Jumanne, 28 Oktoba 2014

Akajifanya Ana Magari Yamekodiwa Na Lowasa!


Nilikaa mahali pale kwa muda mrefu sana nikimsubiri, Hatimaye alitokea, Alikuwa amevaa suti nzuri sana na alikuja na gari aina ya Corrola.Nilimsogelea na kumsalimia aliitikia na kuniambia nipande garini huyu alikuwa ni rafiki yangu mpya wa kiume, Kwa kweli ndio nilikuwa nimemaliza kidato cha sita  na nilikuwa kwenye maisha yangu, Huyu nilimkubalia kwa sababu nilihisi nampenda, siku hiyo ndiyo ilikuwa outing yetu ya kwanza  tangu tukutane naye nayeye kunitaka. 

Niliingia kwenye gari na kabla sijasema lolote alisema samahani tunatumia  haka kagari ambako najua sio ka hadhi yako, kwani gari zangu mbili ziko katika kazi maalumu, zimeazimwa na ofisi ya waziri mkuu, hjaka ndiko kagari kangu ka awali kukanunua huwa anakatumia mdogo wangu kwendea chuoni, nilisema mbona ni gari zuri tu, tena  linaonekana jipya , alicheka  kama vile nilikuwa nimezungumza lugha kutoka kwenye sayari nyingine “hapana hili ni gari wanalotumia watu ambaokidogo bado wako kwenye kujifunza kutafuta vijisenti vya kula, nilicheka kwa kujilazimisha  kwani nilijisikia vibaya  sana.

Tulikwenda hadi kwenye klabu moja maarufu kando ya bahari ya Hindi hapo tuliingia na kuamua kula na kunywa, mwenzangu aliagiza pombe na mimi juisi kwa sababu sinywi pombe, Hapo alianza kunielezea jinsi ambavyo ana malengo yake , Muda wote alikuwa anaongea yeye tu tena kwa kujisifu sana.Kwenye saa mbili hivi usiku waliingia watu watatu pale ukumbini na kuja moja kwa moja  pale tulipokuwa tumekaa, walipofika mmoja ambaye alionekana kuwa Baunsa  alisema ulidhani hutapatikana eh! Leo utakunaya hela yetu kutokea mdomoni au kokote ndio maana tulikataa kufanya kazi na mtu wa kula kulala…’

Yule jamaa yangu alikuwa ameshaanza kulewa, hivyo alipandisha na kusema hajui watu wale wanachokisema , ilibidi kuzuke vurugu, watu wale watatui walimshika jamaa yangu pamoja na mimi  na kutupakia ndani ya gari tuliyokuwa nayo, wewe ni mjinga sana  tunakupa gari  unasema una mteja kumbe unakuja kutanulia leo utatuambia udongo unaitwa nini kwa kizaramo mmoja wao alisema halafu aliongeza umepewa helka na …(Alimtaja mtu) unadai umetufikishia  kumbe ndio hizo unakwenda kutanulia na mademu zako..’Yule jamaa yangu alikuwa amenyamaza. Yule jamaa aliniambia anaishi sinza  lakini tulielekea Tandale na kufika kwenye nyumba moja gari, lilisimamishwa  na wale jamaa wakamshusha kwa nguvu, jamaa yangu na mimi  pamoja waliingia  kwenye ile nyumba  ‘fungua  tujue nini kimebeki tusipoteze kila kitu’ jamaa yangu alifungua mlango unajua nini nkilikuwa ni chumba chake.


 Haki ya Mungu huwezi kuamini kulikuwa na kitanda cha futi nne, stuli nne, ndoo ya maji na redio kubwa (music system). Hakuwa na kitu kingine, wale wenzake walianza kupekua chumba na kuchukua hela zilizokuwa kwenye godoro chini halafu walimuomba funguo za gari aliwapa.
Mmooja wao alisema  hatuna haja ya kufanya dili na mtu wa dizaini yako.Sister kama unadhani umepata hapo jua kuwa utalia kilio cha mbwa, Nilishangaa kwamba jamaa yangu hakuweza hata kujitetea , wakati huu sikusikia tena habari ya magari yake mawili yaliyokuwa yamekodiwa kwa Ofisi ya waziri mkuu wakati ule Lowasa, kwa kweli sikumuaga niliondoka kimya kimya,huku umati wa watu ukiwa una tukodolea mimacho nashukuru Mungu kuwa ilikuwa usiku kama ningelikuwa sijaolewa hadi sasa niliapa nikimwona mwanaume mwenye kujipa misifa  na kujivuna hata kama angekuwa vipi  na ningemtemea mate. Nikakumbuka ule usemi wa Masiha kuwa kweli ajikwezaye atashushwa!

Rev. Innocent Kamote.
Mkuu wa wajenzi Mwenye Hekima
0718990796
0784394550

Hakuna maoni: