Alhamisi, 6 Oktoba 2016

Nabii Amosi


AMOSI: NABII WA UTAKATIFU

A.      UTANGULIZI
-          Amosi alikuwa miongoni mwa wanamapinduzi wakubwa katika Isarael huduma yake ilifanyika kipindi ambacho Israel walikuwa wameharibika vibaya  na walikuwa katika wakati wa mafanikio na starehe ambazo ziliwafanya Israel  kuishi maisha ya dhambi
-          Jina lake maana yake ni “Mbeba mzigo” alikuwa na mzigo wa kutimiza agizo Mungu alilokuwa amempa kulitangaza neno la bwana wakati wa ukengeufu mkubwa wa Israel alizaliwa katika kijiji kiitwacho Tekoa miles 12 hivi kutoka Yerusalem
-          Alikuwa Mchungaji wa Kondoo na mtunzaji wa miti ya mikuyu hakuwa Nabii aliyesomea  7;14 lakini alikuwa mnenaji Hodari “Great orator”Asili ndiyo ilikuwa shule yake na anga ubao wake 5;8 Neno lake linaonyesha historia yeke 3;8
-          Amosi alikuwa mtu wa Yuda ingawa alitumwa kwa Ufalme wa Israel

 
Pichani Juu wachungaji wakichunga kondoo katika uwanda wa mashamba ya ngano huko Tekoa mahali alikotokea Nabii Amosi Tekoa iko mail 12 hivi kutoka Yerusalemu katika tawala za Yuda Picha kwa hisani ya maktaba ya Mchungaji Innocent Samuel Kamote 

B.     TAREHE YA UIANDISHI.
-          Kitabu kiliandikwa mwaka wa 755 K.K. wakati wa utawala wa Yeroboamu II mfalme wa Isarael na Uzziah Mfalme wa Yuda


C.     WASIFU WAKE.
-          Amosi alikuwa Mnyenyekevu na wala hakijaribu kuficha maisha yake ya huko nyuma 7;14
-          Alikuwa na Hekima  katika kupeleka kwake ujumbe alimtumia misamiati amabayo ilikuwa wazi na ya kivitendo
-          Alikuwa mtu Imara thabiti alikataa kugeuzwa na Amazia kuhani mwakilishi wa Yeroboamu huko Betheli 7; 10-17.

D.     HISTORIA YA WALENGWA.
-          Wakati huu Israel walikuwa wanaishi maisha ya anasa na mafanikio makubwa sana hata hivyo baadhi ya matajiri waliupata kutokana na dhuluma
*      Masikini walikandamizwa Amosi 5;7,11
*      Mahakimu au Waamuzi walikuwa wakipokea Rushwa Amosi 5;12
*      Wafanya Biashara hawakutumia mizani za halali Amosi 8;5-6
*      Wenye haki waliuzwa utumwani amosi 2;7
*      Kulikuwa na uashaerati usio wa kawaida hata Baba na Mtoto waliweza kutembea na mwanamke mmoja Amosi 2;7.
*      Waliwakataza Manabii kuhubiri Amosi 2;7.
*      Watu walioishi maisha ya Stareha na anasa Amosi 6;1
*      Uasi wa kidini ulitawala Amosi 4;4-5, 5;21-23
-          Utawala ambao ungeiangamiza Israel ingawa haujaelezwa ni Ashuru.

E.     WAZO KUU NA MISTARI YA MSINGI.
-          Wazo kuu katika kitabu hiki ni Samaria Inavuna hukumu,amosi alikuwa  ni Nabii wa kwanza kutamka anguko la Samaria au Israel ambalo lilitimia miaka 40 baadaye ujumbe wake ulikuwa hukumu ya Mungu kwa sababu ya Kukosekana kwa haki katika jamii
-          Mstari mkuu au wa msingi ni
-          Amosi 3;3 Je wawili waweza kutembea Pamoja isipokuwa wamepatana?
-          Amosi 4;11-12 “Jiandae kukutana na bwana Mungu wako”
-          Amosi 6;1 ole wao wanaostareha katika Sayuni

F.      MGAWANYIKO WA KITABU CHA AMOSI.
-          Hukumu ya mataifa sura ya 1-2
-          Hukumu ya Israel sura ya 3-6
-          Uchanganuzi wa hukumu 7-9;10
-          Ahadi ya kurejeshwa upya 9; 11-15.

G.     MCHANGANUO WA KITABU CHA AMOSI
-           Kabla ya kutangaza hukumu  dhidi ya Yuda na Israel Nabii anachagua mataqifa kama sita hivi  ambayo pia aliyatangazia hukumu ya Mungu
-          Matatu kati ya hayo ni Dameski Syria,Gaza kwa wafilisti na Tiro ambao hawa hawakuwa na uhusiano wa kindugu na Israel bna yuda
-          Mataifa mengine matatu ambao walikuwa na uhusiano wa kidugu na Israel na Yuda ni Edomu, Ammoni na Moabu.
-          Kila tamko la hukumu kwa mataifa ya jirani na Israel na Yuda ilianza na “Haya ndiyo asemayo Bwana kwa makosa matatu naam kwa makosa manne sitazuia adhabu….”
-          Mtindo huu unamaanisha maovu yaliyopita kiasi na ya kuwa maovu hayo yaliongezeka mwaka kwa mwaka
-          Amosi ndiye mwanzilishi wa mtindo wa kuliita taifa kupitia jina la mji mkuu wake mfano anapoizungumzia Yuda anaitaja kama Yerusalem na Israel kama samaria.

A.      HUKUMU DHIDI YA DAMESKI SYRIA 1;3-5
-           Dameski ulikuwa ni mji mkuu wa Syria na hapa Syria inatangqaziwa hukumu kwa sababu ya kulitendea vibaya Gileadi Gileadi ulikuwa mji wa kale wa kabila ya nusu ya Manase ambao walibaki ng’ambo ya Yordani watu walipokuja kuitamalaki inchi ya mkanaani,
-          Dameski waliwachukuwa watumwa au mateka kwa vyombo vya chuma na kuwaburu za kama mtu avunaye ngano mungu anahaidi kushusha moto na kuwateketeza

B.      HUKUMU DHIDI YA GAZA 1;6-8
-          Gaza ulikuwa mji mkuu wa wafilisti  kusini magharibi ya Yerusalem,Dhambi yao ilikuwa ni kusafirisha watumwa waliwachukuwa watu walioishi vijijini  hususani waisreal na kuwauza huko edomu kama watumwa
-          Mungu anaahidi kuwaletea hukumu ya kuwateketeza kwa Moto na kuuchoma mji na majumba yake.

C.      HUKUMU DHIDI YA TIRO 1;9-10
-          Tiro iko kaskazini mwa pwani ya Israel na mji uliokuwa kutuo kikuuu cha bahari au bandari Isaya ,Yeremia na Ezekiel waliitangazia hukumu maalumu ulikuwa mji mkuu sana wa kibiashara  na kajhba mkuu wa wakati ule
-          Inaonekana waliwachukuwa watu fualni kabila nzima huenda Waisrael na kuwatia mikononi mwa Edomu hivyo dhambi yao ilikuwa ni kufanya biashara ya utumwa na Edomu na walisahau agano la undugu huenda hili lilikuwa ni agqano walilolifanya Daudi na Hiramu katika 2samuel 5;11
-          Hukumu yao ni moto na kuharibiwa majumba yake na ni kweli Nebukadneza alijaribu kuuteka tiro lakini si kwa mafanikio sana na mwishoni  uliharibiwa vibaya na Alexander mkuu.

D.      HUKUMU DHIDI YA EDOMU 1;11-12
-          Hwa walikuwa ni uzao wa Esau pacha wa Yakobo na walioishi kusini mwa bahari iliyokufa  sehemu iliyoitwa araba, wao wanahukumiwa kwa Matendo yasiyo ya kindugu,alimtumia upanga na mateso hawakuwa na huruma na walikuwa na kisasi cha hasira kwa siku nyingi na wanatangaziwa hukumu nya moto juu ya temmani na Borsa  miongoni mwa miji yao mikubwa na kuiteketeza.

E.       HUKUMU DHIDI YA WAAMONI 1;13-14
-          Waamoni na wamoabu ni Watoto,wajukuu wa Lutu waliozaliwa kutokana na zinaa ya baba na watoto wake wa kike  Mwazno 19;30-38
-          Wao wanahukumiwa kwa sabau ya ukatili wao kwa Gileadi ,waliwapasua wanawake wenye mimba wa Gileadi wanatangaziwa hukumu dhidi ya mji wao mkuu  Raba au Raboth-ammoni
-          Inaaminika kuwa huko ndiko Daudi alikoagiza Yoabu kuhakikisha Uria anauwa vitani 2Samuel 11.

F.       HUKUMU DHIDI YA WAMOABU 2;1-3
-          Hawa walikuwa na kosa la kuichoma moto mifupa ya mfalme wa Edomu  hata ikawa chokaa inaonekana hawakumpata akiwa hai hivyo kwa hasira walilipa kisasi kwa mifupa ya mfalme Isaya 15;5,16;11 Yeremia 48;36
-          Wamoabu walihukumiwa kwa moto ,na kuuawa kwa Viongozi ,Waamuzi na watu wakuu
-          Mungu anafuatilia sio tu mataifa wanavyolifanyia taifa la watu wake bali hata kila taifa linavyolifanyia lingine.

G.      HUKUMU DHIDI YA YUDA 2;4-5
-          Tofauti na mataifa haya mengine ya kidunia sita Nabii anaigeukia Yuda ambao ni ufalme wa kusini lakini hawa wanahukumiwa kwa kutokishika Sheria ya Mungu hivyo wao wanahukumiwa kwa maswala ya kidini yaani walikengeika na kuiacha Shetia ya Bwana
-          Waliishi kama watu wa dunia  nao watahukumiwa kwa moto na majumba yao kuteketezwa

H.      HUKUMU DHIDI YA ISRAEL 3;1-6
-          Pamoja na matangazo yoote hayo ya hukumu mungu alikuwa akiilenga Israel wao ndio wanaoonekana kuwa na dhambi nyingi zaidi kuliko mataifa mengine mlomlongo wa msururu wa dhambi kwa Israel ni mkuu sana  walionea masuikini,waliwauza watu wenye haki ,waliabudu sanamu,waliifanya biashara ya utumwa, waliwafanya wanadhiri kuvunja nadhiri zao na kulitii unajisi jina la bwana
-          Amosi aliorodhesha dhambi nyingi za Israel kuliko za mataifa mengine huenda ili kuonyesha hatia kubwa waliyokuwa nayo na pia kwa sababu alikuwa akiihubiri Israel na kuwaonyesha uhakika ya kuwa Mungu angewahukumu wao.
-          Mungu anaihukumu Israel na kuwatangazia hukumu hivyo akisisitiza katika matangazo makuu matatu yoote yakianzia na neno lisikieni 3;1,4;1,5;1 na katika 3;3 anauliza je wawili waweza kutembea Pamoja isipokuwa wamepatana? Mungu alikuwa anahoji anawezaje kutembea na Israel na kukubaliana nao huku wanatembea dhambini
-          Amosdi alimtumia hata mifano kama simba na mawindo,Mtego na tarumbeta  ili kuwaaamsha Israel kutoka katika usingizi wa maovu na starehe
-          Mungu hawezi kutuma hukumu kwanza kabla hajaifunua siri hiyo kwa watumishi wake Manabii amosi 3;8
-          Israela walikuwa wameingia katika ile dhambi ya kuabudu miungu 1Falme 12;25-33 na dhambi za starehe 3;15
-          Katika Sura ya 4 amosi aliendelea na ujumbe wake wa hukumu aliwaita Israel Ng’ombe za bashani Bashani palijulikana sana kwa  utajiri wa mifugo na mafuta na wanyama waliolishwa vizuri sana  Kumbukumbu 32;14-15, Wanawake matajiri waliokuwa wabinafsi waliitwa ng’ombe za bashani walijali maswala yao ya starehe na anasa na waliwatia moyo waume zao kujitajirisha na kuwaonea masikini 4;4 inaonekana kulikuwa na shughuli nyinfgi za kiibada na za kidini lakini  hakukuwa na kujitoa kwa kweli kwa Mungu
-          Mungu alihaidi kuwatumia Mapigo makuu matano  4;6-11 yaani njaa ,ukavu dhuruba,nzige,magonjwa
-          4;6 Lugha ya kimafumbi inatumika “Euphenism language” nimewapa usafi wa meno maana yake njaa. 4;12 wanaambiwa wajitayarishe kukutana na Mungu.
-          Katika sura ya 5 nabii anaomboleza kwa ajili ya dhambi ya Israel, wako watu ambao hudhani kuwa kuudhuria kwao ibada ni kwa muhimu zaidi au kunaweza kuwapa kibali kwa mungu na kusahu wajibu wa kujitoa kwake.

H.    UFAFANUZI WA HUKUMU AMOSI 7;-9;10
a.       Eneo hili lina ufafanuzi wa hukumu tano ambazo Mungu alimuonyesha Amosi katika maono
i.        Nzige- Mungu wakati mwingine hutimia majanga ya asili  katika kuhukumu amosi aliomba kwa niaba ya taifa likasamehewa pigo hilo 7;1-3
ii.   Moto Mungu alikusudia uteketeze na kuangamiza lakini pia amosi alimuomba    Mungu asamehe na ikawa hivyo  7;4-5
iii.      Timazi kilikuwa kipimo cha kuonyesha kuwa wamepotoka kiasi gani Bwana alimuonyesha amosi na wakati huu ikawa ndio mwisho wa kusamehewa mungu ana kipimo chake kwa ajili ya maisha yetu
iv.      Kikapu cha mavuno ya wakati wa hari 8;1-3 kuonyesha kuwa wanvuna kile walichokipanda
V. Kuvunjwa kwa madhabahu 9;1-10 huku ni kuharibiwa kwa hekalu lililokuwako huko Betheli kwa ufalme wa kaskazini
·         Amazia ambaye alikuwa ni kuhani mkuu kwa upane wa Betheli 7;10-17 alishutumu Amosi na kumshutumu kuwa amafanya uongo fitina juu ya Israel na hivyo hawawezi kustahimili Maneno yake na Amosi alisisitiza kuwa wito wake ni kutoka kwa Mungu

I.  AHADI YA KUREJEZWA TENA 9;11-15.
- Amosi anamalizia kitabu chake kwa ahadi ya kurejezwa tena kwa Israel
- Kwamba watatawanywa hukona huko kati ya mataifa lakini mabaki watarejezwa
- Nchi itastawi na hawataweza kutawanywa tena 9;11-15

Hakuna maoni: