Alhamisi, 6 Oktoba 2016

Nabii Habbakuki


A.      Mwandishi wa Kitabu cha Habakuki
 
-          Aliyeandika kitabu hiki anajitambulisha kama Nabii Habakuk i(1:1 ; 3: 1). Hakuna maelezo mengine ya ziada kuhusu maisha ya binafsi au ya familia ya huyu mwandishi yaliyopo po pote katika Maandiko. Alikuwa nabii wa Yuda na inajulikana kutokana na zaburi yake (sura ya tatu) na kwenye maelekezo kwa mkuu wa waimbaji (3:19) kwamba alikuwa wa kabila la Lawi, mmoja wa waimbaji wa hekaluni. Habakuki maana yake Kumbatia
-          .Kitabu cha Habakuki kimeandikwa kwa mtindo wa mazungumzo kati ya Mungu na Nabii.
-          Habakuki aliona kwamba viongozi wa Yuda walikuwa wanawaonea maskini, kwa hiyo aliuliza swali kwamba ni kwa nini Mungu anawaruhusu watu hawa waovu kustawi.
-          Mungu alipomwambia kwamba Wakaldayo wangekuja kuwaadhibu Yuda, Habakuki aliumia zaidi. Hakuelewa ni kwa jinsi gani Mungu angeweza kuwatumia Wakaldayo ambao walikuwa waovu kuliko Wayahudi waovu, ili kutekeleza hukumu dhidi ya watu walikuwa watu waliochaguliwa na Mungu. Jibu la Mungu lilikuwa kwamba wenye haki wangeishi kwa imani kwa Mungu na kwamba walikuwa na uhakika kwamba Mungu alikuwa anafanya lililo sahihi. Mungu alimwambia Habakuki kwamba punde si punde Wakaldayo wangehukumiwa na kwamba hatimaye haki ingeshinda kwa ajili ya watu wa Mungu. Habakuki anamalizia kitabu kwa zaburi ya sifa. 

B.      Kiini Cha kitabu cha Habakuki.
-          Mungu anavyotumia waovu kuadhibu watu wake wanapotenda uovu kwa nia ya kuwarudisha ili wamrudie, lakini hao waovu wakiisha kutimiza kusudi la Mungu, wao huadhibiwa zaidi.
-          Yuda walitenda dhambi ikiwa ni pamoja na kuabudu sanamu, lakini Mungu anatumia Wakaldayo walio waovu zaidi kuwaadhibu na hatimaye Mungu anawaadhibu Wakaldayo.
-           Ilimshangaza Habakuki kuona waovu wakistawi huku wakiendelea kutenda dhambi nyingi wala Mungu hawaadhibu upesi! Habakuki anaelezea imani yake katika mamlaka ya Mungu na katika uhakika kwamba Mungu ana haki katika njia Zake zote.
-           Ufunuo wa Mungu kwa wenye haki na nia Yake ya kuiangamiza Babeli iliyokuwa ovu iliamsha wimbo wa sifa wa kinabii na ahadi kuhusuwokovu katika Sayuni (3:1-19)
C.      Kusudi
-          Kuonyesha kwamba bado Mungu anaitawala dunia hata kama tunaona kwamba uovu unashamiri na ya kwamba iko siku Mungu atauhukumu na kuadhibu huo uovu hatimye kuuangamiza kabisa usiwepo tena.
D.      Wahusika Wakuu
-          Habakuki, Wababeli.
E.       Tarehe
-          Kitabu hiki hakikuwekewa tarehe, lakini bila shaka kilikuwa kipindi cha Wakaldayo.
-           1.Hekalu bado limesimama (2 :20) na huduma ya uimbaji inafanyika (3 :19),
-          2. Kuinuka kwa Wakaldayo kuwa dola inayotisha miongoni mwa mataifa kunatokea wakati wa kizazi hicho (1 :5,6) na kuchinjwa kwa mataifa na Wakaldayo tayari kulishaanza
-          (1 :6,7).Wakaldayo walijulikana na Wayahudi muda mrefu kwa kuyashinda mataifa mengine hadi kuongoza katika dola za ulimwengu wakati wa kuanguka kwa Ninawi 612 K.K. au 606 K.K. na kwa ushindi wao juu ya Wamisri huko Kerkemishi mwaka 605 K.K.
F.       Mgawanyo
-          Swali la Habakuki na jibu la Mungu. (1 :1-11)
-          Swali la pili la Habakuki na jibu la Mungu. (1 :12-2 :20)
-          Maombi ya Habakuki. (3 :1-19) 

                                                           
Hekalu lililokarabatiwa wakati wa Herode na kutumiwa Na Yesu na wanafunzi wake kama linavyoonekana katika Nyumba za mfano za kale hii ilitiza kwa sehemu unabii  utukufu wa mwisho wa nyumba hii utakuwa mkuu kuliko ule wa kwanza kama alivyotia Moyo Nabii Haggai na Zekaria Picha na maelezo kwa hisani ya Mwalimu wa somo Rev.Innocent Kamote Home Bible library 2007

Hakuna maoni: