Jumatano, 2 Machi 2016

Wala Msiache Kukusanyika !



Andkiko la Utangulizi Waebrania 10; 25, “Wala tusiache kukusanyika pamoja kama ilivyo desturi ya wengine bali tuonyane na kuzidi kufanya hivyo kwa kadiri mwonavyo siku ile kuwa inakaribia”tutajifunza somo hili kwa kuzingatia vipengele vikuu viwili.



§  Kukusanyika Nyakati za Kanisa la kwanza
§  Umuhimu wa kukusanyika pamoja

Kukusanyika Nyakati za Kanisa la kwanza.
Yakati za kanisa la kwanza watu wote waliookoka siku zote kwa moyo mmoja walidumu ndani ya hekalu na kufanya ibada zao nyumba kwa nyumba Matendo 2;46 swala la ibada kwao lilikuwa DESTURI kama ilivyo kwa wanadamu ni kawaida kula na kunywa  nyakai za kanisa la kwanza walihudhuria kila ibada , ni muhimu kufahamu kuwa mtu anayesema kuwa ameokoka kisha akashindwa kuhudhuria ibaa lilkuwa jamo la kushangaza sana, kwa namna hii Neno la bwana lilizidi kuenea na kushinda katika ulimwengu wa nyakati zao Matendo 19;20. Hata hivyo hatimaye watu kadhaa wakaanza tabia ya kuacha kukusanyika  pamoja na wengine kaka ibada na jambo hili linanyonya sana kiwango cha kiroho ni kwa sababu hii Roho wa Mungu alimuongoza mwandisi wa kitabu cha waebrania  kuwaonya watu wasiache kukusanyika Waebrania 10;25, Agizo hili ni kwa kila mmoja wetu pia katika nyakati hzi za leo, Mtu awaye yote asiyehudhuria ibada nguvu zake za kiroho hunyonywa na hatimaye kudhoofika  na kaa kanisa litakuwa wau wake wana tabia hizo litadhoofika lote  ni muhimu kwa kila moja wetu kuwa naufahamu kuwa kutokuhudhuria ibada ni kukiuka Neno au agizo la Bwana.

Umuhimu wa kukusanyika pamoja.
Ziko fikra potofu kuwa unaweza kujisomea Biblia wewe mwenyewe nyumbani na kufanya ibada pamoja na familia yako au kujiombea mwenyewe pamoja na uzuri wa kufanya mambo hayo mwenyewe nimuhimu kufahamu kuwa tunapokusanyika kunakuwa na kiu za ziada zaidi Bwana alisema  wakusanyikapo wawili watau kwa jna langu mimi niko katikati yao Mathayo 18;20 wawili watati ina maana zaidi ya familia moja  watu wanapokusanika pamja Mungu huwepokwa namna ya kipekee sana Zaburi 82;1 Biblia inasema katika andiko hilo “Mungu husimama katika kusanyiko la Mungu katikai ya miungu anahukumu” Kiongozi wa familia anapokuwa na jambo maalumu la kuzungumza na familia ni lazima aikusanye familia yake  ndivo ilivyo kwa Mungu hupenda tukusanyike ndipo anene kipekee Zaburi 50;5,7,. Mwili wa kristo yaani kanisa lna viuno tofauti tofauti na kila kiungo ni cha muhimu 1Wakoritho 12; 26-27. Tunapokusanyika miguu yetu husimama sawa mbele za Bwana Zaburi 26; 12 Bwana ampe neema kila mmoja wetu kuwa na moyo wa kupenda kuhudhuria Ibada katika maisha yaker na kuzidi amen.

Kumbuka pia kuwa Mungu ana tabia ya ujitukuza katika kusanyiko kubwa  Zaburi 35;18 mahali penye watu wengi Nguvu za Mungu hushuka  kipekeee na tunapoomba kwa pamoja Mungu husikia Matendo 4;4,31 visingizio vovyote vle vinavyotuzuia khudhuria ibada  hatuna budi kuvitupilia mbali, shuhuli za dunia na udanganyifu wa mali hulisonga neno la Mungu na kutufanya tusizae matunda yanayompendeza Mungu Mathayo 13;22 hatuna budi kuhakikisha kuwa tunayatupilia mbali udhuru wa aina yoyote  unaotuzuia kuhudhuria ibada  wala tusiache kukusanyika kama ilivyo desturi yaw engine Mungu akubariki sana.

Hakuna maoni: