Jumatatu, 27 Oktoba 2014

Maana Ya Namba 40.

Ndugu msomaji wangu Hivi karibuni nimepokea Maswali kadhaa kutoka kwa watu mbalimbali wakiuliza swali kuhusu 40 Arobaini, watu walioniuliza swali hini ni wengi kiasi ambacho kilinisukuma kujua kuwa inatupasa kulifahamu swala hili kwa kina kwa kujaribu kulikumbuka swali lilikuwa katika mtindo huu hapo

Swali lenyewe lilikuwa namna hii

“Kwa nini arobaini?
Mtoto akizaliwa akilazwa anatolewa nje baada ya siku 40, mtu akifa siku ya arobaini anafanyiwa ibada, waswahili wana usemi za mwizi 40, Waisrael walikaa nyikani kwa muda wa miaka 40, Yesu alifunga siku 40, pasaka huadhimishwa baada ya siku 40 za mfungo,Kipindi cha Nuhu mvua ilivyesha kwa siku 40 je Hii arobaini ina maana gani naomba nisaidie”

Maana ya namba 40.

Ni muhimu kufahamu kuwa kwanza nilipoulizwa swali hili sikufanya Haraka kutaka kutoa majibu ya papo kwa papo kwani sikutaka kutoa majibu nisiyoyafanyia utafiti, Ilinigharimu Muda kwani binafsi sikuwahi kujiuliza swali kama hilo na ingawa mimi ni muhubiri sikuwahi na sipendi sana kuhubiri kuhusu Namba au vitu ambavyo vinaweza kuwachanganya akili waamini wetu hata hivyo swali hili limenipa uzoefu mkubwa ambao sasa naweza kushirikiana na kila mtu mwenye mapenzi mema anayependa kujifunza.
Namba 40 Katika Biblia ni alama yenye kumaanisha kipindi cha wakati mgumu! Wakati wa maumivu, kukata tama ya maisha, masumbufu na changamoto mbalimbali tunazokutana nazo tunapoishi ulimwenguni, Wakati wa Nabii Nuhu mvua ilinyesha kwa siku “40” haukuwa wakati mwepesi ulikuwa wakati wa Misiba mikubwa kwani Ingawa Nuhu alikuwa ameokolewa na familia yake tu lakini ni ukweli uliowazi kuwa alikuwa na huzuni kubwa kufiwa na majirani zake ndugu na jamaa ambao huenda hawakutaka kusikiliza maonyo hivyo kimsingi ulikuwa wakati wa majaribu, Wana wa Israel nao walipita katika jangwa refu kubwa lenye kutisha na kukatisha tama kwani kadiri walivyokuwa wakisonga mbele matumaini ya uhai yalikuwa yakipotea kabisa, ulikuwa ni wakati mgumu kiasi ambacho hata uhuru wa kutoka Misri ulionekana kana kwamba hauna maana waliteseka na kupoteza matumaini jangwa hili refu kutoka Misri hata kufika Israel liliwagharibu safari ya mapito ya miaka “40”,Naye Masihi Mkuu Yesu Kristo wa Nazareth kabla ya kuanza kuwahudumia watu aliongozwa na Roho wa Mungu kuelekea nyikani ili kujaribiwa akiwa amefunga kwa siku “40” hata baada ya Pasaka kuna sikukuu iitwayo Pentekoste huazimishwa siku 40 tangu pasaka wayahudi huadhimisha sikukuu hiyo kwa kukaa katika vibada wakikumbuka jinsi wazee wao walivyoteseka jangwani kwa miaka 40, Naye Yesu alipaa mbinguni baada ya kuwa amewatokea wanafunzi wake kwa siku 40

Kwa ujumla namba 40 imekuwa sasa ikitumika kwa maeneo mbalimbali duniani na inakubalika kama namba maalumu na wakati wote huo ikimaanisha kipindi Fulani kigumu cha kupitia majaribu hata kama kipindi hicho sio lazima kihesabike kama siku 40 lakini ni kipindi Fulani cha mapito na changamoto wakati mwingine kisichohesabika au kinachohesabu kabisa siku 40 zenyewe.
Namba 40 ni uzao wa namba 5 na 8 na mara nyingi hulenga kwenye tendo la kuhitaji Neema na kuelekea kwenye kufanywa upya, baada ya kutoka katika mapito namba nyingine ni 4 na 10 na ni dhahiri kabisa kuwa 4 na 8 zinawakilisha pande kuu za dunia.
Kibiblia Waisrael walipita kwenye Jangwa la kutisha na kukatisha tama kwa miaka 40 Kumbukumbu 8;2-5, Zaburi 95: 10 Matendo 13;18, 



Nabii Musa aliishi miaka 120 na Miaka 40 katika nyumba ya farao akiyafurahia maisha ya anasa na miaka 40 Jangwani huko Midiani akiishi katika taabu za dunia na miaka 40 akiishi kama Kiongozi wa Israel kuwapeleka Kanaani 40 mpaka alipofariki mlimani kabla ya kufika Kanaani.
Baada ya kusulubiwa Kwa masihi ilipita miaka 40 tu na mji wa Yerusalemu uliharibiwa hivyo namba 40 bado ni moja ya namba muhimu za kibiblia
40 pia humaanisha kipindi cha mafanikio na ukombozi au raha kupumzika mfano waamuzi walipowaokoa Waisrael kulipita wakati wa utulivu wa miaka 40- 40 hivi

Mfano

·         Chini ya Utawala wa Othiniel mwamuzi alitawala miaka 40 Waamuzi 3;11
·         Chini ya Utawala wa Baraka  mwamuzi alitawala miaka 40 Waamuzi 5;31
·         Chini ya Utawala wa Gideon mwamuzi alitawala miaka 40 Waamuzi 8;28
·         Wakati wa Tawala zenye mafanikio pia viongozi wengi walitawala kwa miaka 40

Mfano
  • Chini ya Utawala wa  Daudi, alitawala kwa miaka 40 2Samuel 5:4,
  • Chini ya Utawala wa  Suleman, 1Wafalme 11:42,
  • Chini ya Utawala wa  Yeroboam II.  2Wafalme 12:17,18, 13:3,5,7,22,25, 14:12-14,23,28,
  • Chini ya Utawala wa  Yehoash, 2Wafalme 12:1,
  • Chini ya utawala wa Yoash 2Nyakati 24:1.
Namba 40 Kibiblia pia ilimaanisha pia vipindi vya kunyenyekea na kuonelewa au kutokuwa na uhuru

·         Mifano ya kibiblia ni pamoja na
·         Wakati wa utawala wa wafilisti Isrel walionewa miaka 40 Waamuzi 13;1.
·         Wakati wa utawala wa Eli wafilisti waliwaonea sana Israel miaka 40 1Samuel; 4;18
·         Wakati wa utawala wa Sauli wafilisti waliendelea kuwasumbua Israel miaka 40 Matendo 13 :21.

Namba 40 pia humaanisha nyakati za kusubiri au subira

·         Musa alisubiri mpaka alipokuwa mtu mzima miaka 40 kuwaokoa watu wake Matendo 7;23
·         Pia alipaswa kusubiri wakati wa Mungu kwa miaka 40kuwaokoa watu wake Matendo 7;30

Katika Biblia kuna Maswala yapatayo nane “8” hivi yanayozungumzia umuhimu wa siku 40

1.       Siku 40 Musa alikuwa mlimani akipokea sheria ya Mungu kwa watu wake Kutoka 24;18
2.       Suku 40 Musa alikuwa mlimani akiwaombea watu wake baada ya kuwakuta wakiabudu sanamu ya ndama wa dhahabu Kumbu 9;18,25
3.       Wapelelezi walitumia siku 40 wakiwakilisha miaka 40 Hesabu 13;26,14;34.
4.       Kwa siku 40 Nabii Eliya alikuwa mlima Horeb 1Wafalme 19;8
5.       Kwa siku 40 mji wa Ninawi ulipaswa kutubu kwa mahubiri ya Yona kabla ya hukumu Yona 3;4
6.       Kwa siku 40 Ezekiel alilalia upande wa kulia akitabiri Miaka 40 ya taabu ya Yuda Ezekiel 4;6
7.       Kwa siku 40 Yesu alijaribiwa na Ibilisi akiwa amefunga Mathayo 4;2
8.       Kwa siku 40 baada ya kufufuka Yesu aliwatokea wanafunzi wake akizungumzia maswala ya Ufalme wa Mungu Matendo 1;2.

Kwa ujumla Namba 40 imetajwa katika Biblia mara 146 na mara zote hizo imeunganishwa na maswala ya  Majaribu, mapito na muda Fulani usiofahamika  wa kipindi cha mapito au mateso.

Ni jinsi gani namba 40 inahusiana na Majaribu na wakati mgumu?
·         Yesu alijaribiwa na Ibilisi siku 40 mchana na Usiku
·         Yesu aliwatokea wanafunzi wake kwa siku 40 baada ya kusulubiwa kufa na kufufuka
·         Baada ya miaka 40 tangu kusulubiwa kwa Yesu Yerusalem Uliharibiwa
·         Musa aliishi miaka 40 Misri, 40 Jangwani na 40 Jagwani akiongoza wana Israel
·         Musa alikaa mlimani siku 40 usiku na mchana akipokea sheria
·         Wapelelezi waliipaleleza kanaani kwa siku 40
·         Eliya alitumia siku 40 katika mlima Herob
·         Yona alihubiri kuhusu Hukumu ya Ninawi kuwa ni baada ya siku 40
·         Kulingana na tamaduni au masimulizi ya kale Adamu na Hawa baada ya kufanya dhambi walifunga na kujuta kwa siku 40 na hivyo kuna uwezekano swala la 40 lilianza zamani sana na baba yetu Adam.

Kwa msingi huo kumbe basi 40 humaanisha Subira, Uvumilivu, mapito, mateso mitihani, maombolezo, hukumu na furaha au kustarehe

·         Mtoto anapozaliwa kunakuwa na mchanganyiko wa Furaha na Huzuni na uvumilivu

a.       Mama anakuwa na muda wa kurejesha Afya yake baada ya uchungu mzito wa kujifungua, huangaliwa kwa ukaribu ili yeye na mtoto waweze kupata nguvu za kutosha kurejea katika hali ya kawaida, wakati Huu Mume au baba anapaswa kuwa katika wakati wa Subira hawezi kumgusa mama kwani afya haijatengemaa  kwahiyo mara baada ya mwanamke kujifungua mwanamume mwenye mke huyo hupaswa kuwa na subira na endapo atakosa subira wengi huharibikiwa na kutoka nje ya ndoa zao hivyo nyumba nzima huonja joto la 40

b.      Mtu anapofariki kwa kawaida watu huingia katika maombolezo na wakati wa huzuni huu pia ni wakati wa subira kutokana na kila mtu anapofariki huwa amefariki mtu nwa pekee na wa muhimu, maombolezo yanapaswa kuwa siku 40, hata hivyo watu wengi sana humaliza msiba ndani ya siku tatu, lakini siku 37 ni muhimu na zinahitaji subira na mwenedno wenye kuheshimu kuondokewa na mtu muhimu, ndani ya siku hizo chache kama utaonekana mwenye tabia za ajabu inaweza kuwa tafasiri mbaya katika uhusiano wako na kifo cha marehemu kwahiyo watu huhesabu 40 tangu kuzikwa au kufa kwa marehemu na huhitiomisha kwa Ibada za shukurani na hapo sasa familia inaweza kuanza kufurahi na kusahau yaliyotokea


c.       Za mwizi 40 “Ni usemi wenye kumaanisha kuna wakati wa Hukumu kwa matukio yoyote yasiyofaa kwa kuwa namba 40 inauhusiano na swala la hukumu “Ninawi baada ya siku 40 utaangamizwa!” hiyo ni hukumu mtu mwenye tabia ya wizi iko siku Mungu atamuhukumu kwa wizi huo Mungu ana namna yake anavyoweza kuhesabu na hatimaye kufichua au kuweka peupe maswala yote yafanyikayo kwa siri hapa duniani kwa hiyo za mwizi arobaini sio lazima uwe ni muda unaohesabika lakini ni siku moja ya hukumu kwa mwizhi au mtu mwenye tabia yoyote isiyofaa kimaadili.Mungu aliwahukumu wenye kumuasi kwa kuleta mvua wakati wa Nuhu mvua na chemichemi zilifunguka kuwahukumu watu waovu hii nayo ni 40 iko siku Mungu atahukumu uovu.

d.      Kufunga siku 40 kwa Yesu na Musa pia au Eliya ni alama ya Unyenyekevu na kumtafuta Mungu kwa neema na Rehema zake ni kukubali kujitesa ili kuruhusu huruma za Mungu kutujilia na ndio maana wakristo wa zamani pia walikuwa wakifunga siku 40 Kwaresma ili kuutafuta uso wa Mungu na kuwahudumia watu

 Ni matumaini yangu kuwa Utakuwa umafaidika na mda hii kwa maswali maoni au ushauri tafadhali acha mchangowako chini ya mada Hii na Mungu awabariki wenu mjoli wa Bwana

Kwa mawasiliano maoni au maswali:-

 Rev, Innocent Kamote. Mkuu wa Wajenzi Mwenye Hakima
0718990796
0784394550

Maoni 18 :

Unknown alisema ...

Nimelipokea neno katika wakati sahihi

Rommy Simfukwe alisema ...

That's great be blessed

rosekamanyile@yahoo.com alisema ...

Neno limenibariki mno. Asante sana Mtumishi wa Bwana Yesu. Barikiwa mtu wa Mungu

Unknown alisema ...

Asante nimejibiwa

Unknown alisema ...

Asante sana mtumishi wa MUNGU, hakika nimeelewa vema.

Unknown alisema ...

Nimebarikiwa kwa kujua maana ya namba 40

Unknown alisema ...

Nimebarikiwa kwa kujua maana ya namba 40

Unknown alisema ...

Kwanini Sikh za mwizi ni 40


Unknown alisema ...

🙏🙏🙏 ahsante kwa maarifa haya

Unknown alisema ...

Thank you so much

Unknown alisema ...

Ahsant kwa ufafanuz

Unknown alisema ...

Ahsante sana kwa maelezo hayo Mungu akuzidishie neema na baraka.Nimebarikiwa na naendelea kujifunza Mtumishi wa Bwana.

Unknown alisema ...

Mungu wa mbinguni akubariki nimepata somo

abuujsamwel@gmail.com alisema ...

Asante kwa majibu mazuri

danifordyaulimwengu@gmail.com Yaulimwengu alisema ...

Asante eeee

Bila jina alisema ...

Asante kwakufanya utafiti wa kina

Bila jina alisema ...

Asnte sana kwa uchambuzi makini kweli nimepata marefu na mapana ya siku 40. Mungu akibariki

Bila jina alisema ...

Naomba kufahamu namba therathini na tatu inawakilisha nini milnisaidie