Alhamisi, 6 Oktoba 2016

Nabii Yona



A.      UTANGULIZI.



Ø  Je umewahi kusikia habari za Mwinjilisti ambaye amekasirika kwa sababu wenye dhambi aliowahubiri wametubu na kuokolewa? Yona ni miongoni mwao
Ø  Yeye anaitwa Nabii  asiyetii au Mmishionari Mzalendo yeye alikuwa na uchungu dhidi ya watu ambao Mungu alikuwa amemtuma akawahudumie, alikuwa mbishi muasi na mwenye ubinafsi wa hali ya juu alikosa upendo na huruma na kama ungekuwa wewe na mimi Tusingelimtuma Yona kuwa Nabii
Ø  Jina lake Yona ni la kiibrania ambalo maana yake ni “Njiwa” Ni mwana wa Amittai  ambaye maana yake ni kweli ya Mungu kutoka Gath-Hepher ambayo ni kana ya wakati wa Agano jipya  na ilikuwa karibu na Nazareth mahali alipokulia Bwana Yesu
Ø  Kitabu kinahusu kufanya umisheni katika nchi ngeni na Mungu anamtumia Nabii asiyependa kufanya umisheni wa kigeni kukiandika, Kitabu kinatufundisha jinsi Mungu anavyojihusisha na mataifa mengine pia na kuwa hana upendeleo.

B.      MWANDISHI 
Ø  Wanatheolojia wengi wanaamini kuwa huenda kitabu kiliandikwa kati ya 780- 753 K.K  mapema wakati wa utawala wa Yeroboamu wa pili 
Ø  Kuna uwezekano kuwa alianza huduma yake wakati wa Nabii Elisha mwishoni kwani kulingana na Tamaduni za Israel inasemekana kuwa ndiye mtoto wa mwanamke mjane wa Sarepter ambaye Eliya alimfufua kutoka kwa wafu tarahe kamili inakisiwa ya uandishi kuwa 780 K.K.
Ø  Yesu alinukuu Matukio ya Yona katika Mathayo 12; 39-41 Jambo linalothibitisha kuwa kitabu chake kimevuviwa na sio hadithi tu kama watu wengine wanavyofikiri Yona pia anatajwa katika 2Falme 14;23-25 kama mtu anayetambuliwa kuwa alikuwa Nabii katika ufalme wa kaskazini wakati wa Yeroboamu wa pili mwaka 792-753 K.K.

C.      HISTORIA YA WAASHURU WALENGWA.
Ø  Watu wa Ashuru walijulikana sana kwa ukatili wao baadhi ya watu waliochukuliwa mateka na wafalme wa kiashuru waliwekwa katika visanduku vidogo vya chuma na misumari  na kupelekwa nje ya mji wa Ninawi mji wao mkuu
Ø  Visanduku hivyo vilikuwa vidogo kiasi ambacho mtu hakuweza kukaa wala kusimamia waashuru waliwaua wafungwa wengi kwa kuwakata miguu kila siku mguu moja na siku nyingine mguu mmoja ili kuwafanya wasikie maumivu makali
Ø  Wengine walilazimishwa kuwachinja rafiki zao waliowafahamu zamani watu wengi waliona ni afadhali kujiua kuliko kuwa kwenye mikono ya waninawi Nahumu 3;19
Ø  Wanawake waja wazito waliwapasua tumboni ili kuona ni jinsi gani kitoto kinakaa ndani ya tumbo la mama zao.
Ø  Inawezekana hii ndio ilikuwa sababu iliyomfanya Yona kuchagua kufa kuliko kuwahubuiri watu hawa katili aliokuwa amesikia habari zao na huenda pia Yona alifahamu kuwa wangetumiwa na Mungu kuwaadhibu wa Israel. kwani mnamo mwaka wa 722 K.K. yaani miaka 38 baada ya mahubiri ya Yona Waashuru waliivamia Israel na kuwachukua mateka huko Ashuru

D.      UPEKEE WA KITABU CHA YONA
Ø  Kitabu cha Yona ni Tofauti na Vitabu vingine vya kinabii kwa sababu ya maswala ya msingi yafuatayo;-
1.       Kimeandikwa katika mtindo wa kihistoria kuliko Vitabu vingine vya kinabii ingawa kina kweli nyingi ambazo zinaweza kuwa ni changamoto kubwa na kweli kuu ambazo zaweza kufanya kazi katika maisha yetu leo.
2.       Matendo ya Mungu kwa asili katika kitabu hiki kina kweli kuu kuhusu Mungu kwa asili hii inafundisha wazi kabisa kuwa Mungu yuko kila mahali na ni vigumu kukimbia au kujificha mbali na uso wake Zaburi 139;7-12, kinafundisha pia kuwa Mungu ni Bwana wa Historia, mataifa na Viumbe vyote na kuwa anahukumu kila jamii inapokosea na anaweza kutumia asili kwa mfano alimtumia upepo, samaki mkubwa mmea wa mtango, mnyoo Jua n.k. katika kukamilisha mpango wake kwa Yona kwenda ninawi.
3.       Kitabu hiki kipekee sana kinasisistiza Umisheni  na kufunua Upendo wa Mungu na mpango wa Mungu wa wokovu sio kwa wayahudi pekee bali kwa watu wote wa mataifa Yoote Matendo 10;34-35
4.       Unabii unaotegemea Conditional natural Prophecy Yona alitangaza kuwa Ninawi utaharibiwa katika siku arobaini lakini haukuharibiwa mji kwa sababu watu walitubu Yeremia 18;7-10
E.       MGAWANYO

Ø  Yona kimegawanyika katika maeneo makuu mawili
1.       Wito wa kwanza na upinzani wa Nabii sura ya 1-2
2.       Wito wa mara ya pili na Manung’uniko ya Nabii 3-4

F.       MSTARI MKUU AU MISTARI YA MSINGI

Ø  2;9 Wokovu unatoka kwa Bwana
Ø  3;9 Nani ajuaye ya kuwa Mungu ataghairi na kusamehe
Ø  4;2 Najua ya kuwa wewe u Mungu mwenye neema, umejaa huruma si mwepesi wa hasira u mwingi wa rehema  nawe wagahiri mabaya.

G.       MCHANGANUO WA KITABU CHA YONA 

Kukimbia wito wa Mungu sura ya 1-2.
Ø  Yona hakuwa na mshaka kuhusu nini Mungu alikuwa anataka kukifanyaalipokea ujumbe kwa Mungu kabla na hivyo alifahamu sauti ya Mungu lakni kile ambacho mungu alikuwa amemtuma kilikuwa kimemshagaza kumbuka wakati Mungu alipomwambia Petro aende kwa Kornelio Matendo 10;1-29
Ø  Ninawi ulikuwa mji wa kipagani na mji mkuu wa Ashuru Utawala ambao ulikuwa ni adui mkubwa wa Israel kwa miaka  Mungu alisema uovu wao umepanda juu mbele zangu Mwanzo 18;25 Kwa hivyo yona aliitwa kwenda kuhubiri dhidi ya Ninawi lakini yona hakutaka kulitimiza Jukumu hilo hivyo alikimbia kwenda mbali ingawa alijua wazi kuwa Mungu yuko mahali kote 
Ø  Kumbuka Ninawi ilikuwa karibu kuluiko alikokuwa anakimbilia yaani Trshishi ambayo inaaminika kuwa ni sehemu za Hispania ya leo  Mbali sana kutoka Yaffa
Ø  Kilichofuata ni adhabu kwa ajili ya kutokutii kwa Yona lakini kwa upande mwinginie ni Rehema za Mungu ni upendo wake kumrejeza Yona katika hali ya utii Waebrania 2;10-11.Mungu alituma upepo mkali na mabaharia walifikiri kuwa meli ingevunjika.
Ø  Katika hali hizo zote za dhuruba Yona alikuwa amelala usingizi na hakuwa anajua nini kinaendelea 1;6 matoleo mengine ya Biblia kama Septuagint inasema alikuwa anakoroma
Ø  Yona alipoamsahwa alitoa ushuhuda wa ajabu kuwa anamwabudu “Mungu wa mbingu aliyeumba bahari na nchi kavu …. Na ya kuwa ninakimbia mbele zake” jambo la kushangaza ni kuwa zaidi ya kuasi kwake Yona alikuwa anashuhudia kuhusu Mungu wa kweli na kabla ya kutupwa watu hao waliomba sasa si kwa miungu yao bali kwa Mungu wa Yona 1;14 walitoa sadaka na kuweka nadhiri kwa Mungu huyo huenda waliahidi kumtumikia Ushuhuda wa Yona ulileta matokeo na watu walitubu ingawaje yeye alikuwa akielezea kukimbia kwake
Ø  Yona aliyatoa maisha yake kwa hiyari yake mwenyewe ili wale walikuwa kwenye meli waweze kuokolewa 1;12
Ø  Huenda Yona alijua wazi kuwa kama Ninawi watatubu Mungu atawasamehe na kuwaokoa lakini la kushangaza Yona mwenyewe hakuwa tayari kutubu na badala yake alikuwa tayari kufa kuliko kwenda Ninawi hii inaonyesha jinsi ambavyo kuna hatari katika kuasi mapenzi ya Mungu na na jinsi chuki dhidi ya wengine inavyoweza kutenda kazi ndani ya mtu.

H.      KUHIFADHIWA NA KUOKOLEWA.
Ø  Mungu hakuwa amemsahau mtumishi wake na bado alikuwa na mpango naye na huduma yake kwa ajili ya watu wa Ninawi aliandaa samaki mkubwa Nyangumi na kummeza Yona baadhi ya matoleo ya Biblia yanasema Mungu akaandaa au akachagua samaki mkubwa hii inaonyesha uweza wa Mungu dhidi ya mambo ya asili kuwa Mungu aweza kuyatumia mazingira au Viumbe katika kutimiza mpango wake,wengine wana fikiri kuwa labda swala la kumezwa na nyangumi ni hadithi lakini kumbuka kuwa ni mpango wa Mungu, Mungu aliandaa samaki mkubwa hii imerudiwa mara nne katika kitabu cha Yona

Ø  MAOMBI KWA AJILI YA WOKOVU.
Yona alifanya maombi na kujiuhukumu mwenyewe ndani ya samaki, lakini Mungu kwa huruma yake na Neema wakati mwingine anaruhusu sisi kupitia hukumu zake ili kwamba tumlilie yeye na kumtegemea yeye na kwa wakati huu sasa Yona alikuwa tayari kwenda Ninawi na kumtii Bwana  alithibitisha kujitoa kwake kwa Mungu na  Furaha ikaujaza moyo wake.

I.         KUTII WITO WA MUNGU MARA YA PILI.
-          Hakuna ajuaye ya kuwa Samaki alimpeleka wapi Yona huenda alimtapika huko Ninawi hata hivyo hili si la muhimu hapa la muhimu ni kuwa Yona alikubali wito wakati, Mungu alipomtuma mara ya pili.
-          Watu wengine hukataa wito wa Mungu na hawapati nafasi ya pili ya kumtumikia Mungu wengine hufikiri ya kuwa huenda Mungu hata watumia tena,Yona alitii neno la Bwana lilipomjia mara ya pili na alikwenda Ninawi
-          Inakisiwa watu wapatao 600,000. Waliishi Ninawi na vitongoji vyake ilimgharimu siku tatu Yona kuihubiri Ninawi ingawa alipewa siku 39. Ujumbe wake ulikuwa katika siku tatu ninawi utaangamia, kwa mujibu wa Luka 11;30  tunajua kuwa huenda Yona alimtumia uzoefu wake wa kumkimbia Mungu na kuokolewa na hii ilikuwa ishara kwa watu wa ninawi kutubu mji mzima na kumrudia Mungu

J.       KUMFAHAMU MUNGU NA MTAZAMO WAKE SURA YA NNE
-          Mwinjilisti anakasirika kwa sababu wenye dhambi wametubu  hiki nacho ni kioja ni wazi kuwa alijua kuwa Mungu ni mwingi wa Rehema na ya kuwa atawasamehe waninawi na ndio maana alikimbia wala hakutaka waninawi waokolewe
-          Wakati waninawi wanatubu kwa kufunga, Yona alikuwa anajijengea kibanda cha mapumziko kwa ajili yake nje ya mji akisubiri kwa tumaini kuwa Mungu atawaangamiza na siku arobaini zikapita patupu!
-          Yona alikasirika alikuwa na tatizo Kiburi,Ubinafsi na kukosa upendo alijihusisha sana na heshima yake kama Nabii ametabiri na Mungu ataitimiza unabii wake alikuwa tayari kufa kuliko kurudi Israel na kusimulia kuwa mahubiri yake yamewafanya Waninawi watubu na kuokolewa
-          Mungu ana namna yake anavyoweza kuyaangalia mambo na kutuonyesha makosa yetu na kutufundisha mtazamo wake aliandaa mtango kumpa Yona kivuli  na Nabii wake mwenye hasira akapumzika kisha akaandaa mnyoo upepo na jua kali vikaharibu kile kivuli Yona akakasirika zaidi
-          Kumbuka kuwa mungu alimuuliza yona unaona vema kukasirika hatupaswi kulaumu kile mungu anachokifanya Yona alijibu kuwa anafanya vema kukasirika hata kufa Hasira husumbua watu wengi na husababisha kifo au kupooza Srtokes
-          Mungu alikuwa akimfundisha Yona na sisi kuwa Yeye ni mwingi wa Rehema  Yona alifurahia faraja zake na starehe zake  kuliko maisha ya watu 120,000 watoto wachanga na wanyonyao Mungu aliwajali wao kwani anaupenda ulimwengu mzima Yohana 3;16.

Hakuna maoni: