye akatoweka, maana Mungu alimtwaa.”

 

Hao walikuwa ni baadhi ya watu muhimu katika biblia ambao walijifanyia tathimini katika maisha yao na kutimiza makusudi ya Mungu vema, kila mmoja anapaswa kutimiza wajibu wake vema, tukikumbuka na kuelewa ya kuwa tutatoa hesabu mbele za Mungu, katia Nyanja yoyote ambayo Mungu amekuita unapaswa kuhakikisha kuwa unafanya vema, Florence Nightingale mwanzilishi wa uuguzi duniani alisimama vema katika kusudi lake mpaka leo anakumbukwa kwa kazi yake katika siku ya wauguzi duniani,  ni vema kila mmoja akafanya vema, mainjinia wasipunje, viwango vya barabara za lami hata kwa chepe moja la kokoto, Mizani za wafanya biashara ziwe za haki, madaktari na wafanye kwa uadilifu, Walimu wafundishe kwa bidii na wanafunzi wasome kwa bidii ni wakati wa kila mmoja kutimiza wajibu wake vema ili mbele za Mungu anwanadamu tuonekane kuwa na haki na kuepuka hukumu wakati kazi zetu zitakapopimwa!

 

Faida za kutimiza kusudi la Mungu!

 

Mungu ataipima kazi ya kila mmoja wetu kama lisemavyo neon la msingi, kila mmoja anapaswa kujifanyia tathimini kama anafanya kwa ubora kile ambacho Mungu amekusudia ndani yake, katika hukumu za Mungu ziko hukumu za aina nne Mungu aatakazowahukumu wanadamu

 

1.       Present judgment – hukumu iliyoko sasa kama mtu hajampokea Yesu hajamuamini huyo kwa sasa tunapozungumza ujumbe huu amekwisha kuhukumiwa angalia Yohana 3:16-18 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. Maana Mungu hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye.  Amwaminiye yeye hahukumiwi; asiyeamini amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu.” Ili kuepuka hukumu hii basi mwanadamu anapaswa kumuamini Yesu

 

2.       Hukumu ya adhabu Warumi 8:1 Sasa, basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu.” Hukumu hii ni hukumu ya aibu hukumu ya adhabu kwa kiyunani inaitwa KRI MA Mungu atafunua siri zote za uovu za wale wasiomuamini Mungu na wale waliotenda vibaya ona Muhubiri 12:14 “Kwa maana Mungu ataleta hukumuni kila kazi, pamoja na kila neno la siri, likiwa jema au likiwa baya.” Mungu atafupisha maisha au hata kazi za mtu asiyetenda vema hakikisha kuwa unatenda vema

 

3.       Hukumu isiyo ya adhabu Warumi 8:1 “Sasa, basi, hakuna hukumu ya adhabu juu yao walio katika Kristo Yesu.” Hii ni hukumu ya watakatifu, pamoja na neema ya kuingia mbinguni Mungu atamlipa kila mmoja sawa na kazi njema aliyoitenda kazi hizo zitajaribiwa kwa moto  kama ni ya majani, miti na nyasi itateketea na haitaleta heshima kwetu, lakini pamoja na kumuamini Yesu tunapaswa kutenda vema hukumu hii kwa kiyunani inaitwa KRINO ni hukumu isiyo ya adhabu kwa wale walio katika Kristo lakini kazi ya kila mmoja itapimwa, Yesu ataketi katika kiti cha Enzi kiitwacho Bema na kutoa thawabu kwa kazi zetu1Wakoritho 3:10-15 “Kwa kadiri ya neema ya Mungu niliyopewa, mimi, kama mkuu wa wajenzi mwenye hekima, naliuweka msingi, na mtu mwingine anajenga juu yake. Lakini kila mtu na aangalie jinsi anavyojenga juu yake. Maana msingi mwingine hakuna mtu awezaye kuuweka, isipokuwa ni ule uliokwisha kuwekwa, yaani, Yesu Kristo. Lakini kama mtu akijenga juu ya msingi huo, dhahabu au fedha au mawe ya thamani, au miti au majani au manyasi, kazi ya kila mtu itakuwa dhahiri. Maana siku ile itaidhihirisha, kwa kuwa yafunuliwa katika moto; na ule moto wenyewe utaijaribu kazi ya kila mtu, ni ya namna gani. Kazi ya mtu aliyoijenga juu yake ikikaa, atapata thawabu. Kazi ya mtu ikiteketea, atapata hasara; ila yeye mwenyewe ataokolewa; lakini ni kama kwa moto  

 

4.       Mungu anajua, un predictable judgment hii ni hukumu isiyotabirika   Warumi 14:4 ” Wewe u nani unayemhukumu mtumishi wa mwingine? Kwa bwana wake mwenyewe yeye husimama au huanguka. Naam, atasimamishwa, kwa kuwa Bwana aweza kumsimamisha.“Yeye ni Bwana ana maamuzi yake kama unavyokwenda kwa hakimu anaweza kuamua lolote kama apendavyo mwenyewe hakuna mtu anayejua rehema za Mungu, haiyamkini bwana anaweza kutyangaza rehema kwa mtu, yeyote au hata kwa watu wote kwani utamwambia nini yeye si ndio Mungu? Ndio anaweza kuamua lolote utamfanya nini aliamua utamuuliza nini, Tufanye kazi zetu kwa bidii kwani maandiko yamesema iko thawabu kubwa sana waongoze wengi katika kutenda haki nawe utafaidika!

 

Daniel 12;3  Na walio na hekima watang'aa kama mwangaza wa anga; na hao waongozao wengi kutenda haki watang'aa kama nyota milele na milele.

 

Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima

0718990796