Jumanne, 28 Oktoba 2014

Jinsi Ya Kumpokea Roho Mtakatifu


“Je Unajua kuwa watumishi wengi sasa wanaogopa kufanya maombezi ya kuombea watu ujazo wa Roho Mtakatifu? Wasaidie ili wapate ujasiri wa kuwaombea watu wangu ili wapokee Roho Mtakatifu hii ni zawadi ya hali ya juu niliyowaahidia watu wangu lakini inakuwa kama Historia unadhani ni kwa nini? Kamote! Ahaa ni kwa sababu wengi wanajifikiri kuwa kuna watu maalumu sana wanaopaswa kufanya maombezi haya tafadhali nikumbushie watu wangu” 

      Yalikuwa maneno ya kuhuzunisha ya Roho wa Mungu wakati ananisukuma kuandika kijitabu hiki kwa hivyo kiko mikononi mwako kwa kusudi la Mungu na kwa mapenzi kamili ya Mungu, unataka nani aje kanisani kwako au nani asaidie wakristo wengine kupokea Roho Mtakatifu? Kwa nini somo hili linakwepwa siku za leo? Watenda kazi wengi hawajajua namna ya kuombea wengine kumpokea Roho Mtakatifu kwa sababu hiyo nawaandikia ninyi watenda kazi ili kwamba mfunguliwe macho na kuona umuhimu wa kuifanya huduma hii ambayo ni mapenzi ya Mungu kabisa.


      Wenzetu nyakati za kanisa la kwanza Tangu walipotambua umuhimu wa waamini kujazwa Roho Mtakatifu walitilia maanani sana swala zima la kufanya maombezi ili watu wampokee Roho Mtakatifu mara tu walipoamini angalia kwa mfano Matendo 8;14-17


       Biblia inasema “Na mitume waliokuwako Yerusalem waliposikia ya kwamba Samaria imelikubali neno la Mungu wakawapeleka Petro na Yohana ambao waliposhuka wakawaombea wampokee Roho Mtakatifu kwa maana bado hajawashukia hata mmoja wao ila wamebatizwa tu kwa jina lake Bwana Yesu Ndipo wakaweka mikono juu yao nao wakampokea Roho Mtakatifu” 



         Swala la maombezi ya aina hii lilikuwa ni swala la kawaida kwa wenzetu walikuwa na ujasiri katika huduma hii ya maombezi kwaajili ya ujazo wa Roho Mtakatifu hawakusita!, kushuka kwa mitume hapa kuna maana zaidi ya kumuunga mkono Filipo na kuonyesha kushirikiana naye katika huduma hii swala hili halina maana ya kutuambia kuwa ni watu maalumu tu wenye mamlaka ya kuombea wengine kumpokea Roho tunachoweza kusema ni kuwa mitume waliona umuhimu mkubwa sana kwa watu kupokea Roho walikuwa na shauku kile walichokipokea na wengine wakipokee.


       Kwa muhktasari tunaweza kusema kuwa Roho Mtakatifu ni Suluhisho la matatizo yoote katika kanisa au kiboko cha matatizo yoote na hii ndio maana Nyakati za kanisa la kwanza alipewa kipaumbele kinachostahiki Luka 24;49 Matendo1;8. Nyakati za kanisa la kwanza swala la Roho Mtakatifu lilipewa kipaumbele kama swala la sala ya toba Matendo 8;14 na 19;1-7 Je mlimpokea Roho takatifu hapo mlipoamini? Lilikuwa moja ya maswali ya muhimu sana alilouliza Paulo mtume katika kutaka kuthibitisha kuwa washirika wake wanakuwa imara katika maswala ya kiroho je wakati wa leo tunatoa nafasi kwa kiasi gani kwa Roho Mtakatifu kupokelewa katika kanisa Bwana anahuzunika sana anapoona tumeacha sio tu kuombea lakini hata kufundisha kuhusu Roho Mtakatifu limekuwa swala adimu sana. 


Wengi wanaogopa wanafikiri kuwa wanaweza kuita watu kupokea Roho Mtakatifu kisha kusitokee lolote Huku ni kukosa Imani na kusababbisha matatizo katika kanisa la Mungu kama kuna upungufu wa aina yoyote leo katika kanisa basi tunapaswa kurudi kwenye msingi na kujiuliza kwa ni nini wenzetu walimpa kipaumbele hii ni kwa sababu walijua kuwa; Roho Mtakatifu ni suluhisho kwa tatizo la Kimaongozi Ni suluhisho la uadui Ni suluhisho la uonevu, suluhisho la upinzani wa kidini Ni suluhisho dhidi ya nguvu za giza uchawi, Ni suluhisho dhidi ya mateso na uonevu wa Ibilisi Ni suluhisho kwa woga kukata tamaa na kukabiliana na changamoto za ulimwengu huu, Nisuluhisho la hekima tunapokuwa katika hali ya kutokujua nini cha kufanya, Ni suluhisho la kutokuweko kwa Karama za Rohoni kwa msingi huo somo hili msikilizaji wangu linakusudia ili uwe Baraka katika maisha yako ya huduma na utumishi naaminikuwa ni kwa ufupi lakini Baraka zake zitakuwa kubwa sana utahisi uwepo wa Mungu tangu unapoanza kufuatilia habari hizi za Roho Mtakatifu na namna ya kuwasaidia watu kupokea Ubarikiwe na Bwana Ndimi mjoli mwenzenu shambani mwa Bwana Mchungaji Innocent Kamote.


SURA YA KWANZA: MAMBO YA MSINGI YA KUZINGATIA.


Kabla ya kujadili kuhusu hatua za kumuongoza mtu anayetaka kubatizwa katika Roho Mtakatifu kwa mara ya kwanza ni muhimu kwetu kuzingatia maswala muhimu yafuatayo. Kwanza ni nani anaweza kujazwa na Roho Mtakatifu, Pili ni nani anaweza kuomba na wengine kumpokea Roho Mtakatifu na Tatu Mambo yanayoambatana na kumpokea Roho Mtakatifu.


Kwanza Ni nani anaweza kujazwa Na Roho Mtakatifu


Roho Mtakatifu ni ahadi ya Mungu Baba na inaweza kupokewa na mtu yeyote aliyezaliwa mara ya pili yaani aliyeokoka, hili ni jambo la msingi. Kwa msingi huo kupokea Roho Mtakatifu sio swala la wakristo waliofikia ngazi Fulani ya kiroho au waliookoka muda mrefu a kufikia ukomavu Fulani wa kiroho wala sio kwa daraja la watu Fulani muhimu katika dhehebu Fulani ni ahadi ya Mungu kwa wakristo wote wamjiao Bwana kwa kila kizazi Matendo ya Mitume 2;17-18,38-39.


Pili Ni nani anaweza kuomba Na wengine kumpokea Roho Mtakatifu


Kumbuka kuwa swala la kuombea wengine kumpokea Roho Mtakatifu pia sio la watu Fulani maalumu hili ni la kila mtu ambaye amekwisha jazwa nguvu na kumpokea Roho Mtakatifu na sharti la kutaka kuwaombea wengine ujazo wa Roho Mtakatifu ni kutamani kuona wengine wakipokea ahadi hii yenye Baraka na kufurahia kuona wengine wakibarikiwa na kutumiwa na Mungu Matendo 8;14-17.



Mambo yanayoambatana na kumpokea Roho Mtakatifu.



Ni muhimu kwa kila mtenda kazi kuwa na ufahamu kwamba kuna maswala matano muhimu yanayohusika kama ishara ya mtu kumpokea Roho Mtakatifu maswala hayo ni shauku au hamu, Imani, maombi, utii, na kujiachilia katika neema ya Mungu.



1.       Shauku au Hamu.


Biblia inakazia umuhimu wa kuwa na kiu au shaku au hamu Biblia inasema “Heri wenye njaa na kiu ya haki maana hao watashibishwa” Mathayo 5;6, mtu mwenye njaa na kiu humtafuta Mungu kwa Bidii na kila unapomtafuta Mungu kwa bidii hupatikana Yeremia 29;13,”Nanyi mtanitafuta na kuniona  mtakaponitafuta kwa moyo wenu wote” Tafuteni nanyi mtaona Luka 11:9 Mtu awaye yote mwenye kiu na hamu na shauku na kuvumilia katika kutamani kuendelea kujazwa na nguvu za Roho Mtakatifu atapewa, kwa hiyo kiu na hamu au shauku ni ya Muhimu sana.



2.       Imani.


Imani ni nguzo ya msingi na muhimu katika kupokea nguvu za Roho Mtakatifu au kiu chochote kutoka kwa Mungu, Paulo anawakumbusha wakristo wa Galatia kuwa walimpokea Roho Mtakatifu kwa imani na sio kwa kutokana na matendo ya sheria ni kwa kuamini Wagalatia 3;2 Yesu alisema yeyote Aniaminiye mimi  kama vile maandiko yalivyonena mito ya maji yaliyo hai (yaani Roho Mtakatifu) atatiririka ndani yake Yohana 7;38 kwa msingi huo ni wajibu wa kila mtu anayetaka kuwaombea wengine ujazo wa Roho Mtakatifu kuwapandisha wapokeaji wake imani


3.       Maombi.


Roho Mtakatifu hutolewa kama jibu la maombi yanayoambatana na imani, Yesu alisema ombeni nanyi mtapewa Luka 11;9, sehemu nyingine alifundisha akisema kila muombalo aminini ya kuwa limekuwa lenu Marko 11;24-25, Kumbuka kuwa wakati Yesu alipokuwa anaomba ndipo Roho alipompaka mafuta Luka 3;21-22, ni jambo kama hilo liliwatokea wanafunzi siku ya Pentekoste walikuwa wamejifungia wakiomba Matendo 1;14, Kabla Paulo mtume hajajazwa Roho alikuwa na Muda wa kuomba Matendo 9;11 kwa msingi huo kila mtu anayetaka kujazwa na nguvu za Roho Mtakatifu anapaswa kuomba kwa bidii na kwa sauti kubwa.



4.       Utii.


Moyo wa utii ni wa muhimu sana katika kumpokea Roho Mtakatifu, Petro alisema Mungu anampa Roho Mtakatifu kwa wote wamtiio Matendo 5; 32, alikuwa akizungumza kuhusu wale watakaomtii Mungu na kuiamini injili yake Mstari 29-32 na kusudi la msingi la kumpokea Roho Mtakatifu pia ni kwaajili ya kushuhudia Matendo 1;8 na Mungu Yuko tayari kumpa nguvu kila mtu ambaye yuko tayari kwaajili ya kazi yake na kutii agizo kuu.



5.       Kujiachilia katika neema ya Mungu.


Kujiachilia kwa Mungu au kujinyenyekeza ni moja ya hatua nyingine muhimu katika kumpokea Roho Mtakatifu, Kama ilivyo kwa mtu anayebatizwa katika maji anapaswa kujinyenyekeza kwa Mchungaji anyembatiza, Kujazwa kwa Roho Mtakatifu nako kwahitajiwa kwa mtu kujiachilia katika neema ya Mungu ni lazima ukubali kufuata maelekezo ya Bwana huku ni kujiachia Mwili nafsi na roho Warumi 6:13, 12:1 ni kwa kupitia kujitoa na kujinyenyekeza katika neema yake ndipo Roho wa Mungu anachukua nafasi na hatimaye kukuwezesha kuzungumza kwa lugha.






HATUA ZA NAMNA YA KUMUOMBEA MTU ILI AMPOKEE ROHO MTAKATIFU


Hapa naweza kupendekeza hatua tatu za kichungaji za kuweza kumuombea mtu akampokea Roho Mtakatifu aina hizi za maombi ni pamoja na mahojiano, kuingia katika maombezi, na Muongozo kabla ya maombi


1.       Hatua za mahojiano.


Endapo utatumia njia hii ya majojiano latika kutaka kumuombea mtu ujazo wa Roho Mtakatifu unapaswa kuzingatia maswala muhimu manne kwanza ikiwa ni pamoja na kustawisha uhusiano mwema na muhitaji yaani kutafuta kujenga mahusiano naye kisha utatakiwa kumshawishi na kuikuza imani ya muhitaji na tatu unatakiwa kuelewa au kugundua hali halisi ya muhitaji kuwa ana kiu kiasi gani na mwisho utamfundisha muhitaji kipi anatakiwa akifanye ili apokee Roho Mtakatifu.

§  Kustawisha uhusiano hili ni kusudi la kwanza kabisa katika kifikia hatua ya kumpokea Roho unapaswa kuwa umemfahamu vema na kama yeye hakufahamu ni vema na yeye akakufahamu unaweza kuzungumza jambo ambalo litamfanya yeye kujisikia vema na salama, kisha mpe nafasi ya kujieleza kila anachokihitaji msikilize vema kila anachokieleza na wakati wote tumia jina lake kila unapowasiliana naye.



§  Chochea na kukuza imani yeke ni muhimu sana kjaribu kuinua imani ya muhitaji na kuichochea unaweza kumueleza jinsi unavyofurahishwa na jinsi alivyoitikia swala la kuja kumpokea Roho Mtakatifu, umefanya uamuzi ulio sahii sana unaweza pia kumuhakikishia kuwa hii itakuwa siku ya kihistoria katika maisha yake na kuwa Mungu ana kitu maalumu sana kwaajili yake  na inawezekana kuwa muhitaji anaweza asiwe na ujuzi kuhusu hilo lakini kwa ujumla linamuandaa katika kufungua moyo wake kumpokea Roho Mtakatifu.



§  Gundua hali halisi ya muhitaji moja ya mambo muhimu ya kutafuta wakati huu ni kujua kwanini muhitaji amekuja mbele na kugundua uthamani na uelewa wake na kuwa yuko kiwango gani cha kiroho unaweza kumuhoji swali kama je unahisi umekuja kujazwa kwa nguvu za Roho Mtakatifu? Usihisi Bali tambua ya kuwa amekuja kujazwa anaweza kuwa amekuja kwa sababu nyingine kwa hiyo unaweza kujenga imani yeke kuwa kupokea hili kunaweza kuwa suluhu pia la mahitaji yake mengine. Mengi ya maelekezo haya pia huweza kutolewa kwa njia ya mahubiri au wakati wa huduma ya madhabahuni.unaweza pia kumuuliza kama aliwahi kujazwa kabla na kama aliwahi kujazwa kabla anaweza kukushirikisha ilivyokuwa japo kwa mukhtasari na kama hakuwa amejazwa atahitaji kujazwa anahitaji maelekezo zaidi. Unaweza pia kumuuliza kama alishawahi kumuona mtu aliyejazwa kwa Roho Mtakatifu anaweza kuwa na wazo sahii ya kile anachokitegemea na kama sivyo anahitaji ufafanuzi zaidi endapo utakuwa umemaliza kumuuliza maswali haya na kumsikiliza vema na kujibu maswali yake vemandipo itakapokuwa rahisi kwako kumpeleka katika hatua nyingine.



§  Mafundisho wakati huu sasa mtenda kazi wa Bwana utatakiwa kufanya maswala ya msingi mawili moja likiwa ni kuchochea imani ya muhitaji katika moyo wake na kumleta sasa katika uelewa halisi wa nini anatakiwa kukifanya  na nini kitatokea wakati tendo la kujazwa Roho linapotokea kuichochea imani ya muhitaji ni pamoja na kumuhakikishia kuwa hii ni ahadi ya Mungu na kuwa Mungu yuko tayari na kuwa kama amezaliwa mara ya pili Mungu atamjaza kwa Roho wake mkumbushe swala la kuomba Luka 11;9-10 na kuwa anapaswa kuamini na kutegemea kuwa atapokea na atanena kwa lugha nyingine kama matokeo ya kuwa Roho anamuwezesha.Mkumbushe kujiandaa na kuwa anapaswa kutambua kuwa kujazwa Roho sio swala gumu na kuwa ni jambo la kawaida kwa wakristo na kuwa hatapokea roho nyingine bali Roho halisi wa Mungu Ukimuomba Munu baba mkate hawezi kukupa jiwe na kuwa kujazwa Roho ni rahisi tu ni kama kupuliziwa pumzi Yohana 20;22. Mkumbushe pia kuwa Roho huyo hayuko mbali kwani alishakaa ndani yake tangu siku aliyookoka kisha muhitaji anapaswa kujua kuwa nini kitatokea hivyo mwambie kuwa tutaomba pamoja kisha nitakuongoza katika maombi yatakayokusaidia kubatizwa katika Roho Mtakatifu tunachotakiwa ni kumuomba Mungu aje na kutubatiza kwa Roho wake Mtakatifu na Mungu ni lazima atatusikia kwa sababu tunaomba sawa na mapenzi yake 1Yohana 5;14 na wakati huu ni muhimu sana kuwa na usikivu mkubwa kwa Roho Mtakatifu na utahisi ujio wake. Na kisha baada ya hilo itakupasa kuchukua hatua ya imani ya kumpokea Roho na kisha nitakuombea na utapokea Marko 11;24 na mara utakapopokea utasema kwa lugha mpya linapotokea hilo usiogope endelea kujiachilia katika neema yake. Muulize kama ana swali lolote na kama hakuna ingieni katika maombi.


2.       Hatua ya Maombezi.


Katika hatua ya maombezi utapaswa kuzingatia maswala muhimu mawili utamuongoza muhitaji kuingia katika maombi ya kumuomba Mungu amjaze kwa Roho Mtakatifu na pia utainua imani yake kwa kumuongoza kumpokea Roho Mtakatifu.

§  Muongoze muhitaji katika kuomba kama unavyomuongoza mtu kumpokea Yesu sasa unaweza kumuongoza muhitaji katika kumuomba Roho Mtakatifu Bwana mwema nimekuja mbele zako sasa na mbele za Roho wako sasa sina ninalohitaji katika maisha yangu sasa zaidi ya ahadi yako nategemea utanihurumia utanipa kibali na utanijaza kwa Roho wako niwezeshe nijaze kwa Roho wako mwambie Bwana nijaze kwa Roho wako jiachilie kwake paaza sauti omba tarajia uwepo wake sasa.

§  Muongoze muhitaji katika hatua ya imani anaweza kuinua mokono yake juu na kuomba kwa imani  nawe waombee wapokee Roho sasa na unapoiona imani yao iko juu amuru wapokee sasa atahisi uwepo wa Mungu kwa ndani sana  na ataanza kunena kwa lugha bila kutumia akili kunena huko hakutakuwa kwa kulazimisha kunakuja tu kama matokeo ya Roho wa Mungu kuja ju yake na inapotokea watie moyo kuwa wasiogope bali waendelee kujiachia katika uwepo wa Mungu mwili nafsi na roho na anaponena kwa lugha tia moyo ili waendelee waache kwa muda waendelee kunena kwa lugha ni raha iliyoje kwani wakti huu sasa unajua kuwa Mungu amemuhudumia muhitaji.


3.       Muongozo kabla ya maombi.


Ni muhimu sana kufanya au kutoa ushauri kabla ya maombi kwa muhitaji kama amekwisha kujazwa na Roho Mtakatifu utampa aina ya ushauri na kama hajajazwa pia atahitaji aina moja ya ushauri

§  Kama amepokea Ujazo wa Roho Mtakatifu na kunena kwa lugha ushauri ufuatao utamfaa sana Mweleze kuwa kumpokea Roho hakujaishia hapo kwani jukumu kubwa la kumpokea Roho Mtakatifu ni kwa kusudil a kumtumikia kwa hivyo huu sio mwisho bali ndio mwanzo Mungu sasa ataanza kukutumia kwa nguu sana unaposhuhudia unapoomba na kuombea wengine kwa msingi huo una wajibu wa kushuhudia wengine na kuendelea kuomba katika Roho haya yatakupa nguvu kubwa  kila siku katika maisha yako pia usisahau kuendelea kujisomea Neno la Mungu.

§  Kama muhitaji ahajapokea  unapashwa kumpa ushauri huu kwamba usikate tamaa kwa sababu hukumpokea Roho wakati huu kumbuka kuwa ahadi ya Yesu Kristo ni dhahiri na ni kwa kila mtu aliyempokea Luka 11;10 kwa hivyo endelea komba na kutafuta na utapokea kama Mungu apendavyo hata ukiwa popote Luka 11;9



SURA YA TATU: MAMBO YA MSINGI YA KUYAZINGATIA


Tunapokwenda kumalizia kijitabu hiki naona ni muhimu nikikukumbusha kwa ufupi maswala matatu ya kuyazingatia unapomuongoza mtu kumpokea Roho Mtakatifu


1.       Ni muhimu kuwa na ujuzi wa kile Biblia inachokisema kuhusu somo hili


Ni muhimu kufahamu kuwa kama mtu anapenda kusaidia wengine kwa kusudi la kumpokea Roho Mtakatifu anapaswa kufahamu na kutafuta kujua kwa undani kuhusu somo la Roho Mtakatifu na hivyo atapaswa kusoma neno la Mungu hususani kitabu cha Matendo ya mitume ili kuona somo hili kivitendo na pia anaweza kusoma Vitabu vingine vizuri vinavyozungumzia kwa undani kuhusu Roho Mtakatifu kwa kadiri mtu anavyomjua Roho Mtakatifu na kazi zake  na utendaji wake katika maisha ya waamini  na umuhimu wake ndivyo anavyokuwa msaada mkubwa na Baraka katika swala hili.


2.       Usikubali uvivu wa kiroho ukuharibie wajibu wako


Kama unasaidia watu kumpokea Roho Mtakatifu ni lazima uhakikishe kuwa unaacha uvivu wa Kiroho kwa sababu sio kazi rahisi kuombea wengine kumpokea Roho Mtakatifu na ndio maana wengine wanaona aibu kufundisha somo hili na kutokujishuhulisha kuwafanya wengine wapokee Roho Mtakatifu na kama una tabia hii unapaswa kutubu, tubia uvivu wa Kiroho ulionao na jitoe kwa ukamilifu katika huduma na Mungu atakutumia


3.       Laizima ufikie ngazi ya kujihusisha sana.


Mwisho msomaji wangu ni muhimukufahamu kuwa kuombea wengine kumpokea Roho Mtakatifu kunaambatana na kufikia ngazi ya kujihusisha  sana na kutaka wengine wajazwe hili ni swala linalohitaji kujituma na kumaanisha na kuhurumia na kutia moyo wengine kupokea Roho wa Mungu uwe na Bidii katika kuomba na hapo utakuwa na mafanikio,  sasa tunafikia mwisho wa somo letu la jinsi ya kumuongoza mtu kupokea Roho Mtakatifu Ni matumaini yangu kuwa sasa utajiweka wakfu katika kazi hii muhimu kama nini na hii ndio kiu kubwa tuliyonayo kuwasaidia watu wajazwe na kuishi katika uwepo na nguvu za Roho wake siku zote za maisha yao Mungu akubariki ni matumaini yangu somo hili litakuwa Baraka na kuwa utalitendea kazi na kulifanya halisi katika maisha yako ya huduma na kuwa tangu sasa utakuwa ukiwafanyia watu maombezi ya kumpokea Roho Mtakatifu bila woga ubarikiwe na Bwana Neema yake iwe juu yako Amen!.

Rev. Innocent Kamote Mkuu wa wajenzi Mwenye Hekima
ikamote@yahoo.com
ikamote@facebook.com
0718990796
0784394550

Maoni 14 :

Unknown alisema ...

mtumishi BWANA Yesu apewe sifa , tafadhari ninaomba unitumie somo hili kuhusu roho mtakatifu katika e mail yangu eddowk2010@yahoo.com
Ubarikiwe.

Edward.

ndio alisema ...

Bwana yesu asifiwe nimepata ujumbe mzuri nimebarikiwa na mimi natamani nijazwe na roho mtakatifu na nipate macho ya rohoni
amina
selinapius840@gmail.com

Unknown alisema ...

Namba zako hazipatikani

Unknown alisema ...

Asifiwe Yesu Mtumishi wa Mungu..Mwenyezi-Mungu akubariki sana na azidi kukutia nguvu za kueneza ujumbe wake..

Unknown alisema ...

Bwana wetu yesu kristo asifiwe ubalikiwe sana mtumishi kwa somo zuri ninaomba unitumie hili somo pia Nina swali apo me nataka kujazwa Bila kuombewa au kuwekewa mikono je inawezekana au

Unknown alisema ...

Naombaa kutumiwa masomo ya Roho mtakatifu kupitia email yangu

Unknown alisema ...

MUNGU AKUBARIKI

Bila jina alisema ...

Nahitaji zaidi masomo ya roho mtakatifu saidilaurent8@gmail.com contact of Sim 0742377340

Bila jina alisema ...

Naitwa Laurent saidilaurent8@gmail.com nahtj masomo ya roho mtakatifu

Bila jina alisema ...

Nimesoma na kuelewa kile Mungu alikupa kuongea na Watumishi wake. Ubarikiwe sana kwa kazi hii ya Uandishi

Bila jina alisema ...

Nimebarikiwa

Bila jina alisema ...

Ujumbe maridhawa

Bila jina alisema ...

Ubarikiwee zaidi na zaidi minister....Yesu azidi kukuinua viwango na viwango kwenye huduma

Bila jina alisema ...

Ubarkiwe umenikuza kiroho