Alhamisi, 27 Oktoba 2016

Mabaya hayatakupata wewe!



Mstari wa Msingi: Zaburi 91:10
 
Mabaya hayatakupata wewe, wala tauni haitakaribia hema yako!”


Utangulizi:

Zaburi hii ni mojawapo kati ya Zaburi zilizotungwa na kuandikwa na Daudi, Inaonekana wazi kabisa zaburi hii ikizungumzia pigo la ugonjwa wa Tauni, ambayo Mungu aliipiga Israel kuokana na kosa la Daudi kuwahesabia wanajeshi wake na kusahau kuwa ushindi unatoka kwa Mungu, katika wakati huu Mungu aliruhusu malaika wake na kuua watu wapatao 70 elfu kwa muda mfupi sana kutoka Dani mpaka Beersheba na sasa malaika wa Bwana alikuwa anaelekea kuuharibu Yerusalem  unaweza kuona vema habari hii katika 2Samuel 24: 10-17

10. Ndipo moyo wake Daudi ukamchoma baada ya kuwahesabu hao watu. Naye Daudi akamwambia Bwana, Nimekosa sana kwa haya niliyoyafanya; lakini sasa, Ee Bwana, nakusihi uuondolee mbali uovu wa mtumishi wako; kwani nimefanya upumbavu kabisa. 11. Na Daudi alipoondoka asubuhi, neno la Bwana likamjia nabii Gadi, mwonaji wake Daudi, kusema, 12. Nenda, ukanene na Daudi, Bwana asema hivi, Nakuwekea mambo matatu; katika haya uchague moja, nikutendee hilo. 13. Basi Gadi akamwendea Daudi, akamweleza, akamwambia, Basi, miaka saba ya njaa ikujie katika nchi yako? Au miezi mitatu ukimbie mbele ya adui zako, huku wakikufuatia? Au siku tatu iwe tauni katika nchi yako? Fanya shauri sasa, ufikiri, ni jawabu gani nimrudishie yeye aliyenituma. 14. Naye Daudi akamwambia Gadi, Nimeingia katika mashaka sana; basi sasa na tuanguke katika mkono wa Bwana; kwa kuwa rehema zake ni nyingi; wala nisianguke katika mkono wa wanadamu. 15. Basi Bwana akawaletea Israeli tauni tangu asubuhi hata wakati ulioamriwa; nao wakafa watu toka Dani mpaka Beer-sheba sabini elfu. 16. Lakini huyo malaika aliponyosha mkono wake kuelekea Yerusalemu ili auharibu, Bwana akaghairi katika mabaya, akamwambia huyo malaika mwenye kuwaharibu watu, Yatosha, sasa ulegeze mkono wako. Naye yule malaika wa Bwana alikuwako karibu na kiwanja cha kupuria cha Arauna, Myebusi.17. Daudi, alipomwoma malaika aliyewapiga watu, akanena na Bwana, akasema, Tazama, ni mimi niliyekosa, ni mimi niliyepotoka; lakini kondoo hawa, wamefanya nini? Mkono wako na uwe juu yangu, na juu ya nyumba ya baba yangu.”

Baada ya tukio hili la kutisha la watu kupigwa kwa tauni, ambalo linaonekana kumuuma moyo sana Daudi, aliamua kumuomba Mungu na ingawa haiku wazi alikuwa anaombea nini lakini bila shaka alijiombea yeye na wakazi wa mji wa Yerusalem na hasa alikuwa anaomba kwa mji wa Yerusalem na maombi yake yalikuwa na uhakika kuwa Mungu hawezi kuipiga Yerusalem, kutokana na uzoefu wake Daudi anaonyesha mambo ya msingi makuu mawili

1.       Kuutafuta uwepo wa Mungu siku zote za masiha yetu Mstari wa 1-9  Katika Mistari hii Daudi alikuwa anaonyesha umuhimu wa kuwa na uhusiano usioonekana na Mungu “AKETIYE MAHALI PA SIRI PAKE ALIYE JUU ATAKAA KATIKA UVULI WA MWENYEZI” Daudi anasisitiza kuwwa na uhusiano usioonekana kati yetu na Mungu, Ukristo wetu sio tu ule unaoonekana, tunapoomba maombi ya kanisani kwa pamoja ni vema lakini uhusiano wetu na Mungu ni zaidi ya maombi ya kanisani, uko uhusiano wa siri kukaa katika uwepo wake  Mathayo 6:2.-4, 7-8.16-18.  Daudi anaonyesha kuwa mtu atakayedumisha uhusiano wa siri na Mungu na kukaa naye katika namna ambayo wengine wanaweza wasijue, Na kumtegemea Mungu, Mungu atakufanyia haya  Zaburi 91:3-9
·         Atakuokoa na mtego wa Mwindaji
·         Mungu atakufunika kwa mbawa zake  na utapata nkimbilio
·         Hutakuwa na hofu ya aina yoyote
·         Mapigo kama tauni na magonjwa ya kutisha  na vita hutaviogopa
·         Hata watu elfu na kumi elfu walianguka mapigo kwao hayatakukaribia wewe
·         Macho yako yataona mwisho wa wabaya

2.       Mabaya hayatakupata wewe.

Ni muhimu kufahamu kuwa Mabaya yanayozungumzwa hapa kama Pestilence (Magonjwa yasio na tiba), au plague (Mapigo ya hukumu) kama biblia nyingi za kiingereza zilivyoandikwa, Biblia ya kiebrania inatumia neno “NEGA ambalo maana yake ni KURUDIWA, au KUADHIBIWA au KUPUNGUKIWA NA NEEMA YA MUNGU, neno hili lina maana kuwa Mungu hatazuia majaribu yasitupate lakini, lakini Mungu hatatuadhibu, au anapotuadhibu hataacha tuangamiie katika mkono wake, atatutisha lakini hataacha tauni disaster zikaribie Hema yako, yaani amakazi yako hayatapigwa Daudi alikuwa anajua kuwa Mungu anaweza kupiga miji Mingine lakini ni vigumu kuruhusu Yerusalem kupigwa , haitakaribiwa ni makazi yake matakatifu, ukifanya masikani na Mungu, Mungu akifanya makazi kwako hakuna mabaya yatakayokupata, Mungu atatuma malaika zake wakulinde, Yeye ana Rehema nyingi hata anapotuadhi,

Mungu hatatuadhibu
Mungu hahatuondolea neema
Hatatupungukia
Hatoondoa rehema zake
Ikiwa tutaimarisha uhusiano wetu wa siri na yeye
Ikiwa tutautafuta uwepo wake, atatuhifadhi, hata wengine wakianguka ka maelfu yao sisi tutabaki salama
Ikiwa Mungu aliwaokoa watu wengi sana katia Biblia wasipatwe na mabaya kuna ushahidi wa
 kutosha kimaandiko kwamba Mungu hatakuacha upatwe na Mabaya 

Rev. Innocent Kamote

Mkuu wa Wajenzi mwenye hekima!

Hakuna maoni: