Ijumaa, 4 Machi 2016

Akanisalimia kwa Kizigua na Kutangaza kunijua kwa Sana!



Sikuwa nafikiria kuwa jambo lile kuna siku litakuja kuniumbua Hata wewe nikikusimulia utakuja kuniunga mkono kwamba isingekuwa rahisi kwangu kuhisi hivyo, mimi ni mzaliwa wa mkata, kijiji kimoja maarufu sana kwa kuuza mbuzi na nyama ya mbuzi, kando ya barabara ya chalinze hadai Segera  kwa wale ambao wamekwisahawahi kupita barabara hiyo, huenda wanakijua vema kijiji hicho. Mzazi wangu mmoja yaani baba alishafariki wakati nikiwa na umri wa miaka sita hivyo nililelewa na mama.
 

 Maeneo fulani hivi ya Mkata wilayani Handeni

Nilifanikiwa mwaka 1998 kuendelea na masomo ya kidato cha kwanza, nilifanya mtihani wa mwaka 1997 ambapo sikufaulu lakini mjomba wangu mmoja alinitafutia shule ya kurudia mkoani Pwani, nilifaulu mwaka uliofuatia na kwenda pale kibaha, ni ujiko eh! Mtu kusoma shule aliyosoma Kikwete! Kila aliyesoma kibaha hivi sasa bila kuulizwa atakuwa anasema mwenyewe.

Mwaka 2002 nikiwa nimemaliza masomo ya kidato cha nne na kuja Dar kwa dada yangu anayeishi tandika, nilifanikiwa kupoata rafiki wa kike, huyu binti ni mtoto wa mtu mkubwa  na alinipenda siku moja nikiwa nimekwenda kutazama matokeo yangu ya Baraza la mitihani, nilikuwa nimefaulu kidato cha tano kwa kweli mimi ninajipenda na jinsi nilivyo mtu akiniona anaweza kuniamini kabisa kwamba natoka kwenye familia babu kubwa, huyu binti naye aliamini hivyo pia, sikutaka kujiangusha, kwani tulipozoeana aliniuliza kuhusu familia yangu nilimwambia mama yangu amekuwa anaishi Namibia kwa miaka mingi anafanya biashara  na baba yangu alikuwa ubalozini Urusi lakini Alisha kufa. 

Naona mtoto kusikia hivyo aliona amekutana na mtu ambaye wanakaribiana kwa uthamani, Basi mwezi wa sita tangu kujuana siku moja Yule binti akaniomba nijifanye kuwa nimesahau nitie timu kwao yaani nimtembelee Nyumbani kwao.

Nilimuuliza kama haita wakera wazazi wake akasema isingewezekana kuwakera, Basi kijana nikaamua siku hiyo ya juumapili, nikaenda kwao huyu binti, nikasema mtoto wa mtu mkubwa ujue maeneo anayoishi sio tandika shauri lako Nilifika kwao kwenye milango ya saa tano asubuhi, Nilipokelewa kwa shangwe sana. Baba wa mtoto hakuweko lakini mama yake alikuweko  nyumbani, nilitambulishwa kwa mama na nikaulizwa kinywaji nikajifanya muungwana, nikaomba maji, halafu tukaanza kupiga stori na Yule binti na mama naye alijiunga na kuniuliza habari, niligundua kuwa huyu mama alikuwa akipenda watu wa bei ghali kidogo, nami nikawa nashindilia mauongo na maujiko mengi sana  katika kujipandisha wakati wa kula ulipofika ndipo balaa lilipoanza na kuishia nikiwa nimekaa aliingia jamaa mmoja mchafumchafu kidogo He kuhiona tu akaniita kwa jina langu na kuanza kuangusha kilugha  yaani lugha ya kizigua  halafu kabla sijajiandaa kuepusha gharika janga lingine lilitokea “mama huyu ndugu yangu kule kijijini tena hata juzi nilipokwenda kule kijijini nilikutana naye akitokea shambani…………”

Unajua kuwa kuna watu ambao akili zao zinafanya kazi kwa kusigishana na midomo yaani vitu hivyo havikubaliani . Aisee nilionana na mama akasema uko shule, alikuwa anatoka kwenye lile shamba lenu la mihogo kule juu…” Mfumo wangu wa kufikiri ulikuwa kama umepigwa radi kwa hiyo netiweki zilidumaa na kukata mawasiliano kwa muda.

Wewe vipi kwani mama yeke huyu yuko kijijini analima au yuko Namibia wewe umechanganyikiwa au unachanganya watu nini? Yule demu wangu alisema akiwa katahayari, Sasa sister wewe na mimi ni nani anamjua huyu jamaa vizuri? Mama yake tunaishi mtaa mmoja kule home tangu tukiwa wadogo ………”
Unategemea kulitokea nini? Kama hujui kulitokea nini huna haja ya kuamini kuwa zako ziko sawa hata mwanao wa miaka sita ukimuuliza atakwambia, niliadhirika na kufedheheka yaani ilikuwa noma la mwaka! siku hizi nikiona kila mkata majani kwenye nyumba ya afisa namchukia tu bila sababu! Unataka kujua yaliishaje Ni umbea unaokusumbua au kitu gani ona mijimacho yako kutaka kujua ya watu we yako lini?

Hakuna maoni: