Alhamisi, 6 Oktoba 2016

Nabii Nahumu


Nabii wa Kuanguka kwa Ninawi yaani Ashuru (Syria)

 Hali ya Syria leo!


      Mwandishi wa kitabu cha Nahumu 

-          Nahumu maana yake ni mwenye kufariji
-          Hakuna linalofahamika kuhusu wazazi wake au historia yake wala mafunzo yake lakini ukweli unabaki kuwa kwa kuwa ujumbe wake unahusu hukumu  ni wazi kuwa ulitolewa wakati mfupi  kabla ya Uamsho mkubwa uliokuja wakati wa Yosia 627-621
-          Nahumu anajulikana kama Nabii wa kisasi au Nabii wa kuanguka kwa Ninawi  kinakisiwa kuwa kiliandikwa 621 K.K. katika mwaka wa 18  wa Yosia mfalme wa Yuda na kabla ya anguko la Ninawi la mwaka 612 K.K
-          Nahumu anajiita mwekloshi 1;1 na Ekloshi yenyewe Haijulikani iko upane gani ila kuna wanaodhani kuwa  ni kijiji kidogo mashariki ya mto Tigrisi sio mbali kutoka Ninawi na wengine wanafikiri kuwa ni kijiji kidogo huko Galilaya karibu na Kapernaumu jina Kapernaumu maana yake ni kijiji cha Nahumu
B.       Kiini cha kitabu
-          Kiini cha ujumbe wa kitabu hiki ni anguko la Ninawi katika Septuagint kitabu hiki kimewekwa mara tu baada ya kitabu cha Yona  ikifikiriwa kuwa ni ukamilisho wa kitabu cha Yona
C.      Historia ya nyuma ya mambo
-          Ninawi ulikuwa ni mji mkuu wa waashuru
-          Kwa karne nyingi waashuru waliwaonea sana watu wa mashariki ya kati na kumuka ukatili waliokuwa nao katika kitabu cha Yona na angalia Isaya 37
-          Lakini kwa huruma zake Mungu alimtumia Yona Ninawi na watu walitubu na kuokolewa hata hivyo baada ya Muda watu walirudi katika njia zao za uovu vilevile
D.      Mistari ya msingi
-          1;3    - Bwana si mwepesi wa hasira lakini ana nguvu
-          2;13 – Niko kinyume nawe asema Bwana
-          1;7 – Bwana ni mwema kimbilio wakati wa Taabu
-          1;15 – Angalia huko milimani miguu yake yeye aletaye habari njema
E.       Uchanganuzi
-          Hasira ya Bwana 1;1-8 Kuna Maneno sita ya nguvu katika Nahumu  yanayoelezea hisia za Mungu  na majibu yake kwa waninawi Wivu, Kisasi, Hasira, Ukali, Ghadhabu, Kumwagwa  Nahumu 1;6. Ingawa nahumu amesema wazi kuwa mungu ni mwingi wa huruma 1;7 na hivyo rehema zake na upendo wake humfanya asihukumu kwa haraka dhidi yao wamtendao mabaya  lakini wakati unakuja ambapo hulazimika kuadhibu maovu
-          Hasira ya Mungu ni Tofauti na ya wanadamu ya wanadamu huchanganyika chuki kwa waliomuuzi na mwanadamu hawezi kujizuia katika hasira yake  yenye ubinafsi, Hasira ya mungu  haina haraka wala ubinafsi, au isiyozuilika kama ya wanadamu 1;3, haki yake na kisasi chake kiko katika kanini ya kupenda na kuvuna wanadamu na mataifa yote yatavuna kile walichokipanda.
-          Wivu wa mungu ni wa haki unasukumwa na upendo wake kwa watu  na unakusudia kuwalinda kutoka kwao wanapojaribu kuwapeleka watu wake mbali na yeye na furaha aliyoikusudia kwao kumbuka alivyomwambia “Sauli Mbaona waniudhi”
-          Kabla ya hasira za mungu milima ilitetemeka  na vilima viliyeyuka na nchi ilitetemeka 1;6
F.       Upekee wa kitabu cha Nahumu na ujumbe wake
-          Nahumu ndiye Nabii pekee anayeuita ujumbe wake kitabu 1;1
-          Nahumu kama Yona na Obadia wanashughulika na  mataifa adui  waliozionea Israel na Yuda
-          Yona aliwahubiri waninawi huko ninawi lakini Nahumu aliizungumzia Ninawi kwa Yuda hivyo ujumbe wake ulikuwa ni faraja kwa Yuda juu ya ukombozi toka kwa adui zao na watesi wao na hakuna mashitaka kuhusu yuda wala wito wa toba
-          Nahumu kinasisitiza Anguko la Ninawi na kinakazia juu ya Hasira takatifu ya Mungu dhidi ya dhambi
-          Kumbuka kuwa ujumbe wa Ninawi kwa Yuda haukutokana na chuki binafsi za Nahumu kwa adui zao Lakini mungu alimpa ili kuthibitisha agano lake dhidi ya Yuda na kuwakumbusha kuwa Mungu atawapigania dhidi ya adui zao Kumbukumbu 28;1,7.
G.      Mgawanyo
-          1  Anguko la Ninawi linatangazwa sura ya 11;1-15
-          2 Anguko la Ninawi lina changanuliwa sura ya 2;1-13
-          3 Anguko la ninawi  linathibitishwa Sura ya 3;1-19

Hakuna maoni: