Jumatatu, 27 Oktoba 2014

Jina La Bwana Mungu Wetu!

Kuwa na Ufahamu kuhusu jina La Bwana Mungu wetu na kisha namna ya kulitumia ni kwa muhimu sana hususani katika kizazi chetu, Jina la Bwana Mungu linafunua uweza Mamlaka na asili ya Mungu wetu (Mithali 18: 10). Nyakati za Agano la kale watu wachache sana walifahamu siri na matumizi ya jina la Mungu na hivyo waliweza kufanya mambo makubwa nay a kupita Kawaida, Hata hivyo jina hili la Bwana Mungu wetu Bahati mbaya sana lilifichwa kabisa kwa watu wa agano la Kale kwa vile Mungu hakupenda walitumie kwa nyakati zao. Mungu alilificha jina hilo kwa faida kubwa sana ya watu wa Nyakati za Agano Jipya.


Tuta jifunza somo hili kwa kuzingatia Vipengele vifuatavyo:-

·         Jina la Bwana wakati kabla ya sheria
 
·         Jina la Bwana wakati wa Nabii Musa
 
·         Jina la Bwana wakati wa Manabii

·         Jina la Bwana wakati wa Agano Jipya



Jina La Bwana wakati Kabla ya Sheria


Ni muhimu kufahamu kuwa nyakati za kale kabla ya sheria ya Musa Jina la Bwana Mungu wetu lilifichwa, ilikuwa ni siri kubwa sana ambayo haikuweza kufunuliwa kwa kila mtu, kuna ushahidi wa kimaandiko kuwa watu wachache sana huenda walilifahamu jina la Bwana Mungu wetu na kulitumia hata hivyo walilitumia mara chache tu wakati wa kuabudu Mwanzo 4:25-26, baadhi ya wataalamu wa Biblia hudai kuwa Mstari huu unazungumzia kuhusu kuabudu kwa wazi jambo ambalo halikuweko wakati wa Adamu Hata hivyo mimi nina mtazamo tofauti kuwa Uzao wa Seth hawakulipuuzia jina la Bwana Mungu bali ulikuwa ni uzao uliolitaja na kulitumia kwa wazi, ni imani yangu kuwa Adamu alilijua jina hilo na Seth pia na Uzao wake jina hili lilihifadhiwa hata katika kizazi cha Shem na huenda Ibrahimu alilijua na kulitumia katika Ibada Mwanzo 12:8 ni ushahidi ulio wazi kuwa Ibrahimu alilijua jina hilo. Jina hili hata hivyo lilikua siri kuubwa sana.


Kulijua jina la Mungu lilikuwa ni shauku kubwa sana nyakati za Biblia katika Agano la kale  inawezekana kuwa ni wazi kabisa watu walisikia kua liko jina la Mungu na kuwa ukilijua na ukalitumia lina uweza mkubwa sana lakini ilikuwa siri kuu kulijua jina hilo Yakobo alikuwa mtu wa kwanza kumbana Malaika ili aweze kumwambia jina hilo hata hivyo hakufanikiwa Mwanzo 32:22-30, Musa alikuwa miongoni mwa watu waliochunguza sana na kutaka kulijua jina hilo na mara alipokutana na Mungu hili lilikuwa swali lake kuu na la kwanza, kwa ujumla Musa alitumia ujanja sana kutaka Mungu amwambia jina lake Kutoka 3:13, kwa nini hawa walitaka kujua Jina la Mungu walijua nguvu ya jina hili siri na utajiri uliomo katika jina hili na walitambua kuwa jina hili lilikuwa ni siri mmo, Inaonekana kwa namna Fulani Mungu alimfunulia Musa Jina hilo lakini kwa vila jina hilo ni siri Musa alilificha sana ni wazi kuwa Mungu mara kadhaa alimfunulia Musa jina hilo nah ii inaonekana ni kwa sababu huenda Musa aliendelea kudadisi sana akitaka kulijua jina hilo


Ø  Kutoka 6:3

Ø  Kutoka 33: 19

Ø  Kutoka 34:5-6


Jina hili ni jina lenye utukufu mwingi na ni jina lenye kuogopwa sana, Waebrania walitambua jina hili kama jina takatifu sana na waliogopa kulitaja jina hilo hovyo kiasi cha kulifanya likapotea Kumbukumbu 28:58-61. Uko ushahidi ulio wazi katika agano la kale ya kuwa mashujaa wengi wa imani waliotenda mambo makubwa nay a kushangaza walilijua jina hilo na kulitukuza 2 Samuel 22: 50-51. Daudi alitabiri kuwa Mataifa yote yataleta utukufu kwaajili ya jina hilo na Kumuabudu Zaburi 86;9.


 Nyakati za agano la kale watu walikatazwa kulitumia jina hili hovyo au kulitaja pasipokuwa na sababu hii ikiwa ni pamoja na kutokuapa au kusema uongo au kuweka nadhiri kwa jina hilo na kutokuitimiza Kutoka 20:7

Haikuruhusiwa kulinajisi jina hili Walawi 18:21

Haikuruhusiwa kulikufuru jina hili Walawi 24:16

Jina hili linapaswa kutukuzwa Mathayo 6: 9

Kuna faida nyingi sana zinazoambatana na Matumizi ya jina hili Zaburi 20:1-7 Kwaajili ya jina hili ni vigumu sana Mtu kuachwa na Mungu kama analifahamu Mungu mwenyewe hawezi kukuacha kama unalijua jina lake 1 Samuel 12: 20 -22, Daudi aliweza kuiondoa aibu ya Isarael dhidi ya Goliath mfilisti kwaajili ya Jina hilo 1 Samuel 17: 45-47.

Pamoja na kujifunza mambo yote haya ya thamani kama mtu akilijua jina la Bwana Mungu swali kuu linabaki katikati yetu lipi ni jina Halisi la Bwana Mungu wetu? Yafuatayo ni majina kadhaa ambayo yanatumika au yametumiwa kumuelezea Bwana Mungu katika mafunuo ya aina mbalimbalinyakati za agano la kale Mungu alijifunua kwa Herufi nne tu YHWH (Yahweh), jina hili linasimama kumfunua Mungu kama Mwokozi, hata hivyo kifurushi cha wokovu kina marupurupu Mengi sana kwa msingi huo Mungu alijifunua kama mwokozi wa mazingira kadhaa ambayo kwa hayo watu walimuita Mungu jina hilo


1.      ELOHIM


Jina ELOHIM ni lenye asili ya Kiibrania ambalo hutafasiriwa Mungu anapojifunua kama Mungu Muumba Creator God na kwa asili ni jila lenye uwingi hivyo lina uhusiano na Utatu wa Mungu jina hili limetumika sana katika kitabu cha Mwanzo.



2.      YEHOVAH


Jina hili Yehova pia lina asili ya kibrania na lilitokana na jina ambalo Mungu alijifunua kwa Musa kwa Herufi kuu nne tu za Kiibrania cha zamani YHWH ambalo hutafasiriwa kama BWANA Hata hivyo jina YHWH linasimama kutokana na shughuli za wokovu jina hili lilibadilika kutokana na kukua kwa Lugha kwani wazee waliotafasiri Biblia toka katika kiebrania kuja katika kiyunani waliweka Herufi za silabu zilizopelekea jina hilo kusomeka YEHOVAH jina hili hata hivyo sio ufunuo kamili wa jina la Mungu kwani haliwezi kusimama pekee hivyo liliunganishwa na sehemu ya wokovu aliotoa Bwana kwa wakati na kwa watu maalumu mfano


*      YEHOVAH – RAPHA – Kutoka 15: 26 Mungu Mponyaji

*      YEHOVAH – NISSI- Kutoka 17:8-15 Mungu Bendera yetu

*      YEHOVAH – SHALOM – Waamuzi 6:24 Mungu amani yetu

*      YEHOVAH – RA’AH- Zaburi 23:1 Bwana Ndiye Mchungaji wangu

*      YEHOVAH – TSDIKENU – Yeremia 23:6 Mungu ndiye haki yetu

*      YEHOVAH – JIREH – Mwanzo 22:14 Mungu atatupatia

*      JEHOVAH – SHAMMAH – Ezekiel 48:35. Mungu yupo

3.      EL


Jina hilo la Mungu El lilikuwa na maana hiyo tu ya Mungu iliyotumika pia nyakati za agano la kale ni jina ambalo pia halikuwa na utoshelevu kwa vile kama Yehova halikuweza kutumika peke yake, jina hilo lilitumika pia kwa kuunganisha El na neon linmgine mfano

*      El – Elyon – ikiwa na maana ya MUNGU aliye juu sana Mwanzo 14:18 – 20

*      El – Shaddai- ikiwa na maana Mungu mwenye kutosheleza Kutoka 6:3

*      El – Olam – ikiwa na maana ya Mungu wa Milele Mwanzo 21:33



4.      ADONAI


Mungu pia alijifunua kwa jina la Adonai wakati wa agano la kale jina hili kwa asili ya nkiibrania ni BWANA au MWALIMU au mmiliki wa mashamba makubwa au mwenye serikali au utawala au mwenye serikali linatumika kuzungumzia ubwana wa Mungu Sovereign Kutoka 23:17

Hata hivyo siri kuhusu jina hili bado ilikuwa imefichwa



Jina la Bwana wakati wa Manabii


Bado kwa Muda mrefu watu walikua na kiu ya kutaka kulijua jina la Mungu iliaminika kabisa kuwa kulijua jina la Mungu kungeweza kutatua kabisa mateso na matatizo yaliyoweza kuisumbua jamii walitambua kuwa kulifahamu jina la Mungu sio tu kungeleta ulinzi na usalama kwao lakini pia kungesababisha kuwashinda adui zao Isaya 7:14 Ishara ya ushindi dhidi ya adui ilitolewa kuwa ni kuzaliwa kwa motto wa kiume ambaye angekuwa anaashiria kuwa Mungu yuko pamoja na wanadamu ni wazi kuwa nabii Isaya alionya kwa wazi kuwa Masihi angezaliwa na kuwa yeye anabeba majina yote ya Mungu lakini angezaliwa kama aina binadamu na kuishi nasi na kututambulisha jina hivyo majina yote ya Mungu sasa yangeweza kupatikana kwa jina moja tu ndani ya Mtoto tutakayepewa sisi wanadamu angalia Isaya 9:6-7

Isaya 9:6-7 ni kifurushi kamili cha wokovu ambacho Isaya anakiona lakini anashindwa kupata wazi kabisa jina la Mungu ingawa anayaona yote ni wazi kuwa ukiichunguza mistari hii utaona Mungu anatajwa kama 


Mungu mwenye nguvu – El shaddai

Mungu wa Milele – El Olam

Mfalme wa Amani – Jehovah Shalom

Uweza wa kifalmeUtawala na Nguvu  – Adonai

Utawala wa haki – Tsdekenu

Kuustawisha - Yire

Kuusimamisha – Rapha

Bwana – aliyeko aliyekuwako na atakayekuwako Niko ambaye niko


Isaya ni kama anaonyesha ya kuwa Mungu ambaye amejifunua kwa namna nyingi na kwa majina mengi akiokoa katika mazingira mbalimbali atakwenda kujidhihirisha katika namna moja au kwa jina moja litakalokuwa na utoshelevu kwa wanadamu, Naye nabii Yoel anathibitisha kuwa wakati Fulani Mungu angeachilia Roho wake kwa watu wote wenye mwili katika wakati huo Mungu atafanya mambo makubwa na kuwa kila atakayeliitia jina la Bwana ataponywa Yoel 2:28-32,Mungu aliwaficha manabii kuhusu mambo haya kwa ajili ya nyakati zetu 1Petro 1: 10-12.





Jina la Bwana wakati wa Agano jipya


Agano jipya ni habari njema kwa watu wote duniani ni habari kuhusu maisha na mafundisho ya Bwana wetu Yesu ni wakati ambao Mungu alitimiza ahadi zake alizonena kwa vinywa vya manabii hii inadhihirika pale malaika alipoleta habari njema ya kuzaliwa kwa motto wa kiume, Malaika alikuja na jina maalumu yaani YESU jina hili linatimiza wazi unabii ya kuwa huyu ndiye Mungu pamoja nasi ni wazi kabisa kuwa jina hili linabeba wokovu wote wa mwanadamu unaohusu kusamehewa Dambi na mahitaji mengine Mathayo 1:20-23. Ni wazi kuwa Jina hili ni jina la Mungu na yesu mwenyewe aliweka wazi kuhusu hilo Yohana 17:11-12, jina Hili Yesu ni jina lenye asili ya kiyunani lakini likitokana na asili ya kiibrania “Ye-ho-shua” au “Yesa” Kwa kiyunani Ieosus au Jesus kwa Kiingereza jina hili lina maana ya  Mungu mwokozi au Mkombozi ni wazi kabisa jina hili kwa kiibrania ndio Yoshua ni wazi kabisa kuwa Musa alilijua jina hilo na kusudi lisisahahulike aliliweka kwa mtumishi wake mwenyewe aliyeitwa HOSHEA Musa aliliweka jina hili kwa Mtumishi wake muaminifu ambaye pia angekuja kuwa mrithi wake na nabii ajaye baada yake Hesabu 13:16  jina Hoshea lilikuwa na maana ya wokovu lakini jina Yoshua lina maana ya WOKOVU WA MUNGU jina hili ndilo jina la YESU ni jina ambalo limeinuliwa juu kuliko majina yote Paulo mtume analiona wazi katika ulimwengu wa kiroho na ufunuo aliopewa kuwa hili sasa ndio jina la Mungu wetu Wafilipi 2:9-11 Jina hili linaashiria kuwa Mamlaka na cheo cha Yesu Kristo kipo juu zaidi.



·         Kila atakayeliitia jina hili ataokoka Matendo 2:21, Warumi 10:13.

·         Hakuna jina lingine tulilopewa litupasalo sisi kuokolewa kwalo isipokuwa jina hili Matendo 4:10-12

·         Jina hili liko juu kuliko majina ya malaika wote Waebrania 1:4.

·         Ukiomba lolote kwa jina hili utapata Yohana 16:23-24.Yohana 14:13-14

·         Asiyeliamini jina hilo atahukumiwa na kuukosa Uzima wa milele Yohana 3:16-18


Jina la Yesu lilipoanza kutumika lilileta athari kubwa sana nyakati za Karne ya kwanza na kuufanya ulimwengu wa wakati huo kutaharuki, viongozi wa dini za kiyahudi waliwaonya sana mitume kuacha kulitumia jina hilo mara moja kwani lilikuwa limeleta mapinduzi makubwa na kuathiri dini zao Matendo 4:5-20, 5:17-33, kumbe ukitaka kuuudhi ulimwengu wa kidini na upinzani wa kiibilisi tumia jina la Yesu, Fundisha kuhusu Yesu hubiri kuhusu Yesu. Matendo 8:4-13,

Rev. Innocent Kamote Mkuu wa wajenzi mwenye Hekima 
ikamote@yahoo.com
0718990796
0784394550

Hakuna maoni: