1Timotheo 2:5-8 “Kwa sababu Mungu ni mmoja, na mpatanishi kati ya Mungu na
wanadamu ni mmoja, Mwanadamu Kristo Yesu; ambaye alijitoa mwenyewe kuwa
ukombozi kwa ajili ya wote, utakaoshuhudiwa kwa majira yake. Nami kwa ajili ya
huo naliwekwa niwe mhubiri na mtume, (nasema kweli, sisemi uongo), mwalimu wa
Mataifa katika imani na kweli. Basi, nataka wanaume wasalishe kila mahali, huku
wakiinua mikono iliyotakata pasipo hasira wala majadiliano.”
Utangulizi:
Ni
muhimu kufahamu kuwa wanaume ni mojawapo ya nguzo muhimu sana katika jamii na
katika Kanisa pia, Kanisa lolote ambalo lina afya ya kiroho kamwe haliwezi
kupuuzia ujenzi wa wanaume kama wanafunzi wa Yesu ambao wanawajibika kwa
kiwango kikubwa katika usimamizi wa jamii, familia na Kanisa, Kanisa linapoweka
mkakati kuwaelimisha vizuri wanaume ni dhahiri litapata nguzo muhimu za kiroho
zenye nguvu, ushawishi na mamlaka ya kuibadili jamii na kuileta kwa Kristo.
Marko 3:13-19 “Akapanda mlimani, akawaita aliowataka mwenyewe;
wakamwendea. Akaweka watu kumi na
wawili, wapate kuwa pamoja naye, na kwamba awatume kuhubiri, tena wawe na amri
ya kutoa pepo. Akawaweka wale Thenashara; na Simoni akampa jina la Petro; na
Yakobo, mwana wa Zebedayo, na Yohana nduguye Yakobo, akawapa jina la Boanerge,
maana yake, wana wa ngurumo; na Andrea, na Filipo, na Bartholomayo, na Mathayo,
na Tomaso, na Yakobo wa Alfayo, na Thadayo, na Simoni Mkananayo, na Yuda
Iskariote, ndiye aliyemsaliti. Kisha akaingia nyumbani.”
Kutokana
na umuhimu wa wanaume Yesu kwanza aliwaita wanaume 12 ili wawe pamoja naye na wawe wanafunzi wake wa msingi, kwa kusudi
la kuwafundisha ili kisha waweze kubeba jukumu la kuweka msingi wa kanisa kwa
kujenga utamaduni mpya jamii mpya na taifa jipya yaani Kanisa la Mungu ambao ni
kama Israel ya Kiroho, Yesu alitamani wajifunze maisha yake ya kila siku, tabia
zake na mafundisho yake, kisha wasambaze ujumbe wake wa ufalme wa Mungu, huku
wakiwa na mamlaka ya kuponya wagonjwa na kutoa pepo, Yesu hakupuuza wanawake
lakini alionyesha wazi kuwa wanaume wana umuhimu mkubwa zaidi katika maongozi
ya Kanisa kama ilivyokuwa wana wa Israel 12 ambao walikuwa kabila 12 za Israel
ambazo zilikuwa chanzo cha taifa la Israel, kwa sababu hiyo Yesu hata leo bado anawategemea
sana wanaume katika kazi yake. Kwa msingi huo leo tutachukua muda kujifunza
somo hili muhimu Nafasi ya Mwanaume katika huduma kwa kuzingatia vipengele
muhimu vikuu vitatu vifuatavyo:-
·
Umuhimu
wa mwanaume kwa mujibu wa maandiko
·
Wajibu
wa mwanaume kwa mujibu wa maandiko
·
Nafsi
ya Mwanaume katika huduma
Umuhimu wa mwanaume
kwa mujibu wa maandiko.
Ni
muhimu kufahamu kuwa mwanaume ana wajibu mkubwa na wa kwanza kabisa katika
jamii duniani kama ilivyo vile vile katika Kanisa mwanaume amaeaminiwa uwakili
na Mungu, Mwanaume ni mfadhili, mwamaume ni mlinzi, mwanaume ni mpiganaji,
mwanaume ni kiongozi, wakati Mungu anaiumba dunia katika mpango wake mwanaume
alipewa kipaumbele kama kiumbe wa kwanza anayeweza kuendeleza na kutunza
uumbaji wa Mungu duniani, kule kuumbwa kwanza kulimfanya awe kiongozi wa asili
Mwanzo 2:15-17 “BWANA Mungu akamtwaa huyo mtu, akamweka katika bustani ya
Edeni, ailime na kuitunza. BWANA Mungu akamwagiza huyo mtu, akisema, Matunda ya
kila mti wa bustani waweza kula, walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na
mabaya usile, kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika.”
1Timotheo 2:11-15
“Mwanamke na ajifunze katika utulivu, akitii kwa
kila namna.Simpi mwanamke ruhusa ya kufundisha, wala kumtawala mwanamume, bali
awe katika utulivu.Kwa maana Adamu ndiye aliyeumbwa kwanza, na Hawa baadaye.
Wala Adamu hakudanganywa, ila mwanamke alidanganywa kabisa akaingia katika hali
ya kukosa.Walakini ataokolewa kwa uzazi wake, kama wakidumu katika imani na
upendo na utakaso, pamoja na moyo wa kiasi.”
Maandiko
yanaonyesha kuwa mwanaume ni nguzo muhimu sana katika jamii na imani na kuwa anamchango mkubwa sana katika
maswala ya ujenzi wa jamii kuanzia na maswala ya kiroho, uongiozi wa familia,
ujenzi wa jamii, uchumi, kufanya kazi, na kuwafundisha wengine, Jamii yoyote
yenye afya ya kijamii ni ile ambayo wanaume wako mstari wa mbele katika kila
jambo, kwa hiyo wanaume wakitangulia huku wakisaidiwa na wanawake wanauwezo
mkubwa sana ya kuifanya jamii hiyo kuwa na nguvu likiwepo Kanisa, Kwa bahati
mbaya tuko katika nyakati ambazo sasa ambao uanaume unapigwa vita sana au
wanaume wanaacha wajibu wao na kuanza kutaka vya dezo, kufanyiwa na kuandalia
kila kitu jambo ambalo litatujengea jamii ya ajabu sana na Kanisa la ajabu pia,
Mungu alimchagua mwanaume mmoja jina lake Abrahamu kwa sababu alimjua kuwa
mwanaume huyu atakuwa mjenzi wa jamii yake hata baada yake akiwafundisha watoto
wake baada yake washike hukumu za Mungu na kutenda haki
Mwanzo 15:17-19 “BWANA akanena, Je! Nimfiche Ibrahimu jambo nilifanyalo,
akiwa Ibrahimu atakuwa taifa kuu, hodari, na katika yeye mataifa yote ya dunia
watabarikiwa? Kwa maana nimemjua ya kwamba atawaamuru wanawe, na nyumba yake
baada yake waishike njia ya BWANA, wafanye haki na hukumu, ili kwamba BWANA
naye akamtimizie Ibrahimu ahadi zake.”
Maandiko
yanaonyesha kuwa wanaume wana umuhimu mkubwa sana katika ujenzi wa jamii
inayomcha Mungu, jamii inayofanyakazi, jamii yenye ugunduzi, jamii yenye
maendeleo, yenye utulivu na mwelekeo mkubwa wa maendeleo ya kiroho, kimwili, kisayansi
na kisaikolojia, bila kujali sera kubwa za sasa zinazokazania usawa wa kijinsia
na utambuzi wa wanawake katika jamii, lakini hii haiondoi ukweli wa neno la
Mungu kuwa wanaume wana mchango wakipekee kuanzia katika usimamizi wa kifamilia mapaka katika maswala ya ibada, uchumi na
ugunduzi wa teknolojia. Wanaume bado wanabaki kuwa ndio washikadau wakubwa wa
mwelekeo wa ulimwengu na kwakweli Mungu anawategemea sana wanaume na anataka
wawe mstari wa mbele kila mahali
Kama
unadhani wanaume sio wa muhimu fanya utafiti mdogo tu waulizie wanawake ambao
wameishi kama “Single Mothers” kwa
muda flani utagundua tu kuwa wana changamoto kubwa zaidi na mateso makubwa ya
kihisia wakiteswa na upweke, kiburi, migandamizo na mateso ya kihisia wengi
wanalia na hata wakikutana na mambo magumu wanasema ninaonewa kwa sababu sina
Mume, Mungu alimuumba kila mwanadamu na upekee wake na kila mmoja anamtegemea
mwingine kwa hiyo haijalishi mwanamke atakuwa na mafanikio makubwa kiasi gani lakini utafiti unaonyesha kuwa bila mwanaume
mwanamke huyo hana ukamilifu. Mungu ameumba watoto wakue wakisikia sauti ya
baba na mama na wanapoikosa sauti mojawapo watakapokuwa watu wazima wataanza
kuuliza yuko wapi baba yangu? au wataonyesha athari zinazoashiria kukosekana
kwa malezi ya upande mmoja
Na
ndio maana leo neno la Mungu linawataka wanaume wasimame katika nafasi yao
kuanzia katika ibada mpaka katika majukumu mengine ya kijamii, kama hesabu za Agano
la kale zingekuwa zinafanya kazi hata leo, Kanisa letu unadhani lingekuwa na
washirika wangapi? Ninene kiwazimu kila
mchungaji asihesabu washirika wanawake, ahesabie wanaume tu kisha tuone!
Mathayo 14:19-21.
“Akawaagiza makutano waketi katika majani; akaitwaa
ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama juu mbinguni, akabariki,
akaimega ile mikate, akawapa wanafunzi, wanafunzi wakawapa makutano.Wakala wote
wakashiba; wakayaokota masazo ya vipande vya mikate, vikapu kumi na viwili,
vimejaa. NAO WALIOKULA WALIKUWA WANAUME WAPATA ELFU TANO, bila wanawake na
watoto.”
Muulize
jirani yako hapo Mtumishi hiyo miujiza unayoifanya unawafanyia wanaume wangapi?
Yesu alifanya miujiza mbele ya wanaume 5000
bila kuhesabu wanawake na watoto, Muulize tena miujiza yako inafanyika mbele ya
nani? muulize Kanisa lako wewe ulianza na kina nani? Tunasoma kuwa Kanisa la
Efeso lilianza na wanaume 12 tu na walipompokea Roho Mtakatifu kazi ya Mungu
ilienea na Kanisa lilikuwa kubwa sana, nadhani kama tungekuwa tunahesabia
wanaume tu kanisani basi utagundua kuwa bado makanisa mengi yanalazimika kuwa
na wajibu wa kuwafikia wanaume na tukiwa na wanaume wengi tuna washirika wengi
Matendo 19:1-7 “Ikawa, Apolo alipokuwa Korintho, Paulo, akiisha kupita
kati ya nchi za juu, akafika Efeso; akakutana na wanafunzi kadha wa kadha huko;
akawauliza, Je! Mlipokea Roho Mtakatifu mlipoamini? Wakamjibu, La, hata kusikia
kwamba kuna Roho Mtakatifu hatukusikia. Akawauliza, Basi mlibatizwa kwa ubatizo
gani? Wakasema, Kwa ubatizo wa Yohana.Paulo akasema, Yohana alibatiza kwa
ubatizo wa toba, akiwaambia watu wamwamini yeye atakayekuja nyuma yake, yaani,
Yesu. Waliposikia haya wakabatizwa kwa jina la Bwana Yesu.Na Paulo, alipokwisha
kuweka mikono yake juu yao, Roho Mtakatifu akaja juu yao; wakaanza kunena kwa
lugha, na kutabiri.Na jumla yao walipata wanaume kumi na wawili.”
Paulo
mtume anamwambia Timotheo nataka wanaume wasimame kila mahali, hili lilikuwa ni
agizo la Mungu kwa Kanisa hata leo, Mungu anawataka wanaume, katika mikakati
yetu ya kuihubiri injili ni muhimu kwetu tukae tujadili na kutafakari kwamba
tunajali ni kwa namna gani tutawapata wanaume? wanaume wakipataikana na wakawa
wanasali na kuinua mikono iliyotakata jamii nzima itabadilika, Shetani
amewachukua wanaume kwenye mpira wa soka, amewachukua baa na kanisani
anatuachia wanawake na kanisa tumekaa na kutumbua macho, mwambie jirani yako
nataka wanaume hapa, Basi nataka wanaume wasalishe kila mahali!
1Timotheo 2:8 “Basi, nataka wanaume wasalishe kila mahali, huku wakiinua
mikono iliyotakata pasipo hasira wala majadiliano.”
Wajibu wa
mwanaume kwa mujibu wa maandiko.
Kufanya kazi kwa
mikono yake mwenyewe
– Moja ya wajibu aliopewa mwanaume hapa duniani ni kufanya kazi, Kazi ina
Baraka nyingi sana hata kama mtu hajaokoka akifanya kazi kazi huleta matokeo
makubwa, Nchi nyingi zenye mafanikio na maendeleo makubwa ni nchi za watu
wanaofanya kazi na sio wale wanaopiga soga, Kazi ilikuwa ni wajibu wa kwanza
aliopewa mwanadamu hata kabla ya kuagizwa kuabudu, Mungu aliagiza wanadamu wafanye
kazi, Mungu mwenyewe aliumba dunia kwa kufanya kazi siku sita, kwa hiyo ni
lazima tufanye kazi, maandiko yanaagiza kila mwanaume kufanya kazi, kazi ni
wajibu ni ibada.
Mwanzo 2:15-17 “BWANA Mungu akamtwaa huyo mtu, akamweka katika bustani ya
Edeni, ailime na kuitunza. BWANA Mungu akamwagiza huyo mtu, akisema, Matunda ya
kila mti wa bustani waweza kula, walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na
mabaya usile, kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika.”
2Wathesalonike
3:6-10 “Ndugu, twawaagiza katika jina la Bwana Yesu
Kristo, jitengeni nafsi zenu na kila ndugu aendaye bila utaratibu, wala si kwa
kufuata mapokeo mliyoyapokea kwetu. Mwajua wenyewe jinsi iwapasavyo kutufuata;
kwa sababu hatukuenda bila utaratibu kwenu; wala hatukula chakula kwa mtu ye
yote bure; bali kwa taabu na masumbufu, usiku na mchana tulitenda kazi, ili
tusimlemee mtu wa kwenu awaye yote. Si kwamba hatuna amri, lakini makusudi
tufanye nafsi zetu kuwa kielelezo kwenu, mtufuate. Kwa kuwa hata wakati ule
tulipokuwapo kwenu tuliwaagiza neno hili, kwamba ikiwa mtu hataki kufanya kazi,
basi, asile chakula.”
Mwanaume anapaswa
kuwa na Ushujaa,
- Maisha ya duniani ni kama mapambano na njia mojawapo ya kufanikiwa ni pamoja
na kuwa na ushujaa, kujiamini kuwa mbali na woga na hofu, kila mwanaume
anapaswa kumcha Mungu na kumtegemea Mungu lakini kujiamini na kujipa ujasiri,
hakuna mafanikio kama hutakuwa na ujasiri, odoa aibu jipe ujasiri pambania
hatima ya jamii yako
Yoshua 1:7-9 “Uwe hodari tu na ushujaa mwingi, uangalie kutenda
sawasawa na sheria yote aliyokuamuru Musa mtumishi wangu; usiiache, kwenda
mkono wa kuume, au wa kushoto, upate kufanikiwa sana kila uendako. Kitabu hiki
cha torati kisiondoke kinywani mwako, bali yatafakari maneno yake mchana na
usiku, upate kuangalia kutenda sawasawa na maneno yote yaliyoandikwa humo;
maana ndipo utakapoifanikisha njia yako, kisha ndipo utakapositawi sana. Je! Si
mimi niliyekuamuru? Uwe hodari na moyo wa ushujaa; usiogope wala usifadhaike;
kwa kuwa Bwana, Mungu wako, yu pamoja nawe kila uendako.”
1Wafalme 2:1-4 “Basi siku ya kufa kwake Daudi ikakaribia, akamwusia
Sulemani mwanawe, akasema, Mimi naenda njia ya ulimwengu wote; basi uwe hodari,
ujionyeshe kuwa mwanamume; uyashike mausia ya Bwana, Mungu wako, uende katika
njia zake, uzishike sheria zake, na amri zake, na hukumu zake, na shuhuda zake,
sawasawa na ilivyoandikwa katika torati ya Musa, upate kufanikiwa katika kila
ufanyalo, na kila utazamako, ili Bwana afanye imara neno lake alilonena kwa
habari yangu, akisema, Ikiwa watoto wako wataiangalia njia yao, wakienda mbele
zangu kwa kweli, kwa moyo wao wote, na kwa roho yao yote, (akasema), hutakosa
mtu katika kiti cha enzi cha Israeli.”
1Wakorintho
16:13-14 “Kesheni, simameni imara katika Imani,
fanyeni kiume, mkawe hodari. Mambo yenu yote na yatendeke katika upendo.”
Wanaume wanaagizwa
kumpenda Mungu
– Kila mwanaume anawajibu wa kumpenda Mungu, Mwanaume aliwekwa duniani na Mungu
kabla ya wanawake na mambo mengine, Mungu alimchagua mwanaume kuwa mtumishi
wake, alikuwa amekusudia awe na uhusiano na yeye, furaha ya mwanaume mkamilifu
kamwe haiwezi kuwa kamili kama hana uhusiano mwema na Mungu, Maandiko yanaamuru
tumpende Bwana Mungu wetu kwa moyo, kwa akili na kwa nguvu na jirani zetu kama
nafsi zetu.
Mathayo 22:37-39
“Akamwambia, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako
wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote. Hii ndiyo amri iliyo kuu,
tena ni ya kwanza.Na ya pili yafanana nayo, nayo ni hii, Mpende jirani yako
kama nafsi yako.”
Wanaume waagiza
kuwa na familia – Mojawapo
ya wajibu muhumu wa kila mwanaume ni kuanzisha familia kwa hiyo mwanaume ni
kiongozi kipenzi wa mkewe, kila mwanaume anatakiwa kuanzisha na kusimamia
familia yenye mamlaka na familia imara akiwa msimamizi wa imani, tamaduni,
sheria na taratibu za kiungu katika familia hiyo, familia itakayostawisha na
mwanaume haiwezi kuwa imara kama mwanaume huyo atamweka Kristo pembeni, mamlaka
ya mwanaume inaweza kuwa kamili na ya amani kama itifaki ya kiungu itakaa sawa
katika familia hiyo na mwanaume anawajibika kuipenda familia yake na kuisimamia
na kuilinda na kuhakikisha kuwa anaipatia mahitaji yao, wale wanaoogopa
majukumu na wanaoogopa kuoa na kuwa na familia uanaume wao hauwezi kuwa uanaume
kamili, Mwanaume hapaswi kuogopa majukumu wala hapaswi kuyakimbia, wengi leo
wamekimbia familia
1Wakorintho 11:3
“Lakini nataka mjue ya kuwa kichwa cha kila
mwanamume ni Kristo, na kichwa cha mwanamke ni mwanamume, na kichwa cha Kristo
ni Mungu.”
Waefeso 5:25-29 “Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye
alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake;
ili makusudi alitakase na kulisafisha kwa maji katika neno; apate
kujiletea Kanisa tukufu, lisilo na ila wala kunyanzi wala lo lote kama hayo;
bali liwe takatifu lisilo na mawaa. Vivyo hivyo imewapasa waume nao kuwapenda
wake zao kama miili yao wenyewe. Ampendaye mkewe hujipenda mwenyewe. Maana
hakuna mtu anayeuchukia mwili wake po pote; bali huulisha na kuutunza, kama
Kristo naye anavyolitendea Kanisa.”
Wanaume
wanawajibika kutawala au kuongoza – Itifaki
ya kiutawala na kiuongozi katika familia inaonyesha kuwa mwanaume ndiye anatakiwa kuwa
Kichwa, neno kichwa ambalo kwenye
kiingereza limetajwa kama “the head” katika lugha ya Kiyunani
ni “Kephalē”
ambalo maana yake ni the brain literal na
Metaphorical ni Chief, Ruler,
Leader, Master, au a person of high status
au the source kwa hiyo kama
Kristo alivyo ndiye mkuu wa Kanisa na mume ndiye mkuu wa familia na mkuu wa mke
wake utaratibu huu ukikiukwa hata kama hamjafanya dhambi uwepo wa Mungu
unaondoka Mungu ni Mungu wa utaratibu na sio Mungu wa machafuko, kwa hiyo mume
anawajibu wa kuongoza na kutawala katika ndoa yake “be the head of your wife”
hili ni agizo:-
Mwanzo 3:16-19 “Akamwambia mwanamke, Hakika nitakuzidishia uchungu wako,
na kuzaa kwako; kwa utungu utazaa watoto; na tamaa yako itakuwa kwa mumeo, naye
atakutawala. Akamwambia Adamu, Kwa kuwa umeisikiliza sauti ya mke wako, ukala
matunda ya mti ambao nalikuagiza, nikisema, Usiyale; ardhi imelaaniwa kwa ajili
yako; kwa uchungu utakula mazao yake siku zote za maisha yako; michongoma na
miiba itakuzalia, nawe utakula mboga za kondeni; kwa jasho la uso wako utakula
chakula, hata utakapoirudia ardhi, ambayo katika hiyo ulitwaliwa; kwa maana u
mavumbi wewe, nawe mavumbini utarudi.”
Waefeso 5:23-26 “Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni
kichwa cha Kanisa; naye ni mwokozi wa mwili. Lakini kama vile Kanisa limtiivyo
Kristo vivyo hivyo wake nao wawatii waume zao katika kila jambo.Enyi waume,
wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili
yake; ili makusudi alitakase na kulisafisha kwa maji katika neno;”
Wanaume
wanawajibu wa kusalisha – Kama
jinsi ambavyo wanaume wamepewa wajibu wa kuwa viongozi wa familia, Mungu
amewapa wajibu pia wa kusimamia shughuli za ibada kila mahali, Mungu anawapa
wajibu sio tu kusimamia ibada lakini kuwa kielelezo kikubwa cha imani katika
familia yake, Neno kusalisha katika Kiyunani ni “Proseuchomai” limetumika mara
90 katika agano jipya kwa kiingereza
“to supplicate worship”, au “to be a
person in authority to God during prayer” Paulo anawataka wanaume huko Efeso
wawe viongozi wa ibada kila mahali, waongoze maombi, waongoze ibada wasalishe
1Timotheo 2:5-8 “Kwa sababu Mungu ni mmoja, na mpatanishi kati ya Mungu na
wanadamu ni mmoja, Mwanadamu Kristo Yesu; ambaye alijitoa mwenyewe kuwa ukombozi
kwa ajili ya wote, utakaoshuhudiwa kwa majira yake. Nami kwa ajili ya huo
naliwekwa niwe mhubiri na mtume, (nasema kweli, sisemi uongo), mwalimu wa
Mataifa katika imani na kweli. Basi, nataka wanaume wasalishe kila mahali, huku
wakiinua mikono iliyotakata pasipo hasira wala majadiliano.”
Nafasi ya
Mwanaume katika huduma!
1Timotheo 2:5-8 “Kwa sababu Mungu ni mmoja, na mpatanishi kati ya Mungu na
wanadamu ni mmoja, Mwanadamu Kristo Yesu; ambaye alijitoa mwenyewe kuwa
ukombozi kwa ajili ya wote, utakaoshuhudiwa kwa majira yake. Nami kwa ajili ya
huo naliwekwa niwe mhubiri na mtume, (nasema kweli, sisemi uongo), mwalimu wa
Mataifa katika imani na kweli. Basi, nataka wanaume wasalishe kila mahali, huku
wakiinua mikono iliyotakata pasipo hasira wala majadiliano.”
Pauilo
mtume hataki wanaume wabweteke tu kanisani anatoa wito kwa kila kanisa kuwa
wanaume ndio wawe mstari wa mbele katika kila mkutaniko wa Kanisa la Mungu tena
sio waje tu mbele na kuongoza ibada kila mahali lakini pia wakiwa na mikono
safi, maana yake wakiwa na maisha matakatifu, wanaume wawe kielelezo, kuwa na
mikono iliyotakata maana yake ni wasio na hatia, walio safi kimaadili, Yesu
Kristo mwokozi wetu alikuwa mwanaume, ukombozi wetu umetoka kwa mwanaume kwa
hiyo kila mwanaume anatakiwa kuwa mstari wa mbele katika kumuunga mkono mwokozi
wetu na sio kukaa nyuma nyuma
Isaya 9:6-7 “Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto
mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa Jina Lake,
Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani. Maongeo
ya enzi yake na amani Hayatakuwa na mwisho kamwe, Katika kiti cha enzi cha
Daudi na ufalme wake; Kuuthibitisha na kuutegemeza Kwa hukumu na kwa haki,
Tangu sasa na hata milele. Wivu wa Bwana wa majeshi ndio utakaotenda hayo.”
Paulo
kwa kusema agizo lake lile alikuwa anamtaka Timotheo kuhakikisha anawekeza kwa
wanaume maswala ya kiroho yote kama mwanaume ndio kiongozi wa familia kumchukua
mke wake na watoto wake kuja ibadani kisha kumuacha yeye ni sawa na kuteka
ufalme wake, na utawala wake. Kanisa
lazima limlenge mwanaume hata kama mwanamke ataokoka kwanza lakini lazima zitafutwe
namna na baba afuate nyakati za kanisa la kwanza alikuwa akiokoka baba kwanza
na nyumba nzima inafuata, na sio hivyo tu Mwanaume akitangaza msimamo moja kwa
moja na familia nzima iliweza kuhusika kuliko mwanamke akitangaza.
Matendo 10:1-5 “Palikuwa na mtu Kaisaria, jina lake Kornelio, akida wa
kikosi kilichoitwa Kiitalia, mtu mtauwa, mchaji wa Mungu, yeye na nyumba yake
yote, naye alikuwa akiwapa watu sadaka nyingi, na kumwomba Mungu daima. Akaona
katika maono waziwazi, kama saa tisa ya mchana, malaika wa Mungu, akimjia na
kumwambia, Kornelio! Akamtazama sana, akaogopa akasema, Kuna nini, Bwana?
Akamwambia, Sala zako na sadaka zako zimefika juu na kuwa ukumbusho mbele za
Mungu. Sasa basi, peleka watu Yafa, ukamwite Simoni, aitwaye Petro.”
Matendo 16:27-32
“Yule mlinzi wa gereza akaamka, naye alipoona ya
kuwa milango ya gereza imefunguka, alifuta upanga, akataka kujiua, akidhani ya
kuwa wafungwa wamekimbia. Ila Paulo akapaza sauti yake kwa nguvu, akisema,
Usijidhuru, kwa maana sisi sote tupo hapa. Akataka taa ziletwe, akarukia ndani,
akitetemeka kwa hofu, akawaangukia Paulo na Sila; kisha akawaleta nje akasema,
Bwana zangu, yanipasa nifanye nini nipate kuokoka? Wakamwambia, Mwamini Bwana
Yesu, nawe utaokoka pamoja na nyumba yako.Wakamwambia neno la Bwana, yeye na
watu wote waliomo nyumbani mwake.”
Yoshua 24:14-16. “Basi sasa mcheni Bwana, mkamtumikie kwa unyofu wa moyo na
kwa kweli; na kuiweka mbali miungu ambayo baba zenu waliitumikia ng'ambo ya
Mto, na huko Misri; mkamtumikie yeye Bwana. Nanyi kama mkiona ni vibaya
kumtumikia Bwana, chagueni hivi leo mtakayemtumikia; kwamba ni miungu ile
ambayo baba zenu waliitumikia ng'ambo ya Mto, au kwamba ni miungu ya wale
Waamori ambao mnakaa katika nchi yao; lakini mimi na nyumba yangu tutamtumikia
Bwana. Hao watu wakajibu wakasema, Hasha! Tusimwache Bwana, ili kuitumikia
miungu mingine;”
Mungu
akianza na wanaume katika kuokoa ni ukweli ulio wazi kuwa wanawake watafuata tu
na watoto pia na migogoro mingi ya watu kuachwa kwaajili ya wokovu itakuwa
haiko, hivi ndio Mungu anavyotaka, wanaume wakiwa mstari wa mbele katika
mikesha kutakuwa na mafarakano nyumbani kweli? Mwanaume akitangaza msimamo
wengine watafuata tu Basi, nataka wanaume wasalishe kila mahali, Mungu
anatamani wanaume wawe kama Yoshua watangaze msimamo na familia zao zifuate
1. Kanisa tusiwasahauu wanaume - Kanisa lolote lenye afya njema
na familia yoyote yenye afya njema itampa mwanaume kipaumbele, tunapoweka
mipango yetu na maombi yetu kwaajili ya wanaume ili waokolewe hata kama
hawatakuwa viongozi kanisani watakuwa viongozi katika familia zao na jamii,
wanaume wana nafasi kubwa ya kuvunja kuta zote za vizuizi katika jamii na
familia na kuwa sauti ya Yesu Kristo kila mahali, mwanaume akipatikana jamii
nzima itapatikana na ndio maana Paulo
anataka wanaume wasalishe kila mahali, Yesu mwenye nguvu ya kuokoa hataokoa kwa
uonevu ataiokoa wanaume pia
1Wakorintho 16:13-14. “Kesheni, simameni imara katika Imani, fanyeni kiume,
mkawe hodari. Mambo yenu yote na yatendeke katika upendo.”
2. Kanisa lazima liwaendeleze
wanaume kama viongozi wa kiroho, Yesu
hakuufikia ulimwengu kwa kuzungumza na watu wengi pee yake lakini aliwekeza
muda mwingi, mrefu na wakutosha akiwa na wanaume 12 aliwaandaa kuwa viongozi,
aliwatia moyo na kuwajenga ili kuwekeza ukomavu wa kiroho kwao, hebu fikiria
nyumba ambayo mama amekomaa kiroho afu baba ni mchanga kiroho? Ukomavu wa kiroho ukiwekezwa kwa wanaume
tunatengeneza jamii yenye amani sawasawa na mpango wa Mungu, ukuaji wa kiroho
ni swala linalohiaji mpango, na wanaume kwa taarifa yako ndio wenye ushawishi
mkubwa utafiti wa kweli unaonyesha kuwa mama akitangulia kuokoka ni asilimia
30% ya wanafamilia ndio watakaomfuata lakini baba akitangulia kuokoka ni
asilimia 93% ya wanafamilia watafuta kwa hiyo tunapopanga kuufikia ulimwengi
fikiria namna ya kuwapata wanaume, mafunzo na mafundisho ya kimkakati kanisani
yasikose kufikiri kuwafikia wanaume.
3. Kanisa linalotaka kukua ni
lazima lilenge kuwahudumia au kuwafikia wanaume – Mungu hajawapuuzia wanaume agizo
la Paulo kwa Timotheo linasisitiza kwamba wanaume wahudumiwe kwa wingi na kwa
kadiri iwezekanavyo, tutengeneze Ujamaa na wanaume kama neno la Mungu lisemavyo
kuwa chuma hunoa chuma, tuwanoe Wanaume tuwafikie wanaume
Mithali 27:17-19 “Chuma hunoa chuma; Ndivyo mtu aunoavyo uso wa rafiki
yake. Yeye autunzaye mtini atakula matunda yake; Naye amhudumiaye bwana wake
ataheshimiwa. Kama uso ufananavyo na uso katika maji; Kadhalika moyo wa mtu na
mwenzake.”
4. Kila
mwanaume kanisani atafute rafiki atakayesimama naye bega kwa bega kwa bega
katika vita hii ya maisha, na kukumbuka ya kuwa mtu akiwa peke yake nguvu yake
inakuwa ndogo lakini unapoungana na mwingine ushindi unakuwa mkubwa lakini watu
wanapokuwa zaidi ya mmoja ushindi unakuwa mkubwa zaidi na hakuna atakayeweza
kuwazuia maandiko yanaonyesha nguvu hizo, kimwili na kiroho
Kumbukumbu
32:29-30 “Laiti wangekuwa na akili, hata wakafahamu
haya, Ili watafakari mwisho wao.Mmoja angefukuzaje watu elfu, Wawili
wangekimbizaje elfu kumi, Kama Mwamba wao asingaliwauza, Kama Bwana asingaliwatoa?”
Yoshua
23:9-11. “Maana Bwana amefukuza mbele yenu mataifa
walio hodari, kisha wenye nguvu, lakini kwenu ninyi hapana mtu aliyesimama
mbele yenu hata leo. Mtu mmoja miongoni mwenu atafukuza watu elfu; maana Bwana,
Mungu wenu, ndiye anayewapigania, kama alivyowaambia. Jihadharini nafsi zenu,
basi, ili mmpende Bwana, Mungu wenu.”
Mathayo
18:18-20 “ Amin, nawaambieni, yo yote
mtakayoyafunga duniani yatakuwa yamefungwa mbinguni; na yo yote mtakayoyafungua
duniani yatakuwa yamefunguliwa mbinguni. Tena nawaambia, ya kwamba wawili wenu
watakapopatana duniani katika jambo lo lote watakaloliomba, watafanyiwa na Baba
yangu aliye mbinguni. Kwa kuwa walipo wawili watatu wamekusanyika kwa jina
langu, nami nipo papo hapo katikati yao.”
Wanaume wakiigundua siri hii na
kuungana na wengine kutakuwa na nguvu kubwa sana katika ufalme wa Mungu ambayo
haitazuilika Mwanaume mwenye nguvu akiunga ana mwenye nguvu mwingine katika
huduma unadhani kanisa litakuwa na nguvu kwa kiasi gani? Ni kwaajili ya swala kama hili Paulo anataka
wanaume wasalishe yaani washiriki maswala yote ya ibada kila mahali na maswala
yote ya kiimani, na wawe mstari wa mbele katika Kanisa wakiitetea imani na
kuitangaza.
5. Kuwawezesha wanaume kutazalisha
ibada zenye nguvu
- Kanisa likiwapa wanaume kipaumbele kutakuwa na mafanikio makubwa sana katika
kazi zake na katika maswala ya uchumi, Mwanafunzi mwanaume anapojifunza
kumtumikia Mungu atamtumikia Mungu pamoja na mali zake, wanaume watataka kuona
kazi ya Mungu inasonga mbele, tukiwaimarisha wanaume tutakuwa na Kanisa imara
sana, tutajenga ushirika wenye kusudi, kadiri mtu anavyokua katika Kristo na
kukomaa nguvu hiyo itawekezwa kwenye kanisa lake, wanaume wanaweza kutoka na
kuhubiri sehemu mbalimbali, wanaweza kufanya mashambulizi yenye nguvu dhidi ya
ufalme wa giza, Kanisa litakuwa lenye afya ya kiroho na ya kudumu wanaume wana
nafasi kubwa zaidi na nzuri zaidi ya kutekeleza agizo kuu kuliko wanawake hata
kimaumbile, fikiria Petro na Yohana!
Mathayo 28:18-20 “Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa
mamlaka yote mbinguni na duniani. Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa
wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu; na
kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja
nanyi siku zote, hata ukamilifu wa Dahari”
Matendo 4:5-13 “Hata asubuhi wakubwa na wazee na waandishi wakakusanyika
Yerusalemu, na Anasi Kuhani Mkuu, na Kayafa pia, na Yohana na Iskanda, na wote
wale waliokuwa jamaa zake Kuhani Mkuu. Walipowaweka katikati wakawauliza, Kwa
nguvu gani na kwa jina la nani ninyi mmefanya haya? Ndipo Petro, akijaa Roho
Mtakatifu, akawaambia, Enyi wakubwa wa watu na wazee wa Israeli, kama
tukiulizwa leo habari ya jambo jema alilofanyiwa yule mtu dhaifu, jinsi
alivyoponywa, jueni ninyi nyote na watu wote wa Israeli ya kuwa kwa jina la
Yesu Kristo wa Nazareti, ambaye ninyi mlimsulibisha, na Mungu akamfufua katika
wafu, kwa jina hilo mtu huyu anasimama ali mzima mbele yenu. Yeye ndiye jiwe
lile lililodharauliwa na ninyi waashi, nalo limewekwa kuwa jiwe kuu la pembeni.
Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine
chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo. Basi
walipoona ujasiri wa Petro na Yohana, na kuwajua ya kuwa ni watu wasio na elimu,
wasio na maarifa, wakastaajabu, wakawatambua ya kwamba walikuwa pamoja na Yesu.”
Pampoja
na ujasiri na ujazo wa nguvu za Roho Mtakatifu hebu jaribu kuwaza kama Petro na
Yohana ndio wangekuwa wanafunzi wa kike tuchukulie Marim Magdalena na Salome
wamesimamishwa mbele ya wanaume 70 wakihojiwa unapata picha gani? Sisiemi kuwa wanawake hawawezi kuitetea imani
kwa kiwango hiki, lakini hata wangerudi nyumbani huenda wangeambiwa na familia
zao usijihusishe na mambo hata tena! Yesu alijua ni kwanini aliwatanguliza
wanaume.
6. Kuendeleza imani ya Wanaume ni
kuendeleza Injili – Luka 10:1-6 “Basi, baada ya
hayo Bwana aliweka na wengine, sabini, akawatuma wawili wawili wamtangulie
kwenda kila mji na kila mahali alipokusudia kwenda mwenyewe. Akawaambia, Mavuno
ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache; basi mwombeni Bwana wa mavuno
apeleke watenda kazi katika mavuno yake. Enendeni, angalieni, nawatuma kama
wana kondoo kati ya mbwa-mwitu. Msichukue mfuko, wala mkoba, wala viatu; wala
msimwamkie mtu njiani. Na nyumba yo yote mtakayoingia, semeni kwanza, Amani
iwemo nyumbani humu;na akiwamo mwana wa amani, amani yenu itamkalia; la,
hayumo, amani yenu itarudi kwenu.”
Kusudi
kuu la huduma ya wanaume ni kuufikia ulimwengu, Kanisa ni lazima tuwafundishe
wanaume kuitafuta sauti yao, na kuieneza injili, wanaume wengi hufikiri ya kuwa
wao sio chombo sahihi cha kuipeleka injili au wanadhani hawana haki ya
kumzungumzia Kristo tunahitaji kuwafundisha, tunahitaji kuwajengea ujasiri na
tunahitaji kuwapa silaha ili wafanye umisheni, wamtumikie Mungu, watengeneze
programu mbalimbali za kuonyesha upendo wa Kristo kwa wengine, wanaume wakiamka
hakuna cha kuwazuia, Yesu kama haitoshi akafundisha darasa lingine tena la
wanaume 70 ukiacha wale 12 na kisha akawatuma wawili wawili kuongeza kasi ya
upelekaji habari njema kwa hiyo tunajifunza hapa kuwa jinsia hii haipaswi
kupuuziwa hata kidogo katika maswala mazima ya kuipeleka injili kokote duniani!
7. Wanaume wanapaswa kuwasaidia
wanaume vijana
- Tito
2:6-10 “Vivyo hivyo na vijana waume uwaonye kuwa na
kiasi; katika mambo yote ukijionyesha wewe mwenyewe kuwa kielelezo cha matendo
mema, na katika mafundisho yako ukionyesha usahihi na ustahivu, na maneno yenye
uzima yasiyoweza kuhukumiwa makosa, ili yule mwenye kupinga atahayarike, kwa
kuwa hana neno baya la kunena juu yetu. Watumwa na wawatii bwana zao,
wakiwapendeza katika mambo yote; wasiwe wenye kujibu, wasiwe waibaji; bali
wauonyeshe uaminifu mwema wote, ili wayapambe mafundisho ya Mwokozi wetu Mungu
katika mambo yote.”
Dunia
inakwenda kwa kasi sana kama Kanisa litachelewa kimkakati kuwavuna wanaume, ni
wazi kuwa pia tutachelewa kuwavuna vijana wa kiume au kizazi kijacho cha vijana
wa kiume kitakosa walimu wazuri wa kuwafundisha, Paulo mtume mapema alikuwa
amemuagiza Tito kuwa wanawake wazee wawafundishe wanawake vijana namna ya
kuishi ona:-
Tito 2:3-5 “Vivyo hivyo na wazee wa kike wawe na mwenendo wa
utakatifu; wasiwe wasingiziaji, wasiwe wenye kutumia mvinyo nyingi, bali
wafundishao mema; ili wawatie wanawake vijana akili, wawapende waume zao, na
kuwapenda watoto wao; na kuwa wenye kiasi, kuwa safi, kufanya kazi nyumbani
mwao, kuwa wema, kuwatii waume zao wenyewe; ili neno la Mungu lisitukanwe.”
Kama
wazee wa kike wanaweza kuwafunza wanawake vijana je vijana wa kiume watafunzwa
na nani? Vijana wanabadilika na wanakua
na dunia inaenda kasi, wakati sisi tunashindwa kuwafikia wanaume na
kuwasababisha wawe walezi wazuri kwa vijana agenda ya Ibilisi lazima
itaelekezwa huko na je tutakua na kizazi cha namna gani, lazima kuweko na
wanaume wakomavu walioiva kimaadili waweze kuwa msaada kwa kizazi kipya cha wanaume vijana, tusipofanya nani atatufanyia,
kama tunahitaji kanisa lenye nguvu basi tusisubiri muujiza ujitokeze lazima
tufanye kazi ya kuwekeza kwa wanaume ili nao wawekeze kwa wanaume vijana,
mwangalie Daudi alivyomuelekeza Suleimani
1Wafalme 2:1-4 “Basi siku
ya kufa kwake Daudi ikakaribia, akamwusia Sulemani mwanawe, akasema,Mimi naenda
njia ya ulimwengu wote; basi uwe hodari, ujionyeshe kuwa mwanamume; uyashike
mausia ya Bwana, Mungu wako, uende katika njia zake, uzishike sheria zake, na
amri zake, na hukumu zake, na shuhuda zake, sawasawa na ilivyoandikwa katika
torati ya Musa, upate kufanikiwa katika kila ufanyalo, na kila utazamako ili
Bwana afanye imara neno lake alilonena kwa habari yangu, akisema, Ikiwa watoto
wako wataiangalia njia yao, wakienda mbele zangu kwa kweli, kwa moyo wao wote,
na kwa roho yao yote, (akasema), hutakosa mtu katika kiti cha enzi cha Israeli.”
Hitimisho!
1Timotheo 2:8 “Basi, nataka wanaume wasalishe kila mahali, huku wakiinua
mikono iliyotakata pasipo hasira wala majadiliano.”
Kushughulika
na wanaume sio program mpya ndani ya Kanisa bali ni swala la lazima kwa afya ya
kanisa na usalama wa familia za Kikristo, Kama familia inaongozwa na wanaume
katika mpango wa Mungu na mwanaume anafananishwa na Kristo katika itifaki ya
uongozi wa Mungu je tunawezaje kuwaweka pembeni wanaume na kuwafikia wanawake
kabla ya waume zao na Baba zao? Je Mungu
angelimtokea Sara na kumwambia toka wewe katika nchi yako wende katika nchi
nitakayokuonyesha Je Abrahamu na Lutu, na mzee Tera nao wangelimfuata Sara? Mwanaume ni kama sindano na mwanamke na
familia ni kama uzi, pale sindano inapopita uzi utafuata, lakini ni vigumu sana
kushina nguo kwa kuutanguliza uzi, Basi nataka wanaume wasalishe ni wito wa
kutoa kipaumbele kwamba wanaume waokoke, wanaume wamtumikie Mungu, wanaume
wakue kiroho, wanaume wawe watakatifu, wanaume wasalishe kila mahali! Wito huu
ni kwa wanaume kwamba wawe viongozi wa
ibada kila mahali, waongoze maombi, waongoze ibada wasalishe, lakini sisemi
kwamba wanawake hawawezi kufanya hilo, lakini mwanamke kufanya hilo ni mbadala.
Na. Rev. Innocent
Samuel Kamote
Mkuu wa wajenzi
mwenye Hekima

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni