Jumatatu, 18 Julai 2022

Mwana wa Muungwana na mwana wa mjakazi


Wagalatia 4:28-31 “Basi, ndugu zangu, kama Isaka sisi tu watoto wa ahadi. Lakini kama vile siku zile yule aliyezaliwa kwa mwili alivyomwudhi yule aliyezaliwa kwa Roho, ndivyo ilivyo na sasa. Lakini lasemaje andiko? Mfukuze mjakazi na mwanawe, kwa maana mwana wa mjakazi hatarithi kabisa pamoja na mwana wa mwungwana. Ndiposa, ndugu zangu, sisi si watoto wa mjakazi, bali tu watoto wa huyo aliye mwungwana.”


Utangulizi:

Ni muhimu kuelewa kuwa Paulo Mtume alikuwa anakamilisha Mafundisho yake kwa Kanisa lililokuwako Galatia ambao walikuwa wamekumbana na kadhia ya  Mateso pamoja na Mafundisho mabaya ya Jamii ya wayahudi waliokuwa waanaamini katika sheria ya Musa na hata baada ya Injili kuhubiriwa wao waliwataka wakristo waendelee kuwa chini ya sheria ya Musa badala ya kuutumia uhuru wao waliokuwa nao katika kristo, Katika kuhitimisha mafundisho yake anaonyesha kuwa kuna wana wa Muungwana na wana wa Mjakazi.  Na anajaribu kuonyesha tofauti zao watoto hao kwamba Mwana wa Mjakazi alizaliwa kwa mapenzi ya Mwili na yule wa  Muungwana alizaliwa kwa kusubiri Ahadi ya Mungu, sawa tu na tukio la kuzaliwa kwa Ishmael na baadaye Isaka, Ishmael Alizaliwa kwa mapenzi ya mwili wakati Isaka alizaliwa kutokana na ahadi ya Mungu ona

 Mwanzo 16:1-4 “Basi Sarai mkewe Abramu hakumzalia mwana, naye alikuwa na mjakazi, Mmisri, jina lake Hajiri. Sarai akamwambia Abramu, Basi sasa, BWANA amenifunga tumbo nisizae, umwingilie mjakazi wangu labda nitapata uzao kwa yeye. Abramu akaisikiliza sauti ya Sarai. Sarai mkewe Abramu akamtwaa Hajiri Mmisri mjakazi wake, baada ya kukaa Abramu katika nchi ya Kanaani miaka kumi, akampa Abramu mumewe, awe mkewe. Basi akamwingilia Hajiri, naye akapata mimba. Naye alipoona ya kwamba amepata mimba, bibi yake alikuwa duni machoni pake.”     Kwa hiyo tunaweza kuona mtoto wa Kwanza wa Abraham anazaliwa kutokana na jitihada za kibinadamu yaani kwa mapenzi ya mwili na kwa mwanamke aliyekuwa mtumwa (Kijakazi)  Na mtoto wa pili alizaliwa kwa uvumilivu na subira kwa kusubiri ahadi ya Mungu na kupitia mwanamke aliyekuwa mtawala (Huru) Mwanzo 21:1-4 “BWANA akamjia Sara kama alivyonena, na BWANA akamfanyia kama alivyosema. Sara akapata mimba akamzalia Ibrahimu mwana wa kiume katika uzee wake, kwa muhula alioambiwa na Mungu. Ibrahimu akamwita jina lake Isaka, yule mwana aliyezaliwa, ambaye Sara alimzalia. Ibrahimu akamtahiri Isaka mwanawe, alipokuwa mwenye siku nane, kama Mungu alivyomwamuru.

Hawa wote ni watoto wa Ibrahimu, mmoja alizaliwa kutokana na mawazo na mipango ya kibinadamu na mwingine alizaliwa kwa kusubiria ahadi ya Mungu, Paulo anajaribu kuunganisha swala hili na hali halisi waliyokuwa wanaipitia Makanisa ya Galatia, taabu kubwa waliyokuwa wanaipitia ni Mateso pamoja na Mafundisho potofu ya wayahudi yanayowataka waishike sheria ya Musa huku wakiwa wamemuamini Yesu Kristo ambaye tayari alikuwa amekwisha kuwaokoa na laana ya torati, Kitendo cha aalimu hawa wa kiyahudii kulisumbua kanisa alikifananisha na Ishamael kumdhihaki Isaka, Ishmael akiwa ni mtoto wa mjakazi na Isaka akiwa ni mtoto wa Muungwana, dhihaka hii haikuweza kuvumilika kiasi ambacho Sara alitoa wazo la mjakazi na mtoto wake kufukuzwa kabisa kwani wangemuharibu kabisa Isaka kutokana na ushawishi wao wa kifisadi

Mwanzo 21:8-12 “Mtoto akakua, akaachishwa kunyonya; Ibrahimu akafanya karamu kuu siku ile Isaka alipoachishwa kunyonya. Sara akamwona yule mwana wa Hajiri Mmisri, ambaye alimzalia Ibrahimu, anafanya dhihaka. Kwa hiyo akamwambia Ibrahimu, Mfukuze mjakazi huyu na mwanawe, maana mwana wa mjakazi hatarithi pamoja na mwanangu, Isaka. Na neno hilo lilikuwa baya sana machoni pa Ibrahimu, kwa ajili ya mwanawe. Mungu akamwambia Ibrahimu, Neno hili lisiwe baya machoni pako, kwa ajili ya huyo mwana, na huyo mjakazi wako. Kila akuambialo Sara, sikiza sauti yake, kwa maana katika Isaka uzao wako utaitwa.”

Unaweza kuwa na swali moyoni ambalo hata mimi nilikuwa nalo, kwamba ni aina gani ya dhihaka ilikuwa inafanyika tena siku ya sherehe hata kumuuzi Sara na kuamuru kuwa mtoto huyo afukuzwe pamoja na mama yake?  Kwa mujibu wa Marabi wa kiyahudi ni kuwa kijana huyu alikuwa na miaka kama 14 hivi na tayari alikuwa ameshaonyesha kutokuishi sawa na njia ya baba yake, na kwamba kulikuweko na dalili nyingi za kukiuka sheria za Mungu ambazo hata Abrahamu alikuwa anazishika, Sara alikuwa amebaini hilo kwa uwazi kuliko Abrahamu, Sara aliona kuwa kuna hatari mtoto wa ahadi akasawishika kufuata njia za kaka yake ambaye kwa siri wayahudi wanaeleza kuwa alikuwa akionekana anaabudu miungu ya mama yake na kushindana na kijana mdogo wa Ibrahimu. Neno dhihaka kwa waebrania linasomeka kama TSACHAQ  kufanya dhihaka katika mambo muhimu na ya msingi, neno hili pia huumika kumaanisha watu wasiomcha Mungu au wenye kupuuzia njia za Mungu. Unaweza kuliona katika zaburi na maandiko mengine ya kiyahudi;-

Zaburi 1:1-2 “Heri mtu yule asiyekwenda Katika shauri la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wakosaji; Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha. Bali sheria ya Bwana ndiyo impendezayo, Na sheria yake huitafakari mchana na usiku.”

Wakati Abraham na watu wake wanafanya karamu ya kumshukuru Mungu Ishamel yeye alikuwa anadhihaki kwa msingi huo kama tungekuwepo kwenye tafrija ile tungebaini kuwa watu wako makini katika kumshukuru Mungu kwa matendo makuu aliyomfanyia Sara na Abraham na kundi la Hajiri  na mwanaye wanapuuzia na kucheka au kuona kinachofanyika ni upuuzi tu na hawajali kile Mungu alichokifanya wala hawaoni kuwa ni jambo kubwa.  Sara aliona hilo na kubaini kuwa kijana huyu na mama yake hawana budi kutimuliwa kwani hawangeweza kuishi pamoja, wala kurithi pamoja na Isaka Mwanzo 21:10 “Kwa hiyo akamwambia Ibrahimu, Mfukuze mjakazi huyu na mwanawe, maana mwana wa mjakazi hatarithi pamoja na mwanangu, Isaka.”

Paulo anautumia mfano huo sasa kulifundisha kanisa kuhusu mateso yanayofanywa na wale wanaolitesa kanisa kwa Mateso na mafundisho yasiyo sahihi ambayo yanalitesa Kanisa Kama Ishamel alivyokuwa akimdhihaki Isaka waalimu wa uongo walikuwa wakilitesa kanisa kwa kufundisha kuwa watu wanaweza kukubaliwa na Mungu kwa sababu ya bidii ya mwilini, wakati kuzaliwa kwa Isaka kulitokana na Mungu kuitimiza ahadi yake na sio juhudi za kibinadamu, Jamii kubwa ya wayahudi hata pamoja na kuiamini injili waligeuka kubwa mwiba mkubwa wa mateso katika kanisa na mafundisho yasiyo sahihi  aidha wakati wote walihakikisha kuwa wanapingana na injili na kuwaudhi wahubiri wa injili ona

Matendo 13:48-51 “Mataifa waliposikia hayo wakafurahi, wakalitukuza neno la Bwana, nao waliokuwa wamekusudiwa uzima wa milele wakaamini. Neno la Bwana likaenea katika nchi ile yote. Lakini Wayahudi wakawafitinisha wanawake watauwa wenye cheo na wakuu wa mji, wakawataharakisha watu wawaudhi Paulo na Barnaba; wakawatoa katika mipaka yao. Nao wakawakung'utia mavumbi ya miguu yao, wakaenda Ikonio.”

Matendo 17:5-9 “Na Wayahudi wakaona wivu, wakajitwalia watu kadha wa kadha katika watu ovyo wasio na sifa njema, nao wakakutanisha mkutano, wakafanya ghasia mjini, wakawaendea watu wa nyumba ya Yasoni, wakataka kuwapeleka mbele ya watu wa mji; na walipowakosa, wakamkokota Yasoni na baadhi ya ndugu mbele ya wakubwa wa mji, wakipiga kelele, wakisema, Watu hawa walioupindua ulimwengu wamefika huku nako, na Yasoni amewakaribisha; na hawa wote wanatenda mambo yaliyo kinyume cha amri za Kaisari, wakisema na kwamba yupo mfalme mwingine, aitwaye Yesu. Wakafadhaisha ule mkutano na wakubwa wa mji walipoyasikia hayo. Nao walipokwisha kumtoza dhamana Yasoni na wenziwe wakawaacha waende zao.”

Matendo 17: 13 “Lakini Wayahudi wa Thesalonike walipopata habari ya kwamba neno la Mungu linahubiriwa na Paulo hata katika Beroya, wakaenda huko nako wakawachafua na kuwafadhaisha makutano.”

Unaweza kuona kuwa kanisa sio tu lilikuwa linapitia mateso ya kawaida na upinzani dhidi ya injili lakini pia lilipingwa kwa mafundisho yasiyo sahihi Na kanisa la Galatia lilikuwa ni moja ya kanisa lililoathiriwa na mafundishi hayo

Wagalatia 3:1-9 “Enyi Wagalatia msio na akili, ni nani aliyewaloga, ninyi ambao Yesu Kristo aliwekwa wazi mbele ya macho yenu ya kuwa amesulibiwa? Nataka kujifunza neno hili moja kwenu. Je! Mlipokea Roho kwa matendo ya sheria, au kwa kusikia kunakotokana na imani? Je! Mmekuwa wajinga namna hii? Baada ya kuanza katika Roho, mnataka kukamilishwa sasa katika mwili? Mmepatikana na mateso makubwa namna hii bure? Ikiwa ni bure kweli. Basi, yeye awapaye Roho na kufanya miujiza kati yenu, je! Afanya hayo kwa matendo ya sheria, au kwa kusikia kunakotokana na imani? Kama vile Ibrahimu alivyomwamini Mungu akahesabiwa haki. Fahamuni basi, ya kuwa wale walio wa imani, hao ndio wana wa Ibrahimu. Na andiko, kwa vile lilivyoona tangu zamani kwamba Mungu atawahesabia haki Mataifa kwa imani, lilimhubiri Ibrahimu habari njema zamani, kusema, Katika wewe Mataifa yote watabarikiwa. Basi hao walio wa imani hubarikiwa pamoja na Ibrahimu aliyekuwa mwenye imani

Wakristo ni watoto wa Mungu kwa njia  imani na ahadi inayotenda kazi kupitia uwezo wa Roho Mtakatifu, na kwamba tunapokea wokovu kwa neema na si kwa juhudi wala kwa matendo ili awaye yote asijisifu:-

Waefeso 2:4-9 “Lakini Mungu, kwa kuwa ni mwingi wa rehema, kwa mapenzi yake makuu aliyotupenda; hata wakati ule tulipokuwa wafu kwa sababu ya makosa yetu; alituhuisha pamoja na Kristo; yaani, tumeokolewa kwa neema. Akatufufua pamoja naye, akatuketisha pamoja naye katika ulimwengu wa roho, katika Kristo Yesu; ili katika zamani zinazokuja audhihirishe wingi wa neema yake upitao kiasi kwa wema wake kwetu sisi katika Kristo Yesu. Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani; ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu; wala si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisifu.”

Katika imani ye Kikristo tunapata kila tunachokipata kwa neema na sio kwa matendo au bidii za kibinadamu hii iko katika kaisha ya kawaida na katika maisha ya wito wa kumtumikia Mungu hakuna juhudi wala matakwa ya kibinadamu bali ya Mungu

Warumi 9:14-15 “Maana amwambia Musa, Nitamrehemu yeye nimrehemuye, nitamhurumia yeye nimhurumiaye. Basi, kama ni hivyo, si katika uwezo wa yule atakaye, wala wa yule apigaye mbio; bali wa yule arehemuye, yaani, Mungu.”

Hata Mungu anapoita watu katika utumishi huu anawaita watu kwa neema yake na sio kwa kujipendekeza au kwa kujidhani ya kuwa ninafaa, wako watu wanaweza kujidhania kuwa wanafaa kuwa watumishi wa Mungu na wengine hawafai, au mtu akajikinai akifikiri yeye ni zaidi ya mwingine jambo la namna hii pia liko kinyume na ile dhana ya kiungu, Mungunhuchagua vile tunavyovidhania kuwa havifai, kumbuka lililotyukuka kwa mwanadamu ni chukizo kwa Mungu!

1Wakoritho 1:26-29 “Maana, ndugu zangu, angalieni mwito wenu, ya kwamba si wengi wenye hekima ya mwilini, si wengi wenye nguvu, si wengi wenye cheo walioitwa; bali Mungu aliyachagua mambo mapumbavu ya dunia awaaibishe wenye hekima; tena Mungu alivichagua vitu dhaifu vya dunia ili aviaibishe vyenye nguvu; tena Mungu alivichagua vitu vinyonge vya dunia na vilivyodharauliwa, naam, vitu ambavyo haviko, ili avibatilishe vile vilivyoko; mwenye mwili awaye yote asije akajisifu mbele za Mungu.”  

Tunawezaje kujua kuwa hawa ni wana wa Muungwana na hawa ni wana wa kijakazi? Maandiko yanaeleza wazi kuwa wana wa muungwana walizaliwa kwa ahadi na wana wa kijakazi walizaliwa kwa mapenzi ya mwili na hivyo tunaweza kuwatambua kwa matendo yao, wale waliokuwa wakiliudhi kanisa na kulitesa ndio wana wa kijakazi na wale waliowapole na waungwana Paulo ana sema

Wagalatia 4:29 “Lakini kama vile siku zile yule aliyezaliwa kwa mwili alivyomwudhi yule aliyezaliwa kwa Roho, ndivyo ilivyo na sasa

Wana wa kijakzi ni wale waliozaliwa kwa mwili na wana wa muungwana ni wale waliozaliwa kwa ahadi na uweza wa Roho Mtakatifu na matunda yao unaweza unaweza kuwatambua

Wagalatia 5:19-21 “Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi, ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.”

Wagalatia 5:22-24 “Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria. Na hao walio wa Kristo Yesu wameusulibisha mwili pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake

-          Wana wa mjakazi hawashindwi kuua  mtu, mioyo yao imejawa na chuki na uchungu ni wakatili na hawana huruma ona Mwanzo 4:1-11 “Adamu akamjua Hawa mkewe; naye akapata mimba, akamzaa Kaini, akasema, Nimepata mtoto mwanamume kwa BWANA. Akaongeza akamzaa ndugu yake, Habili. Habili alikuwa mchunga kondoo, na Kaini alikuwa mkulima ardhi.     Ikawa hatimaye Kaini akaleta mazao ya ardhi, sadaka kwa BWANA. Habili naye akaleta wazao wa kwanza wa wanyama wake na sehemu zilizonona za wanyama. BWANA akamtakabali Habili na sadaka yake; bali Kaini hakumtakabali, wala sadaka yake. Kaini akaghadhibika sana, uso wake ukakunjamana. BWANA akamwambia Kaini, Kwa nini una ghadhabu? Na kwa nini uso wako umekunjamana? Kama ukitenda vyema, hutapata kibali? Usipotenda vyema dhambi iko, inakuotea mlangoni, nayo inakutamani wewe, walakini yapasa uishinde. Kaini akamwambia Habili nduguye, [Twende uwandani]Ikawa walipokuwapo uwandani, Kaini akamwinukia Habili nduguye,akamwua. BWANA akamwambia Kaini, Yuko wapi Habili ndugu yako? Akasema, Sijui, mimi ni mlinzi wa ndugu yangu? Akasema, Umefanya nini? Sauti ya damu ya ndugu yako inanililia kutoka katika ardhi. Basi sasa, umelaaniwa wewe katika ardhi, iliyofumbua kinywa chake ipokee damu ya ndugu yako kwa mkono wako; utakapoilima ardhi haitakupa mazao yake; utakuwa mtoro na mtu asiye na kikao duniani.”

 

-          Hawaishi kuwa na Makundi wala Mafarakano  1Wakoritho 3:1-9 “Lakini, ndugu zangu, mimi sikuweza kusema nanyi kama na watu wenye tabia ya rohoni, bali kama na watu wenye tabia ya mwilini, kama na watoto wachanga katika Kristo. Naliwanywesha maziwa sikuwalisha chakula; kwa kuwa mlikuwa hamjakiweza. Naam, hata sasa hamkiwezi,kwa maana hata sasa ninyi ni watu wa tabia ya mwilini. Maana, ikiwa kwenu kuna husuda na fitina, je! Si watu wa tabia ya mwilini ninyi; tena mnaenenda kwa jinsi ya kibinadamu? Maana hapo mtu mmoja asemapo, Mimi ni wa Paulo; na mwingine, Mimi ni wa Apolo, je! Ninyi si wanadamu?Basi Apolo ni nani? Na Paulo ni nani? Ni wahudumu ambao kwao mliamini; na kila mtu kama Bwana alivyompa. Mimi nilipanda, Apolo akatia maji; bali mwenye kukuza ni Mungu. Hivyo, apandaye si kitu, wala atiaye maji, bali Mungu akuzaye. Basi yeye apandaye, na yeye atiaye maji ni wamoja, lakini kila mtu atapata thawabu yake mwenyewe sawasawa na taabu yake mwenyewe.Maana sisi tu wafanya kazi pamoja na Mungu; ninyi ni shamba la Mungu, ni jengo la Mungu.

 

-          Wanaweza kupelekana hata mahakamani  wala kudhulumiana 1Wakorintho 6:1-10 “ Je! Mtu wa kwenu akiwa ana daawa juu ya mwenzake athubutu kushitaki mbele ya wasio haki, wala si mbele ya watakatifu?Au hamjui ya kwamba watakatifu watauhukumu ulimwengu? Na ikiwa ulimwengu utahukumiwa na ninyi, je! Hamstahili kukata hukumu zilizo ndogo? Hamjui ya kuwa mtawahukumu malaika, basi si zaidi sana mambo ya maisha haya? Basi, mkiwa na mahali panapohukumiwa mambo ya maisha haya, mwawaweka kuwa waamuzi hao waliohesabiwa kuwa si kitu; katika kanisa? Nasema hayo nipate kuwatahayarisha. Je! Ndivyo, kwamba kwenu hakuna hata mtu mmoja mwenye hekima, awezaye kukata maneno ya ndugu zake? Bali mwashitakiana, ndugu kwa ndugu, tena mbele yao wasioamini. Basi imekuwa upungufu kwenu kabisa kwamba mnashitakiana ninyi kwa ninyi. Maana si afadhali kudhulumiwa? Maana si afadhali kunyang'anywa mali zenu? Bali kinyume cha hayo ninyi wenyewe mwadhulumu watu na kunyang'anya mali zao; naam, hata za ndugu zenu. Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti, wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang'anyi.”

Unapoangalia kwa kina na upana na urefu, watu wenye matendo haya ya mwilini wanaweza kuwapo hata makanisani katika siku za leo,  na wanaweza kuwa na muda mrefu sana katika wokovu au hata kufikia ngazi Fulani ya kiroho lakini maandiko yanasema mtawatambua kwa matunda yao, kuwajua wana wa muungwa na wana wa kijakazi kwa mujibu wa maandiko ni rahisi sana kila mmoja anapaswa kujihoji na kujichunguza kama ni mwana wa Muuungwana au ni mwana wa kijakazi na kama ni wa kijakazi au kuna tabia ya kijakazi hatuna budi kutubu na kubadilika , tuongeweze neema

 

Na Rev. Innocent Samuel Kamote

Mkuu wa Wajenzi mwenye Hekima!



Jumatatu, 11 Julai 2022

Mungu wa falme zote za Dunia !


2Wafalme 14-19 “Basi Hezekia akaupokea waraka katika mikono ya wale wajumbe, akausoma; kisha Hezekia akapanda, akaingia katika nyumba ya Bwana, akaukunjua mbele za Bwana. Naye Hezekia akaomba mbele za Bwana, akasema, Ee Bwana, Mungu wa Israeli, ukaaye juu ya makerubi, wewe, naam, wewe peke yako, ndiwe Mungu wa falme zote za dunia; wewe ndiwe uliyeziumba mbingu na nchi. Tega sikio lako, Ee Bwana, usikie; fumbua macho yako, Ee Bwana, uone; uyasikie maneno ya Senakeribu, ambayo amemtuma mtu aje nayo ili kumtukana Mungu aliye hai. Ni kweli, Bwana, wafalme wa Ashuru wamewaharibu mataifa na nchi zao, na kuitupa miungu yao motoni; kwa maana haikuwa miungu, bali ni kazi ya mikono ya wanadamu; ilikuwa miti na mawe tu, ndiyo sababu wakaiharibu. Basi sasa, Ee Bwana, Mungu wetu, utuokoe na mkono wake, nakusihi, ili kwamba falme zote za dunia zipate kujua ya kuwa wewe ndiwe Bwana Mungu, wewe peke yako.”



Utangulizi:

Ni muhimu kufahamu kuwa Maandiko yanatufunduisha kuwa maombi ndiyo nyenzo pekee inayoweza kutusaidia  wakati wowote tunapokutana na changamoto za aina yoyote zile tuwapo duniani, Jambo lolote ambalo linaweza kukuletea fadhaa katika maisha yako au familia yako, au taifa lako, tunaelekezwa kuwa wakati wa changamoto hizo ziwe za kitaifa, au kifamilia au za taasisi au mtu mmoja mmoja kwamba tumtwike yeye fadhaa zetu zote  angalia

1Petro 5:7 “huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu.”

Unaona sio fadhaa ya mtu mmoja mmoja tu bali hata fadhaa za kitaifa au kitaasisi au familia, Mungu anatuthibitishia wazi katika neno kuwa atasikiliza maombi yetu ona  2Nyakati 7:13-15 “Nikizifunga mbingu isiwe mvua, tena nikiamuru nzige kula nchi, au nikiwapelekea watu wangu tauni; ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha, na kuomba, na kunitafuta uso, na kuziacha njia zao mbaya; basi, nitasikia toka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao, na kuiponya nchi yao. Sasa macho yangu yatafumbuka, na masikio yangu yatasikiliza maombi ya watu waombao mahali hapa.”

Ni kupitia maombi Mungu atakutana na mahitaji yetu yote  kwa kadiri ya utajiri alionao katika Kristo Yesu Wafilipi 4:19 “Na Mungu wangu atawajazeni kila mnachokihitaji kwa kadiri ya utajiri wake, katika utukufu, ndani ya Kristo Yesu.”

Katika kifungu cha maandiko ya msingi Mfalme Hezekiah anaomba Hekaluni Nyumbani mwa Bwana, Hezekia alikuwa ameletewa ujumbe kwa njia ya Barua kutoka kwa mfalme Senekarebu  ambaye alikuwa mfalme mkubwa na mwenye nguvu katika nyakati zile, mfalme huyu aliweza kuwa na historia ya kuwa mshindi kwa kila taifa ambalo lilipigana naye  alipiga kila taifa na kila ufalme pamoja na miungu yao na kuichoma moto na sasa mfalme huyu alikuwa anaukaza uso wake kumjia Hezekiah kwa maana nyingine kumjia Hezekia pamoja na Mji wa Yerusalem na Israel kwa ujumla, Lakini kabla ya kumjia aliamua kumpa taarifa ya kile alichokusudia kuja kukifanya ona

2Wafalme 18:28-37 “Kisha yule amiri akasimama akalia kwa sauti kuu kwa lugha ya Kiyahudi, akasema, Lisikieni neno la mfalme mkuu, mfalme wa Ashuru. Mfalme asema hivi, Hezekia asiwadanganye; kwa maana, hataweza kuwaokoa katika mkono wake. Wala Hezekia asiwatumainishe katika Bwana, akisema, Hakika Bwana atatuokoa, wala mji huu hautatiwa mkononi mwa mfalme wa Ashuru. Msimsikilize Hezekia; kwa sababu mfalme wa Ashuru asema hivi, Fanyeni suluhu na mimi, mkatoke mnijie; mkale kila mtu matunda ya mzabibu wake na matunda ya mtini wake, mkanywe kila mmoja maji ya birika lake mwenyewe; hata nije nikawachukue mpaka nchi iliyo kama nchi yenu wenyewe, nchi ya nafaka na divai, nchi ya chakula na mashamba ya mizabibu, nchi ya mafuta ya mzeituni na asali, ili mpate kuishi, msife; wala msimsikilize Hezekia, awadanganyapo, akisema, Bwana atatuokoa. Je! Yuko mungu mmoja wa mataifa aliyewaokoa watu wake wakati wo wote na mkono wa mfalme wa Ashuru? Iko wapi miungu ya Hamathi, na ya Arpadi? Iko wapi miungu ya Sefarvaimu, na ya Hena, na ya Iva? Je! Imeuokoa Samaria na mkono wangu? Katika miungu ya nchi hizi zote, ni miungu gani iliyookoa nchi yao na mkono wangu, hata Bwana auokoe Yerusalemu na mkono wangu?  Lakini hao watu wakanyamaza kimya; wala hawakumjibu hata neno moja; maana amri ya mfalme ilikuwa kwamba, Msimjibu neno. Ndipo Eliakimu, mwana wa Hilkia, aliyekuwa msimamizi wa nyumba ya mfalme, na Shebna, mwandishi, na Yoa, mwana wa Asafu, mwenye kuandika tarehe, wakaenda kwa Hezekia, na nguo zao zimeraruliwa, wakamwambia maneno ya yule amiri.”

Vitisho hivi vilikuwa vitisho vya kweli, Mfalme Senekarebu alikuwa ameshiba kiburi cha ushindi wake kila mahali alikopita, alipiga mataifa na miungu yao aliichoma moto,  Hezekia alikuwa  hana jinsi ya aina yoyote ya kufanya ilikuwa lazima akubali kushindwa na kuweka silaha chini na kukubali kulipa kodi kwa Mfalme Senekarebu, au aingie kwenye mapigano, ilikuwa ni rahisi katika wakati kama huu kwa Hezekia kutafuta ushauri wa kibinadamu, au kuuliza kwa wenye hekima, au aingize majeshi yake vitani  au awe tayari kuharibiwa  au kukutwa na jambo baya tu huku macho yake yakishuhudia, Hezekia aliwashauri watu wake wasijibu kitu, Moyoni mwake alikuwa anajua, Mungu wa Israel ni Mungu wa tofauti na kuwa Mungu wetu ndiye Mungu wa falme zote za dunia, hivyo hangeweza kutafuta msaada wa kibinadamu, au msaada wa kijeshi kutoka kwa mataifa rafiki, Yeye alijikita katika kuutafuta uso wa Mungu aliye hai Mungu wa falme zote za dunia, na hivyo Ndipo mfalme Hezekia alipoamua kumuomba Mungu na kupeleka zile nyaraka za vitisho alizoandikiwa  kwa Mungu wa Falme zote za dunia  kwa kuwa alimjua Mungu na kumtegemea alimsifia kutoka moyoni akitambua kuwa ni Mungu pekee mwenye uweza wa kumsaidia ona

2Wafalme 14-19 “Basi Hezekia akaupokea waraka katika mikono ya wale wajumbe, akausoma; kisha Hezekia akapanda, akaingia katika nyumba ya Bwana, akaukunjua mbele za Bwana. Naye Hezekia akaomba mbele za Bwana, akasema, Ee Bwana, Mungu wa Israeli, ukaaye juu ya makerubi, wewe, naam, wewe peke yako, ndiwe Mungu wa falme zote za dunia; wewe ndiwe uliyeziumba mbingu na nchi. Tega sikio lako, Ee Bwana, usikie; fumbua macho yako, Ee Bwana, uone; uyasikie maneno ya Senakeribu, ambayo amemtuma mtu aje nayo ili kumtukana Mungu aliye hai. Ni kweli, Bwana, wafalme wa Ashuru wamewaharibu mataifa na nchi zao, na kuitupa miungu yao motoni; kwa maana haikuwa miungu, bali ni kazi ya mikono ya wanadamu; ilikuwa miti na mawe tu, ndiyo sababu wakaiharibu. Basi sasa, Ee Bwana, Mungu wetu, utuokoe na mkono wake, nakusihi, ili kwamba falme zote za dunia zipate kujua ya kuwa wewe ndiwe Bwana Mungu, wewe peke yako.”

Hezekia alikuwa anataka Mungu atukuzwe, alikuwa anataka Mungu ajidhihirishe mwenyewe kuwa yeye ni Mungu wa wote wenye mwili, na kuwa hakuna lisilowezekana kwake, Hezekia alimsifu Mungu, Hezekia hakuwa na woga alikuwa na ujasiri mkuu alimsihi Mungu aone yeye mwenyewe na kusikia maneno ya Senekarebu alionyesha ya kuwa anamtegemea Mungu tu na sio wanadamu, wala hekima ya kibinadamu, alimwambia Mungu ni kweli Senekarebu ameshambulia mataifa mengi na miungu mingi ameichioma moto na kuziharibu lakini hiyo haikuwa miungu na hayo mataifa hayakumjua Mungu aliye hai, lakini yeye alijitegemeza kwa Mungu mwenye uwezo mkubwa sana ambaye alimtambua kama Mungu wa falme zote za Dunia  nani ukweli kuwa Mungu alimjibu Hezekia kwa njia rahisi sana, Mungu ni Mungu anayesikia aliyasikia maombi ya Hezekiah na kuyajibu ona kwa kinywa cha Nabii Isaya

2Wafalme 19:32-34 “Basi Bwana asema hivi katika habari za mfalme wa Ashuru, Yeye hatauingia mji huu, wala hatapiga mshale hapa, wala hatakuja mbele yake kwa ngao, wala hatajenga boma juu yake. Njia ile ile aliyojia, kwa njia iyo hiyo atarudi zake, wala hataingia ndani ya mji huu, asema Bwana. Maana nitaulinda mji huu, niuokoe, kwa ajili yangu mwenyewe, na kwa ajili ya Daudi, mtumishi wangu.”

Wakati huu Mungu aliona afupishe safari ya mfalme Senekarebu kwa kumtumia malaika wake mmoja tu, ambaye aliwatandika jeshi zima na Senekarebu akarudi nyumbani kwake kwa njia ile ile aliyoijia sawa na lile neno ambali Bwana alinena kwa kinywa cha nabii Isaya, na kwenda kuuawa na watu wake mwenyewe ona katika ;-

2Wafalme 19:35-37 “Ikawa usiku uo huo malaika wa Bwana alitoka, akakiingia kituo cha Waashuri, akawapiga watu mia na themanini na tano elfu. Na watu walipoondoka asubuhi na mapema, kumbe! Hao walikuwa maiti wote pia. Basi Senakeribu mfalme wa Ashuru akaondoka, akaenda zake, akarudi akakaa Ninawi. Ikawa, alipokuwa akiabudu nyumbani mwa Nisroki, mungu wake, Adrameleki na Shareza wakampiga kwa upanga; wakaikimbilia nchi ya Ararati. Na Esar-hadoni mwanawe akatawala mahali pake.”

Ziko vita nyingine ambazo watu watadhani uko mwenyewe kumbe liko jeshi la malaika nani makomandoo, Mungu  na atume malaika wake akusaidie katika kila changamoto unazokutana nazo, Wakati huu Mungu alimtumia malaika mmoja tu aliyepiga watu 185000 kumbuka hii ilikuwa ni kwa watakatifu wa agano la kale, katika agano jipya tunaambiwa kuwa Malaika ni roho wanaotumwa kuwahudumia wale watakaourithi wokovu ona Waebrania 1:13-14 “Je! Yuko malaika aliyemwambia wakati wo wote, Uketi mkono wangu wa kuume Hata nitakapoweka adui zako chini ya nyayo zako? Je! Hao wote si roho watumikao, wakitumwa kuwahudumu wale watakaourithi wokovu? unaona umuhimu wa kumuomba Mungu msaada wako utakujaje Bwana anajua wewe tambua tu kuwa ndiye anayemiliki tawala zote za dunia, ninakuombea kwamba katika hali uliyo nayo Bwana Mungu na atume malaika wakabiliane na changamoto unazokutana nazo, wala usiogope liamini neno hili ambalo Bwana amenipa kwaajili yako nakuhakikishia hutalia tena wala hutafadhaika nina Mungu aliye hai kama wa Hezekia Na Mungu wangu atakutana na changamoto zako zote zinazokukabili kwa ushindi mkubwa, kisha wataaibika wanaoshindana nawe!

 

Na. Rev. Innocent Samuel Kamote         

Mkuu wa wajenzi Mwenye hekima!

Jumatatu, 4 Julai 2022

Msiwape Mbwa kilicho kitakatifu, wala msitupe lulu zenu mbele ya nguruw

Matthayo 7:6 “Msiwape mbwa kilicho kitakatifu, wala msitupe lulu zenu mbele ya nguruwe, wasije wakazikanyaga chini ya miguu yao, wakageuka na kuwararua.”                  


Utangulizi:

Ni muhimu kufahamu kuwa hapa Yesu anatumia lugha ya mfano (mficho) iitwayo Metaphor ambapo neno au maneno yanayotumika katika hali ya kawaida yanaweza kumaanisha matumizi,  ya kitu au jambo lingine au linalofanana na hilo, Yesu anawatumia umbwa na nguruwe hapa akiwaonya wanafunzi wake kuwa na ufahamu na kuelewa unyeti wa kuwapa vitu vya thamani watu wasio na shukrani, Wanyama kama mbwa na nguruwe hawawezi kufurahia uadilifu, wala kushukuru kwa sababu hawajui thamani ya kile wanachofanyiwa

2Petro 2:20-22 “Kwa maana wale waliokwisha kuyakimbia machafu ya dunia kwa kumjua Bwana na Mwokozi Yesu Kristo, kama wakinaswa tena na kushindwa, hali yao ya mwisho imekuwa mbaya kuliko ile ya kwanza. Maana ingekuwa heri kwao kama wasingaliijua njia ya haki, kuliko kuijua, kisha kuiacha ile amri takatifu waliyopewa. Lakini imetukia kwao sawasawa na ile mithali ya kweli, Mbwa ameyarudia matapiko yake mwenyewe, na nguruwe aliyeoshwa amerudi kugaa-gaa matopeni.”

Hali kadhalika wako wanadamu, ambao kwa namna moja ama nyingine, sio waadilifu, hawana moyo safi, wenye nia ovu, waliokataa kuwa na Mungu nafsini mwao hawawezi kwa namna yoyote ile  kukubaliana na maelekezo mema yanayotolewa kuhusu injili aidha pia mwisho wa kila kitu wanaweza kuwadhuru hata wale wanaoihubiri injili,  kwa ujumla ujumbe unahusu wale ambao hawawezi kukubali habari njema lakini sio tu kuikubali hatimaye kuwakataa wanaoihubiri. Au hata anayehubiriwa !

Kwa muda Mrefu sana wayahudi walikuwa wakimsubiri Masihi aliyeahidiwa kama mkombozi wao, na zaidi ya yote walikuwa wamechoshwa na hali ya kuwa watumwa wa mataifa mengine na walikuwa wkiutazamia uhuru wa kweli chini ya serikali ya kweli ambayo ingeongozwa na Masihi yaani ufalme wa Mung, Yesu alikuja akiwa anahubiri habari hizo na kuwathibitia shia kuwa ufalme wa Mungu umekaribia ona Mathayo 4:17 “Tokea wakati huo Yesu alianza kuhubiri, na kusema, Tubuni; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia.” Wale waliomuamini na kumkubali walikuwa tayari kuwashirikisha na wengine habari hii njema, lakini hata hivyo wengi hawakuiamini, badala yake walimuona kuwa mzushi na mtu ambaye anakufuru

Mark 14:61-65 “Lakini akanyamaza, wala hakujibu neno. Kuhani Mkuu akamwuliza tena, akamwambia, Wewe ndiwe Kristo, Mwana wake Mtukufu? Yesu akasema, Mimi ndiye, nanyi mtamwona Mwana wa Adamu ameketi mkono wa kuume wa nguvu, akija na mawingu ya mbinguni. Kuhani Mkuu akararua nguo zake, akisema, Tuna haja gani tena ya mashahidi? Mmesikia kufuru yake; mwaonaje ninyi? Wote wakamhukumu kuwa imempasa kuuawa. Wengine wakaanza kumtemea mate, wakamfunika uso, na kumpiga makonde, na kumwambia, tabiri. Hata watumishi nao wakampiga makofi.”

Yesu aliyasema haya mapema akiwa anaelewa kuwa ni watu wa namna gani wanamzunguka nan i mambo gani yatawatokea, watu wanaolihubiri neno la Mungu hawapendwi, ni vigumu kuwakubali watu wanaosema kweli, wanaoongoza wengi katika njia ya haki, hivyo japokuwa wanaifanya kazi iliyo njema lakini matokeo yake ni kuwa watalipwa mabaya

Yohana 16:1-4 “Maneno hayo nimewaambia, msije mkachukizwa. Watawatenga na masinagogi; naam, saa yaja atakapodhania kila mtu awauaye ya kuwa anamtolea Mungu ibada. Na hayo watawatenda kwa sababu hawakumjua Baba wala mimi. Lakini nimewaambia hayo, ili makusudi saa ile itakapokuja myakumbuke ya kuwa mimi naliwaambia. Sikuwaambia hayo tangu mwanzo, kwa sababu nalikuwapo pamoja nanyi.”

Kazi kubwa ya injili pamoja na mafanikio yake yote ni kuwapa watu uzima wa milele Yohana 10:28 Nami nawapa uzima wa milele; wala hawatapotea kamwe; wala hakuna mtu atakayewapokonya katika mkono wangu. Zawadi hii inatolewa kwa kuitangaza injili, lakini ni katika namna ya kushangaza sana wahubiri wa injili mara kadhaa wameonekana kama kitu cha kukataliwa kutupwa na kufanywa kuwa takataka za dunia, kusema vibaya kama watu waliotolewa wahukumiwe kuuawa ona

1Wakorintho 4:9-13 “Maana nadhani ya kuwa Mungu ametutoa sisi mitume mwisho, kama watu waliohukumiwa wauawe; kwa sababu tumekuwa tamasha kwa dunia; kwa malaika na wanadamu. Sisi tu wapumbavu kwa ajili ya Kristo, lakini ninyi ni wenye akili katika Kristo; sisi tu dhaifu, lakini ninyi mna nguvu; ninyi mna utukufu, lakini sisi hatupati heshima. Hata saa hii ya sasa, tuna njaa na kiu, tu uchi, twapigwa ngumi, tena hatuna makao; kisha twataabika tukifanya kazi kwa mikono yetu wenyewe. Tukitukanwa twabariki, tukiudhiwa twastahimili; tukisingiziwa twasihi; tumefanywa kama takataka za dunia, na tama ya vitu vyote hata sasa.”

Katika tamaduni za kiyahudi Umbwa na Nguruwe ni alama ya wanyama wachafu na Najisi sawa na wanavyotamkwa katika maandiko Walawi 11:7-8 “Na nguruwe, kwa sababu yeye anazo kwato, ni mwenye miguu iliyopasuka kati, lakini hacheui, yeye ni najisi kwenu. Msiile nyama yao, wala msiiguse mizoga yao; hao ni najisi kwenuwanyama hawa wanakula chochote kile na ni wakali hasa wanapojisikia njaa, wanapotumika kama mfano katika mithali kuwawakilisha wanadamu, au watu wachafu, baradhuli, wasio na uadilifu, na wapuuzi, ni ukweli ulio wazi kuwa ni udhalilishaji wa hali ya juu sana mtu akikutukana au kukuita Mbwa au nguruwe! Hususani katika jamii ya kiyahudi, lakini hata hivyo Yesu hasiti kufananisha mtu, umbwa na Nguruwe, akiwalinganisha na watu waliomkataa masihi, kusudi lake sio kuwadhalilisha, lakini mkazo wake sio watu wengine lakini wale wanaodhaniwa kuwa watu wa Mungu na kisha wanakataa karama za Mungu, na mwito wake, Hivyo Yesu anaonya kuwa usipoteze Muda na watu wanaojiita Ndugu lakini hawayahsiki mafundisho nan i wakristo wa uongo

1Wakoritho 5:11-12 “Lakini, mambo yalivyo, naliwaandikia kwamba msichangamane na mtu aitwaye ndugu, akiwa ni mzinzi au mwenye kutamani au mwenye kuabudu sanamu au mtukanaji au mlevi au mnyang'anyi; mtu wa namna hii msikubali hata kula naye.Maana yanihusu nini kuwahukumu wale walio nje? Ninyi hamwahukumu hao walio ndani?

Neno la Mungu limeagiza kuendelea kuihubiri injili na hivyo lazima tutakutana na watu mbalimbali katika kuihubiri injili 1Petro 3:15 “Mwe tayari siku zote kumjibu kila mtu awaulizaye habari za tumaini lililo ndani yenu; lakini kwa upole na kwa hofu.” Kwa hiyo hatupaswi kuogopa kuwahubiria watu habari njema, lakini wakati mwingine hatuna budi kuwa makini kwamba wako mbwa na nguruwe ambao kile unachokitoa kwao, hakitazaa matunda yanayokusudiwa na badala yake watakurarua kwa sababu hawaijui thamani ya neno la Mungu, wala hawajui thamani ya Yesu unayemuhubiri na hivyo hawawezi kukukubali wewe unayebeba mambo yale ya thamani, hii haimaanishi tuwachukie wasioamini au wale wanaoipinga injili lakini kuwa makini na kutambua kuwa tutakataliwa, na tusipoteze muda na watu wasioona umuhimu wa injili, zawadi za Mungu na kuwekeza muda wetu kwa wapinzani wa injili ambao wanaelekea shimoni na wakiishikia injili au mafundisho wanachukizwa

Mathayo 15:12-14 “Ndipo wanafunzi wake walipomwendea, wakamwambia, Wajua ya kuwa Mafarisayo walipolisikia neno lile walichukizwa? Akajibu, akasema, Kila pando asilolipanda Baba yangu wa mbinguni litang'olewa. Waacheni; hao ni viongozi vipofu wa vipofu. Na kipofu akimwongoza kipofu mwenzake, watatumbukia shimoni wote wawili.”            

Wale ambao wataipinga injili na mafundisho yetu simple rahisi tu Yesu aliagiza kuwa sio tu tuwache lakini vilevile tukung’ute mavumbi ya miguuni mwetu

Mathayo 10:14-15 “Na mtu asipowakaribisha wala kuyasikiliza maneno yenu, mtokapo katika nyumba ile, au mji ule, kung'uteni mavumbi ya miguuni mwenu. Amin, nawaambia, itakuwa rahisi nchi ya Sodoma na Gomora kustahimili adhabu ya siku ya hukumu, kuliko mji ule.”

Hata hivyo wahubiri wa injili hawapaswi kukata tamaa, na wanapaswa kuendelea kuihubiri injili, kwani sio watu wote wataipinga injili wako wale wanaomcha Mungu ambao Bwana atafungua mioyo yao ili wayatunze yale tunayoyahubiri;-

Matendo 16:13-15 “Hata siku ya sabato tukatoka nje ya lango, tukaenda kando ya mto, ambapo tukadhani ya kuwa pana mahali pa kusali; tukaketi, tukasema na wanawake waliokutana pale. Mwanamke mmoja, jina lake Lidia, mwenye kuuza rangi ya zambarau, mwenyeji wa Thiatira, mcha Mungu, akatusikiliza, ambaye moyo wake ulifunguliwa na Bwana, ayatunze maneno yaliyonenwa na Paulo.Hata alipokwisha kubatizwa, yeye na nyumba yake, akatusihi, akisema, Kama mmeniona kuwa mwaminifu kwa Bwana, ingieni nyumbani mwangu mkakae. Akatushurutisha.”

Aidha ikumbukwe kuwa wakati wote mlango mmoja wa kuihubiri injli ukifungwa Mungu atafungua mlango mwingine, kwani wako watu wenye kiu ya neno la Mungu ambao Mungu amewaandaa kuipokea injili na habari njema za Yesu Kristo bila kikwazo japo changamoto zitaendelea kuwepo ona Matendo 16:6-10 “Wakapita katika nchi ya Frigia na Galatia, wakikatazwa na Roho Mtakatifu, wasilihubiri lile neno katika Asia. Walipofika kukabili Misia wakajaribu kuenda Bithinia, lakini Roho wa Yesu hakuwapa ruhusa, wakapita Misia wakatelemkia Troa. Paulo akatokewa na maono usiku; alimwona mtu wa Makedonia amesimama, akimsihi, na kumwambia, Vuka, uje Makedonia utusaidie.Basi alipokwisha kuyaona yale maono, mara tukataka kutoka kwenda Makedonia, kwa kuwa tuliona hakika ya kwamba Mungu ametuita tuwahubiri Habari Njema.”

Aidha wahudumu wa injili wanapaswa kutambua kuwa sio kila wakati watakutana na changamoto kwani iko miji Mingine ambako Mungu ana wau wake na usalama kwaajili yetu upo Matendo 18:9-10 “Bwana akamwambia Paulo kwa maono usiku, Usiogope, bali nena, wala usinyamaze, kwa kuwa mimi ni pamoja nawe, wala hapana mtu atakayekushambulia ili kukudhuru; kwa maana mimi nina watu wengi katika mji huu.”               

Ni maombi yangu kuwa Mungu anipe watu, watakaofunguliwa na Bwana wayatunze ninayoyahubiri na kuyafundisha badala ya kuturarua, Aidha Roho Mtakatifu aendelee kufungua milango ya injili kwa wale wenye uhitaji wa kusaidiwa na Mungu atupe kukaa kwa amani pale ambako ana watu wengi na utisho wake utufunike ili maadui wa injili na ndugu za uongo wasigeuka na kutusumbua, tuendelee kulinena neno la Mungu kwa ujasiri tukijua wazi kuwa Yesu yuko Pamoja nasi, lakini tusiache kuwang’utia mavumbi wale wanaoikataa injili ili Mungu awaletee hukumu kwa haraka, kama yanenavyo maandiko! Awaye yote atakayejaribu kukupinga kwa sababu yu waihubiri injili Mungu akakutane naye, Bwana akulinde na Mbwa na Nguruwe wasioelewa utathamani wa kile ulichikibeba katika jina la Yesu!

Na. Rev. Innocent Samuel Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima!


Jumatatu, 27 Juni 2022

Imani ya kuhamisha Milima !


1Wakorintho 13:1-3 “Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao. Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, si kitu mimi. Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, kama sina upendo, hainifaidii kitu.”



Utangulizi:

Imani imekuwa ni mojawapo ya jambo Muhimu sana ambalo limeelezewa kwa ajabu katika maandiko, Imani imetumiwa na mashujaa wote wa imani tunaowasoma katika maandiko kama nyenzo ya kipekee sana ambayo iliwaletea matokeo makubwa sana katika maisha yao

Waebrania 11:32-35 “Nami niseme nini tena? Maana wakati usingenitosha kuleta habari za Gideoni na Baraka na Samsoni na Yeftha na Daudi na Samweli na za manabii; ambao kwa imani walishinda milki za wafalme, walitenda haki, walipata ahadi, walifunga vinywa vya simba, walizima nguvu za moto, waliokoka na makali ya upanga. Walitiwa nguvu baada ya kuwa dhaifu, walikuwa hodari katika vita, walikimbiza majeshi ya wageni. Wanawake walipokea wafu wao waliofufuliwa. Lakini wengine waliumizwa vibaya hata kuuawa, wasikubali ukombozi, ili wapate ufufuo ulio bora;”

Maandiko yanasema pasipo imani haiwezekani kumpendeza Mungu, mtu awaye yote anayemuendea Mungu ni lazima aamini kuwa Mungu yupo na kuwa huwapa thawabu wale wawamtafutao Waebrania 11:6 “Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao.”     Kwa msingi huo basi ni muhimu kufahamu kuwa mashujaa wote wa imani tunaowasoma katika maandiko, pamoja na mambo mengine vilevile walimuamini Mungu katika kiwango cha imani ya juu sana kiasi cha kukubalika kwa Mungu, Abraham kwa mfano alipojaribiwa na Mungu kumtoa Isaka kwa imani alikubali, yeye aliamini ya kuha hata akimkata kichwa Mungu atamfufua tena kutoka kwa wafu na atarejea na mwanaye  Waebrania 11:17-19 “Kwa imani Ibrahimu alipojaribiwa, akamtoa Isaka awe dhabihu; na yeye aliyezipokea hizo ahadi alikuwa akimtoa mwanawe, mzaliwa pekee; naam, yeye aliyeambiwa, Katika Isaka uzao wako utaitwa, akihesabu ya kuwa Mungu aweza kumfufua hata kutoka kuzimu; akampata tena toka huko kwa mfano.”

Aina za imani!

Katika agano jipya iko imani iokoayo, imani hii ni kumuamini Bwana Yesu kwa kukubali kazi aliyoifanya pale msalabani, na kwamba alikufa na kufufuka imani hii hutupa zawadi ya wokovu, imani hii kila mmoja anaweza kuipata kwa kumkubali Yesu kuwa bwana na mwokozi

Warumi 10:9-12 “Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka. Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu. Kwa maana andiko lanena, Kila amwaminiye hatatahayarika. Kwa maana hakuna tofauti ya Myahudi na Myunani; maana yeye yule ni Bwana wa wote, mwenye utajiri kwa wote wamwitao;”

Vilevile iko imani inayotokana na kuwepo kwa karama ya Roho Mtakatifu, ambayo huitwa neno la Imani au neno la mamlaka hii imetajwa katika 1Wakoritho 12:4-11 “Basi pana tofauti za karama; bali Roho ni yeye yule. Tena pana tofauti za huduma, na Bwana ni yeye yule. Kisha pana tofauti za kutenda kazi, bali Mungu ni yeye yule azitendaye kazi zote katika wote. Lakini kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa kufaidiana. Maana mtu mmoja kwa Roho apewa neno la hekima; na mwingine neno la maarifa, apendavyo Roho yeye yule; mwingine imani katika Roho yeye yule; na mwingine karama za kuponya katika Roho yule mmoja; na mwingine matendo ya miujiza; na mwingine unabii; na mwingine kupambanua roho; mwingine aina za lugha; na mwingine tafsiri za lugha; lakini kazi hizi zote huzitenda Roho huyo mmoja, yeye yule, akimgawia kila mtu peke yake kama apendavyo yeye.” Karama ya imani ni karama kwa mtu aliyeokoka kumuwezesha mtu huyo kuwa na uwezo wa kutamka neno na likawa au likasababisha muujiza mfano 1Wafalme 17:1 “Basi Eliya Mtishbi, wa wageni wa Gileadi, akamwambia Ahabu, Kama Bwana, Mungu wa Israeli, aishivyo, ambaye ninasimama mbele zake, hakutakuwa na umande wala mvua miaka hii, ila kwa neno langu.” Hapa Eliya anatamka kwa neno la Mungu na kile anachokitamka kinakuwa vilevile, Elisha pia alitamka kuuzwa kwa chakula kwa bei nafuu wakati kulikuwa na njaa kali haijawahi kutokea njaa ambayo ilipelekea hata watu kula watoto wao 2Wafalme 6:24-30 24. “Ikawa baada ya hayo, Ben-hadadi mfalme wa Shamu akakusanya majeshi yake yote, akakwea akauhusuru Samaria. Njaa ikawa kuu huko Samaria; na tazama, wakauhusuru, hata kichwa cha punda kikapata kuuzwa kwa vipande themanini vya fedha, na kibaba cha mavi ya njiwa kwa vipande vitano vya fedha. Ikawa mfalme wa Israeli alipokuwa akipita ukutani, mwanamke mmoja akamwita akisema, Unisaidie, bwana wangu, mfalme.  Akasema, Bwana asipokusaidia, nikusaidieje mimi? Ya sakafuni, au ya shinikizoni? Mfalme akamwambia, Una nini? Akajibu, Mwanamke huyu aliniambia, Mtoe mtoto wako, tumle leo, na mtoto wangu tutamla kesho.Basi, tukamtokosa mtoto wangu, tukamla; nikamwambia siku ya pili, Mtoe mtoto wako, tumle; naye amemficha mtoto wake. Ikawa, mfalme alipoyasikia maneno ya huyo mwanamke, aliyararua mavazi yake; (naye alikuwa akipita juu ya ukuta;) na watu wakaona, na tazama, alikuwa amevaa magunia ndani mwilini mwake.”  Wakati hali halisi ikiwa ngumu kwa kiasi hicho Elisha anatamka kuwa kesho panapo saa hii chakula kipimo cha unga mzuri kitauzwa kwa shekeli ona 2Wafalme 7:1-10, “Elisha akasema, Lisikieni neno la Bwana; Bwana asema hivi, Kesho panapo saa hii, kipimo cha unga mzuri kitauzwa kwa shekeli, na vipimo viwili vya shayiri kwa shekeli, langoni pa Samaria. Basi yule akida, ambaye mfalme alikuwa akitegemea mkono wake, akamjibu yule mtu wa Mungu, akasema, Tazama, kama Bwana angefanya madirisha mbinguni, je! Jambo hili lingewezekana? Akamwambia, Angalia, wewe utaliona kwa macho yako, lakini hutakula. Basi walikuwapo watu wanne wenye ukoma, penye lango la mji; wakasemezana, Mbona tunakaa hapa hata tufe?  Tukisema, Tutaingia mjini, mjini mna njaa, nasi tutakufa humo; nasi tukikaa hapa, tutakufa vile vile. Haya! Twende tukaliendee jeshi la Washami; wakituhifadhi hai tutaishi; wakituua, tutakufa tu. Basi wakaondoka kabla ya mapambazuko, ili waende mpaka kituo cha Washami; na walipofika mwanzo wa kimo cha Washami, kumbe! Hapana mtu. Kwa maana Bwana alikuwa amewasikizisha Washami kishindo cha miendo ya magari, na kishindo cha farasi, kama kishindo cha jeshi kubwa; wakaambiana, Tazama, mfalme wa Israeli amewaajiri wafalme wa Wahiti, na wafalme wa Wamisri, waje wapigane nasi. Kwa hiyo wakaondoka, wakakimbia kungali giza bado, wakaziacha hema zao, na farasi zao, na punda zao, na kimo chao vile vile kama kilivyokuwa, wakakimbia wapate kujiponya nafsi zao. Basi wale wenye ukoma walipofika mwisho wa kituo, waliingia katika hema moja, wakala, na kunywa, wakachukua fedha, na dhahabu, na mavazi, wakaenda wakavificha; wakarudi, wakaingia katika hema ya pili, vile vile wakachukua vitu, wakaenda, wakavificha. Ndipo wakaambiana, Mambo haya tufanyayo si mema; leo ni siku ya habari njema, na sisi tunanyamaza; mkingoja hata kutakapopambazuka, madhara yatatupata; basi twende tukawaambie watu wa nyumba ya mfalme. Basi wakaenda, wakawaita mabawabu wa mji; wakawaambia, Tulifika kituo cha Washami, na tazama, hapana mtu ye yote huko, wala sauti ya mtu, ila farasi wamefungwa, na punda wamefungwa, na hema zao kama walivyoziacha.”  Kisha ikawaje ona neno la Mungu alilolisema Elisha lilitimizwa vilevile kama alivyotamka 2Wafalme 7:16-20 “Basi watu wakatoka, wakaziteka nyara hema za Washami. Ikawa kipimo cha unga mzuri kikauzwa kwa shekeli, na vipimo viwili vya shayiri kwa shekeli, sawasawa na neno la Bwana. Naye mfalme akamweka yule akida, ambaye alitegemea mkono wake, awasimamie watu langoni; na watu wakamkanyaga langoni, akafa; kama alivyosema yule mtu wa Mungu, aliyenena hapo mfalme alipomshukia. Ikatukia kama vile yule mtu wa Mungu alivyomwambia mfalme, Vipimo viwili vya shayiri kwa shekeli, na kipimo cha unga mzuri kwa shekeli, ndivyo vitakavyokuwa kesho, panapo saa hii, katika lango la Samaria; na yule akida akamjibu mtu wa Mungu, akasema, Sasa tazama, kama Bwana angefanya madirisha mbinguni, je! Jambo hili lingewezekana? Akasema, Angalia, wewe utaliona kwa macho yako, lakini hutakula. Ikampata vivyo hivyo, kwa kuwa watu wakamkanyaga langoni, akafa.”   

Mungu anatutaka tuwe na imani, tujiungamanishe naye katika kiwango cha kuwa na imani ya kuhamisha milima, kimsingi Mungu hafurahii sana kuona wakristo wanashindwa jambo, Yesu aliwakemea wanafunzi wake mara kwa mara kwa sababu walikuwa wanakosa imani hii

Mathayo17:15-20 “Bwana, umrehemu mwanangu, kwa kuwa ana kifafa, na kuteswa vibaya; maana mara nyingi huanguka motoni, na mara nyingi majini. Nikamleta kwa wanafunzi wako, wasiweze kumponya. Yesu akajibu, akasema, Enyi kizazi kisichoamini, kilichopotoka, nitakaa pamoja nanyi hata lini? Nitachukuliana nanyi hata lini? Mleteni huku kwangu. Yesu akamkemea pepo, naye akamtoka; yule kijana akapona tangu saa ile. Kisha wale wanafunzi wakamwendea Yesu kwa faragha wakasema Mbona sisi hatukuweza kumtoa? Yesu akawaambia, Kwa sababu ya upungufu wa imani yenu. Kwa maana, amin, nawaambia, Mkiwa na imani kiasi cha punje ya haradali mtauambia mlima huu, Ondoka hapa uende kule; nao utaondoka; wala halitakuwako neno lisilowezekana kwenu.”          

Sasa ni imani ya namna gani inahitajika ili kuhamisha milima Yesu anasema mkiwa na imani ndogo tu kiasi cha punje ya haradali mtauambia mlima huu ondoka hapa nao utaondoka huitaji imani kubwa sana unahitaji imani kidogo sana katika Mungu kukuletea ushindi na kutoa matamshi yenye mamlaka ya kiungu na mara moja utaweza kuona dunia ikishikishwa adabu

Mathayo 13:31-32 “Akawatolea mfano mwingine, akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na punje ya haradali, aliyoitwaa mtu akaipanda katika shamba lake; nayo ni ndogo kuliko mbegu zote; lakini ikiisha kumea, huwa kubwa kuliko mboga zote, ikawa mti, hata nyuni wa angani huja na kukaa katika matawi yake.”

Kumbe kiasi cha imani kinachohitajika ni kidogo tu nah ii ni kuonyesha kuwa watu wengi hawana imani, Mungu arupe kuwa na imani, Musa alikuwa mtu wa imani na alipokuwa akitamka jambo wakati mwingine hata kabla, hajaliomba Mbingu ziliweza kutekeleza matakwa yake ona:-

Hesabu 16:28-32 “Musa akasema, Kwa jambo hili mtajua ya kwamba Bwana amenituma, ili nifanye kazi hizi zote; kwa kuwa mimi sikuzifanya kwa akili zangu mwenyewe. Kama watu hawa wakifa kifo cha sikuzote, kama watu wote wafavyo, au kama wakipatilizwa kwa mapatilizo ya watu wote; hapo basi Bwana hakunituma mimi. Lakini Bwana akiumba kitu kipya, na hiyo nchi ikifunua kinywa chake na kuwameza, pamoja na wote walio nao, nao washukia shimoni wali hai; ndipo mtatambua ya kwamba watu hawa wamemdharau Bwana Basi ilikuwa, hapo alipokwisha kusema maneno haya yote, nchi iliyokuwa chini yao ikapasuka; nchi ikafunua kinywa chake, na kuwameza, na watu wa nyumba zao na wote walioshikamana na Kora, na vyombo vyao vyote.”

Matamshi haya ya kimamlaka yatatuletea ukombozi, mkubwa sana katika maisha yetu Mungu ataifanya dunia ijuie na ifahamu ya kuwa yuko Mungu, mwenye nguvu na mamlaka nay a kuwa neno lake haliongopi kamwe, wakristo tuinuke na kuwa waombaji na kuitafuta mamlaka hii ili kushikisha adabu watu wasio na uelewa kuhusu Mungu

Ni milima ya namna gani inayozungumzwa hapa?

Niliwahi kumsikia mwanatheolojia mmoja mkubwa sana na msomi akizungumzia kuwa Yesu alipokuwa akizungumzia mlima au milima alikuwa akizungumzia mlima halisi au milima halisi, ni ukweli ulio wazi kuwa lugha inayozungumzwa kibiblia ni lugha ya kinabii,  na kinabii maandiko yanapozungumzia mlina yanamaanisha kikwazochochote kigumu, jambo lolote lililogumu, kwa hiyo inahitajika wazo la kinabii na kimaandiko kujua kuwa Yesu aliposema utahamisha mlima au Paulo mtume anapozungumzia imani ya kuhamisha milima wote kwa pamoja katika mioyo yao na jamii ya wale waliokuwa wakizungumza nao walielewa alikuwa anazungumzia vikwazo vinavyoinuka juu ya mtu, au jaribu au jambo gumu unaweza kuona, Milima hii ni vikwazo vya namna mbalimbali vinavyoweza kujitokeza katika maisha yetu, lolote linalozuia breakthrough au mpenyo katika maisha yako, upinzani, magonjwa, kifo, Magumu, yanayoonekana hayawezekani, na hali zenye utata katika maisha yetu hizi zote zinaweza kuitwa mlima ona

 Zakaria 4:6-7 “Akajibu akaniambia, akisema, Hili ndilo neno la Bwana kwa Zerubabeli, kusema, Si kwa uwezo, wala si kwa nguvu, bali ni kwa roho yangu, asema Bwana wa majeshi. Nani wewe, Ee mlima mkubwa? Mbele ya Zerubabeli utakuwa nchi tambarare; naye atalileta lile jiwe la kuwekwa juu kabisa pamoja na vigelegele vya, Neema, neema, ilikalie.”

Unaona lugha ya kinabii kamwe haimaniishi kuwa mlima unaotajwa ni mlima halisia HAPANA Mungu hawezi kupinga ana kanuni yake ya kimaumbile kumbuka wakati anaumba ulimwengu alihitimisha kwa kusema tazama kila kitu ni chema, sisi tu nao uwezo wa kuchagua ni mahali gani pa kuishi unaweza kuamua kuishi bondeni au mlimani kwa kadiri ya uumbaji wa kiungu, hatusomi katika historia wala shuhuda kuwa kuna mtu aliweza kuondoa mlima mahali, lakini kwa lugha ya kinabii mlima ni changamoto ngumu zinazikinzana na maisha yetu ya kila siku

Isaya 40:3-5 “Sikiliza, ni sauti ya mtu aliaye, Itengenezeni nyikani njia ya Bwana; Nyosheni jangwani njia kuu kwa Mungu wetu. Kila bonde litainuliwa, Na kila mlima na kilima kitashushwa; Palipopotoka patakuwa pamenyoka, Na palipoparuza patasawazishwa; Na utukufu wa Bwana utafunuliwa, Na wote wenye mwili watauona pamoja; Kwa kuwa kinywa cha Bwana kimenena haya.”

Unaona? milima hapa sio halisi ndugu zangu, milima inayotajwa hapa ni lugha ya mficho (Figurative) kama nilivyosema awali ni imani pekee ndiyo inayoweza kutuondolea mambo magumu ya kuyasawazisha hii maana yake yala yaliyoinuka juu yetu yanakuwa si kitu tena mbele yetu, kwa hiyo hakuna kitakachoweza kusimama mbele yako kutoka kwa mwaname au mwanamke kama utakuwa na imani

Marko 11:22-24 “Yesu akajibu, akamwambia, Mwaminini Mungu. Amin, nawaambia, Ye yote atakayeuambia mlima huu, Ng'oka ukatupwe baharini, wala asione shaka moyoni mwake, ila aamini kwamba hayo asemayo yametukia, yatakuwa yake. Kwa sababu hiyo nawaambia, Yoyote myaombayo mkisali, aminini ya kwamba mnayapokea, nayo yatakuwa yenu.

Mathayo 21:21-22. “Yesu akajibu, akawaambia, Amin, nawaambia Mkiwa na imani, msipokuwa na shaka, mtafanya si hilo la mtini tu, lakini hata mkiuambia mlima huu, Ng'oka, ukatupwe baharini, litatendeka. Na yo yote mtakayoyaomba katika sala mkiamini, mtapokea.”

Lugha hiyo pia ni lugha ya kukazia (hyperboles)kuonyesha namna na jinsi imani isivyoshindwa kitu na kuwa tunapomuamini Mungu na hata tunapomuomba Mungu kwa imani ni lazima tuamini na kusadiki kuwa lazima kutakuwepo matokeo makubwa sana.

Je imani yetu inaweza kuhamisha milima?

Ndio wakati wote tunapokuwa na imani imani hufanya mambo makubwa sana, lakini kuna maswala kadhaa ambayo yakikosekana katika maisha yetu tunaweza kuona mambo yakiwa ndivyo sivyo! Mathayo 17:14-21 1 “Nao walipoufikia mkutano, mtu mmoja akamjia, akampigia magoti, akisema, Bwana, umrehemu mwanangu, kwa kuwa ana kifafa, na kuteswa vibaya; maana mara nyingi huanguka motoni, na mara nyingi majini. Nikamleta kwa wanafunzi wako, wasiweze kumponya. Yesu akajibu, akasema, Enyi kizazi kisichoamini, kilichopotoka, nitakaa pamoja nanyi hata lini? Nitachukuliana nanyi hata lini? Mleteni huku kwangu. Yesu akamkemea pepo, naye akamtoka; yule kijana akapona tangu saa ile. Kisha wale wanafunzi wakamwendea Yesu kwa faragha wakasema Mbona sisi hatukuweza kumtoa? Yesu akawaambia, Kwa sababu ya upungufu wa imani yenu. Kwa maana, amin, nawaambia, Mkiwa na imani kiasi cha punje ya haradali mtauambia mlima huu, Ondoka hapa uende kule; nao utaondoka; wala halitakuwako neno lisilowezekana kwenu. [Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga.]

Wanafunzi wa Yesu walishindwa kumtoa pepo na Yesu aliwaonyesha sababu za kushindwa kwao, na kwanza aliwakemea mara kadhaa kwa sababu ya kukosa imani, kutia shaka, kuogopa jambo ambalo ni kinyume na imani.

Marko 4:40  Akawaambia, Mbona mmekuwa waoga? Hamna imani bado?”

Marko 9:19 “Akawajibu, akasema, Enyi kizazi kisichoamini, nikae nanyi hata lini? Nichukuliane nanyi hata lini? Mleteni kwangu.”

Mathayo 14:31 “Mara Yesu akanyosha mkono wake, akamshika, akamwambia, Ewe mwenye imani haba, mbona uliona shaka?

hawakuwa na imani kabisa kuna maswala kadhaa ambayo yakikosekana kwako hutawexa kuona Baraka za kiutendaji katika imani

1.       Ukikosa imani

2.       Ukiacha kuomba

3.       Ukiacha kufunga

4.       Ukiacha kulitumia neno la Mungu

Siri kubwa ya ushindi na imani inayoweza kuleta matokeo inakaa katika maswala hayo niliyoyataja ukiwa na tabia hizo unaweza kuondoa mlima wowote unaoweza kujitokeza katika maisha yako, Mathayo 17:21 “[Lakini namna hii haitoki ila kwa kusali na kufunga.]” Lakini kama inavyoelezwa katika maandiko ya kwamba silaha za vita vyetu zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome 2Wakoritho 10:4 (maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;) ni kukosa muda wa kuomba, kusoma neno la Mungu na kufunga ndiko kunakotuletea changamoto kuwa gumu katika maisha, tunapofanyia kazi maombi, neno na kufunga tunaifanya imani yetu kukomaa na kuwa kali sana  na kwa sababu hiyo hakuna mlima unaowezxa kusimamam mbele yetu neno la Mungu ambalo ni upanga war oho utarahisisha sana kazi yetu ya kuhamisha milima kwa haraka wakati wote Yesu alikema kukosekana kwa imani na mambo yanayoweza kuifanya imani kuwa imara ni hayo

Na Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima

Jumapili, 19 Juni 2022

Waandaa meza mbele yangu, Machoni pa watesi wangu !

Zaburi 23:1-6Bwana ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu. Katika malisho ya majani mabichi hunilaza, Kando ya maji ya utulivu huniongoza. Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake. Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji. Waandaa meza mbele yangu, Machoni pa watesi wangu. Umenipaka mafuta kichwani pangu, Na kikombe changu kinafurika.  Hakika wema na fadhili zitanifuata Siku zote za maisha yangu; Nami nitakaa nyumbani mwa Bwana milele.”



Utangulizi:

Moja ya zaburi maarufu zaidi duniani labda kuliko zaburi zote ni zaburi ya 23, Zaburi hii imetumiwa sana na Wayahudi na Wakristo katika ibada na maombi lakini vilevile kwaajili ya kujenga imani, Kiini kikuu cha zaburi hii ni yale maneno Bwana ndiye Mchungaji wangu maneno haya yanazigusa jamii nyingi sana Duniani, Hata huko Mesopotamia, Inasemekana kuwa Mfalme Hammurabi katika mojawapo ya hutuba yake muhimu sana aliyowahi kuitoa alihitimisha kwa kusema “Mimi ndiye Mchungaji ninayehakikisha usalama na mafanikio ya watu wangu, utawala wangu utakuwa wa haki, wenye nguvu hawatawaonea wanyonge, na hata yatima na wajane watatendewa kwa haki” maneno ya kiongozi huyu wa zamani sana yalikuwa maarufu na huenda yakawa yalichangia mtunzi wa Zaburi hii kuyachanganua kwa kina katika uimbaji wake kwa kusudi la kutambua uhusiano wake na Mungu.

Zaburi hii ina mistari michache sana lakini yenye kubeba maana pana sana na hatuwezi kwa somo moja kama hivi kugusia kila neno linalozungumziwa na zaburi hii, Hata hivyo leo Mwalimu mkuu Roho Mtakatifu anatupeleka kuutazama mstari wa tano (5) katika zaburi hii ya (23) ili tuweze kujifunza kile ambacho Mungu amekikusudia kwetu .

Katika Zaburi 23:5 Daudi anasema “WAANDAA MEZA MBELE YANGU, MACHONI PA WATESI WANGU maneno haya peke yake yanaashiria uhusiano mkubwa sana na wa karibu ulioko kati yake na Mungu, lakini sio hivyo tu mstari huu unafunua heshima kubwa sana ya kifalme ambayo mwandishi anapewa na Mungu, kwani kumbuka kuwa anayeandaa meza hapa sio Daudi bali Mungu anamuandalia Daudi meza hivyo kimsingi mahali hapa pana maana pana na kubwa sana ambayo inaweza kumfaa kila mmoja wetu leo!

Ni muhimu kufahamu kuwa katika taratibu za kifalme, unapomualika mtu ambaye unamuheshimu sana katika utawala wako basi mgeni huyo rasmi labda ni rais au mfalme wa taifa lingine kama alikuja aidha kwa mazungumzo au kwa mualiko wa serikali yako au ziara ya kuimarisha uhusiano basi inapofika jioni kiongozi huyo mualikwa huandaliwa chakula maalumu ambacho huitwa dhifa ya kitaifa kwa kusudi la kusalimiana, kubadilishana mawazo, kufarijiana, kutiana moyo kujenga mahusiano, kufurahi na kisha kula pamoja, na unapokuwa umemualika kiongozi huyo mfalme au Rais aliyemualika mfalme mwingine anapaswa vilevile kuhakikisha kuwa anatoa na huduma zote ikiwemo ulinzi mkali na hata kama ana ulinzi wake, Kwa msingi hata kama ana maadui katika taifa lake au mataifa yanayomzunguka hawawezi kumgusa akiwemo katika himaya yako na itakuwa ni aibu kubwa sana kushindwa kuimarisha ulinzi wa mgeni wako huyu wa heshima endapo atauawa mbele yako, Dhifa hii kwa kawaida huonyesha kuwa umempa heshima ya juu sana mgeni wako! Na haya ni maswala muhimu katika mambo ya kidiplomasia.

Mwaka 1969 Mwenyekiti wa chama cha ukombozi wa Msumbiji Edward Mondlane aliuawa makao makuu ya chama cha FRELIMO yaliyokuwa jijini Dar es salaam baada ya kuletewa kikapu cha zawadi ya kitabu alichokuwa akikifungua kwenye nyumba ya rafiki yake wa kimarekani aliyeitwa Betty King, bomu lililipuka na kumuaa na mpaka leo haujajulikana aliuawa na nani ingawa inahisiwa ni wapinzani wa ukomonisti, hii inatufundisha kuwa mtu anaweza kuuawa hata mahali anakodhania kuwa ni salama!

Mungu aliwahi kuwapa heshima ya kidiplomasia na kuwaandalia meza wazee 74 wanaoheshimika sana katika Israel akiwemo Musa na haruni ingawa maandiko hayaelezei kwa kina ilikuwaje kuwaje ona lakini waliandaliwa meza mbinguni

Kutoka 24:9-11 “Ndipo akakwea juu, Musa, na Haruni, na Nadabu, na Abihu, na watu sabini miongoni mwa wazee wa Israeli; wakamwona Mungu wa Israeli; chini ya miguu yake palikuwa na kama sakafu iliyofanyizwa kwa yakuti samawi, kama zile mbingu zenyewe kwa usafi wake. Naye hakuweka mkono wake juu ya hao wakuu wa wana wa Israeli; nao wakamwona Mungu, wakala na kunywa.”

Hii ilikuwa ni neema kubwa na heshima ya juu zaidi kuwahi kutokea!, Daudi anaonyesha kuwa alikuwa ana uhusiano na Mungu wa karibu mno na anadhihirisha wazi kuwa neema ya Mungu ilikuwa juu yake kiasi cha kualikwa katika uwepo wa Mungu na kuandaliwa meza, huku Mungu akimlinda dhidi ya adui zake  na kumhakikishia usalama, huku akiendelea kuonyesha wema wake kwake, Daudi alikuwa mtu wa vita kwa hiyo alikuwa na maadui wengi sana, lakini kwa heshima hii aliyopewa na Mungu, hakuna adui anaweza kumgusa watamuona tu maana ameketi kwenye meza ya mwenye nguvu na hakuna mtu wa kumgusa kwa gharama yoyote.

Jambo hili pia vilevile licha ya kumhusu Daudi, lakini pia linaihusu Israel yote, nchi ya mkanaani haikuwa ya Israel kwa asili, lakini ilikuwa ni Mungu aliyemuahidi Ibrahimu kuwa atawapa, kwa msingi huo basi Israel wamealikwa katika nchi ya Mkanaani, Mwenyeji wao ni Mungu, Israel kule kaskazini inapakana na nchi ya Lebanon, na Syria, magharibi inapakana na Jordan na kusini iko Misri na eneo la wafilisti pale Palestina (Ukanda wa Gaza) kwa kawaida  wote tunafahamu namna na jinsi Israel inavyostawi na jinsi inavyokuwa na nguvu kubwa sana ya kijeshi, huku tukifahamu kuwa inazungukwa na adui pande zote na ambao wangetamani ifutwe mara moja, lakini wako salama kwa sababu wameandaliwa meza machoni pa watesi wao mwenyeji aliyewaalika ni Mungu.

Jambo hili vilevile linaweza likalihusu kanisa kwani kanisa limepewa kazi ngumu ya kuipeleka injili lakini kwa mfano wa kondoo na mbwa mwitu, aliyetualika kuihubiri injili alisema atakuwa pamoja nasi hata ukamilifu wa dahari. Haijalishi kuwa ni changamoto za aina gani tunapitia yeye mwenyewe anajua kuwa ametutuma kama kondoo katikati ya mbwa mwitu!.

Mathayo 10:16-20 “Angalieni, mimi nawatuma kama kondoo kati ya mbwa-mwitu; basi iweni na busara kama nyoka, na kuwa watu wapole kama hua. Jihadharini na wanadamu; kwa maana watawapeleka mabarazani, na katika masinagogi yao watawapiga; nanyi mtachukuliwa mbele ya maliwali na wafalme kwa ajili yangu, kuwa ushuhuda kwao na kwa mataifa. Lakini hapo watakapowapeleka, msifikiri-fikiri jinsi mtakavyosema; maana mtapewa saa ile mtakayosema. Kwa kuwa si ninyi msemao, bali ni Roho wa Baba yenu asemaye ndani yenu.”

Hata hivyo pamoja na hatari zote zinazoweza kumzunguka mtu mmoja mmoja au Israel au kanisa au wewe kumbuka Zaburi hii ya 23 ina maana panasana katika maisha yako yenyewe inaaanza kwa kusema Bwana ndiye Mchungaji wangu, sitapungukiwa na kitu, Na katika kuandaliwa meza kumbuka kuwa ni Mungu mwenyewe ndiye aliyekualika na ni yeye ndiye aliyekuheshimisha kwa hiyo zaburi hii inataka tuwe na ujasiri uliopitiliza na kutokuogopa!.

Zaburi hii inamtia nguvu kila mmoja kujua ya kuwa Mungu yuko pamoja nasi, na kuwa hatutapungukiwa na kitu, na kuwa lazima tuwe na ujuzi kuwa Mungu yuko pamoja nasi na kuwa hatatupungukia wala hatatuacha, haijalishi tunapitia maswala gani magumu au laini hata yawe mazingira yenye kutishia amani yetu na usalama wetu, Mungu atajishughulisha na kutupatia mahitaji yetu huku akituhakikishia usalama wetu.

Wafilipi 4:19 “Na Mungu wangu atawajazeni kila mnachokihitaji kwa kadiri ya utajiri wake, katika utukufu, ndani ya Kristo Yesu.”

Mungu anapotuandalia meza kazi yetu ni kusubiri tu, hatupaswi kuwa na wasiwasi kama ilivyo kwa wageni wengine unatulia tu mwenyeji wako anajua unachohitaji na anaweza kukuuliza akuletee kinywaji gani, unapokuwa unaandaliwa meza haupambani ukae wapi, haupambani ule nini,   haupambanii usalama wako ni yeye aliyekualika anajua unayoyahitaji kwa msingi huo unapaswa kuwa na utulivu, huwezi kujiandalia mwenyewe  ni aibu umealikwa sebuleni kwa mtu kisha unaanza kufungua friji, unaingia jikoni, unaulizia matunda na kadhalika  Hapana haipaswi kuwa hivyo kwani yeye anayeandaa meza ataleta kila tunachiokihitaji, Israel walipokuwa wanaalikwa katika inchi ya kanaani mwenyeji wao aliwapa maji, aliwapa na mana wakala na aliwapa kware walipolilia.

Kutoka 16:14-16 “Na ulipoinuka ule umande uliokuwa juu ya nchi, kumbe! Juu ya uso wa bara kitu kidogo kilichoviringana, kidogo kama sakitu juu ya nchi. Wana wa Israeli walipokiona, wakaambiana, Nini hiki? Maana hawakujua ni kitu gani. Musa akawaambia, Ndio mkate ambao BWANA amewapa ninyi, mle. Neno hili ndilo aliloagiza BWANA, Okoteni ninyi kitu hicho kila mtu kama ulaji wake ulivyo; kichwa pishi, kama hesabu ya watu wenu ilivyo; ndivyo mtakavyotwaa, kila mtu kwa ajili ya hao walioko hemani mwake.”

Daudi kwa zaburi hii alikuwa anamuamini Mungu ana ujasiri katika Mungu anamjua Mungu kuwa hawezi kumuangusha yeye atatupa mahitaji yetu kwa kadiri ya neema ya uhitaji wetu maandiko yanaema katika  Waebrania 4:16 “Basi na tukikaribie kiti cha neema kwa ujasiri, ili tupewe rehema, na kupata neema ya kutusaidia wakati wa mahitaji.”

Mungu ndiye mwenyeji amemkaribisha mgeni kwenye dhifa maana yake ni nini kila kitu kimekwisha kuandaliwa kwaajili yake, ni yeye ndiye aliyetupa mwaliko sisi sio wazamiaji, hivyo tunamtegemea yeye kwa mahitaji yetu yote ya kimwili na kiroho na muhimu zaidi atatulinda Mungu sio tu atatupatia kila tunachikihitaji katika ulimwengu huu lakini kama Mungu atakuwa pamoja nasi milele

2Petro 1:3 “Kwa kuwa uweza wake wa Uungu umetukirimia vitu vyote vipasavyo uzima na utauwa, kwa kumjua yeye aliyetuita kwa utukufu wake na wema wake mwenyewe.”

Kwa msingi huo Zaburi ya 23:5 inapandisha chati ya mwamini ambaye amealikwa katika karamu ya mwana kondoo na katika uwepo wa Mungu uhakika wa wema na fadhili za Mungu kutufuata siku zote za maisha yetu na kukaa katika uwepo wake milele

 

Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima.

Jumanne, 14 Juni 2022

Kaburi liko wazi!

Luka 24:1-3 “Hata siku ya kwanza ya juma, ilipoanza kupambazuka, walikwenda kaburini, wakiyaleta manukato waliyoweka tayari. Wakalikuta lile jiwe limevingirishwa mbali na kaburi, Wakaingia, wasiuone mwili wa Bwana Yesu.”


Utangulizi: 

Moja ya mambo ambayo wanadamu wengi sana huyaogopa duniani ni pamoja na Kaburi, au eneo la makaburini, sehemu nyingi sana duniani na katika jamii nyingi duniani kumekuwepo na hofu ya aina Fulani ambapo watu huogopa sana kaburi au makaburini, lakini sio hivyo tu hata pamoja na kuweko kwa hofu ya kifo, bado watu wengi wanahofia tukio la kuzikwa wakifikiri ni moja ya tukio gumu, au wakidhani kuwa wanaweza kuzikwa wakiwa na fahamu zao, au wakifikiri itakuwaje kama itatangazwa kuwa nimekufa kwa bahati mbaya kisha nikashituka nikiwa kaburini hofu ya aina hii imekuwepo kwa miaka mingi, katika lugha ya kiyunani (Greek) hofu hii ya kisaikolojia kwa kiyunani inaitwa TAPHOPHOBIA  neno hilo ni neno la kiyunani lenye muunganiko wa maneno makuu mawili TAPHO – ambalo maana yake ni Kaburi (Grave) na PHOBIA – Maana yake hofu, kwa hiyo neno TAPHOPHOBIA maana yake ni hofu ya kaburi, kwa hiyo kimsingi watu wengi sana wanaogopa kifo lakini hata hivyo ni ukweli uliowazi kuwa watu wengi wanaogopa zaidi kaburi, kwa hiyo kuna hofu ya kifo na kuna hofu ya kaburi, au hofu ya kufikia mwisho!, sasa basi ni muhimu kufahamu kuwa kufufuka kwa Yesu, sio tu kunatusaidia kutokuogopa kifo lakini vilevile kunatusaidia kutokuogopa nguvu za kaburi au kuzimu! Tutajifunza somo hili kwa kuzingatia vipengele vitatu vifuatavyo:-

·        
  
Kuzikwa kwa Yesu Kristo.

·         Umuhimu wa kaburi lililo wazi.

·         Kaburi liko wazi.

Kuzikwa kwa Yesu Kristo.! 

Mara kadhaa tumezungumzia sana kuhusu Mateso ya Bwana wetu Yesu, na huenda wahubiri wengi hawajawahi kuzungumzia kuhusu kuzikwa kwa Yesu Kristo, lakini ni muhimu sana kuuthibitishia ulimwengu kuwa Kristo alizikwa, kuzikwa kwa Yesu Kristo ni moja ya jambo, Muhimu sana katika injili kwa sababu Manabii waliliona  na kulitabiria pia kama walivyotabiria mambo mengine. 

Isaya 53:8-9 “Kwa kuonewa na kuhukumiwa aliondolewa; Na maisha yake ni nani atakayeisimulia? Maana amekatiliwa mbali na nchi ya walio hai; Alipigwa kwa sababu ya makosa ya watu wangu. Wakamfanyia kaburi pamoja na wabaya; Na pamoja na matajiri katika kufa kwake; Ingawa hakutenda jeuri, Wala hapakuwa na hila kinywani mwake.” 

Unaweza kuona Isaya nabii aliyeishi miaka 700 kabla ya Kristo, alitabiri kuhusu kuzikwa yaani kufanyiwa kaburi kwa Yesu Kristo, Hili ni jambo la msingi sana kama sehemu ya injili unapozungumzia mateso ya Kristo na hata kufufuka kwake basi tukio la kuzikwa ni la muhimu na ni sehemu ya injili ambayo hata Paulo Mtume alikabidhiwa ona 

1Wakorintho 15:1-4 “Basi, ndugu zangu, nawaarifu ile injili niliyowahubiri; ambayo ndiyo mliyoipokea, na katika hiyo mnasimama, na kwa hiyo mnaokolewa; ikiwa mnayashika sana maneno niliyowahubiri isipokuwa mliamini bure. Kwa maana naliwatolea ninyi hapo mwanzo yale niliyoyapokea mimi mwenyewe, ya kuwa Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu, kama yanenavyo maandiko; na ya kuwa alizikwa; na ya kuwa alifufuka siku ya tatu, kama yanenavyo maandiko;” 

Unaweza kuona kumbe unabii na injili vyote vinakazia swala zima la kuwa Yesu alizikwa, mtu akifa hilo ni jambo lingine na akizikwa hilo ni jambo lingine, Neno kuzikwa katika kiingereza linatumika neno “Burial” au “Interment” au “inhumation” ambalo maana yake ni hatua ya mwisho kabisa ya kuwepo duniani kwa kuuweka mwili wa Mwanadamu chini au kuuchoma (Cremation) au kuufungia na kuhitimisha huzuni au huruma kwa kumuweka mtu au mwili wake na kuufunika kabisa, kwa hiyo licha ya kufa ukizikwa maana yake umetoweka kabisa, kibinadamu imethibitika na kukubalika kuwa huwezi kuweko tena, Hivyo Yesu alizikwa maana yake ilithibitishwa kuwa hawezi kuweko tena kabisa duniani, lakini na pamoja na tendo hilo, serikali ya kirumi iliweka walinzi ili kuhakikisha kuwa pale alipozikwa hakuna kitu kinaweza kubatilika. Kimsingi jamii inapomzika mtu maana yake imekubali kuwa asiweko tena kabisa duniani! Sasa Yesu alizikwa lakini sio kuzikwa tu na ulinzi uliwekwa kuhakikisha kuwa amezikika. 

Mathayo 27:62-66 “Hata siku ya pili, ndiyo iliyo baada ya Maandalio, wakuu wa makuhani, na Mafarisayo wakamkusanyikia Pilato, wakasema, Bwana, tumekumbuka kwamba yule mjanja alisema, alipokuwa akali hai, Baada ya siku tatu nitafufuka. Basi amuru kwamba kaburi lilindwe salama hata siku ya tatu; wasije wanafunzi wake wakamwiba, na kuwaambia watu, Amefufuka katika wafu; na udanganyifu wa mwisho utapita ule wa kwanza. Pilato akawaambia, Mna askari; nendeni mkalilinde salama kadiri mjuavyo. Wakaenda, wakalilinda kaburi salama, kwa kulitia lile jiwe muhuri, pamoja na wale askari walinzi.” 

Asee sio tu kuwa mtu amekufa hapa lakini AMEZIKWA na hata maziko yake yanawekewa ulinzi kwa siku tatu, kuhakikisha kuwa hafufuki mtu, ndio maana katika nguvu ya injili hatuwezi kamwe kupuuzia swala la kuzikwa “ALITESWA, AKAFA AKAZIKWA…”  Wako watu katika maisha yako sio tu unapokuwa umesitawi inawapa shida sana, na watatamani uharibikiwe, upotee na ikiwezekana historia yako ifutike na usambaratike kabisa wanaweza hata kulinda hata taarifa zako zisisambae watakuchafua ikiwezekana usisimame milele hawa wanataka kukufuta “inhumation” “Cremation” kuhakikisha kuwa hauko tena hata tuta lako la kaburi lisiweko, ni kama kwa kaburi la Colonel Muammar Gadafi, au Osama Bin Laden wameuawa na makaburi yao yamefutika hawako kabisa, waliochukizwa nao hawakutaka hata wazikwe katika hali ya kawaida, wawe wamefutika hivyo ndivyo adui za Kristo Yesu walivyotaka iwe, kwa hiyo kuzikwa, kutoweka kusahaulika ni sehemu ya injili unaposema Yesu aliteswa, akafa usiseme tu akafufuka siku ya tatu kumbuka alizikwa! 

Umuhimu wa Kaburi lililo wazi. 

Kufufuka kwa Yesu Kristo ndio moja ya muujiza Mkubwa sana katika ukristo, kama Yesu hangelifufuka imani yetu ingekuwa ni imani potofu na ya hovyo kabisa kuliko zote, nisikilize ni kufufuka kwa Yesu Kristo pekee kunakotuthibitishia uwezo wa Mungu kwamba hatuwezi kukata tamaa katika jambo lolote lile, Kaburi lililo wazi ni ushahidi ulio wazi wa kutimizwa kwa unabii wa Mfalme Daudi ya Kwamba Mungu hatamuacha Mtakatifu wake aone uharibifu

Zaburi 16:10 “Maana hutakuachia kuzimu nafsi yangu, Wala hutamtoa mtakatifu wako aone uharibifu.”

Kaburi lililo wazi ni ishara iliyowazi ya ushindi unaobainisha kuwa Mungu anauwezo wa kufufua hata pale mtu anapofikia hatua ya kuzikwa, Yesu yuko hai nani wazi kuwa nguvu ileile iliyomfufua Yesu Kristo ina uwezo wa kufufua lolote katika maisha yetu ambalo linaonekana kama linataka kufa na hata kama limekufa machoni pa watu, Bado ana uwezo wa kulifufua.

Warumi 8:11 “Lakini, ikiwa Roho yake yeye aliyemfufua Yesu katika wafu anakaa ndani yenu, yeye aliyemfufua Kristo Yesu katika wafu ataihuisha na miili yenu iliyo katika hali ya kufa, kwa Roho wake anayekaa ndani yenu” 

Nyakati za zamani sana alama ya wakristo ilikuwa sio msalaba ilikuwa ni kaburi lililowazi, kaburi lililo wazi ni ishara ya kuwa Yesu amefufuka na kuwa Mauti haimuwezi, ni ishara kwetu kuwa hakuna mtu anaweza kuifuta historia ya kuwepo kwa masihi, ni ushahidi kwetu kuwa Mungu wetu yu hai na ana nguvu, ni ishara kwetu kuwa hata kama watu watakukusudia ufutike hawataweza kukufuta wewe juu ya uso wa dunia, Kaburi lilowazi ni ushahidi kuwa yuko mwenye mamlaka mmoja tu mwenye ufunguo ambao akifunga hakuna afunguaye wala akifungua hakuna awezae kufunga mwenye mamlaka ya kufisha na kuhuuisha ni Yesu pekee! 

Ufunuo 1:17-18 “Nami nilipomwona, nalianguka miguuni pake kama mtu aliyekufa. Akaweka mkono wake wa kuume juu yangu, akisema, Usiogope, Mimi ni wa kwanza na wa mwisho, na aliye hai; nami nalikuwa nimekufa, na tazama, ni hai hata milele na milele. Nami ninazo funguo za mauti, na za kuzimu.” 
     

Kaburi liko wazi!

Msikilizaji wangu mpendwa nimepewa mamlaka ya kukutangazia ya kuwa kaburi liko wazi, tutaweza kupitia kila aina ya changamoto tuwapo duniani, kila aina ya mawimbi na mateso na matukano na dharau za watu, watu wanaweza kupanga mikakati ya kishetani katika kuhakikisha kuwa tunapotea na kutoweka na kuwa historia yetu inafagiliwa na kufutiliwa mbali na tunazikwa na kaburi zetu zinawekewa muhuri kuhakikisha ya kuwa hatuchomoki lakini nataka nikutangazie kuwa kaburi liko wazi, hakuna mahali ambako mkono wa Mungu hauwezi kufika na kukuchomoa, alimezwa Yona na nyangumi na nyangumi akamtapika, alimezwa Yesu na Kaburi na kaburi likamtapika, aliwekwa Danieli katika tundu la simba na makanwa ya simba yakazuibwa, walitupwa Daniel, Shadrak na Abednego na katika tanuri ya moto yaani kaburi la moto ili wafanyiwe “Cremation” lakini mauti ilishindikana nakutangazia kwa jina la Yesu Kristo hakuna mauti katika kazi yako, hakuna mauti katika masomo yako, hakuna mauti katika ndoa yako, hakuna mauti katika biashara yako, hakuna mauti katika sifa zako, hakuna mauti katika familia yako hakuna mauti kokote kule itakayokuweza! Ndio maana kaburi liko wazi, kaburi lililo wazi ndio kiini cha injili inayotuthibitishia kuwa Yesu yu hai, mtetezi wetu yu hai hajafa naye atasimama juu ya nchi apate kututetea, kila mauti inayokusudiwa, katika kila sehemu ya maisha yako naitangazia kuwa Kaburi liko wazi, mwambie shetani kaburi liko wazi, mwambie adui yako kaburi liko wazi, kaburi lililo wazi ni ishara ya kuwa kuna maitumaini kila wakati na kuwa Mungu hatatuacha tuone uharibifu wa namna yoyote! Na badala yake tutawaona adui zetu wakitoweka kwa haraka.!

 

Rev. Innocent Samuel Kamote

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima!