Alhamisi, 6 Oktoba 2016

Nabii Malaki



MALACHI: NABII WA SIKU ZA UAMSHO
A.       Mwandishi


-          Malaki aliishi katika nusu ya pili ya karne ya tano Kabla ya Kristo, baada ya ujenzi wa hekalu kumalizika. Malaki ambalo ni neno la Kiebrania ‘‘Malaki’’ kama lilivyo kwenye Kiswahili, maana yake ‘‘Mjumbe wangu.’’. Jina hili ni kifupi cha ‘‘Malakia’’ ambalo maana yake ni ‘‘Mjumbe wa Bwana‘’ (1:1).
-          Jina hili la kitabu limetumika vivyo hivyo kwenye maandiko ya Kiebrania na Kiyunani likionyesha kwamba hili likuwa jina la nabii ambaye ujumbe wake umenukuliwa humu. Hakuna habari nyingine zo zote za kibinafsi zinazofahamika za huyu nabii. Maisha ya kidini ya Wayahudi yalikuwa mabaya :
-           Walikuwa wamekengeuka, wakawa wameoa wanawake wa mataifa mengine, wakaacha kutoa zaka (fungu la kumi) na dhabihu ambayo na sehemu ya Mungu, hata wakawa wamemwacha Mungu, hali ambayo ilifanana sana na ile iliyokuwepo wakati wa Nehemia (444-432 K.K.). 

B.      Kiini cha ujumbe wa kitabu cha Malaki

-          Masikitiko makubwa ya Malaki ni uhusiano kati ya Waisraeli na Mungu haukuwa kama ulivyopaswa uwe. Walimwacha Mungu na kumdharau, wala hawakumheshimu inavyostahili, wakashindwa kufuata yale Mungu aliyowaagiza. Matokeo yake hukumu ikawa inawangoja, lakini watu wanaomcha Mungu wamehakikishiwa kuwa wameandikwa kwenye kitabu cha Mungu, nao watafuhia wokovu wa Mungu milele. 

C.      Kusudi
-          Kuwahimiza watu wafanye mabadiliko thabiti ya kimsingi katika maisha yao, kwa kuwakumbusha upendo wa Mungu (1:1-5) na pia kwamba adhabu yake iko karibu (2:17; 3:13)

D.      Mchanganuo wa kitabu cha malaki

-          Kitabu hiki kinaonyesha kuwa:(1)Hekalu lilijengwa tena (516/515 K.K.), dhabihu na sikukuu zilirudishwa. (2)Ufahamu wa jumla wa sheria ulirudishwa tena na Ezra (kama 457-455 K.K. ; tazama Ezra 7 :10, 14, 25-26) na (3).Kurudi nyuma kimaadili kulikofuatia kulitokea miongoni mwa makuhani na mwa watu pia (kama mwaka 433K.K.). Kutokana na hali hii hali ya kiroho na upuzi Malaki anaouzungumzia kwa karibu vilifanana sana n aile hali aliyoikuta Nehemia aliporudi kutoka uhamishoni Uajemi (kama 433-425 K.K.) ili kuwa mtawala wa Yerusalemu (ling. 13 :4-30).
E.       Mahali
-          Yerusalemu. Malaki, Hagai na Zekaria walikuwa manabii katika Yuda (Ufalme wa kusini) baada ya watu kurudi kutoka uhamishoni.. Hagai na Zakaria waliwakemea watu kwa kutokumalizia ujenzi wa hekalu. Malaki alipambana nao kwa sababu walipuuzia hekalu na kutokumjali Mungu.
F.       Tarehe
-          Yale yaliyomo kwenye kitabu hiki yanaonyesha kwamba huduma ya Malaki ilikuwa kwenye utendaji mnamo sehemu ya pili ya karne ya tano Kabla ya Kristo. Hekalu lilikuwa tayari limeshajengwa tena upya. Kutokana na wakati alioishi Malaki na yale yaliyomo kwenye kitabu hiki, inawezekana kiliandikwa 557- 525 K.K.
G.      Wahusika wakuu
-          Malaki na makuhani
H.       Mgawanyo
-          Upendo wa Mungu kwa Israeli. (1:1-5)
-          Israeli yamtukana Mungu. (1:6-2:16)
-          Hukumu ya Mungu na ahadi yake. (2:17-4:6)

Hakuna maoni: