Jumatano, 29 Oktoba 2014

Ufahamu Kuhusu Malaika


UTANGULIZI
     Karne tisa kabla ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo nchini Israel kulikuwa na ukengeufu mkubwa kwani watu wengi waliiacha imani, waliacha kumcha Mungu na Mungu aliruhusu vita pamoja na mateso ya aina mbalimbali, kwa ujumla ulikuwa ni wakati mgumu sana kwa Israel, Washami walikuwa wameivamia Israel na kuizingira pande zote, na walikuwa wakitafuta  kila iwezekanavyo kuangamiza kila kilichosalia katika jeshi la Israel, habari hizi zilikuwa zikienea mji kwa mji hofu ilitawala katika kila eneo  watu wakihofia kupoteza kila walicho nacho, Hatimaye siku moja ilisikiwa kuwa washami wanauvamia mji wa Dothan, kwa msingi huo mapema alifajiri mtumishi wa nabii Elisha aliamka kwenda kuthibitisha kama habari hizo ni kweli  na aliona jeshi kubwa sana la washami wakiwa wameuzingira mji pande zote kwa mshangao alipiga kelele Ole wangu Bwana wangu tunaangamia tutafanya nini? Elisha alijibu kwa kumthibitishia mtumishi wake “Usiogope kwani walio upande wetu ni wengi  kuliko wao” Mpaka wakati huu mtumishi alikuwa bado hajatia akilini kuwa bwana wake alikuwa anamaanisha nini Elisha aliomba maombi mafupi ili kwamba bwana amfungue macho 2Wafalme 6;13-17 mara moja mtumishi wa Elisha alifunguliwa macho yake  na aliona jeshi kubwa sana la kiroho (Malaika), hata ingawa jeshi la washami lilipozwa na Israel walipata ushindi wa bila mapigano lakini tunapata ufunuo mkubwa wa kuweko kwa kundi kubwa la malaika wanaowahudumia wale wanaourithi wokovu.Ikiwa huduma hii kubwa ya malaika ilikuwa hivi wakati wa Elisha  ni muhimu kufahamu kuwa nyakati za agano jipya sisi tuko chini ya agano lililo bora zaidi na roho hawa hutumwa kwaajili ya kutuhudumia Biblia inasema hivi katika Waebrania 1;13-14 “ Je yuko malaika aliyemwambia wakati wowote Uketi mkono wangu wa kuume Hata nitakapoweka adui zako  chini ya nyayo zako? Je hao wote si roho watumikao wakitumwa kuwahudumu wale watakaourithi wokovu?

Agano jipya pia linatupa ufunuo Fulani kuhusu malaika na huduma zao  aidha, Paulo mtume alikuwa akiwafundisha wakristo kule Efeso kuwa na Ufahamu kuhusu maswala ya ulimwengu wa kiroho, Waefeso 6;10-18, Ulimwengu wa kiroho una majeshi makubwa ya makundi ya malaika , makundi haya yamegawanyika katika sehemu kuu mbili, Malaika wateule yaani wale walioonyesha utii kwa Mungu walipopata nafasi ya kutumia utashi wao na kundi linguine ni la malaika walioasi hili ni kundi lenye asili ya moja ya tatu 1/3 kutoka katika kundi la malaika wateule lakini waliamua kwa utashi wao kumfuata shetani na hivyo kuwa pamoja na shetani na kumtumikia yeye  na kupewa majina mengi yanayofanana na utendaji wao wa kazi majina waliyopewa ni Mashetani, majini, mapepo, roho chafu, maruhani, na kadhalika, jina linalotumika katika Biblia kuhusu viumbe hao ni Pepo wachafu, hili ndilo tutakalolitumia zaidi katika kitabu hiki au somo hili. Ni jambo la furaha sana kujifunza kuhusu malaika.

Biblia inasema pia Atakuagizia malaika zake wakulinde katika njia zako zote Zaburi 91;11 Kumbe wako viumbe ambao wamewekwa  na Mungu kwa shughuli mbalimbali ikiwa ni pamoja na ulinzi wa watu wa Mungu, wakati lile kundi la pili si kundi jema wao wapo kwa ajili ya kudhuru, kushawishi kutenda uovu, kukatisha tamaa na kuwapinga wanadamu wenye asili ya uumbaji wa Mungu kwa sura na mfano wake wakitesa na kuua na kuharibu, haya sio mawazo ya kipuuzi kama wanavyofikiri wana sayansi  ambao hawaamini katika mambo yasiyoweza kupimwa na kuthibitika kwa kuonekana kwa macho, wazo kuhusu viumbe vya kiroho yaani malaika  ni wazo la kweli  na pia kuhusu uwepo wa pepo ni wazo la kweli na so ushirikina kwani Neno la Mungu linatufundisha hivyo. Ni imani yangu kuwa Mungu ata kusaidia kupitia Roho wake mtakatifu ili uweze kuelewa na kupata ufahamu wa kutosha kuhusu malaika.

***********************************************************

MALAIKA NI NANI.
Neno au jina malaika lina asili ya kiyunani  ambayo ina maana pana kadhaa jina hilo kwa kiingereza ni Angel ambalo limetokana na jina la kiyunani Angelos (Angelos)ambalo lina maana ya mjumbe na kwa kiebrania ni Malakh (Malakh) ambalo pia maana yake ni mjumbe wa Mungu lakini pia jina hili lilitumiwa wanadamu au kwa kumaanisha maswala kadhaa yafuatayo;-
·         Neno hili angelos lilitumika pia kumaanisha “roho ya mtu aliyekufa” na matumizi kama hayo yanaonekana katika sehemu chache za agano jipya Mathayo 18;10 na katika Matendo 12;15 ambapo wanafunzi walifikiri Malaika wa Petro alikuwa anagonga mlango hii ni kwa sababu kimsingi wengi walifikiri Petro angekuwa ameshauawa na isingeliwezekana kutoka gerezani na kurudi nyumbani katika hali ya muujiza kama vile hii ni kwa sababu walishaomba kwaajili ya Yakobo na labda kuuawa kwa Yakobo pamoja na kuwa waliomba kuliwafanya waamini kuwa si rahisi kwa Petro kuweza kuwa hai. Jambo lingine ni lile fundisho kuwa wenye haki wanapokufa huwa kama malaika kwa msingi huo ni wazi kuwa roho ya mtu aliyekwisha kufa pia ilimaanisha wazi kutumiwa kama neno malaika.
·         Neno malaika pia linaweza kumaanisha “mjumbe wa Mungu aliye mwanadamu” mfano katika ufunuo 2;1-7, ingawaje pia kunauwezekano kuwa katika eneo hilo kitaalamu inakisiwa kuwa linaweza kumaanisha mambo manne hivi yaani  wajumbe ambao wanabeba gombo la chuo kwaajili ya kila kanisa, katika makanisa ambayo Yohana alikuwa akiyaandikia, 1Makabayo 1;44 hili linaweza kuthibitishwa na  ufunuo 1;11, ambapo agizo linaonyesha kuwa haya uyaonayo uyaandike katika chuo ukayapeleke kwa hayo makanisa saba  Efeso, na Simirna,  na Pergamo na Thiatira, na Sard na Filadelfia na Laodikia kutokana na mfumo wa lugha hii kunauwezekano wale waliopeleka magombo hayo wakaitwa wajumbe yaani Malaika, Pili inaweza kuwa inamaanisha  viongozi wa kila kanisa ambao husimamia makanisa  na huwasomea watu maandiko kama ilivyokuwa wakati wa matumizi ya masinagogi kwani nyakati za kanisa la kwanza kazi ya kiongozi ilikuwa ni kuwasomea watu maandiko kwa jamii ya wakristo walikuwa ni watu wanaowajibika kwa Mungu kama watu watakaotoa hesabu hivyo viongozi hao pia waliitwa malaika yaani wajumbe wa Mungu, Au malaika pia humaanisha viumbe wa kiroho wa Mungu ambao wanawakilisha maeneo halisi yaliko makanisa yale na imani hii ina mzizi katika fundisho la kitabu cha Daniel kuweko kwa malaika wa kila eneo, na pia kanisa lenyewe ni uwakilishi halisi wa maswala ya mbinguni hapa duniani.
·         Kwa msingi huo sasa tunapojifunza somo hili Angelology inamaana ya angelos-logos yaani Elimu kuhusu malaika au Ufahamu kuhusu malaika
·         Malaika ambao tunajifunza habari zao ni viumbe wa kiroho  wenye maadili na uwezo mkubwa wa Ufahamu ambao hawana miili ya kibinadamu na wale wa aina hiyo lakini wakaasi na kuitwa mashetani kwa msingi huo somo hili halitahusu aina nyingine za malaika zile ambazo zimetwajwa hapo juu kama roho ya waliokufa, wanadamu, wasomaji maandiko , wasimamizi wa kanisa au sinagogi au wachungaji ama kanisa lenyewe ambalo humwakilisha Mungu duniani
·         Malaika pia wana majina kadhaa katika maandiko kama vile Wana wa Mungu Ayubu 1;6,2;1,Watakatifu Zaburi 89;5,7. Roho Waebrania 1;14, Walinzi Daniel 4;13,17,23,Enzi, Falme , mamlaka na usultani Wakolosai 1;16 na nguvu Waefeso 1;21.

MALAIKA WALIUMBWA LINI?

Malaika kuna uwezekano mkubwa kabisa kuwa waliumbwa kabla ya siku saba za uumbaji ‘Basi mbingu zikakamilika na jeshi lake lote’ Mwanzo 2;1  ni muhimu kufahamu kuwa jeshi wakati mwingi humaanisha viumbe vya kiroho au mbinguni, lakini mtu anaweza kubisha kutokana na andiko hili Kutoka 20;11 ambao unasema Katika siku sita Mungu aliziumba mbingu na nchi na vyote viujazavyo na siku ya saba akapumzika kwa hiyo mtu anaweza kudai kuwa malaika nao waliumbwa ndani ya siku sita za uumbaji.
     Ni muhimu kufahamu kuwa  tunaweza kupata vidokezo mkuhusu kuumbwa kwa malaika kabla ya ndani ya siku sita tunaposoma Mwanzo 1;1 Biblia inasema hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi na mara baada ya kulisoma hili ndipo tunapata taarifa kuwa nao ulimwengu ulikuwa mkiwa tena, utupu…’ lakini wakati huu hatuambiwi kitu kuhusu mbinguni Mwanzo 1;2 hivyo huenda ni wazi kuwa Mungu alikuwa tayari amekwisha kushughulika na uumbaji kuhusu Mbingu na alikuwa tayari amekwisha weka uataratibu unaokusudiwa Hapo nyota za asubuhi zilipoimba pamoja na wana wa Mungu walipopiga kelele kwa furaha  ni wakati gani wakati misingi ya dunia ilipowekwa  Ayubu 38;6-7. Kama malaika walishangilia wakati Mungu alipouumba ulimwengu ni wazi kuwa malaika waliumbwa mapema kabla ya ulimwengu, lakini kwa ujumla wake Mungu hatupi uwazi sana kuhusu alivyoumba malaika swala kama hili laweza kuwa siri Kumbukumbu 29;29. Hata hivyo tunapata vidokezo kadhaa kuhusu malaika Kwa mafano shetani alitokea na kumjaribu Hawa Mwazo 3;1 pia tunaambiwa kuwa kuna baadhi ya malaika waliasi 2Petro 2;4, Yuda 6, lakini maandiko haya hayatupi uwazi kamili lini malaika waliumbwa na kufanya maasi hayo, hususani pale Mungu anaposema tazama kila kitu kimekuwa chema Mwanzo 1;31 lakini ni wazi kuwa waliumbwa kabla ya wanadamu au kabla ya ulimwengu .

A.      Malaika ni viumbe.

Tunaposema kuwa malaika ni viumbe maana yake wameumbwa na Mungu kwa neno lake pasipo chanzo chochote  ni kwa nguvu za Mungu, hatuambiwi kuwa waliumbwa wakati gani, lakini ni wazi kuwa waliumbwa kabla ya wanadamu, wamekuweko muda mrefu sana  na baadhi yao walioasi wamekuwa chini ya shetani  2Petro 2;4 Yuda 6 kwa msingi huo tuna aina mbili kuu za malaika wema na wabaya ,Kama viumbe malaika hawakubali kuabudiwa Ufunuo 19;10,22;8-9 na mwanadamu kwa sehemu yake amekatazwa kuwaabudu malaika Wakolosai 2;18.Paulo anaeleza kuwa Mungu aliumba vyote vinavyoonekana na visivyoonekana  hii ikimaanisha kuwa ni pamoja na malaika Wakolosai 1;16, Ezara alisema Wewe Bwana peke yako umeumba mbingu na nchi na mbingu za mbingu na jeshi lake lote, Malaika wana uwezo mkubwa kiakili na hutumwa kuzungumza na wanadamu kama maandiko yasemavyo Mathayo 28;5,Matendo 12;6-11, na huimba na kumsifu Mungu Ufunuo 4;11,5;11

B.      Malaika ni viumbe vya kiroho.

Malaika ni viumbe wa kiroho, sio kama wanadamu, hawafungwi na mipaka ya kibinadamu,au asili ya kawaida, wanatokea na kupotea kama watakavyo, wanauwezo wa kusafiri kwa kasi ya kushangaza bila kutumia njia za kawaida za asili, na ingawa ni roho wana nguvu ya kuchukua miili ya kibinadamu ili kwamba waweze kuonekana katika muonekano unaoleta maana kwa mwanadamu Mwanzo 19;1-3, Malaika hata hivyo ni viumbe bvya kiroho ambao hutumwa kuwahudumia wale watakao urithi wokovu Waebrania 1;14, kwa kuwa ni viumbe vya kiroho hatuwezi kuwaona kwa macho isipokuwa Mungu anapotupa uweza maalumu kuweza kuwaona Hesabu 23;31, 2Wafalme 6;17, Luka 2;13, ni wenye kuongoza na kulinda na pia hujiunga pamoja nasi katika kuabudu Waebrania 12;22, hawawezi kuonekana lakini katika wakati Fulani hutumia huchukua miili ya kibinadamu ili kutokea Mathayo 28;5, Waebrania 13;2.

C.      Malaika wana miili ya kudumu.

Malaika tayari wana miili ya milele, au miili ya kudumu kwa msingi huo kifo hakiwawezi, Luka 20; 34-35 Yesu aliwafafanulia masadukayo ambao walikuwa hawaamini katika ufufuo kwamba watakatifu watakao fufuliwa watakuwa kama malaika wa Mungu kwa maana kuwa hawataweza kufa tena
D.      Malaika hawahesabiki.

Maandiko yanatufundisha wazi kuwa idadi yao ni kubwa mno Maelfu elfu…na makumi elfu mara kumi elfu, Daniel 7;10,majeshi zaidi ya kumi na mbili ya malaika, Mathayo 26;53 Jeshi kubwa la mbinguni, Luka 12;22Kundi kubwa la malaika, Waebrania 12;22, Muumba wao na Bwana wao kwa hiyo anatajwa kama Bwana wa majeshi.

E.       Malaika hawana viungo (Via) vya Uzazi.

Malaika siku zote wanaelezwa kama wanaume lakini katika hali halisi hawana via vya uzazi na kwa sababu hiyo hawana uwezo wa kuzaliana Luka 20; 34-35. Wala hawana uhusiano wa kama familia za wanadamu na kwakuwa maandiko hayaweki wazi zaidi kuhusu via vya uzazi au uwezo wa kuzaa na wanadamu ni muhimu kukaa kimya badala ya kujaribu kubuni mambo yasiyokuwa ya uhakika.

F.       Malaika na tabia za ainabinadamu.

Kwa kawaida malaika huwatokea watu wakiwa na umbile la kibinadamu isipokuwa Maserafi tu kama tnavyoona katika Kitabu cha Isaya 6;2, hawana tabia ya kujitokeza kama wanyama hata kidogo, wala kitu wala moto au nyani ama aina ya mnyama awaye yote, Hakuna pia nukuu katika maandiko inayoonyesha malaika wema wakimtokea mtu muovu Mathayo 24;37-39 siku zote malaika wema huwatokea watu wema, Malaika wamewahi kumtokea Abrahamu, Musa, Daudi, Daniel, Yesu, Petro, Paulo, Filipo na wengineo, na kila wakati malaika wamejitokeza kama wanaume na sio wanawake au watoto na siku zote wanakuwa wamevaa nguo na sio uchi. Kama Kristo alivyojifananisha na wanadamu kwa kuchukua mwili wa kibinadamu Incarnation Malaika huutwaa mwili wa kibinadamu kwa muda wanapotaka kujidhihirishwa kwa wanadamu na hujitokeza katika namna ambayo unaweza kufikiri ni wanadamu,Abrahamu aliwahudumia malaika watatu na kuwaandalia chakula cha jioni wakizunumza katika hali ya kawaida na mmoja akiwa amebakia kuzungumza nae wawili walielekea Sodoma na kuwa na Muda na Lutu Mwanzo 18;2,19;1, kupitia tukio hili mwandishi wa kitabu cha waebrania anatuasa kuwa makini kuwakarimu wageni Waebrania 13;2, Yoshua kabla ya kuinia kanaani kivita Mtu mmoja alisimama akiwa na upanga na huyu alikuwa Malaika wa Bwana! Yoshua 5;3 Gidion halikadhalika hakujua kuwa mtu aliyekuwa akizungumza nae alikuwa malaika mpaka alipokuwa amemhudumia kwa chakula na baadaye wote kuandaa sadaka ya kuteketezwa kwaajili ya Bwana Waamuzi 6;21-22 na Malaika wa bwana mara nyingi alijitokeza kama mtu akiwamo Manoa na Mkewe Waamuzi 13;21 ni katika matkio machache malaika wa Bwana hujitokeza katika hali za kushangaza mfano ni wazi kuwa alipomtokea mke wa manoa muonekano wake ulikuwa dhahiri kuwa ni kama malaika wa Bwana! Na ilitisha Waamuzi 13;6, Wanawake walioamka asubuhi na mapema waliwaona malaika kama wanaume wawili waliowatokea na kuwapa taarifa Luka 24;4 jambo ambalo pia liliwatokea wanafunzi wote wakati Kristo alipopaa kwenda mbinguni wanaume wawili walisimama wakiwa na mavazi meupe Matendo 1;10.
Ujuzi zaidi wa namna malaika walivyo unaweza kupatikana katika kitabu cha Daniel ambapo Daniel anapambanua muonekano wa malaika jinsi ulivyokuwa kwani alikuwa akiwaka uso wake kwa mwanga mkali na miguu yake na mikono yake ikiwa kama shaba iliyosuguliwa sana Daniel 10;5-6 na wakati mwingine malaika ufafanuliwa kama wanadamu au wene mfano wa wanadamu Ezekiel 40;3,Daniel 10;18 Zekaria 2;1 na katika mazingira yote haya malaika walifanya wajibu wao kwa haraka na kueleweka baadaye kuwa malaika , matukio yanayoashiria malaika kutoea na kujulikana mapema sana ni kama wakati alipomtokea Balaam Hesabu 22;31 na Daudi 2Samuel 24;17 na Zekaria hekaluni na Mariam mamaye Yesu Luka 1;11 na 26.

UTARATIBU WA MAMLAKA ZA MALAIKA.
Kwa kuwa utaratibu ni sheria kwanza ya mbinguni inategemewa kwamba malaika wana mamlaka ambazo zimepangiliwa katika madaraja maalumu kama inavyoonekana katika 1Petro 3; 22 Bliblia inasema “Naye yupo mkono wa kuume wa Mungu amekwenda zake mbinguni malaika na enzi na nguvu zikiishwa kutiishwa chni yake Kwa msingi huo tunapoona mamlaka na nguvu maana yake tunajifunza kuhusu mamlaka mza malaika katika madaraja hayo tutayachambua kama ifuatavyo

Malaika wa Bwana

Maandiko kadhaa hususani katika agano la kale yanaeleza kwa undani kuhusu malaika wa bwana katika namna ambayo inasadikika kuwa ni Mungu mwenyewe, anachukua namna ya mwili wa kibinadamu na kujitokeza kwa Muda wakati mwingine neno malaika wa Bwana hutajwa katika namna inayoashiria kuwa ni Mungu mwenyewe Lakinni hata namna anavyozungumza huashiria kuwa ni Mungu mwenyewe mfano Mwanzo 16;10 “Hakika Nitauzidisha uzao wako” na kasha Hajiri alijibu kwa wazi kuwa Amemuona Mungu aonaye Mwanzo 16;13. Jambo la jinsi hii tena linaonekana wakati Ibrahimu alipokuwa anataka kumtoa Isaka sadaka ya kuteketezwa malaika wa Bwana alimtokea na kusema  Sasa najua ya kuwa unamcha Mungu kwa kuwa hukunizuilia mwanao mwanao wa pekee Mwanzo 22;12, malaika huyu wa Bwana alipomtokea Yakobo katika ndoto alisema Mimi ni Mungu wa baba zako Mwanzo 31;11,13, Pia Malaika huyu wa Bwana alipomtokea Musa katika mwali wa moto  alisema Mimi ni Mungu wa Baba zako, Mungu wa Ibrahimu,Mungu wa Isaka, Mungu wa Yakobo, Kutoka 3;2,6 kwa m,sigi huo kunaushahidi kuwa malaika huyu wa bwana hutokea katika hali inayoashiria kuwa huenda alikuwa ni Mungu mwenyewe aliyekuwa akijitokeza katika mwili wa kibinadamu kwa muda  mfupi ili kujiwakilisha kwa mwanadamu,Ingawa pia kuna uwezekano kuwa malaika huyu wa Bwana akawa ni Bwana Yesu mwenyewe kabla ya kuja ulimwenguni katika mwili, lakini tunaweza kuwatambua kwa utendaji wao ili kutofautisha Baba mwenyewe na Kristo mwenyewe wakati wa agano la kale walipokuwa wakija katika matukio kama malaika (Theophany) tutaona tofauti zao wakati tutakapokuwa tukijifunza kuhusu malaika wa uso wake kipengele kinachofuata. Lakini wakati mwingine malaika huyu wa Bwana hutajwa katika namna tofauti na Mungu  kwa mfano katika 2Samuel 24;16, Zaburi 34;7, Zekaria 1;11-13 na katika Luka 1;11 katika mazingira kama haya ilimaanisha kuwa ni malaika aliyetumwa na Mungu.

Malaika wa uso wake.

Malaika huyu anaitwa malaika wa uso wake, The angel of His Presence au uso wangu, kwa kawaida ni malaika anayehusika na uwepo wa Mungu, malaika huyu naye hutajwa akiwa na sifa za Mungu kamili lakini zaidi sana Malaika huyu Israel wanaaswa wasimtia kasirani kwani hata wasamehe makosa yao kwa kuwa jina la Mungu limo ndani yake Kutoka 23;20-23. Huyu ni malaika anayeshughulika na kazi za Maongozi, kwa kawaida wana theolojia wengi wanaamini juu ya Mungu Baba kuja katika umbile la kibinadamu na kuzungumza akiwa kama Mungu mwenyewe mfano alipozungumza na Ibarahimu soma Mwanzo 18; 1-15, Ni wazi kuwa malaika huyu alikuwa Mungu Baba lakini malaika huyu wa Uso wa Mungu yaani malaika wa uwepo wake au uso wake huyu ni tofauti Isaya anamtaja vizuri kuwa ni Roho Mtakatifu Isaya 63;9 – 14 , Ni wazi kuwa malaika huyu ni Roho Mtakatifu kwani ikiwa tunaamini kuwa Mungu baba, au wakati mwingine Mungu mwana waliwahi kujihusisha na Mwanadamu katika ukombozi wakati wa agano la kale na kama hivyo ndio ilikuwa tabia ya Mungu na tunaamini kuwa Roho Mtakatifu ni Mungu mimi naamini kuwa katika somo kuhusu malaika kamwe hatuwezi kumuacha Roho wa Mungu kwani ni wazi tabia zake kama zinavyotajwa katika agano jipya ndivyo zinavyodhihirika katika agano la kale malaika huyu hushughulika na maongozi na hutajwa kama uwepo wa Mungu au uso Kutoka 32;34, 33;14-15, kwa sababu malaika ni mjumbe na tunawezaje kuwatofautisha malaika hawa kwa nia Rahisi tunaweza kumtambua
·         Mungu baba kwa shughuli za Mipango na majira
·         Mwana wa Mungu kwa shughuli za ukombozi na wokovu au uponyaji
·         Roho Mtakatifu kwa kazi au shughuli za maongozi.

Kwa msingi huo ni wazi kuwa malaika aliyemtokea Ibrahimu na kufanya agano naye na kumtakia Sara ahadi ya kuzaliwa Isaka alikuwa ni Mungu baba kwa sababu alishughulika na majira Mwanzo 18;1-15. Na ni wazi kuwa Malaika aliyemtokea Yoshua alipokua akiikabili Yeriko alikuwa ni Bwana Yesu Yoshua 5; 13-15. Na Ni wazi kabisa malaika huyu anayetajwa kama malaika wa uso wake ni Roho Mtakatifu Kutoka 23;20-23, Na unapofuatilia sifa zinazo tajwa hapo na kuchunguza tabia za Roho na mafundisho ya Kristo kuhusu Roho unapata picha kuwa akikosewa kuna uwezekano wa kutokusamehewa makosa bila shaka inazungumziwa dhambi ya kumkufuru Yeye na hapa ndipo inapotajwa na Mungu kuhusu malaika huyu.

Malaika mkuu.

Malaika mkuu Biblia inamtaja kwa jina lake wazi wazi kuwa ni Mikaeli unaweza kuona hili katika Yuda 9., Ufunuo 12;7 Habari zake nyingine katika maandiko zinatajwa katika 1Thesaloooniiike 4;16, Malaika Mikaeli pia hujitokeza kama malaika mlinzi wa Taifa la Israel Daniel 12;1, katika namna nyingine malaika Gabiel huonakana kuwa katika daraja linguine chini kidogo ya malaika mkuu mikael kwa sababu husimama katika uwepo wa Mungu Luka 1;19 na kupitia yeye ametumwa mara kadhaa kuleta habari muhimu sana kuhusiana na ufalme wa Mungu Daniel 8;16, Daniel 9;21, Kutajwa kwa Mikaeli kama malaika mkuu kunaashiria kuwa ana mamlaka juu ya malaika wote , hutwa moja ya wakuu katika Daniel 10;13 na ndiye pia mkuu wa majeshi ya malaika , ndiye aliyelipiga joka ambalo pamoja na malaika zake jaka lilipigwa Ufunuo 12;7-8, Biblia inapotaja kuja kwa bwana katika 1Wathesalonike4;16 huenda inamaanisha Mikael au huenda kuna malaika wengine wakuu maandiko hayatuwekei wazi.

Makerubi

Cherub ni neno la Kiebrania  ambalo wingi wake ni cherubim,  Wanaonekana kuwa malaika wa ngazi ya juu zaidi wanaonekana kuwa na Mungu sambamba katika jambo lolote ikiwamo ulinzi katika maagizo ya Mungu mfano walitumiwa kulinda mti wa Bustani ya Eden baada ya Adamu na Hawa kuasi Mwanzo 3;24 na pia katika maswala ya kusaudi la ukombozi Kutoka 25;22., hutumiwa na Mungu pia kama magari ya safari Zaburi 18;10, Ezekiel 10;1-22, wakati wa Sanduku la agano wawili waliwekwa kufunika kiti cha enzi cha Mungu kiti cha rehema Mbawa zao zikiwa zimefunika kiti cha rehema  na ni hapo Mungu alihaidi kuwa angekutana na watu wake , na kusema na watu wake  na kukutana nao kwaajili ya rehema Kutoka 25;22,18-21., Makerubi ni aina za malaika wanaohusiana na maswala ya kijeshi au vita na ulinzi

Maserafi

Ni aina nyingine ya kundi la malaika ambao pia wako katika daraja la juu sana hakuna habari nyingi sana za kutosha kuwahusu lakini tunawaona katika Isaya 6;1-7,wanatajwa katika sifa za tofauti na inaonekana kuwa wana upendo mkubwa sana kwa Mungu  upendo ambao huwaka kama moto kwani maanga ya Maserafi ni wanaowaka  Neno Seraph ni lenye asili ya kiebrania ambalo wingi wake ni Seraphim, ni wenye kuabudu Mungu kwa kiwango cha juu sana wanaonekana wakiitana wenyewe kwa wenyewe wakisema Mtakatifu , Mtakatifu, Mtakatifu ndiye Bwana wa majeshi Mbingu na nchi zimejaa uwake Isaya 6;3.

Malaika wa mataifa.

Daniel 10;13,20, Katika maandiko haya tunajifunza kuwa kila taifa au kila kabila lina malaika wake ambao hujihusisha na ulinzi dhidi ya taifa hilo, wakati jamii ya wayahudi walipokuwa wakijiandaa kurudi Yerusalem na Daniel nabii alipokua anaomba na kufunga kwaajili ya kurejeshwa baada ya wiki tatu Malaika alimtokea na kumpa sababu kuwa ni kwanini alichelewa kuleta majibu  kumbe mkuuu wa anga la uajemi alikuwa amemzuia Daniel 9;1-2, na penngine malaika huyu alikuwa akimzuia kwa makusudi ya kutokupoteza umaarufu kwaajili ya uajemi,kutokana na kuondoka kwa wayahudi, malaika alikuja kusaidiwa na malaika Mikael ambaye ni mlinzi mkuu wa taifa la Israel Daniel 10;21. Na muu wa anga wa uyunani hakuwa ameng’ang’ania sana kama ilivyokuwa kwa mkuu wa anga wa uajemi kuhusiana kuondoka kwa wayahudi kutoka utumwani Daniel 10; 10, kwa msingi huo katika angano jipya neno lile wakuu wa anga huenda linamaansisha kundi hili la malaika ambao huusika na mataifa na wakuu wa anga hutumika kwa pande zote mbili kwa malaika waovu na kwa malaika wema Waefeso 3; 10; Wakolosai 2;15, Waefeso 6;12.

Viumbe wenye uhai.

Kitabu cha Ezekiel na ufunuo vinatuambia kuwa kuna aina nyingine za Malaika ambao wana daraja Fulani miongoni mwa malaika  na wanatajwa kama viumbe vyenye uhai ambaovyo viko karibu na kiti cha enzi cha Mungu Ezekiel 1;5-14, Ufunuo 4;6-8 huenda waliitwa vimbe vyenye uhai kwa sababu ya aina za maumbile yao vina uso wenye sura nne kama simba, ng’ombe, mwanadamu na tai, huenda wana wakilisha ukuu wa uumbaji wa Mungu katika maeneo mbalimbali wakiwemo wanyama wa angani, mwituni, wa kufugwa na binadamu, hawa humuabudu Mungu wakati wote  wakimsifu kuwa ni mtakatifu ,mtakatifu,mtakatifu ni bwana Mungu mwenye enzi, aliyekuweko, aliyeko na ajaye Ufunuo 4;8.

Malaika wateule 

Malaika kwa ujumla wake wako katika makundi makuu mawili yaani malaika wateule na malaika waovu. Malaika wateule hili ni lile kundi ambalo wakati wa matukio ya uasi kule mbinguni waliendelea kuwa watii kwa Mungu na hivyo walipata thawabu ya kudumu ya kuwa wateule, na wale walioungana na shetani katika kuasi wali walipata thawabu ya kuwa mashetani na kuhukumiwa milele 1Timotheo 5;21, Mathayo 25;41.

Malaika wa kuharibu.

Malaika wa kuharibu pia huitwa “Muharabu” destroyer au Malaika wa mauti 1Koritho 10; 10 malaika huyu hushughulika maalumu na kusababisha maafa pale watu wanapokuwa wameasi Hesabu 16; 41-49, ni wazi kuwa huyu ni mjumbe wa Mungu kwa sababu maalumu za hukumu mara nyingi hutumia tauni katika kuangamiza kama ilivyokuwa kwa mapigo ya tauni za aina mbalimbali katika mapigo yale kumi kule Misri Kutoka 10; 12-13 niliaminilo ni hili ingawa Bwana anasema maana nitapita.... Bwana anazungunza kuwa atapita na kuipiga Misri, je unafikiri Bwana ndiye aliyekuwa anapita Hapana ni Malaika wake maalumu wa kushughulika na hukumu alipita akiwa ametumwa na Bwana,Mara nyingi Mungu anaporuhusu hukumu huhesabika moja kwa moja kuwa ni yeye anayehusika kuleta tauni au mapigo kwa sababu yeye ndiye ameruhusu lakini ni muhimu kufahamu kuwa malaika wake hushika Upanga na kuanza kupiga kwa Tauni ona mfano 1Nyakati 21: 14-22 Mstari wa 15  unaonyesha kuwa Bwana alituma malaika wake na jina la malaika huyu ni Aharibuye (Auaye) malaika huyu hutenda kazi ya kuua anapotumwa na mara nyingi mapigo yake huzimwa kwa sadaka aidha ya kuteketeza au uvumba wa chetezo malaika huyu ndipo hasira yake hupoa, kwa namna Fulani malaika huyu huweza kutumiwa kwa mauaji kama wa upande wa shetani wanavyomtumia jinni makata.huenda mwandishi wa Zaburi ya 35 ambaye ni Daudi alikuwa akiomba kwa Bwana malaika wa aina hii awashughulikie adui zake Zaburi 35;1-28 mstari wa 8 kuna neno “Uharibifu na umpate” ni wazi kuwa muomaji anaomba malaika huyu wa kuharibu alete uharibifu dhidi ya adui, katika mazingira Fulani ni ruhusa kuwatumia aku kumtumia malaika huyu wa kuharibu na kusababisha uharibifu dhidi ya yale yaliyo kinyume nasi, kuna uwezekano mkubwa kuwa malaika huyu alitumiwa na Eliya kushusha moto kutoka mbinguni na kuharibu vikosi viwili vya maakida waliomuita bila nidhamu 2Wafalme 1;9-15 ni wazi kuwa hatimaye malaika huyo alimsihi Eliya kukubali ombi la Akida wa tatu kwa sababu alikuja kwa unyenyekevu. 

SIFA ZA MALAIKA

Malaika wana Utii uliotimia.(Obedient)

Malaika ni watii hutii maagizo yao bila kusita na ndio maana tunaomba mapenzi yako yatimizwe hapa duniani kama huko mbinguni Mathayo 6;10, Zaburi 103;20, Yuda 6, 1Petro 3;22 malaika hutii kile walichoagizwa na sio vinginevyo kama kuna kitu ambacho hawakuagizwa hawakifanyi hata kama ni malaika mkuu sawa na Yuda 6.

Malaika ni waabudu (Reverent).

Kazi yao kubwa ni kuabudu , wanamuabudu m,ungu wakati wote wanamuheshimu na kumsikia na kumtii wanamfanyia bwana ibada katika kila tendo lake jema Nehemia 9;6,Wafilipi 2;9-11. Waebrania 1;6

Malaika ni wenye hekima (Wise)

Nyakati za zamani za wafalme katika Israel mtu alipokuwa na hekima na ujuzi wa kupambanua mema na mabaya aliitwa mwenye hekima kama malaika 2samuel 14;17 ni wazi kuwa hekima ya malaika inazidi ile ya wanadamu katika maisha haya, ingawaje malaika hawawezi kusoma mawazo yetu 1Wafalme 8;39 na ujuzi wao kuhusu neema ya Mungu kwetu kwao ni siri 1Petro 1;12.

Malaika ni wapole na wanyenyekevu (Meek).

Kwa kawaida hawapeleki mashitaka ya mtu awaye yote wala hawapigani na wale wanao wapinga husikiliza na kuyatii maagizo ya Bwana wao tu 2Petro 2;11 Yuda 9.

Malaika ni wenye nguvu (Mighty)

Malaika wana nguvu za kupita kawaida lakini sio wenye nguvu zote nguvu zaoi zinazidi zile za kibinadamu Zaburi 103;20.

Malaika ni watakatifu (holy)

Kwa kuwa wamewekwa wakfu kwaaajili ya Mungu na wako kwaajili yake malaika wametakaswa ni watakatifu Ufunuo 14;10.

KAZI ZA MALAIKA:

Ni Mawakili wa Mungu (God’s Agents)

Malaika wanatajwa kama mawakili wa Mungu humwakilisha Mungu  katika kazi ya hukumu Mwanzo 3;24, Hesabu 22;22-27, Mathayo 13;39, 41, 49, 16;27, 24;31, Marko 13;27, Mwanzo 19;1, 2Samuel 24;16, 2Wafalme 19;35, Matendo 10;4;13-17

Ni wajumbe wa Mungu (God’s Messengers)

Kwa ufupi malaika maana yake ni mjumbe kwa msingi huo moja ya kazi kubwa ya malaika ni kupeleka ujumbe kutoka kwa Mungu kuja kwa wanadamu , kupitia wao Mungu huwatuma kutangaza Luka 1;11-20 ,Mathayo 1;20,21. Malaika pia hutumwa kuleta maonyo Mathayo 2;13,Waebrania 2;2,Hutumwa kutoa  Maelekezo Mathayo 28;2-6, matendo 10;3, Daniel 4;13-17,Malaika hutumwa kutia moyo  Matendo 27;23,Mwanzo 28;12, Aidha malaika pia hutumwa kuleta mafunuo au ufunuo Matendo 7;53, Wagalatia 3;19,Waebrania 2;2, Daniel 9;21-27 Ufunuo 1;1.

Ni watumishi wa Mungu (God’s Servants).

Je wao si roho wanaotumwa kuwahudumia wale watakao urithi wokovu,Waebrania 1;14Malaika hutumwa kutia nguvu Mathayo 4;11Luka 22;43,1falme 19;5 , hutumwa kulinda Mwanzo 16;7,24;7,Kutoka 23;20,Ufunuo 7;1, hutumwa kuwaokoa watu Hesabu 20;16Zaburi 34;7,91;11 Isaya 63;9,Daniel 6;22Mwanzo 48;16 Mathayo 26;53 huingilia kati Zekaria 1;12 Ufunuo 8;3,4 Kuwahudumia watakatifu baada ya kufa Luka 16;22.

NAFASI YA MALAIKA KATIKA KUSUDI LA MUNGU
1.     
  Malaika wanaonyesha ukuu wa upendo wa Mungu na mpango wake kwetu.

Malaika pamoja na wanadamu ndio viumbe wa pekee wenye akili na maadili katika viumbe ambavyo Mungu ameviumba, kwa msingi huo tunaweza kufahamu kwa uapana na kina kuhusu mpango wa Mungu na upendo wake kwetu  hususani tunapojilinga sisi na Mungu.
         Moja ya jambo la kwanza la msingi tunalijifunza kati yetu na malaika ni kuwa malaika hawatajwi kuwa wameumbwa kwa sura na mfano wa Mungu wakati wanadamu wanatajwa kuwa wameumbwa kwa mfano na sura ya Mungu Mwanzo 1; 26-27,9;6 kuwa na sura na mfano wa Mungu maana yake ni kuwa kama Mungu  kwa hivyo si vibaya tukihitimisha kuwa Wanadamu wana fanana na Mungu zaidi kuliko malaika.
         Jambo kama hilo linathibitishwa na ukweli kuwa iko siku Mungu atatupa mamlaka dhidi ya malaika na kuwa tutawahukumu Je hamjui ya kuwa ninyi mtahukumu malaika?  1Wakoritho 6;3 ingawa kwa muda huu sisi ni wadogo ukilinganisha na malaika  Waebrania 2;7, wakati wokovu wetru utakapokamilika  tutakuwa juu ya malaika na tutawatawala  na kwa ujumla hata sasa malaika ni tayari wanatutumikia Waebrania 1;14.
         Jambo lingine ni kuwa Mungu alimpa binadamu uwezo wa kuzaa na Adamu akazaa watoto kwa sura na mfano wake  Mwanzo 5;3 hii ni alama nyingine ya Ubara ambayo Malaika hawana  kwani wao hawana uwezo wa kuzaliana na kuongezeka Mathayo 22;30, Luka 20;34-36
          Malaika wanawakilisha ukuu wa na upendo wake kwa wanadamu kwani ingawa wao ni wengi lakini mara walipofanyadhambi na kuasi hakuna hata mmoja wao aliyeokolewa Petro anatuambia kuwa …Mungu hakuwaachilia malaika waliokosa bali aliwatupa shimoni akawatia katika vifungo vya milele walindwe hata ije hukumu” 2Petro 2;4 Yuda anawaita malaika wasioilinda enzi yao  wenyewe  lakini wakayaacha makao yao ya asili  imewekwa kuwa dalili wakiadhibiwa katika moto wa milele Yuda 1;6.
          Aidha tunaona kuwa Kristo Yesu alipokuja duniani badala ya kutwaa asili ya Malaika alitwaa asili ya Binadamu kwa uzao wa Ibrahimu Biblia inasema haya katika Waebrania 2;16 “Maana ni hakika hatwai asili ya maklaika  ila atwaa asili ya mzao wa Ibarahimu” Kwa msingi huo ingawa Mungu aliumba makundi makuu mawili ya viumbe wenye akili  yaani malaika na wanadamu na ingawa malaika ni bora zaidi ya aina binadamu Neema kubwa ya mahusiano inaonekana kuwa pamoja na wanadamu Bwana asifiwe sana ni upendo mkubwa na neema ya ajabu! Kwa nini ndani ya makundi haya mawili Malaika hawakuasi wote baadhi tu waliasai lakini kwa upande wa wanadamu woote waliasi Mungu angepaswa atuache woote na kututupia ,mbali katika hukumu ya milele  na hakuna ambaye angelaumu ingeuwa ni haki tu kufanyiwa hilo Lakini Mungu alikusudia kutuokoa sisi wanadamu na hata kama angeokoa watano tu miongoni mwa wana wa aina binadamu  pia ingelikuwa haki naangekuwa ameonyesha rehema na neema na angekuwa sahii lakini Mungu amekusudia kutuokoa kwa wingi wa mamilioni wasiohesabika na wote watakao kubali neema yake jamii hiyo anayoiokoa ni kutoka katika kila jamii ya aina binadamu kabila na taifga Ufunuo 5;9 huu ni upendo neema na rehema zisizoweza kufahamika  ni zaidi ya uwezo wetu wa kuelewa ni upendeleo usiostahili ukweli huu unatufanya sisi tuwe na uwezo wa kuimba  wimbo ambao malaika  hawangeweza kuimba, huenda watausikia na kuufurahia wimbo wa kumsifu Mungu kwa neema yake isiyoweza kupimika lakini kamwe hawawezi kuufanya kuwa wimbo wao.

2.       Malaika wanatukumbusha kuwa ulimwengu wa roho ni halisi.

Nyakati za maisha ya Kristo duniani dhehebu la masadukayo walikuwa wanaamini kuwa Hakuna ufufuo,Hakuna malaika wala roho Matendo 23;8, hata katika nyakati zetu wako watu wanaoamini kuwa maswala ya ulimwengu wa kiroho sio Halisi, wengine hawaamini katika lolote wasiloliona, Lakini mafundisho ya kibiblia yanaonyesha kuwa  kuna malaika na biblia inatukumbusha mara kwa mara kuhusu ulimwengu wa kiroho usioonekana na kuwa ulimwengu huo ni halisi, hatuwezi kuuona ulimwengu huo kwa macho ya kawaida lakini Mungu atakapotupa neema hiyo au kufungua macho yetu kama ilivyokuwa kwa mtumishi wa nabii Elisha utaweza kuliona jeshi kubwa la malaika na magari yao ya moto 2Wafalme 6;17. Waandishi wa zaburi pia wanatukumbusha kuhusu ulimwengu wa kiroho na kuwasihi malaika waimbe sifa za Mungu Zaburi 148;2, mwandishi wa kitabu cha Waebrania  anatukumbusha kuwa tutaingie Yerusalemu ya Mbinguni pamoja na jeshi kubwa la malaika  Waebrania 12;22, walimwengu wa kawaida wanaweza kudhani kuwa swala kuhusu malaika ni swala la kichawi lakini maandiko yanatukumbusha kuwa ni halisi.

3.       Malaika ni mfano kwetu.

Kwa namna iwayo yote malaika ni mfano kwetu namna wanavyo tii na wanavyoabudu  wanatupa sisi mfano wa kuiga, Yesu alipofundisjha kuhusu kuomba alisema Yatendeke hapa duniani kama huko mbinguni Mathayo 6;10, huko mbinguni mapenzi ya Mungu hutimizwa na malaika kwa ukamilifu, kwa haraka , kwa furaha bila maswali  kwa msingi huo ni muhimu kuomba kuwa utii wetu na wa wengine uwe kama ule wa malaika mbinguni, wao ni watumishi wa Mungu wanyenyekevu na waaminifu na hufanya wajibu wao kwa furaha  liwe jukumu kubwa au dogo.
Malaika pia wanatufundisha jinsi wanbavyoweza kuabudu  na kumtumikia Mungu wao kwa mfano maserafi kwa humuona Mungu kuwa ni Mtakatifu wanatambua hivyo na humsifu kwa kurudia tena na tena  Mtakatifu, mtakatifu matakatifu ni BVwana Mungu wa majeshi nchi yote imejawa na utukufu wake  Isaya 6;3, aidha Yohana aliona kundi kubwa la malaika wakiwa wamekizunguka kiti cheke cha enzi maelfu kwa maelfu wakimsifu  mwana kondoo  aliyechinjwa na kusema kuwa anastahili  nguvu na utajiri na hekina na mamlaka  na utukufu na abarikiwe Ufunuo 5;11-12 kama malaika wanavyo msifu Mungu kwa furaha kila siku na kila wakati  wakitambua kuwa ni mkuu na anastahili  je inatupasaje sisi katika wakati huu tulio nao?

4.       Malaika hutimiza majukumu kadhaa ya Mungu.

Maandiko yanawaona malaika  kama watumishi wa Mungu  ambao hutimiza majukumu kadhaa ya Munguna mipango yake hapa duniani, Wanatumika kuleta ujumbe wa Mungu kwa wanadamu Luka 1;11-19, Matendo 8;26, 10;3-8,22, 27;23-24, wanabeba baadhi ya majukumu ya kuleta hukumu na mapigo mfano kwa Israel 2Samuel 24;16-17, kuwapiga viongozi wa Ashuru 2Nyakati 32;21, kupigwa kwa mfalme Herode kwa sababu ya kutokumpa Mungu utukufu Matendo 12;23 na kumwaga  hasira za Mungu duniani wakati wa dhiki kuu Ufunuo 16;1 na wakati Kristo atakapokuja Duniani ayakuja na jeshi kubwa linaloambatana na mfalme Mathayo 16;27, Luka 9;26 2Thesalonike 1;7, Malaika pia huzunguka duniani kama wawakilishi wa Mungu  Zekaria 1;10-11, pia hufanya vita dhidi ya mapepo  Daniel 10;13, Ufunuo 12;7-8 Yohana katika maono yake aliona shetani akifungwa na malaika  miaka 1000 ufunuo 20;1-3 na Masihi  atakapokuwa akirudi Malaika watatangaza  ujio  wake  1Thesalonike 4;16 Ufunuo 18;1-2,21,19;17-18.

5.        Malaika humtukuza Mungu.

Malaika hufanya kazi nyingine ya kumtukuza Mungu moja kwa moja kupitia utumishi wao kwa msigi huo katika uumbaji wa Mungu na viumbe wenye akili wanaomtukuza Mungu malaika humtukuza Mungu kwa jinsi alivyo katika njia iliyo bora zaidi Zaburui 103; 20 Mhimidini Bwana enyi Malaika zake Ninyi mlio hodari, mtendao neno lake Mkiisikiliza sauti ya neno lake.Pia Zaburi 148;2 Maserafi huendelea kumsifu Mungu kwa utakatifu wake Isaya 6;2-3 jambo ambalo pia hufanywa na viumbe wale wenye uhai Ufunuo 4;8,
    Malaika pia humtukuza Mungu kwa mpango wake mkuu wa wokovu, tunawaonawalivyo mtukuza Mungu alipozaliwa Kristo huko Bethelehemu Luka 2;14 Waebrania 1;6 Yesu alisema Pia kuna furaha kubwa mbele ya Malaika wa Mungu mwenye dhambi mmoja atubupo Luka 15;10 hii yote inamaanisha kuwa malaika hufurahia hufurahia kila wakati Mtu anapokuwa anaokolewaPaulo mtume anaeleza kuwa Mungu alimtuma kuihubiri injili kwa Mataifa katika hekima ili kwamba uweza wa Mungu upate kujulikana kwa Falme na mamlaka Katika ulimwengu wa roho, Petro anatuambia kuwa mambo haya malaika wanatamani kuyachungulia 1Petro 1;12 kwa ajili ya utukufu mkubwa na mpango mzima wa wokovu unaotenda kazi ndani ya kila aaminiye,Malaika pia hushuhudia maisha ya waamini wanapokuwa ibadani na humtukuza Mungu kwa ajili ya ibada zetu na utii wetu 1Koritho 11;10, Aidha Paulo alipokuwa akiagiza jambo la Muhimu kwa Timotheo kwa ajili ya kusisitiza  alisisitiza kuwa nakuagiza mbele  zake mungu na Yesu Kristo na Malaika wateule  1Tomotheo 5;21,1Koritho 4;9 maana yake ni kuwa wakati timotheo atakapokuwa akitii maagizo aliyopewa Malaika watashuhudia utii wake na watamtukuza Mungu na kama hato tii malaika wataona na kusikitishwa.

UHUSIANO WA WANADAMU NA MALAIKA 

1.       NI LAZIMA TUWE WAANGALIFU KUHUSU MALAIKA.

Maandiko yanatuwekea wazi kuwa Mungu anataka tuwe makini na kuweko kwa malaika na utendaji wao , hii haina maana kuwa kujifunza kuhusu malaika hakuna umuhimu katika maisha yetu hapana  lakini katika mazingira Fulani tunapaswa kuwa makini  kuhusu kuweko kwao na huduma zao hata wanazozifanya leo duniani,Tunapomwabudu Mungu sio tu kuwa tunaungwa moja kwa moja na watakatifu ambao wamekwisha kufa katika bwana na roho zao zimekamilishwa kwake lakini pia tunaungana na jeshi kubwa la amalaika wanaomwabudu Mungu ambao hawahesabiki Waebrania 12;22-23, kwa msingi huo ingawa katika hali ya kawaida hatuwezi kusikia au kuona namna Fulani ya ibada za kimbinguni  lakini kwa namna Fulani tunashuhudiwa na furaha na uwepo mkubwa wa Mungu nah ii inatupa uhakika kuwa malaika wanaungana na si kila tusimamapo kuabudu
Lakini tunapaswa kuwa makini kwani malaika wanaangalia kutii kwetu na kutokutii kwetu  katika siku nzima, kama tunafikiri kuwa dhambi zetu tunazofanya sirini ni siri na kuwa haiwezi kuhuzunisha wengi ni muhimu kukumbuka kuwa malaika kwa maelfu yao wanashuhudia na kuhuzunishwa na dhambi yetu hali kadhalika tunapokuwa tunamtii Mungu hata katika hali ya kuwa wenyewe ni muhimu kufahamu kuwa kutii kwetu hata kama hakuonekani kwa wanadamu Mungu aoneaye sirini anaona lakini pia maelfu ya majeshi ya malaika wanaangalia kutii kwetu  na jinsi tunavyotaabika peke yetu katika kumtii Mungu na kujiepusha na kumkosea yeye na tunatiwa moyo kuwa Malaika wanashuhudia jinsi tunavyoheshimu kazi kubwa ya ukombozi iliyofanywa na kristo katika maisha yetu.
Akifundisha jinsi utendaji wa malaika ulivyo mwandishi wa kitabu cha waebrania anasema kuwa tusiache kuwa wakarimu kwa wageni kwani katika namna isiyo ya kawaida huchukua miili ya kibinadamu na kutembelea kwa lengo la kuchunguza kwa kusudi la kuthibitisha maswaka kadhaa Waebrania 13;2, Mwanzo 18;2-5,19;1-3 hili linatutia moyo katika swala zima la kuendelea kuwahudumia wenye uhitaji hata wale tusiowajua siku moja mbinguni tutakutana na malaika ambao yuliwahudumia bila kujijua kuwa tunahudumia malaika
Wakati mwingine tunapokuwa tumeokolewa na ajali mbaya ni muhimu kufahamu kuwa huenda Mungu alimtuma malaika wake kutuokoa na tunapaswa kumshukuru Mungu, Malaika walifunga vinywa vya simba ili wasimdhuru nabii Daniel, Daniel 6;22, waliwafungulia mitume kutoka gerezani Matendo 5;19-20 na baadaye walimtoa Petro gerezani Matendo 12;7-11, walimuhudumia Bwana Yesu huko jangwani  wakati wa kumalizia majaribu Mathayo 4;11.
Ni muhimu kukumbuka kuwa wakati gari linapotaka kutugonga na likatukosa ni lazima tukumbuke kuwa sio tunapswa kuhisi kuwa Mungu ametuma malaika zake kutuokoa lakini tunapswa kuwa na ufahamu kuwa aliahidi  kumtuma malaika wake kutulinda  katika njia zake zote Zaburi 91;11-12 kwa msingi huo kumshukuru Mungu kwa kumtuma malaika wake kutulinda ni swala sahii.

2.       MAONYO KUHUSU UHUSIANO WETU NA MALAIKA.

a.       Uwe makini kupokea Mafundisho potofu kutoka kwa malaika.

Biblia inatuonya kuhusu kupokea mafundisho potofu yanayodaiwa kutoka kwa malaika Wagalatia 1;8 “Lakini ijapokuwa sisi au malaika  wa mbinguni atawahubiri ninyi injili iwayo yote isipokuwa hiyo tuliyowahubiri  na alaaniwe”Paulo anatufundisha swala hili kwa sababu alijua kuwa kuna uwezekano wa kudanganyika  kwa sababu alisema pia wala si ajabu kwani hata shetani mwenyewe hujigeuza awe kama malaika wa Nuru  2 Wakoritho 11;14 hii ni sawa na nabii wa uongo aliyemrubuni mtu wa Mungu  katika Wafalme 13;18 huku maandiko yakiweka wazi kuwa lakini alimdanganya, huu ni mfano wa mafundisho potofu huu ni mfano wazi wa utendaji wa shetani katika kutaka kutukosesha  ili tusiyatii maagizo na amri za Mungu 1Wafalme 13;9 hili ni onyo kwa wakristo wote kuwa makini na aina hizi za mafunuo yaliyo kinyume na injili ya kweli mfano ni madhehebu ya Mormonism wanaodai kuwa malaika NMoroni alizungumza na Joseph Smith na kumfunulia kuhusu dini ya Mormonism ambayo mafunuo yake yakoi kinyuma na injili ya kweli Mafundisho ya kweli na sahii yamefungwa katika neno la Mungu na ni Muhimu kwetu kufahamu kuwa ufunuo wowote ambao utadaiwa kutoka nje ya neon la Mungu kana kwamba mtu huyo ana laziada kuliko maandiko tunapaswa kuwa makini na mafundisho ya aina hiyo.

b.      Hatupaswi kuwaabudu, kuwaomba au kuwatafuta malaika.

Kuabudu malaika Wakolosai 2;18 ni moja ya mafundisho potofu yaliyokuwa yamelivamia kanisa la Kolosai na ingawaje malaika walimtokea Yohana mtume na kumpa kitabu cha ufunuo Yohana alionywa asimwabudu malaika bali amuabudu na kumsujudia Mungu Ufunuo 19;10, aidha hatupaswi kuwaomba malaika  bali tunapaswa kumuomba Mungu yeye anauwezo wa kusilkia maombi yetu hata kama ni ya watu wengi yaya ni Mungu anayejua yote  pia Mungu ana nguvu zote anajua yote Mungu mwana na Roho Mtakatifu pia wanaweza kuombwa  lakini hili sio halkali kwa kiumbe kingine zaidi ya hao tu, Paulo anaonye pia kuwa hakuna mpatanishi mwingine kati  ya Mungu na wanadamu  bali mpatanishi kati ya Mungu na wanadamu ni mmoja Kristo Yesu 1Timotheo 2;5, tunapowaomba malaika maana yake ni kuwa tumawapa cheo kimoja sawa na Mungu  na hakuna mahali kokote katika maandiko ambapo mtu Fulani alimuomba malaika kwa jambo lolote. Wala pia maandiko hayajatuagiza kuutafuta uso wa malaika wao hujitokeza wenyewe kwa maagizo au neema ya Mungu tu endap[o wametumwa kutimiza jukumu Fulani  wajibu wetu mkubwa ni kutembea na Mungu  ambaye yeye ni Kamanda wa majeshi ya malaika  ingawaje si vibaya kumkumbusha mungu sawa na ahadi yake kumtuma malaika ili kutulinda  Zaburi 91;11 wakati wa mahitaji.

c.       Je malaika hutokea watu leo?

Nyakati za kanisa la kwanza vipindi vya mwanzoni malaika walikuwa wakijitokeza kufanya kazi, ni malaika aliyemwambia Filipo  kuelekea kusini  mwa njia ya kuelekea Gaza kwaajili ya wokovu wa towashi wa kushi Matendo 8;26, Malaika alimwelekeza Kornelio kutuma mtu kwenda Yafa  kumuita Petro Matendo 10;3-6, walimsihi Petro kuamka na kutoka gerezani Matendo 12;6-11, alimuhakikishiaPaulo kuwa hakuna mtu aliye katika meli yao atakayepoteaMatendo 27;23-24 mwandioshi wa kitabu cha waebrania alioonya watu kuendelea kuwa wakarimu kwani wanaweza kuwakarimu malaika hii maana yake ni kuwa kuna uwezekano hata sasa kwa mujibu wa Biblia tunaweza kuwaona malaika lakini jambo la msingi la kuzingatia ni kuwa hatuwezi kukubaliana  na kupokea muongozo mpya kutoka kwa malaika kuhusu injili jambo hili litakuwa sio la kawaida na kwa vyovyote vile yatakuwa mafundisho potofu ya shetani 2Koritho 11;14 maandiko yataendelea kuwa muongozo wetu dfaima malaika hawawezi kwa namna yoyote ile kuleta ufunuo mpa ulio kinyume na injili Wagalatia 1;8.

UFAHAMU KUHUSU SHETANI.
Baadhi ya watu hawaamini kuwa kuna kiumbe cha aina hii kinachoitwa shetani, lakini unapoziangalia kazai za uoavu zinazofanyika hapa duniani katika namna iliyo rahisi sana unaweza kujiuliza ni nani aana simamia zoezi hili la uovu ulimwenguni? Biblia inatuambia kuwa yuko na anaitwa shetani.

1.       Asili ya shetani.

Isaya 14;12-15, Ezekiel 28;12-19. Kuna wazo maarufu sana ambalo limo miongoni mwa watu ambao hufikiri kuwa shetani ni wazo tu lililochukuliwa miongoni mwa wapagani na sio la kibiblia, Lakini kwa mujibu wa maandiko Shetani kwa asili ndiye Lusifa (Lucifer – ambalo maana yake ni mwenye kuwaka) alikuiwa mionbgoni mwa malaika wenye utukufu mkubwa, lakini kwa majivuno alitamani kujiinua na kuwa kama Mungu na akaangukia katika hukumu ya Mungu na kuwa shetani kama sehemu ya hukumu yake 1Timotheo 3;6.
Kwa mujibu wa historia ya maandiko ya Isaya 14 na Ezekiel 28 watu hushangaa kwanini Wafalme wa Babel na Tiro ndio wanatajwa kwanza kabla ya kutajwa kwa shetani? Moja ya majibu juu ya hilo ni kuwa  Manabii wanaelezea kusudi la kuanguka kwa shetani kwa kusudi la kivitendo, Wafalme wa Babeli na Tiro walikuwa ni wenye kukufuru wakitaka waabudiwe kama Mungu mwenyezi Linaghanisha na Daniel 3;1-12; Ufunuo 13;15, Ezekiel 28;2 na Matendo 12;20-23, na kwa sababu hiyo mfano wao unakuwa ni somo la wazi wa tabia aliyokuwa nayo lusifa , kwa kusudi la kuwaonya viongozi wao nabii anavuviwa kunukuu tukio lililotokea huko nyuma sana  la malaika hao na huyj aliyeasi na kutaka kuwa kama Mungu, kwa msingi huo kama Mungu aliweza kumuhukumu malaika wake aliyekufuru hatashindwa kuwahukumu kiburi cha wafalme hawa wa Babeli na  Tiro  wanaotaka kujiinua kiasi cha kuchukua nafasi ya Mungu, mashambulizi ya aina hii na aina hii ya kiburi hutoka kwa Yule muovu, ni katika namna kama hiyo kumbuka kuwa alitaka kuwaingizia Tabia hii wazazi wetu wa kwanza Adamu na Hawa Soma Mwanzo 3;5 na Isaya 14;14 na hii ndio roho ya Ibilisi, wakati wote anatamani sana kuabudiwa  angalia Mathayo 4;9 Kama Mungu wa dunia hii 2Koritho 4;4 ni tama ambayo itatimizwa kwa Muda wakati atakapokuja kusimamisha utawala wake kupitia mpinga Kristo Ufunuo 13;4.
Kama adhabu ya uovu wake shetani alitupwa nje  pamoja na jeshi lake  walioungana naye katika tabia ya uasi Mathayo 25;41, Ufunuo 12;7, Waefeso 2;2, Mathayo 12;24, alijaribu kumpata eva kama njia ya kuingiza uasi lakini Mungu alikuwa na mpango wa kuuleta ukombozi kwa njia yua mwanamke  Mwanzo 3;15

2.       Sifa za Shetani.
Sifa za Shetani ziko wazi kupitia majina yake aliyopewa 

a.       Anaitwa shetani.

Shetani maana yake ni adui, mpinzani, kazi yake siku zote ni kuzuia makusudi upinzani huu unaonekana wazi katika majaribio yake ya kuharibu kabisa mpango na makusudi ya Mungu alijaribu kuharibu mpango wa Mungu wa kumleta masihi aliyetabiriwa katika Mwanzo 3; 15 na mapema sana aliweka nguvu zake kupitia Kaini na kumuua habili 1Yohana 3; 12, Mungu alimpa Hawa mtoto mwingine  ambaye alikuwa kama mbegu iliyochaguliwa kwaajili ya kumleta mwokozi ulimwenguni huyu ni Seth lakini sumu ya nyoka huyu ilijaribu kuharibu uzao huo kwa kuuchanganya na uovu kiasi ambacho ilimlazimu Mungu kuleta mafuriko ya gharika, lakini angalau kupitia Nuhu mtu mwenye haki Mungu alianzisha  ukoo mpya wa ukombozi na hivyo shetani alishindwa katika mpango wake kuzuia kusudi la Mungu.
Na kutokana na mwana wa Nuhu Shemu  alikuja kutokea Abrahamu ambaye alikuwa ni chaguo la watu wa Mungu ambaye kupitia yeye Mungu angeleta wokovu kwa Dunia, Na kupitia asili shetani alijaribu sana kuweka uadui dhidi ya watu wa Mungu, Ishimael alimpinga Isaka, Essau alijaribu kumuua Yakobo, Farao alijaribu kuwakandamiza Israel, Hali kadhalika shetani anajaribu sana kuliangamiza kanisa  kwa njia kuu mbili kupitia mafundisho potofu hii ni mashambulizi ya ndani (1Timotheo 4;1 na Mathayo 13;38-39) na mashambulizi kutoka nje yaani mateso Ufunuo 2;10 na ule ukweli kuwa Israel ni kanisa  la nyakati za agano la kale , ile hali ya kutengenezwa kwa sanamu ya dhahabu ni jaribio endelevu katika historia nzima ya kujaribu kuwafanya watu kuabudu mungu mwingine, Na katika kitabu cha Esta kuna mfano ulio hai dhidi ya kuwaharibu watu wa Mungu. Lakini wakati wote watu wa Mungu wameendelea kuweko kwa sababu ya neema ya Mungu kila wakati Mungu hujisazia mabaki na wakati mkamilifu ulipokuja Mkombozi alizaliwa Herode alijaribu kutaka kumuangamiza mapema lakini Mungu alimchenga shetani na shetani akachanganyikiwa, huko jangwani shetani alijaribu kumzuia masihi wa Mungu na kumzuia katika mpango wake lakini alishindwa vibaya tena na kisha Kristo aliendeliendelea kutenda mema akiwaponya wote walioonewa na shetani. Hata hivyo mapambano haya dhidi ya shetani na kazi za Mungu yatafikia ukomo wake katika kilele wakati Shetani atakapomuingia mpinga Kristo ambaye ataharibiwa wakati wa kuja kwa Kristo.

b.      Mshitaki

Shetani huitwa mshitaki wetu Ibilisi ni mmshitaki dhidi ya Mungu na watu wake Mwanzo 3;2,4,5. Na Mwanadamu, Ufunuo 12; 10, Ayubu 1;9, Zekaria 3;1,2, Luka 22;31.

c.       Muharibifu.

Shetani anaitwa muharibifu au muharabu kwa kiyunani ni Apollyon na kwa kiebrania Abaddon Ufunuo 9;11 akiwa amejawa na chuki  dshidi ya Muumba  na kazi zake  anajiweka mwenyewe kama Mungu wa uharibifu.

d.      Nyoka 

Shetani huitwa Yule nyoka wa zamani Ufunuo 12;9 huenda inatumika kukumbushia namna alivyojibadili  zamani akimtumia nyoka  kama njia ya kupitisha majaribu na kusababisha anguko la mwanadamu.

e.      Mjaribu.

Mathayo 4;3  kujaribu maana yake kuonja au kuweka majaribuni wakati mwingine Mungu hujaribu lakini kujaribu kwake ni kwaajili ya kutoa mtihani test kwaajili ya kutupandisha daraja  kwaajili ya wema wake  Mwanzo 22;1  wakati Mungu huwajaribu wanadamu kwaajili ya mema yao zaidi Shetani huwajaribu watu kwa kusudi la kuwaangusha na kuwaangamiza.

f.        Anaitwa mfalme na Mungu wa dunia hii.
Yohana 12;31 2Wakoritho 4;4,Majina haya yanahusiana na kazi anazozifanya dhidi ya jamii kama zilivyogawanywa na Mungu mwenyezi ulimwenguni Ulimwengu huu uko chini ya uovu dhidi ya ibilisi 1Yohana 2;16,ulimwengu unaotajwa kimaandiko unahusu utaratibu wa kibinadamu ambao unaongozwa na utatu wa Heshima, anasa na faida , sheatani anashikilia kila kitu ulimwenguni anatawala njia za uchumi na anasa na faida akiwa na mamlaka aliyoipora kutokana na mwanadamu kushindwa kutawala vyote kama Mungu alivyomuamuru, ni katika anguko la mwanadamu shetani amekuwa mtawala wa ulimwengu huu akitumia tamaa ya macho, kiburi cha uzima.

3.       Kazi za Shetani.
a.       Kwa asili kazi za shetani  ni kupingana na mpango wa Mungu 1Thesalonike 2;18, hufanya kazi ya kupingana na injili Mathayo 13;19 2Wakoritho 4;4, anafanya uvamizi,anapiga upofu, anadanganya anaweka mitego, Luka 22;3,2,Wakoritho 4;4, Ufunuo 20;7,8 1Timotheo 3;7, Anafanya mashambulizi Ayubu 1;12 anajaribuwatu wa Mungu,1Wathesalonike  3;5
Anasemekana ni mwenye hila na hupindua maandiko 4;4,5, Anakiburi na majivuno  1Timotheo 3;6, Ni mwenye nguvu Waefeso 2;2  ni mchonganishi, Ayubu 2;4 ni mwerevu Mwanzo 3;1  ni mdanganyifu Efeso 6;11 ni mkatili na mkali 1Petro 5;8
b.      Hutenda kazi kam malaika wa Nuru, katika namna isiyokuwa ya kawaida shetani hujifanya kama malaika wa nuru katika utendaji wake wa kazi 2Wakoritho 11;14, inaonekana kuwa tangu mwanzo amekuwa akijihudhurisha  katika makundi ya wana wa Mungu mfano ayubu 1.Kwa kusudi kama hilo huweza kujipenyeza katika kanisa la Mungu na kupenyeza mafundisho yake 1Timotheo 4;1 au kwa lugha nyingine sinagogi la shetani Ufunuo 2;9 na watumishi wake pia hujifanya kama malaika wa nuru 2Wakoritho 11;15 makusudi makubwa ya utendaji wake  anapojiingiza katika makundi ya watu wa Mungu  ni kwaajili ya kuliharibu kanisa  kwani anajua kuwa akifanikiwa kuwaharibu wale ambao ni chumvui ya ulimwengu na kuwateka watu kuwa watumishi wake  itakuwa rahisi kwakekupata mawindo na kupanda roho ya kuasi  kwa jamii ya ulimwengu wote.
c.       Hutenda kazi kwa chuki kubwa sana unaweza kujiuliza kwanini shetani hutaka watu wabakie kama magofu tu? hii ni kwa sababu shetani anachukizwa sana na ile sura na mfano wa Mungu ambao mwanadamu aliumbwa nayo na itakuwa ndani yetu, anachukizwa na ile hali ya kuwa wanadamu lakini wakati huohuo tumefananishwa na wana wa Mungu, ana chukizwa na utukufu wa Mungu tulio nao na mpango wa Mungu wa kumtukuza na haimaye kuwa na mwisho wenbye furaha anachukizwa na furaha iliyo ndani yetu tunayopewa na Mungu ambayo tutakuwa nayo milele, kwa ujumla anachukizwa nasi kwa sababu maelfu elfu kama myahudi mmoja wa zamani alivyosema kuwa  ni kwa wivu wa shetani kifo kilikuja ulimwenguni  na wale wamfuatao wako upande wake.
d.      Sheatani ana mipaka, Pamoja na kuwa shetani anatajwa kuwa mwenye nguvu lakini ni muhimu kufahamu kuwa hana nguvu zote, kwa wale wamwaminio Kristo shetani amekwisha shindwa hana kitu kwetu  Yohana 12;31  na ana nguvu kwao wale wasioamini  na kwetu sisi tunaoamini hana nguvu na kama tunampinga anaweza kutukimbia  Yakobo 4;7, ana nguvu lakini nzinz mipaka  anaweza hata kuleta majjaribu au vishawishi Mathayo 4;1 anashambulia Ayubu 1;16 anaweza kuua Ayubu 2;6, Waebrania 2;14 na anaweza kumgusa mwamini kwa ruhusa ya Mungu tu.
e.      Shatani ana mwisho,  tangu mwanzo Mungu alikuwa amekwisha kuhaidi kuwa  atashughulika na nguvu zilizopelekea mwanadamu kushindwa Mwanzo 3;15 huyu ni uzao wa mwanamke ambao utamponda shetani kichwa, shetani alikwisha kutupwa kutoka mbinguni tangu zamani  na wakati wa dhiki kuu  atatyupwa hata nchi Ufunuo 12;9 na wakati wa millennium atafungwa  katika shimo kwa miaka 1000 na baada ya miaka 1000 atatupwa katika ziwa liwakalo moto Ufunuo 20;10 wakati huu Neno la Mungu linatuthibitishia kuwa uovu utakuwa umefikia ukingoni.

UFAHAMU KUHUSU MALAIKA WALIOASI.

1.       Malaika walioasi.

Malaika waliumbwa wakiwa wakamilifu, wasio na doa wala waa kama ilivyokuwa kwa mwanadamu, lakini Mungu aliwaumba wakiwa na utashi yaani uwezo wa kuamua, chini ya uongozi wa shetani wengi wa malaika hao waliasi na kufukuzwa mbinguni Yohana 8; 44, 2Petro 2;4 Yuda 6 Dhambi kubwa waliyokuwa nayo na aliyokuwa nayo kiongozi wao ni kiburi baadhi wamefikiri kuwa tukio hili la kuasi ni ufunuo ujao wa wakati wa kuzaliwa kwa Kristo  na shetani kutaka Kuabududiwa Lakini Yesu alimshinda.
     Baadhi ya kundi hili la malaika walioasi wamewekwa katika kifungo 2Petro 2;4 na baadhi wamo ulimwenguni, angani na kila mahali wakituzunguka 1Yohana 12;31,14;30.2Koritho 4;4, Ufunuo,12;4,7-9, kwa kuwa walifanikiwa kumuingiza mwanadamu katika dhambin wamekuwa na nguvu kubwa kuliko wanadamu 2Wakoritho 4;3-4, Waefeso 2;2,6;11-12, Lakini nguvu hizo zimeharibiwa kwa wale waliookolewa  na wanaodumu kwa uaminifu katika Kristo kwa ajili ya ukombozi mkuu alioufanya Kristo Ufunuo 5;9,7;13,14. Malaika hawa kwa bahati mbaya hawajapewa nafasi ya ukombozi 1Petro 1;12 Lakini moto wa milele umeandaliwa kwaajili yao kwaajili ya hukumu Mathayo 25;41.

2.       Mapepo.
Maandiko hayaelezi kwa asili mapepo chanzo chake ni nini, kwa sehemu kubwa inaonekana  siri inayozunguka ulimwengu wa uovu, lakini yanashuhudia  kwa uwazi kuweko kwao na vitendo vyao Mathayo 12;26,27, Katika injili tunawaona kama roho wabaya wasio na mwili na huwavamia watu na kuwatesa hususani wale wanaoitwa kuwa wamepagawa na pepo na inaonekana kuwa wakati mwingine pepo hao kwa wingi wao huweza kumkalia mtu mmoja  Marko 16;9,Luka 8;2 na athari za kukaa kwa wingi ndani ya mtu ni pamoja na kuweko kwa kichaa, kupooza,na magonjwa mengine, hususani  yale yanayohusiana na mfumo wa fahamu Mathayo 9;33,12;22, Marko 5;4,5 Mtu anayemilikiwa au aliyepagawa na mapepo huwa wakati mwingine hawezi kujidhibiti mwenyewe na roho hao wachafu huweza kutumia hata kinywa chake na kuzungumza, au wanaweza kumfanya mtu kuwa bubu au asiyesikia  na huweza kuwaendesha wanaowavamia bila wao kupenda  kama chombo chao na wakati mwingine kumpa nguvu zao

UFAHAMU ZAIDI KUHUSU PEPO.
Pepo kwa kiingereza ni Demon ambalo limetokana na neno la kiyunani Daimon (Dainamon) ambalo maana yake ni roho chafu zenye akili na uweza wa kufanya maajabu na kazi nyinginezo mbalimbali
Mawazo ya kiyunani kuhusu Mapepo.
Kwa wayunani neno Daimon lilitumika na wazo kuhusu Mungu, au nguvu za Mungu ambalo lilimaanisha pia nguvu zenye vurugu kuhusu Mungu au mtu mwenye akili za kupita kawaida na mwenye uwezo wa kutabiri au kupiga ramli au nafsi ya mwanadamu iliyoishi zamani na inayoweza kuunganisha watu na miungu, hata hivyo pia neno hili lilitumiwa  likihusihwa moja kwa moja na nguvu zinazohusiana na kuleta magonjwa ambazo ziliaminika kuwa zinatawala mazingira na maisha aidha pia mapepo walifikiriwa kuwa ni wazuri na wabaya na wengine waliwafikiria kuwa ni mizimu, wengine walifikiria kuwa ni roho zinazomwangalia mwanadamu na kumfuatilia tangu anapozaliwa na ambazo zinaweza kuwa rafiki au adui, wengine waliwafikiria kuwa ni nguvu za kisasi zinazotoa adhabu kwa sababu ya makosa Fulani, Baadhi ya wanafalsafa wa kiyunani kama Thales alisema kuwa “kila kitu kimejaa miungu” wakati mwanafalsafa Pythagoreans Yeye alifundisha kuwa anga lote limejawa na nafsi zinazoitwa Mapepo na mashujaa na ni nafsi zisizo na mwili ambazo ziliaminiwa kuwa zimetumwa kushughulika na Afya na magonjwa kwa wanyama na wanadamu ili kwamba wanadamu watafute utakaso na kurejesha mahusiano na Mungu na kutenda mema, na kuishi kwa utaratibu uliokusudiwa, Mwanafalsafa Heraclitus aliamini kuwa kila mtu ana pepo linalomkalia na kumuongoza au kumdhibiti, na mwanafalsafa Empedocles alichangia kuwa pepo ni roho wenye kutia shaka wasioweza kuelezeka vema wenye kushughulika na uovu na kuna uwezekanao wakawa ni wanadamu waliogeuka kuwa kitu kingine baada ya kufa kwao, Mwanafalsafa maarufu Socrates yeye alisema hapendelei kuzungumzia swala lolote linalohusiana na mawazo yenye kuhusu uungu au vile visivyoweza kuthibitika ingawaje aliheshimu kuwa huenda maswala hayo yako kutokana na uzoefu anaokutanao mtu mmojamoja kupokea maoni ya kimungu na ishara mbalimbali, Mwana falsafa Plato yeye alisema kuwa Pepo ni nafsi za watu waliokufa ambao hutumika kufanya kazi tofautitofauti ikiwa ni pamoja na kutafasiri maswala kadhaa kuhusu Mungu na wanadamu akiunga mkono hoja ya mwanafalsafa Heraclitus yeye Plato aliamini kuwa  kuwa muongozo wa kweli wa mwanadamu uko katika akili zake ambazo ndio nafsi ambayo ni zawadi kutoka kwa Mungu. Mwanafalsafa Aristotle hakuwa na wazo kubwa sana kuhusu mapepo ingawa kwa kiasi Fulani aliamini kuwa kila mwanadamu ana mapepo ambayo huambatana naye siku zote za maisha yake.Mwanafalsafa Stoics ni kundi lililokuwa likiamini kuwa kila kitu kina Mungu Pantheism pia waliamini katika maswala kuhusu nguvu za giza ambazo kwa uwezo wa kipepo mwanadamu anaweza kuonyesha kuvumilia, kuonyesha hisia, maumivu na furaha na kadhalika waliamini kuwa pepo wako katika hali ka hizo wakifurahia kuwepo kwao milele na kuwa wako katika maeneo yote karibu na mwezi, wakati kundi la wanafalsafa wa Epicurus wao walikwenda nje kabisa wakiamini kuwa  hakuna mapepo na kuwa kama wako hawana uwezo wa kuwasiliana na aina binadamu kwa njia yoyote.

Mawazo ya kikaldayo (Mesopotamia) kuhusu pepo.

Tangu mwanzo watu wa ukaldfayo au Mesopotamia walikuwa ni wachawi kupindukia hii huenda ni kwa sababu ya kuishi katika mazingira yaliyozingukwa na mfumo huo wa maisha uliochangiwa na dini zao, kama ilivyo huko Misri mpango wao wa kimaendeleo ulikuwa ukichangiwa na kuwako kwa mto Nile huko Mesopotamia nako waliishi wakipambana na mfumo kama huo wa kuzungukwa na mto Tigris na Frati jamii ya kusumerian ilitoa tafasiri ya maswala kadhaa kutokana na dini za asili za kimesopotamia  na kujenga mawazo na kanuni huku wakiwa na ufahamu wa juu kuwa mwanadamu ndie kiumbe wa juu zaidi kuliko uungu na hivyo walikuwa na vihadithi vingi kuhusu ulimwengu wa chini yaani kuliko na miungu kuwa kuna Anunnaki na miungu wengine waovu saba walioitwa Assakki au mapepo ambao pia walikuwa wakishikilia nyadhifa za maeneo yao, ilifahamika wazi kuwa kazi ya Pepo ni pamoja na kupigia ramli,kusababisha magonjwa hususani pepo wanapoingia kichwani na katika maeneo ya kichwa na sehemu za ndani na ili kufanikisha maswala hayo ilikuwa ni lazima kazi za kichawi zifanyike zikihusisha uvaaji wa vifaa Fulani kama shanga na mapambo ya thamani na yanayofanana na hayo,Pia walikuwa na imani kwamba ili kujilinda kutoka katika mashambulizi ya magonjwa yatokanayo na nguvu za kichawi ambayo hupitia katika mdomo pua na masikio miungu kama Ea ambaye ni miungu ya maji waliombwa ili kusaidia aina hizo za uvamizi, Miungu hiyo ambayo ilikuwa na makuhani maalumu pia ilikuwa na kazi za kutafasiri ndoto na kuondoa mapepo, mungu huyu Ea pia aliitwa Madruk!, aidha mtu alipokufa katika mazingira ya kutatanisha baada ya kuzikwa utafiti ungeganyika kuweza kubaini sababu za kifo hicho kama ni mizimu au mengineyo Mizimu hiyo ilijulikana kwa jina la Etimmu na makuhani wake maalumu waliitwa Eship, Wakaldayo pia waliwapa pepo majina kulingana na utendaji wa kazi wa mapepo hayo kwa mfano wako pepo walioitwa Rabisu au The Croucher  pepo huyu aliaminika kuwa na uwezo wa kulala chini akijificha na kuvizia maadui ili kuwadhuru na kuwashughulikia au kuwaua kwa msingi huo tendo kama lile la kaini kumuua Habili alipoambiwa dhambi iko inakuotea kwa wakaldayo dhambi hiyo ni Pepo Rabisu aliyemuingia Kaini ili kuvizia Habili na kumuua Mwanzo 4;7
     Huenda ni katika sababu kama hizo Pepo walipewa majina katika jamii ya kisumerian, watu wa Babeli walitoa nguvu kubwa sana katika kuamini juu ya kuwepo kwa mapepo na kuamini nguvu za kichawi waliamini pia kuwa ili mtu amtoe Pepo ilikuwa ni lazima awe ni kuhani anayejua jina la Pepo huyo na tabia zake ndipo amtoe Marko 5; 9, Luka 8; 30 aidha katika mazingira Fulani aina Fulani za magonjwa na matukio husababaishwa na mapepo.

Mawazo ya kimisri kuhusu pepo.

Kama ilivyo kwa tamaduni za mataifa mengine hapo juu wamisri nao zamani sana waliamini kuweko kwa mapepo wengi sana, na waliamini na kuzitegemea nguvu za mapepo hayo katika kila jambo, wao waliwahusisha miungu yao na mapepo bila kuwatofautisha, waliamini kuwa ndio waliohusika na kila aina za matukio yakiwemo mafuriko, dhuruba, kama ilivyo kwa wakaldayo wamisri waliamini pia kuwa kila aina ya magonjwa ilisababishwa na mapepo hao kuja na kumuibia mtu hali yake ya kawaida na kumuachia maumivu homa na hata kifo na hivyo ili kujilinda nao ilikuwa lazima mtu kuvaa hirizi na vitu vingine vya ulinzi, waliaminiwa pia kuwa pepo wanamiliki anga, pia wamisri waliogopa sana mapepo yaliyokuwa na uwezo wa kuvaa mwili wa aliyekufa na kuja kama mizimu ili kulipiza kisasi kwa binadamu wenye matendo maovu hivyo waliogopewa sana na kupewa majina kama walipizi,wauaji,makata,na majina mengineyo, waliamini pia kuwa pepo hao pia huja kuwa miungu, hata hivyo katika Misri hwakuwa na imani kuwa kuna mapepo wanaoweza kuwavamia watoto au mapepo waliokuwa na uwezo wa kunywa damu ya mtu kama ilivyo sehemu za Babeli.

Mawazo kuhusu pepo katika agano la kale na Vitabu vya apokrifa.

Katika jamii za kale za kiebrania hakukuwa na hali kamili inayoeleweka kuhusu Pepo badala yake kuna majina yaliyotumika kuwahusu kama mungu yalitumika pia kumaanisha pepo, Mungu aliitwa Lohim na mtu mwenye kuvuviwa na aina Fulani ya nguvu za Mungu aliitwa mtu wa lohim yaani mtu wa Mungu, au muonaji, kwa hiyo jina lohim lilitumika kumaanisha nguvu Fulani inayojitengeneza na kusababisha ushindi au aina Fulani ya ushindi kupitia mieleka mfano wa lugha hizi unaonekana katika Mwanzo 30;8, kwa hiyo aina hiyo ya nguvu inapomjia mtu na kumuwezesha kutabiri  ilifikiriwa kuwa ni nguvu ya Mungu au upepo Ruah lohim mfano wa maswala kama hayo ni kama swala la Balaam Hesabu 24;2 au kile kilichomtokea Sauli 1Samuel 10;11,19;20-23 na matumizi ya lohim yakihusishwa na pepo pia yanaonekana katika  2Samuel 16;15-16,23
      Yako matukio ambayo waebrania walifikiri moja kwa moja kuwa yanatokana na Mungu, hata kama matukio hayo yalisababishwa na shetani katika hali ya kawaida ilionekana ni kama Mungu ndiye anayeruhusu shetani au mapepo kushughulika na mtu huyo mfano tukio kama la Saul 1Samuel 19;9-10, hali kadhalika hali mbaya iliyompata Ayubu ilifikiriwa kuwa inatoka kwa Mungu Ayubu 2;7 kwamba maovu yaliyompata yalitoka kwa Mapepo au shetani yakliruhusiwa na Mungu, Kwa msingi huo agano la kale lina maswala ya kufikirika tu kuhusu elimu au ujuzi wa utendaji wa mapepo na shetani kwa ujumla “It is some illusions” kwa msingi huo waebrania walikuwa na ujuzi kuhusu mapepo na utendaji wa kichawi kutoka kwa mataifa mageni yaliyokuwa yakiwazunguka tu Kumkukumbu 32;16;17, Biblia ya Septuagint ilitumia neno miungu migeni ambayo kwa kawaida ilikuwa ikihusisha au ikizungumzia mapepo au mashetani  Zaburi 106;37 pia iliitwa, miumgu ya kipagani na kwa namna Fulani Biblia inawataja hao kuwa majini katika Mambo ya Walawi 17;7,2Nyakati 11;15 pia waliitwa jeshi la mbinguni Matendo 7;42-43.

Mawazo kuhusu pepo katika vitabu vya Apokrifa

Mafundisho kuhusu malaika kama yanavyoonekama katika Apokrifa yana utata kama ilivyo katika khadithi za kiislamu kuhusu Mapepo a majini mfano tunaona katika Kitabu cha 1Enoko15;9-16 kwamba malaika wenye tama walijaribu kutatua tatizo la kuweko kwa dhambi kwa kuwaoa wanawake  wa kibinadamu duniani. Kwa ujumla mafundisho kuhusu viumbe hao wa kiroho katika apokrifa ni kama maluweluwe “illusions” ingawa wengine inaonekana kuwa walinukuu historia kadhaa za kweli ya kibiblia kuhusu msaada wa malaika kwa mfano 1Makabayo 7;41 tunaona Yuda makabayo akiomba malaka kuwasaidia katika vita kama alivyofanya wakati wa Hezekia na pia 2Makabayo 11;6, 15;22-23 inaonekana wazi kuwa Yuda Makabayo mara kwa mara aliomba Munu kusaidia kmtuma malaika wake kwaajli ya msaada wa kivita  na Mungu aliwapa ushindi,wakati kitabu cha kiapokrifa cha hekima ya Suleimani hakina nukuu yoyote kuhusu malaika au pepo zaidi ya kunukuu kila kinachofanana na ufafanuzi wakitabu cha kutoka Hekima ya Suleimani 18;15. Vitabu vingine vya apokrifa vina hadithi ambazo zimetiwa chumvi sana kuhusu malaika na mapepo baadhi wanaamini katika malaika wema na wabaya lakini katika hali iliyotiwa chumvi mmno na wengine wanaaamini kazi zao mfamo kitabu cha Tobia, agano la mababa 12, ufunuo wa Baruku, 2Edras na kitabu cha jubilee. Mwandishi anaonekana kuzungumzia akihisisha matukio ya asili na maswala ya kiroho kama ilivyo katika kitabu cha Ayubu. Ayubu 2;2,10;5 wakati kitabu cha agano na mababa 12 kinazungumzia  kuweko kwa tabia mbaya kwa wanadamu kama matokeo ya kazi za kipepo wakiwemo pepo saba wa udanganyifu, roho hizo ndio zinazowaongoza wanadamu katika kufanya dhambi na kwa ujumla ilikuwa ikifikiriwa kuwa utendaji huo unafanyika chini ya uongozi wa Beliariau Shetani kama inavyogusiwa katika Zaburi ya 18;4-5.

Vitabu vya ufunuo vya kiapokrifa vingi vinamaoni kuwa Mungu alimpindua shetani na nguvu ya wema ikaanza kutawala kabla ua ulimwengu kuumbwa Asher 1;9,6;2 Jarubu la Daniel 1;6 Jaribu la Yuda 13;3,14;2 kwa ujumla kuna mawazo mengi ya kipagani katika apokrifa kuwahusu Pepo au malaika kwa ujumla wayahudi wenye msimamo mkali walikuwa wanachangamoto za kutaka kuonyesha uwezo wa Mungu na ili kuueleza vema kwa wanadamu wengi walimfikiri shetani kuwa pepo mkuu aliyejaribu kumpotosha mwanadamu Hekima ya Suleimani 2;4 na Enoko 3;31 waandishi hao walimpa jina shetani kama Diabolos yaani asi wakimuonyesha sawa na nyoka aliyemdanganya Hawa katika Bustani ya aden, aidha wengine walikuwa na mashaka kuwa viumbe hao mashetani walimuasi Mungu pale walipojaribu kuwaingilia wake za Binadamu Mwanzo 6;1-4 na Ezekiel 28;13-17 inasemekana mazwazo uya aina hii yanadhaniwa kupandikizika na watu walioamini kuwa kila kitu ni kiovu hivyo kwa tendo la amalaika kuwaingilia Binadamu walitenda uovu “Dualism” imani inayoamini kuwa kila kitu ni kiovu ukiwem mwili.

Katika vitabu vyenye asili ya kiapokrifa habari za kusisimua zaidi kuhusu malaika tunaipata katika kitabu cha Tobia  au tobiti pia tunaona habari ya utendaji wa kijini (Pepo) na kutajwa kwa malaika Rafael ambaye anajitambulisha kuwa mmoja wa malaika saba walio watakatifu na wanaopeleka sala za watakatifu na kuingia katika utukufu wa Mungu Kitabu cha Tobia 12;15-21. Kwa ufupi katika kitabu cha tobiti  tunaona jina la msichana aliyekuwa akiitwa Sara ambaye kila alipokua anakaribia kuolewa Mumewe aliuawa na jinni  usiku wa siku ya harusi na ilitokea hivyo mara saba  Jini lililokuwa likihusika na kazi hiyo liliitwa Asmodeo jinni la kiume kwa sababu ya misiba hiyo Tobiti na Sara waliamu kumuomba Mungu  ili wafe kwa kukata tama lakini Mungu aliwahurumia na kugeuza huzuni yao kuwa furaha  akamtuma malaika Rafael amsindikize mwanadamu Tobia  kwa Raguel baba wa sara , huo wakaozwa  na kifo hakikutokea tena, Hizi ni habari za kusisimua kuhusu malaika na majini katika utendaji wao kama tuonavyo katika kitabu hki cha Tobiti chenye asili ya kiapokifa kwa ufupi kinaonyesha kazi za majini na kazi za Malaika katika jukumu lilelile la kuwahudumia wanaomcha Mungu.

Mwandishi na mchoraji maarufu Francesco Botticini alichora habari kutoka kwenye vitabu vya apokrifa akionyesha malaika watatu wakimsindikiza Tobia Malaika aliyemshika mkono tobia ndiye malaika Rafael Picha hii ilichorwa mwaka 1470 na ilihifadhiwa huko Uffiz Gallery huko Flolrence Italy. (Tobiti 12;1-21)

Mtazamo wa waislamu na Quran kuhusu Mashetani, Majini na Malaika   

    Waislamu wanaamini kuwa kuna viumbe walioumbwa na Mungu ambao hawaonekani kwa macho ya kibinadamu viumbe hawa wamegawanyika katika makundi makuu matatu.

  • Shetani
    Shetani ambae hutambulika pia kama ibilisi “iblis” ameitwa hivyo kwa sababu alilaaniwa na Allah  kwa kukataa kumtii allah alipomuamuru kumsujudia Adamu mara baada ya kuwa amemuumba (Surat al-baqara 2;28-38 na al aaraf 7;10 na al khaf 18:50) kutokana na laana hiyo alipewa muda na Allah ili awapoteze watu kwa kuwakalia pande zoote na alipewa ruhusa baada ya kujiombea kufanya hivyo(al-aaraf 7;16-17)Allah alitoa nafasi ya kuingia motoni kwa yeyote atakayemfuata shetani,Hivyo kwa waislamu shetani ni adui mkubwa na hulaaniwa kila mwislamu anapotaka kufanya jambo lolote hujikinga na muovu huyu kwa dua hii “ aaudhubiiIlah mina shaytwaani rajiim” yaani najikinga kwa allah na shetani apigwae mawe,ameitwa apigwae mawe kwa kuwa Ibrahimu na mwanawe Ismael walimpiga mawe Punde alipotaka kuwadanganya wasiitii amri ya Allah ya kutaka kumtoa Ismail dhabihu,Mashetani ni kundi kubwa sana na baba yao majini ni shetani.Vitabu maarufu vya kiislamu vinathibitisha soma (Itqaan fiy’uluwmi al-juzuu 4 uk 374,hadith 5,553).

·         Majini

    Kumbuka shetani alikuwa miongoni mwa majini(al-kahf 18;50) hivyo shetani ni jinni na jinni ni shetani,quran inafundisha kuwa viumbe hawa waliumbwa kwa ndimi za moto(al-Hijir 15;26-27,ar –Rahman 55:14-15) woote wanaofanana na shetani woote wamezaliwa na shetani woote kazi zao zinafanana,Hivyo majini yana nafasi kubwa sana katika uislamu kujaribu kuwatenga majini na mashetani  ni kiini macho tu kwani majini yalisilimu (surat 72;1-14) ingawa kuna kundi lingine halikuslimu, Hata hivyo Allah aliwatumia woote katika kazi mbalimbali  mfano kumsaidia Sulemani katika kazi zake mbalimbali za ujenzi, kumletea johari na vito vya thamani toka baharini,kumjengea nk.Soma (Surat al anbiyaa 21;81-82)Allah alikuwa mlinzi yaani msimamizi, Allah pia huwatumia majini kufarikisha watu aliwatumia huko Babeli na kufundisha watu uchawi hawa mashetani huitwa Haruta na Maruta soma (al-Baqara 2;102) aidha katika namna ya kushangaza Allah alimletea kila nabii maadui aliowatuma mwenyewe yaani majini na Mashetani (surat al anam 6;112 na al-Hajj 22;52).Baadhi ya Madhehebu kama ahmadiyya walipogundua kuwa majini ni mashetani na mashetani ni majini walianza kukataa dhana hii na shehk Farsiy anawakanusha vikali katika ufafanuzi chini,Waislamu wanatambua kuwa majini ni ndugu zao na ndio maana moja ya mashart ya swala katika kumalizia kikao cha mwisho kiitwacho (atahiyat) lazima kwa kila Muislamu asalimie pande zoote mbili yaani kwa kugeukia kushoto na kulia,kushoto ni kusalimia muislamu mwenzako na kulia ni kusalimia kundi kubwa la majini ambao hujumuika na waislamu katika swala (arshad-alMuslim) hii ni lazima hata kama mwislamu atakuwa pekeyake wakati wa swala kwani majini hujumuika nae.Aidha muhamad anasema kila muislamu anapozaliwa anapata ulinzi toka kwa majini na mashetani (soma al-muslim,Miskat), Majini yana ufahamu mkubwa sana wa quran na uislamu, yameslimu Muhamad alipokwenda kwa majini na kuanza kuwauliza mambo ya uislamu majini yalijibu vizuri kuliko wanadamu soma (surat al ahqaf 46;29-30) soma pia ufafanuzi wa aya hiyo chini katika quran ya Farsiy.Kwa ujumla hutakutana na jinni ambalo lina jina la kikristo majini yoote yana majina ya kiislamu anaeleza Desmon Mkumbo moja ya wataalamu wa huduma ya biblia ni jibu Tanzania.Majini pia huhubiri Uislamu  kwa nguvu na huhusika kusilimisha watu ukiwa na ugonjwa au pepo limekupagaa ukipelekwa kwa sheikh au maalim akusomee duwa utapewa masharti ya kubadili dini,jina, kusilimu au kuswali haya ni maagizo ya majini Mwenye masikio na asikie!.

·         Malaika (malaikat)

   Hili ni kundi la tatu katika imani ya kiislamu kuhusu viumbe wasioonekana kumbuka waislamu huamini malaika na inasemekana kuwa Allah aliwaumba viumbe hao kwa nuru,Idadi yao haijulikani,kazi yao ni kumsifu Allah wako malaika wa muhimu watano nao ni jibril huyu ndiye malaika mkuu Allah humtuma kuwasiliana na manabii wake Quran humuita Roho mtakatifu (surat an nahl 16:102). Ni Roho wa mafunuo na Nguvu Laylatul-Qadr (surat al qadr 97;1-4)Mikail huyu yuko chini ya jibril (al baqara 2;98),Israfiil ni malaika anayeaminika sana,anasifika sana hatajwi katika quran lakini anaaminika kuwa ndiye atakaye puliza parapanda siku ya mwisho,  Izrail pia hatajwi katika quran lakini anaaminika kuwa ndiye mtoa roho za watu (al anam 6:61),Hamalat al arsh hawa wako nane inaaminiwa kuwa watabeba kiti cha Allah siku ya hukumu  (al- haqqah 69;17), Waislamu huamini pia wako malaika wengine watano ambao hujulikana kwa kazi zao hao ni hafadhan hulinda binadamu kutoka katika mikosi na balaa kwa mujibu wa Muhamad katika hadithi zake anadai wako kumi.Katibun hawa huandika habari za mtu wako wawili mmoja huandika habari za matendo mabaya na mmoja mema, wa mabaya hukaa kushoto wa mema hukaa kulia kila mtu anao wawili (az-zukhuf 43;80 na qaf 50;17-18),Malik ni mlinzi wa moto wa Jehanam(az-zukhuf 43;77),Ridhiwan hulinda pepo (paradiso),Munkar na Nakir  hawa ni wakali sana huuliza maswali kaburini mtu anaezikwa huulizwa maswali juu ya uislam, hivyo muislamu anapozikwa Masheikh humfundisha namna ya kujibu maswali hayo mtu aliyezikwa ili kumuepusha na adhabu ya malaika hao.

Mtazamo wa mapepo katika agano Jipya:

Wakati waandishi wengi wa nyakati za agano la kale hawakuwa na mvuto wowote kuandika habari kuhusu mapepo waandishi wengi wa Agano jipya walizungumzia sana swala la mapepo huenda ni kwa sababu labda Yesu alikuwa na huduma ya kutoa pepo  kwa sababu hiyo katika agano jipya kuna nukuu nyingi sana kuhusu pepo ambao kimsingi walifikiriwa kuwa ni viumbe vya kiroho ambavyo ni adui wa Mungu na wanadamu na mkuu wao alifikiriwa kuwa ni Belizebuli Marko 3;22 ingawaje pia kuna nukuu chache sana  kuwahusu Pepo pia walifikiriwa kuwa ni miungu migeni Matendo 17;18, Waliitwa pia mashetani 1 Koritho 10;20,Ufunuo 9;20 kwa kiyunani neno mashetani linasomeka “Dainamonia” ambayo ilimaanisha miungu ya kipagani na sio “Demons” yaani mapepo na hii ilitokana na kutolewa sadaka kwa miungu, kwa mafundisho ya Kristo kuhusu uwezekano wa kutokuwatumikia mabwana wawili Mathayo 6;24, Luka 16;13 kuweko kwa huduma za kiinjili za utoaji mapepo katika agano jipya  ni wazi kuwa inaashiria uwezo wa Kristo wa kuwa kinyume na Mapepo na Nguvu za giza na Biblia agano jipya linaonyesha wazi kuwa kutoa pepo sio kazi rahisi ni vita Mathayo 17;19, Marko 9;28 na ni uthibitisho ulio wazi kuwa Yesu Kristo ana nguvu kubwa kiasi gani na ni uthibitisho ulio wazi kuwa Pepo wanatambua  wazi kuwa asili ya Kristo ni Mungu Luka 11;15, Yohana 7;20,10;20 na hii inathibitisha wazi kuwa ule usemi wa Yesu kuwa ufalme hauwezi kusimama ukifitinika kwa nafsi yake kwani utaanguka Luka 11;17-18 kwa msingi huo Kristo aliweka wazi kuwa anatoa Pepo kwa Chanda cha Mungu kwa hiyo kutoa pepo ni sehemu ya kuusimamisha ufalme wa Mungu na kubomoa ule wa Shetani Mathayo 12;28 Yesu pia alishirikisha karama hii ya utioaji wa mapepo kwa wanafunzi wake Luka 9;1 na 10;17 ni wazi kuwa walirudisha Ripoti kuwa Pepo wana watiii kwa jina la Yesu.

Katika agano jipya maneno mawili pia yalitumika “Ponera” la kiyunani kumaanisha Pepo na “akatharta” ikimaanisha roho chafu ingawaje katika mazingira dulani roho chafu na pepo hutumika kwa kubadilishana  Luka 8; 27-29 ni katika Luka 11;24 kwa Kiswahili neno pepo mchafu hutumika zaidi Marko 1;23,7;25, Kwa msingi huo ni wazi kuwa pepo ni jeshi la shetani a,bal liko kinyume na Mungu na wanadamu na kuwafukuza na kuwatoa kwa jina la Yesu ni fundisho lililo wazi kuwa ufalme wa Mungu uko kazini na ni wazi kuwa Yesu ana nguvu dhidi ya kazi za shetani na kuwa Yesu ni Mungu.

MAPEPO NA ASILI YA UOVU:

Kwa asili Biblia agano jipya inatufunulia wazi na kutufundisha wazi kuwa kuna uhusiano wa Karibu kati ya uovu au mambo mabaya au magonjwa na mapepo ingawa tunaweza kusema kuwa si yote lakini katika mazingira kadhaa aliyokutana nayo Yesu katika huduma yake na katika swala zima la ufukuzaji wa Pepo ni wazi kuwa uko uhusiano huo Mathayo 4;1-11 Marko 1;12-13 na Luka 4;1-13 mjaribu aliyetaka Kristo atende uovu alikuwa ni shetani, pia tunaona asli ya uovu sehemu nyingine ni waz kuwa muhusika wa aina hiyo ya uovu ni shetani na majeshi ake yaani pepo Marko 5;9, Luka 8;30 ni wai kuwa Kristo alitaka kuonyesha ni kazi gani mbaya wazifanyazo mashetani na wanapowaingia binadamu husababbisha maovu makuu mmno na zaidi ya yote ni wazi kuwa nguvu zao hazina kitu dhidi ya utendaji wa Mungu Mathayo 7;22.
      Pepo kutoka kwa jina la Yesu swala hili lilimaanisha kuwa kuna nguvu katika jina la Mungu au ni wazi kuwa Kristo alikuwa anabeba nguvu ya uungu tangu zamani waandishi walionyesha uhusiano ulioko wenye nguvu katika jina la Mngu Zaburi 20;7, 118;12 ni wazi kuwa tangu zamani Mungu aliwapa watu wake ushindi kupitia jina lake maadui wa watu wa Mungu waliweza kukatiliwa mbali, na kwa sababu weng walifahamu uwea unaotenda kazi ndani ya Yesu Kristo walishawishika kulitumia jina lake kwa ajili ya kufukuza Pepo Matendo 19;13
Jina Muharabu (Muharibu) “destroyer one” anayetajwa katika 1Koritho 10;10 huwa haimaanishi kuwa ni shetani au pepo lakini ni wazi kuwa ni malaika wa Bwana aliyepita jioni ile kuwahukumu Wamisri alihusika katika kuhukumu waovu au waasi 2Samuel 24;16,  pia yuko malaika ambaye ni mfalme  aliitwa pia malaika wa kuzimu kwa kiebrania Abadoni na kwa kiyunani Apolioni Ufunuo 9;11 huyu naye inaonekana kuwa ni shetani.
Makala na 
Rev. Innocent Kamote Mkuu wa Wajenzi Mwenye Hekima
ikamote@yahoo.com
+255718990796
+255784394550

Maoni 8 :

Unknown alisema ...

Mafundisho mazuri

Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima alisema ...

asante sana Charles Bieda Mungu akubariki kwa kufaidika na Mafundisho hayo

Unknown alisema ...

Mafundisho yako ni mazuri, Asante Kuna vitu vingi nimejifunza.

Isipokuwa waislamu wanapotoa salamu baada ya sala, ni wanamsalimia Malaika wa ulinzi aliyeko kushoto na aliyeko kulia. Sio kweli kuwa kulia wanasalimia muislam mwezao na kushoto wanalima majini. Waislamu wanaamini Kuna Malaika wa ulinzi aliyeko kulia ambae kazi yake ni kuandika mema yake, na yule Malaika wa kushoto kazi yake ni kuandika maovu yake. Inaweza fanana na Malaika aliyetajwa zaburi ya 91:11 ambae anakuwa na sisi kila mahali.

Otherwise nimependa mafundisho yako

Unknown alisema ...

Asante kwa mafundisho.mazuri, nimejifunza sana

Unknown alisema ...

Good!

Unknown alisema ...

Mafundisho mazuri sana ubarikiwe

Unknown alisema ...

Mafundishi mazuri

Bila jina alisema ...

Haya mafundisho yameshiba barikiwa sana mtumishi wa Mungu.