Alhamisi, 6 Oktoba 2016

Nabii Hagai



HAGGAI: MTIA MOYO WA UJENZI WA HEKALU

A.      Mwandishi
-          Hagai ni moja ya vitabu vitatu vya kinabii vya Agano la Kale vilivyoandikwa baada ya uhamisho ambavyo ni Hagai, Zekaria na Malaki.
-          Hagai anatajwa kwa jina mara mbili katika kitabu cha Ezra (Ezr 5:1,6:14) kama “mjumbe wa Bwana” (1: 13). Inawezekana alikuwa mmoja wa wale waliorudi kutoka uhamishoni waliorudi Yerusalemu, walioweza kulikumbuka hekalu la Solomoni lilivyokuwa kabla halijaharibiwa na majeshi ya Nebukadneza mwaka 586 K.K. (2:3). Hagai na Zekaria ndio waliowatia moyo wale watu waliorudi kutoka uhamishoni kujenga upya hekalu.
-          Ilikuwa ni mnamo mwaka 538 K.K., miaka kumi na minane ilikuwa imepita tangu Dario alipopitisha amri kuwaruhusu Wayahudi kurudi Yerusalemu kutoka uhamishoni. Watu walikuwa bado wanashughulika kujenga nyumba zao, hivyo ujenzi wa hekalu la Mungu ulikuwa bado haujakamilika.
-          Kundi la kwanza la Wayahudi lililorudi Yerusalemu liliweka msingi wa hekalu jipya.mnamo mwaka 536 K.K.wakiwa na furaha na matumaini makubwa (Ezr 3:8-10).
-          Hata hivyo Wasamaria na majirani wengine walipinga ujenzi huo kwa nguvu nyingi na kuwakatisha tamaa wafanya kazi hata ikafanya ujenzi huo usimame mwaka 534 K.K..
-          Watu waliacha ujenzi wa hekalu, wakageukia ujenzi wa nyumba zao wenyewe. Ujumbe wa Hagai ulikuwa kwamba ni wakati wa kujenga nyumba ya Mungu. Hagai akiwa amefuatana na Zekaria (taz.utangulizi wa kitabu cha Zekaria), yeye alianza kumhimiza Zerubabeli na watu wote kuanza tena kujenga nyumba ya BWANA. Chini ya uongozi wa Zerubabeli mtawala na Yoshua kuhani mkuu na kule kuhimiza kwa Nabii Hagai hekalu lilijengwa mnamo 520 K.K. Miaka minane baadaye hekalu lilimalizika kujengwa na kuwekwa wakfu (ling.Ezr 4-6). 

B.      Kiini cha ujumbe wa Haggai

-         Hagai aliwaambia watu kwamba utukufu wa hekalu walilokuwa wanajenga ungekuwa mkubwa kuliko ule wa hekalu lililotangulia, ingawaje halingekuwa imara kama la kwanza. Hili hekalu lingekuwa bora zaidi kwa sababu Mungu angelijaza utukufu Wake ndani yake.

-          Kuwahimiza watu kujenga upya hekalu la BWANA na kuwahamasiaha kuyatengeneza maisha yao upya na Mungu ili waweze kupata baraka Zake.

C.      Historia ya nyuma ya mambo
-          Hekalu la Yerusalemu lilibomolewa mnamo mwaka 586 K.K. Mwaka wa 538 K.K,
-          Mfalme Koreshi wa Uajemi alitoa amri Wayahudi warudi ili kujenga upya mji wa Yerusalemu na hekalu.Mwaka 536 K.K.walianza kujenga hekalu lakini ilikuwa vigumu kumalizia kutokana na upinzani waliokutana nao kutoka kwa Wasamaria na mataifa ya jirani.
-          Kupitia huduma ya Hagai Zekaria na Yoshua, mwaka 520 K.K., walianza kujenga tena hekalu.Miaka minane baadaye kazi hiyo ya ujenzi wa hekalu ilimalizika.

                           

Mabaki ya ikulu ya Mfalme Dario Mmedi /Mmuajemi ni katika utawala wake ndipo Nabii Haggai aliandika kitabu chake cha kuhamasisha ujenzi wa Nyumba ya bwana makazi haya ya iliyokuwa ikulu yako mahali paitwapo Persepolis Nyakati za Leo Picha na maelezo kwa hisani ya Maktaba ya mwalimu Innocent KamoteMchungaji.

D.      Tarehe  ya uandishi
-          Tarehe ya kuandikwa kwa kitabu kwa hiki ni ya uhakika, yaani, mwaka wa pili wa Mfalme Dario wa Uajemi (mwaka 520 K.K. (1:1).
-          Mpangilio wa kihistoria ni wa muhimu sana ili kuuelewa ujumbe wa kitabu hiki. Mnamo mwaka 538 K.K., Mfalme Koreshi wa Uajemi alitoa amri ikiwaruhusu Wayahudi waaliokuwa uhamishoni kurudi nchini mwao ili kuujenga upya Yerusalemu na hekalu katika kutimiza unabii wa Isaya na wa Yeremia (Isa45:1,3; Yer 25:11-12; 29:10-14) na maombezi ya Danieli (Dan 9). 

E.       Wahusika Wakuu 

-          Hagai, Zerubabel, Yoshua.

F.       Mgawanyo
-          Wito wa kujenga hekalu. (1:1-15)
-          Matumaini ya hekalu jipya. (2:1-9)
-          Baraka zilizoahidiwa. (2:10-19)
-          Ushindi wa mwisho wa Mungu. (2:20-23)

Hakuna maoni: